Simulizi: Sasha Mlinzi wa Nafsi - 1

Simulizi: Sasha Mlinzi wa Nafsi - 1

SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........16
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Mmesababisha majanga makubwa sana ndani ya ISRA, kutoweka kwa msitu wa Bi Noha ni laana kubwa ndani ya ISRA, ni lazima muwajibike kwa hili" Alisema Dumayo.

Je nini kitafuata?

SASA ENDELEA...
ISRA ...
Mkuu wa ISRA Gu Gamilo pamoja na askari na baadhi ya wafanyakazi wengine ndani ya Ikulu ya ISRA walionekana pembeni ya shimo kubwa mahali palipokuwepo msitu mkubwa maarufu kama msitu wa Bi Noha.
Walikuwa wakitazama maafa makubwa yaliyotokea kiasi cha kusababisha msitu huo kutoweka wote kwa namna ya ajabu sana. Ilikuwa ni hali iliyomshangaza kila mmoja. Hakuna aliyekuwa na jibu sahihi ni kipi hasa kimepelekea msitu huo kupatwa na majanga na mwisho kuzama wote ardhini.
Gu Gamilo baba yake Sasha alitazama kwa umakini huku uso wake ukionekana kujawa na wasiwasi mwingi.
Gu Gamilo alikuwa ni mzee kiasi sura yake iliyokunjamana wakati wote, ilikuwa ni adimu kuliona tabasamu la mzee huyo. Nywele zake ndefu na nyeupe alizozifunga kwa juu, huku kidevu chake kikiwa kimefunikwa na ndevu zenye rangi nyeupe vilevile vilimfanya mzee huyo kuwa na muonekano wa pekee katika ISRA.

Mpaka dakika hiyo hakuna aliyejua sekeseke lilotokea upande wa pili wa shimo hilo kule walipo Dumayo Sasha na akina Handan.

Tukio la kutoweka kwa msitu huo lilionekana kumtisha sana Gu Gamilo kiasi cha mkumfanya akumbuke kwa mara ya mwisho alivyoingia ndani ya msitu huo akafanikiwa kuonana na Bi Noha ambaye kwa sasa ni marehemu. Gu Gamilo aliyakumbuka vizuri maneno mazito aliyowahi kuelezwa na bibi kizee huyu, alisema...

...... Umefanya kosa kubwa bila kufikiria kwa makini Gu Gamilo, kumfukuza Kaka yako MAGNUS nje ya ISRA bado hujamaliza tatizo, kwa kosa alilofanya alistahili adhabu kubwa zaidi ya hiyo. Ipo siku utayakumbuka maneno yangu Siku ambayo Magnus atarudi tena ISRA na kuitikisa kwa mara nyingine. Haijarishi itachukua miaka mingapi lakini jua kwamba Magnus ni lazima atarudi tena akiwa amejipanga vilivyo. Atakushambulia kutoka pande zote, mashariki magharibi kaskazini na kusini. Itakuwa ni siku ambayo utakosa kwa kukimbilia hata msitu wangu ambao pengine ungeweza kujificha hautokuwepo tena, litakuwepo shimo kubwa lisilo na mwisho Gu Gamilo..........
Haya yalikuwa ni maelezo ya Bi Noha ambaye ni kama alijua siku moja msitu wake utatoweka na kubaki shimo.

........Bi Noha, nifanyaje sasa kuzuia hili lisitokee tafadhali nisaidie, nawezaje kumzuia kaka Magnus...........

........Hakuna mtu yeyote ISRA atakae weza kumzuia Magnus, isipokuwa yupo Mwanadamu mmoja ambaye ataweza kupambana naye na kumzuia Magnus asirudi tena ISRA, mwanadamu huyo anahitaji ulinzi. Kama atakufa basi ISRA itakuwa kwenye wakati mgumu, kama akiwa hai basi ISRA itaendelea kusimama...........

........Ni mwanadamu gani huyo Bi Noha, unaweza kuniambia tafadhali.........

.........Mtafute, na hakikisha unamlinda kabla Magnus hajamtambua........

Hizi zilikuwa ni kumbukumbu za Mkuu wa ISRA Gu Gamilo. Baada ya hapo aliondoka kinyonge yeye na watu wake huku kila mmoja akisubiri kwa hamu Gu Gamilo atasema nini baada ya tukio hilo ambalo wengi waliliona kama ishara mbaya kwa ISRA.
Hatimae Gu Gamilo alilejea Ikulu ya ISRA yeye na msafara wake, wakati anaingia lango kuu la Ikulu alipokelewa kwa shauku na mkewe kipenzi Malkia Hella(Mama yake Sasha). Alikuwa akimsubiri Mumewe kwa hamu ili amueleze ni nini hasa kimetokea maana kila mtu alionekana kuogopa.
Alipoiona Sura ya huzuni kwa mumewe Gu Gamilo ilikuwa ni tafsiri tosha kuwa mambo hayakuwa mazuri kabisa.

"Ni nini kinaendelea huko nje Gu Gamilo..." Aliuliza Malkia Hella
"Umetoweka.." Gu Gamilo alijibu kinyonge
"Nini? Nini kimetoweka!?"
"Msitu wa Bi Noha" Ilikuwa ni kauli iliyo muacha kinywa wazi Malkia Hella.
Akiwa katika hali hiyo ya mshangao mara wakasikia mlio wa farasi langoni. Gu Gamilo na mkewe wakageuka taratibu kutazama.
Uso kwa uso wakamuona Dumayo anaingia taratibu na msafara wake. Gu Gamilo aliikunja sura yake akionyesha wazi ni jinsi gani alikuwa anamchukia shemeji yake huyo. Lakini tofauti na Malkia Hella yeye alitabasamu mara baada ya kumuona kaka yake Dumayo anaingia.

Katika hali ya kushangaza nyuma ya msafara wa Dumayo walionekana wanawake wanne wakiwa wamefungwa kamba mikokoni huku wakivutwa na watu wa Dumayo waliokuwa juu ya farasi. Wanawake hawa walikuwa ni Sasha, Handan pamoja na wale walinzi wengine wawili.
Gu Gamilo alitoa macho kwa mshangao asiamini anachokiona.
"Sasha" Gu Gamilo aliita kwa sauti ya chini.
Wakati huo Dumayo yeye awaka anatabasamu tu kama kawaida yake.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili......
David alifumbua macho yake taratibu fahamu zikiwa zimemrejea. Hali akiwa na maumivu makali ya kichwa, alitazama mahali alipo. Alikuwa ndani ya chumba kimoja kipana huku mikono na miguu yake ikiwa imefungwa na vyuma maalumu vilivyokuwa ukutani. Alikuwa ametanuliwa mikono yake na kusimamishwa kama vile yupo msalabani.
Alipotazama mbele akawaona wale jamaa wenye helmet zenye vioo vyekundu wakimalizia kuwafunga watu wengine watatu ukutani kama vile walivyomfunga yeye baada ya hapo wakafungua mlango wa chumba hicho wakatoka na kuondoka. David alitazama kushoto na kulia kwake ndipo akagundua kuwa karibu kuta zote nne za chumba hicho kulikuwa na watu wamefungwa kama yeye na wengi wao walikuwa wamepoteza fahamu hawajitambui. Kwa Haraka haraka aliwahesabu walifika kumi na mbili. David aliogopa sana, hakuelewa ni wapi yupo na amefikaje. Bado kumbukumbu zake zilikuwa hazijakaa sawasawa.

"Oya nyie, nifungueni, njooni mnifungue....mnajua mimi ni nani!??" David alianza kupiga kelele huku akifoka.
"NYIE JAMAAAAAAA..."
David alizidi kupiga kelele.
"Kelele zako hazito saidia kitu, unamaliza nguvu zako bure..."
Mara sauti hii ya kike ilisikika kutoka pembeni yake upande wa kushoto. Haraka David akageuka kutazama ni nani aliyemuongelesha.
Uso kwa uso akagonganisha macho yake na mmoja kati ya wale wanawake waliokuwa wakimfuatilia tangu awali. Alikuwa ni Femi, naye alikuwa amefungwa vilevile kama yeye.

David aliogopa sana alipomuona lakini alipogundua naye amefungwa kama yeye aliduwaa huku kumbukumbu za matukio kadhaa yaliyotokea tangu alipoanza kuwaona wanawake hao wa ajabu zikijirudia kichwani kwake kama filamu.

"We..we. ni nani?"
"Naitwa Femi..." Alijibu Femi huku akitema mate chini, mate yaliyochanganyikana na damu ya kijani.
David alitazama yale mate pale chini kisha akageuka tena na kumtazama yule mwanamke akiwa katika hali ya mshangao mkubwa.

"Fe..femi wa wapi? Kwa nini mlikuwa mnanifuatilia?"
"Kwa sababu tunataka kukuua" Femi alieleza bila kusita
"Bado unaendeleza ukichaa wako Femi si ndiyo?" Mara sauti ya Zucc kutoka upande wa kulia kwa David ilisikika. David alishtuka na kugeuka kumtazama.
"Na wewe pia ulikuwa ukinifuatilia..!" Alisema David lakini bado alionekana kuogopa.
"Achana naye huyo!" Alisema Femi akimtaka David asiendelee kuzungumza na Zucc, David akageuka tena upande wake wa kushoto alipo Femi.

"Mnataka kuniua nimewakosa nini kwani?"
"Tumeagizwa tukuue..." Alijibu Femi lakini kabla hajaendelea zaidi Zucc akamkatisha kwa sauti kali iliyojaa hasira, hakupendezwa kabisa na anachokifanya mwenzake.
"Femi nimesema acha ujingaaaa ..." Alifoka
"Zucc hakuna tulichobakiza kwani hata nikimwambia ukweli kuna ubaya gani? Unafikiri tutapona na tayari tumeshafanya uzembe wenyewe mwisho tumeingia kwenye mikono ya MAGNUS" Alieleza Femi.
"Ma..ma.. Magnus ndio na..nani kwani?" Aliuliza David akiwa ndio kwa mara yake ya kwanza analisikia jina la mtu huyo MAGNUS , mtu ambaye kwa mujibu wa maelezo ya marehemu Bi Noha anatakiwa kupambana naye siku za usoni.
Kabla David hajajibiwa swali lake mara wakasikia mtikisiko mkubwa na baadae wakahisi kama wanasogea mbele.
Kumbe chumba hicho kilikuwa ni moja kati ya vyumba vingi ndani ya Meli moja kubwa ambayo sasa iling'oa nanga na kuanza kukata mawimbi taratibu kuelekea kusiko julikana.

ITAENDELEA...

0756862047
 
0756862047

Ipo tayari
IMG-20230307-WA0047.jpg
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya..........17
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Kumbe chumba hicho kilikuwa ni moja kati ya vyumba vingi ndani ya Meli moja kubwa ambayo sasa iling'oa nanga na kuanza kukata mawimbi taratibu kuelekea kusiko julikana...

SASA ENDELEA...

Zilikuwa zimepita dakika 55 tangu Tesha alipolejea kutoka kule mgahawani. Sasa alikuwa ndani ya sebule moja kubwa nyumbani kwake.

Tesha hakuwa ametulia kabisa, bado alikuwa akilitafakari lile tukio la kutekwa kwa David na watu wasiojulikana. Alikuwa akimsubiri kaka yake Godfrey kwa hamu kubwa ili aje ampatie maelezo kwa kina kwani alionyesha wazi anajua kila kinachoendelea ndio sababu alimzuia kupiga simu polisi.

Tesha alikosa amani kabisa, tangu afike nyumbani kwake hakupata muda wa kukaa, wakati wote alikuwa amesimama wima akizunguuka zunguuka sebuleni huku akili yake ikiwa imetawaliwa na taswira ya Mwanaume David. Akazidi kumuomba Mungu wake amuepushe na kila aina ya ubaya ambao David anaweza kufanyiwa na watu wale wenye helmet kichwani.

Dakika chache baadae Tesha alisikia muungurumo wa gari nje ya nyumba yake haraka akakimbia dirishani kwenda kuchungulia. Baada ya kufunua pazia aliona gari mbili zikiwa zimeongozana kuingia ndani. Moja aliifahamu ni gari ya kaka yake Godfrey lakini nyingine hakujua ni ya nani.
Alirudi na kukaa juu ya sofa akawa anamsubiri kaka yake kwa hamu ambaye punde aliingia akiwa ameongozana na mwanamke mmoja mweusi na mnene aliyevalia suti ya damu ya mzee na miwani ya jua myeusi, alikuwa ni Brandina.
Baada ya salama Godfrey akafanya utambulisho.

"Aaa.. karibu sana nyumbani kwetu Brandina, huyu ni mdogo wangu anaitwa Tesha, Tesha huyu ni Askari mpelelezi anaitwa Brandina. Ni rafiki yangu pia" Alieleza Godfrey kisha Tesha akamkaribisha Brandina kwa mara nyingine.

"Tesha najua unamaswali mengi ya kuniuliza juu ya tukio uliloliona masaa machache yaliyopita pale mgahawani, nimekuja hapa na Brandina kwa makusudi kwa sababu yeye ndiye atakueleza japo kwa ufupi kila kilichotokea, atakuwa na maswali machache ya kukuuliza na mwisho atatupa ufafanuzi nini kifanyike, karibu Madam Brandina"
"Asante sana God...Tesha"

"Abeeh!"

"Kwanza kabisa pole, najua utakuwa na wasiwasi mwingi ila nikutoe hofu kwamba utakuwa salama wala hakuna shida kubwa"

"Kuwa salama mimi sio tatizo afande, vipi kuhusu David,?"Aliuliza Tesha, Brandina akasita kujibu akageuka na kutazamana na Godfrey.

"Aah.. ukweli tunajaribu kupambana kuhakikisha David pamoja na wengine wote waliotekwa na watu hawa wanapatikana haraka iwezekanavyo"
"Ina maana kuna watu wengine wengi wametekwa?"
"Ndiyo, serikali inajaribu kulifuatilia suala hili kimya kimya ili kuepuka kuzua taharuki kwa Raia. Ni miaka minne sasa imepita tangu matukio kama haya yaanze kutokea hapa nchini" Alieleza Brandina, akatulia kwa muda kisha akaendelea...

"Nimeanza kufuatilia suala hili miaka mitatu iliyopita kabla sijakutana na kaka yako Godfrey ambaye naye alipotelewa na mpenzi wake Dayana mwaka jana katika mazingira ya kutatanisha kama hivi leo. Tangu siku hiyo nimekuwa nikishirikiana na kaka yako Godfrey ambaye sio siri amekuwa akinisaidia sana sana kuwafuatilia hawa watekaji"

"So ni akina nani wanafanya huu utekaji na huwa wanawapeleka wapi watu wanaowateka?" Aliuliza Tesha

"Hatujui, nachoweza kusema watu hawa wamekuwa wakifanya matukio ya utekaji kwa kujirudia rudia na huwa tunashindwa kuwakamata kwa sababu kuna mambo ya ajabu kidogo huwa yanaambatana na matukio haya, ni kama kuna nguvu zisizo za kawaida huwa zinatumika"

"Una maana gani?"

"Anamaanisha uchawi, yaani nguvu za giza" Godfrey akadakia.

"Mmh!" Tesha akaguna

"Tesha.." Aliita Brandina

"Abeeh"

"Ni kitu gani ulikiona mara baada ya kuingia mle mgahawani kabla kaka yako hajaja kukutoa?"

"Aaa! ukweli niliona tu wanaume wanne wale wenye helmet wakiwa wamesimama mbele ya wanawake wawili waliovaa magauni mekundu wakiwa wamelala chini pembeni yao nlimuona pia David akiwa amelala chini. Aliweza kufumbua macho na kunitazama ghafula ndio kaka akatokea na kunitoa pale" Alieleza Tesha

"Sawa pole sana, vipi kabla ya hapo David aliwahi kukueleza jambo lolote ambalo uliona sio la kawaida au unahisi linaweza kuhusiana kwa namna yoyote na huu utekaji?"

"Mmh! Hapana sina mazoea ya mda mrefu na David, nina mda mfupi sana tangu nijuane naye....aah! Kuna kitu Nimekumbuka... Leo hii kabla hatujatoka humu ndani David alikuwa hapa sebuleni mimi na kaka tulikuwa chumbani ghafula alikuja akikimbia akasema ameona watu wa ajabu hapa dirishani"

"Enhe! Ikawaje? Godfrey ulikuwepo pia?"
"Yes madam nilikuwepo"
"Sasa mbona hujanieleza kitu muhimu kama hiki, ni watu gani aliwaona?"

"Nilipitiwa tu, ila ni kweli David alidai ameona watu wa ajabu hapo dirishani na tulipokuja kutazama ni kweli kioo kilikuwa kimepasuka ajabu ni kwamba tulipo wauliza walinzi wakadai hawajaona mtu yeyote nje"

"Ni dirisha lipi?"
"Hilo hapo mbele yako"

Brandina alisimama akapiga hatua hadi pale dirishani akawa anachunguza kwa makini. Macho yake yalitua kwenye picha moja kubwa ukutani, ilikuwa ni picha ya mwanaume mmoja mtanashati akiwa amepiga picha hiyo pamoja na Tesha nje ya kampuni yake ya mitindo Tesha Fashion.
Brandina alionyesha mshtuko mkubwa sana mara tu baada ya kuitazama picha hiyo, lakini akajitahidi kuficha mshtuko wake.

"Huyu mwanaume ni nani?" Aliuliza Brandina.
Kabla ya kujibu Tesha na Godfrey wakatazamana.

"Anaitwa Felix ni mchumba wa Tesha" Alijibu Godfrey.

"Mchumba!? And David who is he?"

"David ni rafiki tu wa kawaida, kwani vipi afande?" Alijibu Tesha akionekana kukerwa na maswali ya Brandina.

"Nothing special" Alijibu Brandina, akarudi kwenye kiti na kuendelea na mazungumzo.

Mwisho kabisa Brandina alishukuru akaaga na kuondoka huku akiahidi kurudi kwa mara nyingine kama itabidi.

Brandina alitoka nje ya jengo hilo la kifahari, akaingia kweye gari yake kisha akachukua faili moja na kulipekua haraka haraka. Alifunua mahali penye picha za watu kadhaa zilizobandikwa juu ya karatasi. Brandina alikaza macho yake kutazama picha moja kati ya zile zote huku akivua miwani.
Amini usiamini picha anayoitazama Brandina ilikuwa ni picha ya Felix mpenzi wa Tesha. Katika picha hiyo Felix alionekana akiwa amesimama pembeni ya Noah nyeusi na mkononi mwake ameshikilia helmet yenye kioo chekundu kama ile waliyovaa watekaji wa David.
Chini ya picha hiyo kulikuwa na maelezo yaliyoandikwa kwa kalamu ya wino yaliyosomeka

'2019-tukio namba 11'

Brandina alivuta pumzi ndefu na kuitoa taratibu kisha akainua macho yake kulitazama jengo hilo la kifahari.
"Anaitwa Felix" Alisema Brandina kisha akatabasamu.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili.......ISRA.
Gu Gamilo alitoa macho kwa mshangao asiamini anachokiona.
"Sasha" Gu Gamilo aliita kwa sauti ya chini.
Wakati huo Dumayo yeye awaka anatabasamu tu kama kawaida yake.

Punde wakaingia viongozi wengine wenye nyazifa za juu ndani ya mji wa ISRA, tayari Dumayo alishasambaza uvumi kabla ya kufika Ikulu kuwa Sasha mtoto wa Gu Gamilo ameingia ndani ya msitu wa Bi Noha bila ruhusa na kisha kusababisha msitu huo kupotea. Viongozi wengi walifika ili kuja kuthibitisha taarifa hizo.

"Sasha ameingia ndani ya msitu bila ruhusa, kinyume na sheria na taratibu zetu za ISRA. Amesababisha msitu pamoja na Bi Noha kutoweka na kuacha shimo la mauti, hii ni laana kubwa ndani ya ISRA laana kubwa mno, ni lazima kifanyike kitu kuondoa laana iliyosababishwa na mtoto wa Gu Gamilo" Dumayo aliongea kwa nguvu huku akinyoosha mkono wake wenye upanga kumuelekea Sasha. Watu wote waliokuwepo mahali hapo waliguna kwa mshangao na kushika midomo yao, zilikuwa ni taarifa mbaya sana kuwahi kutokea ISRA.

Maneno haya ya Dumayo yalipenya kama msumali wa moto kwenye moyo wa Gu Gamilo, aligeuka taratibu na kumtazama binti yake Sasha, Wakatazamana. Sasha akainamisha kichwa chake chini. Hii ilikuwa ni ishara tosha kwa Gu Gamilo kuwa tuhuma alizozitoa shemeji yake Dumayo ni kweli tupu.

Gu Gamilo alifumba macho yake akiwa na uchungu mkubwa, hakika alikuwa na mtihani mkubwa sana mbele yake hakujua ni jinsi gani ataweza kumtoa binti yake kipenzi Sasha kwenye balaa kubwa lililoko mbele yake.

[emoji294][emoji294][emoji294]
Katikati ya Bahari Meli iliyowabeba David, Zucc, Femi pamoja na mateka wengine iliendelea kuchana mawimbi ikizidi kusonga mbele. Hakuna aliyeelewa ni wapi wanapelekwa...

ITAENDELEA....
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............18
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
Brandina Askari mpelelezi anayo picha ya Felix mchumba wa Tesha katika faili lake la kazi. Wakati huo meli iliyowabeba mateka David akiwa mmoja wapo inaendelea kusonga mbele kuelekea kusiko julikana.
Upande wa pili Dumayo anatangaza hadharani kosa kubwa alilolifanya Sasha.

ITAENDELEA...
ISRA.
Gu Gamilo alifumba macho yake akiwa na uchungu mkubwa, hakika alikuwa na mtihani mkubwa sana mbele yake hakujua ni jinsi gani ataweza kumtoa binti yake kipenzi Sasha kwenye balaa kubwa lililoko mbele yake.

"Mchukueni Sasha na wenzake wawekeni gerezani" Hatimae Mkuu wa ISRA Gu Gamilo alitoa amri kwa Askari ambao walitii na kuwabeba Sasha, Handan pamoja na wale wanawake wawili wakawakokota kuwapeleka gerezani kama walivyoagizwa.

"Unafanya nini Gu Gamilo?" Aliuliza mkewe (Malkia Hella) kwa sauti ya chini ambayo ni mumewe pekee ndiye aliyeweza kusikia.
"Unahisi nitafanya nini!? Inabidi kila kitu kiende kama sheria inavyosema... Sasha ataadhibiwa" Alisema Gu Gamilo akionyesha msimamo wake kama Mkuu wa ISRA lakini ukweli ukawa pale pale hata yeye mwenyewe alikuwa akiumia mno ila hakuwa na namna.
Malkia Hella alionekana kufedheheshwa mno na maneno hayo ya Gu Gamilo lakini alipotazamana na kaka yake Dumayo wakatabasamu na kukonyezana kwa siri.

Gu Gamilo akiwa ameweka mikono yake nyuma akapiga hatua kusogea hadi karibu na viongozi wa ISRA ambao walifika punde mara baada ya kusikia uvumi wa taarifa za Sasha binti wa Gu Gamilo kukamatwa.

"Tukutane kesho asubuhi kwa ajili ya kujadili hukumu ya Sasha" Alisema Gu Gamilo huku akiwatazama wale viongozi kwa macho makali.
"Mkuu sizani kama kuna sababu ya kusubiri hadi asubuhi ya kesho, hili suala ni kubwa mno. Angalia tayari msitu wa Bi Noha umetoweka haupo tena, hili sio suala la kulisubirisha hata kidogo. Aliyekosa aadhibiwe haraka iwezekanavyo kuepuka laana ndani ya ISRA" Aliongea kiongozi mmoja huku wengine wakitikisa vichwa vyao kukubaliana na maelezo yake.

"Kwa hiyo mnanifundisha cha kufanya si ndiyo, kwani mimi sijui kama hili nikosa kubwa linastahiri adhabu? Nawauliza mimi sijuiii?" Gu Gamilo alifoka huku midomo yake ikitetemeka kwa hasira.
Mara Dumayo akadakia...
"Mkuu amekwisha wapa maelezo mfike kesho asubuhi haraka ya nini. Muhimu mshtakiwa yupo mikononi mwake hakuna kitakacho haribika" Alisema Dumayo kauli iliyojaa unafiki mwingi ndani yake. Akageuka kumtazama shemeji yake Gu Gamilo, wakatazamana.
Mwsho wale viongozi waliondoka, Dumayo yeye akabaki hapo kama mgeni ndani ya Ikulu ya ISRA.
Wakati huo jua lilikuwa linakaribia kuzama.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Kabla ya jua kuzama tayari meli iliyowabeba akina David na wale wanawake wa ajabu kutoka ISRA (Zucc na Femi) ilitia nanga katika fukwe ya kisiwa kimoja kidogo.
Tayari kulikuwa na watu zaidi ya kumi ambao walikuwa wamesimama kwenye fukwe hiyo wakiisubiri meli hiyo kwa hamu. Walivalia nguo sawa kabisa na wale jamaa wenye helmet waliofanya utekaji wa watu waliopo melini.
Mara tu baada ya meli kusimama mateka walianza kushushwa mmoja baada ya mwingine, wakapokelewa na watu waliokuwa ufukweni kisha wakapakizwa kama magunia ndani ya gari linalofanana na lile gari la wakandarasi ambalo hubeba mchanga (tipper).
Wakati huo wale mateka waliokuwa wamepoteza fahamu tayari wote walikuwa wamerejewa na fahamu zao, wakawa wanaogopa na kupiga kelele kwa hofu lakini hakuna aliyeonyesha kuwajali.
Kulikuwa na mlima mkubwa katika kisiwa hicho, mara baada ya kumaliza kuwashuka mateka kutoka kwenye meli na kuwapakiza katika gari, safari ilianza huku gari hilo likifuata barabara moja iliyojengwa kwa namna ya ajabu sana.
Barabara hiyo ilikuwa ikikatiza chini ya ardhi katikati ya mlima na kutokea upande wa pili.
Dakika saba pekee zilitosha gari hilo kutokea upande wa pili wa mlima ambako huko kulikuwa na uwazi mkubwa na majengo kadha wa kadha yaliyozunguushiwa ukuta mrefu na mpana sana.
Kulikuwa na ulinzi mkubwa sana eneo hilo. Walinzi kadhaa wenye siraha mkononi walionekana wakirandaranda ndani na nje ya ngome hiyo huku wengine wakionekana wako juu kabisa mlimani.

David pamoja na mateka wengine walipokelewa na watu wengine tofauti ambao walifanya kazi ya kuwavua nguo zote wakawaacha na nguo za ndani pekee. Isipokuwa Zucc na Femi wao hawakuvuliwa yale magauni yao badala yake walitenganishwa na mateka wengine wao wakabebwa kuelekea katika jengo moja kubwa la ghorofa.

David pamoja na mateka wengine wakiwa na nguo za ndani pekee waliamrishwa waingie tena ndani ya lile gari lililowaleta, wakafanya hivyo. Baada ya hapo lile gari lilianza kurudi nyuma hadi mahali fulani ambapo Dereva alibinya kitufe fulani lile bodi la nyuma waliko David na wenzake likaanza kubinuka kama vile linamwaga mchanga.
David na wenzake walipiga kelele za kuomba msaada huku wakijaribu kujizuia wasidondoke lakini hakuna aliyewaonea huruma mwisho walijikuta wakimwagwa wote katika bonde moja kubwa ambako huko walipokelewa na watu wengine wengi waliokuwa wamevuliwa nguo na kuachwa na nguo za ndani tu kama wao.

David alianguka katika bonde hilo na kuumia vibaya sana, kichwa na mguu wake wa kushoto.
Akiwa amelala pale chini alishuhudia watu wengi karibu mia moja na kidogo wakiwa katika bonde hilo. Walikuwa wamechakaa sana kutokana na mazingira na maisha magumu wanayopitia wakiwa katika bonde hilo.
David alijikuta akikata tamaa ya maisha, hakujua ameletwa hapo kwa ajili gani na kwa nini. Hali ilitisha mno.
Wakati akiwa pale chini asijue cha kufanya. Mara aliona wale watu wakitimua mbio kuelekea kwenye kona moja ya bonde hilo. Walikuwa wakikimbia kwa kasi huku wakisukumana na wengine kuanguka chini.
David alipoinua macho yake kutazama juu zaidi aliona gari kama lile lililowaleta likimwaga chakula amacho ni mikate na maji. Wale watu walianza kugombaniana kila mmoja akipambana apate angalau maji au mkate. Hali ilikuwa ni tete, hadi dakika tano zinakatika bado mapambano hayo yalikuwa yakiendelea na kila aliyepata angalau maji au mkate alikimbia Kwenye kona yake na kuanza kukifakamia kile alichopata kwa kasi sana, walionekana ni watu wenye njaa kali sana.
David na wenzake wageni walipigwa na butwaa wasielewe A wala B.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Muda ukazidi kwenda jua likazama na sasa giza likaingia.
Sasha alionekana akiwa amekaa na kujiinamia ndani ya chumba kimoja kichafu chenye kitanda cha nyasi. Chumba kingine kinachofuata alionekana mlinzi wake namba moja Handan kisha vyumba vingine walikuwepo wale wanawake wengine walinzi wa Sasha. Lilikuwa ni gereza mahali walipofungiwa kama alivyoagiza baba yake Gu Gamilo.

Sasha alikuwa amezama kwenye dimbwi la mawazo asielewe nini hatima yake. Hakujua ni hukumu gani ingetolewa asubuhi ya siku inayofuata.
Lakini pamoja na yote hayo bado Sasha hakuacha kuyakumbuka maelezo aliyopewa na marehemu Bi Noha kuhusu jukumu kubwa la kumlinda mwanadamu aitwae David ili tu kuiokoa ISRA isiingie mikononi mwa mtu mbaya aitwae Magnus ambaye ni baba yake mkubwa.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa piliii...
David akiwa ndani ya bonde lile la ajabu alikaa na kujikunyata mahali huku akiwa ameegemea ukuta wa bonde hilo. Kulikuwa na baridi kali sana mahali hapo, lakini hakuna aliyejali labda kuwapa mashuka ya kujifunika, la hasha hakuwepo mtu wa aina hiyo.
Kijana David alikuwa akitafakari namna mambo yalivyobadirika ghafula na kujikuta ameingia kwenye maisha ya ajabu sana.
Anakumbuka kwa mara ya mwisho alipokuwa katika msiba wa hayati Mheshimiwa Rais JPM ndipo mambo yalibadilika ghafula baada ya kukutana na yule msichana mwenye gauni jekundu (Sasha).

David akiwa katika dimbwi la mawazo mara alisikia vishindo na mwisho kuna mtu akawa amesimama mbele yake.
Aliinua uso wake taratibu sana kumtazama kuanzia chini, akaona miguu na mapaja akagundua alikuwa ni mwanamke, akaona chupi yake yenye rangi ya bluu, hips, tumbo, matiti yaliyofunikwa na sidiria iliyochakaa sana kisha akaitazama sura nzuri ya mwanamke huyo lakini ilikuwa imefubaa kutokana na aina ya maisha wanayoishi kule bondeni.
Yule mwanamke akanyoosha mkono wake uliokuwa na kipande cha mkate na maji akawa anampatia David.

David alimtazama kwanza kwa sekunde kadhaa kisha akapokea. Yule mwanamke akakaa pembeni yake.

"Asante" David alishukuru kinyonge.
Kimya kikatawala kwa sekunde kadhaa kisha yule mwanamke akaongea.

"Naitwa Dayana, nilitekwa na kuletwa hapa kama wewe, ni mwaka mmoja sasa umepita, niko hapa" Alieleza Dayana...
"Mwaka?" David aliuliza kwa mshangao.
Naam huyu ni Dayana yule yule ambaye Godfrey kaka yake Tesha alidai amempoteza mwaka mmoja uliopita.

0756862047

Je, nini kitafuata?
Ni wapi hapa wameletwa mateka hawa?
Zucc na Femi wamepelekwa wapi?
Sasha atapewa adhabu gani?
Vipi kuhusu Brandina na ile picha ya Felix?

Mambo ni mengi, Endelea kuungana nami katika mfululizo wa simulizi hii MARIDHAWA
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
Ila mwanangu inaenda kinyonge sana! Kama umeamua kutuburudisha bure we tuburudishe tu! Hatulazimishi utupostie daily lkn hiki unachofanya ni unyanyasaji wa ki hisia!
 
Ila mwanangu inaenda kinyonge sana! Kama umeamua kutuburudisha bure we tuburudishe tu! Hatulazimishi utupostie daily lkn hiki unachofanya ni unyanyasaji wa ki hisia!
[emoji3064][emoji3064][emoji3064]
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............19
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Naitwa Dayana, nilitekwa na kuletwa hapa kama wewe, ni mwaka mmoja sasa umepita, niko hapa" Alielaza Dayana...
"Mwaka?" David aliuliza kwa mshangao.
Naam huyu ni Dayana yule yule ambaye Godfrey kaka yake Tesha alidai amempoteza mwaka mmoja uliopita.

SASA ENDELEA....

"Ndio nina mwaka na mwezi mmoja tangu nimetupwa ndani ya hili bonde" Alijibu Dayana.

David alitulia kwa sekunde kadhaa akijaribu kulitafakari jibu hilo kutoka kwa Dayana. Aligeuka kumtazama mwanamke huyo ambaye wala hakuwa na hata chembe ya aibu kwa namna alivyokuwa amevaa, asilimia kubwa ya mwili wake ulikuwa wazi, chupi na sidiria aliyovaa ndio angalau vilimsitiri sehemu zake nyeti lakini bado hata sidiria yake ilikuwa imechanika upande hivyo kufanya nusu ya matiti yake madogo kuwa wazi.

"Kwa hiyo mkiwa humu huwa mnafanya nini? Kuna kazi mnafanya kama watumwa?" Mwisho David akauliza.

"Wala tunaishi tu kama unavyotuona. Mimi pia wakati nimefika nilihisi labda tumeletwa kama watumwa tutafanyishwa kazi usiku na mchana lakini hapa mambo ni tofauti kabisa tunaamka tunakula tunalala tunaamka tunakula tunalala hayo ndio maisha yetu. Isipokuwa chakula ni cha shida sana. Kama ulivyoona, tunaishi kwa kugombaniana chakula mwenye nguvu ndio ataishi. Wapo watu waliofia humu kwa sababu ya kukosa chakula na maji"
Maelezo haya kutoka kwa Dayana yalizidi kumtisha David. Akatamani kujua zaidi.

"Kwa hiyo sababu ya hawa watu kutuleta hapa ni nini?"

"Sijui, kwa kweli sijui kabisa! Huwa mwanatuita sisi wote ni FUNGUO, funguo ya mkuu wa eneo hili anaitwa MAGNUS" Kwa mara ya pili Sasa David analisikia jina la mtu huyu aitwae Magnus. Mara ya kwanza alilisikia kutoka kwa Femi wakati ule wakiwa ndani ya meli.

"Funguo?"

"Ndiyo SISI NI FUNGUO"

"Funguzo za nini?"

"Funguo za Magnus"

"Kufungua nini?"

"Sielewi, inaonekana alishafungwa mahali kwa hiyo sisi ni kama funguo zake. Huwa anakuja kutusalimia mara moja moja, akisimama pale juu utasikia anapaza sauti anasema HABARI ZA LEO FUNGUO ZANGU.... Huwa simpendi yule mzee, anatisha hana utu ndani yake, anakera hata kumtazama" Alieleza Dayana.
Kimya kikatawala tena kwa muda

"Kwa hiyo hakuna namna yoyote ya kutoka humu? Hakuna aliyewahi kutoroka akafanikiwa?" Aliuliza David

"Hahahah! Utatoroka uende wapi, utatokaje kwenye hili bonde? Kila aliyejaribu kutoroka aliishia kufa. Kifupi hakuna namna yoyote ya kutoroka.."

"Ipo namna! ipo sema ni uwoga wako tu..." Mara sauti ya kiume ilisikika ikipingana na maelezo ya Dayana. Akatokea jamaa mmoja mwembamba na mrefu, akafika na kukaa pembeni ya David, alikuwa ni mmoja wao ndani ya bonde lile.

"Zungu..!!" Dayana aliita kwa mshangao.

"Nini!? Naona umepata boyfriend mpya umeamua kunikimbia"

"Acha masihara yako bwana huyu ni mgeni nimekuja kumriwadha kidogo..."

"Upo kamati ya mapokezi humu bondeni au? halafu mbona wamekuja wageni kibao mbona umewaacha umekuja kwa huyu mwamba hapa, umeshampenda tayari?" Aliuliza Zungu huku akichukua mkate ambao Dayana alimpa David akaanza kula.

"Unaitwa nani jamaa?" Aliuliza Zungu, David akawa kimya.
"Huna jina?"

"David.."

"David wow! Napendaga watu wenye majina ya Biblia kidogo huwa wanakuwa waelewa, sasa sikia David usimsikilize huyu Dayana ni muoga, kutoroka hapa inawezekana kabisa kama tukiamua mtu wangu, sema tawile" Alieleza Zungu

"Muongo usimsikilize anataka akufanye chambo, utakufa David" Dayana akadakia

"Kausha basi na wewe... Tangu lini nikaongopa au unafikiri mimi muongo muongo kama wewe!?"

"Kwani mimi niliwahi kukudanganya nini?"

"Hujui au?"

"Nini...!!"

"Unasikia David huyu demu alipofika kwenye hili bonde kwa mara ya kwanza wahuni walitaka kupita naye, walitaka kumbaka, mimi ndio nikamtetea. Mpaka leo hajawahi kunipa chochote anazingua"

"Kwa hiyo ulitaka nikupe nini!?"

"Kwani wewe hujui au?"

"Sijui, nitakupa nini sasa"

"Wewe ni mwanamke alafu hujui cha kunipa..."

"Kwa hiyo umesema kutoroka inawezekana?" David akaingilia kati mazungumzo ya Dayana na Zungu.

"Yes! Wewe uko safi sana, subiri watu walale nitakupeleka mahali, kila siku mimi huwa nafanya utafiti namna ya kutoroka tayari nazijua njia nyingi zinazotoka hadi nje kabisa ya hili bonde ishu ni kuvuka huo mlima hadi upande wa pili kule ufukweni" Alieleza Zungu
[emoji294][emoji294][emoji294]

ISRA
Mkuu wa ISRA Gu Gamilo alionekana akiwa amekaa meza moja na shemeji yake Dumayo. Ilikuwa ni muda mfupi umepita tangu awatawanye wale viongozi wa ISRA na kuwaambia wafike asubuhi ya siku inayofuata kujadili hukumu ya SASHA.

"Unajua huwa siamini kabisa mtu ambaye tulishirikiana naye bega kwa bega hadi tukafanikiwa kumuondoa MAGNUS hapa ISRA leo hii amegeuka na kuwa msaliti kama vile Magnus mwenyewe" Alisema Gu Gamilo huku akimtazama Dumayo usoni.

"Ah! Tatizo Shemeji unashindwa kunielewa, mimi siku zote huwa nasimama upande wenye haki. Ndio maana nilipambana kufa na kupona hadi tukamshinda na kumuondoa Magnus" Alieleza Dumayo. Gu Gamilo akawa anamtazama akijua kabisa Dumayo hakuwa anamaanisha anachokisema hata kidogo bali moyo wake umejaa chuki na wivu mkubwa.

"Kwa hiyo ulishindwa kumstiri binti yangu? kulikuwa na ulazima gani wa kumdharirisha Sasha namna ile, huoni kama umenichafua hata mimi?''

"Sasha kavunja sheria na kusababisha balaa kubwa ndani ya ISRA shemeji. Lazima aadhibiwe, Nilikuwa na uwezo wa kufanya hivyo unavyotaka lakini unajua kwa nini sijafanya?"

"Kwa nini?"

"Kwa sababu siku zote umekuwa ukimpendelea Sasha kuliko watoto wako wengine? Kuna kila dalili kuwa hata kiti chako cha uongozi siku moja utamrithisha Sasha na sio mtu mwingine ndio maana nataka nimfutilie mbali huyu binti"
"Kwanini, unahisi Sasha hastahiri kuwa mkuu wa ISRA hapo baadae?"

"Gu Gamilo, unajua kabisa Sasha sio familia yako! Sasha sio damu yako Sasha sio mtoto wenu wala sio...." Alisema Dumayo lakini kabla hajamalizia sentensi yake tayari upanga wa Gu Gamilo ulikuwa kwenye shingo yake.

"Katu! Nisije sikia kwa mara nyingine unaongea huo upuunzi mbele yangu wala mbele ya mtu yeyote yule Dumayo ni marufuku. Siku nikikusikia tena nitakukata shingo yako bila huruma.... Sasha ni mwanangu...ni binti yangu" Gu Gamilo aliongea kwa msisitizo akionekana mwenye jazba sana kisha akatupa upanga chini, akainuka na kuondoka.

"Ahahah! Nimekugusa pabaya... Hata hivyo huna utakalo fanya tayari Sasha ameshavuruga mambo..." Dumayo alijisemea mwenyewe. Wakati huo mdogo wake yaani Malkia Hella akajitokeza mahali alipokuwa amejificha akifuatilia maongezi ya mumewe na kaka yake.

"Sijui ni mdudu gani alishamuingia huyu mwanaume huwa hataki kabisa kusikia mtu akisema Sasha sio mtoto wetu" Alisema Malkia Hella huku akisogea na kukaa pale alipokuwa amekaa Gu Gamilo kabla hajaondoka.

"Usijali dada tayari tumeshapata njia ya kumtoa Sasha hapa Ikulu na ikiwezekana atanyang'anywa nguvu zake na kufukuzwa kabisa hadi nje ya ISRA kama vile alivyofanyiwa Magnus" alisema Dumayo

"Mmh! Kwa kweli sidhani, kwa namna anavyompenda Sasha sijui kama ataweza kuruhusu hili litoke"

"Ataruhusu tu apende asipende, halafu ni kwa nini anakapenda sana haka ka binti"

"Hata sielewi kaka yangu! Niliwahi kumpeleleza siku moja akadai kuwa aliambiwa na mtabiri mmoja kuwa Sasha ndiye atakuja kuiokoa ISRA hapo baadae kama ikiingia kwenye matatizo"

"Hahahahah hahahahah! Mtabiri gani huyo.. ni Bi Noha au?" Dumayo alicheka sana na kuuliza.
"Hapana sio Bi Noha"
Dumayo akazidi kucheka tena na tena.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Baada ya Gu Gamilo kuondoka, alienda ndani ya chumba kimoja cha siri akaagiza askari wake mashuhuri sana ISRA aitwe.

Baada ya muda askari huyo alifika na kumsalimia mkuu wa ISRA Gu Gamilo kwa heshima kubwa.

"Dojin" Gu Gamilo aliita

"Ndiyo Mheshimiwa"

"Nimekwita hapa nataka nikupe kazi moja ngumu ambayo itakuwa ni kubwa pengine kuliko kazi zote nilizowahi kukupa hapo kabla"

"Niko tayari kufanya kazi yoyote utakayonipa Mheshimiwa"

"Dojin.." Gu Gamilo aliita tena

"Ndiyo mkuu"

"Siku zote tumekuwa tukipambana kuiweka ISRA kwenye mikono salama, tumepigana vita nyingi na ngumu tukiwa pamoja. Vita hivyo bado havijafika mwisho Dojin. Unakumbuka kuna mtoto tuliwahi kumuokota wakati ule tukipigana vita na Magnus miaka mingi iliyopita?"

"Nakumbuka mkuu wangu"

"Unakumbuka nini kilitokea siku hiyo baada ya kumuokota huyo mtoto mchanga?"

"Nakumbuka kila kitu Mheshimiwa, alitokea bibi kizee mmoja wa ajabu akasema tumlee na kumlinda huyo mtoto kwa sababu ameibeba hatima ya ISRA hapo baadae"

"Vizuri kumbe unakumbuka, basi hayo maneno hata Bi Noha alishawahi kuniambia pia siku nilipo kutana naye. Unajua huyo mtoto mchanga tuliyemuokota ni nani?"
"Hapana sijui Mheshimiwa!?"

"Ni Sasha... Huyu binti yangu ambaye natakiwa kuitoa hukumu yake kesho" Alisema Gu Gamilo kauli iliyomshtua na kumuacha kinywa wazi Dojin. Siku zote alikuwa anaamini Sasha ni mtoto halisi wa Gu Gamilo kama wengine wanavyoamini. Hakuwa akijua kama yule mtoto waliyemuokota wakati ule alilelewa na Mkuu wa ISRA na ndio Sasha mwenyewe, hii ilikuwa ni siri kubwa.

"Nakata umtoroshe Sasha, kimbia nenda naye mbali hakikisha anakuwa salama, ikiwezakana toka naye hadi nje ya ISRA usirudi mpaka pale nitakapo kutaarifu" Alisema Gu Gamilo kauli iliyomfanya Dojin atoe macho kwa mshangao.

Je nini kitafuta?

Ni shillingi elf 1 tu 0756862047

Tayari tumeifahamu historia ya SASHA kwa ufupi...

Sasha ataweza kutoshoshwa?

Vipi kuhusu David naye ataweza kutoroka kutoka kwenye lile Bonde?

ITAENDELEA....
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............20
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...

"Nakata umtoroshe Sasha, kimbia nenda naye mbali hakikisha anakuwa salama, ikiwezakana toka naye hadi nje ya ISRA usirudi mpaka pale nitakapo kutaarifu" Alisema Gu Gamilo kauli iliyomfanya Dojin atoe macho kwa mshangao.

SASA ENDELEA...

"Siko tayari kumuona binti yangu anapewa adhabu ya kifo au hata kufukuzwa ISRA, kama atanyang'anywa nguvu zake na kufukuzwa sito isamehe nafsi yangu milele. Kumbuka tuliagizwa kumlinda tangu akiwa ni mtoto mchanga, nimefanya hivyo mpaka sasa ana umri wa miaka 23. Siwezi kukubali kumpoteza Sasha kirahisi namna hii" Gu Gamilo alitoa maelezo ambayo kwa kiasi yalimuingia askari wake mashuhuri Dojin. Lakini bado jukumu analopewa kumtorosha Sasha lilikuwa ni gumu mno.

Dakika chache baadae Gu Gamilo akiongozana na Dojin waliingia hadi gerezani kule alipofungiwa Sasha na wenzake.
Ulinzi ulikuwa ni mkali sana eneo hilo lakini kwa kuwa ni Mkuu wa ISRA basi aliachwa apite pasipo pingamizi lolote.

"Babaaa.." Sasha aliita hali akionekana kuwa na uchungu mkubwa mara tu baada ya kumuona baba yake Gu Gamilo akija pale alipo.

"Nisubiri hapa.." Gu Gamilo alimwambia Dojin naye akatii, hakutaka askari huyo asikilize maongezi kati yake na binti yake Sasha.
Gu Gamilo alipiga hatua akasimama nyuma ya uzio wa nondo za chuma ambao uliwatenganisha yeye na binti yake aliyepo ndani ya gereza hilo.

"Mwanangu..." Aliita Gu Gamilo huku akikumbatiana na binti yake kwa taabu sana wakipitisha mikono yao katikati ya zile nondo. Gu Gamilo akambusu Sasha katika paji la uso.

"Nisamehe baba, nisamehe sana"

"Usijali Sasha naelewa, ni kosa langu mimi.... Kwa mara ya kwanza nilikuacha utoke nje ya Ikulu lakini sikukupa maelezo ya kutosha nini ufanye na nini usifanye. Nisamehe mimi mwanangu" Gu Gamilo aliongea kwa uchungu mkubwa.
Wakazidi kukumbatiana na mwanae ambaye alilia kwa uchungu sana.

"Yako wapi machozi uliyokusanya?" Aliuliza Gu Gamilo, Sasha akaingiza mkono wake ndani ya mfuko wa gauni lake akatoa ile chupa aliyokuwa akiitumia kukusanya machozi akamkabithi baba yake.

"Sikufanikiwa kujaza machozi, nisamehe baba yangu"

"Usijali ni mara yako ya kwanza, hata hivyo umejitahidi sana"
Kimya kilitawala kwa sekunde kadhaa..

"Sasha" Gu Gamilo aliita.

"Abee..."

"Najua ni kweli uliingia kwenye ule msitu! Niambie ni nini uliona? Je ulifanikiwa kukutana na Bi Noha?" Gu Gamilo aliuliza maswali mfululizo kwa sauti ya chini na tulivu huku akionekana kuwa na shauku ya kujua.

Sasha akawa kimya hakujibu kitu.

"Nambie tu mwanangu usiogope.. Bi Noha alikwambia nini?"

Sasha aliendelea kuwa kimya, alikumbuka vizuri katazo alilopewa kuwa kila alichoambiwa na Bi Noha kinatakiwa kubaki siri, hakutakiwa kumweleza mtu yeyote yule kuhusu jukumu zito la kumlinda mwanadamu aitwae David.

"Sikumbuki kitu baba, sikumbuki kabisa, kumbukumbu zangu zimepotea" Sasha alidanganya.
Gu Gamilo alimtazama usoni akajua wazi binti yake hayuko radhi kueleza ukweli.

"Sawa mwanangu, basi nisikilize kwa makini, sitaki kesho uadhibiwe tayari kuna mtu nimemuandaa atakutorosha usiku wa leo, mtakimbia na kwenda mbali mahali ambapo hawawezi kuwapata"

"Hapana! Hapana baba huwezi kufanya hivyo"

"Nisikilize mimi baba yako Sasha! Unatakiwa kuondoka ISRA haraka iwezekanavyo"

"Hapana! Siwezi baba... Tayari nimekuweka kwenye matatizo, sitaki niendelee kuwa mzigo kwako. Acha waniadhibu vile wanavyotaka wao wewe baki kama Mkuu wa ISRA simama kwenye sheria za ISRA"

"Sasha...!" Gu Gamilo alifoka.

"Baba siwezi. Hata nikitoroka kila mtu atajua kuwa wewe ndio umenitorosha. Ya nini hayo yote, acha tu baba usihangaike na mimi"

"Sijali hayo yote mwanangu! Ni lazima uwe hai ni lazima uishi Sasha, wewe ni muhimu kuliko unavyofikiri"

"Ni muhimu kwako baba lakini sio muhimu kuliko sheria za ISRA" Sasha aliendelea kushikilia msimamo wake.
Kimya kilitawala tena kwa muda...

"Hii ni amri, sio ombi tena. Mimi kama mkuu wa ISRA nataka uishi, usiku wa leo ni lazima utoroshwe na Dojin" Aliongea Gu Gamilo kwa sauti iliyojaa mamlaka.

"Ni kheri nife kuliko kufanya hivyo baba..." Alisema Sasha kisha taratibu akaanza kufungua kamba za gauni lake.
Hii ilikuwa na maana kwamba, kwa sheria za ISRA mwanamke yeyote ambaye ataonyesha mwili wake mbele ya mwanaume asiye mume wake basi hastahiri kuishi. Hata sehemu ya mabega yake ikiwa wazi tayari anakuwa amevunja sheria hiyo ya ISRA. Baada ya kulazimishwa sana na baba yake Sasha aliona ni heri ajitengenezee adhabu hiyo ya kifo kwa kuivunja sheria hiyo ya ISRA kwani tayari mbele yake kulikuwa na wanaume wawili, Dojin na Gu Gamilo baba yake. Aliona ni heri kufa kuliko kuendelea kuwa mzigo kwa baba yake.

"Sasha achaaa...." Alisema Gu Gamilo huku akitazama pembeni na kuondoka haraka, Dojin naye aliziba macho yake akageuka na kumfuata Gu Gamilo nyuma, wakaondoka upesi huku Gu Gamilo alionekana mwenye hasira sana.

Hali machozi yakimtoka Sasha alisitisha kufanya kile alichokusudia kufanya, akafunga tena kamba za gauni lake akaegemeza kichwa chake ukutani huku machozi yakimbubujika kama maji.

Wakati haya yakiendelea kulikuwa na askri mmoja mpambe wa karibu wa Dumayo, alikuwa akifuatilia kwa karibu nyendo zote za Gu Gamilo. Mara baada ya kuondoka askari huyu alikimbia kupeleka habari kwa Dumayo juu ya kila alichokiona na kusikia. Alifika akaingia ndani ya chumba alichoandaliwa Dumayo kama mgeni katika Ikulu ya ISRA, akawa anamnong'oneza.

Dumayo alitabasamu mara baada ya kusikiliza maelezo ya askari huyo.

"Kwa hiyo Sasha amekataa kutoroshwa?" Aliuliza Dumayo.
"Ndiyo, kagoma kabisa..."

"Pumbaaafu, angejichanganya kidogo tu basi ndio ulikuwa mwisho wake yeye na baba yake" Alisema Dumayo, kisha akamgeukia askari wake.

"Endelea kuwafuatilia, ukiona kitu chochote cha tofauti njoo haraka unipe taarifa"

"Sawa Mheshimiwa" Alijibu yule askari kisha akaondoka. Dumayo naye akaingia chumbani na kujitupa kitandani.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Ulikuwa ni usiku mzito mno. Usiku mzito kwa Dumayo, Gu Gamilo, Malkia Hella na Sasha. Usiku mzito pia kwa Tesha, Brandina na David.

Dumayo yeye alikuwa akiisubiri kwa hamu asubuhi ya siku inayofuata ili kujua ni hukumu gani itapitishwa na Mkuu wa ISRA Gu Gamilo.

Hali ilikuwa mbaya zaidi kwa Gu Gamilo mwenyewe. Usiku huo akiwa kitandani alitazama juu ya paa huku akili yake ikiwaza nini afanye, tayari binti yake Sasha amekataa katakata kutoroshwa na ameona ni heri kufa kuliko kuzidisha matatizo kwa baba yake. Kichwa kikazidi kumuuma Gu Gamilo, muda ulizidi kusonga bado hakuwa na jibu nini afanye.
Pembeni yake alilala mkewe Malkia Hella, naye hakuwa na usingizi, alikuwa akiisubiri kwa hamu asubuhi ya siku inayofuata ili ashuhudie mtoto wake wa kumlea ambaye ni kipenzi cha mumewe akipewa adhabu ambayo aliamini lazima itamfurasha.

Hali ilikuwa hivyo kwa Sasha pia kule gerezani, tayari alishakata tamaa ya kila kitu. Hakujua hatima yake itakuwa ni ipi itakapofika asubuhi. Lakini kila alipokumbuka maelezo aliyopewa na marehemu Bi Noha kule msituni, moyoni akapata tumaini.
"Sitokufa" Sasha alijisemea mwenyewe.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili kwa mwanamke mrembo kupindukia na mwanamitindo maarufu nchini Tanzania Tesha, naye hakupata hata repe la usingizi. Wakati wote alikuwa akimfikiria David. Ni mwanaume aliyemzoea kwa muda mfupi sana lakini anashangaa kuona moyo wake unatamani kuendelea kuwa karibu naye. Hakujua kama yuko salama au laa! yuko hai au wamemuua.
Kwa muda mfupi Tesha alijikuta anamsahau kabisa mpenzi wake Felix ambaye kwa sasa amemtelekeza na kwenda zake Marekani.

Usiku huo pia polisi mpelelezi Brandina naye hakuwa amelala. Alikuwa nyumbani kwake ndani ya chumba kimoja kidogo. Ukutani kulikuwa na ubao wenye picha nyingi zikiwemo zile picha alizopiga Godfrey kaka yake Tesha wakati wa tukio la kutekwa kwa David pale mgahawani.
Brandina alikuwa akiichimba kwa undani kesi ya utekaji wa watu katika maeneo mbalimbali nchini.
Ni muda mrefu tangu Brandina na askari wenzake wameanza kuipeleleza kesi hii lakini mpaka sasa hawakuwa na majibu kamili ni wapi wanapelekwa mateka hao? Ni nani kiongozi wa oparesheni hiyo ya utekaji? Ni nini sababu ya kufanya utekaji huo?, Hakuna aliyejua.
Lakini moja kati ya picha zilizokuwa katika ubao ule ilikuwa ni picha ya Felix mpenzi wa Tesha. Ilionekana wazi Brandina anamjua Felix vizuri na ni mmoja kati ya watu anaowafuatilia.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande mwingine usiku ulikuwa ni mrefu pia kwa kijana David akiwa ndani ya lile bonde la ajabu.
Tayari maisha yake yamebadilika ghafula na kujikuta ni mmoja kati ya mateka wanaoshinda wakiwa wamevaa nguo za ndani pekee, si wanaume si wanawake. Wote walikuwa ni mateka wa mtu wanayemuita Magnus.
Huyu alikuwa ni Magnus yule yule kutoka ISRA kaka yake Gu Gamilo na baba mkubwa wa Sasha. Alifukuzwa ISRA miaka mingi iliyopita mara baada ya kufanya uasi mkubwa, tangu siku hiyo hakuwahi kurudi tena ISRA.

David alikuwa amekaa na kuegemea ukuta wa bonde hilo huku yule mwanamke Dayana akiwa amelala usingizi miguuni pake.
David alikuwa akisubiri wakati ufike ambao Zungu alimuahidi atamuonyesha njia za kutoka katika bonde hilo.

Ni tsh elf 1 tu 0756862047

Je nini hatima ya MKASA huu?
Endelea kuwa nami Katika sehemu zinazofuata.

ITAENDELEA....

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............21
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

MAREKANI
Ni Katika hoteli moja ya kifahari na maarufu nchini Marekani - LUXOR LAS VEGAS ndani ya mji wa Nevada. Mwanaume mmoja wa ki-afrika anaonekana akiwa ndani ya bwawa la kuogelea 'swimming pool' alikuwa amejilaza juu ya boya lililomfanya aelee juu ya maji huku akiwa ameitanua mikono na miguu yake.
Kijana huyu anaeonekana kuwa na pesa ndefu aliyafumba macho yake na kutulia. Alionekana mtu mwenye mawazo sana.

Mara simu yake iliyokuwa juu ya meza pembeni ya bwawa hilo ilitoa muungurumo 'vibration'.
Mwanaume huyu alifumbua macho yake kisha akajivuta hadi pembeni ya bwawa akajifunga taulo lake na kuifuata simu yake.
Kulikuwa na jumbe sita zilizoingia mfululizo kwenye programu ya WhatsApp akazifungua. Akaona ujumbe wa maandishi ulioambatana na picha nne pamoja na video moja.
Mwanaume huyo alifungua na kuzitazama kwanza zile picha.
Zilikuwa ni picha zilizomuonyesha mwanamitindo maarufu nchini Tanzania Tesha akiwa kwenye mazungumzo nyeti na kijana mmoja aitwae David mgahawani.
Kama utakumbuka wakati ule Tesha na David walipokuwa mgahawani wakifanya mazungumzo kuna mtu alionekana anawapiga picha kwa siri.

Mwanaume huyo alionyesha mshtuko kiasi mara baada ya kuziona picha zile, haraka akausoma ujumbe wa maandishi kabla ya kuicheza ile video. Ujumbe ulisomeka hivi...

,,,,,,Bro Felix huyu ndio jamaa anaonekana kuwa karibu sana na Shem Tesha siku za hivi karibuni na hii ni video ya majibu aliyoyatoa leo kuhusu uhalisia wa mahusiano yake wakati akihojiwa na waandishi wa habari,,,,,,

Alimaliza kuusoma ujumbe huo taratibu mapigo yake ya moyo yakaanza kumuenda mbio
Ndiyo, Mwanaume huyu alikuwa ni Felix yule mpenzi wa Tesha ambaye amekuwa akitajwa mara nyingi kuwa ameondoka na kumtelekeza Tesha akaja Marekani. Bado haikujulikana sababu hasa ya Felix kufanya hivyo lakini pamoja na hayo yote Felix alimuajili mtu nchini Tanzania ambaye alikuwa akimfuatilia Tesha kwa ukaribu na kumpa habari kwa kila anachokifanya. Hii ni ishara tosha kwamba bado Felix anamuhitaji Tesha.

Ujumbe huo ulimfanya Felix kuingiwa na ubaridi wa hofu, haraka bila kupoteza muda akaicheza ile video. Ilikuwa ni kipande kifupi cha video kilichomuonyesha Tesha akifanya mahojiano na waandishi wa habari wakati ule pale hospitali alipomsindikiza David kumuona mama yake.

" Na vipi kuhusu msimamo wa mahusiano yako kwa sasa , still upo single kama unavyosema siku zote ?" Aliuliza mwandishi wa habari

"Hahahah Nooo! Am not single ... soon nitaenda kumuweka wazi mkalia ini wangu "

" Wow tutegemee lini miss Tesha ..."
" Nimesema soon, so ni suala la kukaa na kusubiri, as you know mimi nikiongea kitu lazima nikitimize "
" Sawa Tesha, Hivi karibuni umekuwa uki ...."
" Hapana jamani inatosha next time "


Video iliishia hapo lakini tayari ilitosha kumfanya Felix awe katika hali ya kupaniki.

Felix akatembea haraka kuelekea chumbani kwake lakini kabla hajafika njiani anakutana na msaidizi wake wa karibu ambaye alitoka kidogo wakati bosi wake akiogelea, aliitwa Haron.

"Bosi vipi kwema!?" Aliuliza Haron

"Sio kwema hata kidogo" alijibu Felix akapiga hatua na kuingia ndani ya chumba chake akakaa kindani.

"Nini shida tena Mkuu?"
Felix hakujibu alitulia kimya akiwa amejiinamia kwa sekunde kadhaa kisha akainua uso wake na kumtazama Haron usoni.

"Hivi ni kwa nini mnaninyima uhuru wangu? Kwa nini wewe na baba mnataka niishi vile mnavyotaka ninyi na sio ninavyotaka mimi?" Felix aliuliza huku akimtazama Haron kwa macho makali, alionekana kuwa na jazba.

"Ni kuhusu Tesha tena au?" Aliuliza Haron

"Ndiyo ni kuhusu mwanamke ninaempenda Tesha, hivi Haron unajua nini kinataka kutokea? Tesha amechoka kusubiri sasa anataka kuniacha kwa sababu ya sheria zenu za ajabu nisizozi....."

"Kaa kimya Felix" Haron alimkatisha Felix aliyekuwa akilalamika huku akitupa mikono yake kama mwendawazimu.

Haron akapiga hatua akasogea karibu kabisa na Felix, sasa wakawa wanatazamana

"Hivi ni mara ngapi tukueleze kwamba hutakiwi kumpenda mwanadamu, Felix wewe sio kama wao. Hapa sio kwenu, inabidi akili yako ipambane kufikiria ni jinsi gani tunamsaidia baba yako MAGNUS kurudi nyumbani kwetu ISRA huna cha....."

"Mimi ni Binadamu Haron, sina tofauti na wao, nina haki ya kupenda kama wengine wanavyopenda. Nampenda Tesha na niko tayari hata kufa kwa ajili yake. Hakuna mtu anaweza kunizuia narudia tena HAKUNAAA" Felix alifoka

"Huna unachokijua Felix, wakati baba na mama yako wanafukuzwa ISRA ulikuwa mtoto mdogo sana, huelewi chochote kwa hiyo sio kosa lako. Ila kaa ukijua hapa sio kwetu na hutakiwi kumpenda mwanadamu yeyote, hizi ni sheria za nyumbani kwetu ISRA unatakiwa kuziheshimu kwa sababu wewe pia umezaliwa huko. Hii ndio sababu baba yako amekuleta Marekani ili kukuweka mbali na yule mwanamke Tesha. Sasa kama utalazimisha basi utamuweka hatarini hata huyo Tesha mwenyewe, Magnus baba yako atamuua"

"Eeh! Atamuua eti eeh! Kwa hiyo mnajaribu kunitishia si ndio?... Sawa, tutaona"
Alisema Felix kisha akainuka pale kitandani, akasogea mbele akachukua wembe uliokuwa mezani, bila kusita akajikata kidogo kwenye mshipa wa damu mkono wake wa kulia.

Haron alitoa macho kumshangaa Felix asijue nini maana yake.

Damu yenye rangi ya kijani ikawa inamtoka Felix mahali alipojijeruhi.

"Unaona hii damu, i swear one day I'll bleed red... Siku moja nitavuja damu nyekundu. Siku ambayo nitajitenga na ninyi, nitaanza maisha yangu nikiwa huru kama watu wengine. Nakwambia wewe na baba pia nitamwambia" Felix aliongea akimaanisha, akachukua simu yake tena na kutazama zile picha alizotumiwa.

"Oda tiketi mbili za ndege kesho asubuhi na mapema tunaanza safari kurudi Tanzania" Alisema Felix

"Nini?"

"Kama hutaki acha nitapiga simu mwenyewe" Alijibu Felix kisha akaondoka na kuingia bafuni.

"Nilijua tu haitokuwa rahisi kukuongoza, ngoja nimtaarifu baba yako tuone, sitaki shida mimi" Haron alijisemea mwenyewe huku akichukua simu yake akapiga namba alizokuwa amezihifadhi kwa jina la 'ISRA KING' ni namba za Magnus.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili simu iliita kwa muda mwisho ikapokelewa.

"Mheshimiwa Felix mwanao anataka kurudi nyumbani, kuna taarifa amezipata hukusu yule mpenzi wake. Sasa analazimisha kurudi nyumbani"

"Naingia darasani kwa sasa, fanya vile anavyotaka. Muache arudi" Sauti nzito na yenye kukwaruza ilijibu kwa ufupi kutoka upande wa pili wa simu kisha ikakatwa.

Katika moja ya majengo makubwa ndani ya kile kisiwa walichopelekwa mateka David na wengine, alionekana Mzee mmoja mwenye umri kama miaka 67 hivi. Alikuwa na uso mweusi wenye sura ngumu iliyokomaa Nywele zake ndefu na nyeupe sana zinazofika mabegani mwake, hata ndevu zake nyingi zilikuwa na rangi nyeupe pia. Macho yake yalikuwa ni mekundu sana, kila alipotembea aliongozana na wanawake wanne ambao mikononi mwao walishikilia visahani vidogo vilivyokuwa na mizizi fulani iliyochomwa na kutoa moshi mwingi mweupe. Harufu ya Moshi huo ilikuwa ni burudani tosha kwa mzee huyo ambaye wakati huu alikuwa amevalia kanzu nzito nyeusi inayoburuza chini pale anapotembea.
Naam huyu si mwingine bali ndiye MAGNUS mwenyewe kutoka ISRA, kaka yake Gu Gamilo na baba mkubwa wa Sasha lakini pia ni baba mzazi wa kijana Felix.
Magnus alitembea taratibu sana huku mikono yake ikiwa nyuma. Kila alipopita askari wake walinzi waliinamisha vichwa vyao chini kwa heshima kubwa.
Mwisho Magnus aliingia katika chumba kimoja kikubwa mithiri wa hekaru. Ndani alikuta kuna watu karibu thelathini wamekaa wanasubiri. Wengi wao walikuwa ni wanawake waliovalia magauni mekundu. Wanaume ambao idadi yao ilikuwa ni watu sita pekee wao walivaa kanzu ndefu zenye rangi nyekundu pia.
Hawa waliitwa wanafunzi wa Magnus. Jambo la kushangaza miongoni mwa wanafunzi hao alikuwepo Zucc na Femi wale wanawake wawili kutoka ISRA waliotumwa kumuua kijana David lakini wakashindwa na mwisho wakajikuta wanatekwa na kuletwa katika kisiwa hicho cha Magnus. Hivi ndivyo Magnus alivyofanya wakati wote. Mateka wote kutoka ISRA aliwageuza wanafunzi wake huku akiwafundisha mambo mengi kiasi cha kuweza kuwashawishi na kuwafanya watu wake waaminifu. Lakini mateka ambao ni binadamu aliwapeleka kule kwenye lile bonde la ajabu kama alivyofanya kwa David na wenzake huku akiwabatiza jina na kuwaita 'Funguo'.

Chumba hicho hakikuwa na taa, badala yake kulikuwa na mishumaa mikubwa iliyowekwa juu ukutani kukizunguuka chumba chote. Pia ukutani kulichorwa michoro mingi inayoonyesha picha na maadhari ya mji wa ISRA.

Magnus alifika na kusimama mbele ya darasa lake, wale wanawake alioongozana nao waliweka vile visahani vinavyotoa moshi mezani kisha wakaondoka na kutoka nje ya darasa hilo.

Magnus akiwa pale mbele aliwatazama wanafunzi wake kwa zamu mmoja baada ya mwingine kisha akaongea kwa sauti kubwa na nzito inayokoroma iliyojaa kitetemeshi.

"Mapinduzi yafanyikeeeee......!!!"

"Kwa ajili ya maisha bora ya ISRA na watu wake"
Wanafunzi wa Magnus waliitikia isipokuwa Zucc na Femi, hii ndiyo ilikuwa kauli mbiu ya Magnus na wanafunzi wake.
Akarudia tena huku safari hii akikunja ngumi mkono wake wa kulia na kuinua.

"MAPINDUZI YAFANYIKEEEEEEE....."

"KWA AJILI YA MAISHA BORA YA ISRA NA WATU WAKE...." Waliitika

Kelele hizo zilisikika mpaka kule bondeni aliko David na wenzake.
David aliinua macho yake kutazama juu ya bonde zinakotokea kelele hizo. Akawa haelewi ni nini kinaendelea.

"Kila siku huwa wanafanya hivyo..." Sauti ya Dayana iliyojaa usingizi ilisikika akiwa amelala pale miguuni pake.

"Kumbe haujalala?" Aliuliza David, huku akimtazama Dayana kwa macho yaliyojaa huruma. Ni mmoja kati ya wanawake wanaopitia mateso wakiishi nusu uchi ndani ya bonde hilo.

"Wameniamsha hao washezi na kelele zao, ujue najisikia vizuri sana kulala hapa miguuni pako David" Alisema Dayana huku akifumbua macho yake yaliyoregea akawa anamtazama David usoni.

ITAENDELEA...
N shillingi elf 1 tu lipia kwa Mpesa namba 0756862047 jna SAUL kisha njoo in-box WhatsApp
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............22
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Wameniamsha hao washezi na kelele zao, ujue najisikia vizuri sana kulala hapa miguuni pako David" Alisema Dayana huku akifumbua macho yake yaliyoregea akawa anamtazama David usoni.

Je, nini kitafuata?

SASA ENDELEA...

Usiku ulikuwa umesogea sana lakini mwanga wa mwezi ulisaidia kuwaangazia katika bonde lile kubwa na la ajabu.

"Kwa hiyo hivi ndivyo huwa unalala siku zote?" Aliuliza David

"Kivipi, kulala kwenye miguu ya watu au?" Dayana naye akajibu kwa swali huku akionekana kukelwa na kauli ya David.

"Hapana namaanisha hakuna sehemu za kulala! Baridi kali namna hii mnaweza kuishi hivi tena bila nguo alafu bado kuna vitu vingi sivielewi elewi Dayana"
Dayana alinyanyua kichwa chake kutoka miguuni kwa David kisha akakaa.

"Hivi kumbe nilivyokwambia awali watu wanakufa humu hukunielewa?"

"Sawa nakumbuka, lakini mbona wewe unaishi na umeniambia umemaliza mwaka mzima kwenye hili bonde, hii inawezekanaje? Kuna mahitaji muhimu ya kibinadamu humu bondeni hamna"

"Mfano nini David? Kama ni chakula umeona wanatupa mikate na maji kila siku asubuhi mchana na jioni, mahitaji gani mengine unataka? Humu ni kama kambi ya jeshi"

"Sawa lakini vipi kuhusu kulala, kuoga, kujisaidia, kujikinga na maradhi, hali ya hewa na mambo mengine mengi"
Aliuliza David, Dayana akacheka sana.

"Wewe ni last-born kwenu eeh! Mbona unadeka hivyo. Anyway David kila mtu humu anaishi kwa kujiongeza. Sio siri maisha ni magumu mno kama unavyosema. Kuna muda hadi unaweza kutamani kufa lakini ndio hivyo bado tunapenda kuendelea kuishi tunaamini siku moja ipo tutaokolewa kutoka kwenye hili bonde la mauti. Kuhusu kuoga sijui nini, kuna mto na chemchem za maji huko mbele nitakupeleka kesho ukaone. Kama ni baridi inazuilika ndio maana unaona watu wamekaa kimakundi makundi wamewasha moto wanaota. Hivyo maisha yanasonga. Wapo wanaojaribu kujenga vibanda humu humu bondeni. Usinione hivi nilikuwa mnene sana na mwili wangu ulionawili lakini sasa nimekonda hatari na bado naendelea kukonda"
Alieleza Dayana.

"Kwa hiyo hapo ndio umekonda?" Aliuliza David huku akiukagua mwili wa Dayana juu hadi chini. Tayari David alianza kuizoea hali ya kukaa nusu uchi wala hakuwa na haya tena ya kumtazama Dayana.

Mara Zungu akatokea akiwa amebeba rundo la kuni na nyasi kiasi. Begani mwake alikuwa na nguo ya ndani (taiti).

"Ooh! Mrembo wangu umeamkaa? Au wamekuamsha hao jamaa wa Mapinduzi Yafanyikeee...Kwa ajili ya maisha bora ya ISRA na watu wake" Alisema Zungu na kuirudia ile kauli mbiu ya Magnus na wanafunzi wake, alikuwa akiisikia kila siku usiku wakati wa darasa la Magnus hivyo aliikalili.

"Huko ISRA wanakotaka maisha bora ndio wapi kwani?" Aliuliza David

"Hakuna mtu anayejua, sisi wenyewe tunaishia kusikia kama wewe. Labda hapa ndio ISRA yenyewe utajuaje" Alisema Zungu huku akiutua ule mzigo wa kuni akauweka chini kisha akachukua ile nguo ya ndani ya kike 'taiti' akamrushia Dayana.

"Umeiba wapi tena? Hata haijakauka maskini umeanua nguo ya watu Zungu" Alisema Dayana akiikagua nguo hiyo.

"Huitaki niirudishe au?"

"Aah! Hapana sijasema hivyo, asante Zungu kama Zungu, tena ngoja niivae sasa hivi" Alisema Dayana, akainuka na kuanza kuelekea kwenye kona moja ya bonde hilo.

"Sasa si uvalie hapa hapa" Alisema Zungu huku akitabasamu.
"Achana na mimi wewe..."

Dayana aliondoka kubadilisha nguo ya ndani aliyoletewa na Zungu. Wakati huo David akawa anamtazama Zungu namna anavyo hangaika kuwasha moto kwa kutumia mawe. Alikuwa akiyagonganisha mawe hayo yaliyotoa cheche za moto.

"Mbona unaniangalia sana mshikaji wangu, haya ndio maisha yetu. Tunapambana"

"Hiyo nguo uliyompa Dayana umetoa wapi kwani?"

"Nmetoa huko mtoni nilipoenda kukusanya kuni, kuna maza alikuwa kaanika alafu akapitiwa na usingizi hapo hapo, nikapita nayo"

"Kwa hiyo akiamka atavaa nini, atabaki uchi?"

"Atajua mwenyewe, mara nyingi huwa tunachukua nguo kutoka kwa watu waliokufa yaani maiti, mtu akifa ukiwahi unachukua nguo zake, angalau unakuwa hata na nguo mbili au tatu za kubadilisha. Mfano hii pensi ya jeans niliyovaa nilichukua kwa mwamba mmoja aliamua kujiua mwenyewe baada ya kuona maisha yamekuwa magumu humu bondeni, alizoea maisha ya kishua huko kwao. Alipoletwa tukamwambia watu tuna miaka humu bondeni akaona bora atembee na mia, akajipiga kitanzi" Alieleza Zungu na mara hiyo Dayana akawa amerejea akiwa amevaa ile taiti ya rangi ya pink.

"Woow! Umependeza mamaa kama Mobeto au Tesha kabisa" Alisema Zungu huku akimtazama Dayana kwa macho yaliyojaa tamaa za kiume.

David alijikuta anakumbuka mbali mara baada ya Zungu kumtaja staa Tesha, akawa amekaza macho yake kumtazama Dayana lakini alikuwa mbali kimawazo.

"Aah! Mwanangu macho hayo, demu wa watu huyu" Alisema Zungu kisha wote wakacheka kwa sauti.

Waliendelea kupiga stori mbili tatu David akionekana kutaka kujua mengi kuhusiana na uhalisia wa maisha ya mateka katika bonde la Magnus.

Mwisho ulifika ule mda ambao Zungu aliahidi angeenda kumuonyesha David njia za kutoka katika bonde hilo la ajabu. Wakainuka tayari kuondoka, Dayana naye akasimama.

"Na wewe vipi!?" Aliuliza Zungu

"Naenda pia, sikuamini kabisa Zungu unaweza ukamfanya chambo mkaka wa watu wakamuua bure."

"Aah! Hapana Dayana, mimi binafsi namuamini Zungu hawezi kunifanyia kitu kibaya, acha tuungane kuangalia ni namna gani ya kutoka kwenye hili bonde na hiki kisiwa. Binafsi siko tayari kumaliza mwaka kama ninyi, nitapambana na tutatoka kurudi nyumbani" David aliongea kwa sauti ya upole yenye kumaanisha, Dayana akatabasamu.

"Naam! Mwamba huyu hapa! Ujue siku zote nimekuwa natamani kushirikiana na mtu mwenye ujasiri kama wako David, sema nini kama anataka kutufuata acha twende naye" Alisema Zungu, mwisho wakakubaliana kuondoka kwa pamoja.

Walitembea kwa tahadhali sana wasije kushtukiwa na wenzao pamoja na askari walinzi ambao walikuwa wakirandaranda juu kabisa ya bonde hilo.

"Mmh! Hili bonde ni kubwa sana eeh!" Aliuliza David baada ya mwendo wa kama dakika tano hivi.

"Saana! Limekaa kama bakuli flani hivi, ni duara, ukuta umetuzunguuka pande zote. Na kila kona kuna walinzi, huwezi kutoka kirahisi mpaka uwe na master mind kama mimi" Alieleza Zungu na kujisifia kama kawaida yake.

Wakatembea tena kwa dakika mbili zaidi mara ghafula Zungu akasimama.

"Sasa sikieni, bakini kwanza kwenye hii kona mimi nikasome ramani hapo mbele. Huwa kunakuwa na walinzi wengi sana hapa tukishavuka tu huko mbele ni kuteleza, acha nicheki kwanza kama dakika 10 nitarudi" Alieleza Zungu kisha wakakubaliana hivyo akaondoka akiwaacha David na Dayana wanamsubiri.

David alisimama akiwa ameegemea ukuta wa bonde hilo, akayafumba macho yake akionekana kutafakari jambo. Kuna wakati alihisi labda yuko kwenye usingizi mzito wenye ndoto ya ajabu ataamka kama kawaida na kuendelea na maisha yake, lakini la hasha, kila kilichokuwa kinatokea kilikuwa ni kweli tupu.

Mara ghafula David alihisi kuna mtu amesimama mbele yake, haraka akafungua macho yake kutazama. Ni kweli kulikuwa na mtu.

"Dayana?" David aliita kwa mshangao

"David please!?" Alisema Dayana kwa sauti ndogo iliyolegea huku akizidi kumsogelea David akamkumbatia.

"Nini tena Dayana...!"

"Nisaidie mwenzio, ni mda sasa sijananlii.."

"Nanlii nini hebu sogea basi Zungu atatukuta hapa"

"Kasema anarudi baada ya dakika 10, Davii..zinatosha sana please nisaidie mwenzio nateseka" Alisema Dayana huku akianza kuushika shika mwili wa David. Ilikuwa ni rahisi kwa sababu pia wote walivaa nguo za ndani pekee

"Da...ya...naaa!!" David aliita kwa taabu kidogo lakini Dayana hakuacha, alidhamiria.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili Godfrey anashtuka ghafula kutoka usingizini, katikati ya usiku mnene huku akiliita jina la mpenzi wake aliyepotea miezi 13 iliyopita, Dayana.

"Dayana.. Dayana uko wapi mama" Alijisemea Godfrey huku akionekana kuhema kwa nguvu, alikuwa ameota ndoto mbaya sana kumhusu mpenzi wake huyo waliyependana sana.

Godfrey aliinuka pale kitandani akawa anaelekea sebuleni angalau apate chochote kutuliza akili.
Akiwa sebureni anamkuta mdogo wake Tesha akiwa bado hajalala.

"Tesha?" Godfrey aliita kwa mshangao, Tesha hakujibu.

"Mbona hujalala mpaka sasa?"

"Sina usingizi kabisa kaka, kila nikifikiria mambo yaliyotokea leo nakosa amani. Sijui David yuko wapi, yuko salama au laa!" Alijibu Tesha kisha akanywa glasi moja ya bia iliyokuwa mezani.

Godfrey alimtazama mdogo wake usoni kwa masikitiko makubwa akaona kabisa ni kweli suala la David lilikuwa likimtesa si kidogo. Alikumbuka hata yeye pia anapitia katika hali kama hiyo tangu siku alipompoteza Dayana katika mazingira ya ajabu sana.
Hakuna aliyejua kuwa usiku huu Dayana na David wako pamoja ndani ya bonde moja la ajabu katika kisiwa alichojichimbia Magnus baada ya kufukuzwa ISRA.

"Tesha.."

"Nambie bro"

"Unampenda?"

"Na..nani?"

"I mean David, do you love him?"
Aliuliza Godfrey huku akimtazama mdogo wake kwa macho ya udadisi

Je, nini kitafuata?

David atafanya nini mbele ya Dayana?
Vipi kuhusu Felix kule Marekani?
Ni ipi itakuwa adhabu ya Sasha asubuhi?
ITAENDELEA...
 
SASHA MLINZI WA NAFSI
Sehemu ya............23
Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047

ILIPOISHIA...
"Tesha.."
"Nambie bro"
"Unampenda?"
"Na..nani?"
"I mean David, do you love him?"
Aliuliza Godfrey huku akimtazama mdogo wake kwa macho ya udadisi

SASA ENDELEA...
"You're not serious bro! Yaani mimi naongelea habari za kijana wa watu kutekwa wewe unaanza kuleta habari za mahusiano. Mimi kweli naweza ku-date na yule mwanaume kaka unanivunjia heshima jamani" Alisema Tesha.

"Naona kabisa unachokiongea na kilichopo moyoni mwako ni vitu viwili tofauti, Tesha kataa au kubali unampenda David, nililiona hilo tangu siku uliyoanza kutuma watu wamfuatilie. Sema unajua nini ni bora kumpenda David ambaye wewe unaona sio type yako kuliko kumpenda Felix mwanaume ambaye hakupendi kakukimbia na kwenda zake Marekani"

"Una mambo ya hovyo sana kaka, hivi wewe leo ni wa kuanza kunichagulia mwanaume wa ku-date naye, like serious? Mbona wewe sikuchagulii wanawake zake"

"Wewe ni mdogo wangu Tesha, ndugu tuliobaki tuko wawili tu mimi na wewe, lazima nikushauri nikiona unapita njia sio. Hata kama uta mind ila mimi sitoacha kukwambia Felix sio mwanaume. Mtu gani kwanza hataki kujulikana, hataki umuweke wazi mahusiano yenu, hataki mpige picha za pamoja, hataki kuongea na waandishi wa habari yani yupo yupo tu kama jambazi bana, asee!!"

"Hiyo ni lifestyle yake aliyochagua kwanini umuingilie, hapendi mambo ya social media. Mbona huongelei kuhusu pesa zake unazotumia kila siku"

"Lifestyle kitu gani mdogo wangu unapigwa hebu amka usingizini. haya mme-date miaka mingapi, siku ile nilikushauri umwambie angalau kama hataki mahusiano yenu yawe wazi basi akupeleke hata nyumbani kwao alikujibu nini?"
Aliuliza Godfrey, Tesha akawa kimya.

"Unajisahaurisha eti! Basi nakukumbusha alisema hana ndugu. Haya mtu gani huyo hana ndugu? Inaingia akilini kweli hiyo? Tesha mdogo wangu utakuja kudate na majini ohoo!" Alisema Godfrey kisha akachukua chupa ya bia aliyokuwa anatumia Tesha akaondoka nayo kurudi chumbani kwake.

"Sasa bia yangu unapeleka wapi?"

"Kalale bana, hii ni saa saba usiku. Kama wewe unamuwaza David hata mimi namuwaza Dayana" Alisema Godfrey huku akifunga mlango wa chumba chake.

"Huna lolote, unajishaua tu hapo" Tesha alijisemea mwenyewe kwa sauti ya chini. Akainuka kuelekea chumbani kwake kulala. Kabla hajafuata korido inayoelekea ulipo mlango wa chumba chake Tesha aliinua macho kutazama juu ukutani mahali ilipokuwepo picha ya Felix akasimama kwa sekunde kadhaa kuitazama.

"Eti hana ndugu, ila kaka ni kama kaongea ukweli flani hivi" Alisema Tesha kisha akaondoka zake, kwa kiasi maneno ya kaka yake yalimuingia.
[emoji294][emoji294][emoji294]

Upande wa pili nyumbani kwa afisa upelelezi wa jeshi la polisi Brandina naye alikuwa bado hajalala. Huyu ni mmoja kati ya askari waliokuwa wakiifuatilia kwa siri kesi ya utekajinyara ulioanza miaka kadhaa iliyopita.

Tayari kuna jambo jipya Brandina alikuwa amelipata katika harakati zake za upelelezi. Ni kuhusu picha ya Felix aliyoiona nyumbani kwa mwadada mrembo na maarufu nchini Tanzania Tesha. Picha hii ndiyo iliyokuwa ikimnyima usingizi Brandina akawa macho mpaka mda huu.

Mara ghafula alisikia mlango wa nyumba yake unagongwa kwa nguvu. Brandina alitahamaki akatazama saa yake ya mkononi akaoni ni saa saba na nusu za usiku. Haraka alifungua droo ya meza kubwa iliyokuwa mbele yake kulikuwa na bastola akaichukua kisha akatoka hadi sebuleni akaelekea mlangoni.
Mlango ulikuwa bado unagongwa kwa nguvu sana.

"Nani?"Brandina akauliza

"Aah! We mwanamke, uniite mwenyewe alafu bado unauliza nani" Sauti ya kiume ilisikika kutoka nje ya nyumba.

"Mmh! Umewahi sana, sijategemea kama ungefika haraka kiasi hiki" alisema Brandina huku akifungua mlango. Akaingia mwanaume mmoja mnene na mrefu aliyevaa koti kubwa jeusi, mkononi alishika tochi yenye mwanga mkali pamoja na begi dogo jeusi.

"Kwa hiyo umekuja kwa mguu?"

"Ndiyo gari yangu haiwaki kabisa, nikaona nisichelewe simu yako ilikuwa ya muhimu sana. Haya niambie kuna nini usiku huu Brandina?" Alieleza mwanaume huyo na mwisho akauliza swali.

"Umekuja na ile CD ya CCTV kamera"

"Kama kawaida, nimeleta kila kitu ulichoniagiza Inspekta"

"Haya twende" Alisema Brandina, kisha akaongozana na yule mwanaume ambaye yeye pia ni afisa upelelezi wa jeshi la polisi anayeshirikiana na Brandina kuifuatilia kesi hii ya utekaji, anaitwa Inspekta Masoud.

Waliongozana na kuingia kwenye kile chumba alichokuwa Brandina awali.

"Woow! Uko Smart sana Inspekta Brandina, kumbe hadi nyumbani unaofisi pia" Alisema Inspekta Masoud huku akitazama maadhari ya chumba kile.

"Unafikiri kuitwa mfanyakazi bora huwa inakuja kirahisi rahisi tu, kazi inakuwa imefanyika kweli, naomba hiyo CD"

"Eeh! Hata mimi naona hakuna kulala, CD hii hapa"

Brandina aliipokea CD Kutoka kwa Masoud kisha akaiweka kwenye kompyuta yake ndogo, akaicheza video iliyokuwa ndani ya CD hiyo.

Ilikuwa ni video iliyerekodiwa na kamera za CCTV nje ya Supermarket moja kubwa jijini Dar es salaam, ilikuwa ni usiku wa tarehe 21/07/2019 siku ya Jumapili, siku ambayo wanaume watatu walevi walitekwa na watu wasiojulikana nje ya Supermarket hiyo.
Kama kawaida watekaji walikuwa ni walewale wanaovaa helmet zenye vioo vya rangi nyekundu. Lakini kwa bahati nzuri mmoja kati ya wale watekaji alivua helmet yake kabla ya kuingia ndani ya gari bila kujua mahali hapo palikuwa na kamera za CCTV, zikamnasa.

Ilipofika wakati ule mtu huyo anavua helmet Brandina akasimamisha video hiyo.

"Unamuona huyu jamaa" Alisema Brandina

"Eeh! Nilishamuona kitambo sana, huyu tumemfuatilia tangu mwaka 2019 mpaka leo hatujajua ni nani, katoka wapi anafanya nini.." Alijibu Inspekta Masoud.

"Sasa mimi leo nimempata huyu mtu"

"Acha utani wako Brandina, unajua hili jambo sio la kutia masihara hata kidogo"

"Amini hivyo Inspekta Masoud, huyu mtu anaitwa Felix ni mpenzi wa Tesha huyu dada maarufu mwanamitindo"

"Tesha? Tesha huyu huyu super star?"

"Ndiyo"

"Acha hizo bwana, enhe! hebu nielekeze vizuri imekuwaje"

Brandina alieleza kila kitu tangu mwanzo alipopigiwa simu na Godfrey wakati wa tukio lingine la utekaji pale mgahawani kisha wakaenda hadi nyumbani kwa Tesha kuongea naye na baadae ndipo alipoiona picha ya Felix ikiwa ukutani.

"Kwa maelezo yao wanadai kwa sasa Felix yupo nchini Marekani, sina kingine nachokijua" Brandina Alimaliza kutoa maelezo.

" Sawa, kazi nzuri, hongera sana Brandina hii ni hatua moja kubwa mno. So tunafanyaje, huyu jamaa lazima tumpate"

"Kabisa, na sijui kwa nini Tesha hajaweka wazi mahusiano yao, nimekagua karibu picha zake zote kwenye mitandao ya kijamii Instagram Twitter Facebook kote sijamuona Felix"

"Kama anafanya hizi kazi hawezi kujiweka wazi mtandaoni" Alieleza Inspekta Masoud.

"Sahihi kabisa"

"Kwa hiyo tumvizie mpaka atakaporudi au tunafanyaje"

"Hatuna mda wa kupoteza Inspekta, huyu tunaanza kumsaka kimya kimya huko huko Marekani, tutafuatilia tangu alipotoka hapa Tanzania, alitumia ndege gani alifikia wapi akaenda wapi. Kila kitu lazima tukijue, inabidi tuombe msaada kitengo cha UJASUSI nchini, wao pia watawasiliana na shirika la Ujasusi nchini Marekani CIA, wote tuungane kuhakikisha tunampata Felix" Brandina alitoa wazo.

"Yes! Uko sahihi"

Naam, sasa nguvu kubwa inakwenda kutumika kumtia nguvuni Felix mtoto wa Magnus kutoka ISRA.
Je, watafanikiwa?
Vipi kuhusu hukumu ya Sasha kule ISRA?
Nini kinaendelea kati ya David na Dayana kule bondeni?

ITAENDELEA.....

Mtunzi: Saul David
WhatsApp: 0756862047.
 
Back
Top Bottom