SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA
Tukiwa njiani kuelekea sehemu ambayo sikujua kwani hawakusema,
Simu yangu ndogo iliita, ni simu ambayo inahusika zaidi na ndugu tu.
Kuangalia anayepiga ni mke wangu. Lakini kabla sijapokea niliporwa ile simu na afande huku akiangalia jina la mtu anayepiga Kisha akanirudishia ikiwa imekata. Baada ya kuita kwa mara ya pili, Nilipokea.
Vipi mume wangu kwani imekuwaje tena mbona sielewi, nimesikia unaitwa jambazi? Halafu mnaelekea wapi saizi? Tafadhali naomba nijue ili nije nijue naanzia wapi. aliongea mke wangu huku nikiwa sijamjibu chochote,kisha afande yule akapokonya simu yangu na kukaa nayo.
Hakuna tena kuongea na simu humu acha ujinga usijione kama nani, halafu na wewe Black (akimaanisha Jastini)
hebu lete simu yako na wewe, nyie mpo chini ya ulinzi, acheni u****
aliongea kwa jazba yule afande huku akitukana.
Lakini Jastini hakuwa na simu jambo ambalo hata Mimi nilishangaa, kwanini asiwe na simu?
muda ule mbona niliwasiliana naye?
Oyaa afande Fox eeh, huyu boya hana simu eti, inawezekanaje?
Hebu simamisha gari. afande ambaye hakuwa na silaha aliamrisha yule dereva niliyesikia akiitwa Fox akimtaka asimame.
Hilo ndiyo tatizo lako afande punguza presha, kama hana simu atatuonesha ilipo ngoja tufike Central kwanza, hiyo ni michezo ya kitoto anafanya na kama Kuna mahali kaificha sisi tutajua tu . Yaani nilivyo na hamu naye huyu boya.
aliongea yule dereva anayeendesha gari akiwa anamjibu afande mwenzie.
Baada ya muda fulani tulifika kituo cha kati huku pilika zikiwa nyingi muda ule, askari wote tuliokuja nao walishuka huku tukipokelewa na askari wengine kabisa wenye maneno ya kejeli.
Hebu muone huyu brazamen eti anaangalia saa, au akili yako unajua unarudi eeh,hapa ninyi ni wateja wetu,ukiwa na hotel lazima utake watu waje walale, wale,si ndiyo eeh?
Huko kwenye ma bar wamiliki wanataka wapate faida mara mia zaidi ya walivyowekeza.yaani wateja wajae,so na hizi Selo lazima wateja wajae,eeeh .aliongea kwa kejeli afande fulani mwenye umri uliosogea huku akiwa kavaa miwani yenye kamba ili isianguke.
Dakika zaidi ya kumi tulikuwa pale Kaunda lengo wachukue maelezo na taarifa fulani toka kwetu,yaani mimi na Jax lakini ikawa ni foleni hawa wamekuja kudhamini ndugu zao hawa ni wahalifu wapya wanaletwa yaani fujo zilikuwa nyingi.hatimaye tukapewa nafasi huku moyo ukiniuma sana kwani nilikuwa nafanyiwa uonevu mkubwa sana kiasi cha kuanza kumchukia Jastini lakini pia niliwaza simu yangu maana yule afande alishuka na sikumuona tena.
Baada ya afande kuchukua taarifa akataka kutuweka mahabusu lakini akaambiwa na mwenzake kwamba twende kwenye chumba cha mahojiano moja kwa moja .halafu baada ya hapo tutarudi mahabusu.
Tuliingia kule tukakuta kuna chumba kidogo chenye vifaa vikuukuu , virungu, pasi na vitu vingine ambavyo wanavijua wao.
Karibuni sana jamani,karibu sana bwana Daniel,alinitaja jina yule afande huku nikishtuka lakini nikaona labda ananifahamu,alikuwa ni kijana fulani mdogo tu mwenye mwili mwembamba ambaye mabegani alikuwa si haba,huku nikimpongeza kwa umri wake na vile vyeo hakika alishajipata
Hey bro unaitwa Jastiniiiiii ...... akimalizia kwa kutaja full name,
Mbona unalidhalilisha kabila letu bro eeeh,sisi sifa yetu kwenye hii nchi ni kujazana kwenye majeshi tu na siyo kuwa na sifa kama zako vipi kaka?
Hebu huyu mpelekeni Selo halafu huyu niongee naye kwanza.
Mimi nilitoka nikiwa na askari mmoja ambaye alikuwa mkalimkali sana,lakini badala ya kupelekwa Selo nikaambiwa nirudi mahali ilipo Kaunda,hapa nilikuta watu wameongezeka,huku wakiwemo wanaonijua huku wakishangaa why niwekwe chini ya ulinzi.
Hata baadhi ya askari ninaowajua wale ambao wanawatoa mahabusu kutoka vituo vidogo na kuwaleta pale nao walishangaa kuniona pale huku nikiona aibu na uoga kwani taarifa zangu zikifika ofisini ni neno lingine,watu wenyewe wanasubiri ujikanyage tu halafu uone nafasi yako itakavyojazwa mapema,wapo waliosoma taaluma yangu vyuo vya nchi za nje na hawana kazi au nafasi kama yangu wengi wanasukumiwa site huko,niliwaza huku mapigo ya moyo yakiongezeka.
Dani ndugu yangu vipi tena,ni leo tu nilikuona kwenye gazeti,nikasema alhamdullilah nitampigia simu rafiki yangu ili tutete jambo cha ajabu napiga simu hupokei na mimi hapa kuna jamaa yangu ni dereva nimekuja kumuwekea dhamana siunajua tena ile gari yangu kirikuu yangu huwa napatia hela ya mboga sasa nasikia jamaa aligonga mtu mbaya zaidi ni kwenye zebra sasa ndiyo nafanya marekebisho.japo wamenikamua vibaya ila nashukuru nimefanikiwa , kwani una kosa gani Daniel?
aliniuliza yule jamaa ,lakini kabla sijamjibu yule jamaa.
Nilimuona Jastini akija akiwa na pingu kabisa mikono nyuma,nikaona mambo yameshakuwa mabaya , nikamsaidia kumvua viatu na mkanda kisha wakaondoka naye kwenda zilipo Selo,kisha na mimi nikarudi kwenye kile chumba cha mahojiano huku askari wakiwa wameongezeka nikaanza kupigwa spana.
Tuache siku zote tuongee ya leo,
Daniel, unaweza kutueleza ratiba zako za leo tangu ulivyoamka zilikuwaje, aliniuliza yule afande mdogo mwenye tabasamu muda wote
Nikajieleza ilivyokuwa na namna nilivyorudi kwa kuomba ruhusa ili nije nikutane na Jastini.
Wewe jana ukienda kituo X kwaajili ya kutoa taarifa za kutishiwa na Jastini,iweje utake kumalizana naye wakati taarifa ipo kituoni na ni mtu alitishia maisha yako,kirahisi tu ukataka kupatana naye kwanini?
Ni kwasababu alinitishia akinituhumu kuwa nimemtorosha mkewe,ila leo hii baada ya kusikia yupo nyumbani akiwa na mkewe,nikaona ngoja nikamsikilize.
Nilimjibu
Hivi unawezaje kuwa mwenye imani kiasi hicho huoni kama unajiweka kwenye hatari,kwanini usingetoa taarifa polisi ili yeye aeleze kampataje mkewe mbele ya polisi ambako wewe ulishitaki?
aliuliza
Nadhani hapa afande nilikosea ,ni mazoea yangu mimi na Jastini nilijua hasira zake zitakuwa zimepungua haswa baada ya kumpata mkewe.kiufupi hangenifanya kitu.
Nilijibu.
Aisseee sawa,wewe ni mfanyabiashara wa madini?
aliuliza.
Hapana afande mimi ni mfanyakazi tu,na nina biashara ya (nikitaja jina)
Halafu wewe upo humble sana na mimi nataka niwe humble kama wewe halafu wewe ni Braza wangu kwa muonekano tu,sitaki nikukosee heshima,mbona mwenzio hapa kasema wewe unafanya biashara ya madini tena yote,si lazima uwe na mabilioni hizo hizo hela za mafuta unazopata si faida ya unachofanya?
Sasa kwa kunidanganya unanikosea.
aliongea yule afande kwa sauti ya juu kidogo akinitisha
Ningependa yeye huyo aliyekwambia kuwa nafanya biashara hiyo athibitishe kwasababu hawezi kunisingizia,ataje wapi nanunua na wapi nauzia,si unasema kakuambia huyu Jastini?hayupo mbali aje aseme nimsikie.
niliongea kwa kujikaza kidogo.
Yule afande aliniangalia kwa muda huku akitabasamu, yule askari mwenye silaha yupo pembeni akiwa anaperuzi tu kwenye simu yake huku akicheka kwa vile alivyokuwa anaviona
Hebu washa hiyo taa wewe mwenzangu ni mrefu braza.aliniambia huku nikishangaa taa ipo karibu yake niiwashe mimi halafu hakuna urefu wowote hata yeye angewasha tu.
Ila Daniel wewe sijui upoje kwani kufanya biashara ya madini ni kosa?
Kwani ni madawa ya kulevya hayo hadi ukatae kiasi hicho,tena usichojua ni kwamba kuna matajiri wa Ruby wamekuja hapahapa nchini wanatoka Sri lanka,unajua wananunua bei gani gram moja?haya wewe jicheleweshe tu utashindwa kupata connection.aliongea kwa upole safari hii huku akitengeneza tabasamu rafiki.
Ukweli afande unaongelea jambo nisilojua na sijui linafananaje ungesema mbao sawa ni biashara naifanya na nina leseni na vibali vyote lakini sijui kitu kuhusu madini.niliongea bila wasiwasi.
Sawa ,afande nenda naye huyu kwa afande Fox kwanza alisema nikimalizana naye na yeye ana maswali anataka kumuuliza.Aliongea huku nikizodolewa na baadhi ya maaskari tuliopishana nao kwenye zile korido hata sikujua kwanini wanafanya vile.
Enheee Daniel nilikuwa nakusubiri maana leo shift yangu nimeanzia kwako nafika tu hapa kazini napewa gari niwafuate wewe na jambazi mwenzio,halafu simu nimezima maana mkeo anakera sana yaani.
aliongea afande aitwaye Fox ambaye alikuwa anaendesha gari wakati wametuchukua pale home.
Itaendelea........................