Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 29
upande kuhakikisha usalama ndani ya nyumba hiyo.
Patricia akabaki akiwa ameduwaa tu, hakuamini kama hapa duniani kulikuwa na nyumba kubwa na nzuri kama ile. Bwawa kubwa la kuogelea, sehemu ya kupaki magari, sehemu iliyokuwa na mbuga ya wanyama, sehemu iliyokuwa na kiwanja cha mpira wa kikapu vilikuwa baadhi ya vitu vilivyokuwa vikionekana katika eneo la nyumba ile.
Hapo ndipo ambapo maisha ya Patricia yalitakiwa kuanzia. Moyoni mwake alitamani kumuita Martin na kisha kuishi nae ndani ya jumba hio la kifahari lakini kitu kama hicho kilionekana kuwa kama ndoto maishani mwake.
“I missed you my only daughter (Nilikukumbuka binti yangu pekee)” Bwana Thomson alimwambia Patricia huku akionekana kuwa na furaha.
Muda wote Bwana Thomson alikuwa akionekana kuwa na furaha. Patricia ndiye alikuwa binti yake pekee ambaye alikuwa akimpenda katika maisha yake, yeye ndiye alikuwa binti na mtoto pekee katika maisha yake. Alimthamini Patricia, alikuwa tayari kupoteza kitu chochote lakini si kumpoteza Patricia.
Baada ya wiki moja Patricia alitakiwa kuanza chuo. Bwana Thomson hakutaka mwanae akae hostel, alikuwa akitamani muda wote amuone. Alichokifanya ni kumpeleka katika chuo cha St’ Mariana ambacho kilikuwa kinachukua watoto wa watu wenye fedha tu na watu ambao walikuwa maarufu nchini Marekani.
Patricia akaanza katika chuo hicho huku akisoma na kurudi nyumbani kwao. Masomo ya Biashara ambayo alikuwa akiyachukua hayakuonekana kuwa magumu kwake kitu ambacho kilimfanya kuyafurahia kupita kiasi.
Mambo yakaanza kuonekana kubadilika. Uzuri ambao alikuwa nao Patricia ukaanza kumvutia kila mwanaume ambaye alikuwa akimwangalia chuoni hapo. Kila mvulana akatamani kuwa pamoja nae, uso wake na mchanganyiko wake wa rangi vilikuwa vitu ambavyo vilimvutia kila mtu.
Wavulana wakaanza kuanzisha ukaribu na Patricia, Patricia akazoeleka lakini kila alipokuwa akitongozwa na wavulana mbalimbali wala hakuwa radhi kuwakubalia. Bado kichwani mwake kulikuwa na mwanaume mmoja, moyo wake haukutaka kumsahau mvulana huyu. Alimpenda na alitamani aje kuishi nae hapo baadae lakini aliona kitu hicho kutokuwezekana kwa kuwa hakuwa
upande kuhakikisha usalama ndani ya nyumba hiyo.
Patricia akabaki akiwa ameduwaa tu, hakuamini kama hapa duniani kulikuwa na nyumba kubwa na nzuri kama ile. Bwawa kubwa la kuogelea, sehemu ya kupaki magari, sehemu iliyokuwa na mbuga ya wanyama, sehemu iliyokuwa na kiwanja cha mpira wa kikapu vilikuwa baadhi ya vitu vilivyokuwa vikionekana katika eneo la nyumba ile.
Hapo ndipo ambapo maisha ya Patricia yalitakiwa kuanzia. Moyoni mwake alitamani kumuita Martin na kisha kuishi nae ndani ya jumba hio la kifahari lakini kitu kama hicho kilionekana kuwa kama ndoto maishani mwake.
“I missed you my only daughter (Nilikukumbuka binti yangu pekee)” Bwana Thomson alimwambia Patricia huku akionekana kuwa na furaha.
Muda wote Bwana Thomson alikuwa akionekana kuwa na furaha. Patricia ndiye alikuwa binti yake pekee ambaye alikuwa akimpenda katika maisha yake, yeye ndiye alikuwa binti na mtoto pekee katika maisha yake. Alimthamini Patricia, alikuwa tayari kupoteza kitu chochote lakini si kumpoteza Patricia.
Baada ya wiki moja Patricia alitakiwa kuanza chuo. Bwana Thomson hakutaka mwanae akae hostel, alikuwa akitamani muda wote amuone. Alichokifanya ni kumpeleka katika chuo cha St’ Mariana ambacho kilikuwa kinachukua watoto wa watu wenye fedha tu na watu ambao walikuwa maarufu nchini Marekani.
Patricia akaanza katika chuo hicho huku akisoma na kurudi nyumbani kwao. Masomo ya Biashara ambayo alikuwa akiyachukua hayakuonekana kuwa magumu kwake kitu ambacho kilimfanya kuyafurahia kupita kiasi.
Mambo yakaanza kuonekana kubadilika. Uzuri ambao alikuwa nao Patricia ukaanza kumvutia kila mwanaume ambaye alikuwa akimwangalia chuoni hapo. Kila mvulana akatamani kuwa pamoja nae, uso wake na mchanganyiko wake wa rangi vilikuwa vitu ambavyo vilimvutia kila mtu.
Wavulana wakaanza kuanzisha ukaribu na Patricia, Patricia akazoeleka lakini kila alipokuwa akitongozwa na wavulana mbalimbali wala hakuwa radhi kuwakubalia. Bado kichwani mwake kulikuwa na mwanaume mmoja, moyo wake haukutaka kumsahau mvulana huyu. Alimpenda na alitamani aje kuishi nae hapo baadae lakini aliona kitu hicho kutokuwezekana kwa kuwa hakuwa