Simulizi: Mimi na Mimi

Simulizi: Mimi na Mimi

Niaje guys mwamshen basi mwandishi atupie vyuma vyuma au so 😄pamoja Sana guys🫵
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI

★★★★★★★★★★★★★★★★


Niliendelea kumkumbatia Miryam kwa sekunde chache nikiwa nahisi furaha sana, kisha nikamwachia na kumtazama usoni kwa hisia sana. Yeye pia alikuwa akiniangalia kwa macho yenye hisia kwelikweli, nami nikatikisa kichwa kidogo nikiwa yaani bado siamini-amini.

"Aisee! Yaani sijui hata niseme nini..." nikaongea hivyo kwa hisia.

Akatabasamu tu na kuendelea kuniangalia kwa upendo.

Nikasema, "Wee... ume... umefikaje hapa haraka hivi? Yaani... usiniambie umekimbia kutokea Kijichi..."

Akacheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Kwani hujui kwamba nina gari?"

"Ahahah... this is amazing..." nikamwambia hivyo kwa sauti yenye hisia sana.

Akabaki akinitazama usoni kwa macho yenye upendo mwingi, nami nikalishika shavu lake kidogo huku nikimwangalia kama vile nataka kumtafuna, siyo kwa ubaya, ila kwa hamu nzuri na kubwa sana niliyokuwa nayo kumwelekea. Ndipo sauti ya koo kusafishwa ikatokea pale sebuleni, nami nikaangalia hapo na kuona Ankia alikuwepo bado. Miryam akageukia huko pia.

Nikasema kwa kujishaua, "Ankia? Kumbe bado upo?"

"Ulifikiri me jini nimepotea, au?" Ankia akaniuliza hivyo.

Miryam akatabasamu kiasi.

"Kwanza unatakiwa uwe umeshapotea, unafanya nini hapa? Hebu... go away..." nikamwambia hivyo Ankia kiutani.

"Mm? Yaani ndiyo umeshaanza na kuringa..." Ankia akaniambia hivyo kwa njia ya nyodo.

"Siyo kuringa, we' si ulikuwa unaenda dukani? Nenda..." nikamwambia hivyo.

Ankia akaniangalia kwa njia yenye nyodo na kuikunja midomo yake, na Miryam akacheka kidogo tu na kujishika shingoni.

Nikamfanyia Ankia ishara ya kumfukuza kwa kiganja na kumwambia, "Shoo!"

Ankia akacheka kwa mguno, naye akamwambia Miryam, "Baadaye mpenzi."

Miryam akatikisa kichwa kukubali heri hiyo, naye Ankia akawa ameondoka hatimaye. Raa!

Miryam akanigeukia na kunitazama usoni tena, nami nikamwangalia na kujichekesha kidogo kwa haya eti. Nikawa nahisi hali ya utete kidogo, nikiangalia pembeni huku napiga-piga kiganja changu kimoja mguuni, kisha namwangalia tena na kukuta amenikazia jicho tu, halafu sote tukajikuta tunacheka kidogo kwa kupatwa na hisia nzuri sana.

Ndipo nikamwambia, "Karibu. Njoo ukae... aa... namaanisha... siyo humu chumba... yaani... kama... utapenda tukae humu... chumbani.... au, pale... sofani... simaanishi ukiingia chumbani nita... siyo kwamba nafikiria hivyo... ila we' ndo' unaweza ukawa unafikiria... siyo kwamba... namaanisha... sikuoni unawaza... dah, naharibu aisee..."

Miryam akacheka kidogo na kutikisa kichwa chake, naye akasema, "Wasiwasi wa nini sasa tena?"

Nikafumba jicho moja na kumwangalia kwa kujihami eti.

"Ahah... me ndiyo ningetakiwa niwe na wasiwasi, maana...."

Kabla hajamaliza kuongea, nikamkumbatia kwa mara nyingine tena ili kumpa kitulizo, ambacho na mimi kwa upande wangu nilikihitaji sana. Nilihisi amani kubwa sana moyoni, na nilihitaji aihisi pia. Nikawa nimemshikilia huku nikiyumbisha miili yetu taratibu kama vile nambembeleza yaani, naye alikuwa ameiweka mikono yake mgongoni kwangu na kuitembeza taratibu huku amenilalia begani kwa raha zote. Yaani!

Nikiwa bado nimemkumbatia, nikasema kwa sauti ya chini, "Vipi tukikaa?"

Akajibu kwa sauti yake tamu, "Wazo zuri."

Nikamwachia taratibu kabisa, halafu tukatazamana machoni kwa hisia sana, kisha nikakishika kiganja chake na kwenda naye mpaka pale sebuleni na kuketi sofani. Akakaa pembeni yangu pia, huku nikiwa nimekishika kiganja chake bado, naye akakiweka kingine juu ya mkono wangu, na chenyewe nikakishika.

"Umeni-surprise sana Miryam..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Najua. Samahani kwa hilo."

"Samahani ya nini sasa? Haujui kwamba umenipa furaha sana?"

"Wakati tayari nilikuwa nimeshakuvunja moyo?" akasema hivyo huku akiniangalia usoni kwa umakini.

Nikatulia tu na kuendelea kumwangalia.

Akasema, "Jayden... I'm sorry. Nimekutesa sana... I know..."

"Usijali. Nilikuwa nakuelewa."

"Still, yaani... nimekufanyia vibaya mno. Pamoja na yote, umefanya vingi sana kwa ajili yangu kunithibitishia unanipenda, lakini nikawa nakupiga mateke tu. Najua nilikuwa nakuonea sana, na naomba tu unisamehe kwa leo... yaani bado nilikuwa nimechanganyikiwa..."

"Ulichanganywa na nini?"

"Kila kitu. Nilikuwa najiuliza... kwa nini niko hivi. Nimekupenda pia, lakini bado tu nikawa najipofusha kwa kiburi changu...."

"Miryam..."

"... ambacho kinanifanya nijione kuwa sahihi kwa kila kitu. Umenifundisha sana, umeshanionyesha kwamba kuwa hivyo haifai, lakini bado nikawa sielewi. Ni kweli," akasema hivyo kwa hisia.

Nikaanza kusugua kiganja chake taratibu.

"Leo... nimeshindwa Jayden. Nimeshindwa kuendelea kujifanya mgumu tena. Nakupenda. Na ninakuhitaji. Sijui kingine tena," akasema hivyo.

Nikatabasamu kiasi kwa hisia.

"Lakini... bado naogopa. Na baada ya ulichoniambia leo, nimetambua kuwa nakuhitaji zaidi sasa ili niache kuogopa tena. Umesema unaniona me kuwa kama msaada kwako..."

"Yeah, kabisa."

"Well, na mimi nakuona kuwa msaada wa moyo wangu. Nimetambua pia kwamba wewe ndiyo kipande cha pili cha moyo wangu kinachokosekana ili kuufanya uwe kamili, na ninakuhitaji uwe karibu nami ili uunganike pia na kuwa kitu kimoja," akaongea kwa hisia sana.

Dah! Alikuwa na maneno matamu!

"Kwa hiyo wakati huu mimi ndiyo nimekuja kukuomba nafasi Jayden. Uko tayari kunibeba?" akaniuliza hivyo.

Nikamkazia macho kiasi, nami nikamuuliza, "Hilo ni swali au jibu?"

Akatabasamu na kuangalia chini.

Nikamshika shavuni taratibu, naye akaniangalia. "Kwa asilimia zote, Miryam. Niko tayari. Unalijua hilo."

Akasema, "Mambo yatakuwa mengi, na magumu sa...."

"Usijali Miryam. Niko nawe. We are two parts of the same whole now, and I intend to keep it together no matter what..." nikatia na kimombo kidogo kumfariji.

Akakishika kiganja changu usoni kwake, naye akasema, "Asante."

Nikampa tabasamu hafifu kwa hisia.

Akashusha pumzi na kuangalia chini kwa utafakari, naye akasema, "Nina hamu kubwa... na matarajio mengi kuona ni wapi hii itanifikisha."

Nikamwachia taratibu usoni na kusema, "Hata mimi. Na ninaiona kuwa sehemu nzuri sana, sema ndiyo nataka niifikie nikiwa pamoja nawe."

Akatabasamu na kuendelea kuniangalia kwa hisia sana machoni.

Nikajikuta nimetulia zaidi, nikimtazama kwa njia hiyo hiyo yenye hisia kama yeye tu, na mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakienda mbio kwa sababu ya hisia zangu kunitaka nifanye jambo fulani. Niliiangalia midomo yake na kuona jinsi ambavyo iliachia uwazi kidogo uliofanya mpaka nikahisi kusisimka yaani, na nilipomtazama machoni, akawa bado ameniangalia tu kwa njia yenye subira.

Nikataka kupiga hatua kumwelekea kwa kuusogeza uso wangu karibu zaidi na wake, lakini akaacha kuniangalia na kusema, "Inabidi niingie nyumbani Jayden."

Nikainamisha uso wangu kiasi na kubana midomo, kisha nikatikisa kichwa kukubali hilo. Nilipomtazama usoni, nikakuta ananiangalia huku akitabasamu kiasi, nami nikajirudisha nyuma na kuangalia pembeni kwa njia ya kujishaua. Alikuwa amenisoma huyo!

Nikasema, "Sawa... najua umechoka. Nenda tu... ukapumzike."

Akatikisa kichwa kukubaliana na hilo, halafu akasema, "Na wewe ndiyo ulikuwa unaingia kupumzika bila shaka..."

"Eeh... nilikuwa nahisi uchovu... sijui hata wa nini, ila... sa'hivi umeisha. Nimepata nguvu mpya," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu na kusema, "Vizuri."

Kulikuwa na kale kahali kenye kusisimua fulani hivi, yaani, mpaka raha. Nilimtazama kwa upendo mwingi sana, naye akawa ananiangalia tu kama vile anasubiri nimuage vizuri.

Ndiyo akaniambia, "Narudi hapo Masai kwanza."

"Masai? Kwa nini? Yaani... hauendi nyumbani? Si umesema...."

"Nililiacha gari pale, ndiyo nikaja hapa," akanikatisha kwa kusema hivyo.

"Oooh, sawa. Ngoja. Kwa nini uliliacha gari Masai?" nikamuuliza.

"Nilipokuwa nakuja... sikutaka kuja mpaka huku na gari, hapo nyumbani wangeona maana... nilikuwa nataka kwanza..." akaishia hapo.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Uje kwangu."

Akatabasamu pia na kutikisa kichwa kukubali.

Nikamwambia, "Okay, nimeelewa. Umetumia akili, maana wambea wengi."

"Hapa penyewe nikitoka wakaniona, inaweza kuzua utata..."

"Oh no, haina shida. Sidhani kama ina shida. Hata hivyo we' siyo mgeni hapa, hao wakina Fatuma watajua umekuja tu kumsalimia Ankia labda..."

"Labda..." akasema hivyo na kuangalia pembeni.

"Ahah... naitamani ifike siku ambayo tutatembea pamoja... proud... kila mtu ajue kwamba wewe ni wangu," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu na kusema, "I hope for that day to come too. Ila kwa sasa... tuweke mambo yetu chini kwanza..."

"Yeah, yeah, najua. Chochote kile unachotaka tufanye, nitafata..." nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

Nikiwa namwangalia kwa hisia, nikamwambia, "Asante Miryam. Kwa kunipa hii nafasi. Nitajitahidi kuwa mume mzuri kwako."

Akatabasamu zaidi na kuuliza, "Mume eeh?"

"Ahahah... kidume wako," nikamwambia hivyo na kupandisha nyusi kichokozi.

"Ahah... sawa. Mimi pia. Nitajitahidi kukupa furaha Jayden," akaongea kwa sauti yake tamu sana.

Nilimwangalia huyu mwanamke kwa mapenzi ya dhati yote niliyohisi moyoni, yaani nilipenda sana hii hali aliyokuwa ananifanya niihisi wakati huu. Akiwa ananitazama kwa hisia pia, akanishika shavuni kwa kiganja chake laini, halafu akausogelea uso wangu karibu zaidi na kunipa busu moja, moja tu, ambayo ilinipa msisimko wa hali ya juu zaidi ya msisimko wa busu mia moja ambazo mwanamke mwingine yeyote angenipa!

Midomo yake laini iliikandamiza ya kwangu na kuvutana nayo mara moja tu na taratibu kabisa, naye akaiachia ikiwa imetoa sauti tamu kama vile ametoka kufyonza pipi tamu sana, kisha akajirudisha nyuma tena na kuniangalia kwa hisia. Sasa hapo mimi! Huo msisimko ulikuwa umeniamshia bonge moja la balaa, damu ilianza kunyanyua mdude fulani kwa nguvu isiyopimika, yaani nilihisi mwili wote unaitikia kitendo chake kidogo tu kwa hamu nzito sana. Nikabaki nikimtazama machoni kwa utulivu, huku hisia zangu zikiwa zinafurukuta huku na huko ndani yangu.

Akiwa anasugua shavu langu kwa kidole chake taratibu, akasema, "Nakupenda."

Yaani aliisema hiyo 'nakupenda' katika ile njia ya kiutu-uzima, uhakika yaani, hakuona aibu wala kuhofia kuniambia hivyo. Alijivunia kabisa.

Nikatabasamu tu na kumwambia, "Nakupenda pia."

Nilikuwa nimeweka mkono wangu usawa wa sehemu ya kati kwenye suruali ili kuficha saibu lililokuwa limenyanyuka baada ya yeye kunipiga busu kwa mara ya kwanza kabisa, na mwanamke wangu akanyanyuka kutoka hapo sofani na kuanza kuelekea mlangoni. Ikanibidi niendelee kutulia tu hapo hapo sofani maana sikutaka aone hili dubwana mapema namna hii, bado hayo mazoea sikuwa nimemwanzishia kwa hiyo kujibana ilikuwa lazima. Akafungua mlango na kuniangalia kwa ufupi, nasi tukapeana tabasamu la furaha kwa pamoja, kisha ndiyo akatoka hatimaye. We!

Yaani ile ametoka tu, nikanyanyuka na kuanza kurukaruka hapo ndani, nikapanda na kwenye sofa na kuanza kuruka kwa furaha tele. Nilihisi furaha isiyo na kifani. Nilikuwa kama nimechanganyikiwa. Nikafata na simu yangu chumbani na kuweka muziki wa Jux na Dayamondi "bora kuenjoiiiiii... maisha mafupi ni simpoo," nami naikaanzisha miuno na dansi za kipuuzi ili tu niitoe furaha yangu. Nilicheza wimbo mpaka mwisho, nami nikajitupia sofani na kubaki najichekea mwenyewe tu kwa kuhisi raha kuu mno moyoni mwangu.

Hatimaye Miryam akawa wangu. Dah! Ingebidi kutokea hapa sasa nimwonyeshe namna gani ambavyo alikuwa akiukosa uhondo wa mapenzi kwa huo muda wote alioukosa. Yaani ningemfurahisha, angenipenda mpaka milele. Sikufikiria kuhusu changamoto, sijui matatizo na vikwazo, yaani nilichowazia juu yake ilikuwa ni furaha tu. Ya nini niteseke roho wakati Miryam alikuwa wangu? Hiyo kitu haingekuwa na nafasi tena!

Na ningehakikisha nampa furaha aliyoistahili kwelikweli, ili nami nitulie kwa furaha na amani tele moyoni mwangu. Siku ile nimemwambia ukweli kuhusu hisia zangu nilijipiga mara mbili kifuani ili kujipa moyo katika mbio za kuhakikisha namkamata, na sasa akawa amekamatika, hivyo ningetakiwa kujipiga mara nyingi zaidi kifuani wakati huu kwa kiburi changu chote kuwa ndiyo, nilimpata! Piga kifua kwa masifa kama King Kong yaani! Araa? Hatimaye Miryam alikuwa bibie wangu!

★★

Haukupita muda mrefu sana na Ankia akawa amerejea tena kutoka kazini kwake, ikiwa imeshaingia saa moja, na alinikuta ndani nikiwa najiandaa kutoka. Nilitaka kwenda gym kwanza kuchangamsha mwili kabla ya kuja kwenda kwa Miryam kuwasalimia wapendwa wangu, na muda ule ambao Miryam aliniacha hapa, tuliwasiliana kupitia sms, nikimuuliza ikiwa alifika kwake bila vilongolongo vingi, naye akawa amekubali. Kwa wakati huu akawa akishughulika na mambo fulani ya hapo kwao.

Ankia alikuwa na hamu ya kutaka kusikia mengi yaliyojiri baada ya kuniacha hapa na Miryam muda ule, nami nilikuwa na furaha sana bado lakini kwa wakati huu nilitulia zaidi. Nikamwambia ningekuja kumpa ukweli wote nikitoka gym, ila kiufupi tu ni kwamba ilikuwa siku iliyogeuka kuwa yenye amani kubwa sana kwangu. Sikutarajia yaani. Kwa hiyo ningetakiwa kwenda kuchangamsha mwili kwanza kisha ndiyo nije kumpa ubuyu aliotaka, na yeye nikamwambia atanipa ubuyu niliotaka kama malipo. Hakuelewa namaanisha nini, ila nilikuwa namwongelea Bobo, hivyo ingekuja kuelezeka baadaye.

Nikatoka hapo na kwenda hadi gym ya pale Mzinga, na tayari nilikuwa nimeshaanza kujuana na baadhi ya mangangali waliokuja hapo lakini sikupitilizisha sana mazoea, nami nikanyanyua na kushusha chuma kwa muda wa kama saa moja na nusu, kisha ndiyo nikarudi tena kwa Ankia. Sasa nilikuwa nimechangamka kwelikweli yaani, nikaoga na kuvaa vizuri, kisha ndiyo nikakaa pamoja na mwanamke huyo sebuleni kupiga story kidogo.

Ikiwa imeshaingia saa tatu, Ankia ndiyo alikuwa anaelekea kuivisha wali huko, nami nilikuwa nimemsimulia namna ambavyo Miryam alinifunulia hisia zake na kukubali tuanze mahusiano rasmi kabisa. Akanipongeza nakwambia, yaani utafikiri hatukuwahi kufanya mineng'emuo kabisa, na ndiyo nikawa nimemuuliza kuhusu Bobo sasa. Ankia alikuwa anajifanya kama vile hajui naongelea nini, lakini mwishowe akakiri kuwa ni kweli alianza kutoka kimahusiano pamoja na yule kaka, ingawa aliyapeleka taratibu ili kuhakikisha haumizwi. Na yeye nikampongeza pia.

Muda huu wote tangia nirudi kutoka gym, nilikuwa nasubiri tu Miryam anitumie ujumbe au nini, lakini hakufanya hivyo. Nikawa nimejaribu kumtumia ujumbe wa salamu, lakini hakujibu, hivyo nadhani alikuwa na shughuli bado. Nilikuwa nimemcheki na Tesha pia, ambaye bado hakuwa amerudi hapo kwao, hivyo nikaona nimuage tu Ankia kwa ufupi ili nikawasalimie wakina Bi Zawadi, kisha ningerudi kula. Kilikuwa kisingizio tu maana niliwashwa kweli kutaka kumwona bibie, kwa hiyo nikavaa malapa na moja kwa moja kwenda hapo kwake.

Nilipoingia tu getini, gari lake Miryam lilikuwa hapo nje, na pale varandani alikuwepo Shadya pamoja na bibie mwenyewe. Miryam aliketi mkekani huku akiwa anakwangua nazi kwenye mbuzi, na Shadya aliketi pembeni yake tu akiwa kama anampa umbeya mpwa wake. Miryam alivalia lile dera lake la kijani huku nywele zake zikiwa zimefunikwa kwa kilemba, na baada tu ya kuniona, akaacha kukwangua nazi na kuachia tabasamu hafifu kunielekea.

Nikaanza kuelekea hapo huku nikijitahidi kubana la kwangu, na Shadya akaita jina langu kama njia fulani ya kuniambia 'karibu.' Hii bado ilikuwa saa tatu, na ilinishangaza kidogo kukuta Miryam anakwangua nazi wakati huu. Alifika mapema nafikiri ile saa kumi na mbili, kwa hiyo sikujua kwa nini upishi ulikuwa umechelewa namna hiyo. Miryam akaendelea kukuna nazi, nami nikasogea mpaka hapo varandani nikiwa natabasamu kumwelekea Shadya.

"Habari za hapa wapendwa?" nikawasalimu.

"Safi tu," Shadya akasema hivyo.

"Salama," Miryam akaitikia pia.

"Ndo' umerudi?" Shadya akaniuliza.

"Ah, hamna, nilikuwepo tu toka kitambo. Kuna mishe nilikuwa nafanya kidogo... nilienda tu na gym kupasha kidogo, nikarudi tena," nikasema hivyo na kumwangalia Miryam usoni.

Miryam yeye akawa amejikausha kama vile hana muda na mimi na kuinamisha uso wake tu. Sikuiona simu yake hapo alipokuwa, hivyo ni wazi aliiacha ndani.

"Ahaa... ulikuwa umeenda kuongeza misuli kidogo," Shadya akasema hivyo.

"Eeeh..." nikakubali.

"Angalia usije ukakonda mashavu," Shadya akaniambia hivyo.

"Hahah... hamna, sizidishi. Halafu kidogo nisahau... jamani, Shadya shikamoo yako mkubwa," nikamwambia hivyo.

"Marahaba mwanangu. Na hili joto, angalau umekuja tununuliwe na soda," Shadya akasema hivyo.

"Ah, hapo usiwaze. Mnyama nmefika," nikamwambia hivyo.

Miryam akanyanyua uso na kunitazama usoni kwa mkazo.

"Hahaaa... eti mnyama! Tutoe jero jero basi tununue Afiya hapo kwa Fatuma," Shadya akasema hivyo.

"Aaaa... jero! Yaani badala uombe elfu kumi, unaomba jero? Jero na we' wapi na wapi?" nikamwambia hivyo.

"Hahaaa... usinifurahishe mie! Mbona itakuwa poa sana!" Shadya akasema hivyo huku akimtazama Miryam.

Miryam akawa ananiangalia kwa macho yenye kuhukumu, kimasihara yaani.

Shadya akasimama kabisa na kuninyooshea kiganja huku akisema, "Nitoe jembe langu la faida. Nachukua hapo sasa hivi."

"We' mwenyewe ndo' unaenda?" nikamuuliza hivyo.

"Eeh, nafata mwenyewe. Nipe," akasema hivyo.

Nikaingiza mkono mfukoni na kujifanya natafuta hela kwa bidii kweli, huku nikiona jinsi Miryam alivyokuwa akinitazama kwa macho makini, nami nikatoa sarafu mbili za mia tano na kumpa Shadya.

"Ih! Sa' ndo' nini JC?" Shadya akauliza.

"Inabidi tu upokee. Elfu kumi imegoma kutoka," nikamtania namna hiyo.

Akacheka kidogo na kusema, "Kumbe na we' mzushi tu..."

"Ahahahah... siyo sana. Maisha magumu..."

"Magumu wapi, mwone! Kama siyo uchoyo... wakati juzi umempa shangazi malaki kabisa..." Shadya akasema hivyo huku akianza kuvaa ndala.

"Ahahah... basi nisamehe. Ila na yako itakuja tu," nikamwambia hivyo.

"Siyo mbaya mwaya. Mimi, ngoja nifate Afiya tupoze koo..." Shadya akasema hivyo.

Akaelekea nje, nami nikamwangalia Miryam na kukuta anaendelea na kazi yake tu. Nikamfanyia 'pss, psss,' naye akaniangalia na kuninyooshea kidole chake kama kunionya nisimfanyie hivyo, nami nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Mbona unakuna nazi muda umeenda?" nikamuuliza.

Akaacha kuniangalia na kusema, "Niliyemwagiza alete vitu alichelewa."

"Mmmm... na tokea muda ule hauku...."

Kabla sijamaliza kuongea, mlango wa kuingilia ndani hapo ukafunguka, na binti Mariam akawa ametoka. Nikatabasamu kiasi, na moja kwa moja binti akawa amenifata na kunisalimia, kisha kwa lazima nikavutwa ili twende ndani. Sikuwa nataka kumwacha bibie, yaani nilitamani nikae tu hapo niendelee kuongea naye kuhusu chochote, ila sikuwa na jinsi. Yeye mwenyewe alikuwa amekaza tu, ile kuvunga kwamba hatuna uvutano wowote bado ni kitu tulichohitaji kufanya kwa sasa na ndiyo alikuwa makini nacho.

Hivyo nikachoma ndani, nikakutana na mama wakubwa tena tokea ule mchana nilipowaacha, nasi tukakaa kupiga story mbili tatu. Shadya alirejea na kumletea Mariam juice ambayo ilipaswa kuwa ya Miryam, kwa kuwa bibie alimwambia ampe mdogo wake kama mbadala. Miryam akawa anapita na vyombo kuelekea jikoni, akishughulika na mapishi, na Mariam alikuwa akimsaidia. Sikupata nafasi ya kutazamana naye tena, wala kumtumia tu ujumbe kwa sababu simu yake ilikuwa chaji, na ile imefika mida ya saa nne, Ankia akanipigia simu kuniambia kwamba alikuwa amenipakulia; niende. Dah!

Ikanibidi niwaage tu hawa, huku moyoni nikiwa nimeumia kutoweza kutoa wonyesho wowote ule wa uvutano baina yangu na bibie, maana aliigiza vyema kama vile hatuna dili. Mariam alikuwa anataka nibaki mpaka chakula kiive hapa kwao, lakini nikamwelewesha tu kuwa Ankia alikuwa ameshapakua kabisa, kwa hiyo ningeenda kula ili asijisikie vibaya. Mama wakubwa wakanipa sapoti pia, na hatimaye binti akaniachia. Nilipotoka tu, nikamtumia Miryam ujumbe mfupi nikimwambia kuwa asiache kunicheki akitulia, nami ndiyo nikaelekea kwa Ankia.

★★

Msosi wa Ankia ulikuwa mzuri, wali na samaki, nasi tukala pamoja huku story zikiwa juu ya suala la Bobo kutoka na Ankia. Mchecheto wangu bado ulikuwepo, yaani nilikuwa nakula huku naongea na Ankia, lakini akili yangu yote ilikuwa kwenye simu. Nilikuwa nimeiweka pembeni nikisubiri iwake, na kila mara ilipowaka kuingiza ujumbe ningeichukua upesi kuangalia kama ni Miryam, lakini matarajio yangu yakawa yanapigwa chini maana ni watu wengine ndiyo waliokuwa wananicheki. Ilikera!

Ankia akawa ameona hilo, naye akaniambia si nimtumie tu ujumbe Miryam badala ya kusubiri yeye ndiyo anitumie, lakini nikazira, nikiiweka simu pembeni na kusema nisingejisumbua mpaka yeye mwenyewe ndiyo anitafute. Ilikuwa ya shingo upande tu hiyo, naye Ankia akasema haya, ila akagusia namna ambavyo aliona nilikuwa situlii kweli. Tulipomaliza kula, nikatulia tu na kuendelea kusubiri lolote kutoka kwa bibie, nikiwa nimeamua kuwa sitamtafuta kweli mpaka yeye ndiyo ashtuke.

Nikakaa na Ankia hapo sebuleni, tukiwaangalia wakina Efendi na nini kwenye TV, hadi inafika saa tano, bibie akawa kimya tu. Mh? Nikawaza labda alikuwa ananisikilizia ili mimi ndiyo nimcheki kwanza, lakini si nilikuwa nimeshatuma sms kadhaa? Kujibu hata mojawapo tu alishindwa? Nikafikiria kuwa inawezekana Miryam angekuwa na shughuli fulani tu iliyomweka bize, hivyo nikaona nikiondoe hiki kimuwasho cha kutaka tuwasiliane muda wote. Sikupaswa kusahau kuwa huyu alikuwa mwanamke mtu mzima mwenye mambo mengi, hakuwa kama pisi nilizopitia.

Ndani ya muda huo huo, Ankia akasema anaenda hapo Masai, Bobo kamwita. Nikampa ile "mhm" kikejeli, naye akanicheka kwa njia ya kejeli na kwenda chumbani kujiandaa. Haya bwana, mimi ndiyo ningebaki na kaupweke wakati ulipaswa kuwa muda wangu wa kuondoa upweke, angalau hata kwa simu tu. Mwenye nyumba wangu akatoka akiwa amevaa T-shirt la mikono mifupi, jeupe, pamoja na kikaptura-skinny kilichofikia mwanzo wa mapaja yake; juu kidogo ya magoti yaani. Alikuwa amejipiga na makunato mwenyewe, naye akaniaga huku akinitania kwa kusema kama vipi nimwite Miryam aje ili nisibaki kununa tu hapo.

Kejeli zote nikazipokea, sawa bwana, naye akawa ameniacha na kwenda huko ikiwa inaingia saa sita. Kwa watu wa aina yake, palikuwa ndiyo pamekucha. Hapo alikuwa ameitwa na bwana wake, wakanywe na kujifurahisha bila shaka, na kama ni kitu ambacho sikuwa nimesema awali, ni kwamba kwa kipindi hiki Bobo ndiye aliyekuwa ameachiwa usimamizi wa Masai YOTE, yaani awe kama mmiliki, lakini kwa muda tu. Kuna madili na madili inaonekana yalikuwa yamefanywa baada ya Bertha kukamatwa na Chalii kuuawa. Hivyo Ankia alikuwa analishwa bata haswa.

Mzee nikabaki sofani tu huku naitazama TV utadhani nina ugomvi nayo, nikiwa nimeshaghairi kuishika tena simu maana saa sita ilikuwa inatembea tu bila ya Miryam kuwa amenicheki. Nikawaza labda hata angekuwa ameshalala, si unajua labda uchovu na nini, kwa hiyo nikaona ni bora nichukue simu tu ili nimtumie ujumbe wa kumtakia njozi njema. Nikaishika simu, na ile nataka kumtumia ujumbe, ikaanza kuita hapo hapo. Tabasamu hafifu likajengeka usoni kwangu, maana ilikuwa ni bibie mwenyewe ndiye aliyepiga, nami nikapokea na kuweka sikioni.

"Hello..." sauti yake tamu ikasikika.

"Ndiyo ukaona unichunie mpaka sa'hivi, eti?" nikamuuliza hivyo nikijifanya nimeudhika.

"Ooh, I'm sorry... yaani, nilikuwa nimetingwa na kazi, yaani.... ah..." akaongea kama vile amechoka mno.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Usijali, naelewa."

"Yaani nisamehe tu. Kuna jambo nafix hapa, kila mara linakua tu... nikashindwa hata kushika simu..."

"Ishu gani unadili nayo?"

"Ni ishu ya Mamu tu, hamna kwere. Nimemaliza kuandika, nilikuwa naandika barua fulani hapa..." akasema hivyo.

"Okay sawa. Nilidhani labda ungekuwa umeshalala..." nikamwambia.

"Hamna, bado niko macho. Yaani ndiyo nimeziona text zako za muda ule sa'hivi. Pole nimekuonea mno, eti?" akaongea kama ananibembeleza yaani.

"Ah, wala usijali. Me niko poa..." nikajibu kwa unyoofu.

"Mbona nahisi kama umenuna?" akauliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Mh? Ninune nini sasa?" nikauliza hivyo huku nikitabasamu.

"Si nimekufanya umenisubiri mno?"

"Wala hata, akusubiri nani? Ndo' kwanza hapa nasinzia," nikamwambia hivyo kiutani.

Akacheka kidogo, naye akaniambia, "Haya, usiku mwema basi..."

"Ih, we' unaenda wapi? Em' tulia hapa," nikamwambia hivyo.

Akacheka tena, kisha akasema, "Sawa. Niambie."

"Ulikuwa umeshapanda bed?" nikamuuliza hivyo.

"Ndiyo nimetoka kujimwagia, nataka kupanda ndiyo," akasema hivyo.

"Nataka kukuona," nikaongea kwa sauti ya chini.

"Tuongee kwa video call?" akauliza.

"Hamna. Nataka nikuone kabisa," nikasema hivyo.

Akatulia kidogo, kisha akasema, "Kivipi, yaani... hapo nje?"

"Mmm," nikakubali.

"Jayden... sa'hivi usiku..."

"Siyo sana bwana..."

"Mh... ahah... umeshaniona leo, mara nyingi tu. Tutaonana kesho, ama tuongee kidogo kwa video call," akasema hivyo.

"Mm-mm... Nataka kuonana nawe live... kidogo tu. Nimeshaku-miss," nikaongea kwa sauti yenye kubembeleza.

"Lakini... wengine washalala...."

"Please... kidogo tu. Natoka hapo nje, nakuona tu ukutani, then unarudi ndani chap," nikamshawishi zaidi.

Nilikuwa napigia picha sura yake nzuri akijishauri na kujishauri, naye akasema, "Sawa. Natoka upesi."

"Me nishafika," nikamwambia hivyo.

Hapo hapo nikaruka kutoka sofani na kuukimbilia mlango, moja moja mpaka nje na kusogea hadi kwenye ukuta wa uzio. Sasa je! Ankia alidhani ningeboeka eti, si niko hapa sasa? Araa!

Sikuwa nimekata simu, nami nilipokuwa nimesimama, matobo ukutani yaliniruhusu kuuona mlango wa kuingilia ndani kwao bibie, na hapo nikauona ukifunguka na Miryam mwenyewe akisimama sehemu hiyo. Akatabasamu, mimi pia nikampa tabasamu, naye akaiweka simu sikioni na kuongea kwa sauti ya chini sana, akisema amefurahi kuniona tena. Lakini mimi nikamwambia nilitaka aje mpaka hapa, hata nimguse tu, naye akawa anaona kama namsumbua.

Nikaendelea kumbembeleza aje, kwa ile sauti ya Alikiba 'ooooh aje...' naye akayeyusha chuma. Akarudi ndani zaidi na kurejea na funguo, kisha akalifungua geti la mlangoni kwa uangalifu na kutoka, akiwa hajasahau kuvaa ndala zake miguuni. Nikakata simu hatimaye na kuendelea kumwangalia hadi alipokaribia sehemu niliyosimama, na alikuwa amevalia ile nguo yake ya kulalia, huku nywele zake akizivalisha kikofia laini kichwani.

Akasogea hadi hapo ukutani, nyuso zetu zikitenganishwa na hilo uzio, na kwa sauti ya chini akasema, "Ila Jayden! Mbona we' msumbufu sana?"

"Yaani kama vile haunijui! Umeshasahau nilivyokuwa nakusumbua mpaka ukakubali muziki wangu? Na bado..." nikamwambia hivyo kiutani.

Akaniangalia kimkazo eti, halafu akasema, "Umeridhika sasa? Nenda ukalale."

"Tesha amerudi?" nikamuuliza.

"Hamna. Amelala huko kwa rafiki yake," akasema hivyo.

"Haya, njoo..." nikamwambia hivyo.

"Wapi?" akauliza hivyo kimshangao.

Nikamwita kwa kiganja huku nikirudi nyuma zaidi usawa wa huo huo uzio na kusimama, ambao kwa upande wake ungekuwa ni ule usawa wa bomba lao la maji hapo nje. Bado palikuwa na ugiza maana taa haikuwa imebadilishwa.

Miryam akatembea kwa uangalifu ili asitoe sauti kubwa ardhini, na alipokaribia hiyo sehemu, akauliza kwa sauti ya chini, "Unataka kufanya nini wewe?"

Nikampitishia simu yangu hapo hapo kwenye tobo moja ukutani, nikimwambia kwa ishara kuwa aichukue, naye akaipokea huku akiniangalia kwa kutoelewa. Hapo hapo nikaanza kupanda huo ukuta, mpaka juu, nikajitahidi kuwa mwangalifu sana ili nisikanyage vyupa na nondo zenye kuchongoka zilizokuwa kwa hapo juu. Miryam alishangaa! Akafunika mdomo wake kwa viganja huku akiniangalia kama vile haamini, nami nikafanikiwa kuvuka upande wetu na kushuka mpaka sehemu aliyokuwa amesimama yeye. Ukuta wa uzio haukuwa mrefu sana.

Baada ya kufika chini na kumgeukia, nikaona namna ambavyo alikuwa ananiangalia kimaswali sana, nami nikajitabasamisha kimchezo tu na kumtikisia nyusi kiuchokozi.

Akasema, "Jayden una... una matatizo gani?"

Nikaichukua simu yangu na kuiweka mfukoni, halafu nikakishika kiuno chake na kumvuta karibu zaidi na mwili wangu kwa makusudi.

"Wewe!" akasema hivyo kwa kunong'oneza huku akiangalia pembeni kwa njia ya tahadhari.

"Niliposema nataka kukuona, nilimaanisha hivi," nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu.

"Ja.... hii siyo akili. Una... unawaonyesha wezi kwamba hapa ni rahisi kuingia..."

"Wezi gani, Miryam? Mwizi pekee aliyepo hapa ni mimi... na tayari nimeshauiba moyo wako," nikamwambia hivyo kizembe.

Akalibana tabasamu lake la haya, kisha akaangalia pembeni na kusema, "We' ni kichaa."

"Umeona eh? Yaani sina akili ikija juu yako..."

Akapiga ulimi kidogo na kusema, "Niachie bwana... hebu nenda. Saa saba inakaribia, halafu... natakiwa niamke mapema."

"Mbona bado mapema?" nikamuuliza hivyo bila kumwachia kiuno.

"Ahh... sitanii Jayden. Natakiwa nilale usingizi wa kutosha hata masaa machache. Nina safari kesho," akasema hivyo.

Kauli yake ikanifanya nimwachie kiuno taratibu, naye akatulia hapo hapo tu akiniangalia kwa hisia. Aliona imevuta umakini wangu.

Nikamuuliza, "Safari ya wapi tena?"

Akainamisha uso wake kwa ufupi, kisha akanitazama na kuniambia, "Nitaenda Morogoro."

"Moro? Unaenda kufanyaje?"

"Naenda tu kucheki haya masuala ya shamba la Mamu. Watunzaji kule wana... malalamiko fulani... so naenda kuweka mambo sawa,"

"Ahaa, ndo' ulichokuwa unafanyia kazi?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Okay. Lakini... kesho si ni send-off ya Doris? Utaikosa?" nikamuuliza.

"No. Nachukua treni ya mwendokasi..." akajibu hivyo.

"Ooh, kwa hiyo unaenda fasta tu na kugeuka..."

"Eeeh... na natakiwa niondoke mapema kabisa. Nataka nifike huko kwenye saa mbili, nishughulike na hayo mambo, halafu niwahi kurudi. Yaani kama ni kuchelewa, kumi na mbili jioni niwe huku tayari..."

"Okay. Na siku hizi Dar na Moro ishakuwa kama Mbagala na Kariakoo..."

"Ahah... teknolojia. Ila ndo' maana nimekwambia nataka kuwahi kulala, saa kumi na moja niwe nimeshaamka... halafu we' kichwa umenibana tu hapa..." akasema hivyo.

"Ahahah... utanilaumu? I'm so addicted to you..."

"Kwani hiyo ni makosa yangu?"

"Ya nani sasa?"

"Ni yako. Jifunze kujizuia. Siyo lazima mpaka unione kila mara..." akaniambia hivyo kwa uhakika.

Nikamkazia macho kiasi.

"Eeeh... si tungeweza hata kuongea kwa video call? Ya nini hadi unaruka ukuta ili eti uniguse? Yaani wewe!" akaongea hivyo huku akiniangalia kama amekerwa.

"Ah, basi tu, sa' nitafanyaje? Sijisikii fresh kutokukuona live kwa muda mrefu. Unakumbuka kama kuna siku yoyote imepita sijakuona tokea nilipokwambia nakupenda?" nikamuuliza.

"Mhm... hapana..."

"Ndiyo hivyo. Yaani we' ni dawa ya kila kitu kwangu, nikikuona napona..."

"Na kesho je? Tuseme nikaenda, nikachelewa kurudi, halafu nikapitilizia kwenye sherehe na tusionane kabisa mpaka kesho-kutwa... itakuwaje?" akauliza hivyo.

Nikatulia kidogo nikimtazama machoni kwa hisia sana, nami nikamwambia, "Tutaenda wote."

Akakunja uso wake kimaswali na kuuliza, "Wapi? Moro?"

Nikatikisa nyusi kukubali.

"Wewe! Acha masihara yako basi... ahahah..." akashangaa kidogo.

"Sitanii. Nataka niende nawe," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

"Ahah... Jayden, hii ni safari ya kikazi, siendi kuzurura...."

"Hata kama. Nataka tu niwe pamoja nawe," nikamwambia hivyo.

"Kwa hiyo... kweli kabisa unataka tuondoke pamoja?"

"Yeah. Nitakusindikiza, na me nina muda sijaondoka jijini... itakuwa kama tour ndogo. Whatcha say?" nikamuuliza hivyo.

"Eh... mhm... yaani naona unataka kukaba kila kitu sasa..."

"Kabisa. Sitaki yaani... sitaki nihisi uko mbali nami kabisa Miryam. Yaani kila mara nataka tu nikuone, niwe karibu yako, nihisi uwepo wako... inanipa amani sana," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Akaniangalia kwa ufikirio kiasi, kisha akaniambia, "Unavyoongea hivyo... inavutia. Lakini sijui kwa nini, nakuwa nahisi ni maneno rahisi sana kwako kusema kwa sababu labda umeshayatumia kwa wengi..."

Nikatikisa kichwa kiasi kukataa na kumshika mkono, nami nikamwambia, "Najua Miryam, najua ndiyo tumeanza, na ninaelewa kwamba hatujatoka pazuri mno. Sitarajii moyo wako uwe umeshafunguka kwa kila kitu, yaani... najua bado unataka kuwa mwangalifu. Sitakuhakikishia kwamba nakupenda kwa maneno tu, nitakuhakikishia na kwa matendo pia. Ndiyo itakuwa sehemu ya kukufanya uache kuogopa."

"Ahah... okay, ni sawa. Nisamehe tu lakini, maana sometimes nakuwa...."

"Usijali. Nakuelewa," nikamwambia hivyo na kumshika shavuni taratibu.

Akabaki akinitazama usoni kwa macho yenye imani sana.

Nikamwambia, "Najua sitaenda na wewe kila sehemu utakayoenda, lakini popote ambapo naweza kuwepo kwa ajili yako... nitakuwa hapo Miryam. Ndiyo nachotaka kufanya hasa kwa wakati huu. Natamani kama... ningeweza ku-rewind muda yaani... ningeurudisha muda nyuma na kukupata kipindi hichoo..."

"Ahah... si ungekuwa mdogo wangu sana?" akauliza hivyo kwa hisia.

"Yeah, lakini haingejalisha. Ningekupata tu na kukupenda, na ningekuonyesha huo upendo kwa muda mrefu zaidi mpaka kufikia huu wakati ambao tumesimama hapa... na kuendelea," nikamwambia hivyo kwa sauti yenye kubembeleza.

Akakishika kiganja changu huku akiniangalia machoni kwa hisia sana.

"Sikudhani ingewezekana tena Jayden kuja kupenda kutoka moyoni. Yaani sikufikiria ningekuja kupenda tena namna hii, na sikujua kama ningekuja kupenda kila kitu kuhusu mtu hadi nilipokutana na wewe Miryam. Yaani ninakupenda zaidi ya ninavyokupenda sana," nikamsemesha kwa hisia.

Akatabasamu zaidi huku akisugua kiganja changu taratibu kwa vidole vyake laini, naye akauliza, "Huwa unayatoa wapi hayo maneno Jayden?"

Nikatabasamu tu na kumwambia, "Nayasomaga tu kwenye mitandao, ndo' nakuja kuyamwaga hapa..."

"Oooh... kwa hiyo kumbe nafikishiwa tu mawazo ya mtu mwingine hapa, eh?" akauliza hivyo kiutani.

"Oops! Nimekamatika..." nikaongea kikejeli.

"You fool!" akaniambia huku akitabasamu.

Sote tukacheka kidogo kwa pumzi.

Akatikisa kichwa kuonyesha uthamini, naye akasema, "Asante sana kwa kunipenda. Ninakupenda sana pia."

"Yaani tulivyo... kama Romeo na Juliet," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu zaidi kwa furaha.

Nikauachia uso wake na kuuliza, "So... kesho nitakusindikiza Moro, eh?"

"Sawa. Tutaenda pamoja. Aa... nafikri hapo stendi zinakuwepo gari zinazoenda Stesheni... sijajua sana, ila tuta...."

"Tutapanga tu pa kukutana, afu' tutaenda pamoja, tutajua," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kukubaliana na hilo.

Nikavishika viganja vyake vyote kwa chini na kusema, "Okay. Basi ngoja nikuache ukalale sasa. Me huwa nina usingizi mzito kwa hiyo nitaweka alarm."

"Kumi na moja, sharp," akaniambia hivyo.

"Mm-hmm," nikakubali.

"Haya, usiku mwema, nenda sasa. Uruke ukuta kwa uangalifu... na iwe mwanzo na mwisho," akasema hivyo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Go!" akaniambia hivyo kwa msisitizo.

Nikaangalia juu, kisha nikaanza kuimba kwa sauti ya chini, "Basi nichumu, ni-kiss mwah.. ai nichumu, ni-kiss mwah..."

Nikamwangalia tena na kukuta anatabasamu kwa ile njia ya kuhukumu, akinishusha na kunipandisha eti, nami nikatabasamu kwa furaha.

Akanicheka kidogo kwa pumzi, kisha akasema, "Una hakika ulikuwa umeshasugua kinywa?"

Nikakunja uso kimaswali.

"Kama huoshagi mdomo kabla ya kulala, hiyo chum ndo' huipati," akasema hivyo kiutani.

"Ih! Kumbe umeshatoa na kitabu cha masharti afu' bado hujaniuzia?" nikamuuliza hivyo kiutani pia.

Akacheka kidogo huku ameziba mdomo.

"Na sasa hivi ndiyo unaniambia sharti la kwanza wakati hata nilikuwa sijaliandaa hili domo? Basi usiku mwema..." nikamwambia hivyo nikijifanya nimeudhika.

Bado alikuwa anacheka, nami nikaigiza kutaka kupanda ukuta, lakini akaishika T-shirt yangu na kuivuta huku akisema, "Hebu njoo hapa..."

Nikageuka na moja kwa moja kukutana na mdomo wake ulionifuata bila kusita. Ah!

Miryam alipatia aisee. Alijua. Zamu hii hakunipiga busu, alinila denda! Denda ya maana! Aliufinya mdomo wangu kwa midomo yake taratibu sana, akiepuka kutumia ulimi mwanzoni na kuacha midomo yetu pekee ndiyo ivutane, kisha ndiyo akaingiza ulimi wake ndani yangu na kutoa penzi la mdomo kwa ufundi ambao sikuwa nimeutegemea kabisa! Alikuwa na midomo mitamu, akipenda nimwachie tu yeye ndiyo aonje kila alichotaka kula, na katika hali ya kunogewa zaidi, akakishika kichwa changu kwa mikono yake yote na kuanza kukipapasa taratibu kama vile hataki tuache. Sijui hata aliweka wapi simu yake. Nilisisimka nyie!

Nikakishika kiuno chake kwa njia ya kukumbatia, kwa nguvu, bibie akiwa amenogewa tu kunipa denda hii tamu sana, miguno laini ya pumzi ikimtoka kadiri alivyoendelea kunipatia utamu wa ulimi wake, na nilikuwa nimeshasimama dede kwa nguvu kubwa sana. Yaani hapo nikasahau yote, nikiwa tayari kwa lolote lile ambalo angefanya lifuate, maana hisia zilikuwa huko juu juu yaani. Ndoto ilikuwa inatimia hapa!

Ilionekana ni kama dakika nzima ilipita akiwa ananipandishia moto kwa denda hii, ndipo akaikatisha taratibu na kuweka paji lake la uso usawa wa shavu langu. Nikafumbua macho na kuona yeye akiwa amefumba ya kwake bado, akiwa anazungusha kichwa chake taratibu na nyuso zetu zikiwa kwa ukaribu mno, nami nikatabasamu na kubana ubavu wake kwa kiganja changu, katika njia ya kumtekenya, naye akapandisha nyonga kidogo na kufumbua macho yake kuniangalia.

Aliniangalia kwa njia yenye hamu, kisha akaweka kiganja chake kifuani kwangu na kusema, "I really like this, Jayden. But I don't want us to go too fast..."

Aliongea kwa sauti tamu mno yenye kunong'oneza kiasi, yaani hata kama hakuwa akitaka tupeleke mambo mengi haraka sana, hapa tu tayari alikuwa ameshanipeleka mawinguni huko.

Nikiwa namwelewa, nikamwambia, "Usijali. I got you."

Akarudisha uso wake nyuma na kunitazama kwa hisia, naye akasema, "Tutaonana baadaye."

Nikatikisa kichwa kukubali hilo, ndiyo nikakiachia kiuno chake na kuusogelea ukuta. Nikapanda taratibu na kwa uangalifu sana, yeye bado akiwa amesimama hapo hapo, nami nikashukia upande wa kwa Ankia na kumtazama tena. Akanipungia mkono wa kwa heri ya sasa, nami nikaunda kopa kwa viganja vyangu na kumwonyeshea kwa kuiweka usawa wa moyo. Akatabasamu kwa hisia sana, kisha huyoo akaelekea ndani kwake.

Nikageuka tu na kuelekea ndani kwetu pia, nami nikafunga mlango na kutulia hapo sebuleni kwanza. Nikajikuta najishika mdomo wangu, nikitabasamu kama zezeta yaani kwa kukumbukia hiyo "chumu" niliyopewa hapo nje, na bado hapa chini palikuwa pamevimba eti! Nilikuwa na hisia nzuri sana, sana, sana, kwa wakati huu, na najua zingeendelea kupanda juu zaidi kadiri ambavyo siku zingeendelea.

Na huyu mwanamke alionekana kuyajua mapenzi kwelikweli, siyo mchezo, yaani nilikuwa nina hamu ya kuyatalii naye mengi sana kutokea hapa. Kwa kuwa siku ya kesho ningekwenda naye Morogoro, ningetakiwa kujiweka katika uimara wa kiume ndani ya akili, ili kama utalii wa kwanza ungefanywa hiyo hiyo kesho, uwe wa maana. Ona, nilikuwa hadi nimeanza kuwaza upuuzi mapema namna hii!

Lakini najua hilo lingekuwa jambo hakika kufanyika baina yangu mimi na yeye, haijalishi lini, kwa hiyo kweli utayari ulihitajika maana nilikuwa nimeshamhamu kwa muda mrefu sana sasa huyu mwanamke. Nikaona nizime taa na kwenda kulala, yaani nikajitupia kitandani huku natabasamu tu na kufurukuta-furukuta huku na huko kwa kuhisi mihemko ya hatari, nikiingoja alfajiri ifike ili niondoke na mwanamke wangu.







★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI

★★★★★★★★★★★★★★★★


Niliendelea kumkumbatia Miryam kwa sekunde chache nikiwa nahisi furaha sana, kisha nikamwachia na kumtazama usoni kwa hisia sana. Yeye pia alikuwa akiniangalia kwa macho yenye hisia kwelikweli, nami nikatikisa kichwa kidogo nikiwa yaani bado siamini-amini.

"Aisee! Yaani sijui hata niseme nini..." nikaongea hivyo kwa hisia.

Akatabasamu tu na kuendelea kuniangalia kwa upendo.

Nikasema, "Wee... ume... umefikaje hapa haraka hivi? Yaani... usiniambie umekimbia kutokea Kijichi..."

Akacheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Kwani hujui kwamba nina gari?"

"Ahahah... this is amazing..." nikamwambia hivyo kwa sauti yenye hisia sana.

Akabaki akinitazama usoni kwa macho yenye upendo mwingi, nami nikalishika shavu lake kidogo huku nikimwangalia kama vile nataka kumtafuna, siyo kwa ubaya, ila kwa hamu nzuri na kubwa sana niliyokuwa nayo kumwelekea. Ndipo sauti ya koo kusafishwa ikatokea pale sebuleni, nami nikaangalia hapo na kuona Ankia alikuwepo bado. Miryam akageukia huko pia.

Nikasema kwa kujishaua, "Ankia? Kumbe bado upo?"

"Ulifikiri me jini nimepotea, au?" Ankia akaniuliza hivyo.

Miryam akatabasamu kiasi.

"Kwanza unatakiwa uwe umeshapotea, unafanya nini hapa? Hebu... go away..." nikamwambia hivyo Ankia kiutani.

"Mm? Yaani ndiyo umeshaanza na kuringa..." Ankia akaniambia hivyo kwa njia ya nyodo.

"Siyo kuringa, we' si ulikuwa unaenda dukani? Nenda..." nikamwambia hivyo.

Ankia akaniangalia kwa njia yenye nyodo na kuikunja midomo yake, na Miryam akacheka kidogo tu na kujishika shingoni.

Nikamfanyia Ankia ishara ya kumfukuza kwa kiganja na kumwambia, "Shoo!"

Ankia akacheka kwa mguno, naye akamwambia Miryam, "Baadaye mpenzi."

Miryam akatikisa kichwa kukubali heri hiyo, naye Ankia akawa ameondoka hatimaye. Raa!

Miryam akanigeukia na kunitazama usoni tena, nami nikamwangalia na kujichekesha kidogo kwa haya eti. Nikawa nahisi hali ya utete kidogo, nikiangalia pembeni huku napiga-piga kiganja changu kimoja mguuni, kisha namwangalia tena na kukuta amenikazia jicho tu, halafu sote tukajikuta tunacheka kidogo kwa kupatwa na hisia nzuri sana.

Ndipo nikamwambia, "Karibu. Njoo ukae... aa... namaanisha... siyo humu chumba... yaani... kama... utapenda tukae humu... chumbani.... au, pale... sofani... simaanishi ukiingia chumbani nita... siyo kwamba nafikiria hivyo... ila we' ndo' unaweza ukawa unafikiria... siyo kwamba... namaanisha... sikuoni unawaza... dah, naharibu aisee..."

Miryam akacheka kidogo na kutikisa kichwa chake, naye akasema, "Wasiwasi wa nini sasa tena?"

Nikafumba jicho moja na kumwangalia kwa kujihami eti.

"Ahah... me ndiyo ningetakiwa niwe na wasiwasi, maana...."

Kabla hajamaliza kuongea, nikamkumbatia kwa mara nyingine tena ili kumpa kitulizo, ambacho na mimi kwa upande wangu nilikihitaji sana. Nilihisi amani kubwa sana moyoni, na nilihitaji aihisi pia. Nikawa nimemshikilia huku nikiyumbisha miili yetu taratibu kama vile nambembeleza yaani, naye alikuwa ameiweka mikono yake mgongoni kwangu na kuitembeza taratibu huku amenilalia begani kwa raha zote. Yaani!

Nikiwa bado nimemkumbatia, nikasema kwa sauti ya chini, "Vipi tukikaa?"

Akajibu kwa sauti yake tamu, "Wazo zuri."

Nikamwachia taratibu kabisa, halafu tukatazamana machoni kwa hisia sana, kisha nikakishika kiganja chake na kwenda naye mpaka pale sebuleni na kuketi sofani. Akakaa pembeni yangu pia, huku nikiwa nimekishika kiganja chake bado, naye akakiweka kingine juu ya mkono wangu, na chenyewe nikakishika.

"Umeni-surprise sana Miryam..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Najua. Samahani kwa hilo."

"Samahani ya nini sasa? Haujui kwamba umenipa furaha sana?"

"Wakati tayari nilikuwa nimeshakuvunja moyo?" akasema hivyo huku akiniangalia usoni kwa umakini.

Nikatulia tu na kuendelea kumwangalia.

Akasema, "Jayden... I'm sorry. Nimekutesa sana... I know..."

"Usijali. Nilikuwa nakuelewa."

"Still, yaani... nimekufanyia vibaya mno. Pamoja na yote, umefanya vingi sana kwa ajili yangu kunithibitishia unanipenda, lakini nikawa nakupiga mateke tu. Najua nilikuwa nakuonea sana, na naomba tu unisamehe kwa leo... yaani bado nilikuwa nimechanganyikiwa..."

"Ulichanganywa na nini?"

"Kila kitu. Nilikuwa najiuliza... kwa nini niko hivi. Nimekupenda pia, lakini bado tu nikawa najipofusha kwa kiburi changu...."

"Miryam..."

"... ambacho kinanifanya nijione kuwa sahihi kwa kila kitu. Umenifundisha sana, umeshanionyesha kwamba kuwa hivyo haifai, lakini bado nikawa sielewi. Ni kweli," akasema hivyo kwa hisia.

Nikaanza kusugua kiganja chake taratibu.

"Leo... nimeshindwa Jayden. Nimeshindwa kuendelea kujifanya mgumu tena. Nakupenda. Na ninakuhitaji. Sijui kingine tena," akasema hivyo.

Nikatabasamu kiasi kwa hisia.

"Lakini... bado naogopa. Na baada ya ulichoniambia leo, nimetambua kuwa nakuhitaji zaidi sasa ili niache kuogopa tena. Umesema unaniona me kuwa kama msaada kwako..."

"Yeah, kabisa."

"Well, na mimi nakuona kuwa msaada wa moyo wangu. Nimetambua pia kwamba wewe ndiyo kipande cha pili cha moyo wangu kinachokosekana ili kuufanya uwe kamili, na ninakuhitaji uwe karibu nami ili uunganike pia na kuwa kitu kimoja," akaongea kwa hisia sana.

Dah! Alikuwa na maneno matamu!

"Kwa hiyo wakati huu mimi ndiyo nimekuja kukuomba nafasi Jayden. Uko tayari kunibeba?" akaniuliza hivyo.

Nikamkazia macho kiasi, nami nikamuuliza, "Hilo ni swali au jibu?"

Akatabasamu na kuangalia chini.

Nikamshika shavuni taratibu, naye akaniangalia. "Kwa asilimia zote, Miryam. Niko tayari. Unalijua hilo."

Akasema, "Mambo yatakuwa mengi, na magumu sa...."

"Usijali Miryam. Niko nawe. We are two parts of the same whole now, and I intend to keep it together no matter what..." nikatia na kimombo kidogo kumfariji.

Akakishika kiganja changu usoni kwake, naye akasema, "Asante."

Nikampa tabasamu hafifu kwa hisia.

Akashusha pumzi na kuangalia chini kwa utafakari, naye akasema, "Nina hamu kubwa... na matarajio mengi kuona ni wapi hii itanifikisha."

Nikamwachia taratibu usoni na kusema, "Hata mimi. Na ninaiona kuwa sehemu nzuri sana, sema ndiyo nataka niifikie nikiwa pamoja nawe."

Akatabasamu na kuendelea kuniangalia kwa hisia sana machoni.

Nikajikuta nimetulia zaidi, nikimtazama kwa njia hiyo hiyo yenye hisia kama yeye tu, na mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakienda mbio kwa sababu ya hisia zangu kunitaka nifanye jambo fulani. Niliiangalia midomo yake na kuona jinsi ambavyo iliachia uwazi kidogo uliofanya mpaka nikahisi kusisimka yaani, na nilipomtazama machoni, akawa bado ameniangalia tu kwa njia yenye subira.

Nikataka kupiga hatua kumwelekea kwa kuusogeza uso wangu karibu zaidi na wake, lakini akaacha kuniangalia na kusema, "Inabidi niingie nyumbani Jayden."

Nikainamisha uso wangu kiasi na kubana midomo, kisha nikatikisa kichwa kukubali hilo. Nilipomtazama usoni, nikakuta ananiangalia huku akitabasamu kiasi, nami nikajirudisha nyuma na kuangalia pembeni kwa njia ya kujishaua. Alikuwa amenisoma huyo!

Nikasema, "Sawa... najua umechoka. Nenda tu... ukapumzike."

Akatikisa kichwa kukubaliana na hilo, halafu akasema, "Na wewe ndiyo ulikuwa unaingia kupumzika bila shaka..."

"Eeh... nilikuwa nahisi uchovu... sijui hata wa nini, ila... sa'hivi umeisha. Nimepata nguvu mpya," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu na kusema, "Vizuri."

Kulikuwa na kale kahali kenye kusisimua fulani hivi, yaani, mpaka raha. Nilimtazama kwa upendo mwingi sana, naye akawa ananiangalia tu kama vile anasubiri nimuage vizuri.

Ndiyo akaniambia, "Narudi hapo Masai kwanza."

"Masai? Kwa nini? Yaani... hauendi nyumbani? Si umesema...."

"Nililiacha gari pale, ndiyo nikaja hapa," akanikatisha kwa kusema hivyo.

"Oooh, sawa. Ngoja. Kwa nini uliliacha gari Masai?" nikamuuliza.

"Nilipokuwa nakuja... sikutaka kuja mpaka huku na gari, hapo nyumbani wangeona maana... nilikuwa nataka kwanza..." akaishia hapo.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Uje kwangu."

Akatabasamu pia na kutikisa kichwa kukubali.

Nikamwambia, "Okay, nimeelewa. Umetumia akili, maana wambea wengi."

"Hapa penyewe nikitoka wakaniona, inaweza kuzua utata..."

"Oh no, haina shida. Sidhani kama ina shida. Hata hivyo we' siyo mgeni hapa, hao wakina Fatuma watajua umekuja tu kumsalimia Ankia labda..."

"Labda..." akasema hivyo na kuangalia pembeni.

"Ahah... naitamani ifike siku ambayo tutatembea pamoja... proud... kila mtu ajue kwamba wewe ni wangu," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu na kusema, "I hope for that day to come too. Ila kwa sasa... tuweke mambo yetu chini kwanza..."

"Yeah, yeah, najua. Chochote kile unachotaka tufanye, nitafata..." nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

Nikiwa namwangalia kwa hisia, nikamwambia, "Asante Miryam. Kwa kunipa hii nafasi. Nitajitahidi kuwa mume mzuri kwako."

Akatabasamu zaidi na kuuliza, "Mume eeh?"

"Ahahah... kidume wako," nikamwambia hivyo na kupandisha nyusi kichokozi.

"Ahah... sawa. Mimi pia. Nitajitahidi kukupa furaha Jayden," akaongea kwa sauti yake tamu sana.

Nilimwangalia huyu mwanamke kwa mapenzi ya dhati yote niliyohisi moyoni, yaani nilipenda sana hii hali aliyokuwa ananifanya niihisi wakati huu. Akiwa ananitazama kwa hisia pia, akanishika shavuni kwa kiganja chake laini, halafu akausogelea uso wangu karibu zaidi na kunipa busu moja, moja tu, ambayo ilinipa msisimko wa hali ya juu zaidi ya msisimko wa busu mia moja ambazo mwanamke mwingine yeyote angenipa!

Midomo yake laini iliikandamiza ya kwangu na kuvutana nayo mara moja tu na taratibu kabisa, naye akaiachia ikiwa imetoa sauti tamu kama vile ametoka kufyonza pipi tamu sana, kisha akajirudisha nyuma tena na kuniangalia kwa hisia. Sasa hapo mimi! Huo msisimko ulikuwa umeniamshia bonge moja la balaa, damu ilianza kunyanyua mdude fulani kwa nguvu isiyopimika, yaani nilihisi mwili wote unaitikia kitendo chake kidogo tu kwa hamu nzito sana. Nikabaki nikimtazama machoni kwa utulivu, huku hisia zangu zikiwa zinafurukuta huku na huko ndani yangu.

Akiwa anasugua shavu langu kwa kidole chake taratibu, akasema, "Nakupenda."

Yaani aliisema hiyo 'nakupenda' katika ile njia ya kiutu-uzima, uhakika yaani, hakuona aibu wala kuhofia kuniambia hivyo. Alijivunia kabisa.

Nikatabasamu tu na kumwambia, "Nakupenda pia."

Nilikuwa nimeweka mkono wangu usawa wa sehemu ya kati kwenye suruali ili kuficha saibu lililokuwa limenyanyuka baada ya yeye kunipiga busu kwa mara ya kwanza kabisa, na mwanamke wangu akanyanyuka kutoka hapo sofani na kuanza kuelekea mlangoni. Ikanibidi niendelee kutulia tu hapo hapo sofani maana sikutaka aone hili dubwana mapema namna hii, bado hayo mazoea sikuwa nimemwanzishia kwa hiyo kujibana ilikuwa lazima. Akafungua mlango na kuniangalia kwa ufupi, nasi tukapeana tabasamu la furaha kwa pamoja, kisha ndiyo akatoka hatimaye. We!

Yaani ile ametoka tu, nikanyanyuka na kuanza kurukaruka hapo ndani, nikapanda na kwenye sofa na kuanza kuruka kwa furaha tele. Nilihisi furaha isiyo na kifani. Nilikuwa kama nimechanganyikiwa. Nikafata na simu yangu chumbani na kuweka muziki wa Jux na Dayamondi "bora kuenjoiiiiii... maisha mafupi ni simpoo," nami naikaanzisha miuno na dansi za kipuuzi ili tu niitoe furaha yangu. Nilicheza wimbo mpaka mwisho, nami nikajitupia sofani na kubaki najichekea mwenyewe tu kwa kuhisi raha kuu mno moyoni mwangu.

Hatimaye Miryam akawa wangu. Dah! Ingebidi kutokea hapa sasa nimwonyeshe namna gani ambavyo alikuwa akiukosa uhondo wa mapenzi kwa huo muda wote alioukosa. Yaani ningemfurahisha, angenipenda mpaka milele. Sikufikiria kuhusu changamoto, sijui matatizo na vikwazo, yaani nilichowazia juu yake ilikuwa ni furaha tu. Ya nini niteseke roho wakati Miryam alikuwa wangu? Hiyo kitu haingekuwa na nafasi tena!

Na ningehakikisha nampa furaha aliyoistahili kwelikweli, ili nami nitulie kwa furaha na amani tele moyoni mwangu. Siku ile nimemwambia ukweli kuhusu hisia zangu nilijipiga mara mbili kifuani ili kujipa moyo katika mbio za kuhakikisha namkamata, na sasa akawa amekamatika, hivyo ningetakiwa kujipiga mara nyingi zaidi kifuani wakati huu kwa kiburi changu chote kuwa ndiyo, nilimpata! Piga kifua kwa masifa kama King Kong yaani! Araa? Hatimaye Miryam alikuwa bibie wangu!

★★

Haukupita muda mrefu sana na Ankia akawa amerejea tena kutoka kazini kwake, ikiwa imeshaingia saa moja, na alinikuta ndani nikiwa najiandaa kutoka. Nilitaka kwenda gym kwanza kuchangamsha mwili kabla ya kuja kwenda kwa Miryam kuwasalimia wapendwa wangu, na muda ule ambao Miryam aliniacha hapa, tuliwasiliana kupitia sms, nikimuuliza ikiwa alifika kwake bila vilongolongo vingi, naye akawa amekubali. Kwa wakati huu akawa akishughulika na mambo fulani ya hapo kwao.

Ankia alikuwa na hamu ya kutaka kusikia mengi yaliyojiri baada ya kuniacha hapa na Miryam muda ule, nami nilikuwa na furaha sana bado lakini kwa wakati huu nilitulia zaidi. Nikamwambia ningekuja kumpa ukweli wote nikitoka gym, ila kiufupi tu ni kwamba ilikuwa siku iliyogeuka kuwa yenye amani kubwa sana kwangu. Sikutarajia yaani. Kwa hiyo ningetakiwa kwenda kuchangamsha mwili kwanza kisha ndiyo nije kumpa ubuyu aliotaka, na yeye nikamwambia atanipa ubuyu niliotaka kama malipo. Hakuelewa namaanisha nini, ila nilikuwa namwongelea Bobo, hivyo ingekuja kuelezeka baadaye.

Nikatoka hapo na kwenda hadi gym ya pale Mzinga, na tayari nilikuwa nimeshaanza kujuana na baadhi ya mangangali waliokuja hapo lakini sikupitilizisha sana mazoea, nami nikanyanyua na kushusha chuma kwa muda wa kama saa moja na nusu, kisha ndiyo nikarudi tena kwa Ankia. Sasa nilikuwa nimechangamka kwelikweli yaani, nikaoga na kuvaa vizuri, kisha ndiyo nikakaa pamoja na mwanamke huyo sebuleni kupiga story kidogo.

Ikiwa imeshaingia saa tatu, Ankia ndiyo alikuwa anaelekea kuivisha wali huko, nami nilikuwa nimemsimulia namna ambavyo Miryam alinifunulia hisia zake na kukubali tuanze mahusiano rasmi kabisa. Akanipongeza nakwambia, yaani utafikiri hatukuwahi kufanya mineng'emuo kabisa, na ndiyo nikawa nimemuuliza kuhusu Bobo sasa. Ankia alikuwa anajifanya kama vile hajui naongelea nini, lakini mwishowe akakiri kuwa ni kweli alianza kutoka kimahusiano pamoja na yule kaka, ingawa aliyapeleka taratibu ili kuhakikisha haumizwi. Na yeye nikampongeza pia.

Muda huu wote tangia nirudi kutoka gym, nilikuwa nasubiri tu Miryam anitumie ujumbe au nini, lakini hakufanya hivyo. Nikawa nimejaribu kumtumia ujumbe wa salamu, lakini hakujibu, hivyo nadhani alikuwa na shughuli bado. Nilikuwa nimemcheki na Tesha pia, ambaye bado hakuwa amerudi hapo kwao, hivyo nikaona nimuage tu Ankia kwa ufupi ili nikawasalimie wakina Bi Zawadi, kisha ningerudi kula. Kilikuwa kisingizio tu maana niliwashwa kweli kutaka kumwona bibie, kwa hiyo nikavaa malapa na moja kwa moja kwenda hapo kwake.

Nilipoingia tu getini, gari lake Miryam lilikuwa hapo nje, na pale varandani alikuwepo Shadya pamoja na bibie mwenyewe. Miryam aliketi mkekani huku akiwa anakwangua nazi kwenye mbuzi, na Shadya aliketi pembeni yake tu akiwa kama anampa umbeya mpwa wake. Miryam alivalia lile dera lake la kijani huku nywele zake zikiwa zimefunikwa kwa kilemba, na baada tu ya kuniona, akaacha kukwangua nazi na kuachia tabasamu hafifu kunielekea.

Nikaanza kuelekea hapo huku nikijitahidi kubana la kwangu, na Shadya akaita jina langu kama njia fulani ya kuniambia 'karibu.' Hii bado ilikuwa saa tatu, na ilinishangaza kidogo kukuta Miryam anakwangua nazi wakati huu. Alifika mapema nafikiri ile saa kumi na mbili, kwa hiyo sikujua kwa nini upishi ulikuwa umechelewa namna hiyo. Miryam akaendelea kukuna nazi, nami nikasogea mpaka hapo varandani nikiwa natabasamu kumwelekea Shadya.

"Habari za hapa wapendwa?" nikawasalimu.

"Safi tu," Shadya akasema hivyo.

"Salama," Miryam akaitikia pia.

"Ndo' umerudi?" Shadya akaniuliza.

"Ah, hamna, nilikuwepo tu toka kitambo. Kuna mishe nilikuwa nafanya kidogo... nilienda tu na gym kupasha kidogo, nikarudi tena," nikasema hivyo na kumwangalia Miryam usoni.

Miryam yeye akawa amejikausha kama vile hana muda na mimi na kuinamisha uso wake tu. Sikuiona simu yake hapo alipokuwa, hivyo ni wazi aliiacha ndani.

"Ahaa... ulikuwa umeenda kuongeza misuli kidogo," Shadya akasema hivyo.

"Eeeh..." nikakubali.

"Angalia usije ukakonda mashavu," Shadya akaniambia hivyo.

"Hahah... hamna, sizidishi. Halafu kidogo nisahau... jamani, Shadya shikamoo yako mkubwa," nikamwambia hivyo.

"Marahaba mwanangu. Na hili joto, angalau umekuja tununuliwe na soda," Shadya akasema hivyo.

"Ah, hapo usiwaze. Mnyama nmefika," nikamwambia hivyo.

Miryam akanyanyua uso na kunitazama usoni kwa mkazo.

"Hahaaa... eti mnyama! Tutoe jero jero basi tununue Afiya hapo kwa Fatuma," Shadya akasema hivyo.

"Aaaa... jero! Yaani badala uombe elfu kumi, unaomba jero? Jero na we' wapi na wapi?" nikamwambia hivyo.

"Hahaaa... usinifurahishe mie! Mbona itakuwa poa sana!" Shadya akasema hivyo huku akimtazama Miryam.

Miryam akawa ananiangalia kwa macho yenye kuhukumu, kimasihara yaani.

Shadya akasimama kabisa na kuninyooshea kiganja huku akisema, "Nitoe jembe langu la faida. Nachukua hapo sasa hivi."

"We' mwenyewe ndo' unaenda?" nikamuuliza hivyo.

"Eeh, nafata mwenyewe. Nipe," akasema hivyo.

Nikaingiza mkono mfukoni na kujifanya natafuta hela kwa bidii kweli, huku nikiona jinsi Miryam alivyokuwa akinitazama kwa macho makini, nami nikatoa sarafu mbili za mia tano na kumpa Shadya.

"Ih! Sa' ndo' nini JC?" Shadya akauliza.

"Inabidi tu upokee. Elfu kumi imegoma kutoka," nikamtania namna hiyo.

Akacheka kidogo na kusema, "Kumbe na we' mzushi tu..."

"Ahahahah... siyo sana. Maisha magumu..."

"Magumu wapi, mwone! Kama siyo uchoyo... wakati juzi umempa shangazi malaki kabisa..." Shadya akasema hivyo huku akianza kuvaa ndala.

"Ahahah... basi nisamehe. Ila na yako itakuja tu," nikamwambia hivyo.

"Siyo mbaya mwaya. Mimi, ngoja nifate Afiya tupoze koo..." Shadya akasema hivyo.

Akaelekea nje, nami nikamwangalia Miryam na kukuta anaendelea na kazi yake tu. Nikamfanyia 'pss, psss,' naye akaniangalia na kuninyooshea kidole chake kama kunionya nisimfanyie hivyo, nami nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Mbona unakuna nazi muda umeenda?" nikamuuliza.

Akaacha kuniangalia na kusema, "Niliyemwagiza alete vitu alichelewa."

"Mmmm... na tokea muda ule hauku...."

Kabla sijamaliza kuongea, mlango wa kuingilia ndani hapo ukafunguka, na binti Mariam akawa ametoka. Nikatabasamu kiasi, na moja kwa moja binti akawa amenifata na kunisalimia, kisha kwa lazima nikavutwa ili twende ndani. Sikuwa nataka kumwacha bibie, yaani nilitamani nikae tu hapo niendelee kuongea naye kuhusu chochote, ila sikuwa na jinsi. Yeye mwenyewe alikuwa amekaza tu, ile kuvunga kwamba hatuna uvutano wowote bado ni kitu tulichohitaji kufanya kwa sasa na ndiyo alikuwa makini nacho.

Hivyo nikachoma ndani, nikakutana na mama wakubwa tena tokea ule mchana nilipowaacha, nasi tukakaa kupiga story mbili tatu. Shadya alirejea na kumletea Mariam juice ambayo ilipaswa kuwa ya Miryam, kwa kuwa bibie alimwambia ampe mdogo wake kama mbadala. Miryam akawa anapita na vyombo kuelekea jikoni, akishughulika na mapishi, na Mariam alikuwa akimsaidia. Sikupata nafasi ya kutazamana naye tena, wala kumtumia tu ujumbe kwa sababu simu yake ilikuwa chaji, na ile imefika mida ya saa nne, Ankia akanipigia simu kuniambia kwamba alikuwa amenipakulia; niende. Dah!

Ikanibidi niwaage tu hawa, huku moyoni nikiwa nimeumia kutoweza kutoa wonyesho wowote ule wa uvutano baina yangu na bibie, maana aliigiza vyema kama vile hatuna dili. Mariam alikuwa anataka nibaki mpaka chakula kiive hapa kwao, lakini nikamwelewesha tu kuwa Ankia alikuwa ameshapakua kabisa, kwa hiyo ningeenda kula ili asijisikie vibaya. Mama wakubwa wakanipa sapoti pia, na hatimaye binti akaniachia. Nilipotoka tu, nikamtumia Miryam ujumbe mfupi nikimwambia kuwa asiache kunicheki akitulia, nami ndiyo nikaelekea kwa Ankia.

★★

Msosi wa Ankia ulikuwa mzuri, wali na samaki, nasi tukala pamoja huku story zikiwa juu ya suala la Bobo kutoka na Ankia. Mchecheto wangu bado ulikuwepo, yaani nilikuwa nakula huku naongea na Ankia, lakini akili yangu yote ilikuwa kwenye simu. Nilikuwa nimeiweka pembeni nikisubiri iwake, na kila mara ilipowaka kuingiza ujumbe ningeichukua upesi kuangalia kama ni Miryam, lakini matarajio yangu yakawa yanapigwa chini maana ni watu wengine ndiyo waliokuwa wananicheki. Ilikera!

Ankia akawa ameona hilo, naye akaniambia si nimtumie tu ujumbe Miryam badala ya kusubiri yeye ndiyo anitumie, lakini nikazira, nikiiweka simu pembeni na kusema nisingejisumbua mpaka yeye mwenyewe ndiyo anitafute. Ilikuwa ya shingo upande tu hiyo, naye Ankia akasema haya, ila akagusia namna ambavyo aliona nilikuwa situlii kweli. Tulipomaliza kula, nikatulia tu na kuendelea kusubiri lolote kutoka kwa bibie, nikiwa nimeamua kuwa sitamtafuta kweli mpaka yeye ndiyo ashtuke.

Nikakaa na Ankia hapo sebuleni, tukiwaangalia wakina Efendi na nini kwenye TV, hadi inafika saa tano, bibie akawa kimya tu. Mh? Nikawaza labda alikuwa ananisikilizia ili mimi ndiyo nimcheki kwanza, lakini si nilikuwa nimeshatuma sms kadhaa? Kujibu hata mojawapo tu alishindwa? Nikafikiria kuwa inawezekana Miryam angekuwa na shughuli fulani tu iliyomweka bize, hivyo nikaona nikiondoe hiki kimuwasho cha kutaka tuwasiliane muda wote. Sikupaswa kusahau kuwa huyu alikuwa mwanamke mtu mzima mwenye mambo mengi, hakuwa kama pisi nilizopitia.

Ndani ya muda huo huo, Ankia akasema anaenda hapo Masai, Bobo kamwita. Nikampa ile "mhm" kikejeli, naye akanicheka kwa njia ya kejeli na kwenda chumbani kujiandaa. Haya bwana, mimi ndiyo ningebaki na kaupweke wakati ulipaswa kuwa muda wangu wa kuondoa upweke, angalau hata kwa simu tu. Mwenye nyumba wangu akatoka akiwa amevaa T-shirt la mikono mifupi, jeupe, pamoja na kikaptura-skinny kilichofikia mwanzo wa mapaja yake; juu kidogo ya magoti yaani. Alikuwa amejipiga na makunato mwenyewe, naye akaniaga huku akinitania kwa kusema kama vipi nimwite Miryam aje ili nisibaki kununa tu hapo.

Kejeli zote nikazipokea, sawa bwana, naye akawa ameniacha na kwenda huko ikiwa inaingia saa sita. Kwa watu wa aina yake, palikuwa ndiyo pamekucha. Hapo alikuwa ameitwa na bwana wake, wakanywe na kujifurahisha bila shaka, na kama ni kitu ambacho sikuwa nimesema awali, ni kwamba kwa kipindi hiki Bobo ndiye aliyekuwa ameachiwa usimamizi wa Masai YOTE, yaani awe kama mmiliki, lakini kwa muda tu. Kuna madili na madili inaonekana yalikuwa yamefanywa baada ya Bertha kukamatwa na Chalii kuuawa. Hivyo Ankia alikuwa analishwa bata haswa.

Mzee nikabaki sofani tu huku naitazama TV utadhani nina ugomvi nayo, nikiwa nimeshaghairi kuishika tena simu maana saa sita ilikuwa inatembea tu bila ya Miryam kuwa amenicheki. Nikawaza labda hata angekuwa ameshalala, si unajua labda uchovu na nini, kwa hiyo nikaona ni bora nichukue simu tu ili nimtumie ujumbe wa kumtakia njozi njema. Nikaishika simu, na ile nataka kumtumia ujumbe, ikaanza kuita hapo hapo. Tabasamu hafifu likajengeka usoni kwangu, maana ilikuwa ni bibie mwenyewe ndiye aliyepiga, nami nikapokea na kuweka sikioni.

"Hello..." sauti yake tamu ikasikika.

"Ndiyo ukaona unichunie mpaka sa'hivi, eti?" nikamuuliza hivyo nikijifanya nimeudhika.

"Ooh, I'm sorry... yaani, nilikuwa nimetingwa na kazi, yaani.... ah..." akaongea kama vile amechoka mno.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Usijali, naelewa."

"Yaani nisamehe tu. Kuna jambo nafix hapa, kila mara linakua tu... nikashindwa hata kushika simu..."

"Ishu gani unadili nayo?"

"Ni ishu ya Mamu tu, hamna kwere. Nimemaliza kuandika, nilikuwa naandika barua fulani hapa..." akasema hivyo.

"Okay sawa. Nilidhani labda ungekuwa umeshalala..." nikamwambia.

"Hamna, bado niko macho. Yaani ndiyo nimeziona text zako za muda ule sa'hivi. Pole nimekuonea mno, eti?" akaongea kama ananibembeleza yaani.

"Ah, wala usijali. Me niko poa..." nikajibu kwa unyoofu.

"Mbona nahisi kama umenuna?" akauliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Mh? Ninune nini sasa?" nikauliza hivyo huku nikitabasamu.

"Si nimekufanya umenisubiri mno?"

"Wala hata, akusubiri nani? Ndo' kwanza hapa nasinzia," nikamwambia hivyo kiutani.

Akacheka kidogo, naye akaniambia, "Haya, usiku mwema basi..."

"Ih, we' unaenda wapi? Em' tulia hapa," nikamwambia hivyo.

Akacheka tena, kisha akasema, "Sawa. Niambie."

"Ulikuwa umeshapanda bed?" nikamuuliza hivyo.

"Ndiyo nimetoka kujimwagia, nataka kupanda ndiyo," akasema hivyo.

"Nataka kukuona," nikaongea kwa sauti ya chini.

"Tuongee kwa video call?" akauliza.

"Hamna. Nataka nikuone kabisa," nikasema hivyo.

Akatulia kidogo, kisha akasema, "Kivipi, yaani... hapo nje?"

"Mmm," nikakubali.

"Jayden... sa'hivi usiku..."

"Siyo sana bwana..."

"Mh... ahah... umeshaniona leo, mara nyingi tu. Tutaonana kesho, ama tuongee kidogo kwa video call," akasema hivyo.

"Mm-mm... Nataka kuonana nawe live... kidogo tu. Nimeshaku-miss," nikaongea kwa sauti yenye kubembeleza.

"Lakini... wengine washalala...."

"Please... kidogo tu. Natoka hapo nje, nakuona tu ukutani, then unarudi ndani chap," nikamshawishi zaidi.

Nilikuwa napigia picha sura yake nzuri akijishauri na kujishauri, naye akasema, "Sawa. Natoka upesi."

"Me nishafika," nikamwambia hivyo.

Hapo hapo nikaruka kutoka sofani na kuukimbilia mlango, moja moja mpaka nje na kusogea hadi kwenye ukuta wa uzio. Sasa je! Ankia alidhani ningeboeka eti, si niko hapa sasa? Araa!

Sikuwa nimekata simu, nami nilipokuwa nimesimama, matobo ukutani yaliniruhusu kuuona mlango wa kuingilia ndani kwao bibie, na hapo nikauona ukifunguka na Miryam mwenyewe akisimama sehemu hiyo. Akatabasamu, mimi pia nikampa tabasamu, naye akaiweka simu sikioni na kuongea kwa sauti ya chini sana, akisema amefurahi kuniona tena. Lakini mimi nikamwambia nilitaka aje mpaka hapa, hata nimguse tu, naye akawa anaona kama namsumbua.

Nikaendelea kumbembeleza aje, kwa ile sauti ya Alikiba 'ooooh aje...' naye akayeyusha chuma. Akarudi ndani zaidi na kurejea na funguo, kisha akalifungua geti la mlangoni kwa uangalifu na kutoka, akiwa hajasahau kuvaa ndala zake miguuni. Nikakata simu hatimaye na kuendelea kumwangalia hadi alipokaribia sehemu niliyosimama, na alikuwa amevalia ile nguo yake ya kulalia, huku nywele zake akizivalisha kikofia laini kichwani.

Akasogea hadi hapo ukutani, nyuso zetu zikitenganishwa na hilo uzio, na kwa sauti ya chini akasema, "Ila Jayden! Mbona we' msumbufu sana?"

"Yaani kama vile haunijui! Umeshasahau nilivyokuwa nakusumbua mpaka ukakubali muziki wangu? Na bado..." nikamwambia hivyo kiutani.

Akaniangalia kimkazo eti, halafu akasema, "Umeridhika sasa? Nenda ukalale."

"Tesha amerudi?" nikamuuliza.

"Hamna. Amelala huko kwa rafiki yake," akasema hivyo.

"Haya, njoo..." nikamwambia hivyo.

"Wapi?" akauliza hivyo kimshangao.

Nikamwita kwa kiganja huku nikirudi nyuma zaidi usawa wa huo huo uzio na kusimama, ambao kwa upande wake ungekuwa ni ule usawa wa bomba lao la maji hapo nje. Bado palikuwa na ugiza maana taa haikuwa imebadilishwa.

Miryam akatembea kwa uangalifu ili asitoe sauti kubwa ardhini, na alipokaribia hiyo sehemu, akauliza kwa sauti ya chini, "Unataka kufanya nini wewe?"

Nikampitishia simu yangu hapo hapo kwenye tobo moja ukutani, nikimwambia kwa ishara kuwa aichukue, naye akaipokea huku akiniangalia kwa kutoelewa. Hapo hapo nikaanza kupanda huo ukuta, mpaka juu, nikajitahidi kuwa mwangalifu sana ili nisikanyage vyupa na nondo zenye kuchongoka zilizokuwa kwa hapo juu. Miryam alishangaa! Akafunika mdomo wake kwa viganja huku akiniangalia kama vile haamini, nami nikafanikiwa kuvuka upande wetu na kushuka mpaka sehemu aliyokuwa amesimama yeye. Ukuta wa uzio haukuwa mrefu sana.

Baada ya kufika chini na kumgeukia, nikaona namna ambavyo alikuwa ananiangalia kimaswali sana, nami nikajitabasamisha kimchezo tu na kumtikisia nyusi kiuchokozi.

Akasema, "Jayden una... una matatizo gani?"

Nikaichukua simu yangu na kuiweka mfukoni, halafu nikakishika kiuno chake na kumvuta karibu zaidi na mwili wangu kwa makusudi.

"Wewe!" akasema hivyo kwa kunong'oneza huku akiangalia pembeni kwa njia ya tahadhari.

"Niliposema nataka kukuona, nilimaanisha hivi," nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu.

"Ja.... hii siyo akili. Una... unawaonyesha wezi kwamba hapa ni rahisi kuingia..."

"Wezi gani, Miryam? Mwizi pekee aliyepo hapa ni mimi... na tayari nimeshauiba moyo wako," nikamwambia hivyo kizembe.

Akalibana tabasamu lake la haya, kisha akaangalia pembeni na kusema, "We' ni kichaa."

"Umeona eh? Yaani sina akili ikija juu yako..."

Akapiga ulimi kidogo na kusema, "Niachie bwana... hebu nenda. Saa saba inakaribia, halafu... natakiwa niamke mapema."

"Mbona bado mapema?" nikamuuliza hivyo bila kumwachia kiuno.

"Ahh... sitanii Jayden. Natakiwa nilale usingizi wa kutosha hata masaa machache. Nina safari kesho," akasema hivyo.

Kauli yake ikanifanya nimwachie kiuno taratibu, naye akatulia hapo hapo tu akiniangalia kwa hisia. Aliona imevuta umakini wangu.

Nikamuuliza, "Safari ya wapi tena?"

Akainamisha uso wake kwa ufupi, kisha akanitazama na kuniambia, "Nitaenda Morogoro."

"Moro? Unaenda kufanyaje?"

"Naenda tu kucheki haya masuala ya shamba la Mamu. Watunzaji kule wana... malalamiko fulani... so naenda kuweka mambo sawa,"

"Ahaa, ndo' ulichokuwa unafanyia kazi?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Okay. Lakini... kesho si ni send-off ya Doris? Utaikosa?" nikamuuliza.

"No. Nachukua treni ya mwendokasi..." akajibu hivyo.

"Ooh, kwa hiyo unaenda fasta tu na kugeuka..."

"Eeeh... na natakiwa niondoke mapema kabisa. Nataka nifike huko kwenye saa mbili, nishughulike na hayo mambo, halafu niwahi kurudi. Yaani kama ni kuchelewa, kumi na mbili jioni niwe huku tayari..."

"Okay. Na siku hizi Dar na Moro ishakuwa kama Mbagala na Kariakoo..."

"Ahah... teknolojia. Ila ndo' maana nimekwambia nataka kuwahi kulala, saa kumi na moja niwe nimeshaamka... halafu we' kichwa umenibana tu hapa..." akasema hivyo.

"Ahahah... utanilaumu? I'm so addicted to you..."

"Kwani hiyo ni makosa yangu?"

"Ya nani sasa?"

"Ni yako. Jifunze kujizuia. Siyo lazima mpaka unione kila mara..." akaniambia hivyo kwa uhakika.

Nikamkazia macho kiasi.

"Eeeh... si tungeweza hata kuongea kwa video call? Ya nini hadi unaruka ukuta ili eti uniguse? Yaani wewe!" akaongea hivyo huku akiniangalia kama amekerwa.

"Ah, basi tu, sa' nitafanyaje? Sijisikii fresh kutokukuona live kwa muda mrefu. Unakumbuka kama kuna siku yoyote imepita sijakuona tokea nilipokwambia nakupenda?" nikamuuliza.

"Mhm... hapana..."

"Ndiyo hivyo. Yaani we' ni dawa ya kila kitu kwangu, nikikuona napona..."

"Na kesho je? Tuseme nikaenda, nikachelewa kurudi, halafu nikapitilizia kwenye sherehe na tusionane kabisa mpaka kesho-kutwa... itakuwaje?" akauliza hivyo.

Nikatulia kidogo nikimtazama machoni kwa hisia sana, nami nikamwambia, "Tutaenda wote."

Akakunja uso wake kimaswali na kuuliza, "Wapi? Moro?"

Nikatikisa nyusi kukubali.

"Wewe! Acha masihara yako basi... ahahah..." akashangaa kidogo.

"Sitanii. Nataka niende nawe," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

"Ahah... Jayden, hii ni safari ya kikazi, siendi kuzurura...."

"Hata kama. Nataka tu niwe pamoja nawe," nikamwambia hivyo.

"Kwa hiyo... kweli kabisa unataka tuondoke pamoja?"

"Yeah. Nitakusindikiza, na me nina muda sijaondoka jijini... itakuwa kama tour ndogo. Whatcha say?" nikamuuliza hivyo.

"Eh... mhm... yaani naona unataka kukaba kila kitu sasa..."

"Kabisa. Sitaki yaani... sitaki nihisi uko mbali nami kabisa Miryam. Yaani kila mara nataka tu nikuone, niwe karibu yako, nihisi uwepo wako... inanipa amani sana," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Akaniangalia kwa ufikirio kiasi, kisha akaniambia, "Unavyoongea hivyo... inavutia. Lakini sijui kwa nini, nakuwa nahisi ni maneno rahisi sana kwako kusema kwa sababu labda umeshayatumia kwa wengi..."

Nikatikisa kichwa kiasi kukataa na kumshika mkono, nami nikamwambia, "Najua Miryam, najua ndiyo tumeanza, na ninaelewa kwamba hatujatoka pazuri mno. Sitarajii moyo wako uwe umeshafunguka kwa kila kitu, yaani... najua bado unataka kuwa mwangalifu. Sitakuhakikishia kwamba nakupenda kwa maneno tu, nitakuhakikishia na kwa matendo pia. Ndiyo itakuwa sehemu ya kukufanya uache kuogopa."

"Ahah... okay, ni sawa. Nisamehe tu lakini, maana sometimes nakuwa...."

"Usijali. Nakuelewa," nikamwambia hivyo na kumshika shavuni taratibu.

Akabaki akinitazama usoni kwa macho yenye imani sana.

Nikamwambia, "Najua sitaenda na wewe kila sehemu utakayoenda, lakini popote ambapo naweza kuwepo kwa ajili yako... nitakuwa hapo Miryam. Ndiyo nachotaka kufanya hasa kwa wakati huu. Natamani kama... ningeweza ku-rewind muda yaani... ningeurudisha muda nyuma na kukupata kipindi hichoo..."

"Ahah... si ungekuwa mdogo wangu sana?" akauliza hivyo kwa hisia.

"Yeah, lakini haingejalisha. Ningekupata tu na kukupenda, na ningekuonyesha huo upendo kwa muda mrefu zaidi mpaka kufikia huu wakati ambao tumesimama hapa... na kuendelea," nikamwambia hivyo kwa sauti yenye kubembeleza.

Akakishika kiganja changu huku akiniangalia machoni kwa hisia sana.

"Sikudhani ingewezekana tena Jayden kuja kupenda kutoka moyoni. Yaani sikufikiria ningekuja kupenda tena namna hii, na sikujua kama ningekuja kupenda kila kitu kuhusu mtu hadi nilipokutana na wewe Miryam. Yaani ninakupenda zaidi ya ninavyokupenda sana," nikamsemesha kwa hisia.

Akatabasamu zaidi huku akisugua kiganja changu taratibu kwa vidole vyake laini, naye akauliza, "Huwa unayatoa wapi hayo maneno Jayden?"

Nikatabasamu tu na kumwambia, "Nayasomaga tu kwenye mitandao, ndo' nakuja kuyamwaga hapa..."

"Oooh... kwa hiyo kumbe nafikishiwa tu mawazo ya mtu mwingine hapa, eh?" akauliza hivyo kiutani.

"Oops! Nimekamatika..." nikaongea kikejeli.

"You fool!" akaniambia huku akitabasamu.

Sote tukacheka kidogo kwa pumzi.

Akatikisa kichwa kuonyesha uthamini, naye akasema, "Asante sana kwa kunipenda. Ninakupenda sana pia."

"Yaani tulivyo... kama Romeo na Juliet," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu zaidi kwa furaha.

Nikauachia uso wake na kuuliza, "So... kesho nitakusindikiza Moro, eh?"

"Sawa. Tutaenda pamoja. Aa... nafikri hapo stendi zinakuwepo gari zinazoenda Stesheni... sijajua sana, ila tuta...."

"Tutapanga tu pa kukutana, afu' tutaenda pamoja, tutajua," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kukubaliana na hilo.

Nikavishika viganja vyake vyote kwa chini na kusema, "Okay. Basi ngoja nikuache ukalale sasa. Me huwa nina usingizi mzito kwa hiyo nitaweka alarm."

"Kumi na moja, sharp," akaniambia hivyo.

"Mm-hmm," nikakubali.

"Haya, usiku mwema, nenda sasa. Uruke ukuta kwa uangalifu... na iwe mwanzo na mwisho," akasema hivyo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Go!" akaniambia hivyo kwa msisitizo.

Nikaangalia juu, kisha nikaanza kuimba kwa sauti ya chini, "Basi nichumu, ni-kiss mwah.. ai nichumu, ni-kiss mwah..."

Nikamwangalia tena na kukuta anatabasamu kwa ile njia ya kuhukumu, akinishusha na kunipandisha eti, nami nikatabasamu kwa furaha.

Akanicheka kidogo kwa pumzi, kisha akasema, "Una hakika ulikuwa umeshasugua kinywa?"

Nikakunja uso kimaswali.

"Kama huoshagi mdomo kabla ya kulala, hiyo chum ndo' huipati," akasema hivyo kiutani.

"Ih! Kumbe umeshatoa na kitabu cha masharti afu' bado hujaniuzia?" nikamuuliza hivyo kiutani pia.

Akacheka kidogo huku ameziba mdomo.

"Na sasa hivi ndiyo unaniambia sharti la kwanza wakati hata nilikuwa sijaliandaa hili domo? Basi usiku mwema..." nikamwambia hivyo nikijifanya nimeudhika.

Bado alikuwa anacheka, nami nikaigiza kutaka kupanda ukuta, lakini akaishika T-shirt yangu na kuivuta huku akisema, "Hebu njoo hapa..."

Nikageuka na moja kwa moja kukutana na mdomo wake ulionifuata bila kusita. Ah!

Miryam alipatia aisee. Alijua. Zamu hii hakunipiga busu, alinila denda! Denda ya maana! Aliufinya mdomo wangu kwa midomo yake taratibu sana, akiepuka kutumia ulimi mwanzoni na kuacha midomo yetu pekee ndiyo ivutane, kisha ndiyo akaingiza ulimi wake ndani yangu na kutoa penzi la mdomo kwa ufundi ambao sikuwa nimeutegemea kabisa! Alikuwa na midomo mitamu, akipenda nimwachie tu yeye ndiyo aonje kila alichotaka kula, na katika hali ya kunogewa zaidi, akakishika kichwa changu kwa mikono yake yote na kuanza kukipapasa taratibu kama vile hataki tuache. Sijui hata aliweka wapi simu yake. Nilisisimka nyie!

Nikakishika kiuno chake kwa njia ya kukumbatia, kwa nguvu, bibie akiwa amenogewa tu kunipa denda hii tamu sana, miguno laini ya pumzi ikimtoka kadiri alivyoendelea kunipatia utamu wa ulimi wake, na nilikuwa nimeshasimama dede kwa nguvu kubwa sana. Yaani hapo nikasahau yote, nikiwa tayari kwa lolote lile ambalo angefanya lifuate, maana hisia zilikuwa huko juu juu yaani. Ndoto ilikuwa inatimia hapa!

Ilionekana ni kama dakika nzima ilipita akiwa ananipandishia moto kwa denda hii, ndipo akaikatisha taratibu na kuweka paji lake la uso usawa wa shavu langu. Nikafumbua macho na kuona yeye akiwa amefumba ya kwake bado, akiwa anazungusha kichwa chake taratibu na nyuso zetu zikiwa kwa ukaribu mno, nami nikatabasamu na kubana ubavu wake kwa kiganja changu, katika njia ya kumtekenya, naye akapandisha nyonga kidogo na kufumbua macho yake kuniangalia.

Aliniangalia kwa njia yenye hamu, kisha akaweka kiganja chake kifuani kwangu na kusema, "I really like this, Jayden. But I don't want us to go too fast..."

Aliongea kwa sauti tamu mno yenye kunong'oneza kiasi, yaani hata kama hakuwa akitaka tupeleke mambo mengi haraka sana, hapa tu tayari alikuwa ameshanipeleka mawinguni huko.

Nikiwa namwelewa, nikamwambia, "Usijali. I got you."

Akarudisha uso wake nyuma na kunitazama kwa hisia, naye akasema, "Tutaonana baadaye."

Nikatikisa kichwa kukubali hilo, ndiyo nikakiachia kiuno chake na kuusogelea ukuta. Nikapanda taratibu na kwa uangalifu sana, yeye bado akiwa amesimama hapo hapo, nami nikashukia upande wa kwa Ankia na kumtazama tena. Akanipungia mkono wa kwa heri ya sasa, nami nikaunda kopa kwa viganja vyangu na kumwonyeshea kwa kuiweka usawa wa moyo. Akatabasamu kwa hisia sana, kisha huyoo akaelekea ndani kwake.

Nikageuka tu na kuelekea ndani kwetu pia, nami nikafunga mlango na kutulia hapo sebuleni kwanza. Nikajikuta najishika mdomo wangu, nikitabasamu kama zezeta yaani kwa kukumbukia hiyo "chumu" niliyopewa hapo nje, na bado hapa chini palikuwa pamevimba eti! Nilikuwa na hisia nzuri sana, sana, sana, kwa wakati huu, na najua zingeendelea kupanda juu zaidi kadiri ambavyo siku zingeendelea.

Na huyu mwanamke alionekana kuyajua mapenzi kwelikweli, siyo mchezo, yaani nilikuwa nina hamu ya kuyatalii naye mengi sana kutokea hapa. Kwa kuwa siku ya kesho ningekwenda naye Morogoro, ningetakiwa kujiweka katika uimara wa kiume ndani ya akili, ili kama utalii wa kwanza ungefanywa hiyo hiyo kesho, uwe wa maana. Ona, nilikuwa hadi nimeanza kuwaza upuuzi mapema namna hii!

Lakini najua hilo lingekuwa jambo hakika kufanyika baina yangu mimi na yeye, haijalishi lini, kwa hiyo kweli utayari ulihitajika maana nilikuwa nimeshamhamu kwa muda mrefu sana sasa huyu mwanamke. Nikaona nizime taa na kwenda kulala, yaani nikajitupia kitandani huku natabasamu tu na kufurukuta-furukuta huku na huko kwa kuhisi mihemko ya hatari, nikiingoja alfajiri ifike ili niondoke na mwanamke wangu.







★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
Duuu kutiana genye tu kundomba aaah
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI

★★★★★★★★★★★★★★★★


Niliendelea kumkumbatia Miryam kwa sekunde chache nikiwa nahisi furaha sana, kisha nikamwachia na kumtazama usoni kwa hisia sana. Yeye pia alikuwa akiniangalia kwa macho yenye hisia kwelikweli, nami nikatikisa kichwa kidogo nikiwa yaani bado siamini-amini.

"Aisee! Yaani sijui hata niseme nini..." nikaongea hivyo kwa hisia.

Akatabasamu tu na kuendelea kuniangalia kwa upendo.

Nikasema, "Wee... ume... umefikaje hapa haraka hivi? Yaani... usiniambie umekimbia kutokea Kijichi..."

Akacheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Kwani hujui kwamba nina gari?"

"Ahahah... this is amazing..." nikamwambia hivyo kwa sauti yenye hisia sana.

Akabaki akinitazama usoni kwa macho yenye upendo mwingi, nami nikalishika shavu lake kidogo huku nikimwangalia kama vile nataka kumtafuna, siyo kwa ubaya, ila kwa hamu nzuri na kubwa sana niliyokuwa nayo kumwelekea. Ndipo sauti ya koo kusafishwa ikatokea pale sebuleni, nami nikaangalia hapo na kuona Ankia alikuwepo bado. Miryam akageukia huko pia.

Nikasema kwa kujishaua, "Ankia? Kumbe bado upo?"

"Ulifikiri me jini nimepotea, au?" Ankia akaniuliza hivyo.

Miryam akatabasamu kiasi.

"Kwanza unatakiwa uwe umeshapotea, unafanya nini hapa? Hebu... go away..." nikamwambia hivyo Ankia kiutani.

"Mm? Yaani ndiyo umeshaanza na kuringa..." Ankia akaniambia hivyo kwa njia ya nyodo.

"Siyo kuringa, we' si ulikuwa unaenda dukani? Nenda..." nikamwambia hivyo.

Ankia akaniangalia kwa njia yenye nyodo na kuikunja midomo yake, na Miryam akacheka kidogo tu na kujishika shingoni.

Nikamfanyia Ankia ishara ya kumfukuza kwa kiganja na kumwambia, "Shoo!"

Ankia akacheka kwa mguno, naye akamwambia Miryam, "Baadaye mpenzi."

Miryam akatikisa kichwa kukubali heri hiyo, naye Ankia akawa ameondoka hatimaye. Raa!

Miryam akanigeukia na kunitazama usoni tena, nami nikamwangalia na kujichekesha kidogo kwa haya eti. Nikawa nahisi hali ya utete kidogo, nikiangalia pembeni huku napiga-piga kiganja changu kimoja mguuni, kisha namwangalia tena na kukuta amenikazia jicho tu, halafu sote tukajikuta tunacheka kidogo kwa kupatwa na hisia nzuri sana.

Ndipo nikamwambia, "Karibu. Njoo ukae... aa... namaanisha... siyo humu chumba... yaani... kama... utapenda tukae humu... chumbani.... au, pale... sofani... simaanishi ukiingia chumbani nita... siyo kwamba nafikiria hivyo... ila we' ndo' unaweza ukawa unafikiria... siyo kwamba... namaanisha... sikuoni unawaza... dah, naharibu aisee..."

Miryam akacheka kidogo na kutikisa kichwa chake, naye akasema, "Wasiwasi wa nini sasa tena?"

Nikafumba jicho moja na kumwangalia kwa kujihami eti.

"Ahah... me ndiyo ningetakiwa niwe na wasiwasi, maana...."

Kabla hajamaliza kuongea, nikamkumbatia kwa mara nyingine tena ili kumpa kitulizo, ambacho na mimi kwa upande wangu nilikihitaji sana. Nilihisi amani kubwa sana moyoni, na nilihitaji aihisi pia. Nikawa nimemshikilia huku nikiyumbisha miili yetu taratibu kama vile nambembeleza yaani, naye alikuwa ameiweka mikono yake mgongoni kwangu na kuitembeza taratibu huku amenilalia begani kwa raha zote. Yaani!

Nikiwa bado nimemkumbatia, nikasema kwa sauti ya chini, "Vipi tukikaa?"

Akajibu kwa sauti yake tamu, "Wazo zuri."

Nikamwachia taratibu kabisa, halafu tukatazamana machoni kwa hisia sana, kisha nikakishika kiganja chake na kwenda naye mpaka pale sebuleni na kuketi sofani. Akakaa pembeni yangu pia, huku nikiwa nimekishika kiganja chake bado, naye akakiweka kingine juu ya mkono wangu, na chenyewe nikakishika.

"Umeni-surprise sana Miryam..." nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Najua. Samahani kwa hilo."

"Samahani ya nini sasa? Haujui kwamba umenipa furaha sana?"

"Wakati tayari nilikuwa nimeshakuvunja moyo?" akasema hivyo huku akiniangalia usoni kwa umakini.

Nikatulia tu na kuendelea kumwangalia.

Akasema, "Jayden... I'm sorry. Nimekutesa sana... I know..."

"Usijali. Nilikuwa nakuelewa."

"Still, yaani... nimekufanyia vibaya mno. Pamoja na yote, umefanya vingi sana kwa ajili yangu kunithibitishia unanipenda, lakini nikawa nakupiga mateke tu. Najua nilikuwa nakuonea sana, na naomba tu unisamehe kwa leo... yaani bado nilikuwa nimechanganyikiwa..."

"Ulichanganywa na nini?"

"Kila kitu. Nilikuwa najiuliza... kwa nini niko hivi. Nimekupenda pia, lakini bado tu nikawa najipofusha kwa kiburi changu...."

"Miryam..."

"... ambacho kinanifanya nijione kuwa sahihi kwa kila kitu. Umenifundisha sana, umeshanionyesha kwamba kuwa hivyo haifai, lakini bado nikawa sielewi. Ni kweli," akasema hivyo kwa hisia.

Nikaanza kusugua kiganja chake taratibu.

"Leo... nimeshindwa Jayden. Nimeshindwa kuendelea kujifanya mgumu tena. Nakupenda. Na ninakuhitaji. Sijui kingine tena," akasema hivyo.

Nikatabasamu kiasi kwa hisia.

"Lakini... bado naogopa. Na baada ya ulichoniambia leo, nimetambua kuwa nakuhitaji zaidi sasa ili niache kuogopa tena. Umesema unaniona me kuwa kama msaada kwako..."

"Yeah, kabisa."

"Well, na mimi nakuona kuwa msaada wa moyo wangu. Nimetambua pia kwamba wewe ndiyo kipande cha pili cha moyo wangu kinachokosekana ili kuufanya uwe kamili, na ninakuhitaji uwe karibu nami ili uunganike pia na kuwa kitu kimoja," akaongea kwa hisia sana.

Dah! Alikuwa na maneno matamu!

"Kwa hiyo wakati huu mimi ndiyo nimekuja kukuomba nafasi Jayden. Uko tayari kunibeba?" akaniuliza hivyo.

Nikamkazia macho kiasi, nami nikamuuliza, "Hilo ni swali au jibu?"

Akatabasamu na kuangalia chini.

Nikamshika shavuni taratibu, naye akaniangalia. "Kwa asilimia zote, Miryam. Niko tayari. Unalijua hilo."

Akasema, "Mambo yatakuwa mengi, na magumu sa...."

"Usijali Miryam. Niko nawe. We are two parts of the same whole now, and I intend to keep it together no matter what..." nikatia na kimombo kidogo kumfariji.

Akakishika kiganja changu usoni kwake, naye akasema, "Asante."

Nikampa tabasamu hafifu kwa hisia.

Akashusha pumzi na kuangalia chini kwa utafakari, naye akasema, "Nina hamu kubwa... na matarajio mengi kuona ni wapi hii itanifikisha."

Nikamwachia taratibu usoni na kusema, "Hata mimi. Na ninaiona kuwa sehemu nzuri sana, sema ndiyo nataka niifikie nikiwa pamoja nawe."

Akatabasamu na kuendelea kuniangalia kwa hisia sana machoni.

Nikajikuta nimetulia zaidi, nikimtazama kwa njia hiyo hiyo yenye hisia kama yeye tu, na mapigo yangu ya moyo yalikuwa yakienda mbio kwa sababu ya hisia zangu kunitaka nifanye jambo fulani. Niliiangalia midomo yake na kuona jinsi ambavyo iliachia uwazi kidogo uliofanya mpaka nikahisi kusisimka yaani, na nilipomtazama machoni, akawa bado ameniangalia tu kwa njia yenye subira.

Nikataka kupiga hatua kumwelekea kwa kuusogeza uso wangu karibu zaidi na wake, lakini akaacha kuniangalia na kusema, "Inabidi niingie nyumbani Jayden."

Nikainamisha uso wangu kiasi na kubana midomo, kisha nikatikisa kichwa kukubali hilo. Nilipomtazama usoni, nikakuta ananiangalia huku akitabasamu kiasi, nami nikajirudisha nyuma na kuangalia pembeni kwa njia ya kujishaua. Alikuwa amenisoma huyo!

Nikasema, "Sawa... najua umechoka. Nenda tu... ukapumzike."

Akatikisa kichwa kukubaliana na hilo, halafu akasema, "Na wewe ndiyo ulikuwa unaingia kupumzika bila shaka..."

"Eeh... nilikuwa nahisi uchovu... sijui hata wa nini, ila... sa'hivi umeisha. Nimepata nguvu mpya," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu na kusema, "Vizuri."

Kulikuwa na kale kahali kenye kusisimua fulani hivi, yaani, mpaka raha. Nilimtazama kwa upendo mwingi sana, naye akawa ananiangalia tu kama vile anasubiri nimuage vizuri.

Ndiyo akaniambia, "Narudi hapo Masai kwanza."

"Masai? Kwa nini? Yaani... hauendi nyumbani? Si umesema...."

"Nililiacha gari pale, ndiyo nikaja hapa," akanikatisha kwa kusema hivyo.

"Oooh, sawa. Ngoja. Kwa nini uliliacha gari Masai?" nikamuuliza.

"Nilipokuwa nakuja... sikutaka kuja mpaka huku na gari, hapo nyumbani wangeona maana... nilikuwa nataka kwanza..." akaishia hapo.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Uje kwangu."

Akatabasamu pia na kutikisa kichwa kukubali.

Nikamwambia, "Okay, nimeelewa. Umetumia akili, maana wambea wengi."

"Hapa penyewe nikitoka wakaniona, inaweza kuzua utata..."

"Oh no, haina shida. Sidhani kama ina shida. Hata hivyo we' siyo mgeni hapa, hao wakina Fatuma watajua umekuja tu kumsalimia Ankia labda..."

"Labda..." akasema hivyo na kuangalia pembeni.

"Ahah... naitamani ifike siku ambayo tutatembea pamoja... proud... kila mtu ajue kwamba wewe ni wangu," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu na kusema, "I hope for that day to come too. Ila kwa sasa... tuweke mambo yetu chini kwanza..."

"Yeah, yeah, najua. Chochote kile unachotaka tufanye, nitafata..." nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa.

Nikiwa namwangalia kwa hisia, nikamwambia, "Asante Miryam. Kwa kunipa hii nafasi. Nitajitahidi kuwa mume mzuri kwako."

Akatabasamu zaidi na kuuliza, "Mume eeh?"

"Ahahah... kidume wako," nikamwambia hivyo na kupandisha nyusi kichokozi.

"Ahah... sawa. Mimi pia. Nitajitahidi kukupa furaha Jayden," akaongea kwa sauti yake tamu sana.

Nilimwangalia huyu mwanamke kwa mapenzi ya dhati yote niliyohisi moyoni, yaani nilipenda sana hii hali aliyokuwa ananifanya niihisi wakati huu. Akiwa ananitazama kwa hisia pia, akanishika shavuni kwa kiganja chake laini, halafu akausogelea uso wangu karibu zaidi na kunipa busu moja, moja tu, ambayo ilinipa msisimko wa hali ya juu zaidi ya msisimko wa busu mia moja ambazo mwanamke mwingine yeyote angenipa!

Midomo yake laini iliikandamiza ya kwangu na kuvutana nayo mara moja tu na taratibu kabisa, naye akaiachia ikiwa imetoa sauti tamu kama vile ametoka kufyonza pipi tamu sana, kisha akajirudisha nyuma tena na kuniangalia kwa hisia. Sasa hapo mimi! Huo msisimko ulikuwa umeniamshia bonge moja la balaa, damu ilianza kunyanyua mdude fulani kwa nguvu isiyopimika, yaani nilihisi mwili wote unaitikia kitendo chake kidogo tu kwa hamu nzito sana. Nikabaki nikimtazama machoni kwa utulivu, huku hisia zangu zikiwa zinafurukuta huku na huko ndani yangu.

Akiwa anasugua shavu langu kwa kidole chake taratibu, akasema, "Nakupenda."

Yaani aliisema hiyo 'nakupenda' katika ile njia ya kiutu-uzima, uhakika yaani, hakuona aibu wala kuhofia kuniambia hivyo. Alijivunia kabisa.

Nikatabasamu tu na kumwambia, "Nakupenda pia."

Nilikuwa nimeweka mkono wangu usawa wa sehemu ya kati kwenye suruali ili kuficha saibu lililokuwa limenyanyuka baada ya yeye kunipiga busu kwa mara ya kwanza kabisa, na mwanamke wangu akanyanyuka kutoka hapo sofani na kuanza kuelekea mlangoni. Ikanibidi niendelee kutulia tu hapo hapo sofani maana sikutaka aone hili dubwana mapema namna hii, bado hayo mazoea sikuwa nimemwanzishia kwa hiyo kujibana ilikuwa lazima. Akafungua mlango na kuniangalia kwa ufupi, nasi tukapeana tabasamu la furaha kwa pamoja, kisha ndiyo akatoka hatimaye. We!

Yaani ile ametoka tu, nikanyanyuka na kuanza kurukaruka hapo ndani, nikapanda na kwenye sofa na kuanza kuruka kwa furaha tele. Nilihisi furaha isiyo na kifani. Nilikuwa kama nimechanganyikiwa. Nikafata na simu yangu chumbani na kuweka muziki wa Jux na Dayamondi "bora kuenjoiiiiii... maisha mafupi ni simpoo," nami naikaanzisha miuno na dansi za kipuuzi ili tu niitoe furaha yangu. Nilicheza wimbo mpaka mwisho, nami nikajitupia sofani na kubaki najichekea mwenyewe tu kwa kuhisi raha kuu mno moyoni mwangu.

Hatimaye Miryam akawa wangu. Dah! Ingebidi kutokea hapa sasa nimwonyeshe namna gani ambavyo alikuwa akiukosa uhondo wa mapenzi kwa huo muda wote alioukosa. Yaani ningemfurahisha, angenipenda mpaka milele. Sikufikiria kuhusu changamoto, sijui matatizo na vikwazo, yaani nilichowazia juu yake ilikuwa ni furaha tu. Ya nini niteseke roho wakati Miryam alikuwa wangu? Hiyo kitu haingekuwa na nafasi tena!

Na ningehakikisha nampa furaha aliyoistahili kwelikweli, ili nami nitulie kwa furaha na amani tele moyoni mwangu. Siku ile nimemwambia ukweli kuhusu hisia zangu nilijipiga mara mbili kifuani ili kujipa moyo katika mbio za kuhakikisha namkamata, na sasa akawa amekamatika, hivyo ningetakiwa kujipiga mara nyingi zaidi kifuani wakati huu kwa kiburi changu chote kuwa ndiyo, nilimpata! Piga kifua kwa masifa kama King Kong yaani! Araa? Hatimaye Miryam alikuwa bibie wangu!

★★

Haukupita muda mrefu sana na Ankia akawa amerejea tena kutoka kazini kwake, ikiwa imeshaingia saa moja, na alinikuta ndani nikiwa najiandaa kutoka. Nilitaka kwenda gym kwanza kuchangamsha mwili kabla ya kuja kwenda kwa Miryam kuwasalimia wapendwa wangu, na muda ule ambao Miryam aliniacha hapa, tuliwasiliana kupitia sms, nikimuuliza ikiwa alifika kwake bila vilongolongo vingi, naye akawa amekubali. Kwa wakati huu akawa akishughulika na mambo fulani ya hapo kwao.

Ankia alikuwa na hamu ya kutaka kusikia mengi yaliyojiri baada ya kuniacha hapa na Miryam muda ule, nami nilikuwa na furaha sana bado lakini kwa wakati huu nilitulia zaidi. Nikamwambia ningekuja kumpa ukweli wote nikitoka gym, ila kiufupi tu ni kwamba ilikuwa siku iliyogeuka kuwa yenye amani kubwa sana kwangu. Sikutarajia yaani. Kwa hiyo ningetakiwa kwenda kuchangamsha mwili kwanza kisha ndiyo nije kumpa ubuyu aliotaka, na yeye nikamwambia atanipa ubuyu niliotaka kama malipo. Hakuelewa namaanisha nini, ila nilikuwa namwongelea Bobo, hivyo ingekuja kuelezeka baadaye.

Nikatoka hapo na kwenda hadi gym ya pale Mzinga, na tayari nilikuwa nimeshaanza kujuana na baadhi ya mangangali waliokuja hapo lakini sikupitilizisha sana mazoea, nami nikanyanyua na kushusha chuma kwa muda wa kama saa moja na nusu, kisha ndiyo nikarudi tena kwa Ankia. Sasa nilikuwa nimechangamka kwelikweli yaani, nikaoga na kuvaa vizuri, kisha ndiyo nikakaa pamoja na mwanamke huyo sebuleni kupiga story kidogo.

Ikiwa imeshaingia saa tatu, Ankia ndiyo alikuwa anaelekea kuivisha wali huko, nami nilikuwa nimemsimulia namna ambavyo Miryam alinifunulia hisia zake na kukubali tuanze mahusiano rasmi kabisa. Akanipongeza nakwambia, yaani utafikiri hatukuwahi kufanya mineng'emuo kabisa, na ndiyo nikawa nimemuuliza kuhusu Bobo sasa. Ankia alikuwa anajifanya kama vile hajui naongelea nini, lakini mwishowe akakiri kuwa ni kweli alianza kutoka kimahusiano pamoja na yule kaka, ingawa aliyapeleka taratibu ili kuhakikisha haumizwi. Na yeye nikampongeza pia.

Muda huu wote tangia nirudi kutoka gym, nilikuwa nasubiri tu Miryam anitumie ujumbe au nini, lakini hakufanya hivyo. Nikawa nimejaribu kumtumia ujumbe wa salamu, lakini hakujibu, hivyo nadhani alikuwa na shughuli bado. Nilikuwa nimemcheki na Tesha pia, ambaye bado hakuwa amerudi hapo kwao, hivyo nikaona nimuage tu Ankia kwa ufupi ili nikawasalimie wakina Bi Zawadi, kisha ningerudi kula. Kilikuwa kisingizio tu maana niliwashwa kweli kutaka kumwona bibie, kwa hiyo nikavaa malapa na moja kwa moja kwenda hapo kwake.

Nilipoingia tu getini, gari lake Miryam lilikuwa hapo nje, na pale varandani alikuwepo Shadya pamoja na bibie mwenyewe. Miryam aliketi mkekani huku akiwa anakwangua nazi kwenye mbuzi, na Shadya aliketi pembeni yake tu akiwa kama anampa umbeya mpwa wake. Miryam alivalia lile dera lake la kijani huku nywele zake zikiwa zimefunikwa kwa kilemba, na baada tu ya kuniona, akaacha kukwangua nazi na kuachia tabasamu hafifu kunielekea.

Nikaanza kuelekea hapo huku nikijitahidi kubana la kwangu, na Shadya akaita jina langu kama njia fulani ya kuniambia 'karibu.' Hii bado ilikuwa saa tatu, na ilinishangaza kidogo kukuta Miryam anakwangua nazi wakati huu. Alifika mapema nafikiri ile saa kumi na mbili, kwa hiyo sikujua kwa nini upishi ulikuwa umechelewa namna hiyo. Miryam akaendelea kukuna nazi, nami nikasogea mpaka hapo varandani nikiwa natabasamu kumwelekea Shadya.

"Habari za hapa wapendwa?" nikawasalimu.

"Safi tu," Shadya akasema hivyo.

"Salama," Miryam akaitikia pia.

"Ndo' umerudi?" Shadya akaniuliza.

"Ah, hamna, nilikuwepo tu toka kitambo. Kuna mishe nilikuwa nafanya kidogo... nilienda tu na gym kupasha kidogo, nikarudi tena," nikasema hivyo na kumwangalia Miryam usoni.

Miryam yeye akawa amejikausha kama vile hana muda na mimi na kuinamisha uso wake tu. Sikuiona simu yake hapo alipokuwa, hivyo ni wazi aliiacha ndani.

"Ahaa... ulikuwa umeenda kuongeza misuli kidogo," Shadya akasema hivyo.

"Eeeh..." nikakubali.

"Angalia usije ukakonda mashavu," Shadya akaniambia hivyo.

"Hahah... hamna, sizidishi. Halafu kidogo nisahau... jamani, Shadya shikamoo yako mkubwa," nikamwambia hivyo.

"Marahaba mwanangu. Na hili joto, angalau umekuja tununuliwe na soda," Shadya akasema hivyo.

"Ah, hapo usiwaze. Mnyama nmefika," nikamwambia hivyo.

Miryam akanyanyua uso na kunitazama usoni kwa mkazo.

"Hahaaa... eti mnyama! Tutoe jero jero basi tununue Afiya hapo kwa Fatuma," Shadya akasema hivyo.

"Aaaa... jero! Yaani badala uombe elfu kumi, unaomba jero? Jero na we' wapi na wapi?" nikamwambia hivyo.

"Hahaaa... usinifurahishe mie! Mbona itakuwa poa sana!" Shadya akasema hivyo huku akimtazama Miryam.

Miryam akawa ananiangalia kwa macho yenye kuhukumu, kimasihara yaani.

Shadya akasimama kabisa na kuninyooshea kiganja huku akisema, "Nitoe jembe langu la faida. Nachukua hapo sasa hivi."

"We' mwenyewe ndo' unaenda?" nikamuuliza hivyo.

"Eeh, nafata mwenyewe. Nipe," akasema hivyo.

Nikaingiza mkono mfukoni na kujifanya natafuta hela kwa bidii kweli, huku nikiona jinsi Miryam alivyokuwa akinitazama kwa macho makini, nami nikatoa sarafu mbili za mia tano na kumpa Shadya.

"Ih! Sa' ndo' nini JC?" Shadya akauliza.

"Inabidi tu upokee. Elfu kumi imegoma kutoka," nikamtania namna hiyo.

Akacheka kidogo na kusema, "Kumbe na we' mzushi tu..."

"Ahahahah... siyo sana. Maisha magumu..."

"Magumu wapi, mwone! Kama siyo uchoyo... wakati juzi umempa shangazi malaki kabisa..." Shadya akasema hivyo huku akianza kuvaa ndala.

"Ahahah... basi nisamehe. Ila na yako itakuja tu," nikamwambia hivyo.

"Siyo mbaya mwaya. Mimi, ngoja nifate Afiya tupoze koo..." Shadya akasema hivyo.

Akaelekea nje, nami nikamwangalia Miryam na kukuta anaendelea na kazi yake tu. Nikamfanyia 'pss, psss,' naye akaniangalia na kuninyooshea kidole chake kama kunionya nisimfanyie hivyo, nami nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Mbona unakuna nazi muda umeenda?" nikamuuliza.

Akaacha kuniangalia na kusema, "Niliyemwagiza alete vitu alichelewa."

"Mmmm... na tokea muda ule hauku...."

Kabla sijamaliza kuongea, mlango wa kuingilia ndani hapo ukafunguka, na binti Mariam akawa ametoka. Nikatabasamu kiasi, na moja kwa moja binti akawa amenifata na kunisalimia, kisha kwa lazima nikavutwa ili twende ndani. Sikuwa nataka kumwacha bibie, yaani nilitamani nikae tu hapo niendelee kuongea naye kuhusu chochote, ila sikuwa na jinsi. Yeye mwenyewe alikuwa amekaza tu, ile kuvunga kwamba hatuna uvutano wowote bado ni kitu tulichohitaji kufanya kwa sasa na ndiyo alikuwa makini nacho.

Hivyo nikachoma ndani, nikakutana na mama wakubwa tena tokea ule mchana nilipowaacha, nasi tukakaa kupiga story mbili tatu. Shadya alirejea na kumletea Mariam juice ambayo ilipaswa kuwa ya Miryam, kwa kuwa bibie alimwambia ampe mdogo wake kama mbadala. Miryam akawa anapita na vyombo kuelekea jikoni, akishughulika na mapishi, na Mariam alikuwa akimsaidia. Sikupata nafasi ya kutazamana naye tena, wala kumtumia tu ujumbe kwa sababu simu yake ilikuwa chaji, na ile imefika mida ya saa nne, Ankia akanipigia simu kuniambia kwamba alikuwa amenipakulia; niende. Dah!

Ikanibidi niwaage tu hawa, huku moyoni nikiwa nimeumia kutoweza kutoa wonyesho wowote ule wa uvutano baina yangu na bibie, maana aliigiza vyema kama vile hatuna dili. Mariam alikuwa anataka nibaki mpaka chakula kiive hapa kwao, lakini nikamwelewesha tu kuwa Ankia alikuwa ameshapakua kabisa, kwa hiyo ningeenda kula ili asijisikie vibaya. Mama wakubwa wakanipa sapoti pia, na hatimaye binti akaniachia. Nilipotoka tu, nikamtumia Miryam ujumbe mfupi nikimwambia kuwa asiache kunicheki akitulia, nami ndiyo nikaelekea kwa Ankia.

★★

Msosi wa Ankia ulikuwa mzuri, wali na samaki, nasi tukala pamoja huku story zikiwa juu ya suala la Bobo kutoka na Ankia. Mchecheto wangu bado ulikuwepo, yaani nilikuwa nakula huku naongea na Ankia, lakini akili yangu yote ilikuwa kwenye simu. Nilikuwa nimeiweka pembeni nikisubiri iwake, na kila mara ilipowaka kuingiza ujumbe ningeichukua upesi kuangalia kama ni Miryam, lakini matarajio yangu yakawa yanapigwa chini maana ni watu wengine ndiyo waliokuwa wananicheki. Ilikera!

Ankia akawa ameona hilo, naye akaniambia si nimtumie tu ujumbe Miryam badala ya kusubiri yeye ndiyo anitumie, lakini nikazira, nikiiweka simu pembeni na kusema nisingejisumbua mpaka yeye mwenyewe ndiyo anitafute. Ilikuwa ya shingo upande tu hiyo, naye Ankia akasema haya, ila akagusia namna ambavyo aliona nilikuwa situlii kweli. Tulipomaliza kula, nikatulia tu na kuendelea kusubiri lolote kutoka kwa bibie, nikiwa nimeamua kuwa sitamtafuta kweli mpaka yeye ndiyo ashtuke.

Nikakaa na Ankia hapo sebuleni, tukiwaangalia wakina Efendi na nini kwenye TV, hadi inafika saa tano, bibie akawa kimya tu. Mh? Nikawaza labda alikuwa ananisikilizia ili mimi ndiyo nimcheki kwanza, lakini si nilikuwa nimeshatuma sms kadhaa? Kujibu hata mojawapo tu alishindwa? Nikafikiria kuwa inawezekana Miryam angekuwa na shughuli fulani tu iliyomweka bize, hivyo nikaona nikiondoe hiki kimuwasho cha kutaka tuwasiliane muda wote. Sikupaswa kusahau kuwa huyu alikuwa mwanamke mtu mzima mwenye mambo mengi, hakuwa kama pisi nilizopitia.

Ndani ya muda huo huo, Ankia akasema anaenda hapo Masai, Bobo kamwita. Nikampa ile "mhm" kikejeli, naye akanicheka kwa njia ya kejeli na kwenda chumbani kujiandaa. Haya bwana, mimi ndiyo ningebaki na kaupweke wakati ulipaswa kuwa muda wangu wa kuondoa upweke, angalau hata kwa simu tu. Mwenye nyumba wangu akatoka akiwa amevaa T-shirt la mikono mifupi, jeupe, pamoja na kikaptura-skinny kilichofikia mwanzo wa mapaja yake; juu kidogo ya magoti yaani. Alikuwa amejipiga na makunato mwenyewe, naye akaniaga huku akinitania kwa kusema kama vipi nimwite Miryam aje ili nisibaki kununa tu hapo.

Kejeli zote nikazipokea, sawa bwana, naye akawa ameniacha na kwenda huko ikiwa inaingia saa sita. Kwa watu wa aina yake, palikuwa ndiyo pamekucha. Hapo alikuwa ameitwa na bwana wake, wakanywe na kujifurahisha bila shaka, na kama ni kitu ambacho sikuwa nimesema awali, ni kwamba kwa kipindi hiki Bobo ndiye aliyekuwa ameachiwa usimamizi wa Masai YOTE, yaani awe kama mmiliki, lakini kwa muda tu. Kuna madili na madili inaonekana yalikuwa yamefanywa baada ya Bertha kukamatwa na Chalii kuuawa. Hivyo Ankia alikuwa analishwa bata haswa.

Mzee nikabaki sofani tu huku naitazama TV utadhani nina ugomvi nayo, nikiwa nimeshaghairi kuishika tena simu maana saa sita ilikuwa inatembea tu bila ya Miryam kuwa amenicheki. Nikawaza labda hata angekuwa ameshalala, si unajua labda uchovu na nini, kwa hiyo nikaona ni bora nichukue simu tu ili nimtumie ujumbe wa kumtakia njozi njema. Nikaishika simu, na ile nataka kumtumia ujumbe, ikaanza kuita hapo hapo. Tabasamu hafifu likajengeka usoni kwangu, maana ilikuwa ni bibie mwenyewe ndiye aliyepiga, nami nikapokea na kuweka sikioni.

"Hello..." sauti yake tamu ikasikika.

"Ndiyo ukaona unichunie mpaka sa'hivi, eti?" nikamuuliza hivyo nikijifanya nimeudhika.

"Ooh, I'm sorry... yaani, nilikuwa nimetingwa na kazi, yaani.... ah..." akaongea kama vile amechoka mno.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Usijali, naelewa."

"Yaani nisamehe tu. Kuna jambo nafix hapa, kila mara linakua tu... nikashindwa hata kushika simu..."

"Ishu gani unadili nayo?"

"Ni ishu ya Mamu tu, hamna kwere. Nimemaliza kuandika, nilikuwa naandika barua fulani hapa..." akasema hivyo.

"Okay sawa. Nilidhani labda ungekuwa umeshalala..." nikamwambia.

"Hamna, bado niko macho. Yaani ndiyo nimeziona text zako za muda ule sa'hivi. Pole nimekuonea mno, eti?" akaongea kama ananibembeleza yaani.

"Ah, wala usijali. Me niko poa..." nikajibu kwa unyoofu.

"Mbona nahisi kama umenuna?" akauliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Mh? Ninune nini sasa?" nikauliza hivyo huku nikitabasamu.

"Si nimekufanya umenisubiri mno?"

"Wala hata, akusubiri nani? Ndo' kwanza hapa nasinzia," nikamwambia hivyo kiutani.

Akacheka kidogo, naye akaniambia, "Haya, usiku mwema basi..."

"Ih, we' unaenda wapi? Em' tulia hapa," nikamwambia hivyo.

Akacheka tena, kisha akasema, "Sawa. Niambie."

"Ulikuwa umeshapanda bed?" nikamuuliza hivyo.

"Ndiyo nimetoka kujimwagia, nataka kupanda ndiyo," akasema hivyo.

"Nataka kukuona," nikaongea kwa sauti ya chini.

"Tuongee kwa video call?" akauliza.

"Hamna. Nataka nikuone kabisa," nikasema hivyo.

Akatulia kidogo, kisha akasema, "Kivipi, yaani... hapo nje?"

"Mmm," nikakubali.

"Jayden... sa'hivi usiku..."

"Siyo sana bwana..."

"Mh... ahah... umeshaniona leo, mara nyingi tu. Tutaonana kesho, ama tuongee kidogo kwa video call," akasema hivyo.

"Mm-mm... Nataka kuonana nawe live... kidogo tu. Nimeshaku-miss," nikaongea kwa sauti yenye kubembeleza.

"Lakini... wengine washalala...."

"Please... kidogo tu. Natoka hapo nje, nakuona tu ukutani, then unarudi ndani chap," nikamshawishi zaidi.

Nilikuwa napigia picha sura yake nzuri akijishauri na kujishauri, naye akasema, "Sawa. Natoka upesi."

"Me nishafika," nikamwambia hivyo.

Hapo hapo nikaruka kutoka sofani na kuukimbilia mlango, moja moja mpaka nje na kusogea hadi kwenye ukuta wa uzio. Sasa je! Ankia alidhani ningeboeka eti, si niko hapa sasa? Araa!

Sikuwa nimekata simu, nami nilipokuwa nimesimama, matobo ukutani yaliniruhusu kuuona mlango wa kuingilia ndani kwao bibie, na hapo nikauona ukifunguka na Miryam mwenyewe akisimama sehemu hiyo. Akatabasamu, mimi pia nikampa tabasamu, naye akaiweka simu sikioni na kuongea kwa sauti ya chini sana, akisema amefurahi kuniona tena. Lakini mimi nikamwambia nilitaka aje mpaka hapa, hata nimguse tu, naye akawa anaona kama namsumbua.

Nikaendelea kumbembeleza aje, kwa ile sauti ya Alikiba 'ooooh aje...' naye akayeyusha chuma. Akarudi ndani zaidi na kurejea na funguo, kisha akalifungua geti la mlangoni kwa uangalifu na kutoka, akiwa hajasahau kuvaa ndala zake miguuni. Nikakata simu hatimaye na kuendelea kumwangalia hadi alipokaribia sehemu niliyosimama, na alikuwa amevalia ile nguo yake ya kulalia, huku nywele zake akizivalisha kikofia laini kichwani.

Akasogea hadi hapo ukutani, nyuso zetu zikitenganishwa na hilo uzio, na kwa sauti ya chini akasema, "Ila Jayden! Mbona we' msumbufu sana?"

"Yaani kama vile haunijui! Umeshasahau nilivyokuwa nakusumbua mpaka ukakubali muziki wangu? Na bado..." nikamwambia hivyo kiutani.

Akaniangalia kimkazo eti, halafu akasema, "Umeridhika sasa? Nenda ukalale."

"Tesha amerudi?" nikamuuliza.

"Hamna. Amelala huko kwa rafiki yake," akasema hivyo.

"Haya, njoo..." nikamwambia hivyo.

"Wapi?" akauliza hivyo kimshangao.

Nikamwita kwa kiganja huku nikirudi nyuma zaidi usawa wa huo huo uzio na kusimama, ambao kwa upande wake ungekuwa ni ule usawa wa bomba lao la maji hapo nje. Bado palikuwa na ugiza maana taa haikuwa imebadilishwa.

Miryam akatembea kwa uangalifu ili asitoe sauti kubwa ardhini, na alipokaribia hiyo sehemu, akauliza kwa sauti ya chini, "Unataka kufanya nini wewe?"

Nikampitishia simu yangu hapo hapo kwenye tobo moja ukutani, nikimwambia kwa ishara kuwa aichukue, naye akaipokea huku akiniangalia kwa kutoelewa. Hapo hapo nikaanza kupanda huo ukuta, mpaka juu, nikajitahidi kuwa mwangalifu sana ili nisikanyage vyupa na nondo zenye kuchongoka zilizokuwa kwa hapo juu. Miryam alishangaa! Akafunika mdomo wake kwa viganja huku akiniangalia kama vile haamini, nami nikafanikiwa kuvuka upande wetu na kushuka mpaka sehemu aliyokuwa amesimama yeye. Ukuta wa uzio haukuwa mrefu sana.

Baada ya kufika chini na kumgeukia, nikaona namna ambavyo alikuwa ananiangalia kimaswali sana, nami nikajitabasamisha kimchezo tu na kumtikisia nyusi kiuchokozi.

Akasema, "Jayden una... una matatizo gani?"

Nikaichukua simu yangu na kuiweka mfukoni, halafu nikakishika kiuno chake na kumvuta karibu zaidi na mwili wangu kwa makusudi.

"Wewe!" akasema hivyo kwa kunong'oneza huku akiangalia pembeni kwa njia ya tahadhari.

"Niliposema nataka kukuona, nilimaanisha hivi," nikamwambia hivyo kwa sauti tulivu.

"Ja.... hii siyo akili. Una... unawaonyesha wezi kwamba hapa ni rahisi kuingia..."

"Wezi gani, Miryam? Mwizi pekee aliyepo hapa ni mimi... na tayari nimeshauiba moyo wako," nikamwambia hivyo kizembe.

Akalibana tabasamu lake la haya, kisha akaangalia pembeni na kusema, "We' ni kichaa."

"Umeona eh? Yaani sina akili ikija juu yako..."

Akapiga ulimi kidogo na kusema, "Niachie bwana... hebu nenda. Saa saba inakaribia, halafu... natakiwa niamke mapema."

"Mbona bado mapema?" nikamuuliza hivyo bila kumwachia kiuno.

"Ahh... sitanii Jayden. Natakiwa nilale usingizi wa kutosha hata masaa machache. Nina safari kesho," akasema hivyo.

Kauli yake ikanifanya nimwachie kiuno taratibu, naye akatulia hapo hapo tu akiniangalia kwa hisia. Aliona imevuta umakini wangu.

Nikamuuliza, "Safari ya wapi tena?"

Akainamisha uso wake kwa ufupi, kisha akanitazama na kuniambia, "Nitaenda Morogoro."

"Moro? Unaenda kufanyaje?"

"Naenda tu kucheki haya masuala ya shamba la Mamu. Watunzaji kule wana... malalamiko fulani... so naenda kuweka mambo sawa,"

"Ahaa, ndo' ulichokuwa unafanyia kazi?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Okay. Lakini... kesho si ni send-off ya Doris? Utaikosa?" nikamuuliza.

"No. Nachukua treni ya mwendokasi..." akajibu hivyo.

"Ooh, kwa hiyo unaenda fasta tu na kugeuka..."

"Eeeh... na natakiwa niondoke mapema kabisa. Nataka nifike huko kwenye saa mbili, nishughulike na hayo mambo, halafu niwahi kurudi. Yaani kama ni kuchelewa, kumi na mbili jioni niwe huku tayari..."

"Okay. Na siku hizi Dar na Moro ishakuwa kama Mbagala na Kariakoo..."

"Ahah... teknolojia. Ila ndo' maana nimekwambia nataka kuwahi kulala, saa kumi na moja niwe nimeshaamka... halafu we' kichwa umenibana tu hapa..." akasema hivyo.

"Ahahah... utanilaumu? I'm so addicted to you..."

"Kwani hiyo ni makosa yangu?"

"Ya nani sasa?"

"Ni yako. Jifunze kujizuia. Siyo lazima mpaka unione kila mara..." akaniambia hivyo kwa uhakika.

Nikamkazia macho kiasi.

"Eeeh... si tungeweza hata kuongea kwa video call? Ya nini hadi unaruka ukuta ili eti uniguse? Yaani wewe!" akaongea hivyo huku akiniangalia kama amekerwa.

"Ah, basi tu, sa' nitafanyaje? Sijisikii fresh kutokukuona live kwa muda mrefu. Unakumbuka kama kuna siku yoyote imepita sijakuona tokea nilipokwambia nakupenda?" nikamuuliza.

"Mhm... hapana..."

"Ndiyo hivyo. Yaani we' ni dawa ya kila kitu kwangu, nikikuona napona..."

"Na kesho je? Tuseme nikaenda, nikachelewa kurudi, halafu nikapitilizia kwenye sherehe na tusionane kabisa mpaka kesho-kutwa... itakuwaje?" akauliza hivyo.

Nikatulia kidogo nikimtazama machoni kwa hisia sana, nami nikamwambia, "Tutaenda wote."

Akakunja uso wake kimaswali na kuuliza, "Wapi? Moro?"

Nikatikisa nyusi kukubali.

"Wewe! Acha masihara yako basi... ahahah..." akashangaa kidogo.

"Sitanii. Nataka niende nawe," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

"Ahah... Jayden, hii ni safari ya kikazi, siendi kuzurura...."

"Hata kama. Nataka tu niwe pamoja nawe," nikamwambia hivyo.

"Kwa hiyo... kweli kabisa unataka tuondoke pamoja?"

"Yeah. Nitakusindikiza, na me nina muda sijaondoka jijini... itakuwa kama tour ndogo. Whatcha say?" nikamuuliza hivyo.

"Eh... mhm... yaani naona unataka kukaba kila kitu sasa..."

"Kabisa. Sitaki yaani... sitaki nihisi uko mbali nami kabisa Miryam. Yaani kila mara nataka tu nikuone, niwe karibu yako, nihisi uwepo wako... inanipa amani sana," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Akaniangalia kwa ufikirio kiasi, kisha akaniambia, "Unavyoongea hivyo... inavutia. Lakini sijui kwa nini, nakuwa nahisi ni maneno rahisi sana kwako kusema kwa sababu labda umeshayatumia kwa wengi..."

Nikatikisa kichwa kiasi kukataa na kumshika mkono, nami nikamwambia, "Najua Miryam, najua ndiyo tumeanza, na ninaelewa kwamba hatujatoka pazuri mno. Sitarajii moyo wako uwe umeshafunguka kwa kila kitu, yaani... najua bado unataka kuwa mwangalifu. Sitakuhakikishia kwamba nakupenda kwa maneno tu, nitakuhakikishia na kwa matendo pia. Ndiyo itakuwa sehemu ya kukufanya uache kuogopa."

"Ahah... okay, ni sawa. Nisamehe tu lakini, maana sometimes nakuwa...."

"Usijali. Nakuelewa," nikamwambia hivyo na kumshika shavuni taratibu.

Akabaki akinitazama usoni kwa macho yenye imani sana.

Nikamwambia, "Najua sitaenda na wewe kila sehemu utakayoenda, lakini popote ambapo naweza kuwepo kwa ajili yako... nitakuwa hapo Miryam. Ndiyo nachotaka kufanya hasa kwa wakati huu. Natamani kama... ningeweza ku-rewind muda yaani... ningeurudisha muda nyuma na kukupata kipindi hichoo..."

"Ahah... si ungekuwa mdogo wangu sana?" akauliza hivyo kwa hisia.

"Yeah, lakini haingejalisha. Ningekupata tu na kukupenda, na ningekuonyesha huo upendo kwa muda mrefu zaidi mpaka kufikia huu wakati ambao tumesimama hapa... na kuendelea," nikamwambia hivyo kwa sauti yenye kubembeleza.

Akakishika kiganja changu huku akiniangalia machoni kwa hisia sana.

"Sikudhani ingewezekana tena Jayden kuja kupenda kutoka moyoni. Yaani sikufikiria ningekuja kupenda tena namna hii, na sikujua kama ningekuja kupenda kila kitu kuhusu mtu hadi nilipokutana na wewe Miryam. Yaani ninakupenda zaidi ya ninavyokupenda sana," nikamsemesha kwa hisia.

Akatabasamu zaidi huku akisugua kiganja changu taratibu kwa vidole vyake laini, naye akauliza, "Huwa unayatoa wapi hayo maneno Jayden?"

Nikatabasamu tu na kumwambia, "Nayasomaga tu kwenye mitandao, ndo' nakuja kuyamwaga hapa..."

"Oooh... kwa hiyo kumbe nafikishiwa tu mawazo ya mtu mwingine hapa, eh?" akauliza hivyo kiutani.

"Oops! Nimekamatika..." nikaongea kikejeli.

"You fool!" akaniambia huku akitabasamu.

Sote tukacheka kidogo kwa pumzi.

Akatikisa kichwa kuonyesha uthamini, naye akasema, "Asante sana kwa kunipenda. Ninakupenda sana pia."

"Yaani tulivyo... kama Romeo na Juliet," nikamwambia hivyo.

Akatabasamu zaidi kwa furaha.

Nikauachia uso wake na kuuliza, "So... kesho nitakusindikiza Moro, eh?"

"Sawa. Tutaenda pamoja. Aa... nafikri hapo stendi zinakuwepo gari zinazoenda Stesheni... sijajua sana, ila tuta...."

"Tutapanga tu pa kukutana, afu' tutaenda pamoja, tutajua," nikamwambia hivyo.

Akatikisa kichwa kukubaliana na hilo.

Nikavishika viganja vyake vyote kwa chini na kusema, "Okay. Basi ngoja nikuache ukalale sasa. Me huwa nina usingizi mzito kwa hiyo nitaweka alarm."

"Kumi na moja, sharp," akaniambia hivyo.

"Mm-hmm," nikakubali.

"Haya, usiku mwema, nenda sasa. Uruke ukuta kwa uangalifu... na iwe mwanzo na mwisho," akasema hivyo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Go!" akaniambia hivyo kwa msisitizo.

Nikaangalia juu, kisha nikaanza kuimba kwa sauti ya chini, "Basi nichumu, ni-kiss mwah.. ai nichumu, ni-kiss mwah..."

Nikamwangalia tena na kukuta anatabasamu kwa ile njia ya kuhukumu, akinishusha na kunipandisha eti, nami nikatabasamu kwa furaha.

Akanicheka kidogo kwa pumzi, kisha akasema, "Una hakika ulikuwa umeshasugua kinywa?"

Nikakunja uso kimaswali.

"Kama huoshagi mdomo kabla ya kulala, hiyo chum ndo' huipati," akasema hivyo kiutani.

"Ih! Kumbe umeshatoa na kitabu cha masharti afu' bado hujaniuzia?" nikamuuliza hivyo kiutani pia.

Akacheka kidogo huku ameziba mdomo.

"Na sasa hivi ndiyo unaniambia sharti la kwanza wakati hata nilikuwa sijaliandaa hili domo? Basi usiku mwema..." nikamwambia hivyo nikijifanya nimeudhika.

Bado alikuwa anacheka, nami nikaigiza kutaka kupanda ukuta, lakini akaishika T-shirt yangu na kuivuta huku akisema, "Hebu njoo hapa..."

Nikageuka na moja kwa moja kukutana na mdomo wake ulionifuata bila kusita. Ah!

Miryam alipatia aisee. Alijua. Zamu hii hakunipiga busu, alinila denda! Denda ya maana! Aliufinya mdomo wangu kwa midomo yake taratibu sana, akiepuka kutumia ulimi mwanzoni na kuacha midomo yetu pekee ndiyo ivutane, kisha ndiyo akaingiza ulimi wake ndani yangu na kutoa penzi la mdomo kwa ufundi ambao sikuwa nimeutegemea kabisa! Alikuwa na midomo mitamu, akipenda nimwachie tu yeye ndiyo aonje kila alichotaka kula, na katika hali ya kunogewa zaidi, akakishika kichwa changu kwa mikono yake yote na kuanza kukipapasa taratibu kama vile hataki tuache. Sijui hata aliweka wapi simu yake. Nilisisimka nyie!

Nikakishika kiuno chake kwa njia ya kukumbatia, kwa nguvu, bibie akiwa amenogewa tu kunipa denda hii tamu sana, miguno laini ya pumzi ikimtoka kadiri alivyoendelea kunipatia utamu wa ulimi wake, na nilikuwa nimeshasimama dede kwa nguvu kubwa sana. Yaani hapo nikasahau yote, nikiwa tayari kwa lolote lile ambalo angefanya lifuate, maana hisia zilikuwa huko juu juu yaani. Ndoto ilikuwa inatimia hapa!

Ilionekana ni kama dakika nzima ilipita akiwa ananipandishia moto kwa denda hii, ndipo akaikatisha taratibu na kuweka paji lake la uso usawa wa shavu langu. Nikafumbua macho na kuona yeye akiwa amefumba ya kwake bado, akiwa anazungusha kichwa chake taratibu na nyuso zetu zikiwa kwa ukaribu mno, nami nikatabasamu na kubana ubavu wake kwa kiganja changu, katika njia ya kumtekenya, naye akapandisha nyonga kidogo na kufumbua macho yake kuniangalia.

Aliniangalia kwa njia yenye hamu, kisha akaweka kiganja chake kifuani kwangu na kusema, "I really like this, Jayden. But I don't want us to go too fast..."

Aliongea kwa sauti tamu mno yenye kunong'oneza kiasi, yaani hata kama hakuwa akitaka tupeleke mambo mengi haraka sana, hapa tu tayari alikuwa ameshanipeleka mawinguni huko.

Nikiwa namwelewa, nikamwambia, "Usijali. I got you."

Akarudisha uso wake nyuma na kunitazama kwa hisia, naye akasema, "Tutaonana baadaye."

Nikatikisa kichwa kukubali hilo, ndiyo nikakiachia kiuno chake na kuusogelea ukuta. Nikapanda taratibu na kwa uangalifu sana, yeye bado akiwa amesimama hapo hapo, nami nikashukia upande wa kwa Ankia na kumtazama tena. Akanipungia mkono wa kwa heri ya sasa, nami nikaunda kopa kwa viganja vyangu na kumwonyeshea kwa kuiweka usawa wa moyo. Akatabasamu kwa hisia sana, kisha huyoo akaelekea ndani kwake.

Nikageuka tu na kuelekea ndani kwetu pia, nami nikafunga mlango na kutulia hapo sebuleni kwanza. Nikajikuta najishika mdomo wangu, nikitabasamu kama zezeta yaani kwa kukumbukia hiyo "chumu" niliyopewa hapo nje, na bado hapa chini palikuwa pamevimba eti! Nilikuwa na hisia nzuri sana, sana, sana, kwa wakati huu, na najua zingeendelea kupanda juu zaidi kadiri ambavyo siku zingeendelea.

Na huyu mwanamke alionekana kuyajua mapenzi kwelikweli, siyo mchezo, yaani nilikuwa nina hamu ya kuyatalii naye mengi sana kutokea hapa. Kwa kuwa siku ya kesho ningekwenda naye Morogoro, ningetakiwa kujiweka katika uimara wa kiume ndani ya akili, ili kama utalii wa kwanza ungefanywa hiyo hiyo kesho, uwe wa maana. Ona, nilikuwa hadi nimeanza kuwaza upuuzi mapema namna hii!

Lakini najua hilo lingekuwa jambo hakika kufanyika baina yangu mimi na yeye, haijalishi lini, kwa hiyo kweli utayari ulihitajika maana nilikuwa nimeshamhamu kwa muda mrefu sana sasa huyu mwanamke. Nikaona nizime taa na kwenda kulala, yaani nikajitupia kitandani huku natabasamu tu na kufurukuta-furukuta huku na huko kwa kuhisi mihemko ya hatari, nikiingoja alfajiri ifike ili niondoke na mwanamke wangu.







★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
hata marefa wana timu zao MIMI apange Matokeo ili JC afunge goli
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★


Nimekuja kushtuka ikiwa bado ni usiku, na tena nikisema kushtuka namaanisha kushtushwa baada ya kupatwa na njozi isiyo nzuri. Yaani niliota niko mahala fulani pamoja na Miryam, halafu ghafla tukavamiwa na watu waliokuwa wamevalia manguo yaliyochanika-chanika kwa muundo kama wa tambi, huku nyuso zao zikiwa za mafuvu. Walitukamata mimi na Miryam na kuanza kututesa, wakisema maneno "apple pie" kwa njia ya kuimba kwa sauti mbaya kweli, halafu mmoja wao akamchinja Miryam mbele ya macho yangu na kukirusha kichwa chake usoni kwangu.

Yaani uso wa kichwa cha Miryam ulipoufikia uso wangu ndotoni ndiyo nilishtuka kwa kufumbua macho, nikijikuta nimelala chali huku chumba kikiwa na giza bado, nami nikaendelea kutulia hivyo hivyo nikisikilizia namna ambavyo mapigo ya moyo wangu yalitembea kwa kasi. Hofu ilikuwa imenivaa kiasi, maana ndoto za namna hii huwa zinaogopesha kwa sababu zinafanya uhisi vitu kuwa halisi kabisa. Nadhani sijui shauri ya kulala chali, yaani ulikuwa umepita muda sijaota ndoto mbaya, ila sikujihisi amani kabisa kumwota Miryam kwa njia hiyo.

Nikajinyanyua taratibu na kuchukua simu kuangalia muda. Ilikuwa ni saa kumi usiku, ikielekea alfajiri, na hapo yaani usingizi wote ukawa umekata. Hata kama ningesema nijilaze kidogo kusubiri hadi muda niliopangia kuanza kujiandaa ufike, nisingeweza kupata utulivu wa kiakili maana hiyo ndoto iliendelea kunisumbua kichwani ingawa nilijitahidi kuacha kuifikiria. Inawezekana labda niliota tu hivyo bila sababu yoyote, lakini hiyo kitu ilinifanya nihisi kama vile kuna kitu nilikuwa nimesahau kufanya. Ni nini ambacho kingenipa wasiwasi kwamba Miryam angeumia baada ya sisi kuanzisha mahusiano ya kimapenzi hatimaye? Ding, ding, ding... Festo!

Ni kweli kabisa nilikuwa nimeshasahau kuendelea kufatilia ikiwa huyo jamaa alikuwa ameondoka, maana sikuridhishwa na uhakika nilioupata kutoka kwa Miryam mwenyewe na askari Ramadhan aliyesema kwamba jamaa alikimbia nchi. Huenda hiki ndiyo kitu kilichonipa wenge bado, hasa kwa kuwa wakati huu Miryam alikuwa wangu. Kwa njia moja ama nyingine, umakini ulitakiwa kuwa muhimu, yaani sikupaswa kumsahau huyo jamaa. Bertha alikuwa ndani na angekarabatiwa na askari Ramadhan, lakini jamaa alikuwa huru. Huru. Hiyo ilikuwa sababu tosha kwangu kujua kuwa hatari ingeweza kurudi muda wowote ule, hivyo sikupaswa kujisahau sana.

Oh, JC nikiwa na wasiwasi yaani ningewaza lolote lile hata kama hakukuwa na ishu kubwa mno ya kuwaza. Uwezekano wa kwamba Festo angekuwa ameondoka kweli na labda hata kwenda kupata mwanamke mwingine ulikuwepo, lakini ulikuwa ni uwezekano tu, sikujua kama ulikuwa ndiyo uhalisia. Ningepaswa kuwa na uhakika zaidi, kwa hiyo ningeendelea kufatilia nyendo zake kokote ambako angekuwa mpaka nijue kama anastahili kuwekwa pembeni, ili nihakikishe usalama wangu na Miryam pia.

Hivyo ili kuyaondoa mawazo na nini nikawa nimeamua tu kuanza kujiandaa, nikitoa nguo safi kabisa na kunyoosha mkunjo wowote usiotakikana, halafu nikatoka na kwenda kuoga hiyo hiyo saa kumi. Kulikuwa na baridi kali kwa mida hii, na najua mpaka wakati ambao tungeondoka na bibie bado lingekuwepo, hivyo nikaona siyo mbaya nikivaa na koti la ile suti ya kisharobaro ambayo madam Bertha alinipa siku kadhaa nyuma. Kufikiria kulivaa koti hilo kukanifanya nimuwaze, kukiwa na ile nia fulani kwa hisia zangu ya kutaka kujua hali yake akiwa huko ndani, lakini naelewa hiyo isingenisaidia kwa lolote. Kuna vitu tu nilipaswa kuviachia.

Nikaamua tu kutulia na kusubiri mpaka imeingia saa kumi na moja, nami nikaamua kumtumia Miryam ujumbe nikisema nipo tayari, hivyo akiamka na kumaliza kujiandaa anishtue. Lakini ni muda huo bibie akawa amejibu, akiniambia kwamba yaani yeye alikuwa ameshajiandaa mapema mno, na nilikuwa nimemwahi tu kwa kutuma ujumbe maana alitaka kunipigia. Kumbe siyo kwamba tungetakiwa kuamka saa kumi na moja, ila kuondoka saa kumi na moja. Ikiwa ile ndoto isingenishtua, basi alarm ingekuja kuniamsha Miryam akiwa ameshamaliza kuvaa!

Kwa hiyo hapo sote tukawa tumekamilisha maandalizi, yaani yeye alimaliza kuvaa na ndiyo alikuwa anatoka, hivyo na mimi nikavaa viatu vyeupe upesi na kusanuka pia. Nilivalia T-shirt langu jeupe la mikono mirefu pamoja na suruali jeans ya blue, huku koti jeusi-kijivu la suti likinifunika kwa juu. Sikuhitaji kubeba madude mengi, ni simu tu na pesa, pamoja na kadi ya mwaliko wa send-off ya Doris niliyokuwa nimeshalipia, nami nikamwachia ujumbe Ankia wa kumuaga, nikimfahamisha kuwa ninamsindikiza Miryam Morogoro lakini nikamwomba awe makini kutosema hilo kwa yeyote.

Nikatoka ndani hatimaye na kuelekea nje, nikifunga milango na geti kwa uangalifu, kisha nikasimama pembeni usawa wa duka la Fatuma na kumtumia Miryam ujumbe kuuliza alitaka niende kumsubiria kwa wapi maana nilikuwa nje tayari. Akasema nimsubirie hapa hapa nilipokuwa kwa sababu alihofia kutembea peke yake, na hiyo ilipatana na akili. Ikiwa ni saa kumi na moja bado, upande huu wa kitaa ulikuwa na giza, ukimya, na utupu. Mwanamke kama yeye atoke tu na kuanza kutembea mwenyewe ingeweza kuwa hatari, najua hilo halingekuwa na shida kama Tesha angekuwepo angalau.

Hivyo nikasubiria hapo dukani kwa dakika chache, nami nikamwona bibie akitoka mule ndani kwao. Akaja mpaka hapo nje, akifunga geti lao kwa umakini na kisha kurusha funguo huko ndani ya geti, ili mama zake wakiamka waweze kufungua bila tabu. Usalama kwanza. Akaja hadi karibu nami, na alikuwa amevalia gauni refu la kike lililobana, lenye muundo wa kitambaa kama jinsi masweta ya shule yalivyo ingawa siyo nzito, likiwa la rangi ya ugoro na lililochoresha mwili wake vizuri sana.

Alivalia koti la jeans pia lenye rangi ya blue, kufunika kifua ili kuipinga baridi hii ya alfajiri, na miguuni alivalia simple nzuri za rangi ya dhahabu. Nywele zake akiwa amezibana juu ya kichwa chake, alionekana kuwa mrembo sana kwa muda huu, yaani ule upya wa siku kwa alfajiri ulimfanya aonekane mweupeeh kuliko kawaida. Alining'iniza mkoba mweupe wa manyoya mkononi, huku akijikumbatia shauri ya kuhisi baridi. Akanifikia karibu, nami nikauchukua mkoba wake na kisha kumpa kumbatio upesi ili ahisi joto kidogo, na mimi vilevile nihisi lake.

"Umeamka poa?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Yeah. Wewe?" akauliza hivyo kwa sauti tulivu pia.

Nikamwachia na kusema, "Niko fresh. Baridi eh?"

Akatikisa nyusi kukubali.

"Haya, twende. Usije ukaganda," nikamwambia hivyo huku nikisugua mgongo wake kwa kubembeleza.

Mdogo mdogo, mimi na mpenzi wangu tukaianza safari kuelekea barabarani, nikitembea pamoja naye kwa ukaribu huku nampigisha story. Wote tulikuwa na kale kahali ka umakini kwa sababu ya hii kuwa mapema mno, hivyo hakukuwa na utani. Nikawa nimemuuliza ikiwa aliwahi kutumia usafiri wa treni ya mwendokasi kabla, lakini akasema ndiyo ingekuwa mara yake ya kwanza.

Vilevile na mimi pia, hii ingekuwa mara yangu ya kwanza. Najua ujenzi wa huo mradi kwa kipindi hiki ndiyo ulikuwa unaelekea kuifikia Dodoma, na safari za mizunguko kutokea Dar mpaka Moro ndiyo zilikuwa zimeanzishwa, kwa hiyo sote tungeenda kujionea jinsi ambavyo ingekuwa, yaani 'experience' ya mara ya kwanza kuzipanda hizo ishu tungeipitia pamoja. Angalau na nchi yetu ilikuwa inapiga hatua kwenye miundombinu na mambo mengi, ingawa najua hujuma zilikuwa nyingi mno... na zingeendelea.

★★

Basi bwana, mimi na Miryam wangu tukawa tumechukua usafiri wa bodaboda hadi kufikia stendi ya Mbagala Rangi Tatu, nasi tukaelekea huko huku nikiwa nimemshika bibie mkono. Kwa muda huu, eneo hilo lilikuwa na watu, wengi wao wakiwa wanasubiri magari ya kuelekea pande walizotaka kwenda, nasi tukakutana na kizungumkuti cha kuhitaji kusubiri magari ambayo yangekwenda moja kwa moja mpaka Stesheni.

Ingekula muda maana tulisimama karibia dakika kumi na tano bila ya magari hayo kufika, hivyo nikamwambia Miryam tukodi bajaji na kwenda barabara ya kuelekea Makumbusho huko, ili tushukie kwenye kituo fulani ambako daladala za kwenda Stesheni zingepita. Likaonekana kuwa wazo zuri kwake, hivyo tukaamua kuchukua bajaji mmoja wa kutupeleka huko, nayo vruum ikatembea kwa kasi kutuwahisha. Miryam alionekana kuwa na usingizi bado, tangia tumeondoka Rangi Tatu akawa amenilalia tu begani na kufumba macho kwa dakika nyingi, huku mie nikikaza macho mbele na kuendelea kutulia tu.

Tukafika eneo hususa nililotaka na kushukia hapo kwa pamoja, daladala ikaja, nasi tukaendelea na safari kwa mara nyingine tena. Niliwahi kufika maeneo ya Stesheni kipindi fulani lakini sikuwahi kwenda kabisa kwenye stesheni yenyewe, hii mpya ya SGR, kwa hiyo hakukuwa na tabu Miryam wangu kuendelea kunilalia tu begani hadi tulipofika maeneo ya huko. Tulikuwa tunatazamwa sana, na nilipenda. Miryam alistareheka kabisa kuwa kando yangu mbele ya watu wote ambao hatukuwafahamu, na nilitaka ije kuwa namna hiyo kwa wale wote waliojalisha kwetu. Safari yetu ya mapenzi ndiyo ilikuwa inaanza.

Baada ya kufika hilo eneo, tukaelekea mpaka kwenye jengo zuri sana la stesheni hiyo ya treni, na ilikuwa imeshaingia mida ya saa moja kabisa. Tulichelewa, lakini hakukuwa na namna. Yaani hilo jengo, halikuonekana kama jengo la stesheni ya treni, ila kama terminal ya uwanja wa ndege. Lilikuwa zuri, safi, likijengwa kwa vioo vizito kulizunguka, yaani... safi! Ndani sasa ndiyo kulikuwa na utaratibu uliofanya pawe kama airport kabisa, kukiwa na mashine za X-ray za kuchunguza vitu haramu na walinzi maaskari, siyo wale uchwara.

Watu waliofika hapo, yaani walionekana kuwa na yale maisha ya uzungu, pesa, hata kama siyo wote, wengi walijiweka hivyo. Wanawake walivaa kwa kujiachia, mapaja nje nje pamoja na hali kuwa yenye baridi, mionekano ya maana, yaani nilihisi nimeingia sehemu maridadi zaidi kuliko hata nyingine nilizowahi kwenda. Sisemi ilipita zoooote ambazo zilikuwa maridadi, ila nasemea kwa hizi tu zilizohusiana na masuala ya safari ukiondoa majengo ya uwanja wa ndege.

Tukapita ukaguzi, kisha tukapanda hadi ghorofa la pili ili kukata tiketi. Miryam wangu akakaa kusubiri nikate tiketi zetu, nakwambia watu waliopanga foleni fupi fupi wakiwa na zile staarabu za kishua, nami nikapata tiketi hatimaye na kurudi kukaa na bibie. Treni ingefika kwenye mida ya saa tatu, na bila shaka Morogoro tungefika kama siyo saa nne, basi saa tano.

Tukaendelea kutulia tu hapo, mara kwa mara nikiangaliana na Miryam na sote kutabasamu bila sababu yoyote ile, basi tu, ushirika wangu karibu naye ulikuwa mzuri sana. Tukashikana viganja kabisa na kutulia hivyo hivyo, na sikuweza kujizuia kuona namna ambavyo baadhi ya wanawake na wanaume walitutazama sana. Siyo kwamba kusema Miryam ama mimi pekee ndiyo tuliokuwa wenye sura nzuri peke yetu humo, lakini nadhani ni jinsi tu tulivyokuwa tunajiweka ndiyo kuliwavutia. Utulivu, kama hatupo vile.

Nikawa nawatikisia tu vichwa wanaume fulani walionipa salamu kwa njia hiyo, huku nikiepuka kukodolea mwanamke yeyote maana wa kwangu alikuwepo hapo hapo. Na wala hata hakuonekana kujali, alikuwa zake ametulia tu kama hana habari kuwa ningeweza kuibiwa, na hiyo ikanipa hali ya kujiamini zaidi hata kwa yeye ambaye angeweza kuibiwa na wanaume wengine waliomwona kuwa mzuri sana. Nikawa namsemesha mara moja moja tu na kumwonyesha video za ucheshi kwenye simu yangu ili kupisha muda.

Tumekaa hapo mpaka saa mbili na nusu hivi, kweli tangazo la treni kuwadia likatolewa. Tukanyanyuka, pamoja na watu wengine, nasi tukaenda huko na kuingia kwenye siti zetu tulizopewa. Ah, yaani hii treni ilikuwa 'magic.' Ilikuwa nzuri, siti laini, TV ndogo kila mstari wa siti kwa juu, AC za maana, na nadhani hata huduma ya choo ilikuwepo, ila nani angejisaidia kwenye mwendokasi? Natania tu!

Kufikia hii mida jua lilikuwa limeshawaka, kwa hiyo nikawa nimevua koti, huku Miryam akiwa amevaa lake tu. Hakutaka kuongea sana, yaani ile tumefika tu na kukaa, akanilalia begani tena. Nikacheka kidogo tu na kumwambia akae tupige story bwana, lakini bibie akaendelea kulala tu utadhani alikuwa amenunua mto mpya, kwa hiyo nikaona nimwache aenjoy usingizi wake tu. Ndiyo ulikuwa mwanzo wake wa kudeka huo. Nikamwashia na AC, kisha nikaingia mtandaoni kuperuzika.

Saa tatu haikukawia kuingia, na ndiyo treni yetu ikaanzisha mwendo.

★★

Hii safari ilikuwa tulivu sana tofauti na vile nilivyotazamia. Yaani treni ilitembea kama vile iko pale pale. Iliseleleka tu. Sikusikia makelele yoyote, ilikuwa kama niko kwenye ndege. Kukawa na wahudumu wanapita nakwambia, wanatupatia vikeki eti vya kuyeyushia meno, na kwa dakika kama 40 tokea tumeondoka, Miryam alikuwa ameupata usingizi ule wa maana, akilala kwa utulivu bila mifurukuto wala kushtuka hata mara moja. Alikuwa na ule uchovu siyo wa jana au juzi tu, bali wa muda mrefu, na sasa angalau akawa ameutoa kidogo kwa msaada wa bega langu. Na sikuachia kiganja chake yaani.

Nilipenda kumwangalia usoni alipokuwa amesinzia, ile amani aliyonipa nikiiona hapo, na hatimaye baada ya hizo dakika kukata akawa ameamka. Akanitazama usoni kukuta namwangalia tu kwa utulivu, naye akanyanyua kichwa chake na kuegamia siti yake huku akiziba mdomo kupiga mhayo.

"Mambo?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

Akaniangalia usoni na kusema, "Poa."

"Kalikuwa kamechoka!" nikamwambia hivyo kiutani.

Akatabasamu kizembe.

"Pole. Sema tatizo unapenda kujipa mikazi mingi mno," nikamwambia hivyo.

"Nisipofanya kazi, nitakula nini?" akauliza hivyo huku akiangalia mbele.

"Kazi ya pesa sawa. Kuna ulazima gani wa kufanya hadi kazi za nyumbani?"

Akaniangalia usoni tena.

Nikamtazama pia na kusema, "Nimekuangalia sana. Unatoka kazini na joto kali, unafika tena nyumbani unaliongeza. Kwa nini mwili usichoke mno?"

"Asa' unataka nani afanye? Akina mama? Au Mamu?" akaniuliza hivyo.

"Hamna. Ila... umeshafikiria kutafuta msichana wa kazi?"

"Hapana. Hizo biashara sitaki tena."

"Ulikuwaga naye hapo?"

"Karibia watatu. Tena kabla hata Tesha hajaja, na alipokuja tena. Ni wasumbufu sana..." akasema hivyo.

"Najua. Ila ni kama tu hawajachunguzwa vizuri..."

"Ah, huo muda... hapana. Wawili waliondoka wanalalamika eti Mariam anawachosha, mara sijui shangazi yangu ana roho mbaya... Shadya yaani, na wa mara ya mwisho alikaa miezi miwili, halafu akatoroka akiwa ameniibia elfu hamsini..." akasema hivyo.

"Doh! Kweli..." nikasema hivyo huku natikisa kichwa.

"Sipendi makelele. Angalau sasa hivi mambo siyo mengi mno kama wakati Mamu ameanza kuumwa, so hizi kazi ndogo ndogo nakuwa tu nafanya. Napenda sana kufanya kazi, ikiwa ulikuwa hujui hilo," akaniambia hivyo.

"Najua. Sema... usizidishe sana, bado mrembo, mikazi mingi itafanya ukongoroke..." nikamwambia hivyo kiutani.

Akatabasamu na kusema, "Ndiyo nachotaka."

"We! Ikitokea hiyo nakukimbia," nikamtania.

"Ahah... yaani nakongoroka halafu ndiyo nakung'ang'ania sasa. Hadi kwenu..."

"Ahahahah... itapendeza sana ukija kufika kwetu," nikamwambia hivyo kwa hisia.

Akaniangalia usoni kwa utulivu.

"Nataka mama akujue," nikamwambia hivyo.

Akaweka uso makini huku akitabasamu kiasi.

"Ahah... serious," nikamwambia.

"Mhm... bado mapema," akaniambia hivyo.

"We' unataka iwe lini?"

"Tutajuana tu, lakini Jayden! Ahahah... yaani ndiyo tumeanza jamani, unataka kusema utanipeleka nikamwone mama yako kesho, au?" akauliza hivyo.

"Yeah!" nikamwambia hivyo kwa uhakika.

"Mm?" akafanya hivyo kunipinga.

Nikaanza kuchezesha mabega huku nikiimba, "Me nataka kesho... twende nikupeleke nyumbani..."

Akaangalia pembeni na kutabasamu.

"Me nataka, kesho... twende ukamwone mamaa..." nikamwimbia na kukikaza kiganja chake kiasi.

"Tulia kijana wangu. Kila kitu lazima kiende kwa hatua. Taratibu. Siyo unipate jana, kesho utangaze ndoa," akaniambia hivyo.

"Kibaya ni kipi hapo?" nikamuuliza.

"Hakuna kibaya, ila... nataka tuweke mambo yetu... sawa kabisa. Nataka... familia yangu wakujue kwanza, yaani, tayari wanakujua, ila... wakutambue kama mwanaume wangu... halafu ndiyo unipeleke nimwone mama," akaniambia hivyo

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Sawa. Siyo mbaya. Na tunayaweka mambo mengi sawa kwa kudili na hili la Mariam kwanza, uwongo?"

"Eeh, lipite hili... na mengine halafu, tutafanya jambo," akasema hivyo kwa uhakika.

"Mhm... alright. Hao wanaoliangalia huko hilo shamba wanataka nini kwani?" nikamuuliza.

"Kulikuwa kumezuka kama mgogoro, kuna mwenyeji alikuwa anadai sehemu fulani ya shamba letu imeingiliana na lake. Sijui anataka kuliuza? Yaani... anasema kama vile tumeiba sehemu yake..." akanifahamisha.

"Ahaa..."

"Eeeh. Kwa hiyo naenda kusambaratisha hiyo ishu, maana nahisi inaweza ikaja hujuma. Nikienda me mwenyewe kuwathibitishia vipimo vya shamba la Mamu, hawawezi kufanya uchakachuzi, si unajua nikikaa mbali muda mrefu..."

"Eee, hiyo inaweza kutokea," nikamwambia hivyo.

"Yeah. Yaani! Kelele ambazo watu wananipigia kwa sababu tu ya shamba la mdogo wangu, hazikomi. Sijui tu ni kwa nini. Nimemaliza ya Joshua, ikapita. Ikaja ile ya kampuni, waliotaka kunitaifishia hadi nyumba... ukanisaidia ikapita. Sasa hivi tena hii. Yaani hakuna kitu mtu anaweza kufanya akanichanganyia habari kuhusu mali ya mdogo wangu. Naitunza mpaka nihakikishe anakuja kuimiliki yeye mwenyewe," Miryam akaongea hivyo kwa sauti tulivu.

Jambo hilo alilosema likawa limenifanya nikumbuke kitu fulani, nami nikatazama mbele na kushusha pumzi.

Miryam alipoona nimebaki kimya tu, akanyanyua viganja vyetu vilivyoshikana na kuvirudisha mapajani tena, nami nikamwangalia usoni. "Vipi?" akaniuliza hivyo kwa utulivu.

"Safi. Kwani vipi?" nikamuuliza pia.

Akaweka uso wenye udadisi na kusema, "Naona kama mood yako imehama. Kuna kitu unawaza?"

Nikabaki nikimtazama machoni kwa utulivu.

Akaniangalia kwa njia fulani ya uelewa na kusema, "Niambie."

Nikakileta kiganja chake usawa wa kifua changu na kusema, "Kuna kitu nilikuwa bado sijakwambia."

"Mbona serious? Ni kibaya?" akauliza hivyo.

"Siyo kibaya, yaani... ni kuhusu tu kampuni ambayo... yaani, wale watu ambao Joshua alikula lile dili la kuuza kiwanja cha mdogo wako," nikamwambia hivyo.

Akaweka uso wake kiumakini.

"Ni mzee wangu ndiyo alikuwa anakitaka... yaani, yeye ndiyo kichwa cha sehemu ya hiyo kampuni iliyokuwa inadili na hilo suala..." hatimaye nikamwambia.

Miryam akaendelea kuniangalia kwa umakini tu.

"Alikuwa anataka kulinunua shamba la Mamu lakini hakujua kuhusu hizi antics za Joshua... tena, ni dili lililokuwa linasimamiwa na mwakilishi wake," nikamfahamisha.

"Mh! Mbona sielewi?" akaniuliza hivyo.

Nikabaki nikimtazama machoni kwa utulivu.

Akaangalia pembeni kwa ufupi, kisha akaniangalia usoni tena na kusema, "Unamaanisha kwamba... haya yote yaliyotokea juzi juzi yamesababishwa na baba yako wa kufikia... yeye ndiye... alitaka hadi kuuza na nyumba yangu!"

"Miryam, hakuwa anajua kuhusu mambo ya Joshua. Alifanya hilo dili, clean kabisa, kwa hiyo yale yote yalipotokea, akapata hasara... kampuni kwa ujumla... yaani iliporudi hasara lazima kampuni ingehitaji fidia, ndiyo maana. Hayakuwa makosa yake, hata kama asingekuwa mzee wangu, unajua hilo..." nikamwambia hivyo kwa upole.

"Kwa hiyo kumbe ndiyo maana ukatoa ile milioni kumi?" akaniuliza.

Nikabaki kimya tu, nikiendelea kumtazama usoni kwa utulivu.

"Ahah... yaani kutokea mwanzo kumbe ulikuwa.... kwa nini hukuniambia?"

"Haingekuwa na utofauti wowote. Na nilikusaidia siyo kwa sababu tu nilijua hayo, nilikusaidia kwa sababu nilitaka kufanya hivyo. Hayo sasa hivi yameshaisha, nimeona nikwambie tu ukweli kukuelewesha..." nikamsemesha kiupole.

"Mhm... ukweli wa kwamba wewe ni mtoto wa tajiri ambaye utatoa tu milioni kumi na kuzigawa bila kuwaza, kwa kuwa daddy haishiwi eh?" akaongea kikejeli.

"Miryam..." nikamwita hivyo kiupole.

"I'm sorry... nimeshangaa tu. Sikutarajia," akasema hivyo huku akiangalia pembeni kwa huzuni kiasi.

Nikakiweka kiganja chake usawa wa shingo yangu na kusema, "I'm sorry too. Sikukwambia mapema maana mambo yalikuwa mengi, na me mwenyewe nikakuchanganya kwa vingi. Ila nimekuchanganya vizuri mpaka sasa hivi tuko hapa, uwongo?"

Akatabasamu kiasi na kuniangalia.

"Naomba tuyaweke tu hayo pembeni. Sasa hivi tupo kwenye chapter nyingine kabisa..." nikasema hivyo.

Akatikisa kichwa kuonyesha uelewa, naye akasema, "Sawa. Nashukuru kuniambia. Mhm... ndiyo tunaanza kujuana sasa."

"Ahah... ni kweli," nikasema hivyo huku nikitabasamu.

Akatulia kidogo, kisha akauliza, "Kwa hiyo... kwanza, mzee wako anaitwa nani?"

"Frank. Frank Manyanza," nikamjibu.

"Mmm... na ndiyo mwenye hiyo kampuni iliyokuwa interested kununua kiwanja cha Mamu?"

"Siyo kwamba ni yake kabisa, hiyo ni... yaani anahusika nayo kama president, wa hii kampuni, kwa huku Tanzania... yaani ni ya watu wa huko New Zealand, na wameijenga na huku, kwa hiyo..."

"Yeye ndiyo CEO," akasema hivyo.

"Yeah. Wako na level zao."

"Inahusiana na nini?" akauliza.

"Haya masuala ya letting..." nikamwambia.

"Ahaa..."

"Yeah. Ngoja nikuonyeshe. Hilo jengo lipo huko Makumbusho, zuri.... hili hapa..." nikawa nimemwonyesha picha ya jengo hilo kwenye simu yangu.

"Sky Tower. Ni pazuri," akasema hivyo baada ya kusoma hapo kwenye picha.

"Mmm... teranova. Wanatoa space za kufanyia biashara, kupangisha nyumba au vyumba, kumbi za mikutano ama sherehe, za gharama yaani, na.... inahusika na mambo mengi sana, na yeye kwa upande wake huku ndo' anaibeba sasa. Wamepanuka zaidi, ndiyo maana wanataka kusambaza upendo wao kwa mikoa mingine. Nadhani Mwanza, Dodoma, na Arusha labda tayari... ndiyo sababu walitaka na kiwanja cha Mamu ili wajengee mradi wao na huko Moro..." nikamwelezea.

"Okay. That's big..." akasema hivyo.

"Yeah... ana hela huyo! Huwa halali. Nikupe namba zake?" nikamwambia hivyo kiutani.

Miryam akacheka kidogo kwa pumzi na kutikisa kichwa.

"Ahahah... sema nikutoe. Anaweza akakununulia hadi hela huyo. Au hupendi hela?" nikamtania zaidi.

Akasema, "Hebu acha mambo yako bwana. Niambie. Ulisemaga alimuoa mama yako wakati uko form four, si ndiyo?"

"A-ah... yaani... wameanza mahusiano me niko form four, amekuja kumwoa niko form six..." nikamwambia.

"Ahaa... basi nilidhani ulimaanisha amemuoa kipindi uko form four..."

"Hamna..."

"Wanapendana eh? Ndiyo maana anawapenda sana na nyie..."

"Ndiyo, ahah... mzee ameanza kutupenda me na Jasmine kabla hata hajamjua mama. Jasmine ndiyo aliwakutanisha..."

"Ooh... kumbe aliwajua nyie kwanza?"

"Mmm. Kwa mtu wa aina yake, siyo rahisi sana kumpata na kumjua, hana ile socializing ya kawaida. Siyo kwamba anabagua watu lakini, ila kazi zake ndiyo zinamfanya anakuwa... muda mwingi juu zaidi yaani..."

"Kwa hiyo nyie aliwajuaje mpaka akakutana na mama yenu?"

"Kupitia binti yake. Ana mtoto wa kike, mdogo wetu sasa hivi yaani, anaiwa Nuru... niliokoa maisha yake, ndiyo mpaka nikaja kukutana na baba yake..." nikamwambia hivyo.

"Alifanyaje?" akauliza.

"Ah, yaani! Tulikuwa kwenye party fulani kule Malaika, Mwanza... mambo ya vijana na nini si unajua, na Nuru akawepo hapo hiyo siku. Alikuwa mdogo, lakini mambo yake!"

"Ya kikubwa?"

"Aah... alikuwa amepelekwa hapo na jamaa fulani hivi, kwa wakati huo huyo jamaa kama Tesha, ila mambo yake yalikuwa siyo. Nuru alikuwa kwenye miaka kumi na nne, lakini alikuwa ananyweshwa pombe..."

"Wewe..."

"Si na ule ushua na nini, Nuru alikuwa changanyikeni sana, afu' kalikuwa na kiburi enzi hizo! Ila alikuwa na umbo kubwa kubwa, kwa hiyo hata akidanganya ana miaka kumi na nane, watu wanakubali. Sa' kukawa kumetokea ugomvi, huyo jamaa yake kapigana na mtu wakapasuliana chupa, Nuru akachanwa shingoni... pembeni hapa. Sisi tumekuja kusikia commotion hao jamaa wamekimbia, kufika hapo Nuru kalala chini, damu inaruka, anahangaika, halafu sasa... waliokuwepo wakawa wanamwangalia tu... ile ya kipindi kile kwamba hatupaswi kumgusa mpaka watu maalumu waje..." nikamsimulia.

"Ukafanyaje sasa?"

"Ah... unacheza na mimi? Genius," nikamwambia hivyo huku nikimwonyesha ishara kuwa na akili.

"Ahah... niambie sasa..."

"Niliona alikuwa anapata shida kupumua, kwa hiyo nikajaribu kitu ambacho... yaani sikuwa hata na uhakika kama kingefanya kazi. Si nilikuwa nasoma sana, nilijua kuna kitu fulani wanaita cricothyrotomy... neno gumu eh?"

Akatikisa kichwa kukubali.

"Eeh, yaani makeshift, kumfanya mtu kwenye hiyo instance kama mshipa wake umepasuka, trachea ama nini... unatumia bomba dogo kuweka kwenye hilo jeraha, ili aanze kupumulia hapo. Ah, yaani Miryam! Sijui nilikuwaje. Yaani eti nikafanya hivyo. Nikapata kibomba cha... kwanza nilikuwa nafikiri labda mrija wa soda ungeweza kufanya kazi, ahahah... lakini nikatafuta bomba la peni kabisa na kufanya hivyo. Nikamwekea hapo alipokuwa amechanika... yaani nikaingiza ndani, aisee! Nikikumbuka..." nikaongea kwa hisia.

Miryam alikuwa ametulia tu, akiniangalia kwa macho yenye umakini.

"Ndiyo wakaja kumchukua sasa, baadaye... wakampeleka hospitali. Nilikuwa hata sijui kama ingefanikiwa... ila ni Mungu tu. Halafu... baadaye nikagundua kwamba hiyo ishu ni hatari. Ilikuwa bahati ilimwokoa, kama ningemwekea vibaya, me ndiyo ningemuua," nikamwambia hivyo.

Miryam akatikisa kichwa kiasi kwa njia ya kusikitika.

"Haikuwa poa. Ndiyo taarifa zikamfikia baba yake sasa, alikuwa huku wakati huo, na me jina langu likafikishwa kwake. Tulikuja kwenda hospitali na Jasmine kumwona Nuru, yaani... baba yake alitutafuta ndiyo tukapelekwa. Kuanzia hapo ndiyo akaanza kutu-favor mpaka akaja kukutana na mama... imekuwa historia nzuri now," nikamwambia hivyo huku nikiangalia mbele tu.

Nikamtazama hatimaye na kukuta amekaza macho yake mazuri kwangu, kwa njia fulani kama vile anataka kuachia tabasamu.

Nikamuuliza kwa sauti ya chini, "Nini?"

Akatabasamu hatimaye na kusema, "Hamna kitu. Napenda tu kukusikiliza ukiongea."

Nikatabasamu kwa hisia na kumwambia, "Well... nafurahi kujua hilo."

"Inaonekana una mambo mengi sana kwenye maisha yako ambayo nitahitaji kujua... kwa hiyo nitakuwa tayari zaidi kukusikiliza. Ninataka uje uniambie... kila kitu kuhusu wewe," akaniambia hivyo kwa sauti yenye hisia.

Nikatikisa kichwa kukubaliana na hilo, naye akalaza chake begani kwangu tena na kunishikilia kwa njia iliyoonyesha amani.

Kauli yake hapo mwishoni ilikuwa imenifanya niwaze kuhusiana na jambo lingine muhimu zaidi nililopaswa kuja kumwelezea. Juu ya ishu ya mwanangu. Sikuona kwamba lingekuwa gumu mno kwake kumeza, lakini najua nilipaswa kulileta mapema kabisa. Ukitegemea na jinsi ambavyo mambo yalikuwa kwa upande wangu na huyo mtoto ambaye hata sikuwa nimekutana naye bado, mwanamke wangu angetakiwa kuelewa hilo suala kwanza ili nipate wepesi zaidi katika hatua zangu za kushughulika nalo ilivyotakiwa.

★★

Safari ya mwendo wa kasi ikatufikisha Morogoro hatimaye ikiwa imeingia mida ya saa tano asubuhi, nami pamoja na bibie wangu tukatafuta mghahawa mzuri ili kupata chakula kwanza. Jua lilikuwa linawaka kweli kuelekea mida ya saa sita, nasi tulipomaliza kula ndiyo tukachukua taxi ambayo ingetupeleka kule ambako Miryam alidhamiria kwenda. Alikuwa ameshawasiliana na familia yake, hususani Bi Zawadi ambaye alimpigia kujua ikiwa ameshafika. Aliwaacha vizuri huko nyumbani, hata kama ingetokea amechelewa kurejea Dar angekutana nao ukumbini kwenye send-off ya Doris.

Kwa hiyo wapendanao tukapelekwa mpaka kwenye eneo lililojulikana kama Mizani, ikiwa ni barabara iliyoelekea Dodoma, nasi tukaingia ndani ndani zaidi kwenye hizo pande zilizokuwa na maeneo yenye mashamba na viwanja na mapori-pori pia. Niliona kwamba sehemu hizi za huu mkoa zilikuwa zinaendesha ujenzi wa miundombinu mbalimbali, yaani ile iliyokuwa inakuja kwa kasi, kwa sababu viwanja vilikuwa vingi na ni sehemu ambayo ingependeza mno kama hizi harakati zisingekoma.

Tukafika sehemu fulani iliyokuwa na shamba kubwa kweli, likiwa limepandwa mazao ya mbogamboga, mahindi, na viazi nadhani, yaani kwa ile njia isiyo ya kipaumbele sana ingawa yalikuwa mengi. Hili ndiyo lilikuwa shamba la Mariam, na hapo walikuwepo watu kadhaa waliokuwa wakisubiri kwenye kibanda kidogo sehemu za mbele huko, nasi tukaanza kukielekea huku na hao watu wakija kukutana nasi. Walikuwa watano, watatu wakiwa wanawake na wawili wanaume, wote watu wazima, na tulipokaribiana maongezi yakaanza kwa salamu.

Miryam alizungumza nao kwa ustaarabu sana, akitaka kujua yaliyokuwa yanaendelea kufikia sasa. Mwanaume mmoja hapo ndiyo alikuwa akidai kwamba sehemu fulani ya kiwanja chake imeingiliwa, yaani kilipakana na shamba la Mariam, na hawa waliolitunza walikuwa wamepanda mazao mpaka kukiingilia kiwanja chake na kudai sehemu hiyo yote ni yao; yaani kwa niaba ya mmiliki. Alikuwa anataka kukiuza kiwanja chake, na hakutaka iwe mgogoro mkubwa sana kuingiliana na nini, ndiyo sababu alitaka uhakikisho kutoka kwa mmiliki halisi wa hili eneo lingine ili wasije kulaumiana baadaye mengine yakitokea na kusababisha mvurugo.

Ikabidi hadi tupelekwe usawa wa hilo eneo ili tuonyeshwe jambo hilo, naye Miryam ndiyo akaanza kubainisha sasa mambo hakika ya eneo lililokuwa la mdogo wake, karatasi za vipimo na nini, na ikaeleweka kwamba huyo jamaa hakuwa ameibiwa chochote. Alikuwa mbishi haswa, huyo jamaa, yaani hata baada ya kuonyeshwa vipimo na nini akawa anapaisha sauti tu hasa kwa sababu Miryam alitumia heshima kuongea naye akiwa kama mtu mzima. Ikanibidi niingilie kati.

Nikamwambia huyo mzee kwamba ikiwa hakuridhika na uthibitisho aliopewa na Miryam, basi afungue kesi. Tungekuwa tayari kupambana nayo, maana hatukutaka mgogoro wowote wa ardhi na kuanza kukatana mapanga, eti aje tu akate ardhi isiyo yake aiunganishe kwenye ya kwake halafu amuuzie mtu mwingine? Hapana. Kama hakutaka kuamini uthibitisho wa wazi alioletewa na Miryam, basi tungelipeleka hili suala mahakamani, na hapo angekuwa anajisumbua tu maana angrlepoteza wakati, pesa, na labda hata nafasi ya kuuza kiwanja chake.

Miryam pia alikuwa ameshaona kwamba huyo shida yake ilikuwa kuongeza tu upana wa eneo lake ili aliuze kwa gharama ya juu zaidi kwa mnunuzi, kwa hiyo akamwambia aache tamaa, hivi vitu vingekuja kumgharimu maana kama angekuwa mwingine hapo asingekuja kistaarabu. Ni yeye Miryam ndiye aliyekuwa karibu kuibiwa hapo, yaani hilo alilijua, kwa hiyo akamwomba huyo baba aachane na hii kitu kabisa, maana sheria zilikuwepo na alijua haki yake. Ndiyo jamaa akawa mpole.

Maongezi yaliyofuata baada ya hapo yakawa yenye amani kiasi, ikieleweka kwamba hilo eneo jamaa alilosema ni lake lilikuwa ni sehemu ya shamba la Mariam kihalali, kwa hiyo hadithi ikawa imeishia hapo. Ilikuwa ni kusumbuana tu, yaani Miryam kuja huku kote ilikuwa kwa sababu tu waliolitunza eneo la mdogo wake hawakujua kukoromea waliowapandishia sauti, kwa hiyo ilikuwa lazima bibie aje mwenyewe kweli kuweka mambo sawa. Tumekaa hapo mpaka saa nane, ndiyo tukawaacha sasa, na Miryam akiwa amewapatia watunzaji kiasi fulani cha pesa sijui kwa ajili ya nini.

Basi, mission ikawa accomplished, moja kwa moja jambo ambalo lingefuata ingekuwa kurudi kwenye kituo cha stesheni ya treni ili kuwahi kurudi Dar. Kama muda ungekuwa unaruhusu, tungefanya matembezi kidogo, lakini kweli tulihitaji kuwahi huko. Miryam hata hakuwa amejiandaa, katika maana ya kwamba labda aende saluni, ahusike kwa ukaribu na ishu za upendezeshaji wa Doris, yeye mwenyewe kuvaa, yaani alikuwa na rundo la mambo mengi aliyohisi angekosa kutimiza hasa kwa kuwa alihusika kama mwanakamati maalumu kwenye hiyo sherehe, kwa hiyo kujaribu kuwahi lilikuwa suala muhimu sana.

★★

Tukafanikiwa kupata treni ya saa kumi jioni, upesi sana ikatukimbiza kuturudisha Dar na hatimaye kutufikisha huko ikiwa imeshaingia saa kumi na mbili jioni. Miryam alikuwa amewasiliana na Doris kumjulisha kuhusiana na hii hitilafu, kwa hiyo huko wote walielewa kwa nini alikosekana hapa na pale lakini la msingi lilikuwa kwamba angefika tu ukumbini. Yaani hakutaka hata kula tena, akili yote ilikuwa kufika kwenye send-off ya ndugu yake ili kutoa 'support' kwa mwenzake. Nilipenda sana huu utu wake wa kujitahidi mno sikuzote kutanguliza maslahi ya wengine; Mariam kwanza kutokea leo asubuhi, na sasa ingekuwa ni Doris.

Muda ulikuwa unaenda shuta, yaani alikuwa anafikiria kurudi nyumbani, avae vizuri, ndiyo tena tuelekee Kigamboni kwenye ukumbi wa hiyo sherehe haraka, lakini nikamtuliza na kumpa wazo lingine. Nikamwambia twende kwenye moja ya maduka makubwa ya nguo na mitindo pande hizo hizo ili aweze kutengeneza mwonekano wake vizuri kwa ajili ya sherehe, halafu tungeenda huko moja kwa moja. Nikamwambia hata mimi nilikuwa naenda kwenye send-off kama yeye tu, na nilijua tukifanya mizunguko mingi mpaka kurudi nyumbani, tungechelewa, kwa hiyo nikamwomba akubali hilo ili tuokoe muda.

Aliona hilo kuwa wazo zuri, na hata akatania kwa kusema sawa, twende, kwa sababu ya mimi kuwa mtoto wa kishua basi anajua ningegharamikia kila kitu bila kumwaga jasho. Nilifurahi kuwa kwa mara ya kwanza aliridhia mimi kufanya jambo fulani kwa ajili yake bila yeye kuweka migomo kama nilivyokuwa nimemzoea, nasi tukafanya kuelekea kwenye duka moja zuri sana la nguo na mitindo ili tujiweke fresh kabla ya kuelekea sendofuni.

Nikalipia nguo mpya kwa ajili yangu na yeye, yaani yoyote ile ambayo na yeye angechagua, na nikawa nimewaomba wavalishaji wa hapo wamwekee mrembo wangu vito vizuri pia. Mimi nikavaa moja ya yale mashati ya uturuki, la kijivu na lenye mtindo mzuri sana, pamoja suruali nyeusi ya jeans laini pia, na nikanunua na viatu vyeusi (formal) vyenye gharama na kuvitupia, yaani mwonekano rasmi, ungeniona! Nilitokelezea.

Miryam sasa, ndiyo aliniacha kinywa wazi. Alichagua gauni lenye kubana na laini, lenye rangi ya maroon-zambarau na mapambo ya vitu vyenye kuling'arisha, likifunika mkono wake mmoja na mwingine kuuacha wazi. Lilikuwa na mpasuo mrefu mpaka mwanzo wa paja lakini alijitahidi kuusitiri vizuri, na alikuwa amesaidiwa kutengenezewa nywele zake kwa kuzibana nyuma na kuachia mkia wa zilizobaki ulale mbele ya bega lake. Alivalishwa hereni ndefu pia, bangili, na pete nzuri za urembo, huku miguuni akikanyagia viatu vifupi vya kuchuchumia vyenye rangi ya kung'aa ya shaba.

Alitoka na kunifata akiwa ananitazama kwa njia ya subira, ili nimwambie nilichofikiria, nami nikaachia tabasamu hafifu huku nikimtazama kwa hisia sana, halafu nikamtikisia kichwa kuonyesha nimeuelewa mtindo wake. Alipendeza! Ilikuwa kama vile yeye ndiyo alikuwa anaenda kuolewa. Watu wa hapo walituangalia kwa yale macho ya kuinua, yaani tulionwa kuwa kama wateja maalumu sana wakati ndiyo ilikuwa mara ya kwanza kufika.

Na gharama ya kila kitu ilikuwa ya juu mno mpaka nikatoa kadi yangu ya benki kulipia, na ilifaa maana kuanzia wakati huu, nilikuwa nataka kumwonyesha mwanamke wangu hadhi yake. Ningempa chochote kile yaani ambacho kilimfaa kwa macho yangu, hapa ilikuwa kidogo. Miryam akanishukuru eti kwa kumfanyia kitu kizuri kama hiki, nami nikamwambia asiwaze, ulikuwa ndiyo mwanzo.

Kwa hiyo tulipomaliza kupendezeshwa hapo na kulipia, tukatoka kwa pamoja ikiwa imeshaingia saa moja kuelekea mbili. Tulipendeza, yaani sana! Nguo zetu tulizokuja nazo mwanzoni nilikuwa nimeweka kwenye mfuko kutokea hapo dukani, nami nikakodi usafiri wa Uber utuwahishe huko Kigamboni upesi. Miryam alifahamu kihususa mahali ambapo ukumbi ulikuwepo, maana ilikuwa ndiyo ile ile sehemu waliyofanyia kitchen party ya Doris juzi, hivyo safari ikaanza upesi.

★★

Tumekuja kufika eneo husika la huo ukumbi ikiwa inaenda kuingia saa tatu usiku, yaani send-off ilikuwa imeshaanza. Miryam alikuwa ametafutwa sana na mama zake, Shadya, Tesha, na hata mama yake Doris mwenyewe kuuliza kwa nini alikawia mno, na jibu la haraka ilikuwa ni matatizo ya usafiri. Walimhitaji sana awepo, yeye ndiyo alikuwa kama roho yao pale. Mimi nilikuwa nimeshawasiliana na Ankia, ambaye alisema ametunza sehemu yangu ya kukaa pamoja naye.

Baada ya kushuka sasa, nikamwambia Miryam atangulie huko ndani, maana kwa wakati huu tusingeweza kuingia kwa pamoja ingawa nilitamani sana tufanye hivyo, lakini Miryam akasema hapana, twende pamoja. Nilishangaa kiasi aliposema hivyo, lakini akaniambia haikuwa na shida tukiingia pamoja, ingeonekana tu kwamba tumekutana hapo hapo, siyo lazima ndugu zake wangefikiri tulikuwa pamoja siku nzima. Kwa kuwa aliona hilo kuwa sawa, tukaelekea ndani ya hoteli pamoja.

Ilikuwa ni hoteli kubwa kiasi, magari kadhaa yenye mapambo yakiwa kwa hapo nje, na mziki mnene ukisikika kutokea huko ndani, tukaelekea mpaka malangoni na kukutana na wasimamizi. Walifahamiana na Miryam, hata wakasalimiana vizuri na kumuuliza kulikoni mpaka kuchelewa huko kote. Akaongea nao kifupi tu, na mimi nikiwa nimetulia nikawaonyesha mwaliko wangu, halafu bibie akamwomba mmoja wao achukue mfuko uliokuwa na nguo zetu atutunzie sehemu fulani mpaka baadaye. Ikawa hivyo, na baada ya hapo ndiyo tukaingia sasa.

Ukumbi ulikuwa mzuri, sana, watu wengi wakipendeza na kukaa kwa utulivu MC alipokuwa akiendelea kuweka mambo, nami nikawa nimewaona ndugu zake Miryam kule mbele, wakikaa kwenye meza ndefu na wakiwa wamependeza sana. Miryam pia alikuwa ameshawaona, nasi tukawa tunatembea kwa pamoja tukivuka meza nyingi za watu waliotutazama kwa umakini sana. Miryam angemfikia mtu fulani aliyemfahamu na kusalimiana au kukumbatiana naye, na mimi ningemsubiria tu. Najua kwa baadhi ya watu ingezua swali la ni kwa nini, lakini sikujali. Tuliangaliwa, siyo poa!

Wakati tukiwa tunaelekea mbele zaidi, nikawa nimemwona Ankia, meza moja akiketi na Bobo, mama Chande, Shadya, na watu wengine, nami ndiyo nikamwambia Miryam naelekea hapo. Hakuwa na neno, na familia yake ilikuwa imeshaniona pia, kwa hiyo nikawapungia mkono kwa chini na kutoa ishara kwamba naenda upande mwingine. Ile nimeanza tu kwenda upande wa Ankia, nikamwona Mariam anasimama kutoka kwenye meza ya familia yao na kukutana na Miryam kabla hajawafikia, halafu akasemeshana naye kwa ukaribu huku watu wakiwaangalia.

Mimi nikasonga tu mpaka kwa Ankia, nikapokelewa vizuri hapo, nakwambia hadi Bobo alikuwa amevaa kijentomani mpaka tukachekana kidogo, kisha ndiyo nikaambiwa niagize vinywaji; wahudumu walikuwa wamesimama kila kona. Wakati nataka kufanya hivyo, nikamwona Mariam anakuja upande wetu mpaka akatufikia, halafu akachuchumaa karibu nami na kunishika mapajani kwa mikono yote, asiseme kitu, bali akawa ananiangalia tu.

Nikamwinamia sikioni na kumwambia, "Umependeza Mamu!"

"Asante," akasema hivyo.

"Umekuja kunisalimia?" nikamuuliza.

"A-aah... nimekuja kukuita uje. Njoo ukae na sisi," akaniambia hivyo.

Nikatabasamu kiasi na kusema, "Nafasi yangu ilikuwa huku... huko wanakaa familia. Wakina nyie tu."

"Me nataka uje ukae na sisi, kuna nafasi yako. Ma' mkubwa amesema uje ukae na sisi," akaniambia hivyo.

Nikakaa kisawasawa na kuwaangalia watu wa familia yake kule mbele, nami nikamwona Bi Zawadi akitoa ishara kuwa niende huko. Miryam tayari alikuwa ameshakaa.

Nikamwambia Ankia sikioni, "Nimeitwa kukaa nao hawa, kwa hiyo nawakimbia."

Ankia, akiwa ameshaanza kunywa, akaniambia sikioni pia, "Naona unaelekea kuwa mwanafamilia original."

Nikatabasamu tu na kunyanyuka, na Mariam akanyanyuka pia.

Nikamshika binti mkono na kuanza kwenda huko kwa ndugu zake, yaani tulishikana viganja, na alikuwa akitembea taratibu tu kwa kufuata mwongozo wangu. Najua tulikuwa tukiangaliwa mno, kwa sababu kwa wasiotujua, ilionekana kama vile ukaribu wangu na Mariam ulikuwa wa hali ya juu zaidi, zaidi ya jinsi ambavyo nilimchukulia binti. Mawazo ya namna hiyo najua yalikuwa rahisi sana kuingia kwenye akili za watu, iwe ni nani au nani ambaye ningetembea naye huku nimemshika namna hiyo, hayo mawazo yalikuwepo. Hasa kwa wanawake, walioniona kuwa sukari ya warembo!

Tukafika mezani kwao, hapo akiwepo Bi Jamila, Bi Zawadi, Tesha, mama yake Doris, Dina, wanaume wengine wawili watu wazima, nafikiri mzazi au walezi wa Doris, watoto wadogo watatu, wanawake vijana wawili waliokuwa mapacha, pamoja na Miryam. Mariam akanionyeshea viti ambavyo kilikuwa wazi pembeni yake Miryam, nasi tukaelekea hapo baada ya mi' kushikana mikono na mama wakubwa na kutoa salamu za ishara kwa wengine. Nikakaa katikati ya Miryam na Mariam, huku Tesha akiwa kwa mbele zaidi, nasi tukatoleana ishara za kishkaji na kuanza kuchat bila kuchelewa.

Tesha alikuwa anataka nimwone Happy wake, ambaye alikuwepo hapo ukumbini pia, lakini alikaa sehemu zingine huko nyuma-kati. Bwana, nikafuafa mwongozo wake mpaka nikamwona, na alikuwa mwanamke mzuri, mweupe. Tesha alikuwa anatamani sana kwenda kukaa naye, lakini hapa hakuwa na jinsi. Huyo Happy alipendeza pia, na nilitambua kwamba alimzidi Tesha umri kiasi, kwa hiyo nikamtania kwamba mimi na yeye tulikuwa ligi moja. Sikuwa nimemweka wazi Tesha kwamba tayari nilianzisha uhusiano pamoja na dada yake, kwa hiyo alifikiri mpaka sasa bado namfatilia tu Miryam.

Mariam alipenda sana hivyo mimi kukaa nao, akawa ananisemesha mara kwa mara na mimi kumjibu kirafiki, na nikaona kwamba ndugu zake na Doris waliniangalia mara nyingi sana, upendezi wa mwanzo au husuda yaani, sikujua. Sherehe ikiwa inatembea kwa mbwembwe na nini, mimi nilijiweka kwa njia tulivu tu, lakini kila mara niliposhusha mikono yangu kwa chini, sikuwa natulia. Nilianza kumchokoza Miryam kwa kumbonyeza mguuni kidogo, na mara ya kwanza aliniangalia kama kuona ikiwa nilihitaji kitu fulani, lakini sikumtazama na kuendelea kumbonyeza tu bila kuweka hisia yoyote usoni.

Akawa anakitoa kiganja changu kwake, chini-chini, lakini mimi nikaendelea kumchokoza hivyo hivyo. Mwanzoni alionekana kutopendezwa na hilo, lakini nilipoendelea tu, nikawa naona akijitahidi kuzuia tabasamu lake, nasi tukawa tunafanya kama kuipiganisha mikono yetu chini kwa chini, na mchezo ukaendelea hivyo bila wengine kutambua hadi Doris alipomtafuta bwana harusi na kumpata mpaka ulipofika wasaa wa kukata keki. Shamrashamra na nini, wakaanza kuitana, na hapo nilikuwa nimepiga kinywaji kidogo kisicho cha ulevi, hivyo nikahisi haja ndogo.

Sehemu hiyo ya kula keki ikamalizika baada ya wanafamilia wote wa bwana harusi na Doris kwenda na kulishwa keki, na mimi nikalishwa pia eti kama sehemu muhimu ya hii familia. Doris alikuwa mshkaji sana. Baada tu ya kutoka kula keki, ndiyo nikaamua sasa nielekee kutafuta vyoo ili nishushe haja maana mkojo ulikuwa umekaza kweli. Nikafanikiwa kukipata choo na kutuliza hali, vyoo vikiwa upande ghorofa la juu kutokea ukumbini, na ile nimetoka tu ili nirejee huko, nikawa nimekutana na mwanamke hapo ambaye alisimama kwa kuegamia ukuta wa korido lililotenganisha sehemu iliyoelekea kwenye vyoo vya wanaume na wanawake.

Alikuwa mtu mzima, mwenye mwili mnono haswa. Nilimwangalia vibaya mwanzoni na kutaka kumpita, lakini nilipoona akinitazama moja kwa moja tu kwa umakini ndiyo nikasimama na kugundua kuwa nilimfahamu. Huyu mwanamke ndiye yule niliyekutana naye kule Masai wiki kadhaa nyuma, ambaye alinielewa sana mpaka tukaja kukutana na kutoka kimapenzi kwa siku moja tu, yaani Rukia. Yule mshangazi! Ulikuwa umepita muda sijamwona, na tuliacha kuwasiliana maana nilimpiga chini kwa kutojibu yoyote kati ya jumbe alizojaribu kunitumia baada ya ile siku niliyomtandika hotelini.

Sikuwa nimetarajia kabisa kumwona tena, hasa sehemu hii, ila kwa jinsi alivyokuwa amesimama hapo, ni kama alikuwa akinisubiria. Watu wengine walionekana wakipita huko mbele mbele na wadada kwenda vyooni. Nikaamua kupiga hatua chache na kufika karibu yake huyu mwanamke, naye akatabasamu kiasi na kuniangalia kwa njia yenye upendezi.

"Mambo?" akaniambia hivyo, na sauti yake tulivu ya kimama.

"Fresh, vipi?" nikamwambia hivyo, nikiwa makini.

"Safi. Umependeza..."

"Na wewe pia."

"Asante. Mbona huonekani siku hizi?"

"Nipo. Na wewe?"

"Mhm... na me nipo. Nimekuona wakati unaingia, ulikuwa na yule dada mzuri wa pale mtaani. Ndiyo nyama yako sasa hivi?" akauliza hivyo.

Nikavuta pumzi na kuishusha taratibu, nami nikamwambia, "Ona dada, najua kuna sehemu nimeshatembea na wewe, na...."

Kabla sijamaliza kuongea, akatupita mwanaume mwingine hapo akiwa anaelekea huku chooni.

Nikamwambia Rukia, "Hii siyo sehemu nzuri, tutaongea siku nyingine."

Nikataka kumpita, lakini akasimama mbele yangu na kuuliza, "Lini?"

Nikabaki nikimtazama usoni kwa utulivu. Alionekana kama amechangamshwa na pombe kwa mbali.

"Nimekutafuta mara ngapi hujanijibu? Tokea siku ile ukaniahidi utakuja kuni...."

"Nisikie. Hayo yameshapita, sawa? Ile ishu...." nikasema hivyo na kutoa ishara kwa kiganja kuwa hiyo ishu nimeichinja.

"Basi kumbe we' ni escort tu," akasema hivyo.

"Nini?"

"Hiyo siku ulisema we' siyo kaka poa, nikakuchukulia serious. Kumbe ulikuwa unadanganya. Unatoka tu na wanawake wenye pesa, halafu unahama ukimaliza..." akasema hivyo.

"Hivi wewe... me nilikufata? Si ulikuja kwangu mwenyewe? Nilikuomba hela kwani?" nikamuuliza hivyo.

"Lakini nilipokupa si uliichukua?"

"Oh, kwa hiyo kumbe unataka tu nikurudishie hela zako?"

"Siyo hivyo..."

"Nikumbushe ulinipa shi'ngapi nikupe," nikamwambia hivyo.

"Sitaki unipe hela... hela ninayo."

"Unataka nini sasa?"

"Nakutaka wewe," akasema hivyo.

"Eh, aheh... dada... sahau. Unanielewa? Nikikwambia imeisha, imeisha. Kuna wanaume wengi humo, katafute yeyote akutulize kama unaona mmeo hakupi satisfaction. Mimi siko available tena," nikamwambia.

"Mmm?" akafanya hivyo kikejeli.

"Eeh. Na kama msemo wa Rose Muhando, 'nipishe nipite,'" nikamwambia hivyo.

"Ngojaaa..." akasema hivyo na kunizibia njia tena.

Yule jamaa aliyekuwa ameenda chooni akapita tena, akituangalia mara mbili mbili.

Nikamwambia Rukia, "Sitaki scene dada'angu. Naomba uelewe hilo."

Akatabasamu na kusema, "Scene kama ile uliyomwonyesha Naomi siku ile Masai?"

Nikaweka uso makini.

"Mdogo wangu aliniambia ulimkataa, ukampasulia na chupa. Alikuwa hajui kama nimeshapita na wewe..." akaniambia hivyo.

"Nisikie. Sitaki niwe mkali. Kuna amount ndogo ya heshima niliyonayo kwako dada, sitaki iishe kwa sababu nikiwa mkali nakuwa mbaya. Naomba uelewe kwamba sita...."

Kabla sijamaliza kuongea, Rukia akaweka mkono wake sehemu ya kati kwenye suruali yangu na kuishika mashine yangu ikiwa kwa ndani, halafu akaikamata kwa nguvu pamoja na mipira ya uzazi na kuviminya kwa njia iliyofanya niumie kiasi!

Nilishtuka, na yeye moja kwa moja akanifata mdomoni huku akinisukuma kuuelekea ukuta. Akanibamiza hapo huku akilazimisha denda na mdomo wake ulionuka pombe, yaani eti akitaka kunipa penzi la kibabe, nami nikautoa mkono wake kwa nguvu hapa chini na kuigeuzia nguvu ya limwili lake igeukie ukutani, hivyo nikawa nimemwepuka na kusogea pembeni.

Nikawa nataka nianze kwa kumnyooshea kidole na kumwambia asije kamwe kurudia kunisogelea tena, lakini pale nimeangalia pembeni tu, hapo mbele niliweza kumwona Miryam akiwa amesimama usawa wa njia iliyoelekea kwenye vyoo vya wanawake, akinitazama kwa macho makini sana. Nilichoka!

Nikamwangalia bibie usoni kwa macho yenye wasiwasi, yeye akiwa ananiangalia mimi na Rukia kwa njia iliyoonekana kuwa ya umakini wa kawaida tu, nami nikajifuta mdomo na kuanza kupiga hatua kumfata huko, lakini Miryam akageuka hapo hapo na kuelekea ndani ya vyoo vya wanawake moja kwa moja. Aisss! Hii ingekuwa mbaya, aisee, CV yangu ilikuwa imechafuliwa ghafla sana. Yaani hapo sijui ingekuwaje!







★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
 
MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★


Rukia akaja mpaka karibu nami na kunishika mgongoni, naye akasema, "Acha kudengua bwana... I know you want it."

Nikaingiwa na hasira kali na kuushika mkono wake kwa nguvu, halafu nikamgeukia huku nikiupindishia pembeni. Akatoa sauti ya maumivu na kuinamia upande mmoja, ndiyo nikamwachia huku nikimsukuma kidogo.

"Iwe mwanzo na mwisho! Usije kunisogelea tena. Ukiniona, pita huko. Sitaki mazoea, umenisikia?" nikamwambia hivyo kiukali.

Akawa ananitazama kwa njia yenye hasira pia.

Wakaja wanaume wengine watu wazima hapo na kukuta hali haiko poa, na mmoja wao akauliza tatizo lilikuwa nini. Nikiwa namtazama Rukia kwa hisia kali, nikavuta ulimi kwa nguvu na kuondoka tu hapo, nikiwa nawaza mengi kweli. Tendo dogo la kipuuzi alilofanya huyo mwanamke lingeweza kunigharimu vikubwa, yaani sijui Miryam angenifikiriaje. Dah, yaani madhambi yangu ya nyuma yalikuwa yameanza kunirudia kwenye wakati ambao nilitaka yasahaulike kabisa, na matokeo ni kwamba yangeweza kuniharibia maisha mazuri ya mbele niliyotaka kujenga.

Nikashuka ngazi na kwenda kusimama sehemu ambayo nilijua lazima Miryam akitoka kule vyooni ni lazima angepita hapo, kama wanaume na wanawake wengine tu. Nilikuwa nimeingiwa na wasiwasi yaani, lakini najua nilitakiwa kuongea naye upesi. Nilitaka kufuta wazo lolote baya ambalo lingekuwa limemwingia baada ya kuona ile ishu. Sijui kwa nini tu alipaswa kuwa sehemu hiyo wakati huo huo Rukia aliponivamia, yaani!

Kumwongelea Rukia, mwanamke huyo akawa amepita hapo hapo nilipokuwa nimesimama, nami nikaendelea kutulia tu nikitazama pembeni kama vile simwoni. Akaendelea kushuka ngazi mpaka kurudi kule ndani ya ukumbi, na baada ya sekunde chache, Miryam akawa amefika hapo pia. Nilipomwona tu, nikamsogelea karibu na kutaka kumshika mikononi, lakini akajiweka katika hali ya kujihami na kurudi nyuma kidogo.

"Miryam..." nikamwita kwa sauti ya chini.

Akaangalia juu na huko chini, naye akasema, "Unafanya nini? Kuna mtu anaweza akatuona..."

"Miryam, sikia... ulichoona muda ule..."

Akatikisa kichwa huku akifumba macho na kusema, "Jayden, tutaongea baadaye. Nahitajika ndani."

"Miryam usinifikirie vibaya. Huyo mwanamke amenifata tu, halafu amelewa, me hata...."

"Najua, Jayden. Najua," akanikatisha kwa kusema hivyo.

Nikatulia.

Akanishika mkono na kusema, "Usihofu. Nakuamini. Najua huyo amekufata mwenyewe, na nimeona ulipomsukuma. Sijachukulia vibaya."

Nikahisi ahueni kidogo, maana hapo nilikuwa nimeshapandisha mzuka wa kufikiri angenitema.

Akasema, "Najua wanawake wengi watakuangalia kwa njia hiyo, hata mimi wanaume wengine hunitazama hivyo, kwa hiyo ninakuelewa. La muhimu ni kwamba nakujua, unanijua... nakuamini, unaniamini... kwa hiyo usihofu. Sijakufikiria vibaya, tuko vizuri."

Nikashusha pumzi kiasi na kusema, "Asante. Ila I'm sorry... haikuwa poa we' ku... kuona hiyo kitu."

Akapita mtu mwingine hapo, naye Miryam akaniachia mkononi na kuanza kushuka ngazi huku akiwa amenionyesha ishara ya mdomo kusema 'baadaye.'

Raa!

Ilinipa faraja kujua kwamba Miryam aliniamini, hata kama asingekuwa amenikuta kwenye hiyo hali aliyonikuta muda mfupi nyuma, alijua kwamba ninampenda. Nikatuliza tu makeke, na najua alichosema ni kweli, wanawake wengi walionyesha kuvutiwa na mimi na najua wanaume wengine walimtaka yeye pia. Kikubwa ndani ya uhusiano wangu na bibie kama kwenye mahusiano yote kilipaswa kuwa uaminifu. Haijalishi tulitoka wapi na tulifanya nini, jambo kuu kwenye mapenzi yangu na Miryam lingetakiwa kuwa uaminifu mpaka mwisho.

Kwa hiyo ingenibidi niwe mwangalifu zaidi kutokuja kumpa Miryam sababu yoyote ile ya kunishuku kabisa, maana mimi nilimwamini yeye kwa asilimia zote, hivyo na yeye ningetakiwa kumpa sababu za kuniamini sikuzote. Na alikuwa na akili tulivu yenye utambuzi mkubwa sana, yaani kama pale ingekuwa mwanamke mwingine mpenzi wangu ndiyo ameniona vile na Rukia, ningechuniwa mwezi mzima kabisa kama siyo kutemwa.

Hivyo hilo likiwa limewekwa pembeni, nikarudisha hali yangu ya kujiamini zaidi na kurudi pale ukumbini kumalizia sherehe ya Doris mpendwa wetu, ambayo ikaendelea kutupa wakati mzuri wa kuwa pamoja na familia na marafiki. Na huyo Rukia hakunisogelea tena, yaani alionekana mtulivu kabisa na kunipotezea, na hilo lilikuwa jambo zuri. Sikutaka tena ije izuke ishu kama hiyo aliyonifanyia huyo mwanamke, na kwa njia hiyo ningeendelea kufanya mapenzi yangu na bibie Miryam yastawi zaidi.


★★★


Basi, Jumapili ikawa imeingia. Namaanisha yaani, tulikaa kwenye hiyo sherehe ya Doris mpaka saa sita usiku, ndiyo tukaitafuta njia ya kurudi nyumbani na kufanikiwa kufika ikiwa ni saa saba inayoikimbilia saa nane kabisa. Mama wakubwa walikuwa wamechoka, hata Miryam na Mariam pia, na walifika kwao na moja kwa moja kwenda vyumbani. Sisi wengine tuliendelea kukaa kuongea kidogo mpaka saa nane yenyewe na ndiyo tukaagana sasa; Tesha na mpenzi wake, Happy, wakilala pamoja hapo kwao. Alikuwa ameshamtambulisha rasmi kwa dada yake.

Mambo baina yangu na Miryam yalikuwa mazuri tu. Hatukuwaonyesha wengine ukaribu wetu, ila hatukukosa kuonyeshana namna tulivyokuwa na uvutano mkubwa baina yetu. Ningemtumia jumbe kadhaa za utani na yeye kunijibu vizuri, akiwa amepotezea kabisa lile suala la Rukia kule ukumbini, kwa hiyo nilikuwa na amani. Niliingia kulala pale kwa Ankia ikiwa ni saa tisa kasoro, na mwanamke huyo vilevile akapumzika mida hiyo baada ya kuagana na Bobo.

Kwa hiyo nimekuja kuamka kwenye mida ya saa tatu asubuhi, na bado nilihisi usingizi lakini nikajitahidi tu kuamka. Umeme ulikuwa umekatika lakini ni vizuri kwamba niliilaza simu ikiwa chaji, hivyo nikanyanyuka, piga push-up sabini kunyoosha mikono, kisha nikatoka na kwenda kuoga.

Ankia alikuwa bado amelala, shauri ya kwamba yeye na Bobo walikunywa bia jana kwenye sherehe, kwa hiyo hapo alikuwa bado amepondeka maana tulirudi wakiwa wamechangamka. Ni mimi tu na Miryam, mama zake wakubwa na Shadya ndiyo ambao hatukunywa pombe jana, na nimseme Mariam pia ingawa ni wazi pombe haikuwa kitu yake kabisa. Lakini kalirudi kwao kakiwa kamebeba majuisi na makuku!

Hivyo, nilipomaliza kuoga nikavaa vizuri kabisa, mtoko wangu tu wa kawaida siyo kama nilivyokuwa nimevaa jana kwenye sherehe. Kuna sehemu nilitaka kwenda, lakini kwanza kabisa ningepita hapo kwake Miryam ili niwasalimie walio macho, halafu ndiyo ningekwenda huko nilikodhamiria. Nikamtumia bibie ujumbe wa salamu kuuliza kama alikuwa ameshaamka, lakini hakujibu. Sijui sana ikiwa angekuwa amekwishaamka lakini kwenda ilikuwa lazima ili kujua. Kwa hiyo nikatoka hapo, T-shirt nyeusi, jeans, raba nyeupe, huyoo nikaenda nje Ankia akiwa bado anakoroma.

Nilipofikia hapo getini kwake Miryam, nikakuta mlango mdogo wa geti uko wazi kiasi, nami nikaingia tu na kukuta gari la bibie likiwepo. Inaonekana kulikuwa na mtu ametoka, kwa hiyo nikaelekea mpaka hapo varandani na kuvua viatu kwanza, na mlango wa kuingilia ndani ulikuwa wazi, wazi kabisa yaani nadhani kuruhusu upepo na mwanga uingie ndani vyema. Kwa ukaribu huo, niliweza kusikia sauti ya Bi Jamila hapo sebuleni akiongea maneno yaliyohusiana na ndoa, nami nikatambua kuwa alikuwa akiongea na Miryam.

"... hadi raha jamani! Kila mtu alikusifia, kuna wengine, yule mama yake Shamte kwa mfano... akawa anasema umependeza mno kumzidi hadi bi harusi, kwamba unafaa kabisa kufanya harusi yako maana... hee... watasema tu!" Bi Jamila akasema hivyo.

Miryam akasikia akicheka kidogo na
kumwambia, "Na wewe unapenda kusikiliza maneno-maneno mama..."

"Ni ukweli! Ulimzidi Doris, sikwambii hivyo kumpakazia mwenzio ubaya, ila hadi mama yake aliona wivu. Sisi tunajua. Ona... najua tumeshaongea, ila... nilikuwa nimepigia picha jinsi send-off yako na wewe itakavyokuwa. Itapendeza sana, sana, sana! Mola ajalie niweze kuiona, yaani Mimi... naisubiri hiyo siku kwa hamu..." Bi Jamila akasema hivyo.

Nikaingia ndani hapo huku nikisema, "Na haitachelewa, mrembo wangu!"

Nilikuta wanawake hawa wawili pekee wakiwa wamekaa hapo sebuleni, Bi Jamila akiketi sofani huku anashona nguo fulani iliyoonekana kuwa ya Mariam, na Miryam akiketi chini kabisa ambapo meza ilisogezwa pembeni, huku kukiwa na beseni dogo lililokuwa na unga wa ngano uliokandwa, na ungo wenye vipande vidogo vilivyokandwa kwa kutenganishwa na bibie mwenyewe; nadhani akiviandaa kwa ajili ya kutengeneza chapati. Kuingia kwangu na kusema hivyo kukafanya wote waniangalie, nami nikakaa pembeni sofani huku nikitabasamu.

"Yaani mama, na Miryam atakuja kufanya bonge la send-off asikwambie mtu! Anatutulizia tu. Au uwongo Miryam?" nikasema hivyo na kumwangalia bibie.

Alikuwa ameshikilia kampira ka unga alikozungusha huku akinitazama kwa utulivu.

"Ahahah... kweli, yaani sipati picha. Ndiyo nachotamani zaidi kuona kwa ajili ya huyu mwanangu," Bi Jamila akaniambia hivyo.

Miryam akaendelea na kazi yake kwa utulivu tu.

"Na imeshasomeka, mrembo wangu. Mungu kashaiandika, inakuja, ni siye kungoja tu. Ahah... shikamoo?" nikamwambia hivyo Bi Jamila.

"Marahaba baba. Umeamkaje?" Bi Jamila akaniuliza.

"Vizuri. Naona nyie ndiyo wa kwanza kuamka. Wengine bado wanavuta mashuka?" nikamuuliza hivyo.

"Aa... ni Zawadi na Mamu tu. Shadya na yeye ameondoka mapema. Tesha ndiyo amemsindikiza mchumba wake huko barabarani, anarudi kwao," Bi Jamila akasema hivyo.

"Dah, na Tesha anaenda kuoa hivyo..."

"Nakwambia! Ahah... kameamka mapema hako kadada, kakapiga deki hapa, kakaosha na vyombo, halafu kamemsalimia Miryam kwa heshima kweli, yaani! Nimekapenda," Bi Jamila akasema hivyo.

"Ahahahah... mmekuza..." nikasema hivyo.

"Eeh, Tesha kawa kidume. Miryam ndiyo... bado bado anajivuta," Bi Jamila akaongea hivyo kwa njia fulani kama amekwazika.

Miryam akamtazama kwa yale macho ya 'aaaa jamani,' naye Bi Jamila akatabasamu.

Nikamwangalia bibie na kusema, "Ila ni kweli. Kuna kale kamsemo sijui 'chelewa chelewa utapitwa,' ndiyo kanamvizia Miryam naona..."

Miryam akanitazama usoni kiumakini, nami nikabana tabasamu langu.

Bi Jamila akasema, "Umeona JC? Me huwa namwambia. Ushauri tu. Afanye upesi, eh? Aolewe, tucheze na wajukuu..."

Miryam akasema, "Mama...."

"Mrembo wangu yuko sahihi kabisa. Ndoa itakupendezea sana Miryam, yaani vile Doris alivyokuwa jana, wewe itakuwa mara mia!" nikamwambia hivyo.

Akakaza midomo yake huku akiniangalia kwa ile njia ya kiukali, kama kuniuliza nafanya nini.

"Kabisa! Atapendeza mno. Sema unajua nini, sasa hivi nimeshaelewa kwamba ni uamuzi wake, na... atapaswa apate mtu wa kumpenda na yeye ampende. Hatuwezi kulazimisha tunayotamani na yeye ayatamani, maisha ya siku hizi siyo kama ya zamani. Uwongo JC?" Bi Jamila akasema hivyo.

"Ni kweli. Mama yaani unasema kweli kabisa. Kwenye suala la uchaguzi ndiyo moyo unahusika, siyo kitu cha kuwahisha tu maana Miryam akisema awahishe anaweza akapata limtu litakalomtendea vibaya baadaye, anakuwa na busara kuangalia kwa umakini ni nani atakayemfaa, na akimpata akaridhika, ndiyo anabebwa naye sasa..." nikasema hivyo na kumkata Miryam jicho la pembeni.

Alikuwa anafinya tu ngano huku akiniangalia kama vile hataki, na mimi hapo nilikuwa nakoleza tu uchokozi.

Bi Jamila akasema, "Ni kweli kabisa. Sisi tulikuwaga tunachaguliwa waume nakwambia. Yaani unakaguliwa, halafu unapelekwa kwa mwanaume anakuoa. Sasa hivi mambo yamebadilika, lazima kuacha mtu achague mtu anayemfaa. Kabisa yaani, nimejifunza hilo."

Nikatabasamu kwa hisia na kumwambia, "Ndiyo hali halisi. Na siyo kwa wanawake tu, hata sisi. Mimi kwa mfano, kama nilivyokwambia siku ile, yaani nahakikisha kwamba nimepata mwanamke ambaye najua nitatulia naye kabisa ndiyo tunafunga ndoa. Lakini hiyo ni mpaka na mimi niwe na uhakika wa kwamba nitatulia. Hakuna kurukaruka kama nyani, no. Ndiyo ndoa itadumu."

Bi Jamila akatikisa kichwa kukubali hilo.

Nikamwangalia bibie na kumtikisia nyusi kidogo, naye akatikisa kichwa kama kuonyesha anakerwa sana na haya maongezi ya kimafumbo kutoka kwangu na mama yake mkubwa, wakati mada iliyemhusu alikuwa yeye, na alikuwa hapo hapo akiongelewa kama vile hayupo.

Bi Jamila akasema, "Kwa hiyo JC, ngoja nikuulize kitu. Hivi... kwa mwanamke kama Miryam, unadhani ni mwanaume wa aina gani anafaa kuwa naye ili ndoa itulie na azae vizuri?"

"Mama!" Miryam akamwita kimshangao.

Mimi mwenyewe nilimshangaa, sikuelewa aliuliza hivyo katika maana ipi, naye Bi Jamila akasema, "Namaanisha kwamba, yaani katika haya masuala ya uzazi, nimeangalia umri wako Mimi. JC ni daktari, yaani nataka kujua anaonaje... usalama uliopo kwako wewe kuzaa umri ukiwa umeshafi...."

"Mama, hilo siyo suala la kuzungumzia tukiwa na...."

"Haina shida, naweza kujibu," nikamkatisha bibie.

Miryam akaniangalia usoni kimkazo.

"Katika njia ya kidaktari zaidi, si eti?" nikasema hivyo kumwelekea Bi Jamila.

Bi Jamila akasema, "Eeeh, yaani nataka tu kujua. Umri wake Miryam ni mkubwa, na hajawahi kupata ujauzito..."

Miryam akafumba macho na kuinamisha uso wake, nami nikabana tabasamu langu kiasi.

"Kwa nyakati hizi tuseme akaolewa, akapata ujauzito, usalama upo mzuri wa yeye kujifungua?" Bi Jamila akamalizia swali lake.

"Naweza kusema ndiyo. Ana afya nzuri..." nikasema hivyo na kumtazama Miryam usoni.

Yeye akawa ananiangalia kwa mkazo.

Nikasema kizembe, "Na ana mwili mzuri pia..."

Miryam akaangalia pembeni huku akizungusha macho kiasi, akiendelea kuikata ngano.

Nikamtazama Bi Jamila na kumalizia kwa kusema, "Na hata kama tuseme kukitokea tatizo linaloweza kufanya iwe ngumu, siku hizi kuna njia za kitaalamu za kuwasaidia wanawake wanaojifungua wapitishe mtoto salama. Kwa hiyo anaweza kujenga familia vizuri tu."

"Eti eh?" Bi Jamila akauliza.

"Kabisa. Yaani kiulaini..." nikasema hivyo.

Niliposema kiulaini, nilikuwa nafikicha viganja vyangu kuonyesha huo ulaini, nami nikamtazama Miryam kukuta amenikazia jicho, kitu ambacho kikafanya nijikaze kutotabasamu.

Bi Zawadi akauliza, "Kwa hiyo hata akifikisha miaka arobaini, bado anaweza kupata watoto bila changamoto?"

"Ih! Tena miaka arobaini tu? Yaani anajifungua mapacha watatu bila tatizo kabisa," nikamwambia hivyo kwa uhakika.

"Kweli?" Bi Jamila akauliza.

"Eeh..." nikasema hivyo.

Miryam akaendelea kuniangalia usoni kwa njia ya kukerwa.

"Tena yaani Miryam, mpe mazingira mazuri sana, mwanaume anayemfaa kabisa, anazaa watoto wazuri bila shida hata chembe," nikamwambia hivyo Bi Jamila.

"Kumbe? Basi ni mwanaume yupi unayefikiri anamfaa? Yaani... apate mume wa aina gani ili amwandilie mazingira ya hivyo?" Bi Jamila akaniuliza.

Nikamwangalia bibie usoni, yeye pia akiwa ananiangalia kwa macho makini, nami kwa makusudi nikasema, "Mwanaume kama... mimi kwa mfanoo...."

Miryam akakaza midomo yake huku akitikisa kichwa chake kwa ukakamavu kunizuia nisiropoke upuuzi.

Nikajitahidi kuzuia tabasamu na kumalizia maneno yangu kwa kusema, "Mimi kwa mfano siwezi kusema kwa uhakika. Hapo ndiyo tutarudi tena kwenye ishu ya yeye kuamua. Maamuzi yote ni yake, maana tunaweza kuorodhesha sifa zote hapa, ila... mwisho wa siku unaelewa kwamba hakuna mtu mkamilifu. Si unajua?"

Bi Jamila akasema, "Hmm... ni kweli."

Miryam akaendelea kusugua ngano mkononi na kunitolea ishara kwa mdomo wake kama kusema 'hivi we ukoje?' nami nikatabasamu kiasi.

Bi Jamila akasema, "Basi me naendelea tu kumwombea binti yangu aolewe, na ajifungue mapema na salama. Ndiyo kitu nachotamani zaidi kuona kabla...."

"Mama..." Miryam akamkatisha kwa kumwita hivyo.

"Ahah, nisamehe mwaya. Naongea mno," Bi Jamila akamwambia hivyo na kumpiga kidogo begani kishosti eti.

Miryam akaendelea na kazi yake. Kwa sababu fulani, niliona ni kama vile hakuwa sawa kabisa kihisia, siyo kwa sababu tu ya hizi mada, ila ni kama kulikuwa na jambo lingine akilini mwake lililomsumbua.

Bi Jamila akasema, "Umeshakunywa chai baba? Nikuwekee japo kavu, bado chapati hazija...."

"Oh mrembo wangu, usijali. Niko poa. Nilikuja kuwacheki kwanza kabla sijatoka. Kuna sehemu naenda," nikasema hivyo na kumwangalia Miryam.

Bibie hakuniangalia machoni, lakini nikaona macho yake yakipanda kiasi baada ya kusikia kauli hiyo.

"Wapi, kanisani?" Bi Jamila akauliza.

"A-ah, naenda tu kufatilia mishe fulani hivi, halafu nageuka," nikamwambia.

"Haya sawa. Siku hizi Mamu ametulia zaidi, hamchezi kama vile mwanzoni, yaani naona anapona kabisa JC," Bi Jamila akaniambia hivyo.

"Yeah, anaendelea vizuri sana. Mungu anasaidia. Nitakuja kumcheki na yeye baadaye pia," nikasema hivyo.

"Sawa baba, uwe na safari njema," Bi Jamila akaniaga namna hiyo.

Nikasema, "Amen. Miryam, me naenda..."

Nilimwongelesha kwa sauti ya chini, naye akapandisha macho yake mazuri kuniangalia huku akiwa kama amevimba yaani, nami nikatabasamu tu na kunyanyuka kutoka sofani, na moja kwa moja nikaelekea nje. Hisia zangu za bibie kusumbuliwa na jambo fulani bado zilikuwepo, hivyo ningetakiwa kujua ikiwa zilikuwa za kweli nikija kukutana ama kuwasiliana naye baadaye, lakini kwa sasa nikaamua kwenda kuchukua usafiri ili nielekee huko Kawe. Ndiyo, Kawe.

Nilitaka kwenda kuhakikisha ishu ya Festo kuondoka, na cha kwanza ingekuwa kujua alikuwa ameiacha nyumba yake katika msimamo upi, ndiyo ningetafuta njia ya kujua pia ikiwa kweli aliondoka nchini ama zilikuwa swaga tu.

★★

Safari ya kuelekea huko Kawe ilichukua muda wa saa kama moja na nusu, nami nikaenda kule ambako nyumba maridadi ya Festo ilikuwepo. Hali ya nyumba hii ilikuwa vile vile tu kwa namna nilivyoikumbuka, hivyo nikasogea mpaka getini na kubonyeza tufe la kengele. Ikanibidi nibonyeze kwa mara nyingine tena baada ya dakika kama mbili kupita bila ya geti kufunguliwa, ndiyo likawa limefunguliwa hatimaye.

Aliyefungua hakuwa mwingine ila yule yule mlinzi wa nyumba hii, na alinikumbuka, hivyo tukasalimiana vizuri kabisa, halafu nikaulizia ikiwa bosi mkubwa alikuwepo. Mwanzoni hakutaka kutoa jibu la moja kwa moja na kunihoji kwa nini nilimuuliza hivyo, nami nikampiga za kijanja kwa kusema nilihitaji tu kuonana naye ana kwa ana maana zilikuwa zimepita siku kadhaa hatujaonana, na kwenye mawasiliano sikuwa nikimpata. Ndiyo akawa ameniambia kwamba jamaa hayupo, amesafiri. Hivyo tu.

Katika ile njia ya kuendeleza maigizo, nikamuuliza ikiwa alijua jamaa angerudi lini maana inaonekana alikuwa akijilinda kutokana na hali fulani ndiyo sababu akawa hapatikani, na ilikuwa muhimu sana niongee naye maana alikuwa bosi wangu pia. Ndiyo huyu mlinzi akasema kwamba Festo alikuwa ameondoka nchini. Yaani hakutakiwa kumwambia yeyote, ila aliniambia kwa sababu tu alielewa hizo mishe zetu na nini, kwa hiyo akasema jamaa ameondoka nchini na hajui atarudi lini.

Ila kama ni kitu ambacho mlinzi alielewa, ni kwamba hii nyumba ingeuzwa, na yeye hapo asingechukua muda mrefu kuondoka. Akasema inawezekana kulikuwa na matatizo na bosi wetu ndiyo alikuwa anayakimbia, kwa hiyo akanishauri niwe makini na mwangalifu sana nisije nikajikuta nakuwa kama yule shefu Saidi. Alijiongelea na yeye pia katika hiyo maana, kwa hiyo nikamwambia alikuwa akisema kweli kabisa. Nikatega pia kwa kuuliza ikiwa Festo aliondoka kwa kutumia ndege, naye mlinzi akasema ndiyo, tena alimsindikiza jamaa mpaka airport na kuhakikisha analirudisha gari lake huku.

Ahaa? Hapo nikawa nimepata nilichohitaji, lakini bado nilitaka kuwa na uhakika ZAIDI. Mlinzi alikuwa msaada tosha, lakini niliona uwezekano wa mambo aliyoniambia kuwa uwongo tu uliopikwa na Festo mwenyewe ili ajilinde zaidi, ningejuaje? Kama nyumba ingeuzwa, ina maana na magari yangeuzwa pamoja nayo? Nikataka kupata uthibitisho mwingine tena.

Kwa hiyo nikampa tu mlinzi heri nzuri na kumwomba samahani ya usumbufu, huku nikielewa wazi kwamba angeweza hata kumwambia Festo kuwa nilikuja kumtafuta. Ila hakungekuwa na shida sana maana niliigiza kutojua kwamba jamaa aliondoka, na kwa upande wake Festo wa mambo hilo lilikuwa kweli.

Baada ya kuondoka eneo hilo, nikavuta simu yangu na kumpigia Adelina. Zilikuwa zimepita siku chache bila ya sisi kuwasiliana tokea ile siku amepewa taarifa kuwa nilikufa, baada ya kuwa nimeibiwa simu na kuirejesha, kwa hiyo alipopokea kukawa na hisia nzuri ya mwanzo baina yetu.

"JC, mambo?" akasikika upande wa pili.

"Safi Adelina. Za kwako?" nikamsalimu pia.

"Nzuri, Mungu anasaidia. Wazima Mbagala?"

"Tunaendelea poa tu. Vipi, uko bize?"

"Hapana, leo nimetulia tu ndani. Jumatatu mpaka Jumamosi ndiyo nakuwa kazini," akasema hivyo.

"Ahaa... kumbe umeshaanza kazi?"

"Yeah, sikukwambia?" akauliza.

Nikakunja ngumi na kufanya 'yes' kimya-kimya, halafu nikasema, "Hapana, ulikuwa hujaniambia kama umeanza tayari, ila ulisema tu unakaribia kuanza. Lazima mambo yawe mengi."

"Eeeh bwana, ndiyo nimeanza hii wiki. Mambo ni mengi ndiyo, si unajua international airport?"

"Wacha we,'" nikasema hivyo.

Akacheka kidogo.

"Unadili na mambo gani?" nikamuuliza hivyo.

"Ninafanya service ya kutoa tiketi na kukagua passport, ama vitambulisho maalumu. Yeah," akaniambia hivyo.

"Umeridhika eeh?"

"Sana. Napenda sana kuwa hapo, ingawa masaa ni mengi ya kazi, ila shift tunabadilishiwa. Najihisi nimefika nyumbani."

"Hongera mwaya. Uko pazuri," nikamwambia hivyo.

"Ahah... asante. Ila siyo pazuri kama kwako wewe daktari..."

"Aa wapi, kwangu ndiyo pagumu, yaani! Asikwambie mtu," nikasema hivyo.

"Ila angalau tukiwa hivi na kazi, maisha yanasonga vizuri. Tunapata chance kuyaboresha, na kuwasaidia wengine. Kama tu wewe unavyofanya," akasema.

Nikatabasamu na kumwambia, "Ni kweli kabisa. Hivi... Adelina, kwa mfano tuseme nataka kujua ikiwa mtu amepaa na ndege kwenda labda nchi jirani, au wapi... ndani ya hizi siku chache... inawezekana?"

"Yaani kama amesafiri kwa ndege jana au juzi?"

"Eeh..."

"Yeah, inawezekana. Rekodi zinakuwepo, ni kutafuta tu jina la mtu unayetaka kujua amesafiri lini, tunaangalia, then...."

"Ooh, sawa," nikawa nimeelewa.

"Kuna mtu unataka kujua kama amepanda ndege?" akauliza.

"Eeh, na nitaomba unisaidie ili kujua kama kweli alipanda ndege. Ni rafiki yangu, nasikia ameenda Nairobi hapo juzi ila sijui lini. Nitakupa jina lake ujaribu kuniangalizia, eti? Ikiwa itakuwa sawa..." nikamwambia hivyo.

"Itakuwa sawa ndiyo, usijali. Si amesafiri hizi siku chache za mwisho?" akaniuliza.

"Eeh, yaani wiki hii hii kutokea Jumamosi iliyopita..."

"Mhm... JC bwana! Usiniambie haya ndiyo yale masuala ya kufatiliana mpaka Nairobi... wivu na nini..." Adelina akasema hivyo huku akicheka.

Nikacheka kidogo pia na kusema, "Hamna, siyo hivyo."

"Mmm, haya. Nitakuangalizia. Usijali. Utanitumia jina la mwenzako, kesho nikiweza nitaangalia," akaniambia hivyo.

"Asante sana. Nitakupa na zawadi," nikasema hivyo.

"Ahahah... kutafuta jina tu?"

"Eeeh, utastahili zawadi. Au hupendi zawadi?"

"Napenda. Utanipa Zawadi gani sasa?"

"We' ungependa ipi?"

"Mmmm... ni wewe tu uchague. Utakayopenda, nitaipenda," akasema hivyo.

"Au siyo?"

"Eeeh. Na uje kututembelea huku kwetu Kinyerezi. Itakuwa zawadi nzuri sana."

"Usihofu. Siku siyo nyingi nitakutembelea. Na si unatulia hasa kwenye Jumapili?"

"Eeh, Jumapili ndiyo nakuwa home. Karibu sana, hata ijayo uje basi," akanisihi.

"Sawa. Nitafanya hivyo. Ndiyo naelekea kupanda gari kurudi home pia, nilikuwa nimetoka," nikamwambia.

"Ahaa, basi sawa, tutawasiliana eh? Ndiyo na me nataka kupika," akaniambia.

"Haya dear, baadaye," nikamuaga.

"Poa."

Baada ya mazungumzo hayo, sasa nikawa nimejipatia uhakika wa kuthibitisha zaidi ikiwa kweli Festo alikuwa ameondoka, na nikawa natumaini kwamba jambo hilo lingekuwa kweli kwa asilimia zote. Ikiwa aliondoka nchini, basi amani yangu na bibie Miryam ilikuwa ya uhakika, hasa kwa wakati huu, hivyo ningetakiwa kulipata jina kamili la jamaa na kumtumia Adelina ili hatimaye niupate uhakika huo.

Nikaamua kwanza kwenda kwenye mgahawa mmoja mzuri ili kupata mlo, maana sikuwa nimekula tokea asubuhi hadi mida hii ya saa saba mchana, na baada ya hapo safari ya kurejea Mbagala ikaanza.

★★

Nimekuja kufika Mzinga kwenye mida ya saa tisa kuelekea kumi, nami nikaelekea kwa Ankia moja kwa moja na kumkuta mwanamke huyo akiwa zake ndani anamalizia kutengeneza mahanjumati. Alikuwa amechelewa kupika cha mchana maana aliamka muda umeenda halafu akanywa supu kwenye saa sita, kwa hiyo wakati huu alikuwa akiunga mboga ili ajilie na wali wake mwenyewe kupata nguvu zaidi. Mimi nikiwa nimeshiba bado, nikamwambia ningeingia tu kupumzika maana nilijihisi uchovu, ule uchovu wa uvivu tu, naye akasema haya, angeendelea kuwepo tu hapo.

Kwa hiyo nikaingia zangu chumbani na kubadili mavazi, nikivaa nguo nyepesi, kisha nikajitupia kitandani na kuwasha simu. Moja kwa moja nikamtafuta bibie wangu, nimchatishe wee maana najua alikuwepo nyumbani kwake tu leo. Wakati natoka huko Kawe nilikuwa nimemtumia jumbe kadhaa, tuka-chat kidogo WhatsApp na yeye kusema yupo tu nyumbani na kuna vitu alikuwa akishughulika navyo, kwa hiyo nilimwacha kwa kumwambia narejea Mzinga na ningemtafuta nikifika. Ndiyo nikawa natimiza ahadi sasa.

Katika suala la kuchat, Miryam alipendelea tutumie zaidi WhatsApp na siyo sms kawaida, kwa hiyo alinipatia pazuri maana mimi pia nilipenda kuwa 'online' muda wote, ikiwa sikuwa tu na mambo mengi yaliyoninyima muda wa kuchat na watu. Hivyo nikamcheki, akajibu, nasi tukaanza kuchat sasa. Nilikuwa nauliza kiutani kama chapati zimebaki ili niende kula, kama Mariam yuko poa, nikaingiza utani na utani mwingi yaani, lakini Miryam hakuwa amezama sana kivile katika mawasiliano haya pamoja nami. Yaani hata tu kwenye kuchat ningeweza kuhisi kwamba hakuwa ndani ya hali ya kawaida kihisia.

Kwa hiyo nikamwambia nataka kumwona. Akasema niende kwake nimwone kama nataka, lakini nikasema nataka yeye ndiyo aje hapa. Akaonyesha kutotaka hilo maana hakupenda kujichoresha kwa kuanza mazoea ya kuja kwa Ankia mara kwa mara, nami nikamwambia asiwe na hofu. Kwa leo tu, muda huu hasa kwa sababu alikuwa huru, ingefaa aje ili tuongee mawili matatu, tukiwa chumbani kwangu, yaani ukaribu wetu ukue zaidi, na nikamwambia nina njia ya kumleta bila kuzua michoro mingi.

Akawa amekubaliana na hilo hatimaye, naye alipouliza ni njia gani, nikamwambia atulie, inakuja muda siyo mrefu. Akaelewa haraka kwamba nilitaka kumtumia Ankia, naye akasema nisimsumbue rafiki yake bwana. Nikamwambia tulia wewe, sikubali kushindwa mpaka nihakikishe anakuja, na ndiyo kweli nikamfata Ankia kumwomba aende hapo kwa bibie kuzuga-zuga na nini, halafu amtoroshe kijanja aje kunipa company kidogo ya ana kwa ana. Ankia alikuwa hataki eti, nami nikamshawishi kwa kumwambia ningempa zawadi nzuri kabisa, nalo ndiyo likanyanyuka na kwenda hatimaye.

Nikajawa na furaha kweli moyoni, nami nikarudi zangu kitandani na kuendelea kuchat na bibie. Nikamjulisha kuwa mpitiaji ameshatumwa, hivyo ningemsubiria yeye mletwaji afike. Nimetulia hapo kwa dakika kama ishirini hivi, ndiyo nikasikia Ankia akiwa amerejea tena huko sebuleni, na alikuwa ameurefusha kweli huo upitiaji. Nilisikia anaongea na mtu, najua ikiwa ni bibie, nami nikaendelea tu kujilaza kitandani kwa utulivu huku nikiegamja mto.

Mlango wa chumba changu ulipofunguliwa, nikatazama hapo na kuachia tabasamu hafifu huku nikimwangalia mwingiaji, malkia wa moyo wangu, Miryam mwenyewe. Alikuwa amevaa T-shirt jeusi wakati huu, la mikono mifupi, pamoja na khanga nzuri nyeupe iliyofunika umbo lake la chini kuficha alivyovaa kwa ndani. Mwonekano wa kawaida tu huku akiwa amezibana nywele zake kwa nyuma, lakini uzuri wake uliufanya hata huo mwonekano uonekane kuwa wa hali ya juu. Hizo nguo zilikuwa na raha sana kuvaliwa naye!

Akiwa ameshika simu yake kiganjani, akarudishia mlango tena mpaka kuufunga, kisha akaanza kuja hadi karibu kabisa na sehemu niliyojilaza na kusimama huku akinitazama kwa utulivu tu. Kulikuwa na nafasi ya wazi usawa wa sehemu niliyojilaza, nami nikakishika kiganja chake na kumvuta kwangu ili akae. Akashuka taratibu na kukaa hapo kitandani, nami nikalalia ubavu na kupitisha mkono wangu kwenye kiuno chake, nikimvuta-vuta kichokozi.

"Mpenzi wangu kafika. Nilikuwa nimem-miss huyo!" nikamwambia hivyo kwa sauti ya chini.

Akaniangalia tu machoni, na kwa sababu fulani, bado niliona kwamba alikuwa makini sana, kama vile kuna jambo lilikuwa linamsumbua.

"Vipi? Mbona kama umenuna?" nikamuuliza kwa sauti ya kudekeza.

Akiwa ananiangalia tu usoni, akatikisa kichwa kuonyesha hakuna kitu.

"Ama ndo' unanipa silent treatment shauri ya yale maongezi yangu na mama mkubwa wako saa zile?" nikamuuliza hivyo huku nikitabasamu.

Akasema kwa sauti ya chini, "Halafu hayo masihara yako wewe! Ulikuwa unamwingizia ma' mkubwa vitu vya ajabu kichwani, sijui ukoje..."

"Ahahahah... natamani useme 'ntakuchhapaa,'" nikamwambia hivyo kiutani.

"Na ipo siku nitakutandika kweli," akasema hivyo na kuangalia pembeni, akiwa makini yaani.

"Ahahahah... basi nisamehe... ikiwa hiyo ndo' imekufanya uwe grumpy namna hii," nikamwambia hivyo kwa sauti ya kudekeza.

Akasema, "Hamna, wala siyo hivyo."

"Sa' mbona umeweka hilo pozi? Kuna mtu amekulazimisha umeze chura hapo ulipotoka?" nikajaribu kumtania.

Akawa ananiangalia tu usoni kwa njia ya kuonyesha utani haujamwingia.

Nikaendelea kwa kusema, "Niambie. Ni nani? Au umemmeza chura kwa kupenda mwenyewe?"

Akaendelea tu kuniangalia kama vile hataki.

Nikamwambia, "Sema kama umekula chura, Miryam. Na me nina kitabu changu cha sheria, nataka nikupige busu, sasa... utapaswa uondoe hilo gaga la chura mdomoni kwanza, siwezi me kupita na huo ulimi aisee. Kuna mswaki hapo.... ila hamna, tumia brashi kabisa la kusugulia jeans liko hapo, afu' finya dawa yote ya mswaki mpaka iishe ndo' u...."

Akaangalia pembeni taratibu na kutabasamu kiasi kwa kukunja midomo yake.

Nikacheka kidogo na kumtikisa kiasi, nami nikaegamia kiwiko changu ili nijinyanyue, halafu nikambusu begani na kisha kusema, "Unaonekana kuchoka. Nilikuwa tayari kwa mechi, ila kama unataka tuiahirishe siyo mbaya, kwanza... hata tiketi za mashabiki hatukuwa tume...."

Akacheka kidogo kwa pumzi na kusema, "Acha ujinga!"

Nikacheka pia na kuishika shingo yake taratibu, naye akanigeukia.

Nilikuwa nimeshapandwa na hisia nzuri sana kwa kuwa karibu naye namna hii. Nikawa naisugua shingo yake taratibu kwa kidole gumba huku nikiashiria kumfata mdomoni, naye akasogea zaidi na kuufata mdomo wangu pia. Hii ndiyo ikawa mara ya tatu midomo yetu kukutana na kupeana denda tamu kabisa. Tukaziunganisha ndimi zetu na kisha kuanza kupiga busu laini za taratibu, kama wazungu vile, naye ndiyo akaikatisha na kuibana midomo yake kiasi. Alikuwa ameshafanya niamshe balaa, lakini nilipomwangalia tena nikaona kwamba hakuwa sawa kabisa. Kuna kitu 'serious' kilikuwa kinaitafuna akili yake.

Akawa ameinamisha tu uso wake kiasi huku naye sasa akiwa amenishika pajani, nami nikamwambia, "Naona kuna kitu kinakusumbua."

Akaniangalia machoni kwa utulivu.

"Niambie. Kuna nini?" nikamuuliza kwa umakini zaidi.

Akashusha pumzi kiasi na kusema, "Sijui ninakuwa paranoid tu, au... yaani sielewi akili yangu imekuwaje."

"Paranoid? Shida ni nini kwani?" nikamuuliza kwa upole.

Akaniangalia na kusema, "Mamu."

Nikawa makini zaidi na kuuliza, "Amefanyaje?"

"Jana usiku, tulipofika ndani tukaongea kidogo kabla ya kulala. Alikuwa ananiuliza vitu, namwelekeza, sasa... mada ikawa imegeukia kwa wanaume. Alitaka kujua mengi... yaani nimfundishe vitu kwa sababu anafikiri mimi nina experience zaidi. Sikutarajia, ila hiyo sudden interest yake ikanifanya nimchimbe zaidi. Ndiyo akawa ameniambia kwamba... kuna mtu anampenda," Miryam akasema hivyo.

Nikakunja uso kimaswali kiasi, kisha nikajikuta naanza kucheka. Nikalalia mto tena na kuendelea kucheka tu, lakini Miryam alikuwa ameangalia pembeni kwa njia fulani kama vile amevunjika sana moyo, kwa hiyo nikajituliza na kukaa vile vile nilivyokuwa nimekaa karibu naye.

"Mariam amekwambia hivyo?" nikamuuliza hivyo huku nikitabasamu.

Akabaki kimya na kuendelea kutazama pembeni tu.

"Miryam... kumbe ni hivyo tu? Me nikafikiri unataka kusema kweli umemeza chura halafu mwenzio hapa nimeshakubusu! Umeniokoa kupata presha," nikamwambia hivyo kiutani.

Akaniangalia machoni kwa njia ile ile ya umakini.

Nikamwambia, "Usiogope Miryam. Najua unachowaza. Sawa... haya mapenzi ya siku hizi huwa yanaleta matatizo tu hasa kwa vijana wadogo, ila... hata ufanye nini... Mariam atayapitia pia. Amekaa ndani muda mrefu, kwa muda huo kuna watu walimwona kama mtoto tu, ila kwa kuwa sasa hivi afya yake inarudi mahala pake, ni lazima mvuto wake utaanza kuonekana tu kwa wengi... na yeye atakuwa na choice zake."

Miryam akaendelea kuniangalia tu kwa umakini.

"Ahah... nafikiri sherehe jana inaweza ikawa ime-trigger something... atakuwa ameona mengi, na ameona wengi. Sikia... naelewa. Najua ni muhimu kumlinda bado, ila huwezi sikuzote kumchunga. Ameshakua, na ameanza kujitambua tena. Kwa hiyo... the best way to protect her ni kumpa mwanga zaidi... mwongozo mzuri sana... akili yake ipo, najua atakuelewa..." nikamwambia hivyo kistaarabu.

Miryam akaendelea tu kuniangalia machoni baada ya mie kusema hayo.

Nikawa naisugua shingo yake taratibu, na nilipenda sana kufanya hivyo maana ilikuwa lainiii, kisha nikamwambia, "Usijali. Bila shaka... hata alipokuwa ameanza kuzinguliwa na lile suala la kichwa mpaka kipindi hiki, haya mambo ya... uanamke... si ulikuwa unamsaidia?"

Akatikisa kichwa mara moja kukubali.

"Basi, najua yuko poa, anajielewa... maana we' dada yake najua unamtunza vizuri," nikasema hivyo na kumbonyeza mbavuni kwa kiganja changu kingine.

Akashtuka kidogo na kupiga ulimi mdomoni kiasi, naye akautoa mkono wangu hapo kama vile hataki yaani, ndiyo akasema, "Tatizo siyo hilo."

"Sasa shida ni nini? Unahofia atapata mtu halafu atatoroka home, au? Asingekuwa ameongea na wewe, anafunguka kwako kwa sababu anajiamini, na anakuamini. Halafu... hebu kwanza niambie huyo jamaa aliyesema anampenda ni nani? Unamjua?" nikamuuliza hivyo.

Akaniangalia machoni kwa njia ya kutatizika.

Nikasema, "Asije akawa muhuni wa hiki kitaa ila, hapo ndiyo itakuwa shida. Au alimwona jana kwenye send-off? Inawezekana ikawa amekumbuka amewahi kwe...."

"Ni wewe," Miryam akanikatisha kwa kusema hivyo.

"Naam? Nini?" nikaitikia kauli yake kwa kutoelewa.

"Mamu anakupenda wewe, Jayden," akaniambia hivyo kwa sauti isiyosikika kuwa na raha.

Eh!

Kwa sekunde chache nikabaki kumwangalia usoni utadhani sikuwa nimesikia alichotoka kusema, naye akawa amenikazia macho yake tu.

"Ahah... Miryam acha masihara basi..." nikamwambia hivyo.

Akaendelea tu kuniangalia machoni kwa njia ya kuonyesha utani haukuwepo hapo.

Nikajivuta na kukaa kitako kabisa, na kwa sauti ya chini nikamuuliza, "Mariam amekwambia ananipenda mimi?"

Akasema, "Ndiyo. Sana."

Nikabaki kumtazama kwa utulivu.

"Hisia zake ziko in check sasa hivi. Anajua anachokitaka, na wewe ndiyo hiyo choice yake. Tena... ameniambia ni tokea muda mrefu tu, sema anakuonea aibu, anasema hajui jinsi ya kuongea na wewe. Leo tena akakuulizia, mida fulani hapo akanisemesha tena, ameniambia nije nimsaidie kumuunganishia kwako... kwa sababu hajawahi kutongoza mwanaume," Miryam akasema hivyo huku akiniangalia kwa ile njia ya ukakasi yaani.

Ohohoo! Tatizo hilo!

Yaani nilikuwa sijategemea kabisa hiki kitu. Nikawa nimetambua sasa kwamba hili suala lilikuwa limemkosesha amani sana Miryam, kwa sababu alikuwa katikati ya uchaguzi wa kuugawanyisha upendo aliokuwa nao kwa mdogo wake, na upendo aliokuwa nao kwangu. Ni wazi kwamba hakutaka kuziumiza hisia za mdogo wake kabisa, lakini hakujua afanye nini ili kutimiza hilo.

Ingekuwa ni juu yangu, na sote tulijua kwamba kwa njia yoyote ile, ningetakiwa kumweka wazi yule binti kuwa nisingeweza kufanya mahusiano naye, sema tu ndiyo hicho ambacho Miryam alikuwa akikiogopa; kujua kwamba kwa vyovyote vile mdogo wake angeumia tu. Nilitakiwa kutafuta njia ya kumwambia yule binti ukweli wa hisia zangu bila kuchukua kisoda na kuukwangua moyo wake mchanga, yaani nimuumize bila kumuumiza sana.

Hali ya ukimya ikakijaza chumba hiki kutokana na sisi wawili kuzama kwenye kina kirefu cha fikira, nami nikamwangalia Miryam na kuona ametazama tu pembeni kwa mawazo. Nikakishika kiganja chake kwenye kitanda taratibu, lakini hakugeuza shingo yake kunitazama.

Kwa upole, nikamwambia, "Miryam... sidhani kama... yaani... itakuwa tu ni suala la kuongea naye. Namwelewa vizuri, kwa hiyo... nitamwelewesha kwamba...."

"Kwamba dada yake ndiyo sababu hawezi kuwa na wewe?" akauliza hivyo kwa sauti ya chini bila kuniangalia.

Nikamwambia, "Miryam, mimi ni mkubwa sana kwake, namwona kuwa kama mdogo wangu kabisa, ananiamkiaga...."

"Kwani mimi siyo mkubwa kwako? Hilo ni tatizo?" akauliza hivyo huku akiniangalia.

"Sina maana hiyo, nasema tu kwamba nimeshamzoea kama mdogo wangu. Sidhani ikiwa atachukulia vibaya nikimwambia ukweli. Na... anachokifikiria nimeshakielewa, hiyo ndiyo kitu tunaita Stockholm Syndrome, mtu anaweza akafikiri anampenda mtu kwa sababu tu amemsaidia, lakini unakuta bado anakuwa hajazielewa hisia zake yeye mwenyewe vizuri... ndiyo inaweza ikawa hivyo kwa Mariam pia. Bado ni mdogo, hajapitia mengi kwenye maisha ya mapenzi, kwa hiyo sidhani...."

Miryam akawa anatikisa kichwa taratibu kama kukataa, naye akasema, "Jayden namjua mdogo wangu. Ninajua anapotaka kitu, anakuwa amekitaka kweli. Amekupenda. Usifikiri hii itakuwa easy, hebu imagine... unamwambia uko na mtu mwingine, anaumia. Mbaya zaidi aje kujua ni dada yake. Vipi kama bila sisi kujua... hicho kitu kikawa kimemsababishia apate hata mshtuko mwingine kwenye ubongo...."

"Miryam..."

"... yale ma-ASD... na PTSD yamrudie... tena vibaya? Tatizo lake la kichwani linaweza kurudi kwa njia tusizotarajia... anaweza hata avunjike moyo, ajiumize... labda hata ajiue!" akaongea kwa hisia.

"Miryam, usiwaze huko bwana. Acha kufikiria hivyo," nikamsihi kwa kubembeleza.

Akashusha pumzi na kufumba macho yake.

"Sikia, usi... usi-panic. Najua unatupenda sisi wote ndiyo maana unawaza sana, lakini niamini... hii ishu itakaa sawa. Usi-stress hivyo. We' tulia tu mama. Haitafika huko kote," nikamwambia hivyo kwa upole.

Akaangalia juu kiasi na kushusha pumzi kama kujipa utulivu, naye akakitoa kiganja changu mkononi kwake na kusimama kabisa, akiashiria kutaka kuondoka.

"Miryam, una...."

"Naenda kujimwagia maji, nahisi joto sana," akanikatisha kwa kusema hivyo, bila hata kuniangalia.

Kwa kumwelewa, nikamwambia tu, "Sawa. Nicheki ukitulia."

Akatikisa kichwa kukubali, kisha akaanza kuondoka hapo.

Alipoufungua tu mlango ili ndiyo atoke, nikamwambia, "Nakupenda."

Miryam akasimama kwanza, akiwa ameushikilia mlango, lakini hakugeuka wala kutoa neno lolote, kisha akaendelea tu kutembea na mlango ukajirudishia mpaka kufunga. Doh!

Kazi nilikuwa nayo. Nilifikiri angekuja hapa na mimi kumpetipeti kidogo aondoke na furaha, lakini ya kuzuka yakawa yamezuka tena. Kwa hiyo kumbe Mariam alikuwa ananipenda. Sijui yaani ila, sikushangaa sana, lakini sikuwa tu nimetarajia kabisa kupatwa na jambo hilo kwa wakati huu, achilia mbali taarifa hiyo kuletwa na mtu ambaye mimi ndiyo nilimpenda; dada yake huyo huyo aliyenipenda. Aisee!

Ningetakiwa kushughulika na hili suala kwa busara sana maana sikatai, kile ambacho Miryam alihofia hata mimi nilihofia pia. Nikawaza sijui nimtafutie tu huyo dogo ka-boyfriend kengine kazurizuri ili anipotezee mimi? Ila hapana, hiyo ndiyo isingekuwa busara. Ningepaswa kumpanga Mariam kwa njia ambayo ingemwelewesha kuwa si kila kitu ambacho mtu hutaka sikuzote huwa anakipata, hasa kama tayari kimeshamilikiwa na mwingine. Lakini katika hilo, ningetakiwa niwe mwangalifu sana ili nisije kuwa sababu ya kumvunja vibaya mno huyo binti.







★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
 
Back
Top Bottom