Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #201
SEHEMU YA 168
Leo Junior aliondoka na Vaileth kuelekea kwa mama yake, na walifika na kumkuta mama yao akiendelea na mambo yake ya siku hiyo, mama Junior aliwakaribisha na kusema,
“Eeeeh leo na wewe Vaileth umetaka kupafahamu kwangu!”
Vaileth akatabasamu tu kisha mama Junior alimwambia mwanae,
“Kwanza hongera sana kwa kumaliza kidato cha nne mwanangu, halafu pili bora umekuja kwani nataka wiki ijayo twende pamoja kwa bibi yako”
“Aaaah mama, nitaenda mwenyewe tu”
“Kheee kwanini wakati mimi nipo?”
“Usijali mama, nitaenda mwenyewe kwa bibi”
Mama Junior hakutaka kuongea zaidi ila pia hakujua ni kwanini mtoto wake ameenda na Vaileth kwa siku hiyo kwani hakujua kazi ya Vaileth ni kitu gani.
Jioni ilipofika, Junior aliaga kuwa anaondoka na Vaileth kuelekea kwa mamake mdogo, mama yake alimsihi sana alale ila Junior alikataa kabisa na hivyobasi akaondoka akiwa ameongozana na Vaileth.
Wakiwa njiani, Junior alimwambia Vaileth,
“Nitakutambulisha kwa ndugu zangu wote, nataka wote wajue ni jinsi gani nakupenda”
“Mmmh Junior, unajua ni tatizo kubwa hilo?”
“Tatizo lipi sasa? Kwani kupenda ni dhambi? Kupenda sio dhambi wala nini, ni kweli nakupenda kweli kwahiyo sioni kama kuna sababu ya kunizuia mimi kufanya kile nitakacho, siwezi kwenda kuishi tena nyumbani kwani nahitaji muda mwingi niwe nakuona wewe”
Vaileth hakuongeza neno lolote zaidi ya kutabasamu tu, kwa upande mwingine alijiona kuwa yupo sawa ila kwa upande mwingine aliona kuwa anafanya makosa makubwa sana.
Mama Angel, leo alirudi mapema tu nyumbani kwake, ila baada ya muda mfupi tu Junior na Vaileth nao walirudi na kumpa salamu za kule walipotoka, basi aliongea nao kidogo na moja kwa moja akainuka na kuelekea chumbani kwake.
Ila alipofika tu chumbani kwake, alipigiwa simu na mama Junior na kuanza kuongea nae,
“Weee mama Angel, hivi huyo Junior na Vaileth nini kinaendelea kati yao?”
“Kwanini dada?”
“Mmmh nahisi kama kuna mahusiano ya kimapenzi kati yao!”
“Mmmh sidhani dada, Vaileth anatambua wazi tabia za Junior, kweli kabisa aanze tu kuwa na mahusiano na Junior jamani! Basi atakuwa hana akili kabisa, ila naona wakiishi tu kama kaka na dada”
“Hebu kuwa makini mdogo wangu, kwa siku hii moja tu nimeweza kuelewa kuwa kuna kitu hakipo sawa kati yao, unajua kama mzazi basi jambo kama hilo lazima liniumize, halafu huyu Vaileth ni mkubwa, halafu si ana mtoto huyu!”
“Ndio ana mtoto, tena mkubwa tu, nadhani kwasasa mwanae ana miaka mitano”
“Haya sasa, mwanamke mwenye mtoto mkubwa wa miaka mitano ndio akawe na mahusiano na mwanangu kweli!! Hapana jamani, sijapenda, hebu fatilia hilo swala kwakweli, unajua sio kawaida eeeh! Ni kweli Junior ana mapungufu yake, ila haijawahi kutokea kwa Junior kugoma kulala hapa nyumbani kwangu na vile vile kugoma kuongozana na mimi kwenda kwa bibi yake na badala yake anadai kuwa ataenda mwenyewe, nahisi kuna kitu kipo juu ya huyu msichana”
“Sawa nimekusikia dada, nakuahidi kuwa nitafanyia kazi hilo swala na nitajua imekuwaje, yani nitaelewa tu mbivu na mbichi”
Mama Angel aliongea na dada yake na kumpa moyo pale, ila baada ya kukata ile simu alijiona wazi kuanza kuhangaika na kazi mpya sasa ya kumfatilia Junior na Vaileth wakati amepumzika kumfatilia Angel.
Ila wakati akiongea na simu ile kumbe mwanae Erica alikuwepo mlangoni, na kwavile alikuwa akiongea kwa nguvu basi mwanae Erica alisikia kila kitu ambacho mama yake alizungumzia kwenye ile simu.
Leo Junior aliondoka na Vaileth kuelekea kwa mama yake, na walifika na kumkuta mama yao akiendelea na mambo yake ya siku hiyo, mama Junior aliwakaribisha na kusema,
“Eeeeh leo na wewe Vaileth umetaka kupafahamu kwangu!”
Vaileth akatabasamu tu kisha mama Junior alimwambia mwanae,
“Kwanza hongera sana kwa kumaliza kidato cha nne mwanangu, halafu pili bora umekuja kwani nataka wiki ijayo twende pamoja kwa bibi yako”
“Aaaah mama, nitaenda mwenyewe tu”
“Kheee kwanini wakati mimi nipo?”
“Usijali mama, nitaenda mwenyewe kwa bibi”
Mama Junior hakutaka kuongea zaidi ila pia hakujua ni kwanini mtoto wake ameenda na Vaileth kwa siku hiyo kwani hakujua kazi ya Vaileth ni kitu gani.
Jioni ilipofika, Junior aliaga kuwa anaondoka na Vaileth kuelekea kwa mamake mdogo, mama yake alimsihi sana alale ila Junior alikataa kabisa na hivyobasi akaondoka akiwa ameongozana na Vaileth.
Wakiwa njiani, Junior alimwambia Vaileth,
“Nitakutambulisha kwa ndugu zangu wote, nataka wote wajue ni jinsi gani nakupenda”
“Mmmh Junior, unajua ni tatizo kubwa hilo?”
“Tatizo lipi sasa? Kwani kupenda ni dhambi? Kupenda sio dhambi wala nini, ni kweli nakupenda kweli kwahiyo sioni kama kuna sababu ya kunizuia mimi kufanya kile nitakacho, siwezi kwenda kuishi tena nyumbani kwani nahitaji muda mwingi niwe nakuona wewe”
Vaileth hakuongeza neno lolote zaidi ya kutabasamu tu, kwa upande mwingine alijiona kuwa yupo sawa ila kwa upande mwingine aliona kuwa anafanya makosa makubwa sana.
Mama Angel, leo alirudi mapema tu nyumbani kwake, ila baada ya muda mfupi tu Junior na Vaileth nao walirudi na kumpa salamu za kule walipotoka, basi aliongea nao kidogo na moja kwa moja akainuka na kuelekea chumbani kwake.
Ila alipofika tu chumbani kwake, alipigiwa simu na mama Junior na kuanza kuongea nae,
“Weee mama Angel, hivi huyo Junior na Vaileth nini kinaendelea kati yao?”
“Kwanini dada?”
“Mmmh nahisi kama kuna mahusiano ya kimapenzi kati yao!”
“Mmmh sidhani dada, Vaileth anatambua wazi tabia za Junior, kweli kabisa aanze tu kuwa na mahusiano na Junior jamani! Basi atakuwa hana akili kabisa, ila naona wakiishi tu kama kaka na dada”
“Hebu kuwa makini mdogo wangu, kwa siku hii moja tu nimeweza kuelewa kuwa kuna kitu hakipo sawa kati yao, unajua kama mzazi basi jambo kama hilo lazima liniumize, halafu huyu Vaileth ni mkubwa, halafu si ana mtoto huyu!”
“Ndio ana mtoto, tena mkubwa tu, nadhani kwasasa mwanae ana miaka mitano”
“Haya sasa, mwanamke mwenye mtoto mkubwa wa miaka mitano ndio akawe na mahusiano na mwanangu kweli!! Hapana jamani, sijapenda, hebu fatilia hilo swala kwakweli, unajua sio kawaida eeeh! Ni kweli Junior ana mapungufu yake, ila haijawahi kutokea kwa Junior kugoma kulala hapa nyumbani kwangu na vile vile kugoma kuongozana na mimi kwenda kwa bibi yake na badala yake anadai kuwa ataenda mwenyewe, nahisi kuna kitu kipo juu ya huyu msichana”
“Sawa nimekusikia dada, nakuahidi kuwa nitafanyia kazi hilo swala na nitajua imekuwaje, yani nitaelewa tu mbivu na mbichi”
Mama Angel aliongea na dada yake na kumpa moyo pale, ila baada ya kukata ile simu alijiona wazi kuanza kuhangaika na kazi mpya sasa ya kumfatilia Junior na Vaileth wakati amepumzika kumfatilia Angel.
Ila wakati akiongea na simu ile kumbe mwanae Erica alikuwepo mlangoni, na kwavile alikuwa akiongea kwa nguvu basi mwanae Erica alisikia kila kitu ambacho mama yake alizungumzia kwenye ile simu.