Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 61
James alimuita Bahati na kumsimamisha, kisha akamnasa kofi,
“Ila kaka unanionea”
“Nakuonea nini mshenzi mkubwa wewe, unataka kuharibu maisha ya Erica nikuangalie tu”
“Nampenda kweli na sina haja ya kuahribu maisha yake”
Akamnasa tena kibao,
“Na ole wako nisikie umetembea nae, nitakuchinja na utanijua vizuri mimi ni nani. Kuanzia sasa, Yule muone kama kituo cha polisi, nitakufunga mimi. Potea mbele yangu”
James alikuwa na hasira sana maana kila akikumbuka jinsi Erica alivyomlaghai halafu anakutana na kijana wa ajabu ajabu alikuwa na Erica roho ilimuuma sana kamavile Erica ni mke wake.
Alirudi nyumbani na kumkuta mkewe sebleni,
“Kheee ulienda wapi na wewe?”
“Yani Yule mjinga nilienda kumpa onyo sababu sikuridhika kabisa”
“Asante mume wangu kwa kumjali mdogo wangu”
“Kwanza yuko wapi? Anatakiwa nae tumpe onyo asituletee tena watu wa kijinga jinga hapa nyumbani”
“Yupo chumbani kwake, ila nishaongea nae”
“Haitoshi, mimi ndio baba mwenye nyumba. Aibu ikija hapa tutadhalilika wote”
“Kweli mume wangu, yupo chumbani kwake kule”
James akaenda kwenye chumba cha Erica na kufungua mlango ila ulikuwa mgumu na kuonyesha kuwa umefungwa kwa ndani, James akasema kwa hasira,
“Wewe Erica fungua mlango”
Erica nae akajibu kwa kwa kujiamini,
“Sifungui mlango, dada ameshanisema inatosha”
“Una kiburi eeh!”
Erica akawa kimya na kumfanya James achukie zaidi, akarudi sebleni alipo mkewe na kumwambia,
“Dogo lako lina kiburi sana, unajua limegoma nisiongee nalo!”
Bite akachukia pia na kuinuka, akafungua mlango wa Erica ukawa haufunguki na kumwambia,
“Wewe Erica nifungulie mlango kichaa wewe”
Erica akafungua mlango, dada yake akamzaba kibao,
“Unajifungia milango nyumba yako hii? Nyumba ni yangu na mume wangu halafu bila aibu unajifungia milango na kugoma kutufungulia. Na kwanini umegoma shemeji yako asikuseme?”
“Dada ulishanisema nimesikia jamani, nianze kusemwa tena kwanini?”
“Hivi unajua kama Yule ndio baba mwenye nyumba?”
“Najua dada”
“Sasa unabishaje kusemwa na shemeji yako?”
“Dada, ngoja nikuulize swali. Hivi ni tamaduni za wapi eti shemeji aje chumbani kwangu kunisema? Hata kama hii ni nyumba yenu, ila hiki chumba nalala mimi na sidhani kama ni jambo linalofaa eti shemeji aingie chumbani kwangu? Hiki ni chumba cha msichana, naweka vitu vya kike, yani shemeji akutane na chupi zangu kweli? Au akutane na pedi zangu? Labda kama nimezidiwa sijiwezi kabisa na hakuna msaada anaweza kuja kunisaidia ila sio nikiwa mzima hivi, ni tamaduni za wapi hizo? Kama mnahitaji kunishambulia kwa kunisema si mniite sebleni hapo, mnisemeee weee hadi yaniingie ila sio kwa shemeji kunifata chumbani kwangu”
Kwa kiasi Fulani haya maneno yalimuingia Bite ila ilibidi ajitete kidogo,
“Sasa kwani wewe unahisi nini kama angeingia na kukusema humu? Yule si kama kaka yako tu?”
“Ni kweli kama kaka yangu ila kumbuka si kaka yangu ni shemeji yangu”
“Usimfikirie vibaya mume wangu, hawezi kufanya ujinga kwako hata mara moja, kwanza anakuona kama mwanae hata sijui umeanzaje kumfikiria vibaya hivyo shemeji yako Erica! Huyu ni mume wangu, hajawahi kuwa na mwanamke mwingine yeyote nje zaidi yangu, iwe kumtamani mdogo wangu kweli?”
“Sijasema hivyo dada labda kama umefikiria vibaya na wewe pia ila nimekwambia sio tamaduni zetu”
Bite kwa kiasi maneno ya mdogo wake yalimuingia na kwa kiasi yalimchukiza na kuamua kutoka zake mule chumbani kwa Erica.
James alimuita Bahati na kumsimamisha, kisha akamnasa kofi,
“Ila kaka unanionea”
“Nakuonea nini mshenzi mkubwa wewe, unataka kuharibu maisha ya Erica nikuangalie tu”
“Nampenda kweli na sina haja ya kuahribu maisha yake”
Akamnasa tena kibao,
“Na ole wako nisikie umetembea nae, nitakuchinja na utanijua vizuri mimi ni nani. Kuanzia sasa, Yule muone kama kituo cha polisi, nitakufunga mimi. Potea mbele yangu”
James alikuwa na hasira sana maana kila akikumbuka jinsi Erica alivyomlaghai halafu anakutana na kijana wa ajabu ajabu alikuwa na Erica roho ilimuuma sana kamavile Erica ni mke wake.
Alirudi nyumbani na kumkuta mkewe sebleni,
“Kheee ulienda wapi na wewe?”
“Yani Yule mjinga nilienda kumpa onyo sababu sikuridhika kabisa”
“Asante mume wangu kwa kumjali mdogo wangu”
“Kwanza yuko wapi? Anatakiwa nae tumpe onyo asituletee tena watu wa kijinga jinga hapa nyumbani”
“Yupo chumbani kwake, ila nishaongea nae”
“Haitoshi, mimi ndio baba mwenye nyumba. Aibu ikija hapa tutadhalilika wote”
“Kweli mume wangu, yupo chumbani kwake kule”
James akaenda kwenye chumba cha Erica na kufungua mlango ila ulikuwa mgumu na kuonyesha kuwa umefungwa kwa ndani, James akasema kwa hasira,
“Wewe Erica fungua mlango”
Erica nae akajibu kwa kwa kujiamini,
“Sifungui mlango, dada ameshanisema inatosha”
“Una kiburi eeh!”
Erica akawa kimya na kumfanya James achukie zaidi, akarudi sebleni alipo mkewe na kumwambia,
“Dogo lako lina kiburi sana, unajua limegoma nisiongee nalo!”
Bite akachukia pia na kuinuka, akafungua mlango wa Erica ukawa haufunguki na kumwambia,
“Wewe Erica nifungulie mlango kichaa wewe”
Erica akafungua mlango, dada yake akamzaba kibao,
“Unajifungia milango nyumba yako hii? Nyumba ni yangu na mume wangu halafu bila aibu unajifungia milango na kugoma kutufungulia. Na kwanini umegoma shemeji yako asikuseme?”
“Dada ulishanisema nimesikia jamani, nianze kusemwa tena kwanini?”
“Hivi unajua kama Yule ndio baba mwenye nyumba?”
“Najua dada”
“Sasa unabishaje kusemwa na shemeji yako?”
“Dada, ngoja nikuulize swali. Hivi ni tamaduni za wapi eti shemeji aje chumbani kwangu kunisema? Hata kama hii ni nyumba yenu, ila hiki chumba nalala mimi na sidhani kama ni jambo linalofaa eti shemeji aingie chumbani kwangu? Hiki ni chumba cha msichana, naweka vitu vya kike, yani shemeji akutane na chupi zangu kweli? Au akutane na pedi zangu? Labda kama nimezidiwa sijiwezi kabisa na hakuna msaada anaweza kuja kunisaidia ila sio nikiwa mzima hivi, ni tamaduni za wapi hizo? Kama mnahitaji kunishambulia kwa kunisema si mniite sebleni hapo, mnisemeee weee hadi yaniingie ila sio kwa shemeji kunifata chumbani kwangu”
Kwa kiasi Fulani haya maneno yalimuingia Bite ila ilibidi ajitete kidogo,
“Sasa kwani wewe unahisi nini kama angeingia na kukusema humu? Yule si kama kaka yako tu?”
“Ni kweli kama kaka yangu ila kumbuka si kaka yangu ni shemeji yangu”
“Usimfikirie vibaya mume wangu, hawezi kufanya ujinga kwako hata mara moja, kwanza anakuona kama mwanae hata sijui umeanzaje kumfikiria vibaya hivyo shemeji yako Erica! Huyu ni mume wangu, hajawahi kuwa na mwanamke mwingine yeyote nje zaidi yangu, iwe kumtamani mdogo wangu kweli?”
“Sijasema hivyo dada labda kama umefikiria vibaya na wewe pia ila nimekwambia sio tamaduni zetu”
Bite kwa kiasi maneno ya mdogo wake yalimuingia na kwa kiasi yalimchukiza na kuamua kutoka zake mule chumbani kwa Erica.