354
Nililiridhika na kile chumba, nikarudi kwenye chumba cha tiba alimolazwa yule mateka na kusimama kando ya kitanda, nikamtazama kwa sekunde kadhaa na kushusha pumzi.
“
Now it’s just me and you. Today I’m your angel of death,” nilimwambia yule jamaa kuwa siku hiyo nilikuwa malaika wake wa kifo endapo asingesema ukweli, nikamwona akinitazama kwa macho yaliyotia huruma.
Nikamweka kwenye kitanda cha kusukuma kilichokuwa na magurudumu, pasipo kujali malalamiko yake kuwa alikuwa anaumia, kisha nikakisukuma kile kitanda hadi kwenye kile chumba cha mahojiano, nikamlaza yule jamaa juu ya kile kitanda chembamba cha chuma chenye mikanda imara, mnyororo mfupi na pingu za miguuni na mikononi za chuma, halafu miguu na mikono yake nikaifunga kwa mikanda imara pasipo kujali kama alikuwa anaumia.
Nilifanya vile kwa sababu nilifundishwa kutomwamini mtu yeyote hata marehemu, hivyo nilipohakikisha mateka wangu hawezi kuleta tabu yoyote nikavuta kiti kimoja na kukiweka mbele ya mateka huyo, nikaketi juu yake na kumtazama.
“
Now tell me, where is the President…?” nilianza kumuuliza yule jamaa nikitaka anieleze mahali walipomficha Rais lakini akanikatisha.
“
Go to hell!” yule mateka aliniambia kwa dharau huku akijaribu kunitemea mate usoni, lakini alikuwa dhaifu na hivyo yale mate hayakufika kwenye uso wangu. Nikamtazama na kuachia tabasamu.
“Ninakukumbusha kuwa hapa ulipo ni nusu ya jehanamu kwa hiyo nataka unijibu kiufasaha kila nitakachokuuliza na kitakachokuokoa utoke humu ndani ukiwa hai ni ukweli tu…
Tell me the truth and you’ll get out of here alive,” nilimwambia yule mateka kwa sauti tulivu.
“
You go to hell. Huna hadhi ya kunihoji, kwanza nakuhurumia sana kijana sijui kwa nini unakubali kutumiwa kirahisi namna hii? Tafadhali achana na huu upuuzi unaoufanya na umwambie aliyekutuma kwamba hawezi kupambana na sisi,” yule jamaa alisema kwa dharau
“Ninyi ni akina nani? Na mmempeleka wapi Rais?” nilimuuliza kwa sauti tulivu pasipo kujali dharau zake.
“Unajisumbua sana asee!” yule jamaa alijibu kijeuri. “Sijui kwa nini unakuwa mgumu kunielewa? Kwa nini unaendelea kuhatarisha maisha yako na kuiweka familia yako katika matatizo makubwa? Tambua kwamba ndani ya muda mfupi ujao utajutia hiki unachokifanya.”
“Kuhatarisha maisha yangu ndiyo jambo ninalolipenda zaidi, na pia huwa napenda kukutana na watu wenye dharau na wanaojiamini kama wewe,” nilimwambia yule mtu huku nikichukua kitu kama mkasi chenye ncha kali sana.
“Sasa unataka kuni-kunifanya ni-ni-nini wewe?” yule jamaa aliuliza kwa woga.
“Usijali, we si jeuri na hutaki kujibu maswali yangu kwa upole, sasa utajibu kwa njia hii!” nilimwambia yule jamaa na wakati huo huo nikashusha kwa nguvu ule mkasi na kuuzamisha kwenye nyama ya paja lake la mguu wa kulia.
"Aaarrrggghhh!” yule jamaa alipiga kelele kubwa. Nikatulia kidogo na kumtazama usoni halafu nikarudia tena zoezi lile kwa mguu ule ule wa kulia. Akaendelea kupiga kelele kubwa.
“Ninyi ni akina nani na Rais mmempeleka wapi?” nilimuuliza kwa sauti ya ukali. Halafu nikatulia. “Niambie, ninyi ni nani na Rais mmemficha wapi?”
“Sijui!” yule jamaa alisema huku akigugumia kwa maumivu. Nikainua tena ule mkasi ili nikite juu ya mguu wake, akapiga kelele.
“
Please, stop that!” yule jamaa alilia. Nikamtazama nikiwa nimekunja sura yangu.
“Haya niambie, Rais yupo wapi na nani mkuu wenu?” nilimuuliza.
“Kweli mimi sijui chochote,” yule jamaa alisema huku akigugumia kwa maumivu makali aliyoyapata.
“
I think this is not working,” nilisema huku nikikirudisha kile kifaa chenye ncha kali, nikachukua bomba la sindano, nikavuta dawa fulani nyeupe toka katika kichupa kidogo. Yule jamaa alinitazama kwa hofu.
“Nilikuonya toka mwanzo lakini umepuuza. Utanieleza kila kitu leo vinginevyo kifo chako kitakuwa cha taratibu na cha mateso sana,” nilimwambia halafu nikadondoshea matone kadhaa pale kwenye nyama ya paja nilipozamisha kile kitu chenye ncha kali, sehemu ambayo ilikuwa inatoa damu.
Yule jamaa alijitingisha kwa nguvu pale kwenye kitanda kutokana na maumivu makali aliyoyapata huku akipiga kelele kubwa. Sikujali, nikachukua gundi na kumfunga mdomo ili asiweze kupiga kelele halafu nikadondoshea tena matone kadhaa pale kwenye paja nilipopachoma na kitu chenye ncha kali. Yule jamaa aliendelea kugugumia kwa maumivu makali. Kisha nikamfungua ile gundi niliyomfunga nayo mdomoni.
“Uko tayari kuniambia ninachokihitaji?” nilimuuliza wakati akiwa ndani ya maumivu makali sana.
“
You go to hell, you devil!” yule jamaa alisema kwa hasira, nikamfunga tena mdomo kwa ile gundi na kuchukua kisu, nikamkata kidogo shingoni halafu nikadondoshea matone kadhaa mahala nilipokata.
Yule jamaa alikukuruka pale kitandani kana kwamba alikuwa katika hatua ya kukata roho. Nilimwangalia kwa sekunde chache halafu nikamfungua ile gundi mdomoni.
“Uko tayari kujibu nilichokuuliza?” nilimuuliza yule jamaa lakini hakujibu kitu, alibaki akilia kwa maumivu makali.
“
C’mon, guy… tell me what I need to know!” nilisema kwa ukali nikimtaka aniambie kile nilichohitaji kukijua. Yule jamaa aliendelea kulia kwa maumivu makali sana aliyoyasikia.
Dah! Jamaa alikuwa na roho ngumu sana! Hata hivyo nilijua tu kuwa mwishoni lazima atapike kila kitu alichokuwa akikijua. Nilimwacha nikaelekea mezani na kuchukua kifaa kidogo cha kukatia, nikakiwasha na kukijaribu. Yule jamaa akanitazama kwa hofu usoni.
“Utanisamehe, umetaka mwenyewe tufike hapa tulipofika na nilikuonya toka mapema.
I’m a monster na ninachokwenda kukufanyia kitabaki katika kumbukumbu za uzao wako daima. Nitakukata kidole kimoja kimoja nikianzia na vidole vya miguu na halafu nitakuja mikononi na halafu nitanyunyiza dawa hii inayouma. Ila ukitaka nisifanye hivyo nijibu haraka kile nilichokuuliza,” nilisema kwa sauti kavu.
Yule jamaa hakujibu kitu bado aliendelea kulia kwa maumivu makali. Nikakiwasha kile kifaa halafu nikakishika kidole cha mwisho cha mguu wake wa kulia na kukikata. Yule jamaa alipiga kelele kubwa sana.
“
C’mon, guy, usilazimishe tufike huku. Niambie kile ninachokitaka,” nilisema kwa ukali. Bado yule jamaa aliendelea kugaagaa huku akilia kwa maumivu makali mno.
“Bado unaendelea kuwa jeuri?” nilimuuliza huku nikiwaza kumbadilisha sura yake. Nikakishika kidole kinachofuata na kukikata. Yule jamaa akapiga kelele kubwa hadi sauti ikaanza kumkauka.
“
Please stop!” yule jamaa aliomba huku akilia kwa uchungu.
“
Are you ready to tell me what I want?” nilimuuliza.
“
I will tell you… I will tell you everything. Please stop hurting me…” yule jamaa alisema huku bado akiendelea kulia kwa maumivu makali.
“
Now tell me everything,” nilisema huku nikiwa nimevaa sura ya kazi iliyokuwa mbali na utani. “Sema, Rais yuko wapi na nani kawatuma kwenda kumuua Samson Dadi?”
“Sijui aliko Rais, mi nimekodiwa tu kumuua Dadi… kwa kweli sijui hasa kazi ni ya na-na-nani,
aaarrgghh please don’t hurt me,” yule jamaa alilalama.
“Nani aliyekukodi na amekulipa nini?” nilimuuliza.
“Chameleon, Chameleon… ni-me-ko-diwa na Chameleon,
oh!” yule jamaa aliongea kwa tabu huku akigugumia kwa maumivu, “ame-ni-ni-lipa vizu-ri…”
“Chameleon ndiye nani na yupo wapi?” nilimuuliza kwa shauku.
“Ni m-m-mku-u wa…” yule jamaa alikuwa akinieleza kwa tabu, muda huo nikahisi uwepo wa mtu mwingine sehemu fulani mle ndani. bila kusubiri nikachupa na kuanguka kando huku risasi zikipita na kumwingia yule jamaa pale kitandani.
Halafu nikasimama haraka na kujibana nyuma ya mlango wa kuingilia kwenye kile chumba, mlango ambao ulikuwa umefunguliwa nusu. Risasi za kutosha ziliendelea kumiminika toka pale mlangoni na kusambaratisha vitu vilivyokuwemo mle chumbani. Kisha ukimya ukatawala huku pande zote mbili, mimi niliyekuwa ndani na mtu aliyekuwa nje, kila mmoja akimtegea mwingine. Sote tulisubiri nani awe wa kwanza kujitokeza.
Niliendelea kubana kimya kabisa pale nyuma ya mlango. Baada ya takriban dakika tatu nikasikia sauti hafifu ya nyayo za mtu ikisonga kuingia ndani. Kwanza ulitangulia mtutu wa bunduki aina ya US Barrett M82 kisha mikono yenye misuli imara ya mikononi iliyotuna kikamilifu, halafu mtu kiwiliwili cha mmoja mrefu aliyezidi futi sita akiwa na mwili wa kimazoezi kikaingia. Yule mtu alikuwa kama kivuli.
Alikuwa ndani ya mavazi meusi na raba nyeusi miguuni na alivalia soksi nyeusi usoni. Wakati akivuta hatua fupi fupi kuingia ndani ya chumba kile huku akipokelewa na ukimya wa hali ya juu, nami nikaamua kujitokeza na kuweka mtutu wa bastola yangu kwenye kisogo chake.
“Tulia kama unanyolewa na weka bunduki yako chini,” nilimwamuru kwa sauti kavu.
Yule jamaa hakuwa mbishi, alifanya hivyo kwa kuinama ili aiweke ile bunduki chini, lakini alipokaribia kuiweka chini akafanya hila dhidi yangu kwa kunipiga kwa miguu yake akifanya kama anaruka sarakasi, kumbe hakujua kuwa alikuwa anapambana na mtu makini zaidi anayeongozwa na hisia ya sita. Nilikuwa nimeshamsoma kitambo tangu alipokuwa akiinama, na hivyo alipojaribu hila hiyo nilimkwepa na kumshushia pigo moja la teke kali la kuzunguka lililotua katika uti wake wa mgongo, yule jamaa akaanguka sakafuni akiwa hana uhai.
Mara nikahisi tena kuwa kulikuwa na mtu mwingine akiingia kimya kimya ndani ya kile chumba, nikageuka haraka huku nikiruka kando, bastola yangu nikiielekeza upande huo, na kwa kufanya vile macho yangu yakakutana na macho ya Daniella akiwa amesimama mlangoni bila wasiwasi wowote, alikuwa akinitazama kwa tabasamu.
“Dah! Naona jamaa amekutana na pigo la mauti!” Daniella alisema huku akitabasamu.
“
Yeah… pigo la kifo,” nilijibu huku nikigeuza shingo yangu kumtazama yule jamaa pale chini. Kisha nikamuuliza Daniella kwa mshangao uliochanganyika na wasiwasi, “Na imekuwaje huyu jamaa akafanikiwa kuingia hadi huku? Mzee Chitemo yuko wapi?”
“Yupo kule chumba cha tiba. Jamaa walimuwahi wakamdhibiti,” Daniella aliniambia huku akiusogelea ule mwili wa yule mtu na kuanza kuupekua.
“Walikuwa wangapi?” nilimuuliza Daniella kwa wasiwasi.
“Wawili… mmoja alibaki nyuma, nikawahi kumzimisha ndiyo nikaja huku,” Daniella alisema huku akitoa bastola moja aina ya
Barretta, kete kadhaa za bangi na kitambulisho, toka kwenye mifuko ya yule mtu. Kisha alikitazama kwa makini kile kitambulisho kabla hajamaka kwa mshangao. “Kapteni Kaike!”
Nikakichukua kile kitambulisho na kukisoma. Yule mtu aliitwa Steven Kaike na alikuwa mwajiriwa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania mwenye cheo cha Kapteni.
* * *
Usichoke kuifuatilia simulizi hii hadi mwisho...