Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Mwacheni wazee siku akiona nasi tuna umuhimu atapost na sisi bila hiyana tutasoma.
Customer n mtu muhim San kwa mfanya biashara. Na msomaji ni muhim san kwa mwandishi kwahy respect kwa wote wasomajii wakisusaah kazi yak ya fasihii ainaah maan wapend watej wako waheshim na ahadii n kitu mhm San kweny maish
 
SEHEMU YA 419

Roma alishanganzwa kwa kiasi flani na nguvu ya kijini iliotoka kwa mwanamke huyo ambayo ipo kwenye levo ya mzuguko kamili , alijiambia ingekuwa siku kadhaa zilizopita angeogopa lakini kwasasa alikuwa ashapita kabisa kwenye hio levo mpaka kupigwa na radi hakuwa na chakuogopa.

Alichokifanya ni kama kupangusa kwa mkono wake wa kulia kama anafukuza nzi na palepale ile nguvu yote ilipotea kama kibatari kilichopulizwa na upepo na kuzima papo papo.

“Sijaja hapa kwa ajili ya kupigana na sipendezwi kabisa na visheria vyenu vya kipuuzi , nimejitahidi kuwasiliana na nyie kwa njia za kistaarabu lakini inaonekana haitoshi na kutaka kuleta mtafaruku hapa , mnafikiri mnaweza kunizidi kwa chochote? Au mnapima kina cha bahari kwa kidole?”Aliongea Roma kwa kibesi

Ijapokuwa hakuachia msisimko mkubwa wa nguvu za kijini lakini Tang Dianshan na wezee wengine wlaiweza kuhisi msuguano usiokuwa wa kawaida ukitoka kwake.

Wote humo ndani kama kuna ambaye ameenda levo za juu ni huyo Master wake Magdalena ambaye alikuwa kwenye mwisho mwa levo ya Mzuguko kamili lakini hata hivyo hakuwa hata na uwezo wa kuangalia ni levo gani ambayo Roma amefikia na kuna muda walijiuliza huenda alikuwa akijifunza mbinu flani za kuvuna nguvu za mapepo ambazo wao wenyewe walikuwa wakishindwa kuzigundua.

“Nilisikia umefikia levo ya Nusu mzunguko , nadhani tulidharau uwezo wako tokea mwanzo? , Lakini usipate kiburi cha kudhania unaweza kuleta machafuko ndani ya jamii yetu , mimi na wazee wenzangu wote tupo kwenye levo ya Mzunguko kamili na kama wote tutaungana kukushambulia hutokuwa na uwezo wa kutushinda”Aliongea Tang Luyi.

“Master kwanini tusiyamalize tu kwa amani”Aliongea Magdalena huku akijisi mkosaji kutokana na mabadiliko ya hewa

“Hebu jiangalie wewe mtoto usie na shukrani , tuliweza kukupokea hapa licha ya kuwa tofauti na jamii yetu na tukakufunza mbinu za mapigano mpaka za kijini na sasa upo na huyu mpuuzi mwenzio unajaribu kumtetea”

“Nisamehe Master”Aliongea Magdalena huku akianza kutokwa na machozi kutokana na kukasirika kwa Master wake.

“Magdalena nani kakupa ruhusa ya kujaribu kunikingia kifua , ukijaribu naanza na wewe”Aliongea Roma.

“Flamingo ngoja nikupe ushauri wa bure , wakati unawasiliana na sisi kama unakuja na Mr Roma hapa tayari nilishaamua kwenye akili yangu kwamba hakuna namna ambavyo anaweza akaingia kwenye maktaba yetu , sio mahali ambapo kila mmoja anaweza kuruhusiwa na akaingia na kufanya atakacho kuna sheria kali zimewekwa ambazo hatuwezi kuzivunja”Aliongea Tang Dianshan.

“Kwahio mlinifanya nitoke Tanzania mpaka kuja hapa kwasababu gani kama hamkuwa na mpango wa kuniruhusu kuingia kwenye hilo pango la kumbukumbu?”Aliuliza Roma

“Upo sahihi hatukukuita hapa kwa ajili ya kukuingiza kwenye pango la nyaraka zetu , bali tumekuita ili utupatie kile kilichokuwa cha kwetu”Aliongea

“Nini! ?ni kitu gani ninachomiliki kutoka kwenu?”

“Acha kujifanysiha mnjanja mbele yetu tunataarifa zote za umiliki wako wa mbinu ya mafunzo ya kijini ya njia ndefu ambayo nayaraka yake iliibiwa hapa na yule mpuuzi Tang Chi na kukukabidhi wewe”Aliongea Tang Luyi na kumfanya Roma sasa kuelewa wanachomaanisha nini.

“Mnamaanisha mbinu ya Maandiko ya urejesho.. Hahaha ,, kwahio maneno yenuu yote ndio mlikuwa mkitaka mbinu yangu”

“Sio mbinu yako ni mali ya wachina na hatuwezi kuruhusu mtu yoyote kuimiliki mathalani mtu kama wewe wa ngozi nyeusi ambaye huna muunganiko wowote na China, mbinu yetu ilikuwa imepotea na sasa tumekuona nayo tunaamini Tang Chi ndio mhusika mkuu aliekukabidhi hivyo huondoki hapa bila kuirejesha”Aliongea Tang Luyi.

“Kwahio ndio mpango wengu tokea mwanzo…”

“Acha maneno mengi , kama unataka ubakie na uwezo wako wa kijini rudisha mbinu yetu”Aliongea

“Kwahio kama nikikataa mtanilazimisha kukubali?”Aliuliza.

“Tunajaribu kutumia busara , maamuzi yako ndio yatatufanya tujue ni hatua ipi tunaichukua dhidi yako”Aliongea

“Okey kama hiuo ndio mipango yenu bado nina swali moja kwanini mnachukua hatua hatarishi kutaka kupata mbinu yangu, labda nyie ndio hamuelewi ila mbinu hii ya maandiko kwangu sikupewa kama karatasi nisome bali ni kwa njia ya kusimuliwa kwa mdomo ndio nikaweza kukariiri na kujjifunza hata hivyo nimesikia sio nyie tu hata Hongmeng mmeshindwa kujifunza sasa hata niwapatie itawasiadia nini”

“Kaaam kimya mpumbavu , hatutaki ngonjera zako”Alifoka Tang Luyi

“Mimi sio mtakatifu sana , lakini naamini utu wa mwanaume lazima uheshimiwe siku zote na nitaulinda kwa namna yoyote ile , haijalishi kama mnataka hii mbinu lakini kwangu haimaanishi kwamba nitatoa kama mnavyotaka kirahisi , mnafikiri nikirudi Bongo nitawaambia nini warembo wangu”Aliongea Roma na kumfanya Magdalena kuwa katika hali isioelezeka.

“Master kama umeamua kutugeuka mimi sitokua na namna tena zaidi ya kukaa upande wa Roma”Aliongea

“Wewe mwanafunzi usie na shukrani nadhani hatua sahihi ni kukuvua nguvu zote nilizokufundisha”Aliongea palepale huku akimsogelea Magdalena kwa kumlenga kwenye shingo kwa spidi lakini Magdalena akiwa kwenye taharuki palapela aliachia visindano flani vya kichawi vingi kuelekea kwa Master wake lakini Tang Luyi alionekana kumtegemea kwani alivikinga kirahisi na vyote vikatua kwenye kiganja cha mkono wake na kisha akatabasamu kifedhuli huku akijiandaa kumshambulia.

“Acha kuendelza upuuzi wako , wewe ndio uliemkuza”Aliongea Roma kwa sauti.

“Kama mimi ndio niliemfudisha vyote basi ninao uwezo na haki ya kumvua nguvu zake zote”Aliongea lakini hata hivyo alionekana kusita sita kwani nguvu isiokuwa ya kawaida iliokuwa iktoka kwa Roma ilimuogopesha lakini hakutaka kushindwa kizembe aligeuza kibao kwenda kwa Roma na palepale visindano vile viliongezeka kuwa vingi kwenyue mikono yake na kisha akaviachia hewani kama vile anamwagia kuku punje za mahindi .

Lakini Roma hakusogea hata nchi na baada ya vijisindano vile kumsogela vilinasa hewani na palepale vikadondoka chini pasipo kumgusa kabisa na kitendo kile kiliwafanya wazee wote kupatwa na mshangao huku wakijiuliza kawezaje kuvizuia bila kufanya chochote.

Lakini Roma hakutaka kuwajali na mshangao wao kwani palepale alimsogelea Tan Luyi na kumshika kiganya chake cha mkono na kisha kwa kutumia nguvu zote alimsukuma na kilichotokea ni kwamba Tang Luti alichomolewa mpaka nje kwa kuvunja milango yao ile miepesi ya kuslide na ilibidi wote wakimbilie nje.

“Tokea niishi hapa sikuwahi kuomba heshima wala mapenzi ya dhati kutoka kwenu lakini nilivumilia yote na kujifunza lakini siamini leo hii Master unataka kunivua nguvu zangu bila ridhaa yangu”Aliongea Magdalena huku akiwa kama mtoto aliefiwa.

“Wewe mwenyewe ndio sabababu wakati ule tulikushauri usiondoke hapa na kwenda kujjiunga na jeshi , lakini haukutusikia na kudharau mbinu zetu kisa zinachukua muda mrefu…”

“Kimya..’Aliongea Roma kwa amri na kisha akamgeukia Magdalena.

“Magdalena kwasababu wameyaanzisha wenyewe basi sitolaumiwa kama nikiwaua wote”Aliongea Roma.

“Kuwa makini”Aliongea Magdalena akimpa Roma ruhusa ya kuua , mpaka hapo aliamini kama isingefanyika hivyo basi wasingetoka salama.

“Hahaha,, Mr Roma unajjifanya kijogoo sana , ijapokuwa umeweza kuelewa kuhusu levo ya Mzunguko kamili lakini haimaanishi kwamba unaweza kutushinda wote hapa tukiaungana , tutanyofoa viungio vyako kimoja kimoja”Aliongea lakini kabla hajamaliza Roma hakutaka aendeelee kuongea kwani palepale aliachia wimbi la kisulisuli ambalo ni kama upepo uliokuwa kwenye mfumo wa kimbunga na kuwafanya waanze kuzungushwa kwa spidi.

“Jaribuni kuwa makini…”Walipiga makelele

“Bang , Bang , Bang , Bang , Bang..”Ni migongano ya wazee wote nane wakijipigiza kwenye kuta za nyumba na kama sio kwa uwezo wao wa kijini basi huenda wangekufa hapo hapo.

“Pumbavu kabisa huyu mtoto mafunzo yake ni ya ajabu mno , hii ni aina ya mbinu ambayo sikuwahi kukutana nayo”Aliongea mmoja wapo akihema kwa tabu huku akijitahidi kusimama.

“Wote kwa pamoja tushambulie..”Aliongea Tang Diashan na wale wazee baada ya kupewa amri hio waliunganisha nguvu zao zote kwa pamoja ili kumshambulia Roma na kila mmoja aliachia siraha yake , kuna walioachia sumu ya Bindii, kuna walioachia siraha yao maarufu ya Chura Chuma, Emei Ying , Muwako wa Yang na nyingine nyingi ilimradi tu kumdhuru Roma sasa waliziunganisha na nguvu zao zote za kishirikina na zile za kijini ili Roma ashindwe kuzizuia , lakini Roma aliona pigo lao ni kama povu la sabuni linaloelea angani kwani alitumbukiza kidole na palepale pigo lao lenye siraha kupukutika kama majani.

“Mchezo wa kitoto mnao fanya huo”Aliongea Roma huku akitabasamu kifedhuli na kupanga ni kipi cha kuwafanya hao wazee.

Magdalena mwenyewe aliekuwa akiangalia kila kitu alishangazwa na uwezo wa Roma kwani hakudhania nagekuwa na uwezo wa kijini wa juu namna hio.

Tang Dianshan baada ya kuangalia wazee wenzake aligundua walikuwa washajichokea ila hata hivyo hakutaka kushindwa na palepale aliita maneno yake kwa Kimandarini na mkono wake ulijaa na kitu mfano wa parachichi.

“Bomu la Kimilenia la Phosphurus”Aliongea Flamingo kwa wasiwasi lakini Roma kabla hajachunguza vizuri lile tufe mfano wa parachini liliachiwa kwao na kuwapasukia mbele yao na Roma ile anajaribu kujikinga alikuwa amechelewa na ile sehemu waliosimama ilizungukwa na moshi mzito kama mabomu ya moshi wanayorusha wanajeshi lakini harufu yake kama itafikia pua za bindamau wa kawaida basi angekufa hapo hapo.

Alichoweza kufanya Roma ni kujizingira yeye na Mage kwa kujifunika na ngao ya kijini aliotengeneza na kuwakinga kutovuta hewa ile mbaya.

“Rudi nyuma?”Aliutoa amri Tang Dianshan mara baadaa ya kuona ule moshi wote kutopotea bali kuanza kujikusanya kama tufe linalozunguka kwenye mhimili na alijua yote hio ni kazi ya Roma sasa baada ya kuona anawalenga ndio alitoa tahadhari lakini Roma alijua wangekimbia kwani aliachia tayari na wale wazee waliweza kufanikiwa kukwepa lakini kilichotokea ni kwamba nyumba yote ilisambaratishiwa na ni moshi pekee ulionekana na kufanya watu waliokuwa hawaelewi kile kinachoendelea kukimbilia eneo hilo.

“Nadhani sasa mmeelewa kwamba mimi sio saizi yenu , hivyo niambie pango la nayaraka za kumbukumbu liko wapi na angalau nitaacha maiti zenu zikiwa hazijaharibika ili mpate kuzikwa kwa heshima”

“Unatangaza vita na China wewe?” Aliongea Tang Danshan huku akihema kama mbwa.

“Hata muungane na Hongmeng hakuna wakunizuia kupata kile kilichonileta hapa unafikiri ninaweza kuogopa baadhi ya wachina, nimekuja kwa maongezi ya kistaarabu ila mnaleta za kuleta , ambao mnakubali kunipatia ninachotaka nitawaacha hai na mnaolera jeuri nitawamaliza kabisa , sina tabia ya kuacha adui zangu wakiendelea kuishi”

Baada ya Roma kutaja Hongmeng Tang Danshan alionekana kutetemeka na kujijuliza inakuwaje anajigamba mpaka kwa kuwataja Hongmeng bila wasiwasi

“Upo levo ya juu kuliko Levo ya Nafsi?”Aliuliza kwa mshangao huku akijiambia huenda ndio maana kila shambulizi letu alilichukulia la kitoto.

“Inawezekanaje ndio kwanza anaonekana kuwa kwenye miaka ishirini , haiwezekanni kufikia levo ya Nafsi kwa umri huo”Aliongea Tang Luyi akikataa.

“Sitaki malumbano yenu yasio na tija , nimekuja hapa kupata kilichonileta sitaki sura zenu za kusikitisha kuendelea kuziangalia” Lakini Roma hajakaa sawa mmoja wapo wa wazee wale alibadilika macho na kuwa menkundu kama damu na kisha alimfuata kuja kwake kwa spidi isiokuwa ya kawaida , lakini Roma alikuwa na spidi ya kumkwepa na kumuacha apite lakini kitendo kile kilimuacha hoi na kugundua swala lingine.

“Nyie watu inaonekana akili zenu kuna mtu anazitawala”Aliongea Roma kwa Mshangao baada ya kugundua yule mzee hakuwa kwenye akili zake timamu na Roma ashazoea mtu akiwa na macho hayo basi anakuwa ni kama mtu mwenye mapepo.

Lakini Roma alishangaza watu waliozunguka kwa kauli yake akiwemo Magdalena.

Mara palepale wale wazee wengine macho yao yote yalibadilika na kuwa kama mwenzao na ilionekana hawakuwa na mpango kabisa wa kuacha kupigana.

“Roma unamaanisha nini akili zao kutawaliwa?”Aliongea Magdalena lakini Roma alishindwa kujibu papo kwa papo , ukweli alikuwa ashasoma kile kinachoendelea tokea mwanzo ndio maana aliamua kuwachezea shea.

Sasa muda ule ule mzee ambaye alimvamia Roma mpaka kudondoka chini mwili wake ulianza kutuna huku tumbo lake likiwa kubwa na kubipu bipu kama linajazwa upepo na Roma hapo hapo alijua alikuwa akitaka kupasuka kama bomu.

Roma alishangazwa na nguvu ya aina hio ya kumfanya mtu kugeuza mwili wake na kuwa kama bomu , Roma aliweza kufananisha na wale watu wanaojitoa muhanga kwa kujilipua katikati ya watu.

Roma alikuwa akisikia kuhusu mbinu ya kijini za kugeuza mwili wa mtu mwenye nishati za za mbingu na Ardhi na kuwa bomu na kwa namna hio aliamini kama ataacha mzee huyo kupasukia hapo chini yeye asingeweza kudhurika lakini eneo lote lingepata madhara makubwa na kumsabibishia kutopata kile kilichomleta hapo.

Alichoamua ni kumrushuha Mzee huyo hewani ili kama ni kupasuka apasukie hewani..

Na maamuzi yake aliyafanya haraka haraka sana na kutokana na na kuwa na uwezo mkubwa sana wa kijini kurusha mwili kwenda angani halikuwa jambo gumu kwake na mwili ule ulienda juu sana angani na kufanya watu wote kuangalia kwa mshangao jinsi mtu alivyokuwa mdogo kwenye hewa kwa kwenda maili kadhaa juu.

Baada ya dakika moja tu mwili wa yule mzee kule angani ulipasuka na kuonekana nyama nyama , ijapokuwa haukuwa mlipuko wa moto lakini nguvu yake ni kama vile upepo unaosababishwa na bomu linapolipuka kiasi kwanba kama ingekuwa ardhini ingekuwa kama Kimbunga asili.

Licha ya kwamba mwili ulikuwa umepasukia hewani lakini watu wa huku chini waliweza kuhisi msuguano wa hewa usiokuwa wa kwaisda.

Magdalena mara baada ya kushuhudia tukio lile la kutisha alijikuta akimsogelea Roma kwa spidi na kumshika mkono huku machozi yakimtoka.

Roma naomba umsaidie master wangu asipasuke”Aliongea kwa huzuni.

“Usiwe na wasiwasi kila kitu kipo chini ya udhibiti wangu”Aliongea Roma na pale pale alimsogela Tang Luyi na kumshika shingoni kwa namna ya kumminya huku akimwangalia usoni kwa macho makali.

“Sijui wewe ni nani lakini kama unataka kweli mbinu yangu acha kuwa muoga na jitokeze tupambane moja kwa moja”Aliongea Roma na kisha aliachia nguvu isiokuwa ya kwaida ya kichawi na kufanya kitu kama kitenesi kuvimba kwenye shingo ya Tang Luyi na palepale kilipotelea chini na macho yake yakatoka ule wekundu wa damu.

“Sikujua kama umeweza kupitia mapigo ya Radi tisa na kuingia levo ya kuipita Dhiki na leo hili limekusaidia , nitarudi siku nyingine na nakuhakikisha nitakporudi hautokuwa na namna ya kunizidi kama siku ya leo”Ilisikika sauti kwa namna ya mwangwi pasipo ya kuonekana inapotokea.

Roma hata yeye mwenyewe alipagawa alijiuliza ni nguvu gani ya kishetani namna hio ikamfanya mtu huo kuongoza akili za watu , lakini wakati huo huo kutoshindwa kuonekana hata kwa msisimko tu.

Alijimbia huenda kuna uwezekano wa mbinu nyingine ambayo mtu huyo alikuwa akiimiliki ndio maana alishindwa kutambua tokea mwanzo , kwani kama ingekuwa mtu huyo kuwa na nguvu kuliko za kwake basi asingekimbia na angendelea kupambana , lakini kitendo cha kukimbia inamaanisha alikuwa na uwezo mdogo , kitendo cha kutokuonekana pia kilimchanganya sana.

Roma mwenyewe alijiambia kadri atakavyokuwa anazidi kuimarika kwenye mbinu za kijini ndio maadui zake watakavyozidi kuongezeka.
 
SEHEMU 420.

Wazee wale wa kichina hali zao za kiafya zilikuja kutengemaa muda wa usiku baada ya kupumzika kwa muda mrefu.

Upande wa Roma na Magdalena walitumia nafasi ya mchana wote kutembelea maeneo mengi ambayo alikuwa akifanyia mafunzo, Magdalena alionekana kuwa na furaha kweli kuliko siku zote ,kitendo cha kuwa karibu na Roma siku nzima wakiongea na kucheka pamoja kwake ilikuwa ni kama ndoto ambayo hakutaka iishe.

Tokea siku ambayo Roma aliweza kumuokoa Magdalena kutoka kukatwa na panga la Lilith wakati wa kugombania kwa Holygrail ndio mapenzi yake kwa mwanaume huyo yalipoanzia.

Familia yake ilikuwa ikijaribu kumfanyia mchakato wa kuoelewa na Jumbe lakini hakuwa akimpenda kabisa , ijapokuwa Jumbe hakuwa na kasoro kama mwanaume lakini hisia zake kwake zilikuwa mbali na hakuwa akihitaji mwanaume wa aina ya Jumbe , alihitaji mwanaume mwenye nguvu na uwezo kama Roma Ramoni.

Lakini hata hivyo mrembo huyu alikuwa vyema zaidi katika kuficha hisia zake , ni kweli kwamba alikuwa akimpenda Roma lakini kutokana na kwamba Roma alikuwa mume wa rafiki yake wa utotoni , lakini pia mpenzi wa pacha mwenzake aliishia kutotaka kuchukua hatua ya ziada juu ya hisia zake , alijiambia ni kheri kubakia na hisia zake ndani ya moyo wake kuliko kuziweka hadharani kwani isingekuwa na maana yoyote.

Upande wa Roma kwakua alikuwa na uzoefu mkubwa sana na maswala yanayohusiana na wanawake , aliweza kugundua Magdalena kuonekana kuwa na hisia nae za kimapenzi lakini hakutaka kabisa kugusia habari hizo , aliamini zingemletea matatizo makubwa mno sio kwa Mage tu lakini pia kwa mke wake Edna.

Muda wa usiku wakiwa wameketi kwenye miti ya Mianzi waliweza kufuatwa na Tang Luyi ambaye ni Master wake Magdalena.

“Naona wenyewe mmekaa ki wapenzi wapenzi”Aliongea Tang Luyi huku akiwa na sura isioelezeka kama alikuwa na furaha au na huzun huku kauli yake ikimfanya Magdalena kuwa na aibu.

“Mbona unaonekana kukasirika kwani tukiwa wapenzi ni jambo baya?”Aliongea Roma bila ya kumzingatia sana lakini kauli yake ilionekana kuwa kejeli kwa Tang Luyi ukizingatia pia siku zote alikuwa ni mwenye kujiamini na uwezo wake.

“Kwasababu umeweza kutuokoa leo , ninakukaribisha kwenye jamii yetu kwa ukalimu”

“Magdalena naona Master wako akili zake zimekaa sawa mara baada ya akili yake kuachiwa huru”Aliongea Roma kwa namna ya kumkejeli Tang Luyi.

“Nyamaza..!”Aliongea huku akionekana kukasirika , hakutaka hata kusikia kama siku zote za kujiona yupo juu kimapigano kuweza kutawaliwa akili yake kizembe na alichoongea Roma ilikuwa ni kama kutonesha kidonda.

“Roma usimtanie hivyo , ni Master wangu na namheshimu sana lakini pia ni mkubwa kwetu’Aliongea Magdalena a kisha akamgeukia Master wake.

“Master naamini kuna jambo limekuleta mpaka kuja kututafuta huku”Aliongea lakini Tang Luyi alimwangalia Magdalena kwa kumchunguza.

“Vipi maendeleao yako huko Tanzania tokea urudi?”Aliongea na kumfanya Magdalena hisia kumjaa hakuamini Master wake angemjali na kumuuliza swali hilo.

“Asante sana kwa kuuliza Master, Maisha yangu yanaendelea vyema nilikumiss sana”Aliongea kwa sauti ndogo.

“Kama ulinimisi kwanini hukurudi hata kwa zaidi ya mwaka tokea uondoke?”Aliuliza na Magdalena alionekana kukosa jibu la kutoa lakini hata hivyo Tang Luyi alipotezea na kumwangalia Roma.

“Mr Roma najua sasa unao uwezo mkubwa kuliko mtu yoyote ndani ya jamii yetu lakini licha ya hivyo siwezi kukuacha ukamfanya Magdalena kitu kibaya , nilimlea mwenyewe tokea alivyoletwa hapa na sasa amekuwa mtu mzima kwangu nilikuwa namchukulia kama mtoto wangu, wakati alipokuwa hapa sikutaka kabisa ajihusishe na maswala ya mapenzi kutokana na kwamba sikutaka apitie maisha niliopitia mimi mwenyewe”Aliongea na kumfanya Roma kushangazwa na maneno ya Master wake Magdalena hakudhania kama angeweza kuongea hivyo.

“Hivi naonekana mimi na Magdalena ni wapenzi?”Aliuliza Roma na kumfanya Tang Luyi kutabasamu kwa kejeli.

“Nimemlea Magdalena mwenyewe kwa anavyokuangalia tu naona kabisa umemchanganya huyu mtoto ndio hofu yangu ilipo”Aliongea nakumfanya Magdalena atamani kujichimbia kwani siri zake zilikuwa zikifichuka.

“Master siohivyo…”

“Nadhani umekuja kwa ajili ya kutuita kwenye chakula nina njaa sana nadhani litakuwa jambo zuri tukiacha kuongea na kuelekea huko”Aliongea Roma akimkatiza Magdalena na Tang Luyi hakuongea zaidi ya kugeuka na wote kwa pamoja wakafuatishana mpaka kwenye nyumba nyingine kabisa ambayo ni ya Tang Dianshan.

Roma mara baada ya kuingia tu ndani aliweza kufurahishwa na harufu nzuri ya vyakula, wazee wote walionekana wapo ndani ya nyumba hio

Hakukua na viti hivyo mara baada ya Roma kuingia alijitafutia nafasi ya kukaa chini kwenye mkeka huku akiangalia mapande ya nyama ya kuku pamoja na ya kitimoto.

Wachina na Korea ndio moja ya mataifa ambayo wanaongoza kula nyama ya nguruwe ni mara chache sana ukawakuta wanakula nyama ya ng’ombe ni kheri kwao kula nyama ya mbwa kuliko ya ng’ombe.

Basi chakula pale kiliandaliwa na wote kwa pamoja walianza kula huku maongezi yakiendelea, Wazee hao walikuwa wakimhusudu Roma kweli kwani wao walikuwa wamejifunza mbinu za kijini kwa muda mrefu pasipo hata ya kufanikiwa kufikisha levo ya Nafsi , lakini ajabu kwa kijana mdogo kama Roma alikuwa amekwisha kufikisha levo za juu kabisa za mafunzo hayo , lilikuwa jambo ambalo sio la kawaida kabisa kwao na ndio maana walijaribu kumdadisi.

“Wapishi wenu ni wataalamu kweli, Wameweka na baadhi ya dawa za kimitshamba nini, nahisi harufu flani ya kuvutia ya miti kwenye hizi nyama”Aliongea Roma huku akilamba vidole..

“Ni vizuri sana kama umependa mapishi yetu , kwetu sisi ni utamadunni kila linapokuja swala la mapishi tunajali sana faida za chakula kwenye mwili tofauti na utamu wake , wapishi wetu kila siku wanafanya utafiti wa mimea ambayo inafaida mwilini na inayoweza kutumika kwenye vyakula mbalimbali”Aliongea Tang Dianshan na Roma alitingisha kichwa kwa namna ya kuelewa hata hivyo alikuwa akielewa tamaduni za China na baadhi ya maeneo yake ya karibu kuanzia Japani , Korea , Thailland , Ufilipino na China yenyewe, ni rahisi sana kukuta nchi za Ulaya watu kushindia vyakula vya supermarket lakini kwenye mataifa haya ya Asia wengi wanapenda kupika sana na vyakula vyao vinazingatia uwiano sawia wa mahitaji ya mwili na ndio maana vifo vingi ndani ya China kiasilia kabisa ni vya wazee kuanzia miaka themanini kuendelea , ni rahisi kusema kwamba China ni mojawapo ya taifa ambalo watu wake wanaishi miaka mingi sana na wana afya nzuri.

“Vipi kuhusu Pango la Scrolls?”Aliuliza Roma.

“Huh!”

“Mbona mnaonekana kama mnapango wa kunikatilia tena?”

“Hapana hatuwezi kukatalia ,ijapokuwa tunazo sheria lakini kwa ulivyoweza kutusaidia leo tutakuruhusu , hata hvyo unaonakana kutokuwa mtu mwenye tamaa sana”

“Kama ni hivyo mnielekeze lipo upande upi?”

“Ni chini ya mlima upande wa pili wa ngome hii , sio rahisi kufika kwani kuna mitego mingi lakini pia kuna watu ambao wanalinda eneo hilo kama mitego ikishindwa kufanya kazi, kama unataka kwenda huko siku ya kesho basi tutaweza kuondoa vizuizi ili uweze kuingia kwa urahisi”Alijibu Tang Luyi na Roma alionekana kuridhishwa na jibu hilo , mpaka hapo alishafanikiwa kile kilichomleta.

“Mr Roma tunaweza kujua yupo levo gani yule mtu alieweza kuingia hapa na kutawala akili zetu?”Aliuliza Tang Dianshan.

“Sina uhakika yupo kwenye levo ipi , ila ninaweza kukisia yupo mwishoni mwa levo ya Nafsi na inaonekana ameweza kufanya baadhi ya vitu kwa kutumia Dhana, ila kwasasa haina haja ya kuhofia naamini hawezi kurudi tena hapa kwani shida yake ilikuwa ni mimi na mbinu yangu ya Maandiko ya Urejesho”Aliongea Roma na kufanya wazee wote kuwa kimya huku wakiangaliana kwa kiulizo.

“Kimantiki ninaweza kusema kwamba licha ya kwamba siwajui sana Hongmeng lakini kwa uchache ninaofahamu wasingeweza kufanya kitu kama kile , kwani anaonekana njaa yake ni kutafuta mbinu ambayo itamuwezesha kupanda levo ya juu zaidi, nahisi ni jini kutoka jamii nyingine kabisa”Aliongea Roma.

“Haiwezekani”Alijibu Tang Luyi na kumfanya Roma kushangaa.

“Kwanini… kuna mtu mnamdhania?”

“Tumeamua kutokwenda moja kwa moja kwenye hitimisho kutokana na mkanganyiko, Mr Roma wewe una nguvu kubwa sana za mafunzo ya kijini na ni sahihi huko mbeleni kukutana na watu wengi maadui kutoka sehemu tofauti tofauti , labda kwa kukupatia taarifa tu ukiachana na Hongmeng kuna jamii nyingine kabisa ya Majini yenye nguvu”Aliongea Tang Luyi na kumfanya Roma kushangaa.

“Unamaanisha kuna jamii nyingine tofauti na Hongmeng ambayo inatumia mbinu za nishati ya Mbingu na Ardhi?”

“Ndio hio ni jamii ambayo haijulikani sana kutokana na kutokuwa na mwingiliano wowote na China, ijapokuwa hata sisi wenyewe hatujawahi kufika huko Hiongmeng na kujua namna wanavyoishi lakini habari za uwepo wa jamii nyingine yenye nguvu ipo na haina mfungamano wa aina yoyote na taifa hili”Aliongea Tang Luyi.

“Kama haina mfungamano na China inamaanisha kwamba ipo nje ya mipaka ya China au vipi?”

“Hatuwezi kufahamu sana kwani jamii hio imekuwa ni ya siri sana na ni mara chache sana kujionyesha hadharani kama majini lakini jambo moja ambalo tunajua hawafungamani na tamaduni zozote za kichina na wanafanya mambo yao kwa kuzingatia tamaduni zote za ulimwengu , ni rahisi kwenye jamii hizo kukuta majini yenye mwonekano wa rangi ya ngozi nyeusi au kuwa na mwonekano wa kizungu kabisa , inasemekana ni jamii iliostaarabika zaidi kuliko hata Hiongmeng” Roma na Magdalena wote walijikuta wakishangaa kwani habari hio ilikuwa mpya kwao.

“Kuna habari nimeweza kusikia kuhusu jamii inayoitwa Pansas ambayo ndio chimbuko ya mbinu yangu hii ya Kimaandiko ya urejesho?”

“Kuhusu Pansas ni jamii ambayo mpaka sasa inasemekana ipo kwenye habari za kihistoria tu na ni kweli kabisa mbinu ya kimaandiko chimbuko lake ni Pansas hata hivyo hatuna taarifa ya kutosha juu ya hilo”Aliongea.

Katika maongezi hayo Roma alijikuta akikumbuka mwanamke aliekutana nae kule Marekani aliefahamika kwa jina la Rufi , alikummbuka mwanamke yule alitaja Hongmeng lakini wakati huo huo akataja wazee waliofahamika kwa jina la Luo ambapo alidai walikuwa wakimtafuta sasa alijiuliza mwenyewe je mwanamke yule alikuwa ni sehemu ya majini kutoka huko.

“Jina la jamii hio linaitwaje?”Aliuliza .

‘Wanajiita kwa lugha yao , lakini mara nyingi walisikika wakijiita kwa neno la Daiva”Aliongea Tang Dianshan na kumfanya Roma kutoa macho.

“Kwa ninavyojua Daiva ni sawa na kusema Daeva yaani viumbe wasiokuwa wa kawaida na neno hili limepatikana kwenye kitabu cha dini ya Zoloastrian kifahamikao kwa jina la Avestas , dini ya Persia ya kale ambapo mpaka leo kuna washirika wake duniani wanaoamini mungu wao ni Ahura Mazda”Aliongea Roma.

“Unaonekana upo na habari nyingi Mr Roma , unachosema ni kweli lakini hizo ni habari za miaka mingi iliopita , jamii hii kama nilivyosema haingiliani kabisa na maswala ya kidunia na kuna uwezekano hata kuibuka kwa Zoloastrian ilikuwa ni sababu yao”Aliongea Tang Luyi na Roma aliona asirefushe maelezo hayo , alijiambia atafuatilia zaidi na zaidi kwa watu wazoefu.

Lakini hisia mbaya juu ya yule mwanamke zilikuwa zikimtekenya ,kitendo cha kuwa na sumu mwilini iliokuwa imewekwa kijini kilimchanganya.

“Kwahio wenyewe mafunzo yao yanakuwaje?”

“Kwa tunavyojua mara nyingi wakifikisha levo ya kuweza kujitengenezea maumbo ,yaani levo ya Nafsi wanatoka kwenye ulimwengu wao na kuja katika ulimwengu wa kawaida huu wa kwetu kwa mafunzo ya levo nyingine ambayo wenyewe wanaiita kuhuisha miili yao na mapepo yanayowatawala akili zao na wakishafanikisha hilo ndio wanarudi tena kwenye miliki yao wakiwa wapya kiroho ,hawana habari kabisa na dunia kwani malengo yao makuu ni kufikia viwango vya juu kabisa ambavyo mababu zao walishawahi kufikia”Aliongea Tang Dianshan

“Kwahio kwa tamaa zao za kufikia levo za juu tunaweza kukisia kwamba wanaotafuta mbinu yangu ni wao?”

“Hilo haliwezekani huenda kuna kitu zaidi wanachokitafuta hata hivyo inawezekana kuna mtu binafsi ambaye anatafuta mbinu yako”Aliongea na wote walionekan kukubaliana na swala hilo na kuona huenda linawezekana.

Katika mazungumzo hayo Roma aliweza kunasa kitu kimoja , kama maneno yao yalikuwa sahihi basi aliamini huenda kuna watu ambao wapo levo kubwa kuliko yeye au wapo levo sawa na yeye alijikuta akipata tamaa ya kupanda levo zaidi na zaidi.

Siku iliofuata Roma aliweza kuingia kwenye pango la hifadhi ya kumbukumbu , lilikuwa ni pango lakini ndani yake lilionekana kama handaki ambalo lilikuwa limejengwa vyema na ilionekana ni sehemu ambayo ilikuwa ikitunzwa kwani haikuwa na uchafu mwingi.

Roma aliweza kupita kwa walinzi hao wa kichina bila ya tatizo lolote kwani taarifa zake zilikuwa zimekwisha kutolewa na sheria moja tu aliopewa asitoke na kitu chochote, yaani anaruhusiwa kusoma tu lakini sio kubeba hivyo alipewa muda wa siku tatu zote lakini ajabu Roma alitumia siku moja tu nzima kukaa ndani ya pango hilo kusoma na usiku akarudi akipokelewa na Magdalena ambaye alionekana kumsubiri.

“Umefanikiwa , nilidhani utachukua siku mbili”Aliongea Magdalena.

“Kama ulijua nitachukua siku mbili mbona unaonekana kama ulikuwa ukinisubiria?”Aliuliza Roma huku akiweka tabasamu.

“Hakuna ni wasiwasi tu , nimekuja ne wewe China chochote kibaya kikikupata unafikiri nitamwambia nini mkeo na Mage”Aliongea .

“Kwahio wasiwasi wako ni juu ya Mage na mke wangu na sio kwako mwenyewe?”

“Ndio , vipi lakini umefanikiwa?”

“Naweza kusema hivyo nimepata baadhi ya vitu muhimu”

“Una mpango wa kuanzisha mbinu yako mwenyewe tofauti na zilizopo za mafunzo ya kijini?”

“Unaweza kusema hivyo , najua hakuna ambaye ashawahi kuthubutu kuanzisha mbinu rahisi na hiki ndio ninachofanya”Waliongea huku wakitembea na walipofika sehemu ya mianzi sehemu ile ile ya jana yake walikaa chini.

Roma alipotoa simu yake aliweza kuona ‘Missed call’ kutoka Tanzania na alipangalia jina ni Omari , alishangaa na kujiuliza ni kipi ambacho anataka kumwambia mpaka kuchukua hatu ya kumpigia akiwa nje ya nchi.

Roma ilibidi yeye mwenyewe kwanza amtafute kwa kumpigia simu na shukrani kwa laini yake ya simu ilikuwa imewezeshwa kupata mtandao ndani ya nchi yoyote.

“Hades bora umenipigia”Ilisikika sauti upande wa pili ambayo ni ya Omari.

“Kuna shida gani?”

“Kuna uchunguzi nimekamilisha na taarifa niliona sio mbaya kama nitakupatia”Aliongea Omari na kumfanya Roma kuguna kidogo.

“Taarifa gani hizo?”

“Kabla sijaendelea nataka kujua kutoka kwako ni adhabu gani ambayo ulimpatia mke wa raisi wa Rwanda Madam Kizwe?”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kidogo.

“Unataka kusema nini?”Aliuliza Roma huku akijiambia huyu mpuuzi kajuaje alikuwa na bifu na Kizwe.

“Nadhani hata wewe unafahamu vyema juu ya kifo cha Mke wa raisi wa Rwanda , sasa habari ambayo nipo nayo mpaka sasa ni kwamba Madam Kizwe yupo hai”Aliongea Omari kwa sauti ya chini lakini iliosokika vyema kwenye sikio la Roma.

“Kizwe yupo hai , linawezekana vipi hilo?”

“Hapo hata mimi mwenyewe nilishangaa lakini taarifa nilionayo kwanza kabisa ni ya uhakika na mzee wangu pia kaithibirisha lakini jambo la kushangaza ni kwamba Kizwe alikufa kweli”

“Kama alikufa kwahio unamaannisha alifufuka au?”

“Ndio ninachotoka kukuuliza wewe je unaamini uwezekano huo upo maana mimi mwenyewe mpaka sasa nahisi akili yangu haifanyi kazi vizuri, kwasababu taarifa nyeti nliopata hapa aliehusika na kurudisha uhai wa Kizwe ni Yan Buwen na hilo liliwezekana mara baada ya mwili wake halisi kubadilishwa ndani ya ikulu na inaonekana moja kwa moja Raisi Kigombola anahusika katika hili”

“Kwaho unachotaka kusema ni kwamba mwili uliozikwa sio wa Kizwe bali mwili wake ulichukuliwa na Yan Buwen na kisha kurudishwa hai?”

“Hio ndio pointi yangu ya msingi”Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu kifedhuli mpaka hapo kuna hisia zishaanza kumcheza alijiambia kama kweli maneno hayo yatakuwa sahihi basi hata tukio la Salah aliemuua yeye menyewe kwa mikono yake na kisha kufufuka na kwenda kushambulia kwenye familia yake kazi yote hio itakuwa imepangwa na Yan Buwen na kazi ya Ressurection fluid imetumika.

“Hades ninachokuambia ni sahihi kabisa , shushu alieko ndani ya ikulu ya Rwanda alituelezea kwamba mwanaume anaefahamika kwa jina maarufu la Lekcha alipelekwa Rwanda pamoja na Kizwe mara baada ya kutolewa Tanzania na siku ya jana katangazwa kama profesa mpya wa chuo kikuu cha Rwanda upande Fizikia”

Roma baada ya kusikia jina hilo akili yake ilimkubuka mwanaume ambaye alikutana nae Club B , kwa haraka haraka alijiambia huyo ndio atakuwa ndio anaezungumziwa lakini sasa alishangaaa kusikia kwamba amepewa nafasi ya kuwa Profesa.

“Kuna taarifa nyingine muhimu zaidi ambayo unahitaji niifahamu?”

“Ndio ukiachana na jibu ninalotaka kutoka kwako lakini pia nimegundua Yan Buwen ana ushirika wa karibu na Denisi Senga pamoja na Desmond Jeremy”Aliongea na kumfanya sasa Roma kuelewa kwanini siku ile aliweza kumuona Desmond akiwa Tanzania.

“Roma nahitaji huyu Yan Buwen kuondoka kwenye taifa la Tanzania mara moja lakini kuna nguvu kubwa ambayo inamlinda mpaka sasa nimejaribu kuongea na baba na ameniambia niachane na maswala yanayohusiana nae kabisa , jambo ambalo hata sijaliafiki na napanga kuendeleza”

“Mbona unaongea kama swala hili limekugusa sana?”Aliongea ni kweli Omari alionekana kuwa na hasira mno kwa namna anavyoongea.

“Huyu mpuuzi ameharibu maisha ya Queen mpaka sasa , kampa ujauzito na kaukataa na Queen ni kama kachanganyikiwa , halafu ndio mwanamke wa ndoto zangu unafikiri kwanin nisiwe na hasira nae”Aliongea na kumfanya Roma kuguna.

“Basi shukrani zimwendeee Yan Buwen kwa kumkataa Queen kwani na wewe utaweza kupata nafasi”Aliongea Roma huku akitamani kucheka maana alijua ni utani wa kuumiza.

“Hades najua mimi na wewe hatulingani na unapendwa sana na wanawake , lakini mimi ni tofauti sitaki wanawake namtaka Queen wangu mambo yaishe”

“Kwahio unachotaka nikusaidie ni nini?”

“Hili sio swala ambalo unapaswa kunisaidia ila ninachojua ni swala ambalo moja kwa moja linaweza kukuletea matatizo lazima tumchukulie siriasi Yan Buwen”

“Unaonekana kumuogopa sana huyu Yan Buwen , nikukumbushe tu yeye ni mwanasayansi tu na hawezi kunifanya chochote na siku akijichanganya ndio mwisho wake”

“Sidhani kama itakuwa rahisi kama unavyoongea jana niliweza kukutana na Denisi ambaye ni mdogo wako anaonekana kuwa wa tofauti sana”

“Unamaanisha nini kuwa wa tofauti?”

“Kwa taarifa nilizokuwa nazo sijawahi kusikia kwamba ashawahi kujifunza mafunzo yoyote ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi”

“Unachoongea ni sahihi mara ya mwisho nilimuona akiwa na nguvu za ziada lakini zinazosababishwa na kirusi cha Wolverine na niliweza kumponyesha lakini sio hivyo tu mwili wake niliuwekea mtego kiasi kwamba hakuna sayansi ambayo ingefanya kazi”

“Kama ni hivyo kwanini amebadilika na sasa hivi kuwa na levo ya juu ya mafunzo ya kijini?”

“Unamaanisha nini kuwa na mafunzo ya juu ya kijini?”

“Denisi nilikutana nae na anaonekana kuwa kwenye levo ya Nafsi ya mafunzo ya kijini”Aliongea Omari na kumfanya Roma kuona swala hilo haliwezekani hata kama Denisi anaweza kujifunza mbinu hizo si ndani ya muda mfupi huo.

“Una uhakika yupo kwenye levo ya Nafsi?”

“Kwanini nishindwe kujua mtu ambaye yupo kwenye levo sawa na yangu , akili yangu inanielezea huenda kuna kitu amefanyiwa kwenye mwili wake, na hisia zangu zinanielezea kabisa atakuwa Yan Buwen , nikijaribu kuunganisha matukio nahisi hata kilichotokea juu ya meli ya Marekani huenda Yan Buwen akawa mhusika , kama mtu ameweza kufufua mtu, na kuweza kumtengenezea Denisi nguvu za kijini ndani ya muda mfupi anashindwaje kutengeneza kopi yako?”Aliongea Omari na kumfanya Roma kufikiria.

Roma alijiambbia kama ni kweli labda Yan Buwen kuwa na umiliki wa Godstone ndio itakuwa mantiki ya kusema ni rahisi kuweza kufanikisha jambo la kutengeneza kopi yake, lakini akili yake bado haikuwa ikikubaliana na jambo moja , alichokuwa akijua jiwe la kimungu ni moja tu na mtu aliempokonya licha ya kutokuwa na uhakika alijua kabisa atakuwa ni Athena.

Au kuna zaidi ya jiwe moja kama Christen alivyosema?”Alijiuliza Roma , ilikuwa ni ngumu kwake kuamini kama Athena anaweza kushirikiana na Yan Buwen halafu watengeneze kopi yake na kisha wapange njama ya kwenda kushambulia meli ya kivita na kisha kumsukumia makosa yeye , ilikuwa ni jambo gumu sana kwake kuamini kwani ilimaanisha Athena ndio amekiuka The Gods treaty na hata kama afanye hivyo ni kwa makusudi yapi?.

Sasa Roma asichokijua ni kwamba si kweli kwamba Omari alifanikisha kutafuta ukweli kwa shushu wala nini , na sio kweli kwamba alikuwa amekamilisha uchunguzi akiwa peke yake.

Lakini muda huo ambao alikuwa akiongea na simu alikuwa ndani ya hoteli moja ndani ya mji wa Bagamoyo akiwa kwenye chumba cha mikutano huku meza ikiwa imezungukwa na sura zaidi ya saba na maongezi simu yalikuwa yakisiikika kwa sauti , kwani simu ilikuwa kwenye mfumo wa Loudspeaker.

“Ni muda wa kumfanya kuchukulia hili kuwa siriasi”Ilisikika sauti mara baada ya Omari kukata simu.

“Shekhe unamaanisha nini?”Aliuliza Nadia Alfonso.

“Mpango wa pili wa kuongezeka umefanikiwa kwa asilimia zaidi ya sabini na mpaka sasa tuna wajumbe wengi kwa kila taifa, hilo ni la kwanza lakini ninayo habari mbaya na nzuri kwa wakati mmoja nikianza na habari mbaya ni kwamba Athena kafanikiwa kupiga hatua moja mbele kwa kuweza kudhibiti Umoja wa mataifa ya Dunnia(UN), habari nzuri kwetu ni kwamba moja ya mwanachama mkongwe mwenye nguvu ndani ya Illuminat ameamua kutuunga mkono”Aliongea Shekhe Idrissa na sura zote zilizokuwa kwenye meza hizo zilimwangalia kwa mshangao.

“Tunaweza kumfahamu”

“Kwasasa hatuwezi kumfahamu kwani sio kama ni mwanachama mtiifu kwetu bali yupo katikati , labda niwaambie tu licha ya kuwa mwenzetu lakini pia ni mwanachama mkubwa wa juu wa Freemason”

“Mheshimiwa huyo si atakuwa hatari kwetu?”

‘Hata mimi nilifikiria hivyo na wajumbe wengine walifikiria hivyo lakini yeye, hana mpango na kile tunachokifanya anachotaka ni uwiano wa nguvu katika dunia hii , najua anapigania maslahi ya taifa lake lakini ili tuweze kufanikiwa lazima tuweze kula nae sahani moja , kwasasa udhibiti wetu ndani ya bara la Ulaya ni nusu kwa nusu , Amerika ni asilimia ishirini tu , Mataifa ya kiarabu ndio tumepiga hatua na Afrika tunaendelea licha ya changamoto nyingi lakini hata hivyo kumtumia huyu bwana kuongeza nguvu yetu ni hatua nzuri”

“Shekhe kwahio mpango wa tatu ni upi?”

“Mpango unaofuatia ni kumfanya Hades kuchukulia haya maswala kwa uzito wake na Agent Omari hio ndio itakuwa kazi yako kwanzia sasa unahitajika kumfanya aone kile kinachoendelea huku sisi tukiendeleza wajibu wetu”Aliongea Shekhe na wajumbe walionekana kunyamaza.

“Shekhe nipo tayari kwa kazi hio , mpaka sasa nimeweza kumfanya Roma kuwa rafiki yangu na ndio kazi niliopewa mara baada ya kufanikiwa kutoka Hongmeng”

“Hilo halina shaka , lakini tunahitaji zaidi ya urafiki , tunahitaji aanze kuchukua hatua mapema na mtu wa kwanza kumpunguza nguvu ni huyu Yan Buwen”Aliongea na kumfanya Omari kutikisa kichwa na kuelewa.

“Linda umefanya kazi nzuri , kwasasa haina haja ya Jeremy kujua mke wake yupo hai , mtu wa kuwa nae makini zaidi ni mtoto wake Desmond hatutaki kuona anafanya jambo lolote kwa baba yake wala kushawishi serikali ya Rwanda kumuunga mkono , kwasasa wote tunajua ana kisasi na baba yake baada ya kufahamu Edna ni dada yake na hilo naamini kwa kuungana na mama yake ni lazima watalifanikisha”Aliongea na Linda alionekana kuelewa na aliitikia kwamba anajua ni kipi akifanye.

Naam watu waliokuwepo hapo ndani alikuwa ni Mellisa ,Phill, Nadia Alfonso , Omari , Shekhe Assad, Linda na mabwana wawili mmoja akiwa mzungu na mwingine alikuwa ni mhindi ni kundi lile ambalo wanajiita Ant Illuminat wato ambao waliokosekana ni Zenzhei , Afande Kweka na Paster Cohen.

“Chriss karibu sana Tanzania tunatumaini unaifahamu misheni yako”.Aliongea na Chriss aliitikia kwa kichwa.

Naam huyu Chriss hakuwa mwingine bali ni jasusi mstaafu wa kitengo cha Secret service ndio huyu ambaye alimpatia DR Elvice Daniel faili la sauti za maongezi ya raisi wa Marekani bwana Barrack Mabo sasa haikueleweka alikuwa nchini Tanzania kwa ajili ya misheni ipi , lakini jambo la uhakika ni kwamba alikuwa na misheni maalumu ya kufanya , lakini wakati huo huo akiwa ni mwanachama wa kikundi hiki cha Ant-Illuminat yaani wale watu ambao walikuwa na Chata la visiwa vya wafu.

Sasa je Omari ameingiaje pia kwenye kundi hili halafu wakati huo huo akawa na misheni ya kiuchunguzi kutoka Hongmeng?”

MWISHO SEASON 14.
 
SEHEMU YA 321.

Siku iliofuatia Roma na Magdalena waliweza kuondoka ndani ya Ngome ya Tang na kuanza safari ya kurudi nchini Tanzania , Roma alikuwa ashaweza kufanikisha jambo lake na kuna vitu vingi ambavyo alijifunza hivyo kubakia ndani ya taifa hilo kwake aliona ni kupoteza muda.

Saa mbili kamili ya asubuhi ndio waliweza kufika ndani ya uwanja wa kimaitaifa wa mwalimu Nyerere , altumia zaidi ya siku sita tokea aanze safari mpaka kurudi lakini kwake ni kama alikaa muda mrefu kutokana na kuikumbuka familia yake.

Baada ya kupanda taksi moja Mage alianza kushushwa nyumbani kwake na akafuatia Roma kufika nyumbani kwake.

Ilikuwa ni siku ya jumapili hivyo Roma hakutarajia kumkuta Edna kwenda kazini.

Lanlan ndio wa kwanza alieweza kuhisi ujio wa Roma hivyo ile anaingia mlangoni tu alikimbiliwa na Lanlan na kukumbatiwa miguuni jambo ambalo lilimfanya Roma kufurahi mno huku akikukumba amesahau kumchukulia Lanlan zawadi.

“Yaani wewe mtoto unapenda kufanya mambo ya kimya kimya ,si ungepiga simu tukafika kukupokea”Aliongea Blandina ambaye alionekana kuketi eneo la sebuleni huku akiwa ameshikilia kitabu.

“Ningekuwa hata na begi ningesema mje kunipokea , lakini niko mimi kama mimi unavyoniona sijaona haja ya kusumbua watu”Alongea Roma , na ni kweli kabisa alikuwa yeye kama yeye na simu yake tu.

“Dadi umemletea zawadi gani Lanlan?”.

“Zawadi yako inakuja ipo njiani”Aliongea Roma akijaribu kumdanganya Lanlan.

“Unanidanganya”

“Haha.. Roma uwe unamletea mtoto wako zawadi tokea jana mama yake anaongea hapa utamletea zawadi , ila naona umekuja mikono mitupu”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kufikiria.

“Lanlan niambie unataka nini , mimi baba yako nitahakikisha unapata kila unachotaka”Aliongea Roma na Lanlan alitabasamu kwanza huku akionekana kuwaza .

“Lanlan B hana nguo”Aliongea na kumfanya Roma kuikiria Lanlan B anaezungumziwa ni nani lakini alipokuja kukumbuka kuna Lanlan mwingine ndani ya nyumba alijikuta akienda kukaa kwenye sofa huku akicheka.

Lanlan B alikuwa ni mbwa wa Lanlan na tokea aletwe hapo nyumbani Lanlan alikuwa ni kama mtumwa , kuna muda Edna hakupenda mbwa akiingia ndani lakini Lanlan alitaka kumuingiza na kucheza nae sebuleni.

“Okey Baba anaahidi kumnunulia nguo Lanlan B”Aliongea Roma na kumfanya Lanlan kuchekelea kwa shangwe na kumfanya Blandina kujikuta akisikitika kwa kutingisha kichwa.

“Mom kuna chochote kitu nina njaa ya asubuhi”

“Tushakunuwa chai tayari ,jikoni yupo Bi Wema nenda kamwambie akupatie tulichobakisha”Aliongea Blandina na Roma alimuweka Lanlan kwenye sofa na kuelekea jikoni na kumkuta Bi Wema akiwa kwenye pilika pilika zake kama kawaida.

Bi Wema baada ya kumuona Roma amerudi alifurahi na kumwandalia kilichobakia kwa kupasha moto haraka haraka na kumpatia.

“Bi Wema Edna kaenda wapi?”Aliuliza Roma kwani tokea afike hajahisi kabisa uwepo wa mke wake”

“Miss kaenda kuchukua mazoezi ya kukimbia huko nje”Aliongea na kumfanya Roma kutoa macho.

“Kaenda kuchukua mazoezi?”

“Ndio siku hizi tatu tokea uondoke alikuwa akichukua mazoezi binafsi jambo ambalo limetushangaza na kujiuliza kwanini kaanza mazoezi”Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu , hakuamini Edna swala lake alichukulia siriasi mapema hivyo.

Kwasababu Roma hakuwa na maelezo ya kutosha kwa Bi Wema alienda na chakula chake hadi kwenye meza na kuendelea kula , huku eneo la sebuleni mama yake pamoja na Lanlan wakionekana wametoka.

Wakati anamalizia kula ndio muda ambao Edna alivalia kijipensi pamoja na tisheti aliingia hapo ndani akionekana kuhema na kumfanya kumshangaza Roma kutokana na staili yake aliovaa.

Edna mwenyewe hakutarajia kama angemkuta Roma na walijikuta wakiangaliana , lakini macho ya Roma yalikuwa kwenye mavazi tu .

“Umeniangalia vya kutosha”Alivunja ukimya Edna mara baada ya kuona aibu maana manyonyo yake yaliotokeza kama mishale yalikuwa yakijionyesha mno.

“Sijatosheka bado…Halafu Wifey wapi ulikuwa unafanyia jogging?”

“Nilizunguka kwenye hio barabara kupitia nyuma na kuja kutokezelea kule mbele karibu na Nyumba ya Mama T”Aliongea Edna.

“Nini!.. Yaani umeenda kuzunguka kote kule ukiwa hivyo na kuruhusu mimacho ya wanaume wenye njaa kukuangalia , kwa staili ya uvaaji huo haiwezi kuendelea kuanzia kesho , kama utakimbia utavaa suruali za track”Aliongea Roma na kumfanya Edna aanze kujichunguza , yeye alijiona yupo kawaida tu lakini alijiambia inakuwaje huyu mtukutu kuona wivu kwa kuvaa hivyo.

Ukweli Edna alichovaa kwa mwanaume yoyote huko mtaani angekuwa kwenye hali mbaya kwani pensi alilovaa lilifanya miguu yake ilionona na milaini kuonekana wazi wazi na hicho ndio kilichokuwa kikimuuma Roma na kuona wanaume wenzake walifaidi.

“Sio kwamba nilikuwa mwanamke pekee niliekuw anikichukua mazoezi , walikuwepo wengi kwanini waniangalie mimi miguu yangu tu”Aliongea Edna huku akijisikia vizuri kwa wakati mmoja kwa namna ambavyo Roma alionenyesha wivu.

“Naweza kujitutumua na kukuangalia juu mpaka chini kwasababu nastahili kufanya hivyo , Hawa wanaume wa barabarani hwatakiwi hata kukusogelea , unaweza kusema mimi ni mchoyo lakini sijali na kuanzia sasa nakuruhusu uwe unavaa kama hivyo ukiwa hapa nyumbani lakini ukienda kukimbia ni mwendo wa suruali kuu kuu , usipo nisikiliza nitakufuata huko huko na nitakuweka begani na kukurudisha nyumbani”Aliongea Roma na kumfanya Edna kushangazwa na maneno yake , lakini hata hivyo alikuwa akimjua Roma anachoongea ni kama sheria hivyo alijimbia inabidi atii hivyo.

Edna alienda juu na kuoga haraka haraka na kisha akavaa nguo za nyumbani na kurudi chini na alimkuta Roma alishamaliza kunywa chai na amekaa kwenye masofa akiangalia runinga, hakumuongelesha bali alinyoosha moja kwa moja mpaka jikoni na kisha akatoka na sahani iliojaa vipande vya keki vilivyokatwa katwa na kwenda kukaa pembeni huku akila na kumfanya Roma kumwangalia.

“Hizo umetoa wapi?”

“Jana Mama yake Nasra aliniletea akisema ni zawadi kwangu”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa.

“Mama yake Nasra amekuja hapa , Mwenyewe?”

“Hapana aliletwa na Nasra na kuondoka”

Ni kweli jana yake Mama yake Nasra aliweza kufika ndani ya familia hio kutoa shukrani kwa familia ya Edna kwa kile walichokifanya kwa mtoto wake Nasra katika kumsapoti katika masomo yake na kufikia hatua aliokwisha kufikia.

Mwajuma aliongea na Edna kumuombea msamaha pia mwanae kwa kujihusisha na mume wake lakini Edna alimwambia hana kinyongo na Nasra kwani hata yeye alikuwa akitafuta furaha , kitendo cha Edna kumuelewa Nasra juu ya hisia zake kilimshangaza mno Mwajuma ambaye ni mama yake Nasra , ilikuwa ni ajabu kuona mke kumkubali mchepuko kirahisi.

Sasa alimletea Edna zawadi ya keki ambayo kwa maelezo yake yeye ndio aliehusika kuipika kwani alikuwa na uzoefu katika maswala ya mapishi.

“Kwaho alivyokuja alikwambia nini?”

“Aliikuja kumshukuru Mama na Bibi kwa kusimamia masomo ya Nasra , lakini pia kuomba msahama kwa mwanae kutembea na mume wangu”Alijibu Edna huku akila kijikeki chake huku akiwa anaangalia runinga na kumfanya Roma kutabasamu kwa uchungu kwa kauli hio.

“Babe kwa jinsi ninavyona unavyofurahia hio keki ni lazima mambo yalienda vizuri hio jana , mimi najua nilioa mke mwenye roho nzuri , nadhani ni jambo jema pia siku moja moja na Nasra kuja hapa nyumbani na kupiga piga stori hehe..”Alitania Roma.

“Wewe usithubutu , unafikiria sijui unachopanga na unafikiria nimekubali matendo yako moja kwa moja”

“Ninakutania mke wangu , hata hivyo nadhani unakumbuka mkataba wetu wa amani tuliokubaliana siku ile?”Aliongea Roma na kumfanya Edna kurudisha kipande cha keki kwa hasira kwenye sahani na kisha kumpotezea na kimya kikatawala.

Baada ya dakika kama ishirini hivi za kuangalia taarifa ya habari ya kituo maarufu cha Aljazeera Roma alisimama na kujivuta kama kawaida yake.

“Ninatoka kidogo naweza nisirudi kwa ajili ya chakula cha mchana”Aliongea Roma.

“Ndio kwanza umefika halafu ndio unaonaoka?”Aliuliza huku akikunja sura.

“Siendi mbali sana , nitawahi kurudi”Aliongea Roma huku akipiga hatua kwenda juu akipanga kwenda kuchukua ufunguo wa gari , lakini alijikuta akihisi ubaridi wa mwili mara baada ya kuangaliwa na macho yasiokuwa ya kawaida na Edna.

“Inaonekana tayari ushawakumbuka wapenzi wako na ndio unakwenda kukutana nao , haishangazi chakula tulichobakisha kikatosha kukushibisha , ninachoona hukushiba ila uliacha nafasi kwa ajili ya chakula cha mchana na mchepuko wako , Naomba nikushukuru baba mapema kwa kutokusubiria chakula cha mchana maana tutapika chakula kidogo ,unaonekana kuwa mkarmu sana kwanini usipate kabisa chakula cha usiku huko huko ukirudi ushashiba..tena hapana itafaa zaidi ukirudi asubuhi bajeti zitapungua”Aliongea Edna kinafiki na kumfanya Roma kumwangalia .

“Kuna maelezo ya mbinu mpya nilizopata huko China nataka kuona kama zitafanya kazi kwa Rose ndio maana natoka , siwezi kuanza na wewe kwasababu bado mwili wako haujakomaa kimazoezi”Aliongea Roma lakini Edna alichukizwa na maelezo yake marahisi , hata hivyo alijua asingeweza kumzuia kufanya kile anachotaka.

“Kwaho ni lini nitakuwa tayari na mimi kujifunza?”

“Inabidi nisubiri kwanza nionea maendeleo yako , mwili wako ni dhaifu mnno kuliko unavyojiona mwenyewe , tabia yako ya kufanya kazi muda mwingi , kutokula vizuri na kutochukua mazoezi kumekufanya kuwa dhaifu kuliko wenzako wote , kwanzia sasa achana na kula makeki hayo yenye sukari nyingi na piga mazoezi, ukiwa tayari utaanza”Aliongea.

Ni Kweli Edna alionekana kuwa dhaifu mno , hakuwa na nguvu kuliko warembo wake wote na ndio maana Roma hakutaka kumfanya kujifunza mbinu zake , kwani zingemletea shida na huenda asingeweza hata kupanda levo.

“Usiwe na wasiwasi kama utaendelea hivi ndani ya miezi miwili ijayo unaweza kuwa vizuri zaidi zaidi na kuanza”Aliongea na Edna aliitikia kwa kichwa huku akijiambia hata hivyo miezi mwili kwake haikuwa mingi sana.

“Halafu Sophia na Qiang Xi , sijawaona wameenda wapi?”

“Sophia kaenda kumsalimia babu yake Mzee Athumani , nasikia ni mgonjwa na atakaa huko kwa muda , kuhusu Qiang Xi nimemuomba kwenda na Derick Kiwangwa kupeleka mahitaji ya watoto”Aliongea Edna na Roma alitikisa kichwa na kisha alipandisha juu na ndani ya madakika kadhaa alishamaliza kujiandaa na kuondoka kuelekea Kimara anapoishi Dorisi na Rose.

Haikumchukua muda mrefu kufika na ile anaingiza gari alikuja kupokelewa na Dorisi ambaye alikuwa amevaa khanga moja tu , kiasi kwamba Roma alishangazwa na uvaaji wake halafu akaja kufungua geti.

“Unafunguaje geti ukiwa umevaa hivyo? Kuna watu wabaya sana ndani ya hili eneo”Aliuliza Roma

“Nilichungulia kwanza na kuona gari yako ndio maana na hata hivyo hapa kuna ulinzi wa kutosha Rose watu wake wanalinda”Aliongea Dorisi mara baada ya Roma kushuka kutoka kwenye gari na kisha wakakumbatiana na Roma alimbeba juu juu.

“Umeniletea chochote kukota China?”Aliongea na kumfanya Roma kujilaumu kwanini amesahau kumletea zawadi.

“Siku nyingine naahidi sawa?”

“Nilijua tu utanisahau tena kuniletea zawadi”Aliongea kwa kulalamika

“Babe nakuahidi nitakupa zawadi nzuri tu”Aliongea huku akimuweka kwenye sofa na kumshika pua.

“Rose yuko wapi?”

“Katoka kuelekea Kisarawe”Aliongea Roma na kutingisha kichwa huku akiangalia umbo zuri la mrembo Dorisi.

Kivazi alichovaa kilikuwa kikitamanisha kweli na ni sahihi kusema ni kwasababu alikuwa akiishi na mke mwenzake ndio maana alikuwa akijiachia kwa namna hio.

Roma alipeleka mkono mpaka kwenye miguu ilionona ya Dorisi na kuanza kuipangusha pangusa kupanda juu.

“Unafanya nini ,ndio nimetoka kuoga tu sasa hivi jamani Roma”

“Ndio maana sitaki kupoteza hii nafasi”Aliongea Roma na kabla hajajibu Roma alimwinua tena na kumpandisha vizuri kwenye sofa juu na kumkalia kwa juu na kufanya nguo yote kuacha mwili wake wazi na kisha akapeleka mdomo wake na kuunganisha na wa Dorisi na kuendelea kupigana denda huku , mkono mwingine ukitalii kwenye mwili wa mrembo huyo kwanzia juu kwenda chini na kumfanya Dorisi kutoa mlio mara baada ya kuzidiwa na hisia kali na kujisahau kabisa kama alikuwa aneo la sebuleni.

Roma na yeye baada ya kuona mzuka umempanda alitoa nguo zake haraka haraka na kubakiwa na boksa tu na kisha aliendelea kumwadhibu Dorisi kwa zaidi ya dakika arobaini na tano kwa kucheza na sehemu zenye ashiki za mwili wake.

Wakati sasa anashuka boksa yake na kutoa mtalimbo kwa ajili ya kufanya… mara ….

“Boom ! , Boom , Boom!!”

Ulikuwa ni mlipuko wa aina yake ambayo ulimfanya Roma palepale kupotea na Dorisi kwa haraka sana na kutokezea nje hukua akiwa amemkinga , haraka haraka alijua lazima litakuwa ni bomu.

Dorisi baada ya akili yake kufanya kazi aliweza kushuhudia jumba lake likifuka moshi mwingi na moto ukiwa unawaka na kujikuta akitetemeka mno.

Roma alijua lazima hilo ni bomu lilikuwa limetegwa ndani ya nyumba hio na ni kama alikuwa akisubiriwa yeye kuingia ndio liteguliwe.

Kwasababu wote walikuwa uchi palepale alimwambia Dorisi asubirie na alipaa na kwenda kutua kwenye balkoni ya juu ambayo bado hakuwa imeshikwa na moto na kuingia kwenye mojawapo ya chumba ambacho kilikuwa cha Dorisi na kisha akatafuta nguo chache na vitu muhimu na kutoka navyo na kisha akampatia Dorisi mavazi na yeye akavaa Track.

Roma hakuwa na muda tena wa kuendesha gari kuondoka eneo hilo ila alichokifikiria muda huo ni kumuondoa Dorisi hapo kwa njia zake za kijini na aliweza kufanya hivyo ndani ya dakika alikuwa ashamfikisha nyumbani kwake Oysterbay na kumlaza kwenye chumba chake akiwa amepoteza fahamu.

Roma baada ya kutoka mtu wa kwanza kumuona ni Blandina mama yake na kwasababu Roma alichafuka kwanzia kichwani Blandina alimshangaa.

“Nini kimetokea mbona uko hivyo?”Aliuliza Blandina na sauti yake ilisikiwa na Edna ambaye na yeye alimsogelea Roma huku akionyesha hali ya wasiwasi na Roma alielezea kile kilichotokea na Edna aliogopa mno.

“Kwaho hujapata majeraha? , vipi Dorisi?”Aliuliza Edna kwa wasiwasi.

“Ni bahati niliwahi la sivyo huenda angedhurika , kwasasa nimekuja nae na nimempuzisha kwenye chumba changu kwani yupo kwenye mshituko , Edna nisaidie kumwangalia natoka tena”Aliongea Roma huku akijaribu kujipapasa na kugundua simu aliacha kulekule Kimara.

“Naombeni mwenye simu yoyote aniazime mara moj nitaondoka nayo”Aliongea Roma na Mama yake ndio aliekuwa wa kwanza kutoa yake na kumpatia.

“Roma kuwa makini unakuoenda”Aliongea kwa wasiwasi na Roma alimtoa wasiwasi na kisha akatoka nje kabisa huku akipiga simu.

“Your Majest Pluto I have been trying to Contact you but your phone isn`t connected , There has been an issue with Miss Rose”Aliongea Diego akimaanisha kwamba kuna tatizo ambalo limempata Rose.

“Unamaanisha nini , si niliwapa pia maelezo kuwa nae karibu”Aliuliza Roma.

“Miss Rose alikuwa Kisarawe na Adeline alikuwa nyuma yake akimpatia ulizni kwa siri, lakini mara baada ya kuingia kwenye jumba moja ambalo ni la kwake ulitokea mlipuko mkubwa na kubomoa jengo lote, tumeweza kupata taarifa za tukio mara baada ya Adeline kupiga simu kuomba msaada na ilionekana aliwahi kuingia kabla ya mlipuko na anatoa taarifa kwamba Rose yupo salama , lakini yeye kaumia na hawezi kutoka mpaka msaada”Aliongea Diego kwa kingereza na kumfanya Roma kung’ata meno kwa hasira.

“Diego hili nitalifanyai kazi mimi mwenyewe , toa baadhi ya vijana wagawane kwenda Kimara kuangalia kama kuna milipuko iliobakia na pia wengine watoe ulinzi kuzunguka nyumba yangu”Aliongea Roma na mara baada ya kumaliza alimpigia simu Nasra.

“Uko wapi?”

“Nipo nyumbani , kumbe usharudi?”

“Ndio nisharudi na nipo katikati ya tukio kwasasa siwezi kukupa maelezo ya kutosha ila nataka utoke na mama yako na uende nyumbani kwangu mkatulie kule mpaka nitakaporudi”Aliongea .

“Roma kuna nini , unanitisha”

“Fanya hivyo , Edna atakuelezea”

“Okey ngoja tufanye hivyo”Aliongea na Roma alitaka simu na kuvuta pumzi ya ahuendi , alijua kuna adui huenda anajaribu kutumia wanawake wake kujaribu kumdhuru na ndio maana aliona achukue tahadhari mapema, kwa upande wa Amina aliamini atakuwa sawa kutokana na ulinzi wa baba yake anaomuwekea , lakini hata hivyo hakutaka kujiridhisha kwa hewa , alichokifanya ni kuandika meseji kwa haraka haraka na kisha akaituma kwa Amina na kisha akaweka simu mfukoni na kutoweka.
 
SEHEMU YA 422.

Roma hakupata tabu ya kuweza kwenda kwenye nyumba ya Rose Kisarawe kwani alikuwa akiifahamu kutokana na kwamba alishawahi kufika hapo , hivyo alikuja kutokezea mbele ya nyumba hio na ni kweli maelezo ya Diego yalikuwa sawa kabisa kulikuwa na uharibifu mkubwa wa nyumba hio , huku watu nje wakiwa wamekusanyika.

Roma hakutaka kuzubaa baada ya kufika alipita watu haraka haraka na kisha akaingia ndani ya ukuta kwa njia zake , alikuwa ashaupata welekeo wa Rose tayari kwani alitumia uwezo wake wa kijini kuwatafuta na walionekana walikuwa ndani ya eneo la chini kabisa na ndio maana walionekana kushindwa kujiokoa na kutoka kutokana na kufunikwa na ukuta mmoja.

Kwa uharibifu huo Roma alijiambia wahusikaji sio watu wa kawaida kabisa na ilionekana mlengwa mkuu alikuwa ni Rose pamoja na yeye.

Roma alitumia nguvu zake za kijini kuanza kutengeneza njia na ndani ya sekunde chache tu aliweza kuingia kabisa mpaka sehemu ya ndani na hapo ndipo alipoweza kumshuhudia Adeline akiwa ameshikilia ukuta kwa mikono yake miwili ili usiwandokee , sehemu waliokaa ndio seemu pekee ambayo ilikuwa na uwazi huku Rose alionekana kuwa chini.

Adeline alionekana kuumia kweli na kama Roma angechelewa kidogo tu basi angeweza kupoteza fahamu na kuachia ukuta na kuwadondokea hata damu zilikuwa zishaanza kumtoka mdomoni na Adeline alijikuta akihema kwa ahueni mara baada ya kumuona Mfalme Pluto.

Lakini muda ule ule Roma alihisi uwepo wa watu ndani ya eneo hilo na watu aliowahisi walikuwa wakiashiria hatari , lakini kwasababu alitakiwa kuwaondoa Rose na Adeline kwanza hapo , ndicho alichofanya.

Alienda ndani ya eneo ambalo Adeline alikuwa ameshikilia ukuta wa zege usiwadondokee na kisha akamwambia atashikilia yeye na amtoe kwanza Rose hapo chini na Adeline alielewa somo na haraka haraka aliachia ukuta na Roma aliushikilia na mkono mmoja tu na baada ya Rose kutolewa na Adeline mpaka nje Roma kwa spidi ya ajabu aliachia ukuta na kutoweka kwa wakati mmoja na kutokea eneo la nje la bustani.

Aliamua kutokezea huo upande kutokana na kwamba alikuwa akihisi hatari kutokea upande huo , lakini ile anatokea ni kama alichelewa kwani aliona mtu akiruka ukuta na kutokezea upande wa pili eneo la msituni.

Nyumba ya Rose ilikuwa imejengwa pembezoni mwa msitu wa hifadhi ya Kizimzumbwi , ni eneo ambalo limejitenga sana , sehemu iliofahamika kwa jina maarufu la Ngekewa , si ajabu kujenga huko kutokana na biashara yake ya madawa ya kulevya.

Roma hakutaka sana kuchelewa alichokifanya na yeye ni kupotea , kuna kitu alihisi ambacho kilimfanya kutabasamu kifedhuli kwanza kabisa mwanaume ambaye aliruka ukuta hakuwa mtanzania kwani alikuwa ni mzungu tena wa rika kama miaka arobaini kwenda mbele hivi ndio maana alijiambia kuna uhusikaji wa watu wakubwa sana kwenye tukio hilo.

Muda huo huo wakati Roma akiwa anamsaidia Rose na Adeline , ndani ya msitu wa Kizimzumbwi lilionekana kundi la watu ambao wamevalia mavazi ya kawaida tu wakiwa kama watalii, mbao walikuwa wamebeba mabegi mazito mazito meusi na watu hao ni kama walikuwa wakisubiria kitu kwani walikuwa wamejikusanya pamoja huku wakiangalia uelekeo wa eneo la barabarani.

Muda ule ule wakiwa kwenye kusubiria mara alitokezea mtu mbele yao kwa namna ambayo wao wenyewe walishindwa kuelewa na hata wakaacha kuongeleshana na macho yao yore yakamwangalia mwanaume aliekuwa mbele yao, Alikuwa ni Roma.

Roma mara baada ya kusimama mita kadhaa mbele yao macho yake yalishuka kwenye mabegi ambayo walikuwa wameshikilia na alianza kuyachunguza kichawi na kutabasamu , baada ya kuona alichokuwa akihitaji , ukweli haikueleweka aliwezaje kugundua watu hao , kwani aliekuwa akimfukuzia ni yule aliemuona akitokomea juu ya ukuta.

“Curl Gustav Missile Launchers Are you from Swedish?”Aliuliza Roma mara baada ya kugundua ndani ya mabegi yale ambayo yalionekana kama ya kitalii kuwa na moja ya siraha ya kutupia bomu kwa umbali, mpaka hapo aliamini nyumba ya Rose sio kwamba imetegwa bomu bali kilichofanyika ilipigwa na bomu kwa mbali , jambo hili lilimshangaza kwani umbali mfupi kutoka hapo kulikuwa na kambi ndogo ya jeshi la Tanzania

“Who are you..”Aliuliza mmoja wa wanaume ambaye alikuwa na nywele ndogo nyeupe ambazo zimeacha uwalalaza, yeye na wenzake wote walikuwa kwenye mshangao.

“Cul Gustav Missile Launcher ni siraha maalumu iliotengenezwa na jeshi la Sweeden, kuna kitu kinaniambia hampo hapa nchini kwa niaba ya serikali bali inawezekana mkawa ni wanajeshi wa kukodi , hususani wale ambao mmestaafu kutoka jeshi”Aliongea Roma kwa lugha ya ki Swedish na kuwafanya wale watu kushangazwa na uwezo wake wa kuongea bila kumung’nya maneno.

“Sasa kama umetujua ndio nini , Unaweza kuwa na spidi lakini huwezi kutuzidi sisi Lapland Rangers , wanajeshi wa juu kabisa kutoka jeshi la serikali ya Sweeden , nini kinakupa kujiamini kwamba tunaweza kukuacha hai hapa mara baada ya kutufahamu?”Aliuliza yule bwana mzee mzee wa kama miaka hamsini hivi na aliongea kwa lugha yao.

Roma alijikuta akishangaa mara baada ya watu hao kujitambulisha kutoka kundi wanalotokea .

“Lapland Rangers Mercenaries group?”Aliongea Roma kwa mshangao kidogo.

“Inaonekana ushawahi kusikia kuhusu sisi”Aliongea mwingine kwa namna ya kujivunia.

Lapland Ranger ni kama The Eagleas au Wagner Group, katika ulimwengu wa kawaida inafahamika kwamba kikosi cha Lapland Ranger ambacho kilikuwa chini ya jeshi kilifutwa , lakini hio sio kweli kabisa, Kikosi hicho kutoka Sweeden hakijawahi kufutwa na mpaka leo hii kipo na kilichofanyika ni kwenda ‘underground’ tu mara baada ya kutangazwa hadharani kimefutwa, ni kama ilivyokuwa mwanzo kwa Wagner Group kutofahamika au kama ilivyo kwa The Eagles kutofahamika.

Ni kikosi chenye weledi wa hali ya juu sana likija katika medani za kombati kwenye maswala ya kijeshi na inasemekana mafunzo ya kikosi hiki hufanyikia ukanda wa kusini mwa dunia eneo ambalo hufahamika kwa jina la kingereza kama Arctic cycle.

Wanafundishwa kwenye baridi kali na kupitia mafunzo maagumu sana ili kuwa vizuri na operesheni zao kubwa ni kufanya Patrol kwenye umbali mrefu sana , kufanya mashambulizi ya umbali mrefu na kuingia ndani ya mipaka kwa siri sana pasipo ya kujulikana na serikali yoyote , yaani wanao uwezo wa kuingia Tanzania wakapiga misheni yao kimya kimya na kisha wakapotea na wasijulikane wala kuacha kivuli chao.

Kipindi cha nyuma Roma akiwa kama Ajent 13 ashawahi kupewa kazi ya kwenda kufanya mauaji ndani ya kambi ya kikosi hiki ukanda wa Arctic cycle na aliweza kukamilisha kazi yake pasipo hata kupigana na kundi hilo la wanajeshi.

Lakini sasa Roma anajua watu hawa watakuwa wanahusika na kuweka mabomu ndani ya nyumba ya Rose na Dorisi kule Kimara lakini pia na hapo Kisarawe swali lililoibuka kwanini wafanya hivyo.

Lakini Roma katika kuwaza , mara akili yake ilipata kitu , katika moja ya maadui wakubwa wa Rose alikuwa ni baba yake mzazi na alikuwa akikumbuka kipindi cha nyuma alishamweleza kwamba alimpeleka Ujerumani kwenye moja ya kisiwa kilichopo ndani ndani.

Roma aliamini kuna uwezekano Situ kuweza kusafiri mpaka Sweden na kuweza kushawishi kundi hilo kwa kuwalipa ili kuja Tanzania kulipa kisasi..

“Mmetumwa kuja Tanzania na Situ?”Aliuliza Roma.

“Unaongea nini , hatumjui mtu anaefahamika kwa jina hilo sisi , Vijana hatuna haja ya kumcheleweisha huyu mtu , tunahitajika kupotea kwenye hili eneo muda huu , mpigeni risasi tuondoke”Aliongea yule mzee na palepale mmoja alitoa siraha yake na kumlenga Roma , lakini ile Risasi haikumfikia Roma na kuwafanya kushangaa kwani Roma hakusogea kabisa na baada kuona tukio hilo haraka sana walitoa wote bastora na kuanza kumlenga kiasi cha kusababisha eneo lote kuwa na makelele ya milio ya bunduki , lakini risasi zote ni kama zilikuwa zikimuogopa Roma ambaye alikuwa amesimama akiwangaalia.

Baada ya kushangaa kwa tukio hilo na kumuona Roma kama kiumbe cha ajabu mmoja alifungua bengi na kutoa Curl Gustav Missile Launcher na kupachika bomu na kisha kumlenga Roma.

Roma alitabasamu kifedhuli kwa jambo lile na baada ya kichwa cha bomu kuachiwa kuja kwake , alichokifanya ni kutengeneza vinyuzi flani kama mfano wa nyumba ya buibui na lile bomu lipokwenda kugusa zile nyuzi lilipunguzwa nguvu na Roma hapo hapo alizungusha mikono yake kwa namna ya ajabu na bomu likanasa angani na hakusubiria hata sekunde ipite aliligeuza kimazingara na kulirudisha lilipotoka na wale wanajeshi walijikuta wakichachawa na kabla hata hawajachukua hatua lilishawafikia na kulipuka mbele yao na ilionekana kwenye mabegi yao pia kulikuwa na mabomu kwani mlipuko uliongezeka na kuwa mkubwa.

Roma aliangalia namna watu walivyosambaratika vipande vipande bila ya kuwa hata na wasiwasi na pale pale alihisi watu nyuma yake na aligeuka kwa spidi na kuachia wimbi la nguvu ya ajabu ambalo lilifanya watu waliokuwa nyuma na wao kufa palepale kwa kutawanyika.

Roma baada ya kuona kazi yake ni njema , alikunja tena mikono kwa namna nyingine bila kueleweka anafanya nini na palepale upepo mkali kama kimbunga ulizingira sehemu ile ambayo ililipuka na wale watu ambao walikufa lakini miiili yao haikuharibika sana ilielelea elea juu na kuyeyuka , mpaka hapo Roma ushahidi pekee alioacha ni wa mchimbuko wa ardhi tu , aliamini jeshi likija kufanya uchunguzi hawatoambulia chochote.

Baada ya kuona ashamaliza aliondoka na kurudi alipotoka na ile anakuja eneo la Ngekewa maili kama moja kutoka Kizimzumbwe , aliweza kumkuta Rose na Adeline wakiwa wanamsubiri nje ya gari.

Rose alimwangalia Roma kwa wasiwasi , huku Adeline akiwa ameshikilia bega lake ambalo lilionekana kuumia , Roma kabla ya kuongea simu yake ilianza kuita mfululizo na alipoangalia jina ni Diego.

“Mfalme Pluto tumeweza kugundua wahusika wakuu waliowezesha mambo yote ni kundi la Tembo Vijana wa Miss Rose , inaonekana wameamua kumgeuka”Aliongea Deigo na kumfanya Roma kushangaa kidogo.

“Mmewezaje kugudua hilo?”

“Tulikamata vijana sita ambao walikuwa wakijaribu kufanya uvamizi ndani ya eneo la nyumba yako na tumekwisha kuwaua wote ndipo tulipogundua wanatokea kwenye kundi la Tembo , inaonekana wanajaribu kudhuru familia yako”Aliongea Diego na kumfanya Roma kuona huenda kilichotokea ni kumtoa nyumbani ili waweze kufanya shambulio nyumbani kwake.

“Hubby kuna sida gani?”Aliuliza Rose aliekuwa kwenye wasiwasi baada ya kuona mabadiliko ya Roma.

“Hivi ulisema ulimpeleka Baba yako Ujerumani?”

“Ndio , nilimpeleka mbali na hapa ili asiwe na nguvu tena, unataka kusema haya yote ni mpango wake?”

“Waliotaka kukuua ni wazungu kutoka Sweeden ambao ni wanajeshi wastaafu , naamini walikuwa wakikulenga wewe na mimi , naamini kabisa adui yetu anatujua vizuri na aliona kwa wanajeshi wa kawaida au majambazi hawawezi kutushinda ndio maana akaamua kutoa pesa nyingi kukodi wapiganaji hao, lazima atakuwa ni baba yako , nadhani alisubiria fursa ya wewe kuachia ngazi ili aweze kupata mtu ndani ya kundi lako kumshawishi kufanya mipango yake”Aliongea Roma na kumfanya Rose kuvuta pumzi za ahueni.

Ila usiwe na wasiwasi , kwasababu amenichokoza mwenyewe nitalipiza kisasi”Aliongea Roma huku akiona ilikuwa ni mantiki , Rose watu aliowapeleka kwenda kulinda nyumba anayoishi hawakuwa watu wake , walikuwa ni watu wa Situ na ndio huenda walitega bomu.

“Kwaho napaswa kufanya nini sasa hivi?”Aliuliza huku akionekana kuwa na wasiwasi.

“Inabidi tusubiri kwanza tupate taarifa kamili ndio nitachukua hatua”

Muda huo huo Zonga aliekuwa kwenye gari aina ya Mercedez aliweza kufika akiwa ametangulizana na baadhi ya vijana.

“Boss , Mister Roma bora mpo salama , nilipatwa na wasiwasi mara baada ya kusikia nyumba uliohamia imelipuliwa na huku pia umefanyiwa shambulizi”Alionea Zonga alievalia tisheti na jeans.

“Mmejua muhusika ni nani?”Aliuliza Roma bila kujali maneno yake.

“Ndio tumeweza kupata habari Situ karudi Tanzania kutokea Sweeden na makisio yetu ni yeye aliepanga njama ya haya yote yaliotokea”Aliongea Zonga.

“Vipi kuhusu eneo alipo kwasasa?”

“Bado hatujaweza kupata uhakika wa eneo alipo”Aliongea Zonga na Roma aliona hana cha kufanya hapo zaidi ya kuondoka , kwanza Adeline alionekana kuwa kwenye maumivu makali.

“Adeline asante sana kwa kumlinda Rose, sasa hivi afya yako ndio kipaumbele”

“Asante sana mfalme Pluto kwa kutambua msaada wangu wangu”Aliongea huku akionyesha kutabasamu kwa furaha.

Baada ya kuongea kwa muda, wote waliingia kwenye gari walizokuja nazo Zonga na kuanza safari ya kurudi , Zonga akikaa mbele huku wao wakikaa nyuma.

“Boss nitume vijana wetu kufanya utafiti wa mahali alipo Situ?”Aliuliza Zonga lakini wakati Rose anataka kuitikia Roma alimzuia.

“Haina haja , Rose nakumbuka ulishawahi kuniambia kundi lenu mmefanikiwa kununua boti ya kifahari?”Aliuliza Roma.

“Ndio ipo bandari ya Dar kwa sasa”

“Zonga nataka ufanye kazi ya kukusanya wahusika wote wanaonufaika na biashara za madawa ya kulevya kutoka kwa kundi la Tembo na wote wakusanyike kwenye hio boti”Aliongea Roma na kumfanya Hata Zonga kushangaa na kujiuliza Roma anataka kufanya nini.

“Mr Roma unaweza kuniambia dhumuni la kufanya hivyo?”

“Fanya kama ninavyokuambia”Aliongea Roma bila kuwa na utani na kumfanya Zonga kuitikia haraka kwa kichwa.

“Waeleze kabisa kuhudhuria ni lazima na ambaye hatofika anajichimbia kaburi”Aliongea Roma na kumfanya Zonga kuitikia huku akiwa na wasiwasi.

Waliweza kurudi ndani ya jiji la Dar nyumbani kabisa kwa Roma na baada ya kushuka nje Zonga aliondoka na Rose alimsaidia Adeline na wakaingia wote ndani ya geti.

“Babe nadhani nifanye mpango wa kununua nyumba nyingine ya kuishi”aliongea Rose.

“Hilo tutazungumza , tuingie kwanza ndani”Aliongea Roma na wote wakaingia ndani ya geti na waliweza kupekelewa na Fanny na wazungu wawili kukamilisha idadi yao jumla watatu.

“Mfalme Pluto tumefanikiwa kudhibiti wasaliti waliofika kufanya fujo hapa nyumbani na tushaweza kusafisha eneo hili”Aliongea Fanny.

“Kazi nzuri nitaongea na Sauroni wote pamoja na Adeline kupatiwa Zawadi pamoja na kuongezewa mshahara”Aliongea Roma na kuwafanya wote kutabasamu kwa furaha.

Roma alimkabidhi Adeline kwa wanajeshi hao na kuwapa maagizo wafanya taratibu za kumpeleka hospitalini kupatiwa matibabu.

Roma mara baada ya kuingia ndani alijikuta akishangazwa na uwepo wa watu wengi eneo la sebuleni.

Alikuwepo Amina ambaye alikuwa akicheza gemu na Lanlan , alikuwepo Nasra, Dorisi pamoja na Lanlan , lakini pia hawakukosekana Qiang Xi, Mama yake Blandina pamoja na Bi Wema.

Nasra na Dorisi walionekana walikuwa wakiongea na Blandina na walikuwa wakisikiliza kwa umakini kama vile wanasikiliza mahubiri.

Mtu wa kwanza kumuona Roma ni Edna aliekuwa amekaa karibu , ambaye alifika hapo akiwa ametangulizana na Rose ambaye alionekana kuchafuka mno..

********

Upande mwingine ndani ya makazi ya mstaafu raisi Kigombola , alionekana kuwa ndani ya chumba maalumu ambacho hupenda mara nyingi kufanyia vikao na watu wake muhimu wanaofika ndani ya jumba lake hilo , ambalo kwake ni kama vile alikuwa bado ni ikulu.

Sasa ndani ya chumba hivho kikubwa kama sebule walionekana watu watano wakiwa wameketi kwenye masofa akiwemo raisi mwenyewe Kigombola.

Moja ya watu hao alikuwepo ni mkuu wa kundi la Black Mamba Bakari Juma , Elvice Temba , Abubakari Hamadi na mheshimiwa mwenyewe.

“Nadhani mpaka sasa mpango umefeli”Aliongea Mheshimiwa akiwa kwenye hali ya utulivu.

“Tokea mwanzo nilisema hili swala tulifanye siku ile ile baada ya Roma kuondoka kuelekea China”Aliongea Juma na Raisi Kigombola alioneka kuwa kwenye hali ya utulivu tu.

“Lakini wewe mwenyewe ndio ulisema hukutaka kuhusika katika hili na Situ ndio afanye kile kinachoweza kufanyika na ndio alichokifanya na sisi tumehusika kumuwezesha pesa tu”

“Najua lakini Situ yule ni mbishi na kufeli kwa huu mpango yeye ndio sababu”

“Yeye ndio kafeli na naamini mpaka sasa hakuna namna ya yeye kuweza kututaja kama wahusika wakuu, nilichokuwa nakusaidia mimi ni kuweza kurudisha utawala wako ndani ya jiji hili la Dar es salam , biashara zetu zimedoda sana kutoka na mwingiliano wa kundi hili la Tembo , lakini hata hivyo naamini nafasi nyingine itajitokeza”Aliongea Raisi mstaafu Kigombola.

“Mheshimiwa kama sio wewe ulienizuia tokea mwanzo , naamini mpaka sasa ningeshalipiza kifo cha mwanangu Karimu”

“Kisasi hakijawahi kumuacha mtu salama , ndio maana kwanzia sasa kila kitu mnafanya kwa maelekezo yangu , Roma mpaka sasa wote mnajua hapa ni mtoto wa Raisi wa nchi hii hivyo ni rahisi kusema kwamba ulinzi wake serikali yetu pia inawajibika..”Kabla hajamalizia kuongea simu ya Mzee Juma ilianza kuita.

“Boss wanufaika wote wa kundi la Tembo wanakusanywa kwa pamoja kwenye boti ya Tembo Cruise Ship”

“Kwanini?”

“Haijaeleweka mpaka sasa , lakini hata wewe pia unahitajika kuhudhuria”iliskika sauti upande wa pili na kumfanya Mzee Juma kumangalia mheshimiwa Kigombola.

“Unapaswa kwenda”

“Unamsemaje mheshimiwa?”

“Namaanisha kwasababu una makubaliano na Kundi la Tembo unapaswa kujitokeza na wewe ili usije ukatiliwa mashaka”Aliongea Raisi Kigombola na kumfanya Mzee Juma kuanza kutokwa na jasho , akiwa haelewi ajibu au anyamaze , lakini muda huo huo mlango ulifunguliwa na akaingia Erick akiwa ameshikilia simu na alienda na kumnong’oneza mheshimiwa na kisha akamwonyesha simu inayopigwa.

“Hapa tushamaliza , Juma utaenda kama unataka kurudisha nguvu ya Black Mamba ndani ya jiji la Dar es salaam na biashara zetu kuimarika”Aliongea Mheshimiwa na kisha alisimama na kutoka.

Baada ya kuingia kwenye chumba kingine alipokea simu ile na kuweka sikioni.

“Kizwe nimekuambia usinipigie mpaka nikutafute mwenyewe , nini unafanya sasa kukiuka makubaliano”

“Kigombola nashukuru sana kwa kunisaidia na mpaka sasa kuwa hai kupitia mwanasayansi wako Yan Buwen, lakini hata hivyo umenipa msaada lakini haimaanishi kwamba nitakuwa mtumwa kwako kwasababu ya msaada ulionipatia”

“Unataka nini kutoka kwangu”

“Nahitaji kurudi Rwanda mara baada ya kumaliza matibabu yangu”

“Hilo haliwezekani kwa sasa na tulishaongea”

“Kama haliwezekani nataka uliwezeshe , Nahitaji mwanangu Desmond kuwa Raisi wa Taifa la Rwanda na kurithi kila kitucha Jeremy na baada ya hapo nataka nimuue Jeremy kwa mikono yangu miwili
 
SEHEMU YA 423.

Alianza Dorisi ambaye aliletwa na Roma na akafuatia Nasra akiwa na sababu inayofanana na Amina ‘tumeagizwa kuja hapa nyumbani kwa usalama wetu’ Nasra alivyofika ndani ya familia hio aliongea hivyo , lakini baada ya kama nusu saa baadae alifika na Amina na yeye akawa na sababu hio kwamba amekuja hapo kwasababu ameambiwa kufika hapo na Roma kwa ajili ya usalama wake.

Blandina aliekuwa akicheza na mjukuu wake Lanlan alishangazwa na ujio huo wa wageni ghafla lakini hakutaka kuuliza maswali mengi kwani Roma alishaeleza hakukuwa na usalama.

Muda huo huo na nyumba nayo ikazingirwa na wazungu ambao waliimarisha ulinzi eneo lote , jambo ambalo halikuwashangaza sana kwasabau walishajua Roma sio mtu wa kawaida , lakini ilikuwa ni nadra sana kuona mwafrika kupewa ulinzi na mzungu ni kama meza zimegeuka.

Edna hakuwa na namna zaidi ya kuwakaribisha wageni ambao anajua ni wake wenzake , alianza na kumwangalia Dorisi ambaye alikuwa hajitambui akiwa chumbani kwa Roma kwa muda na hapo alipotoka sebuleni ndipo alipokutana na ujio wa Nasra na hatimae akaingia na Amina.

Ukweli Amina sio kwamba hakuwa na ulinzi , lakini alipopokea ujumbge kutoka kwa Roma alijiambia ni huko huko kwa mama mkwe akamtambue , alikuwa akijua Roma ana mama lakini hakuwahi kukutana nae.

Blandina kati ya wanawake wa Roma ambao alikuwa akiwatambua kwa kukutana nao na kuwaona ni Nasra halafu pia Amina ambaye anamuona mara kwa mara kama mtangazaji ila wengine hakuwa akiwajua.

Hivyo baada ya nyumba yake kufurika warembo hao , alijikuta akichukua nafasi ya kuwajua zaidi, alivyomwangalia Dorisi alikuwa mzuti m akimwangalia Nasra alikuwa ni mzuri , akimwangalia na Amina uwii alikuwa mzuri balaa , licha ya kwamba Edna alikuwa mzuri kuliko wanzake lakini kuna baadhi ya vitu vingi Edna hakuwa hana , kwa mfano Amina alikuwa mchangamfu sana na kitendo cha kufika tu hapo nyumbani alikuwa ashayazoea mazingira haraka na kila mtu aliekuwepo hata kumpeti mpeti Blandina mara baada ya kujua ni mama mkwe wake, jambo la Amina kupatana kwa haraka na Blandina lilimfanya Edna kuwa katika hali ya wakati mgumu na kuona hatari kwa wakati mmoja.

Blandina yeye kariba yake ni ya kucheka na kila mtu na alikuwa na roho ya ukarimu hivyo alikuwa ni rahisi kuzoeleka na alijikuta akicheka mno kutokana na vituko vya Amina na mpaka akajikuta akijaribu kuwatofautisha na Edna kutokana na sifa zao , lakini mwisho wa siku alijiambua huenda kuna sababu kubwa ya Edna kuwa mke wa Roma tofauti na wanawake hao.

Sasa baada ya Roma tena kuja na Rose mrembo mwingine alijikuta akishangaa zaidi na kujiambia licha ya jambo hilo kutokuwa zuri kwa tamaduni za kiafrika lakini alijivunia kuwa na mtoto mwenye uwezo wa kuweza kuwapagawisha wanawake wazuri kama hao.

Roma mara baada ya kufika hapo hakukuwa na maongezi zaidi , alimpa ruhusa Rose kuweza kusalimiana na mama yake pamoja na wengine na kisha aliaga kwamba anaondoka na Rose kwani hawajakamilisha jambo lao huko nje na hali kuwa tulivu.

Kuhusu wengine aliwaambia waaendeleee kukaa hapo mpaka atakaporudi na mama yake mzazi alimwambia wala asiweze yeye na Edna watahakikisha wageni wanajisiikia huru.

Roma alimkonyeza Edna aliekuwa akimwangalia kwa wasiwasi akionekana kama katelekezwa mpaka na Lanlan mtoto wake, siku zote Edna akimuona Roma akimfanyia hivyo ni kama ishara ya kumwambia kwamba kila kitu kitakuwa sawa.

Roma na Rose waliondoka kuelekea bandari ya Dar es salaam , kwa ajili ya kuhudhuria mkusanyiko wa wanufaika wote wa biashara zinazoendeshwa na mtandao wa kundi la Tembo ambalo wiki kadhaa nyuma kiongozi wake mkuu alikuw ani Rose , lakini mara baada ya Rose kustaafu katika nafasi yake akamwachia Zonga.

Kundi la Tembo ndani ya Tanzania halikuwa dogo , lilikuwa na muunganiko wa watu wengi mno kuanzia wafanyabiashara maarufu , vigogo wa serikali na baadhi ya wasannii mpaka waandishi wa habari.

Kutokana na ukubwa wake ilikuwa sahihi kwa Rose kuwa na pesa nyingi sana, kwani tokea Rose afanikiwe kupindua kundi la baba yake ambalo lilikuwa na makazi ndani ya mkoa wa Mwaza kundi maarufu la Fupa Faru , lakini vile vile Roma alipoweza kumsaidia kupunguza nguvu kundi la Black Mamba ni kama biashara zake zilimaarika sana na kumfanya kuwa na koneksheni nyingi za biashara za siri zinazofanyika ndani ya jiji la Dar es salaam na baaadhi ya maeneo ya karibu na pwani ikiwemo Zanzibar na katika kufanikisha biashara zke kuendelea kwa haraka alikuwa akihusisha watu wengi ambao walikuwa wakipenda pesa kwa njia za haraka na hapo ndipo waliingia watu kama wafanyabiashara , waandishi wa habari , wasanii na vigogo wa serikali.

Ndani ya Bandari ilisimama boti hio kubwa ya kifahari nyenye nembo ya Tembo Cruise Ship, boti hii ilikuwa ikimilikiwa na tajiri mmoja kutoka Sudani na ilipowekwa Sokoni ndipo Rose alipoinunua huku madhumuni makuu ni kuweza kufungua club ndani ya Boti hio kwa ajili ya wale wateja wao wakubwa kuweza kupata huduma zao kwa urahisi , lakini pia wakati huo huo kuweza kufanya biashara kwa urahisi wakati boti hio ikiwa kwenye maji ya kimataifa.

Ilikuwa ni mbinu kubwa sana kwa Rose kufanya hivyo ,kama ilivyokuwa sahihi kwa Edna kuwa kinara wa kufanya biashara za halali ndivyo ilivyo kwa ?rose kuwa na uhodari wa kufanya biashara za magendo pamoja na zile ambao hazikuwa kihalali kisheria ndani ya Tanzania na kilichompa nguvu pia ya kuaminika kwa wateja wakubwa ni pale alipotumia jina la Hades yaani Mungu wa wafu.

Ieleweke Roma licha ya kwamba alikuwa na umiliki wa jeshi lakini pia alikuwa na kundi la kihalifu maarufu kwa jina la New Zero Assasination Group , hili kundi bado lipo na linajiendesha na shughuli zake nyingi zipo ndani ya jiji la Palermo huko Italy na ndio kundi ambalo lilimtambulisha zaidi kama Agent 13, sasa New Zero ndio inayosifika zaidi kwenye ulimwengu usio onekana , ulimwengu wa wahalifu au kwa jina la kingereza Underworld.

Kwahio kitendo cha Rose kuwa na ‘back up’ ya Hades mfalme wa wafu kilimpa wateja wengi wapya tena wale wakubwa, lakini hata hivyo mrembo huyu hakutaka kuendelea na biashara hio zaidi ya kutaka vijana wake kuendeleza , lakini siku chache tu baada ya kutoa madaraka kwa mwingine hali mbaya inaibuka.

Wakati Rose na Roma wanafika na kuingia kwenye boti , bado watu wengi hawajafika bado , walikuwa wakiingia mmoja mmoja kutokana na kwamba wengi walikuwa maeneo ya mbali , hivyo hata matarajio ya watakaofika ni wale ambao wangeweza kupata taarifa za haraka.

Roma hakujali sana alijiambia ambao hawatofika lazima watoe sababu na wengine ambao wapo maeneo ya karibu watawasubiria mpaka kufika., wengi walikuwa wakimjua Rose na wachache walimfahamu Roma katika uhusikaji wa biashara za kundi la Tembo na mara nyingi kwa wale vidume ambao walitamani kumng’oa mrembo Rose waliishia kupata habari za chini chini kwamba kuna mwamba anashikilia na ni ngumu sana kutia mguu kwenye jimbo hilo.

Baada ya lisaa limoja kupita hatimae asilimia zaidi ya tisini walifika na wale ambao walikuwa mbali walitoa taarifa kwamba wamesafiri kutoka nje ya nchi.

Roma alimpa maagizo Zonga kuwakusanya watu wote kwenye sehemu ya kikao na kitendo kicho kilifanyika kwa haraka sana na baada ya watu wote kukamilika hatimae honi ya boti ilipigwa na ikaanza kuondooka eneo hilo kuelekea majji ya katikati ya bahari..

Upande wa Roma yeye alikuwa kwenye chumba chake akiwa na laptop ambayo aliunganisha na Wifi na aliweza kufanya mawasilianao na Sauroni ambaye alikuwa ndani Uingereza.

Licha ya utofauti wa majira kutokana na ‘timezone’ kuwa tofauti lakini Sauroni aliweza kuingia online kwa njia ya Vidio.

Sauroni muda huo alionekana alikuwa akifanya uzinifu , kwani alikuwa na bukta tu na Roma aliweza kuona mwili wa mwanamke nyuma yake , Sauroni alionekana kuwa na mwili uliotuna kwa mazoezi makali kuzidi hata mwili wa Roma.

“Your Majest Pluto although I am aware that you have something urgent to discuss with me, I have t o say you called at a bad time”Aliongea Sauroni kwa Kingereza akimaanisha kwamba ijapokuwa ana jambo la muhimu kuongea nae lakini amepiga muda mbaya, lakini Roma wala hakumjali .

“Nataka unisaidie kutafuta uelekeo wa mtu mmoja hivi , ambaye ameweza kukodi kungi la wapiganaji wa Lapland Ranger kutoka Sweeden kuniwinda mimi pamoja na kundi la Tembo ambalo lipo hapa Dar es salaam , hisia zangu zinaniambia hayupo hapa Tanzania na mipango yake anajaribu kuifanyia akiwa mbali , huenda yupo kwenye meli au boti”Aliongea Roma.

“Naweza kujua jina lake Mfalme”

“Anafahamika kwa jina la Situ Kulubembe”Aliongea Roma

“Nipe nusu saa , haiwezi kuwa ngumu kumfahamu kwa haraka kama wapiganaji wa Lapland Mercenaries wanahusika”Aliongea Sauroni na Roma aliridhika na jibu lake na kukata mawasiliano na kisha akatoka hapo na kurudi sehemu ya kikao.

Boti hii ilikuwa ni kwa ajili ya burudani , lakini leo hii haikuwa kwa ajili ya burudani , zaidi ya wahudhuriaji ndani humo kunywa vinywaji huku wakiongea kwa furaha kupoteza muda.

Rose aliekuwa pamoja na Zonga aliweza kutoa maelezo ya kilichotokea na kufanya watu wote kushangaa , mmoja wapo aliekuwa kwenye kundi hilo ni Juma wa kundi la Black Mamba ambaye pia kundi lake lilikuwa chini ya Rose , hivyo alikuwa hapo kama muwakilishi wa kundi lake.

Kila mmoja aliweza kushangaa kusikia kwamba Situ ameweza kurudi nchini na kuweza kufanikisha matukio ya aina hio , kwani walitegemea angeweza kufia huko huko Ujerumani.

Wakati watu wakijairbu kujadili kilichotokea wao kwa wao Roma aliweza kufika ndani ya eneo hilo.

Roma siku hizi alikuwa akitambulika kwa wengi kama mtoto wa Raisi Senga na hili limekuwa jambo la kivutio zaidi kwa watukutu hao wajiji wanaojipatia pesa kwa njia zisizo za halali , kumuona mtoto wa Raisi kati ya wahalifu walijiambia na wao wapo salama, lakini pia sasa wale waliokuwa wakimmezea mate mrembo Rose wanafahamu kwamba bwana huyo ndio aliekuwa akibeba mrembo huyo wa haja.

Roma mara baada ya kufika nyuma ya Rose alijikuta akishangaa mara baada ya kusogelewa na jamaa mmoja kibonge , Roma alikuwa akimkumbuka huyo bwana kwani siku ambayo anaenda kwenye usaili ndani ya kampuni ya Vexto alikuwepo peke yake akiwa katikati ya wanawake , alikuwa ni bwana ambaye anafahaika kwa jina la Jacob.

“Mr Roma tunakutana kwa mara nyingine baada ya kipindi cha muda mrefu kudogo”Aliongea Kibonge na kumfanya Roma kutabasamu.

“Nakukumbuka , jina lako ni…”

“Jakob Duwale “Aliongea Jacob.

“Kumbe mlishawahi kukutana hapo kabla?”Aliuliza Rose mara baada ya kuona Jacob anafahamina na Roma.

“Ni stori ndefu Boss nilivyokutana na Mr Roma”Aliongea na Rose alitabasamu.

“Hubby huyu ni Jacob Duwale ni moja ya vijana wangu tegemezi sana ndani ya hili kundi , ni mwenye akili sana na mtiifu lakini pia napenda anajiamini , nilimfanya kuwa msaidizi wa Zonga”Aliongea Rose na kumfanya Roma kuelewa.

“Jacob uwe makinni kwa sasa mambo hayajatulia?”Alitahadharisha Rose.

“Mambo yamekuwa kimya mpaka leo hii kutibuka , huenda muda kama huu ningekuwa nyumbani na mke wangu nafurahia chakula chake”Aliongea Jacob.

“Umeoa? Nakumbuka ulikuwa ukimpenda Boss wa kampuni ya Vexto mapenzi yako yaliishia wapi?”Aliuliza Roma kwa kejeli.

“Nilimpata mwanamke mzuri kuliko Boss wa kampuni ya Vexto ambaye ni mke wangu”

“Mkeo hawezi kuzidi mke wangu kwa uzuri , acha kujifariji”Aliongea Roma na kumfanya Zonga kucheka lakini Rose aliyaingilia maongezi maana hakupenda namna Roma aanavyojigamba na mke wake mbele yake.

“Alimpatia mwanamke wa watu mimba ndio maana akalazimika kuoa, huyo mwanamke lazima utakuwa unamjua”Aliongea Rose na kumfanya Roma aone inawezekanaje yeye kumjua.

“Siwezi kumjua”

“Mr Roma nakushukuru sana kama sio wewe huenda nisingepata mwanamke mtiifu na mzuri kama Chaneli”Aliongea Kibonge Jacob na hapo hapo kumbukumbu za Roma zilifanya kazi na kumkumbuka mwanamke ambaye alikuwa na jinsia mbili ambaye alishawahi kumtamkia wazi wazi kwamba anampenda na ndio yeye aliempatia hamasa ya kuweka wazi vile ambavyo ameumbwa.

Imani Maseko ndio jina lake kabla ya kuwa na jina la Chaneli , alikuwa ni binadamu aliezaliwa na mwonekano wa kiume lakini akajaaliwa jinsia mbili kwa wakati mmoja huku jinsia ya kike ikiwa na nguvu zaidi kuliko ya Kiume , akaishi miaka mingi kwa kuigiza akiwa mwanaume mpaka kujizolea umaarufu kama mmiliki wa benki ya baba yake Mchungaji Maseko , benki maarufu ya Chatex , benki ambayo ilikuwa ikitumiwa na wafanyabiashara wengi haramu kutakatisha fedha zao.

Sasa Imani Maseko mara baada ya mara ya mwisho kuagana na Roma alikuwa akienda nje ya nchi kufanya Plastic surgery kwa ajili ya kubadilisha mwonekano wake na kuwa wa kike, likuwa jambo la kushangaza kwa Roma kusikia huyo Chaneli au Imani Maseko kupewa ujauzito na Kibonge Jacob mpaka kufikia hatua ya kumuoa.

Hata hivyo hakutaka kutia neno kabisa ila alijiambia licha ya umalaya wake, asingeweza kutoka na Chaneli huku angeulizwa sababu angekosa kuitaa hadharani.

“Nimemkumbuka sasa , hongera sana kumuopoa mrembo Chaneli”Aliongea Roma.

“Asante sana Mr Roma lakini pia nakushukuru sana , kwani kama sio wewe nisingeweza kumpata Chaneli”Aliongea Jacob.

“Hivi biashara zao ziliishia vipi?”Aliuliza Roma.

“Benki ya Chatex ipo chini ya Chaneli anaiendeleza baada ya kurithi mali za baba yake ni benki huru kwenye ufanyaji wake wa biashara lakini imekuwa na msaada sana katika biashara zangu , kwani madili mengi yalifanikiwa hapa nchini kupitia kwa Chanel na katika harakati za biashara ndio Jacob aliweza kukutana na Chaneli”Aliongea Rose na kumfanya Roma kuelewa.

“Wote washafika?”Aliuliza Roma.

“Kuna wawili hawajafika hapa”Aliongea Zonga.

“Sababu zao ni zipi?”

“Wamesema wakija hapa watatibua ratiba zao zingine”

“Uliwaambia anaewahitaji ni Rose?”

“Ndio nilifanya hivyo, huenda labda wakawa na kazi zingine muhimu zaidi”Aliongea kwa kutetea Zonga.

“Hawa ambao wamekataa nitaonyesha nini maana ya kutoiii maagizo , nipatie simu”Aliongea Rose huku akibadilika na kuwa mkali lakini Zonga alisita sita , alikuwa akijua ni nini Rose angekifanya kwani hakuwa na huruma likija kwenye swala la utomvu wa nidhamu , ni rahisi kusema Rose alikuwa na upande mwingine wa roho ya kikatili kama Roma , hata hivyo ni haki kusema hivyo kutokana na aina ya biashara yake.

Baadhi ya watu walisikia mazungumzo yao na kujikuta wakimwangalia Rose kwa wasiwasi kuona ni hatua fani angechukua.

“Wamepatiwa taarifa lakini wanajiona wao ni wajuaji na kutotaka kutii maagizo yangu , wananichukuliaje labda , Halafu kwanini unawatetea , inamaana maeneno yangu kwako si kitu?”Aliuliza Rose kwa hasira akimwangalia Zonga.

“Sio hivyo Boss ni..” lakini alijikuta akitoa simu pasipo ya kupenda , baada ya kuona hasira yake imepanda maradufu, baada ya Rose kuchukua simu , aliweza kupiga mara moja.

“Nahitaji kusikia habari ya vifo vya Zwange pamoja na Mani , mali zote walizochuma wakiwa chini ya Tembo wanyang’anywe haraka sana na kurudishwa kuwa mali ya Tembo”.

“Umeeleweka Madam”Iliitikia sauti ya kiume upande wa pili na Rose alitupa simu kwenye meza na kufanya watu wote kushikwa na ubaridi kutokana na kauli ya Rose isiokuwa na huruma hata Zonga mwenyewe aliogopa.

“Unahisi mimi ni mkatili eh?”Aliuliza Rose huku akiweka tabasamu lisilokuwa la kawaida.

“Siwezi kuthubu..”Alijibu kwa kusita sita .

“Zonga nilishakuambia tokea mwanzo ukishaingia kwenye biashara hii kosa kubwa ni kuwa na huruma, nataka wote hapa mnisikilize kwa umakini kama mtu unaamua kukiuka maagizo yangu bora ufanye hivyo ukiwa unaamini una nguvu kuliko mimi , ila kama ni dhaifu na unajikuta mbabe basi sitokuwa na huruma zaidi ya kukutana na upanga wangu mkali, sitaki kuona yoyote hapa anakiuka maagizo yangu naweza nisiongoze shughuli za kawaida za biashara lakini haimaanishi kwamba mimi sio bosi wenu, Narudia tena Ole”Aliongea Rose kwa sauti na watu wote wakubwa kwa wadogo walitingisha vichwa vvyao kuelewa na kumfanya Roma kujikuta akizidi kumuona Rose kuwa mrembo kwa charisma aliojaaliwa.

Ilikuwa ngumu kuamini kundi la Tembo lenye nguvu liliweza kuendeshwa na Rose na kufikia ukubwa huo , tena mwanamke mwenyewe kuwa mdogo tu kiumri na mrembo mayai mayai,lakini ukweli kuna siri kubwa sana kwenye maisha ya nyuma ya Rose , ukiachana kwamba alikuwa akijua mafunzo ya Kung Fu na Kithai lakini changamoto kali za kimaisha alizopitia ndio zilimkomaza sana na kuwa mgumu na huenda ndio maana kati ya wanaume aliotokea kuwapenda kuwa Roma ambaye siku zote alikuwa akimchukulia kama malaika.

Baada ya nusu saa kupita Roma aliweza kupata simu kutoka kwa Sauroni kupitia kwa Diego na alielezwa kwamba ni kweli matarajio yake yalikuwa ni sahihi , Situ aliweza kukodi kundi la Lapland vikosi vitatu na muda huo yupo kwenye meli kwenye maji ya kimataifa akiwa anajaribu kutoka Tanzania kuingia Kenya na ilionekana alikuwa akikimbia kutokana na meli yake kutembea kwa ‘Nautical miles’ nyingi kwa saa.

“Mfalme Pluto kwa msaada wa haraka zaidi ambao unaweza kuutumia kumkamata ni kutumia Yamata Sect , tumejaribu kuangalia hapa wana meli ndogo ya kivita wameikodisha ukanda huo na inafanya dolia mpakani mwa Somalia na Kenya”Aliongea Sauroni.

“Kama ni hivyo mtafute Tanya atoe maelekezo waizuie haraka sana”Aliongea Roma na Sauroni aliitikia na kisha akakata simu na Roma alitoa maelekezo ya boti hio kuelekea upande wa Kenya.

Mpaka hapo Roma alijua itawachukua zaidi ya masaa mawili matatu mpaka kuwafikia , hivyo baada ya lisaa limoja hatimae walienda eneo la mgahawa ndani ya boti hio akiwa na Rose kwa ajili ya kujipatia chakula cha mchana,alijiambia mwenyewe kama ni mtu wa kwaida asingeweza kufanya vitu vyote hivyo mara tu baada ya kutua na ndege.

Ni kama lisaa limoja tu mara baada ya Roma kumaliza kujipatia chakula cha mchana ndani ya boti hio ya kifahari hatimae Kapteni alitoa taarifa juu ya kuonekana kwenye rada meli mbili ndogo za kivita moja ikiwa na bendera za Japani pamoja na kundi la Yamata Sect na nyingine iliweza kuonekana wazi kabisa ambayo ilikuwa ni ya Lapland Rangers.

Kuna mtu anakwenda kufa kifo kibaya sana [emoji3]
ITAENDELEA JUMATANO
0687151346 watsapp only
 
Ohoooo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…