Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #261
SEHEMU YA 221
Siku hii baba Angel aliamka na uchovu kiasi na asubuhi hii aliongea kidogo na mke wake,
“Eeeeh mke wangu, kuna mahitaji gani ambayo yanatakiwa humu ndani?”
“Hamna mume wangu, yangekuwepo ningekwambia kabla ya kuuliza, ila umenikumbusha kitu kumbe ulimnunulia Erick simu!!”
“Ndio, sababu Sia alikuwa akimfatilia nikaona vyema nimnunulie simu ili akiwa anamfatilia aniambie”
“Jamani mume wangu, mfano shuleni atakwambiaje wakati wanakatazwa simu shuleni! Mimi nimempokonya maana Erica nae alinunuliwa simu na Junior sababu tu Erick anatumia simu”
“Sijakuelea hapo, Erica alinunuliwa simu na Junior kivipi?”
Ikabidi mama Angel amsimulie baba Angel vile alivyomkamata Erica na simu, basi baba Angel alielewa ile hoja ya mke wake na kuamua kujiandaa kwaajili ya kwenda kwenye kazi yao.
Alipomaliza kujiandaa alimuaga mke wake na kuondoka, ila wakati anatoka getini muda huu alimuona Sia akiwa amesimama na mtoto wa kiume mwenye umri kama wa Erick, kiukweli baba Angel hakumpenda mwanamke huyu kwahiyo alimpita kamavile hamuoni wala nini, yani baba Angel alikuwa akienda kazini huku akiwa na mawazo sana kwani aliona huyu mwanamke anamchanganya akili yake, ila akiwa barabara kuu kuna mtu alisimamisha gari yake ikabidi asimame na alipomuangalia vizuri mtu yule akamuona kuwa ni madam Oliva, basi yule madam aliingia kwenye gari ya baba Angel na kukaa kwenye siti huku akisema,
“Yani nilivyoona gari yako tu nikahisi moyo wangu ukidunda ndio nikakusimamisha”
“Oooh jamani, sasa moyo wako umedunda kwanini madam?”
“Aaaah tuachane na hayo, unaenda wapi muda huu?”
“Naenda ofisini”
“Basin i vyema nikafahamu ofisi yako ilipo”
“Sawa, hakuna tatizo lolote. Karibu sana”
Basi baba Angel alienda na madam Oliva hadi ofisini kwake na kumkaribisha, kwakweli Oliva aliipenda ofisi ya baba Angel kwani ilipangwa vizuri sana, kwahiyo aliingia nae ofisini na kuanza kuongea nae mawili matatu,
“Nimeipenda ofisi yako baba Erick jamani”
“Oooh asante sana”
“Halafu mke wako natamani sana kumfahamu jamani! Naamini nitamfahamu tu, ila baba Erick unaonekana ni mwanamke mstaarabu sana wewe, kwakweli mkeo ana bahati kubwa sana ya kukupata. Sema itakuwa ni vyema sana mimi na wewe tukiwa tunaonana na kuongelea maendeleo ya watoto shuleni au unasemaje?”
“Ni kweli kabisa, sina usemi kuhusu hilo”
“Basi, nitapenda upafahamu nyumbani kwangu pia”
“Sawa madam, nitapafahamu tu”
“Hata leo ukitaka”
“Hapana, kwa leo kuna kazi imenitinga labda siku nyingine”
“Basi tutawasiliana na nitafurahi sana juu ya hilo, maana ni vyema sana kwa wazazi kubadilishana mawazo”
Kisha Oliva alimuaga baba Angel kwani alitakiwa pia kuwahi kwenye kazi yake ambapo alikuwa akifundisha kwenye shule aliyosoma Erick.
Mama Angel akiwa katoka kumuogesha mtoto wake ambaye mara nyingi sana akioga tu analala, alishangaa mlinzi kufika sebleni na moja kwa moja aliitwa yeye na Vaileth,
“Samahani mama, nje ya geti kuna mgeni wako nimemwambia aingie ila alikataa”
Basi mama Angel akajiuliza ni mgeni gani huyo? Ila akatoka kwenda nje kumuangalia, alishtuka sana baada ya kukuta mgeni mwenyewe ni Sia na Elly yani Sia alikuwa kamshika mkono Elly basi mama Angel alipofika pale Sia alimkabidhi mama Angel mkono wa Ellyn a kumwambia,
“Mtoto hajaenda shule huyo leo sababu anaumwa na mimi sina pesa ya matibabu, kwahiyo ukamtibie”
Halafu Sia alimuacha pale Elly na mama Angel kwakweli mama Angel hakuwa hata na la kusema kwani Sia alikuwa kama kaongea na dereva wa bodaboda sababu alipomaliza tu kuongea hayo, ilifika bodaboda na kumchukua halafu akaondoka nayo.
Basi mama Angel alimuangalia Elly huku akimuangalia na Sia anayeishia na bodaboda kisha akamuuliza Elly,
“Kwani unaumwa nini?”
“Kichwa ndio kinakuuma”
“Huyu mama yako huwa unamuelewa!”
“Namuelewa ndio”
“Kakwambia anakuleta hapa ndio hospitali?”
“Hapana, ila kasema sababu naumwa na yeye hana pesa ya kunipeleka hospitali basi amesema ni bora anilete hapa kwa ndugu zetu”
“Ndugu zenu!! Huyu mwanamke ana wazimu eeeh! Kuna ndugu zenu hapa? Si unafahamu hapa ni kwakina Erica?”
“Nafahamu ndio ila Erica ni dada yangu, nimeambiwa hivyo na mama na nyie ni ndugu zetu”
“Jamani huyu Sia jamani! Ana nini lakini aaarhg!”
Ila mama Angel alipomuangalia Elly vizuri aligundua kuwa Ellyn i mgonjwa, basi aliingia nae ndani ila kwenda nae hospitali hakuweza zaidi zaidi alimpatia pesa na kumwambia kuwa aende hospitali kisha akamwambia,
“Huyu mama yako ni chizi’
“Ila ndio mama yangu, na mama ni mama nampenda na yeye ananipenda sana”
“Mama anayekupenda hawezi kuja kukubwaga sehemu kama hivyo, mfano na mimi nikakutimua ingekuwaje? Huyo mama yako hakupendi wala nini, haya nenda kawahi hospitali huko, upande bajaji hapo ikusaidie kufika haraka hospitali”
Basi Elly alimshukuru pale na kutoka nje ya ile nyumba.
Ila alipotoka tu, alimkuta mama yake nje ya geti lile na kuondoka nae ambapo alimuuliza,
“Amekupa pesa ngapi mwanangu”
Elly akampa mama yake hela ambayo kapewa na mama Angel, basi Sia aliihesabu na kutabasamu maana ilikuwa laki moja, basi akasema,
“Nilijua tu, maana huyu mwanamke ana kisirani na kila kitu huchukulia hasira tu! Haya twende mwanangu, shule utaenda kesho, kama unavyonijua mama yako ni mtu wa…”
Elly akamalizia,
“Mtu wa ukipata tumia ukikosa jutia”
“Ndio mwanangu, Mungu anipe nini mimi eeeh! Anipe zigo la misumari nijitwike na kichwani nina kipara kisa nini!!”
Elly akacheka pale, ila kwa muda huo Elly na mama yake walipitia kwenye mgahawa ili wapate supu kidogo halafu ndio waende nyumbani kwao.
Siku hii baba Angel aliamka na uchovu kiasi na asubuhi hii aliongea kidogo na mke wake,
“Eeeeh mke wangu, kuna mahitaji gani ambayo yanatakiwa humu ndani?”
“Hamna mume wangu, yangekuwepo ningekwambia kabla ya kuuliza, ila umenikumbusha kitu kumbe ulimnunulia Erick simu!!”
“Ndio, sababu Sia alikuwa akimfatilia nikaona vyema nimnunulie simu ili akiwa anamfatilia aniambie”
“Jamani mume wangu, mfano shuleni atakwambiaje wakati wanakatazwa simu shuleni! Mimi nimempokonya maana Erica nae alinunuliwa simu na Junior sababu tu Erick anatumia simu”
“Sijakuelea hapo, Erica alinunuliwa simu na Junior kivipi?”
Ikabidi mama Angel amsimulie baba Angel vile alivyomkamata Erica na simu, basi baba Angel alielewa ile hoja ya mke wake na kuamua kujiandaa kwaajili ya kwenda kwenye kazi yao.
Alipomaliza kujiandaa alimuaga mke wake na kuondoka, ila wakati anatoka getini muda huu alimuona Sia akiwa amesimama na mtoto wa kiume mwenye umri kama wa Erick, kiukweli baba Angel hakumpenda mwanamke huyu kwahiyo alimpita kamavile hamuoni wala nini, yani baba Angel alikuwa akienda kazini huku akiwa na mawazo sana kwani aliona huyu mwanamke anamchanganya akili yake, ila akiwa barabara kuu kuna mtu alisimamisha gari yake ikabidi asimame na alipomuangalia vizuri mtu yule akamuona kuwa ni madam Oliva, basi yule madam aliingia kwenye gari ya baba Angel na kukaa kwenye siti huku akisema,
“Yani nilivyoona gari yako tu nikahisi moyo wangu ukidunda ndio nikakusimamisha”
“Oooh jamani, sasa moyo wako umedunda kwanini madam?”
“Aaaah tuachane na hayo, unaenda wapi muda huu?”
“Naenda ofisini”
“Basin i vyema nikafahamu ofisi yako ilipo”
“Sawa, hakuna tatizo lolote. Karibu sana”
Basi baba Angel alienda na madam Oliva hadi ofisini kwake na kumkaribisha, kwakweli Oliva aliipenda ofisi ya baba Angel kwani ilipangwa vizuri sana, kwahiyo aliingia nae ofisini na kuanza kuongea nae mawili matatu,
“Nimeipenda ofisi yako baba Erick jamani”
“Oooh asante sana”
“Halafu mke wako natamani sana kumfahamu jamani! Naamini nitamfahamu tu, ila baba Erick unaonekana ni mwanamke mstaarabu sana wewe, kwakweli mkeo ana bahati kubwa sana ya kukupata. Sema itakuwa ni vyema sana mimi na wewe tukiwa tunaonana na kuongelea maendeleo ya watoto shuleni au unasemaje?”
“Ni kweli kabisa, sina usemi kuhusu hilo”
“Basi, nitapenda upafahamu nyumbani kwangu pia”
“Sawa madam, nitapafahamu tu”
“Hata leo ukitaka”
“Hapana, kwa leo kuna kazi imenitinga labda siku nyingine”
“Basi tutawasiliana na nitafurahi sana juu ya hilo, maana ni vyema sana kwa wazazi kubadilishana mawazo”
Kisha Oliva alimuaga baba Angel kwani alitakiwa pia kuwahi kwenye kazi yake ambapo alikuwa akifundisha kwenye shule aliyosoma Erick.
Mama Angel akiwa katoka kumuogesha mtoto wake ambaye mara nyingi sana akioga tu analala, alishangaa mlinzi kufika sebleni na moja kwa moja aliitwa yeye na Vaileth,
“Samahani mama, nje ya geti kuna mgeni wako nimemwambia aingie ila alikataa”
Basi mama Angel akajiuliza ni mgeni gani huyo? Ila akatoka kwenda nje kumuangalia, alishtuka sana baada ya kukuta mgeni mwenyewe ni Sia na Elly yani Sia alikuwa kamshika mkono Elly basi mama Angel alipofika pale Sia alimkabidhi mama Angel mkono wa Ellyn a kumwambia,
“Mtoto hajaenda shule huyo leo sababu anaumwa na mimi sina pesa ya matibabu, kwahiyo ukamtibie”
Halafu Sia alimuacha pale Elly na mama Angel kwakweli mama Angel hakuwa hata na la kusema kwani Sia alikuwa kama kaongea na dereva wa bodaboda sababu alipomaliza tu kuongea hayo, ilifika bodaboda na kumchukua halafu akaondoka nayo.
Basi mama Angel alimuangalia Elly huku akimuangalia na Sia anayeishia na bodaboda kisha akamuuliza Elly,
“Kwani unaumwa nini?”
“Kichwa ndio kinakuuma”
“Huyu mama yako huwa unamuelewa!”
“Namuelewa ndio”
“Kakwambia anakuleta hapa ndio hospitali?”
“Hapana, ila kasema sababu naumwa na yeye hana pesa ya kunipeleka hospitali basi amesema ni bora anilete hapa kwa ndugu zetu”
“Ndugu zenu!! Huyu mwanamke ana wazimu eeeh! Kuna ndugu zenu hapa? Si unafahamu hapa ni kwakina Erica?”
“Nafahamu ndio ila Erica ni dada yangu, nimeambiwa hivyo na mama na nyie ni ndugu zetu”
“Jamani huyu Sia jamani! Ana nini lakini aaarhg!”
Ila mama Angel alipomuangalia Elly vizuri aligundua kuwa Ellyn i mgonjwa, basi aliingia nae ndani ila kwenda nae hospitali hakuweza zaidi zaidi alimpatia pesa na kumwambia kuwa aende hospitali kisha akamwambia,
“Huyu mama yako ni chizi’
“Ila ndio mama yangu, na mama ni mama nampenda na yeye ananipenda sana”
“Mama anayekupenda hawezi kuja kukubwaga sehemu kama hivyo, mfano na mimi nikakutimua ingekuwaje? Huyo mama yako hakupendi wala nini, haya nenda kawahi hospitali huko, upande bajaji hapo ikusaidie kufika haraka hospitali”
Basi Elly alimshukuru pale na kutoka nje ya ile nyumba.
Ila alipotoka tu, alimkuta mama yake nje ya geti lile na kuondoka nae ambapo alimuuliza,
“Amekupa pesa ngapi mwanangu”
Elly akampa mama yake hela ambayo kapewa na mama Angel, basi Sia aliihesabu na kutabasamu maana ilikuwa laki moja, basi akasema,
“Nilijua tu, maana huyu mwanamke ana kisirani na kila kitu huchukulia hasira tu! Haya twende mwanangu, shule utaenda kesho, kama unavyonijua mama yako ni mtu wa…”
Elly akamalizia,
“Mtu wa ukipata tumia ukikosa jutia”
“Ndio mwanangu, Mungu anipe nini mimi eeeh! Anipe zigo la misumari nijitwike na kichwani nina kipara kisa nini!!”
Elly akacheka pale, ila kwa muda huo Elly na mama yake walipitia kwenye mgahawa ili wapate supu kidogo halafu ndio waende nyumbani kwao.