Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Noted [emoji120]At least hata vipande vitatu mpaka vitano italeta maana hiki kimoja kimoja na kutuma mwendelezo mpaka wiki ipite inaboa na tunasahau tumeishia wapi.
Badirika SIMULIZI RIWAYA
Lipia mkuu si umeambiwa n buku tu [emoji16]hi thread chenga sana
wengine tunatumia vitochLipia mkuu si umeambiwa n buku tu [emoji16]
Asant kingineSASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya...........39 -40
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA...
"Njia gani mkuu?"
"Ushawishi, tumpe anachokitaka. Nitacheza na saikolojia yake" Alisema Magnus na tayari walishafika chumba cha mateso, mlango ukafunguliwa wakaingia.
SASA ENDELEA....
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili mbele ya macho yake Inspekta Brandina anashuhudia supermarket ya MINI ikiteketea kwa moto hii ikiwa ni tafsiri kwamba hakukuwa na namna nyingine ya kupata kopi ya ile video ya ushahidi iliyorekodiwa na kamera za CCTV.
Haraka alichukua simu yake kutoka mfukoni kisha akampigia Jasusi Jacob ili kusikia upande wake kama kuna chochote amekipata.
"Hallo Inspekta" sauti ya Jacob ilisikika simuni.
"Ndiyo Jacob, hali sio nzuri huku. Wameichoma moto ile supermarket hivi ninavyoongea kila kitu kinageuka majivu. Hatuwezi kupata kopi ya ile CD kabisa" Alieleza Brandina.
"Aisee! Hawa watu mbona wako serious sana..."
"Sana tena sana, na sisi tusipokuwa serious watatupiga bao kila mahali, tunatakiwa kuwa hatua moja mbele yao. Tayari wameshatuzidi akili, tutafute maarifa mapya ya kupambana nao"
"Tunafanyaje sasa Inspekta?"
"Hamna kurudi nyuma, Felix ni lazima aendelee kubaki mikononi mwetu Jacob, tutafute sababu yoyote ya kuendelea kumshikilia"
"Nimepata wazo Inspekta"
"Ndiyo nakusikiliza Jacob"
"Nakumbuka wakati nafuatilia mahojiano yako na Felix mwanzoni kabisa kuna kitu niliona si cha kawaida"
"Kipi hicho Jacob?"
"Ni kuhusu jina halisi la Felix, alidai kuwa alibadili jina baada ya kuhama dini. Lakini akaongeza na kusema alishauriwa na mchungaji, vipi kwa muonekano wa Felix jinsi alivyo unaona ni mtu wa dini kweli?"
Brandina alitulia kidogo kisha akajibu...
"No, hawezi kuwa mtu wa dini yule, uko sahihi Jacob. Tunatakiwa tuchimbe zaidi kuhusu historia ya huyu mtu huenda tukapata kitu"
"Yes! sure, kwani tumebakia na muda gani mpaka sasa?"
"Eee! hapa tuna kama masaa mawili na kidogo..."
"Okay basi wacha tuingie kazini wewe pambana huko na mimi nipambane huku ofisini kwetu tunayo mifumo mizuri ya kuweza kutambua historia ya maisha ya nyuma ya kila mtu. Nitafanya mawasiliano na watu wanaoweza kumfahamu kama ikibidi. Nitafuatilia kila kitu kuanzia alipozaliwa shule aliyosoma na kadharika"
"Inawezekana Jacob? Ndani ya huu mda?"
"Bila shaka Inspekta kama mtu ameweza kusafiri hadi Marekani na kapanda hizi hizi ndege zetu basi lazima taarifa zake tutazipata tu..."
"Okay wazo jema"
"Nitajie basi yale majina yaliyopo kwenye kitambulisho chake"
"Sawa anaitwaa..."
"Sorry ngoja kidogo nichukue pen na karatasi....okay nitajie sasa"
"Anaitwa Feisal Ayoub Suleiman"
"Sawa basi baada ya nusu saa tukutane kituoni pale tuunganishe taarifa..hallo... Inspekta...hallo..." Jacob aliita lakini Brandina akawa kimya ghafula, tayari alishafika pale mahali alipoacha gari lake ajabu hakuliona, akawa anaangaza macho yake huku na kule kulitafuta, hakumjali tena jasusi Jacob aliyekuwa akiita simuni.
"... Inspekta??"
"Eeh nakupata Jacob nusu saa nusu saa tukutane" Brandina aliongea haraka haraka kisha akakata simu.
"Ooops! One mistake one goal!! wanaume wa dar pumbavu kweli" Brandina alijisemea mwenyewe huku akiwa ameshika kiuno chake, tayari alishatambua kuwa gari yake imeibiwa.
Pamoja na yote bado mwanadada huyu machachali hakutoka kwenye lengo, alimpigia simu dereva taksi mmoja anayemfahamu na punde alifika na kumchukua wakaondoka. Bado alikuwa kwenye mapambano makubwa kuhakikisha Felix hatoki kwenye mikono yake, tayari alishajua kuna njama za makusudi zinaendelea.
Ni kweli mara baada ya Inspekta Brandina kuondoka maeneo ya MINI supermarket kwa mbali alionekana mwanamke mmoja mrembo akiwa ndani ya gari dogo Nissan, huyu alikuwa ni mtu kutoka kundi la kigaidi MG Family kazi yake kubwa ni kufuatilia nyendo zote za Inspekta Brandina na kutoa taarifa.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Nusu saa baadae....
Tayari Inspekta Brandina na jasusi Jacob walikutana kituo cha polisi. Sasa waliungana pia na Inspekta Masoud pamoja na askari wengine watatu, wakawa wanajadili taarifa walizozipata.
Jasusi Jacob ndiye aliyeanza kuzungumza akaeleza akisema...
"Anaitwa Feisal Ayoub Suleiman, mtoto wa kwanza wa marehemu mzee Suleiman. Amezaliwa tarehe 19/9/1992. Mwaka 2008 Feisal akiwa na miaka 16 alikuwa akisoma kidato cha pili shule ya Sekondari Mkwawa Mbeya- chunya. Kwa bahati mbaya wakati akicheza na mdogo wake alipata ajali na kutumbukia darajani ndani ya maji. Hakuna aliyefanikiwa kuupata mwili wake zaidi ya mwili wa baba yake marehemu mzee Suleiman ambaye alijitosa majini kujaribu kumsaidia mwanae lakini alishindwa na kujikuta anapoteza maisha."
"Kwa hiyo Feisal alikufa?" Aliuliza Masoud
"Iko hivyo kila mtu kwenye kijiji chake anaamini Feisal alishakufa lakini hakuna aliyewahi kuthibitisha hilo kwa sababu mwili wake haukuonekana mpaka leo, ni miaka 13 imepita tangu kutokea kwa tukio hilo"
"Kwa hiyo inaweza kuwa Felix ndiyo Feisal mwenyewe?" Aliuliza Brandina
"Hii ndiyo maana yake.. huyu ndiye Feisal mwenyewe hakufa alipona na anaishi mpaka leo huku watu wakiamini alishakufa" askari mmoja alitoa wazo.
"Acha kurahisisha mambo afande Chopa, hapa naona kuna akina Feisal wawili huyu wa utotoni na huyu wa ukubwani tunachotakiwa kuthibitisha ni je huyu ni mtu mmoja au ni watu wawili tofauti. Na kama ni tofauti kwa nini Felix anatumia jina la marehemu Feisal? Lazima hapa atakuwa na kesi ya kujibu, au mnasemaje?" Alieleza Jacob na mwisho akauliza swali
"Ni sawa lakini tutathibitisha vipi sasa, hata picha zake za utotoni hatuna" Aliuliza Inspekta Masoud
"Nimepata hii picha moja tu ni kama passport aliyotumia shuleni wakati akiingia kidato cha kwanza na alikuwa na miaka 15 pekee. Nimetumiwa na mwalimu mkuu Sekondari ya Mkwawa huko chunya" alieleza Jacob
"Hebu subiri kwanza, Inspekta Brandina unakumbuka jina la yule kijana ambaye ametekwa juzi pale mgahawani anaitwa nani ulisema?" Aliuliza Inspekta Masoud
"Woow! Uko smart sana Inspekta, yule kijana ni David, anaitwa David Ayoub Suleiman" alisema Brandina kila mmoja akaguna na kujaribu kuwaza.
"Ni majina tu yanafanana au wanaweza kuwa ndugu? Feisal Ayoub Suleiman, David Ayoub Suleiman.... Kwamba hawa wawili ni ndugu yaani mtu na kaka yake?" Aliuliza Masoud
"Ngoja kwanza..." Alisema Jacob kisha akawa anapiga simu mahali, simu iliita na kupokelewa.
"Hallo Headmaster, ni mimi tena kutoka Idara ya usalama wa Taifa... Ndiyo... samahani naomba nikusumbue tena, ulisema yule kijana Feisal aliyefariki alikuwa na mdogo wake unaweza kukumbuka jina la huyo mdogo wake...eeh ndiyo...nani....sawa... asante sana mzee wangu....." Jacob alimaliza maongezi kisha akakata simu. Wote wakawa makini kumsikiliza atasema nini.
"Mdogo wake Feisal anaitwa David" alisema jasusi Jacob, ilikuwa ni taarifa iliyozidi kumfikilisha kila mmoja.
"Kwa hiyo basi ni kweli David na Feisal ni ndugu...kuna mtu mmoja tunaweza kumtumia kuthibitisha kama kweli Felix huyu ndiyo Feisal mwenyewe" Alisema Inspekta Brandina.
"Ni nani..?"
"Ni Mama David"
"Yupo? Huyo mama yuko wapi?"
"Yupo hapa hapa Dar, acha nitafute mawasiliano yake..." Alisema Inspekta Brandina kisha akatoka nje ya kile chumba.
Wakati wote huo Felix alikuwa ndani ya kile chumba cha mahojiano akisubiri, tayari alishachoka. Akawa anahesabu masaa huku akiamini kabisa hakuna watakachopata, mwisho atatoka, watamuachia huru. Mpango wa MG Family kuhakikisha anakuwa huru ulikuwa umesukwa ki ufundi sana.
Ni kweli kabisa wakati Magnus amefukuzwa ISRA akiwa na mtoto wake mdogo Felix aliyaanza maisha yake kule kisiwani lakini wakati wote Felix alikuwa akimsumbua akitaka kuingia uraiani. Baadae sana Magnus aliwapa jukumu hili MG Family watafute namna ambayo mwanae Felix atatambulika kama Raia wa kawaida nchini. Ndipo hapo MG Family walipoingilia taarifa za mtu aliyewahi kupotea Feisal Ayoub Suleiman wakazibadilisha taarifa hizo zikawa za Felix.
Felix akaingia uraiani akiishi kwa jina la Feisal, vitambulisho vyake na kila kitu vikapewa jina la Feisal. Hii ndiyo sababu hata wakati ule Tesha alipouliza abiria aliyepanda ndege ya BOENG 707 mwenye jina la Felix hakulipata.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili nyumbani kwa Mama David. Bado mama huyu alionekana kuwa kwenye majonzi makubwa tangu siku ya jana alipotembelewa na ugeni wa ghafula pale alipotoka hospitali.
Sasa Mama David alikuwa amekaa varandani nje ya nyumba yake huku akilia kwa kwikwi akisema...
"Mwanangu alishakufa...hawezi kuwa hai...mwanangu Feisal alikufa, mrudisheni Tatu wangu, eeh! Mungu kwa nini unaruhusu nipitie kwenye huu mtihani. Nalazimishwaje kukubali mwanangu anaishi wakati najua ulishamchukua.. Eee Baba nitazame mimi mwanao, ni nini hiki mbona sielewi" Mama David alikuwa akilia na kulalamika.
Siku ya jana alipotembelewa na Husnata kutoka MG Family hali ilikuwa hivi....
[emoji294][emoji294][emoji294]
NYUMBANI KWA MAMA DAVID JANA BAADA YA KUTOKA HOSPITALI...
Kulikuwa na gari tatu za kifahari zimepaki nje ya nyumba yake.
"Karibuni" Alisema Mama David mara baada ya kufika nyumbani kwake, ingawa aliogopa lakini alijikaza na kuongea.
"Asante mama vipi hali yako? Unaendeleaje?" Aliuliza Husnata kauli iliyomshangaza sana Mama David, ni vipi mtu huyo katambua kama yeye anaumwa.
"Asante"
"Tunaweza kukaa na kuzungumza kidogo mama..."
"Sawa tu karibu ndani" Alijibu mama David. Akafungua mlango kisha wakaingia ndani yeye na Husnata pekee, Tatu na wengine wote wakabaki pale nje.
"Nakusikiliza mwanangu"
"Asante mama. Nikulize kitu...hivi utajisikiaje kusikia mwanao anaishi." Alisema Husnata kauli iliyo mshtua sana Mama David, akauliza...
"Mwanangu yupi?"
"Mwanao Feisal, ukisikia kuwa hakufa ule mwaka 2008 yupo hai na anaishi mahali fulani..!!"
Mama David alijisikia vibaya sana kuulizwa swali la namna ile, lilimtonesha kidonda ambacho kilishapona muda mrefu na kubaki kovu. Aliinua uso wake taratibu na kumtazama Madam Husnata kwa macho makali.
"Ulishawahi kuzaa we binti?"
"Mmh?"
"Nauliza una mtoto?"
Madam Husnata akatikisa kichwa kukataa.
"Ndiyo maana, basi nikwambie kitu usichokijua sisi akina mama Mungu ametuumba kwa namna ya ajabu sana tuna muunganiko wa kipekee na wanetu tuliowazaa, kama Feisal angekuwa hai au kungekuwa na dalili za kumpata basi ningepata ishara kabla hata hujaja. Feisal mwanangu alishakufa, nambie unataka nini kwangu nikusaidie" Alisema Mama David maneno ambayo kwa kiasi hayakumfurahisha Madam Husnata akaamua aende kwenye lengo moja kwa moja.
"Sawa mama basi kama ni hivyo kuna taarifa muhimu nataka nikupe, ni kweli mwanao Feisal alishakufa lakini kuna mtu ambaye yupo anaishi kwa jina na taarifa zake. Kwa sasa huyu mtu yupo kwenye matatizo makubwa sana. Itafika wakati polisi watahitaji taarifa zake nyingi kutoka kwako na ikibidi uthibitishe kama mtu huyo ndiye mwanao Feisal au laa. Sisi tupo hapa kwa ajili ya kukuomba ufanye hivyo. Kubali huyu mtu ni mwanao Feisal aliyepotelea majini miaka 13 iliyopita" Alieleza Husnata Mama David akahisi mwili wake unakufa ganzi.
"Binti.." aliita mama David kwa sauti ya upole
"Ndiyo mama nakusikiliza, kuna pesa nyingi sana tumekuandalia kwa ajili ya kazi hii, hili begi linapesa nyingi zitakazo kufanya uuage umaskini"
"Achana na hizo pesa kwanza... Je, unafikiri hakuna namna nyingine ya kuthibitisha kuwa huyo mtu wenu sio mwanangu Feisal? Ni kauli yangu pekee ndio inatosha?"
"Najua kuna namna nyingine, lakini wewe kazi yako ni hiyo tu kubali huyu mtu ni mwanao hayo mengine tuachie sisi"
"Siwezi na naomba uondoke" sasa Mama David alifoka.
"Sawa naondoka tutakupa maelezo nini cha kufanya zaidi subiri simu yetu, hizi pesa baki nazo na ukijaribu kutoa taarifa kokote basi utampoteza mwanao wa pili ambaye ni huyu binti mdogo hapo nje tunaondoka naye. Narudia tena kaa usubiri simu yetu kesho" Alisema Husnata na kuondoka.
Mama David alipojaribu kutoka kumfuata alizuiliwa mlangoni na mwanaume mlinzi mmoja wa Husnata. Alishuhudia kwa macho yake mawili mwanae Tatu akikamatwa na watu hao kisha wakapanda garini na kuondoka kwa kasi. Mama David alilia sana pasipo msaada. Siku hiyo ilikuwa ngumu mno kwake, hakula kunywa wala kulala. Hadi kunapambazuka bado alikuwa katika hali ya huzuni Feisal hayupo, David hayupo na Tatu pia hayupo, mama huyu alipata maumivu yasiyo na mfano. Kwa ajili ya usalama wa mwanae ilimbidi Mama David afanye kama alivyoelezwa akawa kimya na kuugulia kwa ndani huku akisubiri simu tukoka MG Family.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati mama David akiwa pale nje valandani akilia mara simu yake iliita haraka akatazama namba ya mpigaji ilikuwa ni namba ngeni, moja kwa moja akaamini watakuwa ni wale watu waliomteka mwanae Tatu. Akapokea haraka.
"Hallo shikamoo mama, unaongea na Inspekta Brandina kutoka kituo cha polisi tafadhali tunamazungumzo muhimu sana na wewe naweza kujua uko wapi kwa sasa nije kuchukua, ni muhimu sana Mama yangu"
Alisikika Inspekta Brandina simuni lakini kabla Mama David hajajibu lolote mara kuna gari ilifika kwa kasi na kufunga breki kali mbele ya nyumba yake. Kufumba na kufumbua mlango wa gari ukafunguliwa, akashuka mwanadada Husnata akiwa na walinzi wawili nyuma yake.
Je nini kitafuata?
ITAENDELEA...
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya.........40
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA...
Alisikika Inspekta Brandina simuni lakini kabla Mama David hajajibu lolote mara kuna gari ilifika kwa kasi na kufunga breki kali mbele ya nyumba yake. Kufumba na kufumbua mlango wa gari ukafunguliwa, akashuka mwanadada Husnata akiwa na walinzi wawili nyuma yake.
SASA ENDELEA....
Baada ya Mama David kumuona Husnata mwanamke ambaye aliondoka na mwanae Tatu siku ya jana alishtuka na kujikuta anashindwa kuijibu simu ya Inspekta Brandina.
Akiwa katika hali hiyo Husnata ambaye alianza kumsogelea taratibu alimuonyesha ishara kuwa aendelee na mazungumzo kwenye simu ile. Mama David aliielewa ishara hiyo kisha akajibu...
"...nipo nyumbani kwangu kwa sasa..."
"Sawa basi tunakuja sasa hivi kukuchukua Mama" Brandina alizungumza upande wa pili wa simu.
"Unapafahamu nyumbani?"
"Yes! Nimepewa adress, dakika kumi tutakuwa hapa"
Simu ikakatwa.
Mama David aliinuka haraka mara baada ya simu ile kukatwa, sasa akawa anatazamana uso kwa uso na Husnata ambaye alishafika na kusimama mbele yake.
"... mwanangu yuko wapi?" Hili lilikuwa ni swali la kwanza kutoka kwa mama David.
"Kuwa mtulivu mama, mtoto wako yuko salama, kama utaifanya kazi yetu ipasavyo nakuhakikishia hatutomgusa hata unywele wake"
"Mnataka nifanye nini sasa?"
"Tuingie ndani kwanza" Alisema Husnata kisha yeye na mama David wakaongozana na kuingia ndani sebuleni.
Baada ya kuingia Husnata alienda moja kwa moja ilipo Televisheni ndogo ya Mama David akaiwasha, akawasha pia na king'amuzi chake aina ya Zuku.
"Hey! Hakuna kifurushi chukua namba ya kadi nunua..." Husnata alimuagiza mmoja kati ya walinzi wake kisha akageuka na kumtazama Mama David ambaye alikuwa akimtazama tu mwanamke huyo asielewe ni nini hasa anafanya.
"Mama David, hii ni picha ya mtu niliyekwambia jana, mtu ambaye anaishi kwa jina la mwanao Feisal. Polisi wanakuja hapa ndani ya muda mfupi kama walivyokupigia simu na kukueleza. Kuna kitu unatakiwa ufanye mara tu watakapofika, hii ni kwa ajili ya usalama wa binti yako. Leo itabidi uwe muigizaji mzuri" Alisema Husnata huku akimkabidhi Mama David picha ya Felix kisha akaanza kumpa maelezo nini cha kufanya. Mama David hakuwa na jinsi, alisikiliza na kukubaliana na kila agizo alilopewa. Alifanya hivi kwa ajili ya usalama wa mwanae mdogo Tatu ambaye mpaka sasa yupo kwenye mikono ya watu hawa.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Wakati huo upande wa pili kituo cha polisi, Inspekta Brandina akiwa pamoja na askari wengine wawili waliingia ndani ya gari la polisi na safari kuelekea nyumbani kwa mama David ikaanza. Kama kawaida yule mwanamke ndani ya gari aina ya Nissan kutoka MG Family hakuwa akicheza mbali. Alipowaona tu wakitoka naye akaingia barabarani na gari yake akawa anawafuata nyuma.
Wakati huo Jasusi Jacob pamoja na Inspekta Masoud wao waliingia chumba kile cha mahojiano mahali walipomuacha Felix kwa muda.
Walimkuta kijana huyo amekaa pasipo kuwa na wasiwasi wowote huku miguu yake akiwa ameinyoosha na kuiweka juu ya meza, wala hakujali.
Baada ya Jacob na Masoud kuingia Felix alitazama saa yake ya mkononi, sasa lilisalia lisaa limoja pekee ili yatimie yale masaa manne ambayo ni ya mahojiano kisheria katika ofisi za kipelelezi. Baada ya hapo kama hatokutwa na shitaka lolote basi ni haki yake kuachwa huru.
Masoud na Jacob walizunguuka upande wa pili wa meza na kukaa kwenye viti, wakawa wanatazamana na Felix ambaye aliishusha miguu yake chini.
"Sasa mnaweza kuniambia kwa nini niko hapa ndugu zangu? maana siwaelewi kabisa"
"Usijali.. iko hivi Bwana Felix, tumetilia shaka jina lako unalotumia yaani Feisal Ayoub Suleiman kwamba huenda sio jina lako halisi. Je, unaweza kutuambia japo kwa kifupi historia ya maisha yako kabla hatujaenda hatua inayofuata" Alizungumza Inspekta Masoud.
"Hebu subiri kwanza, sijaelewa mnata kujua kwa nini watu wananiita Felix badala ya Feisal? Mbona nilishamwambia yule askari wa kike tayari!!"
"Hapana hujatuelewa, tunataka utueleze kwa kifupi historia ya maisha yako tangu kuzaliwa kwako mpaka hapa ulipo, kwa kifupi tu halafu mambo mengine yataendelea..."
"Mmm!! Basi sawa, kwa kifupi kama mlivyosema mimi naitwa Feisal Ayoub Suleiman, nimezaliwa Mbeya-chunya na kusoma huko mpaka kidato cha pili, mwaka 2008 nilipata ajali mbaya nikatumbukia majini, sikujitambua hadi siku nne baadae ndipo nilipata fahamu nikajikuta niko jijini mbeya mikononi mwa mtu nisie mfahamu ambaye alitaka kunitumia katika biashara zake ovu. Kwa bahati mbaya pia nilipoteza kumbukumbu zangu baada ya ajali ile sikuwa nakumbuka chochote, hata jina langu tu sikulikumbuka pia. Kwa bahati nzuri niliweza kusaidiwa na mtu mmoja ambaye ndiye amenilea na kunikuza hadi hapa nilipofikia. Nilikaa kwa kipindi kirefu sana ndipo baadae kumbukumbu zangu zilianza kurejea upya taratibu. Mwisho nilirudi nyumbani Chunya kuwatafuta ndugu zangu sikuwapata niliambiwa walihama zamani sana mara baada ya mazishi ya baba yangu, nimehangaika kwa kipindi kirefu mno kuitafuta familia yangu bila mafanikio mpaka sasa tunavyoongea. Huwa naumia sana afande, nimeishi kwenye mazingira ambayo sina hata ndugu mmoja wa damu ninaemjua, nipo mimi kama mimi" Felix alimaliza simulizi yake yenye uongo uliokubuhu. Historia iliyowafanya Inspekta Masoud na Jasusi Jacob watazamane na kushika tama. Ingekuwa ni mechi mpaka sasa tungesema Felix anaongoza mbili bila. Kila kete waliyojaribu kusukuma askari hawa waliambulia patupu. Mwanzo waliamini kama Felix sio Feisal basi angejichanganya mahali katika maelezo yake, la hasha maelezo ya Felix yalijitosheleza mno. Sasa ni mama David pekee ndiye aliyekuwa akitegemewa kwa muda uliobaki.
Huwezi kuamini mpaka dakika hii bado polisi hawa walikuwa hawajazungumza chochote mbele ya Felix kuhusu kesi kubwa ya utekaji. Wangeanzia wapi kueleza? Kwa ushahidi upi? CD yenye ushahidi haipo na hata Felix bado anatengeneza mazingira ya kuwafanya waamini yeye ndiye mmiliki wa jina la Feisal Ayoub Suleiman.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili kule mkoani Mtwara katika kijiji cha Nagaga tayari kikosi cha uokoaji kilishawasili na sasa zoezi la uokoaji kwa wahanga wa janga la mafuriko lilikuwa likienda vizuri.
Feisal ambaye huyu ndiye Feisal halisi kaka yake David, alimchukua Sasha mpaka nyumbani kwake katika kijiji jirani cha Nachingwea wilaya hiyo ya Masasi. Feisal alipanga kumsaidia dada huyo(Sasha) mpaka pale kumbukumbu zake zitakapo rejea. Hakujua kuwa Sasha alikuwa akijitambua vizuri tu lakini aliamua kutumia uongo wa kujifanya kapoteza kumbukumbu ili tu kuficha asili yake kwamba ni mtu wa ajabu kutoka ISRA.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Gari la polisi lilifunga breki kali nje ya nyumba ya Mama David. Inspekta Brandina alikuwa ni wa kwanza kushuka, akawa anapiga hatua ndefu ndefu kuuelekea mlango wa nyumba hiyo ambao ulikuwa wazi, askari wenzake wakawa wanamfuata nyuma. Wakati huo hakukuwa na gari lolote nje ya nyumba ya Mama David, Husnata na wenzake hawakuwepo.
"Hodi hapa, ma...."Alisema Inspekta Brandina lakini mara akasita kuendelea baada ya kumuona mama David akitoka chumbani kwake kwa kasi huku akijifunga kitenge chake, alionekana kuwa na haraka sana.
"Vipi mama uko sawa?" Brandina aliuliza huku akipiga hatua zaidi kuingia ndani.
"Mwanangu jamani mwanangu...." Alisema mama David hali akizunguuka huku na kule mle sebuleni kama anaetafuta kitu. Alionekana kuchanganyikiwa haswa.
"Hebu tulia basi mama, unashida gani? Sisi ni polisi mimi ndio niliongea na wewe kwenye simu muda si mrefu.."
"Ninyi ni polisi? Ooh! Sawa..." Alisema mama David, akaelewa zaidi mara baada ya kuwaona wale askari nyuma ya Inspekta Brandina ambao wao walivalia sare zao za polisi.
".....nimemuona mwanangu kwenye Tv, mmemkamata mwanangu Feisal, ni mwanangu alipotea miaka mingi sana iliyopita. Naomba nipelekeni nikamuone" Alisema Mama David kauli iliyomuacha kinywa wazi Inspekta Brandina. Akageuka na kutazama Tv ni kweli kabisa wakati huo kupitia chaneli ya MMD TV walikuwa wakirusha habari za mwanamitindo maarufu nchini Tesha ambaye alionekana uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere asubuhi ya siku hiyo akiwa katika hali ya huzuni kubwa mara baada ya kushuhudia mwanaume mmoja(Felix) ambaye bado mahusiano yao hayajajulikana akikamatwa na polisi. Katika Tv Tesha alionekana wakati ule akiwa amekaa chini baada ya kuishiwa nguvu eneo la mapokezi alipoambiwa na Inspekta Brandina kuwa Felix anahusika na utekaji wa David na wengine.
Inspekta Brandina aliitazama taarifa hiyo kisha akageuka kumtazama Mama David ambaye aliendelea kusisitiza kuwa wampeleke kituo cha polisi akamuone mwanae Feisal aliyempoteza kwa muda mrefu.
Brandina alijikuta anachoka mwili na akili, hata kabla hajaeleza kilichomfanya kuja kwa mama huyo tayari alikuwa na majibu ya maswali yake yote. Tayari Mama David kamfahamu mwanae hata kabla ya kuulizwa.
"Kwa hiyo kumbe ni kweli Felix ni Feisal... nafanyaje sasa" Aliwaza Brandina huku akikaa Kwenye kiti. Hakujua ni ushahidi gani ambao utamfanya aendelee kumshikilia Felix kwa kesi ile ya utekaji. Ingawa ni kweli kabisa Brandina pamoja na askari wengine waliishuhudia ile video orijino ambayo Felix alionekana dhahiri akiwa miongoni mwa watu waliofanya utekaji pale supermarket ya MINI lakini video hiyo imeibiwa haipo kwenye mikono yao tena. Watamshitaki Felix kwa lipi? Kwa ushahidi gani? Hawawezi hata kupeleka kesi mahakamani bila vielelezo muhimu.
Dakika mbili baadae gari hilo la polisi liliondoka kwa kasi huku mama David akiwa pamoja nao.
Kwa mbali Husnata na watu wake walionekana pembeni ya barabara wakilisindikiza kwa macho gari hilo la polisi.
"Mama ni muigizaji mzuri zaidi hata ya watu wa bongo muvi..." Alisema Husnata huku akitabasamu na kuweka simu yake sikioni.
"Hallo.. tuko kwenye hatua za mwisho endelea kuwafuatilia" Alisema Husnata kisha akakata simu. Alikuwa akiwasiliana na yule dada ndani ya gari la Nissan ambaye kazi yake kubwa ni kumfuatilia Inspekta Brandina.
ITAENDELEA....
Simulizi hii inapatika kwa tsh elfu 1 tu njoo WhatsApp namba 0756862047
Bila shidafb unarusha wengne hatuna whatsap
nakupataje fbBila shida
Njoo hpanakupataje fb