Simulizi : Nguvu ya Mapenzi

Simulizi : Nguvu ya Mapenzi

SEHEMU YA 186

Kulipokucha siku hiyo Vaileth alichelewa sana kuamka, yani tofauti na siku zingine na hii ilitokana na sababu ya yeye na Junior kutumia muda mwingi sana katika kubembelezana usiku wa siku hiyo, basi bibi wa Angel alienda moja kwa moja chumbani kwa Vaileth na kufungua mlango ila leo Vaileth hakukumbuka kufunga mlango kwani Junior alivyoingia usiku alikuwa na kisirani nae kwahiyo walijikuta tu wakiongea huku mlango umefungwa kawaida na hata hivyo familia hii haikuwa sana na utaratibu wa kufunga milango ndiomana watu walijikuta wakiingia tu ndani.
Ila kwa muda huu Junior alikuwa ameenda chooni, kwahiyo huyu bibi alimkuta Vaileth amelala mwenyewe na kumshtua,
“Wewe Vaileth, mpaka muda huu kweli! Unalala vipi hadi saa hizi!”
Vaileth alishtuka na kumsalimia huyu bibi huku akimuomba samahani, basi bibi nae katika kupepesa macho yake mule chumbani akaiona suruali ya Junior, sema kwavile hakuijua suruali ile kama ni ya Junior akauliza,
“Wewe Vaileth, ile nguo ya kiume inafanya nini chumbani kwako?”
Vaileth nae akaiangalia ile suruali na kupumua kidogo kwani hakuwa hata na jibu la kusema, basi yule bibi akaguna na kutoka ila kumbe hakwenda mbali kwani alikuwa pale pale mlangoni.
Basi Junior nae alitoka chooni ila Vaileth alimuwahi kule kule chooni na kumwambia,
“Mmmh bibi aliingia huku muda sio mrefu ujue, sijui umemsikia?”
“Dah! Hata sijamsikia maana nilikuwa na mawenge ya usingizi”
“Halafu kaona suruali yako, kaniuliza nimekosa jibu la kumjibu. Kwahiyo ni vyema kama ukiondoka muda huu”
“Weee huyu bibi tunamjua wenyewe, wewe toka tu, halafu mimi nitatoka kwa muda wangu au ukiona kaenda chumbani kumuogesha mtoto ndio uje unitonye nitoke, bibi ni mchunguzi huyu balaa”
Mara mlango wa chumbani ulifunguliwa tena halafu bibi akasema,
“Wewe Vaileth, unajikanyaga kitu gani sasa?”
Basi Vaileth alitoka kule chooni na kufunga ule mlango vizuri ila huyu bibi aliguna tena yani mawazo ya huyu bibi alihisi kuwa Vaileth alikuwa na mlinzi wa nyumba hiyo tu yani hakuwaza kuwa ni Junior ndio alikuwepo chumbani kwa Vaileth.
Baada ya muda kidogo ndio Vaileth alikuja na kumwambia Junior kuwa atoke maana yule bibi tayari alienda kumuogesha mtoto.
Muda Junior anatoka kama mwizi, alikutana na Angel ambaye alimuangalia kwa muda na kucheka ila muda huo Junior alikuwa kashaondoka na kuelekea chumbani kwake, yani Angel alicheka na kujisemea,
“Jamani mapenzi haya loh! Sasa huyu Vaileth wa kuwa na Junior kweli jamani! Yani mapenzi ni upofu”
Halafu akaondoka zake na kuelekea jikoni kwani ilitakiwa siku hiyo wajiandae kwaajili ya kwenda kanisani kwani ilikuwa ni siku ya Jumapili.
 
SEHEMU YA 187

Baba Angel na mke wake walikuwa nyumbani tu siku hii pamoja na mama yao, na Vaileth. Basi bibi Angel alianza kuongea na mwanae kuhusu alichokiona siku hiyo,
“Hivi mwanangu hapa nyumbani kwako umeshawahi kuchunguza?”
“Kitu gani mama?”
“Yule mlinzi wako unajua kuwa ana mahusiano na Vaileth?”
“Kheee kumbe! Mama hata sikujui kabisa, kumbe Vaileth ana mahusiano na yule mlinzi! Jamani, ujue mama yule mlinzi ana mke?”
“Kheee kumbe ana mke wake! Basi msichana wako ndio anadanganywa hapo, ukiona mambo hayaeleweki humu ndani jua ni mlinzi wako na msichana wako wa kazi”
“Ngoja niwe vizuri mama ndio nitaweza kushughulika na hawa watu, ila nitafanyeje sasa?”
“Waambie kama wanapendana waoane, oooh ila ndio hivyo kumbe mlinzi ni mume wa mtu. Sikia mwanangu ongea nae Vaileth vizuri, mwelezee kuhusu maisha yalivyo unajua sio vizuri aharibikie nyumbani kwako”
Mama Angel hata hakutaka kupoteza muda kwani muda huo huo alimuita Vaileth ambaye moja kwa moja alienda chumbani, kwa kipindi hiki yani mchana basi mama Angel alikuwa akishinda kwenye chumba maalum ambacho kiliwekwa kwaajili ya mtoto, kwahiyo moja kwa moja Vaileth alienda kwenye chumba hiko kusikiliza, ila muda huu bibi Angel nae aliitwa mara moja na baba Angel kwahiyo aliinuka hapo na kwenda kumsikiliza mkwe wake, kwahiyo mule ndani alibaki Vaileth na mama Angel.
“Hebu kaa chini Vai”
Basi Vaileth alikaa na kuanza kumsikiliza,
“Eti una mahusiano na mlinzi?”
Vaileth alibaki akishangaa bila kujibu chochote, mara simu ya mama Angel iliingia ujumbe kwahiyo alichukua na kusoma kwanza ule ujumbe,
“Hongera sana kwa kupata mtoto wa kike, yani wewe uzao wako ni wanawake tupu. Ni mimi Sia”
Kwakweli mama Angel alichukia sana kusoma ujumbe huu na kujikuta akimwambia Vaileth akaendelee tu na kazi zake hata hakuweza kuongea nae tena.

Leo ni Angel pamoja na wadogo zake na Junior tu ndio walioenda Kanisani, kwakweli ilikuwa ni siku nzuri sana kwa upande wa Angel na ilikuwa siku nzuri sana kwa upande wa Erica kwani walijiona kuwa watakuwa huru sana katika mambo yote ya siku hiyo na hawatafatiliwa sana.
Wakati Erica akiwa Kanisani siku hiyo alijikuta kila muda akiinuka na kutoka nje kidogo, muda ulipokaribia kutoka na yeye aliinuka na kutoka nje kabisa na alipofika nje alionana na Bahati kanakwamba Bahati nae alikuwa mitaa hiyo akimuangalia Erica, basi alisogea karibu na kuanza kumsalimia,
“Kwani wewe unakaa karibu na hili Kanisa au na wewe unasali hapa?”
“Hapana, mimi nilipita tu ili nikuangalie kama wewe umekuja leo. Huwa napita mara kwa mara ila leo nimebahatika kukuona tena”
“Unaonekana ni mstaarabu sana wewe”
Bahati akawa anatabasamu tu, ila muda kidogo alisogea pale Erick na alionekana kuchukizwa sana kwani muda huo huo alianza kumsema mdogo wake,
“Yani wewe Erica kweli unatoka Kanisani na kuja nje kufanya upuuzi?”
Basi akamzaba kibao maana Erick kwa kawaida yake alikuwa ni mtu wa hasira sana, alishangaa baada ya kumzaba kibao alitokea Elly kumbe naye alikuwepo kwenye ibada kwahiyo muda huo walitoka, Elly alimuuliza Erick,
“Sasa Erick ndio unapata faida gani kumpiga kibao Erica?”
“Usiingilie mambo ya undugu wetu hayakuhusu”
“Jiheshimu wewe, hayakuhusu ndio nini?”
Erick alichukia na kutaka kumzaba kibao na Elly, ila gafla mkono wa Erick ulishikwa na muda huo huo Elly alisikika akiwaambia wenzie huku akitabasamu,
“Jamani, huyo ndio mama yangu”
Alikuwa ni mwanamke ambaye alimshika mkono Erick ili asimnase kibao Elly, basi Erick alimuangalia mwanamke yule na kuona kuwa ni yule yule mwanamke ambaye anadai kuwa ndiye mama yake.
 
SEHEMU YA 188

Erick alichukia na kutaka kumzaba kibao na Elly, ila gafla mkono wa Erick ulishikwa na muda huo huo Elly alisikika akiwaambia wenzie huku akitabasamu,
“Jamani, huyo ndio mama yangu”
Alikuwa ni mwanamke ambaye alimshika mkono Erick ili asimnase kibao Elly, basi Erick alimuangalia mwanamke yule na kuona kuwa ni yule yule mwanamke ambaye anadai kuwa ndiye mama yake.
Kwakweli Erick alichukia zaidi muda huu kwa kitendo cha kumuona huyu mama tena kwani kila alipomuona huyu mama alihisi kuharibiwa siku kabisa, basi muda huo huo alimsjika mkono Erica na kuanza kuondoka nae, ila Angel na Junior walimuona kwahiyo walimfata kwa nyuma na moja kwa moja alienda kuingia nae kwenye gari na kuanza kuendesha akielekea nyumbani kwao yani akili yake ilikuwa haisomi kabisa kwa muda huo, basi Angel alimuuliza,
“Erick, unajua sijakuelewa leo, mbona imekuwa hivi!”
Erica akajibu,
“Unajua hata mimi nimemshangaa Erick, kwanza kanipiga kibao bila hata kuniuliza chochote kile, halafu katokea Elly na mama yake pale ndio Erick kachukia hatari na kunishika mkono huku akinikokota tuondoke”
“Kheee Erick jamani mdogo wangu, unakuwaje wewe?”
Junior akawasema wale waliokuwa wakimsema Erick,
“Jamani, hebu mambo mengine subirini tufike nyumbani, yani anayeendesha gari ni Erick halafu ndio mnamshambulia kwa maneno mnataka nini? Subirini tufike nyumbani”
Basi walinyamaza kimya ila Erica alichukia sana kwa kitendo ambacho kimefanywa na kaka yake ingawa yeye hakujua ukweli kuhusu mama yake Elly ndio anayemwambia Erick kuwa ni mtoto wake.

Mama Angel muda huu alikuwa na hasira sana halafu akili yake ilikosa muelekeo kabisa, moja kwa moja mama yake alivyorudi chumbani mule hata hakumuuliza kuwa alikuwa akiongea nini na mumewe wala nini kwani muda huo huo alitoka na kumkimbilia baba Angel ambapo alimuita na kwenda nae chumbani kuzungumza, na kabla ya kusema nae chochote alimpa ule ukumbe ambao alitumiwa na Sia,
“Chukua usome”
Basi baba Angel alisoma na kukunja sura pia huku akisema,
“Jamani, huyu Sia ananitakia nini na familia yangu lakini?”
Kisha mama Angel alianza kumsimulia kisa cha siku ile ambapo walienda na Erick kule dukani hadi akapatwa na uchungu,
“Yani chanzo ni huyo mwanamke, kamlisha sumu mwanangu kuwa mimi sio mama yake. Unajua mwanzoni wakati Erick akinielezea sikumuelewa kabisa maana hata Erick hakumfahamu Sia, ila tulivyofika pale dukani ndio nikafahamu. Jamani Sia ana nini na mimi lakini? Eti anasema uzazo wangu ni wanawake tu, kwahiyo Erick sio mwanangu? Inamaana sikuzaa mapacha au ni nini mbona sielewi?”
Baba Angel akapumua kidogo na kumwambia mke wake,
“Unajua ndiomana siku hizi huwa wanataka hadi baba ande akashuhudie watoto wanavyozaliwa, ila mimi nitashuhudiaje wakati unajifungua na mar azote inakuwaga kama gafla? Ila mke wangu usiwe na mawazo, kuna mambo ya kujiuliza”
“Mambo gani sasa? Kama Erick sio mwanangu inamaana mwanangu yuko wapi? Sitaki kukubaliana na hilo jamabo kabisa, Erick ni mtoto wangu, inamaana nilizaa mapacha wakike tupu? Je mwenzie na Erica yuko wapi? Hapana, hawa ni watoto wangu”
“Mke wangu naomba uondoe hayo mawazo kabisa, hebu kumbuka siku ile mimba yako tulipoamua kwenda kupiga ultrasound, tulikuta kuna mapacha wakike na wakiume na hiyo ikawa ni furaha kubwa sana kwangu na kwako mke wangu. Na siku umejifungua, ingawa ulijifungua kwa operesheni ila ulikuwa peke yako, na nilifanya yote kuhakikisha unapata huduma inayotakiwa, kisha tulikabidhiwa watoto wetu wawili yani wale wale tulioambiwa kabla, na hapo kwa furaha tuliyonayo tuliamua kuwapa hawa watoto majina yetu japo wengi sana walipinga ila sababu ya upendo wetu tuliamua kufanya hivyo na hawa watoto tuliona kuwa ni kiunganisho chema zaidi kwetu kwani watafanya tuzidi kudumisha upendo wetu. Leo hii atokee mjinga mmoja, mwendawazimu mmoja, asiye na akili mmoja aje kuchanganya akili zetu sijui mtoto sio wa kwetu, sijui huwa unazaa watoto wa kike tupu. Kwanini akili iharibiwe na chizi? Watu husema chizi akikwapua nguo zako kisha ukaanza kumkumbiza basi utaonekana chizi maana utakuwa mtupu halafu unakimbiza mwenye nguo. Yule mwanamke ni chizi, hata siku ukipata muda wa kuonana nae na kuongea nae utaona kuwa ni chizi na zaidi ya chizi, nakuomba mke wangu uwe na amani katika moyo wako. Mimi ndio baba wa Angel, na mimi ndio baba wa Erick na Erica na tena ni baba wa Ester, hata jamii nzima itokee na kusema hawa watoto wote sio wangu sioni tatizo lolote kwani hawa ni watoto wangu, nakupenda mke wangu na ninakuamini kwa vyovyote vile. Achana na chizi asiharibu mawazo yako, na hata ungezaa wa kiume tupu au wakike tupu basi bado ningekupenda. Naomba mke wangu kuwa na amani katika moyo wako, watoto wangu wote nawapenda, haijalishi chochote. Huyo Angel washaongea hadi basi na mimi ukweli naujua ila hata siku moja hujawahi kunisikia wala hutowahi kunisikia nikisema kuwa sio mwanangu, hawa ni watoto wangu na wote nawapenda”
Maneno ya baba Angel yalisuuza moyo wa mama Angel na kujikuta faraja na amani ya moyo wake ikirudi upya kabisa, alijikuta akimkumbatia mume wake kwa furaha kwani alimuona kuwa ni mwanaume wa pekee sana katika maisha yake, basi baba Angel nae alimkumbatia kisha akamuuliza,
“Mke wangu, unataka nikuletee zawadi gani leo maana nitatoka kidogo!”
“Mmmh, yoyote tu utakayoichagua wewe na utakayoipenda wewe”
“Haya mke wangu, nakupenda sana”
Basi wakakumbatiana tena pale halafu baba Angel alitoka zake na kuondoka kisha mama Angel alirudi kule chumbani alipo mama yake na mtoto.
Basi mama yake alimuuliza,
“Kheee mwanangu, ndio ulienda kumuuliza mumeo kitu alichokuwa akizungumza na mimi?”
“Hapana mama sio hivyo, nilienda kuongea nae kuhusu mambo mengine kabisa, wala sio hayo mama yangu”
“Haya sawa, ila huyu mtoto anaonekana atakuwa mtu wa dini sana”
“Kwanini mama?”
“Hata mimi namuona, anaonekana atakuwa vizuri mwanangu. Nilikuwa naongea na mumeo mambo ya maana tu ni kuhusu mkwe wako ila usijali tutazungumza mwanangu na kuyaweka sawa”
Mama Angel alijua tu yatakuwa yanaendelea yale yay eye kumchukua mtoto kinguvu ila kwavile mama yake alisema kuwa atamwambia basi hakuwa na papara kuhusu hilo.
 
SEHEMU YA 189

Wakati baba Angel anatoka ndipo alipokutana na watoto wake wakiwa wametoka Kanisani, ila aliona kuwa Erick kama hayupo sawa, ilibidi amuite mwanae kwenye gari lake ambapo Erick alienda moja kwa moja kwenye gari ya baba yake halafu baba Angel hakuongea nae jambo lolote kwa muda huo zaidi ya kuondoka nae na kwenda nae mahali ambapo palikuwa na mgahawa halafu akaagiza chakula na kumtaka Erick nae aagize chakula ambapo alifanya hivyo halafu alianza kuongea nae,
“Eeeeh mwanangu Erick unajua nimewaangalia pale mlivyoingia ndani nimeona kuwa haupo sawa kabisa, kwani tatizo ni nini mwanangu?”
“Unajua baba sielewi kabisa, kwa kifupi simuelewi yule anayedai ni mama yangu”
“Kwani kakufata tena?”
“Ni hivi baba, ile shule niliyohama ambapo nilimuacha Erica, alikuja kijana mmoja kusoma pale na alikuwa akiitwa Elly, yani stori za Erica kwa kipindi hiko ni Elly Elly tu”
“Oooh nimemkumbuka mwanangu, nakumbuka kuna siku Erica alileta visheti nyumbani na vikanidhuru, alisema kapewa na Elly sijui”
“Ndio, kumbe yule mwanamke ndiye mama yake Elly, na leo tumesali nao Kanisani”
“Kumbe!! Sasa kwanini anaifatilia familia yangu kiasi hiki jamani! Mwanangu niskilize, mimi ni baba yako naomba unisikilize kwa makini sana. Upo tayari kunisikiliza?”
“Nipo tayari baba”
“Nakumbuka nishawahi kukwambia jambo hili, katika maisha inatakiwa mtu uwe makini sana usijaribu kuharibu maisha yako au kuyachanganya kwa chochote kile. Mimi nilichanganya maisha yangu mwanangu na mwisho wa siku nikakutana na watu wasiokuwa na akili timamu kama huyo mwanamke, hata namshangaa kuifatilia familia yangu, hakuna nilichomkosea hata kimoja ila namshangaa sana. Mwanangu ninachotaka kukwambia sasa ni wewe uwe makini sana na huyo mwanamke, yani ni chizi asije siku akakudhuru mwanangu, kama aliweza kumpa visheti huyo Ellyn a akaniletea mimi vikanidhuru je hawezi kutenda jambo baya? Halafu anadai kuwa ni mama yako, toka lini mtu unakuwa na mama asiyekupenda? Yani mama gani ambaye hakupendi? Kwa mujibu wa Steve pale dukani ni kuwa yule mama anang’ang’ania duka lile kwaajili ya mwanae na sasa nimepata picha, kumbe mwanae ni huyo Elly. Jamani mwanangu acha kuumia kichwa kabisa, huyo mama ni chizi najua ataendelea kufatilia familia yetu ila wewe ni mtoto wa kiume nan i wajibu yako kuilinda hii familia ili isisambaratike. Je mwanangu unahitaji nikupatie nini ili kuboresha mawasiliano baina yetu maana huyu mwanamke sitaki tena awe anakutia ujinga, popote utakapokutana nae na chochote atakachokuambia nataka unitaarifu”
“Sijui baba, labda simu”
“Umejibu vyema kwani ndicho nilichokuwa namaanisha mwanangu, uwe na simu ili tuwe tunawasiliana na hiyo ni muhimu sana kwa baba na mtoto”
Kuna mtu alisogea pale na kuvuta kiti kisha kuwasalimia baba Angel na Erick, mtu huyu Erick alimfahamu maana alikuwa ni mwalimu wake basi Erick alimtambulisha yule mwalimu kwa baba yake,
“Baba, huyu ni mwalimu wangu, tumemzoea kwa jina la madam Oliva, madam huyu ndio baba yangu”
“Oooh nafurahi sana kukufahamu baba Erick jamani, kwanza hongera sana. Nilipowaona hapa nikaamua nisogee ili niwasalimie, na nimefurahi sana kugundua kuwa wewe ndiye baba Erick”
“Na mimi nimefurahi pia kukufahamu madam”
Ila baba Angel alikuwa akijiuliza kuwa huyu mwalimu alimpa hongera ya nini, ila aliwaza kuwa pengine ni sababu ya kupata mtoto ila huyu mwalimu anatambua swala hilo? Basi alimuuliza,
“Hey, ila sijakuuliza umenipa hongera ya nini?”
“Ooooh! Nimekupa hongera juu ya kijana wako Erick, kwakweli hapa mtoto umepata jamani. Hongera sana, huyu mtoto sio namsifia tu sababu yupo ila hata kama asingekuwepo basi ningekwambia hili. Umepata mtoto mwerevu, na mtoto asikivu na siye na makuu kabisa. Hongera sana”
“Asante sana madam”
“Ni vyema kama nikipata mawasiliano yako ili niwe nakwambia maendeleo ya mtoto darasani”
Baba Angel hakuona kama hilo ni tatizo kabisa, basi alimpa yule madam kadi yake ya namba za simu ili kuweza kuwasiliana nae kwa kipindi kingine.
Basi yule madam hakuondoka pale kwani alikaa nao hadi mwisho yani muda baba Angel na Erick waliaga ndipo yule madam pia alipoondoka.
Basi baba Angel alienda na Erick moja kwa moja dukani ili achukue simu ya kutumia, na alipoichagua alimnunulia na kwenda kununua laini kwaajili ya mwanae huyo kisha akamuuliza,
“Mama yako nimpelekee zawadi gani maana nilimuuliza na akasema yoyote, sasa nimpelekee nini?”
“Mmmh baba, huo mtihani mgumu ila mpelekee zawadi rahisi kabisa ambayo hawezi kuifikiria kuwa utampelekea halafu utaona atasemaje?”
“Zawadi gani sasa?”
“Twende dukani baba, ukaone ni zawadi rahisi kabisa ambayo hata mtoto anaweza kuinunua”
Basi Erick alienda dukani na baba yake kisha akachukua zawadi na kusema kuwa ni zawadi ya mama yake, kwakweli hata baba Angel alishangaa sana ila aliichukua tu na kumwambia mwanae,
“Ila dah! Yani sijafikiria ujue kama zawadi yenyewe ndio hii!”
“Safari ijayo atakutajia zawadi anayoitaka baba, ila ukiona kasema tena yoyote basi atakuwa ameipenda hata hii”
Baba yake alicheka tu kisha wakaingia kwenye gari na kurudi nyumbani moja kwa moja.
 
SEHEMU YA 190

Ilikuwa ni usiku tayari wakati baba Angel na Erick wamerudi nyumbani, kisha baba Angel alienda kumsalimia mke wake ambaye kwa muda huo alikuwa ameenda kulala kwahiyo alikuwa chumbani, mkewe alimuuliza cha kwanza,
“Nasikia ulipotoka tu ukaongozana na Erick, ulienda nae wapi?”
“Aaah nilienda kuongea nae, unajua huyu mtoto amechanganywa sana akili na Sia. Nilimuona kama hayupo sawa, kumbe ni kweli walikutana na Sia”
“Kheee alikutana nae wapi tena?”
“Kumbe leo Sia alienda kusali Kanisa lile lile ambalo huwa tunasali, basi ndio wameonana nae, halafu kumbe yule Elly ndio mtoto wa Sia maana walikutana nae na akawatambulisha mama yake”
“Kheee kumbe Sia ndio aliyetoa vile visheti jamani, ana nini yule mwanamke lakini!”
“Ndiomana nilikwambia mke wangu kuwa yule mwanamke ni chizi, hata asiumize akili yako”
“Ila licha ya uchizi wake, kuna mambo lazima tuwe makini nayo. Kwanza hakupenda tufahamu kuwa yeye ni mama yake Elly kumbuka, nimeenda pale kwake kama mara mbili ila siku mkuta. Kama angekuwa mtu mzuri tungemfahamu kitambo kuwa ni yeye, halafu jambo lingine kamtuma Elly ampe Erica visheti ambavyo vilikudhuru ulipokula. Mume wangu inatakiwa kuwa makini sana na huyo mtu, kwamaana hiyo watoto wasiende tena kusali pale Kanisani”
“Kheee watoto wasisali sababu ya huyo chizi?”
“Ndio, bora wakasali Kanisa la mjini”
“Jamani mke wangu, unaweza kwenda na huko akatufata pia. Kumbuka chizi huwa hachoki”’
“Kwahiyo unafurahia anachokifanya?”
“Hapana sifurahii ila nimejaribu tu kusema mke wangu”
Kisha baba Angel akamtolea ile zawadi mke wake na kumwambia,
“Haya, zawadi hii hapa!”
“Kheee yani ndio umeniletea pipi ya kijiti jamani! Zawadi ya kumpa Ester ndio umeniletea mimi!”
“Aaaah mke wangu, nimekuuliza nikuletee zawadi gani ukanijibu yoyote. Sasa mimi ningekuletea nini jamani!”
“Mbona siku zote huwa nakwambia yoyote ila hujawahi kuniletea pipi?”
“Ila hii ni idea ya Erick, nilipomwambia akuchagulie zawadi basi ndio akakuchagulia hii”
“Mwambie nimeipenda sana”
Kisha mama Angel akaifungua ile pipi na kuanza kuila huku akitoka sebleni, nia yake ilikuwa ni Erick kumuona akiila ile pipi, ni kweli aliwakuta watoto wake sebleni wakila chakula cha usiku na moja kwa moja Erica alianza kucheka na kusema,
“Mama jamani, unakula pipi kama mtoto!”
Erick akajibu,
“Ni wapi pipi imeandikwa kuwa ni ya mtoto tu!!”
Mama Angel nae akasema,
“Nyie watoto ni washamba sana, hii ni zawadi yangu nimepewa na mtu muhimu sana katika maisha yangu ndiomana naila kwa madaha. Kwakweli aliyemshauri baba yenu aniletee zawadi hii nimemfurahia sana, nilikumbuka pipi jamani mimi! Nilikumbuka sana”
Kitendo kile kilimfanya Erick ajihisi raha sana kwenye moyo wake, alifurahi mno kuona kuwa zawadi yake imependwa na mama yake.

Erick alienda kulala baada ya kula tu kwani alikuwa amechoka kwa siku hiyo kutokana na ile mizunguko ya kutoka Kanisani na moja kwa moja kwenda kuzunguka na baba yake, basi alipoingia chumbani, dada yake alimfata na kuanza kuongea nae,
“Eeeeh na mimi zawadi yangu?”
“Kheee zawadi ya nini sasa wewe?”
“Mbona mama kaletewa zawadi na baba?”
“Sasa mama akiletewa zawadi na baba ndio lazima mimi nikuletee wewe zawadi?”
“Mama si Erica, kaletewa zawadi na baba ambaye ni Erick. Sasa wewe ni Erick gani ambaye huna upendo wa baba? Ndiomana mama yako ni mwingine?”
Halafu akaondoka na kuelekea chumbani kwake, ile kauli ilimchukiza sana Erick, hivyobasi na yeye kwa hasira alienda chumbani kwa Erica ili akamseme, alifika na kufungua mlango na kumkuta Erica akivua nguo, yani Erica alipiga kelele zilizofanya hadi mama yao akimbilie chumbani ajue kuna nini,
“Nyie watoto vipi jamani! Mtatuumiza kwa presha!”
Alimkuta Erica kajifunga khanga, huku Erick akiwa amesimama pembeni kwani nae alikuwa akishangaa jinsi dada yake alivypoga kelele, wakati yeye ni mara nyingi tu anamkuta akivua nguo ila hajawahi kupiga kelele, akamshangaa sana ila Erica alimjibu mama yake,
“Niliona mende mama, nadhani hata Erick kakimbia kuangalia tatizo gani”
“Mende kwenye nyumba yangu! Nyie watoto hebu achene masikhara, kesho itabidi nimuite yule mtu wa dawa, yani mende anafanya nini sasa?”
“Ila nahisi ni mawenge yang utu”
“Muone vile, yani wewe utaniumiza kichwa kwa kelele zisizokuwa na maana”
Basi mama yao akatoka, na yeye Erick alitoka zake na kumuacha Erica mwenyewe mule chumbani.
 
SEHEMU YA 191

Muda Erica anapiga kelele, ni muda ambao Junior alikuwa chumbani kwa Vaileth na zile kelele walizisikia ila walizipuuzia sababu ile sauti ni ya Erica na wanaifahamu, basi Vaileth akamwambia Junior,
“Kheee hutaki hata kwenda kuangalia mdogo wako ana tatizo gani?”
“Aaaah yule mtoto mwenyewe mbea balaa, nikamuangalie ana tatizo gani ili iweje? Atajijua mwenyewe na wazazi wake huko, kwasasa ni wewe unayeshughulisha moyo wangu”
Vaileth alitabasamu tu kwani aliona ni fahari na raha kupendwa na Junior ila muda kidogo mlango wa Vaileth uligongwa kwani leo alifunga mlango, basi Vaileth alishtuka na moja kwa moja Junior alienda kujificha chooni ila kwa muda huu alikimbia na nguo zake.
Vaileth akafungua, na mgongaji alikuwa ni bibi yake Angel ambaye alimuuliza Vaileth,
“Mbona leo umelala mapema sana?”
“Bibi, nimeona nimemaliza kazi halafu nilikuwa na uchovu ndiomana nimelala mapema”
“Sawa”
Kisha bibi aliingia chumbani kwa Vaileth na kukaa kitandani halafu akaanza kuongea nae,
“Vaileth usifikirie kuwa nakuingilia maamuzi yako au uhuru wako, unajua kwa nguo niliyoiona asubuhi nimejitafakari sana na kama sitokwambia sasa basi ni nani atakwambia haya! Hivi wewe si una mtoto?”
“Ndio, nina mtoto bibi”
“Baba wa mtoto wako yuko wapi?”
Vaileth aliinama chini na kujibu,
“Hata sijui bibi, alinikimbia”
“Je unataka kuzaa mtoto wa pili na kukimbiwa na huyo mwanaume? Najua jibu litakuwa hapana, starehe zipo na zinafanywa kila leo, zilikuwepo, zipo na zitaendelea kuwepo kwahiyo akili kichwani mwako. Wanaume ni waongo sana, kama wanaume anakupenda kweli mwambie aende kwenu akutambulishe na muoane ila mwanaume wa kukutumia tu mwili wako huyo hakupendi mjukuu wangu. Nimeona nije kukupa hili angalizo kabisa, huyo mwanaume ambaye unamahusiano nae, achana nae maana atakupeleka pabaya. Anayekupenda kweli mwambie akuoe, maisha ya ndoa ni matamu sana na sio maisha haya ya kuruka tuka na kuszalishwa watoto halafu unaachwa. Yangu kwa leo ni hayo tu, saa hizi ni usiku ndio nimekuja kukwambia haya ili uyatafakari muda wote unaolala. Usiku mwema”
Bibi alitoka na kumuacha Vaileth akifunga tena mlango wake kisha Junior alitoka kule chooni alikokuwa amejificha na kurudi kitandani, basi Vaileth akamwambia,
“Umesikia maneno ya bibi? Unatakiwa unioe Junior”
“Ila na wewe Vaileth jamani, huyu ushasema ni bibi sababu mambo yake yamepita ndiomana kaitwa bibi. Sikia nikwambie, mimi nitakuoa tu, ndoa sio kitu cha kukurupuka. Hivi kwasasa nikuoe twende tukaishi wapi? Tule nini? Mimi nilishakwambia sitakuongopea kitu chochote, kwasasa sitaweza kukuoa maana bado sijajipanga kimaisha, hivi huoni raha, tunaishi hapa vizuri tu kama mke na mume, tunakula, tunashiba na tuna sehemu nzuri ya kulala, hakuna tunacholipia, si bili ya umeme, ya maji wala hatununui chakula ila tunakula tunachotaka na mambo yetu tunafanya. Unajua huyu bibi anapokwambia kitu kuna vingine unaweza hata kumshushua maana havina mantiki yoyote, hebu achana na maneno yake. Mimi nitakuoa tu, ila sio kwasasa. Tukijipanga nitakuoa. Achana na maneno ya bibi na tuendelee kula raha tu, kila kitu kipo hapa unataka tuhofie nini jamani Vai? Achana na maneno ya bibi”
Vaileth akapumua kidogo huku Junior akianza kumpapasa na kujikuta hata akisahau yale maneno ya bibi kabisa.
 
SEHEMU YA 192

Muda huu bibi alienda pia chumbani kwa Angel, ila naye Angel alikuwa amefunga mlango kwani kwa muda huo alikuwa akitumia ile simu yake ya magendo ambayo wazazi wake hawaijui, kwahiyo bibi aligonga mlango na Angel alienda kumfungulia.
Kama kawaida bibi alimpa maidha yake pale Angel ila kwa muda huo ilikuwa ni kazi kwani Angel mawazo yake yalikuwa kwenye simu tu, hata hakuwa na wazo la kusema kuwa bibi yake kuna kitu cha muhimu anamwambia,
“Angel mjukuu wangu, kuwa makini sana. Ni wengi watakwambia kuwa wewe ni mzuri ila hawana upendo wa aina yoyote na wewe, unatakiwa kuwa makini na kuyajali maisha yako”
“Sawa bibi nimekusikia ila muda huu nina usingizi sana, nahitaji kulala”
“Basi tutaongea kesho maana nina mengi sana ya kuzungumza na wewe”
“Sawa bibi, usiku mwema”
Yani Angel alimuaga haraka haraka bibi yake ilia pate muda wa kuwasiliana na ile simu yake, basi bibi yake aliondoka na kufanya Angel akafunge mlango kwanza na kuendelea kuwasiliana na simu yake,
“Oooh Samir, bibi yangu alikuja humu chumbani kwangu mara moja”
“Ila Angel nimekumiss sana, yani natamani hata kukuoana. Sikia nikwambie kitu, kesho asubuhi kabisa nitapita hapo kwenu, naomba utoke ili angalau nikupungie mkono tu”
“Sawa hakuna shida, basi nitatoka ule muda ambao wadogo zangu wanaenda shule, kwa kesho nitajifanya nawasindikiza nje ya geti kidogo”
“Nitafurahi sana Angel, yani nimerudi leo mara moja na kesho natakiwa kuondoka tena, kwahiyo nakuomba hiyo asubuhi nikuone hata kwa mbali”
“Usijali utaniona”
Angel aliwasiliana na Samir kisha kuagana na kulala tu moja kwa moja.

Kulipokucha, wakati wakina Erica wakitoka ndani, Angel nae alitoka nao kama alivyopanga na Samir, yani wakati wanatoka hata Erick alimuuliza,
“Dada, leo vipi?”
“Jamani nawasindikiza, kwani vibaya?”
“Sio vibaya dada”
Basi wakatoka wote hadi nje ya geti ambapo Erick alikuwa akisubiri gari la shule akiwa pamoja na Erica, ila ilitangulia gari ya shuleni kwakina Erica na kufanya Erica aondoke ila muda ule ule alifika yule mwanamke ambaye huwa anadai Erick ni mtoto wake, yani Sia ila wakati wanamshangaa pale mara alifika na Samir, ila ni tofauti na jinsi Samir alivyopanga na Angel kuwa atampungia mkono tu kwani cha kushangaza Samir alisogea pale karibu na kumzaba yule mama kibao.

Basi wakatoka wote hadi nje ya geti ambapo Erick alikuwa akisubiri gari la shule akiwa pamoja na Erica, ila ilitangulia gari ya shuleni kwakina Erica na kufanya Erica aondoke ila muda ule ule alifika yule mwanamke ambaye huwa anadai Erick ni mtoto wake, yani Sia ila wakati wanamshangaa pale mara alifika na Samir, ila ni tofauti na jinsi Samir alivyopanga na Angel kuwa atampungia mkono tu kwani cha kushangaza Samir alisogea pale karibu na kumzaba yule mama kibao.
Kitendo kile kiliwashangaza wote pale haswaa Angel ambaye alishangaa zaidi na kumfata Samir,
“Hey mbona unampiga mama wa watu hivyo? Huoni kama huyo ni sawa na mzazi wako!”
Mara gari ya shule yakina Erick lilifika kwahiyo Erick alienda kupanda na kuondoka, basi Samir alionekana kuwa na hasira sana na yule mwanamke na kumwambia Angel,
“Laiti siku ukimfahamu huyu mwanamke vizuri basi utamchukia maisha yako yote”
Yule mwanamke nae akamuangalia Samir na kumwambia,
“Nakushangaa huna adabu kiasi hiki!! Ila baba yako hayupo hivi, na wewe laitti ukijua baba yako wa kweli ni nani basi hata huyu Angel hutomfatilia tena”
Halafu Sia akaondoka zake, na kufanya Samir na Angel watazamane pale, kisha Samir akamwambia Angel,
“Umeona huyu mwanamke alivyo! Yani huyu mama huwa anajifanya anaifahamu sana familia yangu, akitokea yeye basi nyumbani hakuna amani, hata mama yangu hapatani nae. Yani huyu mama huyu hapana”
“Ila sawa na mama yako huyo”
“Weee siwezi kuwa na mama wa dizaini ya huyu mama, hawezi kuwa mama yangu kamwe. Labda niwe kaburini, nakwambia ukimfahamu huyu mama vizuri basi utamchukia maisha yako yako, na ukijua sababu ya mimi kumnasa kibao muda huu basi utaelewa kwanini nimekuwa na hasira hivi!! Kwanza kashaniharibia siku kabisa, Angel ngoja niondoke”
Basi Samir akaondoka zake, yani inaonyesha Samir kachukizwa sana na yule mama hata Angel hakuelewa ni kwanini maana kwa muonekano wa haraka haraka basi Sia alionekana ni mama mmoja mstaarabu sana na asiye na makuu, kwahiyo Angel alibaki akishangaa tu na kuamua kurudi ndani kwao yani ile furaha ambayo alijua ataipata kwa kumuona Samir alishangaa tu kutokuwa nayo kabisa.
Moja kwa moja na yeye alijikuta akimchukia yule mama kwani aliona amekatisha furaha yake, ila wakati anaingia ndani tu mama yake alimuuliza,
“Angel, umetoka wapi hii asubuhi?”
“Mama, nilienda kuwasindikiza wakina Erick, kwahiyo nilikuwa nao hapo nje ya geti wamepanda gari basin a mimi nimerudi ndani”
“Umeanza lini hiyo tabia?”
“Mama jamani, yani nimekaa na kujikuta nakumbuka shule, nakumbuka kuamka asubuhi kwahiyo nikaona ni vyema kama nikianza kuwasindikiza wakina Erick mama, kwani vibaya?”
“Si vibaya, ila kabla hujafanya hivyo uwe unakuja kuniambia”
Angel aliondoka kuelekea chumbani kwake huku akiilalamikia tabia ya mama yake ya kumfatilia sana hadi kumkosesha uhuru.
 
SEHEMU YA 193

Erick nae akiwa kwenye gari alikuwa na mawazo sana, yani moyoni mwake alichukia mno kwa kitendo cha kufatwa na yule mwanamke nyumbani kwao, basi alipokuwa amekaa muda ule ule alisogea Sarah karibu yake yani Sarah alipishana na mtu ili akae karibu na Erick, basi Sarah alimuuliza Erick,
“Yule mama ambaye alikuwa amesimama nanyi getini ni ndugu yenu?”
“Kwanini umeuliza hivyo? Yani hujaulizia wote pale zaidi ya yule mama?”
“Nimeuliza tu Erick nina maana yangu, nijibu kwanza ni ndugu yenu?”
“Hapana, ni mpita njia tu”
“Jamani yule mama simpendi, unajua simpendi balaa”
“Kwanini humpendi sasa, kafanyaje kwani?”
“Yule mama ni mshirikina, hata mama yangu kagombana nae tayari. Ila ugomvi wa huyu mama na mama yangu hata huwa siuelewi mwanzo wala mwisho maana huwa wakikutana ni wanarushiana maneno tu. Kwa kifupi huyu mama ni mkorofi halafu anajifanya anajua maisha ya kila mtu, hebu fikiria mimi mwenyewe huwa ananiambia kuwa anamfahamu baba yangu ni nani!”
“Kheeee! Kwahiyo kakwambia ni nani?”
“Hapana, ila kasema nikitaka kujua ukweli basi niende nyumbani kwake ila mimi siwezi kwenda kwani yule mama ni mshirikina sana”
“Kwani wewe humjui baba yako?”
“Simjui ila kwa mujibu wa mama ni kuwa baba alikufa wakati nipo mdogo sana, aliniacha nikiwa na miaka miwili na huwa mara kwa mara tunaenda na mama kupalilia kaburi la baba, kwahiyo huyu mama huwa namshangaa sana kwa kusema aliyekufa si baba yangu ila baba yangu yupo na yeye ndio anayemfahamu. Yani mama aliyenizaa amfahamu mwingine halafu yeye amfahamu mwingine! Mama hafai yule, nahisi ni mchonganishi wa familia za watu, msimkaribishe kwenu yani familia yenu nzima mtajikuta mnagombana sababu yake”
“Kumbe!! Nashukuru kwa kunipa huo ujumbe, halafu kwasasa nina simu Sarah”
“Ooooh katika habari njema ulizowahi kunipa, ya kwanza ni hiyo, naomba namba zako”
Basi Erick alimtajia namba zake, yani Erick kwa muda huo alikuwa na furaha kidogo baada ya kujua tabia ya yule mwanamke na kuona kuwa sio peke yake anayemfatilia bali ni wengi anawafatilia.
Siku hiyo Erick aliongea vizuri sana na Sarah kiasi kwamba hata Sarah alifurahia yale mazungumzo yake na Erick hadi walipofika shuleni ambapo kila mmoja alienda kwenye darasa lake kwani Sarah alikuwa kidato cha pili, wakati huo Erick akiwa kidato cha kwanza.
 
SEHEMU YA 194

Basi siku ya leo Steve akiwa dukani akiendelea na kazi yake, alipigiwa simu na dada yake na kumuelekeza ambapo lile duka lilipo kisha dada yake alienda kumtembelea kwa siku hiyo hiyo, Steve alifurahi kuonana na dada yake maana kwa kipindi hiko walikuwa hawaishi pamoja wala nini, basi alianza kuongea nae,
“Unajua kwanini nimekutafuta leo?”
“Kheee kwanini dada?”
“Basi leo nimekutana na kale kasichana ambako ulikuwa unakapenda sana, kumbe ana mtoto”
“Kheee dada ulikuwa hujui jamani! Toka kipindi hiko asiwe na mtoto kweli! Kwanza sio kasichana bali atakuwa ni mmama. Ila nilimpenda sana yule, isingekuwa kuingiliwa na huyu jini basi ndio angekuwa mke wangu yule”
“Jini mkata kamba alikuvuruga akili mdogo wangu, ila unajua huwa najilaumu sana, yani mimi tabia zangu za awali ndio zimeniathiri na familia yangu kwa kiasi kikubwa sana. Nakumbuka yule Sia hakuwa na mambo ya waganga kabisa yani yeye alikuwa na upendo wake anaouamini katika moyo wake, yani mimi sijui kilanga gani kikanituma kumueleza kuhusu babu wa Bagamoyo na kumpeleka kule, mwisho wa siku dawa zikaja kukuathiri mdogo wangu. Halafu mpaka leo maisha yako hayapo vizuri sababu ya kuchanganywa akili na yule mwanamke. Pole mdogo wangu”
“Asante sana, yani kiukweli hata nikifikiria kuishi na mwanamke basi moyo wangu huwa naona tu umesizi, hakika alichonifanya Sian i Mungu tu anajua”
Muda kidogo Sia nae alifika pale dukani na kumfanya Dora amshangae na kusema,
“Hutajwi?”
“Ndio sitajwi, kwanza kwanini mnanitaja? Ndio kusema mnanipenda sana? Halafu wewe Steve mara nyingine hebu kuwa mwanaume, achana na maneno ya hawa ndugu zako yatakuharibu. Huyo dada yako amedanga weee, nani ambaye hakujui Dora kama ulikuwa ni mdangaji maarufu hadi umelizoa la kulizoa ndio umejifanya umeokoka na kusema wenzio vibaya. Hii Mbingu kama inapokeaga watu wa aina yako basi kwa hakika kila mtu ataenda Mbinguni. Hivi Dora ni kipi unaweza kunisema mimi? Yule James alikuoa wewe na amekufa na kukuachia mali zake zote si kwasababu yay ale madawa uliyompindua pindua nayo! Mali zote unazo wewe, unatumia wewe na kile kitoto chako tu, kwani James hakuwa na watoto wengine! James nae ana watoto tu wa kutosha, kama umeokoka kweli kwanini usikae chini na kusema watoto wote wa James waje niwape urithi wao? Ila mali zote za James unatumia wewe, hakuna kazi unayoifanya ila kutwa kucha kutembea na biblia na vitabu vya nyimbo, sababu uanjua unakula hela za James muda wote unaoutaka. Kama kuna mtoto mwenye haki zaidi na mali za James basi ni mtoto wa Bite, ila kwasasa eti kachukuliwa na Erica ndio anaishi nyumbani kwake wakati yule mtoto hata angeamua kuwa na mjengo wake angeweza. Kuwa na huruma wewe mwanamke, sio kila muda Sia kafanya hivi, Sia kafanya vile, ushawahi kufikiria dhambi zako au unaziona dhambi za Sia tu ndio kubwa sana! Na hii tabia wala sijaitoa mbali bali nimeitoa kwako mwenyewe, tulichotofautiana na wewe, ni kwamba mimi nampenda mwanaume mmoja maisha yangu yote na nitampenda hadi naingia kaburini ila wewe unampenda kila mwanaume unayemuona mbele ya macho yako. Tutaona na hiko kitoto chako Leah kitakuwaje? Nahisi kitatembea na kaka zake wote”
Dora alichukia sana kwa maneno ya Sian a kumsogelea karibu ili amnase kibao ila Sia alidaka ule mkono wa Dora na kumwambia,
“Hujawahi kunipiga na hutowahi kunipiga, mimi ndio Sian i namba nyingine mimi. Huwa naongea kile ninachojisikia, na huwezi kunipangia cha kuongea, na maneno yangu haya siku moja yataokoa familia nyingi sana. Umechukua pesa za James na kwenda kujengea familia yako, siku zote ulipenda wanaume sababu ya pesa, wewe hata shemeji yako huyo Erick ulimtaka sababu ya pesa zake ila leo hii unaona Sia ndio anafanya mambo ya ajabu kupita wote duniani, na wewe utajiacha na nani! Ptuuu! Endelea na ulokole wako feki kwa kudanganya watu, yani na wewe umeokoka! Nicheke mie, dunia simama nishuke labda njiani kuna mti wa mapera, nichume pera moja nitafune halafu nikateseke chooni, wewe mwanamke loh!”
Halafu Sia akaondoka zake na kumuacha pale Steve na Dora wakiwa kimya tu, yani kimya kilitawala kwa muda kidogo halafu Dora alikaa chini na kuinama, alijikuta machozi yakimtoka tu na kukumbuka maisha yake ya nyumba, jinsi alivyosababisha wengi wapate ukimwi sababu yake, ila atawezaje kwasasakugawa mali za James ikiwa hafanyi kazi yoyote na anategemea mali hizo zimlishe na kila kitu katika maisha yake? Aliwaza sana, basi mdogo wake alimwambia,
“Dada, yani ndio kitu cha kuumia hiko jamani, yule Sia achana nae, hata bosi hapa husema kuwa Sian i chizi na ukimfatiliza utapata tabu sana dada yangu, achana na maneno yake. Wewe umeokoka basi amini hivyo”
“Mmmh mdogo wangu ila ulokole mgumu jamani, sasa mimi nikitoa kila kitu nitaishije? Nitaenda wapi? Si ndio nitakuwa kama yule mwanamke wa kuitwa Ester jamani ambaye waumini ndio wamemuonea huruma na kumjengea nyumba, dah sijui katumwa huyu!!”
“Achana nae dada, angalia maisha yako ila ukifatilia maneno ya Sia utaumia sana, yani huyu kafanya hadi Erica apatwe na uchungu hapa na kwenda kujifungua”
“Kheee kumbe Erica ana mtoto mwingine?”
“Ndio, tena wa kike”
“Oooh ngoja nikamuone rafiki yangu, kwaheri mdogo wangu”
Basi Dora aliondoka pale dukani na muda huo alielekea moja kwa moja nyumbani kwa mama Angel.
 
SEHEMU YA 195

Mama Angel akiwa na mama yake ndani huku wakiongea habari mbalimbali ikiwa na namna ya kuishi na kufundisha watoto wake,
“Ila hawa watoto wako unatakiwa kuwa nao makini sana mwanangu na ikiwezekana basi kila siku uwe na utaratibu wa kuongea nao”
“Mama, unajua kuna muda hadi nahisi kuchanganyikiwa sababu ya hawa watoto haswaa Angel na Erica, ni bora ya Erica mambo yake mengi yapo wazi, sababu anapenda umbea na hilo linajulikana, yani Erica kama akiwepo anaweza hata kunyata na kusimama mlangoni wa chumba change ili tu kusikia mimi na baba yake tunazungumza kitu gani hadi sijui hiyo tabia niidhibiti vipi. Halafu huyu Angel ndio ananiumiza kichwa kabisa, maana huyu mtoto ana mchezo wa kufanya mambo kimya kimya, yani kuna mambo yake mengine huwezi kuyatambua kabisa”
“Ila usishangae, huyu Angel kabeba tabia zako ujue, ulikuwa ukinipa shida sana. Mtoto unajifanya una siri yani kila kitu unaficha, hadi mambo ya muhimu yanakusibu ila huwezi kukaa chini na kunieleza mama yako, sasa huyu Angel kafata tabia zako yani na yeye namuona ana mtindo wa kufanya mambo ya kimya kimya, kiasi kwamba hataki kuweka wazi mambo anayoyafanya na ukienda kuongea nae anakujibu juu juu”
“Sasa mama nifanyeje na hao watoto?”
“Nadhani njia pekee ni kuwa uongee nao mara kwa mara na kama utaweza basi hata kila siku hebu wafundishe maisha ni nini, huyo mbea mfundishe vizuri kuna mahari atapata shida sababu ya umbea wako, na huyo msiri hebu ongea nae vizuri maana kuna vitu sio vya kuficha kabisa”
“Sawa mama, nitaongea nae”
Basi Dora nae alifika muda huu na moja kwa moja alipelekwa na Vaileth kwenye kile chumba cha mtoto maana alienda kumuona mtoto, basi aliingia huku akifurahi sana.
Basi bibi Angel nae alimkaribisha vizuri tu Dora, halafu akainuka kwenda kumuelekeza Vaileth kitu cha kupika kwa muda huo, basi ndani mule alibaki mama Angel pamoja na Dora na mtoto tu ambaye kwa muda alikuwa amelala, basi Dora alianza kuongea na rafiki yake huyo,
“Mmmh unajua habari hii nimeenda kuipata dukani nilipoenda kumtembelea Steve, ndio akaniambia. Ila unajua maajabu niliyoyakuta dukani kwako?”
“Maajabu gani kwani?”
“Mwenzangu, nimekaa kidogo pale nazungumza na mdogo wangu si akaja yule jini mkata kamba jamani! Yani yule mwanamke simpendi tena simpendi kabisa”
“Yupi huyo?”
“Sia huyo”
“Nahisi unapoishia wewe kutokumpenda ndio mimi ninapoanzia, yani kanitoka huyo mwanamke namshangaa hadi leo hataki kuiacha familia yangu kwa amani”
“Anaiacha vipi? Kaniambia kuwa katika ameisha yake amempenda mwanaume mmoja tu na atampenda mpaka kufa kwake, yani huyo sio mwingine ni mume wako, kwakweli unakazi ya ziada kwa yule mwanamke”
“Ila nifanyeje sasa?”
“Yani Sia ashukuru Mungu kwasasa sina mambo ya ajabu ila ingekuwa enzi zangu, mbona Sia angenielewa vizuri yule. Ila nahisi huyu Sia kuna kipindi ataniangusha tena tu kwa maneno yake”
“Aaaah usiseme hivyo Dora, kumbuka ulipotoka na uliposasa, maisha ni safari na kuna siku utafika sehemu ile unayoitaka wewe. Usikatishwe tamaa na maneno ya mtu”
Basi Dora aliongea ongea pale kidogo kisha akaaga kwani alipitia tu mara moja ukizingatia hakujipanga kabisa kufanya hivyo kwa siku hiyo.
Dora alipoondoka tu, ndipo bibi Angel nae alienda na kuanza kuongea na mtoto wake,
“Kheee kumbe bado una urafiki na huyu mtu!”
“Mama, Dora amebadilika ujue”
“Hata kama ila yeye ndio chanzo cha dada yako kuachana na mumewe”
“Mmmh mama jamani hayo si yalishapita lakini, dada mwenyewe kwa kushauriana na wewe alienda mahakamani kudai talaka, haya si akapata mtu mwingine wa kumuoa, sasa utasema nini mama”
“Unajua siku zote ndio ya kwanza ndio tamu, si unaona hiyo ndoa ya pili ya dada yako haikuwa na shamra shamra zozote, yani wale kama wamevutana tu kwenda kuishi pamoja. Ni kama dada yako Mage na mume wake, yani ndoa iliyofanyika ni wewe na Erick, na Tumaini na Tony, hizi ndio ndoa ila ya huyu dada yako na huyo mwanasheria wake sio ndoa wala nini ni kuvutana tu. Hebu kumbuka kipindi dada yako alipokuwa akiolewa na James! Ingawa ulikuwa mdogo ila najua ile ndoa ilikuvutia na wewe ndiomana ulikuwa ukililia mapenzi ya kweli, mwanangu huyu rafiki yako hata ajisafishe vipi ila bado ni mbaya kwani aliiba mume wa dada yako”
“Ila mama hayo mambo yaliisha ujue, hata dada Bite hana tatizo kabisa”
“Hana tatizo wapi, anaumia moyoni sana tu. Unafikiri huwa hamkumbuki mume wake? Mwanaume kachuma nae mali mbalimbali ila kuna mwanamke mwingine ndio anazifaidi, hata Junior hajaambulia kitu, unafikiri haumii! Huyo Deo unadhani kuna kitu atampa Junior, mtu mwenyewe wala hakai kama baba wa Junior wala nini, unafikiri huyo Junior bila kujiendeleza mwenyewe atafika popote!”
“Halafu ndio muhuni balaa”
“Hapana, Junior kwasasa katulia sana. Kumbuka Junior huwa hatoki kabisa, unajua Junior kabadilika, nishamkuta hadi anamsaidia Vaileth kuosha vyombo, kwakweli Junior kabadilika na kawa mtoto mzuri, ila simshangai kwanini hataki kurudi kwa baba yake yule ni sababu yule baba hana upendo na mtoto kwahiyo Junior anaona ni vyema akae huku tu”
“Ila baba Angel alisema ataongea na mama Junior, na pia ataongea na Deo kwani Junior bado anahitaji upendo wa wazazi kwa ukaribu zaidi”
“Ila kaukosa sababu ya huyo rafiki yako Dora, na ushukuru tu wewe baba Angel alikuwa na msimamo ila isingekuwa hivyo basi huyu rafiki yako lazima angempitia tu”
“Jamani mama!”
“Ndio hivyo”
Bibi Angel alionekana kutokumpenda kabisa Dora ingawa ni rafiki wa mwanae wa muda mrefu sana ila hakuwa na upendo nae.
Vaileth alifika na kumletea chakula mama Angel ambaye alianza kukila huku akikisifia,
“Jamani, mbona chakula cha leo kitamu sana”
“Umesahau kuwa nilikuwa jikoni kumuelekeza”
“Oooh nimekumbuka mama, yani hizi ndizi za leo balaa, zimekolea nazi hadi nimezipenda”
Vaileth alicheka tu na kurudi zake jikoni, ambapo Junior alikuwa sebleni nae akila zile ndizi huku akisifia,
“Kheee ndizi tamu hizo, kukaa nyumba moja na mama aliyejifungua raha sana”
Vaileth akacheka tu ila kwa muda huo Angel alienda kubeba chakula na moja kwa moja kwenda nacho chumbani, alikuwa anataka ale huku akitumia simu kwahiyo kwa pale sebleni asingeweza kabisa kwani ile simu kwake ilikuwa ni simu ya magendo.
 
SEHEMU YA 196

Na kweli Angel alikuwa kila huku akiwasiliana na simu kwa njia ya ujumbe, na muda huo alikuwa akiwasiliana na Samir pamoja na Mussa, na wote walimuuliza kuwa anakula nini, kwahiyo alipiga picha zile ndizi na kuwatumia, basi alianza Samir kumwambia,
“Hizo ndizi zinaonekana ni tamu sana, ama kwa hakika mke wangu wewe ni mpishi hodari”
Mussa nae alimtumia ujumbe,
“Nina hakika hizo ndizi umepika wewe Angel, chakula chako kitamu kama jina lako”
Basi Angel alikuwa akijihisi raha sana yani alikuwa akisoma zile jumbe huku akitabasamu na kufurahi, ila Mussa akatuma ujumbe tena kwa Angel,
“Kwani Angel unaishi wapi? Nielekeze ili nije nikusalimie maana pale kwa bibi yako haupo tena”
“Mmmh kwetu ni geti kali balaa, yani sina sehemu ninayotoka nisiulizwe, sasa nitawezaje kuonana na wewe”
“Aaaah Angel jamani, unajua wewe ni mdada mkubwa, je huwa huendagi dukani?”
“Nitaenda dukani kufanya nini sasa?”
“Kheee kwenu, hakuna mahitaji ya kwenda kununua dukani?”
“Vitu vingi unakuta vipo ndani na ukitaka kitu, basi mama yupo radhi amtume dereva akanunue”
“Duh! Hebu aga unaenda kununua pedi”
“Humu ndani kwetu, huwa mama anamtindo wa kununua dazani ya pedi yani sijui ni kitu gani, huoni hata vocha mara nyingi huwa nakuomba, yani kwetu kutoka ndio balaa”
“Jamani Angel sasa itakuwaje? Nahitaji sana kukuona kwakweli!”
“Sijui sasa”
“Hebu nielekeze kwenu kwanza”
Basi Angel alimuelekeza kwao na Mussa akamwambia,
“Nitakuja, yani nitakutumia tu ujumbe kuwa nipo nje kwenu hata utoke mara moja tu, kiukweli Angel natamani sana kukuona”
Angel akajifikiria kidogo na kumwambia tu karibu maana aliona kuzidi kumkatalia ni kama kumfanya ajihisi vibaya ukizingatia mara kwa mara huwa anamuomba Mussa amtumie vocha.
Basi ujumbe mwingine uliingia toka kwa Samir,
“Angel, unajua leo yule mbibi kaniharibia siku sana ila nitakuja tena tuonane hata nikukumbatie kidogo tu kipenzi changu”
“Ila si unajua kama kwetu geti kali jamani Samir?”
“Naelewa, ila utafanya kama leo Angel, siku nikija nitakutumia ujumbe hata utoke kidogo tu nikukumbatie jamani Angel”
Basi Angel alihisi rah asana kuambiwa vile na Samir, wala hakuwaza jinsi kwao walivyowakali ila alichowaza ni kuonana na Samir tu.
Kisha alipomaliza kula aliinuka na sahani yake kuirudisha jikoni ila njiani alikutana na bibi yake ambaye alianza kumsema,
“Kheee Angel, ndio tabia gani hiyo ya kwenda kula chumbani? Meza ya chakula imewekwa ya kazi gani? Na huko chumbani kuna nini hadi uende kula huko”
“Samahani bibi”
“Oooon naona umeanza tabia ya mama yako, kufanya kosa makusudi na kukimbilia samahani, sijaipenda hiyo tabisa, siku nyingine ule mezani pale sio kukimbilia na chakula chumbani”
“Sawa bibi”
Yani Angel hakuwa muongeaji sana, mara nyingi yeye mtu akimsema basi atamsikiliza tu na sio kuanza kujibishana nae.
 
SEHEMU YA 197

Muda wa kulala ulipofika, kama kawaida Junior alienda chumbani kwa Vaileth maana kwa kipindi hiko Junior alifanya kwa Vaileth kama ndio chumbani kwake maana muda wa kulala ulipofika tu alikimbilia huko, basi walianza kuongea na Vaileth,
“Eeeeh Junior, kama bibi siku akienda chumbani kwako halafu asikukute itakuwaje?”
“Weee yani ambacho huwa nafanya pale ni kuzima taa ya chumbani halafu huwa nafunga na funguo nahisi huyo bibi atagonga hadi vidole viingie tumboni”
Basi Vaileth akawa anacheka huku wakiendelea kuongea na kutaniana, ila muda kidogo mlango wa Vaileth uligongwa na kumfanya Junior akimbilie chooni kama kawaida, ikabidi Vaileth ainuke na kwenda kufungua, na kweli alikuwa ni bibi yao ambaye aliingia chumbani kwa Vaileth na kuanza kuongea nae,
“Mbona nimesikia kama ukiongea na mtu Vai?”
“Hapana bibi, sikuwa naongea na yeyote”
“Bado nakusisitiza, maisha ni tofauti na unavyofikiria, unaweza kupoteza maisha yako ndani ya siku moja tu. Kuwa makini, wanaume ni waongo sana. Upo ndani ya nyumba hii kwasasa na atakwambia nakupenda kwasana ila siku utakapoondoka hapa na hauna kazi tena basi hayo maneno yake ya nakupenda sana hutoyasikia kabisa, kuwa makini sana. Usiku mwema”
Kisha bibi aliinuka na kuondoka zake, halafu Vaileth akafunga tena mlango na Junior alitoka chooni na kusema,
“Jamani mtoto akue tu ili huyu bibi arudi kwake, yani ananiumiza kichwa huyu bibi hadi nakosa raha jamani!”
Vaileth alikuwa akicheka, kisha yeye na Junior walilala kama kawaida yani maneno ya yule bibi yalikuwa ni kama kumpigia mbuzi gitaa tu.

Kulipokucha kila mmoja aliendelea na mambo yake siku hiyo, na wanafunzi walienda shuleni kama kawaida yao, ila siku hii Angel alishikiliwa na mama yake kuwa aoshe vyombo kwahiyo alikuwa akiosha vyombo halafu mama yake alienda karibu na kuongea nae,
“Unajua Angel siku hizi umebadilika sana mwanangu, yani humu ndani hufanyi kazi yoyote muda wote unalala kwani huko kulala kunakusaidia nini mwanangu?”
“Mama, huwa najihisi uchovu tu ndiomana naamua kulala”
“Haya hapo kuosha vyombo tu ila umejinunisha utafikiri unafanya kazi gani”
Kisha mama yake akaondoka na kumuacha Angel akiosha vile vyombo na baada ya kumaliza alirudi chumbani kwake na kuchukua simu yake ila alikutana na ujumbe toka kwa Mussa,
“Angel, nipo hapa nje ya geti lenu”
Akakuta ujumbe mwingine toka kwa Mussa tena,
“Mbona Angel unanifanyia hivyo jamani, toka kidogo tu nikuone”
Basi Angel aliweka simu pembeni na kuamua kutoka nje, na moja kwa moja alienda getini na kutoka nje ya geti ila alipofika nje alimkuta Mussa kasimama na kijana mwingine ila alipomuangalia vizuri aligundua kuwa kijana huyo ni Samir tena ilionekana wanaongea kama watu wanaofahamiana sana.
 
SEHEMU YA 198

Basi Angel aliweka simu pembeni na kuamua kutoka nje, na moja kwa moja alienda getini na kutoka nje ya geti ila alipofika nje alimkuta Mussa kasimama na kijana mwingine ila alipomuangalia vizuri aligundua kuwa kijana huyo ni Samir tena ilionekana wanaongea kama watu wanaofahamiana sana.
Angel alisimama kwa muda kidogo akiwashangaa, kisha aliwafata kuwauliza,
“Tuseme mnafahamiana?”
Halafu na wao wakaulizana kwa pamoja,
“Tuseme tulikuwa tunamfata msichana mmoja?”
Angel akatabasamu, kisha Samir akamwambia Angel,
“Sisi tunafahamiana ndio ni ndugu huyo kwenye ukoo ukoo”
“Aaaah kumbe!!”
Mara Angel alisikia sauti ya mama yake ikiita, ikabidi Angel awaache pale nje na akimbilie ndani alipokuwa akiitwa na mama yake, yani aliposogea karibu tu na mama yake alinaswa kibao na mama yake halafu ndio swali likafatia,
“Kule nje ya geti ulienda kutafuta nini? Una nini wewe mtoto lakini eeeh!”
Angel alikaa kimya tu na kumfanya mama Angel azidi kuchukia kwakweli, kisha akamwambia,
“Sasa ole wako nikuone umetoka tena mjinga wewe!”
Halafu mama yake akaelekea chumbani ila Angel alielekea bustanini ambako alimkuta Junior amekaa naye Angel alienda kukaa pembeni yake huku kainama chini, basi Junior alimuuliza tatizo ni nini,
“Mbona hivyo Angel, tatizo ni nini?”
“Unajua mama yangu huwa simuelewi kabisa, watoto wengine wapo huru majumbani mwao ila mimi nachungwa utafikiri kitu gani, yani sipumui jamani, nikitoka hata nje ya geti ni tatizo sijui mama anafikiria nini kuhusu mimi?”
“Mimi nadhani mama yako kuna kitu anaogopa kuhusu wewe, hebu jaribu kumuuliza kwa ukaribu kuwa mama unataka mimi niweje? Kwanini hutaki nitembee tembee, yani unakaa ndani kama mfungwa jamani, umekuwa kuku wewe! Ndio nyie mkipata siku upenyo lazima wanaowachunga wajute maana huwa mnaota mapembe”
“Unamaanisha nini?”
“Unadhani siku ukiachiwa wewe si utaenda hadi kukutana na wasiopaswa kukutana nao jamani! Ila mama inabidi aangalie kila kitu, atakuchunga hadi lini? Wewe unakua kila siku, na mwisho wa siku utaanza chuo, je huko atakuchunga? Si ndio akili itakuwa imekuruka kabisa”
“Mmmmh wewe nawe, mie akili iniruke kwa mtindo upi? Najitambua mimi na siwezi kurukwa na akili, sikia nikwambie, mama anadhani nitakuwa na wanaume, ila mimi wanaume wa kazi gani? Yupo mmoja tu nimpendaye”
“Na huyo mmoja umpendaye ndio mwenye uwezo wa kuchanganya akili yako wewe au kukuacha ubaki na akili timamu, Angel mapenzi ni matamu sana ila mapenzi usipotumia akili utaumia mno”
“Aaaaargh na wewe sijui unazungumzia nini, unadhani mimi ni kama wewe mwenye wanawake kila kona!”
“Sasa unafikiri nilikuwa napenda kuwa na wanawake kila kona? Unakuwa na huyu, mnakuwa vizuri kabisa, siku mnafumaniwa na jamaa yake, kumbe ana mtu wake, basi unaachwa kwenye mataa, unadhani nitafanya nini zaidi ya kutafuta mwingine? Unampata na anajua kabisa kuwa mimi ni mwanafunzi yani sina pesa sababu sifanyi kazi nasoma tu, ila unamkuta anakuorodheshea mahitaji hayo hadi kichwa kinapasuka, kuna demu jamani hadi nilihisi kizunguzungu, mwanzoni nilikuwa najikakamua ila badae nilivyoshindwa ikabidi niachane nae na niwe na mwingine”
“Sasa alikuwa akitaka umnunulie nini?”
“Yani yeye matatizo yote ya nyumbani kwao basi niyatatue mimi, sijui mara mama yake anaumwa, mara baba yake anaumwa, mara anataka sijui hela ya saluni, mara dawa za mama yake zinahitajika, hivyo sio shilingi mbili utakuta ananiambia laki mbili au laki tatu, jamani nikashindwa, mwingine kila atakachokiona wakati tumeongozana anakitaka, yani mapenzi yanaumiza kichwa hatari ndiomana ukipata sehemu ya kutulia unaona bora utilize moyo wako. Namuonea huruma Erick ambaye hajui hata mapenzi ni kitu gani yani akianza kupenda uwiii atafilisi biashara za baba yake”
“Wewe nawe, hivi unajua kama Erick yupo tofauti sana yani hata baba huwa anamsifia, yani Erick huo ujinga labda aanze badae ila wewe nadhani ulipoanza kutembea tu”
Wote wakacheka kwa muda huo na kuanza kuongea habari za kuwafurahisha ili kupoteza mawazo na malengo ya kitu ambacho kimetokea kwa siku hizo.
 
SEHEMU YA 199

Muda wa kutoka shule ulipofika, Sarah kama kawaida alienda kupanda kwenye gari ya shule na kukaa karibu na Erick kwani alikuwa anahisi furaha sana kukaa na Erick, basi alianza kuongea nae,
“Lini nije kumuona wifi yangu mdogo Erick?”
“Kheeee kashakuwa wifi yako?”
“Ndio”
“Hivi Sarah huna aibu kabisa, maana kila siku upo kuniambia habari za kuwa wapenzi”
“Sasa aibu ya nini Erick, nakwambia kweli wewe ni mtanashati na kama mabinti hawakuwa wakikufata labda sababu ya ulivyo maana una hasira sana na hupendi kucheka, ila wadada wengi wangekufata na wengi wanaumia juu yako Erick, ila nadhani mimi ndio zaidi yani mpaka nimejitoa muhanga kuongea ujue sio kawaida”
Erick alitabasamu tu na kuamuangalia Sarah, basi waliendelea kuongea mambo mbalimbali kisha Erick alipofika kwao alishuka na kuingia ndani kama kawaida, ila leo alipoingia tu alikutana na mama yake ambaye alimuuliza,
“Vipi leo yule shetani hujakutana nae tena?”
“Sijakutana nae mama”
“Aaaah sawa, ila ukikutana nae niambie mwanangu yani usiache kusema”
“Sawa mama, nimekuelewa”
Basi Erick akaenda zake chumbani kwake na kubadili sare za shule, kisha alienda moja kwa moja kula chakula ambapo alimkuta Junior na Angel wakila pia huku wakiongea ongea mambo ya utani utani, basi Angel akamtania pale mdogo wake,
“Eti Erick, nani wifi yangu?”
Muda huo Erica nae alisogea kula na kusema,
“Kheee dada na wewe umeanza mambo kama ya Junior jamani!! Sasa Erick wifi wa kazi gani? Huoni kama Erick bado mdogo?”
Junior akadakia,
“Ana udogo gani sasa Erick jamani!! Kidato cha kwanza ni mdogo, nani kasema”
Mama Angel nae alikuwa akipita pale na kuwafokea,
“Halafu Junior ujinga kwenye nyumba yangu sitaki, na kesho nina kikao na nyie watoto naona mmezidisha ujinga kwenye nyumba hii”
Wote wakanyamaza kimya na kuendelea kula maana huyu mama yao walimfahamu vizuri sana.

Usiku wa siku hiyo, mama Angel alikaa na baba Angel na kuanza kuzungumza kuhusu mtoto maana ile tabia ya Angel ya kutoka nje ya geti kidogo ilimkosesha raha na amani mama Angel,
“Unajua siku hizi Angel kaanza tabia ya kutoka nje ya geti sijui hata huwa anafanya nini, jamani mtoto ananichanganya huyu hata sijui cha kufanya kwakweli!”
“Ila mke wangu, nadhani umuulize Angel kitu gani anataka, unajua kwasasa wamemaliza shule na wapo tu nyumbani inawezekana anachoka sana kukaa nyumbani. Nadhani itakuwa ni vyema sana kama ukimuuliza kitu anachotaka kufanya”
“Sasa kitu gani jamani mume wangu? Unajua huyu mtoto tusipokuwa makini nae basi ataleta mabalaa hapa nyumbani!!”
“Naelewa mke wangu, ila ndio tuwe makini ila mtoto kumbana sana nako sio umakini ila ni kumfundisha mtoto atambue jema na baya, unajua akili ya Angel ishaanza kuchanganywa na mapenzi kwasasa, kwahiyo tusipokaa chini kumfundisha basi tunampoteza”
“Na tumfundishaje sasa?”
“Wewe ni mama, lazima utajua namna ya kumfundisha. Hebu angalia njia ulizopita wewe kwanza halafu ujue jinsi gani uweze kukaa na huyu mtoto na kumuelekeza cha kufanya ili asitende makosa ambayo ulishayapitia”
“Umeanza sasa, kwani mimi nilipenda kutenda makosa”
“Hilo ndio tatizo lako, mtu akiongea basi huhisi anataka kukusema. Mimi nimemaliza kwa upande wangu, tusigombane mke wangu kwa vitu vidogo vya watoto, sisi tulianza kabla ya hawa watoto, tushikamane tu na tuwalee vizuri”
Kisha baba Angel aliamua kulala kwani hakutaka kufanya mabishano na mke wake.
 
SEHEMU YA 200

Angel nae wakati amelala, alitafutwa kwenye simu na Samir ambaye alianza kuongea nae,
“Angel kipenzi, kumbe huwa unaongea na Mussa mara kwa mara?”
“Nitumie ujumbe Samir, kuongea na simu hapa nyumbani ni tatizo kidogo”
Basi Samir akamtumia ujumbe na kumuuliza kuhusu yeye na Mussa,
“Eeeh naomba nieleze mahusiano yako na Mussa”
“Sina mahusiano yoyote na Mussa, ni vile alikosea namba ya simu na tukaanza kuwasiliana na huwa tunawasiliana kawaida tu”
“Mussa hajawahi kukutongoza?”
“Hapana, sijawahi kutongozwa na Mussa kabisa huo ndio ukweli, yani huwa tunawasiliana tu kama marafiki”
“Naona kabisa wazi kuwa penzi langu litaibiwa, Mussa ni ndugu yangu ila simuamini hata kidogo. Naomba Angel uache tabia ya kuwasiliana na Mussa”
“Ila sina mahusiano na Mussa jamani”
“Ila Angel kuna jambo ngoja nikushauri”
“Jambo gani?”
“Kwanini usimwambie mama yako kuwa akupeleke kwenye chuo cha kujifunza kompyuta ili ujifunze funze wakati unasubiria matokeo ya kidato cha nne? Najua huko itakuwa rahisi sana kwa mimi na wewe kuonana mara kwa mara”
“Mmmh wazo zuri, sasa chuo gani?”
“Usijichagulie, mwache mamako akuchagulie mwenyewe, maana ukijichagulia utamfanya akuhisi vibaya, mwache akuchagulie halafu tutajua cha kufanya”
“Sawa, nitaongea nae kuhusu hilo”
“Ila Angel nakuomba acha kuwasiliana na Mussa jamani, mimi ndio namjua Mussa ni ndugu yangu na sio mtu mzuri kwako”
“Nimekuelewa Samir, hakuna tatizo na hata sitawasiliana nae tena”
“Nakupenda sana Angel, yani kumbuka hilo. Muache Mussa kabisa”
Basi Angel na Samir waliongea sana kiasi kwamba Angel alichelewa kulala, kwahiyo alilala saa kumi alfajiri.

Kesho yake kama ambavyo mama Angel alipanga na mumewe, kwanza alimuita Angel na kuanza kuongea nae,
“Angel mwanangu kitu gani unataka kufanya, ni nini kipo katika akili yako kwa muda huu?”
“Mama, kwakweli nimechoka kukaa nyumbani. Mimi nilikuwa napenda labda hata nikasome kozi ya kompyuta”
“Oooh sawa, itabidi basi uende kusoma na Junior”
Hapo kidogo Angel alikaa kimya kwa muda kwani hakufikiria kama mama yake anaweza kutoa wazo la yeye kwenda kusoma na Junior, ila hakuwa na budi zaidi ya kukubali tu,
“Sawa mama,hakuna tatizo”
Basi mama Angel akawaita wote yani watoto wote kwenye nyumba yake maana siku hiyo ilikuwa Ijumaa na wakina Erica waliwahi kutoka shule, akaanza kuongea nao,
“Jamani, nyie watoto nimewaita hapa ili niongee nanyi mambo ya msingi yanayoendelea, kwakweli tabia mbaya kwenye familia yangu sitaki, mambo ya ajabu ajabu kwenye familia yangu sitaki. Junior, mambo ya kumwambia mwanangu Erick aanze kuwa na wanawake sitaki kuyasikia, Angel na Erica kama ambavyo huwa naongea na sasa naongea tena sitaki kusikia wala kuona marafiki zenu wa kiume hapa nyumbani, nilipiga marufuku hata marafiki wa Erick sababu yenu halafu nyie ndio mniletee maajabu ya dunia sitaki huo upuuzi kabisa. Na wewe Erick, fanya kile unachoona sahihi katika maisha sio kile unachoshauriwa na mtu, kwa kifupi stori za ajabu ajabu kwenye nyumba yangu sitaki. Halafu wazo la Angel nalifanyia kazi, kwahiyo Junior jiandae utakuwa ukienda na Angel kwenye chuo cha kompyuta mkajifunze huko. Sasa Junior wewe ndio utakuwa kama mlinzi wa Angel, akipatwa na tatizo lolote ni wewe ndiye utakaye nijibu, nadhani nimemaliza sasa, mmenielewa lakini?”
Wote waliitikia,
“Tumekuelewa mama”
“Haya mwenye swali aniulize, au kama hamna maswali sasa basi muda wote mtakapokuwa na maswali yenu njooni mniulize nami nitawajibu”
Kisha mama yao akainuka na kuondoka zake, basi watoto wakabaki wanaangaliana na Angel ndio akaanza kusema,
“Ila jamani, mbona siku hizi kama mama kawa mkali zaidi? Yani kila kitu anasema hapendi, tatizo ni nini?”
Junior akajibu,
“Itakuwa mumewe hampi utamu vizuri”
Wote waliinuka na kumuacha Junior peke yake kwani ujinga ujinga walioambiwa kuwa wasizungumze basi ndio Junior alikuwa kama anataka kuuanzisha tena.
Ila kama kawaida ya Erica alipoinuka pale alikuwa na yake kichwani tayari na moja kwa moja alienda kwa mama yao na kumueleza swali alilouliza Angel na jinsi Junior alivyosema, kiukweli mama Angel alichukia sana na kuuliza,
“Kwahiyo mkasemaje wengine?”
“Tuliondoka mama”
“Mnaujua utamu nyie? Hivi Junior ana akili gani lakini jamani! Aaaargh mitoto mingine sijui imelelewajwe”
Kisha mama Angel alimuita Junior kwa nguvu sana na Junior akaenda kisha akamnasa vibao vya kutosha na kumuuliza,
“Unaujua utamu wewe? Unazungumzia nini? Mbona una tabia mbaya sana?”
“Nisamehe mamdogo, nisamehe sana nilichokuwa nazungumzia ni kingine kabisa ila sijui wamefikiria nini”
“Haya ulikuwa ukizungumzia nini, yani bila aibu sababu hapewi utamu wa kutosha na mume wake, hivi una nini wewe mtoto? Nitakurudisha kwa mama yako!”
“Nisamehe mamdogo jamani, sikumaanisha hivyo unavyomaanisha. Yani nilikuwa nasema bamdogo hajawahi kukuletea vitu vitamu kama keki”
Mama Angel akamnasa kibao kingine na kumfanya Junior apige na magoti kuomba msamaha, kwani hapo wazo lilikuwa la kurudishwa kwao tu ambapo alikuwa hataki iwe hivyo, basi alipiga magoti na kuendelea kumuomba mamake mdogo msamaha,
“Sasa nenda ukawaambie hao ulikuwa unawaambia huo upuuzi na ukarekebishe hiyo kauli yako, mjinga wewe. Toka hapa”
Basi Junior aliinuka lakini moja kwa moja alihisi mpeleka maneno ni Erica tu, ila ilibidi afanye kama alivyotumwa na kuwaita wote yani Angel, Erick na Erica kisha kuanza kuongea nao,
“Jamani, mmenifikiria vibaya, mimi sikumaanisha utamu wowote zaidi ya utamu wa keki na pipi na juisi, haya Erica mpeleka maneno umemaanisha utamu gani? Unaujua utamu wewe? Jamani katika maisha yangu sijawahi kuona mtu mbea kama wewe Erica, yani hufai hata kidogo, nimetengua kauli yangu jamani, sijamaanisha hivyo, mistake nifukuzwe kwenye nyumba hii, mimi nimependa kuishi hapa, niacheni niishi kwa furaha”
Angel alimuangalia Junior alivyokuwa akiongea halafu alimuangalia Erica kwani mdogo wake kweli alikuwa mbea tena wa kutosha tu, ila walikubaliana pale na kila mmoja kuelekea tena chumbani kwake. Ila kiukweli Junior nae alimchukia Erica, yani katika ile nyumba ni Erick pekee ambaye kidogo alikuwa akikaa kaaa na kuongea mengi na Erica kwani hata Angel alikuwa hapendi kuongea na mdogo wake huyo tena kwa kipindi hiko ambacho ana simu ya magendo ndio kabisa, akaona akiwa anaongea nae mara kwa mara basi atapeleka maneno kwa mama yao.
 
SEHEMU YA 201


Leo usiku wakati Erica kaka zake chumbani huku kajiinamia tu, Erick alienda kuongea nae kwani alikuwa akimfahamu vizuri na alijua lazima Erica atakuwa kachukia vile kusemwa na Junior,
“Erica, vipi mdogo wangu umejiinamia tu”
“Unajua humu ndani hawanipendi yani hakuna anayenipenda hata mmoja”
“Usijali mimi nakupenda mdogo wangu”
“Kila mtu ananisema mimi mbea, ila umbea wangu ni nini wakati nasema ukweli?”
“Hata kama unasema ukweli ila huo ndio umbea, yani umbea ni kutoa maneno sehemu moja na kuyapeleka sehemu nyingine, mfano umesikia mtu anasemwa, halafu wewe kuchukua yale maneno na kuyapeleka kwa muhusika basi huo ndio unaitwa umbea na uongo ni kusema maneno ambayo hayapo yani unajitungia tu”
“Ila mimi nasema ukweli”
“Ndio unasema ukweli ila unausema katika sehemu ambao hauhitajiki, mdogo wangu hiyo ndio sababu ila usiwe na mawazo sana”
“Kwahiyo na wewe hupendi?”
“Aaaah mimi nishawahi kusema kuwa sipendi? Wala sina tatizo juu ya hilo, ila tu nikuulize mdogo wangu kwani utamu ambao uliuelewa wewe ni upi?”
“Aaaah jamani achana na mambo hayo, yameshapita jamani Erick”
“Nilikuwa nakutania tu, ila nimemiss ile tabia yako ya kuja chumbani kwangu bila hodi ila mimi siku ile kuja kidogo tu umepiga kelele hadi mama akaja jamani!”
Erica alicheka na kusema,
“Unajua siku ile sikutarajia kama unakuja, halafu nilikuwa sijavaa”
“Ila hujawahi kushtuka kiasi kile, ulikuwa na mambo yako wewe ndiomana kama sio ulikuwa ukimuwaza yule jamaa wa Kanisani sijui”
“Jamani Erick sio hivyo jamani!”
Basi siku hii waliongea vizuri tu na kuamua kuanza kucheza karata zilizowapelekea kulala mule mule chumbani kwa Erica.

Usiku wa leo Junior alimwambia Vaileth kuwa itanidi autumie kupunguza machungu yake ya kupigwa na mama yake mdogo,
“Unajua sijapenda kabisa jinsi mamdogo alivyonipiga ila yote ni sababu ya umbea wa Erica”
“Pole Junior jamani!”
“Sio pole tu, unatakiwa leo unipe vitu adimu hadi nisahau haya maneno ya mamdogo”
“Vitu gani Junior, yani wewe umenifanya mimi kama mke wako jamani!”
“Ndio wewe ni mke wangu yani mimi na wewe ni mke na mume ila tu hatujaenda kuhalalisha ila mimi na wewe ni wanandoa, neno la Mungu linasema kilichofunguliwa duniani na Mbinguni kimefunguliwa kwahiyo mimi na wewe tumeshakubalika na Mungu, achana na watu kutushuhudia”
“Ila Junior una vituko jamani wewe, hadi umeanza kuongea na neno la Mungu jamani!”
“Ndio, kwani neno halisemi hivyo!! Mimi na wewe Vaileth ni wanandoa tayari, ukisikiliza maneno ya yule bibi utapata shida sana, unatakiwa kunisikiliza mimi mumeo kama mama mdogo anavyomsikiliza bamdogo”
Basi Vaileth alikuwa akitabasamu tu kwani maneno ya Junior yalikuwa yakimfurahisha, kwa kipindi hiko Junior alimfanya Vaileth kama mke wake kwahiyo alikuwa akimtumia kwa muda wowote anaoutaka yeye ila usiku wa leo walitumia muda mrefu sana kuwa pamoja kiasi kwamba walichelewa sana kulala yani nao walilala kwenye saa kumi alifajiri sababu ya uchovu na kila kitu.

Kulipokucha bibi Angel na mama Angel walikuwa macho ila leo humu ndani palikuwa kimya sana yani inaonekana watoto wote walikuwa wamelala, basi bibi Angel alimuuliza mwanae,
“Inamaana leo hadi Vai bado kalala?”
“Hata mimi nashangaa mama, sijui jana wamelala muda gani watoto wa nyumba hii jamani!”
“Ila unajua kuw awatoto wako siku hizi wana mtindo wa kwenda ile sebule ya juu kuangalia mikanda ya ngumi, usikute jana wameangalia sana na ndiomana wamelala hadi muda huu, ngoja nikamuite Vai kwanza”
Bibi aliondoka na kwenda kugonga chumba cha Vaileth, yani kwakweli alikurupuka pia kwani hata hakutegemea kwa muda kuwa umeenda kwa kiasi hiko, basi alimshtua Junior pale,
“Uwiiii nahisi bibi anagonga, tumechelewa sana kuamka leo”
Junior nae alikurupuka kama kawaida na kwenda kujifungia chooni, basi Vaileth akafungua mlango huku akiwa amechoka sana,
“Kheee wewe Vai una nini leo? Mbona umechelewa kuamka hivi!!”
“Nisamehe bibi”
“Hebu nenda ukaanze usafi huko”
Kisha bibi alitoka kwa Vaileth na moja kwa moja kwenda chumbani kwa Angel ambapo aligonga mlango na kufunguliwa na Angel ambaye nae alichoka na usingizi, kwakweli bibi alitingisha kichwa sana,
“Yani nyie watoto jamani, hivi mnajua ni muda gani huu? Mbona mna mambo ya ajabu sana! Hebu amka na leo ndio umuandalie mama yako chakula cha asubuhi”
Basi Angel alijivuta vuta na kutoka chumbani kwake, kisha moja kwa moja bibi alielekea chumbani kwa Erica, ila alikutana na Erick akiwa anatokea chumbani kwa Erica akamuuliza,
“Na wewe vipi asubuhi asubuhi kwenye chumba cha dada yako?”
“Nilienda kumuamsha bibi maana leo kachelewa sana kuamka”
“Ooooh umefanya vizuri sana, kwani jana usiku mlikuwa mnafanya nini watoto wa nyumba hii? Mlikuwa mnaangalia mikanda eeeh!”
“Hapana bibi”
“Hiyo tabia nitaikomesha, watoto gani nyie”
Kisha bibi Angel akarudi tena kwa mama Angel na kuongea nae,
“Inatakiwa uwe makini sana na hawa watoto, ujue wanakesha kuangalia mikanda ndiomana wanachelewa kuamka”
“Mama, umemuamsha na Junior?”
“Ngoja niende”
Bibi wakati anaenda kwa Junior ndio alimkuta Junior mlangoni kwake akifungua mlango kwa funguo, kwakweli bibi alishangaa sana na kumuuliza,
“Wewe Junior, inamaana hukulala chumbani kwako au kitu gani?”
“Kwanini bibi?”
“Mbona muda huu ndio unafungua na funguo?”
“Hapana bibi, nilitoka kidogo bustanini na nikajisahau na kufunga mlango”
Basi bibi aliamuangalia kwa muda kidogo ila hakuwa na uhakika na mashaka yake, ikabidi tu arudi kuendelea kuwahimiza wakina Vaileth katika kufanya kazi za siku hiyo.
 
Back
Top Bottom