FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #61
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 40
“Hivyo kitu ambacho kimeniweka mimi hapa ni kwamba nahitaji jambo hili lipatiwe majibu, nataka mtu huyu achunguzwe kwa umakini bila kuumizwa au kuvamiwa kutekwa. Nataka taarifa zake zote, nahitaji historia yake sahihi na kama kuna ndugu zake basi wapatikane, nahitaji kila taarifa juu ya ukuaji wake na maisha yake ya nyuma na nijue hizi habari yeye alikuwa anazipatia wapi. Baada ya hapo nitafanya maamuzi ya nini cha kufanya juu yake, Aaliyah nakupa masaa arobaini na nane, utajua namna ya kufanya na vijana wako ila nayahitaji hayo majibu kwa huo wakati ambao nimeutaja hapo” Alimaliza bila kuruhusu swali lolote kutoka kwa hao vijana wake, alitoka humo ndani. Hakuonekana kuwa na amani, jambo hilo lilimvuruga pakubwa na kumpa hofu kwa wakati mmoja, lilikuwa jambo zito kutokana na aina ya mtu ambaye walikuwa wanaingia naye kwenye ulingo huo. Mwanaume ambaye aliijua sheria vilivyo nayo ikamtii, alikuwa ana uwezo wa kufanya lolote kwenye sheria na kila kitu kinaenda atakavyo yeye, ungemwambia nini JACK kuhusu sheria? Mkurugenzi hakujali kama mwanaume huyo alikuwa sahihi au hakuwa sahihi ila jambo hilo kufanyika hatari yake ilikuwa ni kubwa kuliko faida ndiyo maana alihitaji kulizuia haraka kabla halijatokea.
Aalyah alisimama na kusogea mbele, ni yeye ambeye alikuwa kiongozi wa wanaume hao. RIGHT HAND, ndilo jina ambalo walikuwa wanalitumia ikiwa na maana ya mkono wa Kulia, kwanini? Kwa sababu waliamini wao ndiyo ilikuwa nguzo mhimu kwenye shirika hilo, wao ndio walikuwa kama mkono wa kulia wa mkurugenzi na kamwe hawakuwahi kumuangusha na ndiyo sababu haswa aliamua kuwapa kesi hiyo akiwa na imani kwamba walikuwa wanaweza kuishughulikia kwa usahihi kuliko mtu yeyote yule.
Wote walibaki kimya kila mmoja akiwa anamtazama mwenzake kwa vituo, kilicho washangaza sio kusikia kuhusu kesi hiyo hapana, walikuwa wanaijua kesi hiyo kwa muda mrefu na ni kesi ambayo walijua kwamba ni serikali iliifuta makusudi kwa sababu ambazo hazikuwahi kuwekwa wazi ila wao kama wapelelezi walijua kabisa mambo hayakuwa sawa ila haikuwa kazi yao hivyo nao wakaachana nayo. Jambo ambalo hata wao liliwashtua ni aina ya mtu ambaye aliamua kulivalia njuga swala hiyo, mwanasheria ambaye hata wao walikuwa mashabiki zake wakubwa kwa namna alivyojua kucheza na kalamu yake pamoja na ubongo wake kwa wakati mmoja.
Hawakuijua sababu ya mwanasheria huyo kujiingiza kwenye sakati zito na baya kama hilo ambalo ni lazima lingeisha vibaya kwa upande wake yeye;
“Mimi nilijua tu ipo siku hili jambo litafufuta. Moja kati ya makosa makubwa ambayo huwa yanafanyika serikalini ni kufanya kila kitu kimazoea, viongozi wakubwa huwa wanahisi kwamba watu wote ndani ya taifa hili akili yao ni moja. Sio kila mtu ni mjinga ila kuna watu huwa wanainamisha vichwa kama hawapo na muda wao sahihi unapofika basi wanaweza kukushangaza kwa mengi na ndiyo haya ambayo yanaanza kutokea. Kosa lililofanywa ni pale ambapo wahusika walilizima jambo hili kiholela wakiamini kwamba halitakuwa na madhara yoyote yale ila walipaswa kuwa smart zaidi ya hapa” Jumapili Magawa, moja kati ya mmoja wa kikosi hicho aliongea kwa masikitiko kuhusu jambo hilo.
“Kuna kitu unahisi labda Jumapili?”
“Ndiyo, Kwenye ile miaka mitano ambayo imepita komando mmoja tena mwenye mafunzo ya hali ya juu hakupatikana eneo la tukio zaidi ya damu yake huku watu ambao walitumwa nao miili yao haikukutwa, nyie hamhisi kwamba kuna kitu hakipo sawa hapo? Mtu huyo licha ya kutafutwa lakini bado hakukuwa na dalili zozote za uwepo wake hapa duniani jambo ambalo lilifanya vyombo vya dola kupoteza matumaini ya kumpata na kuamua kuachana na habari yake ukizingatia wakati huo huo mtu huyu anapotea kulikuwa na habari kwamba aligundulika kuwa mtoto wa yule mwanasayansi wa zamani ambaye naye alipotea kwenye mazingira ya kutatanisha kwa kudaiwa kupelekwa Israeli”
“Wakati huo huo anakuja kugundulika mchungaji akiwa anaingia katikati ya haya, halafu baadae baada ya komando huyo kupotea anatokea mwanasheria nguli anadai kwamba ana ushahidi wa mambo yote hayo ambayo yalitokea tena akiwa anajiamini kabisa na mtu yule hajawahi kuongea jambo ambalo hana uhakika nalo ndiyo sababu hajawahi kupoteza kesi hata moja kwenye maisha yake na nina uhakika serikali wakikubali kwenda naye mahakamani basi lazima serikali ipoteze”
“Maana yako ni ipi hasa?”
“Nina uhakika huu unaweza kuwa mpango wa yule komando ambaye alipotea kwa sababu ndiye alikuwa na taarifa zote hivyo huenda ndiye alimpatia huyu mtu taarifa hizo, uzembe mkubwa ulifanyika kuruhusu yule mchungaji kuuawa kwa sababu angeturahisishia jambo hili. Na kama haipo hivyo basi huyu mtu atakuwa na taarifa za namna ya kumpata huyo komando” maelezo yake yaliwafungua wenzake kiasi fulani kiasi kwamba kila mtu akawa anawaza mara mbili mbili.
Wanaume wawili walikuwa wametulia wakiwa wanasikiliza kwa umakini mazungumzo ya wenzao, wanaume hao walikuwa ni mmoja kutoka ardhi ya watu wajivuni, mhaya David Mbatina pamoja na mkurya mmoja Ruben Magesa jitu la miraba minne ambalo lilikuwa linajiamini kwa kiasi kikubwa. Mjivuni David Mbatina alisogea mbele na kujikohoza kidogo ili kuwapa ishara wenzake kwamba alikuwa na jambo.
“Kwa sasa kuna jambo la mhimu hapa katikati ambalo linaweza kutupatia msaada mkubwa, kwenye moja kati ya habari za ajabu ambazo huyu mwanasheria aliwahi kuzitoa ni kuvujisha siri kwamba anaishi kwenye sura ya mtu mwingine. Habari hii ilionekana kama kiki tu na maneno ya kuzushwa ila ndani yake huenda ina maaan kubwa, nadhani hapa ndipo tunaweza kuanzia kufanyia uchunguzi ili tujue kama anaishi kwenye sura ya mtu mwingine kweli, ni sura ya na nani na kwanini afanye hivyo? Jibu likiwa ni kweli basi tuna asilimia themanini mpaka sasa za kuupata ukweli wa jambo hili haraka na mapema” jambo hilo lilionekana kuwa la maana hivyo walikubaliana kuingia kazini na asubuhi hiyo hiyo alitakiwa Aaliyah kwenye kwenye ofisi ya mwanasheria huyo ili kuteta naye jambo kama mwanzo wa kufanya uchunguzi wao ambao walitakiwa kuukamilisha ndani ya masaa arobaini na manane tu.
JACK THE LAWYER asubuhi alikuwa ndani ya ofisi yake, alikuwa ametulia kwa ajili ya kuweza kuianza siku hiyo mpya. Nje ya jengo hilo la ghorofa ambalo ndipo ilikuwepo ofisi yake kulikuwa na kelele nyingi za watu wakiwa wanamshangilia, watu hao walikuwa wanalitaja jina lake kwa msisitizo huku wakilinadi na kumuona kama shujaa wa taifa. Alikuwa amezisikia kelele hizo tangu anafika ila hakutaka kwenda, sio kwa sababu aliwapuuza wananchi hao, lahasha! Bali kwa sababu aliupa muda nafasi na angewaonyesha na kuja kufanya mahojiano yake baada ya serikali kutoa jibu la kueleweka, hakuwa mtu wa kuyafanya mambo kwa haraka.
Aliingia katibu muhtasi wake, mwanamke mrembo ambaye kwa mwonekano wake miaka ilikuwa inaelekea thelathini.
“Bosi kuna mtu hapa anadai kwamba ni askari anahitaji kuonana na wewe, nimempa taarifa kwamba hauna muda saivi ila kasisitiza hivyo nimekuja kukuuliza kama utaongea naye au nimtoe aondoke” sauti hiyo ilimfanya aache kila alichokuwa anakifanya, alisimama na kusogea pembezoni mwa dirisha ambalo lilikuwa na vioo vilivyo mfanya auone mji kwa usahihi.
“Mwambie aingie” alijibu akiwa hajajisumbua hata kuangalia nyuma. Mlango ulifunguliwa, aliye ingia, alikuwa ni Aaliyah Beka.
“Naitwa Warda Abdul, ni askari mpelelezi kutoka ndani ya ofisi ya afisa upelelezi wa mkoa; Naomba muda wako kidogo niweze kukuuliza maswali kadhaa” Aaliyah aliongea kwa kujiamini kwa sababu hakuwa na papara na kazi yake, Jack bado alikuwa amempa mgongo lakini hakuchukua muda, aliogeuka akiwa na tabasamu usoni kwake huku akiwa anamwangalia kwa umakini mwanamke ambaye alikuwa mbele yake akiwa amezifunika vyema nywele zake kiasi kwamba yale maadili yaliendana na jina lake ambalo alilitambulisha hapo.
“Nambie kilicho kuleta kwenye ofisi yangu asubuhi yote hii Aaliyah Beka” Alibaki ameduwaa kiasi kwamba alilegea na kuyumba ila alijikaza kukaa vizuri. Alibaki ametweta kwenye uso wake asielewe lile jambo ambalo lilikuwa linaendelea pale wakati ule, maisha yake yalikuwa ya usiri mkubwa lakini mwanaume huyo alikuwa akilifahamu jina lake. Sasa kivipi? JACK alisogea kwenye kiti chake na kuketi huku akimuonyesha ishara mwanamke huyo ambaye aliishiwa pozi naye aketi.
“Nadhani umenielewa vibaya, umenitajia jina ambalo sio langu na sijui ni mtu yupi ambaye unamaanisha” Aaliyaha alijitetea.
UKURASA WA 40 unafika mwisho.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 40
“Hivyo kitu ambacho kimeniweka mimi hapa ni kwamba nahitaji jambo hili lipatiwe majibu, nataka mtu huyu achunguzwe kwa umakini bila kuumizwa au kuvamiwa kutekwa. Nataka taarifa zake zote, nahitaji historia yake sahihi na kama kuna ndugu zake basi wapatikane, nahitaji kila taarifa juu ya ukuaji wake na maisha yake ya nyuma na nijue hizi habari yeye alikuwa anazipatia wapi. Baada ya hapo nitafanya maamuzi ya nini cha kufanya juu yake, Aaliyah nakupa masaa arobaini na nane, utajua namna ya kufanya na vijana wako ila nayahitaji hayo majibu kwa huo wakati ambao nimeutaja hapo” Alimaliza bila kuruhusu swali lolote kutoka kwa hao vijana wake, alitoka humo ndani. Hakuonekana kuwa na amani, jambo hilo lilimvuruga pakubwa na kumpa hofu kwa wakati mmoja, lilikuwa jambo zito kutokana na aina ya mtu ambaye walikuwa wanaingia naye kwenye ulingo huo. Mwanaume ambaye aliijua sheria vilivyo nayo ikamtii, alikuwa ana uwezo wa kufanya lolote kwenye sheria na kila kitu kinaenda atakavyo yeye, ungemwambia nini JACK kuhusu sheria? Mkurugenzi hakujali kama mwanaume huyo alikuwa sahihi au hakuwa sahihi ila jambo hilo kufanyika hatari yake ilikuwa ni kubwa kuliko faida ndiyo maana alihitaji kulizuia haraka kabla halijatokea.
Aalyah alisimama na kusogea mbele, ni yeye ambeye alikuwa kiongozi wa wanaume hao. RIGHT HAND, ndilo jina ambalo walikuwa wanalitumia ikiwa na maana ya mkono wa Kulia, kwanini? Kwa sababu waliamini wao ndiyo ilikuwa nguzo mhimu kwenye shirika hilo, wao ndio walikuwa kama mkono wa kulia wa mkurugenzi na kamwe hawakuwahi kumuangusha na ndiyo sababu haswa aliamua kuwapa kesi hiyo akiwa na imani kwamba walikuwa wanaweza kuishughulikia kwa usahihi kuliko mtu yeyote yule.
Wote walibaki kimya kila mmoja akiwa anamtazama mwenzake kwa vituo, kilicho washangaza sio kusikia kuhusu kesi hiyo hapana, walikuwa wanaijua kesi hiyo kwa muda mrefu na ni kesi ambayo walijua kwamba ni serikali iliifuta makusudi kwa sababu ambazo hazikuwahi kuwekwa wazi ila wao kama wapelelezi walijua kabisa mambo hayakuwa sawa ila haikuwa kazi yao hivyo nao wakaachana nayo. Jambo ambalo hata wao liliwashtua ni aina ya mtu ambaye aliamua kulivalia njuga swala hiyo, mwanasheria ambaye hata wao walikuwa mashabiki zake wakubwa kwa namna alivyojua kucheza na kalamu yake pamoja na ubongo wake kwa wakati mmoja.
Hawakuijua sababu ya mwanasheria huyo kujiingiza kwenye sakati zito na baya kama hilo ambalo ni lazima lingeisha vibaya kwa upande wake yeye;
“Mimi nilijua tu ipo siku hili jambo litafufuta. Moja kati ya makosa makubwa ambayo huwa yanafanyika serikalini ni kufanya kila kitu kimazoea, viongozi wakubwa huwa wanahisi kwamba watu wote ndani ya taifa hili akili yao ni moja. Sio kila mtu ni mjinga ila kuna watu huwa wanainamisha vichwa kama hawapo na muda wao sahihi unapofika basi wanaweza kukushangaza kwa mengi na ndiyo haya ambayo yanaanza kutokea. Kosa lililofanywa ni pale ambapo wahusika walilizima jambo hili kiholela wakiamini kwamba halitakuwa na madhara yoyote yale ila walipaswa kuwa smart zaidi ya hapa” Jumapili Magawa, moja kati ya mmoja wa kikosi hicho aliongea kwa masikitiko kuhusu jambo hilo.
“Kuna kitu unahisi labda Jumapili?”
“Ndiyo, Kwenye ile miaka mitano ambayo imepita komando mmoja tena mwenye mafunzo ya hali ya juu hakupatikana eneo la tukio zaidi ya damu yake huku watu ambao walitumwa nao miili yao haikukutwa, nyie hamhisi kwamba kuna kitu hakipo sawa hapo? Mtu huyo licha ya kutafutwa lakini bado hakukuwa na dalili zozote za uwepo wake hapa duniani jambo ambalo lilifanya vyombo vya dola kupoteza matumaini ya kumpata na kuamua kuachana na habari yake ukizingatia wakati huo huo mtu huyu anapotea kulikuwa na habari kwamba aligundulika kuwa mtoto wa yule mwanasayansi wa zamani ambaye naye alipotea kwenye mazingira ya kutatanisha kwa kudaiwa kupelekwa Israeli”
“Wakati huo huo anakuja kugundulika mchungaji akiwa anaingia katikati ya haya, halafu baadae baada ya komando huyo kupotea anatokea mwanasheria nguli anadai kwamba ana ushahidi wa mambo yote hayo ambayo yalitokea tena akiwa anajiamini kabisa na mtu yule hajawahi kuongea jambo ambalo hana uhakika nalo ndiyo sababu hajawahi kupoteza kesi hata moja kwenye maisha yake na nina uhakika serikali wakikubali kwenda naye mahakamani basi lazima serikali ipoteze”
“Maana yako ni ipi hasa?”
“Nina uhakika huu unaweza kuwa mpango wa yule komando ambaye alipotea kwa sababu ndiye alikuwa na taarifa zote hivyo huenda ndiye alimpatia huyu mtu taarifa hizo, uzembe mkubwa ulifanyika kuruhusu yule mchungaji kuuawa kwa sababu angeturahisishia jambo hili. Na kama haipo hivyo basi huyu mtu atakuwa na taarifa za namna ya kumpata huyo komando” maelezo yake yaliwafungua wenzake kiasi fulani kiasi kwamba kila mtu akawa anawaza mara mbili mbili.
Wanaume wawili walikuwa wametulia wakiwa wanasikiliza kwa umakini mazungumzo ya wenzao, wanaume hao walikuwa ni mmoja kutoka ardhi ya watu wajivuni, mhaya David Mbatina pamoja na mkurya mmoja Ruben Magesa jitu la miraba minne ambalo lilikuwa linajiamini kwa kiasi kikubwa. Mjivuni David Mbatina alisogea mbele na kujikohoza kidogo ili kuwapa ishara wenzake kwamba alikuwa na jambo.
“Kwa sasa kuna jambo la mhimu hapa katikati ambalo linaweza kutupatia msaada mkubwa, kwenye moja kati ya habari za ajabu ambazo huyu mwanasheria aliwahi kuzitoa ni kuvujisha siri kwamba anaishi kwenye sura ya mtu mwingine. Habari hii ilionekana kama kiki tu na maneno ya kuzushwa ila ndani yake huenda ina maaan kubwa, nadhani hapa ndipo tunaweza kuanzia kufanyia uchunguzi ili tujue kama anaishi kwenye sura ya mtu mwingine kweli, ni sura ya na nani na kwanini afanye hivyo? Jibu likiwa ni kweli basi tuna asilimia themanini mpaka sasa za kuupata ukweli wa jambo hili haraka na mapema” jambo hilo lilionekana kuwa la maana hivyo walikubaliana kuingia kazini na asubuhi hiyo hiyo alitakiwa Aaliyah kwenye kwenye ofisi ya mwanasheria huyo ili kuteta naye jambo kama mwanzo wa kufanya uchunguzi wao ambao walitakiwa kuukamilisha ndani ya masaa arobaini na manane tu.
JACK THE LAWYER asubuhi alikuwa ndani ya ofisi yake, alikuwa ametulia kwa ajili ya kuweza kuianza siku hiyo mpya. Nje ya jengo hilo la ghorofa ambalo ndipo ilikuwepo ofisi yake kulikuwa na kelele nyingi za watu wakiwa wanamshangilia, watu hao walikuwa wanalitaja jina lake kwa msisitizo huku wakilinadi na kumuona kama shujaa wa taifa. Alikuwa amezisikia kelele hizo tangu anafika ila hakutaka kwenda, sio kwa sababu aliwapuuza wananchi hao, lahasha! Bali kwa sababu aliupa muda nafasi na angewaonyesha na kuja kufanya mahojiano yake baada ya serikali kutoa jibu la kueleweka, hakuwa mtu wa kuyafanya mambo kwa haraka.
Aliingia katibu muhtasi wake, mwanamke mrembo ambaye kwa mwonekano wake miaka ilikuwa inaelekea thelathini.
“Bosi kuna mtu hapa anadai kwamba ni askari anahitaji kuonana na wewe, nimempa taarifa kwamba hauna muda saivi ila kasisitiza hivyo nimekuja kukuuliza kama utaongea naye au nimtoe aondoke” sauti hiyo ilimfanya aache kila alichokuwa anakifanya, alisimama na kusogea pembezoni mwa dirisha ambalo lilikuwa na vioo vilivyo mfanya auone mji kwa usahihi.
“Mwambie aingie” alijibu akiwa hajajisumbua hata kuangalia nyuma. Mlango ulifunguliwa, aliye ingia, alikuwa ni Aaliyah Beka.
“Naitwa Warda Abdul, ni askari mpelelezi kutoka ndani ya ofisi ya afisa upelelezi wa mkoa; Naomba muda wako kidogo niweze kukuuliza maswali kadhaa” Aaliyah aliongea kwa kujiamini kwa sababu hakuwa na papara na kazi yake, Jack bado alikuwa amempa mgongo lakini hakuchukua muda, aliogeuka akiwa na tabasamu usoni kwake huku akiwa anamwangalia kwa umakini mwanamke ambaye alikuwa mbele yake akiwa amezifunika vyema nywele zake kiasi kwamba yale maadili yaliendana na jina lake ambalo alilitambulisha hapo.
“Nambie kilicho kuleta kwenye ofisi yangu asubuhi yote hii Aaliyah Beka” Alibaki ameduwaa kiasi kwamba alilegea na kuyumba ila alijikaza kukaa vizuri. Alibaki ametweta kwenye uso wake asielewe lile jambo ambalo lilikuwa linaendelea pale wakati ule, maisha yake yalikuwa ya usiri mkubwa lakini mwanaume huyo alikuwa akilifahamu jina lake. Sasa kivipi? JACK alisogea kwenye kiti chake na kuketi huku akimuonyesha ishara mwanamke huyo ambaye aliishiwa pozi naye aketi.
“Nadhani umenielewa vibaya, umenitajia jina ambalo sio langu na sijui ni mtu yupi ambaye unamaanisha” Aaliyaha alijitetea.
UKURASA WA 40 unafika mwisho.