Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Narudi
 
Mmm msaidieni akiwa huko huko kizunguzi kilosa msimiweke karibu huyu simuamini kabisa uyu zai kijiwenongwa
 
Hii riwaya ishakua changamoto mpk unasahau uliishia wapi[emoji119]
Simulizi za Bishop zinataka moyo maana ni nzuri saaaana af hauzi af anatuma anapoamua kuna mda nataka kususa kbs kuisoma af nashindwa...
 
Hii riwaya ishakua changamoto mpk unasahau uliishia wapi[emoji119]
Simulizi za Bishop zinataka moyo maana ni nzuri saaaana af hauzi af anatuma anapoamua kuna mda nataka kususa kbs kuisoma af nashindwa...
Haha! Tuvumiliane wakuu, sometimes natingwa sana na majukumu au nakuwa safarini, tena wakati mwingine kwenye maeneo ambayo hakuna mtandao. Ila tupo pamoja...
 

205

Simanzi…



Saa 1:30 asubuhi…

BASI la Shabiby lilipiga honi kali za kuashiria kuwa lilikuwa mbioni kuondoka pale kwenye kituo kikuu cha mabasi cha Nanenane, Jijini Dodoma. Honi hizo ziliwafanya wapiga debe wa kituo hicho cha mabasi jijini humo kushangilia na wengine kupiga mbinja kwa fujo.

Zainabu aliyekuwa amekaa kiti cha dirishani alitutazama mimi na Rehema kwa uchungu mkubwa, macho yake yalionesha uchungu mkubwa na machozi yalikuwa yanamlengalenga machoni. Hilo halikunistaajabisha kabisa. Sikustaajabu kwa kuwa niliamini kuwa alikuwa na huzuni ya kumwachia mwanamke mwenzake mwanamume aliyempenda sana.

Kilichonistaajabisha ni baada ya kumwona Rehema naye akilengwalengwa na machozi. Niliwatazama wote wawili, Rehema na Zainabu, nikaona kitu ambacho ilikuwa vigumu sana kwa mtu asiye mdadisi kama mimi kukiona na kukielewa.

Kwa haraka haraka mtu angeweza kusema kuwa kulikuwa na ladha ya upendo wa dhati iliyokuwa inawakilishwa na machozi ya wanawake hao wawili, lakini mimi sikuona kitu kama hicho, niliona kitu cha ziada. Kitu ambacho kila nilipojaribu kukitafakari sikuweza kupata jibu la haraka!

Hatimaye Zainabu alikuwa anarejea kwenye makazi yake mjini Kilosa baada ya kuwa amekaa nasi pale Jijini Dodoma kwa kipindi cha juma moja. Katika muda wote wa juma moja aliokuwa hapo Dodoma alionekana kuwa na furaha kubwa na hakuonesha tofauti yoyote kati yake na Rehema.

Almasi kwa upande wake alikaa pale Dodoma kwa siku moja tu na siku iliyofuata aliondoka kurudi Kilosa. Hata hivyo kwa siku hiyo moja nilikuwa nimepata wasaa mzuri sana wa kuongea naye na kupanga naye mambo mengi mazuri kwa ajili ya future. Kwa ujumla Almasi alikuwa mtu mwenye akili kubwa sana, he was well educated, ingawa hata mara moja hakupenda kugusia kuhusu elimu yake.

Katika siku hiyo moja niligundua kuwa ufahamu wake kuhusu mambo mbalimbali ulikuwa mkubwa mno na alikuwa na uwezo wa kuchambua mambo kiasi cha kunifanya nijione bado natakiwa kurudi shule.

Sasa Zainabu naye alikuwa safarini kurudi Kilosa, na katika safari hiyo, Zainabu alikuwa ameambatana na Grace ambaye alipanga kwenda kukaa Kilosa na Zainabu kwa siku kadhaa. Zainabu sasa alianza kuchukuliwa kama mmoja wa wanafamilia, na kiukweli, familia ilionesha kumkubali. Alikuwa ameambiwa kuwa anaruhusiwa kufika hapo nyumbani kwa Mchungaji Ngelela au kwa ndugu yangu yeyote, wakati wowote.

“Zainabu… ukifika tu naomba unifikishie ujumbe wangu kwa Almasi. Mwambie azingatie sana kile tulichoongea siku alipokuwa anaondoka, na mimi pia nitampigia simu nikifika Kahama,” nilimwambia Zainabu wakati lile basi la Shabiby likianza kuondoka taratibu.

Zainabu aliitikia kwa kichwa huku akifuta machozi yaliyoanza kumtoka na kutiririka mashavuni kwake na kisha tulipungiana mikono ya kwaheri. Mimi na Rehema tulilisindikiza kwa macho lile basi wakati likiondoka hadi pale lilipoingia barabarani na kutoweka kabisa kwenye upeo wa macho yetu.

Nikashusha pumzi ndefu kama niliyemaliza mbio ndefu za marathoni kisha mimi na Rehema tukaangaliana na kukumbatiana. Muda wote Rehema alikuwa mkimya sana na bado aliendelea kulengwalengwa na machozi.

Tulipoachiana tuliongozana hadi kwenye gari lililotuleta, tukaingia na kuondoka kurudi nyumbani kwa Mchungaji Ngelela kwa ajili ya maandalizi ya safari yetu ya kuelekea Kahama siku iliyofuata… safari ya kwenda kuyaanza maisha mapya kama wapenzi tuliohalalishwa yaani wanandoa na pia wazazi wa mtoto Jason Sizya Junior.

Hata hivyo, bado kichwani kwangu kulikuwa swali lililoendelea kunitesa, swali kuwa; hali ile ya upendo na kutokuwepo kwa tofauti yoyote iliyooneshwa na Zainabu kwa Rehema (japo sikuwa na uhakika sana na jambo hilo) ingeendelea kuwepo au ingekuwa ya muda tu? Hadi hapo nilijikuta nikibaki njia panda na nisijue nini cha kufanya.

Huu ni mwisho wa Msimu wa Nne kwenye mfululizo wa Harakati za Jason Sizya. Usikose Msimu wa Tano katika mkasa uitwao “Ufukweni Mombasa”.
 
Dondoo:

Kuanzia msimu wa tano wa Harakati za Jason Sizya stori inabadili kabisa mkondo, utakayoyashuhudia humo yatazidi kukuacha mdomo wazi. Endelea kufuatilia...
 
Dondoo:

Kuanzia msimu wa tano wa Harakati za Jason Sizya stori inabadili kabisa mkondo, utakayoyashuhudia humo yatazidi kukuacha mdomo wazi. Endelea kufuatilia...
kuna mda natamani uuze tusio na subra tujilipue asa hivi ndo nn jmn kimoja tu apo inaitwa tuonane wiki ijayoooooooooooooo wewe ni mtunzi kwelikweli askofu
 
kuna mda natamani uuze tusio na subra tujilipue asa hivi ndo nn jmn kimoja tu apo inaitwa tuonane wiki ijayoooooooooooooo wewe ni mtunzi kwelikweli askofu
Usijali. Shida ni kwamba nina stori nyingi mno nilizoziandika kitambo, hivyo kabla sijaiachia stori yoyote huwa naipitia tena na kurekebisha baadhi ya vitu viendane na hali ya sasa jambo linalonifanya wakati mwingine kuchelewa hasa ukizingatia kuna majukumu mengine yananibana. Hata hivyo ndo maana huwa nikiachia naacha mzigo wa kutosha (isipokuwa leo tu[emoji23][emoji23])...
 
Unaonaje ukiuza mkuu wangu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…