Simulizi: Sasha Mlinzi wa Nafsi - 1

Simulizi: Sasha Mlinzi wa Nafsi - 1

SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............31-32
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Dayana mbona kama hauko sawa" David aliuliza wakati wakipiga hatua kusonga mbele lilipo pango hilo.
"Huwezi kuamini David moyo wangu hauna amani kabisa, napata hisia mbaya sana. Sidhani kama huku tunakokwenda ni salama" Alisema Dayana.

SASA ENDELEA...
"Huo ndiyo uchawi sasa kama hutaki kwenda ni heri ukabaki sawa Dayana" Zungu alifoka akionekana kutofurahishwa kabisa na kauli ya Dayana.

"Jamani sasa kwani mimi kusema vile najisikia ni kosa?" Dayana alijitetea.

"Sawa lakini hakuna ambaye hana hisia mbaya hapa, kila mtu anaogopa ila tunafanya kwa sababu tumechoshwa na maisha ya humu bondeni"

"Oya! yaishe basi jamani tu-focus kwenye lengo, kwanza mnapiga kelele tu hapa" David aliingilia kati.

Waliendelea kutembea na kusonga mbele huku mwanga wa mwezi ukiwa ni msaada mkubwa kwao. Baada ya mwendo kama wa dakika saba hivi mwisho Zungu alisimama ghafula.

"Ni hapa, inabidi tupite kwenye huo uchochoro hapo mbele" Alisema Zungu akinyoosha kidole chake kuelekea kwenye ukuta wa bonde hilo mahali kulipokuwa na ufa mkubwa.

"Tunapita kwenye huo ufa?" Aliuliza Dayana.

"Ndiyo ila kuweni makini kuna shimo hapa mbele inabidi turuke kwanza..." Alisema Zungu akiwa ndio wa kwanza kuruka.
David alisimama na kulitazama lile shimo macho yake yakionekana kuwa na wasiwasi.

"Unaanza au nitangulie mimi?" Dayana alimuuliza mara baada ya kuona David ni kama anasita

"Aa..we..we anza tu" Alijibu David huku akijaribu kuficha wasiwasi aliokuwa nao.

Dayana akaruka hadi upande wa pili kule alipo Zungu. Sasa ikawa ni zamu ya David. Ajabu ni kwamba David alionekana kuogopa sana kiasi cha kuwashangaza Zungu na Dayana. Shimo halikuwa kubwa sana la kutisha hata mtoto mdogo wa miaka kumi akijitahidi sana anaweza kuruka lakini kwa David ilionekana kuwa mtihani mgumu.

"Oya acha utani basi ujue tunakusubiri wewe" Zungu aliongea akihisi labda David anawatania, mwisho japo kwa taabu sana David aliruka hadi upande wa pili, lakini alikuwa akihema sana huku mapigo yake ya moyo yakimuenda mbio isivyo kawaida akawa ameinama na kushikilia magoti yake. Mara baada ya David kuruka Zungu aliendelea na safari lakini Dayana alimfuata David akamshika mgongoni.

"Davii.. shida nini unaumwa?"

"Hapana niko poa" Alijibu David huku akiinuka, akavuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu, kisha akampa ishara Dayana kuwa waendelee kwenda.

"Sitaki kuamini kama kuruka lile shimo ndio unahema kiasi hicho?"

"Aah! We acha tu, ni historia ndefu"

"Historia tena?" Aliuliza Dayana lakini wakakatisha mazungumzo yao mara baada ya kumfikia Zungu.

Sasa wakaanza kupenya kwenye ule uchochoro mahali ambapo kuta za bonde hilo zilikuwa zimeachana na kuacha ufa mkubwa. Walitembea kwa tahadhali kila mmoja akiwa makini asije kukanya kitu chochote cha kudhuru mwili.

Baada ya hatua kama arobaini hivi mara waliona pango kubwa mbele yeo. Pango liliokuwa na giza nene ndani yake.

"Ni hapa, hii ndiyo njia yenyewe David" Alisema Zungu. David akapiga hatua mbele akawa anaangalia kwa makini.

"Kwa hiyo tunatakiwa kulifuata uelekeo wa hili pango mpaka litakapoishia?"

"Ndiyo David"

"Vipi kuhusu hili giza, tutaonaje mbele tunapokwenda?"

"Mbele kuko salama, niliingia mchana, lakini hata hivyo kuna mwanga upo utatusaidia. Nilishaandaa kila kitu msijali. Subirini hapa" Alijibu Zungu, akapiga hatua kusogea mbele akaingia ndani zaidi kwenye lile pango, akawa haonekani kabisa kutokana na giza nene lililokuwepo mle ndani.

Dayana na David walibaki wamesimama pale nje ya pango wakimsubiri kiongozi wao Zungu aseme neno.

"Sio muoga kabisa huyu jamaa.." Alisema David.

"Inaonekana wazi harakati zake hazijaanza leo" Alijibu Dayana na mara hiyo walisikia sauti za mawe yakigongana mle pangoni. Haukupita muda wakaona mwanga wa moto. Zungu alikuwa amewasha moto kwenye nyasi na baadae akaweka kipande cha mti ambacho juu yake alifunga majani fulani mabichi lakini hushika moto na kuwaka kwa muda mrefu. Aliwasha kipande cha kwanza kisha cha pili.

"Njooni basi" Zungu aliita.
David na Dayana walisogea wakaingia mle pangoni. Zungu akampatia David kile kipande cha mti chenye moto juu yake, yeye akabaki na kile kipande kingine.

"Hizi ndio tochi zetu kwa leo, haya twendeni..." Alisema Zungu.

Safari ikaendelea. Vijana hawa watatu wakawa wanakatisha ndani ya pango lile la kutisha. Hii yote ikiwa ni Katika harakati za kupambana kuhakikisha wanajitioa kwenye mikono ya Magnus.

"Unajua nini David" Alisema Zungu

"Niambie kamanda"

"Natamani sana kama tutafanikiwa kwenye hili basi tuwatoe watu wote mle bondeni"

"Yeah! Ni kweli yaani umewaza kama mimi Zungu, kama tukifanikiwa basi tusiwaache wenzetu" David aliongezea.

"Mmh! Ndugu zangu vipi tena, yaani mambo ndio kwanza yaanza mshaanza kuweka mipango. Nyie ndio huwa mnapigia bajeti hela za kubeti hata kabla hamjashinda" alisema Dayana.

"Kwa hiyo umeona hapa tunabeti au sio?" Aliuliza Zungu kisha wote wakacheka kwa furaha. Licha ya kwamba walikuwa kwenye eneo la kutisha lakini hawakuacha kuleta utani wa hapa na pale na hii iliwasaidia sana kuwaondolea hofu.

Waliendelea kusonga mbele wakifuata uelekeo wa lile pango. Safari ilikuwa ni ndefu na ngumu mno huku ile miale ya moto waliyobeba ikiwasaidia kuwaangazia. Kwa bahati nzuri katika pango hilo hakukuwa na vitu vyovyote vyenye kutishia usalama wao kama Zungu alivyosema. Hali ilikuwa ni shwari kabisa. Sasa walianza kupanda juu kufuata uelekeo wa pango hilo.

"Tumeshavuka kule kwa Magnus hapa tunapanda ule mlima wenye walinzi kibao" Zungu alitoa maelezo.

"Dah! Hii ni hatari kweli kweli, imenikumbusha filamu ya kirikuu. Alipita kama hivi chini ya nyumba ya mchawi karaba" Alisema Dayana.

"Hahaha! Kwa hiyo Magnus ndio mchawi karaba mwenyewe tumepita chini ya nyumba yake au sio" Zungu akaongezea.

"Alafu kitu kingine hata kirikou alikuwa uchi kama sisi hivi" David naye akaongezea, wote wakacheka kwa sauti.

"Kaka kumbe na huwa unaangalia katuni?"

"Aah! Zungu kuna katuni nyingine nzuri hata mtu mzima unaweza kuangalia. Zipo nzuri kuliko hata muvi zenu za kibongo"

"Hahaha zile muvi ni hatari lakini salama"

Baada ya kupandisha kwa zaidi ya dakika tatu hatimae pango hilo likawa tambalale tena. Zungu, David na Dayana wakazidi kusonga mbele.

"haya tumefika ndugu zangu" Hatimae Zungu aliongea na kusimama, wote wakasimama.

"Mnaona lile jiwe pale mbele, sasa chini ya lile jiwe ndio kuna ile barabara niliyowambia. Ni barabara inayotoka ufukweni mwa bahari hadi kule kwenye majengo ya Magnus lakini imepita chini ya mlima huu" Alieleza Zungu

Baada ya hapo wote walisogea hadi kwenye lile jiwe analolisema Zungu. Kwa pamoja walisaidiana kuliinua lile jiwe waliweka pembeni.

Amini usiamini chini ya lile jiwe kulikuwa na uwazi mkubwa uwazi ambao chini yake ilionekana barabara inayokatiza chini ya mlima huo. Ilikuwa ni ile ile barabara ambayo hutumika kuwaleta mateka wanaoshushwa na meli kuwaingiza ndani ya himaya ya Magnus.

David, Dayana na Zungu waliinama kuchungulia chini wakishuhudia mafanikio makubwa waliyoyapa hadi kufika eneo hilo. Katika kuta za barabara hiyo kulikuwa na miale ya moto pembeni hivyo ilikuwa inaoneka vizuri.

"Inatakiwa tushuke hapo chini tutafuata hiyo barabara mpaka tutakapofika ufukweni" Alieleza Zungu.

"Sasa tunashukaje hapa?" Aliuliza Dayana

"Tutatumia kamba ipo niliiandaa" Alijibu Zungu huku akianza kutafuta sehemu aliyoihifadhi kamba hiyo. Dayana naye akasimama kumsaidia.

"Uliitoa wapi hiyo kamba?" Dayana aliuliza swali lingine lakini kabla Zungu hajajibu mara ghafula wote wawili walishangaa kumuona David anasimama taratibu huku macho yake yakionekana kuwa na wasiwasi mwingi. Ni hali ileile kama iliyomkuta wakati ule wanaruka juu ya shimo muda mfupi uliopita. Sasa kwa mara nyingine tena baada ya David kutazama chini ilipo ile barabara anapatwa na kizunguzungu cha ajabu akaanza kurudi nyuma taratibu huku akiyumbayumba.

Ilikuwa ni hatari kubwa kwani alikokuwa anaelekea kudondokea ndipo kuna ule uwazi(shimo).

Zungu hakutaka kujiuliza mara mbili mbili alikimbia haraka na kwenda kumsukuma David pembeni. Huu ulikuwa ni msaada tosha kwa David kwani alimbadilishia uelekeo David akaanguka pembeni badala ya kudondokea ulipo ule uwazi. Lakini wakati Zungu akifanya hivyo kwa bahati mbaya na yeye akateleza na kuangukia moja kwa moja kwenye ule uwazi huku miguu ndiyo ikitangulia kwenda chini. Licha ya kujitahidi kujizuia lakini ilikuwa ni ngumu kwani tayari alishakosa balance.

Sasa Zungu akawa ameshikilia pembeni kwenye kingo za ule uwazi lakini tayari mwili wake wote ulikuwa umetoka, akawa anabembea kutumia mikono yake. Laiti kama kungekuwa na mtu kule chini barabarani angeweza kumuona.

Hadi dakika hii Dayana alikuwa katika hali ya mshtuko mkubwa mara baada ya kushuhudia tukio hilo la David kutaka kuanguka lakini Zungu anamsaidia mwisho na yeye anateleza na kuangukia shimoni kwenye ule uwazi.
Dayana aliiona mikono ya Zungu akining'inia huku akipambana kupanda juu, kwa bahati mbaya mikono yake ilikuwa ikiteleza kutokana na hali ya unyevu mahali pale.
Zungu alihitaji msaada, tena msaada wa haraka sana la sivyo angeangukia kule chini barabarani jambo ambalo lilikuwa ni hatari kwa usalama wake.
Wakati Dayana anakimbia haraka ili awahi kuishika mikono ya Zungu tayari alikuwa amechelewa kwani ndio kwanza mikono ya Zungu ilikuwa ikiteleza na kuishia.

"Zuuuuunguuu" Dayana aliita kwa sauti huku akiweka mikono yake kichwani, aliogopa mno.
Kufumba na kufumbua mara alimuona David akiruka kwa kasi kama mshale. Wakati Zungu akiwa anakwenda chini mara David alimuwahi na kumshika mkono wake mmoja. Lakini jambo baya na la kutisha ni kwamba hata David naye hakuwa amejishikilia kikamilifu kwani nusu ya mwili wake ilikuwa tayari imetoka nje kwenye ule uwazi kilichobaki huku juu pangoni ni miguu pekee ambayo ndiyo iliyokuwa ikimpa nguvu kidogo sana ya kuweza kumzuia Zungu asiende chini.

Dayana alikimbia na kwenda kushika miguu ya David kumzuia asianguke. Sasa ikawa kama mchezo wa kuokoana.

Zungu ambaye mwili wake wote ulikuwa ukielea alikuwa ameshikwa mkono wake wa kulia na David. Lakini hata David naye karibu nusu ya mwili wake ulikuwa nje na isingekuwa Dayana kumshika miguu yake kule juu basi David na Zungu wote wangeangukia kule chini barabara. Hali ilitisha mno wakati huo.

Sasa mtihani ukawa ni namna gani Zungu ataweza kupanda na kurudi juu. Si kweli kwamba Dayana angeweza kuwavuta wote wawili kuwarudisha juu, hakuwa na nguvu hizo.

"David jitahidi usiniachie jamaa yangu" Zungu aliongea huku akianza kutafuta namna yakupanda juu, lakini ilikuwa ni ngumu tena ngumu mno.

"Nimekushika Zungu..." Alisema David huku kijasho chembamba kikimtoka. David alionekana kuweweseka sana licha ya kujikaza na kumshika Zungu lakini bado hakuwa sawa hata kidogo.
Tukio kama hili liliwahi kumtokea miaka kadhaa iliyopita wakati akiwa bado ni mdogo, tukio lililopelekea David kumpoteza kaka yake ambaye alitumbukia na kupotelea majini.

Leo tena inajirudia kwa mara nyingine huku safari hii akiwa si kaka yake bali ni Zungu mtu muhimu sana kwake.

Tukio hilo lilikuwa likijirudia kwenye akili ya David na kumuumiza kichwa. Hii ndiyo sababu akawa katika hali ya kuweweseka. Ni tukio ambalo lilipelekea David akapatwa na ugonjwa wa kisaikolojia ambao kitaalam unaitwa 'Acrophobia' yaani hofu ya Urefu au hofu ya kilele.
Watu wenye tatizo hili hawawezi kupanda juu ya kitu chochote kilicho mbali kutoka ardhini. Hata kupanda juu ya meza huwa ni tatizo, wanakuwa wanaogopa sana.
Hii ndiyo sababu David alipata shida sana wakati ule wanaruka lile shimo. Hakuliweka wazi tatizo lake isipokuwa aliishia kumwambia Dayana kuwa ni historia ndefu.
Hata wakati huu alipopata kile kizunguzungu cha ghafula ni baada ya kuchungulia chini barabarani kupitia ule uwazi kwa muda mrefu. Tatizo la hili la Acrophobia lilimpata na kupelekea janga zito walilonalo wakati huu.


Dayana alikuwa akijitahidi kuivuta juu miguu ya David lakini bado kazi hiyo ilionekana kumzidi uwezo. Wakati huo Zungu naye akawa anajitahidi kuushika mkono wa David kwa nguvu ili apande juu lakini bado hali ilikuwa ni tete, na tayari alishaanza kuchoka.

Mara ghafula katika hali wasiyoitegemea Zungu, David na Dayana walisikia muungurumo wa gari linakuja. Ni gari ambalo lilikuwa nilakwenda kuwachukua mateka wapya ufukweni mwa bahari walioletwa na meli usiku huo.

Wote watatu walitoa macho kwa mshangao ulioambatana na hofu, walijua kwa vyovyote vile lazima Zungu na David wataonekana wakielea pale juu.

"Mungu wangu tumekosa nini" Alisema Dayana akionekana kukata tamaa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Wakati hayo yakiendelea katika kisiwa cha Magnus, upande wa pili usiku huo huo Mama yake David alionekana amekaa nje ya nyumba yake akilia kwa uchungu mkubwa mno. Kama utakumbuka jioni ya siku hiyo Mama David alipata ugeni wa ghafula nyumbani kwake. Alitembelewa na Mwanamke Hustana kutoka kundi la kigaidi MG Family.
Haikujulikana ni nini hasa kilitokea nyumbani kwa mama David lakini kwa namna ambavyo mama huyu alionekana akilia kwa uchungu usiku wa giza nene ni wazi hali si shwari hata kidogo.
Lakini hali si shwari pia hata kwa mwanae anayemtegea David akiwa kule kisiwani kwa Magnus.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Wakati huo Ndege aliyopanda Felix iliendelea kupasua mawingu angani. Yalikuwa yamesalia masaa machache sana pale ndege hiyo itakapotua na kugusa ardhi ya Tanzania.

ITAENDELEA...
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
We jamaa bwana, yan ukimya wote uo,alaf unakj na vpande viwili,!! ata ka atulipii, ila kurud kwak kunapaswa kuwa na kixhndo
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............33
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Wote watatu walitoa macho kwa mshangao ulioambatana na hofu, kwa vyovyote vile ni wazi Zungu na David wataonekana wakielea pale juu.
"Mungu wangu tumekosa nini" Alisema Dayana akionekana kukata tamaa.

SASA ENDELEA...
Walibaki katika hali ya kuduwaa wasijue la kufanya. Zungu alikuwa akielea huku mkono wake wa kulia ukiwa umeshikwa na David, lakini David naye miguu yake ilikuwa imeshikwa na Dayana. Walidumu katika hali hiyo kwa zaidi ya sekunde kumi, kila mtu akawa anasikiliza ule muungurumo wa gari, mwisho Zungu akaongea.

"David niache mkono wangu, niachie sasa hivi nyie jificheni huko juu wasije wakawaona"

"Unasema nini Zungu... Hapana siwezi kukuacha, siwezi..."

"David fanya hivyo! Unataka tukamatwe wote? hatuna muda David achia mkono wanguuu..." Zungu alisisitiza.

"Hapana Zungu...siwezi kukuacha uanguke chini"

"Nisikilize mimi David... Mimi ndio nmeamua, niachee..."

"Zungu usifanye hivyo tafadhali, David usiuachie mkono wake nakuomba" Sauti ya Dayana iliyoambatana na kilio cha kwikwi ilisikika kutoka kule juu pangoni. Bado alikuwa ameishikilia na kuing'ang'ania miguu ya David kwa nguvu, jasho likawa linamtiririka kwa wingi kama maji.

Wakati wakiendelea kubishana muungurumo wa gari nao ulizidi kusikika jirani kabisa na eneo walilopo, ni kona moja tu ilisalia gari hilo kuweza kujitokeza, kwani tayari kwa mbali mwanga wa taa za gari hilo ulianza kuonekana.

"David... Dayana, hebu nisikilizeni kwa makini..." Zungu aliongea kwa hisia kali huku chozi la kiume likimtoka, akaendelea na kusema...

"....Kuliko tupoteze na kukamatwa wote ni heri mimi peke yangu nijitoe sadaka kwa ajili ya watu wengine. David wewe niache, lakini hakikisha unapambana na kuwatoa mateka wote kule bondeni sawa..." Alisema Zungu huku akiangaliana na David kwa macho ya kwa heri. Baada ya hapo Zungu aliuachia mkono wa David. Lakini bado David hakutaka kuuachia mkono wa Zungu.
Ilikuwa ngumu kuendelea kumshikilia zaidi kwa sababu Zungu alikuwa akiunyonga nyonga mkono wake kwa makusudi ili David asiweze kumshika kikamilifu. Na ndivyo ilivyokuwa taratibu mkono wa Zungu ulianza kuteleza, sasa David akabaki ameshika ncha ya vidole vya Zungu.

"Zungu acha, nasema usifanye hivyo zungu...zungu..." David alipaza sauti na kujitahidi kwa uwezo wake wote kumshika Zungu bila mafanikio.

"David usimuache Zungu nakuomba, please David..." Dayana naye aliendelea kusisitiza, moyoni akiwa na hofu kubwa ya kumpoteza Zungu.

Lakini mwisho mkono wa Zungu uliteleza na kumtoka David, Zungu akaanza kwenda chini.

"Zunguuuuuuuuu......"

"Zunguuuuuuuuuu...."

David na Dayana waliita kwa pamoja.

Kishindo kikubwa kilisikika mara baada ya Zungu kufika chini. Haraka Dayana alimvuta David na kumpandisha hadi kule juu pangoni kisha akachukungulia kule chini. Hakuamini alichokiona, hali ilitisha mno. Wakati huo David alikuwa ni kama amepatwa na wazimu, bado alikuwa haamini kama ni kweli ameshindwa kumzuia Zungu asianguke.

"Zungu..zungu...zungu..." David aliita kwa sauti ya chini huku akiangaza macho yake kila upande ndani ya lile pango, akawa anatambaa na kurudi nyuma. Hakuwa sawa kabisa kiakili. Hizi zilikuwa ni miongoni mwa dalili za ugonjwa wa kisaikolojia aliokuwa nao 'Acrophobia'.
Wakati David akizidi kuweweseka hakuchukua muda akaanguka chini na kuzimia.
Hali ilikuwa ni tete pia kwa Dayana, naye alikuwa akilia sana ingawa hakutoa sauti lakini bado uso wake ulionekana kubeba uchungu mkubwa usio na mfano.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Mara baada ya Zungu kuanguka kule chini barabarani aliumia vibaya sana. Miguu yake yote miwili, kiuno na mkono wake wa kulia vyote vilivunjika papo hapo. Alikuwa hoi taabani, damu ikawa inamtoka mdomoni na puani.
Lakini pamoja na kuwa katika hali mbaya Zungu alianza kujivuta kusogea mbele, akawa anatambaa chini akijivuta kwa mkono wake mmoja, hakuwa na uwezo wa kusimama kabisa.

Alichowaza ni kutoka usawa ule ambao kulikuwa na shimo juu yake ili hata atakapokamatwa na watu wa Magnus basi iwe ni ngumu kung'amua ule uwazi pale juu.

Wakati Zungu akizidi kuhangaika kujivuta kusogea mbele lile gari likawa tayari limekwisha fika.
Dereva alifunga breki ghafula mara baada ya kuona kuna mtu amelala mbele yake katikati ya barabara.

"Oya nini kile?" Dereva alimuuliza mtu aliyekaa pembeni yake. Yule mtu alivua helmet yake yenye kioo chekundu ili aweze kutazama vizuri.

"Ni mtu yule" Alijibu

"Ni nani katoka wapi?" Aliuliza dereva lakini kabla hajajibiwa tayari wenzake waliokuwa wamepanda nyuma ya gari hilo walishuka, wakawa wanasogea taratibu kumfuata Zungu huku silaha zao zikiwa mbele. Kila mmoja alitembea kwa tahadhali kubwa, wote walikuwa wamevaa zile helmet zenye vioo vyekundu.

"Ni mateka wetu.." alisema mmoja wao ambaye yeye alifika karibu kabisa na Zungu. Alimgundua kwa urahisi kutokana na namna alivyo. Ile nguo ya ndani pekee aliyovaa Zungu ilitosha kuwathibitishia kuwa ni kweli mtu huyo ni mateka kutoka kwenye lile bonde. Swali ambalo kila mtu alibaki akijiuliza ni vipi mateka huyo kaweza kutoka bondeni.

"Wewe ni nani?" Aliuliza mmoja wa wale watu huku akichuchumaa mbele ya Zungu.

"Nakuliza wewe ni nani, umetoka wapi?" Yule mtu aliuliza mara ya pili kwa msisitizo huku akimshika Zungu na kumuinua kichwa chake juu.

Badala ya kujibu Zungu akawa anacheka, meno yake yakionekana kutapakaa damu.

"Oya huu ni msara tumuue kabla mambo hayajawa mengi" Alisema mmoja wa wale watu waliosimama.

"Kwa nini tumuue?"

"Sasa unafikiri tutafanyaje? Bosi akijua kama kuna mtu ametoroka kule bondeni si itakuwa tatizo?"

"Mmh! Ni sawa lakini vipi kama hajatoroka peke yake wako wengi, inatakiwa tumbane atueleze katokaje mle bondeni na ninani anashirikiana naye?"

Baada ya wale watu kujadili kwa muda wazo la kumshikilia Zungu mpaka atakapotaja wenzake lilipita.

Kwa bahati nzuri hakuna aliyepata wazo la kutazama juu pengine wangeweza kuuona ule uwazi ingawa tayari Zungu alikuwa amesogea mbele lakini si mbali sana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Dakika kumi baadae fahamu za David akiwa bado ndani ya pango zilianza kumrudia taratibu. David akawa anaweweseka huku lile tukio la miaka mingi iliyopita siku aliyompoteza kaka yake likijirudia kichwani kwake.

Ilikuwa ni siku moja majira ya jioni David(miaka 11) na kaka yake Feisal (miaka 16) walikuwa wakicheza na kufukuzana huku wakinyang'anyana mpira. David akiwa ndio mwenye mpira alikimbia lakini hakufika mbali kaka yake Feisal alimkamata. Wakati huo walikuwa katikati ya daraja moja dogo ambalo chini yake kulikuwa na mto wa maji. Wakati wakizidi kunyang'anyana mpira kwa bahati mbaya uliwaponyoka ukawa unaelekea kwenye kingo za daraja hilo.
Feisal alikimbia kuufuata huku mdogo wake akimfuatilia nyuma. Wakati amekaribia kuufikia mpira ule mara David alifika na kumsukuma kaka yake akitaka yeye ndio awe wa kwanza kuuwahi mpira ule bila kujua tayari kaka yake alikuwa pembezoni mwa daraja. Feisal alikosa balance akashindwa kujizuia akajikuta anaenda kuangukia darajani lakini kwa bahati nzuri akawahi kushikilia ubao mmoja uliokuwa pembeni ya daraja hilo ingawa tayari mwili wake wote ulikuwa ukielea.

Ule ubao ulikuwa hauko imara sana hivyo kutokana na uzito wa Feisal ubao ule ukaanza kukatika taratibu.

"David njoo unishike, nisaidie David...." Feisal aliita kwa hofu huku akijitahidi kupanda juu lakini ikawa ngumu. Badala ya David kwenda kumsaidia kaka yake yeye akawa analia kwa hofu, bado alikuwa na akili za kitoto.

Muda ulizidi kwenda huku Feisal akipambana bila mafanikio. Kwa bahati nzuri baba yao mzazi aliyekuwa akiwatafuta alifika karibu na daraja hilo, ndipo hapo alipomuona mwanae mkubwa Feisal akiwa kwenye hatari kubwa.
Haraka alikimbia kumuwahi lakini tayari alishachelewa Feisal akadumbukia darajani ndani ya maji. Mzee huyo hakutaka kujiuliza mara mbili mbili naye akajitosa darajani kwa haraka kumfuata mwanae. Kwa bahati mbaya mzee huyo hakuwa mtaalamu wa kuogelea.

Siku mbili baadae mwili wa baba yake David ulionekana akiwa amepoteza maisha lakini mwili wa Feisal kaka yake David haukuwahi kuonekana, wote wakaamini kuwa hata Feisal naye alifia majini kama baba yake ingawa mwili wake haukuonekana.
[emoji294][emoji294][emoji294]

"Zunguuuuuu....." David alizinduka ghafula na kuliita jina la Zungu. Aliangaza macho yake huku na kule akaona bado yuko pangoni. Pembeni yake alimuona Dayana akiwa amekaa kinyonge mno. Usoni alikuwa na alama za machozi yaliyokauka.

"Inuka tuondoke..." Alisema Dayana.

"Zungu..! vipi kuhusu Zungu?" Aliuliza David.

"Wamembeba" Dayana alijibu kifupi, David akageuka kutazama ile sehemu kuliyokuwa na uwazi, haikuwepo tena. Tayari Dayana alishalisukuma lile jiwe akalirudisha mahala pake.

David alilia kwa uchungu mno, alijua wazi kwa vyovyote vile Zungu watamuua tena kifo kibaya mno. Alilia na kuilaumu nafsi yake, yeye ndiye alikuwa sababu ya yote hayo. Sababu ya kifo cha Zungu lakini pia aliwahi kuwa sababu ya kifo cha Baba na kaka yake Feisal. David alilia mno, wakati huo Dayana hakusema neno, alitulia kimya kichwani kwake akiwa na mawazo rukuki. Mwisho David na Dayana walikokotana kurudi walikotoka
[emoji294][emoji294][emoji294]

Nusu saa iliwatosha David na Dayana kufika bondeni. Wakiwa wamebakiza hatua kadhaa kufika kule ambako huwa wanakaa pamoja mateka wengine mara wote walipigwa na butwaa baada ya kuona tukio ambalo hawakulitegemea.

Walinzi zaidi ya 50 walikuwa wameshuka kule chini bondeni wakiwa na silaha za moto mikononi mwao, wakawakusanya mateka wote na kuwaweka sehemu moja.

"Ooh! Mungu wangu balaa jingine hili David, tunakamatwa. Wameshajua kuna watu zaidi wametoroka..." Alisema Dayana akionekana mwenye hofu kubwa.

ITAENDELEA...
Simulizi ni shillingi 1,000/= lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina saul au Airtel money namba 0788967317 jina saul kisha njoo WhatsApp inbox namba hizo hizo
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............34
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Ooh! Mungu wangu balaa jingine hili David, tunakamatwa. Wameshajua kuna watu zaidi wametoroka..." Alisema Dayana akionekana mwenye hofu kubwa.

SASA ENDELEA...
Mateka wote walikusanywa sehemu moja huku walinzi zaidi ya 50 wakiwa wanamiminika kwa wingi kuingia ndani ya lile bonde. Tayari mambo yalikuwa yameharibika mara baada ya Zungu kukamatwa kule barabarani.

"Panga mstari mmojaaa ..." Mmoja kati ya wale walinzi alitoa amri.
Mateka wote wakatii amri hiyo huku bado wakiwa katika hali ya mshangao. Lilikuwa ni tukio geni kwao, hata siku moja hawakuwahi kushuhudia kitu kama hicho kikitokea mle bondeni.

Punde walinzi wengine wanne walionekana wakiteremka kupitia ngazi iliyowekwa kwa dharula, wakashuka chini bondeni wakiwa wamemshikilia mtu mmoja ambaye hali yake haikuwa nzuri hata kidogo, si mwingine bali ni mateka Zungu aliyeonekana kuwa hoi taabani, hata kutembea kwake ilikuwa ni ngumu, miguu yake yote ilikuwa imevunjika. Walinzi walimshika mkono wake wa kulia na kushoto kisha wakawa wanamburuza chini, hali ilitisha mno. Kila mateka aliyemuona aliogopa sana.

"Huyu mwenzenu alikuwa anajaribu kutoroka. Hakujua kama anajipeleka mwenyewe kwenye mdomo wa mamba. Sasa kama unajijua umeshirikiana naye kwa namna yoyote ile jitokeze haraka, au kama unawajua watu alioshirikiana nao wataje haraka kabla oparesheni kali haijaanza..." Yule mlinzi ambaye alionekana kuwa kiongozi wa wengine alipaza sauti na kuwachimba mkwara mzito wale mateka. Walichotaka walinzi hao ni kujua namna gani Zungu ameweza kutoka bondeni hadi kufika kule barabarani. Ni wazi haikuwa rahisi hata kidogo, hivyo kabla taarifa haijamfikia Mkuu wao Magnus waliamua kufanya oparesheni hiyo kimya kimya. Pamoja na kumtesa sana Zungu lakini bado hakuwa amezungumza chochote hadi dakika hiyo.

Mateka wote walitulia kimya kwa hofu. Haikuwa rahisi kwao kuamini kwa mtu mwenye akili timamu anaweza kujaribu kutoroka eneo lenye ulinzi mkali kama lile.

"Ni zungu..."

"Zungu...?"

"Ndio mtazame vizuri ni yeye...maskini kaumia vibaya, watamuua"

"Vipi yule mwenzake Dayana yupo wapi?"

"Hata hatujui..."

Baadhi ya mateka walisikika wakinong'ona kwa sauti ya chini sana. Walimuonea huruma mwenzao kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo wakati huo.

"David tunafanyaje..?" Aliuliza Dayana, hofu ikizidi kumtawala.

"Hatuwezi kusogea pale watatugundua...." Alijibu David

"Kwa hiyo tunafanyaje sasa David jamani" Dayana aliuliza akilalamika.

"Subiri kwanza..."

"Turudi basi kule pangoni tukajifiche..."

"Hapana lile pango libaki kuwa siri kubwa litatusaidia baadae"

"Kwa hiyo tunafanyaje David, tutaendelea kusimama hapa mpaka saa ngapi?"

"Hapana lazima tutafute namna ya kujichanga na wenzetu Dayana"

"Kivipi Sasa?"

"Subiri" Alisema David akiendelea kuumiza akili yake kufikiri namna watakavyoweza kujitoa kwenye janga hilo kubwa.

Wakiwa hawajajua nini wafanye mara ghafula walisikia sauti ya king'ora kikilia kwa nguvu. Sauti hiyo ilitokea juu ya bonde kule yalipo majengo ya Magnus. Haraka wale walinzi wakaanza kukimbizana wakipanda ngazi kutoka mle bondeni. Mmoja kati yao alimfuata kiongozi wao akamnong'oneza.

"Tayari Mkuu amepata taarifa kuwa kuna mateka alijaribu kutoroka"

"Nini? Hizi taarifa zimemfikiaje Magnus mbona tulikubalina tufanye siri?" Aliuliza yule kiongozi wa walinzi akionekana kukasirika.

"Sielewi amejuaje, hivi anatuita wote tukusanyike kule kwake"

Zilikuwa ni taarifa za kushtua mno, walinzi wote waliogopa. Walimjua vizuri Magnus hakuwa mtu wa masihara hata kidogo. Kuua kwake lilikuwa ni jambo la kawaida mno.

Dakika tano baadae tayari walinzi wote walitoka mle bondeni, wakamchukua Zungu na kuondoka naye. Walimfungia ndani ya chumba kimoja kidogo(sero). Baada ya hapo wakakimbia haraka na kukusanyika mahala pamoja, nje ya jengo kubwa la Magnus.

Baada ya walinzi kuondoka hali hii ikawa ni ahueni kwa David na Dayana ambao walikimbia haraka wakaenda kijichanganya na wenzao kwa urahisi sana.

Kwa bahati mbaya na nzuri kwa mateka, walinzi hao waliisahau ile ngazi waliyotumia kushuka bondeni kutokana na haraka waliyokuwa nayo.

Kwa mara nyingine tena minong'ono ya hapa na pale ilianza kusikika miongoni mwa mateka ambao sasa walijikusanya kimakundi makundi wakijadili nini wafanye. Ni kweli ngazi ilikuwa mbele yao na sasa walinzi wote walikuwa wamekusanyika kule kwa Magnus. Lakini bado mateka walikuwa na hofu kubwa, tayari walishamuona mwenzao Zungu akiwa hoi taabani mara baada ya kujaribu kutoroka, waliogopa.

Mara kuna mateka mmoja mwanaume mrefu na mnene akasimama mbele ya wenzake na kupaza sauti.

"Mnasubiri nini? Hii ni nafasi tumepata, tutaendelea kuteseka humu hadi lini. Wote inatakiwa tuwe kitu kimoja. Kama tunaamua kuondoka tuondoke kwa pamoja. Tusipo jaribu kujiokoa wenyewe kwa kuzitumia nafasi kama hizi basi nawaapia kwa jina la Mwenyezi Mungu hakuna siku tutatoka kwenye haya mateso. Angalia leo bahati imekuja yenyewe bado tunajiuliza maswali badala ya kuondoka . Mimi nina miaka minne humu sikuwahi kupata nafasi kama hii leo imejitokeza siwezi kuipoteza nawambia"

Minong'ono iliendelea huku wengi wakianza kukubaliana na maelezo ya mateka huyo. Waliona kuna haja ya kuyaamini maneno yake yenye tija.

"David, what do you think?" Dayana alimuuliza David kwa sauti ya chini.

"Ni kweli walinzi hawapo lakini kutoka hapa hadi kufika kule ufukweni sio rahisi ni lazima watakamatwa"

"Nimewaza hivyo pia, tufanyaje sasa?"

"Acha nijaribu kuwashauri" Alisema David kisha akapiga hatua akasogea na kusimama pembeni ya yule mateka ambaye ndiye alikuwa akiwahimiza wenzake watoroke.

"Jamani nisikilizeni, hiki mnachokiwaza ni hatari sana, sio rahisi kama mnavyodhani. Kuna umbali mkubwa sana kutoka hapa hadi kufika ufukweni. Na hata mkibahatika mkafika kule ufukweni bado hamna uhakika wa kupata usafiri wa majini. Nakubali sawa inatakiwa tuwe kitu kimoja lakini basi tutafute namna nzuri ya kutoroka lakini sio hii..."

"Kaa kimya wewe hujui lolote. Ndiyo kwanza unasiku mbili humu bondeni utatuambia nini. Sisi tuliokaa kwa zaidi ya miaka ndio tunajua shida na karaha za hili bonde, huna unachokijua, huna haki ya kuongea. Tunatamani kila siku kutoroka lakini hatujawahi pata nafasi kama hii. Oya sasa nasemaje hapa tunazidi kupoteza muda wa kutoka atoke wa kubaki abaki" Alisema yule mateka wa kiume kisha bila kusita akatimua mbio na kwenda kuzipanda zile ngazi. Alipanda hadi juu kabisa, akaendelea kukimbia na kutokomea. Sekunde chache baadae akaongezeka wa pili, wa tatu, wanne......sasa wakawa wengi wanang'ang'aniana kupanda ile ngazi.

"Mungu wangu ni hatari kubwa David" Alisema Dayana

"Acha tuone pengine watafanikiwa" Alijibu David.

Dakika tano baadae karibu robo ya idadi ya mateka katika lile bonde walikuwa wamepanda ngazi na kukimbia huku wengine wakiendelea kuongezeka. Lakini mara ghafula pasipo kutegemea milio ya risasi zikifyatuliwa mfululizo ilianza kusikika juu ya bonde hilo kule walikokimbilia mateka.

Wale ambao walikuwa hawajafika mbali walianza kurudi kwa kasi kusalimisha maisha yao. Lakini wale waliofika mbali hawakurudi tena walipigwa risasi na kuuawa.

Hili lilikuwa ni tukio lingine la kutisha lililozidi kuutesa moyo wa David usiku huo. Ulikuwa ni usiku ambao ama kwa hakika hawezi kuusahau katika kipindi chote cha maisha yake. David aliumia mno huku akitambua fika yeye ndiyo sababu ya kila kitu, yeye ndio chacho cha Zungu kuwa katika hali ili mbaya, yeye ndio chanzo hata cha mateka wengine kufa kwani kama sio kukamatwa kwa Zungu basi haya yote yasinge tokea. Hadi kunapambazuka asubuhi ya siku inayofuata David bado hakuwa amepata hata repe la usingizi, usiku mzima alikuwa akitafakari na kujiuliza hatima ya hayo yote itakuwaje.

"David.." Dayana aliita mara baada ya kuamka. Alikuwa amelala kwenye miguu ya David usiku wote

"Nitamuua..." Badala ya kuitika David aliongea huku akiwa amevaa sura ya kazi, hakuwa na hata chembe ya masihara usoni kwake.

"Nini tena utamuua nani?" Dayana aliuliza huku akiinuka taratibu akawa anamtazama David kwa macho ya kuuliza.

"Nitamuua.."

"Nani huyo?"

"Magnus nitamuua... Nitakisambaratisha hiki kisiwa" Alijibu David akionekana kumaanisha anachokisema.
Tayari moyoni aliweka kisasi kizito dhidi ya mtu aitwae Magnus. Bila kujali nguvu kubwa na uwezo aliokuwa nao mtu huyo. Taratibu maneno ya marehemu Bi Noha kule ISRA yalianza kuonyesha dalili za kutimia.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Ni asubuhi katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere, mambo yalikuwa yamepamba moto.
Oparesheni nzito inayoongozwa na afisa mpelelezi kutoka jeshi la polisi mwanadada Brandina pamoja na Jacob kutoka idara ya usalama wa Taifa ilikuwa ikiendelea kuhakikisha wanamkamata kijana Felix anayetarajiwa kutua asubuhi hiyo na Ndege akitokea nchini Marekani.

Kama Brandina alivyoahidi kuongeza nguvu na ndivyo ilivyokuwa, polisi walikuwa wamezagaa karibu kila mahali huku wengine wakiwa wamevalia mavazi ya kiraia wakijifanya kama watu wanaosubiri kuwapokea ndugu na jamaa zao watakaowasili mda mfupi ujao.

Si hivyo tu hata wapambe kutoka mtandao wa kigaidi MG Family walikuwa wamesambazwa eneo hilo wakiwa na oparesheni maalumu kuhakikisha Felix mtoto wa Mkuu wao Magnus anakuwa salama salmini.
Kiongozi wa oparesheni hiyo madhubuti alikuwa si mwingine bali Careem Abdul Razzaq moja kati ya viongozi wakubwa wa mtandao wa kigaidi MG Family. Yeye alikuwa ndani ya chumba kimoja juu ghorofani katika jengo moja kubwa lilokuwa jirani na Uwanja huo wa Ndege. Alikuwa akifuatilia kila kinachoendelea kupitia darubini yake. Sikioni alikuwa amevaa kifaa maalumu cha mawasiliano ambacho alikuwa akiwasiliana moja kwa moja na wapambe wake waliokuwa tayari maeneo ya uwanja wa ndege. Pembeni yake alisimama mwanadada Hustana naye pia alikuwa na darubini mkononi mwake. Wakawa wanafuatilia kwa makini kila kinachoendelea.

Dakika chache baadae katika eneo maalumu la kusimamisha gari. Lilifika gari moja la kifahari aina Cadillac ESC na baada ya kusimama akashuka mwanamke mmoja mrembo sana. Huyu hakuwa mwingine bali ni mwanamitindo maarufu nchini Tesha.
Naye alifika kwa ajili ya kukutana na mpenzi wake Felix ambaye anawasili dakika chache zijazo na ndege ya BOENG 707 AIRWAY kutokea nchini Marekani.

Je, nini kitafuata?

ITAENDELEA...

Simulizi ni shillingi 1,000/= lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina saul au Airtel money namba 0788967317 jina saul kisha njoo WhatsApp inbox namba hizo hizo
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........16
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Mmesababisha majanga makubwa sana ndani ya ISRA, kutoweka kwa msitu wa Bi Noha ni laana kubwa ndani ya ISRA, ni lazima muwajibike kwa hili" Alisema Dumayo.

Je nini kitafuata?

SASA ENDELEA...
ISRA ...
Mkuu wa ISRA Gu Gamilo pamoja na askari na baadhi ya wafanyakazi wengine ndani ya Ikulu ya ISRA walionekana pembeni ya shimo kubwa mahali palipokuwepo msitu mkubwa maarufu kama msitu wa Bi Noha.
Walikuwa wakitazama maafa makubwa yaliyotokea kiasi cha kusababisha msitu huo kutoweka wote kwa namna ya ajabu sana. Ilikuwa ni hali iliyomshangaza kila mmoja. Hakuna aliyekuwa na jibu sahihi ni kipi hasa kimepelekea msitu huo kupatwa na majanga na mwisho kuzama wote ardhini.
Gu Gamilo baba yake Sasha alitazama kwa umakini huku uso wake ukionekana kujawa na wasiwasi mwingi.
Gu Gamilo alikuwa ni mzee kiasi sura yake iliyokunjamana wakati wote, ilikuwa ni adimu kuliona tabasamu la mzee huyo. Nywele zake ndefu na nyeupe alizozifunga kwa juu, huku kidevu chake kikiwa kimefunikwa na ndevu zenye rangi nyeupe vilevile vilimfanya mzee huyo kuwa na muonekano wa pekee katika ISRA.

Mpaka dakika hiyo hakuna aliyejua sekeseke lilotokea upande wa pili wa shimo hilo kule walipo Dumayo Sasha na akina Handan.

Tukio la kutoweka kwa msitu huo lilionekana kumtisha sana Gu Gamilo kiasi cha mkumfanya akumbuke kwa mara ya mwisho alivyoingia ndani ya msitu huo akafanikiwa kuonana na Bi Noha ambaye kwa sasa ni marehemu. Gu Gamilo aliyakumbuka vizuri maneno mazito aliyowahi kuelezwa na bibi kizee huyu, alisema...

...... Umefanya kosa kubwa bila kufikiria kwa makini Gu Gamilo, kumfukuza Kaka yako MAGNUS nje ya ISRA bado hujamaliza tatizo, kwa kosa alilofanya alistahili adhabu kubwa zaidi ya hiyo. Ipo siku utayakumbuka maneno yangu Siku ambayo Magnus atarudi tena ISRA na kuitikisa kwa mara nyingine. Haijarishi itachukua miaka mingapi lakini jua kwamba Magnus ni lazima atarudi tena akiwa amejipanga vilivyo. Atakushambulia kutoka pande zote, mashariki magharibi kaskazini na kusini. Itakuwa ni siku ambayo utakosa kwa kukimbilia hata msitu wangu ambao pengine ungeweza kujificha hautokuwepo tena, litakuwepo shimo kubwa lisilo na mwisho Gu Gamilo..........
Haya yalikuwa ni maelezo ya Bi Noha ambaye ni kama alijua siku moja msitu wake utatoweka na kubaki shimo.

........Bi Noha, nifanyaje sasa kuzuia hili lisitokee tafadhali nisaidie, nawezaje kumzuia kaka Magnus...........

........Hakuna mtu yeyote ISRA atakae weza kumzuia Magnus, isipokuwa yupo Mwanadamu mmoja ambaye ataweza kupambana naye na kumzuia Magnus asirudi tena ISRA, mwanadamu huyo anahitaji ulinzi. Kama atakufa basi ISRA itakuwa kwenye wakati mgumu, kama akiwa hai basi ISRA itaendelea kusimama...........

........Ni mwanadamu gani huyo Bi Noha, unaweza kuniambia tafadhali.........

.........Mtafute, na hakikisha unamlinda kabla Magnus hajamtambua........

Hizi zilikuwa ni kumbukumbu za Mkuu wa ISRA Gu Gamilo. Baada ya hapo aliondoka kinyonge yeye na watu wake huku kila mmoja akisubiri kwa hamu Gu Gamilo atasema nini baada ya tukio hilo ambalo wengi waliliona kama ishara mbaya kwa ISRA.
Hatimae Gu Gamilo alilejea Ikulu ya ISRA yeye na msafara wake, wakati anaingia lango kuu la Ikulu alipokelewa kwa shauku na mkewe kipenzi Malkia Hella(Mama yake Sasha). Alikuwa akimsubiri Mumewe kwa hamu ili amueleze ni nini hasa kimetokea maana kila mtu alionekana kuogopa.
Alipoiona Sura ya huzuni kwa mumewe Gu Gamilo ilikuwa ni tafsiri tosha kuwa mambo hayakuwa mazuri kabisa.

"Ni nini kinaendelea huko nje Gu Gamilo..." Aliuliza Malkia Hella
"Umetoweka.." Gu Gamilo alijibu kinyonge
"Nini? Nini kimetoweka!?"
"Msitu wa Bi Noha" Ilikuwa ni kauli iliyo muacha kinywa wazi Malkia Hella.
Akiwa katika hali hiyo ya mshangao mara wakasikia mlio wa farasi langoni. Gu Gamilo na mkewe wakageuka taratibu kutazama.
Uso kwa uso wakamuona Dumayo anaingia taratibu na msafara wake. Gu Gamilo aliikunja sura yake akionyesha wazi ni jinsi gani alikuwa anamchukia shemeji yake huyo. Lakini tofauti na Malkia Hella yeye alitabasamu mara baada ya kumuona kaka yake Dumayo anaingia.

Katika hali ya kushangaza nyuma ya msafara wa Dumayo walionekana wanawake wanne wakiwa wamefungwa kamba mikokoni huku wakivutwa na watu wa Dumayo waliokuwa juu ya farasi. Wanawake hawa walikuwa ni Sasha, Handan pamoja na wale walinzi wengine wawili.
Gu Gamilo alitoa macho kwa mshangao asiamini anachokiona.
"Sasha" Gu Gamilo aliita kwa sauti ya chini.
Wakati huo Dumayo yeye awaka anatabasamu tu kama kawaida yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili......
David alifumbua macho yake taratibu fahamu zikiwa zimemrejea. Hali akiwa na maumivu makali ya kichwa, alitazama mahali alipo. Alikuwa ndani ya chumba kimoja kipana huku mikono na miguu yake ikiwa imefungwa na vyuma maalumu vilivyokuwa ukutani. Alikuwa ametanuliwa mikono yake na kusimamishwa kama vile yupo msalabani.
Alipotazama mbele akawaona wale jamaa wenye helmet zenye vioo vyekundu wakimalizia kuwafunga watu wengine watatu ukutani kama vile walivyomfunga yeye baada ya hapo wakafungua mlango wa chumba hicho wakatoka na kuondoka. David alitazama kushoto na kulia kwake ndipo akagundua kuwa karibu kuta zote nne za chumba hicho kulikuwa na watu wamefungwa kama yeye na wengi wao walikuwa wamepoteza fahamu hawajitambui. Kwa Haraka haraka aliwahesabu walifika kumi na mbili. David aliogopa sana, hakuelewa ni wapi yupo na amefikaje. Bado kumbukumbu zake zilikuwa hazijakaa sawasawa.

"Oya nyie, nifungueni, njooni mnifungue....mnajua mimi ni nani!??" David alianza kupiga kelele huku akifoka.
"NYIE JAMAAAAAAA..."
David alizidi kupiga kelele.
"Kelele zako hazito saidia kitu, unamaliza nguvu zako bure..."
Mara sauti hii ya kike ilisikika kutoka pembeni yake upande wa kushoto. Haraka David akageuka kutazama ni nani aliyemuongelesha.
Uso kwa uso akagonganisha macho yake na mmoja kati ya wale wanawake waliokuwa wakimfuatilia tangu awali. Alikuwa ni Femi, naye alikuwa amefungwa vilevile kama yeye.

David aliogopa sana alipomuona lakini alipogundua naye amefungwa kama yeye aliduwaa huku kumbukumbu za matukio kadhaa yaliyotokea tangu alipoanza kuwaona wanawake hao wa ajabu zikijirudia kichwani kwake kama filamu.

"We..we. ni nani?"
"Naitwa Femi..." Alijibu Femi huku akitema mate chini, mate yaliyochanganyikana na damu ya kijani.
David alitazama yale mate pale chini kisha akageuka tena na kumtazama yule mwanamke akiwa katika hali ya mshangao mkubwa.

"Fe..femi wa wapi? Kwa nini mlikuwa mnanifuatilia?"
"Kwa sababu tunataka kukuua" Femi alieleza bila kusita
"Bado unaendeleza ukichaa wako Femi si ndiyo?" Mara sauti ya Zucc kutoka upande wa kulia kwa David ilisikika. David alishtuka na kugeuka kumtazama.
"Na wewe pia ulikuwa ukinifuatilia..!" Alisema David lakini bado alionekana kuogopa.
"Achana naye huyo!" Alisema Femi akimtaka David asiendelee kuzungumza na Zucc, David akageuka tena upande wake wa kushoto alipo Femi.

"Mnataka kuniua nimewakosa nini kwani?"
"Tumeagizwa tukuue..." Alijibu Femi lakini kabla hajaendelea zaidi Zucc akamkatisha kwa sauti kali iliyojaa hasira, hakupendezwa kabisa na anachokifanya mwenzake.
"Femi nimesema acha ujingaaaa ..." Alifoka
"Zucc hakuna tulichobakiza kwani hata nikimwambia ukweli kuna ubaya gani? Unafikiri tutapona na tayari tumeshafanya uzembe wenyewe mwisho tumeingia kwenye mikono ya MAGNUS" Alieleza Femi.
"Ma..ma.. Magnus ndio na..nani kwani?" Aliuliza David akiwa ndio kwa mara yake ya kwanza analisikia jina la mtu huyo MAGNUS , mtu ambaye kwa mujibu wa maelezo ya marehemu Bi Noha anatakiwa kupambana naye siku za usoni.
Kabla David hajajibiwa swali lake mara wakasikia mtikisiko mkubwa na baadae wakahisi kama wanasogea mbele.
Kumbe chumba hicho kilikuwa ni moja kati ya vyumba vingi ndani ya Meli moja kubwa ambayo sasa iling'oa nanga na kuanza kukata mawimbi taratibu kuelekea kusiko julikana.

ITAENDELEA...

0756862047

Safi
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............34
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Ooh! Mungu wangu balaa jingine hili David, tunakamatwa. Wameshajua kuna watu zaidi wametoroka..." Alisema Dayana akionekana mwenye hofu kubwa.

SASA ENDELEA...
Mateka wote walikusanywa sehemu moja huku walinzi zaidi ya 50 wakiwa wanamiminika kwa wingi kuingia ndani ya lile bonde. Tayari mambo yalikuwa yameharibika mara baada ya Zungu kukamatwa kule barabarani.

"Panga mstari mmojaaa ..." Mmoja kati ya wale walinzi alitoa amri.
Mateka wote wakatii amri hiyo huku bado wakiwa katika hali ya mshangao. Lilikuwa ni tukio geni kwao, hata siku moja hawakuwahi kushuhudia kitu kama hicho kikitokea mle bondeni.

Punde walinzi wengine wanne walionekana wakiteremka kupitia ngazi iliyowekwa kwa dharula, wakashuka chini bondeni wakiwa wamemshikilia mtu mmoja ambaye hali yake haikuwa nzuri hata kidogo, si mwingine bali ni mateka Zungu aliyeonekana kuwa hoi taabani, hata kutembea kwake ilikuwa ni ngumu, miguu yake yote ilikuwa imevunjika. Walinzi walimshika mkono wake wa kulia na kushoto kisha wakawa wanamburuza chini, hali ilitisha mno. Kila mateka aliyemuona aliogopa sana.

"Huyu mwenzenu alikuwa anajaribu kutoroka. Hakujua kama anajipeleka mwenyewe kwenye mdomo wa mamba. Sasa kama unajijua umeshirikiana naye kwa namna yoyote ile jitokeze haraka, au kama unawajua watu alioshirikiana nao wataje haraka kabla oparesheni kali haijaanza..." Yule mlinzi ambaye alionekana kuwa kiongozi wa wengine alipaza sauti na kuwachimba mkwara mzito wale mateka. Walichotaka walinzi hao ni kujua namna gani Zungu ameweza kutoka bondeni hadi kufika kule barabarani. Ni wazi haikuwa rahisi hata kidogo, hivyo kabla taarifa haijamfikia Mkuu wao Magnus waliamua kufanya oparesheni hiyo kimya kimya. Pamoja na kumtesa sana Zungu lakini bado hakuwa amezungumza chochote hadi dakika hiyo.

Mateka wote walitulia kimya kwa hofu. Haikuwa rahisi kwao kuamini kwa mtu mwenye akili timamu anaweza kujaribu kutoroka eneo lenye ulinzi mkali kama lile.

"Ni zungu..."

"Zungu...?"

"Ndio mtazame vizuri ni yeye...maskini kaumia vibaya, watamuua"

"Vipi yule mwenzake Dayana yupo wapi?"

"Hata hatujui..."

Baadhi ya mateka walisikika wakinong'ona kwa sauti ya chini sana. Walimuonea huruma mwenzao kutokana na hali mbaya aliyokuwa nayo wakati huo.

"David tunafanyaje..?" Aliuliza Dayana, hofu ikizidi kumtawala.

"Hatuwezi kusogea pale watatugundua...." Alijibu David

"Kwa hiyo tunafanyaje sasa David jamani" Dayana aliuliza akilalamika.

"Subiri kwanza..."

"Turudi basi kule pangoni tukajifiche..."

"Hapana lile pango libaki kuwa siri kubwa litatusaidia baadae"

"Kwa hiyo tunafanyaje David, tutaendelea kusimama hapa mpaka saa ngapi?"

"Hapana lazima tutafute namna ya kujichanga na wenzetu Dayana"

"Kivipi Sasa?"

"Subiri" Alisema David akiendelea kuumiza akili yake kufikiri namna watakavyoweza kujitoa kwenye janga hilo kubwa.

Wakiwa hawajajua nini wafanye mara ghafula walisikia sauti ya king'ora kikilia kwa nguvu. Sauti hiyo ilitokea juu ya bonde kule yalipo majengo ya Magnus. Haraka wale walinzi wakaanza kukimbizana wakipanda ngazi kutoka mle bondeni. Mmoja kati yao alimfuata kiongozi wao akamnong'oneza.

"Tayari Mkuu amepata taarifa kuwa kuna mateka alijaribu kutoroka"

"Nini? Hizi taarifa zimemfikiaje Magnus mbona tulikubalina tufanye siri?" Aliuliza yule kiongozi wa walinzi akionekana kukasirika.

"Sielewi amejuaje, hivi anatuita wote tukusanyike kule kwake"

Zilikuwa ni taarifa za kushtua mno, walinzi wote waliogopa. Walimjua vizuri Magnus hakuwa mtu wa masihara hata kidogo. Kuua kwake lilikuwa ni jambo la kawaida mno.

Dakika tano baadae tayari walinzi wote walitoka mle bondeni, wakamchukua Zungu na kuondoka naye. Walimfungia ndani ya chumba kimoja kidogo(sero). Baada ya hapo wakakimbia haraka na kukusanyika mahala pamoja, nje ya jengo kubwa la Magnus.

Baada ya walinzi kuondoka hali hii ikawa ni ahueni kwa David na Dayana ambao walikimbia haraka wakaenda kijichanganya na wenzao kwa urahisi sana.

Kwa bahati mbaya na nzuri kwa mateka, walinzi hao waliisahau ile ngazi waliyotumia kushuka bondeni kutokana na haraka waliyokuwa nayo.

Kwa mara nyingine tena minong'ono ya hapa na pale ilianza kusikika miongoni mwa mateka ambao sasa walijikusanya kimakundi makundi wakijadili nini wafanye. Ni kweli ngazi ilikuwa mbele yao na sasa walinzi wote walikuwa wamekusanyika kule kwa Magnus. Lakini bado mateka walikuwa na hofu kubwa, tayari walishamuona mwenzao Zungu akiwa hoi taabani mara baada ya kujaribu kutoroka, waliogopa.

Mara kuna mateka mmoja mwanaume mrefu na mnene akasimama mbele ya wenzake na kupaza sauti.

"Mnasubiri nini? Hii ni nafasi tumepata, tutaendelea kuteseka humu hadi lini. Wote inatakiwa tuwe kitu kimoja. Kama tunaamua kuondoka tuondoke kwa pamoja. Tusipo jaribu kujiokoa wenyewe kwa kuzitumia nafasi kama hizi basi nawaapia kwa jina la Mwenyezi Mungu hakuna siku tutatoka kwenye haya mateso. Angalia leo bahati imekuja yenyewe bado tunajiuliza maswali badala ya kuondoka . Mimi nina miaka minne humu sikuwahi kupata nafasi kama hii leo imejitokeza siwezi kuipoteza nawambia"

Minong'ono iliendelea huku wengi wakianza kukubaliana na maelezo ya mateka huyo. Waliona kuna haja ya kuyaamini maneno yake yenye tija.

"David, what do you think?" Dayana alimuuliza David kwa sauti ya chini.

"Ni kweli walinzi hawapo lakini kutoka hapa hadi kufika kule ufukweni sio rahisi ni lazima watakamatwa"

"Nimewaza hivyo pia, tufanyaje sasa?"

"Acha nijaribu kuwashauri" Alisema David kisha akapiga hatua akasogea na kusimama pembeni ya yule mateka ambaye ndiye alikuwa akiwahimiza wenzake watoroke.

"Jamani nisikilizeni, hiki mnachokiwaza ni hatari sana, sio rahisi kama mnavyodhani. Kuna umbali mkubwa sana kutoka hapa hadi kufika ufukweni. Na hata mkibahatika mkafika kule ufukweni bado hamna uhakika wa kupata usafiri wa majini. Nakubali sawa inatakiwa tuwe kitu kimoja lakini basi tutafute namna nzuri ya kutoroka lakini sio hii..."

"Kaa kimya wewe hujui lolote. Ndiyo kwanza unasiku mbili humu bondeni utatuambia nini. Sisi tuliokaa kwa zaidi ya miaka ndio tunajua shida na karaha za hili bonde, huna unachokijua, huna haki ya kuongea. Tunatamani kila siku kutoroka lakini hatujawahi pata nafasi kama hii. Oya sasa nasemaje hapa tunazidi kupoteza muda wa kutoka atoke wa kubaki abaki" Alisema yule mateka wa kiume kisha bila kusita akatimua mbio na kwenda kuzipanda zile ngazi. Alipanda hadi juu kabisa, akaendelea kukimbia na kutokomea. Sekunde chache baadae akaongezeka wa pili, wa tatu, wanne......sasa wakawa wengi wanang'ang'aniana kupanda ile ngazi.

"Mungu wangu ni hatari kubwa David" Alisema Dayana

"Acha tuone pengine watafanikiwa" Alijibu David.

Dakika tano baadae karibu robo ya idadi ya mateka katika lile bonde walikuwa wamepanda ngazi na kukimbia huku wengine wakiendelea kuongezeka. Lakini mara ghafula pasipo kutegemea milio ya risasi zikifyatuliwa mfululizo ilianza kusikika juu ya bonde hilo kule walikokimbilia mateka.

Wale ambao walikuwa hawajafika mbali walianza kurudi kwa kasi kusalimisha maisha yao. Lakini wale waliofika mbali hawakurudi tena walipigwa risasi na kuuawa.

Hili lilikuwa ni tukio lingine la kutisha lililozidi kuutesa moyo wa David usiku huo. Ulikuwa ni usiku ambao ama kwa hakika hawezi kuusahau katika kipindi chote cha maisha yake. David aliumia mno huku akitambua fika yeye ndiyo sababu ya kila kitu, yeye ndio chacho cha Zungu kuwa katika hali ili mbaya, yeye ndio chanzo hata cha mateka wengine kufa kwani kama sio kukamatwa kwa Zungu basi haya yote yasinge tokea. Hadi kunapambazuka asubuhi ya siku inayofuata David bado hakuwa amepata hata repe la usingizi, usiku mzima alikuwa akitafakari na kujiuliza hatima ya hayo yote itakuwaje.

"David.." Dayana aliita mara baada ya kuamka. Alikuwa amelala kwenye miguu ya David usiku wote

"Nitamuua..." Badala ya kuitika David aliongea huku akiwa amevaa sura ya kazi, hakuwa na hata chembe ya masihara usoni kwake.

"Nini tena utamuua nani?" Dayana aliuliza huku akiinuka taratibu akawa anamtazama David kwa macho ya kuuliza.

"Nitamuua.."

"Nani huyo?"

"Magnus nitamuua... Nitakisambaratisha hiki kisiwa" Alijibu David akionekana kumaanisha anachokisema.
Tayari moyoni aliweka kisasi kizito dhidi ya mtu aitwae Magnus. Bila kujali nguvu kubwa na uwezo aliokuwa nao mtu huyo. Taratibu maneno ya marehemu Bi Noha kule ISRA yalianza kuonyesha dalili za kutimia.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Ni asubuhi katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere, mambo yalikuwa yamepamba moto.
Oparesheni nzito inayoongozwa na afisa mpelelezi kutoka jeshi la polisi mwanadada Brandina pamoja na Jacob kutoka idara ya usalama wa Taifa ilikuwa ikiendelea kuhakikisha wanamkamata kijana Felix anayetarajiwa kutua asubuhi hiyo na Ndege akitokea nchini Marekani.

Kama Brandina alivyoahidi kuongeza nguvu na ndivyo ilivyokuwa, polisi walikuwa wamezagaa karibu kila mahali huku wengine wakiwa wamevalia mavazi ya kiraia wakijifanya kama watu wanaosubiri kuwapokea ndugu na jamaa zao watakaowasili mda mfupi ujao.

Si hivyo tu hata wapambe kutoka mtandao wa kigaidi MG Family walikuwa wamesambazwa eneo hilo wakiwa na oparesheni maalumu kuhakikisha Felix mtoto wa Mkuu wao Magnus anakuwa salama salmini.
Kiongozi wa oparesheni hiyo madhubuti alikuwa si mwingine bali Careem Abdul Razzaq moja kati ya viongozi wakubwa wa mtandao wa kigaidi MG Family. Yeye alikuwa ndani ya chumba kimoja juu ghorofani katika jengo moja kubwa lilokuwa jirani na Uwanja huo wa Ndege. Alikuwa akifuatilia kila kinachoendelea kupitia darubini yake. Sikioni alikuwa amevaa kifaa maalumu cha mawasiliano ambacho alikuwa akiwasiliana moja kwa moja na wapambe wake waliokuwa tayari maeneo ya uwanja wa ndege. Pembeni yake alisimama mwanadada Hustana naye pia alikuwa na darubini mkononi mwake. Wakawa wanafuatilia kwa makini kila kinachoendelea.

Dakika chache baadae katika eneo maalumu la kusimamisha gari. Lilifika gari moja la kifahari aina Cadillac ESC na baada ya kusimama akashuka mwanamke mmoja mrembo sana. Huyu hakuwa mwingine bali ni mwanamitindo maarufu nchini Tesha.
Naye alifika kwa ajili ya kukutana na mpenzi wake Felix ambaye anawasili dakika chache zijazo na ndege ya BOENG 707 AIRWAY kutokea nchini Marekani.

Je, nini kitafuata?

ITAENDELEA...

Simulizi ni shillingi 1,000/= lipia kwa mpesa namba 0756862047 jina saul au Airtel money namba 0788967317 jina saul kisha njoo WhatsApp inbox namba hizo hizo
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............35
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Huyu hakuwa mwingine bali ni mwanamitindo maarufu nchini Tesha.
Naye alifika kwa ajili ya kukutana na mpenzi wake Felix ambaye anawasili dakika chache zijazo na ndege ya BOENG 707 AIRWAY kutokea nchini Marekani.

Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA...
Tesha alipendeza si kidogo, ingawa uso wake ulikuwa na tabasamu hafifu wakati huo lakini bado uzuri wake ulitawala zaidi. Bado Tesha alikuwa akiwaza ni nini kitakachotokea mara baada ya kukutana na Felix mwanaume ambaye ni kila kitu kwenye maisha yake. Je, atamkataa? Au atamjali? Bado anampenda? Au ni kweli hamtaki?. Haya yalikuwa ni maswali ambayo Tesha alitamani kupata majibu yake hii leo. Alivua miwani yake na kuiweka kwenye mkoba wake baada ya hapo akawa anapiga hatua kuelekea pale walipokuwa wamesimama watu wengine waliofika kuwapokea ndugu na jamaa zao.

Hayawi hawayi sasa yakawa, Ndege iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa BOEING 707 AIRWAY kutokea nchini Marekani sasa ilifika na kuigusa ardhi ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere. Baada ya kufanya mizunguuko kadhaa hatimae ikasimama mahala pake. Mlango ulifunguliwa na taratibu abiria mmoja baada ya mwingine wakaanza kushuka.

Felix akiwa na msaidizi wake wa karibu Haron wao walitulia kwanza kwa muda wakisubiri watu wote washuke ndipo nao washuke. Kila mmoja akawa anahangaika kuwasha simu yake baada ya kuizima kwa masaa 19 mfululizo tangu walipotoka uwanja wa ndege wa JK Kennedy jijini New York huko Marekani.

Simu ya Haron ilikuwa ni ya kwanza kuwaka.
,,,,,,Nipigie haraka mara baada ya kupata ujumbe huu,,,,,,
Huu ulikuwa ni moja kati ya ujumbe wa maandishi aliokutana nao Haron kutoka kwa moja kati ya viongozi wakubwa wa MG Family alikuwa ni Kareem anamfahamu vizuri, haraka akapiga.

"Hallo" Alisema Haron mara baada ya simu yake kupokelewa, wakati huo yeye na Felix walisimama na kuanza kupiga hatua kushuka kwenye ndege.

"Ndio......what?......polisi?......kivipi?.....ndiyo nakupata......sawa.....sawa.......baada ya hapo.....sawa Kareem...."
Haron alimaliza mazungumzo na kukata simu sura yake ikionekana kuwa na wasiwasi mwingi.

"Vipi kwema?" Aliuliza Felix huku akiendelea kuchezea simu yake.

"Sio kwema Felix, kuna polisi hapo nje wanataka kukukamata?"

"Kukukamata umefanyaje.?"

"Sio kunikamata mimi, kukukamata wewe?"

"Mimi?"

"Ndiyo"

"Felix mimi?"

"Ndiyo wewe"

"Sasa mimi nahusiana vipi na Wanadamu, si tulishakubaliana mimi sio binadamu Haron?" Aliuliza Felix huku akitabasamu wala hakuonekana kujali kabisa. Taarifa hizo hazikumshtua hata kidogo, wakati huo tayari walishashuka kwenye ndege wakawa wanapiga hatua kuelekea mlango wa kutokea. Haron akawa anaangalia kushoto na kulia ni kweli aliwaona askari walinzi wa airport ambao mara baada ya wao kushuka walianza kuwafuata nyuma taratibu, mara kuna wengine tena wakaongezeka wakitokea upande wao wa kushoto.

"Nisikilize vizuri Felix...."

"Aah! We..hiyo michezo yenu mimi siitaki kwanza nahitaji kuonana na Tesha kabla ya kingine chochote"

"Unawazimu Felix? Tesha wa nini wakati kama huu? Hivi huoni hapa tayari tumeshazunguukwa na polisi, hebu angalia kushoto na kulia kwako ndio utajua kama sitanii" Alisema Haron.
Badala ya kufanya kama alivyoelezwa Felix alisimama na kumtazama Haron usoni.

"Kwa hiyo kama kuna polisi mimi nafanyaje.." Aliuliza Felix akionekana kutokujali kabisa habari hizo.
Siku zote Felix alikuwa ni aina ya mtu asiyejali, alikuwa ni mtu mwenye kiburi na dharau pia. Jambo kubwa ambalo lilimfanya Felix kuwa hivyo ni kutokana na uwezo na nguvu kubwa aliyonayo baba yake mzazi Magnus. Alijua wazi hakuna jambo linaweza likatokea halafu likamshinda. Ni aina ya mtu ambaye alipata kila anachokitaka na jambo jema zaidi ni kwamba baba yake Magnus alikuwa akimpenda mno.

Haron alitaka kuzungumza jambo lakini akasita mara baada ya kuona kundi la watu zaidi ya sita wakija pale walipo. Wawili kati yao walikuwa wamevalia sare za polisi huku mikononi mwao wakiwa na bunduki.
Felix aligeuka kutazama kule anakotazama msaidizi wake Haron, naye akawaona watu hao ambao walitembea kwa haraka wakafika pale walipo na kusimama mbele yao.

"Sisi ni maasifa kutoka jeshi la polisi, tafadhali tunaomba uongozane nasi kituo cha polisi" Alisema mwanamke mmoja ambaye yeye alivalia mavazi ya kawaida, akamuonyesha Felix kitambulisho chake. Hakuwa mwingine bali Inspekta Brandina.

Felix aliwatazama wale polisi mmoja baada ya mwingi kisha akavua miwani yake akawa anaisafisha.

"Kwa hiyo ninyi ni polisi si ndiyo? Mimi mnanifahamu?" Felix aliuliza huku akiivaa tena miwani yake.

Kwa haraka haraka Brandina aliweza kuisoma akili ya Felix akatambua fika ni mtu mwenye dharua na nilazima kuna kitu kinachompa jeuri hiyo. Bila kusema neno Brandina akatoa ishara furani kwa askari waliokuwa pembeni yake haraka wakasogea mbele wakamkamata Felix wakarudisha mikono yake nyuma na kumfunga pingu.

"Utajua zaidi tukifika kituo cha polisi..." Alisema Brandina. Felix aligeuka na kumtazama Haron. Haron naye akampa ishara kuwa afanye kama wanavyotaka, Tayari alikuwa na maelezo kamili kutoka kwa Kareem namna mpango wa MG Family ulivyokaa.

Askari hao walimzingira Felix pande zote kisha wakaanza kutembea pamoja naye kutoka nje ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa mwalimu Julius Nyerere.
Haron alipiga simu kwa mara nyingine kuzungumza na Kareem.

"Wamemkamata tayari" Alisema Haron mara baada ya Kareem kupokea simu yake.

"Sawa, kila kitu kitaenda kama nilivyokwambia. Tutaonana baada ya muda mfupi" Kareem alisikika upande wa pili wa simu ile kisha ikakatwa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Nje ya uwanja wa ndege Tesha alikuwa akimuangalia kila abiria anayetoka. Alimuona rafiki yake kipenzi Mina ambaye ndiye haswa aliyempa taarifa kuhusu ujio wa Felix siku hiyo. Tesha akajifanya kama hajamuona akaangalia pembeni hadi pale Mina alipopita na kuondoka, kifupi hakuta kabisa Mina afahamu kama amekuja kumpokea Felix.
Mwisho Tesha aliendelea na zoezi lake la kukagua abiria mmoja baada ya mwingine lakini ajabu hadi abiria wote wanakwisha Tesha hakufanikiwa kumuona Felix.

"Uko wapi Felix mbona sikuonii?" Tesha alijiuliza mwenyewe pasipo kupata jibu, sasa alikuwa amebaki mwenyewe eneo lile la kupokea wageni kila mtu alikuwa ameonana na mtu aliyekuja kumpokea isipokuwa yeye.

Mwisho Tesha alipata wazo akaenda hadi eneo la mapokezi kuuliza.

"Sahamani dada kuna ndugu yangu alikuwa kwenye ndege iliyofika muda huu kutokea nchini Marekani lakini sijamuona akitoka hapa, unaweza kunisaidia namna ya kumpata au labda atakuwa ametokea mlango mwingine tofauti na huu?" Aliuliza Tesha.

"Hakuna mlango mwingine wakutokea zaidi ya huu dadangu" Alijibu yule dada mhudumu eneo la mapokezi.

"Lakini sijamuona akitoka"

"Unauhakika alisafiri na ndege hii?"

"Mmh! Ndiyo.."

"Anaitwa nani? Nitajie majina yake matatu"

Tesha alitulia kwa muda akijaribu kufikiri, ukweli kwa kipindi chote cha mahusiano yake na Felix alikuwa akimtambua kwa jina moja tu yaani Felix.

"Aash! Mi ni mzembe sana..." Aliwaza Tesha huku akijipigapiga kichwa chake akijilaumu kwa kutokuyajua majina kamili ya mpenzi wake.

"Aah! Sahamani nalijua jina lake moja tu la kwanza anaitwa Felix.."

"Lakini si umesema ni ndugu yako?....okay anyway ngoja niangalie hapa...Felix, Felix, Felix....no BOEING 707 haikuwa na abiria yeyote mwenye jina la Felix dadangu?" Alisema yule muhudumu mara baada ya kukagua kwenye kompyuta yake. Ilikuwa ni taarifa iliyopita kama msumari wa moto kwenye moyo wa Tesha.

"Eti nini Felix hayupo? Lakini mbo..." Alisema Tesha lakini kabla hajamalizia sentensi yake mara ghafula pembeni yake katika mlango ule wa kutokea anaona watu zaidi ya kumi wakitoka huku baadhi yao wakiwa wamevalia sare za polisi na mmoja kati yao akiwa amefungwa pingu. Tesha aliweza kumfahamu, ni mpenzi wake Felix.

"Felix" Tesha aliita kwa sauti ya chini hali akiwa amepigwa na butwaa, hakuamini kile anachokiona.
Wakati akizidi kutazama ndipo hapo alipoweza kumuona pia askari mpelelezi anayemfahamu vizuri na siku ya jana alikutana naye wakafanya mazungumzo mafupi, Inspekta Brandina.

Tesha alizidi kuchanganyikiwa, hakuelewa ni nini hasa kinaendelea.

"Feliiiiix" Hatimae Tesha aliita kwa sauti.
Felix, Inspekta Brandina pamoja na baadhi ya askari waligeuka kwa pamoja kutazama mahali sauti hiyo ilipotokea.

Uso kwa uso Felix akagonganisha macho yake na macho ya kipenzi cha moyo wake Tesha.

"Te..Te...Tesha" Felix aliita kwa sauti ya chini naye akiwa haamini macho yake, hakutegemea kabisa kukutana na mwanamke huyo mazingira yale. Licha ya kumpenda sana lakini ni kwa muda mrefu Felix amekuwa akimkwepa Tesha kutokana na shinikizo kubwa kutoka kwa baba yake Magnus, hakuwa akiyataka kabisa mahusiano ya wawili hao kiasi cha kutishia kumuua Tesha.

"Yule mwanamke ni nani Tena?" Ilikuwa ni sauti ya Hustana akimuuliza mwenzake Kareem, wakati huo wakiwa juu kabisa ghorofani wakitazama kila kinachoendelea uwanja wa ndege kupitia darubini zao.

"Anaitwa Tesha, ni mpenzi wa Felix?"

"Khaa! Felix anampenzi, sikujua. Vipi hawezi kuharibu mpango wetu?" Aliuliza Hustana

"Sina hakikia acha tuone" Alijibu Kareem.

Wakati huo Tesha na Felix waliendelea kutazamana, hali hiyo ikidumu kwa zaidi ya sekunde 60 kila mmoja akiwa haamini anachokiona.

Je, nini kitafuata?
ITAENDELEA...

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
Back
Top Bottom