Simulizi: Harakati za Jason Sizya

Simulizi: Harakati za Jason Sizya

taharuki..jpg

333

Mpambano mwingine…




Saa 7:00 usiku…

MVUA kubwa ilianza kunyesha sambamba na upepo wa wastani na hivyo kuifanya sehemu kubwa ya Jiji la Dar es Salaam kwa wakati huo wa usiku kutawaliwa na hali ya baridi. Hii ilitokea muda mfupi tu tangu tulipofika kwenye nyumba za maofisa wa Usalama wa Taifa eneo la Makumbusho, nyumbani Pamela.

Tulipofika hapo Pamela hakutaka niondoke kama alivyoniambia hapo awali kuwa nimpitishe kisha ndiyo nielekee nyumbani kwangu Upanga, na badala yake kupitia ushawishi wake kama mwanamke tukajikuta tukitumbukia tena kwenye mtego mwingine wa mapenzi mazito.

Yalikuwa mapenzi motomoto yaliyonifanya nitamani kuitangazia dunia kuhusu utamu wa mwanamke huyo. Pamela alikuwa mwanamke mtundu sana aliyejua jinsi ya kucheza vizuri na hisia za mwanaume na kwa kweli aliniwezea sana na kunifanya nisahau mikasa yote niliyokuwa nimekumbana nayo katika harakati za kumsaka Bosco Gahizi na wenzake.

Mara tu tulipoingia nyumbani kwake tukaanzia bafuni tulikokwenda kuoga ili kutoa uchovu na kuipoza miili yetu na tukiwa huko bafuni Pamela akaanza vitimbi vyake vya hapa na pale. Wakati tukioga kwenye bomba la mvua alinivuta na kunikumbatia huku akiipitisha mikono yake nyuma ya shingo yangu na kufanya joto kali la mwili wake linipe faraja kubwa.

Nilishindwa kuvumilia, nami nikazungusha mikono yangu kumshika kiunoni kisha nikawa nakiminya minya kiuno chake. Tukatazama machoni kisha tabasamu maridhawa likachomoza kwenye nyuso zetu. Kisha Pamela akapeleka mkono wake kwenye malighafi zangu na kuanza kuzitomasa kwa namna ya kunipandisha mdadi halafu akaanza kunichua taratibu mshumaa wangu katika namna ya kuamsha vilivyolala, kwa kweli sikuweza kukivumilia kitendo kile, nikaamua kumpelekea moto huko huko bafuni.

Na tulipomaliza ngwe moja tukaoga na kisha tukaelekea chumbani ambako sasa kila mmoja alikuwa amempania mwenzake, maana tulipoingia tu chumbani Pamela akaanza uchokozi, nikambeba na kumtupia kitandani huku wote tukiangua vicheko hafifu vya mahaba. Kisha kama watu tuliopandwa na wazimu wa mapenzi tukaingia mchezoni na muda mfupi uliofuata tulijikuta tukimezwa na ulimwengu wa huba. Ilikuwa ni kama sinema ya kusisimua yenye kila aina ya vionjo vya kumtoa nyoka pangoni.

Tulikuwa kwenye ulimwengu mzito wa mapenzi na dunia ilikuwa kama kisiwa cha raha kwa ajili yetu. Tukizisahau shida zote. Pamela alikuwa amezitendea vyema hisia zangu na raha tuliyoipata macho yetu hayakuweza kutazama. Muda huo hatukukumbuka kitu kingine chochote isipokuwa kuivunja amri ya sita, huku mapenzi yakionekana kunoga kwa namna yake na miguno ya mahaba ikihanikiza kila mahali mle chumbani.

Tulivingirishana kwa sarakasi za aina yake pale kwenye uwanja wa sita kwa sita huku mechi yetu ikitawaliwa na rafu za kila aina kwa kuwa mchezo wetu haukuwa na refa wala kamisaa, na kila mtu alijaribu kuonesha ufundi wake pasipo kujali kama alikuwa anafuata sheria za mchezo au la.

Nilicheza sana rafu kwa kuwa nilikuwa nimegundua hila ya Pamela kuwa aliamua kutumia utundu wa hali ya juu ili kunifanya niongee lugha aliyoitaka, kwani Waswahili husema kuwa “kichwa cha chini kikisimama cha juu huwa hakifanyi kazi sawa sawa.”

Tulipambana kwa takriban saa nzima na hatimaye mchezo wetu ulifika tamati huku wote wawili tukiwa hoi kabisa, kila mmoja wetu akionekana kutosheka na mwenzake.

_____



Saa 3:30 asubuhi…

Nilishtuka toka katika usingizi wa fofofo na kuyafumbua macho yangu taratibu kisha nikayatembeza mle chumbani kuangalia huku na kule nikijaribu kusikiliza kwa umakini. Sikujua kitu gani kilikuwa kimenishtua na kuukatisha ghafla usingizi wangu uliokuwa umenichukua ghafla! Ilikuwa ni siku nyingine na muda huo tulikuwa bado tumelala.

Nilipotupa macho yangu kando nikagundua kuwa hata Pamela pia alikuwa bado amelala fofofo. Kwa mbali nilisikia sauti hafifu ya mkoromo wake wa uchovu. Nikaitupia jicho saa yangu ya mkononi na kushtuka. Muda huo miale ya jua la asubuhi ilikuwa inapenya dirishani na kutuama pale kitandani tulipolala.

Kwa mara kwa kwanza tangu nianze harakati za upelelezi kuhusu tukio la kigaidi lililosababisha kuteketea kwa jengo la Alpha Mall nilikuwa nimelala usingizi mtamu sana wa kueleweka kiasi cha kuchelewa kuamka.

Hakika penzi zito la Pamela lilikuwa limeamsha ari mpya nafsini mwangu na kupitia ukaribu ule kitu fulani kilikuwa kimeanza kujengeka moyoni mwangu. Hata hivyo tumbo langu lilikuwa dhaifu sana kwa njaa. Njaa ilikuwa inauma sana utadhani nilikuwa na vidonda tumboni na kichwa changu kilinivangavanga sana.

Kichwa kilikuwa kizito sana mithili ya mtu aliyekuwa ametwishwa kiroba cha mchanga na nilihisi kuchoka mno, kichwani nilikuwa na mawenge ya usingizi yaliyonipa hali ya kutaka kuendelea kulala. Pilika pilika za siku iliyotangulia, pombe kali na ukichanganya na mahaba mazito basi hali ikawa si hali.

Hata hivyo, akilini mwangu niliutaka utulivu kwa gharama yoyote ile japo nipate kupumzisha mwili na kupata japo lepe la usingizi. Nilichotamani ni kulala tu mpaka pale ambapo mwili wangu ungeniruhusu kuamka. Niliuhisi uzito wa kichwa changu na mawenge ya usingizi yakinitesa na hivyo hali hiyo ilikuwa inanipa hali ya kutaka kuendelea kuuchapa usingizi. Lakini sasa nilijikuta nimeamka na sikujua nini kilikuwa kimeniamsha.

Nikayatega masikio yangu kwa umakini kusikiliza na hapo nikagundua kuwa sauti ya simu yangu ya mkononi iliyokuwa ikiita kwa fujo ndiyo iliyonishtua kutoka usingizini. Nikaitazama na kuiona namba ngeni, nikataka niipuuzie lakini hisia zangu zikaniambia kuwa ilikuwa simu muhimu sana. Nikaipokea na kuipeleka sikioni.

“Hallo!” nilisema kivivu vivu na kushusha pumzi ndefu.

“Jason!” sauti ya mkurugenzi mkuu iliita kutoka upande wa pili wa simu. Nikashtuka sana na kujikuta nikiinuka toka pale kitandani na kuketi kitako.

“Naam. Shikamoo, mkuu!” nilisalimia kwa unyenyekevu mara tu nilipogundua kuwa nilikuwa naongea na mkurugenzi mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa aliyeamua kunipigia simu moja kwa moja.

“Marahaba, Jason, habari za tangu usiku?” mkurugenzi mkuu aliniuliza kwa upole kama mzazi anayeongea na mwanawe wa kwanza, mara tu baada ya kumuoza mke.

“Salama, mkuu,” nilimjibu mkurugenzi mkuu kwa unyenyekevu.

“Sasa ni hivi… Mheshimiwa Rais anakupongeza sana kwa kazi uliyoifanya ambayo imetusaidia kuubaini mtandao hatari wa kihalifu, yeye pia anakubali sana uwepo wako katika idara nyeti kama hii… nimetoka kuzungumza naye sasa hivi na kuna jambo ameniambia…” mkurugenzi mkuu alisema na kunyamaza kidogo kuruhusu mate yapite kohoni mwake.

Muda huo huo nikamwona Pamela akishtuka na kunitazama usoni kwa aibu, alipogundua kuwa nilikuwa naongea na simu akajiinua na kusogea karibu yangu ili asikie.

“…Waswahili wanasema ‘mcheza kwao hutunzwa’. Hivyo wewe na wenzako Luteni Lister na Pamela mnatakiwa leo saa saba mchana muwepo Ikulu kuonana na Mheshimiwa Rais, ana mambo mazuri ya kuongea nanyi. Naomba mwambie na Pamela, najua uko naye,” mkurugenzi mkuu alisema.

Pamela ambaye muda huo alikuwa ameweka sikio lake kwenye simu yangu kusikiliza akashtuka sana na kuweka kiganja cha mkono wake mdomoni kuziba mdomo kwa woga, huku akinikodolea macho.

“Sawa mkuu. Nashukuru sana kwa taarifa hii, nashukuru sana sana…” nilisema kwa unyenyekevu. Haha…! niligundua kuwa mkurugenzi mkuu alishakata simu wakati nikiendelea kushukuru. Kisha mimi na Pamela tukatazama na kucheka.

Huu ni mwisho wa Msimu wa Sita kwenye mfululizo wa Harakati za Jason Sizya. Usikose Msimu wa Saba katika mkasa uitwao “Utata”.
 
Asante sana askofu kwakweli una namna unasimulia ambayo haielezeki nlikua natamani kuuliza khs mkuu Koba na yule secretary wa Jason lakini acha nikae kwa kutulia pengine yatajibika utatani...asante sana mkuu
 
Asante sana askofu kwakweli una namna unasimulia ambayo haielezeki nlikua natamani kuuliza khs mkuu Koba na yule secretary wa Jason lakini acha nikae kwa kutulia pengine yatajibika utatani...asante sana mkuu
Haha! Ni kweli bado kuna "Utata". Endelea kufuatilia...
 
Nilianza na SAFARI YA BUZWAGI iliyonihakikishia ajira ndipo nikasema kuwa NARUDI BUZWAGI kujiandaa na FUNGATE ambalo lilikuja kumleta MGENI MWEMA ambaye hatimaye akafunga safari nyingine kwenda kupumzika UFUKWENI MOMBASA na aliporudi ikazuka TAHARUKI kubwa inayokwenda kuishia kwenye UTATA...

Dah, sijui itakuwaje. Tusubirie...
 
Nilianza na SAFARI YA BUZWAGI iliyonihakikishi ajira ndipo nikasema kuwa NARUDI BUZWAGI kujiandaa na FUNGATE ambalo lilikuja kumleta MGENI MWEMA ambaye hatimaye akafunga safari nyingine kwenda kupumzika UFUKWENI MOMBASA na aliporudi ikazuka TAHARUKI kubwa inayokwenda kuishia kwenye UTATA...

Dah, sijui itakuwaje. Tusubirie...
Pamoja sn mkuu[emoji120]
 
View attachment 2392257
330

Niliporudia tena kuitazama sura ya yule mtu mara moja nikahisi kumfahamu lakini tatizo likaja, ni nani na nilimwona wapi? Hata hivyo sikutaka kuendelea kujiuliza kwa kuwa nilijua kuwa eneo lile halikuwa eneo salama hivyo muda wote nilitakiwa kuwa katika tahadhari kubwa sana. Nikawasiliana na akina Luteni Lister kupitia kile kifaa maalumu cha mawasiliano kuwauliza kama walikuwa wanaona chochote, wakaniambia kuwa walikuwa wanaona kila kitu kupitia ile runinga ndogo iliyofungwa ndani ya lile gari.

Nikawaambia kuwa nilikuwa napanga kuingia mle ndani, hivyo Luteni Lister awe tayari kuja kulinda usalama wangu wakati nikigonga pale kwenye geti. Na wakati huo nikimtaka Pamela abakie kwenye gari ili kama ingetokea dharura yoyote basi aweze kuwasiliana na makao makuu kwa ajili ya msaada. Kisha nikaanza kulisogelea lile geti huku nikiwa makini halafu nikabonyeza kitufe cha kengele ya getini, nikaisikia kengele ikiita kule ndani. Nikasimama kwa kujiamini pale getini nikiifanya sura yangu ionekane ya kawaida isiyo na wasiwasi wowote.

Kupitia simu yangu ya mkononi niliyokuwa nikiitazama kama niliyekuwa naperuzi mitandao ya kijamii, nikamwona yule mlinzi akishtuka na kuipapasa bastola yake kiunoni kisha akawa kama aliyekuwa anasikilizia. Kitendo kile kikanifanya nirudie kubofya tena ile swichi ya kengele kwa mara ya pili, na hapo nikamwona yule mlinzi akiinuka haraka na kugeuka kuitazama ile runinga kubwa iliyokuwemo ndani ya kibanda cha mlinzi, aliitazama kwa makini kwa sekunde kadhaa, na hapo akaniona wakati nilipokuwa nimesimama pale nje ya geti nikiwa sina wasiwasi wowote.

Nikamshuhudia akijaribu kuwa makini kunitazama huku akiwa kama aliyekuwa akinitathmini. Sikujua alikuwa anawaza nini. Kisha nikamwona akishusha pumzi, huenda mavazi yangu ya gharama, suti nzuri ya kijivu niliyokuwa nimeivaa na kofia ya pama kichwani na namna nilivyokuwa nimesimama kwa kujiamini pale nje ya geti vilimchanganya.

Muda huo nilikuwa naomba asije akanishtukia, na nilijiuliza haraka haraka vipi endapo angenishtukia ningefanya nini! Lakini kabla sijapata jibu nikamwona akipiga hatua kuja pale getini. Alipofika pale getini akalifungua lile geti na hapo akajikuta akitazamana nami uso kwa uso, akanitazama kuanzia chini hadi juu kwa macho yenye kuashiria shari muda wote. Nikamtambua.

Nilijikuta nikitazamana uso kwa uso na yule mwanamume mrefu aliyekuwa amevaa ovaroli la rangi ya samawati, kofia ya pama ya rangi ya samawati aliyoishusha hadi usawa wa macho ili kuficha paji la uso wake, miwani mikubwa myeusi iliyoyafunika macho yake na buti ngumu miguuni aina ya ‘safari boot’ za rangi ya hudhurungi, aliyefika kwenye jengo la Alpha Mall na kuegesha pikipiki yake ya magurudumu matatu kwenye nafasi finyu iliyokuwa katikati ya magari ya Waziri Ummi Mrutu na Daniel Kayera!

Ndiyo… alikuwa yeye na niliweza kubaini kuwa macho yake yalikuwa na dalili zote za ukatili, dharau, unyama na dhihaka ya hali ya juu. Dah…! Mara moja nikajikuta nikisisimkwa mwili wangu na damu ikaanza kumchemka na kukimbia kwenye mishipa yangu ya damu, vinyweleo mwilini na nywele kichwani zikanisisimka kwa hasira na hali ile ikasababisha mapigo ya moyo wangu yaanze kwenda mbio! Nikapeleka mkono wangu kiunoni kwa uficho kuipapasa bastola yangu.

“Nikusaidie nini, ndugu?” yule mlinzi aliniuliza kwa sauti yake nzito inayokwaruza huku akinitazama kwa umakini usoni.

Akili ya haraka haraka ikanijia kwamba nilipaswa kufanya jambo la haraka pasipo kuchelewa kwani sikuwa na muda, hivyo badala ya kumjibu kwa maneno, kwa kasi ya aina yake nikampiga ngumi nzito ya usoni iliyomfanya apepesuke. Kufumba na kufumbua nikaruka na kumpiga teke kali sana la shingo lililomtupa mita kadhaa.

Haraka sana nikatoa bastola na kuishika vizuri tayari kwa kummaliza endapo angeleta matata, lakini nikamwona akiwa ametulia. Nilikuwa nimempiga teke baya sana la shingoni na hivyo sikuwa na imani kama angeweza kuamka tena kwa pigo lile. Hata hivyo bado sikuwa na imani naye, nikasimama na kumwangalia kwa umakini pale chini alipokuwa amelala kimya kisha nikamwendea kwa tahadhari na kumchunguza. Nikagundua kuwa mapigo ya moyo wake yalikuwa yanapiga kwa mbali kuashiria kuwa alikuwa bado ana uhai.

Muda huo huo nikahisi kama kulikuwa na mtu mwingine nyuma yangu, nikageuka haraka huku nikiruka kando na kwa kufanya vile macho yangu yakakutana na macho ya Luteni Lister akiwa amesimama akinitazama kwa tabasamu.

Good job,” Luteni Lister alisema. Sikujibu kitu nikasimama na kuangaza angaza ndani ya ule uzio mpana na lile jumba la kifahari, kisha ndani ya kile kibanda cha mlinzi kuona kama kulikuwa na chochote ambacho kingeweza kutusaidia lakini hakukuwa na chochote cha maana kuweza kutusadia kwa wakati ule.

Kwa kusaidiana na Luteni Lister tukamfunga pingu miguuni yule jamaa na kumvutia ndani ya kile kibanda cha mlinzi kisha tukampekua haraka haraka na kumkuta akiwa na bastola mbili, kete kadhaa za dawa za kulevya na kitambulisho cha kazi kilichoonesha kuwa alikuwa akiitwa Luis Ryoba, mwajiriwa wa kampuni ya ulinzi ya Gadi Security Agency kama mlinzi maalumu.

“Hii kampuni ya ulinzi ya Gadi Security Agency itabidi ichunguzwe ili tujue ni ya nani na ina uhusiano gani na mtandao huu hatari,” nilimwambia Luteni Lister kisha nikaongeza, “Sasa… mimi natangulia kuingia ndani kwa kutumia mlango huo mkubwa wa mbele. Naomba unilinde.”

Na hapo, kwa tahadhari ya aina yake, nikakiacha kile kibanda cha mlinzi na kuanza kuelekea pale barazani lakini machale yakanicheza nikaamua kubadili uelekeo na kuanza kutembea kwa tahadhari kuelekea upande wa kulia wa ile nyumba nikiizunguka katika namna ya kupata uhakika wa hali ya usalama wa eneo lile. Bastola yangu ikiwa mkononi, sikutaka tena kurudi nyuma.

Wakati nikitembea niliyatembeza macho yangu kupeleleza mandhari ya ile nyumba. Ilikuwa nyumba kubwa ya kisasa ya ghorofa mbili yenye madirisha makubwa ya kisasa na baraza kubwa mbele yake iliyopangwa seti moja ya makochi ya sofa.

Sehemu ya mandhari ya nyumba ile ilizungukwa na miti midogo kadhaa na miwili mikubwa ya kivuli na matawi ya miti ile usiku ule yalikuwa makubwa yaliyotengeneza vichaka vya giza la kutisha. Sehemu ya mbele ya ile nyumba ilikuwa imezungukwa na bustani nzuri ya maua ya kupendeza na katikati ya bustani ile kulitengenezwa njia nzuri ya kutembea kwa miguu kwa vitofali vidogo vinavyovutia.

Bastola yangu ikiwa imetulia vyema kwenye kiganja cha mkono wangu wa kulia nilizidi kusonga mbele kwa tahadhari huku masikio yangu yakiwa makini kusikiliza kama mbwa mwindaji. Nilichogundua ni kwamba nyumba ile ilikuwa kimya kabisa na hapakuwa na dalili zozote za uwepo wa kiumbe hai mle ndani, hisia zangu zikaniambia vile, hata hivyo sikutaka kuridhika na hali ile.

Mwishowe nikaifikia sehemu ya nyuma ya ile nyumba na kuanza kupanda ngazi chache za kibaraza cha nyuma kuelekea mlango wa nyuma wa nyumba ile, halafu nikageuka na kumwona Luteni Lister akiwa amejibanza katika pembe fulani akiwa makini kufuatilia nyendo zangu. Nikiwa pale kwenye baraza ya jikoni nikatafuta japo upenyo na kuchungulia ndani lakini sikuweza kuona chochote kwa sababu mle ndani kulikuwa na giza. Taratibu nikausogelea ule mlango na kutega sikio langu, bado hapakuwa na dalili zozote za uwepo wa kiumbe hai.

Endelea...
Tuko
Nilianza na SAFARI YA BUZWAGI iliyonihakikishia ajira ndipo nikasema kuwa NARUDI BUZWAGI kujiandaa na FUNGATE ambalo lilikuja kumleta MGENI MWEMA ambaye hatimaye akafunga safari nyingine kwenda kupumzika UFUKWENI MOMBASA na aliporudi ikazuka TAHARUKI kubwa inayokwenda kuishia kwenye UTATA...

Dah, sijui itakuwaje. Tusubirie...
Na bado utata utaibua kisa kingine. Hii straight forward umeitendea haki .big up bishop
 
Nilianza na SAFARI YA BUZWAGI iliyonihakikishia ajira ndipo nikasema kuwa NARUDI BUZWAGI kujiandaa na FUNGATE ambalo lilikuja kumleta MGENI MWEMA ambaye hatimaye akafunga safari nyingine kwenda kupumzika UFUKWENI MOMBASA na aliporudi ikazuka TAHARUKI kubwa inayokwenda kuishia kwenye UTATA...

Dah, sijui itakuwaje. Tusubirie...
Shukran sana bishop,naamini washabiki wako kindakindaki tuna maswali lakini naamini yatajijibu mbeleni,afande koba,secretary wake Jason nafikiri utatuondolea huu utata!
 
Nilianza na SAFARI YA BUZWAGI iliyonihakikishia ajira ndipo nikasema kuwa NARUDI BUZWAGI kujiandaa na FUNGATE ambalo lilikuja kumleta MGENI MWEMA ambaye hatimaye akafunga safari nyingine kwenda kupumzika UFUKWENI MOMBASA na aliporudi ikazuka TAHARUKI kubwa inayokwenda kuishia kwenye UTATA...

Dah, sijui itakuwaje. Tusubirie...
Kongole kwako Bishop huwa na furahia Sana kazi zako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukran sana bishop,naamini washabiki wako kindakindaki tuna maswali lakini naamini yatajijibu mbeleni,afande koba,secretary wake Jason nafikiri utatuondolea huu utata!
Kubaki na maswali ndo kunakoleta mshawasha na raha ya stori. Hata hivyo mtakachokutana nacho ni UTATA mtupu...
 
Nilianza na SAFARI YA BUZWAGI iliyonihakikishia ajira ndipo nikasema kuwa NARUDI BUZWAGI kujiandaa na FUNGATE ambalo lilikuja kumleta MGENI MWEMA ambaye hatimaye akafunga safari nyingine kwenda kupumzika UFUKWENI MOMBASA na aliporudi ikazuka TAHARUKI kubwa inayokwenda kuishia kwenye UTATA...

Dah, sijui itakuwaje. Tusubirie...
Dah, Kiukweli imekua ni muendekezo wenye kuburudisha sana. Ubarikiwe sana mkuu
 
Kubaki na maswali ndo kunakoleta mshawasha na raha ya stori. Hata hivyo mtakachokutana nacho ni UTATA mtupu...
Kwa kweli ndio raha ya story zako,na mume wa muheshimiwa waziri sijui atabinjukiwa hukohuko south?wacha tukusubirie mtaalamu wetu utujibie haya maswali!
 
Haha! Naona umeamua kutangulia mbele, mkuu. Leo nina nafuu kidogo. Baadaye kidogo nitashusha vitu..
Naam shida ya hawa watu unapewa kazi alafu nyuma unapewa mtu wa kujufutilia kushindwa kwako na kushinda...na unichi wako!! Unafekishaje kazi ya 100% kuwin? Lazima upotee
 
Haha! Naona umeamua kutangulia mbele, mkuu. Leo nina nafuu kidogo. Baadaye kidogo nitashusha vitu..
Pole sana mkuu, Mungu akuponye chaaap kwa haraka hakika unatupa burudani na mafundisi...somo la kunusa hatari ni muhimu sana hata kwa maisha ya kawaida sio lazima uwe kipenyo.
 
Shukrani saaana! Umalaya wa Jason jamani! Ananikera mimi huyu!
 
Ungetuacha na utata ata kidogo mkuu na sio hili fukuto arosto unalotuachia
 
Back
Top Bottom