Elton Tonny
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 396
- 2,976
- Thread starter
- #221
MIMI NA MIMI
A Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Inashangaza kidogo, eh? Ndiyo. Huyu jamaa aliyekuwa kwenye dili la kununua shamba la Mariam kupitia wawakilishi wake waliompata Joshua kama dalali, alikuwa ni mzee wangu. Ni kitu ambacho sikuwa nimetarajia kabisa mpaka Joshua alipotaja jina lake muda mfupi nyuma kule kituoni, na ndiyo maana nilihisi labda kuna mambo mengi kwenye visa vyote vilivyokuwa vikitokea sasa yalionekana kuwa kama yamepangwa fulani hivi na majaaliwa.
Yaani kweli, ilipaswa tu kuwa mzee wangu akawa ndiyo mnunuzi wa hiyo mali mpaka kusababisha hayo mambo yote mabaya kutokea! Ila sidhani ikiwa alijua undani wa visa hivyo vyote, na ndiyo nilikuwa nimekuja kusahihisha mambo. Oh, na kuhusu JC kuwa kijana wa jamaa mwenye pesa namna hii ni suala ambalo tutaliongelea baadaye. Ikiwa baadaye itakuja!
Baada ya kuwa ameniambia nikaribie, nikakisogelea kiti kimoja karibu na meza yake na kisha kukaa.
"Imeshapita miezi miwili toka mara ya mwisho tumeonana, eti?" mzee akaniuliza hivyo.
"Ee, nafikiri," nikamjibu.
"Okay. Umenikuta niko bize, ila nambie. Kuna tatizo?" akauliza.
"Ee, naweza kusema ni tatizo. Kuna jambo nahitaji unisaidie kulisuluhisha," nikamwambia.
Akashusha pumzi kiasi kama kutoa uchovu wa kifikira, naye akasema, "Ni kuhusu ishu ya dada'ako?"
Sikutarajia hilo, hivyo nikasema, "Hapana. Kwa nini kwani? Jasmine ana tatizo lolote?"
"Hawajakwambia?"
Nikatikisa kichwa kukanusha.
"Labda hawajaona ni busara kukwambia, hata hivyo haikuwa..."
"No, mzee... niambie. Kilichonileta ni kitu tofauti, ila... niambie kwanza Jasmine ana tatizo gani. Amebakiza miezi michache ajifungue, si ndiyo?"
"Yeah, miezi miwili au mmoja na nusu."
"Shida ni nini?"
"Wameachana na mume wake," akaniambia hivyo.
Nikakunja uso kimaswali kiasi, nami nikaangalia pembeni.
"Wamekorofishana sana juzi hapo, ilikuwa ugomvi mkubwa over a petty misunderstanding, na unajua jinsi dada yako alivyo. Ilikuwa karibu apate miscarriage. Mimba ingetoka," akasema hivyo.
Nikawa nimeshangazwa na hili, nami nikauliza, "Ulikuwa ugomvi... yaani, huyo jamaa wake alifanyaje, alimpiga au?"
"Hamna, walirushiana maneno tu. Huyo Kevin akaondoka zake, ndo' dada'ako akapata mshtuko. Ila walimpeleka hospital, sa'hivi yuko vizuri tu."
"Yuko wapi sasa hivi?"
"Yupo nyumbani. Imebidi akae na mama yenu mpaka akijifungua."
"Dah! Siyo poa. Itabidi nije niende kumwona," nikamwambia.
"Labda waliona wasikwambie ili wasikuharibie likizo yako. Kwanza umeenda wapi kwenye hiyo fungate lonesome?" akaniuliza hivyo.
Nikatabasamu kiasi na kusema, "Niko Mbagala."
"Kule nyuma kwenye jalala?" akauliza kiutani.
"Ahahahah... pazuri siku hizi, siyo kama Mondi alivyopaacha," nikamwambia.
"Okay, sawa. Niambie sa' ishu ni nini kama siyo Jas," akasema hivyo huku akiangalia karatasi moja mezani.
"Yeah, aa... kuna kiwanja, au niseme shamba. Kuna shamba unalotaka kununua, si ndiyo?" nikamuuliza.
"Shamba?"
"Eee. Kuna shamba linamilikiwa na mwanamke fulani nje ya mkoa, najua unataka kulinunua mzee."
Akaniangalia, kisha akasema, "Kuna vitu vingi kampuni inanunua J. Kuna miradi inaendeshwa, na ndiyo... kuna viwanja au mashamba tunayo-target hapa au kule ili kujenga mambo yetu fasta. Be specific."
Sikuwa najua shamba la Mariam lilipokuwa kihususa, hivyo nikamwambia, "Hili shamba liko nje ya jiji. Mkoa mwingine. Kuna, mwakilishi wako... alimlipa mwanaume fulani pesa in advance ili akuhalalishie kulipata, lakini najua mpaka sasa hivi haujalipata na ulikuwa unataka kuangalia upande mwingine, ila... ndiyo unahitaji jamaa arudishe pesa zako kwanza maana kakucheleweshea. Si unaipata hiyo?"
Akaweka uso wa kutafakari kiasi, naye akasema, "Yeah. Unaongelea shamba la... lile lililo Morogoro la mwanamke fulani anaitwa... Mariam Constantine?"
Sikujua Constantine kuwa jina la pili la binti Mariam, lakini nikamwambia, "Yes! Huyo huyo."
"Ndiyo. Nimejaribu kulipata hilo shamba tokea wiki chache zilizopita ila napewa tu delay. Umejuaje kuhusu hilo?" akauliza.
"Mmiliki namfahamu, yupo huko huko Mbagala," nikamwambia.
"Ooh! Well that's good then. Sijui kwa nini hawa watu wangu wanakuwa slow kunikamilishia, ila aliyekuwa anawakilisha kunirasmishia hilo shamba ndiye anayetuzungusha. Kama utaweza kumleta huyo mtu tufanye makubaliano hapa hapa face to face tutaimaliza hii yote haraka...."
"A.. ha-hapana mzee. Yaani, mmiliki ni msichana mdogo, anayesimamia hiyo mali ni dada yake. Sasa...."
"Shida ni nini, J?" akanikatisha.
Nikatulia kidogo, kisha nikamwambia, "Nakuomba usifanye taratibu za kununua hilo shamba."
"Nini?"
"Ni kiwanja kwa ajili ya huyo msichana, ana... ana tatizo fulani ambalo... yaani dada yake ndiyo anamsimamia, na hakuwa... ameliweka market, ila... kaka yake ndiyo alifanya kama deceit kuliweka market, nyie mkafikiri..."
"J subiri, sikuelewi. Ongea ueleweke vizuri maana nachanganyikiwa," akanikatisha kwa kusema hivyo.
Nikashusha pumzi tu na kuangalia pembeni.
"Hautaki ninunue hilo shamba kwa sababu gani? Huo ni mradi wa kampuni, na nilikuwa nimeshatoa pesa nyingi. Watu ambao wanahusika ndiyo wanatakiwa kuniletea taarifa za ni nini kinaendelea, wewe... unahusika vipi, halafu uje useme nisilichukue?" akauliza hivyo.
Nikamwambia, "Iko hivi. Tuseme kwa mfano, wewe unataka kununua shamba ambalo ni la Jasmine, sawa? Unatuma mwakilishi akuletee huo mchongo. Huyo mwakilishi akimtafuta Jasmine, anakutana na mimi kaka yake, namwambia kwa sababu me ni wa familia moja na mmiliki, nitamrahisishia kulipata, kwa hiyo atoe tu hela halafu mimi nita-deliver. Wakati huo huo kumbe Jasmine hataki kuliuza shamba, halafu hajui kuhusu haya makubaliano ambayo me nimefanya na mwakilishi wako, afu' hizo hela nimekula. Sasa, nachokifanya ni kuamua kuunda mpango wa kumwondoa Jasmine, sawa? Yaani nimuue, halafu nihalalishe umiliki wa hiyo mali kwangu mimi mwenyewe, ili ndiyo niitoe kwa niliowauzia. Sijui umenielewa hapo?"
Mzee akawa ananiangalia kwa utulivu tu.
"Ndivyo ilivyo na hii hali mzee. Dada yake na huyo binti ndiyo msimamizi wa hilo shamba, hakuwa na habari kwamba kaka yake kakubali dili la kuliuza kwa mtu mwingine. Huyu jamaa alikuwa anajua dada yake asingekubali kuliuza, kwa hiyo akajaribu kumuua mdogo wao halafu ahamishe haki ya kulisimamia hilo shamba kwake yeye mwenyewe, ili ndiyo akupe wewe," nikamwambia hivyo.
"Are you serious?" akauliza kwa sauti makini.
"Kabisa. Ni juzi tu hapa ndiyo alikuwa amemteka huyo msichana ili amuue, lakini mapolisi wakamkamata mapema kabla hajafanikiwa. Tena hapa ndiyo nilikuwa nimetoka alikofungiwa, akaniambia sasa nyie ndiyo mnao... mnaolihitaji hilo shamba," nikaeleza.
Akashikanisha viganja vyake na kuegamiza mikono mezani, naye akasema, "Kwa hiyo unataka kusema kwamba wameniibia, si ndiyo?"
"A.. ah, siyo kihivyo, yaani... ni huyu jamaa. Familia yake, na huyu dada mwenye haki ya usimamizi wa hilo shamba hakujua lolote. Mpaka sasa navyoongea na wewe yaani hajui kama jitihada za kununua hilo shamba ni zako, kaka yake yuko rumande, kwa hiyo wanafikiri imeshaisha. Ila najua mwenye deni la pesa zako ni huyu jamaa, siyo familia yake, kwa hiyo ndiyo maana nikaona nije kukuambia ili kukuelewesha... namna mambo yalivyo," nikamwambia.
"Aisee! Kwa hiyo mwenye shamba haliuzi, aliyesema linauzwa yuko ndani, pesa kala na sijapata faida yoyote, ila ni hasara anayotakiwa alipie, lakini yuko jela kwa hiyo hataweza kulipa, si ndiyo?" akauliza hivyo.
Nikaangalia chini kiasi na kutikisa kichwa kukubali.
"Kwa hiyo huyo jamaa alikuwa amepanga kumuua mdogo wake ili alipate... halafu ndiyo atuuzie?" akauliza.
"Ndiyo. Na alikuwa karibu kufanikiwa," nikamjibu.
"Kwa nini afanye hivyo?"
"Ni mjinga tu. Alikuwa eti anaogopa kwamba mtamfanya kitu kibaya kwa sababu tayari alikuwa amekula hela mliyompa mwanzoni na kalenda ilikuwa imeisha."
"Aliyemwambia tutamfanya kitu kibaya hakukosea. Nimetoa pesa nyingi kama kianzio J, halafu aje tu kusema kala na dili limefeli? Asingekuwa ndani sasa hivi angenitambua," akaongea kwa kuudhika.
"Achana naye tu, hafai. Ingawa hivyo... sijui sasa kwa upande wa pesa zako ndo' inakuwaje," nikamwambia.
"Tutamtoa, auze hata figo zake zote, arudishe hizo pesa!" akaongea kwa mkazo.
"Mzee..."
"Usini-mzee mimi! J, tumetoa hela nyingi kama kianzio, sawa? Tena mimi personally ndiyo nilikuwa nahitaji hicho kiwanja, nataka nijenge ishu nzuri sana itakayoleta matokeo mazuri. Kampuni inapanuka vibaya mno sasa hivi, nasambaza upendo nchini kote kwa kujenga matawi, watu wanufaike na sisi tukue zaidi. Halafu uje tu useme niiachie hii ipite? Hela siyo ya kuchezea kiurahisi namna hiyo. You should know that," akaniambia hivyo kwa mkazo.
"Najua, ila usitoe mtu figo zake kurudisha hicho kilichopotea... siyo fresh. Lakini pia najua... ukiangalia na jinsi hali ilivyo... unahitaji alternative nyingine mzee," nikamwambia hivyo kwa upole.
"Ipi sasa, J?"
"Lazima itakuwepo tu. We' ndo' boss."
"Ahah... sikia. Pesa siyo zangu tu, zinahusika kwenye kampuni pia. Me ni boss wa ma-boss sita, lakini jua nina ma-boss watatu juu zaidi yangu. I answer to somebody too. Hapa siyo sehemu ya kusema milioni 5 ime-slip tu, hatujui imeenda wapi, halafu ah... ma-boss wapuuzie. Every penny matters. Ikiwa pesa niliyotoa kwa masilahi ya kampuni haitarudi on the deadline, inamaanisha niirudishe kwa kutoa kwenye ya kwangu mwenyewe. Hiyo inamaanisha nini J?"
Nikaangalia chini na kusema, "Hasara."
"Exactly. Kwa hiyo usifikiri nitaliachia kiurahisi tu. Kinachotakiwa... si umesema unamjua huyo mwanamke?"
"Ndiyo, lakini...."
"Nipe contact zake, nitazungumza naye moja kwa moja..."
"Sikia mzee, siyo rahisi kama hivyo. Yaani... hawezi akakupa hilo shamba..."
"Kwa nini asiweze? Sawa, naelewa hakujua, lakini hata me nimepoteza kitu fulani. Tena kikubwa. Look... nitaongea naye. Hata ukitaka, sitagusia pesa iliyopotea, lakini naweza nikamshawishi vizuri sana hadi akanipatia hiyo ishu. Nimekwambia niliilenga hiyo tokea muda, so... pamoja na haya yote ila bado naweza nika-fix something," akaniambia hivyo.
"Naelewa. Sema... sababu inayomfanya asikitoe kama kiwanja, ni mdogo wake. Huyo mdogo wake ndiyo Mariam, ni mgonjwa. Ninawajua hawa watu vizuri kwa sababu... me ndiyo namsaidia huyu binti ili apone..."
"Unamsaidia? Huko huko Mbagala?"
"Ndiyo."
"Ni mgonjwa wa nini?"
"Ana kitu... kiko kama ASD. Equivalent ya PTSD. Aliipata baada ya wazazi wao kufa kwenye ajali, na sasa hivi inaweza ikawa mbaya zaidi shauri ya mambo ambayo kaka yake amemfanyia hiyo juzi... ni hatari endapo kama ataachwa bila msaada unaomfaa yeye," nikaelezea.
"Na wewe ndiyo unampa huo msaada? Wakati huu huu wa mapumziko yako?"
"Ndiyo, ndiyo nilikutana nao huko. Dada yake anampenda sana, anamtunzia hilo shamba kwa ajili ya future akiwa na matumaini kwamba mdogo wake atapona ili aje kukimiliki yeye kama yeye, na kisha ajenge maisha yake kwa njia yoyote atakayoamua kutumia mali aliyoachiwa. Isingekuwa ya tamaa ya kaka yao, wala hata usingeingia kwenye hilo dili mzee, yaani siyo fair kwako kama ilivyo siyo fair kwao pia. Ni watu wazuri, wame... wamelaghaiwa tu. Nakuomba uangalie njia nyingine mzee. Ukitaka... nitasaidia kukutafutia shamba, au kiwanja sehemu fulani nyingine, but... nakuomba uangalie utaratibu wa kuliacha shamba la huyu binti. Tafadhali sana," nikaongea kwa hisia za wazi.
Mzee mkubwa akawa ananiangalia kwa ufikirio sana, huku akipiga-piga kidole chake kimoja mezani, kisha akasema, "Nina mambo mengi ya kufikiria J. Sikuwa nimetarajia uje uniletee na hili, kwa hiyo... hhh... anyway, nitaangalia cha kufanya ili tuepuke kuzunguka kwingi. Nitaongea na niliyemweka kufatilia hiyo ishu halafu tutaona."
"Asante sana. Nashukuru," nikamwambia hivyo kwa heshima.
"Huyo binti ana miaka mingapi?" akauliza.
"19. Anaelekea 20," nikamwambia.
"Kwa hiyo kaka yake akamteka halafu... akataka kumchinja, au?"
"Mara ya kwanza alitaka kumgonga na gari, akashindwa. Juzi ndo' ametuma watu wakamteka, wakataka na kumbaka kabisa halafu ndiyo wamuue," nikamwambia kwa hisia za hasira ya mbali.
"Na ni mdogo wake tumbo moja?"
"Baba mmoja, mama mmoja."
"Aisee! Huyo jamaa ni fala, eti?"
"Sana!" nikasema hivyo na kuvuta ulimi mdomoni kwa hasira kiasi.
Mzee akacheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Haya, sawa. We' nenda, me nakomaa na huu udambwi hapa."
Nikacheka kidogo kwa kupata ahueni, nami nikasimama huku nikisema, "Asante sana. Ukitaka kunijulisha au kuniuliza lolote, nishtue tu."
Akiwa ameshayarudia makaratasi yake tena, akasema, "Sawa, usijali. Tutawasiliana. Unaenda kupita nyumbani?"
"Ee, kuna sehemu naingia kwanza. Muda ukiruhusu nitapita kumwangalia Jas na mama, kama siyo... basi nitawapigia," nikamwambia hivyo.
"Haya, baadaye. Kuwa care huko," jamaa akaendelea na ubize wake.
Nikatoka sehemu hiyo ya ofisi na kuelekea nje hatimaye, nikiwa nahisi ahueni kidogo ndani ya moyo wangu. Najua ni mambo mengi ambayo JC sijaelezea kujihusu bado, lakini utapata nafasi nzuri tu ya kunijua kwa ubora zaidi. Huyo ndiyo alikuwa mdingi. Mdingi mwenye nazo, halafu alikuwa mshkaji sasa. Hadi neno fala alilijua!
Niliondoka kutoka jengoni hapo baada ya kuagana na secretary wake, mtoto Faima, nami nikaenda kutafuta daladala ambazo zingeelekea maeneo ya ile hoteli ya Royal Village ili nikamwone mamaa kibosile Bertha. Angalau nilikuwa na uhakika sasa kwenye suala la ishu ya shamba la Mariam, kwamba utatuzi ungefanywa bila kuwasumbua wanafamilia wale maana nilikuwa nimetafuta suluhisho kutoka kwenye meza kuu ya wahusika. Tena ni mhusika, na alikuwa ni mshua wangu.
Sikutaka tu Miryam asumbuliwe zaidi kwa makosa ambayo kaka yake alipaswa kuyalipia. Najua kama ingetokea mzee wangu akamwita yule mwanamke kumwambia kuhusu hasara yake, Miryam angeweza hata kujichanga kabisa ili ailipie wakati haikuwa yeye aliyeisababisha. Alikuwa na mambo mengi ya kuangalia hata hivyo, kwa hiyo niliona hili lingine lingekuwa la kumwongezea mzigo juu ya mizigo. Joshua alikuwa anamkosti sana yaani, basi tu.
Nimesema mzee wangu alikuwa mshkaji, ila kwenye masuala ya kampuni yake hakutakaga mchezo. Kiukweli, kama angetaka, hizo figo za Joshua zingeenda kunyofolewa na kuuzwa ili pesa yake irudi kweli, lakini hakuwa na ukatili wa aina hiyo, ni basi tu najua alikasirishwa na mambo kwenda kinyume na matarajio yake. Hivyo, ningepaswa kuwa tayari kwa lolote kutokea hapa ili likija niwe na njia ya kuliitikia kwa uharaka, na kufanya mambo yaendelee kuwa na amani kwa pande zote mbili.
Umakini wangu sasa ungetakiwa kuwa kwenye upande wa tatu; madam Bertha.
★★
Baada ya kuchukua daladala na kufika eneo lililo karibu na Royal Village Hotel, nikawa nimeshuka na kutambua kitu fulani ambacho sikuwahi kugundua. Yaani, kumbe mara zote nilipokuwa nakuja huku kutokea Mbagala, daladala ingepita usawa wa hoteli hiyo kabisa kabla ya kukunja kona kwenye eneo la Vunja Bei ili kuelekea stendi ya Makumbusho.
Ikiwa ningekuwa nimetambua hilo mapema basi kila mara nilipokuja huku ningekuwa tu nashukia hapo na kwenda hotelini kwa madam badala ya kupoteza gharama zile zote kulipia Uber. Dah! Ila sema tu haikuwahi kuniingia akilini maana sikuwaga natazama sana nje, lakini kwa wakati huu hilo lingebadilika.
Kwa hiyo nikaanza kutembea kuielekea hoteli, mida ikiwa ni saa sita mchana sasa kuelekea saba, jua likiwa kali mno, nami nikampigia madam Bertha. Akawa amepokea, ndiyo nikamwambia nilikuwa naelekea hapo hotelini kwake ili kukutana naye, na kumuuliza kama alikuwepo kwa muda huu. Kwa njia ya kistaarabu tu, akanijibu kuwa ndiyo alikuwepo, ila muda siyo mrefu angetoka hivyo niwahishe kufika la sivyo nisingemkuta. Nikamwambia niko nje ya jengo kabisa hivyo ni sasa hivi tu naingia huko kwake, ndipo nikakata simu.
Nilitaka kujua sasa ni yapi yaliyokuwa mapya kwa upande wa mwanamke huyu tokea mara ya mwisho tumeachana pale Uhasibu ile jana tukiwa tumeahidiana mimi kurudi kwake ili nianze kuishi naye. Haikuonekana kwamba alikasirika nilipomwambia kuwa kuna ishu iliyozuka na kufanya jambo hilo lishindikane, na ndiyo nilitaka kujua kwa nini. Sikujutia kuamua kubaki Mzinga ili niendelee kumsaidia Mariam, ila bado na upande wa Bertha nilitakiwa kuwa "active" sana kwa sababu nilitaka suala la kumkamatisha limalizike upesi.
Nikapanda mpaka huko ghorofani na kukifikia chumba chake, nami nikaugonga mlango na kusubiri. Kidogo tu ukafunguliwa, madam mwenyewe akiwa hapo mbele yangu huku ananiangalia kwa utulivu machoni. Mwonekano wake ulionyesha kwamba kweli alikuwa anaelekea kuondoka.
Alivalia T-shirt jeupe la mikono mirefu lenye kubana kama sweta, likiziba mpaka sehemu ya juu ya shingo yake, pamoja na suruali ya jeans ya blue iliyokoza yenye urembo wa kuchanika-chanika mbele ya mapaja yake, ikilibana vyema umbo lake kwa chini. Miguuni alivaa mabuti ya kike mekundu yenye muundo wenye vichuchumio virefu kwa nyuma, huku urembo wa hereni, mikufu, na pete za dhahabu ukimpendezesha hata zaidi.
"Umependeza," nikamwambia hivyo.
"And I'm just getting started. Ingia," akaniambia hivyo na kurudi ndani.
Nikatabasamu kiasi na kuingia pia, kisha nikaufunga mlango na kumfata. Alikuwa ameelekea upande wenye sofa na kuketi, nami nikaelekea hapo pia huku nikiona laptop ndogo kwenye kistuli cha manyoya karibu na sehemu aliyokaa, pamoja na mkoba sofani. Akaanza kubofya-bofya kompyuta hiyo.
"Umenunua laptop?" nikamuuliza nikiwa nimesimama.
"Ilikuwepo mbona? Hujawahi tu kuiona," akajibu bila kunitazama.
"Kuna mishe unaenda kupiga sa'hivi?" nikamuuliza.
"Yeah," akajibu tena, umakini wake ukiwa kwenye laptop.
Nikashusha pumzi kiasi, kisha nikasema, "Madam... najua... sijawa keen kwenye kutimiza ahadi niliyokupa, ila... ni kwamba tu nadili na mambo mengi sana yaani, sikuwa nimetarajia kabisa kwamba yangeongezeka kwa hiki kipindi ndiyo maana mishe zinakuwa zinaingiliana mno. Inabidi nikae kwa muda fulani kule kuangalia mahitaji ya yule msichana baada ya kilichompata ile juzi, so... kuja kukaa huku moja kwa moja itachukua muda..."
Akaendelea tu ku-type bila kunipa itikio lolote.
"Najua huelewi mengi ila ndiyo hali halisi ilivyo, yaani... inanihitaji. Hata huku ni muhimu pia, natamani sana niwe hapa muda wote na wewe, lakini kwa hilo itabidi tu unipe muda Bertha," nikamwambia hivyo.
Hakuniangalia hata mara moja, lakini akaweka kiganja chake sofani na kukipiga hapo mara mbili, ishara ya kuniambia kuwa nikae karibu yake. Nikatii na kusogea hapo, kisha nikakaa. Akawa akiendelea na jambo alilokuwa akilifanya kwenye laptop hiyo kwa sekunde chache, kisha akaifunga na kunigeukia. Yaani akapandisha mguu mmoja sofani kwa kuukunja na kulaza goti lake kwenye paja langu, naye akawa ananiangalia huku akitabasamu.
"Mambo yameiva! Tunaanza kazi muda siyo mrefu," akaniambia hivyo kwa shauku kiasi.
"Unamaanisha..."
"Nimeshapata spot tutakayotumia kuanzishia ile ishu yetu. Mahesabu tumeshafanya, watu wangu watakuwa tayari kuanza kazi pamoja nawe ukiwafundisha kuunda ile kitu, so business itakuwa underway baada ya muda mfupi tu. Njia tumeshasafishiwa so, let's get crackin'!" akaongea kwa njia ya furaha.
Bado sikuwa nimeelewa kwa asilimia zote, kwa hiyo nikamuuliza, "Umeshapata sehemu inayofaa tutakayotengenezea madawa?"
"Yeah. Wakati wewe ulipokuwa umeenda ku-solve hayo matatizo yako, me nikafanya hiyo ishu itiki fasta. Kila kitu kiko tayari. Kilichopo tu ni wewe kuanza kupika dawa, uwaelekeze na watu wangu, then... money," akasema hivyo.
Nikalazimisha tabasamu, kisha nikamwambia, "Well that was fast. Hongera."
"Usiseme hongera mpaka kazi ianze na ikamilike. Yaani HB hii kitu ikikubali haraka, nitauza sana! I can't wait. Najihisi kama bonge moja la mwekezaji wa shilingi mia tu kwenye business itakayozalisha milioni mia. This is going to be so lit!" akaongea kwa furaha.
"Kabisa. Ahah... ni vizuri mambo yameenda fresh, ila... bado ulikuwa hujanionyesha mtandao unavyokaa Bertha..."
"Ningekuonyesha vipi wakati unakaa tu kuzurura huko?"
Nikaangalia pembeni tu.
"Sikia. We' usiwaze kuhusu network yetu, utaijua tu. La muhimu sasa hivi ni hili. Nitakuweka hiyo sehemu ufanye miujiza yako, faida ije upesi. Hapa tutachoangalia ni nini vinahitajika kwa ajili ya miujiza yako ili uanze kupika, watu wangu wajifunze pia, mizigo ianze kujaza maghala. Tusichezee muda yaani," akasema hivyo.
Nikatikisa kichwa kukubaliana na hilo.
"Na usijali. Kila kitu kitakuwa kwa muda wake. Kama unakuwa unataka kwenda kumsaidia mdogo wako, sijui nani, unakuwa unaenda kwa muda fulani, lakini muda wa kazi unatakiwa uwe sehemu ya kazi. Ukizingua, umeharibu kila kitu... maana sasa hivi tunaenda kwa umakini sana," akasema hivyo.
Kiukweli, sikutegemea kabisa aseme maneno hayo, lakini nikamwambia, "Sawa. Ondoa shaka kabisa."
Akaniangalia kwa upendezi na kushusha pumzi kwa kuridhika.
"Ahah... madam, sikuwa nime... yaani, nilifikiri basi ningefika hapa nikakuta labda ume..."
"Nini? Nimenuna?" akanikatisha.
"Eeeh..."
"Kisa?"
"Si kama hivyo tulikuwa... nilikuwa nimeahidi kuja kukaa hapa, halafu...."
"Agh, wala hata usijali. Dili na mambo yako kwa muda ambao nitakupa, lakini mambo yangu pia utadili nayo kwa muda nitakaokupa. Nimeshaona siwezi kukuchukua kimoja, so... nimekubaliana na hilo tu," akasema hivyo.
"Mh? Kweli ni wewe madam?"
"Kwani me nikoje?"
"Siyo jinsi nilivyokuzoea. Kwa leo? Siyo jinsi nilivyokuzoea kabisa. Yaani nilifikiri ningefika hapa ukaanza kunirushia maneno na chupa ya chai au ndala kuuliza kwa nini nakuwa sieleweki..."
Bertha akacheka kidogo kwa furaha.
"Ni lazima niulize. Hii sudden change imetokana na nini?" nikamuuliza.
Akanishika sikioni na kuanza kulivuta-vuta kwa vidole vyake taratibu na kusema, "Basi tu. Nimejisikia kuwa generous kidogo. Au ni dhambi?"
"Siyo dhambi. Inafanya tu una... unapendeka zaidi," nikamwambia hivyo.
"Kumbe? Ndo' napendeka zaidi ya unavyonipenda?" akauliza hivyo kwa sauti ya chini.
"Yeah. Hata zaidi," nikamsemesha kwa njia ya utongozi.
"Well, endelea kuonyesha kwamba uko serious na mimi. Labda huo upendo utarudi kwa asilimia zote siku moja," akaongea kama vile ananitongoza yaani.
Nikatabasamu na kuuliza, "Nini kimekufanya umekuwa generous namna hii madam wangu?"
"Mhm... nilikutana na Festus, akaniambia mlivyoonana na kuzungumza," akasema hivyo.
Kauli yake ikanifanya nimtazame kwa njia makini kiasi.
"Mbona hukuniambia ulienda kwake?" akauliza.
"Aa... sikudhani alitaka, yaani..."
"Ndiyo, najua mambo yenu wanaume. Siyo lazima mpaka uniambie. Ila... mpaka Festus kukupeleka huko inaonyesha amekukubali sana," akasema hivyo.
"Kwa hiyo alikwambiaje?" nikamuuliza.
"Siyo mengi. Zaidi tu, jinsi ambavyo unafanya haya yote kwa sababu unampenda sana madam Bertha," akasema hivyo na kutabasamu.
Ahaa! Hapo sasa nikawa nimeelewa kwa nini madam alikuwa kwenye mood nzuri sana. Bila shaka Festo alimwambia kwamba ninampenda sana, na kutokana na jinsi alivyoaminiana na yule jamaa, nadhani maneno yaliyohusika huko kwenye maongezi yao ndiyo yalitosha kumfanya mwanamke huyu alegee namna hii kunielekea. Hapa udhaifu wake ukawa umeanza kuonekana wazi. Alihitaji kupendwa, na sasa ndiyo akawa ameona kuwa angekipata hicho kitu kutoka kwangu. Mchezo ukawa unaenda vizuri.
Nikatabasamu kiasi na kusema, "Dah! Kumbe jamaa na ye' naye mbea."
"Hahah... haongeagi ovyo, nilimlazimisha tu mpaka akaropoka. Nilifurahi tu kujua kwamba ulimaanisha yote uliyoniambia siku ile tuko bed. Umeanza kujiweka sehemu nzuri HB wangu. Keep it up," akaniambia hivyo kwa sauti tulivu lakini iliyoonyesha hisia.
Nikamshika shingoni kwake na kumkaribia usoni, kisha nikasema, "Chochote kwa ajili yako madam wangu."
Akatabasamu na kusema, "Mmm, usiwe cozy kupita kiasi. Bado unatakiwa uni-impress. Nilikwambia hili tako la gharama, unatakiwa kuendelea kupanda madaraja."
"Naelewa. Maneno hayatoshi. Ndiyo maana niko hapa. Nitajitahidi nisikuangushe," nikamwambia hivyo.
"That's my boy," akasema hivyo na kunirushia busu kwa ishara ya mdomo wake.
Nikatabasamu kiasi.
Akakaa vizuri zaidi na kusema, "Naelekea location kukutana na mtu. Mtumishi."
"Wa kilokole?" nikamuuliza.
"Yeah. Na yeye anahusika kupitisha madini. Naenda kumpanga," akasema hivyo huku akivuta mkoba wake.
"Dah! Kweli, Mungu walishagamwona kama boya," nikamwambia hivyo.
"Ahahah... ni kwa sababu ye' ni boya. Watumishi wake ndiyo wanahalalisha tu hilo," akasema hivyo.
"Ahahahah... ila Bertha!"
Akawa ametoa miwani yake ya urembo na kusema, "Me natoka sa'. Nakuacha hapa, au?"
"Oh no, naingia kule kitaa sa'hivi, labda nitarudi baadaye," nikamwambia.
"Poa."
Akasimama na kuvaa miwani yake, nami nikasimama pia.
"Vipi kuhusu... ile ishu ya Chalii, madam? Umemwangalia?" nikamuuliza.
Akatabasamu na kunishika shavu, naye akasema, "Usijali kuhusu Chaz. Hawezi kutusumbua. Sasa hivi utakuwa kwenye focus ya kazi yetu, basi. Umeelewa?"
Nikatikisa kichwa kukubali.
"Twende. Nitakupanga kuhusu spot yetu mpya ya kazi baadaye..."
Baada ya mwanamke huyu kuniambia hivyo, akanipita na kuelekea nje, huku nami nikifuata nyuma yake taratibu.
Mambo yalikuwa yanajijenga upesi sana, na hivyo nilielewa haingechukua muda mrefu kwa huu mchezo wangu na madam Bertha kufikia ukomo. Lakini kutokea hapa ningepaswa kuwa makini SANA, kwa sababu ni pande nyingi zilikuwa zikihusika. Kumwagusha Bertha kusingekuwa kwa ajili ya kumuumiza yeye tu, bali na watu wake wengi aliojihusisha nao. Naongelea na huyo Festo.
Jamaa alikuwa anajua yule, na nilihofia angeweza kuwa mvurugaji wa mpango wangu kwa muda wowote ule kwa sababu alikuwa makini sana, kwa hiyo mimi ningehitaji kuwa hatua mbili mbele zaidi yake badala ya kusubiri tu mambo yaje halafu ndiyo nitoe itikio. Ningetakiwa kuhakikisha kwamba Bertha akianguka, aende chini pamoja na Chalii Gonga na Festo pia, na wasiwe na njia ya kurudi juu tena. Muda ndiyo ungeongea.
★★
Nikawa nimepewa lifti na madam mpaka kufikia maeneo ya Uhasibu kama tu siku ya juzi, naye akaniachia hapo na kuendelea na safari yake ya kwenda kumwona "mtumishi" wa kupitisha madawa. Nilikuwa nataka kwenda nyumbani kwetu kule kwanza ili nikawasalimu mama yangu pamoja na dada yangu, lakini kutokana na Bertha kunishurutisha nipande gari lake ili anilete huku, nikaona nighairi kwa leo. Sikutaka aanze maswali ya naenda kwa nani na kuanza kufatilia mengine asiyojua kunihusu, na ambayo sikutaka ajue.
Kwa hiyo, nikapanda usafiri ili nielekee Rangi Tatu kisha Mzinga, na nikiwa njiani nikaamua kumpigia mama yangu. Tukasalimiana vizuri, akiwa anaendelea salama tu toka mara ya mwisho tumeongea kwa simu, ndiyo nikamuulizia na dada yangu pia, Jasmine. Akasema kwa sasa Jasmine alikuwa akiendelea vizuri tu na kusubiri muda wake wa kujifungua ufike, ila ndiyo hakuwa na raha sana kutokana na matatizo yaliyokuwa yamempata wiki chache zilizopita.
Hivyo, nikaamua kuagana na mama na kumwambia ningekuja kwenda kuwasalimia, lakini Jasmine ningempigia pia ili tuongee kwa kina. Akasema hamna shida. Nikatulia kwanza ili nimpigie dada yangu nikishafika pale kwa Ankia, maana sikuona busara yoyote kuongea naye kwa marefu nikiwa ndani ya daladala.
Nimekuja kufika Mzinga ikiwa ishaingia saa nane ya saa tisa huko, hapo njaa ikiwa imenikong'oli vibaya mno, na nilielewa kukosa mlo wa asubuhi mara kwa mara ingekuwa na madhara ikiwa ningeifanya kuwa zoea maana ndiyo mlo muhimu zaidi, kwa hiyo nikaelekea pale kwenye ule mgahawa niliokaa na Miryam jana ili kupata chakula kwanza, halafu ndiyo ningejitahidi kuiboresha upya ratiba yangu ya ulaji mzuri baadaye.
Ugali wa nguvu, nyama, marage, mchicha, na maziwa, aaah mzee nikala kama vile nimepikiwa na mke kabisa. Hali nzuri ya nguvu mwilini ikarudi mahala pake baada ya kuwa nimemaliza msosi, nami nikalipia na kuanza kuelekea majumbani kwa Ankia. Nilipopita usawa wa Masai nikawa nimemwona Bobo pia, nasi tukasimama na kupeana salamu na maongezi ya hapa na pale, kisha ndiyo nikaendelea na safari mpaka nilipokuwa naishi.
Nilipoingia ndani, sikumkuta Ankia, bila shaka akiwa ameondoka kama alivyoniambia asubuhi na kusema tungeonana jioni, kwa hiyo nikaingia chumbani na kuanza kubadili mavazi ili niingie kwenye nguo nyepesi kwanza, halafu nimpigie dada yangu, kisha niende kujimwagia na kujiweka fresh nikaonane na binti Mariam.
Nikavaa T-shirt nyepesi na bukta, halafu nikafungua droo moja niliyokuwa nimekiweka kile kifaa cha piano, kinanda, ambacho nilinunua wiki chache zilizopita kule Kariakoo kwa ajili ya Mariam. Niliona kuanzia wakati huu ndiyo ingekuwa muhimu kuanza kukitumia pamoja naye, nami nikakiweka kitandani kwanza, kisha nikavuta simu na kumpigia Jasmine.
Dada yangu huyu alikuwa mtu wa mambo mengi sana kama tu mimi kaka yake. Yaani hata wakati huu aliokuwa na mimba ya miezi saba huko bado alipenda kujishughulisha na mambo mengi sana kwa sababu alipenda kufanya kazi, lakini hata zaidi wakati huu ni ile tu kutaka maisha yaendelee baada ya tatizo lake na aliyekuwa mume wake kuwafanya waachane.
Alipopokea na kuanza kuongea nami, ikabidi nikae kitandani kabisa na kumsikiliza kwa umakini. Alikuwa mwanamke mwenye hisia kali na za karibu sana, kwa hiyo akaongea vitu na mambo mengi sana ili kunifanya nimwelewe kwa undani wa mambo yote aliyopitia. Nikampa pole na kumwambia kwamba ningekuja kuonana naye hapo hapo nyumbani ndani ya siku hizi hizi mbeleni, na kumshauri ale vyakula fulani kuilinda afya ya mtoto, na kujitahidi kupumzika vya kutosha.
Akawa hana neno, akisema tu alikuwa amenikosa sana, na nilipokuwa nataka kumwambia nimem-miss pia, nikasikia mlango wa kuingilia kule sebuleni ukigongwa kuashiria mgeni alikuwa amefika. Kwa hiyo nikaagana vizuri na Jasmine na kurudia kumwahidi kwenda kumwona, kisha ndiyo nikatoka kwenda kufungua mlango ili nimsikilize mja aliyefika.
Ile nafungua mlango nikiwa na uso makini tu, nikajikuta nauyeyusha umakini wote baada ya kuona ilikuwa ni bibie Miryam! Yaani huyu mwanamke alikuwa ananikamata nyakati ambazo sikumtarajia kabisa. Akaachia tabasamu hafifu la kirafiki, nami nikatabasamu pia.
"Za sa'hizi?"
Kasauti kake katamu kakanipa salamu hiyo laini, lakini sikutoa jibu na kubaki kumtazama tu machoni.
"Za sa'hizi kaka?" akarudia tena.
Nikavuta pumzi upesi na kusema, "Nzuri... ni nzuri. Karibu."
"Asante. Nimekuja tuongee mara moja, kama hauko na... kazi labda...."
"Oh, sina kazi yoyote, karibu. Ingia," nikamkaribisha.
Akavua ndala zake za kike na kunipita, nami nikaivuta harufu ya marashi iliyotoka mwilini mwake kwa umakusudi kabisa wa kuisikilizia. Alikuwa amevaa ile Punjabi yake ya zambarau, huku nywele zake ndefu akiwa amezibana juu ya kichwa. Zilikuwa lainiii, yaani dah! Kuziangalia nyuma ya shingo yake zilifanya nitamani hata kuzigusa na kuzilaza-laza kama manyoya ya mnyama kipenzi, lakini nikaachana na mawazo ya kishetani na kufunga mlango tu.
"Nimekuona wakati unaingia hapo nje, nikasema nije ili tuongee kidogo," akasema hivyo akiwa amesimama bado.
"Kumbe? Nimepita kama upepo yaani, hata sikukuona. Karibu ukae," nikamwambia hivyo.
Akakaa sofani huku akitabasamu kiasi, nami nikakaa pembeni yake pia. "Za mizunguko?" akauliza.
Huku nikiwa nasugua goti langu kwa kiganja, nikamwambia, "Nzuri tu. Nilienda Makumbusho hapo mara moja kuonana na rafiki, ndiyo nimeingia mida hii. Nilikuwa ndo' nataka nije kumwona Mamu. Yupo?"
Akatabasamu na kusema, "Yupo. Ndiyo amemaliza kula mida hii."
"Okay, itabidi nimwahi, maana najua anapendaga kulala mchana pia. Vipi dawa anazokunywa lakini?"
"Anaendelea kunywa. Hapendi sana dawa, inabidi kulazimisha... lakini zinaenda," akasema hivyo.
"Ahah... angalau. Na wewe... haujaenda kazini?"
"Nimeenda asubuhi, leo nimewahi tu kurudi. Nilikuwa nataka niwepo pia ukija, nilifikiri ningefika kukuta mmeshaanza, kwa hiyo... nafurahi nimewahi..."
"Sawa kabisa. Wote tukiwepo na kutoa support kama hivyo, itamzidishia hali ya uchangamfu na kujiamini zaidi. Mwishowe hiyo kitu itaondoka maishani mwake. Ni suala la muda tu," nikamwambia hivyo.
Akatikisa kichwa kukubali na kusema, "Yeah."
Akawa ameingiza mkono wake kwenye mfuko wa nguo yake ya juu na kutoa bahasha fupi iliyokunjwa na kisha kuielekeza kwangu, nami nikamtazama machoni.
Akasema, "Ninataka kushukuru kwa kusaidia kulipia bili ya Mamu kwenye ile hospitali ya mwanzo. Na ilikuwa kubwa, ulilipia dawa na vipimo vyote yaani... nimeona nikurudishie tu kwa sababu unafanya mambo mengi sana kwa ajili yetu. Asante sana, ila pokea tu hii. Itakuwa kama tulisaidiana wote... kulipia."
Nikabaki namwangalia tu kwa umakini. Ule umakini kwa makusudi yaani.
Akasema, "Acha kuniangalia hivyo bwana. Usifikirie vibaya, ni... shukrani tu."
Nikaendelea kumkazia macho.
"Wewe, jamani..." akaongea kwa njia iliyoonyesha hakupenda nilivyokuwa namwangalia.
Nikacheka kwa pumzi na kuangalia pembeni, kisha nikasema, "Inaonekana mpaka leo bado hujanielewa tu."
Akashusha macho yake kwa njia ya kukwazika kiasi.
Nikamwangalia na kusema, "Acha kufikiria kwamba unahitaji kunilipa Miryam. Nakuelewa. Ila sihitaji malipo, nimeshakwambia. Mamu... Mamu atapona. Ninachotaka kuona zaidi kuliko mambo yote ni Mamu akipona. Hayo ndiyo malipo nayotarajia, na yatafanikiwa kwa sababu wote tutashirikiana ili kumsaidia. Yakitimia, nitaridhika."
Akawa ananiangalia kwa utulivu tu.
"So... hiyo weka pembeni. Ukitaka itumie, we' itumie kwa mambo mengine tu, ila siyo mimi. Kofi ulilonitandika siku ile lilinitosha," nikamwambia hivyo kiutani.
Midomo yake ikajikunja akijaribu kuzuia tabasamu, lakini akashindwa na kuangalia chini huku akicheka. Alipendeza sana kiasi kwamba mpaka nikajikuta namtazama tu huku nikitabasamu kwa hisia.
Akaniangalia na kusema, "Sa' si ndiyo uchukue hii iwe kama pole?"
"A-ah, lile kofi lilikuwa zawadi, hujui hilo?"
"Kivipi?"
"Ndiyo liliniongezea moto mpaka tukafanikiwa kum-nab kaka yako. Kwa hiyo silalamiki, ninakushukuru," nikamwambia kwa uhakikisho.
Akaonekana kutafakari kitu, kisha akasema, "Nikuombe jambo fulani tafadhali."
"Ndiyo. Niambie..."
"Kuanzia wakati huu... sitotaka... yaani, usimwongelee tena huyo mwanaume. Hata tu kumwita kaka yangu... sitaki tena," akasema hivyo.
Nikamwangalia usoni kwa uelewa mpana wa kile alichomaanisha, nami nikamwambia, "Sawa. Nimeelewa."
"Nataka kuanzia sasa... kila kitu kiwe ni focus ya kumfurahisha mdogo wangu ili akae sawa zaidi. I'll contribute on anything required to help you help her," akasema hivyo.
"Wow! Tesha hakukosea. Unaongea kiingereza vizuri," nikamwambia hivyo.
Akatabasamu huku akinitazama kwa utulivu.
"Uko sahihi. Kikubwa sasa hivi itakuwa ni furaha ya Mamu, so mambo yote yenye kuvunja moyo yatatakiwa kutupwa bin... iwe kama hayajawahi kutokea. Mariam... ana-progress haraka sana, haitachukua muda mrefu atakuwa sawa kabisa," nikamwambia.
"Sawa. Ubarikiwe sana."
"Amen."
"Mhm... sasa hivi ndiyo nataka kwenda sambamba na kila kitu mtakachofanya ili nihusike kwa lolote, na... nijue naweza...."
"Miryam... usijali. Nimeshakuelewa," nikamwambia hivyo kwa kumtuliza.
Akatabasamu kiasi na kuangalia chini, nami nikawa namwangalia kwa upendezi. Yaani haka kahali kote kalikuwa kanafanya damu yangu irukeruke tu sijui hata kwa nini!
"Unajua sina namba yako?" akasema hivyo.
"Ih, kweli? Ahh hata me sina ya kwako mpaka leo..." nikamwambia hivyo.
Akasema, "Jamani! Yaani, utafikiri tulikuwa maadui..."
"Eti! Yaani hata namba tu?" nikamwambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo.
Akarudisha bahasha mfukoni na kutoa simu yake, naye akanipatia akiwa ameweka sehemu ya kuandikia namba huku akisema, "Sasa hivi mambo yatabadilika. Nataka tuwe marafiki."
Nilikuwa nimeshaanza kuandika namba yangu kwenye simu yake aliposema hivyo, nami nikawa natabasamu kiasi baada ya kusikia kauli yake ya kutaka tuwe marafiki. Nikamrudishia simu, naye akaipigia namba hiyo. Simu yangu ikaita, nikiwa napewa namba ya bibie Miryam rasmi kwa mara ya kwanza kabisa na yeye mwenyewe, nami nikaitunza kwa jina lake.
Nikamwangalia usoni kukuta ananitazama kwa utulivu, nami eti nikaingiwa na haya na kutazama pembeni kisha kutabasamu kidogo.
"Nini?" akauliza hivyo.
Nikatikisa kichwa kuonyesha hakuna kitu, kisha nikamwangalia tena.
"Mbona unatabasamu sana? Nini kimekufurahisha?" akaniuliza na sauti yake tamu.
"Sikuwahi kudhani... yaani, ungetaka tuwe marafiki. Nilikuwa nakuona wa kivyako mno, au labda unanichukulia kuwa siko..."
"Usiwaze hivyo tena. Hayo yamepita. Sisi ni marafiki sasa, sawa?" akanikatisha kwa kusema hivyo.
"Sawa. Lakini unajua nini?"
"Niambie."
"Toka tumejuana... sijawahi kukusikia ukilitaja jina langu," nikamwambia hivyo.
Akatabasamu huku akitazama pembeni.
"Yeah. Sijawahi kabisa. Huwa unaniita tu kaka, kijana, we' kaka... wewe..."
Akacheka kidogo kwa furaha.
"Tukiwa washka... ah, namaanisha, marafiki... nitapenda kusikia ukiniita kwa jina langu," nikamwambia hivyo huku nikitabasamu.
Akasema, "Haina shida. Nisamehe kwa kukuita hayo majina wakati huo, ila... sijawahi kutaja jina lako kwa sababu silijui."
Ka!
Kauli yake ikanifanya nimtazame kimaswali kiasi, nami nikamuuliza, "Hulijui jina langu?"
"Yeah," akajibu.
"Yaani... unatania, au? Maana, nakuja hapo kwako... unawasikia kabisa warembo wangu wanasema 'JC karibu,' 'JC za nyumbani?' 'JC hivi, JC vile...' halafu unaniambia hujui naitwa nani? Kweli Miryam?" nikamuuliza kwa kusuta.
Akacheka kidogo kwa pumzi na kusema, "Najua hilo siyo jina lako, hicho ni kifupi tu, ama nickname, kama wao wanavyoniita mimi 'Mimi!'"
Aliongea kwa njia ya masihara, lakini kauli yake ikanifanya nimtazame kwa njia makini kiasi.
"Nitapenda nikikuita kwa jina lako kabisa. Kama wewe unavyoniita 'Miryam,'" akasema hivyo.
Dah!
Nikaangalia tu chini kiasi nikiwa natabasamu. Bila kutambua, mwanamke huyu alikuwa amegusa sehemu fulani ya maisha yangu ambayo mpaka sasa bado sijaiweka wazi, na kauli yake ilifanya niikumbuke. Alinifanya nihisi raha ya kina sana, ile raha kama ya wimbo wa Bebe Rexha 'say my name.' Hehe! Hapa uhondo ndiyo ulikuwa umeanza.
Nikamwangalia usoni tena, naye akasema, "So... ukitaka nikuite kwa jina lako, niambie unaitwa nani."
Nikatabasamu kiasi, kisha nikamwambia, "Naitwa Jayden."
Akatabasamu pia, kisha akasema, "Jayden..."
Ah! Jina langu ndani ya hiyo sauti? Ilikuwa kama vile limeimbwa!
"Sawa. Me sitakuita JC. Nitakuita Jayden. Kama Jaden Smith," akasema hivyo.
"Ahahah... Tesha si amesema hauangaliagi movie, hilo jina umelijuaje?" nikamuuliza kiutani.
"Tesha anaongea mno, najua vitu vingi pia, siboi sana kama mnavyofikiria," akaniambia hivyo.
Nikatabasamu kwa hisia.
Akaninyooshea kiganja chake na kusema, "So Jayden... friends?"
Dah! Sikufikiria huyu dada angekuwa na uzungu mwingi namna hii, lakini ulimfaa, na alipendezea sana. Nikakishika kiganja chake pia na kuviunganisha kwa pamoja ili kukubali mwaliko wake wa kuwa marafiki rasmi.
"Friends," nikamwambia hivyo.
Tukaendelea kuangaliana kwa upendezi mwingi sana, nikiwa najihisi vizuri mno kupata ukaribu na mwanamke huyu baada ya misukosuko yote aliyopitia na familia yake siku chache nyuma. Nilitazamia mengi mazuri yaje kutokana na uhusiano huu mpya niliokuwa nimejipatia kwa huyu mwanamke, ambayo yangesaidia kumweka huru mdogo wake kutokana na tatizo alilokuwa nalo. Na kilikuwa ndiyo kitu nilichokitamani sana tokea siku ya kwanza kabisa nilipokutana naye.
Sasa huu ndiyo ungekuwa mwanzo wa mambo mengi ambayo yangebadili maisha yangu mimi, na Mimi.
END OF SEASON ONE
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
A Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Kazi, Tamaa, Hila, Usaliti, Siri, Mambo Yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Inashangaza kidogo, eh? Ndiyo. Huyu jamaa aliyekuwa kwenye dili la kununua shamba la Mariam kupitia wawakilishi wake waliompata Joshua kama dalali, alikuwa ni mzee wangu. Ni kitu ambacho sikuwa nimetarajia kabisa mpaka Joshua alipotaja jina lake muda mfupi nyuma kule kituoni, na ndiyo maana nilihisi labda kuna mambo mengi kwenye visa vyote vilivyokuwa vikitokea sasa yalionekana kuwa kama yamepangwa fulani hivi na majaaliwa.
Yaani kweli, ilipaswa tu kuwa mzee wangu akawa ndiyo mnunuzi wa hiyo mali mpaka kusababisha hayo mambo yote mabaya kutokea! Ila sidhani ikiwa alijua undani wa visa hivyo vyote, na ndiyo nilikuwa nimekuja kusahihisha mambo. Oh, na kuhusu JC kuwa kijana wa jamaa mwenye pesa namna hii ni suala ambalo tutaliongelea baadaye. Ikiwa baadaye itakuja!
Baada ya kuwa ameniambia nikaribie, nikakisogelea kiti kimoja karibu na meza yake na kisha kukaa.
"Imeshapita miezi miwili toka mara ya mwisho tumeonana, eti?" mzee akaniuliza hivyo.
"Ee, nafikiri," nikamjibu.
"Okay. Umenikuta niko bize, ila nambie. Kuna tatizo?" akauliza.
"Ee, naweza kusema ni tatizo. Kuna jambo nahitaji unisaidie kulisuluhisha," nikamwambia.
Akashusha pumzi kiasi kama kutoa uchovu wa kifikira, naye akasema, "Ni kuhusu ishu ya dada'ako?"
Sikutarajia hilo, hivyo nikasema, "Hapana. Kwa nini kwani? Jasmine ana tatizo lolote?"
"Hawajakwambia?"
Nikatikisa kichwa kukanusha.
"Labda hawajaona ni busara kukwambia, hata hivyo haikuwa..."
"No, mzee... niambie. Kilichonileta ni kitu tofauti, ila... niambie kwanza Jasmine ana tatizo gani. Amebakiza miezi michache ajifungue, si ndiyo?"
"Yeah, miezi miwili au mmoja na nusu."
"Shida ni nini?"
"Wameachana na mume wake," akaniambia hivyo.
Nikakunja uso kimaswali kiasi, nami nikaangalia pembeni.
"Wamekorofishana sana juzi hapo, ilikuwa ugomvi mkubwa over a petty misunderstanding, na unajua jinsi dada yako alivyo. Ilikuwa karibu apate miscarriage. Mimba ingetoka," akasema hivyo.
Nikawa nimeshangazwa na hili, nami nikauliza, "Ulikuwa ugomvi... yaani, huyo jamaa wake alifanyaje, alimpiga au?"
"Hamna, walirushiana maneno tu. Huyo Kevin akaondoka zake, ndo' dada'ako akapata mshtuko. Ila walimpeleka hospital, sa'hivi yuko vizuri tu."
"Yuko wapi sasa hivi?"
"Yupo nyumbani. Imebidi akae na mama yenu mpaka akijifungua."
"Dah! Siyo poa. Itabidi nije niende kumwona," nikamwambia.
"Labda waliona wasikwambie ili wasikuharibie likizo yako. Kwanza umeenda wapi kwenye hiyo fungate lonesome?" akaniuliza hivyo.
Nikatabasamu kiasi na kusema, "Niko Mbagala."
"Kule nyuma kwenye jalala?" akauliza kiutani.
"Ahahahah... pazuri siku hizi, siyo kama Mondi alivyopaacha," nikamwambia.
"Okay, sawa. Niambie sa' ishu ni nini kama siyo Jas," akasema hivyo huku akiangalia karatasi moja mezani.
"Yeah, aa... kuna kiwanja, au niseme shamba. Kuna shamba unalotaka kununua, si ndiyo?" nikamuuliza.
"Shamba?"
"Eee. Kuna shamba linamilikiwa na mwanamke fulani nje ya mkoa, najua unataka kulinunua mzee."
Akaniangalia, kisha akasema, "Kuna vitu vingi kampuni inanunua J. Kuna miradi inaendeshwa, na ndiyo... kuna viwanja au mashamba tunayo-target hapa au kule ili kujenga mambo yetu fasta. Be specific."
Sikuwa najua shamba la Mariam lilipokuwa kihususa, hivyo nikamwambia, "Hili shamba liko nje ya jiji. Mkoa mwingine. Kuna, mwakilishi wako... alimlipa mwanaume fulani pesa in advance ili akuhalalishie kulipata, lakini najua mpaka sasa hivi haujalipata na ulikuwa unataka kuangalia upande mwingine, ila... ndiyo unahitaji jamaa arudishe pesa zako kwanza maana kakucheleweshea. Si unaipata hiyo?"
Akaweka uso wa kutafakari kiasi, naye akasema, "Yeah. Unaongelea shamba la... lile lililo Morogoro la mwanamke fulani anaitwa... Mariam Constantine?"
Sikujua Constantine kuwa jina la pili la binti Mariam, lakini nikamwambia, "Yes! Huyo huyo."
"Ndiyo. Nimejaribu kulipata hilo shamba tokea wiki chache zilizopita ila napewa tu delay. Umejuaje kuhusu hilo?" akauliza.
"Mmiliki namfahamu, yupo huko huko Mbagala," nikamwambia.
"Ooh! Well that's good then. Sijui kwa nini hawa watu wangu wanakuwa slow kunikamilishia, ila aliyekuwa anawakilisha kunirasmishia hilo shamba ndiye anayetuzungusha. Kama utaweza kumleta huyo mtu tufanye makubaliano hapa hapa face to face tutaimaliza hii yote haraka...."
"A.. ha-hapana mzee. Yaani, mmiliki ni msichana mdogo, anayesimamia hiyo mali ni dada yake. Sasa...."
"Shida ni nini, J?" akanikatisha.
Nikatulia kidogo, kisha nikamwambia, "Nakuomba usifanye taratibu za kununua hilo shamba."
"Nini?"
"Ni kiwanja kwa ajili ya huyo msichana, ana... ana tatizo fulani ambalo... yaani dada yake ndiyo anamsimamia, na hakuwa... ameliweka market, ila... kaka yake ndiyo alifanya kama deceit kuliweka market, nyie mkafikiri..."
"J subiri, sikuelewi. Ongea ueleweke vizuri maana nachanganyikiwa," akanikatisha kwa kusema hivyo.
Nikashusha pumzi tu na kuangalia pembeni.
"Hautaki ninunue hilo shamba kwa sababu gani? Huo ni mradi wa kampuni, na nilikuwa nimeshatoa pesa nyingi. Watu ambao wanahusika ndiyo wanatakiwa kuniletea taarifa za ni nini kinaendelea, wewe... unahusika vipi, halafu uje useme nisilichukue?" akauliza hivyo.
Nikamwambia, "Iko hivi. Tuseme kwa mfano, wewe unataka kununua shamba ambalo ni la Jasmine, sawa? Unatuma mwakilishi akuletee huo mchongo. Huyo mwakilishi akimtafuta Jasmine, anakutana na mimi kaka yake, namwambia kwa sababu me ni wa familia moja na mmiliki, nitamrahisishia kulipata, kwa hiyo atoe tu hela halafu mimi nita-deliver. Wakati huo huo kumbe Jasmine hataki kuliuza shamba, halafu hajui kuhusu haya makubaliano ambayo me nimefanya na mwakilishi wako, afu' hizo hela nimekula. Sasa, nachokifanya ni kuamua kuunda mpango wa kumwondoa Jasmine, sawa? Yaani nimuue, halafu nihalalishe umiliki wa hiyo mali kwangu mimi mwenyewe, ili ndiyo niitoe kwa niliowauzia. Sijui umenielewa hapo?"
Mzee akawa ananiangalia kwa utulivu tu.
"Ndivyo ilivyo na hii hali mzee. Dada yake na huyo binti ndiyo msimamizi wa hilo shamba, hakuwa na habari kwamba kaka yake kakubali dili la kuliuza kwa mtu mwingine. Huyu jamaa alikuwa anajua dada yake asingekubali kuliuza, kwa hiyo akajaribu kumuua mdogo wao halafu ahamishe haki ya kulisimamia hilo shamba kwake yeye mwenyewe, ili ndiyo akupe wewe," nikamwambia hivyo.
"Are you serious?" akauliza kwa sauti makini.
"Kabisa. Ni juzi tu hapa ndiyo alikuwa amemteka huyo msichana ili amuue, lakini mapolisi wakamkamata mapema kabla hajafanikiwa. Tena hapa ndiyo nilikuwa nimetoka alikofungiwa, akaniambia sasa nyie ndiyo mnao... mnaolihitaji hilo shamba," nikaeleza.
Akashikanisha viganja vyake na kuegamiza mikono mezani, naye akasema, "Kwa hiyo unataka kusema kwamba wameniibia, si ndiyo?"
"A.. ah, siyo kihivyo, yaani... ni huyu jamaa. Familia yake, na huyu dada mwenye haki ya usimamizi wa hilo shamba hakujua lolote. Mpaka sasa navyoongea na wewe yaani hajui kama jitihada za kununua hilo shamba ni zako, kaka yake yuko rumande, kwa hiyo wanafikiri imeshaisha. Ila najua mwenye deni la pesa zako ni huyu jamaa, siyo familia yake, kwa hiyo ndiyo maana nikaona nije kukuambia ili kukuelewesha... namna mambo yalivyo," nikamwambia.
"Aisee! Kwa hiyo mwenye shamba haliuzi, aliyesema linauzwa yuko ndani, pesa kala na sijapata faida yoyote, ila ni hasara anayotakiwa alipie, lakini yuko jela kwa hiyo hataweza kulipa, si ndiyo?" akauliza hivyo.
Nikaangalia chini kiasi na kutikisa kichwa kukubali.
"Kwa hiyo huyo jamaa alikuwa amepanga kumuua mdogo wake ili alipate... halafu ndiyo atuuzie?" akauliza.
"Ndiyo. Na alikuwa karibu kufanikiwa," nikamjibu.
"Kwa nini afanye hivyo?"
"Ni mjinga tu. Alikuwa eti anaogopa kwamba mtamfanya kitu kibaya kwa sababu tayari alikuwa amekula hela mliyompa mwanzoni na kalenda ilikuwa imeisha."
"Aliyemwambia tutamfanya kitu kibaya hakukosea. Nimetoa pesa nyingi kama kianzio J, halafu aje tu kusema kala na dili limefeli? Asingekuwa ndani sasa hivi angenitambua," akaongea kwa kuudhika.
"Achana naye tu, hafai. Ingawa hivyo... sijui sasa kwa upande wa pesa zako ndo' inakuwaje," nikamwambia.
"Tutamtoa, auze hata figo zake zote, arudishe hizo pesa!" akaongea kwa mkazo.
"Mzee..."
"Usini-mzee mimi! J, tumetoa hela nyingi kama kianzio, sawa? Tena mimi personally ndiyo nilikuwa nahitaji hicho kiwanja, nataka nijenge ishu nzuri sana itakayoleta matokeo mazuri. Kampuni inapanuka vibaya mno sasa hivi, nasambaza upendo nchini kote kwa kujenga matawi, watu wanufaike na sisi tukue zaidi. Halafu uje tu useme niiachie hii ipite? Hela siyo ya kuchezea kiurahisi namna hiyo. You should know that," akaniambia hivyo kwa mkazo.
"Najua, ila usitoe mtu figo zake kurudisha hicho kilichopotea... siyo fresh. Lakini pia najua... ukiangalia na jinsi hali ilivyo... unahitaji alternative nyingine mzee," nikamwambia hivyo kwa upole.
"Ipi sasa, J?"
"Lazima itakuwepo tu. We' ndo' boss."
"Ahah... sikia. Pesa siyo zangu tu, zinahusika kwenye kampuni pia. Me ni boss wa ma-boss sita, lakini jua nina ma-boss watatu juu zaidi yangu. I answer to somebody too. Hapa siyo sehemu ya kusema milioni 5 ime-slip tu, hatujui imeenda wapi, halafu ah... ma-boss wapuuzie. Every penny matters. Ikiwa pesa niliyotoa kwa masilahi ya kampuni haitarudi on the deadline, inamaanisha niirudishe kwa kutoa kwenye ya kwangu mwenyewe. Hiyo inamaanisha nini J?"
Nikaangalia chini na kusema, "Hasara."
"Exactly. Kwa hiyo usifikiri nitaliachia kiurahisi tu. Kinachotakiwa... si umesema unamjua huyo mwanamke?"
"Ndiyo, lakini...."
"Nipe contact zake, nitazungumza naye moja kwa moja..."
"Sikia mzee, siyo rahisi kama hivyo. Yaani... hawezi akakupa hilo shamba..."
"Kwa nini asiweze? Sawa, naelewa hakujua, lakini hata me nimepoteza kitu fulani. Tena kikubwa. Look... nitaongea naye. Hata ukitaka, sitagusia pesa iliyopotea, lakini naweza nikamshawishi vizuri sana hadi akanipatia hiyo ishu. Nimekwambia niliilenga hiyo tokea muda, so... pamoja na haya yote ila bado naweza nika-fix something," akaniambia hivyo.
"Naelewa. Sema... sababu inayomfanya asikitoe kama kiwanja, ni mdogo wake. Huyo mdogo wake ndiyo Mariam, ni mgonjwa. Ninawajua hawa watu vizuri kwa sababu... me ndiyo namsaidia huyu binti ili apone..."
"Unamsaidia? Huko huko Mbagala?"
"Ndiyo."
"Ni mgonjwa wa nini?"
"Ana kitu... kiko kama ASD. Equivalent ya PTSD. Aliipata baada ya wazazi wao kufa kwenye ajali, na sasa hivi inaweza ikawa mbaya zaidi shauri ya mambo ambayo kaka yake amemfanyia hiyo juzi... ni hatari endapo kama ataachwa bila msaada unaomfaa yeye," nikaelezea.
"Na wewe ndiyo unampa huo msaada? Wakati huu huu wa mapumziko yako?"
"Ndiyo, ndiyo nilikutana nao huko. Dada yake anampenda sana, anamtunzia hilo shamba kwa ajili ya future akiwa na matumaini kwamba mdogo wake atapona ili aje kukimiliki yeye kama yeye, na kisha ajenge maisha yake kwa njia yoyote atakayoamua kutumia mali aliyoachiwa. Isingekuwa ya tamaa ya kaka yao, wala hata usingeingia kwenye hilo dili mzee, yaani siyo fair kwako kama ilivyo siyo fair kwao pia. Ni watu wazuri, wame... wamelaghaiwa tu. Nakuomba uangalie njia nyingine mzee. Ukitaka... nitasaidia kukutafutia shamba, au kiwanja sehemu fulani nyingine, but... nakuomba uangalie utaratibu wa kuliacha shamba la huyu binti. Tafadhali sana," nikaongea kwa hisia za wazi.
Mzee mkubwa akawa ananiangalia kwa ufikirio sana, huku akipiga-piga kidole chake kimoja mezani, kisha akasema, "Nina mambo mengi ya kufikiria J. Sikuwa nimetarajia uje uniletee na hili, kwa hiyo... hhh... anyway, nitaangalia cha kufanya ili tuepuke kuzunguka kwingi. Nitaongea na niliyemweka kufatilia hiyo ishu halafu tutaona."
"Asante sana. Nashukuru," nikamwambia hivyo kwa heshima.
"Huyo binti ana miaka mingapi?" akauliza.
"19. Anaelekea 20," nikamwambia.
"Kwa hiyo kaka yake akamteka halafu... akataka kumchinja, au?"
"Mara ya kwanza alitaka kumgonga na gari, akashindwa. Juzi ndo' ametuma watu wakamteka, wakataka na kumbaka kabisa halafu ndiyo wamuue," nikamwambia kwa hisia za hasira ya mbali.
"Na ni mdogo wake tumbo moja?"
"Baba mmoja, mama mmoja."
"Aisee! Huyo jamaa ni fala, eti?"
"Sana!" nikasema hivyo na kuvuta ulimi mdomoni kwa hasira kiasi.
Mzee akacheka kidogo kwa pumzi, naye akasema, "Haya, sawa. We' nenda, me nakomaa na huu udambwi hapa."
Nikacheka kidogo kwa kupata ahueni, nami nikasimama huku nikisema, "Asante sana. Ukitaka kunijulisha au kuniuliza lolote, nishtue tu."
Akiwa ameshayarudia makaratasi yake tena, akasema, "Sawa, usijali. Tutawasiliana. Unaenda kupita nyumbani?"
"Ee, kuna sehemu naingia kwanza. Muda ukiruhusu nitapita kumwangalia Jas na mama, kama siyo... basi nitawapigia," nikamwambia hivyo.
"Haya, baadaye. Kuwa care huko," jamaa akaendelea na ubize wake.
Nikatoka sehemu hiyo ya ofisi na kuelekea nje hatimaye, nikiwa nahisi ahueni kidogo ndani ya moyo wangu. Najua ni mambo mengi ambayo JC sijaelezea kujihusu bado, lakini utapata nafasi nzuri tu ya kunijua kwa ubora zaidi. Huyo ndiyo alikuwa mdingi. Mdingi mwenye nazo, halafu alikuwa mshkaji sasa. Hadi neno fala alilijua!
Niliondoka kutoka jengoni hapo baada ya kuagana na secretary wake, mtoto Faima, nami nikaenda kutafuta daladala ambazo zingeelekea maeneo ya ile hoteli ya Royal Village ili nikamwone mamaa kibosile Bertha. Angalau nilikuwa na uhakika sasa kwenye suala la ishu ya shamba la Mariam, kwamba utatuzi ungefanywa bila kuwasumbua wanafamilia wale maana nilikuwa nimetafuta suluhisho kutoka kwenye meza kuu ya wahusika. Tena ni mhusika, na alikuwa ni mshua wangu.
Sikutaka tu Miryam asumbuliwe zaidi kwa makosa ambayo kaka yake alipaswa kuyalipia. Najua kama ingetokea mzee wangu akamwita yule mwanamke kumwambia kuhusu hasara yake, Miryam angeweza hata kujichanga kabisa ili ailipie wakati haikuwa yeye aliyeisababisha. Alikuwa na mambo mengi ya kuangalia hata hivyo, kwa hiyo niliona hili lingine lingekuwa la kumwongezea mzigo juu ya mizigo. Joshua alikuwa anamkosti sana yaani, basi tu.
Nimesema mzee wangu alikuwa mshkaji, ila kwenye masuala ya kampuni yake hakutakaga mchezo. Kiukweli, kama angetaka, hizo figo za Joshua zingeenda kunyofolewa na kuuzwa ili pesa yake irudi kweli, lakini hakuwa na ukatili wa aina hiyo, ni basi tu najua alikasirishwa na mambo kwenda kinyume na matarajio yake. Hivyo, ningepaswa kuwa tayari kwa lolote kutokea hapa ili likija niwe na njia ya kuliitikia kwa uharaka, na kufanya mambo yaendelee kuwa na amani kwa pande zote mbili.
Umakini wangu sasa ungetakiwa kuwa kwenye upande wa tatu; madam Bertha.
★★
Baada ya kuchukua daladala na kufika eneo lililo karibu na Royal Village Hotel, nikawa nimeshuka na kutambua kitu fulani ambacho sikuwahi kugundua. Yaani, kumbe mara zote nilipokuwa nakuja huku kutokea Mbagala, daladala ingepita usawa wa hoteli hiyo kabisa kabla ya kukunja kona kwenye eneo la Vunja Bei ili kuelekea stendi ya Makumbusho.
Ikiwa ningekuwa nimetambua hilo mapema basi kila mara nilipokuja huku ningekuwa tu nashukia hapo na kwenda hotelini kwa madam badala ya kupoteza gharama zile zote kulipia Uber. Dah! Ila sema tu haikuwahi kuniingia akilini maana sikuwaga natazama sana nje, lakini kwa wakati huu hilo lingebadilika.
Kwa hiyo nikaanza kutembea kuielekea hoteli, mida ikiwa ni saa sita mchana sasa kuelekea saba, jua likiwa kali mno, nami nikampigia madam Bertha. Akawa amepokea, ndiyo nikamwambia nilikuwa naelekea hapo hotelini kwake ili kukutana naye, na kumuuliza kama alikuwepo kwa muda huu. Kwa njia ya kistaarabu tu, akanijibu kuwa ndiyo alikuwepo, ila muda siyo mrefu angetoka hivyo niwahishe kufika la sivyo nisingemkuta. Nikamwambia niko nje ya jengo kabisa hivyo ni sasa hivi tu naingia huko kwake, ndipo nikakata simu.
Nilitaka kujua sasa ni yapi yaliyokuwa mapya kwa upande wa mwanamke huyu tokea mara ya mwisho tumeachana pale Uhasibu ile jana tukiwa tumeahidiana mimi kurudi kwake ili nianze kuishi naye. Haikuonekana kwamba alikasirika nilipomwambia kuwa kuna ishu iliyozuka na kufanya jambo hilo lishindikane, na ndiyo nilitaka kujua kwa nini. Sikujutia kuamua kubaki Mzinga ili niendelee kumsaidia Mariam, ila bado na upande wa Bertha nilitakiwa kuwa "active" sana kwa sababu nilitaka suala la kumkamatisha limalizike upesi.
Nikapanda mpaka huko ghorofani na kukifikia chumba chake, nami nikaugonga mlango na kusubiri. Kidogo tu ukafunguliwa, madam mwenyewe akiwa hapo mbele yangu huku ananiangalia kwa utulivu machoni. Mwonekano wake ulionyesha kwamba kweli alikuwa anaelekea kuondoka.
Alivalia T-shirt jeupe la mikono mirefu lenye kubana kama sweta, likiziba mpaka sehemu ya juu ya shingo yake, pamoja na suruali ya jeans ya blue iliyokoza yenye urembo wa kuchanika-chanika mbele ya mapaja yake, ikilibana vyema umbo lake kwa chini. Miguuni alivaa mabuti ya kike mekundu yenye muundo wenye vichuchumio virefu kwa nyuma, huku urembo wa hereni, mikufu, na pete za dhahabu ukimpendezesha hata zaidi.
"Umependeza," nikamwambia hivyo.
"And I'm just getting started. Ingia," akaniambia hivyo na kurudi ndani.
Nikatabasamu kiasi na kuingia pia, kisha nikaufunga mlango na kumfata. Alikuwa ameelekea upande wenye sofa na kuketi, nami nikaelekea hapo pia huku nikiona laptop ndogo kwenye kistuli cha manyoya karibu na sehemu aliyokaa, pamoja na mkoba sofani. Akaanza kubofya-bofya kompyuta hiyo.
"Umenunua laptop?" nikamuuliza nikiwa nimesimama.
"Ilikuwepo mbona? Hujawahi tu kuiona," akajibu bila kunitazama.
"Kuna mishe unaenda kupiga sa'hivi?" nikamuuliza.
"Yeah," akajibu tena, umakini wake ukiwa kwenye laptop.
Nikashusha pumzi kiasi, kisha nikasema, "Madam... najua... sijawa keen kwenye kutimiza ahadi niliyokupa, ila... ni kwamba tu nadili na mambo mengi sana yaani, sikuwa nimetarajia kabisa kwamba yangeongezeka kwa hiki kipindi ndiyo maana mishe zinakuwa zinaingiliana mno. Inabidi nikae kwa muda fulani kule kuangalia mahitaji ya yule msichana baada ya kilichompata ile juzi, so... kuja kukaa huku moja kwa moja itachukua muda..."
Akaendelea tu ku-type bila kunipa itikio lolote.
"Najua huelewi mengi ila ndiyo hali halisi ilivyo, yaani... inanihitaji. Hata huku ni muhimu pia, natamani sana niwe hapa muda wote na wewe, lakini kwa hilo itabidi tu unipe muda Bertha," nikamwambia hivyo.
Hakuniangalia hata mara moja, lakini akaweka kiganja chake sofani na kukipiga hapo mara mbili, ishara ya kuniambia kuwa nikae karibu yake. Nikatii na kusogea hapo, kisha nikakaa. Akawa akiendelea na jambo alilokuwa akilifanya kwenye laptop hiyo kwa sekunde chache, kisha akaifunga na kunigeukia. Yaani akapandisha mguu mmoja sofani kwa kuukunja na kulaza goti lake kwenye paja langu, naye akawa ananiangalia huku akitabasamu.
"Mambo yameiva! Tunaanza kazi muda siyo mrefu," akaniambia hivyo kwa shauku kiasi.
"Unamaanisha..."
"Nimeshapata spot tutakayotumia kuanzishia ile ishu yetu. Mahesabu tumeshafanya, watu wangu watakuwa tayari kuanza kazi pamoja nawe ukiwafundisha kuunda ile kitu, so business itakuwa underway baada ya muda mfupi tu. Njia tumeshasafishiwa so, let's get crackin'!" akaongea kwa njia ya furaha.
Bado sikuwa nimeelewa kwa asilimia zote, kwa hiyo nikamuuliza, "Umeshapata sehemu inayofaa tutakayotengenezea madawa?"
"Yeah. Wakati wewe ulipokuwa umeenda ku-solve hayo matatizo yako, me nikafanya hiyo ishu itiki fasta. Kila kitu kiko tayari. Kilichopo tu ni wewe kuanza kupika dawa, uwaelekeze na watu wangu, then... money," akasema hivyo.
Nikalazimisha tabasamu, kisha nikamwambia, "Well that was fast. Hongera."
"Usiseme hongera mpaka kazi ianze na ikamilike. Yaani HB hii kitu ikikubali haraka, nitauza sana! I can't wait. Najihisi kama bonge moja la mwekezaji wa shilingi mia tu kwenye business itakayozalisha milioni mia. This is going to be so lit!" akaongea kwa furaha.
"Kabisa. Ahah... ni vizuri mambo yameenda fresh, ila... bado ulikuwa hujanionyesha mtandao unavyokaa Bertha..."
"Ningekuonyesha vipi wakati unakaa tu kuzurura huko?"
Nikaangalia pembeni tu.
"Sikia. We' usiwaze kuhusu network yetu, utaijua tu. La muhimu sasa hivi ni hili. Nitakuweka hiyo sehemu ufanye miujiza yako, faida ije upesi. Hapa tutachoangalia ni nini vinahitajika kwa ajili ya miujiza yako ili uanze kupika, watu wangu wajifunze pia, mizigo ianze kujaza maghala. Tusichezee muda yaani," akasema hivyo.
Nikatikisa kichwa kukubaliana na hilo.
"Na usijali. Kila kitu kitakuwa kwa muda wake. Kama unakuwa unataka kwenda kumsaidia mdogo wako, sijui nani, unakuwa unaenda kwa muda fulani, lakini muda wa kazi unatakiwa uwe sehemu ya kazi. Ukizingua, umeharibu kila kitu... maana sasa hivi tunaenda kwa umakini sana," akasema hivyo.
Kiukweli, sikutegemea kabisa aseme maneno hayo, lakini nikamwambia, "Sawa. Ondoa shaka kabisa."
Akaniangalia kwa upendezi na kushusha pumzi kwa kuridhika.
"Ahah... madam, sikuwa nime... yaani, nilifikiri basi ningefika hapa nikakuta labda ume..."
"Nini? Nimenuna?" akanikatisha.
"Eeeh..."
"Kisa?"
"Si kama hivyo tulikuwa... nilikuwa nimeahidi kuja kukaa hapa, halafu...."
"Agh, wala hata usijali. Dili na mambo yako kwa muda ambao nitakupa, lakini mambo yangu pia utadili nayo kwa muda nitakaokupa. Nimeshaona siwezi kukuchukua kimoja, so... nimekubaliana na hilo tu," akasema hivyo.
"Mh? Kweli ni wewe madam?"
"Kwani me nikoje?"
"Siyo jinsi nilivyokuzoea. Kwa leo? Siyo jinsi nilivyokuzoea kabisa. Yaani nilifikiri ningefika hapa ukaanza kunirushia maneno na chupa ya chai au ndala kuuliza kwa nini nakuwa sieleweki..."
Bertha akacheka kidogo kwa furaha.
"Ni lazima niulize. Hii sudden change imetokana na nini?" nikamuuliza.
Akanishika sikioni na kuanza kulivuta-vuta kwa vidole vyake taratibu na kusema, "Basi tu. Nimejisikia kuwa generous kidogo. Au ni dhambi?"
"Siyo dhambi. Inafanya tu una... unapendeka zaidi," nikamwambia hivyo.
"Kumbe? Ndo' napendeka zaidi ya unavyonipenda?" akauliza hivyo kwa sauti ya chini.
"Yeah. Hata zaidi," nikamsemesha kwa njia ya utongozi.
"Well, endelea kuonyesha kwamba uko serious na mimi. Labda huo upendo utarudi kwa asilimia zote siku moja," akaongea kama vile ananitongoza yaani.
Nikatabasamu na kuuliza, "Nini kimekufanya umekuwa generous namna hii madam wangu?"
"Mhm... nilikutana na Festus, akaniambia mlivyoonana na kuzungumza," akasema hivyo.
Kauli yake ikanifanya nimtazame kwa njia makini kiasi.
"Mbona hukuniambia ulienda kwake?" akauliza.
"Aa... sikudhani alitaka, yaani..."
"Ndiyo, najua mambo yenu wanaume. Siyo lazima mpaka uniambie. Ila... mpaka Festus kukupeleka huko inaonyesha amekukubali sana," akasema hivyo.
"Kwa hiyo alikwambiaje?" nikamuuliza.
"Siyo mengi. Zaidi tu, jinsi ambavyo unafanya haya yote kwa sababu unampenda sana madam Bertha," akasema hivyo na kutabasamu.
Ahaa! Hapo sasa nikawa nimeelewa kwa nini madam alikuwa kwenye mood nzuri sana. Bila shaka Festo alimwambia kwamba ninampenda sana, na kutokana na jinsi alivyoaminiana na yule jamaa, nadhani maneno yaliyohusika huko kwenye maongezi yao ndiyo yalitosha kumfanya mwanamke huyu alegee namna hii kunielekea. Hapa udhaifu wake ukawa umeanza kuonekana wazi. Alihitaji kupendwa, na sasa ndiyo akawa ameona kuwa angekipata hicho kitu kutoka kwangu. Mchezo ukawa unaenda vizuri.
Nikatabasamu kiasi na kusema, "Dah! Kumbe jamaa na ye' naye mbea."
"Hahah... haongeagi ovyo, nilimlazimisha tu mpaka akaropoka. Nilifurahi tu kujua kwamba ulimaanisha yote uliyoniambia siku ile tuko bed. Umeanza kujiweka sehemu nzuri HB wangu. Keep it up," akaniambia hivyo kwa sauti tulivu lakini iliyoonyesha hisia.
Nikamshika shingoni kwake na kumkaribia usoni, kisha nikasema, "Chochote kwa ajili yako madam wangu."
Akatabasamu na kusema, "Mmm, usiwe cozy kupita kiasi. Bado unatakiwa uni-impress. Nilikwambia hili tako la gharama, unatakiwa kuendelea kupanda madaraja."
"Naelewa. Maneno hayatoshi. Ndiyo maana niko hapa. Nitajitahidi nisikuangushe," nikamwambia hivyo.
"That's my boy," akasema hivyo na kunirushia busu kwa ishara ya mdomo wake.
Nikatabasamu kiasi.
Akakaa vizuri zaidi na kusema, "Naelekea location kukutana na mtu. Mtumishi."
"Wa kilokole?" nikamuuliza.
"Yeah. Na yeye anahusika kupitisha madini. Naenda kumpanga," akasema hivyo huku akivuta mkoba wake.
"Dah! Kweli, Mungu walishagamwona kama boya," nikamwambia hivyo.
"Ahahah... ni kwa sababu ye' ni boya. Watumishi wake ndiyo wanahalalisha tu hilo," akasema hivyo.
"Ahahahah... ila Bertha!"
Akawa ametoa miwani yake ya urembo na kusema, "Me natoka sa'. Nakuacha hapa, au?"
"Oh no, naingia kule kitaa sa'hivi, labda nitarudi baadaye," nikamwambia.
"Poa."
Akasimama na kuvaa miwani yake, nami nikasimama pia.
"Vipi kuhusu... ile ishu ya Chalii, madam? Umemwangalia?" nikamuuliza.
Akatabasamu na kunishika shavu, naye akasema, "Usijali kuhusu Chaz. Hawezi kutusumbua. Sasa hivi utakuwa kwenye focus ya kazi yetu, basi. Umeelewa?"
Nikatikisa kichwa kukubali.
"Twende. Nitakupanga kuhusu spot yetu mpya ya kazi baadaye..."
Baada ya mwanamke huyu kuniambia hivyo, akanipita na kuelekea nje, huku nami nikifuata nyuma yake taratibu.
Mambo yalikuwa yanajijenga upesi sana, na hivyo nilielewa haingechukua muda mrefu kwa huu mchezo wangu na madam Bertha kufikia ukomo. Lakini kutokea hapa ningepaswa kuwa makini SANA, kwa sababu ni pande nyingi zilikuwa zikihusika. Kumwagusha Bertha kusingekuwa kwa ajili ya kumuumiza yeye tu, bali na watu wake wengi aliojihusisha nao. Naongelea na huyo Festo.
Jamaa alikuwa anajua yule, na nilihofia angeweza kuwa mvurugaji wa mpango wangu kwa muda wowote ule kwa sababu alikuwa makini sana, kwa hiyo mimi ningehitaji kuwa hatua mbili mbele zaidi yake badala ya kusubiri tu mambo yaje halafu ndiyo nitoe itikio. Ningetakiwa kuhakikisha kwamba Bertha akianguka, aende chini pamoja na Chalii Gonga na Festo pia, na wasiwe na njia ya kurudi juu tena. Muda ndiyo ungeongea.
★★
Nikawa nimepewa lifti na madam mpaka kufikia maeneo ya Uhasibu kama tu siku ya juzi, naye akaniachia hapo na kuendelea na safari yake ya kwenda kumwona "mtumishi" wa kupitisha madawa. Nilikuwa nataka kwenda nyumbani kwetu kule kwanza ili nikawasalimu mama yangu pamoja na dada yangu, lakini kutokana na Bertha kunishurutisha nipande gari lake ili anilete huku, nikaona nighairi kwa leo. Sikutaka aanze maswali ya naenda kwa nani na kuanza kufatilia mengine asiyojua kunihusu, na ambayo sikutaka ajue.
Kwa hiyo, nikapanda usafiri ili nielekee Rangi Tatu kisha Mzinga, na nikiwa njiani nikaamua kumpigia mama yangu. Tukasalimiana vizuri, akiwa anaendelea salama tu toka mara ya mwisho tumeongea kwa simu, ndiyo nikamuulizia na dada yangu pia, Jasmine. Akasema kwa sasa Jasmine alikuwa akiendelea vizuri tu na kusubiri muda wake wa kujifungua ufike, ila ndiyo hakuwa na raha sana kutokana na matatizo yaliyokuwa yamempata wiki chache zilizopita.
Hivyo, nikaamua kuagana na mama na kumwambia ningekuja kwenda kuwasalimia, lakini Jasmine ningempigia pia ili tuongee kwa kina. Akasema hamna shida. Nikatulia kwanza ili nimpigie dada yangu nikishafika pale kwa Ankia, maana sikuona busara yoyote kuongea naye kwa marefu nikiwa ndani ya daladala.
Nimekuja kufika Mzinga ikiwa ishaingia saa nane ya saa tisa huko, hapo njaa ikiwa imenikong'oli vibaya mno, na nilielewa kukosa mlo wa asubuhi mara kwa mara ingekuwa na madhara ikiwa ningeifanya kuwa zoea maana ndiyo mlo muhimu zaidi, kwa hiyo nikaelekea pale kwenye ule mgahawa niliokaa na Miryam jana ili kupata chakula kwanza, halafu ndiyo ningejitahidi kuiboresha upya ratiba yangu ya ulaji mzuri baadaye.
Ugali wa nguvu, nyama, marage, mchicha, na maziwa, aaah mzee nikala kama vile nimepikiwa na mke kabisa. Hali nzuri ya nguvu mwilini ikarudi mahala pake baada ya kuwa nimemaliza msosi, nami nikalipia na kuanza kuelekea majumbani kwa Ankia. Nilipopita usawa wa Masai nikawa nimemwona Bobo pia, nasi tukasimama na kupeana salamu na maongezi ya hapa na pale, kisha ndiyo nikaendelea na safari mpaka nilipokuwa naishi.
Nilipoingia ndani, sikumkuta Ankia, bila shaka akiwa ameondoka kama alivyoniambia asubuhi na kusema tungeonana jioni, kwa hiyo nikaingia chumbani na kuanza kubadili mavazi ili niingie kwenye nguo nyepesi kwanza, halafu nimpigie dada yangu, kisha niende kujimwagia na kujiweka fresh nikaonane na binti Mariam.
Nikavaa T-shirt nyepesi na bukta, halafu nikafungua droo moja niliyokuwa nimekiweka kile kifaa cha piano, kinanda, ambacho nilinunua wiki chache zilizopita kule Kariakoo kwa ajili ya Mariam. Niliona kuanzia wakati huu ndiyo ingekuwa muhimu kuanza kukitumia pamoja naye, nami nikakiweka kitandani kwanza, kisha nikavuta simu na kumpigia Jasmine.
Dada yangu huyu alikuwa mtu wa mambo mengi sana kama tu mimi kaka yake. Yaani hata wakati huu aliokuwa na mimba ya miezi saba huko bado alipenda kujishughulisha na mambo mengi sana kwa sababu alipenda kufanya kazi, lakini hata zaidi wakati huu ni ile tu kutaka maisha yaendelee baada ya tatizo lake na aliyekuwa mume wake kuwafanya waachane.
Alipopokea na kuanza kuongea nami, ikabidi nikae kitandani kabisa na kumsikiliza kwa umakini. Alikuwa mwanamke mwenye hisia kali na za karibu sana, kwa hiyo akaongea vitu na mambo mengi sana ili kunifanya nimwelewe kwa undani wa mambo yote aliyopitia. Nikampa pole na kumwambia kwamba ningekuja kuonana naye hapo hapo nyumbani ndani ya siku hizi hizi mbeleni, na kumshauri ale vyakula fulani kuilinda afya ya mtoto, na kujitahidi kupumzika vya kutosha.
Akawa hana neno, akisema tu alikuwa amenikosa sana, na nilipokuwa nataka kumwambia nimem-miss pia, nikasikia mlango wa kuingilia kule sebuleni ukigongwa kuashiria mgeni alikuwa amefika. Kwa hiyo nikaagana vizuri na Jasmine na kurudia kumwahidi kwenda kumwona, kisha ndiyo nikatoka kwenda kufungua mlango ili nimsikilize mja aliyefika.
Ile nafungua mlango nikiwa na uso makini tu, nikajikuta nauyeyusha umakini wote baada ya kuona ilikuwa ni bibie Miryam! Yaani huyu mwanamke alikuwa ananikamata nyakati ambazo sikumtarajia kabisa. Akaachia tabasamu hafifu la kirafiki, nami nikatabasamu pia.
"Za sa'hizi?"
Kasauti kake katamu kakanipa salamu hiyo laini, lakini sikutoa jibu na kubaki kumtazama tu machoni.
"Za sa'hizi kaka?" akarudia tena.
Nikavuta pumzi upesi na kusema, "Nzuri... ni nzuri. Karibu."
"Asante. Nimekuja tuongee mara moja, kama hauko na... kazi labda...."
"Oh, sina kazi yoyote, karibu. Ingia," nikamkaribisha.
Akavua ndala zake za kike na kunipita, nami nikaivuta harufu ya marashi iliyotoka mwilini mwake kwa umakusudi kabisa wa kuisikilizia. Alikuwa amevaa ile Punjabi yake ya zambarau, huku nywele zake ndefu akiwa amezibana juu ya kichwa. Zilikuwa lainiii, yaani dah! Kuziangalia nyuma ya shingo yake zilifanya nitamani hata kuzigusa na kuzilaza-laza kama manyoya ya mnyama kipenzi, lakini nikaachana na mawazo ya kishetani na kufunga mlango tu.
"Nimekuona wakati unaingia hapo nje, nikasema nije ili tuongee kidogo," akasema hivyo akiwa amesimama bado.
"Kumbe? Nimepita kama upepo yaani, hata sikukuona. Karibu ukae," nikamwambia hivyo.
Akakaa sofani huku akitabasamu kiasi, nami nikakaa pembeni yake pia. "Za mizunguko?" akauliza.
Huku nikiwa nasugua goti langu kwa kiganja, nikamwambia, "Nzuri tu. Nilienda Makumbusho hapo mara moja kuonana na rafiki, ndiyo nimeingia mida hii. Nilikuwa ndo' nataka nije kumwona Mamu. Yupo?"
Akatabasamu na kusema, "Yupo. Ndiyo amemaliza kula mida hii."
"Okay, itabidi nimwahi, maana najua anapendaga kulala mchana pia. Vipi dawa anazokunywa lakini?"
"Anaendelea kunywa. Hapendi sana dawa, inabidi kulazimisha... lakini zinaenda," akasema hivyo.
"Ahah... angalau. Na wewe... haujaenda kazini?"
"Nimeenda asubuhi, leo nimewahi tu kurudi. Nilikuwa nataka niwepo pia ukija, nilifikiri ningefika kukuta mmeshaanza, kwa hiyo... nafurahi nimewahi..."
"Sawa kabisa. Wote tukiwepo na kutoa support kama hivyo, itamzidishia hali ya uchangamfu na kujiamini zaidi. Mwishowe hiyo kitu itaondoka maishani mwake. Ni suala la muda tu," nikamwambia hivyo.
Akatikisa kichwa kukubali na kusema, "Yeah."
Akawa ameingiza mkono wake kwenye mfuko wa nguo yake ya juu na kutoa bahasha fupi iliyokunjwa na kisha kuielekeza kwangu, nami nikamtazama machoni.
Akasema, "Ninataka kushukuru kwa kusaidia kulipia bili ya Mamu kwenye ile hospitali ya mwanzo. Na ilikuwa kubwa, ulilipia dawa na vipimo vyote yaani... nimeona nikurudishie tu kwa sababu unafanya mambo mengi sana kwa ajili yetu. Asante sana, ila pokea tu hii. Itakuwa kama tulisaidiana wote... kulipia."
Nikabaki namwangalia tu kwa umakini. Ule umakini kwa makusudi yaani.
Akasema, "Acha kuniangalia hivyo bwana. Usifikirie vibaya, ni... shukrani tu."
Nikaendelea kumkazia macho.
"Wewe, jamani..." akaongea kwa njia iliyoonyesha hakupenda nilivyokuwa namwangalia.
Nikacheka kwa pumzi na kuangalia pembeni, kisha nikasema, "Inaonekana mpaka leo bado hujanielewa tu."
Akashusha macho yake kwa njia ya kukwazika kiasi.
Nikamwangalia na kusema, "Acha kufikiria kwamba unahitaji kunilipa Miryam. Nakuelewa. Ila sihitaji malipo, nimeshakwambia. Mamu... Mamu atapona. Ninachotaka kuona zaidi kuliko mambo yote ni Mamu akipona. Hayo ndiyo malipo nayotarajia, na yatafanikiwa kwa sababu wote tutashirikiana ili kumsaidia. Yakitimia, nitaridhika."
Akawa ananiangalia kwa utulivu tu.
"So... hiyo weka pembeni. Ukitaka itumie, we' itumie kwa mambo mengine tu, ila siyo mimi. Kofi ulilonitandika siku ile lilinitosha," nikamwambia hivyo kiutani.
Midomo yake ikajikunja akijaribu kuzuia tabasamu, lakini akashindwa na kuangalia chini huku akicheka. Alipendeza sana kiasi kwamba mpaka nikajikuta namtazama tu huku nikitabasamu kwa hisia.
Akaniangalia na kusema, "Sa' si ndiyo uchukue hii iwe kama pole?"
"A-ah, lile kofi lilikuwa zawadi, hujui hilo?"
"Kivipi?"
"Ndiyo liliniongezea moto mpaka tukafanikiwa kum-nab kaka yako. Kwa hiyo silalamiki, ninakushukuru," nikamwambia kwa uhakikisho.
Akaonekana kutafakari kitu, kisha akasema, "Nikuombe jambo fulani tafadhali."
"Ndiyo. Niambie..."
"Kuanzia wakati huu... sitotaka... yaani, usimwongelee tena huyo mwanaume. Hata tu kumwita kaka yangu... sitaki tena," akasema hivyo.
Nikamwangalia usoni kwa uelewa mpana wa kile alichomaanisha, nami nikamwambia, "Sawa. Nimeelewa."
"Nataka kuanzia sasa... kila kitu kiwe ni focus ya kumfurahisha mdogo wangu ili akae sawa zaidi. I'll contribute on anything required to help you help her," akasema hivyo.
"Wow! Tesha hakukosea. Unaongea kiingereza vizuri," nikamwambia hivyo.
Akatabasamu huku akinitazama kwa utulivu.
"Uko sahihi. Kikubwa sasa hivi itakuwa ni furaha ya Mamu, so mambo yote yenye kuvunja moyo yatatakiwa kutupwa bin... iwe kama hayajawahi kutokea. Mariam... ana-progress haraka sana, haitachukua muda mrefu atakuwa sawa kabisa," nikamwambia.
"Sawa. Ubarikiwe sana."
"Amen."
"Mhm... sasa hivi ndiyo nataka kwenda sambamba na kila kitu mtakachofanya ili nihusike kwa lolote, na... nijue naweza...."
"Miryam... usijali. Nimeshakuelewa," nikamwambia hivyo kwa kumtuliza.
Akatabasamu kiasi na kuangalia chini, nami nikawa namwangalia kwa upendezi. Yaani haka kahali kote kalikuwa kanafanya damu yangu irukeruke tu sijui hata kwa nini!
"Unajua sina namba yako?" akasema hivyo.
"Ih, kweli? Ahh hata me sina ya kwako mpaka leo..." nikamwambia hivyo.
Akasema, "Jamani! Yaani, utafikiri tulikuwa maadui..."
"Eti! Yaani hata namba tu?" nikamwambia hivyo, nasi kwa pamoja tukacheka kidogo.
Akarudisha bahasha mfukoni na kutoa simu yake, naye akanipatia akiwa ameweka sehemu ya kuandikia namba huku akisema, "Sasa hivi mambo yatabadilika. Nataka tuwe marafiki."
Nilikuwa nimeshaanza kuandika namba yangu kwenye simu yake aliposema hivyo, nami nikawa natabasamu kiasi baada ya kusikia kauli yake ya kutaka tuwe marafiki. Nikamrudishia simu, naye akaipigia namba hiyo. Simu yangu ikaita, nikiwa napewa namba ya bibie Miryam rasmi kwa mara ya kwanza kabisa na yeye mwenyewe, nami nikaitunza kwa jina lake.
Nikamwangalia usoni kukuta ananitazama kwa utulivu, nami eti nikaingiwa na haya na kutazama pembeni kisha kutabasamu kidogo.
"Nini?" akauliza hivyo.
Nikatikisa kichwa kuonyesha hakuna kitu, kisha nikamwangalia tena.
"Mbona unatabasamu sana? Nini kimekufurahisha?" akaniuliza na sauti yake tamu.
"Sikuwahi kudhani... yaani, ungetaka tuwe marafiki. Nilikuwa nakuona wa kivyako mno, au labda unanichukulia kuwa siko..."
"Usiwaze hivyo tena. Hayo yamepita. Sisi ni marafiki sasa, sawa?" akanikatisha kwa kusema hivyo.
"Sawa. Lakini unajua nini?"
"Niambie."
"Toka tumejuana... sijawahi kukusikia ukilitaja jina langu," nikamwambia hivyo.
Akatabasamu huku akitazama pembeni.
"Yeah. Sijawahi kabisa. Huwa unaniita tu kaka, kijana, we' kaka... wewe..."
Akacheka kidogo kwa furaha.
"Tukiwa washka... ah, namaanisha, marafiki... nitapenda kusikia ukiniita kwa jina langu," nikamwambia hivyo huku nikitabasamu.
Akasema, "Haina shida. Nisamehe kwa kukuita hayo majina wakati huo, ila... sijawahi kutaja jina lako kwa sababu silijui."
Ka!
Kauli yake ikanifanya nimtazame kimaswali kiasi, nami nikamuuliza, "Hulijui jina langu?"
"Yeah," akajibu.
"Yaani... unatania, au? Maana, nakuja hapo kwako... unawasikia kabisa warembo wangu wanasema 'JC karibu,' 'JC za nyumbani?' 'JC hivi, JC vile...' halafu unaniambia hujui naitwa nani? Kweli Miryam?" nikamuuliza kwa kusuta.
Akacheka kidogo kwa pumzi na kusema, "Najua hilo siyo jina lako, hicho ni kifupi tu, ama nickname, kama wao wanavyoniita mimi 'Mimi!'"
Aliongea kwa njia ya masihara, lakini kauli yake ikanifanya nimtazame kwa njia makini kiasi.
"Nitapenda nikikuita kwa jina lako kabisa. Kama wewe unavyoniita 'Miryam,'" akasema hivyo.
Dah!
Nikaangalia tu chini kiasi nikiwa natabasamu. Bila kutambua, mwanamke huyu alikuwa amegusa sehemu fulani ya maisha yangu ambayo mpaka sasa bado sijaiweka wazi, na kauli yake ilifanya niikumbuke. Alinifanya nihisi raha ya kina sana, ile raha kama ya wimbo wa Bebe Rexha 'say my name.' Hehe! Hapa uhondo ndiyo ulikuwa umeanza.
Nikamwangalia usoni tena, naye akasema, "So... ukitaka nikuite kwa jina lako, niambie unaitwa nani."
Nikatabasamu kiasi, kisha nikamwambia, "Naitwa Jayden."
Akatabasamu pia, kisha akasema, "Jayden..."
Ah! Jina langu ndani ya hiyo sauti? Ilikuwa kama vile limeimbwa!
"Sawa. Me sitakuita JC. Nitakuita Jayden. Kama Jaden Smith," akasema hivyo.
"Ahahah... Tesha si amesema hauangaliagi movie, hilo jina umelijuaje?" nikamuuliza kiutani.
"Tesha anaongea mno, najua vitu vingi pia, siboi sana kama mnavyofikiria," akaniambia hivyo.
Nikatabasamu kwa hisia.
Akaninyooshea kiganja chake na kusema, "So Jayden... friends?"
Dah! Sikufikiria huyu dada angekuwa na uzungu mwingi namna hii, lakini ulimfaa, na alipendezea sana. Nikakishika kiganja chake pia na kuviunganisha kwa pamoja ili kukubali mwaliko wake wa kuwa marafiki rasmi.
"Friends," nikamwambia hivyo.
Tukaendelea kuangaliana kwa upendezi mwingi sana, nikiwa najihisi vizuri mno kupata ukaribu na mwanamke huyu baada ya misukosuko yote aliyopitia na familia yake siku chache nyuma. Nilitazamia mengi mazuri yaje kutokana na uhusiano huu mpya niliokuwa nimejipatia kwa huyu mwanamke, ambayo yangesaidia kumweka huru mdogo wake kutokana na tatizo alilokuwa nalo. Na kilikuwa ndiyo kitu nilichokitamani sana tokea siku ya kwanza kabisa nilipokutana naye.
Sasa huu ndiyo ungekuwa mwanzo wa mambo mengi ambayo yangebadili maisha yangu mimi, na Mimi.
END OF SEASON ONE
★★★★★★★★★★★★★★★★★★