Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Uyu jasoni simpendi ni muhuni mtu unaenda kwa mkeo unalala na mwanamke same day unaenda kulala na mkeo mchafu mchafuzi mchafukoge ndo mana walimpa za chembe kule ughaibuni mfyuuuu
[emoji23][emoji23]...
 
Uyu jasoni simpendi ni muhuni mtu unaenda kwa mkeo unalala na mwanamke same day unaenda kulala na mkeo mchafu mchafuzi mchafukoge ndo mana walimpa za chembe kule ughaibuni mfyuuuu
NA HUYO BEKI TATU WAKE ATAMLA MDA SI MREFU
.
.
SI KAMA MABAHARIA TUMEPANGA TUMJENGEE SANAMU LAKE MITAA YA IKULU MANA ANAWAKILISHA CHAMA VIZURI
 
NA HUYO BEKI TATU WAKE ATAMLA MDA SI MREFU
.
.
SI KAMA MABAHARIA TUMEPANGA TUMJENGEE SANAMU LAKE MITAA YA IKULU MANA ANAWAKILISHA CHAMA VIZURI
Na kweli kabisa ana hulka mbaya na kuna tetesi ameukwaa tayari
 
NA HUYO BEKI TATU WAKE ATAMLA MDA SI MREFU
.
.
SI KAMA MABAHARIA TUMEPANGA TUMJENGEE SANAMU LAKE MITAA YA IKULU MANA ANAWAKILISHA CHAMA VIZURI
Haha[emoji23][emoji23][emoji23]... Dah, nimecheka sana...
 
ufukweni mombasa.JPG

230

Vitengo…




Saa 1:25 asubuhi…

NILIKUWA nafahamu nini maana ya kuzingatia muda, hivyo hadi inatimu saa moja na robo asubuhi nilikuwa ndani ya gari langu aina ya Toyota Lexus RX Hybrid la rangi maruni nikielekea zilipo ofisi za SPACE. Muda huo nilikuwa nimefika eneo la Oysterbay nikiiacha Barabara ya Ali Hassan Mwinyi na kuingia kulia kuifuata barabara ndogo iliyoniingiza Mtaa wa Bongoyo.

Asubuhi hiyo nilikuwa nimevaa suti maridadi nyeusi, shati zuri la mikono mirefu la rangi ya samawati, tai ya bluu shingoni, viatu vyeusi vya ngozi halisi ya mamba, na nilijipulizia manukato ghali aina ya Dolce & Gabbana. Na nilikuwa na mkoba wangu wa kiofisi aina ya Pad & Quill.

Nikiwa kwenye ule mtaa wa Bongoyo nikaanza kupunguza mwendo wakati nilipokuwa nikiutafuta mtaa wa Kimweri na nilipouona nikaingia huku nikiyakaza macho yangu kuzisoma vizuri namba za nyumba kwenye mtaa ule. Sikukawia kuiona nyumba iliyopo kwenye Plot Namba 26 nyumba namba B-22 ambapo ndipo zilipokuwa ofisi za SPACE.

Ilikuwa nyumba kubwa na nzuri kama zilivyokuwa nyumba zote za eneo lile la Oysterbay zilizokuwa zikimilikwa na serikali, na wengi wa wakazi wake walikuwa watumishi wa ngazi za juu serikalini, wakurugenzi wa mashirika ya umma, au viongozi wastaafu.

Nilikuwa nimeambiwa kuwa Idara ya Usalama wa Taifa ilikuwa ikimiliki nyumba kadhaa maeneo hayo na ilizitumia nyumba hizo kama ofisi, makazi ya maofisa wake au nyumba salama za kificho (safe house) kwa ajili ya kazi maalumu. Lango kuu la kuingilia kwenye jengo la ofisi za SPACE lilikuwa limefungwa.

Nililisogeza gari langu hadi mbele ya lango kuu la ofisi za SPACE. Na hapo nikapiga honi mara moja tu, ofisa mmoja wa ulinzi akajitokeza, alikuwa na mwili uliojengeka vyema na mkononi alishikilia bunduki aina ya SMG. Nikashusha kioo changu na kuchungulia nje ili anione.

Alinitazama usoni kwa umakini katika namna ya kunikagua lakini hakuonesha kunifahamu, hivyo akataka nijitambulishe kabla ya kuingia. Nikajitambulisha nikimweleza kwa kifupi mimi ni nani, na kwa nini nilikuwa pale. Baada ya maelezo hayo nikamwonesha ile barua ya utambulisho niliyopewa na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Bila kusema neno ofisa yule aliiangalia ile barua kwa makini halafu kama kwamba ambaye hakuwa ameridhika na alichokisoma, akatoa simu ya mkononi toka mfukoni mwake na kupiga namba fulani. Upande wa pili ulipopokea tu, akataja jina langu na kuuliza kama nilikuwa naruhusiwa kuingia mahala hapo. Baada ya kupokea maelezo mafupi, alikata simu na kufungua lango huku akinielekeza mahali nilipotakiwa kwenda kuliegesha gari langu kisha nichukue kibali cha kuniruhusu kuingia ndani ya jengo lile (gate pass).

Niliingiza gari langu na kwenda kuliegesha mahali nilipokuwa nimeelekezwa ndani ya uzio wa lile jumba. Niliposhuka nikaanza kuzitupa hatua zangu kikakamavu nikiwapita maofisa wengine wawili wa ulinzi waliokuwepo eneo lile wakiwa wamebeba bastola kwenye mifuko (hoster) zilizofungwa mapajani mwao.

Niliwasalimia na kwenda moja kwa moja kwenye dirisha lililokuwa umbali wa mita kumi hivi kutoka nilipokuwa nimeegesha gari langu, hapo nikamkuta ofisa mmoja aliyekuwa ndani ya chumba cha walinzi akiikodolea macho CCTV monitor iliyokuwa mbele yake. Nikajitambulisha jina langu na baada ya takriban sekunde therathini nikapewa kitambulisho chenye utepe wa kuvaa shingoni.

“Ahsante sana,” nilimwambia yule ofisa wa ulinzi kisha nikaufuata uelekeo niliooneshwa na kujikuta nikitokea katika eneo la mapokezi. Hapo nikaiendea meza ya mama mmoja niliyemkuta hapo, ambaye kwa mwonekano alionekana kuwa na umri wa miaka kati ya 40 na 45. Nikamsalimia kwa heshima na kisha nikajitambulisha.

Mama huyo alinyanyua simu iliyokuwepo pale juu ya meza yake na kupiga, kisha akaongea na mtu wa upande wa pili akimfahamisha kwamba nilikwisha fika pale mapokezi. Alipokata simu akasema, “Karibu sana, boss amesema msubiri anakuja kukuchukua sasa hivi.”

“Sawa,” nilimjibu huku nikianza kukiendea kiti kilichokuwa karibu ili nikae lakini nikasita baada ya kumwona mdada mmoja mrefu akinijia haraka haraka huku akiwa makini sana akinitazama.

Alikuwa mdada ambaye hakuwa amezidi miaka therathini, alikuwa mrefu na maji ya kunde na mwenye umbo matata sana lenye kuweza kuitaabisha vibaya nafsi ya mwanaume yeyote. Nywele zake zilikuwa fupi na laini na alikuwa na sura ya duara yenye macho legevu na pua ndefu, na midomo yake ilikuwa na kingo pana kiasi zilizopakwa rangi nzuri ya pink.

Nilipomchunguza zaidi nikagundua kuwa alikuwa na vishimo vidogo mashavuni mwake, na asubuhi ile alikuwa amevaa suti nzuri ya rangi ya pink na viatu vya rangi ya pink vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio.

“Naamini wewe ndiye Jason Sizya?” mdada yule aliniuliza huku akinitazama usoni.

“Ndiyo,” nilijibu kwa sauti tulivu huku nami nikimtazama usoni kwa shauku ya kutaka kusikia alitaka kuniambia nini.

“Naitwa Tunu Michael, mimi ndiye Mkuu wa Taasisi ya SPACE,” yule mdadada alijitambulisha kwangu huku akinyoosha mkono wake kunipa.

Kwanza ilinibidi nimpigie saluti mdada huyo baada ya kutambua kuwa alikuwa ndiye mkuu wangu wa kazi. Kisha nikanyoosha mkono wangu kukutanisha na wa kwake. Tukasalimiana. Kisha akaniongoza kuelekea ofisini kwake.

Tulikatisha kwenye ukumbi mpana hadi tulipoufikia mlango mmoja, Tunu akaufungua na hapo tukajikuta tukitokea kwenye chumba cha katibu muhtasi wake, mwanamama mrefu na mwenye umbo kubwa lakini lililokuwa linavutia, likiwa limesheheni vyema na kunesanesa. Kwa mwonekano tu alionekana kuwa na umri usiopungua miaka 40. Alikuwa mweupe, weupe wake si ule wa kujichubua bali wa asili.

Mwanamama huyo alikuwa ameelekeza macho yake kwenye tarakilishi akiwa amehemewa na kazi za kiofisi. Kuingia kwetu kukamfanya ainue uso wake kututazama, macho yetu yakakutana na kumfanya aachie tabasamu la bashasha la makaribisho. Tunu akatoa utambulisho mfupi na kunifanya nilijue jina lake, aliitwa Salha Mwapachu.

Tulisalimiana kwa bashasha zote kisha Tunu alinikaribisha ofisini kwake, nikaufuata mlango wa ofisi yake na kuingia, na hapo nikajikuta nikiwa ndani ya ofisi moja pana na yenye mazingira nadhifu mno, nilivutiwa na mpangilio wa samani za kisasa zilizokuwemo mle ndani, na ilikuwa na zulia jekundu sakafuni na meza ndefu ya ofisini yenye viti kumi na viwili, viti sita upande wa kushoto na viti vingine sita upande wa kulia.

Nyuma ya ile meza ndefu ya ofisini, mwisho wa ofisi ile upande wa kulia kulikuwa na kiti kikubwa cha kiofisi cha ngozi halisi kinachozunguka na chenye magurudumu madogo, na pembeni kulikuwa na kochi la wastani la sofa la kukaliwa na watu wawili.

Juu ya ile meza ya ofisini kulikuwa na tarakilishi mpakato (laptop) ya kisasa aina ya Apple Air ya inchi 13.3 na kando ya ile tarakilishi kulikuwa na printa aina ya Epson L805, vitabu na majarida kadhaa, kidau cha wino, mhuri na kichupa kidogo chenye wino mweupe wa kufutia maandishi. Pia kulikuwa na simu ya mezani.

Kwa mtazamo wa haraka haraka tu niliweza kugundua kuwa nilikuwa nimeingia kwenye ofisi ambayo hapakuwa na mazingira ya kuleta mzaha kama vile ilivyokuwa kawaida ya ofisi nyingi za idara za serikali. Tunu alinikaribisha kwenye lile kochi la sofa huku yeye akiketi kwenye kiti chake kikubwa cha kiofisi cha kuzunguka na chenye magurudumu madogo, nami nikaketi pale kwenye sofa baada ya kumkabidhi ile barua niliyopewa na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, mzee Rajabu Kaunda.

Endelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

231

Aliipokea na kuipitia haraka haraka kisha akaiweka kwenye faili moja la rangi nyekundu huku akiniambia kuwa muda wa kuanza kikao maalumu ulikuwa umefika kwani kikao hicho kilitakiwa kuanza katika muda usiozidi dakika tano kuanzia muda ule.

Kikao hicho kilikuwa cha kupashana taarifa za kiitelejensia (Situation Report - SITREP) kuhusu ya hali ya ulinzi na usalama nchini, na kupanga mikakati ya kukamilisha malengo ya kazi zilizokuwa zikitukabili. Wakati Tunu akinieleza hayo mlango wa ofisi yake ukagongwa na kisha ukafunguliwa na kusukumwa kwa ndani, wakaingia maofisa kumi, wanawake wanne na wanaume sita.

Tulisalimiana kwa bashasha na kisha kila mmoja akaketi kwenye kiti tayari kwa kusubiri kikao maalumu cha kupashana taarifa za kiitelejensia. Hata hivyo kabla ya kikao hicho Tunu alitoa utambulisho kwa pande zote mbili. Baada ya utambulisho wale maofisa walioneshwa kufurahishwa sana na ujio wangu kwenye ile taasisi.

Kwa haraka haraka niliweza kuwakariri baadhi ya maofisa hasa wale walionivutia zaidi akiwemo Ofisa mwandamizi Nuru Kabwe, Ofisa mwandamizi Jonas Marwa, Ofisa mwandamizi Gloria Tesha, Ofisa mwandamizi Juma Ndekule, na maofisa Venance Masele, Philip Bundala na Hawa Kiluvya.

Katika kikao hicho mzungumzaji mkuu alikuwa kiongozi wetu, Tunu Michael, ambaye kutokana na wadhifa wake na kwa mujibu wa chain of command ndiye aliyekuwa akipokea maagizo kutoka makao makuu kupitia channel husika, kutupa maelekezo na kusimamia utekelezaji.

Kwa kuwa kilikuwa kikao changu cha kwanza kabisa nikiwa Ofisa Usalama wa Taifa, muda mwingi nilikuwa msikilizaji wakati Tunu alipokuwa akitoa maagizo ya jumla na kisha kutoa nafasi ya kujadili agizo moja moja na hata kuuliza maswali kwa mambo yaliyokuwa hayaeleweki vyema. Binafsi nilijikuta nikivutiwa sana na vikao vya aina hii, kwani niliamini vilisaidia sana kujua matukio yaliyokuwa yakiendelea duniani hususan kiuchumi, kisiasa, na kijamii.

Pamoja na hilo, vikao hivi pia vilisaidia kujifunza mbinu mpya za kukabiliana na changamoto za kazi ya uofisa usalama. Kikao kile kilichukua muda wa saa nzima. Na tulipokuwa mbioni kumaliza kikao Tunu alimkabidhi kila mmoja, isipokuwa mimi tu, hati za maagizo ya kazi aliyotakiwa kuishughulikia kama alivyokuwa ameelekeza.

Hati hizo zilikuwa zikiitwa ‘Simu’ na zilikuwa zikiletwa kwa mfuko maalumu (private bag) kutoka makao makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa, na au kupokelewa kwa vyombo vya kijasusi zikiwa zimefungwa katika mafumbo (codes). Kama nilivyosema, mimi peke yangu sikupewa hati ya maagizo ya kazi kwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Rajabu Kaunda alikuwa ameagiza nipewe mapumziko ya mwezi mmoja kabla sijaanza rasmi kazi zangu.

Kisha tulimalizia SITREP kwa kuzungumzia mambo tuliyopaswa kuishauri serikali hususan hatua za kuchukua kupambana na ufisadi uliokuwa umeshamiri serikalini. Wakati tukiinuka ili watu wakaendelee na majukumu waliyopewa, Tunu akatutaka mimi, Nuru Kabwe, Jonas Marwa na Venance Masele kubaki ofisini kwake kwa dakika chache.

Wenzetu walipotoka, Tunu akatuambia kuwa alikuwa ametuteua rasmi kuwa kwenye kitengo maalumu ambayo ingeshughulikia jumbe mbalimbali zilizokuwa zikitumwa kwenye mitandao, akiamini kuwa kwa taaluma zetu tulikuwa na uwezo mkubwa wa kujua kama ujumbe fulani ni ‘serious and sensitive’ ama sivyo. Na kwamba ni sisi tu tuliopaswa kushughulikia jambo hilo kwani lilikuwa limeshaingia katika utaratibu wa usiri (compatimentation).

Tulielezwa kuwa endapo mtu yeyote angechapisha au kutuma chochote kwenye mtandao ambacho tungekiona ni hatarishi kwa usalama wa taifa basi mara moja kila taarifa kuhusu mtu huyo zingeanza kuchunguzwa kwa kuwahoji watu wake wa karibu, majirani, wafanyakazi wenziwe, hata walimu waliowahi kumfundisha na baada ya hapo hatua sahihi zingefuata iwapo mtu huyo apewe onyo, achukuliwe kwa mahojiano zaidi au ahukumiwe kwa kosa hilo.

Na hapo ndipo nilipogundua kuwa takriban asilimia kubwa ya wafanyakazi wa Taasisi ya SPACE walikuwa wabobezi wa masuala ya teknolojia ya habari na mawasiliano (ICT). Hata mkuu wetu Tunu Michael, mbali ya urembo aliokuwa nao, alikuwa amebobea mno kwenye masuala ya teknolojia ya habari na mawasiliano kiasi cha kucheza na tarakilishi kwa kadri alivyotaka.

Na hapo ndo nilipogundua kwa nini Tunu aliteuliwa kuwa mkuu wa Taasisi ya SPACE. Alikuwa na Shahada ya Kwanza katika Computer System Analysis aliyoipata nchini Marekani katika Taasisi ya Teknolojia ya Georgia (Georgia Tech) baada ya kusoma kwa miaka minne.

Aliporudi nchini alichaguliwa kujiunga na programu maalumu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kwa ajili ya vijana wasomi walioandaliwa kwenda kuchukua mafunzo ya awali ya ujasusi. Baada ya kumaliza mafunzo ya kijeshi Tunu alilitumikia jeshi kwa muda mfupi na kituo chake kilikuwa kikosi namba tisini na mbili (92KJ) Ngerengere.

Akiwa Ngerengere alipata pia mafunzo maalumu ya silaha (Special Forces and Tactical Weapons Training) na baadaye akapelekwa nchini Israel katika taasisi ya IDC Herzliya (ICT International Institute for Counter-Terrorism) ambako alihitimu Shahada ya Umahiri ya Ujasusi ikihusisha pia masuala ya usalama wa ndani na mapambano dhidi ya ugaidi, na teknonojia ya habari na mawasiliano.

Akiwa huko huko Israel pia alihitimu kwa kiwango cha juu sana mafunzo ya kujihami katika michezo ya karate and judo. Aliporejea nchini alianza kazi katika Idara ya Usalama wa Taifa na muda mfupi tu tangu alipojiunga idarani hapo alionesha uwezo mkubwa sana kiasi cha kuaminiwa na kupewa nafasi mbalimbali za kufanya kazi ndani na nje ya nchi, huku akipenyezwa kwenye idara mbalimbali za serikali na hata kwenye sekta binafsi.

Tunu alikuwa anaheshimika mno kwa uwezo wake mkubwa wa kusimamia operesheni, kuhamasisha maofisa walio chini yake kufanya kazi kwa bidii na weledi, na kutoa ushauri bora kwa viongozi wa juu. Sifa hizo pamoja na nyingine nyingi ndizo zilizofanya akabidhiwe dhamana ya kusimamia taasisi nyeti ya SPACE iliyokuwa ngumu kuliko zote nchini.

Kama ungekutana naye mitaani bila shaka usingeamini kuwa mwadada mrembo uliyekuwa ukimwona alikuwa mmoja wa watu muhimu mno katika Idara ya Usalama wa Taifa. Sura yake nzuri iliyoambatana na umbo lake la kuvutia, akiwa na urefu wake wa futi tano inchi kumi, iliwafanya wanaume wengi kumwona kama mmoja wa wanamitindo maarufu, au kama si hivyo basi alikuwa mtoto wa kigogo serikalini, au mwanaume wake alikuwa ni mtu mwenye fedha!

Tunu alizitumia vyema sifa hizi katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku, akiiwakilisha vyema Idara ya Usalama wa Taifa kila mahali alipokwenda na kuibua uozo.

Mojawapo ya operesheni ngumu alizowahi kuzifanya na zikampatia sifa kubwa ni ile operesheni iliyokuja kuandikiwa hadithi ya “Taxi” pale alipopambana sana kuhakikisha kuwa kundi hatari lililokuwa limekusanya wafanyabiashara wakubwa, wanasiasa, vigogo wa polisi na maofisa usalama, likiongozwa na mfanyabiashara na mwanasiasa maarufu Hassan Oduya, linaibuliwa na uozo wao wote unafahamika.

Kundi hilo lilikuwa linamwandaa Hassan Oduya kuwa Rais wa nchi, na ilibaki kidogo angefanikiwa kama uozo wake usingefichuliwa na Tunu.

Tunu, kwa kushirikiana na ofisa mwingine wa usalama Faustine Ndejembi na wapelelezi wawili wa kujitegemea walifanya kazi kubwa mno iliyomfanya Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (DGIS) wakati huo, Dk. Mgaya Kingoba, kukiuka taratibu za chain of command kwa kumpigia simu Tunu akimwita makao makuu ya TISS pale Oysterbay baada ya Rais kufurahishwa na kazi yake.

Endelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

232

Kwa mujibu wa cheo na wadhifa aliokuwa nao Tunu wakati huo ndani ya Idara ya Usalama wa Taifa, hakuwa miongoni mwa watu wanaoweza kupigiwa simu na DGIS kwa sababu yoyote ile. Chain of command ilimtenga na wakubwa wa Idara hata alipokuwa katika operesheni nyeti.

Mara zote wakuu wa operesheni hizo ndiyo waliokuwa na nafasi ya kuzungumza na wakurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa kwa niaba yetu wakati sisi tukiwa katika mapambano. Watu wa medani (field), kama ilivyokuwa kwangu au kwa Tunu wakati huo, kumbukumbu zetu zilibaki katika mafaili na katika vichwa vya wale tulioshirikiana nao katika vita. Basi!

Kisha Tunu alinitaka nimfuate anitembeze kuyaona mazingira ya ofisi za Taasisi ya SPACE na namna kazi zinavyofanywa (orientation), na kisha angeniruhusu niondoke nikaanze mapumziko yangu, na kwamba nilitakiwa kufikiria ni nchi gani ambayo ningependa kwenda kutembea kwani gharama zote zingelipwa na Idara ya Usalama wa Taifa.

Tuliinuka tukaelekea kwenye mlango mkubwa wa chuma ukiwa umepachikwa bandiko jeupe lililosomeka ‘SPACE’. Pembezoni mwa mlango huo kulikuwa na kifaa cha kuweka nywila (password) kabla hujaingia humo. Tunu akabofya hapo mara kadhaa na mara mlango ukafunguka. Tukazama ndani na kupokelewa na maofisa ambao walitukaribisha kwa bashasha.

Wakati Tunu akinitembeza ndani ya ofisi hizo niligundua kuwa kulikuwa na vitengo vikuu kadhaa vikiwemo vya Accounting, Surveillance, Graphics, Hacking na Coding. Gloria Tesha ndiye alikuwa akiongoza kitengo cha Surveillance na alishirikiana na maofisa wengine akiwemo Philip Bundala.

Kisha tuliingia kwenye ofisi za kitengo cha Graphics, humo nilimkuta Juma Ndekule akikiongoza kitengo hicho, nikashuhudia maofisa mbalimbali wakiwa wamehemewa (busy) na kazi. Sauti ya vibofyeo vya tarakilishi zao zilikuwa zinagonga gonga na kuacha. Muda wote Ndekule alikuwa mbele akikodolea kioo cha tarakilishi yake.

Halafu kwenye kitengo cha Hacking alikuwepo Hawa Kiluvya akishirikiana na maofisa wengine watatu. Hata hivyo, Tunu alinikumbusha kuwa Taasisi ya SPACE ilikuwa ni sehemu ya Idara ya Usalama wa Taifa, na hivyo pamoja na kuwa ofisi ya kitengo kimoja ilikuwa kwenye jengo moja na kitengo kingine, maofisa wa vitengo hivyo hawakuruhusiwa kutembeleana ofisini bila ruhusa au sababu za msingi.

Endapo ofisa wa kitengo kimoja angelazimika kwenda katika ofisi ya kitengo kingine, yaani nje ya kituo chake cha kazi, kwa dharula au sababu nyingine yoyote angetakiwa kuomba kibali (gate pass) cha kumruhusu kufanya hivyo. Ni utaratibu ule ule uitwao compatimentation ambao uliisaidia Idara nzima ya Usalama wa Taifa kutunza siri, kuendesha operesheni zinazojitegemea, na kuwazuia maadui wa taifa kujipatia taarifa muhimu kwa urahisi (endapo wangepenyeza mtu wao ndani ya idara).

Huo ulikuwa utaratibu wa lazima wa Idara, kuweka kanuni na taratibu hizo ili kulinda nyaraka na siri za Idara, na pia kujenga nidhamu ya maofisa wake na kila ofisa alikuwa anajua kwamba muda wowote katika ajira yake angeweza kufuatiliwa nyendo zake kwa sababu mbalimbali, iwe kwa lengo la kuthibitishwa uwezo na umakini wake ili apandishwe cheo na kupewa madaraka makubwa, au kwa kutiliwa mashaka.

Baada ya kutembezwa kwenye vitengo vyote hatimaye tulirudi tena ofisini kwa Mkuu wa Taasisi ya SPACE, ambapo Tunu alinipatia maelezo muhimu ya kuzingatia niwapo kazini na hata nje ya kazi, kisha akaniomba nifikirie haraka ni wapi ambapo ningependa kwenda kwa mapumziko halafu nimwambie ili aandae utaratibu.

“Nadhani Mombasa patanifaa zaidi,” nilisema pasipo hata kuushirikisha ubongo wangu. Hata hivyo jambo moja lilikuwa wazi akilini mwangu, nilitamani sana kuwa na Leyla kwenye mapumziko yangu.

Tunu alinitazama kwa mshangao kwa kitambo, huenda alihisi kuwa hajanisikia vizuri. “Mombasa?” aliniuliza huku akinikazia macho yaliyojaa mshangao. “Kwa nini isiwe maeneo kama Dubai au hata…”

“Mombasa ndiyo sehemu pekee kwa sasa nadhani itanifaa kurefresh my mind,” nilimkata kauli nikiongea kwa kujiamini, na hapo Tunu akabetua mdomo wake na kunyanyua juu mabega yake kwa kebehi.

“Mh! Si bure, kuna mtu tayari kishakulisha limbwata huko maana inaelekea akili yako yote ipo Mombasa,” Tunu aliongea huku akiuvuta mdomo wake. Sikujua kama alifanya vile kwa utani au alianza kusumbuliwa na wivu.

“Acha wivu, mkuu,” nilisema na kuangua kicheko hafifu na kumfanya Tunu aachie msonyo wa nguvu.

“Hata kama... hii ni dalili tosha kwamba umeshatekwa,” Tunu alisema huku naye akiangua kicheko hafifu.

“Si bora nitekwe na huyo wa Mombasa kuliko kutekwa na wale makomando wa kule Shamba,” nilisema kwa utani na kumfanya Tunu aangue kicheko kikubwa. Sasa tulijikuta tukizungumza kana kwamba ni washkaji tu waliokuwa kijiweni badala ya ofisa usalama na mkuu wake wa kazi.

“Yaelekea wale makomando wamekunyoosha kweli kweli!” Tunu alisema huku akiendelea kucheka.

“Dah, we acha tu,” nilisema huku nikishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Baada ya maelezo machache Tunu aliniruhusu kuondoka ofisini hapo ili nikaendelee na shughuli zangu za kawaida wakati taratibu zingine za kiofisi zikifanywa. Niliinuka nikapiga saluti ya heshima kisha nikamuaga kwa kumpa mkono, halafu nikageuka na kutembea taratibu kuelekea chumba cha katibu muhtasi wake, mahali palipokuwa na mlango wa kutokea ukumbini.

Nikaingia katika ofisi ya katibu muhtasi wa Tunu na wakati nikitaka kumuaga simu iliyokuwa juu ya meza yake ikaanza kuita kwa sauti ya chini. Salha akanyoosha mkono wake wa kushoto kuinyanyua huku akininyooshea mkono wake wa kulia kuniashiria nisubiri kidogo.

“Mkuu amesema usubiri kidogo kuna mtu anakuja kukuona sasa hivi,” Salha alinieleza baada ya kumaliza kuongea na simu hiyo.

Okay,” nilimjibu huku nikiketi kwenye kiti kilichokuwa karibu yangu. Sikujua ni mtu gani niliyekuwa nikimsubiri, na alikuwa anataka nini kwangu, au kunieleza jambo gani! Nilichokuwa nafahamu kwa wakati huo ni kwamba nilikuwa nimesharipoti kazini na kupewa mapumziko ya mwezi mmoja kabla ya kuja kuanza kazi rasmi. Hata hivyo, sikuwa na la kufanya ila kusubiri.

Nilikaa hapo kwa takriban dakika kumi hivi ndipo mlango wa ofisi ile ukafunguliwa. Ofisa mmoja, mwanaume mwenye umri usiopungua miaka therathini akaingia ndani. alikuwa amevaa suti nzuri ya kijivu. Baada ya kutusalimia akajitambulisha jina lake, nami nikamfahamisha jina langu.

“Kumbe wewe ndiye Ofisa ninayekutafuta,” yule Ofisa aliniambia huku akinipa mkono kisha akaendelea kuniambia, “Mkuu ameniagiza nikupe hii OP.” Alisema na kunyoosha mkono wake kunipa bahasha nyeupe iliyokuwa imeandikwa jina langu.

“Ahsante, nashukuru sana,” nilimjibu yule Ofisa huku nikiipokea ile bahasha na kuitumbukiza katika mfuko wa koti langu. Sikuwa na haja ya kujiuliza kilichokuwemo maana aliyenipa alishaniambia kuwa ni OP yaani “operation fund”. Nilitambua kuwa hilo lilikuwa neno la ki-idara lenye maana ya “fedha za kufanyia kazi”. Ingawa sikuwa nakwenda kufanya kazi lakini mapumziko niliyokuwa nakwenda yalikuwa yanagharamiwa na Idara. Na hivyo bila kupoteza muda nikamuaga katibu muhtasi wa mkuu na kutoka.

Niliitupia jicho saa yangu ya mkononi wakati nikielekea kwenye gari langu, nikagundua kuwa ilikuwa saa tano na nusu asubuhi. Sikuwa na sababu ya kurudi nyumbani muda huo hasa kwa kuwa Rehema hakuwepo nyumbani, na hivyo nikaona nielekee benki.

* * *

Tukutane wakati mwingine. Endelea Kufuatilia simulizi hii hadi mwisho...
 
Yani huyu Jason hajakoma tu na umalaya wake! Na litamkuta jambo huko Mombasa mbwa huyu
 
Bishop siku ya sensa tuburudishe na dozi kubwa ili tutulie nyumbani kusubiri makarani
Sensa... Itakuwa J'nne Agosti 23? Ngoja nione dozi ya kiasi gani itawafaa, naogopa nisije nikazidisha kipimo maana huko tunakokwenda ni zaidi ya hatari yenyewe...
 
Sensa... Itakuwa J'nne Agosti 23? Ngoja nione dozi ya kiasi gani itawafaa, naogopa nisije nikazidisha kipimo maana huko tunakokwenda ni zaidi ya hatari yenyewe...
Naomba utuovadozi tuzidiwe mpk tuzimie kabisa mkuu hyo siku
 
Back
Top Bottom