SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............22
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
ILIPOISHIA...
"Wameniamsha hao washezi na kelele zao, ujue najisikia vizuri sana kulala hapa miguuni pako David" Alisema Dayana huku akifumbua macho yake yaliyoregea akawa anamtazama David usoni.
Je, nini kitafuata?
SASA ENDELEA...
Usiku ulikuwa umesogea sana lakini mwanga wa mwezi ulisaidia kuwaangazia katika bonde lile kubwa na la ajabu.
"Kwa hiyo hivi ndivyo huwa unalala siku zote?" Aliuliza David
"Kivipi, kulala kwenye miguu ya watu au?" Dayana naye akajibu kwa swali huku akionekana kukelwa na kauli ya David.
"Hapana namaanisha hakuna sehemu za kulala! Baridi kali namna hii mnaweza kuishi hivi tena bila nguo alafu bado kuna vitu vingi sivielewi elewi Dayana"
Dayana alinyanyua kichwa chake kutoka miguuni kwa David kisha akakaa.
"Hivi kumbe nilivyokwambia awali watu wanakufa humu hukunielewa?"
"Sawa nakumbuka, lakini mbona wewe unaishi na umeniambia umemaliza mwaka mzima kwenye hili bonde, hii inawezekanaje? Kuna mahitaji muhimu ya kibinadamu humu bondeni hamna"
"Mfano nini David? Kama ni chakula umeona wanatupa mikate na maji kila siku asubuhi mchana na jioni, mahitaji gani mengine unataka? Humu ni kama kambi ya jeshi"
"Sawa lakini vipi kuhusu kulala, kuoga, kujisaidia, kujikinga na maradhi, hali ya hewa na mambo mengine mengi"
Aliuliza David, Dayana akacheka sana.
"Wewe ni last-born kwenu eeh! Mbona unadeka hivyo. Anyway David kila mtu humu anaishi kwa kujiongeza. Sio siri maisha ni magumu mno kama unavyosema. Kuna muda hadi unaweza kutamani kufa lakini ndio hivyo bado tunapenda kuendelea kuishi tunaamini siku moja ipo tutaokolewa kutoka kwenye hili bonde la mauti. Kuhusu kuoga sijui nini, kuna mto na chemchem za maji huko mbele nitakupeleka kesho ukaone. Kama ni baridi inazuilika ndio maana unaona watu wamekaa kimakundi makundi wamewasha moto wanaota. Hivyo maisha yanasonga. Wapo wanaojaribu kujenga vibanda humu humu bondeni. Usinione hivi nilikuwa mnene sana na mwili wangu ulionawili lakini sasa nimekonda hatari na bado naendelea kukonda"
Alieleza Dayana.
"Kwa hiyo hapo ndio umekonda?" Aliuliza David huku akiukagua mwili wa Dayana juu hadi chini. Tayari David alianza kuizoea hali ya kukaa nusu uchi wala hakuwa na haya tena ya kumtazama Dayana.
Mara Zungu akatokea akiwa amebeba rundo la kuni na nyasi kiasi. Begani mwake alikuwa na nguo ya ndani (taiti).
"Ooh! Mrembo wangu umeamkaa? Au wamekuamsha hao jamaa wa Mapinduzi Yafanyikeee...Kwa ajili ya maisha bora ya ISRA na watu wake" Alisema Zungu na kuirudia ile kauli mbiu ya Magnus na wanafunzi wake, alikuwa akiisikia kila siku usiku wakati wa darasa la Magnus hivyo aliikalili.
"Huko ISRA wanakotaka maisha bora ndio wapi kwani?" Aliuliza David
"Hakuna mtu anayejua, sisi wenyewe tunaishia kusikia kama wewe. Labda hapa ndio ISRA yenyewe utajuaje" Alisema Zungu huku akiutua ule mzigo wa kuni akauweka chini kisha akachukua ile nguo ya ndani ya kike 'taiti' akamrushia Dayana.
"Umeiba wapi tena? Hata haijakauka maskini umeanua nguo ya watu Zungu" Alisema Dayana akiikagua nguo hiyo.
"Huitaki niirudishe au?"
"Aah! Hapana sijasema hivyo, asante Zungu kama Zungu, tena ngoja niivae sasa hivi" Alisema Dayana, akainuka na kuanza kuelekea kwenye kona moja ya bonde hilo.
"Sasa si uvalie hapa hapa" Alisema Zungu huku akitabasamu.
"Achana na mimi wewe..."
Dayana aliondoka kubadilisha nguo ya ndani aliyoletewa na Zungu. Wakati huo David akawa anamtazama Zungu namna anavyo hangaika kuwasha moto kwa kutumia mawe. Alikuwa akiyagonganisha mawe hayo yaliyotoa cheche za moto.
"Mbona unaniangalia sana mshikaji wangu, haya ndio maisha yetu. Tunapambana"
"Hiyo nguo uliyompa Dayana umetoa wapi kwani?"
"Nmetoa huko mtoni nilipoenda kukusanya kuni, kuna maza alikuwa kaanika alafu akapitiwa na usingizi hapo hapo, nikapita nayo"
"Kwa hiyo akiamka atavaa nini, atabaki uchi?"
"Atajua mwenyewe, mara nyingi huwa tunachukua nguo kutoka kwa watu waliokufa yaani maiti, mtu akifa ukiwahi unachukua nguo zake, angalau unakuwa hata na nguo mbili au tatu za kubadilisha. Mfano hii pensi ya jeans niliyovaa nilichukua kwa mwamba mmoja aliamua kujiua mwenyewe baada ya kuona maisha yamekuwa magumu humu bondeni, alizoea maisha ya kishua huko kwao. Alipoletwa tukamwambia watu tuna miaka humu bondeni akaona bora atembee na mia, akajipiga kitanzi" Alieleza Zungu na mara hiyo Dayana akawa amerejea akiwa amevaa ile taiti ya rangi ya pink.
"Woow! Umependeza mamaa kama Mobeto au Tesha kabisa" Alisema Zungu huku akimtazama Dayana kwa macho yaliyojaa tamaa za kiume.
David alijikuta anakumbuka mbali mara baada ya Zungu kumtaja staa Tesha, akawa amekaza macho yake kumtazama Dayana lakini alikuwa mbali kimawazo.
"Aah! Mwanangu macho hayo, demu wa watu huyu" Alisema Zungu kisha wote wakacheka kwa sauti.
Waliendelea kupiga stori mbili tatu David akionekana kutaka kujua mengi kuhusiana na uhalisia wa maisha ya mateka katika bonde la Magnus.
Mwisho ulifika ule mda ambao Zungu aliahidi angeenda kumuonyesha David njia za kutoka katika bonde hilo la ajabu. Wakainuka tayari kuondoka, Dayana naye akasimama.
"Na wewe vipi!?" Aliuliza Zungu
"Naenda pia, sikuamini kabisa Zungu unaweza ukamfanya chambo mkaka wa watu wakamuua bure."
"Aah! Hapana Dayana, mimi binafsi namuamini Zungu hawezi kunifanyia kitu kibaya, acha tuungane kuangalia ni namna gani ya kutoka kwenye hili bonde na hiki kisiwa. Binafsi siko tayari kumaliza mwaka kama ninyi, nitapambana na tutatoka kurudi nyumbani" David aliongea kwa sauti ya upole yenye kumaanisha, Dayana akatabasamu.
"Naam! Mwamba huyu hapa! Ujue siku zote nimekuwa natamani kushirikiana na mtu mwenye ujasiri kama wako David, sema nini kama anataka kutufuata acha twende naye" Alisema Zungu, mwisho wakakubaliana kuondoka kwa pamoja.
Walitembea kwa tahadhali sana wasije kushtukiwa na wenzao pamoja na askari walinzi ambao walikuwa wakirandaranda juu kabisa ya bonde hilo.
"Mmh! Hili bonde ni kubwa sana eeh!" Aliuliza David baada ya mwendo wa kama dakika tano hivi.
"Saana! Limekaa kama bakuli flani hivi, ni duara, ukuta umetuzunguuka pande zote. Na kila kona kuna walinzi, huwezi kutoka kirahisi mpaka uwe na master mind kama mimi" Alieleza Zungu na kujisifia kama kawaida yake.
Wakatembea tena kwa dakika mbili zaidi mara ghafula Zungu akasimama.
"Sasa sikieni, bakini kwanza kwenye hii kona mimi nikasome ramani hapo mbele. Huwa kunakuwa na walinzi wengi sana hapa tukishavuka tu huko mbele ni kuteleza, acha nicheki kwanza kama dakika 10 nitarudi" Alieleza Zungu kisha wakakubaliana hivyo akaondoka akiwaacha David na Dayana wanamsubiri.
David alisimama akiwa ameegemea ukuta wa bonde hilo, akayafumba macho yake akionekana kutafakari jambo. Kuna wakati alihisi labda yuko kwenye usingizi mzito wenye ndoto ya ajabu ataamka kama kawaida na kuendelea na maisha yake, lakini la hasha, kila kilichokuwa kinatokea kilikuwa ni kweli tupu.
Mara ghafula David alihisi kuna mtu amesimama mbele yake, haraka akafungua macho yake kutazama. Ni kweli kulikuwa na mtu.
"Dayana?" David aliita kwa mshangao
"David please!?" Alisema Dayana kwa sauti ndogo iliyolegea huku akizidi kumsogelea David akamkumbatia.
"Nini tena Dayana...!"
"Nisaidie mwenzio, ni mda sasa sijananlii.."
"Nanlii nini hebu sogea basi Zungu atatukuta hapa"
"Kasema anarudi baada ya dakika 10, Davii..zinatosha sana please nisaidie mwenzio nateseka" Alisema Dayana huku akianza kuushika shika mwili wa David. Ilikuwa ni rahisi kwa sababu pia wote walivaa nguo za ndani pekee
"Da...ya...naaa!!" David aliita kwa taabu kidogo lakini Dayana hakuacha, alidhamiria.
[emoji294][emoji294][emoji294]
Upande wa pili Godfrey anashtuka ghafula kutoka usingizini, katikati ya usiku mnene huku akiliita jina la mpenzi wake aliyepotea miezi 13 iliyopita, Dayana.
"Dayana.. Dayana uko wapi mama" Alijisemea Godfrey huku akionekana kuhema kwa nguvu, alikuwa ameota ndoto mbaya sana kumhusu mpenzi wake huyo waliyependana sana.
Godfrey aliinuka pale kitandani akawa anaelekea sebuleni angalau apate chochote kutuliza akili.
Akiwa sebureni anamkuta mdogo wake Tesha akiwa bado hajalala.
"Tesha?" Godfrey aliita kwa mshangao, Tesha hakujibu.
"Mbona hujalala mpaka sasa?"
"Sina usingizi kabisa kaka, kila nikifikiria mambo yaliyotokea leo nakosa amani. Sijui David yuko wapi, yuko salama au laa!" Alijibu Tesha kisha akanywa glasi moja ya bia iliyokuwa mezani.
Godfrey alimtazama mdogo wake usoni kwa masikitiko makubwa akaona kabisa ni kweli suala la David lilikuwa likimtesa si kidogo. Alikumbuka hata yeye pia anapitia katika hali kama hiyo tangu siku alipompoteza Dayana katika mazingira ya ajabu sana.
Hakuna aliyejua kuwa usiku huu Dayana na David wako pamoja ndani ya bonde moja la ajabu katika kisiwa alichojichimbia Magnus baada ya kufukuzwa ISRA.
"Tesha.."
"Nambie bro"
"Unampenda?"
"Na..nani?"
"I mean David, do you love him?"
Aliuliza Godfrey huku akimtazama mdogo wake kwa macho ya udadisi
Je, nini kitafuata?
David atafanya nini mbele ya Dayana?
Vipi kuhusu Felix kule Marekani?
Ni ipi itakuwa adhabu ya Sasha asubuhi?
ITAENDELEA...