Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 1,479
- 3,229
- Thread starter
- #41
MA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA KUMI NA SITA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA KUMI NA TANO: Mama Frank akiwa na tochi mkononi, akaingia ndani ya kiji mlango kile, kwa kutanguliza miguu, ambapo miguu yake iligusa ngazi, na baada ya hatua mbili, akakanyaga aridhi, “mpokee huyo” alisema bwana Frank, huku anampatia mtoto Deusi, ambae muda wote alikuwa anatazama kila kilichokuwa kinatokea usiku ule, hakika ilikuwa jambo geni na la kutisha sana kwake, lakini uwezi kuamini ujasiri wa mtoto huyu, ambae akuonyesha uoga wala wasi wasi, uso macho yake yakiwa makavu kabisa, pasipo dalili ya machozi wala kilio. …..ENDELEA…..
Baada kuhakikisha kuwa, tayari familia yake imeingia ndani ya shimo hilo, hapo bwana Frank akachukuwa, panga lake na ile tochi, aka ingia ndani ya lile shimo, “pumbavu jamaa wametuzidi akili” ilisikika sauti, toka upande wajikoni kabla bwana Frank ajafunga kile kimlango taratibu na kwa umakini mkubwa sana, “haraka sana watu wasambae mji mzima, askari wakae kwenye barabara zote, kabla hajavuka na kutoka nje ya jiji, kumbuka mtu huyu hatakiwi kufika asubuhi akiwa anapumua” ilisikika kwa mbali sauti, hiyo toka upande wa jikoni, Frank hakujari tena sauti hizo, zaidi aliiongoza familia yake, mle ndani handaki lenye upanda hafifu, na hewa nzito.********
Naam askari walionekana wametapakaa ndani ya jiji la TT, ambalo sasa hakukuwa na raia wa kawaida alie kuwa anazunguka, kutoka na mvua kali iliyokuwa inanyesha kwa nguvu na kuogofya, pengine ungeona gari moja moja likikatikiza kwa mwendo wa taratibu, kutokana na mvua nyingi iliyokuwa inanyesha, na kusababisha ukungu mwingi sana.
Bwana Frank Nyati na familia yake waliibuka mita kama hamsini toka kwenye nyumba yake, usawa wa kichaka cha mauwa kilicho pandwa kama fensi ya eneo lile, la nyumba ya bwana Frank, ambae yeye alikuwa ndie wa kwanza kuibuka, na kuangalia pande zote, kujiridhisha, kama ilikuwa ni sehemu salama, kwa yeye na familia yake kutoka shimoni, lakini wakati anatazama eneo lile, upande wa nyumbani kwake, akaona miili ya watu kadhaa ikiwa imelala eneo la mbele la nyumba yake, ikiwa ni matokeo ya Uzi gan, “sidhani kama kuna cha kusubiri hapa, cha msingi hakikisheni huyu mpuuzi anapatikana na muna muuwa yeye na familia yake yote” wakati huo huo, Frank akasikia sauti toka upande wa barabarani.
Alipo tazama upande huo, kwa tabu sana, akaweza kuona watu kadhaa waliosimama pembeni ya magari binafsi aina ya land rover mia na kumi, yanayofanana na magari yanayotumiwa na jeshi lao, jeshi la nchi hii ya #mbogo_land, waliozuiwa na vichaka vile vya maua, hivyo Frank akatoka na kutambaa usawa wa maua yale mpaka alipo pata sehemu nzuri ya kuwaona watu hao, ambao sasa walikuwa wananyeshewa na mvua, “vipi kuhusu miili ya wenzetu?” aliuliza mmoja kati ya watu wale, aliesimama na mwenzie mmoja alie valia koti refu la mvua, wakiwa ubavuni mwa moja kati ya magari yale matatu, nawasiliana na boss yeye atajuwa la kufanya, nyie wahini mkamsake huyu mpuuzi” alisema yule jamaa mwenye kuvalia koti refu, ambae sauti yake haikuwa ngeni masikioni mwa Frank.
Baada ya hapo Frank akawaona watu wale wenye kuvalia nguo nyeusi, wakiingia kwenye magari, mawili na kuondoka zao, huku wakimwacha yule mwenye kuvalia koti ra mvua, akiwa pamoja na derea wa gari moja lililobakia, Frank alimwona yule jamaa mwenye sauti anayo ifananisha, mtu ambae ni wazi kabisa kuwa ndie aliekuwa mkubwa wao pale walipokuwepo, akitembea kuja upande alipokuwa yeye, hapo Frank anajiweka sawa na panga lake mkononi, tayari kwa lolote.
Frank, anamkazia macho mtu yule kwa lengo la kumtambua, mpaka anapomwona anasimama mita chache, pembeni ya barabara, mita kama sita toka kwenye kile kichaka alichokuwepo yeye, kisha anafungua zip ya suruali yake na kutoa kifaa chake cha kukojolea, kisha anaanza kuumwaga mkojo, Frank hajari kuhusu kifaa hicho, ambacho hata yeye anacho pia, yeye anatazama uso wa jamaa huyu, ambae kiukweli uso wake una gubikwa na giza, na kushindwa kumtambua.
Lakini haikuwa hivyo muda wote, maana baada ya kusubiri kujitahidi kumtambua mtu yule, na kushindwa, Frank akaona kuwa anaweza kumkabili peke yake yule jamaa kwa kutumia upanga wake, maana mpaka muda yule, jamaa alikuwa pake yake, yani mbali na gari, ambalo kulikuwa na dereva peke yake.
Sasa basi, Frank hakumsubiri jamaa amalize kumwaga haja ndogo, aka hesabu “moja… mbili… tat..” kabla haja maliza tatu, mara ghafla mwanga mkali wa gari uka angaza eneo lile, likitokea mjini, na kumfanya jamaa huyu ageuke kulitazama gari lile, Frank akabonyea zaidi kukwepa mwanga, na kuelekeza macho kule alikokuwepo yule, jamaa ambae bila shaka, alikuwa analitarajia gari lile.
Maana yule jamaa alimaliza kukojoa na kukugeuka tena, kulitazama lile gari, ambalo lilikuwa limesha sogea na kupunguza mwendo, huku mwanga wagari lile dogo la kifahari, ukimuangazia usoni, kamanda huyu, alievalia koti kubwa jeusi la mvua, na kwa msaada wa mwanga huo ndipo Frank alipo pata nafasi ya kumtambua mtu huyu, utambuzi ambao ulimstua na kumshangaza bwana Frank, ambae alijikuta anatoa macho ya mshangao wa kutokuamini macho yake.
Huyu alikuwa ni Canal Erasto Kadumya, afisa mtoro wa jeshi, anae kiongoza kikundi cha wahasi wa UMD, ambacho sasa mamluki wake wanasakwa kwa udi na uvumba ndani ya serikali, sasa inakuwaje anamwona kati ya watu wanao msaka yeye, kwa tuhuma za uhaini, wakati kiongozi wa zoezi hili ndie muasi mkubwa sana, anae tafutwa usiku na mchana na jeshi la serikali, ambae sasa alikuwa analisogelea gari lililokuwa limesimama, na mlango wa upande wa dereva ukafunguliwa.
Ukweli ungeweza kusema kuwa, kumwona Erasto Kadumya, akishiriki operation hii ya kusaka wa saliti, kuwa ndio ulikuwa mshangao mkubwa sana, kwa bwana Frank, lakini hapana, sikuwa hivyo, ukweli ni kwamba, mshangao mkubwa ulikuwa ni pale, alipomwona mtu alieshuka toka garini, mtu mfupi kiasi, alie valia koti refu la mvua, kama la Bwana Kadumya, “mawazo yangu yalikuwa sawa, huyu mpuuzi anajaribu kuiangusha serikali” alinong’ona, Frank huku anawatazama wawili wale, walio salimia kwa salamu za kijeshi.
Huyu alikuwa ni Major Chitopelah, mkuu wa operation ya kuwasaka wahasi ndani ya serikali, yani amempumbaza mfalme, huku anaendelea kumpunguzia nguvu ya watu ambao wengemsaidia kuzuwia mapinduzi” alijisemea Frank, huku anaendelea kuwatazama wawili wale, “Erasto kumbuka uzembe hautakiwi kabisa, katika swala la Frank, maana ni mtu hatari sana” alisikika Chitopela, ambae kijeshi alikuwa na cheo kidogo kuliko Kadumya, lakini pale alionekana kuwa ndie mwenye madaraka makubwa zaidi ya Kadumya, “hakika afande, wala usiwe na wasi wasi, nitamnasa ndani ya usiku huu, na nitakuonyesha mwili wake” alisema Kadumya kwa kujiamini.
Baada ya maongezi mafupi, Frank aliwaona wawili wale wakimaliza maongezi yao, na bwana Dickson Chitopelah, akifungua tena mlango wa gari lake na kutoa bagi dogo, ambalo alimpatia Kadumya, “hii ni motisha kwa vijana, zidi kuwapa moyo kuwa, endapo tutafanikiwa kuichukuwa nchi, watakuwa na maisha mazuri sana” alisisitiza Chitopelah, kabla awajaagana na kila mmoja kuondoka na gari lake.
Hii ilimpatia picha pana sana bwana Frank, ambae aligundua kuwa uasi ulikuwa katika vitengo nyeti vya serikali, ikiwa na kiengo cha siri cha mawakala wa usalama wa taifa ili tajiri, linalo tawaliwa katika mfumo wa kifalme, na kwa haraka Frank alijuwa fika kuwa singweza kubadilisha hisia za king Eugen juu yake, na kumwaminisha kuwa Chopelah, alikuwa ndie muasi na msaliti.
Hapo ndipo bwana Frank alipochukuwa familia yake na kuitorosha kuelekea nje ya nchi, na njia aliyo itumia, ilikuwa ni njia ngumu sana, njia ambayo, katika hali ya kawaida, asinge kubali kuipitisha familia yake, maana ukiachilia, hatari ya kuwepo kwa waasi, pia msitu huu, ulikuwa unaongoza kwa wanyama hatarishi, kama vile simba, chui, na wegine wa jamii hiyo pasipo kusahau nyoka wakubwa, sana wakila aina, na wanyama wakubwa ambao siyo rafiki sana kwa binadamu, kama vile faru na tembo.
Mito mikubwa, ambayo ilikuwa inatiririsha maji kwa fujo, huku mvua na milipuko ya radi, ikiendelea kulindima, hakika iligopesha tochi zote zilisha zima, na sasa walitembea kwa kutegemea mwanga wa radi, sidhani kama kuna sehemu ambayo haikulowa katika miili yao, Deus na mama yake walikuwa wanatetemeka kwa baridi kali, kiasi cha meno kugongana, huku bwana Frank akifyeka vicha na magugu marefu, ndani ya madimbwi, ya maji, akitengeneza njia kwakutumia panga kali, mfano wa jambia, alilokuwa amelishika mkononi, mke wake akimfwaa nyuma, akiwa amembeba mtoto.
Ndani ya masaa matatu, tayari walisha vuka mpaka wa inua kisigino, wa kuelekea Tanzania, mpaka ambao, kila mtu huuchukulia kama mpaka mgumu sana kwa mtu kuupitia, kutokana na vikwanzo vya eneo hilo lenye milima na mabonde….…..#NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI, inayo kujia hapa hapa jamii forums
SEHEMU YA KUMI NA SITA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA KUMI NA TANO: Mama Frank akiwa na tochi mkononi, akaingia ndani ya kiji mlango kile, kwa kutanguliza miguu, ambapo miguu yake iligusa ngazi, na baada ya hatua mbili, akakanyaga aridhi, “mpokee huyo” alisema bwana Frank, huku anampatia mtoto Deusi, ambae muda wote alikuwa anatazama kila kilichokuwa kinatokea usiku ule, hakika ilikuwa jambo geni na la kutisha sana kwake, lakini uwezi kuamini ujasiri wa mtoto huyu, ambae akuonyesha uoga wala wasi wasi, uso macho yake yakiwa makavu kabisa, pasipo dalili ya machozi wala kilio. …..ENDELEA…..
Baada kuhakikisha kuwa, tayari familia yake imeingia ndani ya shimo hilo, hapo bwana Frank akachukuwa, panga lake na ile tochi, aka ingia ndani ya lile shimo, “pumbavu jamaa wametuzidi akili” ilisikika sauti, toka upande wajikoni kabla bwana Frank ajafunga kile kimlango taratibu na kwa umakini mkubwa sana, “haraka sana watu wasambae mji mzima, askari wakae kwenye barabara zote, kabla hajavuka na kutoka nje ya jiji, kumbuka mtu huyu hatakiwi kufika asubuhi akiwa anapumua” ilisikika kwa mbali sauti, hiyo toka upande wa jikoni, Frank hakujari tena sauti hizo, zaidi aliiongoza familia yake, mle ndani handaki lenye upanda hafifu, na hewa nzito.********
Naam askari walionekana wametapakaa ndani ya jiji la TT, ambalo sasa hakukuwa na raia wa kawaida alie kuwa anazunguka, kutoka na mvua kali iliyokuwa inanyesha kwa nguvu na kuogofya, pengine ungeona gari moja moja likikatikiza kwa mwendo wa taratibu, kutokana na mvua nyingi iliyokuwa inanyesha, na kusababisha ukungu mwingi sana.
Bwana Frank Nyati na familia yake waliibuka mita kama hamsini toka kwenye nyumba yake, usawa wa kichaka cha mauwa kilicho pandwa kama fensi ya eneo lile, la nyumba ya bwana Frank, ambae yeye alikuwa ndie wa kwanza kuibuka, na kuangalia pande zote, kujiridhisha, kama ilikuwa ni sehemu salama, kwa yeye na familia yake kutoka shimoni, lakini wakati anatazama eneo lile, upande wa nyumbani kwake, akaona miili ya watu kadhaa ikiwa imelala eneo la mbele la nyumba yake, ikiwa ni matokeo ya Uzi gan, “sidhani kama kuna cha kusubiri hapa, cha msingi hakikisheni huyu mpuuzi anapatikana na muna muuwa yeye na familia yake yote” wakati huo huo, Frank akasikia sauti toka upande wa barabarani.
Alipo tazama upande huo, kwa tabu sana, akaweza kuona watu kadhaa waliosimama pembeni ya magari binafsi aina ya land rover mia na kumi, yanayofanana na magari yanayotumiwa na jeshi lao, jeshi la nchi hii ya #mbogo_land, waliozuiwa na vichaka vile vya maua, hivyo Frank akatoka na kutambaa usawa wa maua yale mpaka alipo pata sehemu nzuri ya kuwaona watu hao, ambao sasa walikuwa wananyeshewa na mvua, “vipi kuhusu miili ya wenzetu?” aliuliza mmoja kati ya watu wale, aliesimama na mwenzie mmoja alie valia koti refu la mvua, wakiwa ubavuni mwa moja kati ya magari yale matatu, nawasiliana na boss yeye atajuwa la kufanya, nyie wahini mkamsake huyu mpuuzi” alisema yule jamaa mwenye kuvalia koti refu, ambae sauti yake haikuwa ngeni masikioni mwa Frank.
Baada ya hapo Frank akawaona watu wale wenye kuvalia nguo nyeusi, wakiingia kwenye magari, mawili na kuondoka zao, huku wakimwacha yule mwenye kuvalia koti ra mvua, akiwa pamoja na derea wa gari moja lililobakia, Frank alimwona yule jamaa mwenye sauti anayo ifananisha, mtu ambae ni wazi kabisa kuwa ndie aliekuwa mkubwa wao pale walipokuwepo, akitembea kuja upande alipokuwa yeye, hapo Frank anajiweka sawa na panga lake mkononi, tayari kwa lolote.
Frank, anamkazia macho mtu yule kwa lengo la kumtambua, mpaka anapomwona anasimama mita chache, pembeni ya barabara, mita kama sita toka kwenye kile kichaka alichokuwepo yeye, kisha anafungua zip ya suruali yake na kutoa kifaa chake cha kukojolea, kisha anaanza kuumwaga mkojo, Frank hajari kuhusu kifaa hicho, ambacho hata yeye anacho pia, yeye anatazama uso wa jamaa huyu, ambae kiukweli uso wake una gubikwa na giza, na kushindwa kumtambua.
Lakini haikuwa hivyo muda wote, maana baada ya kusubiri kujitahidi kumtambua mtu yule, na kushindwa, Frank akaona kuwa anaweza kumkabili peke yake yule jamaa kwa kutumia upanga wake, maana mpaka muda yule, jamaa alikuwa pake yake, yani mbali na gari, ambalo kulikuwa na dereva peke yake.
Sasa basi, Frank hakumsubiri jamaa amalize kumwaga haja ndogo, aka hesabu “moja… mbili… tat..” kabla haja maliza tatu, mara ghafla mwanga mkali wa gari uka angaza eneo lile, likitokea mjini, na kumfanya jamaa huyu ageuke kulitazama gari lile, Frank akabonyea zaidi kukwepa mwanga, na kuelekeza macho kule alikokuwepo yule, jamaa ambae bila shaka, alikuwa analitarajia gari lile.
Maana yule jamaa alimaliza kukojoa na kukugeuka tena, kulitazama lile gari, ambalo lilikuwa limesha sogea na kupunguza mwendo, huku mwanga wagari lile dogo la kifahari, ukimuangazia usoni, kamanda huyu, alievalia koti kubwa jeusi la mvua, na kwa msaada wa mwanga huo ndipo Frank alipo pata nafasi ya kumtambua mtu huyu, utambuzi ambao ulimstua na kumshangaza bwana Frank, ambae alijikuta anatoa macho ya mshangao wa kutokuamini macho yake.
Huyu alikuwa ni Canal Erasto Kadumya, afisa mtoro wa jeshi, anae kiongoza kikundi cha wahasi wa UMD, ambacho sasa mamluki wake wanasakwa kwa udi na uvumba ndani ya serikali, sasa inakuwaje anamwona kati ya watu wanao msaka yeye, kwa tuhuma za uhaini, wakati kiongozi wa zoezi hili ndie muasi mkubwa sana, anae tafutwa usiku na mchana na jeshi la serikali, ambae sasa alikuwa analisogelea gari lililokuwa limesimama, na mlango wa upande wa dereva ukafunguliwa.
Ukweli ungeweza kusema kuwa, kumwona Erasto Kadumya, akishiriki operation hii ya kusaka wa saliti, kuwa ndio ulikuwa mshangao mkubwa sana, kwa bwana Frank, lakini hapana, sikuwa hivyo, ukweli ni kwamba, mshangao mkubwa ulikuwa ni pale, alipomwona mtu alieshuka toka garini, mtu mfupi kiasi, alie valia koti refu la mvua, kama la Bwana Kadumya, “mawazo yangu yalikuwa sawa, huyu mpuuzi anajaribu kuiangusha serikali” alinong’ona, Frank huku anawatazama wawili wale, walio salimia kwa salamu za kijeshi.
Huyu alikuwa ni Major Chitopelah, mkuu wa operation ya kuwasaka wahasi ndani ya serikali, yani amempumbaza mfalme, huku anaendelea kumpunguzia nguvu ya watu ambao wengemsaidia kuzuwia mapinduzi” alijisemea Frank, huku anaendelea kuwatazama wawili wale, “Erasto kumbuka uzembe hautakiwi kabisa, katika swala la Frank, maana ni mtu hatari sana” alisikika Chitopela, ambae kijeshi alikuwa na cheo kidogo kuliko Kadumya, lakini pale alionekana kuwa ndie mwenye madaraka makubwa zaidi ya Kadumya, “hakika afande, wala usiwe na wasi wasi, nitamnasa ndani ya usiku huu, na nitakuonyesha mwili wake” alisema Kadumya kwa kujiamini.
Baada ya maongezi mafupi, Frank aliwaona wawili wale wakimaliza maongezi yao, na bwana Dickson Chitopelah, akifungua tena mlango wa gari lake na kutoa bagi dogo, ambalo alimpatia Kadumya, “hii ni motisha kwa vijana, zidi kuwapa moyo kuwa, endapo tutafanikiwa kuichukuwa nchi, watakuwa na maisha mazuri sana” alisisitiza Chitopelah, kabla awajaagana na kila mmoja kuondoka na gari lake.
Hii ilimpatia picha pana sana bwana Frank, ambae aligundua kuwa uasi ulikuwa katika vitengo nyeti vya serikali, ikiwa na kiengo cha siri cha mawakala wa usalama wa taifa ili tajiri, linalo tawaliwa katika mfumo wa kifalme, na kwa haraka Frank alijuwa fika kuwa singweza kubadilisha hisia za king Eugen juu yake, na kumwaminisha kuwa Chopelah, alikuwa ndie muasi na msaliti.
Hapo ndipo bwana Frank alipochukuwa familia yake na kuitorosha kuelekea nje ya nchi, na njia aliyo itumia, ilikuwa ni njia ngumu sana, njia ambayo, katika hali ya kawaida, asinge kubali kuipitisha familia yake, maana ukiachilia, hatari ya kuwepo kwa waasi, pia msitu huu, ulikuwa unaongoza kwa wanyama hatarishi, kama vile simba, chui, na wegine wa jamii hiyo pasipo kusahau nyoka wakubwa, sana wakila aina, na wanyama wakubwa ambao siyo rafiki sana kwa binadamu, kama vile faru na tembo.
Mito mikubwa, ambayo ilikuwa inatiririsha maji kwa fujo, huku mvua na milipuko ya radi, ikiendelea kulindima, hakika iligopesha tochi zote zilisha zima, na sasa walitembea kwa kutegemea mwanga wa radi, sidhani kama kuna sehemu ambayo haikulowa katika miili yao, Deus na mama yake walikuwa wanatetemeka kwa baridi kali, kiasi cha meno kugongana, huku bwana Frank akifyeka vicha na magugu marefu, ndani ya madimbwi, ya maji, akitengeneza njia kwakutumia panga kali, mfano wa jambia, alilokuwa amelishika mkononi, mke wake akimfwaa nyuma, akiwa amembeba mtoto.
Ndani ya masaa matatu, tayari walisha vuka mpaka wa inua kisigino, wa kuelekea Tanzania, mpaka ambao, kila mtu huuchukulia kama mpaka mgumu sana kwa mtu kuupitia, kutokana na vikwanzo vya eneo hilo lenye milima na mabonde….…..#NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI, inayo kujia hapa hapa jamii forums