Simulizi: Harakati za maisha

Simulizi: Harakati za maisha

SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA

Tulifika nyumbani huku nikitambua wife kachukia kiasi lakini nilipanga kutomwambia chochote hata akilazimisha .lakini muda ule hakuongea chochote.

Usiku wa saa tisa mke wangu aliniamsha , akinambia anahisi kuna mtu anatembea nje,
Nikatoka kwa tahadhari huku nikichukua manati yangu ili kama Kuna hatari yeyote nijihami huku nikiwaza huyo mtu atakuwa karukaje uzio, na kama kafanikiwa basi ni mtu hatari, nilichukua tahadhari nikizunguka nyumba yote lakini sikuona wala kushitukia jambo baya. nikawasha tochi kujiridhisha hasa sehemu ambazo mwanga haukufika vizuri. Lakini hakukuwa na jambo lolote nililoona nikahakiki mageti yote yakawa salama .

Nilirudi ndani na kumkuta mke wangu sebuleni akiwa kashika tama , kama mwenye jambo kubwa moyoni,

Mwenzetu vipi mbona umekuja huku si ulale, eeh muda bado wa kuamka.
Nilimwambia.

Nilale Nina raha gani hata usingizi sipati, Kila nikijaribu kujilazimisha , wapi nashindwa Nina mawazo sana, ni kwamba baba Jack utaniua kwa presha , na hii aibu unayonitia hakika unaenda kupotea mume wangu, kama siyo jela basi utakufa vibaya .

Mume wangu kumbe ni jambazi? Tena ni tapeli mkubwa nasikia , mwanzo nilikuwa nakataa ,napinga , naona ni majungu na fitina za walimwengu lakini kwasasa taarifa zimeenea mtaani hapa kote nasemwa mimi, kwani unataka Nini haswa kwenye maisha yako.
Mbona una kazi nzuri tu japo huwezi kukidhi mambo yote lakini angalau upo kwenye level ambayo ni ya kawaida.

Sisi ni masikini sawa, lakini hatuna umasikini wa kushindwa kumudu mambo madogo madogo.
Halafuuuu kama ni kweli unadhulumu pesa za watu, mbona sioni jambo jipya? Kama ni projects zako, najua unaendesha kwa namna gani kwani mambo yako mengi unanishirikisha. Lakini kwa hili hapana.
aliweka kituo.

Umeongea sana,
Umeuliza maswali umejijibu mwenyewe,
Unasema kama ni projects zangu unazijua kwani huwa nakushirikisha, hivyo tambua kuwa unayoyasikia ni uongo na fitina za walimwengu tu, tena ni vyema ukaniambia ni nani kasema Mimi ni jambazi na umemsikia lini.
niliuliza.

Usinitishe kwahiyo unataka ukamfanye Nini huyo mtu, kumbe ndiyo maana unarudi saa tano za usiku mara nyingi,
mara boss kasema niende huku mara nani kanituma, kumbe hutumwi Wala Nini ni habari zako za kitapeli tu na plani za kijambazi Sasa mwisho wako nauona, na nadhani ni muda wa Kila mmoja kuangalia ustaarabu wake siwezi tena kuendelea kudhalilika, ni kweli tulifunga ndoa,yenye mashahidi pale altareni na mbele ya yule padre lakini sidhani kama ni vigumu kuachana na wewe nitaenda hukohuko kwenye baraza la mapadre niwaelekeze hizi habari , siwezi kuishi na wewe tena.nitapeleka cheti ili kama vipi ndoa ivunjwe

Umeacha kwenda kanisani nikikukumbusha unaleta visingizio visivyo na maana, unalewa sana unakunywa sana pombe ,
Hivi hujihurumii, hutuwazii sisi kama familia, huwazi kuhusu wanao maana urithi wa watoto ni Elimu Sasa bado tuna safari ndefu ya kuwatengenezea
Njia watoto wetu,
Sasa leo na kesho unaingia jela, au unaviziwa unauawa, eeenhee niambie itakuwaje.

Mimi sina Elimu yeyote, na Kila ninachofanya leo ni kutokana na sapoti yako, hata biashara zangu ni za kwako kwani Kila ninapoyumba huwa unaniinua.Daniel (akinitaja jina)
tafuta polepole , nakuamini na nakukubali sana una Kila sifa ya kuitwa mume,baba wa watoto wangu na mlezi
Sasa kwa njia uliyochagua na unayoenda nayo siyo sahihi Daniel utakufa.yule mwenzako Jastini ni mkongwe na ameshakata tamaa wewe je,na nashangaa wewe umeponaje pale central ukashindwa kukaa mahabusu?
aliweka kituo huku nikimwacha aongee, ajimalize atoe dukuduku lake lote sikutaka nimkatishe kwani anadai hizi taarifa kazisikia kwa watu wengi hivyo napaswa kutumia busara kuzungumza naye ili anielewe na si vinginevyo.

Mke wangu tumechelewa kulala , halafu tena unaniamsha mara nani anatembea huko nje, Ina maana uliniamsha ili uniambie hizi habari,
Si ungesema tu. nilimwambia kwa mshangao.

Nilitaka usingizi ukutoke kwanza kwa kutembea tembea huko nje nikijua utanisikiliza ninachosema,lakini pia Kwa taarifa za wewe kusikia ni jambazi nilitaka nikupime una uoga gani.alinijibu kuwa alinisumbua tu.

Haya umegundua Nini baada ya Mimi kutoka nje.
niliuliza huku nikiwa nimeshakasirika.

Ni Siri yangu , ila tambua unanitisha sana tena mengi nayasikia ni mengi sana wewe endelea tu muda wako utafika tu ipo siku yako isiyo na jina.

aliendelea kulalamika lakini Mimi niliamua kurudi ndani chumbani nikimuacha sebuleni Kisha nikajiinamia nikiwa mwenye mawazo kiasi.

Kwanini nahusishwa na skendo za utapeli na ujambazi, ni dhahiri kuna roho ya kishetani inanifuatilia na nisipochukua hatua mapema nitaangamia mke wangu kashalishwa maneno, kule kazini ndiyo hivyo tena, hata da Vero sikupokea simu yake sijui hata alitaka kusema nini, pia ni mtu ambaye ameshaanza kunidharau. au niende kwa sangoma nikapandishwe nyota?

Au nianze kushiriki kanisani,nitapokelewa kwa heshima kama zamani?maana hata kwenye jumuiya yangu nina miaka kadhaa sijashiriki.

Mimi sijawahi kuiba na sina hizo sifa licha ya kupitia magumu mengi kipindi cha nyuma lakini sijawahi kuwaza kuiba kitu cha mtu , haya ya sasa yanatoka wapi?
Ee MUNGU nisaidie maana naona kama anayosema mke wangu yanaenda kunitokea masaa machache yajayo.

Nikiwa nimejiinamia huku nje kukiwa kunapambazuka, mke wangu aliniita.
Mume wangu nakuona unavyowaza na kutafakari naona ni muda sahihi wa kuweza kuacha mara Moja tabia zako hujachelewa bado....... Kabla hajamalizia sentensi yake

Niliinuka na kumkaba shingoni nikimkaba kama napigana na mwanaume mwenzangu , Kisha nikamtupia kitandani huku nikihema hata yeye aliishia kujishika shingoni huku akiugulia maumivu.

Wewe ni mpuuzi hukai chini na Mimi ukaniuliza kwa adabu, unaanza kuropoka Ukiwa hujui hata kinachoendelea , halafu bila hata kufikiri unaniambia eti umesikia watu wanasema, kwahiyo hao watu wanaujua ukweli kuliko Mimi muhusika, kiasi cha wewe kuchukua maneno kama yalivyo na kuniambia mimi. nilifoka kwa sauti

Mume wangu unataka kuniua, wewe niue tu nimalizie, alilalamika mke wangu.

Sikujali nilimnasa vibao kadhaa ,nikavaa nguo zangu sikutaka hata kuoga then, nikachukua wallet yangu na kujiridhisha kuwa ipo vema nikatoka ,kufika sebuleni namuona dada wa kazi akiwa na wasiwasi akiwa kasimama tu.
Huenda alitamani kuniuliza lakini angeanzaje .jamani hakuna anayepanga kumpiga mkewe ila ni mambo hutokea unajikuta umeshafanya maamuzi Kuna vitu vinakera sana.

Nilipanda pickup yangu huku nikiwa naelekea njia ya shamba lengo niende kwa mtaalamu ambaye nasikia yupo vizuri maana mazingira na upepo niliopitia ilikuwa ni hatari mno kwangu. Kwakuwa boss alinipa permission ya siku kadhaa hivyo nikaona ni muda wa kuweza kufanya ukarabati wa vitu kadhaa.

Saa mbili ya asubuhi ilinikuta nikiwa nimeshauacha Mkoa wa
Dar es salaam , nikichanja mbuga kwenda uzaramoni .

Nikiwa nimekaribia kwenye Kijiji mahali ambako nasikia mtaalamu anapatikana, huku nikipunguza mwendo na kuuliza uliza wenyeji sehemu anayopatikana yule mtaalamu.Nikaelekezwa.

Kabla sijafika simu iliita namba ikiwa ngeni, moyo ulienda mbio huku nikipokea kishingo upande maana ni kipindi nikiona namba ngeni nawaza polisi tu.

Mimi ni Mzee wako mjumbe wa huu mtaa, vipi mwanangu uko wapi?
aliuliza yule Mzee mara tu baada ya kusalimiana.

Nipo mbali sana Mzee vipi una shida gani? niliuliza.

Sawa, mkeo kaniletea malalamiko hapa si muda mrefu,na kwanini umparueparue mtoto wa kike vile shingoni,
Jamani Daniel hata wewe?
Si kwamba nashangaa wanandoa kuumizana ila sikutegemea namna ulivyo ukapige mwanamke, tafadhali huko ulikoenda ukirudi nipigie simu, na mtoto wa watu hajataka kwenda polisi , unadhani akienda na makovu uliyomsababishia utakuwa kwenye wakati gani kijana . aliweka kituo yule mjumbe.

Dah Mzee wangu nikirudi tutaongea,nilijibu kwa kifupi Kisha nikakata simu.

Huku nikisimama katikati ya barabara nikiwa na mawazo kadhaa,
Kwanza nilianza kujuta kwa niliyoyafanya kwa mke wangu, nilimuhurumia sana, nilijiona mjinga kwa kitendo cha kumpiga ni ukatili nimefanya.

Mke wangu si Malaya jamani, na hata kama anafanya huenda ni kwa Siri sana maana uchunguzi wangu wote sijawahi kumuhisi, na hizi ndiyo kesi kubwa kwa wanandoa
Nilijiwazia.

Nilishtuliwa na honi ya gari Canter moja iliyojaza mihogo ikiwa imepangwa kiustadi.Nikawapisha huku nikiwaomba msamaha.

Wewe Nini bro, unawaza nini au tukupe msuba uvute? Unakaa kiboya boya barabarani. nilitukanwa lakini sikujibu chochote. Huku taratibu nikielekea nilipokusudia.

Itaendelea.................. .
Yes tupo pamoja

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA

Tulifika nyumbani huku nikitambua wife kachukia kiasi lakini nilipanga kutomwambia chochote hata akilazimisha .lakini muda ule hakuongea chochote.

Usiku wa saa tisa mke wangu aliniamsha , akinambia anahisi kuna mtu anatembea nje,
Nikatoka kwa tahadhari huku nikichukua manati yangu ili kama Kuna hatari yeyote nijihami huku nikiwaza huyo mtu atakuwa karukaje uzio, na kama kafanikiwa basi ni mtu hatari, nilichukua tahadhari nikizunguka nyumba yote lakini sikuona wala kushitukia jambo baya. nikawasha tochi kujiridhisha hasa sehemu ambazo mwanga haukufika vizuri. Lakini hakukuwa na jambo lolote nililoona nikahakiki mageti yote yakawa salama .

Nilirudi ndani na kumkuta mke wangu sebuleni akiwa kashika tama , kama mwenye jambo kubwa moyoni,

Mwenzetu vipi mbona umekuja huku si ulale, eeh muda bado wa kuamka.
Nilimwambia.

Nilale Nina raha gani hata usingizi sipati, Kila nikijaribu kujilazimisha , wapi nashindwa Nina mawazo sana, ni kwamba baba Jack utaniua kwa presha , na hii aibu unayonitia hakika unaenda kupotea mume wangu, kama siyo jela basi utakufa vibaya .

Mume wangu kumbe ni jambazi? Tena ni tapeli mkubwa nasikia , mwanzo nilikuwa nakataa ,napinga , naona ni majungu na fitina za walimwengu lakini kwasasa taarifa zimeenea mtaani hapa kote nasemwa mimi, kwani unataka Nini haswa kwenye maisha yako.
Mbona una kazi nzuri tu japo huwezi kukidhi mambo yote lakini angalau upo kwenye level ambayo ni ya kawaida.

Sisi ni masikini sawa, lakini hatuna umasikini wa kushindwa kumudu mambo madogo madogo.
Halafuuuu kama ni kweli unadhulumu pesa za watu, mbona sioni jambo jipya? Kama ni projects zako, najua unaendesha kwa namna gani kwani mambo yako mengi unanishirikisha. Lakini kwa hili hapana.
aliweka kituo.

Umeongea sana,
Umeuliza maswali umejijibu mwenyewe,
Unasema kama ni projects zangu unazijua kwani huwa nakushirikisha, hivyo tambua kuwa unayoyasikia ni uongo na fitina za walimwengu tu, tena ni vyema ukaniambia ni nani kasema Mimi ni jambazi na umemsikia lini.
niliuliza.

Usinitishe kwahiyo unataka ukamfanye Nini huyo mtu, kumbe ndiyo maana unarudi saa tano za usiku mara nyingi,
mara boss kasema niende huku mara nani kanituma, kumbe hutumwi Wala Nini ni habari zako za kitapeli tu na plani za kijambazi Sasa mwisho wako nauona, na nadhani ni muda wa Kila mmoja kuangalia ustaarabu wake siwezi tena kuendelea kudhalilika, ni kweli tulifunga ndoa,yenye mashahidi pale altareni na mbele ya yule padre lakini sidhani kama ni vigumu kuachana na wewe nitaenda hukohuko kwenye baraza la mapadre niwaelekeze hizi habari , siwezi kuishi na wewe tena.nitapeleka cheti ili kama vipi ndoa ivunjwe

Umeacha kwenda kanisani nikikukumbusha unaleta visingizio visivyo na maana, unalewa sana unakunywa sana pombe ,
Hivi hujihurumii, hutuwazii sisi kama familia, huwazi kuhusu wanao maana urithi wa watoto ni Elimu Sasa bado tuna safari ndefu ya kuwatengenezea
Njia watoto wetu,
Sasa leo na kesho unaingia jela, au unaviziwa unauawa, eeenhee niambie itakuwaje.

Mimi sina Elimu yeyote, na Kila ninachofanya leo ni kutokana na sapoti yako, hata biashara zangu ni za kwako kwani Kila ninapoyumba huwa unaniinua.Daniel (akinitaja jina)
tafuta polepole , nakuamini na nakukubali sana una Kila sifa ya kuitwa mume,baba wa watoto wangu na mlezi
Sasa kwa njia uliyochagua na unayoenda nayo siyo sahihi Daniel utakufa.yule mwenzako Jastini ni mkongwe na ameshakata tamaa wewe je,na nashangaa wewe umeponaje pale central ukashindwa kukaa mahabusu?
aliweka kituo huku nikimwacha aongee, ajimalize atoe dukuduku lake lote sikutaka nimkatishe kwani anadai hizi taarifa kazisikia kwa watu wengi hivyo napaswa kutumia busara kuzungumza naye ili anielewe na si vinginevyo.

Mke wangu tumechelewa kulala , halafu tena unaniamsha mara nani anatembea huko nje, Ina maana uliniamsha ili uniambie hizi habari,
Si ungesema tu. nilimwambia kwa mshangao.

Nilitaka usingizi ukutoke kwanza kwa kutembea tembea huko nje nikijua utanisikiliza ninachosema,lakini pia Kwa taarifa za wewe kusikia ni jambazi nilitaka nikupime una uoga gani.alinijibu kuwa alinisumbua tu.

Haya umegundua Nini baada ya Mimi kutoka nje.
niliuliza huku nikiwa nimeshakasirika.

Ni Siri yangu , ila tambua unanitisha sana tena mengi nayasikia ni mengi sana wewe endelea tu muda wako utafika tu ipo siku yako isiyo na jina.

aliendelea kulalamika lakini Mimi niliamua kurudi ndani chumbani nikimuacha sebuleni Kisha nikajiinamia nikiwa mwenye mawazo kiasi.

Kwanini nahusishwa na skendo za utapeli na ujambazi, ni dhahiri kuna roho ya kishetani inanifuatilia na nisipochukua hatua mapema nitaangamia mke wangu kashalishwa maneno, kule kazini ndiyo hivyo tena, hata da Vero sikupokea simu yake sijui hata alitaka kusema nini, pia ni mtu ambaye ameshaanza kunidharau. au niende kwa sangoma nikapandishwe nyota?

Au nianze kushiriki kanisani,nitapokelewa kwa heshima kama zamani?maana hata kwenye jumuiya yangu nina miaka kadhaa sijashiriki.

Mimi sijawahi kuiba na sina hizo sifa licha ya kupitia magumu mengi kipindi cha nyuma lakini sijawahi kuwaza kuiba kitu cha mtu , haya ya sasa yanatoka wapi?
Ee MUNGU nisaidie maana naona kama anayosema mke wangu yanaenda kunitokea masaa machache yajayo.

Nikiwa nimejiinamia huku nje kukiwa kunapambazuka, mke wangu aliniita.
Mume wangu nakuona unavyowaza na kutafakari naona ni muda sahihi wa kuweza kuacha mara Moja tabia zako hujachelewa bado....... Kabla hajamalizia sentensi yake

Niliinuka na kumkaba shingoni nikimkaba kama napigana na mwanaume mwenzangu , Kisha nikamtupia kitandani huku nikihema hata yeye aliishia kujishika shingoni huku akiugulia maumivu.

Wewe ni mpuuzi hukai chini na Mimi ukaniuliza kwa adabu, unaanza kuropoka Ukiwa hujui hata kinachoendelea , halafu bila hata kufikiri unaniambia eti umesikia watu wanasema, kwahiyo hao watu wanaujua ukweli kuliko Mimi muhusika, kiasi cha wewe kuchukua maneno kama yalivyo na kuniambia mimi. nilifoka kwa sauti

Mume wangu unataka kuniua, wewe niue tu nimalizie, alilalamika mke wangu.

Sikujali nilimnasa vibao kadhaa ,nikavaa nguo zangu sikutaka hata kuoga then, nikachukua wallet yangu na kujiridhisha kuwa ipo vema nikatoka ,kufika sebuleni namuona dada wa kazi akiwa na wasiwasi akiwa kasimama tu.
Huenda alitamani kuniuliza lakini angeanzaje .jamani hakuna anayepanga kumpiga mkewe ila ni mambo hutokea unajikuta umeshafanya maamuzi Kuna vitu vinakera sana.

Nilipanda pickup yangu huku nikiwa naelekea njia ya shamba lengo niende kwa mtaalamu ambaye nasikia yupo vizuri maana mazingira na upepo niliopitia ilikuwa ni hatari mno kwangu. Kwakuwa boss alinipa permission ya siku kadhaa hivyo nikaona ni muda wa kuweza kufanya ukarabati wa vitu kadhaa.

Saa mbili ya asubuhi ilinikuta nikiwa nimeshauacha Mkoa wa
Dar es salaam , nikichanja mbuga kwenda uzaramoni .

Nikiwa nimekaribia kwenye Kijiji mahali ambako nasikia mtaalamu anapatikana, huku nikipunguza mwendo na kuuliza uliza wenyeji sehemu anayopatikana yule mtaalamu.Nikaelekezwa.

Kabla sijafika simu iliita namba ikiwa ngeni, moyo ulienda mbio huku nikipokea kishingo upande maana ni kipindi nikiona namba ngeni nawaza polisi tu.

Mimi ni Mzee wako mjumbe wa huu mtaa, vipi mwanangu uko wapi?
aliuliza yule Mzee mara tu baada ya kusalimiana.

Nipo mbali sana Mzee vipi una shida gani? niliuliza.

Sawa, mkeo kaniletea malalamiko hapa si muda mrefu,na kwanini umparueparue mtoto wa kike vile shingoni,
Jamani Daniel hata wewe?
Si kwamba nashangaa wanandoa kuumizana ila sikutegemea namna ulivyo ukapige mwanamke, tafadhali huko ulikoenda ukirudi nipigie simu, na mtoto wa watu hajataka kwenda polisi , unadhani akienda na makovu uliyomsababishia utakuwa kwenye wakati gani kijana . aliweka kituo yule mjumbe.

Dah Mzee wangu nikirudi tutaongea,nilijibu kwa kifupi Kisha nikakata simu.

Huku nikisimama katikati ya barabara nikiwa na mawazo kadhaa,
Kwanza nilianza kujuta kwa niliyoyafanya kwa mke wangu, nilimuhurumia sana, nilijiona mjinga kwa kitendo cha kumpiga ni ukatili nimefanya.

Mke wangu si Malaya jamani, na hata kama anafanya huenda ni kwa Siri sana maana uchunguzi wangu wote sijawahi kumuhisi, na hizi ndiyo kesi kubwa kwa wanandoa
Nilijiwazia.

Nilishtuliwa na honi ya gari Canter moja iliyojaza mihogo ikiwa imepangwa kiustadi.Nikawapisha huku nikiwaomba msamaha.

Wewe Nini bro, unawaza nini au tukupe msuba uvute? Unakaa kiboya boya barabarani. nilitukanwa lakini sikujibu chochote. Huku taratibu nikielekea nilipokusudia.

Itaendelea.................. .
Mkeo anaongea sana Aisee hampi mtu nafasi ya kumuuliza yeye lawama tu kha!
 
Hata ningekuwa ni mimi kwa uongeaji wa mkeo angelamba vibao mtu unakaa unashangaa hali inavyokwenda yeye anaongea Kama vile ana uhakika kibaya zaidi anataka muachane!
 
Nimetoka kwa "mr the dragon" holaa, Nimekuja apa amna kitu,nkaenda kwa 'insider man' napo patupu, nikaona haitoshi nkasema ngoja niende kwa 'singano jr" napo pia patupu,,wakuu nielekezeni chimbo lingine tafadhar...
 
Nimetoka kwa "mr the dragon" holaa, Nimekuja apa amna kitu,nkaenda kwa 'insider man' napo patupu, nikaona haitoshi nkasema ngoja niende kwa 'singano jr" napo pia patupu,,wakuu nielekezeni chimbo lingine tafadhar...
nipe link ya mr the dragon nikapoze arosto
 
Nimetoka kwa "mr the dragon" holaa, Nimekuja apa amna kitu,nkaenda kwa 'insider man' napo patupu, nikaona haitoshi nkasema ngoja niende kwa 'singano jr" napo pia patupu,,wakuu nielekezeni chimbo lingine tafadhar...
Singano jr tayari keshapost
 
Nimetoka kwa "mr the dragon" holaa, Nimekuja apa amna kitu,nkaenda kwa 'insider man' napo patupu, nikaona haitoshi nkasema ngoja niende kwa 'singano jr" napo pia patupu,,wakuu nielekezeni chimbo lingine tafadhar...
Nenda kwa JBourne59 ana msegemnege 😁
 
SEHEMU YA THELATHINI

Niliulizia ulizia hadi nikafika pale kwa mganga ambaye niliambiwa huku nikijiuliza mbona sioni hata hekaheka. Nilitafuta sehemu nzuri nikapaki Samaki wangu Kisha taratibu nikajisogeza karibu na sehemu husika huku nikikaribishwa na akina mama wa pale Kisha tukasalimiana.

Karibu sana baba
karibu . Nilikaribishwa karibu na mti fulani wa mfenesi ambako kulikuwa na mbaombao fulani ikionesha ni sehemu ya fundi selemala kwani kulikuwa na milango na vitanda kadhaa local iliyotengenezwa kienyeji.

Hapa ni kwa Mzee (Nikitaja jina)
Niliuliza.

Ni kweli baba, ningependa kuuliza kwani una shida gani baba. aliniuliza yule mama aliyeonekana ni mpole lakini pia Dini ilimkaa vyema sana.

Nasikia hapa Kuna mtaalamu wa zile tiba zetu. Hivyo Kwa kuuliza majirani nimeambiwa ni hapa, vipi mama au nimekosea siyo penyewe. Niliongea huku nikijichekesha yaani ile ugenini.

Ni sahihi wala hujakosea ni hapa hapa ila Mzee katoka kidogo Wala hayupo mbali sana, ngoja tumtume kijana akamuite. aliongea yule mama aliyeonekana ni mwenye adabu ile ya kijijini, ile ya asili yaani nilifurahi sana namna anavyoongea huku nikiletewa maboga yaliyochemshwa kwa kukatwa vipande na chai iliyopo kwenye kikombe Cha plastic, nilipokea kwa mikono miwili. Huku nikikumbuka mbaaaaaaaaali. Nikaanza kula taratibu.

Baada ya kumtuma mwanaye na yeye akaingia ndani nadhani alitaka niwe huru.
Nilitulia huku nikitoa simu mfukoni ili nizugezuge nayo wakati nikimngoja mwenye nyumba. Missed calls zilikuwa nyingi huku wakiwa ni wapuuzi tu wakiwemo wale jamaa wanaotaka nishiriki kwenye mambo ya mpira.nikawapuuza tu.
Mtu pekee ambaye niliona simu yake ni ya muhimu ni Saidi, nikampigia maana yule ni dereva wetu hivyo simu yake ilikuwa ya maana muda ule nikaipiga.

Hello bro vipi kwema, uko wapi leo sijakuona job vipi kaka, nadhani ni siku ya pili . aliniuliza

Nipo mdogo wangu Nina dharula hivyo nadhani kuanzia keshokutwa nitakuwepo . Nilimjibu.

Sawa kaka Mimi ilikuwa niende mkoani Mwanza nimfuate rafiki yako , ila Leo nafika hapa asubuhi naambiwa safari imeahirishwa kwani jamaa kachukua ndege tayari, yaani nimeboreka kinoma kaka. aliongea yule dogo akionesha hakulala akiiwaza ile safari.

Basi sawa mdogo wangu Mimi naona imekuwa nafuu kwako pia maana safari hatua. niliongeza

Nafuu wapi kaka Mimi nilitaka leo niburuze chombo hadi Rock City mwisho wa siku wenye mamlaka wameghairi, baadaye basi bro.akakata simu.

Kwanza nilicheka kimoyomoyo huku nikiwaza namna dogo alivyo na wenge yaani safari ambazo watu hatuzitaki yeye ndiyo kwanza anazifurahia , Sasa ngoja wewe muache GM akijua huwa anapenda safari ndiyo kwanza atatumwa Hadi akome , unatoka Mbeya ukifika Dar es salaam unaambiwa uende Mtwara umpeleke mtu fulani, ukifika tu Mtwara unapigiwa simu urudi haraka , uende wapi sijui ndani ya wiki moja ushamaliza mikoa kibao. Halafu hupewi siku za kupumzika , huku hupati bakhishishi yeyote zaidi ya pongezi za mdomo.

Utasikia, wewe ndiye mwenye nidhamu namba moja kwenye hii taasisi hii hivyo ongeza bidii utafika mbali, huku siku zikikatika bila majibu. yaani upande cheo au daraja kwa nidhamu na heshima yako?
Huku CV yako ikiwa ni kilomita mbili?
Thubutuuuu. Nilijiwazia.

Lakini nilifurahi kwa ujio wa jamaa yangu maana tangu wamsukumie Mwanza huwa anarudi lakini huwa sipati muda wa kuongea naye ila kwasasa nitahakikisha nafanya mpango nipige naye stori ni agemate, mnywaji kama Mimi, halafu ni bonge la mjanja yaani mishe anazijua kubwa zaidi ni msomi Mimi mwenyewe simkaribii, na sijui ana mkosi gani miaka yote hapandishwi daraja

Dakika zilikatika huku kukiwa hakuna mtu anayekuja licha ya kuambiwa amefuatwa, nikaamua kumpigia mke wangu lakini simu iliita bila kupokelewa, nilijua tu hakuwa mbali na simu bali aliamua tu kunikalia kimya.

Baada ya muda kidogo alikuja Mzee fulani mwenye kanzu kuukuu , akanisalimia huku akiwa kama na kauoga fulani.

Karibu sana ndugu yangu, vipi labda nikusaidie nini . aliuliza yule Mzee.

Siku nyingi sana nilisikia wewe ni mtaalamu wa mambo yetu hivyo kama ujuavyo kwenye maisha Kuna mambo mengi hivyo nimekuja uniangalie . niliongea kwa sauti ya chini huku nikiwa makini.

Mmmh pole sana, ni kweli nilikuwa nafanya kazi hiyo zaidi ya miaka kumi na tano lakini kufikia mwaka jana nikaamua kuachana nayo, nimemrudia mola wangu , kiufupi naswali kwasasa.
Iko hivi matatizo na mitihani ipo kwa mtu yeyote yule huwezi ikwepa ni namna MUNGU alivyotuumba huwezi kunyoooka muda wote. na hupaswi
Kuona unanyanyaswa ukipatwa na mitihani hivyo ni kiasi cha wewe kukabiliana nayo tu kwani Kuna muda MUNGU hutoa mitihani ili tumkumbuke

Pia unatakiwa kuwa makini kwenye maisha yako kwasababu yapo mambo yanatokea kwa bahati mbaya, lakini mengine ni uzembe wetu wenyewe, Ukiwa mstaarabu na mwenye kiasi basi mwenyezi MUNGU atakusaidia. aliweka kituo yule Mzee huku akinikatisha tamaa sana kwani lengo langu halikutimia .

Nilitamani nimuulize kama Kuna mtaalamu mwingine tofauti na yeye lakini nikaona hawezi kuniambia kwasababu inaonesha Imani Imani imemkolea. Na hata ndiyo madhara ya kujulia kitu ukubwani . Ulimbukeni tu, nilijiwazia.

Karibu sana ndugu yangu huyu ni mke wangu mdogo, na hapa ndipo hata shughuli zangu nilikuwa nafanyia baada ya kuwa mke wangu mkubwa kuwa hataki , nadhani ndiyo maana umeelekezwa hapa , lakini kwanini wakusumbue, hakuna asiyejua kuwa Mimi nilishaachana na habari hizo .

alinitembeza kwenye mashamba yake ya mihogo huku nikienjoy sana , matunda kama mafenesi nilibeba ya kutosha na vitu vingine vingi. Huku nikipuuza hata yaliyonipeleka kule.

Unajua watu wengi wa mjini Wana dharau sana na majivuno , lakini wewe upo tofauti licha ya muonekano wako kuonesha kama nilivyofikiria.alivunja ukimya yule Mzee

Hapana Mzee,dharau ni namna ya mtu alivyo tu hakuna uhusiano wowote na kuishi mjini. nilimjibu.

Wewe Mimi nimefanya kazi ya uganga wa kienyeji kwa muda wa miaka zaidi ya kumi nimepokea wateja wa Kila aina , Kuna watu wanakuja kwaajili ya huduma tu hawataki story Wala nini, hata wewe nilitegemea baada ya kukukatalia kuwa nimeacha hiyo kazi ungeinuka na kuondoka muda huohuo. Lakini nimepokea moja ya mtu wa tofauti sana. aliongea yule Mzee huku mkewe akichuma ndimu na kuniletea Zikiwa nyingi sana..

Yaani mume wangu huyu ni mtu wa pekee sana alivyokuja nilimchukulia tofauti sana lakini mmmmh kweli umdhaniaye siye, aliongea yule mwanamke akimwambia mumewe.

Weweee Mimi nimezaliwa kijijini tena ndani ndani hivyo haya ni Moja ya maisha niliyokulia. Nilifafanua kwani huwa sipendi kujikweza hata kama ni ..............

Jamani msalimie sana mke mwenzangu natamani angekuwepo maana ulivyo naamini hata yeye yupo kama wewe . aliongea mke wa yule Mzee Kisha tukacheka tukifurahi.

Pickup yangu ilijaa zawadi kibao, hakika nilifurahi sana, ndimu, mihogo na mafenesi yaani kama naenda kufungua genge, hakika nilitamani kulima maana Nina ekari kibao za mashamba na nisiite shamba maana huwa hayalimwi labda nikistaafu nitalima. nilijiwazia huku wenyeji wangu wakiingia ndani Kisha wakatoka huku nikipewa karanga
ambazo zipo kwenye maganda yake, zikiwa kwenye mfuko fulani.
Ilikuwa ni siku ya aina yake haswa ukizingatia ni jana tu nilikuwa kwenye korido za central nikiponea kwenye tundu la sindano kuwekwa ndani.

Tuliagana na wale wenyeji wangu nikaondoka huku nikiwa njiani nikifikiria namna ambavyo mke wangu angefurahi kuona zile zawadi Lakini tulikuwa tumeshatofautiana.
Nikaamua kumpigia simu, baada ya kumsumbua mara nyingi akapokea .

Enhee kwahiyo umeshamalizana na wanawake zako, uko vizuri ndiyo unampigia mama Jack si ndiyo, Mimi nakuruhusu lala huko huko. Saa nane hii mchana si bado masaa tu tuimalize siku , hebu achana na mimi Kisha akakata simu.

Itaendelea.............
 
Back
Top Bottom