NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA THEMANINI NA MBILI
MTUNZI :
Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA THEMANINI NA MOJA: “ipo hivi dogo, usalama wa abiria ni juu yako usalama wa mzigo ni juu yako, cha msingi tunacho hitaji mzigo ufike salama, taja malipo yako” ilisikika sauti upande wapili wa simu, hapo Deus akatulia sekunde chache akifikiria uzito wa kazi ile, ambayo inafanyika mita chache toka nyumba ya uhifadhi hazina binafsi, abiria ni mwanamke mwenye begi na usalama ni juu yake yani kwa mwanamke na hilo begi, kwahiyo hivyo vyote ni muhimu kwake, “millioni mia mbili” alisema Deus, kwa sauti tulivu. ……….ENDELEA…
Sidhani kama kulikuwa na sababu ya huyu jamaa kucheka kicheko chake cha dharau, baada ya kusikia jibu la Deus, maana alicheka kidogo, kabla ya kujibu, “nitakulipa mara mbili, vipi kuna lolote jingine?” aliuliza huyu jamaa mwenye dharau, “jingine ni juu ya sheria zangu boss, kwanza sihitaji kujua jina la mtu yoyote, pili malipo ni fedha tasilimu sio benk wala mkopo, tatu sihitaji matumizi ya bunduki kwenye gari langu wala kati kati ya mpango, namba nne hakuna mpango ndani ya mpango, tunamaliza kazi kisha tuna anza kazi nyingine kama ipo, namba saba, nidhamu kwa kila mmoja na sheria namba nane, zingatia muda” alimaliza Deus, na hapo yule jamaa upande wapili akatoa sheria yake, mimi ninasheria moja bwana mdogo, nayo usije ukafungua mzigo” alisema yule jamaa kwa msisitizo.
Lakini hapo akakutana na jibu la haraka toka kwa Deus, “usijali hiyo ni sheria yangu ya kumi, hata kama ni asali sitotia hata ncha ya kidole, nahitaji uaminifu ndio maana ninakuwa muaminifu” alisema Deus, kabla hawajakati simu.
Hapo Deus akaweka simu pembeni na kuchukua simu yake ya kawaida, ambayo tayari ilikuwa na jumbe mbili, jumbe zote zikitoka kwa Veronica, “yaani natamani nikutane na wewe, unamambo makubwa sana mchoraji wangu” huo ulikuwa ujumbe wa kwanza, na ujumbe wapili ulikuwa ni “sasa mchoraji wangu, nitakuchek baadae, wacha mimi nijiande nielekee nyumbani, maana ndio mida ya kutoka chuo sasa” alisema Pacha, na Deus hakujibu kitu, baada yake akajisemea mweyewe, “nenda ukashangazwe huko, na kitacho kutokea sijui kama utaweza kusimulia” alijisemea Deus, ambae hakuishia hapo, “nani alikuambia kuna mapenzi ya kupapasana tu” *******
Naam saa kumi kasoro, King Elvis, akiwa ofisini kwake, anaendelea na kazi zake huku anapekuwa jarida lililofungwa la mwaka 1992/92, lililohusu operation ya kuondoa waasia akitazama majina ya washukiwa ambao kwa namna moja au nyingine waliweza kutoroka nchini, ndipo alipoliona jina la James Kervin, tajiri mkubwa aliepo Tanzania, “hivi huyu mzee hawezi kuwa ndie anaefadhiri hawa washenzi?” alijiuliza mfalme Elvis, huku kashika kofia yake ya kifalme iliyotengenezwa kwa dhahabu halisi na kunakshiwa kwa almas halisi.
“Hapana huyu nae ni lazima achunguzwe” alijisemea Elvis, huku ana chukuwa simu yake ya mezani yenye kutengenezwa kwa dhahabu, huku vile vitufe vya namba vikiwa ni almas pia, akaanza bonyeza namba kadhaa na kuweka mkonga sikioni kusikiliza simu ilivyokuwa inaita, bahati nzuri haikuchelewa kupokelewa, “salaam mtukufu mfalme wa Mbogo land” ilisikika salamu toka upande wa pili wa simu, “salaam General, nimekupigia ilinikueleze jambo” alisema mfalme Elvis na kwa sauti tulivu kabisa alisema king Elvis, “nipo tayari kusikiliza chochote utakachoeleza mtukufu” alijibu general Sixmund kwa sauti ya kinyenyekevu, “nahitaji mumfuatilie James Kervin, yule mfanyabiashara aliekimbia mwaka 92, pengine anafadhiri kikundi hiki cha waasi” alisema mfalme Elvis.
Na kabla ya kukata simu, General Sixmund akawahi, “mtukufu mfalme pia naomba nitumie muda huu, kuwakilisha taarifa ya maandalizi ya kikundi na safari ya Tanzania” alisema General kwa sauti ile ile yenye unyenyekevu, “hooo sawa, tena nimeshaongea na balozi ambae aliwakilisha ombi langu la siri na limekubalika” alisema King Elvis na hapo General, akaanza kueleza alipofikia kwenye mpango wake wa kuandaa askari wa kwenda Tanzania.
Ilikuwa hivi, General Sixmund alifanikiwa kuandaa askari kumi na sita, ikiwa ni troop moja ya askari wa uchunguzi wa kivita, AR kwa maana ya Amoured Recconices, wenye mafunzo mazuri ya hali ya juu ya kijeshi, katika mbinu za medani, miongoni mwao alikuwepo captain Amos Makey, na sajent Girbart Ngasa.
Pia kulikuwa na koplo wawili ambao ni Amadeus Peter na Side Nyenza, wote wanne kila mmoja akiwa na askari watatu, kwa maana ya timu, “sawa wataondoka nchini kwa jukumu bandia, nalo ni mafunzo ya dharura” alisema King Elvis, ambae pia alisema ataagiza wizara iandae mpango wa safari na watu waondoke usiku ule ule kuelekea Tanzania, ambapo watatuwa kwenye kiwanja cha ndege cha songea, lengo la kudanganya jukumu ni kuepuka usaliti katika jukumu lililopo mbele yao.********
Yap! saa kumi jioni, mwana dada Veronica, alikuwa nyumbani kwao kinyerezi amejifungia chumbani kwake yupo juu ya kitanda, simu yake mkononi anacharti na mpenzi wake JJ, yani John Joseph, huku amevalia kijigauni fulani chepesi sana, kijigauni ambacho ukaaji wake kwenye mwili huu wenye hips mchomozo, kifua mchongoma,makalio msuso, kingemfanya mtu kusahau majukumu yake, pengine hata risasi kukataa kutoka kwenye mtutu kwa kushindwa kuuwa mtoto mzuri kama huyu, “lakini John, itawezekana kweli, maana watu wanasema huwa haiwezekani” alinadika Vero na kutuma kwenda kwa JJ.
Ujumbe haukukaa sana ukajibiwa, “achana na watu Vero, nisikilize mimi, ikishindikana si tunaacha tu” alisisitiza JJ, ila hata mimi naungana na Deus kwamba haiwezekani, Veronica ajiandae kutoa andazi, maana sio kwa muonekano huu, ambao nauona hapa kitandani, “Veronica James akaachia tabasamu kidogo na kuzidi kuwa mzuri, maana vile vijishimo vya mashavuni vikaonekana, wakati huo vidole vyake vizuri vinavyo weza hata kumaliza haja ya mfungwa, vikigusa gusa simu yake kuandika ujumbe, “sawa nitakuja, lakini tukubaliane kitu” ndivyo ujumbe ulivyo sema, ujumbe mbao mara baada ya kumaliza kuuandika akautuma kwenda kwa JJ, ambae pia hakuchelewa kujibu, “poa nakusikiliza” alijibu JJ.
Hapo haraka sana Veronica akaanza kutoa masharti yake, “kwanza kabisa hakuna kuvua nguo zote, pili hakuna kuingizana vidole, tatu mwisho kushikana kwenye maziwa tu, hakuna kushikana sehemu za siri” duh! sijuwi kama JJ, hakununa au kucheka, maana sijui ingekuwaje.
Lakini kwa wewe ambae umejitabiria jibu lako kama ungekuwa John, naamini umekosea, “wala usiwe na wasi wasi, nitafanya kile unachosema, sitaki kukukwaza” hilo ndilo jibu la kijana ambae tunamfahamu kama John Joseph Daud, mchumba wa mschana mrembo Veronica James, mtoto wa tajiri mmoja mkubwa sana mwenye asili ya nchi ya #mbogo_land, anaeishi Tanzania kama mkimbizi wa kisiasa, anaeshustumiwa kwa kufadhiri kikundi cha waasi wa UMD, wanao pambana na serikali ya nchi ya #mbogo_land.
Kwajibu hilo Verinoca aliachia tabasamu pana sana, huku anapiga picha zile sms alizotumiana na JJ mara ya mwisho na kutuma kwenda kwa mchoraji wake, akisindikiza na ujumbe, “umeona mchoraji, mume mwenzio amekubali masharti, wewe sijui kama ungeweza” akimalizia kwa vikaragosi vya kicheko cha furaha.
Hii ilichukuwa muda mrefu kidogo kujibiwa, kiasi kwamba Veronica akaanza kuhisi kuwa mchoraji wake amekosa amani kwa kitendo cha yeye kukubari kwenda kupapasana na mchumba wake JJ, “hata akikasirika shauri zake kwani yeye ni nani wangu” alijisemea Veronica huku anaweka simu pembeni na kuinuka toka kitandani.
Kaenda moja kwa moja kwenye kabati la nguo la ukutani, akafungua mlango na kutufanya tuweze kuona nguo nzuri za kisasa zilizopangwa ungesema ni dukani, hasa kwa uwingi wake na utofauti wa rangi, akachagua gauni moja zuri refu lenye rangi ya blue na mauwa ya samawati na nyekundu, akachukuwa viatu vyekundu na vyenye visigino virefu akajaribu kupatanisha rangi, akaona inafaa, kisha akarudisha kila kitu sehemu yake na kuelekea kitandani, ambako alikuta ujumbe umeingia kwenye simu.
Veronica akaufungua haraka na kuusoma, “mh! sina hakika kama unachokifikiria ni kitu cha kweli, nakushauri ujiandae kwa mabadiliko ya ratiba” ulikuwa ujumbe toka kwa mchoraji wake, ambao Veronica aliusoma huku akicheka kwa sauti ya chini, “anaona wivu hata bado hajaniona, sasa akiniona si atachanganyikiwa” alijisemea Veronika huku anaandika ujumbe, “usiwe na shaka juu ya hilo” akautuma kwa mchoraji, kisha akaandika nyingine, “wacha nijiandae nitakupa matokeo baadae” kisha akautuma kwa Mchoraji, na kuirushia simu kitandani, kisha akasaula nguo zote za mwilini mwake na kuingia bafuni.******
Naaaam saa kumi na mbili na robo za jioni, mbezi msakuzi ndani ya nyumba moja kubwa ambayo pengine ilijengwa kwa minajili ya ukumbi fulani au bar kubwa, lakini bado ilikuwa haijaanza kutumika, nje ya ukumbi huo tunaona magari sita, aina ya Land Rover pumer, mapya kabisa, yalikuwa yamejipanga huku kila moja lilikuwa na dereva ndani yake.
Tunapoingia ndani kabisa ya jengo lile kubwa, ambalo ndani yake lina viti vichache na mabaki ya vitu vilivyotumika kwenye ujenzi wa ukumbi ule, mkubwa ulioambatana na majengo mengine madogo madogo, tunawakuta wanaume kadhaa mle ndani wenye kufikia idadi ya watu thelathini pamoja na vingozi wao wanne waliokuwa wamesimama mbele yao.
Ukiachilia viongozi wao wanne, ambao tunapo watazama tuna muona Kadumya, Tambwe, Mbwambo, na Enock Kafulu, watu hawa waliogawana katika makundi manne ambayo ungeyatambua kwa utofauti wa mavazi yao.
Wakati kundi la kwanza, lenye watu kumi wakiwa wamevalia suruali nyeusi na zenye kufanana umbo na sare za majeshi ya ulinzi, chini walivalia viatu vyeusi vyenye shingo ndefu, yani buti za kijeshi na juu walivalia tishert nyeusi, kati yao walikuwa wenye muonekano wa watu waishio porini.
Mfano walikuwepo wenye ndevu nyingi, zilizokosa matunzo mazuri, pia walikuwepo wenye nywele ndefu zilizo jisokota hovyo hovyo, pia wapo walionyoa vipara tofauti na wenzao sita, wa kundi la pili, wao valia suit nyeusi na viatu kama vya wenzao, yani buti za kijeshi, hao walionekan kuwa smart kidogo, kundi la tatu, lilikuwa na watu wanne, tu, ambao walikuwa wamevalia nguo za kawaida, yani suruali ya jinsi na raba na tishert, huku kundi la nne likiwa ni kundi la vijana kumi nadhifu waliovalia sare za jeshi la polisi, hakika walikuwa polisi, maana ukiachilia uvaji wao, pia hata unadhifu wao katika unyoaji wa nywele za kichwani hata ndevu pia, iliwatambulisha kuwa ni askari wa jeshi la polisi. ……….ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa
NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa
jamii forums