Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #301
SEHEMU YA 237
Aliporudi kwenye kazi zake akakumbuka kuwaandalia ratiba wale wakina Dora kuhusu kuja kuzungumzia bidhaa zao, kwahiyo aliangalia namba zao na kupiga kuwa kashawaandalia barua ya ratiba waende kuchukua.
Baada kama ya lisaa limoja, Dora alikuwa mahali pale kuchukua barua kutoka kwa Erica alisalimiana nae vizuri sana kisha Erica akampa ile barua ila kiukweli Erica hakutaka ukaribu wa haswaa na Dora ila kwa Dora ilikuwa tofauti maana alionyesha kutaka ukaribu zaidi na Erica.
“Erica hongera sana rafiki yangu, umepata kazi sehemu nzuri sana, nani alikuunganishia?”
“Kwanini umeniuliza hivyo?”
“Na mimi Erica, kama kuna aliyekuunganishia na mimi nahitaji”
“Hakuna aliyeniunganishia, mimi nilituma maombi ya kazi tu na kupata”
“Basi na mimi nilete maombi yangu ya kazi, na ukisikia kama kuna nafasi ya kazi uniambie Erica, tafadhali maisha ni kusaidiana”
“Leo ndio unalijua hilo?”
“Erica, ulisema tusahau yote yaliyopita na tuanze mapya”
“Haya yameisha”
“Nashukuru Erica, kwaheri eeh!”
Dora akaaga na kuondoka, Erica alikuwa akiongea na Dora ilimradi tu maana alishamwambia kuwa amemsamehe kwahiyo hakuona kama ni swala zuri kutokuongea vizuri na Dora.
Alipomaliza kazi zake kama kawaida, alienda kumuaga shemeji yake na kukumbushwa swala la kesho yake kutafuta sehemu atakayo somea udereva.
Kwahiyo Erica aliondoka na kwenda kupanda daladala ili kuelekea nyumbani kwao, alipokuwa kwenye daladala ile wakati akiwa na uchovu uchovu sababu ya kukaa kwenye kompyuta kwa muda mwingi, alijikuta tu akisinzia kwenye kiti cha daladala , mara akashtuliwa na mkaka mmoja aliyekuwa pembeni yake,
“Pole sana dada, inaonyesha umechoka sana”
“Asante”
“Samahani dada yangu unaitwa nani?”
“Naitwa Erica”
“Basi mimi naitwa Juma, nimefurahi kukufahamu. Napenda tuwe marafiki, naomba namba zako”
“Umesema unaitwa nani?”
“Naitwa Juma”
“Namba zangu za nini?”
“Nahitaji tuwe tunawasiliana Erica”
“Unikome tena unikome kabisa, sipendi mazoea ya kijinga. Nikome, sihitaji kuzoeana na wewe”
Huyu kaka alimshangaa sana Erica kuwa ana tatizo gani maana kamjibu kwa hasira utafikiri kuna jambo baya amemwambia, hadi mkaka wa watu akajihisi vibaya kuwa pale hajamtongoza je akimtongoza itakuwaje? Alibaki akimshangaa kisha akamwambia,
“Kwani dada tatizo ni nini? Kufahamiana na mtu ni tatizo? Kama hutaki kunipa namba yako si ungesema tu sitaki kuliko kuanza na mada za unikome sijui nini na nini jamani?”
“Tena usinizoee wala usiendelee kuniongelesha, kwenye daladala yote hujaona wadada wa kuwasemesha zaidi yangu? Sitaki mazoea”
Huyu kaka alimshangaa sana Erica ila ilibidi awe mpole tu na kumwambia kwa upole,
“Binadamu hatwendi hivyo Erica, unaweza ukaanguka nikakuinua au mimi nikaanguka ukaniinua. Binadamu hatujibishani vibaya”
“Sikia wewe, sijui Juma sikia nikwambie yani mimi hata ukiniona nakufa hapo niache nife ila mazoea na wewe sitaki”
“Kwanini umekuwa mkali hivyo dada?”
“Nyie wanaume ni watiu wabaya sana, yani hapo utakuwa unajiongelesha sijui namba yako namba yako ila lengo lako ni kunitongoza. Nishakwambia naitwa Erica, na wewe Juma umeona kabisa itikadi zetu hazifanani ila unakazana kutaka namba yangu. Unanitakia nini mimi? Sitaki yani sitaki kabisa, mwisho wa siku ndio uniambie badili dini nikuoe, nikisema nipo tayari ulete propaganda zingine, sitaki na usiniongeleshe tena”
Kituo kilichofuata Erica alishuka sio kwamba alifika ila hakutaka kuendelea kuongea na huyu Juma ndiomana alishuka kituo ambacho sio chake.
Kisha alipanda daladala nyingine na kwenda hadi kituo chake akashuka na kuelekea nyumbani.
Aliporudi kwenye kazi zake akakumbuka kuwaandalia ratiba wale wakina Dora kuhusu kuja kuzungumzia bidhaa zao, kwahiyo aliangalia namba zao na kupiga kuwa kashawaandalia barua ya ratiba waende kuchukua.
Baada kama ya lisaa limoja, Dora alikuwa mahali pale kuchukua barua kutoka kwa Erica alisalimiana nae vizuri sana kisha Erica akampa ile barua ila kiukweli Erica hakutaka ukaribu wa haswaa na Dora ila kwa Dora ilikuwa tofauti maana alionyesha kutaka ukaribu zaidi na Erica.
“Erica hongera sana rafiki yangu, umepata kazi sehemu nzuri sana, nani alikuunganishia?”
“Kwanini umeniuliza hivyo?”
“Na mimi Erica, kama kuna aliyekuunganishia na mimi nahitaji”
“Hakuna aliyeniunganishia, mimi nilituma maombi ya kazi tu na kupata”
“Basi na mimi nilete maombi yangu ya kazi, na ukisikia kama kuna nafasi ya kazi uniambie Erica, tafadhali maisha ni kusaidiana”
“Leo ndio unalijua hilo?”
“Erica, ulisema tusahau yote yaliyopita na tuanze mapya”
“Haya yameisha”
“Nashukuru Erica, kwaheri eeh!”
Dora akaaga na kuondoka, Erica alikuwa akiongea na Dora ilimradi tu maana alishamwambia kuwa amemsamehe kwahiyo hakuona kama ni swala zuri kutokuongea vizuri na Dora.
Alipomaliza kazi zake kama kawaida, alienda kumuaga shemeji yake na kukumbushwa swala la kesho yake kutafuta sehemu atakayo somea udereva.
Kwahiyo Erica aliondoka na kwenda kupanda daladala ili kuelekea nyumbani kwao, alipokuwa kwenye daladala ile wakati akiwa na uchovu uchovu sababu ya kukaa kwenye kompyuta kwa muda mwingi, alijikuta tu akisinzia kwenye kiti cha daladala , mara akashtuliwa na mkaka mmoja aliyekuwa pembeni yake,
“Pole sana dada, inaonyesha umechoka sana”
“Asante”
“Samahani dada yangu unaitwa nani?”
“Naitwa Erica”
“Basi mimi naitwa Juma, nimefurahi kukufahamu. Napenda tuwe marafiki, naomba namba zako”
“Umesema unaitwa nani?”
“Naitwa Juma”
“Namba zangu za nini?”
“Nahitaji tuwe tunawasiliana Erica”
“Unikome tena unikome kabisa, sipendi mazoea ya kijinga. Nikome, sihitaji kuzoeana na wewe”
Huyu kaka alimshangaa sana Erica kuwa ana tatizo gani maana kamjibu kwa hasira utafikiri kuna jambo baya amemwambia, hadi mkaka wa watu akajihisi vibaya kuwa pale hajamtongoza je akimtongoza itakuwaje? Alibaki akimshangaa kisha akamwambia,
“Kwani dada tatizo ni nini? Kufahamiana na mtu ni tatizo? Kama hutaki kunipa namba yako si ungesema tu sitaki kuliko kuanza na mada za unikome sijui nini na nini jamani?”
“Tena usinizoee wala usiendelee kuniongelesha, kwenye daladala yote hujaona wadada wa kuwasemesha zaidi yangu? Sitaki mazoea”
Huyu kaka alimshangaa sana Erica ila ilibidi awe mpole tu na kumwambia kwa upole,
“Binadamu hatwendi hivyo Erica, unaweza ukaanguka nikakuinua au mimi nikaanguka ukaniinua. Binadamu hatujibishani vibaya”
“Sikia wewe, sijui Juma sikia nikwambie yani mimi hata ukiniona nakufa hapo niache nife ila mazoea na wewe sitaki”
“Kwanini umekuwa mkali hivyo dada?”
“Nyie wanaume ni watiu wabaya sana, yani hapo utakuwa unajiongelesha sijui namba yako namba yako ila lengo lako ni kunitongoza. Nishakwambia naitwa Erica, na wewe Juma umeona kabisa itikadi zetu hazifanani ila unakazana kutaka namba yangu. Unanitakia nini mimi? Sitaki yani sitaki kabisa, mwisho wa siku ndio uniambie badili dini nikuoe, nikisema nipo tayari ulete propaganda zingine, sitaki na usiniongeleshe tena”
Kituo kilichofuata Erica alishuka sio kwamba alifika ila hakutaka kuendelea kuongea na huyu Juma ndiomana alishuka kituo ambacho sio chake.
Kisha alipanda daladala nyingine na kwenda hadi kituo chake akashuka na kuelekea nyumbani.