Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 87
Leo Erick aliwahi kurudi nyumbani tofauti na siku zote ambazo huwa anarudi na Erica, basi akabadili sare zake na kwavile alijihisi kuchoka
aliamua kuchukua zile karata zilizoletwa na Erica ili acheze kidogo.
Basi alikaa kitandani na kuzichukua ambapo alizichanga ila kuna kikaratasi kilianguka ikabidi akiokote na kukisoma,
“Nakupenda sana Erica”
Erick alishtuka mno na kujiuliza,
“Inamaana Elly ndio kamuandikia Erica huu ujumbe? Mmmh nae ameanza huu ujinga kweli!”
Erick alishangaa sana ila alimngoja Erica arudi na aliposikia tu kuwa amerudi basi aliinuka na kwenda chumbani kwake, naye alifika
chumbani kwa Erica na kufungua tu mlango yani hakugonga wala nini na kumfanya Erica apige kelele maana kifuani alikuwa wazi, ila
alipoona ni Erick alinyamaza na kujifunga na khanga kisha akamsema,
“Erick tabia mbaya hiyo, unaingia chumbani kwangu bila hodi!”
“Mbona na wewe huwa unaingia chumbani kwangu bila hodi?”
“Kwahiyo ndio umenilipizia? Muone vile”
“Ila kifua chako kimekuwa kizuri”
“Sitaki ujinga Erick, muone vile haya sema kilichokuleta”
“Chukua ujumbe wako wa kwenye karata”
Basi akampa ile karatasi na kumuuliza,
“Inamaana Elly ndio kakuandikia hivyo!! Elly si huwa unasema ni kaka yako?”
“Mmmmh aaaah karata hajanipa Elly”
“Ila alikupa Abdi eeeh!”
“Ndio”
“Nilijua tu, yani Erica unataka kuruhusu ujinga wa huyu mapema ukuharibie masomo!! Bora nilihama hiyo shule, sitaki kujiumiza kichwa,
sasa endelea na ujinga wako halafu utaona nitakacho kifanya”
Halafu Erick aliondoka zake, huku Erica akisoma kile kiujumbe kifupi na kwenda kukitupia chooni.
Mama Angel alifika kwa wifi yake akiwa na hasira sana, aliingia sebleni na kuita kwa hasira,
“Angel, Angel, Angel”
Wifi yake alitoka na kumuuliza,
“Kuna nini kwani?”
Angel nae alitoka, basi mama yake alimvuta na kumzaba kofi mbili mbili huku akimsema,
“Hivi wewe mtoto unataka hadi usikie mamako amekufa ndio utafurahi”
Shangazi yake akauliza,
“Kafanyaje tena?”
“Yani huwezi amini wifi, leo nikasema ngoja nikamuangalie Angel shule na nimchukue mwenyewe hadi dereva nikamtumia ujumbe kuwa
asiende kumchukua Angel, nilichokikuta sasa? Eti Angel yupo na yule mjinga mwenzie Samir wakielekea kwenye kituo cha daladala, mjinga
huyu kafanya leo bado kidogo tu nipate ajali jamani”
“Kheee pole wifi yangu jamani”
Kisha Shangazi akamuangalia Angel na kumuuliza,
“Inamaana Samir nae anasoma hapo shuleni kwenu?”
“Ndio shangazi, hata mimi sikujua kumbe aliahamia pale”
“Haya niambie imekuwaje mpaka ukaongozana nae kurudi nyumbani”
“Shangazi ni hivi, mimi na Husna tulipanga leo kurudi pamoja tu, ila Husna akaumwa gafla na kurudi kwao basi wakati wa kutoka ikabidi tu
niondoke mwenyewe, ila dereva hahusiki kwa hili maana nilimdanganya kuwa asije kunichukua, ila wakati naondoka gafla alikuja Samir ila
kweli kabisa shangazi sikutaka kuongozana nae”
“Haya, nenda chumbani kaendelee na ratiba yako ya leo”
Mama Angel alimshangaa wifi yake kujibu kirahisi hivyo, pia alishangaa mwanae kwa mpangilio wa lile jibu na kumuuliza wifi yake,
“Una uhakika alichokujibu ni cha ukweli?”
“Mimi sitaki kumjengea mtoto mazingira ya uoga ila namjengea mazingira ya kuniheshimu, na nikisema nitakupiga basi ujue nishampiga
maana sina msemo wa nitakupiga, atazoea na kujua ni uongo tu. Halafu huwa nawafundisha kuwa wakweli maana mimi ni mchunguzi kupita
unavyoelewa, kwahiyo swala la Angel niachie mimi mwenyewe tu kwani huyu Angel nitamnyoosha, kama alikuwa akikudanganya ni wewe
maana mimi sidanganywi kirahisi namna hiyo”
“Kheee saa wifi tufanyeje? Tumuhamishe shule au?”
“Hapana wala usiingie gharama nyingine wifi yangu ila mimi nitakula nae sahani moja huyu hata usiwe na mashaka wifi yangu”
Mama Angel alikaa sasa akapumua kisha wifi yake aliamua kumletea juisi ili ashushie na zile hasira alizokuwa nazo.
Aliongea kidogo tu na kuaga maana dereva alimuacha ndani ya gari.
Leo Erick aliwahi kurudi nyumbani tofauti na siku zote ambazo huwa anarudi na Erica, basi akabadili sare zake na kwavile alijihisi kuchoka
aliamua kuchukua zile karata zilizoletwa na Erica ili acheze kidogo.
Basi alikaa kitandani na kuzichukua ambapo alizichanga ila kuna kikaratasi kilianguka ikabidi akiokote na kukisoma,
“Nakupenda sana Erica”
Erick alishtuka mno na kujiuliza,
“Inamaana Elly ndio kamuandikia Erica huu ujumbe? Mmmh nae ameanza huu ujinga kweli!”
Erick alishangaa sana ila alimngoja Erica arudi na aliposikia tu kuwa amerudi basi aliinuka na kwenda chumbani kwake, naye alifika
chumbani kwa Erica na kufungua tu mlango yani hakugonga wala nini na kumfanya Erica apige kelele maana kifuani alikuwa wazi, ila
alipoona ni Erick alinyamaza na kujifunga na khanga kisha akamsema,
“Erick tabia mbaya hiyo, unaingia chumbani kwangu bila hodi!”
“Mbona na wewe huwa unaingia chumbani kwangu bila hodi?”
“Kwahiyo ndio umenilipizia? Muone vile”
“Ila kifua chako kimekuwa kizuri”
“Sitaki ujinga Erick, muone vile haya sema kilichokuleta”
“Chukua ujumbe wako wa kwenye karata”
Basi akampa ile karatasi na kumuuliza,
“Inamaana Elly ndio kakuandikia hivyo!! Elly si huwa unasema ni kaka yako?”
“Mmmmh aaaah karata hajanipa Elly”
“Ila alikupa Abdi eeeh!”
“Ndio”
“Nilijua tu, yani Erica unataka kuruhusu ujinga wa huyu mapema ukuharibie masomo!! Bora nilihama hiyo shule, sitaki kujiumiza kichwa,
sasa endelea na ujinga wako halafu utaona nitakacho kifanya”
Halafu Erick aliondoka zake, huku Erica akisoma kile kiujumbe kifupi na kwenda kukitupia chooni.
Mama Angel alifika kwa wifi yake akiwa na hasira sana, aliingia sebleni na kuita kwa hasira,
“Angel, Angel, Angel”
Wifi yake alitoka na kumuuliza,
“Kuna nini kwani?”
Angel nae alitoka, basi mama yake alimvuta na kumzaba kofi mbili mbili huku akimsema,
“Hivi wewe mtoto unataka hadi usikie mamako amekufa ndio utafurahi”
Shangazi yake akauliza,
“Kafanyaje tena?”
“Yani huwezi amini wifi, leo nikasema ngoja nikamuangalie Angel shule na nimchukue mwenyewe hadi dereva nikamtumia ujumbe kuwa
asiende kumchukua Angel, nilichokikuta sasa? Eti Angel yupo na yule mjinga mwenzie Samir wakielekea kwenye kituo cha daladala, mjinga
huyu kafanya leo bado kidogo tu nipate ajali jamani”
“Kheee pole wifi yangu jamani”
Kisha Shangazi akamuangalia Angel na kumuuliza,
“Inamaana Samir nae anasoma hapo shuleni kwenu?”
“Ndio shangazi, hata mimi sikujua kumbe aliahamia pale”
“Haya niambie imekuwaje mpaka ukaongozana nae kurudi nyumbani”
“Shangazi ni hivi, mimi na Husna tulipanga leo kurudi pamoja tu, ila Husna akaumwa gafla na kurudi kwao basi wakati wa kutoka ikabidi tu
niondoke mwenyewe, ila dereva hahusiki kwa hili maana nilimdanganya kuwa asije kunichukua, ila wakati naondoka gafla alikuja Samir ila
kweli kabisa shangazi sikutaka kuongozana nae”
“Haya, nenda chumbani kaendelee na ratiba yako ya leo”
Mama Angel alimshangaa wifi yake kujibu kirahisi hivyo, pia alishangaa mwanae kwa mpangilio wa lile jibu na kumuuliza wifi yake,
“Una uhakika alichokujibu ni cha ukweli?”
“Mimi sitaki kumjengea mtoto mazingira ya uoga ila namjengea mazingira ya kuniheshimu, na nikisema nitakupiga basi ujue nishampiga
maana sina msemo wa nitakupiga, atazoea na kujua ni uongo tu. Halafu huwa nawafundisha kuwa wakweli maana mimi ni mchunguzi kupita
unavyoelewa, kwahiyo swala la Angel niachie mimi mwenyewe tu kwani huyu Angel nitamnyoosha, kama alikuwa akikudanganya ni wewe
maana mimi sidanganywi kirahisi namna hiyo”
“Kheee saa wifi tufanyeje? Tumuhamishe shule au?”
“Hapana wala usiingie gharama nyingine wifi yangu ila mimi nitakula nae sahani moja huyu hata usiwe na mashaka wifi yangu”
Mama Angel alikaa sasa akapumua kisha wifi yake aliamua kumletea juisi ili ashushie na zile hasira alizokuwa nazo.
Aliongea kidogo tu na kuaga maana dereva alimuacha ndani ya gari.