Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 119
Kulipokucha kama kawaida walijiandaa kwenda shuleni huku baba Angel na mama Angel wakitoka pamoja pia kwani nao waliaenda kwenye kazi zao.
Vaileth alibaki nyumbani ila alikuwa na mawazo sana na kujisemea,
“Ona sasa hata siaminiki tena kama zamani, kwakweli shangazi na Prisca wameniponza. Ningejua bora hata Prisca asingefika hapa au bora nisingeenda”
Mara simu yake ilianza kuita, alipoangalia aliona ni namba ya shangazi yake basi ilibidi aipokee na kuanza kuongea nayo,
“Shangazi shikamoo”
“Haina haja, ushafanya hiyo dawa?”
“Mmmh shangazi, kwanza nimepata aibu sana yani kwasasa naishi kwa fedheha kubwa”
“Khaaa unasemaje wewe”
Ilibidi Vaileth amueleze shangazi yake kuhusu yote yaliyotokea, jinsi yeye alivyobambwa na zile dawa, yani shangazi yake alichukia sana,
“Mjinga sana wewe, yani kumbe zile dawa uliweka kwenye mkoba?”
“Ndio shangazi, ningeweka wapi sasa?”
“Si nilikwambia uweke kwenye maziwa mjinga wewe? Kwani hujui ni wapi ambapo wanawake huwa wanaficha vitu vyao muhimu? Yani umenikera sana, kwahiyo umechukua uamuzi gani?”
“Wale watoto walienda kumwaga zile dawa, kwakweli nimelia sana kwa kuwasihi wasinisemee kwa wazazi wao, yani nina mawazo hatari”
“Hebu niondolee ujinga ujue, kesho nitamuagiza Prisca aje huko na atakuletea dawa yani atakuja mara moja na kuondoka na ole wako ufanye ujinga tena”
“Jamani shangazi, sitaki hayo mambo”
“Mjinga wewe, hutaki nini? Yani jua kuwa usipofanya hivyo undugu na wewe umeisha, na katika maisha usiombee kabisa kutengwa na shangazi maana ukoo mzima utakutenga, yani wewe unataka kuniletea ujinga muda wote? Umenikera sana mjinga wewe. Sasa Priscaatakuletea kesho hizo dawa”
“Mmmmh shangazi”
“Sitaki miguno wala nini, nimemaliza. Kesho Prisca atakuja na lazima uifanye hiyo dawa, utake au usitake”
Halafu shangazi yake alikata simu ile na kumfanya Vaileth apate maswali zaidi.
Erica kama kawaida mda wa mapumziko alikaa na Elly na kuanza kuongea nae mambo mbalimbali, basi Erica aliamua kumueleza kuhusu yaliyotokea Jumamosi nyumbani kwao, yani kuhusu yule mdada wao wa kazi, kwakweli Elly alishangaa sana na kusema,
“Kheee huyo mdada hawafai ujue, kumbe ni mshirikina”
“Ndio, nimechukia sana kwakweli”
“Anaitwa nani?”
“Anaitwa Vaileth, jamani kwakweli nimebaki tu kumshangaa kuwa mchawi halafu anajifanya kutuchekea chekea”
“Muwe nae makini sana huyo jamani. Kwenu sipajui ila nahisi huyo kawaonea wivu tu”
“Halafu Erick anasema eti tusiwaambie wazazi”
“Mmmh sijui, ila nitamuhadithia na mama yangu najua atanipa ushauri uliobora”
“Sawa sawa Elly”
Basi walirudi darasani na kuendelea na masomo.
Muda wa kutoka ulipowadia, Erica moja kwa moja alielekea kwenye gari ya kurudi kwao ila Abdi alimsogelea na kumwambia kwa sauti ndogo,
“Kuna jambo kati ya mama yako na baba yangu”
Halafu Abdi akaondoka, kwakweli Erica hakumuelewa ila alimuangalia tu.
Kulipokucha kama kawaida walijiandaa kwenda shuleni huku baba Angel na mama Angel wakitoka pamoja pia kwani nao waliaenda kwenye kazi zao.
Vaileth alibaki nyumbani ila alikuwa na mawazo sana na kujisemea,
“Ona sasa hata siaminiki tena kama zamani, kwakweli shangazi na Prisca wameniponza. Ningejua bora hata Prisca asingefika hapa au bora nisingeenda”
Mara simu yake ilianza kuita, alipoangalia aliona ni namba ya shangazi yake basi ilibidi aipokee na kuanza kuongea nayo,
“Shangazi shikamoo”
“Haina haja, ushafanya hiyo dawa?”
“Mmmh shangazi, kwanza nimepata aibu sana yani kwasasa naishi kwa fedheha kubwa”
“Khaaa unasemaje wewe”
Ilibidi Vaileth amueleze shangazi yake kuhusu yote yaliyotokea, jinsi yeye alivyobambwa na zile dawa, yani shangazi yake alichukia sana,
“Mjinga sana wewe, yani kumbe zile dawa uliweka kwenye mkoba?”
“Ndio shangazi, ningeweka wapi sasa?”
“Si nilikwambia uweke kwenye maziwa mjinga wewe? Kwani hujui ni wapi ambapo wanawake huwa wanaficha vitu vyao muhimu? Yani umenikera sana, kwahiyo umechukua uamuzi gani?”
“Wale watoto walienda kumwaga zile dawa, kwakweli nimelia sana kwa kuwasihi wasinisemee kwa wazazi wao, yani nina mawazo hatari”
“Hebu niondolee ujinga ujue, kesho nitamuagiza Prisca aje huko na atakuletea dawa yani atakuja mara moja na kuondoka na ole wako ufanye ujinga tena”
“Jamani shangazi, sitaki hayo mambo”
“Mjinga wewe, hutaki nini? Yani jua kuwa usipofanya hivyo undugu na wewe umeisha, na katika maisha usiombee kabisa kutengwa na shangazi maana ukoo mzima utakutenga, yani wewe unataka kuniletea ujinga muda wote? Umenikera sana mjinga wewe. Sasa Priscaatakuletea kesho hizo dawa”
“Mmmmh shangazi”
“Sitaki miguno wala nini, nimemaliza. Kesho Prisca atakuja na lazima uifanye hiyo dawa, utake au usitake”
Halafu shangazi yake alikata simu ile na kumfanya Vaileth apate maswali zaidi.
Erica kama kawaida mda wa mapumziko alikaa na Elly na kuanza kuongea nae mambo mbalimbali, basi Erica aliamua kumueleza kuhusu yaliyotokea Jumamosi nyumbani kwao, yani kuhusu yule mdada wao wa kazi, kwakweli Elly alishangaa sana na kusema,
“Kheee huyo mdada hawafai ujue, kumbe ni mshirikina”
“Ndio, nimechukia sana kwakweli”
“Anaitwa nani?”
“Anaitwa Vaileth, jamani kwakweli nimebaki tu kumshangaa kuwa mchawi halafu anajifanya kutuchekea chekea”
“Muwe nae makini sana huyo jamani. Kwenu sipajui ila nahisi huyo kawaonea wivu tu”
“Halafu Erick anasema eti tusiwaambie wazazi”
“Mmmh sijui, ila nitamuhadithia na mama yangu najua atanipa ushauri uliobora”
“Sawa sawa Elly”
Basi walirudi darasani na kuendelea na masomo.
Muda wa kutoka ulipowadia, Erica moja kwa moja alielekea kwenye gari ya kurudi kwao ila Abdi alimsogelea na kumwambia kwa sauti ndogo,
“Kuna jambo kati ya mama yako na baba yangu”
Halafu Abdi akaondoka, kwakweli Erica hakumuelewa ila alimuangalia tu.