Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 31
SURA YA TATU
Ile Palee, Nchi Wahaya
ulifika nchi ya Wahaya bila kutegemea. Mimi binafsi nilikuwa nimechoka kwa mwendo wa muda mrefu, kulala sehemu za ajabuajabu na
kula chochote kilichoweza kulika, jioni hiyo nilikuwa nikitembea kwa kujivutavuta, kama mzigo. Tulikuwa tukishuka toka juu ya kilima tulichopanda mchana wa jua kali, niliposikia ukelele wa furaha toka kwa mmoja wa watu tuliokuwa nao. Kelele hizo zilipokelewa na watu wengine zikifuatiwa na vicheko vya furaha.
Nilipoinua uso wangu kutazama huko wanakotazama wengine nilipigwa na butwaa. Takriban dunia nzima mbele ya macho yetu iligeuka kuwa uwanda mkubwa, mweupe unaomeremeta hadi upeo wangu kuona. Sikuelewa ninachokitazama hadi pale babu aliponishika bega na kuniambia, “Tumefika!” huku akitabasamu.
Sikumwelewa, “Tumefika wapi? Na kile nini
kinachomeremeta kiasi kile?” nilimuuliza.
“Yale ni maji. Lile ni ziwa Lweru, ambalo siku hizi nasikia linaitwa Victoria. Tumefika salama mwisho wa safari yetu. Ile pale nchi ya Wahaya.”
Ziwa! Ndio kwanza nikaelewa kile ambacho nimekuwa
nikikisikia juu ya maziwa na bahari. Katika safari yetu hiyo ndefu nilipata kuiona mito mingi, mikubwa, na kuivuka kwa mitumbwi. Kamwe sikupata kufikiria kuwa ziwa lingeweza kuwa kubwa na lenye maji mengi kiasi hiki! Niliduwaa kwa muda mrefu, nikiwa nimelitumbulia macho ziwa hilo kwa shahuku. Nilihisi uchovu ulikuwa umeniteka mwili mzima ukitoweka na nguvu mpya na ari mpya kuchukua nafasi yake katika nafasi yangu.
Msafara wetu huo ulioanza kwa upweke mkubwa kati yangu na babu, sasa ulikuwa wa kundi la watu wasiopungua kumi na wawili. Watu hao, Mwarabu mmoja mwenye ndevu nyingi nyeupe na upara kichwani, ambaye baadaye tuliambiwa kuwa anaitwa Sheikh Seif, alitajwa kama mfanyabiashara wa chumvi na pembe za ndovu. Mtu mmoja kati yao, mrefu sana, mweusi sana, tuliambiwa kuwa ni Mnubi toka Uganda na kwamba alikuwa msaidizi wake mkubwa kibiashara. Wengine, mmoja, akiwa Muha aliyelowea Kagera, wawili Wamanyema wa Kongo na waliobaki wakiwa Wanyamwezi wa Tabora walikuwa wapagazi wake, walioajiriwa kwa safari hiyo pekee.
Tulikutana na watu hao katika kijiji kidogo kilichoitwa Kakonko. Siku hiyo babu alishauri tutafute eneo lenye watu ili tuombe msaada wa chakula cha binadamu zaidi, baada ya kukinaishwa na matunda na nyama za kuchomwa ambazo tulizila bila ugali wala chumvi. Mzee mmoja kijijini hapo alitudokeza juu ya kuwepo kwa wageni wengine kama sisi, waliokuwa wakitokea kwenye biashara ya kubadilishana nguo na shanga kwa chumvi za magadi iliyokuwa ikipatikana katika mabwawa ya maji huko Uvinza, Kigoma.
Tulitambulishwa na watu hao na mara moja wale Wahaya wakaanza kumtania babu kwa kumwita ‘mtani’.
SURA YA TATU
Ile Palee, Nchi Wahaya
ulifika nchi ya Wahaya bila kutegemea. Mimi binafsi nilikuwa nimechoka kwa mwendo wa muda mrefu, kulala sehemu za ajabuajabu na
kula chochote kilichoweza kulika, jioni hiyo nilikuwa nikitembea kwa kujivutavuta, kama mzigo. Tulikuwa tukishuka toka juu ya kilima tulichopanda mchana wa jua kali, niliposikia ukelele wa furaha toka kwa mmoja wa watu tuliokuwa nao. Kelele hizo zilipokelewa na watu wengine zikifuatiwa na vicheko vya furaha.
Nilipoinua uso wangu kutazama huko wanakotazama wengine nilipigwa na butwaa. Takriban dunia nzima mbele ya macho yetu iligeuka kuwa uwanda mkubwa, mweupe unaomeremeta hadi upeo wangu kuona. Sikuelewa ninachokitazama hadi pale babu aliponishika bega na kuniambia, “Tumefika!” huku akitabasamu.
Sikumwelewa, “Tumefika wapi? Na kile nini
kinachomeremeta kiasi kile?” nilimuuliza.
“Yale ni maji. Lile ni ziwa Lweru, ambalo siku hizi nasikia linaitwa Victoria. Tumefika salama mwisho wa safari yetu. Ile pale nchi ya Wahaya.”
Ziwa! Ndio kwanza nikaelewa kile ambacho nimekuwa
nikikisikia juu ya maziwa na bahari. Katika safari yetu hiyo ndefu nilipata kuiona mito mingi, mikubwa, na kuivuka kwa mitumbwi. Kamwe sikupata kufikiria kuwa ziwa lingeweza kuwa kubwa na lenye maji mengi kiasi hiki! Niliduwaa kwa muda mrefu, nikiwa nimelitumbulia macho ziwa hilo kwa shahuku. Nilihisi uchovu ulikuwa umeniteka mwili mzima ukitoweka na nguvu mpya na ari mpya kuchukua nafasi yake katika nafasi yangu.
Msafara wetu huo ulioanza kwa upweke mkubwa kati yangu na babu, sasa ulikuwa wa kundi la watu wasiopungua kumi na wawili. Watu hao, Mwarabu mmoja mwenye ndevu nyingi nyeupe na upara kichwani, ambaye baadaye tuliambiwa kuwa anaitwa Sheikh Seif, alitajwa kama mfanyabiashara wa chumvi na pembe za ndovu. Mtu mmoja kati yao, mrefu sana, mweusi sana, tuliambiwa kuwa ni Mnubi toka Uganda na kwamba alikuwa msaidizi wake mkubwa kibiashara. Wengine, mmoja, akiwa Muha aliyelowea Kagera, wawili Wamanyema wa Kongo na waliobaki wakiwa Wanyamwezi wa Tabora walikuwa wapagazi wake, walioajiriwa kwa safari hiyo pekee.
Tulikutana na watu hao katika kijiji kidogo kilichoitwa Kakonko. Siku hiyo babu alishauri tutafute eneo lenye watu ili tuombe msaada wa chakula cha binadamu zaidi, baada ya kukinaishwa na matunda na nyama za kuchomwa ambazo tulizila bila ugali wala chumvi. Mzee mmoja kijijini hapo alitudokeza juu ya kuwepo kwa wageni wengine kama sisi, waliokuwa wakitokea kwenye biashara ya kubadilishana nguo na shanga kwa chumvi za magadi iliyokuwa ikipatikana katika mabwawa ya maji huko Uvinza, Kigoma.
Tulitambulishwa na watu hao na mara moja wale Wahaya wakaanza kumtania babu kwa kumwita ‘mtani’.