Donnie Charlie
JF-Expert Member
- Sep 16, 2009
- 16,908
- 19,123
Weka vitu wewe
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mbona fupi leo? Yani moja ukaondoka kakaNYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA HAMSINI NA TISA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA NANE: “ni upuuzi, hebu fuatilia ni nani aliejichukulia maamuzi hayo kisha nipe jibu kesho saa mbili asubuhi kwenye kikao na huyo askari atafutwe haraka kesho areport hapo ofisini kwako na kufutiwa adhabu hiyo” alisema CDF kwa sauti iliyo onyesha kuwa ilikuwa na hasira kali sana, kisha akakata simu akimwacha COT, yaani Chief Of Treaning akiwa ameacha mdomo wazi kwa mshangao jinsi haya mambo yalivyoenda…..endelea…
Gen Mbike hakutaka kupoteza muda kushangaa, hapo hapo akapiga simu kwenda kwa Chief Of Defance MP, na simu ikaanza kuita mara moja.*****
Wakati huo huo kijana wetu Deus, akiwa ndani ya gari waliingia kiluvya madukani na kwenda kusimama njia panda ya kuelekea kisarawe sehemu aliyoelekezwa na na mtu aliempigia simu.
Deus alilipa kiasi cha Tsh 15000 kama malipo ya usafiri, kisha akashuka na kuchukuwa begi lake kubwa la mgongoni na kusimama pembeni ya barabara iendayo kisarawe kisha akatazama kama angeona kitu chochote ambacho kingempa ishara ya gari au mtu ambae anatakiwa asafiri nae, lakini hakuona dalili yoyote zaidi ya watu waliokuwepo eneo lile wakiendelea na shughuri zao za kibiashara, kama vile boda boda mama ntilie wa mama wauza samaki na wasafiri waliokuwa wanaendelea kusubiri daladala, huku wapiga debe wakiendelea kuwashawishi kupanda magari yale, japo nilazima wangepanda hata bila ushawishi ule wa wapiga debe.
Baada ya kuona hivyo Deus akaona kuwa ule ndio wakati ambao angeutumia kuwasiliana na wazazi wake, kuwaeleza kilichotokea kwake mara baada ya kuingia Tanzania ya kwamba amefukuzwa kazi na pia awajulishe kuhusu mizigo ambayo ameituma kwenye bus, hivyo waende kuipokea siku baada ya kesho, ambayo kwa Kiswahili inaitwa keshokutwa.
Naaam wakati Deus anaendelea kuongea na simu yake mara akaliona gari dogo aina BMW S7 jeus, likiwa linaingia pale njia panda likitokea upande wa kisarawe, macho yalimtoka akilitazama lile gari ambalo kiukweli ndiyo gari la ndoto yake, gari ambalo kuna muda fulani aliliona maeneo ya airport japo hakuwa na uhakika kama ndiyo lile lile au la, ila kwa hakika alikjikuta anazidi kutamani kumiliki gari kama lile, na wakati anaendelea kuongea na simu, mara simu yake ikaanza kutoa ishara ya simu nyingine kutaka kuingia kwenye simu yake, akaitoa sikioni na kutazama mpigaji wa simu ya pili.
Kwa macho yake akaona ile namba ngeni ya nchi za nje, namba ambayo ilitoka kumpigia dakika ishirini na saba au nane zilizopita, “baba subiri kidogo nitakupiga baadae” alisema Deus na kukata simu ya kwanza kisha akapokea ile ya pili.******
Mkuu wa polisi jeshini Brigedia SS Chawe, mida hii alikuwa ndani ya gari la jeshi analotembelea siku zote, ikiwa ni safari ya kuelekea nyumbani kwake huku moyoni akijisifu kwa kumaliza jukumu la kufungua mashitaka na kumaliza kesi ya askari mtovu wa nidhamu, yaani Deus Nyati, ambae kisheria adhabu yake ni kufukuzwa jeshi kwa kulitia aibu jeshi hilo lenye kusifiwa kwa nidhamu, “hivi afande unadhani ni sawa kumfukuza jeshi privae Deus Nyati?” aliuliza msaidizi na mwangalizi (mpambe) wa mkuu wa polisi jeshi, mwenye cheo cha luteni, “hakuna mtu muhimu jeshini, kama amefanya makosa basi sheria lazima ichukuwe mkondo wake” alisema brigedia yule, ambae juu ya mfuko wake wakulia wa shati la kombani, kulikuwa na jina SS Chawe yaani Salum Said Chawe, “lakini afande UN ilibaini kuwa hakuwa na kosa zaidi ya kuvunja taratibu ndogo ambazo askari wengi huzivunja” alisema yule msaidizi.
Hiyo ilimfanya Chawe akasirike, “kwahiyo unanifundisha majukumu yangu” aliuliza Chawe kwa sauti kavu, huku wakitazama jengo la diamond jubilee, kwa maana walikuwa wanakatiza hapo na wakati huo huo simu ya mkononi ya Chawe ikaanza kuita, akaichukuwa haraka na kuitazama, mpigaji alikuwa ni major General Mbike, yaani COT, moyo wa Chawe ukalipuka kwa mshtuko, maana alikumbuka kuwa licha ya kumpokea na kumshtaki Deus, lakini hakuwa amepeleka taarifa yoyote kwa Mkuu wa mafunzo.
Chawe akaipokea haraka simu ile na kuiweka sikioni, “jambo afande” alisalimia brigedia Chawe, “Chawe toka lini umepewa jukumu la kupokea watu wanaotoka operation nje ya nchi?” aliuliza Mbike kwa sauti iliyojilazimisha kuzuwia jazba, “afande huyu ni tofauti kidogo, huyu ni mwalifu, hivyo ni jukumu la MP kwenda kumuweka chini ya ulinzi” alijibu Chawe kwa sauti yenye uzito mkubwa wanidhamu, “uliagizwa na nani brigedia, ofisi yangu si ndiyo yenye jukumu la kukuagiza kuwa fulani akamtwe, maana bado alikuwa chini yangu” aliuliza Mbike, safari hii akiongeza sauti kidogo na kuwa yenye ukali, “afande nadhani msaidizi wangu ndie aliamua kujiongeza baada ya kuona taarifa inachelewa, sababu mimi nililetewa akiwa amesha toka airport” alisema Chawe kwa sauti ya kujitetea “kwahiyo jukumu la kufungua mashaka nalo ulijiongeza au uliagizwa na nani?” aliuliza Mbike, kwa sauti yenye hasira ya wazi na hapo ndipo Chawe alipokumbuka maneno ya huyu msaidizi wake (mpambe)
“afande tulitoa taarifa kwa mnadhimu, tukiomba kibali cha kufungua mahakama, nae akakubali, na sisi tukafanya hivyo” alijibu Chawe, na hapo kikasikika kicheko cha uchungu, “Chawe ulikuwa na maslahi yoyote kwa kumshtaki Deus, mbona ulikiuka sheria na nidhamu ya kijeshi ambayo unaisimamia kila siku, ni kweli ulitakiwa uende kwa mnadhimu kabla yangu? wewe ndie ulietakiwa ukampokee Deus airport na siyo mimi, hata jukumu la kumshtaki Deus, lilikuwa la kwangu, hakika hii imekuchafua, anyway jiandae kwa kile kitakacho kutokea kwa kosa la kufukuza askari ambae bado jeshi lilikuwa linamuhitaji” alisema Mbike na kukata simu, akimuacha Chawe ameshikilia simu huku macho ameyatoa kama vile amefumaniwa.******
Yap! Saa nane na nusu, ndio muda ambao, Sheba alisimamisha gari maeneo ya kiluvya madukani, akitokea upande wa kisarawe kupitia barabara ya tondoroni mpaka mdidimue, Sheba kama alivyoelekezwa na boss wake Atshen akasimamisha gari mita chache toka barabara hiyo iendayo Morogoro, ambapo aliambiwa kuwa atampata mtu mwenye uwezo mkubwa wa kuendesha gari na pia ni mpiganaji mkubwa sana mwenye uwezo mkubwa.
Sheba akatazama kushoto na kulia mwa barabara ya vumbi ya kiluvya madukani kama angemuona mtu analifwata gari lile, lakini hakuona mtu yoyote anae lifuata gari lake, zaidi aliwaona watu wengi wakiwa wanaendelea na shughuri zao, wakiwa wauza samaki, mama nitilie wapiga debe wa daladala, pia madereva wa boda boda na watu waliokuwa wanafika pale kutafuta mahitaji au usafiri wa kwenda maeneo mbali mbali ya mji.
Wakati Sheba anatazama kushoto na kulia, mara macho yake yakakwama kwa kijana mmoja mrefu wa wastani, mwenye umbo fulani ambalo lilimtambulisha kuwa ni kijana aliependa mazoezi, au kufanya mazoezi kwa muda mrefu siku za hivi karibuni, ambae alikuwa amebeba begi kubwa mgongoni mwake, “mh! mbona sikuwhai kuona kijana mtanzania mwenye kufanana na wewe” aliwaza Sheba, ambae sio kwaajili ya lile begi, ila ni kwaajili ya uso wa upole wakijana huyu, ambae sasa alikuwa anaongea na simu, huku macho yake anapepesa kushoto na kulia na mwisho macho yake yakaganda kwenye gari lake, ambalo alilitazama kwa muda mrefu kidogo huku anaendelea kuongea kwa simu yake.
Dakika moja baadae, akamuona kijana yule, akibofya simu yake na kuiweka tena sikioni, ilionyesha wazi kuwa kuna simu nyingine ilikuwa imeingia wakati akiwa anaongea na hata alipoongea na ile simu ya pili alionekana akitazama tena gari la Sheba, na kuanza kutembea kulifuata, mpaka alipolifikia gari lile, hapo Sheba akajikuta anatabasamu, maana alishajuwa kuwa kijana huyu mwenye umbo la pekee, ndie mtu aliekusudiwa kuwa dereva na mlinzi wake katika safari mpya ya kuelekea kaskazini mwa Tanzania,
Kijana yule alipolikaribia gari, Sheba akafungua mlango na kushuka akiliacha lina unguruma, na kuzunguka upande wa kushoto wa gari, akaingia kwenye upade huo kwa maana seat ya abiria wa mbele na Deus nae hakujiuliza, akausogelea mlango wa abiria wa nyuma na kuufungua mlango ule akaliona begi dogo ambalo hakulijali, yeye akaweka begi lake na kuufunga mlango ule, kisha akaingia kwenye seat ya dereva, ambayo mlango wake ulikuwa wazi.
Baada ya kuingia akafunga mlango na kumtazama Sheba, “habari yako dada” alisalimia Deus kwa sauti yake ya upole, “nzuri, nadhani maelekezo unayo, mzigo wako huo hapo seat ya nyuma” alisema Sheba, huku akionyesha lile begi dogo lililopo seat ya nyuma, Deus alilitazama lile begi dogo, kisha akalinyoosha mkono na kulichukuwa, halafu akafungua lile begi, ambalo ndani yake kulikuwa na bando za fedha za kitanzania, noti za elfu kumi kumi, akafunga na kulirushia tena kule nyuma, “ok! boss wako yupo vizuri, anaenda na muda na mkweli anatimiza ahadi” alisema Deus, huku anatazama dash board ya gari lile ambao leo ni mara yake ya kwanza kuingia ndani yake, “una uhakika tutafika salama?” aliuliza Sheba kwa saut ya kutilia mashaka, maana kwa muonekan wa sura na muonekano wa Deus, upole wake na uongeaji wake, usingemuweka katika kundi kama hili.
“Tuna BMW S7, sina wasi wasi” alisema Deus, huku anapachika gia na kuondoa gari taratibu, kuingia barabara kuu, usingewaza kama walikuwa na safari ya mbali kiasi hicho, zaidi ya kilomita mia tatu, taratibu gari liliingia barabara ya morogoro na kushika uelekeo wa kushoto, ambao ni wa morogoro, likitembea kwa speed ndogo, kama linaishia mzani, wakati huo hapo, pale kibaha mpakani hawakujuwa kuwa, mita chache toka pale njia panda ya kisarawe walipokuwepo, kuna askari wa jeshi la polisi alievalia nguo za kiraia alikuwa analitazama gari lile la kisasa, lenye mwonekano wa upya…....…….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
Unajuaga hapa pamefika panono ngoja niwaache na arostoNYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA HAMSINI NA TISA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA NANE: “ni upuuzi, hebu fuatilia ni nani aliejichukulia maamuzi hayo kisha nipe jibu kesho saa mbili asubuhi kwenye kikao na huyo askari atafutwe haraka kesho areport hapo ofisini kwako na kufutiwa adhabu hiyo” alisema CDF kwa sauti iliyo onyesha kuwa ilikuwa na hasira kali sana, kisha akakata simu akimwacha COT, yaani Chief Of Treaning akiwa ameacha mdomo wazi kwa mshangao jinsi haya mambo yalivyoenda…..endelea…
Gen Mbike hakutaka kupoteza muda kushangaa, hapo hapo akapiga simu kwenda kwa Chief Of Defance MP, na simu ikaanza kuita mara moja.*****
Wakati huo huo kijana wetu Deus, akiwa ndani ya gari waliingia kiluvya madukani na kwenda kusimama njia panda ya kuelekea kisarawe sehemu aliyoelekezwa na na mtu aliempigia simu.
Deus alilipa kiasi cha Tsh 15000 kama malipo ya usafiri, kisha akashuka na kuchukuwa begi lake kubwa la mgongoni na kusimama pembeni ya barabara iendayo kisarawe kisha akatazama kama angeona kitu chochote ambacho kingempa ishara ya gari au mtu ambae anatakiwa asafiri nae, lakini hakuona dalili yoyote zaidi ya watu waliokuwepo eneo lile wakiendelea na shughuri zao za kibiashara, kama vile boda boda mama ntilie wa mama wauza samaki na wasafiri waliokuwa wanaendelea kusubiri daladala, huku wapiga debe wakiendelea kuwashawishi kupanda magari yale, japo nilazima wangepanda hata bila ushawishi ule wa wapiga debe.
Baada ya kuona hivyo Deus akaona kuwa ule ndio wakati ambao angeutumia kuwasiliana na wazazi wake, kuwaeleza kilichotokea kwake mara baada ya kuingia Tanzania ya kwamba amefukuzwa kazi na pia awajulishe kuhusu mizigo ambayo ameituma kwenye bus, hivyo waende kuipokea siku baada ya kesho, ambayo kwa Kiswahili inaitwa keshokutwa.
Naaam wakati Deus anaendelea kuongea na simu yake mara akaliona gari dogo aina BMW S7 jeus, likiwa linaingia pale njia panda likitokea upande wa kisarawe, macho yalimtoka akilitazama lile gari ambalo kiukweli ndiyo gari la ndoto yake, gari ambalo kuna muda fulani aliliona maeneo ya airport japo hakuwa na uhakika kama ndiyo lile lile au la, ila kwa hakika alikjikuta anazidi kutamani kumiliki gari kama lile, na wakati anaendelea kuongea na simu, mara simu yake ikaanza kutoa ishara ya simu nyingine kutaka kuingia kwenye simu yake, akaitoa sikioni na kutazama mpigaji wa simu ya pili.
Kwa macho yake akaona ile namba ngeni ya nchi za nje, namba ambayo ilitoka kumpigia dakika ishirini na saba au nane zilizopita, “baba subiri kidogo nitakupiga baadae” alisema Deus na kukata simu ya kwanza kisha akapokea ile ya pili.******
Mkuu wa polisi jeshini Brigedia SS Chawe, mida hii alikuwa ndani ya gari la jeshi analotembelea siku zote, ikiwa ni safari ya kuelekea nyumbani kwake huku moyoni akijisifu kwa kumaliza jukumu la kufungua mashitaka na kumaliza kesi ya askari mtovu wa nidhamu, yaani Deus Nyati, ambae kisheria adhabu yake ni kufukuzwa jeshi kwa kulitia aibu jeshi hilo lenye kusifiwa kwa nidhamu, “hivi afande unadhani ni sawa kumfukuza jeshi privae Deus Nyati?” aliuliza msaidizi na mwangalizi (mpambe) wa mkuu wa polisi jeshi, mwenye cheo cha luteni, “hakuna mtu muhimu jeshini, kama amefanya makosa basi sheria lazima ichukuwe mkondo wake” alisema brigedia yule, ambae juu ya mfuko wake wakulia wa shati la kombani, kulikuwa na jina SS Chawe yaani Salum Said Chawe, “lakini afande UN ilibaini kuwa hakuwa na kosa zaidi ya kuvunja taratibu ndogo ambazo askari wengi huzivunja” alisema yule msaidizi.
Hiyo ilimfanya Chawe akasirike, “kwahiyo unanifundisha majukumu yangu” aliuliza Chawe kwa sauti kavu, huku wakitazama jengo la diamond jubilee, kwa maana walikuwa wanakatiza hapo na wakati huo huo simu ya mkononi ya Chawe ikaanza kuita, akaichukuwa haraka na kuitazama, mpigaji alikuwa ni major General Mbike, yaani COT, moyo wa Chawe ukalipuka kwa mshtuko, maana alikumbuka kuwa licha ya kumpokea na kumshtaki Deus, lakini hakuwa amepeleka taarifa yoyote kwa Mkuu wa mafunzo.
Chawe akaipokea haraka simu ile na kuiweka sikioni, “jambo afande” alisalimia brigedia Chawe, “Chawe toka lini umepewa jukumu la kupokea watu wanaotoka operation nje ya nchi?” aliuliza Mbike kwa sauti iliyojilazimisha kuzuwia jazba, “afande huyu ni tofauti kidogo, huyu ni mwalifu, hivyo ni jukumu la MP kwenda kumuweka chini ya ulinzi” alijibu Chawe kwa sauti yenye uzito mkubwa wanidhamu, “uliagizwa na nani brigedia, ofisi yangu si ndiyo yenye jukumu la kukuagiza kuwa fulani akamtwe, maana bado alikuwa chini yangu” aliuliza Mbike, safari hii akiongeza sauti kidogo na kuwa yenye ukali, “afande nadhani msaidizi wangu ndie aliamua kujiongeza baada ya kuona taarifa inachelewa, sababu mimi nililetewa akiwa amesha toka airport” alisema Chawe kwa sauti ya kujitetea “kwahiyo jukumu la kufungua mashaka nalo ulijiongeza au uliagizwa na nani?” aliuliza Mbike, kwa sauti yenye hasira ya wazi na hapo ndipo Chawe alipokumbuka maneno ya huyu msaidizi wake (mpambe)
“afande tulitoa taarifa kwa mnadhimu, tukiomba kibali cha kufungua mahakama, nae akakubali, na sisi tukafanya hivyo” alijibu Chawe, na hapo kikasikika kicheko cha uchungu, “Chawe ulikuwa na maslahi yoyote kwa kumshtaki Deus, mbona ulikiuka sheria na nidhamu ya kijeshi ambayo unaisimamia kila siku, ni kweli ulitakiwa uende kwa mnadhimu kabla yangu? wewe ndie ulietakiwa ukampokee Deus airport na siyo mimi, hata jukumu la kumshtaki Deus, lilikuwa la kwangu, hakika hii imekuchafua, anyway jiandae kwa kile kitakacho kutokea kwa kosa la kufukuza askari ambae bado jeshi lilikuwa linamuhitaji” alisema Mbike na kukata simu, akimuacha Chawe ameshikilia simu huku macho ameyatoa kama vile amefumaniwa.******
Yap! Saa nane na nusu, ndio muda ambao, Sheba alisimamisha gari maeneo ya kiluvya madukani, akitokea upande wa kisarawe kupitia barabara ya tondoroni mpaka mdidimue, Sheba kama alivyoelekezwa na boss wake Atshen akasimamisha gari mita chache toka barabara hiyo iendayo Morogoro, ambapo aliambiwa kuwa atampata mtu mwenye uwezo mkubwa wa kuendesha gari na pia ni mpiganaji mkubwa sana mwenye uwezo mkubwa.
Sheba akatazama kushoto na kulia mwa barabara ya vumbi ya kiluvya madukani kama angemuona mtu analifwata gari lile, lakini hakuona mtu yoyote anae lifuata gari lake, zaidi aliwaona watu wengi wakiwa wanaendelea na shughuri zao, wakiwa wauza samaki, mama nitilie wapiga debe wa daladala, pia madereva wa boda boda na watu waliokuwa wanafika pale kutafuta mahitaji au usafiri wa kwenda maeneo mbali mbali ya mji.
Wakati Sheba anatazama kushoto na kulia, mara macho yake yakakwama kwa kijana mmoja mrefu wa wastani, mwenye umbo fulani ambalo lilimtambulisha kuwa ni kijana aliependa mazoezi, au kufanya mazoezi kwa muda mrefu siku za hivi karibuni, ambae alikuwa amebeba begi kubwa mgongoni mwake, “mh! mbona sikuwhai kuona kijana mtanzania mwenye kufanana na wewe” aliwaza Sheba, ambae sio kwaajili ya lile begi, ila ni kwaajili ya uso wa upole wakijana huyu, ambae sasa alikuwa anaongea na simu, huku macho yake anapepesa kushoto na kulia na mwisho macho yake yakaganda kwenye gari lake, ambalo alilitazama kwa muda mrefu kidogo huku anaendelea kuongea kwa simu yake.
Dakika moja baadae, akamuona kijana yule, akibofya simu yake na kuiweka tena sikioni, ilionyesha wazi kuwa kuna simu nyingine ilikuwa imeingia wakati akiwa anaongea na hata alipoongea na ile simu ya pili alionekana akitazama tena gari la Sheba, na kuanza kutembea kulifuata, mpaka alipolifikia gari lile, hapo Sheba akajikuta anatabasamu, maana alishajuwa kuwa kijana huyu mwenye umbo la pekee, ndie mtu aliekusudiwa kuwa dereva na mlinzi wake katika safari mpya ya kuelekea kaskazini mwa Tanzania,
Kijana yule alipolikaribia gari, Sheba akafungua mlango na kushuka akiliacha lina unguruma, na kuzunguka upande wa kushoto wa gari, akaingia kwenye upade huo kwa maana seat ya abiria wa mbele na Deus nae hakujiuliza, akausogelea mlango wa abiria wa nyuma na kuufungua mlango ule akaliona begi dogo ambalo hakulijali, yeye akaweka begi lake na kuufunga mlango ule, kisha akaingia kwenye seat ya dereva, ambayo mlango wake ulikuwa wazi.
Baada ya kuingia akafunga mlango na kumtazama Sheba, “habari yako dada” alisalimia Deus kwa sauti yake ya upole, “nzuri, nadhani maelekezo unayo, mzigo wako huo hapo seat ya nyuma” alisema Sheba, huku akionyesha lile begi dogo lililopo seat ya nyuma, Deus alilitazama lile begi dogo, kisha akalinyoosha mkono na kulichukuwa, halafu akafungua lile begi, ambalo ndani yake kulikuwa na bando za fedha za kitanzania, noti za elfu kumi kumi, akafunga na kulirushia tena kule nyuma, “ok! boss wako yupo vizuri, anaenda na muda na mkweli anatimiza ahadi” alisema Deus, huku anatazama dash board ya gari lile ambao leo ni mara yake ya kwanza kuingia ndani yake, “una uhakika tutafika salama?” aliuliza Sheba kwa saut ya kutilia mashaka, maana kwa muonekan wa sura na muonekano wa Deus, upole wake na uongeaji wake, usingemuweka katika kundi kama hili.
“Tuna BMW S7, sina wasi wasi” alisema Deus, huku anapachika gia na kuondoa gari taratibu, kuingia barabara kuu, usingewaza kama walikuwa na safari ya mbali kiasi hicho, zaidi ya kilomita mia tatu, taratibu gari liliingia barabara ya morogoro na kushika uelekeo wa kushoto, ambao ni wa morogoro, likitembea kwa speed ndogo, kama linaishia mzani, wakati huo hapo, pale kibaha mpakani hawakujuwa kuwa, mita chache toka pale njia panda ya kisarawe walipokuwepo, kuna askari wa jeshi la polisi alievalia nguo za kiraia alikuwa analitazama gari lile la kisasa, lenye mwonekano wa upya…....…….endelea…. kufwatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
😅Unajuaga hapa pamefika panono ngoja niwaache na arosto
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA TANO
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WATSAPP: 0743632247
ILIPOISHIA SEHEMU YA NNE: “ok! nipe hali ya uzito wa mzigo, daraja la mzigo, na usalama wa usafirishaji” aliuliza kijana wetu, ambae alikuwa anaendelea kuendesha gari kwa speed kama vile analazimika kwenda na muda flani, wakati huo walikuwa wanakaribia njia panda ya Moroco, “uzito, haufiki hata kilo, usalama ni mkubwa sana, thamani yake laki mbili” alijibu yule mwanamke kwa sauti ile ile, ambayo kama unauwezo wa kujaji mtu kupitia sauti ungejuwa kwa, uzuri wa mwanamke huyu, siyo wataratibu, na ni mwanamke wa mjini, mwenye maisha ya hali ya juu. endelea
Hapo dereva wetu akashusha pumzi ndevu ya kuchoka, maana yeye amezowea kusafirisha mizigo ya hatari, lakini sasa anaambiwa kuwa, mzigo hakuwa na hatari yoyote, na thamni yake ni laki mbili, hapo akaona kuwa ni utani, lakini kutokana na utaratibu wake namba 7, hakutakiwa kudharau kitu wala mtu, “ok! malipo elfu hamsini, utanipatia nikifisha mzigo, lakini utatakiwa kuzingatia kuwa, hakuna ujanja, huo ni utaratibu namba 5” alisema dereva, akitaja elfu hamasini kwa kutegemea kuwa mwanamke huyu, angeona bei kubwa, na kughairi mpango, “wala usiwe na wasi wasi, natukienda sawa, nita kuongezea mala dufu ya elfu hamsini” alisema yule mwanamke, huku akizidi kuipooza sauti yake, “ok! mpango umekubaliwa” alisema dereva na kukata simu, wakati huo, anapunguza mwendo kuingia njia panda ya Moroco, na kukata kushoto kuelekea barabara ya mwenge, kisha akaongeza mwendo, pasipo kujari sms zilizokuwa zinaingia kwenye ile simu yake nyingine, muda wote mschana mdogo Zamda akiwa anamtazama kijana huyu, kwa macho ya viulizo, na kushindwa kupata jibu.*******
Yap! wakati kama huu, kusini mashariki mwa Tanzania, pembezoni mwa mto Ruvuma, kaskazini mashariki mwa msumbiji, ndani ya nchi ndogo ya kifalme, nchi iliyosaahulika katika ramani ya dunia, kutokana na kuchelewa kutambuliwa na umoja wa mataifa, nchi ya mbogo #land_land, inayoongozwa na mfalme Elvis Mbogo wa kwanza, mwenye makazi yake katika ngome ya dhadhabu, kwamaana ya Golden Castle, iliyopo ndani ya jiji la Treanch Town, kwa maana ya Treanch Town City.
Tuachane na King Elvis, twende kusini mwa mji huu wa TT, mpaka nje kidogo ya jiji Hilo la Trench Town, ni pembezoni mwa barabara ya kuelekea upande wa msumbiji, katika kitongoji kidogo cha Mmajile, (mmemaliza), mji ulikuwa umechangamka kwa burudani, kama ujuwavyo mji huu, jioni na nyakati kama hizi, watu hutumia muda wao na familia zao, au wapenzi wao, kupata burudani katika bustani za viunga vya jiji, huku wakipata vinywaji na vitafunwa mbali mbali.
Hayatuhusu hayo, sisi twendeni moja kwamoja mpaka kwenye jengo moja kubwa, la ghorofa kumi na mbili, ambao lilikuwa alijamaliziwa ujenzi wake, lililokuwa limezungushiwa uzio wa mabati, kama wafanyavyo wakandarasi wengine wanapofanya ujenzi mkubwa kama huu.
Ndani ya uzio huo yana onekana magari nane ya kifahari, ni jambo la kawaida kwa nchi hii kuona magari kama haya, maana wanachi wengi ni mtajiri, lakini licha ya magari hayo nane, pia kulionekana vijana kumi na tano, walio valia nguo nyeusi, kwa maana ya suruali nyeusi za jinsi, na tishert nyeusi, zilizo kamata miili yao, kichwani kofia nyeusi za cap, waswaili uita kapelo, mikononi mwao wakiwa na bunduki aina ya HECKLER &KOCH G95 toka GERMANY ASSAULT RFLE 5.56MM, H K G 95, yaani hecler & koch G 95, iliyotengenezwa nchi germany assault refle yenye mtutu wa mzingo mill miter 5.56, kwa faida ya msomaji, ni aina ya silah iliyotumika kumuuwa Osama bin laden mwaka 2011.
Wakionekana kuwa makini sana, katika ulinzi wa eneo hilo, lenye mwanga hafifu, vijana hawa walionekana wakiwa wamejipanga kwa kuachiana nafasi ya mita kati ya kumi mpaka kumi natano eneo lote la mbele.
Achana na eneo ili kwa nje, huko ndani katika moja kumbi za jengo hilo, lenye giza, zilionekana taswira za vimvuli vya giza, vya watu kama sita hivi, ambao kiukweli usingeweza kuona sura zao, walionekana kuwa katika mpango flani mzito sana, “bwana James Carvin, alitoroka nchini mwaka 1988, na kukimbilia tanzania, ambako anaalianzisha tena biashara zake na kuwa mfanyabiashra mkubwa na tajiri” alisema mmoja wao, aliekuwa amesimama mbele yao, huku wengine watano, wakiwa wamesima kwa kutengeneza nusu mwezi, huku wakionekana kumsikiliza kwa umakini mkubwa sana.
“bwana James Carvin, ambae kwa sasa anamiliki viwanda vikubwa vya vyakula unga na vinywaji, huko Tanzania, alikimbia nchini, akikwepa tuhuma za uhaini, alionekana kuwa alikuwa anafadhiri kikundi cha kijeshi cha waasi wa zamani, kilicho fahamika kwa jina la harakati za uhuru kwa damu” alisema tena yule ambae walikuwa wanamtazama, ambae kwa haraka alionekana kuwa na umri mkubwa zaidi yao, “naamini bwana James atakuwa na hasira kali sana na serikali, hivyo akielezwa anachotakiwa kufanya juu yetu, lazima ataungana na sisi, na kutusaidia kulipia kontena ishirini za silaha mabomu na risasi, kwaaajili ya mapinduzi, pamoja na kutusaidia chakula kwaajili ya askari wetu waliopo msituni” alisema yule jamaa, ambae licha ya kuwa gizani, na rangi yake kuwa nyeusi, pia alikuwa amevalia koti refu jeusi, suruali nyeusi, viatu vyeusi, na kofia ya duara yeusi yenye kuziba uso wake.
“Lakini mheshimiwa, itakuwaje kama atakataa, maana Jemes nikama mtu wa kufata sheria pia” aliuliza mmoja kati yao, ambae alionekana kuvalia nguo zinazofanana na wale vijana wa nje, “sikia bwana Tambwe, fanya kama nilivyo kuagiza, mweleze kwamba, mimi nimesema, kuwa, endapo tutachukuwa nchi hii, yeye atakuwa huru kuchimba dhahabu, kufanya biashara bila ushuru wowote, pia atapewa eneo kubwa sana la kufungua biashara yake na pia atapewa kandarasi ya kuchimba gass na mafuta, lazima atakubari tu, na kumbukeni kuwa mzigo hupo njiani, sikutatu baadae unatia nanga Queen Irine Bay, lazima tuwe na fedha ya kulipia kwa wale jamaa watukabidhi mzigo wetu” alisema yule alie itwa Mheshimiwa, safari hii akionyesha msisitizo mkubwa, “lakini mheshimiwa, nadhani itakuwa vizuri kama tukiwa na mpango mwingine, maana uwezi kujuwa James atasemaje” safari hii alishauri mtu mwingine, na siyo yule alie itwa Tambwe, huyu alikuwa amevaa suit nyeusi na kofia nyeusi.
Hapo mheshimiwa akatulia kidogo kama sekunde tano hivi, kisha akamtazama yule alie shauri, “sasa nimekuelewa, bwana Kadumya, mpango wapili upo, na utatekelezwa muda mchache sana baada ya huu wa kwanza kushindikana” alisema mheshimiwa ambae mpaka sasa hatuja mfahamu kwa jina, huku wale wengine wakimsikiliza kwa umakini mkubwa sana, “Kadumya hakikisha vijana wako wanafwata maelezo, ikiwa pamoja na endapo huu wakwanza utashindikana, wamuuwe James, kisha watahamia kwenye mpango wa pili, ambao nita wapa muda mfupi baada ya mpango wa kwanza, japo sitegemei kama James akiona mitutu ya bunduki usoni mwake, ataweza kusema hapana” alisema Mheshimiwa akionekana kuwa mwenye uhakika zaidi.
Naam baada ya hapo hawa kutumia muda mrefu mahala pale, wakaagana, “Kadumya, hakikisha vijana wako, wanapanda ndege kesho mapema, kuelekea Tanzania, nguo na silaha watazikuta huko huko, kwa bwana Mbwambo, kule temeke kaburi moja” alielekeza Mheshimiwa, kabla hawajaondoka zao, kwa namna ya siri kama vile Hawakuwa pamoja.******
Naam turudi kigamboni, ambako tayari polisi walisha kagua magari yote yaliyokuwa yana subiri kuingia kwenye kivuko yani Pantoni, pasipo kuliona BMW jeusi, na kuamua kurudi walikotoka, huku CP Ulenje akitoa maagizo askari wasambae maeneo yote kulisaka gari ilo, na yeye pamoja na askari watano wakaelekea upande wa mji mwema, kwenda kumwona bwana Songoro.
Ilikuwa ni safari ya dakika kumi na tano, mpaka kufika kwenye nyumba ya bwana Songoro, iliyo jitenga ndani ya eneo moja kubwa lililozingikwa na vichaka vifupi na minazi mirefu, sehemu ambayo walipofika tu, wakapokelewa na bwana Songoro alie simama sambamba na yule mwanamke, ambae sasa alikuwa amevalia chupi aina ya bikini na sidilia kifuani kwake, kati kati ya eneo la mbele la ile yumba kubwa, huku wakionekana watu waliokuwa wanagala gala chini kwa maumivu makali, huku wengine wakiwa wamepoteza fahamu zao, idadi yao ikifika zaidi ya kumi, huku zikionekana silaha mbali mbali zajadi na zile za kisasa, yani visu mapanga na bastora, vikiwa vimetawanyika eneo lile, huku baadhi ya ya watu hao wakionekana kuvujwa na damu , toka kwenye majelaha mbakubwa, katika sehemu mbali mbali za miili yao.
CP Ulenje alitoa macho kwa mshangao, “Songoro unasema alikuwa kijana mmoja tu?” aliuliza CP Ulenje kwa mshangao, “ukweli sikuwai kufikiria kama kuna mtu anaweza kuwa kama yule kijana, hakika namwitaji na tena namwitaji nimkate kiungo kimoja baada ya kingine” alisema Songoro kwa sauti iliyo jaa chukizo na kasiriko, “vijana tayari wapo kazini, naamini muda siyo mrefu watamtia nguvuni” alisema Ulenje, wakati huo wanaingia ndani, na kukagua watu wengine walio kuwa bado wanagala gala kwa maumivu, wapo waliolalamikia mbavu wapo waliolalamikia nyuso zao, na wapo walio lalamikia miguu yao, ilimradi kila mmoja wao alipata anacho stahili, “unampango gani na hawa watu Songoro” aliuliza Uledi , wakati wanaendelea kukagua mle ndani, “wajinga hawa wanawezaje kupigwa na mtoto mrembo kama yule” alisema Songoro ambae hakuonyesha dalili ya kuwa saidia vijana wake, waliokuwa wanataabika pale chini, “huyo kijana atakuwa tatizo hapa mjini, inabidi apatikane haraka sana” alisema CP Ulenje, huku anatoa simu, kubofya namba kisha akaipiga na kuweka sikioni.
Simu haikuita muda mrefu, ikapokelewa, “OCD mambo ni mazito, kuna uvamizi mkubwa umetokea huku mji mwema kigamboni, kwa mfanyabiashara Songoro, agiza gari la wagonjwa lije huku, pia peleka taarifa vituo vyote vya polisi, hapa mjini, msako mkali uendelee, malengo ni BMW jeusi, kamata kila anae hisiwa mpaka apatikane, na taarifa itolewe kuwa ni mtu hatari sana huyo” alisema CP Ulenje, mara tu baada ya simu kupokelewa, “sawa mkuu inatekelezwa” alijibu OCD, na hapo Ulenje akakata simu, kisha akamtazama Songoro, “hakiki hakikisha unaondoa hizo silaha hapo nje” alisema Ulenje, kwa msisitizo.*******
Naam barabara ya bagamoyo, mtaa wa tegeta, njia panda ya kwasharifu, linaonekana gari moja jeusi aina ya ford ranger likiwa limesimama pembeni ya barabara hiyo, huku mtu mmoja, mwenye mwonekano wa miaka 40, akiwa amesimama ubavuni mwa gari ilo, huku uso wake, ukionekana kujawa na mashaka mengi, mara kwa mara alikuwa anatazama saa yake, na kisha kutazama upande wa mjini, ni wazi alikuwa anatarajia kuona mtu au gari likitokea upande huo….. hivi huyo mzee James atakubari mpango wa mheshimiwa, ebu tuone kitakacho tokea. basi… endelea kufwatilia mkasa huu wa #NYUMA_YA_MLANGO_WA_ADUI, inayo kujia hapa hapa jamii forums[/
[/QUOTE]
Aaah eddy,ndo kukatisha utamu katiHaya Sheba anataka kumshikia bastola Deus na sisi tunajua kuwa Dues hapendi tena bastola 🙄
Kesho nishtueni mapemaaaaa tuone ni nini kiliendelea
Mi nakushitua mapema kabisa hii shusha episodesHaya Sheba anataka kumshikia bastola Deus na sisi tunajua kuwa Dues hapendi tena bastola 🙄
Kesho nishtueni mapemaaaaa tuone ni nini kiliendelea
Aaah! Nikisubr matokeo bhana huko mlimanAaah eddy,ndo kukatisha utamu kati
Shukran mkuu acha niandae episode 2 nilete kisha nikajenge taifaMi nakushitua mapema kabisa hii shusha episodes
🪑Shukran mkuu acha niandae episode 2 nilete kisha nikajenge taifa