Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #221
SEHEMU YA 176
Walifika hotelini na kuingia kwenye chumba ambacho Erica alimkodia Rahim, kisha kabla ya vyote Rahim alitaka kwenda kuoga kwanza ila Erica alitoka mule ndani na kwenda kuagiza chakula, alipoenda kuagiza chakula aliwasha tena simu yake na kukuta jumbe kama tatu za Babuu akilalamika kuwa mbona simu haipokelewi, Erica aliamua kumtumia ujumbe,
“Mwenzio nimeshikwa na tumbo la kuhara, nimeona unachelewa nikaamua kukodi bajaji. Nipo nyumbani saivi”
“Sasa ile shida yangu ya maongezi na wewe”
“Tutaongea siku nyingine Babuu, mwenzio naugulia tumbo”
“Pole Erica”
Basi aliposoma huo ujumbe, akazima tena simu yake kwani hakutaka iwe wazi akihofia kupigiwa tena na Babuu.
Alirudi chumbani huku akisubiri kile chakula ambacho alimwagizia Rahim, na chakula kilifika kisha yeye na Rahim wakala na kukaa wakifanya maongezi huku Rahim akimtolea zile zawadi ambazo alimuagiza na Erica alizipenda sana kwani zilikuwa za kuvutia, ilipoanza kuingia jioni Erica alimwambia Rahim kuwa anarudi kwao,
“Yani unamaanisha unataka uondoke Erica uniache peke yangu!”
“Sasa Rahim si nishafanya vyote ulivyosema?”
“Ndio umefanya ila leo huondoki hapa, yani tutalala wote kwakweli, huwezi ukaniacha peke yangu niboreke basi haikuwa na maana ya mimi kutokufikia nyumbani kwetu”
“Ila sijaaga nyumbani Rahim!”
“Sio tatizo, piga simu nyumbani kwenu waambie kuna sehemu umeenda kufanya project ili wasiwe na mashaka ila leo huondoki hapa”
Ilibidi Erica awashe simu na kupiga simu kwa mama yake kwani ndio anakuwaga wa kwanza kushikwa na uoga, akamwambia kuwa kuna sehemu ya gafla wamesafiri kimasomo na wamechelewa kurudi kwahiyo kwao ataenda kesho, mama yake aliitikia ila kwa shingo upande tu, ilibidi amuamini hivyo hivyo ingawa ilikuwa ni ngumu sana kuamini kile alichoambiwa na Erica.
Erica hakuwa na namna nyingine zaidi ya kuwa pamoja na Rahim tu kwani alishajitoa kuwa ndiye mpenzi wake, kwahiyo siku hiyo usiku mzima alikuwa pamoja na Rahim.
Palipokucha alikuwa amechoka kwakweli na hakuweza tena kuendelea na chochote zaidi ya kumuomba Rahim arudi kwao tu,
“Nitakuruhusu Erica ila bado sijaridhika”
“Basi naomba nikapumzike kidogo tu nyumbani”
“Mmmh mbona umeanza kunitisha mapema hivyo? Hivi utaweza kweli kuishi kwenye ndoa?”
“Nitaweza ndio”
“Sasa, mume mwenyewe si ndio mimi. Ndoa inahitaji uvumilivu Erica, sasa kama vitu vidogo hivi kuvumilia huwezi vikubwa je?”
“Sio hivyo ila kumbuka nyumbani nimewaambia kuwa narudi leo sasa mama hawezi kunielewa”
“Sikia nikwambie kitu, tutakodi usafiri kwenda kwenu halafu utamuaga mama yako kuwa mnasafiri kimasomo, utajiandaa halafu tutarudi tena hapa hotelini. Hupendi kuwa na mimi Erica?”
“Napenda”
“Sasa kama unapenda mbona unachoka mapema sana?”
Erica hakuwa na jibu zaidi ya kukubaliana na kile alichosema Rahim, kisha kujiandaa na kuondoka nae hadi kwao ambapo Rahim alikaa mahali akimsubiri atoke kwao.
Erica aliingia kwao ila alikuwa na mawazo sana kwani katika maisha yake ya mapenzi yote, siku hiyo alichoka na kuumia halafu mtu ndio anamsubiri bado ila kwavile alikuwa akiiota ndoa ilibidi avumilie tu kwani aliona uvumilivu ndio utamsaidia.
Hakumkuta mama yake ndani, akajiandaa kisha akamuandikia mama yake barua na kumuwekea laki mbili ndani yake kwani ugonjwa wa mama yake ni hela na alishaujua kwahiyo alivyomuwekea hivyo alijua mama yake asingemsumbua tena na angemuamini hiyo safari aliyoenda.
Kisha akatoka na kumpigia simu Rahim ambapo alikodi tena gari na kurudi nae tena hotelini.
Walikaa huko hotelini na Rahim ila baada ya siku tatu uzalendo ukamshinda Erica, ingawa aliandika barua kwa mama yake kuwa ni safari ya wiki ila baada ya siku tatu aliomba tu kurudi kwao,
“Rahim, sidhani kama tunachofanya ni sawa. Maana sie bado hatujaoana”
“Ndio umetambua leo kwamba bado hatujaoana?”
Erica aliitikia tu ila alitamani apate nafasi ya kwenda kupumzika, na kwa wakati huu Rahim alimruhusu kwani alisema kuwa ameridhika kiasi, kisha akamwambia,
“Swala langu linabaki pale pale, usiwe karibu na mama yangu sawa!”
“Sawa”
Kisha ukafanyika mpango wa kurudi nyumbani kwao.
Walifika hotelini na kuingia kwenye chumba ambacho Erica alimkodia Rahim, kisha kabla ya vyote Rahim alitaka kwenda kuoga kwanza ila Erica alitoka mule ndani na kwenda kuagiza chakula, alipoenda kuagiza chakula aliwasha tena simu yake na kukuta jumbe kama tatu za Babuu akilalamika kuwa mbona simu haipokelewi, Erica aliamua kumtumia ujumbe,
“Mwenzio nimeshikwa na tumbo la kuhara, nimeona unachelewa nikaamua kukodi bajaji. Nipo nyumbani saivi”
“Sasa ile shida yangu ya maongezi na wewe”
“Tutaongea siku nyingine Babuu, mwenzio naugulia tumbo”
“Pole Erica”
Basi aliposoma huo ujumbe, akazima tena simu yake kwani hakutaka iwe wazi akihofia kupigiwa tena na Babuu.
Alirudi chumbani huku akisubiri kile chakula ambacho alimwagizia Rahim, na chakula kilifika kisha yeye na Rahim wakala na kukaa wakifanya maongezi huku Rahim akimtolea zile zawadi ambazo alimuagiza na Erica alizipenda sana kwani zilikuwa za kuvutia, ilipoanza kuingia jioni Erica alimwambia Rahim kuwa anarudi kwao,
“Yani unamaanisha unataka uondoke Erica uniache peke yangu!”
“Sasa Rahim si nishafanya vyote ulivyosema?”
“Ndio umefanya ila leo huondoki hapa, yani tutalala wote kwakweli, huwezi ukaniacha peke yangu niboreke basi haikuwa na maana ya mimi kutokufikia nyumbani kwetu”
“Ila sijaaga nyumbani Rahim!”
“Sio tatizo, piga simu nyumbani kwenu waambie kuna sehemu umeenda kufanya project ili wasiwe na mashaka ila leo huondoki hapa”
Ilibidi Erica awashe simu na kupiga simu kwa mama yake kwani ndio anakuwaga wa kwanza kushikwa na uoga, akamwambia kuwa kuna sehemu ya gafla wamesafiri kimasomo na wamechelewa kurudi kwahiyo kwao ataenda kesho, mama yake aliitikia ila kwa shingo upande tu, ilibidi amuamini hivyo hivyo ingawa ilikuwa ni ngumu sana kuamini kile alichoambiwa na Erica.
Erica hakuwa na namna nyingine zaidi ya kuwa pamoja na Rahim tu kwani alishajitoa kuwa ndiye mpenzi wake, kwahiyo siku hiyo usiku mzima alikuwa pamoja na Rahim.
Palipokucha alikuwa amechoka kwakweli na hakuweza tena kuendelea na chochote zaidi ya kumuomba Rahim arudi kwao tu,
“Nitakuruhusu Erica ila bado sijaridhika”
“Basi naomba nikapumzike kidogo tu nyumbani”
“Mmmh mbona umeanza kunitisha mapema hivyo? Hivi utaweza kweli kuishi kwenye ndoa?”
“Nitaweza ndio”
“Sasa, mume mwenyewe si ndio mimi. Ndoa inahitaji uvumilivu Erica, sasa kama vitu vidogo hivi kuvumilia huwezi vikubwa je?”
“Sio hivyo ila kumbuka nyumbani nimewaambia kuwa narudi leo sasa mama hawezi kunielewa”
“Sikia nikwambie kitu, tutakodi usafiri kwenda kwenu halafu utamuaga mama yako kuwa mnasafiri kimasomo, utajiandaa halafu tutarudi tena hapa hotelini. Hupendi kuwa na mimi Erica?”
“Napenda”
“Sasa kama unapenda mbona unachoka mapema sana?”
Erica hakuwa na jibu zaidi ya kukubaliana na kile alichosema Rahim, kisha kujiandaa na kuondoka nae hadi kwao ambapo Rahim alikaa mahali akimsubiri atoke kwao.
Erica aliingia kwao ila alikuwa na mawazo sana kwani katika maisha yake ya mapenzi yote, siku hiyo alichoka na kuumia halafu mtu ndio anamsubiri bado ila kwavile alikuwa akiiota ndoa ilibidi avumilie tu kwani aliona uvumilivu ndio utamsaidia.
Hakumkuta mama yake ndani, akajiandaa kisha akamuandikia mama yake barua na kumuwekea laki mbili ndani yake kwani ugonjwa wa mama yake ni hela na alishaujua kwahiyo alivyomuwekea hivyo alijua mama yake asingemsumbua tena na angemuamini hiyo safari aliyoenda.
Kisha akatoka na kumpigia simu Rahim ambapo alikodi tena gari na kurudi nae tena hotelini.
Walikaa huko hotelini na Rahim ila baada ya siku tatu uzalendo ukamshinda Erica, ingawa aliandika barua kwa mama yake kuwa ni safari ya wiki ila baada ya siku tatu aliomba tu kurudi kwao,
“Rahim, sidhani kama tunachofanya ni sawa. Maana sie bado hatujaoana”
“Ndio umetambua leo kwamba bado hatujaoana?”
Erica aliitikia tu ila alitamani apate nafasi ya kwenda kupumzika, na kwa wakati huu Rahim alimruhusu kwani alisema kuwa ameridhika kiasi, kisha akamwambia,
“Swala langu linabaki pale pale, usiwe karibu na mama yangu sawa!”
“Sawa”
Kisha ukafanyika mpango wa kurudi nyumbani kwao.