SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya...........45 - 46
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA....
“Sawa upesi wasiliana na MG Family wambie namuhitaji huyu binti aletwe hapa kisiwani haraka”
“Sawa mkuu, nawasilaina na Kareem sasa hivi…”
“Sawa, wambie haina haja ya kutumia king’ora, hana nguvu zozote kwa sasa” Magnus alisisitiza.
SASA ENDELEA…
****
Tunarudi ndani ya kisiwa cha Magnus katika bonde alilowahifadhi mateka wake. Maisha yaliendelea kama kawaida, taratibu mateka hao walijikuta wanaanza kulisahau tukio la usiku wa jana pindi wenzao walipojaribu kutoroka na mwisho wakajikuta wanauawa kwa kupigwa risasi na walinzi wa Magnus. Tayari walishaizoea hali hii ya kuona wenzao wanakufa mara kwa mara pale wanapojaribu kutoroka lakini pia wapo wale wanaofariki baada ya kushindwa kukabiliana na maisha magumu ndani ya bonde hilo.
Hali ilikuwa nitofauti kabisa kwa kijana David na binti Dayana ambao wao ndio walijiona kama ni chanzo cha wenzao kuuawa kikatiri usiku wa jana. Wakati wote David alikuwa amekaa na kujiinamia. Hakuwa amekula wala kunywa chochote hadi dakika hiyo. Alimuwaza rafiki yake Zungu ambaye kwa sasa anapitia mateso mazito mno kwa sababu yake.
“Tayari tumeshapata njia, kilichobaki ni kutafuta namna nzuri ya kutoroka hapa kisiwani…” Hatimae David alizungumza baada ya ukimya wa muda mrefu.
“David” Dayana aliita, David akageuka na kumtazama
“…..unajua mimi sikuelewi kabisa”
“Kwanini…?”
“Sikuelewi ani, unauoga ambao sio wa kawaida hivi unakumbuka sababu hasa ya Zungu kuteleza na kuangakua kule juu pangoni ni nini?...wewe ndiyo sababu David, alikuwa anajaribu kukusaidia wewe na baadae akajikuta yeye ndio anaingia kwenye matatizo zaidi. Sasa nashangaa huo ujasiri wa kuongea maneno hayo unaotoa wapi wakati tukiingia kwenye vitendo unakuwa na woga si woga…ani hueleweki” Dayana aliongea maneno ambayo kwa kiasi kikubwa yalimgusa sana David. Ni kweli kabisa alikuwa na aina fulani ya woga kutokana na lile tatizo lake la Acrophobia.
“Dayana ni kweli kabisa unavyosema, lakini sikufanya vile kwa kupenda ninalo tatizo moja kubwa tangu nikiwa mdogo, pamoja na hayo yote haimaaniishi kwamba sitakiwi kupambana, ninayo imani kuwa nitaweza kutoroka hapa ingawa nina hili tatizo”
“Ni tatizo gani David?”
Aliuliza Dayana akitamani kujua zaidi kuhusu tatizo hilo la kiafya linalomsumbua David. Hapo David alimsimulia Dayana kwa kina ni wapi hasa tatizo hili la afya ya kisaikolojia lilianzia yaani siku ile alipomshuhudia kaka yake Feisal pamoja na baba yake Mzee Selemani wakitumbukia majini na mwisho wakapoteza maisha. Ilikuwa ni kisa kizito kilichomsisimua sana Dayana akajikuta anamuonea huruma mno David.
“Kwa hiyo mwili wa kaka yako Feisal haukuwai kuonekana kabisa?”
“Ndiyo, alifia majini na kupotelea huko huko, mwili wake ukawa chakula cha samaki. Kila nikikumbuka hili tukio sio siri huwa naumia sana Dayana. Laiti siku zingekuwa zinarudi nyuma na kutupa nafasi ya kurekebisha makosa yetu basi nisinge thubutu kurudia ule upuuzi wa kumsukuma kaka Feisal ili tu niuwahi mpira. Ona sasa ile dhambi inanitafuna hadi leo. Kifo cha kaka na baba hakijatosha, safari hii tena nampoteza mtu muhimu kama Zungu kwa sababu ya uzembe kama ule ule niliowahi kuufanya miaka ile”
“It’s okay David hutakiwi kujilaumu sana, hata hivyo ulikuwa bado ni mtoto… sio kosa lako kabisa” Alisema Dayana akijaribu kumtuliza David na baadae akatulia.
“Kwa hiyo sasa kama unahilo tatizo la saikolojia tutawezaje kutoroka David?”
“Sio ishu kubwa nina uwezo wa kujizuia na….” Alisema David lakini kabla hajakamilisha sentesi yake mara alisita kuendelea macho yake akia ameyagandisha mbele kumtazama mateka mmoja ambaye alikuwa akipita mbele yao hatua kadhaa kutoka pale walipokuwa. Dayana naye akaelekeza macho yake kuelekea kule anakotazama David. Wote walimuona yule jamaa ambaye usiku wa jana ndiye aliyekuwa akiwashawishi wenzake wapande ngazi wakimbie, lakini ajabu yeye hakupigwa risasi kama wengine. Alioneakna kuwa mzima wa afya tele.
“Huyu fara kwa hiyo yeye hawakumuona au…we jamaa! Oyaa! Oyaa! Wewe…” David alionge mwisho akawa anamwita.
“Anitwa bonge, ita Boaz …” Dayana akamsaidia
“Oyaa Boaziiiiiiii …..” aliita David safari hii kwa sauti kubwa sana yule mtu(Boaz) akasimama na kugeuka.
Alipogonganisha macho na David Boaz akaonekana kuogopa, alikumbuka vizuri usiku wa jana alibishana vikali na David wakati akiwashauri wasitoroke. David akawa anapiga hatua kumfuata, Dayana naye akafuata nyuma.
“Inakuwaje umewapeleka wenzako kwenye kifo alafu wewe umerudi mzima?” Aliuliza David huku akimsogelea Boaz kwa mikwara mizito, hakujali umbo kubwa la mwili wa Boaz.
“mimi pia nimenusurika kufa ndugu yangu angalia” Boaz alijitetea, akageuka na kuwaonyesha eneo la mgongo mahali alipoparazwa na risasi.
“Lakini niliwambia, unaona sasa madhara yake, wenzako wamekufa”
“Hata mimi naona ni heri nife tu maana nishachoka….”
“Kama ni hivyo basi si ungebaki huko juu wakupige risasi na wewe pia”
“Mwanangu unaongea kirahisi sana hivi unajua kwa nini mimi natamani sana kutoka kwenye hichi kisiwa?” Aliuliza Boaz
“Hakuna asiyetamani kutoka kila mtu humu anataka uhuru”
“Lakini mimi ni zaidi ya ninyi wote, unajua kwa nini?”
“Mmnh….”
“Twende tukakae niwasimulie kitu” Alisema Boaz, David na Dayana wakatazamana kisha wakapeana ishara kuwa wakubali tu kumsikiliza Boaz
Walikaa mahali walipozoea kukaa kila siku kisha Boaz akaanza kueleza ni kipi hasa kinachomfanya ahisi yeye ni muhimu zaidi kutoka kuliko mateka wengine wote.
Akaanza kwa kusema…
“mimi ni mzaliwa wa Mtwara wilaya ya masasi, natokea familia ya chini sana kiuchumi, mimi na kaka yangu mmoja ambaye si ndugu yangu wa damu tulikuwa tukifanya kazi kama vibarua katika shughuli za uchimbaji wa madini kwenye migodi ya matajiri kule mtwara. Siku moja alikuja kijana mmoja ambaye ni mtoto wa mmiliki wa mgodi ambao tulikuwa tunafanya kazi siku hiyo. Alikuja kukagua kazi za baba yake jinsi zinavyokwenda. Siku hiyo aliingia ndani zaidi ya mgodi kwa bahati mbaya ikatokea ajali yule kijana akafunikwa na na kifusi. Ilikuwa ni siku ngumu sana kwake lakini mimi na ndugu yangu pamoja na wenzangu wengine wawili tuliweza kupambana na mwisho tukafanikiwa kumtoa yule kijana kwa haraka akakimbizwa hospitali. Baada ya kurudi nyumbani kwao Dar es salaam mzee wake yaani mmiliki wa ule mgodi alitupatia mimi na wenzangu mwaliko maalumu nyumbani kwake ili aweze kutoa shukrani kwa kazi kubwa tuliyoifanya kumokoa kijana wake. Lakini kabla tujaondoka alituuliza kama kuna mtu kati yetu ana akaunti ya benki, hakuna hata mmoja aliyekuwa nayo. Ilibidi mimi nifungue akaunti haraka kabla hatujaondoka, nilifanikiwa na mwisho mimi ndugu yangu na wenzangu wawili tulisafiri hadi jijini Dar es salaam tukafika hadi nyumbani kwa mzee, unajua nini kilitokea? ” Aliuliza Boaz, David na Dayana wakatamani kusikia zaidi.
“….Alituzawaidia pesa nyingi sana na zote zikawekwa kwenye akaunti niliyofungua kule Mtwara, akatutaka tugawane pasu kwa pasu. Aisee yule mzee alijua kutufurahisha, zilikuwa ni pesa nyingi mno. Kila mmoja akaona ameuaga umaskini, lakini kuna kauli inasema ng’ombe wa maskini hazai, ni kweli kabisa. Siku hiyo usiku tukiwa na furaha kubwa tulilewa sana na baadae tukawa tunarudi katika hoteli tuliyopangiwa kupumzika. Nakumbuka tulifika eneo moja lenye supermarket Fulani hivi kubwa MINI supermarket, ndugu yangu akaomba tumsubiri ajisaidie haja ndogo akazunguuka nyuma ya lile jengo. Tukiwa tunamsubiri pale nje ghafula inatokea gari ya hawa jamaa wakatuteka mimi na wenzangu na kutuleta huku, kwa bahati nzuri ndugu yangu yeye hawakumuona. Inauma sana, nimekaa huku kwa miaka mitatu mpaka sasa wenzangu watatu wote walishakufa nimebaki mimi na pesa zetu kwenye akaunti.” Boaz alimaliza kusimulia.
“pole sana Boaz”
“Asante Dayana, unajua kadi yangu ya benki alibaki nayo yule ndugu yangu,ilikuwa kwenye begi lake lakini kinachoniumiza hawezi kuzitoa zile pesa, ni mimi pekee ndio najua namba za siri. Angalau angekuwa anajua hizo namba za siri atoe pesa aendelee kumsaidia Mama na Sikujua ambao wote walikuwa wanatutegemea.”
“Sikujua ndio nani, mkeo?”
“Hapana ni mdogo wangu wa kike, alikatisha masomo yake kwa sababu ya kukosa pesa. Nilimuahidi siku moja nitamtafutia kazi nzuri na atakuwa na maisha mazuri, ni miaka mitatu mpaka sasa sijui hali yake”
“Usijali Boaz kuwa mtulivu, ipo namna ya kutoka hapa lakini inahitaji umakini wa hali ya juu” Alisema David
“Unasema kweli?”
“Ndiyo, nakuhakikishia tutatoka hapa na utakuwa huru, utatoa pesa zako na kumsaidia mdogo wako Sikujua” David aliongea kwa kumaanisha.
****
Usiku huo upande wa pili kijijini Nchingwea mkoani Mtwara, daladala moja ilisimama na akashuka binti mmoja aliyekuwa amevalia gauni la kijivu lililombana. Kichwani alivaa kofia yenye paa la duara iliyolegea. Mkononi alikuwa na mkoba mdogo wenye mikanda mirefu. Alishuka na kuanza kukatiza kwenye mitaa ya kijiji hicho kisicho na umeme. Huyu binti alikuwa ndiye Sikujua mwenyewe mdogo wake Boaz ambaye tumeona stori zake zikisimuliwa kule bondeni. Bonge
“Eeeh! Sikujua nilijua tu lazima utarudi kutoka mjini…” Ilikuwa ni sauti ya dada mmoja rafiki wa Sikujua ambaye walikutana akiwa karibu kufika nyumbani kwao.
“Mambo vipi…” Sikujua akasalimia
“Poa tu za huko town… eeh! Naona kaka yako Feisal kapata zari, kaja kutembelewa na mkuu wa mkoa hadi nyumbani kwenu na amepewa ofa ya kwenda kusoma Dar”
“Najua, tutaonana kesho” Sikujua alijibu kifupi kisha akaondoka zake kuelekea nyumbani.
Alifika na kabla ya kuingia ndani mlango ulifunguliwa ghafula uso kwa uso Sikujua akagonganisha macho yake na macho ya Feisal aliyekuwa anatoka.
IKO HIVI….
Yule ndugu asiye wa damu ambaye Boaz alikuwa akisimulia taarifa zake kule bondeni ni Feisal huyu aliyemuokoa Sasha kwenye mafuriko. Kwa kipindi kirefu Feisal na Boaz wameishi kama mtu na kaka yake mkoani Mtwara, na hawa ndio walioshiriki kumuokoa yule kijana aliyefunikwa na kifusi na baadae wakasafiri hadi Dar es salaam kwa tajiri mmliki wa mgodi ambaye aliwapatia fedha nyingi sana kama shukrani. Siku ile ya utekaji ni Feisal ndiye aliyewaomba wenzake wamsubiri na kisha yeye akazunguuka nyuma ya jengo la MINI supermarket kujisaidia, lakini anaporudi anakutana na tukio la wenzake kutekwa. Ni Feisal ndiye alinusurika kwenye utekaji huo huku kwenye begi lake akibaki na ile kadi ya benki ambayo hajui namba zake za siri mpaka hii leo.
SASA TUENDELEE…
“sikujua?” Feisal aliita kwa mshangao.
“Ndiyo, ni mimi…uko powa Feisal” Alijibu Sikujua, akapiga hatua kuingia ndani. Alipofika sebuleni anakutana na sura ngeni ya binti mzuri na mrembo Sasha. Bado alikuwa ndani ya nyumba hiyo, hakuondoka na msafara wa mkuu wa mkoa kama alivyosema.
“Habari yako dada” Sikujua alisalimia.
“Ni nzuri tu karibu”
“Asante karibu wewe. Mimi hapa ni mwenyeji…”
“Asante nimeshakaribia…”
“Pole kwa maafa yaliyowakuta…..” Alisema Sikujua akionekana tayari anataarifa juu ya kile kilichotokea siku hiyo. Wakati huo bado Feisal alikuwa amesimama pale mlangoni akiwa katika hali ya mshangao, hakutegemea kabisa ujio wa Sikujua usiku huo.
“Sikujua tunaweza kuongea kidogo…” Alisema Feisal
“Yes, bila shaka” Alijibu Sikujua kisha yeye na Feisal wakaongozana kuingia chumbani.
“Kabla ya yote inakuwaje huyu mwanamke bado yuko hapa nyumbani, kwani si umeshamsaidia inatosha?” Sikujua alikuwa ni wakwanza kuanzisha mazungumzo.
“Hilo sio la muhimu kwa sasa, naomba uniambie mama umemuacha wapi, yupo na nini?” Feisal naye akauliza swali badala ya kujibu swali.
“Mama yuko salama usijali”
“Umemuacha na nani usiku huu, mara ya mwisho nakumbuka ulinambia kuwa anaumwa”
“Hali yake sio mbaya sana na tulikuwa wote wakati taarifa zako zinatangazwa kwenye runinga, kafurahi sana kuona umepata bahati kubwa kama hiyo serikalini, hongera Feisal ”
“Asante…”
“Kwa hiyo vipi utaenda Dar?”
“Swali gani hilo unauliza?”
“Hamna nataka tu kujua”
“Nitaenda ndiyo, si umesikia nitajiunga na jeshi la zimamoto na uokoaji”
“Ooh! That’s why nimekuja usiku huu…”
“Una maana gani Sikujua?”
“About your promise Feisal, uliniahidi siku ukirudi Dar utaanza kazi ya kumtafuta kaka yangu Boaz”
“Nakumbuka, siwezi sahau hata siku moja. Iwe walimuua au yuko hai ila tambua lazima nitamtafuta popote alipo na hii ndiyo sababu kubwa nikubali kwenda Dar. Pamoja na kwamba naenda kusoma lakini jukumu langu namba moja litakuwa ni kutafuta Boaz.”
“Nafurahi kusikia hivyo Feisal, niliposikia umepewa ofa kwenda kusoma Dar es salaam sikutaka kupoteza muda nikaona nije haraka nikukumbushe na hili. Nimemkumbuka sana kaka yangu”
“Hata usijali Sikujua, wala hukuwa na haja ya kuja kunikumbusha…”
“Naomba ufanye hivyo Feisal…” Alisema Sikujua wakati huo simu yake ikawa inaita, akatoka nje kuipokea.
Feisal alibaki chumbani amesimama wima akionekana kuzama katika tafakuri nzito, kwa muda alijikuta anazisahau kabisa habari za mwanamke mrembo Sasha pale sebuleni.
Feisal aliinama akavuta sanduku moja chakavu lililokuwa chini ya uvungu wa kitanda, akapekuwa vitu vilivyo ndani yake, mwisho akachukua karatasi moja lililokuwa limekunjwa vizuri, akalikunjua. Ndani ya karatasi hilo kulikuwa na kadi ya benki. Ni ile kadi ya Boaz ambayo akaunti yake inapesa nyingi sana walizopewa na tajiri mmliki wa migodi kama shukrani.
“Nina imani bado uko hai Boaz, nakuja kukutafuta popote ulipo… Nitahakikisha nakurudisha nyumbani na kuwashikisha adabu wale wote waliohusika kukutenga na familia yako” Alisema Feisal, akavuta kumbukumbu zake siku ya tukio la utekaji wa Boaz na wale rafiki zake wengine pale MINI supermarket.
Wakati ule Feisal anarudi kujisaidia haja ndogo ndipo alipokutana na tukio hilo la ndugu zake ambao walikamatwa na watu wa ajabu waliovaa helmet kichwani zenye vioo vya rangi nyekundu. Feisal anakumbuka alijificha na kujibana ukutani kwenye kona ya ukuta akawa anachungulia na kushuhudia rafiki zake wakiingizwa ndani ya gari mmoja baada ya mwingine na kisha wale watekaji wakamaliza na kuingia ndani ya gari pia. Lakini mmoja kati yao alivua helmet yake kabla ya kuingia garini na hapo Feisal akafanikiwa kuiona sura ya mtu huyo.
Kama utakumbuka tukio hili la utekaji pale supermarket ya MINI lilirekodiwa pia na kamera za CCTV na mtu aliyevua helmet alikuwa si mwingine bali Felix mtoto wa Magnus. Pamoja na kwamba kundi la kigaidi MG Family lilifanikiwa kuiiba video ile iliyorekodiwa na kamera za CCTV kwa lengo la kupotea ushahidi lakini kumbe kuna mtu mwingine alikuwepo eneo la tukio na aliweza kuiona sura ya Felix na huyu si mwingine bali Feisal kaka yake David wanaeamini kuwa amekufa.
Katika harakati za kuanza kumtafuta Boaz, Feisal alijua hatua sahihi ya kuanzia ni kumtafuta yule jamaa (Felix) aliyefanikiwa kuiona sura yake siku ya utekaji. Alijua wazi kama atampata Felix basi ataweza kuwapata ndugu na rafiki zake. Lakini jambo ambalo Feisal hakujua ni kwamba kwa sasa Felix ni mtu anayeishi kwa jina na taarifa zake zote baada ya yeye kuaminika kwamba amekufa, na mbaya zaidi hata Mama David ameshinikizwa kumpokea Felix kama mwanae. Lakini vilevile hata Felix na kundi lake hawajui kama Feisal yupo hai na sasa amepata ofa ya kuja jijini Dar es salaam kimasomo.
Ni vita nyingine kati ya Felix na Feisal….
Wakati huo ndiyo kwanza Sasha anajitafuta namna ya kumpata kijana David aliyebeba hatima ya mji wa ajabu ISRA….
Lakini Sasha hajui kama tayari Magnus ameshaagiza watu kuja kumteka na kumpeleka kwenye himaya yake kule kisiwani…..
Felix naye anajitoa ufahamu na kurudisha penzi lake kwa Tesha bila kujali baba yake Magnus atachukua hatua gani…..
Tesha bado yuko gizani hamfahamu ki undani mpenzi wake Felix….
Madam Husnata naye yuko mbioni kuuwasha moto…
Lakini vipi hisia za kimapenzi kati ya Tesha na David ambao tuliona zinaanza kuchipua kati yao Je baada ya ujio wa Felix zitapotea?
Huu ni mwisho wa MSIMU WA PILI (season 2).
Karibu msimu wa tatu kujua zaidi nini kiliendelea katika mfululizo wa mkasa huu wenye matukio ya kusisimua.
MSIMU WA 3 UKO TAYARI NI TSH ELFU 1 TU LIPA KWA MPESA NAMBA 0756862047 KISHA NJOO WHATSAPP NAMBA HIYO HIYO
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
HAKI ZOTE ZIMEHIFADHIWA