Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #381
SEHEMU YA 296
Walifika na kushuka kisha Moses akawaaga na kuondoka zake, Erica aliingia ndani na mwanae na kumkuta mama yake ambapo alianza kumuonyesha zile nguo alizopewa Angel.
“Kweli siku hizi kuna rah asana, yani mtoto anapata nguo za bure tu. Ndiomana umemshikilia huyo mwanaume, aje nyumbani sasa”
Erica akacheka tu kisha akamuuliza mama yake kuhusu dada yake Bite kuwa anaendeleaje,
“Anaendelea vizuri tu, ila unajua shemeji yako ni aibu tele imemshika hataki kurudi kwake”
“Kutokutaka kurudi sio tatizo, ila tatizo ni kuwa analala wapi? Dada aende kazini kwa shemeji jumatatu, na amtishie jambo moja tu kuwa ataondoka na amtishie kuwa akiulizwa atasema ukweli wa kilichomfanya aondoke, mama shemeji atarudi tu nyumbani sidhani kama atataka aumbuke mara mbili”
Mama yake alikubali swala hilo maana aliona ni jambo jema sana, kisha Erica alienda kufanya kazi zake zingine na kumpa mwanae chakula.
Muda wa kulala ulipofika, Erica alienda kulala na mwanae ila kabla hajalala alipigiwa simu na Erick,
“Erica, si nilikwambia uwe unanieleza kila kitu kinachotokea kwako?”
“Ila hakuna kilichotokea”
“Mbona nimesikia leo hadi ulitaka kuondoka dukani sijui sababu ya Tumaini, kwani tatizo ni nini?”
“Hamna tatizo ila sijui ni kwanini hadi leo dada yako hanipendi”
“Erica swala hilo lisikupe shida hata kidogo, yule ni dada yangu na wewe ni mpenzi wangu, nyie wawili mnacheza nafasi tofauti katika maisha yangu sidhani kama kuna sababu ya nyie kuchukiana. Erica, mimi ndio nakupenda wewe, si lazima dada yangu akupende, cha muhimu ni mimi kukupenda wewe. Halafu kingine lile ni duka langu, sio duka la Tumaini lile, naomba uwe huru kabisa unapoenda pale, sawa”
“Sawa nimekuelewa”
“Sitaki tena uwe na simanzi kipenzi changu, nakupenda Erica, sitanii namaanisha nisemayo, nakupenda”
“Asante, nakupenda sana”
Basi akaagana nae na kulala ila alikuwa na furaha sana kwa siku hizo Erica, alihisi kama kaibeba dunia.
Kama kawaida ya siku hii mama yake alijiandaa na kwenda kwenye ibada na kumuacha Erica akiwa mwenyewe, ila leo alipigiwa simu na dada yake Mage na kumsalimia,
“Erica, mdogo wangu kuna habari nimepata nahisi ni ya kweli ila ulinificha kwasababu zako binafsi”
“Habari gani dada?”
“Nasikia umewahi kulala na Derick”
Erica alishtuka kuona ile habari imefika kwa dada yake, akamuuliza kwa uoga,
“Nani amekwambia maneno hayo dada?”
“Dunia haina siri Erica, usidhani ukificha wewe kila mtu ataficha tena habari yote nimeipata”
“Si kweli dada”
“Usitake kupinga wala kukataa Erica, ni Derick mwenyewe kanieleza mambo haya. Erica nilikuuliza kwa kukupenda kabisa maana hiyo ni laana ambayo wewe na Derick mmeifanya”
“Ila Dada, sijui niseme vipi naomba nisamehewe sikujua kama Derick ni ndugu yangu hata hivyo alininywesha pombe. Naomba hii habari isifike kwa mama”
“Kwa mama labda uifikishe mwenyewe, sina huo mpango wa kufikisha habari hii kwa mama, ni aibu na fedheha kwakweli ila mimi kama dada natakiwa nisimamie swala hili maana ni laana kwenye ukoo”
“Sasa tutafanyaje dada?”
“Natakiwa nikawashirikishe kwanza wakina bamdogo na wao wataniambia cha kufanya ila lazima wewe na Derick muwepo, kwakweli mlifanya kitendo cha ajabu sana, ndugu jamani mmmh!”
“Sikujua dada”
“Basi ngojea nitakupigia simu nikishajua cha kufanya, ndiomana nilikuwa nakuuliza mapema kuwa kuna lolote mmefanya mkawa mananikatalia wakati mnajua fika mshaharibu”
Kisha Mage akakata simu, kwakweli Erica alichukia sana kwa Derick kutoa ile siri maana hakutaka ile siri ifichuke maana aliona inamuoinyesha yeye kama mtu mchafu sana wa kutembea hadi na kaka yake.
“Nakuchukia Derick, na wewe George nakuchukia maana ndio chanzo cha kufanya Derick na mimi tuwe karibu maana kunibaka kwako ndio nikapata msaada kwa Derick, jamani sijui hata nifiche wapi aibu hii, kama hadi wakina bamdogo wanaenda kuambiwa ni lazima mama nae atajua tu”
Kiukweli alikosa raha kabisa, hadi mama yake anarudi kanisani bado hakuwa na raha ila alijaribu kujigelesha kwenye macho ya mama yake asionekane kuwa na matatizo.
Walifika na kushuka kisha Moses akawaaga na kuondoka zake, Erica aliingia ndani na mwanae na kumkuta mama yake ambapo alianza kumuonyesha zile nguo alizopewa Angel.
“Kweli siku hizi kuna rah asana, yani mtoto anapata nguo za bure tu. Ndiomana umemshikilia huyo mwanaume, aje nyumbani sasa”
Erica akacheka tu kisha akamuuliza mama yake kuhusu dada yake Bite kuwa anaendeleaje,
“Anaendelea vizuri tu, ila unajua shemeji yako ni aibu tele imemshika hataki kurudi kwake”
“Kutokutaka kurudi sio tatizo, ila tatizo ni kuwa analala wapi? Dada aende kazini kwa shemeji jumatatu, na amtishie jambo moja tu kuwa ataondoka na amtishie kuwa akiulizwa atasema ukweli wa kilichomfanya aondoke, mama shemeji atarudi tu nyumbani sidhani kama atataka aumbuke mara mbili”
Mama yake alikubali swala hilo maana aliona ni jambo jema sana, kisha Erica alienda kufanya kazi zake zingine na kumpa mwanae chakula.
Muda wa kulala ulipofika, Erica alienda kulala na mwanae ila kabla hajalala alipigiwa simu na Erick,
“Erica, si nilikwambia uwe unanieleza kila kitu kinachotokea kwako?”
“Ila hakuna kilichotokea”
“Mbona nimesikia leo hadi ulitaka kuondoka dukani sijui sababu ya Tumaini, kwani tatizo ni nini?”
“Hamna tatizo ila sijui ni kwanini hadi leo dada yako hanipendi”
“Erica swala hilo lisikupe shida hata kidogo, yule ni dada yangu na wewe ni mpenzi wangu, nyie wawili mnacheza nafasi tofauti katika maisha yangu sidhani kama kuna sababu ya nyie kuchukiana. Erica, mimi ndio nakupenda wewe, si lazima dada yangu akupende, cha muhimu ni mimi kukupenda wewe. Halafu kingine lile ni duka langu, sio duka la Tumaini lile, naomba uwe huru kabisa unapoenda pale, sawa”
“Sawa nimekuelewa”
“Sitaki tena uwe na simanzi kipenzi changu, nakupenda Erica, sitanii namaanisha nisemayo, nakupenda”
“Asante, nakupenda sana”
Basi akaagana nae na kulala ila alikuwa na furaha sana kwa siku hizo Erica, alihisi kama kaibeba dunia.
Kama kawaida ya siku hii mama yake alijiandaa na kwenda kwenye ibada na kumuacha Erica akiwa mwenyewe, ila leo alipigiwa simu na dada yake Mage na kumsalimia,
“Erica, mdogo wangu kuna habari nimepata nahisi ni ya kweli ila ulinificha kwasababu zako binafsi”
“Habari gani dada?”
“Nasikia umewahi kulala na Derick”
Erica alishtuka kuona ile habari imefika kwa dada yake, akamuuliza kwa uoga,
“Nani amekwambia maneno hayo dada?”
“Dunia haina siri Erica, usidhani ukificha wewe kila mtu ataficha tena habari yote nimeipata”
“Si kweli dada”
“Usitake kupinga wala kukataa Erica, ni Derick mwenyewe kanieleza mambo haya. Erica nilikuuliza kwa kukupenda kabisa maana hiyo ni laana ambayo wewe na Derick mmeifanya”
“Ila Dada, sijui niseme vipi naomba nisamehewe sikujua kama Derick ni ndugu yangu hata hivyo alininywesha pombe. Naomba hii habari isifike kwa mama”
“Kwa mama labda uifikishe mwenyewe, sina huo mpango wa kufikisha habari hii kwa mama, ni aibu na fedheha kwakweli ila mimi kama dada natakiwa nisimamie swala hili maana ni laana kwenye ukoo”
“Sasa tutafanyaje dada?”
“Natakiwa nikawashirikishe kwanza wakina bamdogo na wao wataniambia cha kufanya ila lazima wewe na Derick muwepo, kwakweli mlifanya kitendo cha ajabu sana, ndugu jamani mmmh!”
“Sikujua dada”
“Basi ngojea nitakupigia simu nikishajua cha kufanya, ndiomana nilikuwa nakuuliza mapema kuwa kuna lolote mmefanya mkawa mananikatalia wakati mnajua fika mshaharibu”
Kisha Mage akakata simu, kwakweli Erica alichukia sana kwa Derick kutoa ile siri maana hakutaka ile siri ifichuke maana aliona inamuoinyesha yeye kama mtu mchafu sana wa kutembea hadi na kaka yake.
“Nakuchukia Derick, na wewe George nakuchukia maana ndio chanzo cha kufanya Derick na mimi tuwe karibu maana kunibaka kwako ndio nikapata msaada kwa Derick, jamani sijui hata nifiche wapi aibu hii, kama hadi wakina bamdogo wanaenda kuambiwa ni lazima mama nae atajua tu”
Kiukweli alikosa raha kabisa, hadi mama yake anarudi kanisani bado hakuwa na raha ila alijaribu kujigelesha kwenye macho ya mama yake asionekane kuwa na matatizo.