Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kweli kabisa.Mwacheni wazee siku akiona nasi tuna umuhimu atapost na sisi bila hiyana tutasoma.
Customer n mtu muhim San kwa mfanya biashara. Na msomaji ni muhim san kwa mwandishi kwahy respect kwa wote wasomajii wakisusaah kazi yak ya fasihii ainaah maan wapend watej wako waheshim na ahadii n kitu mhm San kweny maishMwacheni wazee siku akiona nasi tuna umuhimu atapost na sisi bila hiyana tutasoma.
Nini ww?Mmmmmm
OhooooSEHEMU YA 321.
Siku iliofuatia Roma na Magdalena waliweza kuondoka ndani ya Ngome ya Tang na kuanza safari ya kurudi nchini Tanzania , Roma alikuwa ashaweza kufanikisha jambo lake na kuna vitu vingi ambavyo alijifunza hivyo kubakia ndani ya taifa hilo kwake aliona ni kupoteza muda.
Saa mbili kamili ya asubuhi ndio waliweza kufika ndani ya uwanja wa kimaitaifa wa mwalimu Nyerere , altumia zaidi ya siku sita tokea aanze safari mpaka kurudi lakini kwake ni kama alikaa muda mrefu kutokana na kuikumbuka familia yake.
Baada ya kupanda taksi moja Mage alianza kushushwa nyumbani kwake na akafuatia Roma kufika nyumbani kwake.
Ilikuwa ni siku ya jumapili hivyo Roma hakutarajia kumkuta Edna kwenda kazini.
Lanlan ndio wa kwanza alieweza kuhisi ujio wa Roma hivyo ile anaingia mlangoni tu alikimbiliwa na Lanlan na kukumbatiwa miguuni jambo ambalo lilimfanya Roma kufurahi mno huku akikukumba amesahau kumchukulia Lanlan zawadi.
“Yaani wewe mtoto unapenda kufanya mambo ya kimya kimya ,si ungepiga simu tukafika kukupokea”Aliongea Blandina ambaye alionekana kuketi eneo la sebuleni huku akiwa ameshikilia kitabu.
“Ningekuwa hata na begi ningesema mje kunipokea , lakini niko mimi kama mimi unavyoniona sijaona haja ya kusumbua watu”Alongea Roma , na ni kweli kabisa alikuwa yeye kama yeye na simu yake tu.
“Dadi umemletea zawadi gani Lanlan?”.
“Zawadi yako inakuja ipo njiani”Aliongea Roma akijaribu kumdanganya Lanlan.
“Unanidanganya”
“Haha.. Roma uwe unamletea mtoto wako zawadi tokea jana mama yake anaongea hapa utamletea zawadi , ila naona umekuja mikono mitupu”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kufikiria.
“Lanlan niambie unataka nini , mimi baba yako nitahakikisha unapata kila unachotaka”Aliongea Roma na Lanlan alitabasamu kwanza huku akionekana kuwaza .
“Lanlan B hana nguo”Aliongea na kumfanya Roma kuikiria Lanlan B anaezungumziwa ni nani lakini alipokuja kukumbuka kuna Lanlan mwingine ndani ya nyumba alijikuta akienda kukaa kwenye sofa huku akicheka.
Lanlan B alikuwa ni mbwa wa Lanlan na tokea aletwe hapo nyumbani Lanlan alikuwa ni kama mtumwa , kuna muda Edna hakupenda mbwa akiingia ndani lakini Lanlan alitaka kumuingiza na kucheza nae sebuleni.
“Okey Baba anaahidi kumnunulia nguo Lanlan B”Aliongea Roma na kumfanya Lanlan kuchekelea kwa shangwe na kumfanya Blandina kujikuta akisikitika kwa kutingisha kichwa.
“Mom kuna chochote kitu nina njaa ya asubuhi”
“Tushakunuwa chai tayari ,jikoni yupo Bi Wema nenda kamwambie akupatie tulichobakisha”Aliongea Blandina na Roma alimuweka Lanlan kwenye sofa na kuelekea jikoni na kumkuta Bi Wema akiwa kwenye pilika pilika zake kama kawaida.
Bi Wema baada ya kumuona Roma amerudi alifurahi na kumwandalia kilichobakia kwa kupasha moto haraka haraka na kumpatia.
“Bi Wema Edna kaenda wapi?”Aliuliza Roma kwani tokea afike hajahisi kabisa uwepo wa mke wake”
“Miss kaenda kuchukua mazoezi ya kukimbia huko nje”Aliongea na kumfanya Roma kutoa macho.
“Kaenda kuchukua mazoezi?”
“Ndio siku hizi tatu tokea uondoke alikuwa akichukua mazoezi binafsi jambo ambalo limetushangaza na kujiuliza kwanini kaanza mazoezi”Aliongea na kumfanya Roma kutabasamu , hakuamini Edna swala lake alichukulia siriasi mapema hivyo.
Kwasababu Roma hakuwa na maelezo ya kutosha kwa Bi Wema alienda na chakula chake hadi kwenye meza na kuendelea kula , huku eneo la sebuleni mama yake pamoja na Lanlan wakionekana wametoka.
Wakati anamalizia kula ndio muda ambao Edna alivalia kijipensi pamoja na tisheti aliingia hapo ndani akionekana kuhema na kumfanya kumshangaza Roma kutokana na staili yake aliovaa.
Edna mwenyewe hakutarajia kama angemkuta Roma na walijikuta wakiangaliana , lakini macho ya Roma yalikuwa kwenye mavazi tu .
“Umeniangalia vya kutosha”Alivunja ukimya Edna mara baada ya kuona aibu maana manyonyo yake yaliotokeza kama mishale yalikuwa yakijionyesha mno.
“Sijatosheka bado…Halafu Wifey wapi ulikuwa unafanyia jogging?”
“Nilizunguka kwenye hio barabara kupitia nyuma na kuja kutokezelea kule mbele karibu na Nyumba ya Mama T”Aliongea Edna.
“Nini!.. Yaani umeenda kuzunguka kote kule ukiwa hivyo na kuruhusu mimacho ya wanaume wenye njaa kukuangalia , kwa staili ya uvaaji huo haiwezi kuendelea kuanzia kesho , kama utakimbia utavaa suruali za track”Aliongea Roma na kumfanya Edna aanze kujichunguza , yeye alijiona yupo kawaida tu lakini alijiambia inakuwaje huyu mtukutu kuona wivu kwa kuvaa hivyo.
Ukweli Edna alichovaa kwa mwanaume yoyote huko mtaani angekuwa kwenye hali mbaya kwani pensi alilovaa lilifanya miguu yake ilionona na milaini kuonekana wazi wazi na hicho ndio kilichokuwa kikimuuma Roma na kuona wanaume wenzake walifaidi.
“Sio kwamba nilikuwa mwanamke pekee niliekuw anikichukua mazoezi , walikuwepo wengi kwanini waniangalie mimi miguu yangu tu”Aliongea Edna huku akijisikia vizuri kwa wakati mmoja kwa namna ambavyo Roma alionenyesha wivu.
“Naweza kujitutumua na kukuangalia juu mpaka chini kwasababu nastahili kufanya hivyo , Hawa wanaume wa barabarani hwatakiwi hata kukusogelea , unaweza kusema mimi ni mchoyo lakini sijali na kuanzia sasa nakuruhusu uwe unavaa kama hivyo ukiwa hapa nyumbani lakini ukienda kukimbia ni mwendo wa suruali kuu kuu , usipo nisikiliza nitakufuata huko huko na nitakuweka begani na kukurudisha nyumbani”Aliongea Roma na kumfanya Edna kushangazwa na maneno yake , lakini hata hivyo alikuwa akimjua Roma anachoongea ni kama sheria hivyo alijimbia inabidi atii hivyo.
Edna alienda juu na kuoga haraka haraka na kisha akavaa nguo za nyumbani na kurudi chini na alimkuta Roma alishamaliza kunywa chai na amekaa kwenye masofa akiangalia runinga, hakumuongelesha bali alinyoosha moja kwa moja mpaka jikoni na kisha akatoka na sahani iliojaa vipande vya keki vilivyokatwa katwa na kwenda kukaa pembeni huku akila na kumfanya Roma kumwangalia.
“Hizo umetoa wapi?”
“Jana Mama yake Nasra aliniletea akisema ni zawadi kwangu”Aliongea Edna na kumfanya Roma kushangaa.
“Mama yake Nasra amekuja hapa , Mwenyewe?”
“Hapana aliletwa na Nasra na kuondoka”
Ni kweli jana yake Mama yake Nasra aliweza kufika ndani ya familia hio kutoa shukrani kwa familia ya Edna kwa kile walichokifanya kwa mtoto wake Nasra katika kumsapoti katika masomo yake na kufikia hatua aliokwisha kufikia.
Mwajuma aliongea na Edna kumuombea msamaha pia mwanae kwa kujihusisha na mume wake lakini Edna alimwambia hana kinyongo na Nasra kwani hata yeye alikuwa akitafuta furaha , kitendo cha Edna kumuelewa Nasra juu ya hisia zake kilimshangaza mno Mwajuma ambaye ni mama yake Nasra , ilikuwa ni ajabu kuona mke kumkubali mchepuko kirahisi.
Sasa alimletea Edna zawadi ya keki ambayo kwa maelezo yake yeye ndio aliehusika kuipika kwani alikuwa na uzoefu katika maswala ya mapishi.
“Kwaho alivyokuja alikwambia nini?”
“Aliikuja kumshukuru Mama na Bibi kwa kusimamia masomo ya Nasra , lakini pia kuomba msahama kwa mwanae kutembea na mume wangu”Alijibu Edna huku akila kijikeki chake huku akiwa anaangalia runinga na kumfanya Roma kutabasamu kwa uchungu kwa kauli hio.
“Babe kwa jinsi ninavyona unavyofurahia hio keki ni lazima mambo yalienda vizuri hio jana , mimi najua nilioa mke mwenye roho nzuri , nadhani ni jambo jema pia siku moja moja na Nasra kuja hapa nyumbani na kupiga piga stori hehe..”Alitania Roma.
“Wewe usithubutu , unafikiria sijui unachopanga na unafikiria nimekubali matendo yako moja kwa moja”
“Ninakutania mke wangu , hata hivyo nadhani unakumbuka mkataba wetu wa amani tuliokubaliana siku ile?”Aliongea Roma na kumfanya Edna kurudisha kipande cha keki kwa hasira kwenye sahani na kisha kumpotezea na kimya kikatawala.
Baada ya dakika kama ishirini hivi za kuangalia taarifa ya habari ya kituo maarufu cha Aljazeera Roma alisimama na kujivuta kama kawaida yake.
“Ninatoka kidogo naweza nisirudi kwa ajili ya chakula cha mchana”Aliongea Roma.
“Ndio kwanza umefika halafu ndio unaonaoka?”Aliuliza huku akikunja sura.
“Siendi mbali sana , nitawahi kurudi”Aliongea Roma huku akipiga hatua kwenda juu akipanga kwenda kuchukua ufunguo wa gari , lakini alijikuta akihisi ubaridi wa mwili mara baada ya kuangaliwa na macho yasiokuwa ya kawaida na Edna.
“Inaonekana tayari ushawakumbuka wapenzi wako na ndio unakwenda kukutana nao , haishangazi chakula tulichobakisha kikatosha kukushibisha , ninachoona hukushiba ila uliacha nafasi kwa ajili ya chakula cha mchana na mchepuko wako , Naomba nikushukuru baba mapema kwa kutokusubiria chakula cha mchana maana tutapika chakula kidogo ,unaonekana kuwa mkarmu sana kwanini usipate kabisa chakula cha usiku huko huko ukirudi ushashiba..tena hapana itafaa zaidi ukirudi asubuhi bajeti zitapungua”Aliongea Edna kinafiki na kumfanya Roma kumwangalia .
“Kuna maelezo ya mbinu mpya nilizopata huko China nataka kuona kama zitafanya kazi kwa Rose ndio maana natoka , siwezi kuanza na wewe kwasababu bado mwili wako haujakomaa kimazoezi”Aliongea Roma lakini Edna alichukizwa na maelezo yake marahisi , hata hivyo alijua asingeweza kumzuia kufanya kile anachotaka.
“Kwaho ni lini nitakuwa tayari na mimi kujifunza?”
“Inabidi nisubiri kwanza nionea maendeleo yako , mwili wako ni dhaifu mnno kuliko unavyojiona mwenyewe , tabia yako ya kufanya kazi muda mwingi , kutokula vizuri na kutochukua mazoezi kumekufanya kuwa dhaifu kuliko wenzako wote , kwanzia sasa achana na kula makeki hayo yenye sukari nyingi na piga mazoezi, ukiwa tayari utaanza”Aliongea.
Ni Kweli Edna alionekana kuwa dhaifu mno , hakuwa na nguvu kuliko warembo wake wote na ndio maana Roma hakutaka kumfanya kujifunza mbinu zake , kwani zingemletea shida na huenda asingeweza hata kupanda levo.
“Usiwe na wasiwasi kama utaendelea hivi ndani ya miezi miwili ijayo unaweza kuwa vizuri zaidi zaidi na kuanza”Aliongea na Edna aliitikia kwa kichwa huku akijiambia hata hivyo miezi mwili kwake haikuwa mingi sana.
“Halafu Sophia na Qiang Xi , sijawaona wameenda wapi?”
“Sophia kaenda kumsalimia babu yake Mzee Athumani , nasikia ni mgonjwa na atakaa huko kwa muda , kuhusu Qiang Xi nimemuomba kwenda na Derick Kiwangwa kupeleka mahitaji ya watoto”Aliongea Edna na Roma alitikisa kichwa na kisha alipandisha juu na ndani ya madakika kadhaa alishamaliza kujiandaa na kuondoka kuelekea Kimara anapoishi Dorisi na Rose.
Haikumchukua muda mrefu kufika na ile anaingiza gari alikuja kupokelewa na Dorisi ambaye alikuwa amevaa khanga moja tu , kiasi kwamba Roma alishangazwa na uvaaji wake halafu akaja kufungua geti.
“Unafunguaje geti ukiwa umevaa hivyo? Kuna watu wabaya sana ndani ya hili eneo”Aliuliza Roma
“Nilichungulia kwanza na kuona gari yako ndio maana na hata hivyo hapa kuna ulinzi wa kutosha Rose watu wake wanalinda”Aliongea Dorisi mara baada ya Roma kushuka kutoka kwenye gari na kisha wakakumbatiana na Roma alimbeba juu juu.
“Umeniletea chochote kukota China?”Aliongea na kumfanya Roma kujilaumu kwanini amesahau kumletea zawadi.
“Siku nyingine naahidi sawa?”
“Nilijua tu utanisahau tena kuniletea zawadi”Aliongea kwa kulalamika
“Babe nakuahidi nitakupa zawadi nzuri tu”Aliongea huku akimuweka kwenye sofa na kumshika pua.
“Rose yuko wapi?”
“Katoka kuelekea Kisarawe”Aliongea Roma na kutingisha kichwa huku akiangalia umbo zuri la mrembo Dorisi.
Kivazi alichovaa kilikuwa kikitamanisha kweli na ni sahihi kusema ni kwasababu alikuwa akiishi na mke mwenzake ndio maana alikuwa akijiachia kwa namna hio.
Roma alipeleka mkono mpaka kwenye miguu ilionona ya Dorisi na kuanza kuipangusha pangusa kupanda juu.
“Unafanya nini ,ndio nimetoka kuoga tu sasa hivi jamani Roma”
“Ndio maana sitaki kupoteza hii nafasi”Aliongea Roma na kabla hajajibu Roma alimwinua tena na kumpandisha vizuri kwenye sofa juu na kumkalia kwa juu na kufanya nguo yote kuacha mwili wake wazi na kisha akapeleka mdomo wake na kuunganisha na wa Dorisi na kuendelea kupigana denda huku , mkono mwingine ukitalii kwenye mwili wa mrembo huyo kwanzia juu kwenda chini na kumfanya Dorisi kutoa mlio mara baada ya kuzidiwa na hisia kali na kujisahau kabisa kama alikuwa aneo la sebuleni.
Roma na yeye baada ya kuona mzuka umempanda alitoa nguo zake haraka haraka na kubakiwa na boksa tu na kisha aliendelea kumwadhibu Dorisi kwa zaidi ya dakika arobaini na tano kwa kucheza na sehemu zenye ashiki za mwili wake.
Wakati sasa anashuka boksa yake na kutoa mtalimbo kwa ajili ya kufanya… mara ….
“Boom ! , Boom , Boom!!”
Ulikuwa ni mlipuko wa aina yake ambayo ulimfanya Roma palepale kupotea na Dorisi kwa haraka sana na kutokezea nje hukua akiwa amemkinga , haraka haraka alijua lazima litakuwa ni bomu.
Dorisi baada ya akili yake kufanya kazi aliweza kushuhudia jumba lake likifuka moshi mwingi na moto ukiwa unawaka na kujikuta akitetemeka mno.
Roma alijua lazima hilo ni bomu lilikuwa limetegwa ndani ya nyumba hio na ni kama alikuwa akisubiriwa yeye kuingia ndio liteguliwe.
Kwasababu wote walikuwa uchi palepale alimwambia Dorisi asubirie na alipaa na kwenda kutua kwenye balkoni ya juu ambayo bado hakuwa imeshikwa na moto na kuingia kwenye mojawapo ya chumba ambacho kilikuwa cha Dorisi na kisha akatafuta nguo chache na vitu muhimu na kutoka navyo na kisha akampatia Dorisi mavazi na yeye akavaa Track.
Roma hakuwa na muda tena wa kuendesha gari kuondoka eneo hilo ila alichokifikiria muda huo ni kumuondoa Dorisi hapo kwa njia zake za kijini na aliweza kufanya hivyo ndani ya dakika alikuwa ashamfikisha nyumbani kwake Oysterbay na kumlaza kwenye chumba chake akiwa amepoteza fahamu.
Roma baada ya kutoka mtu wa kwanza kumuona ni Blandina mama yake na kwasababu Roma alichafuka kwanzia kichwani Blandina alimshangaa.
“Nini kimetokea mbona uko hivyo?”Aliuliza Blandina na sauti yake ilisikiwa na Edna ambaye na yeye alimsogelea Roma huku akionyesha hali ya wasiwasi na Roma alielezea kile kilichotokea na Edna aliogopa mno.
“Kwaho hujapata majeraha? , vipi Dorisi?”Aliuliza Edna kwa wasiwasi.
“Ni bahati niliwahi la sivyo huenda angedhurika , kwasasa nimekuja nae na nimempuzisha kwenye chumba changu kwani yupo kwenye mshituko , Edna nisaidie kumwangalia natoka tena”Aliongea Roma huku akijaribu kujipapasa na kugundua simu aliacha kulekule Kimara.
“Naombeni mwenye simu yoyote aniazime mara moj nitaondoka nayo”Aliongea Roma na Mama yake ndio aliekuwa wa kwanza kutoa yake na kumpatia.
“Roma kuwa makini unakuoenda”Aliongea kwa wasiwasi na Roma alimtoa wasiwasi na kisha akatoka nje kabisa huku akipiga simu.
“Your Majest Pluto I have been trying to Contact you but your phone isn`t connected , There has been an issue with Miss Rose”Aliongea Diego akimaanisha kwamba kuna tatizo ambalo limempata Rose.
“Unamaanisha nini , si niliwapa pia maelezo kuwa nae karibu”Aliuliza Roma.
“Miss Rose alikuwa Kisarawe na Adeline alikuwa nyuma yake akimpatia ulizni kwa siri, lakini mara baada ya kuingia kwenye jumba moja ambalo ni la kwake ulitokea mlipuko mkubwa na kubomoa jengo lote, tumeweza kupata taarifa za tukio mara baada ya Adeline kupiga simu kuomba msaada na ilionekana aliwahi kuingia kabla ya mlipuko na anatoa taarifa kwamba Rose yupo salama , lakini yeye kaumia na hawezi kutoka mpaka msaada”Aliongea Diego kwa kingereza na kumfanya Roma kung’ata meno kwa hasira.
“Diego hili nitalifanyai kazi mimi mwenyewe , toa baadhi ya vijana wagawane kwenda Kimara kuangalia kama kuna milipuko iliobakia na pia wengine watoe ulinzi kuzunguka nyumba yangu”Aliongea Roma na mara baada ya kumaliza alimpigia simu Nasra.
“Uko wapi?”
“Nipo nyumbani , kumbe usharudi?”
“Ndio nisharudi na nipo katikati ya tukio kwasasa siwezi kukupa maelezo ya kutosha ila nataka utoke na mama yako na uende nyumbani kwangu mkatulie kule mpaka nitakaporudi”Aliongea .
“Roma kuna nini , unanitisha”
“Fanya hivyo , Edna atakuelezea”
“Okey ngoja tufanye hivyo”Aliongea na Roma alitaka simu na kuvuta pumzi ya ahuendi , alijua kuna adui huenda anajaribu kutumia wanawake wake kujaribu kumdhuru na ndio maana aliona achukue tahadhari mapema, kwa upande wa Amina aliamini atakuwa sawa kutokana na ulinzi wa baba yake anaomuwekea , lakini hata hivyo hakutaka kujiridhisha kwa hewa , alichokifanya ni kuandika meseji kwa haraka haraka na kisha akaituma kwa Amina na kisha akaweka simu mfukoni na kutoweka.