NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA THEMANINI NA TISA
MTUNZI :
Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA THEMANINI NA NANE: “khaaaaaa! huyu shot chases anataka nini tena?” aling’aka Songoro, kabla hajaipokea simu na kuweka sikioni, “unasemaje wewe, unapigwa na mke nije nikuamulie au?” aliuliza Songoro kwa sauti iliyoonyesha wazi kuwa ameona usumbufu, kuipokea simu ile, “acha ujinga wewe, nina habari muhimu kwako kuhusu yule jamaa aliekunyea jana” alisikika Eze toka upande wapili wa simu. …….ENDELEA…
Hapo ni kama akili ilimtulia Songoro, “nani huyo, unamaanisha yule kijana mshenzi?” aliuliza Songoro kwa sauti ya mshtuko na shauku, “huyo huyo, vijana wameliona gari lake pale Sisterfada hotel, mitaa ya shekilango, ngoja nikutumie picha ulione” alisema Eze na kabla hajakata simu Songoro akamuwahi, “sikia Eze nani yupo hapo SisterFada mida hii” aliuliza Songoro kwa shauku, “yupo kijana wangu Inno, kuna mtu anamfuatilia pale, unaweza kuchukuwa namba yake kwa side ukaongea nae akueleze zaidi” hapo songoro hakujibu, akakata simu mara moja, “side mpigie Inno haraka” alisema Songoro, huku yeye anapiga simu sehemu, simu ambayo ilipokelewa mapema zaidi, “Bakari kusanya vijana wote sasa hivi, waambie vijana wawe tayari kwa kazi, hakikisha mnabeba bunduki na risasi zote tulizo nazo kisha subiri maelekezo yangu” alisema Songoro kwa sauti iliyojaa amri, “ndiyo boss imetekelezwa hiyo”, ilisikika sauti upande wa pili wa simu, sauti ambayo Songoro hakusubiri imalize kutoa jibu akakata simu na kumtazama Side.
Naam said anaonekana akimsogelea Songoro, huku ameshika simu mkononi, “ameshapokea boss” alisema Said, huku anampatia simu Songoro, “Inno huyo mpuzi anae endesha hilo gari umefanikiwa kumuona?” aliuliza Songoro, ambae kulitambua gari ingekuwa inshu kidogo, lakini ageweza kumtambua dereva wa gari, “ndiyo mzee, yupo hapa Hotelini ameingia chumba namba nane ghorofa ya nne na sisi tunamfuata huyo huyo, alisikika innocent akionyesha kuwa alikuwa anatembea kwa haraka, unaweza kuniambia anaonekanaje” aliuliza Songoro huku yeye mwenye akianza kuvuta taswira ya kijana huyo ambae jana amemuonyesha kitu ambacho, hakutarajia kuonyeshwa na mtu mmoja, “ni dogo fulani hivi mrefu kiasi, ana sura ya mtoto wa mama, ila inaonekana huwa anaingia gym” kila innocent alivyotoa maelezo ndivyo Songoro alivyo ipata taswira ya kijana yule mwenye BMW jeusi, “ni huyo huyo mshenzi huyo, hakikisheni hatoki hapo, mpuuzi nataka nimuue kwa mkono wangu” alisema Songoro huku anasimama toka kwenye kochi, “tuondoke haraka tunaelekea sheklango” alisema Songoro huku anampatia Side simu yake.
Wote wakaanza kutembea kutoka nje ya jengo lile, wakimuacha yule mwanamke peke yake mle ndani, na walipofika nje ambako kulikuwana vjana wanne wanalinda jumba lile akawasemesha, “hakikisheni haingii mtu yoyote hapa, sisi tunaenda kumuadabisha mpuuzi mmoja, alisema Songoro, huku anatoa simu na kupiga kwa bakari, kumueleza wakutane wapi usiku ule kwaajili ya kumnasa Deus.*******
Ghorofa ya tatu chumba namba nane, Sisterfada Hotel, kikao kilikuwa kinaendelea huku bwana Kadumya akiendelea kunywa pombe na kuvuta sigara mfululizo na kujaza moshi chumba kile namba nane kiasi cha kumfanya bwana James ashikwe na chafya za mara kwa mara, “sidhani kama swala la umwagaji damu ni muhimu kwa faida utakayoipata bwana James, maana ukiachilia mbali kurudi #mbogo_land ukiwa mtu huru, pia utaendesha biashara zako pasipo kulipa kodi yoyote, wewe ndie utakuwa msimamizi wa mauzo yote ya madini na utapewa migodi kadhaa ya almas na dhahabu, hivyo ndivyo utavyoweza kurudisha fedha utakazo zitoa kwenye malipo ya usafirishaji wa silaha, na michango mingine ambayo tutahitaji kwa huduma za askari wetu” alimaliza kuongea Kadumya.
Naam wakati Kadumya anasubiri, James akubaliane na mpango wake mara ghafla akasikia kicheko toka kwa mzee huyo tajiri, ambae waliamini ndie kikamilishi cha mpango wao wa silaha, “sikuwahi kudhani kama mwisho wa haya yote itakuwa hivi, yani kumbe bwana Chitopelah, ndie mpangaji wa haya yote?” aliuliza James, ambae hakusubiri jibu, “kiukweli sitoweza kutumia jasho langu na juhudi zangu kuibomoa nchi yangu, japo kwa sasa naishi kama mkimbizi, lakini najua hii ilifanywa makusudi ili niingie mtegoni, hakika siwezi kufanya hivyo” alisema James kwa sauti ambayo haikuonyesha dalili yoyote ya utani.
Hapo bwana Kadumya akatulia kama sekunde kadhaa akiwaza kitu fulani, kisha akatoa simu na kupiga kwa mtu fulani huku akiweka sauti ya wazi wote wakasikia ikianza kuita, hata ilipo pokelewa, “niambie Kadu, mpango umeendaje?” ili uliza sauti fulani ambayo ilijawa na mikwaluzo toka upande wa pili wa simu, “muheshimiwa tuna tatizo, bwana James amekataa” alisema Kadumya kwa sauti iliyopooza huku wote wakisikia, “ok! muuweni kufuta ushaidi, maana kiukweli kuna watu wamekuja huko Tanzania na hatujui wana mpango gani mpaka sasa, kisha anzeni mpango wa pili, mukikamilisha anzeni safari kwa magari kupitia kusini mwa Tanzania” ilisikika ile sauti ya mikwaluzo, ambayo niwazi ilikuwa katika ulevi, “ndiyo mheshimiwa” aliitikia Kadumya kabla mheshimiwa hajakata simu, tayari bwana James alikuwa anatetemeka kama vile amesimama mbele ya simba mla watu, kijasho kinamtoka kwenye paji la uso wake.*******
Yap! mara baada ya kukata simu ya bwana Songoro, bwana Eze ambae alikuwa ameipakata miguu na mapaja mazito ya mke wake kipande cha mtu, mara simu yake inaita tena, ana chukua na kuitazama haraka, alikuwa ni innocent Matius, kijana wake aliemtuma kumfuatilia hawara yake Emmy.
Eze akamtazama mke wake, ambae alikuwa anatazama TV, akaipokea simu, “niambie Inno” alisema Eze akitegemea taarifa zaidi, “boss tayari mtu kaingia mtegoni, kuna kijana kaingia chumba namba nane alichoingia shemeji” alisema Inocent, taarifa hiyo ilimuumiza moyo sana Eze, sio tu kwaajili ya gharama anazotumia kwa Emmy, lakini pia kwabjinsi alivyompenda mwanamke huyo na kumfanya kuwa ndiyo burudani yake na kipoozeo cha kero anazozipata kwa mke wake, “ok! mkamateni huyo mshenzi, na niwakute nae hapo ili nimfundishe kuheshimu mali za watu” alisema Eze, huku anaiinua miguu ya mke wake na kuibwaga pembeni kiasi cha mke wake kushangaa na kumtazama mume wake huyo ambae katika hali ya kawaida hawezi kuthubutu kufanya ujinga kama huo.
Mke wa Eze akamuona mume wake anatembea kueleka chumbani huku anakata simu na kuiweka mfukoni, “wewe hebu kuja hapa, umeifanyaje miguu yangu?” alisema mke wa Eze huku anamtazama mume wake aliekuwa anaingia chumbani bila kujibu kitu, ambako hakukaa sana kule chumbani akatoka akiwa na koti na bastora mkononi akatembea kueleka usawa wa meza na kuchukua funguo ya gari kisha akaanza kutembea kuelekea nje, muda wote akijisemesha mwenyewe, “Eze unatafuta kipigo, hebu rudi haraka na unieleze unaenda wapi” alisema mke wa Eze huku anainuka na kukimbilia nje, kule alikokuwa anaenda Eze, “we nisubiri bwana tutamalizana nikirudi” alisema Eze huku na yeye akianza kukimbia kulifuata gari lake lilipokuwa limeegeshwa,
Mke wa Eze ambae uzito wake unamfanya ashindwe kukimbia zaidi, anasimama huku anahema kwa nguvu na kubakia kumtazama mume wake aliekuwa anaingia kwenye gari na kuondoka zake, “we mshenzi leo nitakuuwa bora ulale huko huko” alisema mke wa Eze, lakini akasita kidogo, “mh! ulale huko huko, mbona nita kusaga saga vibaya sana” alisema mwana mama huyo kibonge cha mtu ambae ana uwezo wa kumpiga mumewe huku anatazama taa za gari la mumewe zikitokomea mbali.*******
Naam ndani ya chumba namba nane cha ghorofa ya tatu, Kadumya alimtazama bwana James aliekuwa amekaa kwenye kochi anatetemeka kwa uoga, “haya bwana James una muda mchache wa kufanya maamuzi, kufadhili UMD au kuuwawa?” alisema Kadumya huku anachukuwa sigara kwenye kasha lake na kuiweka domoni, kisha anaiwasha, “kwa kweli ndugu zangu siwezi kuisaliti nchi yangu” alisema mzee James, huku akionekana amejawa na uoga wa hali ya juu, “acha ujinga wewe, unawezaje kuikumbatia nchi ambayo ilikusaoiti?” aliuliza Kadumya kwa sauti ya dharau, hapana haikuwa serikali, huo ulikuwa ni mpango wenu, ili baadae munitumie kufanikisha lengo lenu huku lawama zikiendelea kunishukia mimi” alisema James kwa sauti ambayo licha ya kuonyesha kuwa na uoga wa hali ya juu, lakini ilikuwa na msisitizo.
Hapo Kadumya akawatazama vijana wake wawili, wale waliokuwa wamewageukia wao, ukiachilia wale ambao walikuwa wametazama dirishani, “ok! askari, tuna mfanyaje huyu, tunaondoka nae, tuka muuwe mbele ya safari au tumuuwa na kuuacha mzoga wake hapa hapa” aliuliza Kadumya, swali ambalo lilimuogopesha sana mzee James, ambae hakuwa tayari kuisaliti nchi yake, japo sasa aliishi kama mkimbizi, “boss nadhani itakuwa vyema tukimalizana nae hapa hapa, maana tukitoka nae tunaweza kushtukiwa” alisema mmoja kati ya wale askari wawili na mwingine akadakia, “mkuu, ni vyema ukatoa kibari kwa akina Kafulu kuanza kwa plan B” alisema yule mwingine.
Hapo Kadumya akamtazama James, “bwana James hauna bahati” alisema Kadumya huku anachukua simu yake na kuipiga kwenye namba, iliyoandikwa Dereva, akaipiga nayo ikaanza kuita, hakujua kama mtu anaempigia alikuwa ghorofa inayofuata juu.*******
Naam wakati huo mita kama mia tano magharibi na mashariki, mwa jengo la hotel ya SisterFada, vikundi vya Songoro vikiwa vinakuja kwa kasi kwa lengo la kukutana pale hotelini ili kumkamata kijana anae endesha BMW jeusi, pia Eze alikuwa anaendesha gari lake kwa speed na fujo ilikuwahi kumshughulikia kijana ambae anaamini anatembea na nyumba ndogo yake, makundi yote yalikuwa yana isogelea hotel kwa kasi sana.
Wakati huo huo vijana wa Eze walikuwa wanapanda ngazi kwa kasi kuelekea ghorofa ya nne, kule ambako kijana wetu Deus alikokuwepo, kumbukeni boss amesema anataka amkute huyo fala” alisema Inno akiwaeleza wenzake wawili aliokuwa nao.
Dakika mbili baadae, walikuwa tayari wamesha fika, ghorofa ya nne na ambako walimkuta yule mwenzao mmoja na kutimia wanne, “ok! wawili bakini hapa nje, kuangalia noma sisi wawili tunaingia kumdhibiti huyo mjinga” alisema Inno, huku anatoa bastora yake na kuikoki na wenzake wakafanya hivyo huku wanausogelea mlango wa chumba namba nane.*******
Wakati huo huo ndani ya chumba namba nane cha ghorofa ya nne, Deus akiwa amesimama na box mkononi ana tazama mazingira ya mule ndani ya chumba cha hotel, ambacho kilikuwa na taa zenye rangi hafifu, anaweza kuona wazi meza iliyojaa vyakula na vinywaji mbali mbali vyote vikiwa ni vilevi, Deus anaona kitanda kikubwa kilichotandikwa vizuri.
“Karibu dereva, jihisi uhuru” alisema yule mwanamke alie valia tauro jeupe huku anachukua box mkononi mwa Deus na kulifungua, “asante boss” aliitikia Deus na wakati huo huo akasikia simu yake inaanza kuita, ilikuwa ni simu ya maswala ya kazi, “samahani boss” alisema Deus kisha akapokea simu, “naaam nakusikiliza” alisema Deus, na kutulia kusikiliza upande wa pili, “mpango unaanza saa nne kamili, zingatia muda” ilisikika sauti toka upande wa pili wa simu, “sawa boss” alijibu Deus, na kukata simu, kisha akatazama muda, ilikuwa ni saa tatu na dakika kumi, “usiniite boss anko, niite Emmy na wewe unaitwa nani?” aliuliza yule mwanamke kwa sauti ya taratibu yenye mbwe mbwe za mbembelezo, “umevunja sheria namba moja, hakuna kujuana majina” aliisema Deus kwa sauti tulivu, huku anainua uso wake kumtazama mwanamke huyu.
Deus anacho kiona kwa Emmy, kinamfanya atoe macho kwa mshangao, maana anamwona mwanamke yule akiwa amepembua lile tauro na kubakia uchi wa mnyama, “jamani Dereva, sasa tutakaaje humu ndani bila kujuana majina?” aliuliza Emmy kwa sauti ya kujidekeza huku anainama kwa kubinua makalio yake, akiacha wazi sehemu hiyo aliyojaaliwa kuliko sehemu nyingine, mwana dada huyu mwenye umbo la kushawishi jambazi kurudisha kisu mfukoni, anachukuwa chupi aina bikini kwenye box, aliloleta Deus na kuitazama kama vile anaikagua, hatari jamani ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa
NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa
jamii forums