Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #181
SEHEMU YA 155
Mama Angel na baba Angel kama ambavyo walikuwa wamepanga, basi leo walienda moja kwa moja kwa Tumaini ili kumuona mtoto wao na kumtakia mtihani mwema, na walipofika tu kweli walimkuta yupo ndani anajisomea, basi walimuita na kumsalimia kisha wakamtaka kuendelea na masomo yake kama kawaida, basi na wao walikaa wakiongea pale na Tumaini kuhusu mambo mbalimbali, na muda kidogo mume wa Tumaini nae aliwasili na kusalimiana nao pale halafu alianza kuongea nao,
“Jamani eeeh! Leo niliamua kufatilia lile tukio mjue, yani nimefatilia nijue yule mdada ofisini kwangu alikuja kufanya ninina kwanini ikawa vile”
“Mmmh kaka, kwahiyo umemgundua sasa?”
“Yani ni hivi, yule binti alikuwa ni mgeni machoni mwa wote pale ofisini, ila nilivyouliza kwa watu wengine walidai kuwa wanamfahamu yule dada, kuwa yule dada ni mpiga madili, watu wakasema kwamaana hiyo kuna mtu atakuwa kampa kazi ya kuja ofisini kwangu ila mpaka muda huu sijajua ni mtu gani na alikuwa na lengo gani”
Pale ndio maneno ya Dora yalianza kufanya kazi vizuri katika akili ya mama Angel na moja kwa moja, na kumfanya azidi kumchukia Sia kwani jibu alilokuwa nalo kwenye akili yake ni kuwa Sia hakuwa mtu mzuri tena, basi alimuuliza tena kaka yake,
“Kaka Tony, hivi hakuna hata mtu mmoja aliyesema kuwa huyo dada huwa anatumiwa na nani?”
“Nasikia huwa anatumiwa na watu mbalimbali, kwa maana hiyo hata kuanguka hakuanguka wala nini, yule alikuwa kwenye maigizo tu”
“Ooooh sema kwa mtindo huo basi inatakiwa kuwa makini sana”
“Ni kweli, haswaaa kwasisi wafanyabiashara maana utakuta mara nyingine unafatiliwa na mtu bila hata kujua kuwa unafatiliwa, ila inatakiwa kuwa makini sana. Nataka kufunga kamera kwenye ofisi yangu”
“Oooh utakuwa umefanya jambo la maana sana”
Kisha mama Angel alimuuliza baba Angel,
“Hivi na ile ofisi mpya mume wangu umefunga kamera kweli!”
“Mmmmh bado sijafunga kule”
“Mi naona ni vyema nako ufunge kamera”
“Sawa sawa, nitafanya hivyo tu”
Basi wakaongea pale na kuamua kuaga, ambapo baba Angel na mama Angel waliondoka kwani waliona muda wao umeisha wa kuendelea kukaa mahali hapo.
Mama Angel na baba Angel walipofika nyumbani waliwakuta watoto wao wakiwa makini sana na kuangalia Tv, kama kawaida mama Angel aliwatimua maana hakupenda wakae pale sebleni kwa muda mrefu ila kitendo cha kuwatimua wale watoto wake muda huo walienda tu chumba kimoja ambapo walienda chumbani kwa Erick na kuanza kuongea mambo mbalimbali, Erica alimuuliza kaka yake,
“Sasa hizo muvi za ngumi Samia akizileta tutakuwa tunaangalia wapi ikiwa mama anatufukuza sebleni?”
“Ooooh mbona jambo dogo hilo, sikia nikwambie mimi na wewe inatakiwa letu liwe moja. Mbona kwenye ile sebule ya juu ina Tv pia, si huwa wanasema hadi wageni waje? Mimi ndio ninafungua za vyumba vyote humu ndani kwahiyo hata usijali tutakuwa tunaenda na kuangalia kule”
“Jamani, ndiomana nakupenda Erick, ila mimi picha za ngumi naogopa sana”
“Sasa unaogopa nini wakati utakuwa unaangalia na mimi? Usiogope maana tutaangalia wote”
“Sawa kaka yangu, basi tucheze karata na leo”
Erick alikubali na kuanza kucheza karata ambapo kama kawaida walicheza sana hadi usiku na wakajikuta wameshikwa na usingizi mule mule chumbani kwa Erick.
Kulipokucha, Erick alikuwa wa kwanza kuamka leo na kumshtua dada yake ambaye nae alikurupuka, kwahiyo ile tabia ilikuwa kawaida kabisa kwao maana haikuwa mara ya kwanza ukizingatia mara nyingi walijikuta wakiwa pamoja.
Basi asubuhi ile nyumba nzima leo walienda kwenye ibada hadi Junior, ingawa huwa ni mbishi kwenda ibadani ila leo alienda, kwahiyo nyumba nzima waliondoka.
Wakiwa ibadani, Erica alitoka mara moja maana kuna kitu alikiona nje ya Kanisa wakati wanataka kuingia, kwahiyo walipokuwa Ibadani tu aliwavizia na kutoka zake nje ili kuangalia kile alichokiona, basi aliondoka hadi lile eneo ila kuna kijana aligongana nae kikumbo na kuanza kuombana nae msamaha,
“Nisamehe tafadhari”
“Nisamehe mimi kwa kutoangalia mbele”
“Aaaah usijali chochote, by the way naitwa Bahati, vipi wewe unaitwa nani?”
“Naitwa Erica”
“Ooooh jina zuri sana, hongera”
“Asante”
Erica macho yote yalikuwa pale alipoona alichokuwa anakitaka ila kuangalia vizuri alikuta kimeshanunuliwa, na kujikuta akisema,
“Aaaargh washachukua tayari”
Yule Bahati alimuuliza,
“Wamechukua kitu gani?”
“Kuna kiatu nilikiona pale, nikakipenda sana, yani nilitaka kukinunua jamani, wamekichukua tayari”
Basi Bahati alisogea pale na Erica na kujua ambaye alichukua kile kiatu kisha kwenda kumuomba ili waweze kununua kile kiatu, yule mtu aliwaambia labda wampe hela mara mbili ya bei ya kawaida ya kile kiatu. Kilikuwa ni kiatu cha kawaida kabisa ila Erica alionekana kukipenda sana, kiliuzwa elfu tano kwahiyo yule mtu alisema labda apewe elfu kumi, Bahati akamuangalia Erica na kumuuliza,
“Je utakinunua kwa bei hiyo?”
Erica aliitikia tu na kufanya Bahati amuulize tena ila Erica alikaa kimya, kwani kiukweli hakuwa na hela yoyote pale ila alikuwa akijitutumua tu kuwa anataka kununua kile kiatu, badae akamwambia Bahati,
“Mwache tu aende, nilikuwa nakiangalia tu”
“Mmmh jamani, hadi tumemrudisha ujue!”
“Aaaaah kumbe hela yenyewe sina”
Basi Bahati alitoa hela yake na kununua kile kiatu kwa yule mtu kisha alimkabidhi Erica kile kiatu, kwakweli Erica alitabasamu na kufurahi sana huku akimwambia,
“Asante sana”
“Usijali, natumaini tutaonana tena”
Basi Erica moja kwa moja alirudi tena kanisani lakini hakuna mwanafamilia wa Erica aliyegundua kuwa Erica alitoka nje ya kanisa ule muda wa ibada.
Mama Angel na baba Angel kama ambavyo walikuwa wamepanga, basi leo walienda moja kwa moja kwa Tumaini ili kumuona mtoto wao na kumtakia mtihani mwema, na walipofika tu kweli walimkuta yupo ndani anajisomea, basi walimuita na kumsalimia kisha wakamtaka kuendelea na masomo yake kama kawaida, basi na wao walikaa wakiongea pale na Tumaini kuhusu mambo mbalimbali, na muda kidogo mume wa Tumaini nae aliwasili na kusalimiana nao pale halafu alianza kuongea nao,
“Jamani eeeh! Leo niliamua kufatilia lile tukio mjue, yani nimefatilia nijue yule mdada ofisini kwangu alikuja kufanya ninina kwanini ikawa vile”
“Mmmh kaka, kwahiyo umemgundua sasa?”
“Yani ni hivi, yule binti alikuwa ni mgeni machoni mwa wote pale ofisini, ila nilivyouliza kwa watu wengine walidai kuwa wanamfahamu yule dada, kuwa yule dada ni mpiga madili, watu wakasema kwamaana hiyo kuna mtu atakuwa kampa kazi ya kuja ofisini kwangu ila mpaka muda huu sijajua ni mtu gani na alikuwa na lengo gani”
Pale ndio maneno ya Dora yalianza kufanya kazi vizuri katika akili ya mama Angel na moja kwa moja, na kumfanya azidi kumchukia Sia kwani jibu alilokuwa nalo kwenye akili yake ni kuwa Sia hakuwa mtu mzuri tena, basi alimuuliza tena kaka yake,
“Kaka Tony, hivi hakuna hata mtu mmoja aliyesema kuwa huyo dada huwa anatumiwa na nani?”
“Nasikia huwa anatumiwa na watu mbalimbali, kwa maana hiyo hata kuanguka hakuanguka wala nini, yule alikuwa kwenye maigizo tu”
“Ooooh sema kwa mtindo huo basi inatakiwa kuwa makini sana”
“Ni kweli, haswaaa kwasisi wafanyabiashara maana utakuta mara nyingine unafatiliwa na mtu bila hata kujua kuwa unafatiliwa, ila inatakiwa kuwa makini sana. Nataka kufunga kamera kwenye ofisi yangu”
“Oooh utakuwa umefanya jambo la maana sana”
Kisha mama Angel alimuuliza baba Angel,
“Hivi na ile ofisi mpya mume wangu umefunga kamera kweli!”
“Mmmmh bado sijafunga kule”
“Mi naona ni vyema nako ufunge kamera”
“Sawa sawa, nitafanya hivyo tu”
Basi wakaongea pale na kuamua kuaga, ambapo baba Angel na mama Angel waliondoka kwani waliona muda wao umeisha wa kuendelea kukaa mahali hapo.
Mama Angel na baba Angel walipofika nyumbani waliwakuta watoto wao wakiwa makini sana na kuangalia Tv, kama kawaida mama Angel aliwatimua maana hakupenda wakae pale sebleni kwa muda mrefu ila kitendo cha kuwatimua wale watoto wake muda huo walienda tu chumba kimoja ambapo walienda chumbani kwa Erick na kuanza kuongea mambo mbalimbali, Erica alimuuliza kaka yake,
“Sasa hizo muvi za ngumi Samia akizileta tutakuwa tunaangalia wapi ikiwa mama anatufukuza sebleni?”
“Ooooh mbona jambo dogo hilo, sikia nikwambie mimi na wewe inatakiwa letu liwe moja. Mbona kwenye ile sebule ya juu ina Tv pia, si huwa wanasema hadi wageni waje? Mimi ndio ninafungua za vyumba vyote humu ndani kwahiyo hata usijali tutakuwa tunaenda na kuangalia kule”
“Jamani, ndiomana nakupenda Erick, ila mimi picha za ngumi naogopa sana”
“Sasa unaogopa nini wakati utakuwa unaangalia na mimi? Usiogope maana tutaangalia wote”
“Sawa kaka yangu, basi tucheze karata na leo”
Erick alikubali na kuanza kucheza karata ambapo kama kawaida walicheza sana hadi usiku na wakajikuta wameshikwa na usingizi mule mule chumbani kwa Erick.
Kulipokucha, Erick alikuwa wa kwanza kuamka leo na kumshtua dada yake ambaye nae alikurupuka, kwahiyo ile tabia ilikuwa kawaida kabisa kwao maana haikuwa mara ya kwanza ukizingatia mara nyingi walijikuta wakiwa pamoja.
Basi asubuhi ile nyumba nzima leo walienda kwenye ibada hadi Junior, ingawa huwa ni mbishi kwenda ibadani ila leo alienda, kwahiyo nyumba nzima waliondoka.
Wakiwa ibadani, Erica alitoka mara moja maana kuna kitu alikiona nje ya Kanisa wakati wanataka kuingia, kwahiyo walipokuwa Ibadani tu aliwavizia na kutoka zake nje ili kuangalia kile alichokiona, basi aliondoka hadi lile eneo ila kuna kijana aligongana nae kikumbo na kuanza kuombana nae msamaha,
“Nisamehe tafadhari”
“Nisamehe mimi kwa kutoangalia mbele”
“Aaaah usijali chochote, by the way naitwa Bahati, vipi wewe unaitwa nani?”
“Naitwa Erica”
“Ooooh jina zuri sana, hongera”
“Asante”
Erica macho yote yalikuwa pale alipoona alichokuwa anakitaka ila kuangalia vizuri alikuta kimeshanunuliwa, na kujikuta akisema,
“Aaaargh washachukua tayari”
Yule Bahati alimuuliza,
“Wamechukua kitu gani?”
“Kuna kiatu nilikiona pale, nikakipenda sana, yani nilitaka kukinunua jamani, wamekichukua tayari”
Basi Bahati alisogea pale na Erica na kujua ambaye alichukua kile kiatu kisha kwenda kumuomba ili waweze kununua kile kiatu, yule mtu aliwaambia labda wampe hela mara mbili ya bei ya kawaida ya kile kiatu. Kilikuwa ni kiatu cha kawaida kabisa ila Erica alionekana kukipenda sana, kiliuzwa elfu tano kwahiyo yule mtu alisema labda apewe elfu kumi, Bahati akamuangalia Erica na kumuuliza,
“Je utakinunua kwa bei hiyo?”
Erica aliitikia tu na kufanya Bahati amuulize tena ila Erica alikaa kimya, kwani kiukweli hakuwa na hela yoyote pale ila alikuwa akijitutumua tu kuwa anataka kununua kile kiatu, badae akamwambia Bahati,
“Mwache tu aende, nilikuwa nakiangalia tu”
“Mmmh jamani, hadi tumemrudisha ujue!”
“Aaaaah kumbe hela yenyewe sina”
Basi Bahati alitoa hela yake na kununua kile kiatu kwa yule mtu kisha alimkabidhi Erica kile kiatu, kwakweli Erica alitabasamu na kufurahi sana huku akimwambia,
“Asante sana”
“Usijali, natumaini tutaonana tena”
Basi Erica moja kwa moja alirudi tena kanisani lakini hakuna mwanafamilia wa Erica aliyegundua kuwa Erica alitoka nje ya kanisa ule muda wa ibada.