Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Najiuliza hiyo Pete inayomfuata Roma kila mahali aliipata wapi?

Naona Ina uhusiano na Umungu wake maana kila anapokoenda nayo wanamuheshimu Kama Mfalme Pluto au Hedes, sasa ikiwa hivyo, Ina maana nguvu zake za kimungu bado zipo?
 
Asalam aleykum kaka singanojr. Kesho imeshafika inaelekea jion mkuu! Ila mwanangu unatulekeza kinoma! Yaan wa huku jf tumekuwa kama watoto wa kufikia! Usitutenge hivi kaka
 
Asalam aleykum kaka singanojr. Kesho imeshafika inaelekea jion mkuu! Ila mwanangu unatulekeza kinoma! Yaan wa huku jf tumekuwa kama watoto wa kufikia! Usitutenge hivi kaka
Hizo ni business strategic huyu jamaa anafanya, ko ni kumsikilizia tu akiona inafaa atatubless tu roma
 
.......Ilipoishia na itavyoendelea kwa mukhutasari:- » Roma baada ya radi mipigo tisa na ile mionzi ya godstone kutoroka mwili kwa muda atakuwa kimodah! na kwa kiu alioonyesha roma kwa sally edna ajipange sawasawa kuliko hata rose muhando mwenyewe
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.

MTUNZI: SINGANOJR

WATSAPP;0687151346



SEHEMU YA 401

Mnada uliendelea kwa haraka huku watu mbalimbali wakijaribu bahati zao za kupata vile vitu ambavyo walikuwa wakitumainia kuvipata ambavyo vimewaleta.

Upande wa Roma na mrembo Rufi waliendelea kuangalia vitu vikiendelea kutolewa na kupigwa mnada , Rufi hakuwa amefikia kwenye kitu ambacho alikuwa akikitaka kama alivyoweza kumwambia Roma , hivyo walitulia kusubiria huku Roma akiendelea kumtania , lakini upande waRufi alijitahidi kuigiza kama alikuwa akifurahia utani wake , lakini kwenye moyo wake alikuwa na mikakati mingi.

Hatimae baada ya kama nusu saa alichokitaka Rufi kiliwekwa mezani kwa ajili ya mnada , ilikuwa ni chupa ya wine kutoka familia ya Rothchild ifahamikayo kwa jina la Chateau Mouton -Rothchild grape Wine ambapo mwendesha mnada alitoa bei ya kianzio ni dollar elfu kumi.

Thamani ya mvinyo haipo kwenye namna ambavyo inakuwa tamu bali kwenye urefu wa muda uliotumiwa kuizeesha , sasa unachotakiwa kuelewa sio kila mvinyo uliodumu miaka mingi unakuwa na thamani , kwasababu unaweza kuharibika , lakini kuna zile ambazo zimetengenezwa kwa ajili ya kudumu mpaka mwaka 2040 bila kuharibika.

Ukija kwenye nchi ambazo zinaendelea kama Afrika mambo ya mvinyo uliozeeshwa kwa muda mrefu na kuuzwa kwa bei kubwa linaweza kuwa jambo la kichekesho , lakini katika ulimwengu wa watu matajiri ambao wana mawasilianao ya moja kwa moja na ulimwengu wa siri , mambo hayo yana maana kubwa sana.

Baada ya Roma kuona wanaotaja bei kuanza kupungua na kubakia wachache kwakushindwa bei yeye aliinua bango lake na kutaja bei kubwa , Dollar laki moja na ishirini na kufanya watu wote wageuke na kumwangalia huku wakimtukana ndani kwa ndani kwa kuwa Tajiri kichaa asie na ustaarabu.

Baada ya mvinyo kupita hatimae ikaja kitu kingine ambacho Rufi alikitaka , pete ya almasi.

“Hii pete ndio kitu cha mwisho kwa mnada wetu wa leo na naamini wengi wenu ndio kilichowaleta , Pete hii imetengenezwa na karati tano za almasi rangi ya waridi , ni moja wapo ya Almasi adimu sana iliochimbwa nchini Tanzania na rangi yake imetokana na joto kali linalozalishwa na msuguano wa sahani za kitektoniki , thamani yake inaanzia dola milioni moja twendeni kazi”Aliongea mwendesha mnada kwa mbwembwe zote na kufanya watu kuanza kuinua vibao vyao kwa kupokezana ilimradi tu kila mtu afanikiwe kuipata , matajiri wlaikuwa wengi kwenye mnada huo kutokana na pete hio , wakiwemo baadhi ya wasanii pia maarufu.

Ni baada ya madakika kadhaa hatimae watu walipungua kutokana na bei kuzidi kupanda juu na mwishoni kabisa akabakia mwanamama mmoja kutoka Urusi , baada ya kuona amebakia mwenyewe alijikuta akijawa na shauku kubwa ya kukabidhiwa pete hio , alikuwa mtu mzima na kwa jinsi ambavo alionekana ni kama akivaa hio pete ingemrudisha kwenye ujana.

“Hey! Wewe dada nitaichukua kwa Dollar milioni kumi na tano na laki nne”Aliongea Roma bila wasiwasi na kumfanya yule mrusi kusimama kwa hasira na kumwangalia Roma na palepale alidondoka chini na kuzimia na kufanya eneo likose utulivu lakini Roma hakujali na mabodigadi walifanya kazi yao na kumtoa mwanamke huyo eneo hilo.

Haikuwa hela kubwa sana hata hivyo kwa vito vya thamani , lakini ukweli ni kwamba hata kama watu wanahela nyingi lakini kutoa pesa Zaidi ya dollar milioni kumi kwa wakati mmoja benki, ni ngumu sana kwani inaharibu mpangilio wa kibiashara na siku zote kama mfanyabiashara anataka kutoa hela zake kwenye benki husika na kiasi ni kikubwa, basi benki wanaweza kuomba muda maalumu kwa ajili ya kukusanya kiasi hiko cha pesa, hio ilikuwa tofauti tu kwa mfalme Pluto ambaye anaweza kupata hata dolla milioni moja kwa wakati mmoja.

“Miss Rufi kiasi cha pesa nilichonunulia hivi vitu vyote ni sawa na miaka ambayo mapenzi yangu kwako yatadumu”Aliongea Roma kiutani huku wakitoka ndani ya eneo hilo na kumfanya Rufi kujifanyisha ni mwenye aibu.

Baada ya kuifikia gari , Roma alimwambia Rufi aingie ili ampeleke mgahawani kwa ajili ya kupata chakula cha mchana , lakini mrembo huyo alikataa huku akiweka kisingizio kwamba anataka kurudi hotelini kwa ajili ya kumlipa Roma hela zake na Roma baada ya kuona Rufi kakomalia kulipa basi waliongozana Kwenda hotelini.

Haikueleweka mrembo Rufi alikuwa na mpango gani na hata gatri yake aliokuwa akiendesha haikujulikana iko wapi lakini aliongozana na Roma kimya kimya , Roma akiwa na mpango wake na Rufi akiwa na mpango wake.

Baada ya kufika na kuingia kwenye Lift walikuja kutokelezea juu kabisa ya hoteli katika chumba ambacho ndio cha mrembo Rufi , harufu nzuri ya kike ilimvutia sana Roma kwenye pua zake mara baada ya kuingia ndani, Rufi alishindwa kuvumilia sura ya kihuni ya Roma na alijitahidi kujituliza.

“Mr Roma nitafanya kazi ya kuhamisha kiasi unachonidai kutoka benki , lakini nikiasi kikubwa mno kukitoa online hivyo itanichukua muda kidogo, ungependa kinywaji chochote wakati nikiendlea na kazi?”Aliuliza.

“Oh chochte tu itafaa hata hivyo sina haraka, hata sumu nakunywa kama utaniandalia wewe mrembo”Aliongea huku akiweka tabasamu lake la kifedhuli na kumfanya Rufi kuziba mdomo na kuona aibu na akachukua mabarafu kwenye friji na kisha akayaweka kwenye glasi na kufungua chupa na kuweka mvinyo kwenye glasi na kisha akampatia.

“Mr Roma naomba usinihisi vibaya , ila najisikia vibaya , naomba nifanye kazi mara baada ya kuoga”

“Unataka kuoga tena?”Aliongea Roma lakini alitingisha kichwa kuashiria kama amemuelewa .

“Kama unataka kuoga sio mbaya , ukitaka hata mimi nitaungana na wewe , naweza kukusaidia kukusugua sehemu ambazo hufikii”

“Khaa.. nitayachukulia maneno yako kama utani Mr Roma , huwezi kufanya hivyo”

“Okey unaweza Kwenda kuoga nilikuwa natania kweli”Aliongea akimwashiria kuondoka.

“Usije ukanichungulia lakini?”

“Hata usijali , unafikiri mimi ni muhuni , kwa taarifa yako mimi Roma Ramoni nafahamika kama Gentlemen”

“Najua kabisa wewe ni mtu mzuri “Alitabasamu na kisha alikimbia kuelekea upande mwingine ambao ulikuwa na bafu na kumuacha Roma ambaye alianza kuchunguza chumba hiko.

Kilikuwa chumba cha hadhi ya juu cha hoteli chenye kila kitu , kuanzia Tv , Spik akubwa za kampuni ya Boss , mapambo mbalimbali ya kitamaduni ya kizungu na chini yake kulikuwa na kapeti zito la kupendezesha.

Ukweli Roma alijua mwanamke huyo alikuwa na mpango wake kichwani , lakini hakutaka kwanza kumuonyesha kajua , alichotaka ni kuona hadi mwisho , Zaidi ya yote kuna kitu kingine Zaidi kilichomvutia.

Alichukua mvinyo uliokuwa mbele yake kwenye meza na kisha akanusa harufu yake na kutabasamu na kisha akaupeleka wote mdomoni na kuunywa , baada ya kuona radha yae sio mbaya alichukua chupa na kumimina wote na kuushusha na kisha akamalizia na uliokuwa kwenye glasi nyingine.

Baada ya kumaliza alivua nguo zake zote na kubakia na boksa ya mua maua bila hata wasiwasi na kisha kujirusha kitandani kwa kuegamia mto na alijikuta hata usingizi ukianza kumjia .

“Miss Rufi maliza haraka najihisi kuchoka mno?”Aliongea Roma

“Okey namalizia Mr Roma , nakuja “Aliongea Roma na ndani ya dakika kama tano mbele mlango wa bafuni ulifunguliwa na Rufi alievaa suruali ya hariri na shati alionekana huku akifuta maji nywele zake na taulo.

“Rufi mvinyo wako ni mzuri sana na umenipandisha mzuka naomba nikukumbatie”Aliongea Roma huku akijinyanyua

Lakini Rufi alionekana kwenye mshangao , hakuamini kama Roma ataendelea kuwa macho mara baada ya kumaliza mvinyo wote .

Hapana , nakumbuka nilitumia dawa sahihi kuweka kwenye huo mvinyo au friji limeharibu makali ya dawa?”Aliwaza huku akijaribu kujitoa kwenye mwili wa Roma uliomkumbatia lakini kila akijitahidi kumsukuma haikuwezekana na kujiuliza kwanini mwanaume huyu ana nguvu kiasi hicho .

“Okey nadhani umefanikiwa kupona kwenye dawa niliokuwekea kwenye mvinyo ,vipi kama nitapulizia na dawa ya usingizi ya mfupa mlaini wa Mamba”Aliwaza huku akijaribu kufungua kidroo kidogo cha kijimeza pembeni ya kitanda na kisha akatoa kijichupa kama cha pafyumu na kisha kwa spidi alimpelekea Roma kwenye pua na kumpuliza na kujikuta akitabasamu huku akijiambia hakuna namna ya mwanaume huyu wa kiafrika kupona kwa mchanganyiko huo.

Mara baada ya Roma kujilaza kitandani akiwa kama mtu ambaye alikuwa amepotelea usingizi ndani ya dakika moja alifumbua macho yake na kumwangalia Rufi.

“Babe sikujua ni muhuni kiasi hicho , nimeamua kukuamni na kutoa pesa zangu nyingi lakini unanilipa kwa kuniwekea sumu kwenye kinywaji na haukutosheka na kunipulizia na dawa yenye mchanganyiko wa mifupa ya Mamba , unataka kuniua?”Aliuliza Roma akiwa kwenye uso wa kawaida

“Haiwezekani …”Aliwaza Rufi huku akianza kutetemeka

“Naona umejikatia tamaa mwenyewe mara baada ya kuona mpango wako haujafanya kazi , hata hivyo usiwe na huzuni nitakufariji kwa hilo”Aliongea Roma na kumvutia kwenye kitandan na kisha akamkalia kwa juu , Rufi alijitahidi kujitoa kutoka kwake , lakini mikono ya Roma ilikuwa imemshika vizuri.

Roma alijikuta akipandwa na mzuka mara baada ya kuangalia uso wa kitoto wa mwanamke Rufi na kujiuliza inakuwaje mwanamke huyu akawa pia na Ngozi laini namna hio.

Rufi ambaye nywele zake zilisambaa kitandani alijikuta akiwa kwenye kiwewe mara baada ya kufahamu mwanaume huyo alikuwa akijua mpango wake wote wa kumuibia tokea mwanzo.

Alijikuta akiwa ni mwenye hasira mara baada ya kugundua kumbe tokea mwanzo yeye ndio aliekuwa akichezewa na mwanaue huyo pasipo kujua.

“Kwahio ulikuwa ukijifanyisha kunisaida..?”Alijitahidi kuongea huku akijitahidi kuyafosi machozi yamtoke

“Miss Rufi kwenye Maisha yangu sijakutana na mwanamke mwenye mwili laini kama wewe , nafikiri ilikuwa bahati kwangu kukutana na wewe”

“Unaongea ujinga , niachilie”

“Haha.. sijakufanya chochote halafu nikuachilie , ungenilipa changu na kukauchia vitu vyako tusingefikia hapa , lakini ukaenda mbali kwa kuniwekea sumu kwenye kinywaji, hivyo ninachokwenda kufanya ni kulipiza kisasi”

“Wewe mwenyewe ndio ulionyesha kuwa na nia ya kihuni juu yangu ndio maana nikataka kukuibia”Aliongea Rufi.

“Mmi ni mwanaume mpole sana na hata nilivyokuona kwenye gari nilivutiwa tu na uzuri wako lakini kuniwekea mtego ilikuwa kosa , hivyo inabidi utulie mambo mengine yafuate”

“Unataka kunifanya nini?”Aliuliza swali la kipuuzi huku akianza kupaniki

“Sidhani wewe ni mtoto kuuliza swali la kipuuzi namna hii”Aliongea namna huku akianza kuangalia mwili wa mrembo Rufi uliosalitiwa na nguo, manyonyo ya mrembo huyo yaliokuwa wazi yalimfanya kuanza kupumua kwa kasi na kukosa nguvu ya aina yoyote ya kujizuia.

Roma wakati akiwaza namna ya kuanza uasherati wake mrembo huyo mwenye asili ya kichina palepale alipeleka pigo kwenye sehemu muhimu za mwili wa Roma kwa namna ya kumdhibiti lakini Roma wala hakujali matendo yake.

“Miss Rufi unaonekana kuwa mwanamke wa kushangaza mno ,kwanza ukaniwekea sumu kwenye mvinyo , ukanipulizia sumu ya mchanganyiko wa mifupa ya Mamba na sasa hivi umeamua kuniadhibu kwa kunipiga kwa kulenga Meridiani za mwili wangu, kwa jinsi ulivyozipatia nakufananisha na wale watawa wanaoabudu katika Budha , lakini kukosa kwako nguvu yoyote ya ziada ndani ya mwili wako inaniambia huna mafunzo yoyote ya kijini”Aliongea Roma akimaanisha kwamba kwa jinsi alivyozipatia kuzipiga Meridiani za mwili wake anamfanananisha na wale watawa wanao abudu masanamu katika dini ya Budha wanaofahamika kwa jina la Monk.

Meridiani kwa kingereza ni ‘Vital Organ’ kwa Kiswahili ni kama sehemu muhimu katika mwili wa binadamu, sehemu hizi zinafahamika kama sehemu muhimu katika mwili kutokana na kwamba ndio sehemu pekee ambazo huunganisha mawasiliano yote katika mwili.

Wale watu wanaojifunza mapigano ya kutumia uchawi mara nyingi wanafundishwa namna ya kuzitambua hizo sehemu kwasababu kama utazipiga na kuzifunga inamaana umezima mawasiliano ya mwili na hapo ndio unakuta mawasiliano ya mwili na ubongo yanakata na kuelekea mtu kupatwa na shida za kiafya..

Hakuna uthibitisho wa kisayansi unaoelezea kuhusu hizi Meridiani kwani zipo kiroho Zaidi na watu wanaotumia nguvu za ziada ndio wanazifahamu na kuzitumia sana , hata wachawi wengi hutumia kanuni hio hio ya Meridiani kumsababishia binadamu matatizo ya kiafya kwa kuzizima jumla yake zipo kumi na mbili.

Hakufanikiwa kwasababu mwili wa Roma haukuwa wa kawaida , lakini kama ingekuwa ni mwanaume wa kawaida ambaye hana mazoezi angepoteza fahamu.

Rufi baada ya Roma kuongea vile alijikuta akianza kuingiwa na wasiwasi tofauti na aliokuwa nao mwanzo kwa Roma kutaka kumfanya bila ya ridhaa yake.

“Umetumwa na Wazee kuja kunikamata?”Aliuliza kwa wasiwasi.

“Huh, Wazee gani tena mrembo?”Aliongea Roma kwa namna kama amechangayikiwa.

“Acha kujifanyisha , kama hujatumwa kunikamata kwanini unajua kuhusu mafunzo ya kijini na mimi kukosa nguvu yoyote ya Ziada”Alionge huku akionekana kukasirika kuliko mwanzo.

“Mtu yoyote hawezi kuongea hadharani maswala ya mafunzo ya kijini ,niambie kama Master Luo kukuagiza kunirudisha China?”Aliongea .

“Hakuna mtu wa kuniagiza na nikafanya , ninachotaka hapa ni mimi kufanya kilichonileta na kisha kuondoka , nakushauri uache kuleta ukinzani ili kisasi changu kiwe rahisi “Aliongea Roma na kumfanya Rufi kuvuta pumzi kwa ahueni.

“Nadhani ni kweli hawajakuagiza kuja kunikamata kama ingekuwa hivyo usingethubutu hata kuugusa mwili wangu kwani ungejua unajitafutia kifo”

“Kama maneno yako ni mtego wa kutaka nigharishe nilichopanga , labda atokee mke wangu kunifumania ndio ninaweza kuacha”

“Yaani mtu umeoa lakini unataka kumsaliti mkeo kwa vitendo kama hivi , naomba uniachie sipo tayari, Wanaume mbona nyie ni mashetani?”

“Ulinianza mwenyewe , nilienda kwenye ule mnada kwasababu nimemkumbuka mke wangu na nilitaka kumnunulia zawadi , lakini ukaharibu kila kitu , kuna haja gani mimi kukuachilia wakati umepoteza muda wangu , unapaswa kuwajibika kwa matendo yako , ukifanya kosa haya ndio matokeo”Aliongea Roma huku akiweka tabasamu lake la kifedhuli kama kawaida

“Naona sasa unanisizingia ili kuuficha umalaya wako , siwezi kukufanya chochote kwasababu wewe ndio mwenye nguvu , kama unataka mwili wangu nakuachia ufanye kila unachotaka , lakini nikutahadhari hautajua namna unavyokwenda kufa”Aliongea na kisha aliacha kuleta ukinzani akimruhusu Roma afanye anavyotaka.

Roma alijikuta akimwachilia kidogo na kuanza kuchunguza mwili wa Rufi na kujikuta akiwa ni mwenye mshangao.

“Mwili wako unaonekana kuwa na sumu nyingi sana , naamini sumu iliopo ndani yako inaweza hata kumuua Tembo , inashangaza bado ukendelea kuwa hai”Aliongea Roma kwa mshangao.

“Umejuaje kama mwili wangu una sumu , wewe ni nani?”Aliongea kwa sauti huku akianza kujisogeza kwa woga.

“Unaniuliza mimi nani tena , nipo hapa nikihitaji mwili wako”

“Naona unakwepa maswali wakati unajua ninachomaanisha, Niambie umefahamu mwili wangu una sumu kali ya kuua mtu , je unataka bado kuendelea unachotaka kufanya?”

“Kwanini nisiendelee , nitakuachaje mrembo kama wewe kisa sumu mwilini mwako?”

“Huogopi kufa?, mwili wangu kila kiungo kina sumu , kuanzia damu mpaka mifupa, hupatwi na shauku ya kujua kwanini nina sumu mwilini mwangu lakini bado naendelea kuishi”

“Haijalishi, ninachotaka ni kufia kwenye kifua cha mrembo kama wewe”

“Naona unakitafuta kifo wewe muhuni uliechanganyikiwa?”Aliongea Rufi , ukweli mrembo huyu alikuwa akijitahidi kumuelezea Roma aelewe mwili wake una sumu ili asije kubeba lawama kama itatokea kifo , kwani kwenye Maisha yake yote kutoka alivyokuwa China mpaka kufika hapo , kila mwanaume ambaye akitaka tu kufanya nae mapenzi anaishia kupoteza Maisha, hivyo hata kitendo cha Roma kuendelea kuishi licha ya kuwa nae na ukaribu namna hio kilimshangaza.

Roma hakujali tena kwani mwili wake muda huo ni kama ukiwaka moto , hivyo alishika vifungo vya nguo ya Rufi na kisha kufungua na kumvua huku akiskilizia harufu nzuri ya sabuni ikitoka kwenye mwili wake na kumfanya kuzidi kuchanganyikiwa.

Upande wa Rufi alikuwa akitoa machozi huku mwili wake ukitetemeka kwa woga , lakini kwa Roma ni kama mtetemo wa mrembo huyo kuwa kachumbali..

“Naona unazidi kutetemeka ,sitaki kuwa mbakaji nitakuacha kama unataka”Aliongea Roma huku akijifanyisha anaghairi.

“Endelea nimekuruhusu”Aliongea Rufi kwa suati ndogo

“Nini , kumbe unapenda?”

“Tokea nizaliwe na kufikia ukubwa huu hakuna mwanaume ambaye ashafanikiwa kunisogelea karibu na kufanikisha kuingiza kiungo chake sehemu zangu za siri , ila wewe umefanikiwa kwa nafasi kubwa hata kwa kunisogelea , kama huogopi kifo nina kuruhusu kuendelea , kwani niliishi kwa kujua sitokuja kufanya mapenzi na mwanaume, mpaka sasa nipo bikra , unaweza kufanikiwa kuitoa lakini utakuwa mwisho wa uhai wako na sitoweza kujilaumu kwani sitokuwa na deni”

“Kama wewe mwenyewe ndio unataka , unaonaje ukarahisisha sasa hili jambo”

“Sijakuelewa?”

“Nakuvuaje sasa hii suruali yako wakati umeibana na miguu”Aliongea Roma bila aibu na kumfanya mtoto wa watu kuona aibu na kujikuta akiwa mwekundu.

“Nakuombea kifo chako kiwe kibaya sana”Aliongea na kisha akasimama mwenyewe kiabu aibu na kuvua nguo zote na kutupia pembeni na kubaki kama alivyoletwa duniani.

“Nadhani umefurahi , nipo sasa kama nilivyozaliwa”Aliongea na kumfanya Roma aendelee kumwangalia huku akimeza mate kwa awamu , hakuamini kama baada ya kupona kwenye radi mwanamke wa kwanza kukutana nae ni mrembo wa aina hio.

“Una mwili mzuri sana”Aliongea Roma na palepale alimsogelea na kumsambaratisha miguu yake na kisha kuyashika manyonyo yake na kuyaminya .

“Ouch,, unafanya nini vinauma.. Assii”Alijikuta akitoa ukulele wa maumivu mara baada ya kuhisi kitu Kizito cha moto kikimwingia sehemu zake za siri , sehemu ambazo hazijawahi kuguswa kwa Zaidi ya miaka ishirini aliokuwa nayo tokea kuzaliwa.

Alijikuta machozi yakianza kumtoka , hakujua kitendo cha kushikwa manyonyo ni kama kuchanganywa na tayari ashaipoeteza bikra yake, lakini wakati huo huo akiamni mwanaume huyo baada ya hapo anakwenda kufa.

“Nkilikuwa na wasiwasi utaleta shida ndio maana nikakuchanganya kidogo ili ushitukie tu ipo ndani, usiwe na wasiwasi maumivu yatakata muda si mrefu na utaanza kujisikia hisia nzuri ambazo utatamani ziendelee, mimi ni mzoefu kwenye hizi mambozi”Aliongea Roma huku akiendelea kazi yake ya kushuka na kupanda.

“Nakuonea huruma baada ya hapa unakwenda kufa, anza kuandaa maneno yako ya mwisho”
 
SEHEMU YA 402.,

Roma aliekuwa juu ya mwili wa mrembo Rufi alijikuta akitoa macho baada ya kugundua kuna kitu hakipo sawa , tofauti na wanawake wengine ambao amefanya nao mapenzi ni Rufi peke yake ambaye alikuwa ni wa tofauti , mwanamke huyo alikuwa na sehemu za baridi mno, ijapokuwa ashawahi kufanya mapenzi na Lilith Vampire kule Ufaransa lakini sehemu za Rufi zilikuwa za baridi mno kuliko isivyokuwa kawaida mara baada ya mrembo huyo kuanza kutoa majimaji.

Roma alijiuliza kwamba je huyo mwanamke ana damu ya baridi, lakini hakupata jibu moja kwa moja.

Kitu kingine licha ya kumtoa mrembo huyo bikra lakini hakukuwa kabisa na tone la damu.

“Naona sumu ambazo zipo kwenye mwili wako zunafanya mwili wako kuwa wa baridi kama barafu”

“Inakuhusu nini, huna muda wa kuanza kufikiria kimantiki ,wewe ni wa Kwenda”Aliongea.

“Siamini kama naweza kufa”Aliongea Roma na kufanya kwa spidi kubwa na kumfanya Rufi kuzidi kutoa malalamishi ya maumivu huku Ngozi yae ikianza kupauka kama mgonjwa asie na maji mwilini.

“Yaani hapa ndio naanza , mpaka nihakikishe kisasi changu kishalipwa ndio nitakuacha”.Aliongea na kuendelea kufanya.

Show ilianza mchana lakini ilikuja kumalizika saa moja za usiku na Roma alifanikiwa kushusha mzigo mara mbili .

Upande wa Rufi hakuweza kumtafsiri mwanaume aliekuwa mbele yake , kwani alitegemea afe lakini alionekana kuzidi kupata nguvu Zaidi na Zaidi na kuendeleza kazi yake,, Baada ya kupumzika kama nusu saa alijikuta akimwangalia Roma.

“Bado hujisikii tu vibaya?”

“Kwanini nijisikie vibaya wakati umenipatia burudani”Aliongea Roma na kisha alimpiga bonge la kibao kwenye paja lake la mguu na kumfanya Rufi kufumba macho kwa maumivu , lakini palepale ni kama shoti za umeme zilikuwa zikitembea kwenye mwili wake kwa namna ya maajabu.

“Unajisikia vizuri?”Aliuliza Roma na kumfanya Rufi kufumbua macho yake taratibu , haikuwa akijisikia vibaya bali alikuwa akijisikia tofauti sana , hisia ambazo hakuwahi kuzisikia katika Maisha yake yote.

“Umefanyaje , mwili wangu nahisi umekuwa mwepesi , nahisi pia sumu zimeisha?”Aliongea huku akianza kutoa machozi.

“Ijapokuwa haujajielezea vya kutosha , lakini nilijua ni nini tatizo kwenye mwili wako , Una mwili wa tofauti sana , huenda tofauti kabisa na binadamu wa kawaida , ijapokuwa mwili wako una sumu nyingi lakini bado zilikufanya uendelee kuishi wakati huo huo ukiwa unapitia maumivu makali ya mara kwa mara”

“Mpango wangu mwanzo nikuachana na wewe na kutafuta mwanamke mwingine bila ya kukufanya kitu , lakini mara baada ya kuniwekea sumu niliona sitakiwi kukuachia kizembe hasa baada ya kugundua wewe ni bikra bado , hivyo kwa kutoa usichana wako nimekusaidia kwa kuponyesha sumu yako yote mwilini”

“Wewe ni nani haswa? , hata wazee ambao walishapewa kazi ya kunisaidia kupona walishindwa , kwanini imekuwa rahisi kwako?”

“Nahisi kuhusu wazee unaowazungumzia ambao siwajui hawajajaribu kukuponyesha , Sumu iliokuwa kwenye mwili wako haikutoka nje bali ilikuwa kwenye veini zako za mwili , hivyo niliitoa kwa kuzuia damu ya veini za upande moja na kuruhusu za upande mwingine”

“Kama tungekutana siku chache zilizopita nisingefanikiwa kukutibu , lakini sasa hivi ninaweza kukutibu , ijapokuwa haujapona kabisa lakini ndani ya miaka hamsini ijayo ndio unaweza kujisikia maumivu tena”

“Mika hamsini?”Aliongea kwa wasiwasi na mshangao juu

“Vipi ni michache , ushukuru tu umeewza kukutana na mimi , naweza kusema ni bahati kwako , hivyo kama hakuna kitu chochote mabacho kitaufanya mwili wako kupata tatizo utaweza kuishi bila tatizo kwa muda mrefu”

“Umeweza kweli kuponyesha Meridiani zangu?” Aliuliza kwa mshangao na Roma hakumjibu Zaidi ya kuingia bafuni na kuoga na ndani ya dakika kama tano tu alitoka na kuvaa nguo zake.

“Rufi nitachukua hii pete kuondoka nayo , ninapanga kumpatia mke wangu kama Zawadi , unaweza kuchukua Wine”Aliongea Roma mara baada ya kumaliza.

“Ndio unaondoka hivyo?”

“Ndio mimi na wewe hatuna deni, no string attached”

“Sijamaanisha hivyo, nataka kujua umefahamu vipi mpango wangu tokea mwanzo?”

“Kwahio unajaribu kutafuta wapi pamevuja mpaka mpango wako kuharibika ili usifanye makosa tena?, labda nikuambie tatizo ulilokosea ni kwenye kuchagua shabaha yako , wakati nafika karibu na jengo la mnada nilishagundua uwepo wako ukiwa katika mgahawa na ulikuwa ukichunguza kila anaefika na gari kali , sasa uliopona nimefika na gari la bei ndio ukaona nafaaa kwa mpango wako, naweza kusema mpango wako ulikuwa ni wa akili sana, kitu cha kwanza ulichofnaya ni kuchagua kitu cha bei rahisi kwenye mnada ambacho ni kinywaji , lakini kitu cha pili ukachagua ambacho ni cha bei ghali sana, yote ilikuwa ni kunijaribu”

“Yaani uliweza kunitamba licha ya kuwa mbali! , kama nitakuwa sahihi wewe ni Master kutoka Hongmeng?”

“Wow! ,sikudhania una ufahamu kuhusu Hongmeng , hata hivyo unakosea sina ukaribu wowote na wao , kama unavyoniona mimi sio mchina”Aliongea Roma na kisha akaondoka na kuacha chumba kuwa kimya.

Rufi mara baada ya kupumzika kwa dakika kadhaa akiwa ni mwenye kuandamwa na mawazo ya kutumiwa na kuachwa , lakini wakati huo huo kuponyeshwa ugonjwa wake wa miaka mingi , alijikuta fuaha yake ikirudi mara baada ya kuona Kamera ya siri alioitega kwenye chumba , alionekana kama mtu ambaye ameokota dodo kwenye muembe.

Roma akiwa anatembea alijikuta akimuwazia mrembo Rufi ,ukweli alijua sio binadamu wa kawaida , ni hisia ambazo hakuweza kuzielezea lakini kila kitu kilimwambia Rufi hatokei katika mazingira ya kawaida ya dunia na kama anatokea duniani basi kuna uwezekano mzazi wake upande wa baba sio binadamu wa kawaida ,lakini hakutaka sana kujihanganisha nae na ndio maana kaamua kuondoka , kwani aliamini kuadamana kwa muda mrefu na mwanamke huyo kungemletea matatizo Zaidi.

Roma mara baada ya kuingia kwenye gari lake na kuliwasha alijiikuta akitabasamu kwa kejeli mara baada ya kuona kitu nyuma yake na kuliondodisha taratibu kuingia barabara kuu.

Baada ya kuendesha gari kwa madakika kadhaa akitafuta mgahawa mzuri kwa ajili ya kupata chakula cha usiku , kwani giza lishaingia alijikuta akisimamishwa na Polisi wa barabarani ambao aliwaona tokea akitoka hotelini na ilikuwa ni kama walikuwa wakimfuata kwa nyuma.

“Sir I’m going to have to see your ID”Aliongea Polisi mweusi baada ya kusogelea dirishani. Akiomba kitambulisho kutoka kwa Roma.

“Samahani sana ndugu polisi ,ila sijakibeba maana ndio ninakwenda kutafuta chakula cha usiku”Aliongea Roma akidanganya maana alijua hata kuletwa ndani ya Marekani sio kwa utaratibu , kwa maana kwamba ni mhamiaji haramu.

“Kama ni hivyo basi nina kila sababu ya kukusindikiza mpaka polisi , tunazo kila sababu za kuamini kwamba umeiba hili gari”Aliongea akiwa siriasis, ni kama walikuwa wakimwambia Roma hana uwezo wa kumiliki hio gari.

“Mr Polisi yanini yote hayo kuipenda sana kazi yako , muda huu ni usku unaonaje ukienda nyumbani kufanya mapenzi na mke wako”Aliongea Roma .

“Please watch your language , I can charge you for verbal assault against a police officer”

“Naomba chunga lugha yako ninaweza kukushitaki kwa kumtukana Polisi”aliongea na palepale alifungua mlango wa gari yake akimwamrisha kushuka.

Roma alijiuliza ni wapi amemtukana afande huyo mpaka akachukia , alijikuta akizima injini ya gari na kisha akashuka na kulifunga na polisi wale walimshika na kumuingiza kwenye gari yao ya kipolisi na dereva mwingine ambaye alikuwa polisi alitoa gari hio akiendelea mbele.

“Ofisa sijala chakula tokea mchana , unachochote hapo kunipatia ili nitulize njaa niliokuwa nayo?”Aliuliza Roma lakini hakuna majibu aliopewa na ndani ya madakika kadhaa tu waliweza kufika kwenye bandari ndogo na Roma alishangaa hakuna aina yoyote ya kituo cha polisi.

“Well , Well! , Who would have thought thet the magnificient Pluto would come to a point where he did not recognize his own enemies “

“Well, Well , nani anaweza kudhania Pluto mwamba ameshindwa hata kuwafahamu maadui zake””

“Ninyi sio polisi?”Aliongea Roma huku akiwa kwenye mshangao.

“All in good time”Aliongea na kisha gari ile ilisimama pembeni kwenye bandari

“Lala chini mpuuzi wewe , hatutaki kuchelewesha wageni wetu” Aliongea na kisha wote kwa pamoja walishuka na kuliacha gari.

Roma alijikuta akiinua uso wake mara baada ya kugundua wametoka nje ya gari,na kisha akaufungua mlango na kushuka na kujikuta akipulizwa na upepo mkali wa baharini na kufanya shati lake jepesi kugandiana mwilini.

Ijapokuwa kulikuwa na giza lakini mwanga wa taa zilizozunguka eneo hilo zlifanya eneo lote kuonekana vizuri.

Polisi wale baada ya kufika mbele kidogo walivua sare zao za kipolisi na kbakiwa na sare nyingine ambazo baada ya Roma kuzikodolea macho tu alizigundua.

“Dhoruba Nyekundu!!!”Aliongea Roma huku macho yake yakiongezeka ukubwa mara baada ya kugundua watu hao ni wanajeshi wa Dhorumba nyekundu.

“It’s an honor to be remembered by Pluto himself, Allow me to introduce myself I am Seidel and this is my partner Stark”

“Ni heshima kwetu kama unatutambua mfalme Pluto , naomba nijitambulishe mimi naitwa Seidel na huyu ni mwenzangu anaitwa Starrk”

“Kwahio mkaamua kunileta kwenye eneo hili pasipo ya kuwa na msaada?”

“Hahaha.. Hapana tulishawataarifu wenzetu kufika eneo hili , hata hivyo una kipi cha kugopesha , tushasikia Habari zako kwamba umebaki kama kuku tu”Aliongea Seidel kwa dharau na palepale Stark alipuliza kipenga na ghafla moja ya Contena lilifunguliwa na wakatoka wanajeshi kwa kujipanga mistari miwili wakimzunguka Roma.

“Mnapanga kuniua?”Aliuliza Roma mara baada kuona jeshi hilo.

“Mimi ndio nitapata heshima ya kukuua Mfalme Pluto”Ilisikika sauti ya mwanaume kutokea kwenye kivuli cha makontena upande wake wa kulia., mwenye nywele ndefu ambazo zilikuwa zikipepewa na upepo.

Alikuwa amevalia vazi la kijapani kama kanzu rangi nyeusi huku mkononi akiwa ameshikilia panga refu aina ya Samurai.

Lakini muda hio huo Roma alishangazwa pia na kuibukia kwa watu wengine kutoka kwenye maji kwa mfano wa kupaa ,wote wakiwa katika mavazi yanayofanana ya utamaduni wa Japani , Kimono.

“Takamagahara!, Nadhani taarifa zinasambaa kama kifuu cha nazi ,kwa hali hii naamini mshafahamu juu ya mimi kupoteza uwezo wangu , Vipi kuna mwakilishi kutoka Dhoruba nyekundu ambaye pia anahitaji kuniua?”

Roma aliweza kumgundua mwanaume aliekuwa mbele yake , alishawahi kukutana nae kule Ufaransa , kwenye mkutano wa siri uliondaliwa na serikali ya Ufaransa, alikuwa ni Nurarihyon ambaye ni generali wa kundi la Takamagahara.

“Inaonekana kweli umepoteza uwezo wako , mwanzoni sikuamini lakini kwa mwili wako ulivyo ni kweli hakuna kilichobakia , nasikia umepoteza uwezo wako mara baada ya kupigana na Poseidon?”Aliongea mwanaume mmoja aliekuwa kati ya maninja walioibuka kutoka kwenye maji halafu akaendelea.

“Nilitamani kuona jinsi ulivyodundwa na Poseidon lakini haima haja tena , naitwa Namera na nipo hapa kwa ajili ya kulipiza kifo cha mpenzi wangu SnowGirl”Aliongea yule ninja.

“Nilifikiria kutokana na kutokuwa na nguvu mngeniacha nikaendelea na Maisha yangu , kwanini nahisi kama mna katabia kakuchokoza watu wadhaifu”Aliongea Roma.

“Sio sisi tuliohusika kukufanya kuwa dhaifu na sio kosa letu wewe kupigwa na Poseidon ,hivyo kukuua leo hii ni jambo ambalo halikiuki kanuni zetu”

“Nurarihyon hatujakubaliana kwamba umuue huyu mtu , unatakiwa kuelewa kwamba anafaida kubwa kwetu akiwa hai kuliko mfu , kama utamuua hakika lazima tutakushugulikia”Aliongea Seidel wa Dhoruba nyekundu..

“Rest assured a powerless Pluto does not interest me , I cant leave empty-handed , however I don’t ask for much , All I want to do is to break every bone in his body”

“Kaa kwa kutulia sina haja ya kumuua Pluto asie na nguvu na siwezi pia kuondoka mikono mitupu , hata hivyo si ombi kitu kikubwa ninachotaka ni kuhakikisha navunja kila mfupa kwenye mwili wake”Aliongea Narurihyon.

“Naona mmechagua mbinu nzuri rafiki yangu , kwanini hamtaki akiniua?”Aliongea Roma akimwangalia Seidel

“Acha kuongea kilicho wazi”Alijibu Stark.

“Haupo imara kama mwanzo , hivyo sio ngumu kwetu kukudhibiti , ila usiwe na wasiwasi hii siri tunaifahamu sisi tu”Aliongea Seidel kisha akendelea.

“Kama utashirikiana na sisi na kutupa Umiliki ya jeshi lako , Hifadhi ya mafuta .siraha na vitu vya thamani tunaweza kukaa chini na kuongea , huenda pia tukawa marafiki ,tunasikia huko Tanzania una warembo kibao , hivyo hatutaki wakapatwa na huzuni”Aliongea Seidel.

“Kwahio hicho ndio mnataka?, basi ngoja niwaulize swali”

“Uliza tu”Alijibu Seidel.

“Nani kawaelezea nimepoteza uwezo wangu?”

“Mfalme Pluto acha maigizo na kuonyesha bado una nguvu ,tusingekuwa na uhakika na taarifa tulionayo tusingekuja wachache hivi ,tumepata taarifa kutokaka chanzo cha kuaminika”Aliongea Seidel.

“Ooh! sasa hivi nadhani naelewa , ukiachana na Prandell pamoja na Christen mtu mweigine niliekutana nae ni mkuu wa kikosi cha Dhoruba nyekundu”

“Kwahio unataka kusema nini? , huna chaguo kwa sasa nashauri utupe ushirikianao na kutuachia vitu nilivyovitaja kabla hawa marafiki zetu kutoka Japani hawajachukua hatua , ukitaka pia tunaweza kuingia makubaliano tukuachie mguu au mkono , Ijapokuwa natamani sana kukuua kulipiuza kisasi cha Judy”Aliongea Stark.

Judy ni moja ya jasusi wa kundi la Dhoruba Nyekundu ambaye Roma alimuua , Judy alikuwa ni mrithi wa Christen ambaye alimchagua , lakini kutokana na tabia zake za kuingilia mambo ya Roma akaja kumuua, sasa hilo ni tukio ambalo Roma alifanya kabla hata hajarudi Tanzania.

Roma alijikuta mwili ukimsisimka maana mpaka hapo watu wote walionekna kuwa na visasi , kwa mfano Namera alionekana kutaka kulipiza kisasi cha mrembo wake Snowgril , lakini wakati huo huo Stark alitaka kulipiza kisasi cha mpenzi wake Judy.

Roma alijikuta akiwaangalia kila mmoja kama vile alikuwa akiwakagua na kisha kutabasamu kifedhuli.

“Mnauhakika ni nyie tu hapa?”Aliuliza.

“Ni sisi tu ndio na tunakushinda jiandae naachia mapigo muda si mrefu”Aliongea Nurarihyon.

Roma alionekana kama mtu ambaye hajaridhishwa na watu wachache namna hio alitembea huku akiwa amekunja mikono yake kwa nyuma huku akiwaangalia, ukweli Roma alitamani sana mtu ambaye alijifanyisha kuwa yeye ndio afike hapo kwenye hilo eneo lakini alikuwa mwingine.

“Nyie watu inaonekana mna muda wa kutosha mpaka kuja hapa , katika watu wote ambao nilitarajia ni yule aliejifanyisha kuwa mimi , lakini nyie mkajiingiza kwenye hili , kwanini hamkuja siku zote hizo mkaja siku ya leo?”Walijikuta wakiangaliana kwa kuchanganyikiwa kwani walishindwa kumuelewa.

“Siwezi kuhisi aina ya msisimko unaotokana na uwezo wako wa kimapigano sasa hivi , ngoja tuone kama utaendelea kubwabwaja mpaka saa ngapi ,nataka uonje joto la upanga wangu”Aliongea na kisha aliuchomoa

“NENEKIRIMARU””

Aliongea kwa sauti na pale pale upanga wake uling’aa kama mwezi na palepale akapotea na ile anakuja kutokea yupo mbele ya Roma akitokezea kwa juu na alishusha upanga wake akidhamria kumkata Roma vipande viwili kutoka kichwani.

Roma hakuondoka aliposimama na alikaa vile vile huku mikono yake akiwa ameikunja nyuma , mpaka wale wenzake kuona labda Roma alishindwa kumkwepa kutokana na kushitukizwa.

Upanga ulivyomfikia Roma karibu na kichwa aliinua mkono wake na kuukinga na ukashuka moja kwa moja kwenye mkono lakini sauti iliotoka hapo ni kama ya panga na kufanya wote kushangaa na kutafuta kilichotoa mlio.

Upanga Nenekirimaru ni kweli ulifika kwenye mkono wa Roma lakini makali yake yalishindwa kupita kwenye Ngozi yake na sio kupita tu hata tone la damu halikuonekana.

“Ndio ushamaliza?”Aliuliza Roma kwa dharau

“Inaonekana licha ya kupoteza uwezo wako lakini mwili wako una Ngozi ngumu kama zamani , pigo la kawaida naona limeshindikana kukumiza?”Aliongea Nurarihyon.

Roma alimwangalia huyu ninja aliekuwa mbele yake , huku akifikiria ni kipi cha kumfanya yaani hakuwa hata na wasiwasi wa aina yoyote kwenye macho yake licha ya kwamba alikuwa amezungukwa na watu wengi

“General kwasababu huyu mpuuzi mwili wake ni mgumu hata panga kushindwa kukata Ngozi yake , nipe nafasi nimuonyeshe uchawi wangu , naamini kuna mapigo akipatiwa ngozi yake haiwezi kuhimili”Aliongea moja ya vijana wa Nurarihyon.

“Gashadokuro fanya kistaarabu tusivute nzi”Aliongea akimwachia.

“Nyie msijali hapa hakuna ambaye anaweza kufika kwani Polisi wanazunguka hili eneo kulinda kinachofanyika hapa“Aliongea Seidel

“Hehe ,, Well then time to have fun”Aliongea Gashadokuro na palepale ulitokea mwanga kama wa radi hafifu kwenye mikono yake na hapo hapo lilionekana fupa , sasa haikueleweka ni mfupa wa mtu au wa mnyama ila ni mfupa uliochongwa kama mkuki kwa mbele huku katikati ukiwa na kinundu ambacho kina matobo ambayo yalionekana kama vile yanatoa moto.

Kitendo kile kiliwafanya wale wanajeshi waliozunguka kurudi nyuma kidogo kupisha mpambano.

Inasemekana enzi hizo wakati wa vita huko Japani , wale wanajeshi wanaokufa vitani mifupa yao haikuwa ikizikwa na wanachokifanya ni kuikusanya sehemu moja, inaaminika kwamba Roho ya mtu hukaa kwenye mifupa mara baada ya kufa hivyo kuamini kwamba kwasababu mwanajeshi amefia vitani basi Roho yake ya machukizo na visasi hufuata mifupa yake , hivyo zile roho za machukizo na visasi kutoka katika mfupa wa kile mwanajeshi ndio wanazikusanya kichawi , sasa wanasema muunganisho wa roho zenye machukizo zikiungana kwa wingi zinatengeneza Pepo.

Ndio maana jamii nyingi za bara la Asia wanaamini kuzika kwa namna ya kumchoma mtu moto mpaka kuwa majivu ili Roho isibakie duniani, wanamini chanzo cha mapepo katika dunia ni mifupa ya binadamu.

Sasa mambo hayo hayatokei kwa wanajeshi wa kawaida , ila ni kwa makundi ya kijapani yaliojikita katika tamaduni za kichawi kama Takamagahara na mengineyo , hivyo fupa la Gashadukuro limejaa pepo moja lililotokana na muuganisho wa Roho kwenye mifupa Zaidi ya elfu moja.

Fupa lake lililikuwa ni kama likiongezeka ukubwa ile sehemu ya nundu yake huku kukiwa na kama wingu linalozunguka pale katikati na ule mchongoko wa mbele ulirudi nyuma na kujaa kwenye ile nundu na kufanya iwe kubwa kama nyungo ya kupasulia miamba saizi ya kichwa cha mtoto.

“Pluto ngoja nikuadhibu na hii nyundo tuone ni ugumu gani unao?”Aliongea na palepale akamsogelea Roma kwa Spidi.

“BANG!”

Nyundo lile lilikwenda kugonga ile sehemu ambayo Roma amesimama na kusababisha vumbi kubwa kama vile ni kimondo kutoka angani kimedondoka.

Walijikuta wote wakishangaa na hawakuelewa ni wakati gani Roma alipotea na kutokezea nyuma ya Gashadukuro akiwa hana maumivu ya aina yoyote, walishindwa kuelewa kwanini akaweza kupotoea na kutokezea.

“Damn it Si tumeambiwa amepoteza uwezo wake huyu?”Aliongea Stark huku akiwa ni mwenye mshangao mkubwa.

“Haiwezekani , Poseidon hawezi kufanya makosa , Kama nipo sahihi naamini licha ya kwamba amepoteza uwezo wake lakini mwili wake bado una baadhi ya vinguvu vinavyomsababishia kupinda pinda ndio maana akakwepa hana lolote huyo”Aliognea Seidel akijipa matumaini na kuwafanya wenzake wote kumuamini na presha ikapungua.

“Bastard”

Aliongea kwa hasira Gashadukuro baada ya pigo lake kugonga ardhi , palepale alirusha nyundo ya fupa la pepo kuelekea kwa Roma.

“Kwepa hio kama wewe ni mjanja”Aliongea na kumfanya Seidel kuwapa ishara baadhi ya wanajeshi wa kawaida kutoka upande wa Roma lakini ni kama wamechelewa kwani walimezwa na moshi mkubwa kwani ilitokea kama mlipuko wa bomu na kufanya nyama za miili yao kuruka hewani .

Upande wa Roma hakusogea kabisa na palepale aliziba pua zake baada ya kuhisii harufu mbaya.

“Nyama zao zinanuka”Aliongea .

Sasa ilionekana baada ya fupa lile Kwenda kwa Roma alilikwepa na likaenda kutua kwa wale wanajeshi na kusambaratishwa vibaya sana.

Gashadukuro mara baada ya Nundu ya fupa lake kuadhibu wanajeshi wale lilimrudia kwenye mikono yake.

“Nitakuwa makini muda huu na nitahakikisha hauna pakukimbbilia au kukwepa pigo langu”Aliongea kwa kijapani na palepale alileta nyundo lake la fupa lililojaa mapepo karibu na usawa wa Roma na ile linafikia nusu nchi kutoka kwenye mwili wa Roma lilisimama lenyewe pasipo ya kuendelea , ni kama limenasa hewani huku Gashadukuro akiwa amelishikilia.

Wenzake walijikuwa wakishangaa na kujiuliza kwanini kaishia njiani.

“Mbona umeishia njiani , mmalize haraka tuondoke?”Aliongea Siedel huku akimwangalia Gashadukuro bado akiwa ameshikilia fupa lake akijaribu kulivuta kurudi nyuma lakini mikono iliishia kumtetemeka.

“Siwezi “Aliongea kwa sauti ya kuchanganyikiwa na kufanya kila mmoja kushangaa .

“Nini kinatokea kwanini sioni ishara yoyote kama ana nguvu hata kidogo kwenye mwili wake?”

Inasemekeana Takamagahara ndio moja ya kundi ambalo linatumia mapepo katika mashambulizi , ndio kundi ambalo linaamini Zaidi katika nguvu zinazotokana na uchawi wa mapepo kuliko hata Yamata Sect , wanajiita The Demons kwa jina lingine na kama utafika kwenye kambi yao wanalo pango ambalo limejaa mifupa ya binadamu tupu kwa ajjili ya kuvuna roho zao na kuzigeuza mapepo , lakini hawachukui tu kila binadamu wanapendelea wale ambao wanakufa kwa visasi na chuki kwani mapepo yao yanakuwa makali Zaidi kuwa siraha.

“TAWANYIKA!!”

Roma aliongea kwa sauti akimwangalia Gashadukuro na palepale kilitokeza kitu cha kushangaza , mwili wa Gashadukuro pamoja na fupa lake vilianza kuyeyuka na kuwa kama unga unga ni kama vile alikuwa akiliwa na mchwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…