Simulizi: Sasha Mlinzi wa Nafsi - 1

Simulizi: Sasha Mlinzi wa Nafsi - 1

SASHA MLINZI WA NAFSI
SEASON 3
Sehemu ya..........47
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA SEASON 2
Ni vita nyingine kati ya Felix na Feisal anayejiandaa kuja mjini kimasomo lakini lengo lake kubwa ni kumtafuta ndugu yake Boaz….
Wakati huo pia ndiyo kwanza Sasha anajitafuta namna ya kumpata kijana David aliyebeba hatima ya mji wa ajabu ISRA….
Lakini Sasha hajui kama tayari Magnus ameshaagiza watu kuja kumteka na kumpeleka kwenye himaya yake kule kisiwani…..
Felix naye anajitoa ufahamu na kurudisha penzi lake kwa Tesha bila kujali baba yake Magnus atachukua hatua gani…..
Tesha bado yuko gizani hamfahamu ki undani mpenzi wake Felix….
Madam Husnata naye yuko mbioni kuuwasha moto…

SASA ENDELEA…

“Usijali Boaz kuwa mtulivu, ipo namna ya kutoka hapa lakini inahitaji umakini wa hali ya juu” Alisema David

“Unasema kweli….?’’

“Ndiyo, nakuhakikishia tutatoka hapa na utakuwa huru, utatoa pesa zako na kumsaidia mdogo wako Sikujua” David aliongea kwa kumaanisha.

“Kivipi jamaa yangu hebu nipe mwanga hata kidogo au mmeshapata namna alafu mpo kimya?” Boaz alizidi kumchimba David.

“Nimekwambia kuwa mtulivu Boaz wakati sahihi ukifika utajua kila kitu…”

“Sawa, ila nikwambie kitu bro… yani kama ukinisaidia kutoka humu nakuahidi kukupa nusu ya pesa zangu zilizopo kwenye akaunti”

“Usitegemee sana pesa ambazo hauko nazo mkononi, pengine huyo ndugu yako alishazitoa na kazitumia zote zikaisha…”

“Aaah! Wapi Feisal hawezi kufanya hivyo…” Alijibu Boaz, David akawa kimya. Kitendo cha Boaz kulitaja jina linalofanana na jina la kaka yake kilimfanya akumbuke mbali, lakini hakujua kuwa Feisal aliyetajwa na Boaz ndiyo Feisal huyo huyo ambaye ni kaka yake anayeamini kuwa alikwisha kufa kitambo. Wala hakutaka kuuliza zaidi akahisi Feisal anayetajwa na Boaz wakati huu wamefanana tu majina na marehemu kaka yake.

“Tutakutafuta tena kesho kuna mahali nataka twende….” Alisema David. Wakakubaliana hivyo na mwisho Boaz akaondoka akiwaacha David na Dayana wakiendelea na mazungumzo.

“Unafikiri ni sahihi kumshirikisha huyu bwana kwenye mpango wetu? Anatakiwa kuijua siri ya ile njia ya pangoni?” Aliuliza Dayana

“Yap sio mbaya, inatakiwa tuongezeke angalau tuwe watu watatu au wanne kama ikibidi. Huyu bwana anaonekana anashauku kubwa ya kutoroka humu bondeni hivyo atatufaa. Changamoto yake kubwa anapapara ila sio kesi tutamdhibiti” Alieleza David

“Okay sasa kwa nini umemwambia hadi kesho? Kwani si ulisema leo pia tunaenda kule pangoni?”

“Yap! Tunaenda ni lazima twende ila leo tutaenda mimi na wewe kwanza, bado hali haijatulia na hatuelewi ni nini kimempata Zungu…Tutawashirikisha hali ikitulia” Alisema David na mwisho wakakubaliana hivyo.
***

Usiku huu pia ulikuwa ni wasaa mzuri wa Felix na mpenzi wake Tesha kutoka kwa ajili ya mazungumzo muhimu. Ni muda mrefu ulikuwa umepita tangu wawili hawa walipotengana lakini leo kwa mara nyingine wamekutana na kuufungua upya ukurasa wa mahusiano yao baada ya misukosuko ya muda mrefu. Walikaa maeneo ya ufukweni mwa bahari nje ya hoteli moja ya kifahari iitwayo Night City Hotel ndani ya jiji la Dar es salaam. Waliutumia muda huo kujadili kwa kina mwenendo mzima wa mahusiano yao walikotoka na wanapokwenda huku kila mmoja akikiri kumpenda sana mwenzake. Felix hakuweka wazi ni kwanini kwa kipindi chote alikuwa akijitenga mbali na mpenzi wake, isipokuwa aliishia kumuomba msamaha kwa dhati na kuahidi hali hiyo kuto kujirudia tena. Tesha hakuwa na hiyana alimuelewa bila kujua kwa kufanya hivyo tayari mpenzi wake alikuwa amejiingiza kwenye vita kubwa na baba yake mzazi Magnus ambaye hatamani kuona mwanae anaingia kwenye mahusiano ya kimapenzi na binadamu.

“So Tesha unaweza kuniambia wewe na mama yangu mlijuana vipi?” Aliuliza Felix kwa makusudi akitaka kujua uhusiano uliopo kati ya Mama David ambaye ni mama yake wa kuigiza pamoja na mpenzi wake Tesha. Lakini kabla ya Tesha kujibu mara simu ya Felix iliita hii ilikuwa ni mara ya nne simu hii inaita lakini Felix hakuipokea.

“kwa nini hupokei simu yako Felix?”

“Aah! Achana nayo, nimetenga muda kwa ajili yako sitaki kujichanganya na mambo mengine…” Alieleza Felix huku akiifunika simu yake juu ya meza hakutaka Tesha aone jina la mpigaji, alikuwa ni Madam Husnata anampigia mfululizo.

“Ni wale watu uliokuwa ukibishana nao wakati ule nyumbani kwa mama?” Aliuliza Tesha

“Hapana, Tesha achana na hizi habari hebu nambie wewe na mama mlijuana vipi”

“I was about to tell you Felix, unajua mdogo wako yupo kwenye matatizo makubwa sana hata mama yako hajui nimemficha kwa sababu ya hali yake, bado ni mgonjwa”

“Mdogo wangu yupi?”

“David, hujui kama unamdogo wako anaitwa David?”

“Aah! okay David, lakini mama kaniambia kuwa amesafiri… anashida gani kwani?”

“Nilimjua mama yako kupitia David, mimi na David ni marafiki…”

“Marafiki? Wewe na David…?”

“Yes just a friend…”

“Enhe…”

“Juzi juzi hapa nilikuwa naye pale mgahawa wa Zonna karibu na hospitali aliyokuwa amelazwa mama, niliondoka nikamuacha, lakini kwa bahati mbaya niliisahau pochi yangu pale wakati narudi kuichukua nikakutana na tukio la ajabu sana, David pamoja na watu wengine wawili walitekwa na majambazi ambao sura zao walikuwa wamezifunika kwa kuvaa helmet zenye vioo vyekundu, waliwabeba mateka kwenye gari na kuondoka nao haraka. Inavyoonekana hawa watekaji wapo kwa muda mrefu na polisi wamekuwa wakiwafuatilia kwa siri sana bila mafaniko. Mpaka sasa haijulikani ni wapi David pamoja na mateka wengine wamepelekwa.…” Tesha alieleza kwa hisia sana.

Zilikuwa ni habari zilizomshtua kwa kiasi kijana Felix, kwa maelezo aliyoyatoa Tesha yalitosha kabisa kumfanya aelewe kuwa watekaji hawakuwa wengine bali ni kikosi hatari cha baba yake chini ya kundi hatari la kigaidi MG Family kwani hata yeye pia aliwahi kuifanya kazi hiyo ya utekaji.

“… kwa hiyo David ametekwa na baba, kwa hiyo yupo kwenye lile bonde….”Aliwaza Felix

“Mbona kimya Felix huna cha kusema kuhusu mdogo wako?”

“Najaribu kufikiri nini cha kufanya, kwani polisi wao wanasemaje?”

“Yule askari wa kike aliyekukamata pale airport asubuhi ndio anafuatilia kesi hii, hakuna cha msingi walichokipata hadi wakati huu… Bado wanaendelea kufanya siri na watu mtaani wanaendelea kupotea…”

“Sawa nitajua cha kufanya muhimu endelea kukaa kimya usimwambie mama…”

“Sawa but nahitaji sana David arudi haraka, he is innocent, he is more than friend to me…” Alisema Tesha kauli iliyomfikirisha sana Felix akahisi lazima kuna kitu kilikuwa kinaendelea kati ya hao wawili. Na hapo ndipo alizikumbuka zile picha alizotumiwa wakati akiwa marekani. Ni picha zilizomuonyesha mpenzi wake Tesha akiwa amekaa na kijana mmoja katika mgahawa wa Zonna. Alipounganisha matukio pamoja na maelezo ya Tesha akajua kabisa kumbe yule kijana kwenye zile picha alikuwa ni David.

“Kama ni David aliyekuwa anataka kunivurugia mahusiano yangu na Tesha basi akae akijua hana bahati, nitammaliza kule kule bondeni kwa baba…” Aliwaza Felix

“Umesemaje…?” Aliuliza Tesha

“Hm kwani nimeongea…?”

“Mimi? Nimesemaje?”

“Sijakusikia ndio maana nauliza…”

‘’Hapana sijasema kitu…”

“Hmm! Haya…”

Baada ya mazungumzo ya muda mrefu hatimae Tesha na Felix walitoka tayari kurudi vyumbani katika hoteli hiyo Nigt City Hotel, ilikuwa ni siku ambayo kila mmoja alikuwa akiisubiri kwa hamu kubwa. Siku ambayo Tesha na Felix watalala katika kitanda kimoja huku kila mmoja akionekana kufurahia uwepo wa mwenzake.

Kulikuwa na umbali mrefu kiasi kutoka pale ufukweni walipo Felix na Tesha hadi kulifikia jengo la hoteli hiyo ingawa eneo lote hili lilikuwa ndani ya uzio wa hoteli ya Night city. Felix na Tesha walitembea taratibu wakiwa wameshikana mikono yao kwa mahaba mazito. Lakini katika hali ya kushangaza chini ya mti mmoja mkubwa usio asili(pambo) jirani kabisa na eneo watakalopita Felix na Tesha walionekana vijana wanne kila mmoja akiwa na pikipiki yake. Wote walikuwa wamevalia mavazi meusi kuanzia juu mpaka chini, wakawa wanawatazama Felix na Tesha wakija taratibu. Haikujulikana ni vipi vijana hao wameweza kuingia na pikipiki zao mpaka ndani ya maeneo ya hoteli hiyo maarufu tena yenye ulinzi mkali.
Wakati Felix na Tesha wakiwa wamekaribia kuwafikia pale walipo vijana hao walichukua vitambaa vyeusi wakajifunga kuziba nyuso zao na baada ya hapo wakavaa helmet tayari kwa kazi.
****

Wakati tukio hilo likiendelea pale hotelini upande wa pili katika kisiwa cha Magnus, David na Dayana walitoka tena kwa mara nyingine kuelekea kule pangoni kama walivyokubaliana. Lakini safari hii wakiwa wamechukua tahadhari kubwa, walitembea na kufuata njia ile ya pango hadi walipofika eneo lile lenye uwazi uliozibwa na jiwe kubwa, wakalitoa.

“Ile kamba iko wapi?” Aliuliza David, Dayana aliitafuta ile kamba mahali ambapo aliihifadhi kisha akampatia David huku akimtazama kwa macho ya wasiwasi, hakuwa na uhakika kama David ataweza kufanya lolote kutokana na lile tatizo lake la kiafya alilomweleza. Lakini ajabu David alionekana kuvaa ujasiri wa ajabu, alikuwa amedhamiria kufanya lolote analoliweza ili kuhakikisha wanatoka kwenye mateso hayo, na hii ndiyo ahadi aliyompatia rafiki yake Zungu ambaye alijitoa sadaka kwa ajili yao.

David aliifunga ile kamba kwenye jiwe vizuri kisha akaidondosha chini kule barabarani.

“Baki hapa, mimi nitashuka hadi chini, nitaenda hadi kule ufukweni kukagua mazingira kisha nitarudi hapa” Alisema David

“Hapana tunaenda wote David, huwezi kwenda mwenyewe ni hatari…”

“Utabaki hapa Dayana nisikilize mimi, kama wote tutashuka chini ni nani ataitoa hii kamba? Itabaki hapa inaning’inia? Huoni kama ni hatari tunaweza kukamatwa kirahisi, usijali nitakuwa salama sawa mama…”
Alieleza David huku akiinua mkono wake na kumshika Dayana shavuni upande wa kushuto. Hakujua kwa kufanya hivyo tayari anaziamsha upya hisia za Dayana ambaye alijikaza kwa muda mrefu tangu pale aliposukumwa na David hakutaka kujiaibisha tena mbele ya mwanaume huyo.

“Sawa basi nenda..” Alisema Dayana huku akiutoa mkono wa David haraka

“Good, umekubali sasa…” Alisema David safari hii akimfinya Dayana shavuni.

“Nenda David muda unakwenda…” Dayana akasisitiza, mwisho wakakubaliana hivyo.

David alipiga hatua na kusogea karibu na ule uwazi ili aweze kushuka chini kupitia ile kamba, ili kuwa ni kazi ngumu mno kwake kutokana na tatizo lake la saikolojia (Acrophobia). Dayana akawa anamtazama kwa hofu akihisi kabisa itakuwa ngumu kwa David na pengine anaweza kuzimia kama ilivyokuwa mwanzo.
***

Upande wa pili wakati Felix na Tesha wakizidi kusogea, ghafula wote walishtushwa na milio ya pikipiki zikiwashwa kwa pamoja.

“Felix ….” Tesha aliita kwa hofu kubwa

“Ni nini?”

“Hata mimi sielewi…”

JE, HAWA NI AKINA NANI?
WANATAKA NINI?
VIPI KUHUSU DAVID, ATAWEZA?

ITAENDELEA….
 
KUPATA SIMULIZI NYINGINE YA SAUL DAVID, BONYEZA HAPA [emoji116][emoji116][emoji116]
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
SEASON 3
Sehemu ya...........48
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA…….
Upande wa pili wakati Felix na Tesha wakizidi kusogea, ghafula wote walishtushwa na milio ya pikipiki zikiwashwa kwa pamoja.

“Felix ….” Tesha aliita kwa hofu kubwa…

SASA ENDELEA…
Mara ghafula kufumba na kufumbua waliona pikipiki moja ikija kwa kasi kutokea mbele yao. Dereve alikuwa amenyoosha usukani kuwaelekea wao pale walipo. Walipokwepa kusogea kulia Dereva naye akakunja kona kulia waliporudi kushoto naye akanyonga usukani kuwafuata, ni wazi dereva wa pikipiki hiyo alikuwa amekusudia kuwagonga.

“Felix…..” Tesha aliita kwa hofu

“Kaa nyuma yangu Teshaaaa…..” Felix alipaza sauti, akamvuta Tesha nyuma yake kwa nguvu kisha yeye akasimama mbele, uso kwa uso akawa anatazamana na taili la mbele la pikipiki hiyo. Dereva akiwa amebakiza hatua kama mbili kumfikia Felix mara alikunja kona kwa kasi kwenda kushoto, badala ya kumgonga akaishia kumparaza Felix katika bega na mguu wake upande wa kulia, Felix akaanguka chini akiwa na maumivu makali.

“Felix….jamani msadaaaa….msaaaada” Tesha alipaza sauti huku akisogea kujaribu kumuinua Felix pale chini.

“Usijali Tesha niko salama…” Felix aliongea akijikaza kiume na kushika bega lake, alikuwa amejeruhiwa na taratibu damu yenye rangi ya ajabu ikawa inamtoka. Sasa akawa na mtihani mwingine wa kuficha jeraha lake ili Tesha asije gundua siri yake kubwa ambayo katu hakuwa akitamani mwanamke wake aijue.
Mara wakasikia tena muungurumo mkali wa pikipiki, ajabu yule dereva baada ya kwenda umbali wa kama hatua ishirini hivi, alikata kona kibabe sana huku taili la nyuma likiserereka kiasi cha kufanya vumbi jingi kutimka hewani, alionekana ni mtaalamu mno wa kucheza na pikipiki.

“Anakuja tena….” Alisema Tesha,hofu ikiwa imemjaa mara dufu, baada ya yule mtu mwenye pikipiki kugeuka kwa mara nyingine alianza kuwafuata Felix na Tesha pale walipo kwa kasi ileile kama mwanzo. Tofauti na walivyo tegemea, safari hii hakuwa peke yake bali waliongezeka wengine na kufanya idadi yao kuwa wanne, kila mmoja akiwa na pikipiki yake. Mmoja akawa anakuja kutokea mbele mwingine kutokea nyuma mwingine kushoto na mwingine wa mwisho anakuja kutokea kulia.
Hali hii ikampa ugumu hata Felix ambaye tayari alishasimama kiume kujaribu kukabiliana na yule anaekuja kutokea mbele yao lakini ghafula wanaongezeka na kuwa wanne. Sasa akawa hana la kufanya akaishia kumshikilia mpenzi wake Tesha huku akijaribu kumkinga kutoka pande zote asidhurike lakini haikuwa rahisi kihivyo. Mwisho wale watu walifika kwa kasi wakapita na kupishana kama upepo, kwa mara nyingine Felix akajikuta anapigwa vikali na pembe ya usukani katika ubavu wake wa kulia akaanguka chini akiwa na maumivu makali mno.
Felix alipokuja kutahamaki akawaona wale jamaa wenye pikipiki wakipotelea gizani na wala Tesha hakuwepo pembeni yake, tayari walishamchua na kuondoka naye kama vile ambavyo kifaranga hunyakuriwa na mwewe.

“Teshaa………” Felix aliita huku akijizoazoa na kusimama akajaribu kukimbia kuwafukuzia wale watu lakini hakufika mbali akaanguka, akasimama tena huku akiwa ameshikiria bega lake mahali alipojeruhiwa, baada ya hatua mbili akaanguka tena.

“Tesha…Tesha …Teshaaaaa….” Aliita Felix akiwa amelala chali na kutazama juu mawinguni. Kijana huyu alikuwa kwenye hali mbaya mno kwa sasa, moyo wake ulimuuma isivyo na mfano. Ni kwa mara ya kwanza anaufungua upya ukurasa wa mahusiano yake yeye na mrembo Tesha lakini hata nafasi ya kulala naye usiku mmoja hajapata tayari penzi lao linakutana na misukosuko mikali.

Wakati akiwa amelala pale chini asijue cha kufanya mara simu yake ikaita tena. Felix alikurupuka akakaa chini mchangani kisha akaitoa simu yake mfukoni akatazama namba ya mpigaji alikuwa ni yule yule Madam Husnata.

“Fuc*** bila shaka ni wewe umefanya hivi…” Alisema Felix akiwa ameuma meno yake kwa hasira kisha akapokea simu na kuiweka sikioni.

“Najua uko hapa Night City Hotel Felix, kabla sijaharibu mambo njoo chumba namba 204 utanikuta…. una dakika 5 tu na ninaanza kuzihesabu kuanzia sasa” Sauti nyororo ya Madam Husnata ilisikika kutoka upande wa pili wa simu kisha ikakatwa. Mwanamke huyu kutoka MG Family alionekana akiwa amelala kitandani ndani ya chumba kimoja chenye kila aina ya fahari, Madam Husnata alilala kitandani hapo akiwa mtupu kama alivyozaliwa. Baada ya kukata simu alichukua glasi yenye kinywaji ndani yake, kisha akanywa fundo moja na kuirudisha. Sasa akawa anautazama mlango wa chumba chake huku uso wake ukionekana kujawa na tabasamu.

“Pumbavuu umenigusa pabaya Hustana, leo ndio utanijua mimi ni nani, haki ya Mungu naapa….” Alisema Felix kisha akainuka na kuanza kupiga hatua ndefu ndefu kuelekea lango la kuingilia ndani ya jengo kuu la hoteli hiyo. Njiani Felix anakutana na walinzi watatu wa hoteli hiyo wakija mkukumkuku.

“Bosi tumesikia makelele yakitokea upande huu vipi kwema? Haujaona chochote?” Aliuliza mlinzi mmoja lakini Felix hakujibu kitu, akapita katikati yao akaenda zake, akawaacha walinzi hao wakimsindikiza kwa macho na mwisho wakatazamana wenyewe kila mmoja akiwa na maswali yasiyo na majibu.
****

Ingawa ni kwa taabu sana lakini amini usiamini David alifanikiwa kushuka hadi chini, akakanyaga ardhi ya barabara ile inayokatiza chini ya mlima kutokea ufukweni hadi kule ilipo himaya ya Magnus. Barabara ambayo kwa kawaida huwa iko bize wakati wote, masaa 24.

“Oooh! Asante Mungu” Alisema Dayana akiwa kule juu pangoni na haraka akaanza kuivuta ile kamba ambayo David aliitumia kushuka. Baada ya kumaliza kuipandisha juu Dayana na David walipungiana mikono na ikiwa ni ishara ya kutakiana heri katika jukumu hilo zito la kujaribu kuitoroka himaya ya Magnus.

David alivuta pumzi ndefu na baada ya hapo akaanza kupiga hatua kusogea mbele hali akiwa na tahadhali kubwa. Miale ya moto iliyokuwa imetundikwa katika kuta za barabara hiyo ilimsaidia David kuona alikotoka na anapokwenda pia. Dayana aliendelea kumsindikiza kwa macho akiwa kule juu pangoni hadi pale David alipopotea kwenye upeo wa macho yake.

“Uuuhu!!….easy easy Dayana, everything will be fine….tutatoka hapa” Dayana alijisemea mwenyewe huku akijipiga piga kifuani akijaribu kuutuliza moyo wake uliokuwa ukidunda kwa kasi wakati huo.

Ni kama vile Dayana alijua kuna hatari inakwenda kutokea kwani ile anamaliza tu kuzungumza neno lake la mwisho mara anasikia muungurumo wa gari na alipotazama chini akaona msafara wa gari nne zikipita kwenye ile barabara kuelekea kule kule alikoelekea David muda mfupi uliopita.

“Shiiiit…” Alisema Dayana, tayari mambo yalikuwa karibu kuharibika kwa mara nyingine.
******

Upande wa pili ndani ya hoteli ya kifahari Night City Hotel katika ghorofa ya kumi na moja, mlango wa lifti ulionekana ukifunguka akatoka Felix akiwa anapiga hatua ndefu ndefu huku uso wake ukiwa umekunjamana kwa hasira, alitembea haraka na mwisho akasimama mbele ya mlango wa chumba kimoja, chumba namba 204. Ndani ya chumba hicho alikuwepo Madam Husnata ambaye tayari alishahisi kuna mtu mlangoni, tabasamu lake likazidi kuongezeka.

ITAENDELEA….
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

Simulizi hii ni Tsh 1000 tu lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina Saul au Airtel money namba 0788967317 jina Saul
Kisha njoo WhatsApp namba hzo hzo
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
SEASON 3
Sehemu ya...........48
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA…….
Upande wa pili wakati Felix na Tesha wakizidi kusogea, ghafula wote walishtushwa na milio ya pikipiki zikiwashwa kwa pamoja.

“Felix ….” Tesha aliita kwa hofu kubwa…

SASA ENDELEA…
Mara ghafula kufumba na kufumbua waliona pikipiki moja ikija kwa kasi kutokea mbele yao. Dereve alikuwa amenyoosha usukani kuwaelekea wao pale walipo. Walipokwepa kusogea kulia Dereva naye akakunja kona kulia waliporudi kushoto naye akanyonga usukani kuwafuata, ni wazi dereva wa pikipiki hiyo alikuwa amekusudia kuwagonga.

“Felix…..” Tesha aliita kwa hofu

“Kaa nyuma yangu Teshaaaa…..” Felix alipaza sauti, akamvuta Tesha nyuma yake kwa nguvu kisha yeye akasimama mbele, uso kwa uso akawa anatazamana na taili la mbele la pikipiki hiyo. Dereva akiwa amebakiza hatua kama mbili kumfikia Felix mara alikunja kona kwa kasi kwenda kushoto, badala ya kumgonga akaishia kumparaza Felix katika bega na mguu wake upande wa kulia, Felix akaanguka chini akiwa na maumivu makali.

“Felix….jamani msadaaaa….msaaaada” Tesha alipaza sauti huku akisogea kujaribu kumuinua Felix pale chini.

“Usijali Tesha niko salama…” Felix aliongea akijikaza kiume na kushika bega lake, alikuwa amejeruhiwa na taratibu damu yenye rangi ya ajabu ikawa inamtoka. Sasa akawa na mtihani mwingine wa kuficha jeraha lake ili Tesha asije gundua siri yake kubwa ambayo katu hakuwa akitamani mwanamke wake aijue.
Mara wakasikia tena muungurumo mkali wa pikipiki, ajabu yule dereva baada ya kwenda umbali wa kama hatua ishirini hivi, alikata kona kibabe sana huku taili la nyuma likiserereka kiasi cha kufanya vumbi jingi kutimka hewani, alionekana ni mtaalamu mno wa kucheza na pikipiki.

“Anakuja tena….” Alisema Tesha,hofu ikiwa imemjaa mara dufu, baada ya yule mtu mwenye pikipiki kugeuka kwa mara nyingine alianza kuwafuata Felix na Tesha pale walipo kwa kasi ileile kama mwanzo. Tofauti na walivyo tegemea, safari hii hakuwa peke yake bali waliongezeka wengine na kufanya idadi yao kuwa wanne, kila mmoja akiwa na pikipiki yake. Mmoja akawa anakuja kutokea mbele mwingine kutokea nyuma mwingine kushoto na mwingine wa mwisho anakuja kutokea kulia.
Hali hii ikampa ugumu hata Felix ambaye tayari alishasimama kiume kujaribu kukabiliana na yule anaekuja kutokea mbele yao lakini ghafula wanaongezeka na kuwa wanne. Sasa akawa hana la kufanya akaishia kumshikilia mpenzi wake Tesha huku akijaribu kumkinga kutoka pande zote asidhurike lakini haikuwa rahisi kihivyo. Mwisho wale watu walifika kwa kasi wakapita na kupishana kama upepo, kwa mara nyingine Felix akajikuta anapigwa vikali na pembe ya usukani katika ubavu wake wa kulia akaanguka chini akiwa na maumivu makali mno.
Felix alipokuja kutahamaki akawaona wale jamaa wenye pikipiki wakipotelea gizani na wala Tesha hakuwepo pembeni yake, tayari walishamchua na kuondoka naye kama vile ambavyo kifaranga hunyakuriwa na mwewe.

“Teshaa………” Felix aliita huku akijizoazoa na kusimama akajaribu kukimbia kuwafukuzia wale watu lakini hakufika mbali akaanguka, akasimama tena huku akiwa ameshikiria bega lake mahali alipojeruhiwa, baada ya hatua mbili akaanguka tena.

“Tesha…Tesha …Teshaaaaa….” Aliita Felix akiwa amelala chali na kutazama juu mawinguni. Kijana huyu alikuwa kwenye hali mbaya mno kwa sasa, moyo wake ulimuuma isivyo na mfano. Ni kwa mara ya kwanza anaufungua upya ukurasa wa mahusiano yake yeye na mrembo Tesha lakini hata nafasi ya kulala naye usiku mmoja hajapata tayari penzi lao linakutana na misukosuko mikali.

Wakati akiwa amelala pale chini asijue cha kufanya mara simu yake ikaita tena. Felix alikurupuka akakaa chini mchangani kisha akaitoa simu yake mfukoni akatazama namba ya mpigaji alikuwa ni yule yule Madam Husnata.

“Fuc*** bila shaka ni wewe umefanya hivi…” Alisema Felix akiwa ameuma meno yake kwa hasira kisha akapokea simu na kuiweka sikioni.

“Najua uko hapa Night City Hotel Felix, kabla sijaharibu mambo njoo chumba namba 204 utanikuta…. una dakika 5 tu na ninaanza kuzihesabu kuanzia sasa” Sauti nyororo ya Madam Husnata ilisikika kutoka upande wa pili wa simu kisha ikakatwa. Mwanamke huyu kutoka MG Family alionekana akiwa amelala kitandani ndani ya chumba kimoja chenye kila aina ya fahari, Madam Husnata alilala kitandani hapo akiwa mtupu kama alivyozaliwa. Baada ya kukata simu alichukua glasi yenye kinywaji ndani yake, kisha akanywa fundo moja na kuirudisha. Sasa akawa anautazama mlango wa chumba chake huku uso wake ukionekana kujawa na tabasamu.

“Pumbavuu umenigusa pabaya Hustana, leo ndio utanijua mimi ni nani, haki ya Mungu naapa….” Alisema Felix kisha akainuka na kuanza kupiga hatua ndefu ndefu kuelekea lango la kuingilia ndani ya jengo kuu la hoteli hiyo. Njiani Felix anakutana na walinzi watatu wa hoteli hiyo wakija mkukumkuku.

“Bosi tumesikia makelele yakitokea upande huu vipi kwema? Haujaona chochote?” Aliuliza mlinzi mmoja lakini Felix hakujibu kitu, akapita katikati yao akaenda zake, akawaacha walinzi hao wakimsindikiza kwa macho na mwisho wakatazamana wenyewe kila mmoja akiwa na maswali yasiyo na majibu.
****

Ingawa ni kwa taabu sana lakini amini usiamini David alifanikiwa kushuka hadi chini, akakanyaga ardhi ya barabara ile inayokatiza chini ya mlima kutokea ufukweni hadi kule ilipo himaya ya Magnus. Barabara ambayo kwa kawaida huwa iko bize wakati wote, masaa 24.

“Oooh! Asante Mungu” Alisema Dayana akiwa kule juu pangoni na haraka akaanza kuivuta ile kamba ambayo David aliitumia kushuka. Baada ya kumaliza kuipandisha juu Dayana na David walipungiana mikono na ikiwa ni ishara ya kutakiana heri katika jukumu hilo zito la kujaribu kuitoroka himaya ya Magnus.

David alivuta pumzi ndefu na baada ya hapo akaanza kupiga hatua kusogea mbele hali akiwa na tahadhali kubwa. Miale ya moto iliyokuwa imetundikwa katika kuta za barabara hiyo ilimsaidia David kuona alikotoka na anapokwenda pia. Dayana aliendelea kumsindikiza kwa macho akiwa kule juu pangoni hadi pale David alipopotea kwenye upeo wa macho yake.

“Uuuhu!!….easy easy Dayana, everything will be fine….tutatoka hapa” Dayana alijisemea mwenyewe huku akijipiga piga kifuani akijaribu kuutuliza moyo wake uliokuwa ukidunda kwa kasi wakati huo.

Ni kama vile Dayana alijua kuna hatari inakwenda kutokea kwani ile anamaliza tu kuzungumza neno lake la mwisho mara anasikia muungurumo wa gari na alipotazama chini akaona msafara wa gari nne zikipita kwenye ile barabara kuelekea kule kule alikoelekea David muda mfupi uliopita.

“Shiiiit…” Alisema Dayana, tayari mambo yalikuwa karibu kuharibika kwa mara nyingine.
******

Upande wa pili ndani ya hoteli ya kifahari Night City Hotel katika ghorofa ya kumi na moja, mlango wa lifti ulionekana ukifunguka akatoka Felix akiwa anapiga hatua ndefu ndefu huku uso wake ukiwa umekunjamana kwa hasira, alitembea haraka na mwisho akasimama mbele ya mlango wa chumba kimoja, chumba namba 204. Ndani ya chumba hicho alikuwepo Madam Husnata ambaye tayari alishahisi kuna mtu mlangoni, tabasamu lake likazidi kuongezeka.

ITAENDELEA….
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

Simulizi hii ni Tsh 1000 tu lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina Saul au Airtel money namba 0788967317 jina Saul
Kisha njoo WhatsApp namba hzo hzo
Hi Nini Sasa Kaka.

Sentensi mbili tatu tu?

Kama hukuwa tayari ungeacha Hadi baadae
 
Kipande kizima kimeelezea Pikipiki tu ilivyomgonga Felix [emoji23][emoji23][emoji23]
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
SEASON 3
Sehemu ya.........49
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA……
Felix alitembea haraka na mwisho akasimama mbele ya mlango wa chumba kimoja, chumba namba 204. Ndani ya chumba hicho alikuwepo Madam Husnata ambaye tayari alishahisi kuna mtu mlangoni, tabasamu lake likazidi kuongezeka.

SASA ENDELEA…
****
Upande wa pili David aliendelea kusonga mbele akipita katika ile barabara iliyochimbwa chini ya ardhi mlimani, baridi ilikuwa ni kali mno na usisahau kuwa David pamoja na mateka wengine wote waliishi siku zote wakiwa wamevaa nguo za ndani pekee, hakika maisha yalikuwa ni magumu mno kwa upande wao.
Mpaka sasa tayari David alishatembea umbali mrefu na sasa alikuwa anakaribia kufika ufukweni ndipo hapo akasikia muungurumo wa gari zaidi ya moja kutokea nyuma yake.

“Wanakuja….” David aliwaza wakati huo akili yake ikifanya kazi upesi kutafuta namna ya kufanya ili asiweze kuonekana. Kwa jinsi barabara ilivyo hakukuwa na namna ya yeye kujificha uamzi pekee ilikuwa ni kwenda mbele au kurudi nyuma, David akachagua kwenda mbele. Alianza kukimbia kwa kasi kusonga mbele huku ule msafara wa gari nne nyuma yake nao ukiendelea kumkaribia. Kilichomsaidia David ilikuwa ni kona nyingi za barabara hiyo, laiti kama ingekuwa imenyooka moja kwa moja basi wangeweza kumuona hata wakiwa bado wako mbali.

Hakika David alikuwa mwanariadha mzuri, ndani ya dakika mbili pekee tayari kijana huyu alikuwa ametoboa na kutokea upande wa pili wa barabara kule ufukweni.
Wakati David anafika ufukweni mara alisimama ghafula baada ya kuona jambo ambalo hakulitegemea mbele yake. Kulikuwa na meli kubwa imetia nanga kwenye fukwe za bahari huku watu kadhaa wakionekana wakishusha mizigo kutoka ndani meli hiyo.

Kwa bahati nzuri hakuna aliyemuona David ambaye alirudi nyuma haraka na kujificha kwenye kuta za barabara. Sasa akawa anapiga hesabu za haraka haraka afanye nini, mbele yake kuna watu ambao watamuona kama atasogea zaidi lakini pia kama ataendelea kubaki pale alipo bado ni hatari kwa sababu nyuma yake kuna msafara wa gari nne zinakuja.

David alibaki amesimama pale alipo asijue cha kufanya, laiti kama kungekuwa na giza totoro pale ufukweni pengine ingemsaidia David kukimbia pasipo kuonekana, lakini ndio kwanza mwezi ulikuwa umeshamiri pande zote na wala hakukuwa na haja ya kuwasha taa kwa vijana waliokuwa wanashusha mzigo kutoka melini.

Hatimae David aliona mwanga wa taa za zile gari zilizokuwa nyuma yake, sasa gari hizo zilikuwa karibu kabisa kumfikia, alipotazama mbele akaona wale wabebaji wa mizigo wote wameingia ndani ya meli, akajua wazi haitochukua sekunde nyingi watatoka, haraka David alikiambia kwa kasi kuelea mahali palipokuwa na mizigo inayoshushwa kutoka melini. David alifika akafunua sanduku moja kubwa akaingia ndani yake na kisha akalifunika, kufumba na kufumbua tayari ule msafara wa gari nne ulifika na kufunga breki pale ufukweni.

Hii ndio ikawa ponepone kwa kijana David, lile sanduku aliloingia lilikuwa na vitundu vidogo vidogo vilivyomuwezesha kupumua lakini pia kupitia vitundu hivyo David aliweza kuona kila kinachoendelea pale ufukweni.

Katika gari la kwanza David alimuona mzee mmoja mweusi mwenye nywele na ndevu nyingi zenye rangi nyeupe akishuka taratibu huku nyuma yake akiwa ameongozana na walinzi sita. Mzee huyo alivalia kanzu nzito nyekundu na mkononi mwake alishikiria mkokongojo. Haikuwa mara ya kwanza kwa David kumuona mzee huyu ambaye si mwingine bali MAGNUS mwenyewe, mtu hatari, mmiliki wa kisiwa hicho na kila kitu kilichopo ndani yake.
Gari la pili walishuka watu wanne na mwingine wa tano alikuwa amebebwa kwenye machela, alionekana mgonjwa kwani hata wale waliombeba walikuwa wamevalia mavazi kama wavaayo wahudumu wa afya wa msaraba mwekundu.

Walimbeba yule mgonjwa wakawa wanapiga hatua kuelekea ilipo meli lakini walipofika karibu na Magnus aliwaonyesha ishara wasimame nao wakatii. Na hapo ndipo David naye akapata wasaa mzuri wa kumuona yule mtu aliyebebwa kwenye machela. David alitoa macho kwa mshangao mara baada ya kumtambua, alikuwa ni rafiki yao Zungu. Hali yake bado ilikuwa ni mbaya mno ingawa alionekana tayari kupatiwa huduma ya kwanza.

“Zunguuu !!….Nini kinaendelea?” David aliwaza akionekana kushangaa mno, haikuwa rahisi kuamini Zungu yule aliyeletwa kule bondeni akiwa hoi taabani sasa anaonekana kupewa msaada na watu wa Magnus na Magnus mwenyewe, ilimshangaza akatamani kujua ni nini kinaendelea.

Magnus alipiga hatua moja akasogea karibu zaidi na ile machela, akawa anatazamana uso kwa uso na Zungu. Magnus akazungumza akisema…

“Kijana siku zote kupanga ni kuchagua, wewe umechagua maisha bora na Magnus, nitatimiza ahadi yangu na wewe utatimiza ya kwako na baada ya hapo nitakwenda kuyabadiri maisha yako kama nilivyofanya kwa wengine. Umechukua maamuzi sahihi kwa wakati sahihi, tunaanza na matibabu yako kwanza alafu mengine yatafuata….” Sauti nzito ya kukwaruza ilisikika kutoka kwa Magnus wakati akizungumza na Zungu ambaye aliishia kumsikiliza pasipo kujibu chochote.
Sauti hiyo pia ilipenya vizuri kwenye masikio yote mawili ya David, ni wazi ilionyesha kuna makubaliano kati ya watu hawa wawili yaani Magnus na Zungu, hakuna aliyejua ni nini walizungumza ndani ya kile chumba cha mateso kiasi cha kufikia hatua ya Magnus kumtoa Zungu na kuruhusu akatibiwe.

Baada ya kuongea hivyo Magnus alitoa ishara akawaruhusu wale watu waliombeba Zungu waendelee na safari. Wakati huo simu ya Magnus ilikuwa ikiita, aliitoa kwenye mfuko wa kanzu yake kisha akatazama namba ya mpigaji, Magnus akatabasamu kidogo.

Magnus aliipokea simu hiyo kisha akapiga hatua na kwenda kukaa juu ya sanduku, sanduku ambalo ndani yake kijana David alikuwa amejificha. Akaanza mazungumzo.
*****

Upande wa pili ndani ya hoteli ya kifahari Night City Hotel katika ghorofa ya kumi na moja, mlango wa lifti ulionekana ukifunguka akatoka Felix akiwa anapiga hatua ndefu ndefu huku uso wake ukiwa umekunjamana kwa hasira, alitembea haraka na mwisho akasimama mbele ya mlango wa chumba kimoja, chumba namba 204. Ndani ya chumba hicho alikuwepo Madam Husnata ambaye tayari alishahisi kuna mtu mlangoni, tabasamu lake likazidi kuongezeka.

Madam Husnata alijifunga taulo jepesi kisha taratibu akatembea kwa madaha kuelekea mlangoni, akazunguusha funguo na kunyonga kitasa. Kabla hajauvuta mlango kuufungua mara ghafula mlango ulisikumwa kwa kasi, akaingia Felix na bila hata kuuliza alimkaba Madam Husnata shingoni, akaingia naye ndani mzima mzima na kumtupa kitandani huku akiwa bado ameikandamiza shingo ya Madam Husnata kwa nguvu. Hustana alijikuta anakosa pumzi kwa sekunde kadhaa, wakati huo taulo lake lilimdondoka akabaki mtupu lakini Felix hakujali, akazidi kuikandamiza mikono yake yote miwili kwenye shingo ya Husnata.

“Yuko wapi Tesha…. Umempeleka wapi Tesha wewe malaya…??” Felix alifoka na kuuliza

“Aaah…uughhh…..Fee…li….aaah” Madam Husnata alikuwa akihangaika akitamani kuzungumza lakini hakuweza, mwisho Felix akalegeza mikono yake na kumuacha Madam Husnata ambaye alianza kukohoa kwa nguvu na kisha akawa anahema upesi upesi kuitafuta pumzi aliyoikosa kwa dakika kadhaa.

“Una…unawazimu wewe Felix eti?” Aliuliza Madam Husnata wakati huo akawa anajifunga shuka kuusitili mwili wake.

“Nasemaje Husnata usiponiambia mahali ulipompeleka Tesha leo nakuua…” Felix aliongea kwa jazba huku akipiga hatua kusogelea Madam Husnata pale kitandani.

“Embu subiri kwanza Felix, tulia hapo hapo ....Tesha yupi ambaye unamuongelea, wewe si ndio ulikuwa naye kule chini ufukweni?” Aliuza Madam Husnata akionyesha hajui kitu.

“Ndiyo nilikuwa naye na wewe umetuma watu waje kumteka… unajifanya hujui au?” Felix alifoka na kuuliza.

“Sio najifanya, ni kweli sijui, mimi sijamteka Tesha, sijatuma mtu yeyote....” Madam Husnata alijibu kwa kumaanisha, Felix alimtazama Hustana usoni ni kweli kabisa alionekana hajui kitu.

“Kwa hiyo kama sio Hustana ni nani kamteka Tesha?...” Aliwaza Felix wakati huo Madam Husnata akawa anamtazama kwa macho ya kuuliza. Baada ya kufikiri kwa muda kidogo tayari wote walikuwa na majibu ni nani aliyemteka Tesha.

“Ni baba” “Ni baba yako”

Felix na Madam Husnata walisema kwa pamoja….
Wote walikuwa na asilimia mia moja kuwa Magnus ndiye aliyemteka mrembo Tesha na hii ni kwa sababu alishamuonya mwanae Felix kukaa mbali na mwanamke huyo.

Hasira ilizidi kuwa kali kifuani kwa Felix, akainua simu yake kumpigia Magnus baba yake, simu ikawa inaita upande wa pili.

Magnus aliitoa simu yake kwenye mfuko wa kanzu yake kisha akatazama namba ya mpigaji, akatabasamu kidogo, akaipokea simu hiyo kisha akapiga hatua na kwenda kukaa juu ya sanduku, sanduku ambalo ndani yake kijana David alikuwa amejificha.

ITAENDELEA….
0756862047
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
SEASON 3
Sehemu ya........50
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA……
Hasira ilizidi kuwa kali kifuani kwa Felix, akainua simu yake kumpigia Magnus baba yake, simu ikawa inaita upande wa pili. Magnus aliitoa simu yake kwenye mfuko wa kanzu yake kisha akatazama namba ya mpigaji, akatabasamu kidogo, akaipokea simu hiyo kisha akapiga hatua na kwenda kukaa juu ya sanduku, sanduku ambalo ndani yake kijana David alikuwa amejificha.

SASA ENDELEA…

“Yuko wapi Tesha?” Hili lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa Felix, hakuwa na muda hata wa kumsalimu baba yake katika simu.

“Usijali yuko salama, unatakiwa kurudi nyumbani mara moja…” Alieleza Magnus maelezo ambayo hata David aliyasikia akiwa ndani ya lile sanduku alilokalia Magnus.

“Kwa nini nirudi?”

“Kama unataka Tesha awe salama basi unatakiwa kurudi huku kisiwani sasa hivi…”

“Unanikosea sana baba, unanikosea mno…”

“Siku zote mzazi humchagulia mwanae njia sahihi ya kupita, hata siku moja siwezi kuruhusu ukaharibikiwa Felix, nitaha….” Aliongea Magnus lakini kabla hajamaliza maelezo yake Felix alidakia akipayuka na kusema.

“…niache na maisha yangu baba, kwa nini lakini? Kwanini hunipi uhuru?”

“Wewe sio kama wao Felix unatakiwa kuelewa na kukubaliana na hilo, haufanani na wao hata kidogo, uhuru pekee unaoutaka ni wewe kurudi nyumbani kwenu, toka huko utumwani…nirudi nyumbani kwa baba yako kijana wangu”

“Mrudishe mwanamke wangu baba, hizo propaganda zako nimeshachoka kuzisikiliza. Kama ukijaribu kumgusa hata unywele wake…nasisitiza baba kama ukijaribu kumgusa Tesha wangu hata kidogo...ni..ni...nita…..” Felix alishindwa kumalizia sentesi yake midomo yake ikawa inatetemeka kutokana na hasira kali aliyonayo. Hata Madam Husnata mwenyewe alishuhudia ni kwa kiwango gani Felix alikuwa akimpenda Tesha.

“Tesha atakuwa salama kama utarudi nyumbani, ni hilo tu hakuna kingine Felix…” Magnus aliendelea kushikiria msimamo wake na kisha akakata simu.

Mazungumzo hayo kati ya baba na mwana yalikuwa yakipenya vizuri kwenye masikio ya David akiwa ndani ya lile sanduku. David alishtushwa sana aliposikia jina la mwanamke Tesha likitajwa katika mazungumzo hayo, ingawa hakuwa na uhakika sana kama Tesha anayezungumziwa hapa ni Tesha yule anayemfahamu lakini nafsi yake ilimwambia ni yeye.

"Kwa hiyo kumbe Magnus ana mtoto anaitwa Felix...." Aliwaza David asijue kwamba Felix kuwa mtoto wa Magnus tu haitoshi ila kubwa zaidi ni kwamba kwa sasa Felix anaishi uraiani kwa jina la kaka yake Feisal.

Mwisho zoezi la kushusha mizigo kutoka ndani ya meli lilikamilika na mizigo hiyo ikawekwa ndani ya zile gari zilizoambatana na msafara wa Magnus. Mizigo yote ikiwa ni pamoja na lile sanduku ambalo ndani yake alikuwepo David, hakupata hata nafasi ya kutoka ikabidi aendelee kujituliza ndani ya sanduku hilo mpaka pale atakapopata maarifa zaidi ya kuweza kutoka pasipo kuonekana.
Magnus na msafara wake walianza safari kurudi ilipo himaya yake. Wakawa wanapita katika barabara ileile iliyochimbwa chini ya mlima na kutokea upande wa pili ilipo himaya ya Magnus.

Dayana ambaye wakati wote alikuwa ametulia kule juu pangoni akimuomba Mungu amnusuru David asiweze kukamatwa aliushuhudia msafara huo wa gari nne ukirudi kutoka ufukweni. Hofu ikazidi kumjaa hakujua ni wapi alipo David kwa wakati huo, yuko salama au laa.
****

Usiku huu ulikuwa ni mrefu pia kwa binti mrembo kutoka ISRA kwa mara ya kwanza Sasha anayaanza maisha yake akiwa nje ya ISRA maisha ambayo yana utofauti mkubwa mno na maisha ya kwao alikotoka. Usiku huu yeye pamoja na Sikujua walilala chumbani huku Feisal yeye akiwa amelala sebuleni. Ni usiku ambao kichwa cha Feisal kilijawa na mawazo mengi mno, kwanza kabisa alikuwa akiwaza ni kwa namna gani ataweza kulitizima jukumu lake mama mara atakapo wasili ndani ya jiji la Dar es salaam jukumu la kumtafuta ndugu yake asiye wa damu Boaz pili aliwaza ni vipi ataweza kutimiza jukumu la pili ambalo hasa ndilo linalompa nafasi kwenda jijini Dar es salaam kujiunga na jeshi la zimamoto na uokoaji.

Katika nyumba hiyo ndogo kijijini Nachingwea-Mtwara si Feisal tu aliyekuwa na mawazo rukuki kichwa laa hasha hata Sasha naye alikuwa akiwaza ni vipi ataweza kumpata kijana David aliyebeba hatima nzito ya mji anaotoka yaani ISRA. Pamoja na yote hayo bado Sasha hakujua kuwa adui mkubwa wa ISRA yaani Magnus tayari ameshatambua uwepo wake na sasa yuko kwenye mikakati madhubuti kuhakikisha anamkamata na kumpeleka kwenye himaya yake, Sasha hakujua hilo akaendelea kuamini kwa sasa yuko salama.
****

Haikuchukuwa muda hatimae msafara wa Magnus uliwasili katika himaya yake, mizigo ikaanza kushushwa mmoja baada ya mwingine na kupelekwa katika chumba maalumu cha kuhifadhia mizigo hiyo. Lile sanduku alilojificha David nalo likabebwa na kuingizwa katika chumba hicho na hatimae zoezi lilimalizika na milango ikafungwa.
Baada ya ukimya wa muda mrefu, David alifungua lile sanduku taratibu akatoka. Alitazama mazingira ya chumba hicho kipana chenye makorokoro ya kila namna. Mwisho macho yake yakaganda kwenye mlangoni. Mlango ulikuwa umefungwa kwa nje.
****

Huku nje baada ya kushuka kwenye gari Magnus alipokelewa na msadizi wake wa kazi ambaye alionekana kuwa na habari muhimu za kumpatia mzee huyo anaetisha hata kwa kumuangalia.

“Mkuu nimepata taarifa kuwa Felix ameomba usafiri wa helkopta kutoka kwa watu wetu MG Family sio muda atafika hapa kisiwani” Alieleza yule bwana msaidizi wa karibu wa Magnus.

“Nilijua atafanya hivyo, anaonekana kumpenda sana huyo mwanamke…”

“Sana…lakini mkuu ni kwa nini umetaka Felix aje huku kisiwani, atatulia kweli bila kuwa na Tesha”

“Kama ugonjwa wa Felix upo kwenye mapenzi basi nitampa anachokitaka, lakini kamwe siwezi kumuunganisha na mwanadamu. Felix atamuoa Sasha…” Magnus aliongea kwa kujiamini, yule msaidizi wake akatoa macho kwa mshangao.

“Atii!! Sasha yupi? huyu binti wa Gu Gamilo mdogo wako?”

“Ndiyo, hebu jaribu kufikiria siku tunarudi ISRA na kuurudisha utawala wetu huku Felix akiwa ni mfalme na Sasha ndiye malkia, unajisikiaje…?” Magnus aliongea huku akitabasamu.

“Mkuu umewaza mbali sana, hata sikuwa nawaza kama unamipango mikubwa kama hiyo”

“Unatakiwa kuwa na macho ya tai, ona kilicho mbali…”

“Lakini utamshawishi vipi Felix kumuoa Sasha?”

“Hahahahah hilo lisikupe wasiwasi, ni jambo rahisi sana kwani kati ya Tesha na Sasha unafikiri Felix atamepnda nani zaidi? Au wewe unaona ni nani mzuri zaidi kati yao?....alafu istoshe Felix kazaliwa ISRA na Sasha naye kazaliwa ISRA, wa ISRA atamuoa wa ISRA mwenzake hahaha”

“Aiseeh! nimeipenda hiyo Mkuu…”

“Muache kwanza aje kila kitu kitajulikana mbele ya safari, enhe! Na vipi kuhusu huyo Tesha yuko wapi kwa sasa?” Aliuliza Magnus

“Wamempeleka kule ulipoagiza apelekwe…”

“Vizuri, kazi nzuri…”
****

Ni katika kiwanda kimoja cha mbolea pembeni kabisa ya mji, kiwanda ambacho hakikuwa kikitumika bali kilitelekezwa kwa muda mrefu mara baada ya kufungiwa kisheria na serikali huku mmiliki wa kiwanda hicho akikatishwa tamaa ya kukifufua upya. Katika kiwanda hicho ndipo alipopelekwa mwanadada mrembo na maarufu nchini Tanzania yaani Tesha. Alifungiwa ndani ya chumba kimoja chakavu mno, huku ulinzi ukiimarishwa mara dufu ndani na nje ya kiwanda hicho. Na hili lilikuwa ni agizo kutoka kwa Magnus mwenyewe

JE NINI KITAFUATA?

ITAENDELEA…..
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
SEASON 3
Sehemu ya.........51
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA….
Katika kiwanda hicho ndipo alipopelekwa mwanadada mrembo na maarufu nchini Tanzania yaani Tesha. Alifungiwa ndani ya chumba kimoja chakavu mno, huku ulinzi ukiimarishwa mara dufu ndani na nje ya kiwanda hicho. Na hili lilikuwa ni agizo kutoka kwa Magnus mwenyewe

JE NINI KITAFUATA?

SASA ENDELEA…
Kabla ya Felix kuondoka kuelekea kisiwani kwa baba yake Magnus, alikutana kwanza na kijana wake wa kazi, kijana aliyekuwa akimtumia katika kutekeleza harakati zake mbalimbali ndani na nje ya jiji la Dar es salaam. Ni huyu kijana ndiye aliyepewa kazi na Felix ya kumfuatilia kwa ukaribu mpenzi wake Tesha kwa kipindi chote ambacho yeye alikuwa marekani. Hata siku ile wakati David na Tesha wakiwa pale mgahawani wakifanya mazungumzo ni huyu kijana ndiye aliyewapiga picha na kumtumia picha hizo Felix bosi wake. Kijana huyu machachari mjuzi wa kuchezea kompyuta na mtandao istoshe alikuwa na uwezo mzuri pia wa matumizi ya silaha za moto (bunduki/bastola) anaitwa Joshi Mahende. Ni mwanaume mrefu mweusi, uso wake uliokunjamana kila wakati, hutomuona anacheka hata kwa bahati mbaya.
Naam huyu ndiye Joshi Mahende mafia aliyejikamilisha kwa kila idara kiasi cha kujibatiza jina na kujiita jeshi la mtu mmoja, ni kweli alikuwa ni jeshi haswa.

“Bosi sio lazima ufanye kama baba yako anavyosema! Niachie mimi hii kazi, ndani ya masaa 24 nitakuwa nimemleta Tesha mikononi mwako…” Alisema Joshi Mahende wakati akifanya mazungumzo na Felix.

“Najua kama hii kazi sio ngumu kwako lakini nahitaji kuoanana na baba ndio sababu nalazimika kwenda…”

“Basi haina shida bosi, nitakuwa nakupa taarifa kwa kila kinachoendelea, nitaanza na kuifuatilia simu ya Tesha kama nilivyokuwa nafanya mwanzo kama bado yuko na simu yake itakuwa rahisi sana kumpata hata kabla hakujapambazuka…”

“Sawa lakini kumbuka unapambana na watu kutoka MG Family, ukileta uzembe kidogo tu basi vita itakugeukia na kuwa kubwa upande wako, unawajua vizuri sana MG Family”

“Usiwe na shaka bosi….”

Waliagana na baada ya hapo Felix alielekea mahali ambapo alikubaliana na MG Family kuwa watakuja kumchukua na kumpeleka ilipo helkopta na kisha atapanda kuelekea kisiwani kwa baba yake Magnus.

Tofauti na alivyotegemea Felix, mtu aliyekuja kumchukua alikuwa ni Kareem kiongozi mkubwa sana wa kundi la kigaidi MG Family, na huyu ndiye alisimamia mpango wote hadi Felix akaachiwa huru kutoka mikononi mwa polisi. Felix aliingia ndani ya gari la Kareem kisha safari yao ikaanza.

“Sikutegema kama ungekuja wewe kunichukua…” Felix alianzaisha mazungumzo mara baada ya salamu.

“Unajua wewe ni kama mboni ya jicho la baba yako Magnus, anakupenda sana ni wajibu wetu kukuthamini kama yeye anavyokuthamini….” Alieleza Felix kauli ambayo haikumfurahisha Felix hata kidogo.

“Nimesikia hukutaka kabisa kurudi kisiwani, unalazimisha kukaa kwa yule mama yako feki. Ni kwa nini hasa unafanya hivyo Felix? ” aliuliza Kareem mara baada ya ukimya wa muda.

“Usiniambie na wewe unafurahia mtoto wa kiume kama mimi kupangiwa kitu cha kufanya na aina ya maisha nayotakiwa kuishi…”

“No... not like that Felix, yule ni baba yako je ulishawahi kumuliza sababu ya yeye kufanya hivyo ni nini? Je, unajua sababu ya yeye kujitenga kule kisiwani… kukaa mbali na makazi ya watu…?” Kareem alihoji.

“Huna unachokijua Kareem, endelea kuwa kibaraka wa huyo mzee pengine hapo ndipo ndoto yako imeishia…” Alijibu Felix.

Baada ya mwendo kama dakika 20 hivi walifika na mara moja taratibu za kupanda helkopta ambayo itawapeleka mpaka kisiwani kwa Magnus zilianza.

“Na wewe unakwenda kisiwani?” Aliuliza Felix baada ya kuona bado Kareem anaendelea kuambatana naye.

“Yap! Nafikiri tunakazi ya kufanya huko mimi na wewe…” alijibu Kareem

“Kazi? Mimi na wewe?”

“Ndiyo, kwa mujibu wa maelezo ya baba yako” Alijibu Kareem kauli iliyomfanya Felix afikiri sana akiwaza ni nini baba yake Magnus alikuwa akikipanga. Wakati huo huo kuna ujumbe mfupi wa maandishi ukaingia kwenye simu ya Felix, akatazama simu yake na kugundua ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa kijana wake wa kazi Joshi Mahende, akausoma haraka…

,,,,,,,,Bosi nimefanikiwa kujua ni wapi walpompeleka Tesha, location ya cm yke inasoma maeneo ya KASILI MINES & FERTILIZERS LTD hik n kiwanda cha zaman cha mbolea, naelekea huko, baada ya dakika 10 hv nitakuwa nimefika,,,,,,,,

Felix alimaliza kuusoma ujumbe huo kisha akamkata jicho kali Kareem aliyekuwa akiibia ibia kutaka kuusoma ujumbe huo kwenye simu yake.

“Am so sorry Tesha, kila kitu kitakuwa sawa mpenzi wangu….” Aliwaza Felix na mwisho yeye Kareem pamoja na vijana wengine watatu rubani akiwa ni wanne waliingia katika helkopta na safari kuelekea kisiwani kwa Magnus ikaanza mara moja.
***

Ndiyo, kama ujumbe wa maandishi ulivyokuwa ukisomeka katika simu ya Felix na ndivyo ilivyokuwa, Joshi Mahende kijana wa Felix alionekana akiwa anakwenda kwa kasi sana na pikipiki yake huku mgongoni akiwa amebeba begi kubwa lenye silaha za aina tofauti tofauti ndani yake. Ukisikia jeshi la mtu mmoja basi ndiyo Joshi Mahende, hakuna kazi aliyowahi kuifanya akashindwa, alikuwa na mbinu za kivita kiasi cha kuwa na uwezo wa kukabiliana na kundi la watu 100 yeye akiwa peke yake na kuwashinda.

Kama alivyo ahidi ni kweli ndani ya dakika kumi tayari alikuwa akilikaribia geti kuu la kuingia katika kiwanda cha mbolea kilichozunguukwa na uzio wa ukuta mrefu. Yalikuwa ni majira ya usiku mnene ingawa mwanga wa mwezi ulikuwa umeshamiri. Joshi Mahende aliificha pikipiki yake nyuma ya kichaka kimoja na baada ya hapo akaanza kunyata kikomandoo kusogea katika geti kuu la kiwanda hicho.

Katika hali ya kushangaza wakati Joshi Mahende ananyata kusogea mbele akitokea upande wa kulia, mara upande wa kushoto kuna mtu mwingine akaonekana naye akinyata kusogea mbele kule anakoelekea Joshi Mahende.

Hakuna aliyemuona mwenzake, kila mmoja akiwa na siraha yake mkononi aliwaza kulifikia geti la kiwanda cha mbolea cha KASILI MINES & FERTILIZERS LTD pasipo kuonekana.

Wakati wakiwa amebakiza hatua kama sita hivi kufika getini ndipo hapo waliweza kuonana, haraka kila mmoja akawahi kuelekeza bastola yake mbele tayari kufyatua risasi, sasa kila mmoja akawa anatazamana na mdomo wa bastola ya mwenzake.

“Nani wewe?” Aliuliza Joshi Mahende akiwa makini kupita kawaida, alijua wazi kama atafanya uzembe hata kwa nusu sekunde basi jina lake litabadilika na kuitwa marehemu.

“Na wewe ni nani?” Sauti ya kike ilisikika kutoka kwa yule mtu wa pili naye akiuliza swali lile lile, amini usiamini mwanamke huyu hakuwa mwingine bali Inspekta Brandina.

Kivipi?
Kafikaje?
Anataka nini?

Ilikuwa hivi….
Kama utakumbuka kwa mara ya mwisho Inspekta Brandina na Felix walitunishiana misuli pale kituo cha polisi huku kila mmoja akitangaza kuingia kwenye vita kali na mwenzake. Inspekta Brandina akaahidi atafanya juu chini kuhakikisha anamtia Felix na mtandao wake gerezani kwa makosa ya utekaji nyara walioanza kuufanya tangu mda mrefu. Ni kweli Inspekta Brandina alimaanisha anachokisema. Kwa kuwa yeye ndiye kiongozi kati ya askari waliopewa jukumu la kuifuatilia kesi hiyo ya utekaji Inspekta Brandina hakuacha kumfuatilia Felix. Aliendelea na utaratibu huo kwa siri na hata wakati Felix na Tesha wameingia ndani ya ile hoteli ya Night City Inspekta Brandina alikuwa akiwafuatilia kimya kimya bila wao kujua. Naye pia akachukua chumba, hii yote ikiwa ni harakati za kupata ushahidi wa kumshikiria Felix kwani tayari alikuwa na uhakika wa asimilia zote kwamba Felix ni moja kati ya wahusika wa matukio ya utekaji.

Wakati Felix na Tesha wakifanya mazungumzo pale ufukweni Inspekta Brandina naye alikuwa umbali wa mita kadhaa akiwatazama ndipo hapo aliposhuhudia lile tukio la uvamizi wa ghafula lililofanywa na wale vijana wenye pikipiki ambao mwisho waliondoka na Tesha. Inspekta Brandina hakutaka kupoteza muda alianza kuwafuatilia vijana hao nyuma kwa siri akiwa na gari yake hadi walipofika katika kiwanda hicho cha mbolea. Inspekta Brandina akiwa ameliacha gari lake mbali na eneo hilo alibaki nje kwa muda akisubiri hali itulie ndipo aingie ndani kumsaidia Tesha. Tayari alishapiga simu kwa askari wenzake na sasa walikuwa njiani kuja kumpa msaada lakini hakutaka kusubiri zaidi kwa ajili ya usalama wa Tesha akaamua kuanza kazi mwenyewe. Wakati akiwa ananyata kuliekea geti la kuingia kiwanda cha mbolea ndipo hapo anapokutana uso kwa uso na kijana wa kazi wa Felix Bwana Joshi Mahende.

“Wewe ni nani?”

“Na wewe ni nani?”

Inspekta Brandina na Joshi Mahende waliulizana maswali huku wakiwa wamenyosheana bastola.

ITAENDELEA…
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
SEASON 3
Sehemu ya........52
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA….

“Wewe ni nani?”

“Na wewe ni nani?”

Inspekta Brandina na Joshi Mahende waliulizana maswali huku wakiwa wamenyosheana bastola…

ITAENDELEA…

“Nimekuuliza wewe kwanza nijibu, umefuta nini hapa?” Aliuliza Joshi Mahende

“Wewe pia umekuja ukinyata kama mimi, wewe nani? nini kimekuleta hapa….?”
Inspekta Brandina na Joshi Mahende walizidi kuulizana maswali huku kila mmoja akijaribu kumsoma mwenzake. Wakati huo wote walikuwa makini kupita maelezo siraha zao zikiwa mbele, kila mmoja alijua kama atafanya uzembe hata chembe basi atatoa mwanya wa mwenzake kumpiga risasi na huo unaweza kuwa ni mwisho wa maisha yake. Hakukuwa mzembe kati yao si Inspekta Brandina wala Joshi Mahende wote walizielewa vizuri mbinu za kumkabili adui mwenye silaha.

Inspekta Brandina alijua wazi kuwa kiwanda hiki kilishafungwa na watu pekee waliokuwa ndani ya kiwanda hicho kwa wakati huu ni wale ni wale waliomteka Tesha pamoja na kumleta hapo. Sasa je huyu aliyekutana naye hapa nje ni nani? Anataka nini? Kwa nini anaingia kwa kuvizia? Haya ni masawli ambayo yalikuwa yakipita kwenye kichwa chake bila ya kuwa na majibu sahihi, si yeye pekee hata Joshi Mahende alijiuliza maswali hayo hayo, hakujua kuwa mwanamke aliyesimama mbele yake ni askari na yupo hapo kwa lengo la kumsaidia Tesha.

Inspekta Brandina aliamini haikuwa maamuzi sahihi kujitambulisha kama askari angali ni mapema. Bado alitamani kumjua vizuri mtu huyo ambaye kwa haraka haraka alionekana ni mtu mwenye uzoefu na matukio ya kiharifu.

“kwa hiyo tutatazamana hivi kwa muda gani…. au tupigane risasi wote tufe…?” Aliuliza Joshi Mahende

“wewe unatakaje, tuweke silaha chini basi…” Alijibu Inspekta Brandina

“Halafu?”

“Tupigane, bila silaha….”

“Unauhakika?” Aliuliza Joshi Mahende huku akitabasamu

“Bila shaka…” Alijibu Inspekta Brandina akionekana kujiamini sana.

Walikubaliana hivyo, taratibu na kwa tahadhari kubwa waliinama kwa pamoja wakaweka silaha zao chini na baada ya hapo kila mmoja akaisukuma pembeni bastola kwa kutumia mguu wake. Sasa kila mmoja akajiweka tayari kukabiliana na mwenzake uso kwa uso. Inspekta Brandina askari mzoefu aliamini katika uwezo wake wala hakujali kupambana na kidume yule, hakujua kuwa Joshi Mahende ni moto wa kuotea mbali.

Wakati hayo yakiendelea nje ya kiwanda hicho, Tesha alikuwa ndani ya chumba kimoja chakavu sana alichofungiwa, vijana wa Magnus nao wakiwa wametawanyika kila mahali ndani ya kiwanda hicho kuimarisha ulinzi kama walivyoagizwa, hakuna aliyekuwa anaelewa uwepo wa Inspekta Brandina na Joshi Mahende kule nje.

Hofu ilikuwa imemjaa Tesha, hakuzoea kabisa maisha ya aina hiyo, siku zote dada huyu maarufu nchini Tanzania aliishi maisha marahisi mno maisha yasiyo na mashaka yoyote. Mambo kama haya yanayomtokea leo alizoea kuyatazama kwenye tamthilia za kihindi alizopendalea kuzitazama. Lakini hivi karibuni amashuhudia na kupitia matukio ya ajabu na kuogopesha sana, tangu kutekwa kwa kijana David, kukamatwa kwa Felix na baadae yeye kutekwa.

Ni mfurulizo ya matukio ambayo ndani yake yalikuwa yamebeba fumbo zito, fumbo ambalo chanzo chake kinaanzia kule katika mji wa ajabu ISRA mahali anapotoka mchumba wake Felix lakini pia Magnus pamoja na Sasha ambao wote hawa kwa wakati huu hawapo ISRA.
Wakati Tesha akiwa katika hali ya hofu ndani ya chumba kile chenye kuogopesha, huku nje watu wawili waliokuja kumsaidia yaani Inspekta Brandina na Joshi Mahende walikuwa kwenye vita kali.
***

Wakati wewe ukiwa umelala ukisubiri kupambazuke ili kuendelea na harakati za maisha ya kila siku wapo ambao harakati zao hazijarishi ni usiku au mchana, muda wote wako macho, muda wote wanapambana na hii ni kutokana na aina ya maisha waliyoyachagua au pengine wanalazimika kuishi hivi. Ukiwa ni usiku sana majira ya saa saba helkopta iliyowabeba Felix Kareem na wenzake iligusa ardhi katika kisiwa cha Magnus. Wa kwanza kushuka alikuwa ni Felix mwenyewe. Kwa mara nyingine tena Felix yupo katika himaya ya baba yake asiyoipenda, himaya ambayo kwake anaiona ni kama gereza, hapati uhuru ule anaoutaka. Na sasa yupo hapa kwa ajili ya kupigania uhuru wake yeye na mpenzi wake Tesha.

Kwa muda kama huu Felix alijua ni wapi atampata baba yake, haraka alinyoosha njia kuelekea kilipo kile chumba ambacho Magnus na wanafunzi wake huwa wanakutana(Darasa) . Haikuwa sahihi kwa yeye kufanya hivyo, Magnus akiwa darasani huwa hapendi kabisa mtu kuingilia kipindi chake, hata kama unataarifa muhimu kiasi gani lazima usubiri amalizie. Felix aliijua vizuri sheria hii lakini akaivunja kwa makusudi. Walinzi walijaribu kumzuia lakini alipowatazama kwa macho makali, macho yaliyojaa mamlaka kama mtoto kidume wa Magnus walinzi hao walirudi nyuma kwa hofu na kumuacha afanye kile anachotoka kufanya.

David ambaye kwa wakati huu alikuwa ndani ya kile chumba kulipohifadhiwa mizigo iliyoletwa na meli hakuwa amelala, bado alikuwa akipiga hesabu ni namna gani ataweza kutoka lakini bado hakupata majibu. Alikaa chini na kujikunyata kwenye kona moja ya chumba hicho akionekana mwenye mawazo sana, alimkumbuka Dayana alimkumbuka Mama yake, mdogo wake Tatu lakini pia hata Tesha mwanamke ambaye walizoeana kwa muda mfupi sana, na tayari kuna aina fulani ya upendo ulianza kuchipua katikati yao lakini ghafula wanatenganishwa na matukio ya kustaajabisha.
Wakati akiwa pale chini ndipo alipoisikia sauti ya helkopta ikiwasili kisiwani hapo. Ni wakati ambao Felix na wenzake walikuwa wakiwasili kisiwani hapo. Taratibu David akainuka na kusogea dirishani kuchungulia kupitia uwazi mdogo uliokuwa dirishani hapo lakini kwa bahati mbaya hakufanikiwa kuona kitu.

David akahamia upande wa pili lilipo dirisha lingine akachungulia, ndipo hapo alipoweza kumuona Felix akitembea kwa kujiamini katika himaya ya baba yake huku walinzi wakisogea pembeni kumpisha. Kwa habati mbaya David hakufanikiwa kuiona sura ya Felix, alikuwa amegeukia upande wa pili na kumpa mgongo, alimuona kwa nyuma tu. Felix kijana ambaye ndiye mpenzi wa Tesha lakini pia kwa sasa anajulikana kama Feisal kaka yake David anaeamini alikufa mda mrefu uliyopita. David akajikuta anapata msukumo wa kumtazama Felix zaidi na zaidi asijue kwa sasa huyu anaishi kama kaka yake na hapa mama yake amekubari kumpokea. David akatamani kuiona sura yake lakini hakuweza, mwisho kabisa Felix akatoweka machoni pake.

Licha ya kwamba Felix alimuamini sana kijana wake wa kazi Bwana Joshi Mahende aliyekwenda kule kiwandani kumuokoa Tesha lakini bado Felix alikuwa na hasira kali dhidi ya baba yake Mzee Magnus, ndiyo sababu hakutaka kumsubri baba yake amalize kipindi chake darasani badala yake akaamua kumfuata huko huko. Kitendo alichokifanya kwa kutuma watu wamteka Tesha kilimuudhi mno, tayari alishaamua kupambana na baba yake nah ii ilikuwa ni hatua yake ya kwanza.

Wakati Magnus akiendelea na darasa akiwa amesimama mbele ya wanafunzi wake mara ghafula mlango wa chumba hicho ukafunguliwa kwa nguvu, wote waliokuwa ndani ya chumba hicho walishtuka wakageuka kutazama mlangoni. Alikuwa ni kijana Felix ambaye aliingia kwa kujiamini akapiga hatua kadhaa na kusimama mbele ya baba yake mzee Magnus. Uso kwa uso Magnus akawa anatazamana na mtoto wake ambaye sura yake alionyesha ni mtu mwenye hasira kali mno. Hali hii iliwashangaza hata wanafunzi wa Magnus wakawa hawaelewi ni nini hasa kinaendelea.

Huku ni Felix dhidi ya baba yake Magnus lakini upande wa pili ni Inspekta Brandina dhidi ya Joshi Mahende.

ITAENDELEA….

WhatsApp: 0756862047
 
Back
Top Bottom