Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Sasa bwana Bishop Hiluka unaogopa nni kuweka hayo mambo?? Huoni unatunyima baadhi ya vitu?? Ama huoni nafsi yako unakusuta kwa kutuibia??

Weka mambo wazi kiongozi acha kufutafuta
Duh, natamani lakini si rahisi kihivyo, nabanwa na Sheria ya Usalama wa Taifa nambari 15 ya mwaka 1996 ...
 
Dah, samahani wadau tumepatwa na msiba, bro wangu kafiwa na kijana wake. Sipo karibu na laptop yangu yenye stori ila kama nitaweza kesho naweza kuitupia hapa stori yote iliyobakia ya Ufukweni Mombasa...
Pole sana bishop,mwenyezi mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu mnachopitiq
 
Dah, samahani wadau tumepatwa na msiba, bro wangu kafiwa na kijana wake. Sipo karibu na laptop yangu yenye stori ila kama nitaweza kesho naweza kuitupia hapa stori yote iliyobakia ya Ufukweni Mombasa...
POLESANA MKUU MUNGU AWE PAMOJA NANYI KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU NA ROHO YA MAREHEMU AIWEKE MAHALA PEMA PEPONI
 
ufukweni mombasa.JPG

262

Saa 7:15 usiku…



Saa saba na robo usiku ilinikuta nikishushwa na teksi katika barabara ya Old Malindi usawa wa ACK St. Mary’s Parish Church – Utange, kisha nilianza kutembea kwa utulivu kando ya ile barabara ya Old Malindi huku mara kwa mara nikigeuka na kutazama nyuma yangu kama kungekuwa na pikipiki, gari au mtu yeyote akinifuatilia. Sikumwona mtu yeyote, pikipiki wala gari hivyo nikaamini kuwa hali bado ilikuwa shwari. Nilikuwa nimechoka sana, mwili na akili kutokana na misukosuko ya siku nzima.

Teksi iliyonileta hadi pale ACK St. Mary’s Parish Church – Utange ni ile ile iliyokuwa imenipeleka nyumbani kwa Miriam Mutua kutokea Bamburi Beach Villa. Nilipotoka nyumbani kwa Miriam nilikuwa na wasiwasi wa kupata usafiri usiku huo lakini nikashangaa kumkuta dereva wa teksi akiwa bado ananisubiria pale pale tulipokubaliana japokuwa nilimweleza kuwa angeondoka endapo asingeniona baada ya nusu saa. Kumbe ni Leyla aliyempa maelekezo ya kutoondoka!

Sasa nikiwa natembea, utulivu katika barabara ile ulinipa hadhari ya namna yake hadi nilipokaribia kwenye Kanisa la Agape Fellowship Center – Shanzu, nikasimama kidogo kando ya ile barabara nikiyatembeza macho yangu kwa makini kuyapeleleza mandhari yale na niliporidhika na tathmini yangu nikaanza tena kutembea taratibu huku mkono wangu mmoja ukiwa ndani ya mfuko wa koti langu umeikamata bastola.

Nilinyanyua mkono wangu uliovaa saa na kutazama saa, ilishatimia saa saba na nusu za usiku. Muda ulikuwa umesonga sana hivyo matumaini ya kumkuta Merina akiwa macho kwa tafsiri nyingine yalikuwa madogo sana.

Mara kumbukumbu juu ya jinsi nilivyoonana na Merina kwa mara ya kwanza kule Serena Beach Resort ikaanza kujengeka taratibu kichwani mwangu. Merina alikuwa msichana mrembo ambaye mwanamume yeyote angejisikia fahari kuwa naye. Japokuwa safari yangu kuja pale Mombasa ilikuwa kwa ajili ya Leyla lakini sasa nilijikuta nikiwa mateka wa nafsi mbele ya Merina.

Baada ya kulivuka Kanisa la Agape Fellowship Center nikageuza shingo yangu na kuyatembeza tena macho yangu kwa makini kisha nikachepuka haraka upande wa kushoto na kuanza kukatiza vichochoro huku nikijihisi mpweke kwani giza lilikuwa zito japokuwa baadhi ya nyumba zilikuwa zikiwaka taa lakini mwanga wa taa zile haukuwa na msaada wowote katikati ya lile giza.

Mara moja nikageuka tena nyuma kuangalia kama kungekuwa na mtu yeyote akinifuatilia. Bado sikumwona mtu yeyote na hivyo nikaamini kuwa hali ilikuwa bado shwari. Nilipoifikia nyumba aliyokuwa akiishi Merina nikasimama tena nikiupima utulivu wa eneo lile. Bado hali ilikuwa shwari na hapakuwa na kiashiria chochote cha uwepo wa kiumbe hai eneo lile. Niliporidhika kuwa mambo yalikuwa shwari nikausogelea mlango na kugonga taratibu.

“Nani?” sauti ya Merina ilisikika toka ndani mara tu nilipogonga, ikiuliza kwa wasiwasi. Nikashangaa kuona kuwa hadi muda huo alikuwa bado hajalala.

“Ni mimi, J,” nilijibu kwa sauti ya chini na mara mlango ukafunguliwa taratibu na Merina akachungulia nje, aliponiona akashusha pumzi na kuufungua mlango huku akinipisha niingie.

Usiku huo alikuwa amevaa nguo nyepesi ya kulalia ambayo ilishindwa kuyaficha maungo yake na kunifanya nizione chuchu zake laini zilivyosimama kwa utulivu kama zilizokuwa zikinidhihaki. Kiuno chake chembamba chenye shanga kilikuwa kimefinyangwa vizuri kuushikilia mzingo wa makalio yake ya wastani usiokinaisha kuutazama. Tumbo lake lilikuwa dogo lenye kitovu laini chenye kishimo na mapaja yake yalikuwa laini na mang’avu yenye misuli imara.

Mwili wangu ulishikwa na ganzi na akili yangu ilianza kuyumba na
kupoteza uelekeo kama bondia niliyetaka kukumbwa na tatizo la kizunguzungu.

“Mbona umesimama, tafadhali pita ndani,” sauti ya Merina ilinizindua toka kwenye mduwao ule. Nikaachia tabasamu la aibu na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Wakati naingia ndani Merina alikuwa bado amesimama pale kando ya mlango na alinitazama kwa tuo kama mtu ambaye hakuamini kuniona tena. Kisha tabasamu jepesi likajitokeza usoni kwake.

“Ndiyo nini kuniweka roho juu kiasi hiki!” Merina aliniuliza kwa sauti ya kulalama huku akiendelea kunitazama usoni.

Nilitabasamu na kumwambia, “Pole sana kwa kunisubiri, hata hivyo sikukusudia.”

Merina hakusema kitu, alifunga mlango vizuri kisha akanikabili. “Mbona hujalala hadi saa hizi?” nilimuuliza huku nami nikimkabili. Tukatazamana.

“Ningewezaje kulala wakati sijui uko katika hali gani? Nimeshindwa kabisa kupata usingizi tangu nilipofika hapa nyumbani,” Merina alinijibu huku akinitazama kama mama amtazamavyo mwanawe mpendwa.

“Ungelala tu!” nilimwambia. “Nilikuwa na uhakika ningerejea tu!”

Merina hakunijibu kitu zaidi ya kutabasamu na hapo nikamkaribia zaidi na kumshika kiunoni bila ruhusa yake, hata hivyo sikukutana na upinzani wowote. Merina alinitazama machoni kisha akaachia tabasamu la aibu. Nikaichukua mikono yake na kuipitisha nyuma ya shingo yangu, nikamwona akinikumbatia na kisha akaniletea mdomo wake na hapo ndimi zetu zikakutana.

Muda mfupi uliofuata tulikuwa kama tuliopagawa, kisha tukachukuana hadi chumbani kwenye kitanda kikubwa cha futi tano kwa sita cha samadari huku kila mmoja akiwa amepandwa na wazimu wa mapenzi. Na kilichoendelea humo chumbani kilituhamisha kutoka dunia hii na kutupeleka kwenye ulimwengu mwingine wa huba, sayari ya raha kwa ajili yetu. Merina alijua namna ya kuzitendea vyema hisia zangu.

* * *

Inaendelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

263

Taharuki…




Saa 12:45 asubuhi…

HISIA za kukumbatiwa na mtu pale kitandani zilinigutusha toka kwenye usingizi mzito, nilijigeuza kivivu na kukutana uso kwa uso na Merina ambaye alikuwa akinitazama kwa tabasamu pana.

“Mmh, kumbe umeamka?” nilimuuliza swali kama punguwani.

“Ndiyo, mpenzi wangu… natakiwa nijiandae niwahi kazini,” Merina aliongea kwa utulivu huku uso wake ukiendelea kupambwa na tabasamu. “Sasa hivi ni saa moja kasorobo, mpenzi.”

“Dah! Kumbe kumeshapambazuka!” niliongea kwa mshangao huku nikiitupia jicho saa yangu ya mkononi. Kisha nikamuuliza, “Kwani kazini unaingia saa ngapi?”

“Saa mbili kamili asubuhi,” Merina alinijibu kwa sauti hafifu huku akionesha kukerwa kidogo, huenda alitamani siku hiyo tushinde wote pale nyumbani. Nikamhurumia, hata hivyo sikuwa na namna ya kufanya.

Kisha tulibaki kimya tukitazamana kwa kitambo fulani huku macho yetu yakiongea na hisia za mapenzi zikifufuka upya nafsini mwetu. Merina akashusha pumzi na kuinuka kisha akaelekea maliwato maana chumba chake, kwenye ile nyumba ya vyumba viwili pamoja na jiko, kilikuwa na maliwato ya ndani kwa ndani. Baada ya takriban dakika tatu alitoka bafuni na kuelekea sebuleni na wakati huo huo mimi nikiamka na kuingia bafuni.

Ilinichukua takribani dakika kumi na tano kumaliza shida zangu, nikatoka bafuni na kuingia chumbani, nikavaa nguo zangu na baada ya kuhakikisha nipo sawa nikajongea sebuleni ambapo nilimkuta Merina akiwa amesimama kwenye meza ya chakula akiwa anapakaa blueband katika slesi za mkate, aliponiona akaachia tabasamu pana na kuniambia, “Karibu chai, mpenzi.”

Nilimtazama kwa mahaba huku nikienda kujipweteka kwenye kiti pembeni yake, Merina akanibusu mdomoni. “Anza kunywa chai, mpenzi, ngoja nami nikajimwagie maji mara moja.” Alisema na kugeuka, akaondoka na hapo nikapata kuona vizuri mtikisiko maridhawa wa umbo lake zuri.

Sikutaka kunywa chai bila Merina, nikaamua kumsubiri. Ilimchukua takriban dakika ishirini na ilipofika saa moja na dakika therathini na tano Merina alikuwa tayari amekwisha maliza kujiandaa. Alipotoka chumbani akanikuta nikiwa nimeketi nikimsubiria.

“Mbona hujaanza kunywa chai?” Merina aliniuliza kwa mshangao huku akinitazama kwa umakini.

“Nisingeweza kunywa bila wewe, mpenzi,” nilimwambia huku nikiachia tabasamu. Merina akaachia tabasamu na kunibusu mdomoni kwa mahaba kisha akanisogezea maji, nikanawa mikono na yeye akanawa tukaanza kunywa chai. Staftahi ile ilikuwa ya chai ya maziwa, slesi za mkate, mayai pamoja na soseji.

Mwanzoni wakati tukipata mlo pale mezani tulikuwa kimya, macho ya Merina yalikuwa yananitazama kiwizi wizi na baada ya muda nikaamua kuvunja ukimya kwa kumdadisi. Sasa kila mmoja akawa anamdadisi mwenzake, hapo nikapata nafasi ya kujua mambo machache kuhusu Merina ingawa kwa upande wangu aliambulia uongo mwingi katika maswali aliyoniuliza.

Tulipomaliza kula alitoa vyombo kisha akarudi pale sebuleni na kusimama mbele yangu huku akinitazama kwa wasiwasi kidogo.

“Jason…” Merina aliniita.

“Naam Merina,” niliitika huku nikimtazama kwa umakini kidogo.

“Nimetokea kukupenda sana, Jason,” Merina aliniambia na kushusha pumzi.

“Mimi pia nakupenda, Merina,” nilimwambia huku nikisimama na kumkumbatia.

“Tafadhali usije ukaniumiza, mpenzi wangu. ikibidi twende wote Tanzania,” Merina alisema kwa sauti ya kunong’ona huku akishusha pumzi ndefu.

“Siwezi kukuumiza, mpenzi. Kuhusu kwenda wote Tanzania itabidi nikaandae mazingira,” nilimwambia Merina huku nikimbusu mdomoni. Hata hivyo nilimhurumia sana kujiingiza kwenye mapenzi na mtu asiyestahili kupendwa.

Kisha aliniaga huku akitaka kujua ratiba yangu siku hiyo, nilimweleza kuwa nilihitaji kupumzika kidogo kwa kuwa nilikuwa na miadi na mtu saa nne asubuhi. Kisha nilimtaka awe makini na anifanyie upelelezi mdogo pale hotelini kujua nini kilikuwa kinaendelea hasa kwa jambo ambalo angehisi linatia shaka, halafu anieleze. Tukaagana huku nikimsisitiza kuendelea kuwa makini na asimwamini mtu yeyote.

_____

Sikujua ni nini kilikuwa kimenishtua kutoka katika usingizi mzito uliokuwa umenichukua kwa muda wa zaidi ya saa mbili. Haraka nikainuka na kuketi pale kitandani huku nikiyatega masikio yangu vizuri. Sikusikia chochote zaidi ya kuona simu yangu ikiwa inatoa mwanga. Nikaichukua na kuitazama vizuri na kuona kulikuwa na mwito wa simu ambayo haikupokelewa (missed call) toka kwa mke wangu Rehema.

Nikakumbuka kuwa sikuwa nimewasiliana naye tangu aliponipigia simu asubuhi ya siku iliyokuwa imetangulia. Nikampigia, na alipopokea nikamwomba msamaha kwa kutowasiliana naye huku nikimdokeza kwa kifupi kuwa safari yangu kuja Mombasa haikuwa kama nilivyotarajia kwani kuna mambo yalikuwa yamejitokeza ambayo nilipaswa kuyatafutia ufumbuzi, nikamwahidi kumjulisha baadaye kilichokuwa kinaendelea.

Rehema hakuwa na maneno mengi alinitaka niwe makini muda wote na kisha akanitakia harakati njema. Tukaagana kisha akakata simu. Wakati nataka kuiweka simu kando macho yangu yakatua kwenye ujumbe mfupi wa maandishi uliokuwa umeingia kwenye simu, nilipoutazama vizuri nikagundua kuwa ni ujumbe uliokuwa umeingia takriban nusu saa kabla na ulitoka kwa Merina.

Nikaufungua ujumbe ule na kukutana na maneno machache: “Friday-16:00-Bamburi Beach”.

Niliutazama ujumbe ule kwenye simu na kujiuliza kulikuwa na nini Bamburi Beach siku ya Ijumaa saa kumi jioni? Mara moyo wangu ukapiga kite kwa nguvu baada ya kukumbuka kuwa siku hiyo ilikuwa ndiyo Ijumaa kwa mujibu wa kalenda na kwamba kuna jambo lilipaswa kufanyiwa kazi.

Nikaitazama saa yangu ya mkononi na kugundua kuwa tayari ilikwisha timia saa nne na dakika tano asubuhi, na hivyo nilikuwa nimepitisha dakika tano zaidi ya muda tuliokubaliana niwasiliane na Leyla.

Kabla sijampigia simu Leyla nikataka kwanza kujua kwa kifupi ujumbe ule ulihusu nini na Merina aliutoa wapi! Nikampigia lakini simu yake iliita mara mbili tu ikakatwa. Nikataka nipige tena lakini nikajionya kuwa huenda hakuwa sehemu nzuri ya kuongea na mimi. Nikaachana naye na kumpigia Leyla. Alipopokea tukasalimiana kisha akanitaka tukutane Red Brick Restaurant katika Barabara ya Mombasa saa tano kamili ya asubuhi.

Sikutaka kushangaa, nilimpigia simu yule dereva wa teksi aliyekuwa amenileta usiku kwani alikuwa amenipa namba zake, kisha nikatoka na kuufunga mlango wa nyumba halafu nikaeleka barabarani kusubiri teksi lengo likiwa niwahi kufika pale Red Brick kabla ya muda tuliokubaliana. Taaluma yangu ya ujasusi ilinifanya kuwa makini mno nikiamini kuwa kufika sehemu ya miadi kwa muda mliokubaliana ni kati ya makosa makubwa maana unaweza kuwa ulipanga muda wa kifo chako.

Nilipofika pale barabara ya Old Malindi nilisimama kwa takribani dakika 25 mara teksi moja ikatokea na kuja kusimama karibu yangu. Hii haikuwa ile teksi niliyokuwa nikiisubiria, lilikuwa gari aina ya Toyota Spacio.

Inaendelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

264

“Habari yako, kaka?” yule dereva wa teksi alinisalimia, nilipomtazama vizuri nikamtambua kuwa ni yule dereva niliyemtarajia lakini alikuwa na gari tofauti. Asubuhi ile alikuwa amevaa shati la kitenge la mikono mirefu, kofia nyeusi ya pama, suruali ya bluu ya dengrizi na viatu vya ngozi miguuni.

“Ah, nzuri sana. Naona umebadilisha gari!” niliitikia huku nikimuuliza kwa mshangao.

“Dah! Niwie radhi kwa kuchelewa. Gari langu liliniletea shida wakati najiandaa kuja, ilibidi niliache kwa jamaa yangu na nichukue gari lake ili nikuwahi,” yule dereva alisema huku tabasamu usoni kwake likizidi kuchanua.

“Oh! pole sana hata hivyo hajachelewa sana,” nilimtia moyo. “Naomba nipeleke Red Brick Restaurant, Barabara ya Mombasa.”

Nilisema huku nikiingia ndani ya teksi ile. Dereva akaliondoa gari lake, tukashika barabara ile ya Old Malindi na baada ya mwendo fulani tukakifikia Kituo cha mafuta cha Habresh Utange na hapo nikamwona akiingia pale kituoni, akaweka mafuta kisha tukaondoka na kuyavuka majengo ya Masjid Irshaad Markaz.

Wakati tukiipita Shule ya Upili ya Wasichana ya Hassan Joho katika barabara ile ya Old Malindi nikaliona gari jeusi aina ya Nissan Patrol likitupita kwa kasi, hakuna kati yetu aliyeonekana kujali. Tulikwenda hadi tulipofika kwenye Hospitali ya Beyondscope nikavutika kulitazama gari jeusi aina ya Nissan Patrol likiwa limeegeshwa kando ya barabara ile jirani na hospitali hiyo, nikalikumbka kuwa ndilo lililotupita dakika chache zilizokuwa zimepita, nikalipuuzia kwani sikuona kama kulikuwa na haja ya kulifikiria gari lile.

Tukiwa tunauvuka Msikiti wa Barsheba nikagutuka baada ya kuliona tena gari lile Nissan Patrol jeusi likiwa nyuma yetu, nikamtazama dereva wangu, hakuonekana kuwa na habari yoyote juu ya gari lile lililokuwa nyuma yetu. Kengele ya hatari ikalia kichwani, na hapo nikahitaji kuwa na uhakika kama gari ile lilikuwa linatufuatilia ama lah, sikutaka kulipuuzia.

Mara nikaliona soko dogo mbele yetu katika eneo lile la Kisauni maarufu kama Mwembeni – Soko Mjinga, na hapo nikapata wazo.

“Dereva, unaweza kusimama mara moja hapa? Kuna kitu nataka kuchukua hapo sokoni” nilimuuliza dereva wa teksi.

Dereva wa teksi hakusema neno na badala yake alikanyaga breki na kuingia upande wa kushoto mwa barabara na kusimamisha gari mbele ya lile soko mjinga. Nikashuka haraka huku nikiwa makini kulitazama lile gari aina ya Nissan Patrol nikaliona likipita kwa mwendo wa taratibu na kuendelea na safari yake. Nikashusha pumzi huku nikijiuliza iwapo hisia zangu zilikuwa sahihi au safari hii zilinidanganya.

“Hivi ni kweli nafuatiliwa au ni mawenge yangu tu?” nilijiuliza lakini sikupata jawabu la moja kwa moja.

“Vipi kuna tatizo?” yule dereva wa teksi aliniuliza baada ya kuniona nimesimama tu pembeni ya mlango wa gari.

"Ah, samahani tuendelee na safari tu maana nimekumbuka sina fedha za kutosha. Nitanunua hata wakati mwingine,” nilimjibu dereva wa teksi huku nikijitoma ndani ya gari.

Safari ikaanza tena, ila safari hii nilikuwa makini sana kulitafuta lile gari aina ya Nissan Patrol jeusi, lakini hadi tunafika kwenye makutano ya barabara za Old Malindi na Nyali sikuwa nimeliona tena gari ile. Na hapo tukaiacha barabara ya Old Malindi na kuchukua barabara ya Nyali, tulizidi kusonga na baada ya muda tukalivuka daraja la Nyali na tulipokuwa tunalivuka jengo la Safaricom Customer Care Center nikagutuka baada ya kuliona tena lile Nissan Patrol jeusi likitupita kwa kasi. Sikujua lilikuwa wapi maana hatukuwa tumeliona wakati tukiingia katika barabara ile ya Nyali.

“Hili gari vipi, silielewi kabisa!” dereva wa teksi alilalama baada kuliona lile Nissan Patrol jeusi lilivyotupita kwa fujo.

“Si wewe tu, hata mimi linanitia shaka sana, hebu angalia linavyopunguza mwendo halafu limekaa katikati ya barabara,” nilimwambia yule dereva wa teksi.

“Duh, hapa tugeuze gari au tuingie barabara hii ya kushoto maana limeshanitia mashaka,” yule dereva wa teksi aliongea huku akionekana wazi kuanza kuhamanika.

“Omba saiti tuone kama atatupisha,” nilimshauri dereva. Na kweli dereva wa teksi akaongeza mwendo na kuwasha taa ya kuonesha kuwa tulihitaji kupita, na hapo lile Nissan Patrol jeusi likaacha nafasi kulia kwetu, tukaanza kulipita lakini tukiwa sambamba nikatupia macho ndani ya gari lile ambalo vioo vyake havikuwa vyeusi, na hivyo niliweza kumwona dereva pasipo shida yoyote. Alikuwa mweusi na mwenye ndevu nyingi. Nilimtazama kwa makini na hapo nikamwona akishusha kioo huku akiwa ameshika bastola aina ya FNX 45 Tactical huku akitabasamu.

“Dereva kanyaga breki fasta,” nilimwambia dereva wangu kwa hamaki baada ya kuona mdomo wa bastola ukielekea upande wetu. Dereva akakanyaga breki na sekunde hiyo hiyo tukashuhudia risasi iliyotoka kwenye bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti ikitoboa kioo cha mbele na kusababisha nyufa, lakini haikumjeruhi yeyote.

“Pumbavu, hebu ongeza mwendo nimwoneshe kazi,” nilimwambia dereva wangu huku nikichomoa bastola yangu. Wakati dereva wa teksi akiongeza mwendo lile Nissan Patrol jeusi nalo likaongeza kasi na kupotea mbele yetu katika Barabara ya Ronald Ngala.

Baada ya hapo hatukukutana nalo tena hadi tunafika Red Brick Restaurant katika Barabara ya Mombasa. Muda wote nilikuwa najaribu kutafakari kuhusu tukio lile.

Nilijiuliza, ni nani yule mwanamume aliyejaribu kutuua? Kwa nini hakuficha uso wake na alikuwa anatabasamu? Na kwa nini akakimbia baada ya kurusha risasi moja tu? Kwanza alijuaje kuwa nilikuwa natokea eneo la Old Malindi - Shanzu na kwamba ningeelekea katikati ya jiji? Swali hili la mwisho lilinifanya niingiwe na woga kiasi chake. Na hapo nikamkumbuka Merina na kuanza kuhofia usalama wake.

Nilimuuliza dereva wa teksi alikuwa anadai kiasi gani, aliponitajia nikamlipa kisha nikatoa simu yangu na kutafuta namba ya Merina, nikaipiga na mara ikaanza kuita upande wa pili. Ilikuwa ni kama bahati kwani ule mwito wa simu ulipoita mara mbili tu ile simu ikapokelewa upande wa pili. Hata hivyo mpokeaji wa ile simu hakuzungumza neno lolote huku dhahiri akionekana kunitegea.

“Merina!” niliita kwa sauti tulivu ya chini lakini pia iliyosikika vizuri hata hivyo Merina hakuitikia mapema badala yake nikasikia akishusha pumzi ndefu kana kwamba alikuwa ametoka kumaliza mashindano ya mbio ndefu.

“Merina, ni mimi Jason…” niliongea kwa msisitizo huku nikianza kuingiwa na hisia mbaya. Kisha nikamuuliza kwa mashaka, “Vipi, kwema?”

“Jason, huku mambo si shwari,” Merina alisema kwa sauti ya chini mno iliyojaa wasiwasi.

“Una maana gani?” nilimuuliza Merina huku sauti yangu ikianza kupoteza utulivu wake.

“Kuna watu wawili wamekuja hapa hotelini, mmoja ana asili ya Kisomali, wakaanza kunihoji kuhusiana na wewe huku wakitaka kuondoka na mimi, nimewatoroka na sasa nimejificha huku stoo. Naogopa sana, Jason…” Merina alisema kwa sauti ilioyojaa hofu.

Inaendelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

265

Oh my God!” nilijikuta niking’aka kwa mshtuko huku nywele zangu zikinisisima na wakati huo huo hasira zikinipanda. Nilipotega vizuri sikio langu nikamsikia Merina akishusha pumzi katika namna ya kukata tamaa kisha kukafuatia kitambo cha ukimya.

“Merina!” niliita lakini hakuitika. “Ondoa hofu na endelea kujificha, nakuja sasa hivi.”

“Kwani upo wapi?” Merina aliniuliza kwa wasiwasi.

“Nipo hapa…” nilikatisha maongezi baada ya kusikia ukelele mkubwa. Ilikuwa ni sauti ya Leyla ikiita, “JASON!”

Niligeuka haraka na hapo macho yangu yakakutana na mtutu wa bunduki toka katika gari moja aina ya Jeep jeusi lililokuwa linapita eneo lile. Kama kima niliruka juu na kutua chini huku nikiviringika na wakati huo huo milio ya risasi ikisikika na kuwafanya watu waliokuwapo eneo lile wakumbwe na taharuki na kuanza kukimbia ovyo kuokoa maisha yao.

Kisha nilijibanza nyuma ya gari moja dogo jeupe aina ya Mazda lililokuwa karibu na mahala nilipoangukia. Jamaa wale waliokuwa ndani ya lile gari aina ya Jeep jeusi waliniona kwa sababu gari lile nililojificha nyuma yake lilianza kumiminiwa risasi na kuvunja vunja vioo. Kwa takriban dakika tatu hali ilikuwa ni ya hatari kubwa. Risasi ziliendelea kuvurumishwa katika lile gari nililokuwa nimejibanza nyuma yake na kuliharibu sana.

Mara nikaanza kusikia risasi zikirindima kila upande na kunifanya niendelee kujibanza pale nyuma ya lile gari aina ya Mazda huku bastola yangu ikiwa mkononi. Baada ya kama dakika tano za mivumo ile ya risasi kutawala eneo lile mara milio ile ikakoma ghafla.

“Jason… Jason!” niliisikia sauti ya Leyla ikiniita kwa wasiwasi. Nikanyanyua kichwa changu na kutazama kwa umakini upande ambao sauti ile ilitokea, na hapo nikamwona Leyla akiwa amesimama katika lile gari aina ya Jeep jeusi walilokuwemo wale jamaa waliotaka kunimaliza huku bastola yake ikifuka moshi. Pembeni yake alikuwa amezungukwa na vijana wengine wawili ambao nao walikuwa wameshika bastola.

Kwa mara nyingine tena Leyla alikuwa ameyaokoa maisha yangu kutoka kwa majahili. Nilitabasamu baada ya kugundua kazi nzuri iliyofanywa na Leyla na vijana wake hodari. Niliamini kuwa majahili wote walikuwa wameteketezwa. Nikasimama na kutembea kwa tahadhari kubwa kuelekea katika gari lile. Eneo hilo lilikuwa halitazamiki kutokana na vioo vya magari kuvunjwa kwa risasi na magari kuharibiwa ovyo hasa lile gari aina ya Mazda nililokuwa nimejibanza nyuma yake. Watu watatu waliokuwa ndani ya lile gari aina ya Jeep walikuwa wamekufa huku damu nyingi zikiwatoka.

Jason, are you okay?” Leyla aliniuliza huku akinitazama kwa umakini, nilikuwa nimejaa vumbi mwili mzima na kijasho kilikuwa kinanitiririka.

Yeah, I’m okay. Are you okay?” nilijibu na kumuuliza swali papo hapo.

Yes, I’m okay!” Leyla alisema.

“Dah, inaonesha hawa jamaa wamejipanga vilivyo,” nilisema baada ya kuziona bunduki walizokuwa wanazitumia wale jamaa. Zilikuwa bunduki za kivita aina ya M4 Carbine.

Mara nikakumbuka kuwa nilimwahidi Merina kwenda kumsaidia kwani alihitaji sana msaada wangu, nikataharuki. Kwani pamoja na mshtuko niliokuwa nimeupata kutokana na shambulizi lile la ghafla lakini akili yangu ilifanya kazi haraka haraka.

“Leyla, nahitaji gari haraka ili niwahi Serena Beach Resort,” nilimwambia Leyla.

“Kuna nini?” Leyla aliniuliza huku akinitazama kwa wasiwasi.

“Kuna informer wangu anahitaji msaada wa haraka, kuna watu wamemfuata wanataka kumteka,” nilisema huku nikihaha.

“Twende gari lile pale” Leyla aliniambia huku akinionesha gari aina ya Toyota Lexus RX Hybrid jeusi lililokuwa limeegeshwa mbali kidogo kutoka pale Red Brick Restaurant.

Wakati nikilifuata lile gari aina ya Toyota Lexus RX Hybrid, Leyla alikuwa anawapa maelekezo vijana wake kisha akaja mbio kule kwenye gari na kuingia. Akaliondoa gari kwa mwendo wa kasi na kusababisha watu wakimbie kujinusuru baada ya kuuona mwendo aliotoka nao. Tukaingia barabarani kwa fujo bila kufuata sheria za barabarani, hatukuwa na muda wa kusubiri kwani sikutaka tuchelewe na wakati huo huo nikijiweka tayari kwa mapambano, niliamini kabisa kwamba kama ni kweli Merina alikuwa amefuatwa na kuhojiwa kuhusiana na mimi basi lazima huko kungetokea mapambano mengine.

Nilipotazama nje nikaona gari letu likikunja kona na kuingia upande wa pili wa barabara ile ya Mombasa na baada ya mwendo fulani tukaiacha barabara ile na kuingia kulia tukiifuata Barabara ya Ronald Ngala. Muda huo huo tukapishana na magari mawili ya Polisi yaliyokuwa yanaelekea pale kwenye eneo la tukio. Hatukusimama.

Nilishusha pumzi na wakati huo huo nikaanza kutafuta simu yangu ili nimtumie ujumbe Merina kumweleza kwamba tulikuwa mbioni kuelekea hapo Serena Beach Resort lakini sikuiona, nikakumbuka kuwa wakati najirusha kukwepa risasi simu yangu iliniponyoka mikononi mwangu na kuanguka na sikukumbuka tena kuiokota. Nikatweta. Hata hivyo kwa kuwa namba ya Merina niliikumbuka kichwani nikamwomba Leyla simu yake na kutuma ujumbe.

Kisha nikachukua nafasi hiyo kumweleza Leyla kwa kifupi kuhusu uamuzi wangu wa kumtumia Merina kunifanyia upelelezi na ujumbe alionitumia, kisha nikamweleza kuhusu lile gari aina ya Nissan Patrol lilivyotufuata barabara nzima na kisha dereva wa gari hilo kutukosa na risasi, nikamalizia na simu niliyompigia Merina na kugundua kuwa wanaume wawili walimfuata, mmoja akiwa na asili ya Kisomali. Jambo ambalo sikutaka kumwambia Leyla ni kwamba usiku wa kuamkia siku hiyo nililala kitanda kimoja na Merina.

Leyla alishusha pumzi na kunipa pole lakini akiamini kuwa ushindi ungekuwa upande wetu. Kisha aliniambia kuwa baada ya kumaliza kuongea nami kwenye simu aliwatuma vijana wake wawili wawahi kufika pale Red Brick Restaurant kwa ajili ya kuangalia usalama wetu kwa kuwa alihisi kuwa kuna watu ndani ya Idara ya Ujasusi ya Kenya walikuwa wanavujisha taarifa za kiusalama na hata kumfuatilia nyendo zake.

Akaniambia kuwa wakati nafika pale Red Brick Restaurant kwa teksi na yeye pia alikuwa anafika muda huo na aliniona wakati nikiteremka toka ndani ya teksi halafu nikaanza kuongea na simu. Akiwa bado ametulia ndani ya gari lake mara akaliona lile gari aina ya Jeep jeusi likija eneo lile na hapo kengele ya hatari ikalia kichwani kwake na kushuka haraka akiwa tayari kwa mapambano huku akinipigia kelele kunitahadharisha. Bahati nzuri nikawa mwepesi kung’amua hatari na kujiokoa.

Wakati akinielezea hayo gari lilizidi kusonga na mwendo wetu ulikuwa wa kasi ila wa uhakika, Leyla alikuwa makini mno barabarani huku injini ya gari lake ikilalamika kwa kulazimishwa na barabara pia ikilalamika kadri mwendo wa gari letu ulivyokuwa unaongezeka. Magurudumu madhubuti yaliitesa lami ile. Lengo letu lilikuwa moja tu; kuokoa kwanza uhai wa Merina.

Inaendelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

266

Wakati tukiivuka Benki ya Gulf African katika barabara ya Nyali askari wa usalama barabarani wakajaribu kutusimamisha lakini hatukusimama. Taa zote za gari letu zilikuwa zikiwaka, honi ikihanikiza na tukiyachenga magari mengine kama mchezaji wa mpira aliyepania kufunga goli.

Kupitia kioo cha pembeni nikawaona wale askari wa usalama barabarani wakiingia ndani ya gari la Polisi aina ya Land Rover Discovery na kuanza kutufuata huku king’ora kikibweka na kimwelumwelu kikimetemeta. Walituandama, huenda walidhani ni wahalifu. Hata hivyo hatukuwa na muda wa kusimama ili kuwaelewesha. Sasa tulikuwa katika Barabara ya Malindi na mwendo wetu bado haukuwa wa kubahatisha.

Tukaanza kuyapita majengo ya Naivas Supermarket, Nakumatt Nyali Shopping Center, City Mall na CTM Mombasa, hoteli za Mlele Beach, Bamburi Beach Villa na hoteli nyingine nyingi za aina ile zilizokuwa ufukweni mwa Bahari ya Hindi.

Kwa kuwa tulikuwa tumewasha taa zote na honi ikihanikiza hivyo magari mengine yaliyokuwa mbele yetu yakitumia barabara ile ya Malindi yalikuwa yanaegeshwa kando kutuachia njia tupite. Bado gari la polisi lilikuwa nyuma yetu huku king’ora kikiendelea kubweka na kimwelumwelu kikimetemeta. Tukawa kama tuliokuwa kwenye mashindano ya magari. Sisi mbele na gari la polisi nyuma!

Tulizidi kukata upepo na mbele tukalivuka Kanisa la AIC na majengo mengine ya makazi ya watu, ofisi na migahawa mbalimbali, mara tukaliona gari lingine la Polisi aina ya Nissan Patrol likitokea katika barabara iliyokatisha mbele yetu na kujaribu kutuzuia kwa mbele lakini mwendo tuliokuwa nao uliwafanya wasite kuingiza gari lao barabarani.

Na hapo nikajua kuwa walikuwa wamepigiwa simu na wenza wao kuongeza nguvu wakidhani tulikuwa wahalifu.

Tukapita kama risasi na baada ya mwendo wa takriban dakika tatu tukaingia katika barabara ya Serena tukiwa katika mwendo ule ule, na wakati huo huo tukikutana uso kwa uso na gari dogo aina ya Honda la rangi nyeusi ambalo pia lilikuwa katika mwendo wa kasi likitokea ufukweni katika barabara ile ya Serena likitaka kuingia barabara ya Malindi.

Nikamwona Lelya akiuma meno na kuuhamisha haraka mguu wake toka kwenye pedeli ya mafuta na kisha kukanyaga breki huku akijitahidi kulikwepa lile gari ili kuepusha ajali ya kugongana uso kwa uso. Kwa kuwa tukio lile lilikuwa la ghafla na magari yote mawili yalikuwa katika mwendo wa kasi ikawa vigumu, tukaligonga gari lile ubavuni kwa kishindo kikubwa na kusababisha lipinduke na kulala chali, magurudumu yakiwa juu.

Na muda huo huo zikasikia sauti za mayowe ya hofu toka ndani ya lile gari. Hata hivyo, kati ya sauti zile niliweza kuisikia sauti moja iliyotoa yowe kubwa zaidi la hofu na maumivu, sauti ambayo nilihisi kuifahamu vyema, ilikuwa ni sauti ya mwanamke… si mwanamke tu bali ilikuwa ni sauti ya Merina.

Nikashuka haraka toka kwenye gari letu na kukimbilia kwenye lile gari aina ya Mazda lililopinduka, bastola yangu ikiwa mkononi. Na muda huo huo nikasikia sauti ya ving’ora vya magari ya Polisi, lile aina ya Land Rover Discovery na lile aina ya Nissan Patrol yaliyokuwa yakija kasi, yakitimua vumbi. Kisha yakaserereka na kusimama.

Nyuma ya lile gari la Polisi aina ya Nissan Patrol kulikuwa na askari watatu waliokuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vimekingwa na mavazi maalumu yanayozuia risasi maarufu kama ‘bullet proof’. Askari wote walikuwa na sura ya kazi.

Wakati huo huo kutoka ndani ya lile gari aina ya Honda lililopinduka waliibuka wanaume wawili mmoja akiwa na asili ya Kisomali na alikuwa ameshika bastola aina ya Revolver tayari kwa kujihami.

Mara moja nikakumbuka kwamba Merina aliniambia kuwa wanaume wawili mmoja akiwa Msomali walimfuata wakaanza kumhoji kuhusiana na mimi. Nikawaelekezea bastola yangu tayari kwa lolote, na wakati huo huo wale Polisi waliokuwa wakitufukuzia wakatuamuru kujisalimisha huku wakituelekezea mitutu ya bunduki. Sikuwajali na hapo nikamsikia Leyla akijitambulisha kwao.

Mara nikamwona yule mwanamume wa Kisomali ambaye muda huo akili yake ilikuwa kwa wale askari akigeuka na kuniona, akasita huku macho yake yakizungumza waziwazi mawazo yake. Alikuwa akikadiria ingemchukua sehemu gani ya sekunde kuuelekeza mdomo wa bastola yake kwangu na wakati huo huo akijaribu kufikiria ingenichukua sehemu gani ya nukta kukivuta kilimi cha bastola yangu iliyokuwa imemlenga.

Aliponitazama vizuri akaona macho yangu yalivyokuwa yanawaka kwa ghadhabu. Nikamwamuru, “Dondosha bastola yako chini na uinue mikono juu.”

Yule mwanamume wa Kisomali hakusalimu amri na badala yake nikashtuka kumwona akiielekeza bastola yake kwangu kwa kasi na kuachia risasi ovyo. Zote zilipita juu kwani nilishashtukia mchezo na kuwahi kuchutama. Kisha nikaachia risasi moja iliyomsomba mzima mzima na kumtupa chini kama kiroba, akadondoka chini kwa kishindo huku akiwa hana uhai. Kuona hivyo yule mwanamume wa pili akanyoosha mikono yake juu kusalimu amri. Polisi wakamfuata na kumtia pingu.

Nikachungulia ndani ya lile gari na kumwona Merina kwenye kiti cha nyuma amelala akiwa hana fahamu huku akitokwa damu sehemu ya kichwani. Nikaushika ule mlango wa nyuma uliopondeka baada ya kugongwa na gari letu na kuuvuta kwa nguvu, ukasalimu amri, kisha nikamtoa Merina na kumbeba huku nikiwafuata wale askari watatu waliokuwa wamebebelea bunduki na vifua vyao vimekingwa na mavazi maalumu yanayozuia risasi.

“Nahitaji msaada wa kumpeleka haraka huyu binti hospitali,” niliwaambia wale askari. Wakanisaidia, tukampakia haraka kwenye gari aina ya Land Rover Discovery, Leyla akanitaka niondoke na Merina hadi hospitali na nimsubiri hapo, yeye angekuja baadaye. Tukajipakia na gari likaondoka huku likipiga king’ora.

* * *

Inaendelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

267

Saa 7:15 mchana…

Nilikuwa nimeketi kwenye benchi nje ya chumba cha mapumziko katika Kituo cha Afya cha Kisimani alichokuwa amepumzishwa Merina tangu alipofikishwa hapo dakika ishirini na tano zilizokuwa zimepita.

Muda wote nilijiinamia kwa huzuni, mambo mengi yalipita kichwani kwangu nikijaribu kuwaza na kuwazua hili na lile pasipo kupata majibu. Nilimhurumia sana Merina kwani nilikuwa nimemwingiza kwenye hatari ambayo hakuitarajia, na hivyo ilitakiwa alindwe kwa gharama yoyote ili asidhuriwe.

Ni mimi niliyekuwa nimeshauri tumpeleke Merina kwenye hospitali yoyote iliyokuwa karibu kwa kuwa nilihisi alihitaji huduma ya haraka, na hivyo tulipofika Kituo cha Afya cha Kisimani kilicho mkabala na mgahawa maarufu wa Acapulco Club & Restaurant gari lililombeba likaingia hapo. Mara tulipomfikisha pale muuguzi aliyekuwa zamu alipomwona akagutuka, “Mungu wangu! Merina!”

“Vipi unamfahamu?” askari mmoja aliyekuwa na cheo cha Sajenti alimwuliza yule muuguzi.

“Ndiyo. Ni jirani yangu,” yule muuguzi alijibu kwa sauti ya mtetemo.

“Mtazameni kama hajaumia ndani kwa ndani,” nilisema wakati wahudumu wa kituo kile cha Afya cha Kisimani walipokuwa wakimbeba kumpeleka kwenye chumba cha daktari. Na baada ya daktari kumchunguza kwa umakini kwa dakika kadhaa alishauri apumzishwe kwenye chumba maalumu cha mapumziko wakati wakichukua vipimo vingine na akatundikiwa nusu lita ya drip aina ya Dextrose 5% yaliyowekwa dawa maalumu.

Nikiwa bado nipo pale kwenye benchi nje ya chumba hicho cha mapumziko wakati Merina akiendelea kuhudumiwa mara nikaliona lile gari lingine la Polisi aina ya Nissan Patrol likifika pale kituo cha afya na kumshusha Leyla kisha likaendelea na safari yake.

Wakati Leyla akikaribia pale nilipokuwa nimeketi mlango wa kile chumba cha mapumziko ukafunguliwa na daktari akatoka huku akinitazama kwa namna ambayo ilinichanganya kidogo. Alikuwa daktari mwanamke, mrefu, na alikuwa amevaa mavazi rasmi ya kidaktari na kuning’iniza kifaa cha kupimia mapigo ya moyo shingoni. Nikainuka haraka na kumkabili huku nikiwa na wasiwasi nikitaka kujua hali ya Merina.

“Amezinduka na tumemchunguza hajaumia sana isipokuwa alipatwa na mshtuko tu…” yule daktari aliniambia. Kisha akaongeza, “Unaweza kwenda kumwona.”

Kusikia hivyo moyo wangu ukararuka kwa furaha, na hapo nikaharakisha kuingia mle chumbani huku Leyla akinifuata nyuma.

“Jason!” Merina aliniita kwa furaha aliponiona nikiingia mle chumbani, akainuka bila kujali sindano yenye mrija wa drip aliyochomwa mkononi na kujitupa kwenye kifua changu huku akicheka na kulia wakati huo huo. Nilimkumbatia kwa upendo kisha nikampiga piga mgongoni huku nikimwambia kwa sauti ya upole iliyojaa mahaba, “It's okay, baby… It's okay!

Leyla alinitazama kwa namna ambayo ilionesha kuwa alikuwa na wivu juu yangu. Hata hivyo hakufanya chochote. Merina naye alimwona Leyla akashtuka sana na kunitazama machoni akionekana kutaka maelezo. Nikachukua nafasi ile kufanya utambulisho mfupi huku nikimtambulisha Leyla kwa Merina kuwa mtu muhimu aliyesaidia katika kumwokoa yeye Merina baada ya kutekwa na wale watu.

Kisha tuliketi mle chumbani na kuhitaji maelezo toka kwa Merina kuhusu jambo lolote alilolifahamu. Merina alitueleza kuwa siku tatu zilizokuwa zimepita walifika watu wawili pale Serena Beach Resort, walikuwa wageni wa meneja mkuu msaidizi ambaye pia alikuwa meneja matukio.

“Wale wageni walinitia shaka sana tangu nilipowaona mara ya kwanza, walikuwa wanaongea na meneja kwenye eneo la maegesho ya magari lakini hawakuwa wameniona na hivyo nikayasikia maongezi yao,” Merina alisema.

“Walikuwa wanazungumza nini?” nilimuuliza Merina kwa shauku.

“Walikuwa wanazungumza jambo fulani ambalo nahisi lilikuwa la siri na la hatari ambalo lilikuwa limepangwa kufanyika hapa Mombasa katika hoteli ya Bumburi Beach Villa. Sikuweza kusikia vizuri mazungumzo yao lakini miongoni mwa maongezi niliyoyasikia ni kuwa walitaka kumshinikiza Rais aviamuru vikosi vya Kenya vilivyopo Somalia viondoke nchini humo mara moja na kurudi Kenya,” Merina aliweka kituo na kututazama.

Nikaachia tabasamu huku nikibetua kichwa changu kama ishara ya kumhimiza aendelee kuelezea. Leyla pia alifanya vivyo hivyo.

“Niliogopa sana ingawa sikuelewa walipanga kufanya nini, nilitaka nimwambie rafiki yangu mmoja ambaye tunafanya kazi wote pale Serena lakini nikasita sana na kuamua kubaki na siri hiyo moyoni mwangu maana sikuwa namwamini yeyote hadi jana uliponiambia niwe makini kuna watu hatari pale hotelini, nikashawishika kukwamini kidogo, japo bado nilikuwa na mashaka na wewe,” Merina aliniambia.

Kisha Merina alifungua kifungo cha mfuko wa koti la suti yake ya kazini na kutoa bahasha ndogo ya rangi ya kaki.

“Hiyo ni nini?” mimi na Leyla tulijikuta tukimuuliza kwa shauku.

“Bahasha, niliificha baada ya meneja kuidondosha siku hiyo baada ya watu hao kuondoka na kuificha nikidhani kuwa huenda ndani yake kungekuwa na fedha. Hata hivyo nilipoifungua baadaye nikagundua kuwa haikuwa na fedha ila karatasi yenye maelezo ambayo yalinitia uvivu kuyasoma,” Merina alisema na hapo nikaichukua ile bahasha na kuifungua na ndani yake niliiona karatasi nyeupe iliyokunjwa mara tatu, nikaitoa na kuifungua kisha nikaanza kuisoma.

Ilikuwa na maelezo yaliyoandikwa kwa lugha ya kijasusi na hapo nikaelewa kwa nini Merina hakuelewa kilichoandikwa humo. Nilipoyasoma nikashtuka sana.

“Inaeleza nini?” Leyla na Merina walijikuta wakiniuliza kwa pamoja baada ya kuona hali yangu inabadilika baada ya kumaliza kuyasoma maelezo yale kwenye karatasi, nikampa Leyla bila kusema kitu huku nikishusha pumzi ndefu.

Leyla aliisoma ile karatasi na kuonesha kutaharuki sana, “Mungu wangu… ni leo saa kumi jioni?” Leyla aling’aka kwa taharuki baada ya kumaliza kusoma yale maelezo kwenye ile karatasi. “Ni lazima tuzuie tukio hili vinginevyo kutakuwa na umwagaji damu mkubwa na wa kutisha.”

Kisha Leyla alishusha pumzi na kuirudisha ile karatasi ndani ya bahasha na kisha alinipa, nikaitia mfukoni huku nikimkabili Merina.

“Kuna nini?” Merina aliniuliza tena huku uso wake ukiwa umejaa wasiwasi.

“Muda wote ulikuwa umeiweka wapi hii bahasha?” nilimuuliza Merina huku nikimtazama kwa umakini.

“Niliificha na leo asubuhi nikaichukua baada ya wewe kuniomba nikupelelezee pale hotelini kujua nini kinaendelea hasa kwa jambo ambalo ningehisi linatia shaka. Nilitamani sana kukwambia muda ule uliponiambia lakini nikasita. Nikaja kujilaumu baada ya wale wageni wawili waliokuja kunihoji kuhusiana na wewe,” Merina alisema huku uso wake ukiwa umejawa na wasiwasi mwingi. Niliyatafakari maneno ya Merina kisha nikashusha pumzi.

“Kwani kuna nini kimeandikwa humo kwenye hizo karatasi?” Merina akauliza tena baada ya kuona nipo kimya nikiwa nayatafakari maelezo yake.

“Kundi la Al Shabab limepanga kufanya shambulio la kigaidi leo Ijumaa kwenye mkutano wa wafanyabiashara pale Bamburi Beach Villa. Mipango yote ya utekelezaji imeshakamilika na kilichobaki ni utekelezaji tu,” nilimwambia Merina baada ya kufikiria kidogo. Nikamwona akitweta.

Kwenye yale maelezo ilionesha kuwa mipango yote ya kigaidi ilikuwa inaratibiwa na watu watatu, Abdoulkader Omar ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya uratibu wa mkutano huo, Kanali Sultan Jamal aliyekuwa mkuu wa operesheni za ndani wa Usalama wa Taifa nchini Kenya, na Ahmed Kareem, meneja mkuu msaidizi wa Serena Beach Resort. Kanali Sultan Jamal na Ahmed Kareem walikuwa Wakenya wenye asili ya Somalia.

Kilitokea kitambo fulani cha ukimya kisha Leyla alinipa ishara tutoke nje mara moja, na tulipotoka tu akanikabili.

“Jason, narudia tena kusema ahsante sana kwa ujio wako hapa Kenya maana bila wewe sidhani kama haya mambo tungeyajua mapema. Kupitia maelezo hayo nimetambua kwa nini taarifa za kiintelijensia zilikuwa zinawafikia hawa jamaa!” Leyla aliniambia na kushusha pumzi. “Sasa itabidi twende kwa mkuu wangu wa Usalama wa Taifa Kaunti ya Mombasa tukamweleze kila kitu kuhusiana na jambo hili.”

“Huyo mkuu wako unamwamini?” nilimuuliza Leyla huku nikimtazama kwa tuo.

Of course! Ni yeye ambaye amekuwa msaada mkubwa sana kwenye operesheni zangu,” Leyla aliniambia.

Sikutaka kubishana naye. Nikatazama saa yangu ya mkononi na kushtuka. Ilikuwa imeshatimia saa saba na dakika hamsini za mchana, hii ilimaanisha kuwa zilibakia saa mbili na dakika kumi tu kabla ya tukio la kigaidi kutokea, na hivyo hatukuwa na muda wa kupoteza. Kila kitu kilipaswa kufanywa chap chap.

* * *

Inaendelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

268

Mshikemshike…




Saa 9:50 alasiri…

SIKU ilikuwa ingali bado changa lakini jua lilikwisha pamba moto. Kila mmoja alikuwa anavujwa na jasho kutokana na pilika pilika za siku hiyo. Magari ya polisi, askari wa kwenye farasi na mbwa wote walijazana kuzunguka hoteli ya Bamburi Beach Villa, ukiachana na wale waliovaa sare za kazi bado kulikuwa na ambao walifika hapo kiraia na walikuwa na kazi maalumu.

Walinda usalama kutoka kwenye Majeshi ya Ulinzi ya Kenya (KDF) wakiwemo wa Kitengo cha Intelijensia ya Jeshi, Jeshi la Polisi la Taifa (NPS) na Usalama wa Taifa (NIS) walishiriki kikamilifu kuhakikisha kunakuwepo ulinzi wa kutosha.

Makachero wa ndani na nje ya ukumbi walikuwa kwenye shughuli mbalimbali wakihakikisha usalama wa viongozi ambao walikuwa wamefika hapo muda mfupi uliokuwa umepita wakiwa ndani ya ukumbi wa Bamburi Beach Villa kulikotarajiwa kufanyika mkutano wa wafanyabiashara wa nchi za Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika. Hata hivyo ilikuwa vigumu kutambua yupi alikuwa upande upi kwa kuwa wapo makachero waliokuwa wakitumikia pande mbili tofauti (double agents).

Mkutano huo ulikuwa umeandaliwa na Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Afrika Mashariki (EABDA), Benki ya Dunia (WB), Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Shirikisho la Wafanyabiashara Afrika Mashariki (EABF) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) na ulitarajiwa kufunguliwa rasmi na Naibu Rais wa Kenya saa kumi kamili za jioni ndani ya ukumbi wa Bamburi Beach Villa wenye kila aina ya starehe.

Ukumbi huo ulikuwa umejitenga na hivyo kutengeneza mgawanyo mzuri wa starehe tofauti zenye utulivu zinazoweza kufanyika kwa wakati mmoja. Ulikuwa mkubwa wa kisasa wenye uwezo wa kumeza watu wasiopungua mia mbili na hamsini kwa wakati mmoja bila bugudha yoyote, huku ukiwa na meza nyingi ndogo fupi na pana za mbao ya mti wa mninga zilizozungukwa na viti vifupi vyenye foronya laini. Meza hizo zilikuwa zimefunikwa kwa vitambaa visafi vya rangi nyeupe.

Katika meza zile wafanyabiashara kutoka nchi mbalimbali za Pembe ya Afrika, wakubwa na wa kati, walikuwa wameketi kwa utulivu kwenye viti vyao huku wakimsikiliza mshereheshaji aliyekuwa akitoa utambulisho kwa wageni waliokwisha fika. Ukutani kulikuwa na runinga pana na kubwa tatu zilizokuwa zinarusha matukio yaliyokuwa yanayorekodiwa mbashara ndani ya ukumbi ule.

Upande wa mbele wa ukumbi ule kulikoitwa meza kuu, kulikuwa na meza kadhaa fupi za vioo na viti vizuri vya sofa vilivyokuwa vimepangwa katika umbo la nusu duara kuzizunguka meza hizo katika mpangilio mmoja uliovutia.

Miongoni mwa wageni ambao tayari walikuwa wamefika ni pamoja na Mawaziri wote wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Gavana wa Benki Kuu ya Kenya, Gavana wa Kaunti ya Mombasa, Seneta wa Kaunti ya Mombasa, Waziri wa Fedha wa Kenya na Waziri wa Biashara na Viwanda wa Kenya.

Pia walikuwepo mabalozi wa nchi wahisani zinazoongoza kwa kutoa misaada kwa nchi za Afrika Mashariki, Balozi wa Umoja wa Ulaya, wawakilishi wa taasisi za fedha za kimataifa kama Benki ya Dunia (WB), Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB). Na pia waliakwa wafanyabiashara kutoka nchi zinazounda BRICS yaani Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini kuja kueleza uzoefu wao.

Nikiwa mmoja wa wanausalama waliokuwemo mle ukumbini kuhakikisha kunakuwa na usalama wakati wote, nilikuwa ndani ya suti maridadi nyeusi, suti ya gharama iliyotafutwa haraka kwa ajili yangu, niliwekelea kila kitu mwilini mwangu yaani silaha na vitu vingine muhimu.

Leyla pia alikuwa ndani ya suti ya gharama na alikuwa amefanya kazi kubwa mno kuishawishi idara yake ya ujasusi ili niwe miongoni mwa wanaohakikisha ulinzi na usalama ndani na nje ya ukumbi wa Bamburi Beach Villa unaimarishwa ili mkutano wa wafanyabiashara wa Afrika Mashariki ufanyike. Wakati huo Kanali Sultan Jamal alikuwa ameshakamatwa kimya kimya.

Kwa kuwa Abdoulkader Omar ndiye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya uratibu wa mkutano huo aliachwa kwanza ili kuwafanya magaidi wasishtuke mapema kwani kwa kupitia yeye tulipanga kumnasa Abshir na wauaji wenzake. Tuliamini kuwa Abdoulkader Omar kwa kutumia nafasi yake ya uenyekiti wa kamati ya uratibu wa mkutano huo angewapenyeza magaidi hao ndani ya mkutano.

Kwa upande wa Merina, baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali alipelekwa kwenye moja ya nyumba salama kwa ajili ya usalama wake na kisha Mkuu wa Usalama wa Kaunti ya Mombasa alitoa maagizo ya usalama kuzingatiwa.

Kilikuwa kimeundwa kikosi kazi maalumu (special task force) kwa ajili ya kufuatilia na kupambana na ugaidi ambao ungejitokeza kwenye mkutano huo, kwa ushawishi wa Leyla. Kikosi kazi hiki kilikuwa cha siri sana na kilipewa kwa jina la Counterterrorism Surveillance and Security Group (kwa kifupi CSSG).

Kilihusisha maofisa usalama sita tu na tulipewa vitambulisho maalumu vilivyotutambulisha kama walinzi wa usalama wa Bamburi Beach Villa ‘Internal Security – Bamburi Beach Villa’. Kiongozi wa kikosi kazi hiki alikuwa Naibu Mkuu wa Usalama wa Taifa Kaunti ya Mombasa, Joram Kamau (aliyekuwa na utambulisho wa siri ‘code’ wa E01), Leyla (E02), mimi (E03), na Maofisa wengine watatu wa Usalama wa Taifa.

Kama kawaida nilikuwa nimefanikiwa kuzidukua kamera zote za usalama ndani na nje ya ukumbi ule na kuziunganisha na tarakilishi maalumu ambayo pia iliunganishwa na miwani maalumu ya kung’amua sura za wahalifu (detector) ambayo Leyla, mimi na Ofisa mwingine wa Usalama wa Taifa aliyeitwa Dennis Njoroge (E04) tulikuwa tumezivaa, na ndani ya miwani hiyo nilizijaza sura za Abshir na washukiwa wengine, zikiwa katika mionekano tofauti. Ilikuwa ukimhisi mtu unafanya kama unampiga picha tu, ukioanisha, hata kama alikuwa amejibadili vipi, kifaa kile kingemtambua tu.

Kwenye tarakilishi ile kulikuwa na wanausalama wengine wawili, Alfred Arap Sang (E05) na Rajab Chege (E06) ambao walikuwa wajuzi kwenye masuala ya Tehama na walikuwa makini kuzichunguza sura zote mle ndani ya ukumbi na kama wangehisi uwepo wa sura yoyote iliyowatia shaka wangewasiliana na sisi haraka iwezekanavyo.

Nilikuwa nimesimama sehemu ya juu kabisa ya ukumbi ule, na kutoka pale juu niliweza kuuona ukumbi wote kwa uzuri kabisa. Hakuna aliyenijali kwani kila aliyenitazama alikutana na kitambulisho kifuani kwangu kilichoandikwa, ‘Internal Security – Bamburi Beach Villa’.

Kutoka hapo niliposimama nikiwatazama watu ndani ya ukumbi huo, nilimwona mwanamke mmoja wa kizungu akiwa ‘busy’ kuandika andika huku kifuani kwake akiwa amening’iniza kamera kubwa na ya kisasa ya ki-uandishi wa habari aina ya Lumix SFX-20 yenye lensi kubwa ya kuona mbali.

Inaendelea...
 
ufukweni mombasa.JPG

269

Nilimtazama kwa chati na kilichonishtua na kunifanya nivutiwe na mwanamke huyo ni namna ambavyo macho yake yalionesha kuwa alikuwa na hofu na kuna wakati alinitazama kwa chati kama aliyekuwa akinifananisha. Nikampiga picha kwa kutumia ile miwani maalumu na kuzisafirisha mpaka kwenye tarakilishi ili kuoanisha sura yake na sura zilizokuwepo, kifaa kile kikambaini kuwa yule alikuwa ni Rahma wa Singida aliyekuwa amechomekwa mle ndani kama mwandishi wa habari.

Kitendo cha kumwona Rahma wa Singida kikanifanya niamini kuwa hata Abshir alikuwemo eneo lile. “Eko Zero Two!” niliita kupitia kifaa maalumu cha mawasiliano nikimwita kwa dharula Leyla kwa kutumia utambulisho wake maalumu ndani ya kikosi kazi cha CSSG. Herufi ‘E’ tuliitamka ‘Eko’ ili iweze kusikika kwa ufasaha. “Tayari Rahma yupo hapa ndani!” nikaongeza.

Copy!” Leyla alijibu kisha akaanza mchakato wa kumfuatilia Rahma wa Singida na kumdhibiti wakati mimi nikimtafuta Abshir.

Sikutaka kupoteza muda, nikaliacha eneo lile na kuteremka chini zaidi ili nikakae katika eneo ambalo ningeweza kuwaona watu kwa usahihi zaidi. Nikawa natembea taratibu kuufuata (corridor) mmoja, miwani yangu iliendelea kupiga picha na kuzisafirisha mpaka kwenye tarakilishi maalumu ambako waliokuwepo huko walifanya wanachoweza ili kuwatambua wale tuliowataka.

Muda wote nilijitahidi kumsoma (kama scanner) kila mtu aliyekuwepo mahali hapo kujua kama kulikuwa na mtu aliyenitia wasiwasi, mara nikamwona mtu mmoja miongoni mwa wanausalama ambaye kwenye paja la mguu wake wa kulia alining’iniza mfuko maalumu (hoster) uliohifadhi bastola akianza kuja ule upande wangu kitendo kilichoufanya moyo wangu ulipuke kwa hofu kisha kwa tahadhari nikaipapasa bastola yangu kiunoni baada ya kuanza kuhisi hali ya hatari.

Yule mwanausalama alikuwa mweusi, mrefu na mwenye misuli imara mwilini na alikuwa amenyoa upara, alivaa mavazi ambayo kutokana na ukubwa wa mwili wake wenye misuli imara yalionekana kama ambayo hayamtoshi vizuri kwa namna yalivyombana. Aliponiona nikiupeleka mkono wangu kiunoni akawahi kuupeleka mkono wake kwenye hoster huku akinikazia macho kunitazama kwa makini.

Nilimeza fundo kubwa la mate huku nikijitahidi kutabasamu na wakati huo yule mwanausalama alikuwa amenikaribia akizidi kukaza uso wake kunitazama huku taratibu akipunguza urefu wa hatua zake na wakati huo mkono wake mmoja ukiwa bado upo kwenye hoster. Haraka nikagundua kuwa alikuwa akitaka kuitoa bastola yake tayari kukabiliana na chochote.

Hofu ikiwa imeanza kuniingia nikapiga moyo konde na kumeza funda la mate kuitowesha hofu hiyo nafsini mwangu na katika harakati za kurudisha hali ya kujiamini wakati nikipishana na yule mtu nikamuuliza huku nikilazimisha tabasamu la kirafiki usoni mwangu. “Hali ni shwari?”

Yule mwanausalama alisita kwanza, macho yake yalikuwa makini kusoma kitambulisho changu maalumu kilichokuwa kikining’inia kifuani kilichonitambulisha kama mlinzi wa usalama wa Bamburi Beach Villa. Nikamwona akishusha pumzi huku taratibu akiutoa mkono wake kwenye hoster. “Shwari kabisa.”

Aliongea kwa sauti tulivu na kuendelea na safari yake. Muda huo moyo wangu ulikuwa ni kama ulioshikwa na ganzi. Hata hivyo nilijitahidi kwa kila namna kuimeza hofu yangu huku nikiendelea kutembea huku macho yangu yakiwa makini zaidi.

Mara nikawaona wanausalama wengine wawili waliovaa suti nyeusi wakiwa wanawasiliana kwa siri sana kwa namna ambayo niliamini hawakutaka wengine wafahamu. Macho yao yalikuwa yamefichwa vizuri nyuma ya miwani nyeusi. Kisha wakaanza kupanda haraka haraka kuelekea kule juu nilikotokea, nilipowatazama haraka nikatambua kuwa walikuwa na ajenda fulani isiyo ya kawaida kutokana na mwonekano wao. Kengele ya hatari ikalia kichwani kwangu na mapigo ya moyo wangu yakaongezeka kasi.

Sikutaka kuzipuuza hisia zangu, nikaamua kuwapiga picha kwa wizi kwa kutumia ile miwani maalumu na kuzisafirisha mpaka kwenye tarakilishi ili kuoanisha sura zao na sura zilizokuwepo. Kifaa hicho hakikumbaini yeyote lakini bado niliendelea kuwa na mashaka nao. Nilipogeuka kuwatazama nikawaona wakiishia kwenye ukumbi mmoja.

Sikusubiri sekunde wala nukta, nikabadili uelekeo na kuanza kurudi kwenye zile ngazi ili niwafuatilie huku nikitoa taarifa kwa wenzangu. Nilipofika juu nikasimama hapo ukumbini na kuangaza macho huku na kule huku nikiyatega vizuri masikio yangu, sikuwaona. Nikajiuliza wangekuwa wameelekea wapi? Mara nikapata wazo la kuufuata mlango wa kuingia ndani ya chumba cha usalama ambacho kilikuwa na tarakilishi zinazoongoza mfumo mzima wa kamera za usalama ndani ya ukumbi.

Niliufikia na kushika kitasa cha mlango, nikakinyonga nikijaribu kuufungua mlango huo kwa tahadhari. Mlango ukafunguka, nikaingia ndani haraka na kuufunga mlango nyuma yangu nikiwa tayari kwa lolote. Lakini ghafla nikasimama na macho yangu yakatua juu ya miili ya wanausalama watatu waliolalia dimbwi la damu. Nikataharuki huku nikiitazama vyema miili ile ya wanausalama wale na kujiridhisha kwa macho kuwa hawakuwa na uhai.

Kabla sijajua nifanye nini nikajikuta nikitazamana uso kwa uso na mtutu wa bastola aina ya FNX 45 Tactical kutoka kwa yule mwanausalama mweusi mwenye mavazi yaliyombana mwili, bastola yake ilifungwa kiwambo maalumu cha kuzuia sauti na ilikuwa inafuka moshi, na hapo nikatambua kuwa ni yeye aliyefanya mauaji hayo ndani ya kile chumba cha tarakilishi zinazoongoza mfumo mzima wa kamera za usalama ndani ya ukumbi. Mwili wangu ukaingiwa na ganzi huku nikipigwa na bumbuwazi.

“Sahamani mkuu, kumbe upo humu basi ngoja mimi nielekee upande mwingine,” niliongea kwa kujiamini huku nikitaka kutoka lakini yule bwana akanizuia.

“Huendi kokote, jasusi,” alisema huku akinielekezea mtutu kichwani, alionesha kuwa hatanii na angeweza kunilipua wakati wowote endapo ningeonesha ukaidi. Hata hivyo nikapiga moyo konde na kujitahidi kuitoa hofu moyoni mwangu ingawa dalili zote ziliashiria kuwa mambo hayakuwa shwari.

“Kwani vipi, mkuu! Naamini mimi na wewe hatuna tofauti yoyote!” nilimwambia yule mtu kwa jazba kidogo.

“Usijidanganye, Jason… usidhani kuwa hatukufahamu vizuri wewe ni nani,” yule mtu alisema huku akiangua kicheko hafifu cha dhihaka. Kauli yake ikanifanya nitambue kuwa nilikuwa nikifahamika vizuri na yule mtu kuliko vile nilivyokuwa nikidhani.

“Mbona sikuelewi unaongea nini?” nilimuuliza yule mtu kwa hasira za kudhihakiwa.

“Usijali, nilidhani kuwa ungeendelea kuwa mwerevu na kuruka kiunzi hiki,” nilisikia sauti nyingine kavu ya kiume kutoka nyuma yangu ikizungumza kwa utulivu hali iliyonishtua na kunifanya nigeuke haraka kutazama nyuma yangu na kwa kufanya vile nikajikuta nikitazamana na na mitutu miwili ya bastola iliyoshikiliwa na wale wanausalama wawili niliokuwa nawafuatilia baada ya kuwatilia shaka.

Bastola zote zilikuwa zimefungwa kiwambo maalumu cha kuzuia sauti. Moyo wangu ukapiga kite kwa nguvu na kijasho chepesi kikaanza kunitoka mwilini.

Sasa nilikuwa na hakika kuwa nilikuwa nimejiingiza mwenyewe kwenye himaya ya adui pasipo kujua. Wale watu walikuwa wananitazama kwa tabasamu jepesi la ushindi wenye dhihaka na kejeli.

Kwa kweli sikuwa nimetarajia kabisa kuwa wanausalama kama wale wangeweza kuwa mamluki waliopandikizwa ili kufanikisha mpango haramu. Sasa hisia zangu ziliniambia kuwa nilikuwa nimekutana na watu hatari sana katika harakati za kijasusi.

Inaendelea...
 
Back
Top Bottom