moneytalk
JF-Expert Member
- Jan 23, 2017
- 7,976
- 16,769
tutapitiwa na usingizi sasaYa kulalia naipika hapa
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
tutapitiwa na usingizi sasaYa kulalia naipika hapa
Daaah! Eti leo ndiyo naiona. Naweka alama, ili nikipata nafasi ya kuisoma, nisipate taabu ya kuitafuta!Tunaendelea Viongozi
KaribuuuDaaah! Eti leo ndiyo naiona. Naweka alama, ili nikipata nafasi ya kuisoma, nisipate taabu ya kuitafuta!
Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Karibu sanaKigongo kikali aiseeee
Mwendelezo lini tena?Karibu sana
Big up mkuuNYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA SITINI NA NNE
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247
TULIPOISHIA SEHEMU YA SITINI TATU: kiti ambacho angekiokota moneytalk au woodpecker24 wange nunua mtaa mzima na majumba na mali zote za mtaa na wakazi wa mtaa huo wangewaajili kulima mashamba, na kufanya kazi kwenye viwanda vyao, ambavyo wange vianzisha kwa fedha hiyo hiyo, pia fedha inayo bakia wangeinunua simba na ndio ingekuwa mwaka wao wa kwanza kuchukua club bingwa maana wangetumia fedha hiyo hiyo kuhonga marefa waibebe timu na Doctor G angeacha hiyo kazi akajenga hospital za kwake (hayo ni mawazo ya rafiki yangu Mduku aliyoyatoa siku alipokiona kile kiti cha King Elvis wa kwanza siku tulivyotembelea #mbogoland kwenye ndoa ya Radhia) endelea nayo ….
“Kuna jambo gani tena, au ni lile la askari kuacha kazi?” aliuliza malkia Vaselisa kwa sauti ya unyenyekevu, sauti ambayo mala nyingi huitumia anapohitaji kumuondoa mume wake toka kwenye mawazo ya kiunyonge, “hilo ni moja wapo maana leo nimengundua kuwa kuna baadhi ya askari waliacha jeshi kipindi cha vugu vugu la kundi la UMD, mmoja wao akiwa askari mtiifu na shujaa luten kanal Frank Nyati, alie muokoa mara kadhaa King Eugen wa 25, lakini pia nimegundua kuwa kuna dalili za kurudi kwa kundi la UMD, inawezekana wakina Frank Nyati wanaunda tena kundi hilo?” aliuliza Elvis, sasa akimtazama mke wake ambae pia alionekana kuvuta kumbu kumbu flani.
Uvutaji wa kumbu kumbu ambao ulimfanya achelewe kumjibu mfalme, ambae alimtazama mke wake kwa umakini mkubwa huku akisubiri jibu la mwanamke huyo, ambae kikawaida Elimu yake haikuwa kubwa sana, ila alikuwa na busara zilizo mzidi kimo, “hapa najaribu kuwaza hilo jina nimelisikia wapi halafu siyo muda mrefu” alisema malkia Vaselina huku akijaribu kuvuta kumbu kumbu zaidi, “Nyati…. nyati … Nyati, hoooo! sawa, huyo ni mtazania” alisema Vaselisa, alijaribu kupotezea habari ya huyo ya mtanzania alieitwa Nyati, “amefanyaje huyo mtazania?” aliuliza King Elvis, huku akitazama mke wake.
Mke wake ambae ukiachikia shuguri zake za kusimamia maswala ya jinsia na watoto pamoja na afya, katika nchi ile ya #mbogo_land, akisaidiana na mwanamama Thesilia Martin, mama yake Careen wa kwenye simulizi ya KIAPO CHA FUKARA hiyo ni baada ya kushindwa kuongoza peke yake, kutokana na Elimu ndogo aliyokuwa nayo Malkia huyo, ambae sasa anaendelea kupata Elimu ya chuo baada ya kushauriwa na mama mkwe wake yaani Malkia doctor Irene Simon wa kwenye simulizi ya UMEKOSEA LAKINI TAMU kwamba ajiendeleze Elimu ili awezekuongoza wizara hiyo, ambayo ni lazima kwa mke wa Mfalme.
Pia mwana huyo ambae pia ni mmoja kati ya waschana wadogo kupata kuwa wake wa viongozi wakubwa wanchi alikuwa anapenda sana kuperuzi mitandao ya kijamii ili kuijuwa dunia na kujifunza zaidi, “hukuwahi kusikia habari za Deus Nyati?” aliuliza Vaselisa kwa mshangao, “nisingekuuliza mke wangu, hebu nipe habari zake” aisema King Elivs na kujiweka sawa ili awezekupata habari za mtu huyo ambae mwanzo alihisi anaweza kuwa ndie Nyati ambae alitoweka nchini kwake.
Naam Malikia Vaselisa akaanza kueleza kisa cha askari mtanzania, alie waokoa mdoctor watatu, wa umoja wa mataifa huko nchini Congo na baadae kukutwa na hatia ya jaribio la ubakaji, akishinda kesi kwa kuonekana amesingiziwa na kwamba ulikuwa ni mpango wa IDFNALLU, lakini anaondolewa UN kwa kosa la kufanya jukumu nje ya mkataba na mwisho nchi yake inamfukuza kazi kwa kuliaibisha taifa, “bado sijafanya ujinga huo, hapo lazima ningevunja sheria za nchi yangu, kwa kumuacha askari aendelee na kazi” alisema King Elvis, mwishoni mwa hadithi toka mke wake, “pengine kuna askari wengi wa namna hii, hivyo hawahofii kumpoeza mmoja kwa heshima ya nchi” alisema Vaselisa ambae licha ya kuchanganya damu ya Mmakonde na mwarabu, lakini maisha yake kwa kiasi kikubwa aliishi Dar es salaam.
Waliongea mawili matatu juu ya Deus Nyati, kabla hawaja badili maongezi, pasipo mfalme kufahamu au kulijuwa jina la tatu la askari huyo, shujaa mwenye bahati mbaya.*********
Yap! saa kumi na moja kasoro gari la polisi, lilikuwa kwenye soko dogo maarufu kama mnadani pale kwa matius, njia ya kwenda Efatha, askari saba, wakiwa nyuma ya gari huku koplo Cheleji, akionekana akiwa amesimama kwenye kibaraza cha nyumba moja, pale pembeni ya barabara inayotenganisha nyumba kadhaa upande wa kushoto na soko likiwa upande wakulia mbele yake wakiwa mafundi wa kushona, tume zowea kuwaita mafundi cherehani, mnasema hamjaliona gari dogo jeusi jipya hivi, BMW likipita hapa?” aliuliza Cheleji, akionekana kuishiwa nguvu, baada ya kukosa kile alicho tegemea, “yaani kaka lingepita tunge liona, maana hapa yanapita magari machache sana na yote tumeyaona kama hilo lingepita nalo tungeliona tu” alisema mmoja kati ya wale fundi cherehani wa kiume alieonekana kuwa na umri mkubwa zaidi ya wote, aliekadiriwa kuwa na miaka hamasini na tano, “ok! sie tunaondoka ila kama mtakumbuka chochote au kuliona gari hilo mutatueleza maana tutapia baadae” alisema Koplo Cheleji, wakati anaaga na kundoka kuelekea kwenye gari.
Naam Koplo Cheleji akaingia kwenye gari ambalo wenzake walikuwa wanamsubiri, kisha gari likaondoka kuelekea barabara ya zamani ya Morogoro na walipoikuta wakafuata upande wa kuelekea picha ya ndege yaani kule ambako yule mwenzao aliliona BMW 7 likielekea.
Gari aina ya land rover mia na kumi, lilitembea taratibu huku wote wakiwa makini kutazama kushoto na kulia kama wangeweza kuliona BMW S7, lakini mpaka wanafika pale kwenye msitu, hawa kuwa wameliona gari lile wala dalili ya uwepo wa gari ilo.
Lakini wakati wanataka kukatiza kwenye njia ya kuingia kwenye ile nyumba iliyopo kwenye kichaka cha miti ya kupanda ghafla dereva akasimamisha gari, “afande naweza kuona kuna gari liliingia barabara hiyo njia hapo” alisema dereva wa lile gari la polisi, ambae alikuwa kule mbele ya gari na Cheleji hapo Cheleji nae akatazama kwenye sakafu ya barabara, inayoingia kwenye ile nyumba na kuona alama za tairi za gari akazifuatilia na kuziona zinatokea kwenye ile nyumba, “mh! mbona kama ni gari la ile nyumba” alisema Cheleji, huku anarudisha macho yake upande wa barabara lakini usawa wa sakafu ya barabara ambapo tairi za gari zilizo futika zilionekana kuvuka barabara, “lakini afande unadhani mwenyeji wa eneo hili anaweza kupitisha gari kwenye barabara hii?” aliuliza dereva, huku wakitazama tairi za gari zilizovuka upande wa pili wa barabara.
Naam! hapo nikama Koplo Cheleji alibaini jambo jipya, mh! hebu subiri kidogo, inawezekana hawa washenzi walishtukia kuwa wanafuatiliwa, wakaja kujibanza hapa na Mao alipopita tu wao wakarudi walikotoka na kubadili njia, kama huamini hebu kwanza uone” alisema Cheleji huku anafungua mlango wa gari na kushuka chini, kisha akaelekea kwenye ile nyumba ya kichakani, huku akimuacha dereva anaegesha gari pembeni ya barabara.
Cheleji alitembea kwa haraka kuifuata ile nyumba, huku anatazama kwa umakini alama zile za tairi za gari mpaka alipofika nazo kwenye ile nyumba, na kuziona zikiwa zimeishia ubavuni mwa nyumba, ile ambayo kiukweli ilikuwa kimya kiasi, japo walionekana kuku na bata wakizurula eneo lile la nyumba ile tulivu.
Cheleji akasogelea lango na kugonga hodi mara kadhaa, lakini hakupata mrejesho wowote toka ndani, akarudia tena na tena lakini mambo yakawa vile vile, Cheleji akiwa amekata tamaa ya uwepo wa wenyeji akageuka ili kuondoka, lakini kabla hajapiga hatua hata moja, akasikia michatoka ya vishindo vya mtu upande wa ndani, akiufuata mlango, Cheleji akasimama na kusikilizia kifuatacho.
Nikweli sekunde chache baadae, mlango ukafunguliwa akaibuka kijana mmoja wakati ya umri wa miaka kumi na tisa au ishirini, mwenye uso wa tabasamu na ukarimu, “karibu bro, pole sana maana nilikuwa na jiuliza hii hodi ni huku au?” alisema yule kijana, ambae alionekana wazi kuwa alikuwa ametoka kwenye kazi fulani ngumu, iliyomfanya achafuke nguo zake chakavu, alizokuwa amezivaa, “kwa hiyo ukashindwa kuacha upuuzi wako nakuja kusikiliza mara moja, ukaamua unichomeshe mahindi hapa mlangoni?” aliuliza Cheleji kwa sauti kavu isiyo na utani hata chembe, kiasi cha yule kijana mkarimu kujikuta akibadiri sura yake toka katika hali ya tabasamu, na kuwa katika hali ya uoga na wasi wasi.
Kijana anatazama barabarani, macho yake yana kutana na gari la polisi, hapo ndio anakosa kabisa uwezo wa kujiamini na kuzidi kujawa na wasi wasi,”samahani kaka nilikuwa ndani ya banda la kuku, nafanya usafi ndio maana sikuweza kusikia vizuri” alisema yule kijana kwa sauti ya kuombeleza….endelea…. kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unaoo kujia hapa hapa jamii forums
Nina njaa haloo ngoja nitafute mlo nijeMwendelezo lini tena?
Humu haijapostiwaga hiyoHadithi swafi. Hivi, kiapo cha fukara upatikana huku jf kweli?
Mbona mapema sana😃R.I.P sheba wanajf tulikupenda ila polisi wa mombo wamekupenda zaidi 😭😭
😅Mbona mapema sana😃