Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #21
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA SITA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA TANO: Naam barabara ya bagamoyo, mtaa wa tegeta, njia pnda ya kwasharifu, linaonekana gari moja jeusi aina ya ford ranger likiwa limesimama pembeni ya barabara hiyo, huku mtu mmoja, mwenye mwonekano wa miaka 40, akiwa amesimama ubavuni mwa gari ilo, huku uso wake, ukionekana kujawa na mashaka mengi, mara kwa mara alikuwa anatazama saa yake, na kisha kutazama upande wa mjini, ni wazi alikuwa anatarajia kuona mtu au gari likitokea upande huo…..
“baba Zamda, umesema Zamda analetwa, sasa mbona simwoni mwanangu” ilikuwa ni sauti ya kike toka ndani yagari, iliyoambatana na kilio cha chini chini, “mama Zam we tulia, ata mimi nina wasi wasi juu ya binti yetu, lakini bosco, amesema yule kijana alie mpigia simu, lazima atarudi na Zamda, ilimradi tu tumkabidhi fedha yake” alisema yule mzee ambae sasa tuna gundua kuwa ndie mzee Simba, yani baba yake Zamda, “kwakweli baba Zamda kama mtoto hatorudi ninaenda kukutolea taarifa kituo cha polisi, na kwenye vyombo vya habari, ilimradi wewe na wenzako wote mkamatwe na mwangu nimpate, nilikuambia achana na hiyo biashra ya dawa za kulevya, tafuta biashara nyingine, lakini wewe hukunisikia” aliendela kulalamika mwanamke alie kuwa ndani yagari.
Hapo Mzee Simba akaachia msonyo mrefu, “lakini hizi fedha ndizo tulizo, mtibia mama yako, na hizi ndizo zinazotufanya tuishi vizuri, halafu nani kakuambia unaweza kuacha ghafla hivyo, unazani wangeniacha hai wakina Songoro?” aliuliza bwana Simba, kwa sauti ya ukali kidogo, na hapo akasikia sauti ya kilio kikiongezeka toka ndani yagari, “sijuwi mwanangu wanamfanyaje huk jamani” hakika ilitia huruma na kuchukiza kwa wakati mmoja.
Lakini kabla hata mzee Simba ajaongea neno lolote, mara wakaliona gari aina BMW 7, likija na kusimama karibu kabisa na gari lake, kisha milango miliwi ya gari ikafunguliwa, hapo mzee Simba akamwona binti yake akiwa anatoka kwenye gari, huku amevikwa shuka kwa mtindo wa kuviligwa mwilini mwake, “mwanangu upo salama kweli” aliuliza mzee Simba, huku anamtazama binti yake kwa macho ya ukaguzi, na swali ilo ndilo lilo mshtua mke wake, ambae alichomoka ndani gari kwa speed ya haraka, usingesema kuwa ndie alikuwa amezimia masaa kadhaa yaliyopita, “jamani mwanangu, hawajakuumiza kweli” alisema mama Zamda huku anamkumbatia binti yao, huku wote wakilia kwa furaha, muda wote kijana wetu derva ambae bado atuja mfahamu kwa jina, akiwatazama kwa macho ya kuvutiwa na tukio lile, “hapana mama, hawajanifanya chochote, dereva aliwai kabla ajanifanya” alisema Zamda huku wote wawili, yani yeye na mama yake wanageuka kumtazama kijana huyu mwenye sura ya upole, ambae mara baada ya macho yao kukutana anatabasamu kidogo.
Hapo Mzee Simba nae akakumbuka anachotakiwa kufanya, hivyo ana fungua mlango wa nyuma wa gari ili, na kutoa begi, “kijana kuna zaidi ya million hamsini, ni za kwako, sina muda wakusubiri wacha nikimbie mji” alisema mzee Simba, huku anampatia begi dereva, ambae alilipokea na pasipo kuongea neno, akalifungua lile begi na, kuchukuwa bunda moja la noti za elfu kumi kumi, na kukagua, kisha akapapasa mabunda mengine, alafu akamtazama mzee Simba, “sikunyingine tukutane kwa yale yaliyomema, siyo kuuza mtoto kwa dawa za kulevya, nitakuwa wa kwanza kukuadhibu” alisema Dereva kisha akamtazama Zamda ambae bado alikuwa ameshikana na mama yake wakimtazama, “nawatakia safari nje, kaeni mbali na watu wale” alisema Dereva kisha akaingia kwenye gari na kuondoka zake, huku akimwacha mzee samba na familia yake wakiingia ndani yagari na kuondoka zao pia, wakati Dereva anageuza gari kurudi mjini, mzee simba alikuwa anaelekea upande wa bagamoyo.*******
Msako ulishika kasi ndani ya jiji la dar es salaam, polisi walizagaa jiji zima, na vitongoji vyake, wakilisaka gari jeusi aina ya BMW, ambayo waliyaona mengi sana, lakini siyo kama lile lililotajwa, na hata dereva hakuwa kama yule waliyoelekezwa, maana pengine wangekuta BMW 3 au 1, tena anaendesha mtu mzima, au kijana mnene au mfupi, pengine mweupe sana, au mweusi sana, au wakati mwingine wange mkuta anaendesha mwanamke.
Lakini msako huo wenye faida kwa askari wajeshi la polisi, haukukoma, uliendelea kushika kasi, huku raia wazurulaji na wachelewaji wa kurudi nyumbani, wakikumbana na dhahama ya polisi hao, ambao walijipatia fedha toka kwa wazurulaji, ambao walilazimika kutoa chochote, ili wasipelekwe mahabusu, ambako kutoka kwake ni gharama kubwa zaidi, wakati huo taarifa zikizidi kusambaa kwenye kamandi nyingine za mikoa ya kipolisi ambayo iliundwa kwa mtindo wa kanda, katika pande kuu nne, yani kaskazini, kusini, mashariki na magharibi, yani pande za temeke, mbezi ya kimara, upende wa ilala, na upande wa mwenge mpaka tegeta.
Taarifa hizo zilifanya askari wengi zaidi waigie barabarani, na kuendeleza msako, wa BMW jeusi, huku wakielezwa kwamba, dereva wa gari ilo ni mtu hatari sana, na askari wanapaswa kuwa makini sana watakapo kabiliana nae, huku akitajiwa kuwa mtu hatari.*******
Usiku huo huo linaonekana gari aina ya Toyota Wish, likiingia Kinyerezi mwisho, kutokea mbezi, kupitia malamba mawili, linaishana na polisi wengi njiani, na linapofika stendi ya kinyerezi, lina ingia upande wa kushoto, na kufwata barabara ya vumbi inayopita chini ya nguzo kuu za umeme, mpaka linapofika mtaa mpya wa njia panda, ambapo linaenda moja kwa moja kwenye lango la uzio mkubwa wa kuta, wenye vitu mbali mbali vya usalama, yani waya wa umeme, na camera za ulinzi.
Licha ya kuwa na vitu vya usalama kama hivyo lakini inashangaza kuona lango la uzio huu likiwa wazi, pasipo mlinzi wala mtu yoyote, na cha kushangaza zaidi ungeweza kuona jumba kubwa la kifahari, ambalo kwa majumba ya kifamilia kwa hapa dar es salaam, ningeweza kusema ni moja kati ya majumba machache yanayoweza kumilikiwa na watu bnafsi, lakini hapa kuwa na umeme wala kandiri, kwa maana hiyo, palikuwa na giza nene la kutisha.
Gari linaingia ndani kwa mwendo wa taratibu sana, dereva akionekana kuwa katika umakini wa hali ya juu, na kwenda kusimama mbele ya jumba hilo la kifahari, huku taa za gari lile likimulika magari jumba lile, ambalo alikuonyesha dalili ya kuwepo kwa watu ndani.
Pasipo kuzima gari wala taa, mlango wa dereva unafunguliwa, kisha anashuka mwanamke mmoja mrembo sana, alie kuwa anaongea na simu, mwenye urefu wa wastani umbo la kuvutia, lenye kila kitu ambacho wanaume wengi utamani kuona kwa mwanamke, pengine ata wanawanawake wenye kutamani kuwa navyo, yani ukiachia sura nzuri aliyokuwa nayo maschana huyu, alie valia suruali nyeusi ya kitambaa chepesi, na shati fupi jeupe, chini akimaliza kwa kiatu cha mikanda chenye unyayo msawazisho yani flat, lakini pia alikuwa na umbo moja matata sana, yani hips pana za wastani, makalio yenye ukubwa wa wastani, na tumbo dogo, lililobebwa na kiuno uzuri cha kufaria nguo yoyote ikaonekana, kifua kilicho beba maziwa yaliyo chaa vyema, na chuchu za kutoboa sidilia, na mbaya zaidi ukiachilia usowake wa duara la yai, mcho makubwa kiasi, pua ya kisomari, lips pana za kulambia vanilla, pia alikuwa na kijimwanya flani, kwenye meno yake ya juu, na tatizo jingine, alikuwa anajisi sima flani kwenye mashavu yake, ambayo kuviona kwake ni mpaka acheke au atabasamu, na wakati mwingine akiwa anakula,
Mschana huyu anatazama ile nyumba kubwa ya kifahari kwa mshangao, huku simu yake bado ikiwa sikioni, “samahani J nitakupigia baadae maana hapa nyumbani hata sipaelewi, yani geti lipo wazi hakuna umeme, wala dalili ya kuwepo mtu” alisema yule mwanamke na kukata simu, kisha akapekuwa namba nyingine ambayo ilikuwa imeandikwa baba, anaipiga lakini haipatikani, ana piga nyingine iliyoandikwa mama, nayo haipatikani, ana jaribu ya dada wakazi, nayo ikaita bila kupokelewa, geukia gari na kuinama kwaajili ya kuchukuwa kitu flani ndani, hapo ungweza kuona jinsi msambwanda wake wakuvutia ulivyoonekana kwa nyuma.
Yule mschana anashika koti moja jeupe la kidoctor lililokuwepo kwenye seat ya gari, na kuanza kulipekuwa kidogo, lakini niwazi alikosa anachokiitaji, anahamia kwenye mkebe wa dash board na kuanza kupekuwa, hapo tunaweza kuona vitu kadhaa, kikiwepo kitambulisho, cha kazi, chenye jina la dr Veronica James Carvine, anapekuwa kwenye ule mkebe na kutoka na tochi ndogo, anajaribu kwa kuiwasha, inatoa mwanga wa kuridhisha, anatoka nakuegesha mlango wagari, ambalo bado lilikuwa linaendelea kuunguruma, yeye akaanza kuelekea kwenye jumba kubwa tena kwa mwendo wa tahadhari. endelea kufwatilia mkasa huu wa #NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI, inayo kujia hapa hapa, jamii forums
SEHEMU YA SITA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA TANO: Naam barabara ya bagamoyo, mtaa wa tegeta, njia pnda ya kwasharifu, linaonekana gari moja jeusi aina ya ford ranger likiwa limesimama pembeni ya barabara hiyo, huku mtu mmoja, mwenye mwonekano wa miaka 40, akiwa amesimama ubavuni mwa gari ilo, huku uso wake, ukionekana kujawa na mashaka mengi, mara kwa mara alikuwa anatazama saa yake, na kisha kutazama upande wa mjini, ni wazi alikuwa anatarajia kuona mtu au gari likitokea upande huo…..
“baba Zamda, umesema Zamda analetwa, sasa mbona simwoni mwanangu” ilikuwa ni sauti ya kike toka ndani yagari, iliyoambatana na kilio cha chini chini, “mama Zam we tulia, ata mimi nina wasi wasi juu ya binti yetu, lakini bosco, amesema yule kijana alie mpigia simu, lazima atarudi na Zamda, ilimradi tu tumkabidhi fedha yake” alisema yule mzee ambae sasa tuna gundua kuwa ndie mzee Simba, yani baba yake Zamda, “kwakweli baba Zamda kama mtoto hatorudi ninaenda kukutolea taarifa kituo cha polisi, na kwenye vyombo vya habari, ilimradi wewe na wenzako wote mkamatwe na mwangu nimpate, nilikuambia achana na hiyo biashra ya dawa za kulevya, tafuta biashara nyingine, lakini wewe hukunisikia” aliendela kulalamika mwanamke alie kuwa ndani yagari.
Hapo Mzee Simba akaachia msonyo mrefu, “lakini hizi fedha ndizo tulizo, mtibia mama yako, na hizi ndizo zinazotufanya tuishi vizuri, halafu nani kakuambia unaweza kuacha ghafla hivyo, unazani wangeniacha hai wakina Songoro?” aliuliza bwana Simba, kwa sauti ya ukali kidogo, na hapo akasikia sauti ya kilio kikiongezeka toka ndani yagari, “sijuwi mwanangu wanamfanyaje huk jamani” hakika ilitia huruma na kuchukiza kwa wakati mmoja.
Lakini kabla hata mzee Simba ajaongea neno lolote, mara wakaliona gari aina BMW 7, likija na kusimama karibu kabisa na gari lake, kisha milango miliwi ya gari ikafunguliwa, hapo mzee Simba akamwona binti yake akiwa anatoka kwenye gari, huku amevikwa shuka kwa mtindo wa kuviligwa mwilini mwake, “mwanangu upo salama kweli” aliuliza mzee Simba, huku anamtazama binti yake kwa macho ya ukaguzi, na swali ilo ndilo lilo mshtua mke wake, ambae alichomoka ndani gari kwa speed ya haraka, usingesema kuwa ndie alikuwa amezimia masaa kadhaa yaliyopita, “jamani mwanangu, hawajakuumiza kweli” alisema mama Zamda huku anamkumbatia binti yao, huku wote wakilia kwa furaha, muda wote kijana wetu derva ambae bado atuja mfahamu kwa jina, akiwatazama kwa macho ya kuvutiwa na tukio lile, “hapana mama, hawajanifanya chochote, dereva aliwai kabla ajanifanya” alisema Zamda huku wote wawili, yani yeye na mama yake wanageuka kumtazama kijana huyu mwenye sura ya upole, ambae mara baada ya macho yao kukutana anatabasamu kidogo.
Hapo Mzee Simba nae akakumbuka anachotakiwa kufanya, hivyo ana fungua mlango wa nyuma wa gari ili, na kutoa begi, “kijana kuna zaidi ya million hamsini, ni za kwako, sina muda wakusubiri wacha nikimbie mji” alisema mzee Simba, huku anampatia begi dereva, ambae alilipokea na pasipo kuongea neno, akalifungua lile begi na, kuchukuwa bunda moja la noti za elfu kumi kumi, na kukagua, kisha akapapasa mabunda mengine, alafu akamtazama mzee Simba, “sikunyingine tukutane kwa yale yaliyomema, siyo kuuza mtoto kwa dawa za kulevya, nitakuwa wa kwanza kukuadhibu” alisema Dereva kisha akamtazama Zamda ambae bado alikuwa ameshikana na mama yake wakimtazama, “nawatakia safari nje, kaeni mbali na watu wale” alisema Dereva kisha akaingia kwenye gari na kuondoka zake, huku akimwacha mzee samba na familia yake wakiingia ndani yagari na kuondoka zao pia, wakati Dereva anageuza gari kurudi mjini, mzee simba alikuwa anaelekea upande wa bagamoyo.*******
Msako ulishika kasi ndani ya jiji la dar es salaam, polisi walizagaa jiji zima, na vitongoji vyake, wakilisaka gari jeusi aina ya BMW, ambayo waliyaona mengi sana, lakini siyo kama lile lililotajwa, na hata dereva hakuwa kama yule waliyoelekezwa, maana pengine wangekuta BMW 3 au 1, tena anaendesha mtu mzima, au kijana mnene au mfupi, pengine mweupe sana, au mweusi sana, au wakati mwingine wange mkuta anaendesha mwanamke.
Lakini msako huo wenye faida kwa askari wajeshi la polisi, haukukoma, uliendelea kushika kasi, huku raia wazurulaji na wachelewaji wa kurudi nyumbani, wakikumbana na dhahama ya polisi hao, ambao walijipatia fedha toka kwa wazurulaji, ambao walilazimika kutoa chochote, ili wasipelekwe mahabusu, ambako kutoka kwake ni gharama kubwa zaidi, wakati huo taarifa zikizidi kusambaa kwenye kamandi nyingine za mikoa ya kipolisi ambayo iliundwa kwa mtindo wa kanda, katika pande kuu nne, yani kaskazini, kusini, mashariki na magharibi, yani pande za temeke, mbezi ya kimara, upende wa ilala, na upande wa mwenge mpaka tegeta.
Taarifa hizo zilifanya askari wengi zaidi waigie barabarani, na kuendeleza msako, wa BMW jeusi, huku wakielezwa kwamba, dereva wa gari ilo ni mtu hatari sana, na askari wanapaswa kuwa makini sana watakapo kabiliana nae, huku akitajiwa kuwa mtu hatari.*******
Usiku huo huo linaonekana gari aina ya Toyota Wish, likiingia Kinyerezi mwisho, kutokea mbezi, kupitia malamba mawili, linaishana na polisi wengi njiani, na linapofika stendi ya kinyerezi, lina ingia upande wa kushoto, na kufwata barabara ya vumbi inayopita chini ya nguzo kuu za umeme, mpaka linapofika mtaa mpya wa njia panda, ambapo linaenda moja kwa moja kwenye lango la uzio mkubwa wa kuta, wenye vitu mbali mbali vya usalama, yani waya wa umeme, na camera za ulinzi.
Licha ya kuwa na vitu vya usalama kama hivyo lakini inashangaza kuona lango la uzio huu likiwa wazi, pasipo mlinzi wala mtu yoyote, na cha kushangaza zaidi ungeweza kuona jumba kubwa la kifahari, ambalo kwa majumba ya kifamilia kwa hapa dar es salaam, ningeweza kusema ni moja kati ya majumba machache yanayoweza kumilikiwa na watu bnafsi, lakini hapa kuwa na umeme wala kandiri, kwa maana hiyo, palikuwa na giza nene la kutisha.
Gari linaingia ndani kwa mwendo wa taratibu sana, dereva akionekana kuwa katika umakini wa hali ya juu, na kwenda kusimama mbele ya jumba hilo la kifahari, huku taa za gari lile likimulika magari jumba lile, ambalo alikuonyesha dalili ya kuwepo kwa watu ndani.
Pasipo kuzima gari wala taa, mlango wa dereva unafunguliwa, kisha anashuka mwanamke mmoja mrembo sana, alie kuwa anaongea na simu, mwenye urefu wa wastani umbo la kuvutia, lenye kila kitu ambacho wanaume wengi utamani kuona kwa mwanamke, pengine ata wanawanawake wenye kutamani kuwa navyo, yani ukiachia sura nzuri aliyokuwa nayo maschana huyu, alie valia suruali nyeusi ya kitambaa chepesi, na shati fupi jeupe, chini akimaliza kwa kiatu cha mikanda chenye unyayo msawazisho yani flat, lakini pia alikuwa na umbo moja matata sana, yani hips pana za wastani, makalio yenye ukubwa wa wastani, na tumbo dogo, lililobebwa na kiuno uzuri cha kufaria nguo yoyote ikaonekana, kifua kilicho beba maziwa yaliyo chaa vyema, na chuchu za kutoboa sidilia, na mbaya zaidi ukiachilia usowake wa duara la yai, mcho makubwa kiasi, pua ya kisomari, lips pana za kulambia vanilla, pia alikuwa na kijimwanya flani, kwenye meno yake ya juu, na tatizo jingine, alikuwa anajisi sima flani kwenye mashavu yake, ambayo kuviona kwake ni mpaka acheke au atabasamu, na wakati mwingine akiwa anakula,
Mschana huyu anatazama ile nyumba kubwa ya kifahari kwa mshangao, huku simu yake bado ikiwa sikioni, “samahani J nitakupigia baadae maana hapa nyumbani hata sipaelewi, yani geti lipo wazi hakuna umeme, wala dalili ya kuwepo mtu” alisema yule mwanamke na kukata simu, kisha akapekuwa namba nyingine ambayo ilikuwa imeandikwa baba, anaipiga lakini haipatikani, ana piga nyingine iliyoandikwa mama, nayo haipatikani, ana jaribu ya dada wakazi, nayo ikaita bila kupokelewa, geukia gari na kuinama kwaajili ya kuchukuwa kitu flani ndani, hapo ungweza kuona jinsi msambwanda wake wakuvutia ulivyoonekana kwa nyuma.
Yule mschana anashika koti moja jeupe la kidoctor lililokuwepo kwenye seat ya gari, na kuanza kulipekuwa kidogo, lakini niwazi alikosa anachokiitaji, anahamia kwenye mkebe wa dash board na kuanza kupekuwa, hapo tunaweza kuona vitu kadhaa, kikiwepo kitambulisho, cha kazi, chenye jina la dr Veronica James Carvine, anapekuwa kwenye ule mkebe na kutoka na tochi ndogo, anajaribu kwa kuiwasha, inatoa mwanga wa kuridhisha, anatoka nakuegesha mlango wagari, ambalo bado lilikuwa linaendelea kuunguruma, yeye akaanza kuelekea kwenye jumba kubwa tena kwa mwendo wa tahadhari. endelea kufwatilia mkasa huu wa #NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI, inayo kujia hapa hapa, jamii forums