Kalpana
JF-Expert Member
- Jun 16, 2017
- 32,603
- 62,269
Abeee ndo naingia sicy
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Abeee ndo naingia sicy
SawA SawAAbeee ndo naingia sicy
[emoji3064][emoji3064][emoji3064]We jamaa bwana, yan ukimya wote uo,alaf unakj na vpande viwili,!! ata ka atulipii, ila kurud kwak kunapaswa kuwa na kixhndo
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........16
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA...
Mmesababisha majanga makubwa sana ndani ya ISRA, kutoweka kwa msitu wa Bi Noha ni laana kubwa ndani ya ISRA, ni lazima muwajibike kwa hili" Alisema Dumayo.
Je nini kitafuata?
SASA ENDELEA...
ISRA ...
Mkuu wa ISRA Gu Gamilo pamoja na askari na baadhi ya wafanyakazi wengine ndani ya Ikulu ya ISRA walionekana pembeni ya shimo kubwa mahali palipokuwepo msitu mkubwa maarufu kama msitu wa Bi Noha.
Walikuwa wakitazama maafa makubwa yaliyotokea kiasi cha kusababisha msitu huo kutoweka wote kwa namna ya ajabu sana. Ilikuwa ni hali iliyomshangaza kila mmoja. Hakuna aliyekuwa na jibu sahihi ni kipi hasa kimepelekea msitu huo kupatwa na majanga na mwisho kuzama wote ardhini.
Gu Gamilo baba yake Sasha alitazama kwa umakini huku uso wake ukionekana kujawa na wasiwasi mwingi.
Gu Gamilo alikuwa ni mzee kiasi sura yake iliyokunjamana wakati wote, ilikuwa ni adimu kuliona tabasamu la mzee huyo. Nywele zake ndefu na nyeupe alizozifunga kwa juu, huku kidevu chake kikiwa kimefunikwa na ndevu zenye rangi nyeupe vilevile vilimfanya mzee huyo kuwa na muonekano wa pekee katika ISRA.
Mpaka dakika hiyo hakuna aliyejua sekeseke lilotokea upande wa pili wa shimo hilo kule walipo Dumayo Sasha na akina Handan.
Tukio la kutoweka kwa msitu huo lilionekana kumtisha sana Gu Gamilo kiasi cha mkumfanya akumbuke kwa mara ya mwisho alivyoingia ndani ya msitu huo akafanikiwa kuonana na Bi Noha ambaye kwa sasa ni marehemu. Gu Gamilo aliyakumbuka vizuri maneno mazito aliyowahi kuelezwa na bibi kizee huyu, alisema...
...... Umefanya kosa kubwa bila kufikiria kwa makini Gu Gamilo, kumfukuza Kaka yako MAGNUS nje ya ISRA bado hujamaliza tatizo, kwa kosa alilofanya alistahili adhabu kubwa zaidi ya hiyo. Ipo siku utayakumbuka maneno yangu Siku ambayo Magnus atarudi tena ISRA na kuitikisa kwa mara nyingine. Haijarishi itachukua miaka mingapi lakini jua kwamba Magnus ni lazima atarudi tena akiwa amejipanga vilivyo. Atakushambulia kutoka pande zote, mashariki magharibi kaskazini na kusini. Itakuwa ni siku ambayo utakosa kwa kukimbilia hata msitu wangu ambao pengine ungeweza kujificha hautokuwepo tena, litakuwepo shimo kubwa lisilo na mwisho Gu Gamilo..........
Haya yalikuwa ni maelezo ya Bi Noha ambaye ni kama alijua siku moja msitu wake utatoweka na kubaki shimo.
........Bi Noha, nifanyaje sasa kuzuia hili lisitokee tafadhali nisaidie, nawezaje kumzuia kaka Magnus...........
........Hakuna mtu yeyote ISRA atakae weza kumzuia Magnus, isipokuwa yupo Mwanadamu mmoja ambaye ataweza kupambana naye na kumzuia Magnus asirudi tena ISRA, mwanadamu huyo anahitaji ulinzi. Kama atakufa basi ISRA itakuwa kwenye wakati mgumu, kama akiwa hai basi ISRA itaendelea kusimama...........
........Ni mwanadamu gani huyo Bi Noha, unaweza kuniambia tafadhali.........
.........Mtafute, na hakikisha unamlinda kabla Magnus hajamtambua........
Hizi zilikuwa ni kumbukumbu za Mkuu wa ISRA Gu Gamilo. Baada ya hapo aliondoka kinyonge yeye na watu wake huku kila mmoja akisubiri kwa hamu Gu Gamilo atasema nini baada ya tukio hilo ambalo wengi waliliona kama ishara mbaya kwa ISRA.
Hatimae Gu Gamilo alilejea Ikulu ya ISRA yeye na msafara wake, wakati anaingia lango kuu la Ikulu alipokelewa kwa shauku na mkewe kipenzi Malkia Hella(Mama yake Sasha). Alikuwa akimsubiri Mumewe kwa hamu ili amueleze ni nini hasa kimetokea maana kila mtu alionekana kuogopa.
Alipoiona Sura ya huzuni kwa mumewe Gu Gamilo ilikuwa ni tafsiri tosha kuwa mambo hayakuwa mazuri kabisa.
"Ni nini kinaendelea huko nje Gu Gamilo..." Aliuliza Malkia Hella
"Umetoweka.." Gu Gamilo alijibu kinyonge
"Nini? Nini kimetoweka!?"
"Msitu wa Bi Noha" Ilikuwa ni kauli iliyo muacha kinywa wazi Malkia Hella.
Akiwa katika hali hiyo ya mshangao mara wakasikia mlio wa farasi langoni. Gu Gamilo na mkewe wakageuka taratibu kutazama.
Uso kwa uso wakamuona Dumayo anaingia taratibu na msafara wake. Gu Gamilo aliikunja sura yake akionyesha wazi ni jinsi gani alikuwa anamchukia shemeji yake huyo. Lakini tofauti na Malkia Hella yeye alitabasamu mara baada ya kumuona kaka yake Dumayo anaingia.
Katika hali ya kushangaza nyuma ya msafara wa Dumayo walionekana wanawake wanne wakiwa wamefungwa kamba mikokoni huku wakivutwa na watu wa Dumayo waliokuwa juu ya farasi. Wanawake hawa walikuwa ni Sasha, Handan pamoja na wale walinzi wengine wawili.
Gu Gamilo alitoa macho kwa mshangao asiamini anachokiona.
"Sasha" Gu Gamilo aliita kwa sauti ya chini.
Wakati huo Dumayo yeye awaka anatabasamu tu kama kawaida yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili......
David alifumbua macho yake taratibu fahamu zikiwa zimemrejea. Hali akiwa na maumivu makali ya kichwa, alitazama mahali alipo. Alikuwa ndani ya chumba kimoja kipana huku mikono na miguu yake ikiwa imefungwa na vyuma maalumu vilivyokuwa ukutani. Alikuwa ametanuliwa mikono yake na kusimamishwa kama vile yupo msalabani.
Alipotazama mbele akawaona wale jamaa wenye helmet zenye vioo vyekundu wakimalizia kuwafunga watu wengine watatu ukutani kama vile walivyomfunga yeye baada ya hapo wakafungua mlango wa chumba hicho wakatoka na kuondoka. David alitazama kushoto na kulia kwake ndipo akagundua kuwa karibu kuta zote nne za chumba hicho kulikuwa na watu wamefungwa kama yeye na wengi wao walikuwa wamepoteza fahamu hawajitambui. Kwa Haraka haraka aliwahesabu walifika kumi na mbili. David aliogopa sana, hakuelewa ni wapi yupo na amefikaje. Bado kumbukumbu zake zilikuwa hazijakaa sawasawa.
"Oya nyie, nifungueni, njooni mnifungue....mnajua mimi ni nani!??" David alianza kupiga kelele huku akifoka.
"NYIE JAMAAAAAAA..."
David alizidi kupiga kelele.
"Kelele zako hazito saidia kitu, unamaliza nguvu zako bure..."
Mara sauti hii ya kike ilisikika kutoka pembeni yake upande wa kushoto. Haraka David akageuka kutazama ni nani aliyemuongelesha.
Uso kwa uso akagonganisha macho yake na mmoja kati ya wale wanawake waliokuwa wakimfuatilia tangu awali. Alikuwa ni Femi, naye alikuwa amefungwa vilevile kama yeye.
David aliogopa sana alipomuona lakini alipogundua naye amefungwa kama yeye aliduwaa huku kumbukumbu za matukio kadhaa yaliyotokea tangu alipoanza kuwaona wanawake hao wa ajabu zikijirudia kichwani kwake kama filamu.
"We..we. ni nani?"
"Naitwa Femi..." Alijibu Femi huku akitema mate chini, mate yaliyochanganyikana na damu ya kijani.
David alitazama yale mate pale chini kisha akageuka tena na kumtazama yule mwanamke akiwa katika hali ya mshangao mkubwa.
"Fe..femi wa wapi? Kwa nini mlikuwa mnanifuatilia?"
"Kwa sababu tunataka kukuua" Femi alieleza bila kusita
"Bado unaendeleza ukichaa wako Femi si ndiyo?" Mara sauti ya Zucc kutoka upande wa kulia kwa David ilisikika. David alishtuka na kugeuka kumtazama.
"Na wewe pia ulikuwa ukinifuatilia..!" Alisema David lakini bado alionekana kuogopa.
"Achana naye huyo!" Alisema Femi akimtaka David asiendelee kuzungumza na Zucc, David akageuka tena upande wake wa kushoto alipo Femi.
"Mnataka kuniua nimewakosa nini kwani?"
"Tumeagizwa tukuue..." Alijibu Femi lakini kabla hajaendelea zaidi Zucc akamkatisha kwa sauti kali iliyojaa hasira, hakupendezwa kabisa na anachokifanya mwenzake.
"Femi nimesema acha ujingaaaa ..." Alifoka
"Zucc hakuna tulichobakiza kwani hata nikimwambia ukweli kuna ubaya gani? Unafikiri tutapona na tayari tumeshafanya uzembe wenyewe mwisho tumeingia kwenye mikono ya MAGNUS" Alieleza Femi.
"Ma..ma.. Magnus ndio na..nani kwani?" Aliuliza David akiwa ndio kwa mara yake ya kwanza analisikia jina la mtu huyo MAGNUS , mtu ambaye kwa mujibu wa maelezo ya marehemu Bi Noha anatakiwa kupambana naye siku za usoni.
Kabla David hajajibiwa swali lake mara wakasikia mtikisiko mkubwa na baadae wakahisi kama wanasogea mbele.
Kumbe chumba hicho kilikuwa ni moja kati ya vyumba vingi ndani ya Meli moja kubwa ambayo sasa iling'oa nanga na kuanza kukata mawimbi taratibu kuelekea kusiko julikana.
ITAENDELEA...
0756862047
Wabheja sana dear ngoja nitulie niisome vizuri!!!
OoohUmerudia mkuu SIMULIZI RIWAYA