Abuu Dharr
JF-Expert Member
- Dec 28, 2017
- 2,911
- 3,016
..
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Weka hata moja tuianze siku yetu vyedi😃 ingawa siku izi naona inakuwa fupi fupi sijui kwann hata dah😅
🪑 ☕Wadau mume ongezeka ngoja niongeze episode
Salute kwako mkuuNYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA SITINI NA SABA
MTUNZI : Mbogo EDGAR
WHATSAPP : 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA SITINI SITA: Lakini ile wanakaa sawa tu, ghafla mita kama mia moja mbele yao, wakaliona gari la polisi, likiwa kati kati ya barabara limesimama kwa mtindo wa kukatiza barabara, yani kizuwizi huku polisi sita wakiwa wamesimama pembeni ya gari lile na bunduki mikononi mwao zikielekea kule waliko kuwa wanatokea wao, huku mmoja wao akiwa amesimama katika kati ya gari, yani ubavuni mwa gari amenyoosha mkono mmoja juu, ikiwa ni ishara ya kusimamisha gari lao, “washenzi wametupata” alisema Deus, huku anaanza kupunguza mwendo kwa nguvu kwaajili ya kusimama……….ENDELEA….
Wote wawili walitulia kimya, wakishuhudia gari likiendelea kusotesha tairi kwenye lami kwaajili ya kusimama, hata liliposimama, Deus alikuwa amefanya juhudi ya hali ya juu sana kulisimamisha gari lile pasipo kusababisha ajari.
Hapo Deus aliekuwa anawaza namna ya kumuokoa yule mschana, ili amfikishe sehemu aliyokusudiwa na yeye kupata malipo yake maana hakujua habari ya dhahabu ambayo msomaji unaifahamu, aliwatazama wale polisi ambao walikuwa wanalizunguka gari na bunduki zao mikononi, mitutu wameilekezea kwenye gari, “hivi uliwafanya nini hawa washenzi?” aliuliza Deus, kwa sauti ya upole kama vile hakuna kitu cha hatari mbele yao, “Deus, acha kuuliza maswali na ikiwezekana ufanye jambo tuondoke mahali hapa” alisema Sheba, huku anapeleka mkono chini ya seat yake.
Kabla Deus ajajibu kitu, tayari polisi mmoja alisha ufikia mlango wa dereva na kujaribu kufungua kitasa, lakini mlango haukufunguka, maana ulikuwa umefungwa kwa ndani, yule polisi akainua bunduki yake, akinyoosha usawa wa kioo cha mlango wa dereva, Deus akiwa anamtazama kwa umakini mkubwa, akamtazama mdomo wake ambao ulikuwa unatamka maneno ambayo yeye Deus, hakuyasikia, lakini niwazi alikuwa “anasema fungua mlango” hapo Deus, akafungua mkanda wa kiti na kutoa lock za milango, kisha akafungua mlango, ile anatokeza tu! akashikwa ukosi wa tisheti lake na kuvutwa nje, ukweli kutokana na uwezo alionao katika mazoezi, hakuyumba sana.
Lakini ile anakaa sawa, tayari Sheba alikuwa amesha toka ndani ya gari, sabamba na milipuko mfululizo ya risasi za bastora, kutahamaki tayari Sheba alikuwa amesha washusha askari wa nne, na kubakia wawili walio simama mmoja akiwa bila silaha yoyote na mwingine akiwa na SMG, karibu kabisa na Deus, lakini ile anainua tu, Deus akamuwahi haraka na kumpiga ngumi nzito ya kisogo, ambayo ilimpeleka chini kama mzigo na kumzimisha kabisa, huku yule mwingine akikimbilia kwenye gari, ambalo dereva alikuwa ndani yake, anajaribu kuwasha ili wakimbie, lakini kama vile amepungukiwa na akili, sheba akamimina risasi tatu, ambazo moja ilipiga kwenye bega la yule aliekuwa anakimbilia gari, huku moja ilipiga kwenye kioo cha gari, na kwenda kuchimba kwenye ubavu wa dereva, ambae tayari alikuwa amesha liwasha gari na kuingiza gia namba moja, ambapo kwa msukumo ule wa risasi, akajikuta akanakanyaga mafuta hovyo na kusonga mbele kwa fujo likiingia mtaroni na kushindwa kuendelea na safari, huku dereva aliekuwa anaugulia maumivu akiwa anajitaidi kujitoa kwenye gari.
“sipendi bunduki, hivi nani kakuambia utumie silaha muda huu?” aliuliza Deus, kwa sauti ambayo licha ya utulivu na utaratibu wake, lakini bado ilionyesha kuchukizwa na kitendo kile, “yaani watu saba, hii ni hatari sana tutalazimika kuwakimbia zaidi” alisema Deus akimtazama Sheba, ambae alikuwa anaichomeka bunduki yake kiunoni kwenye pindo ya suruali yake usawa wa kati ya makalio, “kwahiyo unadhani wangekuacha hawa, lazima wangetuuwa kisha kuondoka na gari letu” alijibu Sheba, huku anainama na kuokota mja kati ya SMG zilizoangushwa na wale polisi waliouwawa, “mh! kwanini watuuwe, nani kakuambia watatuuwa?, hebu ingia kwenye gari tuondoke hapa, kabla hatujakutwa” alisema Deus, huku anaingia kwenye gari.
Lakini sasa kabla hajafungu mlango akasikia mlipuko wa kwanza wa risasi, ile kutazama mbele yule jamaa aliekuwa anakimbia bila bunduki alikuwa hewani anaenda chini kama mzigo, huku damu nyungi sana zina vuja kichwani, ni wazi ilikuwa risasi iliyompata ilipiga kichwani, “we mwanamke acha upuuzi, huo ni sawa na ujambazi” alisema Deus, huku anashuka toka kwenye gari, macho yake yapo kwa Sheba, ambae alikuwa anaelekeza silaha kwenye gari la polisi, ambako yule dereva polisi, alikuwa anahangaika kushuka huku anaugulia risasi ya tumbo.
Fumba na kumbua, tayari risasi ilikuwa imesha toka kwenye mtutu wa SMG na kugonga kwenye kioo cha nyuma na kufanya kitawanyike, huku zikifuatia risasi nyingine tano mfurulizo, zilizo ambatana na milipuko yenye kelele mfano wa kiwanja cha majaribio ya shabaha, huku gari likiwa ndio ubao wa shabaha, risasi zilichakaza mwili wa yule askari, “sheba, unaniweka katika wakati mgumu, unadhani nitaishi vipi ndani ya nchi niliyo shiriki mauwaji ya wanausalama wake” alifoka Deus, huku anapokonya silaha toka kwa Sheba, “mbona mgumu kuelewa Deus, unadhani ni wanausalama hawa, hawa ni wanyang’anyi tu, wapo hapa kutuibia” alisema Sheba, huku anageuka na kurudi kwenye gari.
Wakati huo huo, yule askari alie pigwa ngumi ya kisogo, ndio alikuwa anazinduka, akanyoosha mkono taratibu kuchukuwa SMG, yake ili awatandike wakina Deus, lakini kwa bahati mbaya au nzuri Sheba akamuona, hapo haraka akachomoa bastora yake toka kiunoni na kumtandika yule jamaa, “pumbavu, ingia kwenye gari haraka” alisema Deus, huku anatupa ile SMG na kuanza kutembea kuelekea kwenye gari, “nakushauri uchome gari moto, ili kupoteza ushaidi” alisema Sheba, ambae sasa alikuwa anaingia ndani ya gari,
Hapo Deus akageuka kulitazama gari la polisi, halafu akamtazama Sheba, ambae pia alikuwa anamtazama, kisha akaanza kuziokota silaha zilizo kuwa zimezagaa pale chini na kuanza kuitupia ndani ya gari akibakiza moja tu.
Alipomaliza akarudi mita chache nyuma, toka lilipo gari la polisi halafu akaiweka SMG usawa wa bega na kulenga tank la mafuta*******
Wakati hayo yanaendelea, nje ya mji wa Mombo, wakati huo huo barabara hiyo hiyo, maeneo ya njia panda ya Sadan, lilionekana gari aina ya land rover diffender, mali ya jeshi la polisi, lenye askari saba nyuma yake, huku wawili yani Dereva na mwenzie mmoja wakiwa mbele, lilionekana liliembea kwa speed ya mia moja hamsini, kuelekea upande wa Mkata.
Ndani ya gari nyuma palionekana SMG nane zikiwa zimewekwa chini, yani kwenye sakafu ya gari lile ambalo lilibeba askari waliovalia nguo za kiraia pasipo kuzingatia unadhifu, wapo waliovaa tisht na jinsi, wapo waliovaa kodrai na shati za kadet, wengine walivalia kaptura za kaki, na makoti mafupi ya baridi, pia wengine walivalia kofia za sueta maarufu kama mzura.
Gari likukuwa linaenda kasi, ni kweli liilikuwa speed, japo kwa kuwa tumezowea speed ya BMW s7, tunaona kama vile gari hili halikuwa katika speed inayo paswa.
Hata walipo karibia Mkata, wakawaona polisi wenzao wakiwa wamesimama pembeni ya barabara pamoja na gari lao, wakionekana katika mshangao fulani, ni wazi muda mchache uliopita, walikuwa wameshuhudia kitu wasicho kitegemea, na wao hawakusimama, walipita na speed yao hiyo hiyo.
Hilo lilikuwa ni kundi la polisi wa Ulenje, walioongozwa na koplo Othman, wenyewe upenda kumwita Ochu, ambae mawazo na akili yake vilikuwa kwenye kulikamata gari aina BMW jeusi, ambalo aliamini kuwa muda wowote wanalifikia, hawakujuwa kuwa lilikuwa kilomita nyingi mbele yao na kila sekunde lilikuwa lina ongeza umbali katiyao.
Tukiachana na hao, tunaenda maeneo ya Msata, mita mia nne toka kwenye round about ya maungio ya barabara ya bagamoyo na chalinze, ambapo tunaweza kuliona gari kama lile la mbele, yani la polisi nalo likiwa na askari saba nyuma wawili mbele, likitembea kwa speed kuelekea upande wa Mkata, nalo pia lilikuwa katika speed kama ya lile la mwanzo, japo lenyewe lilikuwa lina fikia wakati lina vuka mpaka speed mia moja sitini.
Ili lilikuwa ni kundi la koplo Cheleji, ambae pia kama mwenzie akili na mawazo yake, yalikuwa juu ya kufanikisha kulikamata BMW, maana ukiachilia kujenga sifa na kuaminiwa na Ulenje, pia wangejipatia fedha nzuri sana, hawakujari wala kuwaza juu mwisho wa wale waliopo kwenye gari hilo, ambalo ingetakiwa warudi nalo dar, wao walicho jari nikutekeleza kile walicho tumwa, ambacho ni kuwauwa wote watakao kuwepo ndani ya gari na kurudi na gari na mzigo uliopo ndani yake.
Kwa kuweka kumbu kumbu sawa nikwamba, koplo Cheleji pekee ndie aliemuona Deus, akiingia kwenye gari, hivyo ndie mwenye kuweza kuitambua sura ya kijana huyo, japo haku fahamu wala kujuwa kuwa kijana yule aliemuona pale kiluvya madukani, akiingia kwenye gari lile BMW jeusi ndie askari aliekuwa anazungumziwa Mitandaoni…..…….ENDELEA kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
Ahsanta mkuu 🤠Salute kwako mkuu
Achia mzigo mkuu tuko machoMushalala? Au tuachie mzigo
ntakufinya ujue,tulale saa hizi tumekuwa watotoMushalala? Au tuachie mzigo
Achia mzigo mkuu tuko macho