FEBIANI BABUYA
JF-Expert Member
- Mar 5, 2022
- 1,916
- 3,850
- Thread starter
- #21
HADITHI: NAFSI ZILIZO TELEKEZWA
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 14
Issa alimsisitiza akitafute kitabu na kukisoma kisha akielewe na wakati huo alikuwa amekipata kitabu chenyewe tayari kwenye mkono wake ila hakuwa amekipitia na kuweza kujua ndani yake kilikuwa kimeandikwa nini. Alizidi kuchanganyikiwa kwa sababu alionekana kutafutwa mno, alikuwa akipata taarifa chache chache kumhusu ikiwa hakuwa anaelewa sababu ya hayo yote kutokea, kichwa chake kilikuwa kizito kufunguka juu ya kila ambacho kilikuwa kinaendelea kwenye maisha yake.
Alikumbuka kwamba kuna siku mchungaji aliwahi kumsihi kwamba ikitokea siku amekufa basi ahakikishe anamtafuta kijana huyo Issa kuna maelekezo ya mhimu angempa, alikuwa na kifaa cha mawasiliano kwenye mwili wake Issa ndiyo maana yeye binafsi hakupata taabu ya kuweza kumpata. Alimuona tangu akiwa anatoka kwenye ile hoteli ambayo alikuwa amekifikia ila hakutaka kukurupuka kwa sababu hawakuwahi kukaa pamoja huko nyuma au kufahamiana hivyo wangefahamiana kwa njia ya kuvamiana, alikuwa anamfuatilia kwa mbali Issa akiwa anapita vichochoro vingine ili mtu huyo asije akashtukia hiyo ishu ila kufanya hivyo kulimfanya apoteze lengo lake baada ya kukuta kuna mtu mwingine ambaye alikuwa amemuwahi ili kulitekeleza jambo hilo na mwisho wake akakosa kumhoji Issa maswali ambayo alitakiwa kumhoji.
Kwenye mfuko wake alikuwa anatembea na picha ya mwanamke ambaye yeye binafsi hakumjua kwamba huyo mwanamke alikuwa ni nani ila aliwahi kusisitiziwa kwamba asije akaipoteza hiyo picha kwa sababu ina mengi ambayo ilikuwa inayazungumza kuhusu maisha yake. Aliitoa hiyo picha na kuiangalia kwa umakini, akairudisha kwenye mfuko wake na kunyanyuka taratibu akaanza kuondoka hilo eneo kuelekea lilipokuwa gari yake aina ya BMWX5 nyeusi. Aliiwasha na kuondoka mitaa hiyo ya Kariakoo na kuelekea huko ilipo hospitali ya Amana.
Alipitia njia ya Fire na kuiacha ambapo aliishika njia ya Msimbazi, kulikuwa hakuna foleni wakati huo zaidi ya utulivu ambao ulishamiri. Alikunja barabara ya Karume na ndani ya muda mfupi akawa amepita mpaka lilipo soko la Ilala, alipunguza mwendo na kuanza kutembea taratibu mpaka alipo ikaribia barabara ya kukunja ilipo hospitali ya Amana akasimamisha gari yake na kuizima. Alitoka na kuanza kutembea kwa miguu mpaka alipo ipita hospitali hiyo akiwa anakagua namba za nyumba taratibu. Aliangalia saa yake ilikuwa inasoma saa tisa usiku.
Alikunja mkono wake wa kushoto, kwa mbali taa ilikuw ainamulika vizuri aliona namba ya nyumba ikiwa inang’aa vyema kupitia ule mwanga uliokuwa unamulika. Alisogea mpaka eneo lile, pembezoni mwa ukuta wa geti aliona damu ambayo baada ya kuigusa aligundua kwamba ilikuwa mbichi bado hivyo akawa na uhakika kwamba mtu wake alikuwa ameingia pale kama ambavyo alielekezwa na kijana Issa. Aligusa geti la mlango huo akagundua kwamba lipo wazi hivyo hakupata shida kuingia na kujua kwamba aliye ingia hapo alionekana kuwa na haraka ndiyo maana hakukumbuka hata kuweza kulifunga vizuri.
Ndani ya geti hilo kulikuwa na uwanja mdogo na nyumba moja tu pekee ambayo ndiyo alikuwa akiitazama, alisogea mpaka ulipo mlango wa kuingilia ndani nao haukufungwa, hapo akawa na imani zaidi kwamba mtu wake aliingia muda mfupi uliopita na huenda ilikuwa ni hofu ya kupoteza damu nyingi ndiyo maana alikuwa anafanya vitu kwa pupa mpaka akasahau kwamba alikuwa anaikaribisha zaidi hatari ndani mwake mwenyewe.
Aliichomoa bastola yake ambayo alikuwa akiitumia mara chache kwenye harakati zake kwa sababu bastola haikuwa njia sahihi kukipata kile ambacho alikitaka kwa kuyatoa maisha ya watu kwa uharaka mkubwa. Aliugusa mlango huo kidogo kuongeza nafasi ya yeye kupita na kutokezea ndani ghafla akiwa tayari kukabiliana na kila hali ambayo angekutana nayo ndani ila sebule haikuwa na kitu zaidi ya masofa, tv kubwa iliyozimwa na friji kubwa likiwa linamtazama.
Alitulia baada ya kusikia kelele za maji yakitiririka bafuni akajua moja kwa moja mtu wake alikuwa bafuni. Aliipakia bastola yake kiunoni kwa sababu hata huyo wa bafuni bila shaka hakuwa na silaha zaidi ya kuingia huko kujisafisha na kujitibia jeraha lake. Edison alikichomoa kisu chake ambacho huenda ndicho alikuwa akikiamini zaidi na kutembea bila hofu kuelekea ndani ya bafu hilo, alipo likaribia alijua kabisa kwamba aliyekuwa ndani hakuwa amejiandaa kwa jambo lolote baya hivyo aliukanyaga huo mlango kwa nguvu na kuingia nao ndani.
Ilisikika sauti ya maumivu ndani bila shaka Jacob alikumbana na hiyo dhahama ya ghafla ambayo hata yeye hakutegemea kukutana nayo wakati huo. Mlango ulivunjika na vipande vya mbao vikampata tumboni, alitoa sauti ya kilio, alikuwa hajapata hata muda wa kujipanga vizuri kwa sababu alikuwa anasafisha na kuweza dawa kwenye mkono ambao ulichanwa muda mfupi uliokuwa umepita ndipo akavamiwa, alishtuka wakati kisu kinampatia maumivu kwenye ubavu wake wa kushoto.
Alijivuta nyuma kisu kicho kikachomoka, mwilini mwake alikuwa amevaa taulo tu pekee hivyo alilivua na kulirusha alipokuwa Edson, lilidakwa na kuvutwa akateleza kwenye maji ya chini akajikuta anaenda mzima mzima, alirudishwa na ngumi ya uso na kudondokea kwenye sinki la maji ya kunawia ambalo lilishikana na kioo. Sinki hilo lilipasuka na kioo kikavunjika, hakukata tamaa Jacob, aligeuka na teke za nyuma ambalo alilizungusha kwa nguvu ila hakuwa na bahati. Mguu wake wakati unazunguka ulikita kwenye kisu ambacho kilizama kwenye kisigino, kisu kilizamishwa zaidi na kutolewa, kisigino kikawa hakifai tena akabaki anatoa sauti ya uchungu na kutia huruma huku akiwa anachechemea.
Edson alikuwa amevaa suti ambayo ilimpendeza ila nafsi yake ilikuwa ni tofauti na kupendeza kwake kwa sababu huruma haikuwa sehemu ya maisha yake.
“Frash iko wapi na kwanini umemuua Issa?”
“Hahahah unahisi unaweza ukasaidia kwa lolote? Issa alitakiwa kufa kama wewe ambavyo unatakiwa kufa mpuuzi wewe”
“Unanifahamu mimi?”
“Hakuna mtu ambaye hakufahamu wewe! Umetafutwa kwa miaka mingi sijui ulijificha wapi ila kwa sasa umeshajulikana kwamba bado upo hapa nchini kwahiyo ni suala la muda tu kabla hujapatikana na kuuawa”
“Mimi ni nani?”
“Inasikitisha mwanaume ambaye una kesi ya kuhusika na mauaji unajifanya haujui wewe ni nani, hahah au ndiyo mbinu ambayo umetumia kujificha kwa wakati wote huu? Lazima ufe kama alivyokuwa mke wako” alikuwa makini kusikiliza maelezo yale ila neno mke ndilo lilimshtua, aliitoa ile picha mfukoni na kumuonyesha Jacob haraka haraka
“Unamaanisha huyu ni mke wangu?”
“Acha kuniigizia, unatembea na picha ya mkeo halafu unaniambia humjui? Mtoto wako si angekuwa mkubwa sasa kama angepewa nafasi ya kujifungua” Jacob alizidi kumshangaza Edison ambaye kila neno alilokuwa anaambiwa lilionekana kuleta kitu kipya kwenye moyo wake mpaka akabaki anajishangaa.
“Bosi wako ni nani?”
“Hilo huwezi kuja kulijua hilo labda siku ambayo utaingia kaburini tena kwa mara nyingine kwa sababu watu walijua umekufa wewe hivyo kwenye dunia hautambuliki kama upo hai tena” kauli hiyo ilimfanya amkwide Jacob kwa sababu alikuwa anahitaji maelekezo ili atoke gizani ambako alikuwepo lakini muda haukuwa rafiki kwake kwa sababu Jacob alianza kutoa damu nyeusi mdomoni akiwa anatapa tapa. Alimfungua mdomo wake akagundua naye alikuwa na kidonge cha kuyatoa maisha yake awapo kwenye hatari ya kutoa siri kama ambavyo ilikuwa kwa yule mwanaume ambaye alimuua Lego wakati anatafuta kile kitabu nyumbani kwa mchungaji japo aina za hivyo vidonge ilionekana kuwa tofauti kuwa kuwa wa kwanza alitoa povu ila huyu wa sasa alitoa sumu nyeusi mdomoni.
Edson alichoka, alisogea kwenye kile kioo ambacho kilikuwa kimepasuka pasuka na kuanza kujiangalia huku naye kwenye vioo hivyo akionekana kama mtu ambaye mwili wake umepasuka pasuka na hivyo ndivyo alivyokuwa anajiona ndani yake. Alijihisi kama mtu ambaye alikuwa ndani ya jangwa asubuhi anapo amka asijue aelekee wapi kwa ajili ya kuupambania uhai wake. Aliangalia kila sehemu ya bafu hilo kuona kama angepata kitu chochote kile lakini hakuna cha maana ambacho alikiona zaidi ya pakiti tano za kondomu ambapo tatu zilikuwa zimetumika tayari.
UKURASA WA 14 umefika mwisho.
MWANDISHI: FEBIANI BABUYA
EMAIL: thomasibabuya@gmail.com
WHATSAPP: 0621567672
AGE: 18+
UKURASA WA 14
Issa alimsisitiza akitafute kitabu na kukisoma kisha akielewe na wakati huo alikuwa amekipata kitabu chenyewe tayari kwenye mkono wake ila hakuwa amekipitia na kuweza kujua ndani yake kilikuwa kimeandikwa nini. Alizidi kuchanganyikiwa kwa sababu alionekana kutafutwa mno, alikuwa akipata taarifa chache chache kumhusu ikiwa hakuwa anaelewa sababu ya hayo yote kutokea, kichwa chake kilikuwa kizito kufunguka juu ya kila ambacho kilikuwa kinaendelea kwenye maisha yake.
Alikumbuka kwamba kuna siku mchungaji aliwahi kumsihi kwamba ikitokea siku amekufa basi ahakikishe anamtafuta kijana huyo Issa kuna maelekezo ya mhimu angempa, alikuwa na kifaa cha mawasiliano kwenye mwili wake Issa ndiyo maana yeye binafsi hakupata taabu ya kuweza kumpata. Alimuona tangu akiwa anatoka kwenye ile hoteli ambayo alikuwa amekifikia ila hakutaka kukurupuka kwa sababu hawakuwahi kukaa pamoja huko nyuma au kufahamiana hivyo wangefahamiana kwa njia ya kuvamiana, alikuwa anamfuatilia kwa mbali Issa akiwa anapita vichochoro vingine ili mtu huyo asije akashtukia hiyo ishu ila kufanya hivyo kulimfanya apoteze lengo lake baada ya kukuta kuna mtu mwingine ambaye alikuwa amemuwahi ili kulitekeleza jambo hilo na mwisho wake akakosa kumhoji Issa maswali ambayo alitakiwa kumhoji.
Kwenye mfuko wake alikuwa anatembea na picha ya mwanamke ambaye yeye binafsi hakumjua kwamba huyo mwanamke alikuwa ni nani ila aliwahi kusisitiziwa kwamba asije akaipoteza hiyo picha kwa sababu ina mengi ambayo ilikuwa inayazungumza kuhusu maisha yake. Aliitoa hiyo picha na kuiangalia kwa umakini, akairudisha kwenye mfuko wake na kunyanyuka taratibu akaanza kuondoka hilo eneo kuelekea lilipokuwa gari yake aina ya BMWX5 nyeusi. Aliiwasha na kuondoka mitaa hiyo ya Kariakoo na kuelekea huko ilipo hospitali ya Amana.
Alipitia njia ya Fire na kuiacha ambapo aliishika njia ya Msimbazi, kulikuwa hakuna foleni wakati huo zaidi ya utulivu ambao ulishamiri. Alikunja barabara ya Karume na ndani ya muda mfupi akawa amepita mpaka lilipo soko la Ilala, alipunguza mwendo na kuanza kutembea taratibu mpaka alipo ikaribia barabara ya kukunja ilipo hospitali ya Amana akasimamisha gari yake na kuizima. Alitoka na kuanza kutembea kwa miguu mpaka alipo ipita hospitali hiyo akiwa anakagua namba za nyumba taratibu. Aliangalia saa yake ilikuwa inasoma saa tisa usiku.
Alikunja mkono wake wa kushoto, kwa mbali taa ilikuw ainamulika vizuri aliona namba ya nyumba ikiwa inang’aa vyema kupitia ule mwanga uliokuwa unamulika. Alisogea mpaka eneo lile, pembezoni mwa ukuta wa geti aliona damu ambayo baada ya kuigusa aligundua kwamba ilikuwa mbichi bado hivyo akawa na uhakika kwamba mtu wake alikuwa ameingia pale kama ambavyo alielekezwa na kijana Issa. Aligusa geti la mlango huo akagundua kwamba lipo wazi hivyo hakupata shida kuingia na kujua kwamba aliye ingia hapo alionekana kuwa na haraka ndiyo maana hakukumbuka hata kuweza kulifunga vizuri.
Ndani ya geti hilo kulikuwa na uwanja mdogo na nyumba moja tu pekee ambayo ndiyo alikuwa akiitazama, alisogea mpaka ulipo mlango wa kuingilia ndani nao haukufungwa, hapo akawa na imani zaidi kwamba mtu wake aliingia muda mfupi uliopita na huenda ilikuwa ni hofu ya kupoteza damu nyingi ndiyo maana alikuwa anafanya vitu kwa pupa mpaka akasahau kwamba alikuwa anaikaribisha zaidi hatari ndani mwake mwenyewe.
Aliichomoa bastola yake ambayo alikuwa akiitumia mara chache kwenye harakati zake kwa sababu bastola haikuwa njia sahihi kukipata kile ambacho alikitaka kwa kuyatoa maisha ya watu kwa uharaka mkubwa. Aliugusa mlango huo kidogo kuongeza nafasi ya yeye kupita na kutokezea ndani ghafla akiwa tayari kukabiliana na kila hali ambayo angekutana nayo ndani ila sebule haikuwa na kitu zaidi ya masofa, tv kubwa iliyozimwa na friji kubwa likiwa linamtazama.
Alitulia baada ya kusikia kelele za maji yakitiririka bafuni akajua moja kwa moja mtu wake alikuwa bafuni. Aliipakia bastola yake kiunoni kwa sababu hata huyo wa bafuni bila shaka hakuwa na silaha zaidi ya kuingia huko kujisafisha na kujitibia jeraha lake. Edison alikichomoa kisu chake ambacho huenda ndicho alikuwa akikiamini zaidi na kutembea bila hofu kuelekea ndani ya bafu hilo, alipo likaribia alijua kabisa kwamba aliyekuwa ndani hakuwa amejiandaa kwa jambo lolote baya hivyo aliukanyaga huo mlango kwa nguvu na kuingia nao ndani.
Ilisikika sauti ya maumivu ndani bila shaka Jacob alikumbana na hiyo dhahama ya ghafla ambayo hata yeye hakutegemea kukutana nayo wakati huo. Mlango ulivunjika na vipande vya mbao vikampata tumboni, alitoa sauti ya kilio, alikuwa hajapata hata muda wa kujipanga vizuri kwa sababu alikuwa anasafisha na kuweza dawa kwenye mkono ambao ulichanwa muda mfupi uliokuwa umepita ndipo akavamiwa, alishtuka wakati kisu kinampatia maumivu kwenye ubavu wake wa kushoto.
Alijivuta nyuma kisu kicho kikachomoka, mwilini mwake alikuwa amevaa taulo tu pekee hivyo alilivua na kulirusha alipokuwa Edson, lilidakwa na kuvutwa akateleza kwenye maji ya chini akajikuta anaenda mzima mzima, alirudishwa na ngumi ya uso na kudondokea kwenye sinki la maji ya kunawia ambalo lilishikana na kioo. Sinki hilo lilipasuka na kioo kikavunjika, hakukata tamaa Jacob, aligeuka na teke za nyuma ambalo alilizungusha kwa nguvu ila hakuwa na bahati. Mguu wake wakati unazunguka ulikita kwenye kisu ambacho kilizama kwenye kisigino, kisu kilizamishwa zaidi na kutolewa, kisigino kikawa hakifai tena akabaki anatoa sauti ya uchungu na kutia huruma huku akiwa anachechemea.
Edson alikuwa amevaa suti ambayo ilimpendeza ila nafsi yake ilikuwa ni tofauti na kupendeza kwake kwa sababu huruma haikuwa sehemu ya maisha yake.
“Frash iko wapi na kwanini umemuua Issa?”
“Hahahah unahisi unaweza ukasaidia kwa lolote? Issa alitakiwa kufa kama wewe ambavyo unatakiwa kufa mpuuzi wewe”
“Unanifahamu mimi?”
“Hakuna mtu ambaye hakufahamu wewe! Umetafutwa kwa miaka mingi sijui ulijificha wapi ila kwa sasa umeshajulikana kwamba bado upo hapa nchini kwahiyo ni suala la muda tu kabla hujapatikana na kuuawa”
“Mimi ni nani?”
“Inasikitisha mwanaume ambaye una kesi ya kuhusika na mauaji unajifanya haujui wewe ni nani, hahah au ndiyo mbinu ambayo umetumia kujificha kwa wakati wote huu? Lazima ufe kama alivyokuwa mke wako” alikuwa makini kusikiliza maelezo yale ila neno mke ndilo lilimshtua, aliitoa ile picha mfukoni na kumuonyesha Jacob haraka haraka
“Unamaanisha huyu ni mke wangu?”
“Acha kuniigizia, unatembea na picha ya mkeo halafu unaniambia humjui? Mtoto wako si angekuwa mkubwa sasa kama angepewa nafasi ya kujifungua” Jacob alizidi kumshangaza Edison ambaye kila neno alilokuwa anaambiwa lilionekana kuleta kitu kipya kwenye moyo wake mpaka akabaki anajishangaa.
“Bosi wako ni nani?”
“Hilo huwezi kuja kulijua hilo labda siku ambayo utaingia kaburini tena kwa mara nyingine kwa sababu watu walijua umekufa wewe hivyo kwenye dunia hautambuliki kama upo hai tena” kauli hiyo ilimfanya amkwide Jacob kwa sababu alikuwa anahitaji maelekezo ili atoke gizani ambako alikuwepo lakini muda haukuwa rafiki kwake kwa sababu Jacob alianza kutoa damu nyeusi mdomoni akiwa anatapa tapa. Alimfungua mdomo wake akagundua naye alikuwa na kidonge cha kuyatoa maisha yake awapo kwenye hatari ya kutoa siri kama ambavyo ilikuwa kwa yule mwanaume ambaye alimuua Lego wakati anatafuta kile kitabu nyumbani kwa mchungaji japo aina za hivyo vidonge ilionekana kuwa tofauti kuwa kuwa wa kwanza alitoa povu ila huyu wa sasa alitoa sumu nyeusi mdomoni.
Edson alichoka, alisogea kwenye kile kioo ambacho kilikuwa kimepasuka pasuka na kuanza kujiangalia huku naye kwenye vioo hivyo akionekana kama mtu ambaye mwili wake umepasuka pasuka na hivyo ndivyo alivyokuwa anajiona ndani yake. Alijihisi kama mtu ambaye alikuwa ndani ya jangwa asubuhi anapo amka asijue aelekee wapi kwa ajili ya kuupambania uhai wake. Aliangalia kila sehemu ya bafu hilo kuona kama angepata kitu chochote kile lakini hakuna cha maana ambacho alikiona zaidi ya pakiti tano za kondomu ambapo tatu zilikuwa zimetumika tayari.
UKURASA WA 14 umefika mwisho.