Simulizi: Mimi na Mimi

MIMI NA MIMI 2

A Story by Elton Tonny

Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa

R-rated 18+

Enjoy!


★★★★★★★★★★★★★★★★★★★

SEHEMU YA THELATHINI NA TATU

★★★★★★★★★★★★★★★★★★★


Baada ya Miryam kuondoka, Ankia akawa amekuja chumbani kwangu. Aliweza kuhisi kwamba kuna jambo halikuwa sawa maana akaniambia kwamba Miryam aliondoka tu bila kumwambia lolote, au kuaga, na alionekana kama ana huzuni. Akaniuliza ikiwa kulitokea tatizo, nami nikamwambia hakuna shida kubwa, bali kuna jambo dogo tu lilituchanganya mimi na bibie lakini tungelishughulikia tu. Mambo yangekuwa sawa.

Akasema haya, ningejua la kufanya tu kudili na mpenzi wangu, na kama nilikuwa nimemuudhi basi nijitahidi kumbembeleza kwa njia yoyote ile mpaka alegee. Nikamshukuru kwa kunisaidia kumleta bibie hapa, na sikusahau kuhusu kumpa zawadi hivyo nikamwambia ningempatia kesho tena nikitoka. Ilikuwa imeshaingia saa kumi na mbili jioni, na Ankia akawa na mpango wa kutoka kwenda kuzurura wapi-wapi sijui na Bobo wake, hivyo hapa alikuwa amekuja kuniambia kwamba kuna msosi umebaki; nikihisi njaa, najua jinsi ya kupakua.

Nikamshukuru, naye ndiyo akaenda kuanza kujiandaa. Nikaendelea kukaa hapo kwa zaidi ya nusu saa nikitafakari tu. Bado ishu aliyoileta Miryam hapa kuhusiana na mdogo wake ilikuwa inazunguka kichwani, na kwa kuwa nilimwahidi Bi Jamila ile asubuhi kwamba ningeenda kuwasalimia tena, nikaona ninyanyuke na kwenda kujimwagia ili nikaitimize hiyo ahadi. Lakini pia nilihitaji kwenda ili nianze kuangalia kama kile ambacho Miryam aliniambia kilikuwa na ukweli.

Yaani, nilitaka kumwona Mariam, nimwangalie, nimtathmini, nimwelewe. Halafu baada ya hapo ndiyo ningejua namna sahihi ya kuja kuzungumza naye ili kuweza kumsaidia kuyaondoa mawazo yake ya kimapenzi aliyokuwa amejenga kunielekea. Bado niliamini huyu binti alikuwa kwenye mwanzo tu wa kuzielewa hisia zake mwenyewe, na labda kweli alivutiwa na mimi, lakini ndiyo angepaswa kuelewa kwamba asingeweza kuwa nami. Ah, ingeeleweka tu, alikuwa mgonjwa wangu hata hivyo, na mimi nilimjua.

Kwa hiyo nikaenda kujiogesha, mpaka namaliza kuvaa vizuri tayari saa moja ilikuwa imeshaingia, na Ankia alikuwa ndiyo anakaribia kuondoka pia. Nikaenda mpaka kwa jirani zetu na kuwakuta mama wakubwa pamoja na Miryam wakiwa wamekaa kwa kutulia sebuleni, Bi Zawadi akifurahi sana kuniona. Nikawasilimu wakubwa na kuketi, story zikianza kwa Bi Zawadi kuniambia kuhusiana na ajali fulani waliyosikia imetokea huko Kongowe, na Miryam alikuwa ametulia tu sofani akionekana kuwa bize na simu yake.

Baada ya dakika chache Mariam akawa amekuja sebuleni pia, akitokea huko chumbani kwao. Alikuwa amevalia T-shirt nyepesi ya pink, suruali nyeupe ya jeans laini iliyombana, na nywele zake zilikuwa kwa msuko ule ule wa mafundo mawili manene ya rasta ndefu yaliyokaa kama mapembe ya ng'ombe yaliyolala. Alikuja moja kwa moja mpaka sofani nilipokaa na kuketi karibu nami, naye akanisalimia vizuri huku akinilalia begani kiasi kuonyesha furaha yake. Alinukia vizuri, harufu kama ya dada yake, na inaonekana alikuwa ametoka kuoga.

Mariam aliendelea kunishikilia mkono huku akinitaka niongee naye kuhusu mambo haya na yale, akiuliza vimaswali vyovyote tu ili umakini wangu wote uwe kwake pekee. Mama wakubwa nao walikuwa wanachangia maongezi yetu na nini, na kila mara nilipomwangalia Miryam, niliona namna ambavyo alijitahidi kuficha hisia zake kila wakati Mariam alipoonyesha uchangamfu wake kwangu kwa ukaribu sana, na najua hilo lilimkosesha amani sana bibie.

Siyo kwamba ni wivu, yaani Miryam aliumia kuona kwamba kilichompa furaha zaidi mdogo wake ni kitu ambacho hangeweza kukipata kwa sababu ni yeye Miryam ndiye aliyekuwa anakimiliki, na nilimwelewa. Alikuwa anaogopa Mariam kuumia sana, lakini hakukuwa na namna. Mwisho wa siku huyu binti angepaswa tu kujua ukweli, kama ndugu zake wote, na ningejitahidi kufanya hivyo kwa busara ili asije kupata mshtuko mwingine. Ndiyo alikuwa yai lao hapa, hawakutaka kabisa avunjike.

Basi, muda ukatembea mpaka kufikia saa mbili, na Tesha akawa amefika pamoja na Shadya. Jamaa alikuwa mizunguko na nini, na hapo alikuwa amekuja pamoja na mifuko iliyobeba vyakula kwa ajili ya familia nzima, ndiyo sababu hakuna mtu aliyekuwa ameingia jikoni leo. Bila kuchelewa maandalizi ya ulaji yakaanza, Mariam akisaidiana na Shadya kuviweka vyakula vizuri huko jikoni ili kuja kuipamba meza, nami nikawa nimepata nafasi ya kumsemesha Miryam kupitia simu.

Nikamtumia ujumbe, nikimwambia asiwe na shaka, suala la mdogo wake nitalishughulikia vizuri kabisa, tena kesho, ili muda mrefu usije kupita zaidi na jambo hilo kuja kuzua utata baadaye sana ikiwa wazi kwa mdogo wake kwamba siwezi kuwa naye. Miryam akanijibu kwa kusema ni kweli ana mashaka, na hofu, lakini ana imani kwamba mambo yatakaa sawa. Kama niliweza kumsaidia mdogo wake akaushinda ule ugonjwa, basi alijua ningeweza kumsaidia asivunjike mno moyo mpaka madhara kutokea. Imani alikuwa nayo, kwa hiyo angesubiri kuona matokeo, na akaomba samahani kwa kuondoka namna ile saa zile tulipokuwa pamoja.

Nikamwambia asiwe na hofu kabisa. Tena nikamwambia kwamba Mariam angefurahi mno siku ambayo dada yake angekuja kunitambulisha kwao kama mume mtarajiwa, nami nikamwona Miryam anatabasamu kiasi kwa kufarijika, naye akanitazama kwa hisia. Nikiwa nimegusia hilo suala la kutambulishwa, ndiyo nikamuuliza tu ikiwa alikuwa na mpango wa kuwaambia ndugu zake kuhusu mahusiano yetu mapema, lakini akanijibu kwamba anataka nitulize hali kwanza kwa upande wa mdogo wake, kisha ndiyo hayo mengine yangefuata.

Aliona nina haraka sana, na kweli, nilitamani mno iwe wazi kwa wote kuhusu uhusiano wetu ikiwa bado mapema, hata kama mwanzoni ingewashangaza lakini najua mwishowe wangepaswa kukubali tu kuwa tulipendana. Na ndiyo baada ya hapo, ningepeleka mahusiano yetu kwenye hatua ya juu zaidi. Sikuwa nikimtania nilipomwambia nataka kumwoa haraka, ilikuwa ni kusubiria tu awaambie mama zake kuhusu sisi, kisha ndoa ingefata bila kuchelewa.

Shadya na Mariam wakaandaa meza vizuri, nasi kwa pamoja tukaenda hapo kushiriki mlo. Zilikuwa zimenunuliwa ndizi za kukaangwa, nyama ya kitimoto kilo tano, vipande vya kuku, chips, na juice. Ah, hii ilikuwa ni kazi ya Tesha bwana, ambaye inaonekana aliangukia bahati nzuri sana leo na kupata mchongo uliomwezesha kuipendezesha meza yao kwa ajili ya familia yake nzima, na hakutaka kutuambia ni mchongo gani ila nahisi ni Happy ndiyo alikuwa amemsababishia. Huyo dada alifanya kazi ya upishi kwenye hoteli kubwa, kwa hiyo uwezekano kwamba jamaa alipewa mavyakula na mpenzi wake ulikuwa wa juu.

Hayo hayakujalisha sana, la muhimu ni kwamba familia yake ilithamini mno, na mimi mwenyewe nikala pia kwa raha zote, huku nikielewa msosi wa Ankia ungegeuka kiporo cha kesho. Tulikula huku tunapiga story zenye kufurahisha, Mariam akiwa ameketi pembeni yangu na amechangamka, yaani ule utu wake wenyewe wa "kidada" ukionekana wazi. Akaanza hadi kutaniwa na mama zake kwamba sasa hivi halishwi kama alivyokuwa amezoea kulishwa, kwamba amekua, naye akasema ndiyo, anakula mwenyewe sasa hivi na anaweza kumlisha yeyote kati yetu kama tukitaka.

Akafanya kuthibitisha hilo kwa kuniwekea nyama karibu na mdomo wangu ili nile, nami nikaipokea na kula. Mama zake na Shadya wakacheka kweli, wakisema sasa hivi Mariam amepona ndiyo atanigeuza mimi mtoto, naye Tesha akamwambia aendelee kunilisha maana nilistahili hilo eti kama zawadi yangu kutokana na msaada wote niliompa binti. Niliona hilo kuwa kama utani, lakini Mariam akalichukulia kikweli. Bila kusita, akaanza kunilisha, yaani akawa anachukua chakula na kuniwekea mdomoni, na sikuwa na jinsi ila kula ili vibe lisiondoke, lakini niliona kwamba jambo hili lilizua utata kiasi kwa upande wa dada yake.

Miryam alikuwa ametulia tu, akiniangalia kila mara nilipolishwa na Mariam na wengine walipocheka kwa furaha, lakini yeye hakutabasamu wala nini, bali akaendeleza utulivu wake tu na kula chake taratibu. Ikanibidi nimwambie Mariam imetosha, kwa upole, aendelee tu kula cha kwake, lakini akaweka ule uso wa kitoto kwamba hataki kuacha, yaani angenilisha mpaka mwisho. Hee, Tesha akasema haya sasa, ndiyo ningetakiwa kula la sivyo ningeliza mtu hapo. Dah!

Ili tu taswira isitoke mbaya, nikaendelea kupokea chakula alichonilisha binti na kuigiza kwamba nimestareheka, lakini nilijisikia vibaya sana kuacha hilo litendeke mbele ya Miryam. Lingekuwa jambo la kawaida tu ikiwa nisingejua kwamba Mariam alikuwa na hisia kwangu, kama tu wengine walivyoliona, lakini mimi na Miryam tulijua halikuwa la kawaida kwa sababu lingefanya binti aendelee kuongeza vitu vingi ndani ya hisia zake kunielekea. Kama leo kaweza kunilisha mbele ya familia yake, kesho angeweza kufanya kitu kingine tena bila hofu. Hii ingepaswa ikome upesi.

Miryam akawa wa kwanza kushiba, na tena hata hakumaliza chakula chake, naye huyo akaelekea jikoni kujisafisha na kisha akaenda chumbani mazima. Inaonekana hali nzima ya hapo ilimboa tu, na kiuhalali kabisa. Sisi wengine tulipomaliza kula pia tukajisafisha na kurudi sebuleni tena kutulia, na Mariam hakutaka kutoka pembeni yangu. Alikuwa na amani kweli mwenyewe, akitulia zaidi wakati huu kuangalia tamthilia pamoja na mama zake na Shadya, na ilipofika mida ya saa tano kasoro ndiyo nikaona niwaage.

Wao pia wakaniaga vizuri, Mariam akinifanya niahidi kuja na kesho asubuhi kumwona, nami nikakubali na kutolewa nje na Tesha ili aende kufunga geti. Akilini mwangu alikuwa anacheza Miryam tu, nikiwa nawaza kufika chumbani kwangu halafu nianze kuchat naye, na tulipokuwa tumelifikia geti, Tesha akanisemesha kidogo.

"Oya, nataka kukuuliza kitu..." Tesha akasema hivyo.

"Ropoka," nikamwambia.

"Aa, bangi za nini sasa?" akaniuliza hivyo.

Nikacheka kidogo kwa pumzi.

"Vipi ishu yako na Miryam bro, inaendeleaje?" akaniuliza.

Nikatabasamu kiasi na kumuuliza, "Kwa nini umeniuliza hivyo?"

"Ahah, we' sema. Nimeona... kakitu-kitu..."

"Kanini?"

"Niliona kama mlikuwa mnachat hivi... kijanja yaani..." akasema hivyo na kuninyanyulia nyusi kidadisi.

Nikatabasamu tu na kuangalia chini.

"Mlikuwa mnajishaua, mnachat kama vile siyo nyie, nimeona. Au nimekosea?" akauliza.

Nikamwangalia na kutikisa kichwa kukanusha.

"Kwa hiyo? Mko pamoja tayari?" akauliza hivyo kwa sauti ya chini.

Nikatikisa nyusi kukubali.

"Ah..."

Akasema hivyo na kunyanyua kiganja chake, nami nikakikutanisha na changu kwa kuviunganisha pamoja, kisha tukavutana na kukumbatiana kishkaji.

"Safi sana bro. Umejitahidi!" Tesha akasema hivyo baada ya sisi kuachiana.

Nikasema, "Yeah, ila... bado bado dada yako anataka tu-lay low, so...."

Akafanya ishara ya kufunga mdomo wake kwa zipu na kuniambia, "Me mtu wako, usijali, sitamropokea yeyote."

"Asante," nikasema hivyo.

"Nilikuwa nimeshaanza kuhisi umesogea close nilipowaona jana mnaingia kwenye send-off. Mwamba uko vizuri, hadi Mimi ameyeyuka!" akasema hivyo.

"Kawaida tu rafiki yangu. Tulikuwa tumeshapendana... nilihitaji tu kumfanya aone hilo, sa'hivi tuko pamoja," nikamwambia.

"Aminia. Fanya mambo sasa, uoe hapa," akasema hivyo.

"Ili?" nikamuuliza.

Akanionyeshea ishara ya kuendesha gari kwa mkono wake.

"Ahahahah... mjinga wewe! Ndo' unachowaza tu," nikasema hivyo.

Tukagonganisha viganja vyetu huku tukicheka kidogo, naye akasema, "Mwana itakuwa poa sana. Ukianza we' na da' Mimi mkafanikisha, nafata me na Happy."

"Uko tayari kumwoa?"

"Anataka tuishi wote. Kwa hiyo hapa mambo yakiwa good kabisa, nitaenda kuishi naye. Ndoa itafata tu. Nimekaribia kupata kazi," akaniambia hivyo.

"Ahaa... safi kaka. Mungu mkubwa, tutafanikiwa tu," nikamwambia.

"Uhakika. Haya mwanangu, usiku mwema. Ila najua huendi kulala sa'hivi wewe, unataka tu ukachat na dada eti?"

Nikaweka kidole mdomoni na kumfanyia, "Shhh..."

Akanisukuma kutoka getini kwao na kusema, "Nenda huko!"

Nikatoka hapo kwao nikiwa nahisi furaha, nami ndiyo nikaenda zangu mpaka chumbani na kujitia wepesi ili nipande kitandani na kweli nimcheki bibie tuweze kuchat kidogo. Lakini ile nimeangalia simu, nikakuta ujumbe kutoka kwake, akiwa ameniambia kwamba anaingia kulala mapema, kwa hiyo akawa amenitumia na 'goodnight' kabisa. Dah! Mambo gani tena haya?

Nikajaribu kumpigia, lakini ikaita tu mpaka ikakata. Labda kweli alikuwa anahitaji kulala ama labda tu hakujihisi amani sana bado, kwa hiyo nikaamua kumtumia ujumbe mzuri wa upendo wangu kwake na kumtakia usiku mwema, bila kusahau kumwakikishia kwamba Mariam angekuwa sawa. Ni hicho tu ndiyo najua kilimnyima raha Miryam kwa leo.

Yaani, katika kumsoma binti Mariam muda ule niko pale kwao, niliona wazi sasa kwamba furaha yake yote alikuwa ameielekeza kwangu, mimi nikiwa kama kitovu cha hiyo furaha, na ndiyo sababu akanipenda pia. Miryam kweli aliogopa kwamba mdogo wake angevunjika moyo sana ikiwa ningemkataa, lakini ningefanya nini? Nisingeweza kutoka nao wote, bibie mwenyewe alilijua hilo.

Hapa ambacho kingetakiwa ilikuwa ni mimi tu kumwelewesha binti vizuri, nihakikishe namwacha mahali salama kihisia, halafu ndiyo tungesonga mbele kwa mengine. Bado alikuwa kijana mdogo, angekuja kuendelea na shule, na najua angepata tu mtu mwingine ambaye angempenda namna ilivyostahili. Kwa hiyo hili suala ningetakiwa kuliua upesi sana ili lisiendelee kumkosesha Miryam wangu amani, na ndiyo hadithi ya mapenzi yetu ingeendelea kusonga vizuri hatua kwa hatua.


★★★


Asubuhi ya siku ya Jumatatu ikafika. Nililala kwenye saa saba jana baada ya kufanya utafiti kidogo juu ya suala la jina kamili la Festo. Haikuwa rahisi, ila nikafanikiwa kulipata, na nikamtumia Adelina kupitia WhatsApp na kumwomba aniangalizie safari ya huyo jamaa, kisha angenipatia jibu. Ndiyo leo kuamka kwenye mida ya saa tatu nikakuta ujumbe kutoka kwa Adelina akisema angenitumia jibu hakika akifanikiwa kujua. Nikamshukuru kwa hilo. Nikaangalia na upande wake Miryam wa jumbe na nini, lakini hakuwa amenitumia chochote. Nikaamua tu kumpigia, na bibie akapokea.

Tayari alikuwa ameelekea kazini kwake, nami nikamwambia kwamba mida ya baadaye ningekwenda huko kumwona. Akasema haikuwa na shida na nikianza kwenda nimjulishe maana angeweza kutoka, nami nikakubali hilo. Lakini nilikuwa nimeshamwelewa huyu. Huenda alitaka nimjulishe muda ambao ningeanza kwenda ili anipige swaga ooh nimetoka, njia yake ya kunikwepa tu ili tusionane mpaka awe na uhakika kwamba suala la Mariam nimedili nalo. Kwa hiyo muda ambao ningeenda huko nisingemwambia, ili nimbambe tu hivyo hivyo bila yeye kutarajia. Akili mtu wangu!

Tulipomaliza kuongea ndiyo nikapiga push-up zangu na nini, kisha nikaelekea kujisafisha. Ankia alirudi hiyo hiyo jana kwenye saa sita, Bobo akiwa amemleta, na walikuwa wamepondeka kiasi kwa kunywa bia na kula vyakula vitamu huko walipokuwa. Bobo alimpenda kweli Ankia, akahakikisha ameingia kulala vizuri, kisha ndiyo tukaagana na yeye kuondoka. Sasa hivi nikiwa nimetoka kwenda kuoga tayari saa nne ilikuwa imeshaingia, na Ankia tayari alikuwa ameamka. Alikuwa kwenye ile hali ya kivivu, hakufanya usafi ila chai alikuwa ameshaandaa, nami nikamtania kwa kumwambia inaonekana alitembezewa kipigo cha maana na Bobo hiyo jana.

Nikaenda kuoga akiwa amenitandika kofi begani, eti hataki nimtanie hivyo, na baada ya kusafisha kinywa na kuoga nikarudi ndani kuvaa vizuri kabla ya kwenda kunywa chai. Na ingenyweka na kiporo, huwa vinakuwa vitamu kweli kuliwa na chai asubuhi, kwa hiyo ningekula. Ankia alikuwa kwenye maandalizi ya kutoka ili akafungue duka lake, na wakati nikiwa chumbani bado nikitengeneza nywele zangu vizuri, akaja mpaka humu na kunisemesha.

"JC..."

"Ankia, me mume wa mtu sa'hivi, uwe unapiga hodi," nikamwambia hivyo kiutani huku nikizipiga-piga nywele zangu kwa chanuo.

Akasonya kidogo na kusema, "Kwa kipi ambacho sijakiona?"

Nikamfanyia kejeli kwa mdomo kama wanawake wanavyofanyiana, 'ng'oo!'

Akasema, "Mamu amekuja."

Nikaacha kutengeneza nywele na kumtazama usoni.

"Yupo hapo anakusubiria. Me ndo' naenda. Harakisha," akaniambia hivyo.

Hakujua ni jinsi gani kauli yake ilinifanya nihisi kuishiwa pozi, siyo kwa njia mbaya, yaani ile tu kwa kutotegemea. Mariam alikuwa amekuja hapa? Ahee... mbona majanga!

Ankia akasema 'baadaye,' nami nikamtikisia kichwa kukubali. Nikasogea mpaka hapo mlangoni na kuchungulia pale sebuleni, na kiuhakika, Mariam alikuwa amekaa sofani, Ankia akimpita na kumuaga vizuri sana, kisha binti akabaki peke yake. Alikuwa amevaa vile vile alivyokuwa amevaa jana nilipokwenda kwao, akikaa kwa kuegamia sofa huku akikumbatia mto mdogo mkononi, na kidole kimoja kikiwa mdomoni mwake huku akitazama TV. Dah!

Aliona nachelewa kwenda kwao, kwa hiyo akawa amenifata. Mhm, haya. Nikaweka chanuo pembeni, maana naona nafasi ya kuyamaliza haya yote ilikuwa imejileta kiulaini mbele yangu. Hakungekuwa na muda mwingine bora zaidi wa kuzungumza vizuri na binti kama siyo sasa, kwa hiyo nikaweka simu mfukoni na kwenda hapo sebuleni, nikiwa ndani ya T-shirt nyepesi na pensi yangu ya kijani. Mariam aliponiona namwelekea, akaachia tabasamu la furaha na kujisawazisha kwa jinsi alivyokuwa ameketi, nami nikaivuka miguu yake na kukaa pembeni yake hapo sofani.

"Good morning," akaniambia hivyo huku akitabasamu.

Nikatabasamu pia na kusema, "Morning. How are you?"

"Very much fine," kakajibu.

"I can see that. Umeshaanza hadi kunizidi kiingereza na mimi, umekuwa mzungu," nikamtania.

"Ahh... unadanganya. We' ndiyo umenifundisha..."

Mariam akasema hivyo huku akianza kuchezea kimkia cha rasta zake taratibu, na aliniangalja kwa njia fulani yenye hisia sana.

Nikaacha kumtazama na kusema, "Leo naona umewahi kuamka sana."

"Eeh, nimeamka saa moja, nikadeki ndani, nikamsaidia mama mkubwa kupika chai... ndiyo nikaja," akasema hivyo.

"Ahaa, safi sana. Unajitahidi. Warembo wangu hawajambo?" nikamuuliza.

"Eeeh. Wapo. Tesha ameondoka, na dada. Wapo wenyewe tu," akaniambia.

"Ndo' ukaona uje unisalimie?"

Mariam akabana midomo huku akiniangalia kwa macho yenye... raha yaani, naye akatikisa kichwa kukubali hilo.

"Sawa. Umeshakunywa chai?" nikamuuliza.

"Eeeh. Na wewe?" akauliza.

"Bado, ila nitakunywa tu. Ndo' nilikuwa nataka ninywe nije niwaone, halafu...."

Akanikatisha kwa kusema, "Ih, kumbe bado? Ona... weka... a-ah, ngoja nikuwekee chai, unywe hapa hapa, halafu ndiyo twende..."

Aliongea hivyo na kuashiria kutaka kunyanyuka, nami nikamshika mkono na kusema, "Hapana, Mamu... nitakunywa baadaye. Usijali."

"A-aaa... acha nikakuwekee..." akaongea kwa sauti ya kudeka kabisa.

Nikafumba macho na kuinamisha uso kiasi, kisha nikatazama pembeni nikiwa nahisi kutatizika yaani.

Akauliza, "Au hautaki nikuwekee?"

Nikamwangalia. Alionyesha hisia sana, yaani kwa alichotaka kufanya, alitaka kukifanya kwa moyo wote na haikumpa raha kuwaza kwamba nisingetaka akifanye kwa ajili yangu. Sikutakiwa kuzunguka sana hapa, yaani nilihitaji nimwambie nilichowaza haraka, maana kumwachia mno afanye hivi vitu kungemfanya adhani navipenda mno. Alikuwa amenilisha jana, leo aniwekee chai tena ili aanze kuninywesha? Hapana. Ningehitaji kuwa thabiti, ila nimfikie kwa upole.

Nikiwa bado nimeushika mkono wake nikamwambia, "Hapana, wala usijali Mamu. Sihisi njaa. Halafu... nataka niongee na wewe kwanza."

Mariam akajilegeza na kukaa vizuri zaidi, huku akiwa ananiangalia kwa macho makini na tabasamu lililojengeka taratibu.

Nikamwachia mkono na kusema, "Mamu... ninafurahi sana kuona kwamba unaendelea vizuri mno sa'hivi. Mwanzoni ulikuwa unaumwa sana, lakini sasa hivi...."

"Nimepona kwa sababu yako," akanikatisha kwa kusema hivyo.

Nikatulia na kuendelea kumwangalia usoni kwa utulivu.

Akajisogeza karibu yangu kidogo na kusema "Mimi ndiyo ninafurahi zaidi JC, maana... umenisaidia mno. Naongea vizuri tena kwa sababu yako, nafikiri vizuri tena kwa sababu yako, yaani...."

"Mamu, sijafanya kila kitu me mwenyewe. Dada yako, Tesha, mama zako, wamekusaidia pia. Jitihada zetu wote ndiyo zimekusaidia," nikamwambia hivyo kwa upole.

"Ni sawa, ila... wewe ndiyo umechangia zaidi. Bila ya wewe, nisingekuwa hivi," akaniambia hivyo.

Aliongea vizuri! Yaani nilimtazama na kuanza kuona mtu mwingine kabisa.

Nikashusha pumzi kiasi, nami nikamwambia, "Mamu... kuna jambo muhimu nahitaji kukuelewesha. Sawa? Ni... najua kwamba we' ni msichana mkubwa sasa, na ni binti mzuri sana..."

Akatabasamu kwa njia ya shau huku akinitazama kwa hisia.

"Nimeshaona maendeleo yako, na ni mazuri. Uko tayari kwa ajili ya mengi, ku... kutoka tena nje, kurudi tena shule, kuwa na marafiki wakubwa kama wewe, na... ukiwa tayari zaidi, zaidi ya sasa namaanisha, unaweza hata kuanzisha mahusiano na mtu ambaye...."

Mariam akanikatisha kwa kucheka kidogo kwa pumzi huku akifunika uso wake.

Nilikuwa najaribu kwenda taratibu ili anielewe vizuri, kwa hiyo nikaendelea kusema, "Nisikie sasa. Yaani, wewe uko sehemu nzuri sana kwa sasa kuanza tena kuishi kawaida, kama vijana wenzako. Utatakiwa kurudi shule, labda chuo... usome, ukutane na vijana wenzako, ujue mambo mengi zaidi yatayokusaidia u...."

Kabla sijamaliza kuongea, nikashtukia Mariam ananisogelea na kunipiga busu kwenye shavu upesi sana, kisha akakaa vizuri tena!

Nikamwangalia usoni, na yeye alikuwa akiniangalia kwa macho yenye matumaini mazuri kweli, halafu akaanza kutoa tabasamu lile la kujirudia-rudia kama vile anajaribu kulizuia. Kuangalia kiganja chake kimoja, nikakuta amejishika sehemu ya paja lake na kulifinya-finya kwa njia iliyoniambia kwamba alikuwa amepandisha hamu, hamu kunielekea. Ha, huu ungekuwa mtihani!

Nikamwangalia machoni tena na kusema, "Mamu... sikia. Nachotaka kukwambia ni kwamba...."

Mariam akanifata tena ghafla na kunipiga busu mdomoni, mpaka nikashangaa! Zamu hii, baada ya kunibusu tu hivyo mara moja, akaweka mto pembeni na kuendelea kuinamishia uso wake karibu kabisa na wangu, akiniangalia kwa njia ya mapenzi yenye dhati yaani, na kwa kweli hali hii nzima ilifanya mwili wangu upandwe na msisimko wa ajabu mpaka nikaanza kuvimba dude. Sikuelewa kwa kweli. Huu ujasiri binti alikuwa anautoa wapi?

Nikiwa nimezubaa kiasi, Mariam akafanya kitu ambacho sikutarajia kabisa, kabisa, kabisa! Akafanya kujinyanyua na kuipitisha mikono yake mabegani kwangu, yaani katikati ya uso wangu hadi kulishika sofa nilipoegamia, halafu akapitisha mguu wake mmoja hapa chini na kupanda juu yangu, akinikalia mapajani na kunitazama usoni kwa macho yenye hisia. Nilishindwa kujua namna ya kuitikia jambo hilo na kubaki nimeganda huku nikimtazama kwa umakini, mapigo ya moyo yakianza kwenda kasi, damu ikichemka, na hisia zangu kuvurugika.

Yaani akawa ameniweka kati, eti kutaka kunionyesha mapenzi. Nilihisi kuchoka! Bila kupenda, mashine yangu ndiyo ikazidi kuvimba, na kwa kuwa nilivaa pensi tu, ilikuwa rahisi sana kuhisi namna ambavyo binti aliikandamiza kwa jinsi alivyokuwa amenikalia, naye akawa ananiangalia kwa macho yaliyojaa... ashiki! Eeh, yaani hilo ndiyo neno. Hakutaka kusikia nini wala nini, Mariam alitaka vitendo.

"Mamu..."

Nikajikuta nanena tu jina lake kwa upole, nikijaribu kumshika sehemu za ubavu wake nimtoe kwangu kwa wepesi ili kuzuia jambo hili, lakini nilipomgusa tu, Mariam akatazamisha uso wake juu na kufumba macho kwa kilichoonekana kuwa kusisimka, halafu akaanza kujivuta-vuta taratibu katikati ya mapaja yangu na kuishika mikono yangu kwa pamoja. Eh!

Nikamwambia, "Mariam, nisikilize. Nisikilize mdogo wangu..."

Akaniangalia na kutabasamu kivivu fulani hivi, halafu akasema, "Nimetamani kwa muda mrefu sana kufanya hivi..."

Nini?! Nikabaki nikimtazama machoni kwa umakini.

Akanishika shingoni na kusema, "Unanisisimua sana..."

"Oh God!" nikanena hivyo kwa sauti ya pumzi.

Yaani hakuwa "binti Mariam" niliyemzoea, hapa alikuwa Mariam mwenyewe sasa, akili yake ikielewa vizuri kile ambacho alitaka. Maneno ya Miryam yalikuwa kweli, na mimi nilikuwa na makosa kudhani ingekuwa rahisi tu kumsemesha shauri ya mazoea, ila hapa ndiyo nikatambua kuwa hii ishu ilikuwa ya daraja lingine. Ningepaswa nimtoe huyu dada juu yangu upesi, lakini kwa uangalifu sana. Bado nilimwona kama mgonjwa wangu hata kama alikuwa amepona-pona.

"Mamu, sikia. Hapa ni kwa... ni kwa watu. Shuka, usinikalie hivi. Kaa hapo nikwambie kitu kwanza..."

Nikamsemesha namna hiyo huku nikiishika mikono yake na kujaribu kujivuta ili nimtoe juu yangu, lakini akaigeuza nguvu yangu kiasi kwa kuirudisha mikono yake mgongoni, yaani iwe kama nimeibana mgongoni kwake, halafu ndiyo akanilalia zaidi kifuani na kukaa mapajani kwangu akiwa amejibinua. Yaani mpaka nikashangaa. Hivi vitu alikuwaga anavijua au?!

Ikabidi niiachie mikono yake ili huo mtazamo umwondoke, na kabla sijaongea, akasema, "Ankia hayupo. Mpaka jioni."

Alikuwa ananiongelesha kwa sauti laini, tamu yaani, mdomo wake ukiwa karibu na wangu, na macho yake yakiwa na mlegeo hafifu huku pumzi zake zikiupa joto mdomo wangu. Nilikuwa nimekaza huko chini, yaani nilihisi kabisa dhambi inaenda kutendeka muda siyo mrefu! Kwa nini alinisisimua namna hii? Sikuelewa kwa kweli.

Akaweka mkono wake mmoja usawa wa kiuno changu na kusema, "Ni muda mrefu sana... sijafanya hivi."

Nikamuuliza, "Unaikumbuka mara ya mwisho?"

Akaangalia pembeni kwa ufikirio, kisha akatikisa kichwa kukanusha. "Nahisi... vitu vingi. Vina... vinapanda kila... nikikuona. Tokea siku ile..." akasema hivyo.

Nikaweka uso makini zaidi, nami nikauliza, "Siku gani?"

Akaniangalia usoni vizuri na kusema, "Ulipokuwa nyuma... na Dina."

Ohohooo!

Aisee! Kumbe siku ile kweli binti alikuwa ameniona nilipofanya na yule Dina pale kwao, na huenda hilo ndiyo jambo lililozidisha mtazamo huu aliokuwa nao sasa kunielekea, ikiwa kama siyo kitu kilichofanya uanzishwe.

"Kumbe ulituona?" nikamuuliza hivyo kwa sauti ya chini.

"Ndiyo. Tokea hapo... nilikuwa natamani... niku... niku...."

Akawa anababaika kiasi. Hadi nikawa namwonea huruma.

Akajitahidi kusema, "Nikuambie nakupenda... ila nikawa naogopa."

"Kwa nini?" nikajikuta namuuliza hivyo.

"Sijawahi.... au... sikumbuki kama nimewahi kupenda mwanaume. Labda... nimeshapendwa, lakini... kwa jinsi navokupenda wewe sasa hivi... sijawahi kuhisi hivyo," akaniambia hivyo kwa njia pole sana.

Unajua hii ndiyo pindi ambayo mpaka mtu unakuwa unatamani kuwa na uwezo wa kuzigawa hisia zako mara mbili, lakini unajua huwezi. Ipo ile kwamba mwanamke anaweza akanifata na kutaka tupige mambo tu, hapo naweza hata nikajifikiria mara mbili mbili na kusema ngoja ninywe pombe kisha nipige tu, halafu nitatubu kwa Mungu, niisingizie na pombe kidogo, Miryam asijue. Si mara moja tu? Ila kwa hii hali, Mariam alikuwa ananiomba nimpende kama yeye alivyonipenda, kitu ambacho hakingewezekana.

Na tena siyo kwa sababu tu ya dada yake, ila kwa sababu yake yeye mwenyewe Mariam. Nisingemuumiza hisia kwa kukubali jambo hilo hata kama ningekuwa na uwezo upi wa kuficha mambo, kiukweli alikuwa ni mwanadada mwenye kuvutia sana; kisura, kiutu, kiumbo, sikuwahi kumchukulia hivyo, ila sasa ndiyo nikawa nimeona hilo. Lakini hiyo haingenipa ruhusa ya kuamua kuzichezea hisia zake hata kama uanaume wangu ungetaka vipi kuvunja amri ya sita. Ila bado nilikuwa nimebanwa kwenye kona kali mno hapa.

Akawa kama anasubiri nimwambie kitu fulani baada ya kuwa ameniambia hayo, lakini mimi nikakosa la kusema zaidi na kubaki kuangalia chini tu. Akili ilikuwa inapingana na hisia. Yaani akili ikawa inanifanya nitamani mambo kuwa tofauti, labda iwe kama kipindi kile ambacho nilikuwa natembeza tu kwa mwanamke yeyote mzuri aliyenikubali, lakini hisia zilikataa. Haikufaa. Hasa kwa huyu mwanadada. Lakini ningetumia njia gani kumwondolea huo mtazamo ambao ni wazi ulikuwa umeshakita mizizi?

Kwa kuona nimetulia kutafakari tu, Mariam akaifinya nyonga yangu kwa kiganja chake, nami nikamwangalia usoni. Hapo hapo mwanadada huyu akanifata mdomoni na kunipiga denda laini, siyo busu, denda! Nikarudisha kichwa changu nyuma, lakini akanifata na kuendelea kulazimisha denda pamoja nami. Ai! Midomo yake ilijaa mate, naye akaona anishike kichwani kabisa na kuendelea kuinyonya midomo yangu kwa hamu kubwa kuliko!

Hisia za kimahaba zikanipanda kuliko ilivyokuwa mwanzoni. Nilikuwa siamini haya yaliyokuwa yanatokea. Mariam alikuwa ananyonya mdomo wangu kwa njia yenye ustadi, yaani ile 'experience' nzuri ya hii kitu alionekana kuwa nayo, na mimi huku mzee nguvu zikaendelea kukimbilia sehemu moja tu. Nilikaza, yaani nilikaza haswa. Nilinyanyua viganja vyangu hewani kiasi, nikivifunga na kuvifungua kwa kutaka kumtoa huyu dada karibu nami, lakini nikawa nashindwa. Na kilichofanya nishindwe, ndiyo kikawa kitu kilichofanya nianze kuanguka.

Viganja vyangu vilikuwa vinatakiwa kumwondoa huyu dada mwilini kwangu, lakini badala yake, nikajikuta namshika nyuma ya kichwa chake kwa mikono yote na kuanza kurudisha denda hiyo kwa hamu kubwa! Ah, siyo poa. Yaani pamoja na yote niliyokuwa nimetoka kuwaza kupingana na hii ishu, JC nikajikuta naanguka. Tena kwenye penzi la mdogo wa mpenzi wangu. Acha kabisa! Hii kitu huwa inatutafuna wanaume vibaya, usiombe. Yaani huwa tukifika hapa, tunasahau kila kitu, na mimi haikuwa rahisi sana kusahau, ila sijui tu kwa Mariam ikawa vipi.

Eh bwana eh, denda ikaendelea. Nilimdendesha huyu binti kwa ufundi, yaani ile denda yenyewe, mpaka nikahisi nafurahia kufanya hivyo. Najua ile hali ya upya, yaani msisimko unaotokana na ishu za mambo yote yaliyopelekea mpaka sisi wote kufika hapa, na ndiyo nikawa nimetambua kwamba nilikuwa dhaifu sana mbele ya huyu binti. Kwa mambo mengi, toka nimeanza kumsaidia mpaka sasa, nilikuwa na udhaifu mkubwa sana kwake. Hisia zangu za kumjali mno ndiyo zikapelekea nimruhusu afike huku pamoja nami, yaani msimamo wangu wote ukalegea mbele yake ndani ya dakika mbili tu. Mambo ikawa kwisha!

Mariam akaonekana kupandwa na hamu zaidi, akajitoa mdomoni mwangu na kuanza kupumua kimahaba sana, na mimi pasipo kuongozwa na akili, nikawa naendelea kubusu kidevu chake hadi kuifikia shingo, na yeye hakuacha kupeleka kiuno chake mbele na nyuma kwa njia ya kusugua mtambo wangu uliokuwa umevimba na kukandamizwa kwa kalio lake. Joto lilinipanda, yaani... sikufikiria la kufanya, nikawa naendelea kubusu tu shingo yake taratibu. Kulikuwa na zile fikira za 'Mungu wangu, nafanya nini?' lakini nikaendelea tu kufanya hiyo nini. Siyo poa!

Mariam alikuwa amelegea kweli, akiushika mkono wangu kwa nguvu na kupumua kwa njia yenye deko, yaani kama anataka kulia vile, nami kwa sekunde chache, nikaacha kumbusu na kumwangalia kwanza. Nilimtazama kwa umakini, bado nikiwa najishangaa yaani, kujiruhusu mpaka nianze kufanya hivyo, naye akaniangalia usoni kwa macho legevu na kunyonya kiasi mdomo wake wa chini. Nilikuwa kwenye fikira iliyotatizika, nikaanza kumfikiria dada yake tena, naye Mariam akafanya kitu kilichonihamishia mawazo hayo upesi.

Akashika T-shirt lake kutokea kiunoni na kuanza kulipandisha juu, mpaka akalifikisha usawa wa vikwapa, halafu ndiyo likajivuta juu lenyewe sehemu ya kifua na kukifichua chote kabisa. Aisss! Moto ukazidi kukolea. Binti hakuwa amevaa sidiria, kwa hiyo kwa mara ya kwanza kabisa nikawa nimekiona kifua chake waziwazi mbele yangu.

Alikuwa amebeba matiti yasiyo na ujazo mwingi, zaidi, kilichofanya yaonekane kuwa makubwa kiasi ni namna ambavyo chuchu zake zilikuwa zimevimba. Yaani alikuwa na chuchu nene zilizonyanyuka kuelekea mbele na hivyo kufanya matiti yazifate, na yalikuwa meupeeh, huku chuchu zikiwa na weusi-kahawia uliozipendezesha mno. Ilikuwa kama naangalia matunda mawili matamu sana ambayo hakuna mtu aliwahi kuyala, na msisimko wa hapo ukafanya nihisi mashine yangu ikikaza mpaka kuanza kuuma.

Sikudhani angekuwa na akili ya kupeleka mambo moja kwa moja hapo, ila hayo yalikuwa ni makosa yangu kwa kumchukulia kuwa kama mtoto mdogo bado. Haya mambo aliyajua, na mimi JC hapo ndiyo akawa amenipatia. Ah, hamu ilikuwa inanitesa kinoma halafu dada yake bado alikuwa ananibania, sikumbuki hata mara ya mwisho kupata huu msosi ilikuwa lini, kwa hiyo yule Shetani ndani yangu alikuwa anailazimu njaa ipande zaidi ili nianze kukamua hiki chakula kitamu sana mbele yangu. Sijui ingekuwaje kwa kweli!

Baada ya Mariam kunifunulia kifua chake, akanishika shingoni taratibu na kufanya kama kunivuta, na bila woga wowote ule, akaniambia kwa hisia, "Come on..."

Ei!

Nilikuwa napewa ninyonye, Mungu wangu, ninyonye matiti ya mdogo wake na mpenzi wangu! Ilikuwa kama ndoto vile, na najua isingekata kwa kufumba na kufumbua macho. Mate yalinijaa, nikiyaangalia matiti yake kwa hamu sana, naye alipoona najishauri bado akaamua kujisogeza kwangu zaidi na kuligusisha titi lake la kushoto midomoni mwangu. Nikafumba macho na kujitoa akili, nami nikalamba chuchu yake kidogo sana, na itikio lake likawa kuikaza zaidi shingo yangu kwa vidole vyake.

Kulikuwa na kautamu ka chumvi-chumvi kwenye ngozi ya chuchu yake, nami nikaanza kuilamba kwa uendelevu. Alinukia vizuri, harufu kama ya dada yake, na nadhani jambo hilo likaongezea hamu yangu ukali kwa kuhisi uvutano wa karibu zaidi kwake ulionifanya niendelee tu kuilamba chuchu yake. Nilikuwa nimefumba macho bado, nami nikaiingiza yote mdomoni na kuinyonya taratibu. Mariam akalegea zaidi, nikihisi kama anataka kuanguka sijui, nami nikamshika kiunoni na kumwangalia usoni.

Akarudisha mhimili wake vizuri, na kwa sauti ya kunong'oneza akasema, "Nhh.. naishiwa nguvu..."

Nikabaki nikimtazama machoni tu kiwasiwasi hivi.

Akanishika shingoni tena na kusema, "Usiache. Nasikia raha sana."

Duh!

Mariam akanisogezea kifua chake usoni kwa mara nyingine tena, nami nikaachama tu bila kupenda na kulipokea titi lake. Zamu hii, nilianza kulinyonya kwa kulivuta ndani ya mdomo kabisa, naye akanishika kichwani kwa mikono yote kwa njia ya kukumbatia na kunikandamizia kwake zaidi. Utamu ambao wanaume huwa tunahisi kunyonya hivi vitu huwa tunaujua siye tu, na kiukweli Mariam alikuwa na utamu wake mtamu.

Nikawa namnyonya huku nikiangalia jinsi alivyoonyesha raha ya hali ya juu, akiyabana mabega yake na kujikunja kiasi, na akilifinya-finya titi lake lingine shauri ya raha hiyo kumkolea, na hata mwili wangu ulisisimka vya kutosha kuonyesha ulifurahia tendo hili kufanyika. Lakini kihalisi, hili jambo lilinitatiza sana. Kumwangalia Mariam usoni ilinifanya nimuwaze dada yake, sana, siyo tu kwa sababu walifanana, ila kwa sababu jambo hili lisingekuwa sahihi kufanya.

Naelewa furaha ya Mariam ilikuwa ni suala muhimu katika kuendeleza hali yake njema, ila nisingeweza kumpa hii furaha aliyokuwa akiitaka. Nilimpenda Miryam, hilo nilihitaji kumweleza Mariam wazi, iwe leo, ama lini, angetakiwa kuelewa. Haingekuwa na maana kuruhusu jambo hili litokee halafu nirudi kwa dada yake tena, hiyo ingenifanya niwe nani? Nisingemfanyia Miryam hivyo. Na sikutaka kumfanyia huyu mwanadada kitendo hiki hata kama ingemuumiza moyoni. Na sijui kwa nini tu hilo dude langu likaamua kunyanyuka, huu haukuwa wakati mzuri hata kidogo!

Nikajitahidi kuzipinga tamaa za kimwili na kuacha kumnyonya namna hiyo, naye akaanza kulivuta-vuta titi hilo kwa kuonekana kuwashwa zaidi. Aisee! Nilikuwa nimefanya nini? Sikupaswa kabisa kumfikisha huyu binti sehemu hiyo. Nikashindwa hata kumwangalia usoni kwa sababu ya kuhisi hatia sana, nikitazama pembeni tu huku moyo wangu ukiingiwa na hofu kutokana na kutambua kosa langu, naye akawa ametulia tu juu yangu, bila shaka akinitazama kwa subira.

Nikasema, "Mamu nisamehe. Nisamehe sana mdogo wangu..."

Mariam akanishika shingoni na kusema, "Umefanyaje kwani? Mbona unaomba msamaha?"

Nikamwangalia usoni kwa huzuni.

Akatabasamu kiasi na kusema, "Usijali. Hujaniumiza. Ninapenda sana unavyonifanya."

Aliongea taratibu, kwa hisia ya dhati, yaani dah! Kwa hiki nilichokifanya mpaka nikajiona Shetani sasa hivi, wakati sekunde chache nyuma nilikuwa nahisi kukifurahia kweli. Sijui nilikuwaje!

Mariam akasema, "Tuendelee..."

"Hapana, Mamu... ime-imetosha," nikamwambia hivyo huku nikijifuta mdomo.

Hapo hapo nikaishika T-shirt yake na kuishusha upesi, naye akawa ananiangalia kwa kutoelewa.

"Mamu, hatuwezi kuendelea. Sawa? Tunaishia hapa... sikupaswa kufanya hivi... nisamehe. Nimekukosea sana," nikamwambia hivyo kwa hisia.

"Kwa nini?"

Aliuliza hivyo kwa sauti yake ya upole sana, akiwa hajanielewa vizuri najua maana hadi tayari nilikuwa nimeshaanza kumpandishia hamu hata zaidi, nami nikabaki nikimtazama machoni kwa hisia sana.

"Au haujapenda? Nimewahisha sana?" akauliza.

"No, siyo hivyo... sijamaanisha hivyo Mamu. Ni kwamba... we' ni rafiki yangu. Sawa? Napenda tukiendelea tu kuwa marafiki..." nikamwambia hivyo kwa upole.

Bado alikuwa amenikalia, naye akasema, "Marafiki. Kwa nini usi... hauja.... haujanipenda JC?"

"Siyo hivyo Mamu, we' ni msichana mzuri sana. Sawa? Mzuri, mrembo, yaani... unawafunika hadi wakina Beyonce kabisa. Hamna mtu asiyeweza kukupenda. Hayupo..." nikamwambia hivyo.

Akaendelea kuniangalia machoni kwa hisia.

"Ila... mimi ni kama kaka yako, sawa? Nakuona we' kama Nuru. We' na Nuru mnafanana sana, wote nawaona kama wadog...."

"JC... acha kuniongelesha hivyo. Me siyo mtoto," akaniambia hivyo kwa hisia.

Nikatatizika kiasi moyoni, maana ni kweli bado nilikuwa namtendea kama mtoto mdogo.

Akasema, "Niambie tu ukweli. Haujanipenda?"

Nikashindwa kumtazama usoni na kutulia tu nikitazama pembeni, maana nilikuwa nimefanya iwe ngumu kupata namna ya kumwambia kwamba nilimpenda mtu mwingine, na alikuwa ni dada yake. Nilipomtazama usoni hatimaye, nikakuta machozi yakiwa yameanza kumlenga kwa kasi, nami nikashtushwa kidogo na jambo hilo. Nikamshika shingoni kwa viganja vyangu vyote huku nikimtazama kwa hisia sana, na yeye akawa ananiangalia kwa macho yenye huzuni.

"Mamu... Mamu usilie. Nisikie. Nakupenda. Sawa? Nakupenda sana. Wewe ni mtu wa muhimu mno kwangu, hilo sikudanganyi. Lakini... ukweli ni kwamba... nakupenda kama mdogo wangu, Mariam. Nakupenda kama Tesha anavyokupenda, kama mdogo wangu. Nime... nimeshakuzoea kwa jinsi hiyo Mamu... kama mdogo wangu. Unaelewa?" nikamwambia hivyo kwa upole.

Machozi yakaanza kumtiririka, naye akasema, "Lakini me nakupenda JC. Nataka tuwe.... wapenzi. Usinione kama mtoto. Naweza kukufurahisha. Nitakufurahisha..."

Alinitia simanzi kali sana, mpaka chozi likanitoka.

Akapindisha shingo yake kidogo na kusema, "Niambie unataka nini... nitakupa..."

Masikini!

Nikajifuta chozi haraka na kuanza kumpangusa yake pia, nami nikamwambia, "Hauhitaji kunipa chochote mama. Wewe ni msichana mzuri, unatosha. Tunaweza kufurahishana kwa kuwa marafiki tu, kama sikuzote tum... tumekuwa tukifanya. Ila hatuwezi kuwa wapenzi Mariam..."

Akaangalia chini huku machozi yakiendelea kumtoka.

Nikamtazamisha usoni kwangu na kumwambia, "Ona... sikwambii hivyo kwa sababu haujanivutia. Kama nilivyokwambia, wewe ni msichana... mzuri sana. Lakini mimi sikufai Mariam. Siyo mimi nayestahili kuwa mpenzi wako. Mimi... unanijua kwa mengi mazuri, lakini... nimefanya mengi yasiyo mazuri pia... nimeumiza watu na kujichukia kwa sababu hiyo, na... ni mengi nayojutia. Sitaki nikuweke kwenye hiyo orodha mdogo wangu... sitaki nikukukubalie, nicheze na hisia zako halafu ifikie sehemu nikuumize.... sitaki kukuumiza Mariam. Wewe ni muhimu SANA kwangu, sitopenda kukudanganya..."

Mariam akaniangalia na kuuliza, "Nani anakusaidia sasa?"

Nikamwangalia usoni kwa umakini kiasi.

"Najua lazima awepo mtu anayekusaidia... usitekwe sana na mapito... uwe mtu bora. Ni nani?" akauliza hivyo.

Aliongea kama mtu-mzima mzima yaani, kwa kweli alikuwa anaelewa vizuri sana mambo haya kuliko nilivyodhani.

"Niambie JC. Una mpenzi?" akaniuliza hivyo.

Nikiwa nimeshauachia uso wake, nikaangalia chini tu na kutikisa kichwa kukubali kwa unyoofu.

Mariam akavuta pumzi ndefu kiasi na kuishusha, akisafisha pua mara kwa mara, naye akaangalia chini na kusema, "Sawa. Nimeelewa."

Mh?

Nikaendelea kutazama chini kwa huzuni na kwa umakini pia, kwa sababu sikujua bado hali ya akili yake ingekuwa vipi baada ya hapo.

Akaniangalia kwa chini huku akidondosha machozi na kusema, "Asante. Kwa kuniambia ukweli."

Nikatikisa tu kichwa kuonyesha uelewa.

Akanishika kiganja kimoja na kusema, "Usijali JC. Nitakuwa sawa. Usiwaze kabisa. Hiki kidogo ulichonipa leo kimefurahisha sana... hujui tu..."

Nikamwangalia usoni kwa hisia.

"Ila wewe kuwa honest na mimi ni... ni kitu nimependa zaidi. Asante. Ndiyo moja ya mambo yanayofanya nikupende sana..." akasema hivyo kwa sauti yenye uchungu fulani hivi.

Nikaingiwa na simanzi zaidi na kushindwa kujizuia kudondosha machozi, nami nikasema, "Nisamehe Mariam..."

"Nisamehe pia JC..." akaniambia hivyo kwa hisia sana.

Nilishindwa hata kumwangalia usoni tena, na akiwa bado amenikalia, Mariam akakishika kichwa changu na kunikumbatia, akikiweka kifuani kwake na yeye kulaza kichwa chake juu ya changu kwa nguvu kiasi. Nikakaza macho huku machozi yakizidi kunitoka tu, nami nikaukumbatia mgongo wake pia huku nikihisi huzuni, hatia, na maumivu mengi sana moyoni mwangu.

Sijui ni kwa nini niliumia kiasi hiki, yaani ih! Roho iliniuma! Na binti kuwa mwelewa namna hiyo ndiyo kitu kilichonizidishia simanzi hata zaidi, yaani kwa huu muda wote wa likizo hakuna mtu mwingine aliyekuwa amenitoa machozi zaidi ya jinsi yeye alivyofanya. Nilikuwa na udhaifu mkubwa mno kwa huyu mwanadada, yaani wa hali ya juu. Sikuweza kuzuia hisia zangu mbele yake kabisa.

Mariam alilia kwa kwikwi na kwa pumzi, hakutoa sauti yaani, naye akaniachia baada ya sekunde chache na kujitoa mapajani kwangu. Akasimama kabisa mbele yangu, mimi nikimwangalia kwa hisia nyingi sana, naye akanionyesha tabasamu hafifu na kisha kuondoka kabisa hapo kwa Ankia.

Nikafunika jicho moja tu kwa kiganja na kujikaza nisilie, lakini ndiyo kile kilio cha uchungu kikaja kwa kasi zaidi. Kile cha ndani sana, kikitaka kitoke kwa nguvu zote, lakini nikajitahidi kuzuia hilo na kubaki sofani hapo nikiwa na huzuni kuu mno. Labda njia yangu ya kumfikia binti kwa asilimia zote haikuwa nzuri, nilikosea kwa vingi, lakini nilishukuru tu kwamba sikupitilizisha hayo makosa, na nikafanikiwa kumwambia ukweli. Alionekana kuumia, lakini alielewa. Ambacho kingebaki sasa ingekuwa kuona ni wapi jambo hilo lingeishia, kwa sababu nisingeacha kuhakikisha kwamba Mariam alikuwa sawa.








★★★★★★★★★

ITAENDELEA

★★★★★★★★★


Pata Full Story WhatsApp au inbox

Whatsapp +255 678 017 280

Karibuni sana
 
Wangapi walikua wanasoma huku wanamwambia jamaa aache asiendelee
Hahah mwanangu Elton unajua tukupe maua yako
Sema Mamu alishasema anapenda simu km ya Da Nuru huu ndo muda wa kumzawaidia ss ili atutolee jamu kwa Mimi
Siku analiwa Mimi nitakaa na Vaseline pembeni
 
dah Pole sana damu yangu JC lakini ndo mitihani ya Mapenzi hiyo
 
Safi sana JC kwa kuweza kuzishinda hisia zako kwa Mamu,ungenihuzunisha sana kama ungefanya naye tendo
 
🤪🤪🤪🤪
 
Ndugu yetu Elton Tonny tupe muendelezo, wala hujawahi kutuangusha
 
Njia ya pekee ya kukomesha michezo ya hatari ni kusamehe na kuyaacha yapite,

Ukiamua kulipiza kisasi, ujue na wengine watakuja kulipiza dhidi yako. Na hiyo itakua ni endless chain
 
Kazi ndo kwanza inaanza, JC kuwa makini ila tu usije ukamua huyo black mamba maana utajiongezea uhatari kwa watu wanaokuzunguka na wewe mwenyew
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…