Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
Simulizi: NGUVU YA MAPENZI
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Mdada mmoja mrembo sana aliyeitwa Angel alionekana siku hii akiwapeleka wadogo zake kuripoti katika shule mpya maana wadogo zake hao walikuwa ndio wanaanza kidato cha kwanza na yeye alikuwa yupo kidato cha nne, basi alifika nao shuleni na kuwakabidhi kwa mwalimu ambaye alimzoea sana sababu alikuwa ni mwalimu wake pia maana ni shule hiyo hiyo ambayo nay eye alikuwa akisoma kwa kipindi hiko, basi aliwakabidhi pale na mwalimu alianza kuongea na Angel,
“Halafu Angel unajua wenzio wa kidato cha nne walianza kuja shule toka wiki iliyopita halafu wewe leo umeleta wadogo zako tu na kutaka kuondoka”
“Sir Harun, sipo vizuri mimi ndiomana sijaja shule”
“Na wazazi wako wako wapi?”
“Wamesafiri ndiomana hata wadogo zangu imebidi niwalete mimi”
“Hata hivyo, bado unatakiwa uje kwenye masomo Angel, upo kwenye level ngumu sana hiyo”
“Sawa, basi kesho nitakuja mwalimu”
Kisha Angel akamuaga pale mwalimu wake na kuondoka zake, siku hiyo Angel hakumwambia dereva wao maana kuna matendo yule dereva alikuwa akiyafanya kwake na kufanya Angel asimuamini kuwa nae karibu kwahiyo aliamua kujiondokea mwenyewe.
Akiwa njiani wakati wa kurudi kwao akapigiwa simu na rafiki yake Hanifa,
“Uko wapi Angel?”
“Nipo karibia na maeneo ya shule ila narudi nyumbani”
“Kheee nilivyosikia shule si nikajua umeenda shule”
“Niende wapi, kwanza nahisi uvivu hatari ila nimekuja kuwakabidhi wadogo zangu wanaanza kidato cha kwanza, kwahiyo ilinilazimu niwalete maana wale watoto wamedekezwa sana na mama”
“Sawa, basi naomba upitie hapa dukani kwetu kuna jambo nataka tuongee”
“Sawa, hakuna tatizo”
Moja kwa moja Angel alielekea dukani kwakina Hanifa ili kuweza kuzungumza nae mawili matatu.
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Mdada mmoja mrembo sana aliyeitwa Angel alionekana siku hii akiwapeleka wadogo zake kuripoti katika shule mpya maana wadogo zake hao walikuwa ndio wanaanza kidato cha kwanza na yeye alikuwa yupo kidato cha nne, basi alifika nao shuleni na kuwakabidhi kwa mwalimu ambaye alimzoea sana sababu alikuwa ni mwalimu wake pia maana ni shule hiyo hiyo ambayo nay eye alikuwa akisoma kwa kipindi hiko, basi aliwakabidhi pale na mwalimu alianza kuongea na Angel,
“Halafu Angel unajua wenzio wa kidato cha nne walianza kuja shule toka wiki iliyopita halafu wewe leo umeleta wadogo zako tu na kutaka kuondoka”
“Sir Harun, sipo vizuri mimi ndiomana sijaja shule”
“Na wazazi wako wako wapi?”
“Wamesafiri ndiomana hata wadogo zangu imebidi niwalete mimi”
“Hata hivyo, bado unatakiwa uje kwenye masomo Angel, upo kwenye level ngumu sana hiyo”
“Sawa, basi kesho nitakuja mwalimu”
Kisha Angel akamuaga pale mwalimu wake na kuondoka zake, siku hiyo Angel hakumwambia dereva wao maana kuna matendo yule dereva alikuwa akiyafanya kwake na kufanya Angel asimuamini kuwa nae karibu kwahiyo aliamua kujiondokea mwenyewe.
Akiwa njiani wakati wa kurudi kwao akapigiwa simu na rafiki yake Hanifa,
“Uko wapi Angel?”
“Nipo karibia na maeneo ya shule ila narudi nyumbani”
“Kheee nilivyosikia shule si nikajua umeenda shule”
“Niende wapi, kwanza nahisi uvivu hatari ila nimekuja kuwakabidhi wadogo zangu wanaanza kidato cha kwanza, kwahiyo ilinilazimu niwalete maana wale watoto wamedekezwa sana na mama”
“Sawa, basi naomba upitie hapa dukani kwetu kuna jambo nataka tuongee”
“Sawa, hakuna tatizo”
Moja kwa moja Angel alielekea dukani kwakina Hanifa ili kuweza kuzungumza nae mawili matatu.