Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #401
SEHEMU YA 312
Kisha Erica aliinuka na kwenda chumbani kwake, na giza lilishaanza kuingia, akaona simu yake inaita kuangalia akakuta Erick anapiga, kwakweli akaogopa kupokea maana alikumbuka maneno yale aliyoambiwa kwenye ndoto na Yule mganga, ndipo akakumbuka hata ile leso ambayo ipo nusu kwahiyo alitoka tena ili kumueleza mama yake.
Akamwambia alivyozungumza na Fetty na jinsi alivyoenda kuangalia pochi yake na kukuta leso nusu,
“Mmmh mwanangu, hatujamaliza hili linazuka lingine jamani tutapona kweli?”
“Sijui mama”
“Hebu mpigie Yule mwanamaombi umueleze hayo na mimi ngoja niwapigie watumishi wengien niwaeleze maana sio kitu cha kawaida hiko”
Basi Erica alichukua simu yake na kumpigia Yule mwanamaombi, kisha baada ya salamu alimueleza Yule mganga alivyomtokea usiku na akamueleza jinsi alivyoongea na rafiki yake na jinsi alivyoona leso yake,
“Erica, kwanza tunatakiwa kumshukuru Mungu sana kwa hilo. Kwakweli Mungu wetu ni muaminifu sana, tulihitaji kujua ni kwanini bado anakufatilia? Ila Mungu katuonyesha kwa wazi kabisa kumbe Yule mganga ana kipande cha leso yako, sasa naomba niingie kwenye maombi ili nijue cha kufanya na hiyo leso. Na wewe uombe tafadhali”
“Sawa, na mimi naomba”
Erica alivyokata simu akamueleza mama yake aliyokuwa akiongea na Yule mwanamaombi,
“Hata mimi watumishiwamesema waombee kwanza swala hilo na kunitaka na mimi kuingia kwenye maombi. Njoo tuombe kwa pamoja mwanangu”
Basi Erica alisogea kwa mama yake na kushikana mikono kisha kuanza maombi ya kwa pamoja ambapo yalifanyika kwa muda kama wa nusu saa, kwakweli Erica alijihisi kuchoka maana hakuyaweza maombi ya vile ila ni mama yake tu ndio alikuwa akiomba.
Basi baada ya maombi wakati wametulia tulia, simu ya Erica iliita tena na alikuwa ni mwanamaombi anapiga, basi Erica alipokea na kuanza kuongea nae,
“Sasa Erica, chukua hicho kitambaa na mtoke nje kabisa ya nyumba yenu kimwagie mafuta ya taa na ukichome moto huku ukiendelea kuomba, maana huyo tayari ni adui kwako hafai”
Basi Erica alipokata simu alimfahamisha mama yake kisha walibeba kile kitambaa mpaka nje na kukitupa kisha kumwaga mafuta ya taa na kukichoma yani kilikuwa kinatoa harufi kama kuna damu inaungulia, hadi mama Erica akasema,
“Mmmmh mara nyingine tunakaa ndani kiajabu jamani, sasa kukaa na kitambaa kinachomwa kinakuna kama damu mmmh! Makubwa haya”
Walihakikisha kitambaa chote kimeungua kisha walirudi ndani na kujiandaa kwaajili ya kulala kwani ilikuwa ni usiku tayari, walifanya tu maombi ya kulala na kwenda kulala.
Kwakweli kwa siku ya leo Erica alilala tu kwani hakutaka hata kuongea na Erick kwenye simu kwani bado alikuwa na uoga nay ale maneno ya Yule mganga.
Kisha Erica aliinuka na kwenda chumbani kwake, na giza lilishaanza kuingia, akaona simu yake inaita kuangalia akakuta Erick anapiga, kwakweli akaogopa kupokea maana alikumbuka maneno yale aliyoambiwa kwenye ndoto na Yule mganga, ndipo akakumbuka hata ile leso ambayo ipo nusu kwahiyo alitoka tena ili kumueleza mama yake.
Akamwambia alivyozungumza na Fetty na jinsi alivyoenda kuangalia pochi yake na kukuta leso nusu,
“Mmmh mwanangu, hatujamaliza hili linazuka lingine jamani tutapona kweli?”
“Sijui mama”
“Hebu mpigie Yule mwanamaombi umueleze hayo na mimi ngoja niwapigie watumishi wengien niwaeleze maana sio kitu cha kawaida hiko”
Basi Erica alichukua simu yake na kumpigia Yule mwanamaombi, kisha baada ya salamu alimueleza Yule mganga alivyomtokea usiku na akamueleza jinsi alivyoongea na rafiki yake na jinsi alivyoona leso yake,
“Erica, kwanza tunatakiwa kumshukuru Mungu sana kwa hilo. Kwakweli Mungu wetu ni muaminifu sana, tulihitaji kujua ni kwanini bado anakufatilia? Ila Mungu katuonyesha kwa wazi kabisa kumbe Yule mganga ana kipande cha leso yako, sasa naomba niingie kwenye maombi ili nijue cha kufanya na hiyo leso. Na wewe uombe tafadhali”
“Sawa, na mimi naomba”
Erica alivyokata simu akamueleza mama yake aliyokuwa akiongea na Yule mwanamaombi,
“Hata mimi watumishiwamesema waombee kwanza swala hilo na kunitaka na mimi kuingia kwenye maombi. Njoo tuombe kwa pamoja mwanangu”
Basi Erica alisogea kwa mama yake na kushikana mikono kisha kuanza maombi ya kwa pamoja ambapo yalifanyika kwa muda kama wa nusu saa, kwakweli Erica alijihisi kuchoka maana hakuyaweza maombi ya vile ila ni mama yake tu ndio alikuwa akiomba.
Basi baada ya maombi wakati wametulia tulia, simu ya Erica iliita tena na alikuwa ni mwanamaombi anapiga, basi Erica alipokea na kuanza kuongea nae,
“Sasa Erica, chukua hicho kitambaa na mtoke nje kabisa ya nyumba yenu kimwagie mafuta ya taa na ukichome moto huku ukiendelea kuomba, maana huyo tayari ni adui kwako hafai”
Basi Erica alipokata simu alimfahamisha mama yake kisha walibeba kile kitambaa mpaka nje na kukitupa kisha kumwaga mafuta ya taa na kukichoma yani kilikuwa kinatoa harufi kama kuna damu inaungulia, hadi mama Erica akasema,
“Mmmmh mara nyingine tunakaa ndani kiajabu jamani, sasa kukaa na kitambaa kinachomwa kinakuna kama damu mmmh! Makubwa haya”
Walihakikisha kitambaa chote kimeungua kisha walirudi ndani na kujiandaa kwaajili ya kulala kwani ilikuwa ni usiku tayari, walifanya tu maombi ya kulala na kwenda kulala.
Kwakweli kwa siku ya leo Erica alilala tu kwani hakutaka hata kuongea na Erick kwenye simu kwani bado alikuwa na uoga nay ale maneno ya Yule mganga.