Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #61
53.
Baada kushuhudia tukio hilo nilitupilia mbali wazo la kukuokoa bali niliamua nikupe mafunzo kama kawaida na uendelee kuwa chini ya uchunguzi maalum. Na ndio maana ulivyotoroka wakati ukiwa na miaka kumi na mbili nilikuachia uishi nje kwa muda wa mwaka mzima, nilifanya hivo ili kukujenga kiakili kuwa kuna maisha nje ya kambi. Na ulivyotoroka mwezi uliopita unadhani nini kilitokea, ulitoroka baada kuona moto umezuka. Moto niliuwasha mimi mwenyewe ili kukupa nafasi hiyo na yote hio ni kukutaka ulipe kisasi cha familia yako" Alimaliza kuongea na kumuangalia Alex usoni.
"Kwa we nani" Alex aliuliza, "we kweli kilaza kama mpaka saa hivi umeshindwa kunitambua, mimi ni General David kiongozi Marine Base 71" alijibu na kucheka kidogo. Alex alitoa macho kama mjusi aliebanwa na mlango maana katika watu ambao alikuwa anawachukia wakati akiwa kambini. "Ina maana mara zote wakati natoroka wewe ndio ulikuwa chanzo" Alex aliuliza kwa mshangao kisha akaendelea "na kule kambini umetokaje sasa".
"Sasa ikiwa nimeweza kukutorosha wewe, iweje mimi nishindwe kutoroka" aliongea General David, "baada ya kupata taarifa za kuthibitika kuwa umefanikiwa kukimbia nilitega bomu ofisini kwangu na kutoroka kabla ya kulipuka na kwasababu lilikuwa kali sana halikuacha ushahidi wowote ule hivyo wanaamini mimi nimekufa" alijibu.
*************************
"Tumepokea taarifa kutoka kwa watu wetu ambao wapo nchini Brazil kuwa Project 75 ameonekana Rio De Janeiro" aliingia Martin ofisini kwa bosi wake na kutoa taarifa. "Vipi umeshatuma vijana huko" aliuliza Mr Clinton, "ndio nimemtuma Project O" alijibu Martin. "Ataweza kutekeleza kazi huyo" aliuliza, "katika wote huyu ndie ana uwezo unaolingana na project 75 kwa hiyo usijali mkuu, mara hii mambo yatakuwa sawa kabisa" Martin alijibu huku akitabasamu. "Tuone wakati huu utatotokea wapi" Mr Clinton alijisemea moyoni. Baada kuwasilisha ripoti hiyo Martin alitoka ofisini, Mr Clinton alinyanyua simu na kumpigia secretary wake. Maggy alifika ofisini mara moja baada kukata simu, Mr Clinton alianza mambo yake yake yakipuuzi lakini alikutana na kibao kizito kilichomuangusha chini. Aliinuka kwa hasira na kutoa bastola lakini alikuwa kashachelewa maana alihisi kitu cha baridi kikigusa katika paji la uso, "ukileta ujinga nakufumua ubongo, kawafanyia malaya wenzako upuuzi kama huu mimi sie tumeelewana" alifoka kwa hasira Maggy. "Sawa nimekuelewa" Mr Clinton alijibu huku akimeza funda kubwa la mate maana alihisi kama kifo chake kina karibia. Baada hapo Maggy alirudisha bastola yake na kuondoka, Mr Clinton aliishia kula kwa macho tu huku akijilaumu kwanini amemuachia kirahisi namna ile.
Beach ya Copacabana ilikuwa imechangamka siku hiyo kuliko siku nyingine nyingi, kwa mbali alionekana kijana mmoja akiwa anatembea taratiu huku mkononi akiwa amebeba boksi dogo. Alionekana hayuko sehemu hiyo kupata upepo bali alikuwepo eneo hilo kikazi zaidi. Alikuwa akielekea sehemu aliokuwa amelala Alex ambae alikuwa akiota jua, alikuwa bize akisikiliza mziki lakini alianza kuhisi hali ambayo si ya kawaida. Mshale wa hatari uligonga kichwani mwake, alitoa earphone masikioni na kuanza kuangaza pande zote za pwani hiyo na ndipo akamuona yule mtu aliekuwa akija upande wake. Yule jamaa alifungua lile boksi na kutoa bastola ndogo iliofungwa kiwambo cha kuzuia sauti na kuanza kumshambulia Alex.
Baada kushuhudia tukio hilo nilitupilia mbali wazo la kukuokoa bali niliamua nikupe mafunzo kama kawaida na uendelee kuwa chini ya uchunguzi maalum. Na ndio maana ulivyotoroka wakati ukiwa na miaka kumi na mbili nilikuachia uishi nje kwa muda wa mwaka mzima, nilifanya hivo ili kukujenga kiakili kuwa kuna maisha nje ya kambi. Na ulivyotoroka mwezi uliopita unadhani nini kilitokea, ulitoroka baada kuona moto umezuka. Moto niliuwasha mimi mwenyewe ili kukupa nafasi hiyo na yote hio ni kukutaka ulipe kisasi cha familia yako" Alimaliza kuongea na kumuangalia Alex usoni.
"Kwa we nani" Alex aliuliza, "we kweli kilaza kama mpaka saa hivi umeshindwa kunitambua, mimi ni General David kiongozi Marine Base 71" alijibu na kucheka kidogo. Alex alitoa macho kama mjusi aliebanwa na mlango maana katika watu ambao alikuwa anawachukia wakati akiwa kambini. "Ina maana mara zote wakati natoroka wewe ndio ulikuwa chanzo" Alex aliuliza kwa mshangao kisha akaendelea "na kule kambini umetokaje sasa".
"Sasa ikiwa nimeweza kukutorosha wewe, iweje mimi nishindwe kutoroka" aliongea General David, "baada ya kupata taarifa za kuthibitika kuwa umefanikiwa kukimbia nilitega bomu ofisini kwangu na kutoroka kabla ya kulipuka na kwasababu lilikuwa kali sana halikuacha ushahidi wowote ule hivyo wanaamini mimi nimekufa" alijibu.
*************************
"Tumepokea taarifa kutoka kwa watu wetu ambao wapo nchini Brazil kuwa Project 75 ameonekana Rio De Janeiro" aliingia Martin ofisini kwa bosi wake na kutoa taarifa. "Vipi umeshatuma vijana huko" aliuliza Mr Clinton, "ndio nimemtuma Project O" alijibu Martin. "Ataweza kutekeleza kazi huyo" aliuliza, "katika wote huyu ndie ana uwezo unaolingana na project 75 kwa hiyo usijali mkuu, mara hii mambo yatakuwa sawa kabisa" Martin alijibu huku akitabasamu. "Tuone wakati huu utatotokea wapi" Mr Clinton alijisemea moyoni. Baada kuwasilisha ripoti hiyo Martin alitoka ofisini, Mr Clinton alinyanyua simu na kumpigia secretary wake. Maggy alifika ofisini mara moja baada kukata simu, Mr Clinton alianza mambo yake yake yakipuuzi lakini alikutana na kibao kizito kilichomuangusha chini. Aliinuka kwa hasira na kutoa bastola lakini alikuwa kashachelewa maana alihisi kitu cha baridi kikigusa katika paji la uso, "ukileta ujinga nakufumua ubongo, kawafanyia malaya wenzako upuuzi kama huu mimi sie tumeelewana" alifoka kwa hasira Maggy. "Sawa nimekuelewa" Mr Clinton alijibu huku akimeza funda kubwa la mate maana alihisi kama kifo chake kina karibia. Baada hapo Maggy alirudisha bastola yake na kuondoka, Mr Clinton aliishia kula kwa macho tu huku akijilaumu kwanini amemuachia kirahisi namna ile.
Beach ya Copacabana ilikuwa imechangamka siku hiyo kuliko siku nyingine nyingi, kwa mbali alionekana kijana mmoja akiwa anatembea taratiu huku mkononi akiwa amebeba boksi dogo. Alionekana hayuko sehemu hiyo kupata upepo bali alikuwepo eneo hilo kikazi zaidi. Alikuwa akielekea sehemu aliokuwa amelala Alex ambae alikuwa akiota jua, alikuwa bize akisikiliza mziki lakini alianza kuhisi hali ambayo si ya kawaida. Mshale wa hatari uligonga kichwani mwake, alitoa earphone masikioni na kuanza kuangaza pande zote za pwani hiyo na ndipo akamuona yule mtu aliekuwa akija upande wake. Yule jamaa alifungua lile boksi na kutoa bastola ndogo iliofungwa kiwambo cha kuzuia sauti na kuanza kumshambulia Alex.