Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #361
SEHEMU YA 277
Kesho yake tu alimuaga mama yake kuwa anatoka kidogo na kwenda kushughulikia cheti cha kuzaliwa cha mtoto wake ambapo aliambiwa kuwa kitatoka baada ya wiki moja.
Yani wakati huo hata aliacha kufatilia mambo ya mkataba wa benki kabisa kwani hakutaka kuwa karibu na mzee Jimmy, ingawa mzee huyo alimtumia ujumbe mara kwa mara kuwa aende benki wakamalizie hatua za mkataba ila Erica hakutaka tena hata alipopigiwa na Yule meneja napo hakutaka kabisa maana alijiona anatosha kwa aliyoyapitia.
Ilimradi Erick kajitolea kumtunza mtoto ilikuwa inamtosha kwakweli.
Siku aliyoenda kufata cheti cha mtoto wake, wakati anarudi alikutana na Yule mama ambaye walikutana dukani akamsaidia kuchukua maji, Yule mama alisimamisha gari yake na kumuita,
“Erica”
Erica alienda kwa Yule mama ambaye alijawa na tabasamu tu, akamsalimia kisha Yule mama akasema,
“Yani nilipoteza namba yako, moyo ukaniuma kweli ila Mungu ni mwema nimekuona tena, ngoja nikuulize swali, una kazi? Yani unafanya kazi?”
“Hapana, nipo nyumbani tu”
“Umesoma mpaka wapi?”
“Chuo, nina shahada ya biashara”
“Jamani, ndio huna kazi kweli binti mzuri kama wewe dah! Sikia, chukua hii kadi yangu ya biashara, wiki ijayo njoo ofisini kwangu na vyeti vyako”
“Asante”
Erica alimshukuru sana Yule mama kwani aliona kama ni kitu cha ajabu ametunukiwa kwa muda huo, kisha akaagana nae na kurudi nyumbani.
Alifika na kujisemea,
“Kweli Mungu ana njia zake za kubariki, nadhani Erick ni baraka tosha katika maisha yangu. Nikijaribu kuunganisha matukio naona wazi kuwa Erick ni baraka tosha kwangu, kwanza Erick alinipigia simu nikawa na kimuhemuhe cha kumpigia na kuamua nikanunue vocha, mama akaamua aniagize na soda ndipo nikakutana na Yule mama mwenye roho nzuri. Haya Erick kasema nifatilie cheti cha kuzaliwa cha mtoto, natoka kukifata nakutana na huyu mama na ananiahidi kazi, wow nadhani Erick ni baraka kwangu”
Alitabasamu maana ilikuwa ni furaha kwake.
Alirudi kwao, kwa kipindi hiko mwanae alikuwa ameanza utundu wa kimya kimya kiasi kwamba alikuwa akirudi tu basi mwanae alichukua mkoba na kuangalia kuwa mama yake kamletea zawadi gani, bibi yake alikuwa akicheka sana na kusema,
“Yani Angel ananikumbusha kipindi kile wakati wewe mdogo, mtu akikuangalia anakuona mtoto mpole kumbe una utundu wa kimya kimya ninaoujua mimi tu, sasa mtu hawezi kudhania kama Angel anaweza fungua mkoba na kupekua ila ona hapo. Hahaha mpaka apate anachotaka”
Kwahiyo Erica alikuwa akinunua matunda mara nyingi ambapo akifika tu anampa mwanae ili mwanae asimpekue mkoba.
Alichukua mkoba wake na kuingia chumbani ambapo aliweka vizuri CV yake na vyeti vyake, aliweka kwenye bahasha nzuri kwaajili ya kuvipeleka kesho kwa Yule mama.
Alipomaliza alimpigia simu Erick kuwa kashapata cheti cha mtoto na picha anazo, basi Erick akamuelekeza mahali pa kupeleka ili mtoto atengenezewe kadi ya bima ya afya, kwahiyo Erica aliona ni vyema afanye vyote kwa pamoja.
Siku hiyo aliondoka asubuhi kwao na kuanza kwenda kwenye ofisi ya Yule mama akifata maelekezo ya kwenye ile kadi aliyopewa na kufika, kisha akaenda mapokezi na kumuulizia,
“Una miadi nae?”
“Ndio”
“Ngoja nimpigie simu, nimwambie unaitwa nani?”
“Erica”
Basi Yule wa mapokezi akapiga simu, Yule mama alipokea ila alionyesha alikuwa na kikao na kuomba kuongea na Erica, ambapo Yule wa mapokezi akamkabidhi simu Erica kisha Yule mama akamwambia aache nakala ya vyeti vyake kwa Yule mtu wa mapokezi, Erica alimshukuru kisha wakakata ile simu na kumuachia Yule wa mapokezi bahasha ya vyeti vyake halafu yeye kuondoka.
Moja kwa moja alienda mahali ambako Erick alimuelekeza kuwa apelike vile vitu kwaajili ya mtoto kupata kadi ya bima ya afya.
Basi alifika kama alivyoelekezwa na moja kwa moja alienda mapokezi na kukutana na mdada ambaye alimsalimia kisha kumuachia vile vitu vya mtoto ambavyo vilikuwa kwenye bahasha iliyoandikwa jina la Erick nje maana ndio maelekezo aliyopewa na Erick,
“Aaaah sawa, basi kikiwa tayari tutakupigia simu uju uchukue”
“Sawa nashukuru”
Basi Erica akaondoka zake, wakati yupo kwenye stendi ya daladala, kuna mdada alifika mbele yake na huyo mdada alionyesha kumfahamu Erica ila Erica alishamsahau, ikabidi Yule mdada aanze kumkumbusha,
“Unakumbuka siku ile umefika kwa Bahati nikakupeleka alipokuwa anaoa Yule Nasma hadi ukaanguka, unakumbuka”
Erica alimtazama huyu mdada na kumjibu,
“Nakumbuka ndio”
“Vipi, uliweza kuacha maisha yaendelee? Mapenzi ndivyo yalivyo mdogo wangu, muda mwingine unaumia hata usipotarajia”
“Nishasahau mie”
“Basi Yule Nasma saivi ni mjamzito, yani Bahati hajachelewesha yupo vizuri huyo”
Erica aliona huyu nae yupo kumchanganya tu wakati yeye ameshaanza kusahau mambo hayo, aliamua kumuaga na kuondoka zake kuelekea kwao, kwani hakutaka kuumiuza kichwa kabisa kwa muda huo kumfikiria tena bahati aliyemshuhudia akifunga ndoa, kwahiyo alipanda basin a kurudi kwao ambapo alimkuta mama yake kama kawaida ila leo mama yake alimwambia,
“Mwenendo wako kwa hivi karibuni umenifurhisha sana, ukienda mahali unawahi kurudi, sijasikia ujinga wa kuleta marafiki wa ajabu ajabu kama Dora. Mwanangu bora umeachana na aina ile ya marafiki, narudia tena, mimi ndio rafiki yako wa kweli. Kama una shida yoyote au una jambo lolote usisite kuniambia mimi rafiki yako wa ukweli”
“Sawa mama”
Basi akafurahi sana maana kwa siku hizo alikuwa akiongea kwa upendo tu na mama yake.
Kesho yake tu alimuaga mama yake kuwa anatoka kidogo na kwenda kushughulikia cheti cha kuzaliwa cha mtoto wake ambapo aliambiwa kuwa kitatoka baada ya wiki moja.
Yani wakati huo hata aliacha kufatilia mambo ya mkataba wa benki kabisa kwani hakutaka kuwa karibu na mzee Jimmy, ingawa mzee huyo alimtumia ujumbe mara kwa mara kuwa aende benki wakamalizie hatua za mkataba ila Erica hakutaka tena hata alipopigiwa na Yule meneja napo hakutaka kabisa maana alijiona anatosha kwa aliyoyapitia.
Ilimradi Erick kajitolea kumtunza mtoto ilikuwa inamtosha kwakweli.
Siku aliyoenda kufata cheti cha mtoto wake, wakati anarudi alikutana na Yule mama ambaye walikutana dukani akamsaidia kuchukua maji, Yule mama alisimamisha gari yake na kumuita,
“Erica”
Erica alienda kwa Yule mama ambaye alijawa na tabasamu tu, akamsalimia kisha Yule mama akasema,
“Yani nilipoteza namba yako, moyo ukaniuma kweli ila Mungu ni mwema nimekuona tena, ngoja nikuulize swali, una kazi? Yani unafanya kazi?”
“Hapana, nipo nyumbani tu”
“Umesoma mpaka wapi?”
“Chuo, nina shahada ya biashara”
“Jamani, ndio huna kazi kweli binti mzuri kama wewe dah! Sikia, chukua hii kadi yangu ya biashara, wiki ijayo njoo ofisini kwangu na vyeti vyako”
“Asante”
Erica alimshukuru sana Yule mama kwani aliona kama ni kitu cha ajabu ametunukiwa kwa muda huo, kisha akaagana nae na kurudi nyumbani.
Alifika na kujisemea,
“Kweli Mungu ana njia zake za kubariki, nadhani Erick ni baraka tosha katika maisha yangu. Nikijaribu kuunganisha matukio naona wazi kuwa Erick ni baraka tosha kwangu, kwanza Erick alinipigia simu nikawa na kimuhemuhe cha kumpigia na kuamua nikanunue vocha, mama akaamua aniagize na soda ndipo nikakutana na Yule mama mwenye roho nzuri. Haya Erick kasema nifatilie cheti cha kuzaliwa cha mtoto, natoka kukifata nakutana na huyu mama na ananiahidi kazi, wow nadhani Erick ni baraka kwangu”
Alitabasamu maana ilikuwa ni furaha kwake.
Alirudi kwao, kwa kipindi hiko mwanae alikuwa ameanza utundu wa kimya kimya kiasi kwamba alikuwa akirudi tu basi mwanae alichukua mkoba na kuangalia kuwa mama yake kamletea zawadi gani, bibi yake alikuwa akicheka sana na kusema,
“Yani Angel ananikumbusha kipindi kile wakati wewe mdogo, mtu akikuangalia anakuona mtoto mpole kumbe una utundu wa kimya kimya ninaoujua mimi tu, sasa mtu hawezi kudhania kama Angel anaweza fungua mkoba na kupekua ila ona hapo. Hahaha mpaka apate anachotaka”
Kwahiyo Erica alikuwa akinunua matunda mara nyingi ambapo akifika tu anampa mwanae ili mwanae asimpekue mkoba.
Alichukua mkoba wake na kuingia chumbani ambapo aliweka vizuri CV yake na vyeti vyake, aliweka kwenye bahasha nzuri kwaajili ya kuvipeleka kesho kwa Yule mama.
Alipomaliza alimpigia simu Erick kuwa kashapata cheti cha mtoto na picha anazo, basi Erick akamuelekeza mahali pa kupeleka ili mtoto atengenezewe kadi ya bima ya afya, kwahiyo Erica aliona ni vyema afanye vyote kwa pamoja.
Siku hiyo aliondoka asubuhi kwao na kuanza kwenda kwenye ofisi ya Yule mama akifata maelekezo ya kwenye ile kadi aliyopewa na kufika, kisha akaenda mapokezi na kumuulizia,
“Una miadi nae?”
“Ndio”
“Ngoja nimpigie simu, nimwambie unaitwa nani?”
“Erica”
Basi Yule wa mapokezi akapiga simu, Yule mama alipokea ila alionyesha alikuwa na kikao na kuomba kuongea na Erica, ambapo Yule wa mapokezi akamkabidhi simu Erica kisha Yule mama akamwambia aache nakala ya vyeti vyake kwa Yule mtu wa mapokezi, Erica alimshukuru kisha wakakata ile simu na kumuachia Yule wa mapokezi bahasha ya vyeti vyake halafu yeye kuondoka.
Moja kwa moja alienda mahali ambako Erick alimuelekeza kuwa apelike vile vitu kwaajili ya mtoto kupata kadi ya bima ya afya.
Basi alifika kama alivyoelekezwa na moja kwa moja alienda mapokezi na kukutana na mdada ambaye alimsalimia kisha kumuachia vile vitu vya mtoto ambavyo vilikuwa kwenye bahasha iliyoandikwa jina la Erick nje maana ndio maelekezo aliyopewa na Erick,
“Aaaah sawa, basi kikiwa tayari tutakupigia simu uju uchukue”
“Sawa nashukuru”
Basi Erica akaondoka zake, wakati yupo kwenye stendi ya daladala, kuna mdada alifika mbele yake na huyo mdada alionyesha kumfahamu Erica ila Erica alishamsahau, ikabidi Yule mdada aanze kumkumbusha,
“Unakumbuka siku ile umefika kwa Bahati nikakupeleka alipokuwa anaoa Yule Nasma hadi ukaanguka, unakumbuka”
Erica alimtazama huyu mdada na kumjibu,
“Nakumbuka ndio”
“Vipi, uliweza kuacha maisha yaendelee? Mapenzi ndivyo yalivyo mdogo wangu, muda mwingine unaumia hata usipotarajia”
“Nishasahau mie”
“Basi Yule Nasma saivi ni mjamzito, yani Bahati hajachelewesha yupo vizuri huyo”
Erica aliona huyu nae yupo kumchanganya tu wakati yeye ameshaanza kusahau mambo hayo, aliamua kumuaga na kuondoka zake kuelekea kwao, kwani hakutaka kuumiuza kichwa kabisa kwa muda huo kumfikiria tena bahati aliyemshuhudia akifunga ndoa, kwahiyo alipanda basin a kurudi kwao ambapo alimkuta mama yake kama kawaida ila leo mama yake alimwambia,
“Mwenendo wako kwa hivi karibuni umenifurhisha sana, ukienda mahali unawahi kurudi, sijasikia ujinga wa kuleta marafiki wa ajabu ajabu kama Dora. Mwanangu bora umeachana na aina ile ya marafiki, narudia tena, mimi ndio rafiki yako wa kweli. Kama una shida yoyote au una jambo lolote usisite kuniambia mimi rafiki yako wa ukweli”
“Sawa mama”
Basi akafurahi sana maana kwa siku hizo alikuwa akiongea kwa upendo tu na mama yake.