Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Simulizi: Harakati za Jason Sizya

ufukweni mombasa.JPG

223

Najua unanisikia…




NILISHTUSHWA toka usingizini na kelele za kitasa cha mlango wa kile chumba kiliponyongwa kwa papara na kisha mlango kusukumwa kwa ndani. Nilikuwa nimepitiwa na usingizi ulionifanya niyasahau yale mateso kwa muda. Niligeuka kutazama kule mlangoni na hapo nikawaona wanaume wanne wakiingia kibabe mle ndani wakiongozwa na yule daktari.

Niliwatambua wale wanaume kuwa ni Meja Saleh bin Awadh, komando mweusi, komando Mwarabu na yule komando Mpalestina.

“Waambie tu ukweli, leo wamepanga kukuua,” yule daktari alininong’oneza sikioni kwa huruma baada ya kunifikia. Taarifa ile ilinifanya niihisi hofu ya kifo ikinitambaa mwilini.

Watu wale hawakunisemesha badala yake walikizunguka haraka kitanda kisha komando mweusi alichomoa sindano za dripu katika mishipa yangu mkononi pasipo kuzingatia utaalamu wa kidaktari na hivyo kunisababishia maumivu makali, hata hivyo yule mtu hakuonekana kujali. Halafu walinishika miguu yangu na kunishusha toka pale kitandani kwa nguvu, nikaanguka kisha wakaniburuta kibabe kuelekea nje ya kile chumba.

Tulipofika nje ya chumba tukaanza kukatisha ukumbi mrefu hadi mwisho kabisa, tukakata kushoto kisha tukaanza kushuka ngazi hadi tulipofika chini tukaingia upande wa kulia. Safari yetu ikaishia sehemu yenye mlango wa chuma upande wa kushoto. Kisha komando Mwarabu akaufungua ule mlango wa chuma. Wakaniingiza humo.

Sikuweza kuona chochote mle ndani kwa vile kulikuwa na giza nene lakini baada ya muda mfupi taa za mle ndani ziliwashwa na hapo nikapata kuyaona vizuri mandhari yale. Kilikuwa chumba kile kile cha mateso. Koo langu likanikauka kwa hofu ya kifo.

Kisha Meja Saleh bin Awadh alinigeukia na kusema, “Nadhani unaelewa fika ni taarifa gani tunazihitaji toka kwako, leo hatutakubembeleza, tueleze ukweli vinginevyo utakufa kifo cha mateso makali.”

“Hata sielewi kwa nini mnaning’ang’aniza niwape majibu kwa kitu ambacho sikijui wala hamjanituma?” nilimwambia Meja Saleh bin Awadh kwa jeuri.

“Endeleeni na kazi,” Meja Saleh bin Awadh aliwaambia wale makomando. Bila kuchelewa makomando wawili walinikamata na kunifunga kamba miguuni na mikononi haraka haraka na baada ya hapo nilijikuta nikibebwa juu juu na kutundikwa kwenye vile vyuma vifupi vilivyokunjwa na kuchongwa mbele yake mfano wa vyuma vya kuning’inizia nyama buchani, nikaning’inia kichwa chini miguu juu.

Kisha yule komando Mpalestina alinisogelea na kunichapa kofi usoni halafu akanifokea huku nikiwa bado nimening’inizwa. “Kama hawa walikuchekea basi mimi sina utani. Hakuna aliyewahi kuingia humu akabaki na siri zake moyoni, hata wewe naamini utasema tu.”

Nilibaki kimya. Yule komando alinitazama kwa ghadhabu kali kisha akashusha pumzi zake na kutazama kando, akakunja sura yake huku akionekana kama aliyekuwa akitafakari jambo fulani. Mara nikamwona akipiga hatua na kwenda kuchukua kibubu chenye gesi kisha aliiwasha ile gesi na kuonekana akijaribu kurekebisha ule moto wa gesi. Baada ya kuweka moto fulani kwenye kile kibubu cha gesi, akanifuata na kuanza kunipitishia usoni bila kunidhuru, nia ilikuwa kunisikilizisha lile joto lililotoka mle kwenye kibubu.

“Nadhani umelisikia joto lake, nakupa sekunde tano tu utuambie vinginevyo joto hili litakwenda kwenye sehemu zako za siri,” yule komando aliongea huku akinitazama kwa hasira.

Nilibaki kimya kwa kuwa muda ule nilikuwa nahisi kizunguzungu kikali, sauti nyembamba mfano wa sauti itokayo kwenye filimbi ilikuwa inalia kwenye masikio yangu na giza zito lilianza kutanda kwenye mboni za macho yangu. Yule komando Mpalestina alinitazama kwa umakini na kusonya.

Bado nilibaki kimya. Hata hivyo niligundua kitu, niligundua kuwa wale jamaa hawakuwa na nia ya kuniua, huenda walitaka kunitumia kama mateka ili kupeleka madai yao sehemu ndiyo maana waliishia kunitisha tu au kunipa mateso waliyoamini kuwa ningeyamudu.

Wakati nikiwaza hayo nikamwona yule komando Mpalestina akiuzima ule moto wa gesi na kukiweka kando kile kibubu cha gesi. Nikiwa nashangaa nikamwona akichukuwa lile betri kubwa la gari lenye kufua umeme ambalo lilikuwa na vishikizo vilivyofungwa mwishoni. Akalisogeza karibu yangu na hapo nikamwona akiijaribu ile nguvu ya betri kwa kuzigusanisha zile nyaya mbili, zikapiga shoti kubwa na kutoa cheche. Akaonekana kufurahi sana.

“Nadhani hii ndo itakufaa zaidi… ila utanisamehe maana sikupenda tufikishane huku, ila kwa vile umetulazimisha kufanya hivi. Hata hivyo muda wa kujiokoa bado upo. Tuambie tunachotaka kusikia halafu tutakuacha,” yule komando Mpalestina aliniambia. Sikumjibu neno kwani hasira ilikuwa imenikaba kooni.

“Luteni, kama hataki kusema mpe dozi,” nilimsikia Meja Saleh bin Awadh akimwambia yule komando Mpalestina.

Na hapo nikajikuta nikianza kuchomwa na zile nyaya kila sehemu mwilini nikilazimishwa kuongea. Mateso yale yaliendelea kwa dakika mbili huku nikihisi maumivu makali mno mwilini, hata hivyo niliendelea kushikilia msimamo wangu wa kutowaeleza chochote. Hakuacha, akaendelea kunipa mateso yale na mengine zaidi kwa muda mrefu na walipoona sielekei kuwaambia chochote cha maana, Meja Saleh bin Awadh akamwambia yule Luteni aniache.

“Naona amedhamiria kufa kiume,” Meja Saleh bin Awadh alimwambia yule Luteni na muda huo huo nikamwona akinisogelea kisha akaanza kunishushia kipigo.

Kilikuwa kipigo hatari sana kwangu, japo tayari nilikuwa nimewiva kwenye mafunzo ya kujihami ya karate lakini sikuwahi kushuhudia kipigo cha aina ile ambapo mtu anapigwa akiwa amefungwa kwa kamba madhubuti na kuning’inizwa kichwa chini miguu juu. Baada ya kama dakika tano hivi nilikuwa nimechakaa vibaya huku uso wangu wote ukiwa umetapakaa kwa damu.

“Naamini sasa upo tayari kutwambia,” nilimsikia Meja Saleh bin Awadh akisema.

Bado niliendelea kushikilia msimamo wangu wa kutowaeleza chochote. Nilishakubali kufa pasipo kutoa siri. Hata hivyo nilipojaribu kufumbua macho yangu kumtazama Meja Saleh bin Awadh nikajikuta nikimwona kama kiumbe cha ajabu kisichoeleweka huku lile eneo nikiliona kama tufe fulani lililokuwa linazunguka angani.

Kisha nilianza kuona giza mbele yangu na kwa mbali niliisikia sauti ya Meja Saleh bin Awadh ikiniambia. “Twambie vinginevyo utakufa kifo kibaya sana.”

Nilijitahidi kukodoa macho yangu lakini nikawa naona giza mbele yangu, na hata nilipotaka kufumbua mdomo wangu ili nimjibu bado sikufanikiwa kwani fahamu zilikuwa mbioni kunitoka. Mwili wangu ulizidiwa na maumivu makali yasiyoelezeka na sasa nilitambua kuwa mwisho wangu ulikuwa umefika. Halafu sikuelewa nini kiliendelea.

* * *

Endelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

224

Nilipokuja kurudiwa tena na fahamu zangu nilikuwa nimelala sakafuni. Walipogundua kuwa nimerudiwa na fahamu mateso yakaendelea, kama kawaida walitaka niwaleleze kuhusu kilichokuwa kinaendelea ‘Shamba’ na niwatajie majina ya walimu. Sikujua kwa nini walitaka taarifa hizo, hata hivyo sikujisumbua kujiuliza swali hilo kwani nilishadhamiria kutosema chochote.

Niliendelea kupata mateso makali sana na yaliendelea kwa wiki nzima, kuna wakati nilitamani kifo kinijie haraka ili niepukane na mateso hayo kwani nilipewa kila aina ya mateso makali ikiwemo kugongelewa misumali mgongoni, kwenye mikono na kwenye mapaja wakisisitiza niwaambie kile walichotaka kukijua.

Sasa mwili wangu ulikuwa umedhoofika sana lakini bado niliendelea na msimamo wangu ule ule wa kutosema, nilikuwa tayari kufa kuliko kusema ingawa ilibaki kidogo tu nibadili msimamo wangu baada ya kuambiwa kuwa Leyla alikuwa ameteswa sana na sasa walitaka kumuua kama nisingesema.

Hata hivyo machale yalinicheza, nilihisi kabisa kuwa walikuwa wanataka kucheza na akili yangu kwani kama Leyla walikuwa naye kwa nini yeye asiwaambie kile walichokuwa wakitaka kujua toka kwangu kwa kuwa nilichokijua mimi ndicho hicho hicho alichokijua Leyla. Nikahisi kuwa huenda yeye alishakufa tayari kwa kushindwa kuhimili yale mateso.

Kiukweli nilipatwa na uchungu mkubwa sana moyoni, nilitamani na mimi nife nimfuate Leyla, sasa nikawa nimekata tamaa. Wakati fahamu zangu zikianza kutoweka kwa mara ya mwisho niliamini kabisa kuwa nisingeweza kuamka tena. Kifo kilikuwa kinanichukua taratibu…

* * *



Nilizinduka tena nikajikuta nipo kwenye chumba kikubwa, nikiwa nimelala kwenye kitanda kikubwa cha chuma cha futi tano kwa sita. Nilishangaa kuona nilikuwa ndani ya chumba tofauti na kile cha mwanzo, hiki kilikuwa nadhifu mno na nilikuwa nimelalia foronya laini na mto wa kuegemeza kichwa.

Ndani ya chumba kile kulikuwa na hewa safi iliyokuwa ikisambazwa taratibu na kiyoyozi kilichokuwa juu ya dari iliyokuwa imetengenezwa kwa gypsum nzuri ya rangi nyeupe na katika sehemu za dari ile kulining’inizwa taa ndefu nzuri.

Nilishangaa kuona kuwa nilikuwa bado mzima nikipumua na sikujua nilikuwa nimepoteza fahamu kwa muda gani. Niliweza kuyakumbuka vizuri masaibu yote yaliyonitokea kule kwenye chumba cha mateso makali. Sikuwa na uhakika nilifikishwa pale kwa gari, mkokoteni, machela au niliburuzwa tena kama ilivyotokea kule kwenye chumba cha mateso, kwa kuwa sikuwa na fahamu yoyote nilipokuwa nikiletwa pale.

Pembeni kidogo ya kitanda kulikuwa na mashine ndogo ikionesha mishale mishale ambayo ilikuwa imepinda pinda, nilipojichunguza vizuri nikajikuta nikiwa nimevalishwa kitu kilichofunika pua na mdomo wangu. Mara moja nikatambua kuwa ilikuwa mashine maalumu ya kunisaidia kupumua na pembeni kulikuwa na kijiruninga (monitor) kikionesha mwenendo wa mapigo ya moyo wangu.

Nilijaribu kujiinua ila nikashindwa, mwili wangu ulikuwa umezingirwa na nyaya mbalimbali zilizounganishwa na tarakilishi kubwa iliyokuwa ukutani, na pia sikuwa na nguvu za kufanya kitu chochote zaidi ya kuendelea kujilaza kitandani.

Wakati nikiwa nimelala nilianza kuyatembeza macho yangu na hapo nikaiona stendi ndefu ya chuma ya kitabibu kando ya kitanda changu ikiwa imetundikiwa drip kubwa ya maji aina ya Dextrose 5% ambayo maji yake yalikuwa yamechanganywa na dawa fulani ya rangi ya njano.

Sasa macho yangu yalikuwa yamepata uhai zaidi, nilipochunguza kwa umakini nikagundua kuwa mrija wa ile drip ulishuka hadi kwenye mkono wangu wa kulia na mwishoni kulikuwa na sindano iliyokuwa imechomekwa kwenye ule mkono na kupeleka maji kwenye mshipa wangu wa damu. Nikashusha pumzi, kisha nikafumba macho yangu nikijaribu kutafakari.

Bado sikuelewa pale nilikuwa wapi, lakini kilichonishangaza mno ni kuona kuwa nilikuwa ndani ya chumba nadhifu chenye mifumo ya kisasa kabisa ya uchunguzi kwa mgonjwa. Nikajiuliza ikiwa pale ni hospitali, je, ilikuwa hospitali gani na nilifikaje? Sikuwa na jibu.

Nikaanza kuyatembeza tena macho yangu taratibu huku na kule katika namna ya kuyatathmini vizuri mandhari ya kile chumba nia yangu kuona kama kulikuwa na kielelezo chochote ambacho walau kingenifanya kuhisi pale nilikuwa katika hospitali gani. Sikugundua haraka hata baada ya macho yangu kuchunguza kwenye yale mashuka niliyofunikwa lakini hisia zangu ziliniambia kuwa nilikuwa sehemu salama zaidi. Na hapo nikajikuta moyo wangu ukipiga kite kwa nguvu!

Nilihisi kuwa nilikuwa ndani ya hospitali maalumu ya chuo cha Zawyet Sidi Abd el-Ati huko Alexandria. Sikujua kama hisia zangu zilikuwa sahihi ila niliamini kuwa nilikuwa nimefikishwa pale chuoni.

Hata hivyo, kulikuwa na hisia nyingine ndani yangu ikipingana na ile hisia ya mwanzo, na wakati mwingine nilihisi labda ilikuwa ndoto ila nikayafukuza mawazo hayo haraka sana kichwani kwangu nikijiambia kuwa ile haikuwa ndoto. Sikujua kwa nini sasa moyo wangu ulianza kuwa na amani, na hapo nikageuza shingo yangu kuutazama mlango wa kile chumba kwa umakini nikauona ukiwa umefungwa ingawa sikuweza kufahamu kama ulikuwa umefungwa kwa funguo au ulikuwa umerudishiwa tu. Nilishindwa kuthibitisha hilo kwani afya yangu ilikuwa dhaifu sana kiasi cha kushindwa hata kunyanyuka na kuketi pale kitandani.

Kutoka pale kitandani nilipolala nilibaki nikiwa mtulivu huku nikiutazama ule mlango huku nikishindwa kuyazuia mawazo yaliyoendelea kupita kichwani mwangu. Muda ule ule nikashtuka kuona kitasa cha ule mlango kikizungushwa taratibu kisha ule mlango ukasukumwa kwa ndani na kufunguka, nikajikuta nikiingiwa na hofu huku moyo wangu ukipoteza utulivu katika kiwango cha hali ya juu.

Nikayafumba haraka macho yangu nikatulia nikijifanya bado sijarudiwa na fahamu ili niweze kubaini kama nilikuwa sehemu salama au la. Nikiwa nimefunga macho nikasikia kishindo cha hatua za mtu akiingia mle ndani na kuja moja kwa moja pale kitandani, kisha nikashtuka baada ya kuhisi mkono laini sana ukinigusa kwenye paji langu la uso. Sikuthubutu kufungua macho yangu bali nilijifanya sijarejewa na fahamu zangu.

Oh! Please God, help him. I still need him…” niliisikia sauti ya mwanamke huyo ikiomba kimya kimya, kisha mtu huyo akavuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu. Ilikuwa sauti niliyoifahamu vyema ila kwa muda huo sikukumbuka ilikuwa ya nani.

“Jason, najua unanisikia… Ni mimi Leyla Slim Abdullas... rafiki na mwandani wako… Najua wewe ni mpiganaji na hutakubali kushindwa. Najua bado unayo ndoto ya kufikia mafanikio yako ya kuwa mpelelezi wa kiwango cha kimataifa. Tafadhali usiondoke mapema ukaniacha. Najuta kusema kuwa lilikuwa kosa langu ila sikujua kama ungefikia hatua hii. Sikujua…” Leyla alisema kwa huzuni kubwa na hapo akashindwa kuendelea na kuanza kulia kilio cha kwikwi.

Nilishindwa kuvumilia, nikayafungua taratibu macho yangu kisha nikageuza shingo yangu kutazama upande ilikotokea sauti yake, na hapo nikamwona Leyla akiwa amesimama kwa unyonge, kidevu chake kikiwa kimeanguka kifuani kwake, msirimbi wa kipaji cha uso wake umeumuka, milizamu imetutusika chini ya masikio yake ikiwa kama iliyopulizwa, shingo yake imevimba na michirizi ya machozi ikimtiririka mashavuni mwake.

Alikuwa amevaa mavazi maalumu mfano wa joho, la rangi ya samawati, kofia maalumu na kitambaa cha kufunika mdomo na pua. Nikajikuta nikipatwa na mshangao mkubwa. Leyla, ambaye niliambiwa kuwa aliteswa sana, alikuwa mzima wa afya na hakuwa na jeraha lolote mwilini kwake jambo lililonifanya nijikute nikiachia mguno wa mshangao. Na hapo Leyla akashtuka na kuyapeleka macho yake kwenye uso wangu.

Alipogundua kuwa nilikuwa nimeamka alipatwa na mshtuko mkubwa wa furaha, kisha nilimshuhudia akijitahidi kuyazuia machozi yamsitoke lakini hakuweza, alijitahidi, akajitahidi na kujitahidi lakini akaonekana kushindwa kabisa kujizuia. Na hapo akaangua kilio kikubwa kilichosikiwa na watu wengine waliokuwa nje ya kile chumba.

Kisha nikashuhudia mlango ukifunguliwa na watu wanne wakaingia haraka mle chumbani. Watu hao ni daktari wa ile hospitali ya chuo, muuguzi pamoja na walimu wawili.

* * *

Tukutane wakati mwingine. Endelea kufuatilia...
 
ufukweni mombasa.JPG

225

Usiku wa kukumbukwa…




Saa 4:00 usiku…

JAPOKUWA nilifahamu kuwa alikuwa mzuri sana lakini usiku huu ndiyo niliweza kuuona waziwazi uzuri wake. Usiku huu uzuri wake ulikuwa umevunja rekodi kutokana na vazi alilolivaa. Alikuwa amevaa fulana nyepesi nyeupe iliyoshindwa kuyaficha matiti yake imara yenye ukubwa wa wastani na chuchu ngumu zilizosimama kama ncha ya mkuki wa Kimasai.

Chini alivaa kaptula fupi nyeusi ya dengrizi iliyoifichua minofu ya miguu yake mizuri na mapaja yake meupe yaliyonona. Miguuni alivaa raba nyeusi na kofia nyeusi ya kapelo kichwani. Nywele zake ndefu zilimwagika kwa nyuma, nyusi alizitinda vizuri na kuzipaka wanja mwembamba mfano wa mwezi mwandamo, kope aliziremba vyema na hivyo kuyafanya macho yake malegevu yaonekane vizuri.

Midomo yake ilikolea lip shine ya kijivu na alivaa mkufu mwembamba wa dhahabu ulioizunguka shingo yake nyembamba na kisha kidani chake kikapotelea katikati ya mfereji wa matiti yake mazuri kifuani.

Kwa nukta kadhaa nilijikuta nikiduwaa na kumkodolea macho kana kwamba nilikuwa namwona kwa mara ya kwanza. Nilimtazama pasipo kukinai, kuanzia miguuni hadi kichwani huku nikijiambia kimoyo moyo kwamba alikuwa anazo sifa zote za kuitwa mrembo, tena mrembo wa dunia.

Usiku huu mimi nilikuwa nimevalia sweta jepesi jeupe lililoungana na kofia iliyofunika kichwa changu, chini nilivaa suruali nyeusi ya dengrizi na buti ngumu nyeusi miguuni.

Tulikuwa tunacheza muziki wa Justin Bieber uitwao ‘Sorry’ kwenye sherehe iliyoandaliwa maalumu ya kutuaga baada ya kumaliza miezi tisa ya ‘misukosuko’ ya mafunzo ya kijasusi. Sasa masomo yalikuwa yamefika tamati na kila mmoja wetu alitakiwa kurudi nchini kwake kujenga taifa.

Kwangu ilikuwa ni zaidi ya furaha. Si tu furaha ya kumaliza ile miezi tisa ya hekaheka za hapa na pale katika kuhakikisha natimiza lengo langu na la taifa langu bali pia furaha ya kurudi nyumbani Tanzania kuwaona ndugu na jamaa niliopoteana nao kwa kipindi chote cha mafunzo yangu.

Pia nilikuwa na haki ya kufurahi na kujipongeza kwa kuwa nilikuwa nimehitimu vizuri kwa kupata alama za juu zilizonifanya kushika nafasi ya juu zaidi katika darasa letu. Na nilikuwa nimeweka rekodi ya kuwa mtu niliyeweza kuvumilia mateso makali kwa muda mrefu zaidi kuliko mtu yeyote mwingine aliyepitia mafunzo ya kijasusi katika kipindi cha miaka 30 iliyokuwa imepita.

Mwanzoni ilikuwa siri ambayo sikutakiwa kuijua lakini baadaye haikuwa siri tena, ikafichuka kuwa, yale mateso niliyoyapata kule porini yalikuwa sehemu ya kuupima ujasiri na uvumilivu wangu katika kuyavumilia mateso makali endapo nikikamatwa na kutakiwa kutoa siri za nchi, na wakati napata mateso hayo darasa lilikuwa linashuhudia kila kitu, ikiwa ni pamoja na huyu mrembo Leyla Slim Abdullas, ambaye sasa nilikuwa nacheza naye muziki.

Kwa upande wangu sikujua kabisa kuwa wakati Leyla akinichukua kwenda matembezi alikuwa anafahamu nini ambacho kingenitokea na hata tuliponasa kwenye mtego alinifanya nidhani kuwa tuliingia kwenye mtego na kutekwa pasipo kujua. Kumbe ulikuwa mpango ambao mimi sikuujua. Hili nalo likawa nimenipa funzo jingine kubwa kwamba; ndani ya kazi ya ujasusi kila mtu kwako ni adui na hutakiwi kumwamini yeyote, vinginevyo utakuwa unakikaribia kifo chako mwenyewe.

Nilikuwa nimemzoea sana Leyla na pia nilimpenda sana. Japokuwa hatukuwahi kushiriki tendo la ngono lakini niliamini kuwa ingenichukua muda mrefu kabla ya kumbukumbu yake kufutika kabisa kichwani mwangu.

Mawazo hayo yalikuwa yanapita kichwani kwangu wakati tukiendelea kucheza. Na kwa jinsi tulivyoendana watu wengi walijikuta wakituangalia sisi tu, kupitia macho yao, nilitambua kuwa wapo waliotuangalia kwa kuvutiwa na uchezaji wetu, na wengine kwa husuda! Tulipendeza mno tukawa kama mapacha.

Wimbo ule ukaisha na wimbo wa pili wa taratibu ukaanza, ulikuwa wimbo wa Judy Boucher unaoitwa ‘Dreaming of a Little Island’. Hatukuondoka pale kwenye eneo la kuchezea. Tulianza kuucheza wimbo huo huku tumekumbatiana, Leyla aliipitisha mikono yake shingoni kwangu na mimi niliizungusha mikono yangu kushika kiuno chake, na tukasahau kama kulikuwa na watu wengine wakituangalia.

Kisha tulianza kuuimba wimbo huo tukiyafuatisha mashairi ya Judy Boucher; I am dreaming of a little Island, there’s space enough for two, I hope my wish be granted, I’ll build a little villa for two. I want you by the seaside, holding hands smiling with the tide, making up for all we’ve been missing, romantic time is here. You’re such good company, and no one can deny, if this is gift thank God it’s meant for me, we’ll have two lovely children, on this land am dreaming on…

Hisia zetu zilikuwa huru, tukiburudika mwili na roho, akili zetu zikajiona kama tuliofika safari yetu baada ya kuvuka milima na mabonde.

“Katika siku zote, naomba siku ya leo isifutike kwenye akili zetu. Tuufanye usiku wa leo uwe wa kukumbukwa,” nilimnong’oneza Leyla sikioni wakati tukiwa tumekumbatiana.

“Kweli eh?” Leyla aliuliza kama mtoto mdogo kisha akaangua kicheko hafifu.

“We unadhani nani atavumilia kumkumbatia mrembo kama wewe halafu aishie kula kwa macho tu?” nilisema huku nikiupapasa mgongo wake. Nikamwona Leyla akiyafumba macho yake huku akiusikilizia mpapaso ule wa mikono yangu.

“Kumbuka kauli yako siku ile kuwa kukutana kwetu hakukuwa kwa bahati mbaya… hii kwetu ndiyo nafasi nzuri, lazima tuifanye siku ya leo kuwa ya kukumbukwa zaidi kwenye maisha yetu,” nilisema na kumfanya Leyla anitazame machoni kwa macho yaliyojawa na aibu.

Mara tukashtuka baada ya kuhisi eneo lote lilikuwa limetawaliwa na ukimya. Kumbe muziki ulikuwa umekwisha kitambo! Ni sisi wawili tu ndio tuliokuwa tumebaki wima kwenye eneo la kuchezea muziki. Kwa aibu tukaongozana kwenda kukaa.

Sherehe ilipokwisha mnamo saa sita usiku nilipanga kumchukua Leyla hadi chumbani kwangu… niligundua kuwa alikuwa 'ameshakolea' ingawa haikuwa rahisi kwake kukubali moja kwa moja. Nilimshika mkono nikamwongoza kwenda kwangu. Hakuleta pingamizi lolote kwani alionekana kutojiweza na uso wake aliuinamisha chini kwa aibu.

Tulipoingia ndani ya chumba changu, chumba namba 20 kilichokuwa kwenye ghorofa ya kwanza ya jengo la hosteli ya wanafunzi wa mafunzo maalumu ya kijasusi liitwalo Block E, nilimvutia kifuani kwangu nikamkumbatia. Leyla alijigandamiza kwenye mwili wangu na kutulia huku akihema kwa nguvu.

Nilipomwona katulia sikutaka kusubiri, nilimbeba Leyla hadi kitandani, nikamwangusha kama mzigo. Nikahisi pumzi zikimpaa! Kilichofuata baada ya hapo kilimfanya Leyla azungumze lugha ambayo hata yeye mwenyewe hakuwa anaijua na wala hakuwahi kuisikia kwani ina utamkaji tofauti wa maneno ya lugha yoyote tuliyoijua.

Nilizidi kumpelekea moto huku mechi ikitawaliwa na rafu mbalimbali kwa kuwa katika mchezo wetu hakukuwa na refa na kila mtu alijaribu kulipiza rafu anayochezewa na mwenzake, mojawapo ya rafu hizo ni vibao ambayo nilikuwa nampiga kwenye makalio yake huku na yeye akinilipizia kwa kunifinya katika mikono yangu.

Moto huo ulimfanya asijimudu na wala asiweze kuvumilia, alitapatapa kama samaki anayekaangwa hai. Alijikuta akiwa taabani huku akiyashuhudia maumivu ya kupendeza yaliyokuwa yakimuua taratibu kama mgonjwa aliye taabani. Kisha akaanza kulia. Kilikuwa kilio cha faraja kilichotokana na adhabu aliyojitakia mwenyewe ambayo wala hakuijutia. Alilia na machozi yakamtoka, sauti ikamkauka. Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwetu sote, usiku ambao kamwe usingepotea katika fikra zetu.

Mechi ilipoisha Leyla hakuweza hata kunitazama machoni, alikuwa anatweta kama aliyemaliza mbio ndefu za kilomita arobaini na mbili baada ya kuvunja rekodi ya dunia. Aliyafuta machozi yake kwa kiganja cha mkono na kushusha pumzi ndefu. Kisha tulijilaza pale kitandani na kuegemeza vichwa vyetu kwenye mito tukiwa watupu. Leyla akiwa pembeni yangu aliutazama kwa huruma mwili wangu uliojaa makovu.

“Mh! Pole sana, Jason, kwa masaibu yaliyokukuta kule Shamba,” Leyla aliniambia kwa sauti ya upole huku akiyatazama yale makovu.

“Ahsante, naamini kama si Mungu na mazoezi magumu ninayoyafanya kila siku pengine ningekufa na tusingeonana tena hapa duniani,” nilimwambia Leyla huku nikitabasamu.

“Dah! Wale makomando hawana huruma kabisa, ona walivyokusulubu! Warembo wakikuona kwa nje umenyuka pamba wanababaika na uzuri sasa shida inakuja pale utakapovua nguo…” Leyla alisema kwa masikitiko.

“Yote haya ni kwa sababu yako…” nilidakia huku nikimtazama Leyla kwa utulivu, kisha nikaongeza, “hivi uliwezaje kunifanyia hivi, Leyla? Kwa nini hukunidokeza kama nilikuwa nakwenda kukutana na mateso makali, labda ningejiandaa kisaikolojia…”

Shhhhh! I’m so sorry…” Leyla alisema kwa sauti ya chini huku akiweka kidole chake cha shahada kwenye mdomo wangu kunizuia nisiongee.

Sorry for what?” niliuliza kwa sauti tulivu huku nikimtazama usoni.

For everything…” Leyla alisema na kuongeza, “Halikuwa kusudio langu bali ilikuwa sehemu ya mafunzo yanayokuandaa kuwa jasusi wa kimataifa. Najua hata taifa lako linajivuna kuwa na mpelelezi kama wewe.”

Ni kweli… taifa lilikuwa linajivuna. Nilifahamu kuwa viongozi wa Idara ya Ujasusi walikuwa wananisubiri kwa hamu pale makao makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa Jijini Dar es Salaam. Walikuwa na taarifa zote kuhusu rekodi niliyoiweka mafunzoni, rekodi ambayo ingechukua miaka mingi sana kutokea mtu wa kuivunja na pengine asitokee kabisa.

Hata hivyo, kwa kiwango kikubwa rekodi hiyo ilikuwa imechangiwa na kauli ya Luteni Lister aliyoniambia siku tulipokuwa tukiagana pale Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam. Aliniambia; “Jason, mafunzo utakayopata huko chuoni pekee hayatoshi, hii ni kazi ambayo wakati mwingine akili yako ya kuzaliwa inahitajika zaidi.”

Kauli hiyo iliendelea kujirudia akilini mwangu kwa muda wote wa mafunzo yangu ya kijasusi pale chuo cha Zawyet Sidi Abd el-Ati.

* * *

Endelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

226

Karibu nyumbani…




Saa 6:30 mchana…

MTIKISIKO uliotokea baada ya magurudumu ya ndege aina ya Boeing 737-800 ya Shirika la Ndege la Ethiopia, Ethiopian Airline, kuanza kutua kwenye ardhi ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere ulinishtua kutoka usingizini. Niliyafumbua macho yangu kivivu na kutazama nje. Nilikuwa na uchovu mwingi. Shughuli pevu ya usiku wa siku iliyotangulia kule chumbani kwangu kwenye jengo la hosteli ya wanafunzi wa mafunzo maalumu ya kijasusi, ilikuwa imeniacha hoi bin taaban.

Wakati ndege yetu ikikimbia kwa kasi kwenye barabara ndefu ya lami maarufu kama ‘runway’ iliyokuwa imewekwa alama elekezi ili kuwaongoza marubani wa ndege, nilichukua nafasi hiyo kuyaangalia mandhari ya kupendeza ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere kupitia ukuta msafi wa vioo vya dirisha pale nilipokuwa nimeketi.

Muda mfupi baadaye ndege yetu ilisimama na kisha milango ya ndege ikafunguliwa na kuturuhusu kushuka. Nilifyatua mkanda wa kiti changu na kusimama kisha nikachukua begi langu dogo la mgongoni kutoka sehemu maalumu ya kuwekea mizigo kwenye sehemu ya juu ya ile ndege halafu nikaunga kwenye foleni ya abiria ili kushuka.

Tuliposhuka tukalikuta basi moja maalumu la pale kiwanja cha ndege likitusubiri, tuliingia kwenye lile basi, likatupeleka hadi kwenye jengo la kituo nambari tatu (terminal 3). Hewa ya joto ilikuwa ishara tosha kuwa tayari nilikuwa nimeikanyaga ardhi ya Jiji la Dar es Salaam, jiji nililoliacha miezi tisa iliyokuwa imepita.

“Ni bahati iliyoje kurudi tena kwenye nchi yangu baada ya miezi mingi ya kuwa nje ya nchi,” nilijiambia nafsini mwangu huku nikiketi vizuri kwenye kiti changu ndani ya lile basi maalumu la pale kiwanja cha ndege.

Nilikuwa nimetinga suti nyeusi ya bei kubwa aina ya Dunhill na shati maridadi la rangi ya samawati aina ya Levi’s, tai yenye rangi za bendera ya taifa shingoni na miguuni nilivaa viatu vya bei kubwa vyeusi vya ngozi halisi.

Lile basi maalumu lilitufikisha mbele ya lile jengo la kituo namba tatu na hapo tukashuka na kuingia ndani ya lile jengo tukipita katika lango kubwa lenye maandishi makubwa ya ‘International Arrivals’. Niliwatangulia abiria wenzangu nikipenya haraka na kulifikia dirisha moja la ofisi za uhamiaji zilizokuwa pale kiwanjani kisha nikapenyeza hati yangu ya kusafiria kwenye dirisha dogo la kioo la chumba kidogo kilichokuwa kimemhifadhi mwanadada mmoja mrembo mwenye sura ya uchangamfu.

Mwanadada yule, ofisa uhamiaji, aliipokea hati yangu ya kusafiria huku akinipa pole ya uchovu wa safari na kuachia tabasamu maridhawa la makaribisho. Kisha mambo yote yakafanywa haraka haraka kwani yule ofisa uhamiaji alimaliza haraka kuingiza taarifa zangu kwenye tarakilishi yake kisha akagonga mhuri kwenye hati yangu ya kusafiria na kuniruhusu kuingia rasmi nchini kwangu.

Bila kupoteza muda niliipokea hati yangu ya kusafiria na kuitia mfukoni kisha nikaanza kuzitupa hatua zangu kwa utulivu kuliacha eneo lile na kuelekea sehemu ya kuchukulia mizigo mikubwa. Hapo nililikuta begi langu kubwa jeusi la magurudumu na kulichukua kisha nikaanza kuliburuta nikielekea nje ya lile jengo huku macho yangu yakiwa makini kuangaza huku na kule nikiwatafuta watu waliofika pale kiwanja cha ndege kunipokea.

Sikuchelewa kumwona mwanadada Pamela Mkosamali akiwa amesimama sehemu ya wazi huku akiwa makini kumtazama kila abiria aliyekuwa anatoka ndani ya lile jengo. Aliponiona tu akaachia tabasamu la makaribisho na kunikimbilia kisha akanikumbatia kwa nguvu, macho yake yakaanza kulengwalengwa na machozi.

Pamela alishindwa kujizuia, alilia kimya kimya akiwa amenikumbatia kwa nguvu kisha aliniachia, akafuta machozi na kuniambia, “Karibu tena Tanzania, mpiganaji.”

“Ahsante sana, Pam,” niliitikia kwa furaha kisha nikaongeza, “Vipi hapa Dar, kazi zinaendeleaje?”

“Hapa mambo ni kama ulivyotuacha,” Pamela alisema huku akinitazama usoni kwa namna ya kunikagua kama mama amtazamaye mwanawe wa pekee aliyepoteana naye kwa muda mrefu.

DGIS kanituma nije kukupokea. Hakika, Jason, umekuwa mtu muhimu sana kwenye taifa hili, umeyafikia malengo yako na ya Idara zaidi ya vile nilivyotarajia, ndiyo maana sioni aibu kujisifia kuwa nilikuwa sahihi kulipendekeza jina lako idarani. Nina imani kwamba utakuwa hodari sana kwenye kazi yako mpya,” Pamela alisema baada ya kitambo fulani.

Kisha alinisaidia begi kubwa hadi nje ya lile jengo, tukaelekea kwenye viunga vya maegesho ya magari pale kiwanjani na safari yetu ikaishia kwenye gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i jeusi lenye vioo vyeusi visivyomruhusu mtu kuona ndani.

Pamela alifungua mlango wa nyuma ya gari hilo, akaweka mizigo yangu vizuri wakati huo mimi nikifungua mlango wa mbele wa gari na kuingia. Kisha Pamela alikuja kuingia mbele, upande wa dereva, akawasha injini ya gari na taratibu gari likaanza kuondoka kutoka eneo lile la maegesho ya magari pale kiwanja cha ndege na safari ya kuelekea mjini ikaanza.

Wakati gari likikata kona na kuingia Barabara ya Nyerere nikageuza shingo yangu kuyatazama mandhari ya kupendeza ya Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Muda huo kulikuwa na magari mengi barabarani hususan daladala, hata hivyo Pamela alikuwa makini zaidi kwenye usukani, na wakati gari letu likizidi kusonga mbele katika barabara ile ya Nyerere nilikuwa nikiitazama mitaa ya Jiji la Dar es Salaam huku kichwani nikikumbuka yale maneno niliyojiambia siku naondoka kwenda mafunzoni nchini Misri kuwa, “siku nyingine ningeipita tena mitaa ile nikiwa mtu tofauti kabisa. Ofisa Usalama wa Taifa mwenye mbinu maalumu (Specialized Skills Officer).”

Niliona vitu vikipita mbele ya macho yangu kwa kasi wakati gari letu likiwa linakwenda, njia nzima kutoka Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere nilikuwa nina shauku ya kukutana na wakuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) jambo ambalo lilinifanya nitamani tupae ili tufike haraka kule ofisi za makao makuu ya idara eneo la Oysterbay kabla sijapelekwa kwenye makazi yaliyoandaliwa kwa ajili yangu kupumzika.

Kichwani kwangu nilikuwa na maswali mengi sana nikifikiria kuhusu majukumu yangu mapya ndani ya Idara. Nilivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu kisha nikaegemeza kichwa changu kwenye siti na kufumba macho.

“Vipi, ulijisikiaje bada ya kugundua yale mateso makali uliyokuwa ukipewa ilikuwa sehemu ya kupimwa?” Pamela aliniuliza pasipo kunitazama.

“Daah, we acha tu, nilifikia hatua ya kusema kama kazi ya ujasusi ndo hivi bora niachane nayo…” niliongea kwa utulivu baada ya Pamela kuyarudisha tena mawazo yangu mle ndani ya gari.

Endelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

227

Kisha nikaanza kumhadithia juu ya mambo yaliyojili tangu Leyla alivyonichukua kwenda matembezi hadi mikasa yote namna nilivyoteswa. Nilipomaliza kumsimulia Pamela alinitazama kama vile alikuwa anaona kiumbe cha ajabu kutoka sayari ya mbali, ni dhahiri alionekana kuogopa sana misukosuko ile.

“Dah! Pole sana, Jason,” Pamela alisema na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Nishapoa,” nilimjibu huku nikiminya midomo yangu. Wakati gari letu lilikuwa linaingia Barabara ya Ali Hassan Mwinyi kutoka Barabara ya Bibi Titi Mohammed, eneo la Posta jirani na Hoteli ya Serena.

* * *



Saa 7:45 mchana…

Saa nane kasorobo ilinikuta nikiwa ndani ya ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (Director General of Intelligence and Security - DGIS), Rajabu Kaunda, katika makao makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa eneo la Oysterbay.

Mkurugenzi Mkuu wa Idara, mzee Kaunda, alikuwa ameketi kwa utulivu kwenye kiti chake kikubwa cha kiofisi cha ngozi halisi kinachozunguka na chenye magurudumu madogo, nyuma ya meza yake kubwa ya ofisini mwisho wa ofisi ile upande wa kulia.

Alikuwa mwanamume mtu mzima wa umri wa miaka 58, kichwa chake kilianza kujaa mvi na alikuwa na ndevu nyingi nyeupe zilizokizunguka kidevu chake. Alikuwa mrefu kiasi na alivaa suti nzuri ya kijivu ya pande tatu brand ya Piacenza kutoka Italia na miwani mikubwa ya macho. Muda huo alikuwa kimya akipitia taarifa maalumu kuhusu mafunzo yangu kwenye faili lenye rangi nyekundu.

Taarifa zile zilionekana kumfurahisha sana Mkurugenzi Mkuu wa Idara. Akaniambia, “Sizya, nimeona si vibaya nikiongea nawe moja kwa moja ili uweze kuona umuhimu wa jambo lenyewe.”

Kisha alinyamaza kidogo kuruhusu mate yapite kohoni mwake halafu akaendelea. “Kwanza nikupongeze sana kwa matokeo mazuri uliyoyapata huko chuoni. Nilijua tu ungefanya vizuri sana kwenye mafunzo yako, na kwa kweli hukutuangusha, umeiwakilisha vyema Idara… Nakupongeza sana.”

Kwa kweli maneno ya Mkurugenzi Mkuu wa Idara yalinitia moyo mno. Kwa unyenyekevu mkubwa mno nilimshukuru kwa kuniamini kiasi hicho, na kumweleza kuwa nilifanya kile nilichoweza tu kwa kadri Mungu alivyoniongoza.

“Sasa, ninakujulisha kwamba kuanzia kesho utaanza kuwajibika kwa uongozi wa Taasisi ya SPACE, na kupokea maagizo huko kupitia channel husika. Mkuu wako wa kazi utamfahamu utakapokwenda kuripoti na maelezo ya namna ya mfumo wa utendaji utafahamishwa utakapokutana na kiongozi wako. Mpaka hapo umenielewa?” Mkurugenzi Mkuu wa Idara aliniuliza huku akinitazama moja kwa moja usoni.

“Nimekuelewa mkuu, na nashukuru sana kwa kuniamini,” nilimjibu huku moyo wangu ukinidunda kwa kasi kutokana na mchanganyiko wa furaha, na wasiwasi wa uzito wa mzigo niliokuwa naenda kutwishwa.

“Ofisi za SPACE zipo Mtaa wa Kimweri, Plot Namba 26 nyumba namba B-22. Hapo utakutana pia na maofisa wengine wa taaluma yako utakaoshirikiana nao katika kazi. Ukifika hapo kiongozi wako atakupatia maelekezo ya awali kabla ya kuanza kazi rasmi.”

Baada ya maelezo hayo Mkurugenzi Mkuu wa Idara akanitakia heri kwa kazi yangu mpya ambayo nilikuwa nakwenda kuianza, kisha akavuta mtoto wa meza na kutoa bahasha ya khaki iliyokuwa na barua ya kunitambulisha kwa mkuu wa Taasisi ya SPACE, akanyoosha mkono wake kunipa huku akinitakia heri.

“Sasa nenda kapumzike hadi hiyo kesho, Pamela atakupeleka kwenye makazi yako yaliyoandaliwa huko Upanga,” Mkurugenzi Mkuu wa Idara aliniambia wakati akiniaga. Na hapo nikawa wa kwanza kusimama muda mfupi kabla Mkurugenzi Mkuu wa Idara kufanya hivyo na hapo nikafunga mguu wangu na kupiga saluti ya heshima mbele ya kiongozi yule mkuu, akaitikia vyema salamu yangu na kunipa mkono wa kuagana.

Nilitoka nje ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa Idara nikaeleka kwenye viunga vya maegesho ya magari pale makao makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa, na hapo nikamkuta Pamela akiwa amejiegemeza kwenye kiti chake akisikiliza muziki wa Bongo Fleva toka kwenye redio ndogo ya gari. Bila kusubiri niliufungua mlango wa mbele wa sehemu ya abiria kando ya dereva na kuingia ndani.

Kabla hajaondoa gari lake Pamela alipiga simu na ilipopokewa na mtu wa upande wa pili akaongea, “Jiandae tunakuja.” Kisha akakata simu na kuliondoa gari lake tayari kwa safari ya kunipeleka Upanga nikapumzike.

“Ulikuwa unaongea na nani?” nilimuuliza Pamela kwa shauku ya kutaka kujua.

“Mtumishi ambaye siku zote amekuwa na jukumu la kukutunzia nyumba na kuifanyia usafi,” Pamela alinijibu pasipo kunitazama, macho yake yakiwa makini barabarani.

Okay!” nilijibu kisha nikajiegemeza kwenye kiti changu.

Gari lilichukua uelekeo wa Posta tukiifuata Barabara ya Ali Hassan Mwinyi. Wakati Pamela akiendesha gari alikuwa akinitazama kwa jicho la wizi. Sikujua kwa nini lakini sikutaka kumnyima nafasi ya kunitazama na hivyo nikawa nazuga kutazama baharini, wakati huo tulikuwa tunalikaribia daraja la Salenda.

Hata hivyo wakati wote tukiendelea na safari akili yangu ilikuwa inaendelea kusumbuka katika namna ya kuwaza kuhusu majukumu mapya ambayo ningepangiwa. Pia nilimfikiria sana mke wangu Rehema na mtoto wetu Junior, ambaye kwa kumbukumbu zangu ilionesha kuwa tayari alikuwa amefikisha miezi kumi na moja, na huenda alikuwa ameshaanza kutembea.

Gari lilipofika kwenye taa za kuongozea magari za Salenda nikamwona Pamela akiingia kulia kuifuata Barabara ya Umoja wa Mataifa. Na hapo tukaenda mwendo wa kama dakika tano hivi kisha tukaingia kushoto kuufuata Mtaa wa Malik kisha tukavipita Viwanja vya Don Bosco na kwenda kuingia kulia kuufuata Mtaa wa Isevya uliopita nyuma ya viwanja hivyo vya Don Bosco, hadi tulipoukuta Mtaa wa Kibasira.

Na hapo nikamwona Pamela akipunguza mwendo na kisha kusimama mbele ya nyumba moja kubwa na nzuri ya ghorofa moja iliyozungukwa na miti mikubwa ya kivuli. Nyumba ile ilikuwa imezungukwa na ukuta na mbele kulikuwa na geti kubwa jeusi.

Pamela alipiga honi na mara mlango mdogo wa lile geti ukafunguliwa kidogo, na hapo nikamwona mdada mmoja, ambaye kiumri hakuwa amezidi miaka ishirini na tano, akichungulia na kuliona lile gari. Akaachia tabasamu na kulifunga lile geti dogo, kisha akalifungua lile geti kubwa na kumruhusu Pamela kuliingiza gari lake ndani ya uzio wa ile nyumba kisha akaliegesha kwenye eneo maalumu la maegesho, jirani na magari mengine mawili, moja lilikuwa Toyota Crown la rangi nyeusi na la pili…

Nilishtuka kidogo kuliona gari lile, nililitazama kwa muda nikijaribu kutafakari kama ndilo au nilikuwa nimelifananisha. Lilikuwa gari letu aina ya Toyota Lexus RX Hybrid la rangi maruni tulilozawadiwa na baba mkwe siku ya harusi. Gari ambalo tuliwahi kupata nalo ajali wakati tukitoka kwenye fungate Serengeti mara baada ya harusi yetu.

Niligeuza shingo yangu kumtazama Pamela lakini nikamwona Pamela akiwa hanitazami bali alizima injini ya gari lake na kushuka haraka huku akionekana mwenye haraka. Nami nikishuka. Yule mdada aliyetufungulia geti alitusalimia kwa unyenyekevu mkubwa, tukamwitikia salamu yake. Akaendelea na kazi zake pale nje wakati mimi nikishusha mabegi yangu ya safari kisha Pamela akanisaidia haraka haraka begi moja, tukaongozana kuelekea kwenye baraza ya ile nyumba.

Endelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

228

Wakati tukitembea nililitazama tena lile gari na kuthibitisha kuwa lilikuwa lenyewe, nikapanga kumuuliza Pamela tukiingia ndani, na hivyo nikawa natembea kimya huku nikiyatupa macho yangu kuangalia huku na huko kuyatazama mandhari ya kupendeza ya ile nyumba. Ilikuwa na madirisha makubwa ya vioo na baraza kubwa mbele yake iliyopangwa seti moja ya makochi ya sofa. Nje ya nyumba hiyo upande wa kushoto kulikuwa na banda la wazi la kuegeshea magari.

Tulipofika kwenye mlango wa barazani wa kuingilia ndani nililazimika kupigapiga miguu yangu kwenye zulia dogo lililokuwa pale nje mlangoni ili kukung’uta vumbi kwenye viatu vyangu kisha nikavivua na kubaki na soksi miguuni. Muda huo Pamela alikuwa ameshaufungua mlango na kuingiza begi langu kisha akasimama kando ya mlango, akinikaribisha niingie ndani.

Bila kusita niliingia na kujikuta nikitokea kwenye sebule pana yenye samani zote muhimu za kisasa, nilitulia kidogo na kuyatembeza macho yangu kuitazama ile sebule. Nikashangaa sana kuona kuwa tayari Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa imeshaniwekea samani kama zile mle ndani.

Hata hivyo kuna kitu kilinishangaza zaidi, mapazia marefu ya sebuleni yalikuwa yamefunikwa na kupafanya pale sebuleni pawe na kiza na kisha pakawashwa mishumaa. Si hivyo tu bali eneo lote la sebule lilikuwa limepambwa kwa maua mazuri aina ya rose na jasmine yaliyosambaza harufu nzuri mle ndani na taa nzuri zinazowaka na kuzima na kulikuwa na maandishi makubwa yanayowaka waka mbele yangu yaliyoandikwa “WEL COME BACK, HONEY”.

Nikiwa bado nashangaa nikagundua kuwa pia kulikuwa na sauti ya chini ya muziki laini toka kwenye redio kubwa (subwoofer) iliyokuwepo pale sebuleni ilikuwa inasikika! Sikuelewa kabisa maana ya makaribisho yale na hivyo nikageuka kumtazama Pamela huku nikishindwa kuuficha mshangao wangu. Pamela hakuwepo! Nikashangaa sana kujiona nikiwa peke yangu pale sebuleni! Sikujua Pamela alienda wapi.

“Pamela!” niliita kwa sauti ya wasiwasi lakini sikupata jibu.

Niliyazungusha macho yangu kutazama eneo lile lakini hakukuwa na dalili ya Pamela isipokuwa mizigo yang utu. Nikataka nitoke ili nimtazame huko nje lakini kabla sijafanya hivyo nikasikia sauti ya miguu ya mtu aliyekuwa anakuja pale sebuleni akitokea upande wa pili wa ile sebule. Nikageuka haraka kutazama upande huo, na hapo nikajikuta nikipatwa na mshango mkubwa nisiamini nilichokiona.

Nilimwona Rehema akitembea taratibu kwa madaha akitokea kwenye mlango fulani ambao ulikuwa upande wa pili wa sebule, mkononi alikuwa kashika ua zuri na alikuwa amevaa gauni zuri jepesi la rangi ya pinki na fupi lililoishia juu ya magoti yake huku likilichora vyema umbo lake la kuvutia.

Wow!” nilijikuta nikimaka kwa mshangao mkubwa.

“Karibu nyumbani, mpenzi,” Rehema aliniambia kwa sauti laini iliyojaa mahaba huku akinisogelea taratibu kisha akanishika mkono na kuniongoza hadi kwenye ngazi za kuelekea juu, kule kule alikotokea.

Ngazi hizo zilikuwa upande wa pili wa sebule, yaani baada ya mlango wa kwanza kulikuwa na ukumbi (corridor) kisha kabla hujaingia sebuleni unakutana na mlango wa kuingia jikoni, halafu upande wa pili wa ile sebule kulikuwa na ukumbi mwingine ambao tulipoufuata tukatokea kwenye ngazi za kuelekea juu.

Tulizipanda zile ngazi taratibu na kutokea kwenye ukumbi mwingine uliokuwa na milango mitatu ikitazamana. Rehema akaniongoza kwenye mlango mmoja na kuufungua huku akinikaribisha, tukaingia.

Kilikuwa chumba kikubwa chenye maliwato ya ndani, kulikuwa na kitanda kikubwa cha kifahari cha futi sita kwa sita cha samadari kilichokuwa katikati ya chumba. Madirisha makubwa mawili ya vioo vya kuteleza yasukumwapo yalikuwa yamefunikwa kwa mapazia marefu mepesi, huku dirisha moja likiwa limeungana na mlango wa kioo wa kutokea kwenye kibaraza kidogo cha juu ghorofani (balcony).

Mle chumbani pia kulikuwa na kochi moja nadhifu na la kisasa la sofa la kukaa watu wawili likiwa juu ya zulia zuri la manyoya lenye rangi za pundamilia, na mbele ya kochi hilo kulikuwa na meza ndogo ya mbao yenye umbo la nusu duara. Pembeni ya kochi hilo kulikuwa na meza nzuri ya vipodozi (dressing table) yenye kioo kirefu cha kujitazama mwili mzima.

Rehema aliniongoza hadi kwenye lile sofa, nikaketi. Na yeye akaketi kando yangu na kuupandisha mguu wake mmoja juu ya mapaja yangu, muda huo alikuwa akinitazama kwa tabasamu la mahaba. Kisha aliniambia kwa sauti ya chini iliyojaa mahaba, “Karibu sana, mume wangu.”

Nilishindwa kumjibu na badala yake nilibaki nikimtazama kwa mshangao, sikuwa nimetegemea kabisa kumkuta pale na hivyo mapigo ya moyo wangu yalikuwa yanaenda kasi sana. Kisha niliitazama nguo yake nyepesi kabisa isiyokuwa na kitu ndani ikiliruhusu joto lake kupenya katika suruali yangu. Na hapo nikajikuta nikipatwa na msisimuko wa ajabu, lakini sikusema neno lolote. Nilikuwa kama mtu aliyepigwa na shoti ya umeme.

Ni kama alikuwa ameisoma akili yangu tayari. Mara mkono wake laini ukajizungusha katika shingo yangu. Bado nilibaki nikiwa nimetulia tuli. Nikaona ule mkono ukikosa utulivu, ukaanza kutambaa hapa na pale na kunifanya nianze kuhema juu juu.

“Rehema!” kwa mara ya kwanza nilijikuta nikiita kwa sauti ya kukwaruza isiyojiamini hata kidogo.

“Abee!” Rehema aliitika kwa sauti laini ya kimahaba huku mkono wake ukiwa kama uliokuwa ikiyapima mapigo ya moyo wangu jinsi yanavyokwenda kasi. Hali ile ya kupapaswa kifuani ikaongeza kasi ya moyo wangu zaidi. Alikuwa anafanya papaso maridhawa katika kifua changu na kunifanya nizizime huku mikono yangu ikipalangana huku na kule kulifunua gauni lake.

Hisia ndiyo kitu pekee ambacho husababisha mapenzi. Hisia kamwe hazizungumziki kwa njia ya mdomo bali husema kupitia moyo kwa njia ya macho. Mioyo ikizungumza kamwe hakuna cha kuzuia, hata wahusika wasiposema wao kwa wao lakini mioyo yao itasema na hatimaye watajikuta katika majaribu yatakayoangukia kwenye mapenzi ya dhati.

Ni hisia hizi nilizoamini kuwa zilikuwa zinanena katika moyo wa Rehema kisha zikanena pia katika moyo wangu. Hisia ambazo zilituleta katika hali ile kimya kimya. Mioyo yetu ikazungumza ikisema kuwa inahitaji faraja. Na hapo hakukuwa na mtu wa kusema “hapana”. Tungeanzaje kusema hapana iwapo mioyo yetu ilikuwa imesema ndiyo?

Rehema alinivuta karibu zaidi na ndimi zetu zikakutana. Kilichofuata baada ya hapo ilikuwa ni sauti ya pumzi zetu nyepesi sambamba na miguno isiyoeleweka ya mahaba. Na kama mtu aliyepandwa na wazimu wa mapenzi, Rehema alianza kunivua nguo zangu na kuzitupa huko kisha akapeleka mikono yake kifuani kwangu na kuanza kunipapasa kwa pupa. Nilitaka kumzuia lakini alining’ata mkono.

“Usinizuie,” Rehema aliongea kwa hasira kama mwehu huku akiivuta chini boksa yangu kwa pupa. Nikabaki kimya. Mbele ya Rehema nilikuwa kama mbwa mwoga mbele ya chatu mwenye njaa kali.

Rehema aliinuka na kuvua haraka gauni lake na kulitupa kando na hivyo kubaki mtupu huku harufu nzuri ya manukato yake ikinishawishi kuendelea na hatua iliyofuata. Sikuwa na ujasiri tena wa kupingana na hisia zangu, hivyo taratibu niliupeleka mkono wangu na kuanza kuyatomasa makalio yake laini yaliyoshiba minofu.

Muda mfupi uliofuata tulijikuta tukiwa tumemezwa na ulimwengu wa huba. Kwa takriban dakika therathini mchezo huo ukafika tamati huku tukiwa hoi na kila mmoja wetu alionekana kutosheka kwa muda huo.

Endelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

229

Rehema alikuwa wa kwanza kuamka halafu taratibu akajitoa toka pale kitandani na kuelekea bafuni. Alitembea kwa madaha kama twiga anayekatisha barabara ya mbugani huku mtikisiko wa makalio na umbo lake lisilositiriwa na nguo yoyote ukitengeneza taswira nzuri ya kuvutia machoni kwangu.

Nilimtazama kwa hamasa huku nikipendezwa na mjongeo ule hadi pale alipoingia bafuni. Kisha nikawa kama niliyezinduka kutoka usingizini, nikamkumbuka mtoto maana hadi muda huo sikuwa nimemwona na sikujua alikuwepo wapi.

“Rehema, yupo wapi Junior?” nilimtupia swali Rehema mara tu alipotoka bafuni, huku nikimtazama usoni kwa wasiwasi,

“Yupo na Sada,” Rehema alinijibu bila wasiwasi wowote.

“Sada ndiyo na…” nilipotaka kuuliza nikakatishwa na sauti ya mtoto aliyekuwa analia kule sebuleni.

Rehema akaharakisha kuchukua gauni lake, akalivaa halafu akachukua khanga na kujifunga vizuri juu yake, kisha akanitupia jicho na kutoka haraka. Nami niliinuka toka pale kitandani, nikaenda bafuni kujimwagia maji ili kutoa uchovu.

Ilinichukua takriban dakika kumi kujimwagia maji na nilipotoka humo ilikuwa tayari imetimia saa 10:35 jioni. Nilifungua kabati la nguo na kutafuta humo nguo yoyote ya kujistiri, nikapata bukta ya bluu ya kitambaa cha kadeti na fulana nzito ya rangi nyekundu. Nikavaa na kutoka, nikaeleka sebuleni.

Pale sebuleni niliwakuta Rehema na mtoto Junior wakiwa wameketi kwenye masofa wakifuatilia vituko vya vikaragosi vya “Tom and Jerry” kwenye runinga bapa iliyokuwa imetundikwa ukutani. Junior alikuwa amevalishwa kaptula nyekundu na sweta la kijivu.

Junior aliponiona akaachia tabasamu huku akifikicha macho yake kisha akainuka pale kwa furaha akiwa na lengo la kunisalimia. Nilimsogelea na kuinama, akanyoosha mkono wake wa kulia na kunishika kichwa.

“Marhaba! Naona mwanangu umeshakua,” nilisema huku nikimnyanyua juu na kumrushia begani kwangu kisha nikaketi pale kwenye sofa jirani na Rehema.

Muda huo huo Rehema alimwita Sada ambaye bila shaka alikuwa huko jikoni. Baada ya sekunde kadhaa Sada alisimama mbele yetu kwa heshima zote. Nilipata nafasi ya kumtazama vizuri nikagundua kuwa alikuwa binti mrembo, tena chipukizi. Chuchu zake zilikuwa zimechomoza juu ya matiti yake magumu ya mviringo ndani ya nguo alizovaa kiasi cha kuvuta hisia. Nywele zake nene nyeusi na laini hazikuwa na ulazima wa kutia dawa na miguu yake iliyoshiba vizuri pia haikuhitaji mazoezi ya kuijenga.

“Sada, tuletee kinywaji,” Rehema alisema na kunigeukia huku akiangua kicheko hafifu, “Utatuwia radhi, humu ndani hatuweki vinywaji vikali, kuna juisi tu… ya embe, nanasi, parachichi na pasheni, hivyo chaguo ni lako.”

“Poa tu… nikipata ya pasheni pia nitashukuru,” nilijibu huku nami nikicheka.

“Nami niletee hiyo hiyo,” Rehema alimwambia Sada. Na hapo Sada akaondoka haraka kueleka jikoni.

“Huyu binti nimetokea kumpenda sana japo ni miezi mitano tu tangu nianze kukaa naye. Ni mchapakazi kweli. Nafikiria ni nini tutamfanyia pindi ikifika wakati akaondoka,” Rehema aliniambia huku akijiegemeza kwenye sofa.

Sada alirejea na sinia lenye bilauri mbili ndefu za juisi ya pasheni. Alisimama mbele yangu kisha akabonyea chini kidogo. “Karibu, baba.”

Nikachukua bilauri yangu na kisha Sada akamsogelea Rehema na kufanya vile vile. Tulipochukua zile bilauri akatusogezea meza ndogo iliyokuwa jirani na kuondoka.

“Hakika ni kati ya juisi bora kabisa nilizowahi kunywa… si mchezo!” nilishindwa kujizuia kuisifia juisi ile baada ya kupiga funda moja.

“Katengeneza mwenyewe,” Rehema alidakia kwa shauku kutokana na pongezi ile.

Nikapiga tena funda jingine na kuiweka ile bilauri mezani taratibu kama vile niliogopa kuvunja bilauri au kumwaga kilichokuwemo ndani yake.

“Safi sana, kwani umemtoa wapi?” nilimuuliza Rehema kwa shauku.

“Nililetewa na Idara mara tu tulipohamia hapa toka Kahama… kwa kweli anajua kujituma sana,” Rehema alisema huku akigeuza shingo yake kumtazama Sada aliyekuwa akikatiza.

“Walimpeleka kozi nini?” niliuliza kwa utani.

“Yeah, ni zao la VETA hilo. Amesomea mapishi na utumishi,” Rehema alijibu huku akitabasamu. Kisha akaichukua remote na kutafuta kituo cha televisheni kilichoonesha mpira. Kulikuwa na mechi kati ya Chelsea na Manchester City. Ilikuwa mechi iliyooneshwa mbashara.

Hadi muda huo Chelsea walikuwa wanaongoza kwa bao mbili kwa sifuri. Nilitaka kusema kitu kuhusu mechi ile lakini nikasita na kupuuzia. Sikuwa mpenzi sana wa soka lakini nilivutiwa sana na ile mechi. Kila nilichokiona pale uwanjani kilinivutia. Kuanzia wingi wa mashabiki na mori waliyokuwa nao juu ya timu zao.

Hakuna sehemu katika jukwaa iliyoonekana kuwa na pengo. Nyasi safi zilizokolea ukijani na madoido kedekede pamoja na matangazo lukuki ya wadhamini. Wachezaji nao walijituma vilivyo wasiwavunje moyo mashabiki wao waliowaunga mkono.

Na hapo ndo nilipoiona tofauti kubwa mno kati ya soka la Ulaya na soka la nyumbani Afrika. Mapengo yalionekana wazi kwenye majukwaa pindi timu zichezapo, nyasi zilipauka na viwanja kukosa mvuto wa kuutazama. Wachezaji nao walikosa mori katika mchezo wenyewe na hivyo walicheza bora liende kusukuma siku.

“Nashukuru sana, Sada. Juisi ni tamu sana,” nilimwambia Sada wakati alipokuwa akitoa vyombo na kisha akafuta meza.

"Asante kushukuru," Sada alisema huku akionekana mwenye aibu nyingi. Muda huo ilishatimu saa moja kamili usiku, kwa mujibu wa saa iliyokuwa ukutani. Rehema alibadili chaneli na kuweka taarifa ya habari kutoka moja ya vituo vya nchini.

“Kwa hiyo, Rehema…” nilianzisha tena maongezi baada ya kukumbuka jambo. “Kipindi chote hiki umekuwa mtu wa kukaa nyumbani tu au kuna kazi unafanya?”

“Kwa sasa nipo NSSF, makao makuu ya NHIF pale jengo la Benjamin Mkapa, Posta…” Rehema aliniambia kisha akaongeza, “nipo hapo kama meneja wa mipango na utawala.”

“Kwa vyovyote Idara ndo itakuwa imekupenyeza pale kama ofisa kipenyo, sivyo?” nilimuuliza huku nikitabasamu.

“Umeanza mambo yako,” Rehema alisema huku akicheka. Kisha akaongeza, "Achana na hayo, wewe subiri tu ya kwako." Nami nikacheka.

“Umeanza kazi lini?” nilimuuliza huku nikiachana na kile nilichomuuliza mwanzo.

“Nina miezi mitano sasa,” Rehema alisema huku akimchukua Junior aliyekuwa amesinzia mikononi kwangu, akaenda kumlaza.

Aliporudi na kuketi akataka kujua machache kuhusu mafunzo yangu kule chuoni Zawyet Sidi Abd el-Ati, nilimsimulia kwa kifupi na jinsi nilivyokutana na masaibu kule Shamba. Rehema alikuwa kimya kabisa akinisikiliza. Mara tukamwona Sada akianza kuandaa meza kubwa kwa mapochopocho.

Alipomaliza alitualika mezani nasi tukajongea pale mezani. Kulikuwa na wali wa nazi, mchuzi mzito wa kuku ulioungwa kwa nazi pia. Bakuli la maharage yaliyoungwa kwa karanga, bakuli la mboga za majani pembeni na saladi, matunda kwenye sinia na kando yake lilikuwepo jagi la maji baridi na bilauri tatu.

Tulikula kimya kimya kila mmoja akitafakari lake huku chakula kikishuka vilivyo kutokana na ustadi wa mapishi. Tulipomaliza kula tukashushia na matunda, kisha maji. Kwa kweli Rehema hakukosea kumsifia Sada kwani alikuwa na utaalamu wa hali ya juu wa huduma za nyumbani.

* * *

Tukutane siku nyingine, usichoke, endelea kuifuatilia simulizi hii ya kusisimua...
 
Uyu jasoni simpendi ni muhuni mtu unaenda kwa mkeo unalala na mwanamke same day unaenda kulala na mkeo mchafu mchafuzi mchafukoge ndo mana walimpa za chembe kule ughaibuni mfyuuuu
 
Back
Top Bottom