Mlundilwa Jr
JF-Expert Member
- Dec 11, 2019
- 3,187
- 4,857
Nice
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Shukrani mamii[emoji120]Lucky93
miss Gf
kowaski
onlyalvira
Unique Flower
Vishu Mtata
Chakula Kibaya
Bangida
@Mwidele Makusu
dong yi
Shetta
Lightone
Valentina
Babu Fyee
Namba Moja AJAE
deecharity
Kelsea
julaibibi
Vina Dayot
@Upamecano
Stori tamu , sana go on go go NANASEHEMU YA SITA
Ndugu Padre alitoa ushirikiano wa kutosha, alitupa mwanga wa jinsi siasa za Tanzania zinafanyika, ingawa palikua na ule muonekano wa nje wa nchi yenye amani, lakini amani ilipatikana kwa kutoligusa tabaka Tawala, nilishajionea kwa vitendo kwani nimehusika kudeliver watu wengi kwa General ambao walikua na uhusiano wa moja kwa moja na siasa.
Maelezo yalitushibisha kwa kile tulichokikusudia, nilijua tu hatodhurika zaidi ya usafi wa hapa na pale wa viungo vyake vya mwili , kwa hiyo nilimfikisha anapohusika kwa sharti kua asije ongea kuhusu kile tulichoongea pale kwangu, kama nimempata leo ,nitampata tena hata akiweka milango ya dharura elfu kumi. Padre alinielewa na rasmi nikamuingiza kwenye mfumo wangu baada ya kunipatia majina kamili na mahali ambapo ninaweza wapata wahusika baadhi wanaopambania mgombea yule wa upinzani apite.
List ilikua ni ndefu, wapo hadi watu wa usalama ambao walikua wamechoka na utawala wa chama kimoja kwa mda mrefu, watu walihitaji mabadiliko lakini hapakua na mwenye ujasiri wa kumfunga paka kengele, kwahiyo wote walijificha nyuma ya pazia huku wakimsapoti mgombea yule wa upinzani wakiwa gizani. Nilichokuja kugundua ni kua ndugu Padre alitolewa kafara, na ile kofia yake ya dini alihisi hawezi kuguswa.
Nilikuja kufahamu kupitia Inno siku mbili baadae kua Padre amesharudishwa kwenye makazi yake ila mwendo ni kama umebadilika, nikawaza aina ya usafi waliomfanyia Padre wa watu , nikajikuta nasikitika tuuu. Watu wanaweza hisi hatuna huruma ila kuna namna ukishaingia kwa hizi kazi unapambana kufanikisha majukumu yako ambayo wakati mwingine yataleta ulemavu au kifo kwa yule aliekusudiwa, kwetu inakua ni siku tu nyingine ofisini.
Nilikua nimepata kwa kuanzia, nikaanza kuwasaka wale niliotajiwa na Padre mmoja mmoja kwa nyakati tofauti. Nilianzia kwa Jaji wa mahakama kuu, huyu aliingia kwenye mfumo wa mgombea kwa ahadi ya kupewa ujaji mkuu na mgombea baada ya kushinda. Kazi yake ilikua kuhakikisha kesi zote za mgombea pamoja na chama anazitolea hukumu kwa wakati sahihi na kwamba matokeo yanakua kwa upande wa chama. Sikufahamu alijiamini nini maana ni kama uhusika wake ulianza kujulikana mapema tu kwa namna alivyokua mwiba na kesi za chama Tawala. Nikaona si vibaya nikamtembelea bwana Jaji nipate vifungu kadhaa toka kwake.
Usiku wa saa nne na madakika kadhaa yalinikuta nyumbani kwa Jaji, huyu bwana alikua akiishi Tabata Kinyerezi, nyumba yake ilizungushiwa ukuta mrefu pamoja na nyaya za umeme. Kibao cha 'Kaa mbali ukuta huu unalindwa na Z.Z security hakikukosekana. Nilikua na zana zangu za kazi, umbali wa sentimeta chache kutoka ulipo ukuta palikua na mti mkubwa tu wa mwembe kwa ndani, niliparamia ule ukuta kwa tahadhari, nilizifika nyaya na kuzikata kwa kutumia kifaa maalumu, nikatandika blanket maalumu ambalo linazuia umeme kunifikia, niliruka na kuingia ndani kupitia ule mti wa mwembe, kwa mwendo wa paka nikamfikia mlinzi, sikua na haja ya kuongeza idadi ya dhambi kwa watu ambao hawajanikosea, nilimpa pigo moja takatifu mlinzi aliekua anasinzia akaanguka chini kama roba, nilimsaidia kumdaka ili anguko lake lisifanye kelele. Baada ya uchunguzi wa muda mfupi kua hapakua na mbwa wala myama mwingine hatarishi, nilijongea nyumba ya Jaji kwa tahadhari.
Dakika ishirini zilinitosha kufanya ziara kwenye vyumba vyote vya nyumba ya mheshimiwa Jaji...kwa tahadhari ileile nikabaini chumba anacholala mheshimiwa yeye na mkewe. Nilinyata na kumuamsha bwana Jaji, kwa tahadhari nikamuwekea kidole cha kuonesha anatakiwa akae kimya huku nikiwa nimemuelekezea mkewe bastola, sikutaka kuacha ushahidi ili hata bwana Jaji atakapopiga yowe baada ya mimi kuondoka ionekane ni uzee tu umemnyemelea hakuna kiumbe yeyote aliyeingia mle ndani.
Kwa taratibu tukaongozana yeye akiwa mbele mimi nyuma, moja kwa moja hadi chumba chake cha kusomea. Nikamwambia bwana Jaji karibu, samahani kwa kukujia bila appointment, na samahani kwa kukata nyaya yako juu ya ukuta, hakikisha unarekebisha pakishakucha wezi wasije kukuotea. Yule bwana alikua katika hamaki, nikamwambia hebu relax , ningekuja kukuua usingekua unapumua hadi sasa...
Nikamwambia lengo langu kua nataka kujua mpango wa chama chao jinsi gani wamejipanga kukitoa chama tawala madarakani. Yule bwana alihamaki, yaani mahangaiko yote yale kumbe ni kuhusu chama tawala, sijui alijua watu aliokula rushwa zao na akaenda kinyume nao walikua wamemfata, atajua mwenyewe....nilimwambia sina mda wa kupoteza aanze kuongea au nimrambe risasi.
Yule bwana akanieleza mipango yao na jinsi walivyojipanga, majukumu aliyopangiwa na idadi ya watu walioahidi kuwasaidia. Kwa kiasi fulani akawa ameniridhisha na majibu yake. Kwa sharti la kutoripoti polisi wala kuongea popote nikaahidi kutomsumbua tena yeye wala familia yake, ila nilimpa angalizo kua akijaribu kufungua mdomo wake hakuna atakaemlinda hata akiweka wanajeshi getini. Nikamwambia alale chini bila ya kutikisika, sio kwa mahangaiko yale niliyompa na kile kitambi, kwa namna ileile niliyoingia nikaitumia kuondoka mahala pale.
Kupitia Jaji nikawa nimepata kitu kipya, sio tu watu baki bali hata wanasiasa wengine toka chama Tawala ambao walikatwa wakati wa kinyang'anyiro cha mchujo kwa siri waliamua kusapoti chama cha upinzani kwa ahadi kua watapata teuzi mbalimbali baada ya wapinzani kupita. Niliona si hoja kumtembelea kiongozi mmoja wa chama tawala nikajifunze uzalendo kiasi .