NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.
MTUNZI: SINGANOJR .
Mono no Aware
SEHEMU YA 786.
Roma sauti yake ilionekana kubadilika na kuonyesha zaidi hali ya kukasirika mara baada ya kuona anasumbuliwa na Sharif.
Alijiambia anaongea nini huyo na methali zake, muonekano ?, ukweli wa moyo?, Kama angekuwa mtu wa dini na angeambiwa aelezee upendo na chuki na yeye angejiuliza swali kama vyote hivyo vipo kweli kwanini ana mahusiano mengi na mikwamo mingi.
Sharif alijikuta akibakia mdomo wazi na aliona ni kama ujinga kwani kijana mdogo kama huyo ndio kwanza yupo kwenye miaka ishirini kuelekea therathini na licha ya kuwa na uwezo usio na mipaka bado ni mtoto tu na kama ataongea kwa namna anavyongea na Aoiline basi anaweza asimsikilize.
Kuhusu Roma kumwambia aondoke wala hakujali sana na mara baada ya kuwaza kwa akika kadhaa alionekana kuwaza kitu na kutingisha kichwa chake kwa mara nyingine.
“Kulingana na utafiti wa kibinadamu juu ya dunia ya kale , Kimondo chenye uzito wa zaidi ya tani trilioni moja kilidondoka duniani miaka milioni sitini na tano iliopita , spidi ya kimondo hiki inakadiriwa kuwa zaidi ya kilomita elfu themanini na tano kwa saa na nguvu yake ni sawa na kulipua vichwa milioni therathini vya mabomu ya nyuklia kwa wakati mmoja, Binadamu wanaweza wasielewe hili lakini kuna uwezekano wa aina ya kimondo cha namna hio kuigonga dunia kila baada ya miaka milionni kumi na kuharibu kabisa sayari ya Dunia , vilevile vimondo vya ukubwa wa wastani upande vinaweza pia kudondoka duniani muda wowote.
Ni miaka elfu hamsini tu iliopita wakati dunia iliopoingia katika vita kali ya majini na binadamu mpaka Wajumbe wa Mkuu wa Enzi kuingilia kati, kipindi hiki ndio wakati ambao Kimondo kilidondoka eneo la jangwa eneo ambalo sasa ni sehemu ya taifa la Marekani , jimbo la Arizona , baada ya kimondo hiki kufika ardhini kilirusha mawe tani milioni mia saba sabini na tano kwenda angani na kutengeneza shimo kubwa ambalo lilikuwa na upanda wa takribani kilomita saba na mita zaidi ya mia kwenda chini , sehemu hii ndio leo hii hufahamika kwa jina la Bariger Crater.
Wakati huo hiki kimondo kilikuwa na ukubwa futi mia tatu therathii ambazo ni sawa na ndege za sasa , baada ya kudondoka kilisababisha joto zaidi ya nyuzi 1600 , joto ambalo liliyeyusha mawe , mchanga na takataka zilisafiri kwa umbali maili sita kwa spidi mara tatu ya risasi , na kwa spidi hio watu wote wlaiokuwa karibu pamoja na wanyama miili yao ilitobolewa na kuvunjika mifupa hata pasipo ya kujua”
Sharif aliongea muda mrefu na haikueleweka alikuwa akielekea wapi katika mazungumzo yake lakini habari hizo zilimfanya Roma asimwambie andoke.
Roma taratibu sana alijinyanya na kukaa kitando na kisha akamwangalia Sharif ambaye alikuwa na uso uliopambwa na tabasamu.
“Ni kitu gani lakini ambacho unakusudia kusema kwa stori yako hii?”\Aliuliza Roma.
“Naona hatimae umevutiwa na kile ambacho nakusudia kuongea, si ndio?”Aliuliza Sharif.
“Kama sio kwasababu ya wewe kuwahi kuniokoa , ningepigana na wewe hata kama ilimaanisha sikuwezi”Aliongea Roma huku sauti yake ikiwa na hali ya mikwaruzo huku akimwangalia Sharif kwa macho makali kama vile ni mbwa mwitu.
“Oh!Umejuaje niliwahi kukuokoa?”Aliuliza Sharif.
“Wakati Yan Buwen alipofanikiwa kuunganisha nishati ya Ant Matter na mwili wake na kupambana nae, ilikuwa ni wewe ambae ulitawala mwili wangu na kutengeneza radi ya Zambarau na haikuwa mara moja , ijapokuwa sauti yako imebadilika lakini siwezi kusahau namna nilivyokuwa nikisikia sauti yako katika akili yangu , kama sijakosea ni wewe pia uliemfana yule mzee kumteka Clark , Wewe ndio Master namba moja”Aliongea Roma na kumfanya Sharif kutingisha kichwa.
“Naona hujalewa na hii inamaanisha hujakata tamaa bado”
“Ninaweza kuwa ziadi ya unavyowaza”Aliongea Roma na palepale alitawanyisha chupa za bia ambazo zilikuwa kwenye meza na mara baada ya kupata iliokuwa na kinywaji aligida yote kiasi kwamba ilimfanya hata kumwagikia kwenye kifua chake lakini hakujali.
“Haha..nini kingine ambacho unajua kuhusu mimi , kwanini usiongee nikakusikiliza?”Aliongea Sharif huku akimwangalia Roma na matarajio.
Roma alicheua kwanza kinywaji alichokunywa kwa pupa na kisha macho yake yalisinyaa kana kwamba alikuwa amelewa.
“Kama nipo sahihi , wewe utakuwa mtu ambae Aoiline alikuwa akizungumzia , wakati nilipokuwa katika ulimwengu wa majini pepo alisema nilikuwa nikifanana kwa kiasi flani na mtu mmoja na alimfikiria huyo mtu mara baada ya mimi kutumbia mbinu ya Andiko la urejesho wa Azimio , hii inamaanisha ni mtu anaetumia mbinu kama yangu”
“Mtaalamu ambae anaweza kumfanya Aoiline kumfikiria lazima atakuwa na nguvu kuliko mii na kwako wewe kuweza kudhibiti mwili wangu kwa kuuazima na kisha kuita radi ya mapigo tisini na tisa bila ridhaa yangu , huyo mtu lazima atakuwa ni wewe.
Aoiline ni jini mtaalamu wa kihistoria ambae aliingia katika ulimwengu wa majini pepo miaka elfu hamsini iliopita , kwa umri wako lazima angalau utakuwa unalinfana nae au umemzidi kidogo , kama wewe ni mtu ambae unaweza kupambana nae au kumshinda kabisa basi lazima utakuwa angalau katika levo ya mapigo elfu tisa tisini na tisa ya radi , zaidi ya yote na uelewa wako wa mbinu ya Andiko la urejesho wa azimio basi kuna uwezekano mkubwa wewe ndio mtu wa kwanza kutumia mbinu hii kama sio kuigundua na kama ni hivyo basi isingewezekana kwa namna yoyote kumshindwa Zeus na Athena miaka elfu ishirini iliopita wakati wanafika duniani , kuna uwezekano wa aina mbili , mosi kuna uwezekano hukushiriki vita ya miungu na majini , pili uliwaacha moiungu wote kumi na mbili makusudi kabisa licha ya kwamba ulkikuwa na uwezo wa kuwaua wote..”
Macho ya Sharif yalichanua kadri ambavyo Roma alikuwa akiongea na aliishia kutingisha kichwa hapa na pale huku akiwa na tabasamu la ajabu usoni mwake.
“Ndani ya ulimwengu wa majini watu niliweza kupata kopi ya andiko la urejesho wa Azimio lakini jina lilikuwa tofauti , kama mawazo yangu yapo sahihi basi kuna uwezekano hii mbinu ilisambazwa kwa viumbe wote wa dunia wanao onekana na wasio onekana kwasababu maalumu ya kumtafuta mtu ambae anaweza kujua siri yake”
“Mtu alietengeneza Andiko hili alijua vizuri nguvu yake ,lakini licha ya hivyo kauonyesha kujali kama watu au viumbe wabaya kujifunza na hili linanipa jibu kwamba mgunduzi alikuwa akijua vizuri kabisa ni ngumu mo kwa viumbe kujifunza mbinu hii kutokana na ugumu wake lakini aliishi katika tumaini siku moja itatokea mtu ambae ataweza kujifunza na kupita levo zote”Roma aliendelea kuongea na akaendelea.
“Na hili ndio ambalo lilifanya mbinu hii kujulikana kwa majina tofauti tofauti kati ya binadamu na viumbe wasioonekana na haya yote ni kwa ajili ya kupata mrithi ambae atafikia juu kabisa mwa levo zote ili kutimiza lengo flani , kama nilichootea kipo sahihi basi sababu inayokufanya kuwa mbele yangu saa hii ni kwasababu mimi ndio kiumbe pekee niliefanikiwa kuzijua siri zote za andiko la urejesho na kuyafkia mafannikio , binadamu ambae unapanga kumchagua …”
“Paah ! Paah!!”Sharif alijitkuta akipiga makofi kwa nguvu mara mbili huku akiwa na tabasamu pana kwenye uso wake.
“Sio mbaya , katika sehemu zote ulizoongea umepatia , hii mbinu licha ya kwamba sijaigundua mimi lakini imechukua nguvu zangu nyingi kuielewa juu ya siri zake na hata kuirahisisha jina ambalo uliipatia mbinu hii ndio jiina hilo hilo ambalo mbinu hii inafahamika, Andiko la Urejesho waAzimio”
“Tofauti kubwa kati ya mbinu zote za kuvuna nishati za mbingu na ardhi na nyingine zote zinazotumiwa na viumbe wa aina zote wenye nguvu ni kwamba mbinu nyingine zinamtengenezea mvunaji njia ya kupita na hatimae kufikia mwisho na kupata ufunuo mpana , lakini mbinu ya Andiko la urejesho wa Azimio inamuonesha Mvunaji kwanza mwisho wa safari ulivyo kabal ya kuianza safari na njia ambayo mtu atatumia kupita mpaka kufikia huo mwisho alioona ni juu yake yeye mwenyewe kuitafuta , ki ufupi ni kwamba ni aidha kupata mafanikio katika hatua ya kwanza au kutumia maisha yao yote kujaribu kusiku kwa faida”
“Katika kipindi cha miaka elfu kumi yote kulikuwa na baadhi ya watu wachache sana tena binadamu ambao waliweza kufanikiwa kujua maana ya Andiko hili ni nini lakini nikiwalinganisha na wewe umewaacha mbali mno , Mastar wako Tang Chi alipata mafanikio ya juu juu ila huwezi kumlinganisha na wewe”Aliongea Sharif lakini Roma hakuonyesha ishara ya furaha wala huzuni.
“Hebu acha kuzunguka zunguka , ni ipi nia yako kamili kwa kufanya na kuongea haya yote?”Aliuliza Roma akiwa siriasi.
“Je unajua ni vimondo na magimba mangapi yanatosha kuharibu uhai wa dunia ambayo yameweza kuikaribia dunia katika miaka elfu hamsini iliopita?”Aliuliza.
“Wewe si umesema mwenye ni kila baada ya miaka milioni kumi”
“Hio ni nadharia tu , ni kama hesabu za Probability na uwezekano huo ni mdogo , lakini haiondoi uwezekano wa magimba na vimondo kuipiga dunia katika kipindi cha muda mfupi tu , kati ya miaka elfu hamsini iliopita na sasa , kimondo kilichosababisha Barringer Crater kuna kubwa zaidi angalau mara ishirini ya kimondo kile na kama kikipiga hapa duniani , inatosha kabisa kuibaribu dunia yote na kufuta uhai”
“Kama ni hivyo si ingekuwa miaka elfu hamsini iliopita ndio maisha yageanza?”Aliuliza Roma.
“Sababu ya Magimba hayo ya anga za juu hayaifikia dunia ni kwasababu ya mimi kama Mjumbe wa mkuu wa Enzi”Aliongea.
“Wewe…!!!”Roma alionekana kufikiria kitu lakini aliona ni nguvu kuvuta taswira.
“Kwahio unataka kusema kwmaba unao uwezo wa kupindisha muelekeao wa vimondo visifikie dunia , hebu acha kunitania , kama ni hivyo si utakuwa na uwezo wa kuupoteza hata mwezi?”
“Unaonekana kushangaa na hii inamaanisha huna imani yoyote nje yako tofauti na uwezo wako pekee , ukweli ni kwamba Wajumbe wa mkuu wa Enzi ambao waliacha dunia na kwenda nje galaksi nyingine wanao uwezo hata wa kuharibu sayari”
Roma alikuwa ni kama anaona muonekano wake mwenyewe , ilikuwa ni dhahiri alikuwa katika bumbuwazi lakini ilionekana ni kama vile Sharif hakuwa akitaniana nae.
Roma alijiuliza maswali mengi juu ya Wajumbe wa mkuu wa Enzi, Galaksi nyingine , alijiambia kwahio hao wakuu wa enzi tuseme wameenda nje ya anga la kawaida , yaani katika mbingu nyingine.
Mara baada ya kumuonaRoma akiwa katika hali ya Bumbuwazi aliona lazima atakuwa ameenda mbali katika maneno yake hivyo alimpa ishara Roma kutosisimkwa na mwili sana na kumsikiliza taratibu taratibu.
Sharif alijiweka sawa kama mtu ambae anakusanya mawazo yake na mara baada ya muonekano wake wa kawaida kurudi alianza kumwelezea kila kitu kuhusu Wajumbe wa mkuu wa Enzi , stori ambayo inaanzia juu ya yeye mwenyewe ni nani haswa.
****
Miaka elfu hamsini iliopita Sharif alikuwa ni mtoto wa kiume aliezaliwa nje ya ndoa ambae alikuwa amechanganya damu , akizaliwa na mama ambae ni binadamu wa kawaida na jini jamii ya mapepo , kutokana na kuzaliwa nje ya ndoa na binadamu ilimfanya kutohesabika kama mtoto mwenye umuhimu ndani ya familia ya baba yake Sharif.
Ikumbukwe kipindi hichi ni wakati ambao binadamu , majini pepo na majini watu walikuwa wakiishi pamoja , yaani kabla ya vita na utenganisho wa jamii hizo na hii ilifanya hata kwa majini pepo kuwa na koo zenye majina ya kufanana na za binadamu leo hii , hivyo Sharif alitokea katika ukoo wa Sharif kutokea bara la Asia yaani Uarabuni.
Ndani ya familia ya Majini Sharif , Sharif uwezo wake wa nishati za mbingu na ardhi ulikuwa mdogo sana zaidi ya kichekesho , mdogo zaidi hata kwa wadogo zake ambao walikuwa ni majini kamili.
Kitu ambacho familia ya Majini Sharif hawakukifahamu ni kwamba Sharif kilichosababisha uwezo wake kuonekana mdogo sio kama alikosa kipaji au elimu bali ni kwamba uwezo wake wa akili ulikuwa mkubwa zaidi kuliko familia nzima , kipindi hichi alikuwa ni kama mtoto ambae alipata maono tayari hivyo mbinu yake ya mafunzo ilikuwa ni tofauti kabisa na ndugu zake.
Mara baada ya kutengwa sana na familia kwa kuonekana mzigo alijifanyisha kufa wakati wa vita ya viumbe wa dunia na hapo ndipo alipoweza kujitenga na familia yake kwasababu ilijua alifariki walimsahau.
Haikueleweka alikuwa na elimu gani wala ufunuo wa namna gani , kwake ilikuwa ni kama Mungu akujie ndotoni na akuonyesha Akhera au Mbinguni kulivyo lakini akuambie shika hili andiko na elewa maana yake ili kuijua njia ya kufika Uzimani yaani Akhera au Mbinguni , hiki ndio kilichomtokea Sharif.
Sharif ambae alikuwa kama binadamu wa kawaida alikuwa tayari ashaingia katika kituo cha juu kabisa cha levo ya mapigo elfu kumi ya radi wakati ambao Aoiline Jini jamii ya Mbweha alipoanza kuupata umaarufu miaka elfu hamsini iliopita.
Ukweli ni kwamba licha ya Sharif mweyewe kutoweza kukutaa ana kwa ana na Wajumbe wa mkuu wa Enzi lakini alikuwa ashawafikia ki uwezo au pengine kuwapita kabisa na alifikia katika levo ambayo ilimuwezesha kufungua malango ya kwenda kwenye Galaksi nyingine ambako Mkuu wa Enzi na wajumbe wake huishi.
Wakati Sharf anafikia levo ya juu kabisa akiwa amejitenga alijikuta akipata uwezo wa kuweza kusafiri katika eneo lolote juu ya dunia , ikiwemo kuingia katika gereza la roho na kutoka ambalo lilitengenezwa na Wajumbe wa mkuu wa enzi , pamoja na kuingia ulimwengu wa kimaajabu wa majini pepo , pamoja na ulimwengu wa jicho la Anga kipindi hicho bado ulimwengu huo haujafahamika bado .
Katika matembezi yake hayo alikuja kujifunza ulimwengu wote wa aina tano umeungana katika sayari moja ya dunia kwa nama ya kipekee.
Mkuu wa Enzi pamoja na wajumbe wake ilionekana walitumia uwezo mkubwa sana wa akili kutengeneza kitu kama hicho.
Na wakati wa utenganisho kuanza kulikuwa na majini wengi wabaya ambao walikuwa wamefungiwa katika gereza la roho lakini kutokana na nguvu kubwa za giza walifanya ulimwengu wa majini wwatu kulemewa
Hivyo ndipo Wajumbe wa mkuu wa enzi walipotengeneza malango ya anga ambayo huunganisha ulimwengu wa jicho la anga na Gereza la roho na kuanza kunyonya nguvu za giza kuzijaza katika ulimwengu huo.
Kwa bahati nzuri ni kwamba nishari hasi inao uwezo wa kunyumbulishwa na kutengeneza radi ya zambarau hivyo walitumia nguvu zilezile za kwao za giza kutengeneza radi katika mnara ili kuzuia majini hao wasitoroke
Mambo haya yote yalifanyika kwa ajili ya usalama wa binadamu kwani kipindi hicho ndio wakati wao uliwadia wa kuondoka duniani na kurudi walikotoka
Walikuwa na uwezo wa ajabu mno zaidi ya nguvu za nishati ya mbingu na ardhi hivyo kuwa na uwezo wa kusafiri kwenda katika mbingu nyingine kabisa ya kushangaza.
Lilikuwa ni jukumu lao kulinda dunia kwa wakati huo lakini haikuwa kazi yao kulinda dunia milele hivyo mara baada ya kumaliza misheni yao walipaswa kurudi.
Misheni yao kubwa ilikuwa ni kwa ajili ya kuendeleza kizazi cha binadamu hivyo walipaswa kuhakikisha dunia sehemu ambapo ni nyumbani kwao panakuwa salama.
Hivyo majini wale wabaya walifungiwa gerezani na wale ambao walionekana kuwa wajanga wakawekewa mtego wa mnara ili kuwavuta kwenda kwenye ulimwengu mwingine
Sasa haya yote yalijulikana kwasababu waliacha maandiko juu kabisa ya mnara wa maajabu.
Ijapokuwa ulimwengu hizo zilionekana kama gereza lakini nia kubwa ya Mkuu wa Enzi kupitia wajumbe wake ni kutenganisha viumbe hatari na binadamu wa kawaida.
Viumbe wa dunia walikuwa ni majini watu , Majini pepo na binadamu na Mkuu wa enzi kupitia wajumbe wake alipanga kuacha mtu ambae anapaswa kuwa mwangalizi wa dunia na mtu ambae alichaguliwa kwa wakati huo ni Sharif lakini hata hivyo hakumpa misheni hio moja kwa moja.
Katika mnara wa Anga kuliwachwa nyaraka za lugha ilioandikwa na wajumbe , naraka hizo zilikuwa zikielezea mtu yeyote ambae ataweza kupitia mapigo tisini na tisa ya radi ya Zambarau na kufika kileleni mwa mnara , iwe ni binadamu , iwe ni jini mtu , iwe ni jini pepo kutoka ulimwengu wa majini pepo ilimaanisha nguvu yake ni kubwa ya kukidhi kigezo cha kurithi cheo cha Uangalizi kwa niaba ya Mkuu wa Enzi.
Ukweli ni kwamba Roma yeye ni Special case kutokana na uwezo wake mkubwa mno , kwanza kabisa mwili wake ulikuwa timamu mno kwa kwa kufanyiwa sayansi nyingi na kupata mabadiliko , pili aliweza kubahatika kumiliki Dhana ya Cauldron ambayo iitumiwa na Wakuu wa Enzi kumfungia mnyama Chaos.
Sababu ya Mkuu wa Enzi kupitia wajumbe wake kuacha nyaraka ya maelekezo juu ya mnara wa anga ilikuwa ni kama misheni ya kukidhi vigezo kwa mtu ambae anapaswa kuwa Mwangalizi kwa niaba.
Mkuu wa enzi aliamini mtu yoyote ambae ataweza kufika katika mnara huo na kuvuka Dhiki ya mapigo ya radi basi moja kwa moja inamaanisha anakaribiana ki uwezo na wajumbe wake hivyo anatosha kuwa mwangalizi.
Hivyo kwa lugha nyepesi ni kwamba wajumbe walikaribiana ki uwezo na mtu yoyote atakaefanikiwa kuingia katika mnara na kufika kileleni na hii ipo hata kwa Aoiline pia.
Wote ambao hufanikiwa kufika katika mnara huo kwa maelekezo ya nyaraka hizo wanapaswa kufanya chaguzi, mosi ni kuchukua Dhana ya Ngoma ya kinaoni na kuondoa radi inayowazuia majini pepo kutotoka katika ulimwengu wa majini pepo , pili ni kuiacha ngoma hio ili kuendelea kutenganisha binadamu na Viumbe hao hatari.
Ilikuwa ni kwa ajili ya kuwapa viumbe wote nafasi sawa , iwe ni majini watu , iwe ni binadamu wenye uwezo wa kuvuna nishati za mbingu na ardhi au majini.
Kama angetokea kiumbe chochote kikawa na nguvu na kuua binadamu basi ilimaanisha hio ndio hatima yao , hivyo hivyo kwa majini pepo.
Sasa Sharif ndio wa kwanza kabisa kuingia katika ulimwengu wa majini pepo kupitia mnara na hio yote ilikuwa ni kutokana na shauku yake tu.
Wakati huo mnara huo ulikuwa wazi masaa yote na miaka yote na haikuwa kila baada ya miaka sitini.
Mara baada ya kudhurula ndani ya ulimwengu huo wa majini pepo kwa muda hatimae aliamua kuondoka kwa kuingia katika floor ya kwanza ya mnara wa mbingu na kupanda juu hatua kwa hatua akipitia mapigo ya radi mpaka kileleni, alikuwa na uwezo mkubwa hivyo ilikuwa rahisi kwake.
Sasa mara baada ya kufika katika kilele cha mnara huo ndipo alipokutana na nyaraka zilizoachwa hapo kwa makusudi maalumu na palepale alijua yeye ndio wa kwanza kama kiumbe wa dunia kufika hapo.
Na ndipo alipokuja kupta ufahamu juu ya uwepo wa viumbe hai kabla ya binadamu katika uso wa dunia ambao walipotea mara baada ya Dunia kupigwa na kimondo , alipata kujua pia ni Mkuu wa Enzi na wajumbe wake waliokuwa wakihakikisha dunia inakuwa salama kwa kupindisha magimba makubwa kutoka angani ili yasiingie katika mzingo wa dunnia.
Haikueleweka kwanini Mkuu wa Enzi alikuwa akijali sana viumbe wa Dunia , haikueleweka kwanini alikuwa akiwalinda lakini mara baada ya Sharif kusoma barua hio alijua kwanzia siku hio amekuwa Mwangalizi wa usalama wa dunia, yaani amekuwa kama Mjumbe wa Mkuu wa Enzi licha ya kwamba ni nusu binadamu nusu jini.
Kila yoyote ambae angeweza kufika kilele cha mnara huo ilimaanisha alikuwa na uwezo wa kuibeba misheni na sio hivyo tu anao uwezo pia wa kuchukua nguvu ya Ngomba kama uwezo huo wanao.
Mwanzoni Sharif mara baada ya kupata misheni mpya alitaka kupotezea , lakini badala yake aliona lazima dhamiri ingemfunga milele hivyo moja kwa moja aliamua kukubali misheni yake na kwanzia hapo ndipo alipoitwa Master namba moja.
Alikuwa na uwezo hata wa kuondoka ndani ya hii syaari lakini hakufanya hivyo na aliamua kuishi kwa zaidi ya miaka elfu hamsini kwa ajili ya kutii maagizo ya mkuu wa enzi.
Lakini Sharif hakuwa na mpango wa kuwa Master namba moja milele , hakuwa akiataka kuwa muangalizi milele na alipaswa kuondoka na kuwafuata Wajumbe wa mkuu wa enzi na ili kuondoka misheni ilikuwa ni kutafuta mrithi wake ambae angeendeleza alipoishia
Kwa lugha nyepesi ilikuwa ni kwamba misheni yake ilipaswa kuisha mara tu baada ya kupata mrithi.
Sasa siku hio hio ambayo aliingia katika mnara huo tayari alikuwa ashaandaa mpango wa kutafuta mrithi , yaani siku ambayo anapata isheni ndio siku ambayo alianza kuanza juu ya kupata mrithi wake.
Sharif alichukua ufunguo wa ulimwengu wa jicho la anga , yaani ile hazina inayofanana na kokoto ya umbo la mviringo na kisha ndipo alipotoka na kurudi ulimwengu wa binadamu.
Wakati anatoka tayari vita baina ya viumbe wa dunia ilikuwa ikiendelea bado na kutokana na uwezo wake aliamua kuzamia katika miliki ya majini chotara yaani Panas na kujiita jina linalofanana na jamii hio lakini licha ya kuwa na uwezo mkubwa hakujionyesha kabisa.
Ilikuwa ndio kipindi hiko hiko aliweza kukutana kwa mara ya kwanza na mrembo Aoiline ambae ndio yupo juu ki uwezo na kuzoeana lakini kwa bahati mbaya wakati huo tayari alikuwa na misheni hivyo ilikuwa ngumu kuwa nae kimapenzi , ijapokuwa mwanamke huyo alikuwa mrembo na alionyesha kila dalili ya kupendwa lakini alimkataa.
Aoiline alikuwa ni jini mwenye akili sana na alikuwa na uwezo wa kukisia mambo mengi hata yale ambayo Sharif hakumweleza na ili kutokuwa kikwazo kwa Sharif aliamua kutorokea kwa hiari yake katika ulimwengu wa majini pepo.
Aoiline hakuvutwa a mnara kama ilivyokuwa kwa majini wengine bali yeye mwenyew kwa hiari yake aliacha ndugu na kupotelea kwenye ulimwengu wa majini pepo.
Sharif hakutaka kumzuia Aoiline kutokana na kwamba alikuwa na vitu vingi vya kufanya.
Sharif ili kumaliza vita aliamua kuwavuta majini pepo wengi kuingia katika ulimwengu wa jicho la anga na mara baada ya kufika huko alijilipua kimaigizo huku akiwaua wote na ndipo walipogeuka mizimu baadae.
Kitendo alichokifanya Sharif katika ulimwengu huo wa jicho la Anga ulifanya kutengeneza upenyo kupitia ulimwengu wa ajini watu kwa kila baada ya miaka mia moja.
Kwasababu alichukua Hazina iliokuwa ni ufunguo unaounganisha ulimwengu wa jicho la anga na mnara geti lilijifunga na kupelekea nguvu hasi ya kutosha kutoingia katika mnara na hatimae kwenye Dhana ya ngoma kirahisi pamoja na kushikiria geti la mnara kwa upande wa majini pepo hivyo kusababisha mnra huo kufunguka kila baada ya miaka sitini kipindi maalumu ambacho Ngoma hio imekusanya nishati za kutosha kushikilia geti la mnara kuwa wazi.
Mara baada ya kutoa hazina hio alirudi katika asili yake sasa ambayo ni familia ya Sharif na kuacha hazina hio pamoja na ujumbe kwa kuwaeleza ili kurudisha wenzao ambao wamepotea yaani wale aliolipua katika jiccho la Anga na ambao wamemezwa na mnara basi Hazina hio ndio njia na hakueleza ni kwa namna gani ni njia na alifanya hivyo kutokana na kwamba aliamini hatima ndio itaamua.
Sharif yeye liacha hazina hio katika mikono ya ndugu zake akichukulia kama zawadi kwao lakini wakati huo akikisia kwamba kama itaokea majini pepo wataiteka miliki ya majini watu hivyo kuna uwezekano wa hazina hio ikafanya kazi kwa kufungua lango , kitu kama kilichomtokea Roma wakati ule , ilikuwa ni kama kitu kilichopangwa ambacho hakiwezi kubadilishika.
Sasa miaka elfu therathini ilipita ya Sharif kuendelea kufanyia kazi misheni aliopewa na kimya kimya aliendelea kuangalia ndugu ake wakati huo huo akiisaidia dunia katika kudili na mambo hatarishi.
Lakini kadiri alivyokuwa akiishi alikuja kugundua alikuwa akizidi kuongezeka ki uwezo maradufu huku binadamu , majini pepo na majini watu wakizidi kupoteza uwezo .
Majini pepo ambao walibakia katika ulimwengu wa kibinadamu ili kuepuka kushambuliwa na majini watu walienda kujichimbia katika ulimwengu wa jangwa tenganifu huku wakiaha Hazina katika ulimwengu wa binadamu wakiamini hio ndio sehemu waliopotea ndugu zao na kama walivyoambiwa ndio njia ya kuwarudisha basi tokea hapo waliifanya kama Dhana ya imani yao.
Upande wa majini watu Sharif pia aliona ni upuuzi mtupu kwani hakukuwa na wapanda levo zaidi ya udanganyifu tu.
Kitendo cha majini kupoteza uwezo kila kukicha ilimfanya kuwa na wasiwasi kama itakuja siku kupata mrithi na kujiuliza kama kuna hata haja ya viumbe hao kubakia katika dunia.
Alijjiuliza maswali mengi na wakati huo moja ya maswali hayo ni je kuwaacha binadamu kuwa watawala wakuu wa dunia kama ilivyoamuliwa na Mkuu wa enzi na kuwatenganisha na majini pepo.
Kadri ambavyo alikuwa akipanda levo ni kama alikuwa akijiweka mbali zaidi na viumbe wa binadamu , alichojali ni usalama wa dunia tu na sio usalama wa binadamu au majini.
Lakini kabla hata hajajua majibu ya maswali yake ikiwa imepita miaka elfu therathini ndipo viumbe kutoka sayari nyingine walitua duniani.
SEHEMU YA 787.
Sharif kwa muda mrefu alikuwa ashajua juu ya kabila la viumbe hao licha ya kwamba hakuwahi kufika katika sayari ya Mars.
Tofauti na kuwa na wasiwasi juu ya ujio wa hawa viumbe alijikuta akifurahi.
Likija swala la nguvu na uwezo miungu walikuwa na nafasi kubwa hapo kutokana na kwamba walizaliwa wakiwa na uungu ambao unawawezesha kuzitambua kanuni za anga.
Uwezo wa namna hio ni kama zawadi kutokana na kuwa na nguvu kubwa mno.
Kitu kingine kilichowapatia faida miungu ni uwezo wao wa kuhamisha nafsi zao kutoka mwili mmoja kwenda mwingine , hivyo walikuwa wakiishi muda mrefu kuliko binadamu.
Ijapokuwa miungu walikuwa na uwezo wa chini kuliko wajumbe walikuwa na uwezo wa kutegemea miili yao tu kusafiri kutoka katika sayari moja kwenda nyingine lakini ilikuwa ngumu kwa majini pamoja na binadamu kusafiri kutoka sayari moja kwenda nyingine na kuweza kupona na adha ya anga labda tu mtu awe levo ya mapigo elfu kumi ya radi.
Kitu kingine ambacho kilionekana kuwa faida kwa miungu ilikuwa ni kwamba wameungana pamoja kifikra yaani miungu yote kumi na mbili na walikuwa na mama mmoja wa kiuungu hili liliwapelekea kupunguza mingongano ya ndani licha ya kwamba kuna kutoridhika kati yao.
Ustaarabu katika sayari ya Mars chini ya miungu ulikuwa umeendelea mno kuliko hata wa dunia ya sasa.
Kama ugefananisha ustaarabu wa miungu na wa sasa wa kibinadamu ni kama vile ndio kwanza tupo katika zama za mawe, miungu walikuwa wa moja na hakukuwa na utofauti wa kidini wala kimsimamo ni kama wote walikuwa na mawazo sawa, ilikuwa ni sahihi kuita ulimwengu wao ni wa kiutopia.
Sasa mara baada ya sayari yao kushindwa kusapoti maisha na mti Mama kunyauka mahai sahihi walipoona ni pakukimbilia ni sayari ya Dunia lakini walijua fika miili yao haiendani na mazingira ya dunia kwa muda mrefu na hapo ndipo maauzi yalipofanyika kuhamisha nafsi zao na uungu wao kwenda kwa nafsi za binadamu.
Miungu kumi na mbili kutokana na kwamba walikuwa ndio uzao wa kwanza wa mti walikuwa na nguvu kubwa na walifanikiwa kuziteka nafsi za binadamu na kutawala miili yao , lakini ndugu zao ambao hawakuwa na nguvu kubwa kama wao waliishia kumezwa na nafsi za binadamu.
Sasa mara baada ya vita kuanza kati ya majini watu na miungu upande wa Sharif yeye alikaa pembeni kuangalia kinachoendelea na hakusaidia upande wowote.
Ijapokuwa Sharif alikuwa na uwezo wa kuua miungu hao kirahisi tu ikiwemo Athena na Zeus lakini hakuwa na sababu ya kufanya hivyo.
Na hio ni kwasababu tokea zamanni alikuwa ashaacha kuingalia dunia kwa mtazamo wa kawaida , binadamu na miungu wote waliishi katika anga na mhimili wao ni sayari zao , ni rahisi kusema wote wana haki ya kuishi katika anga hivyo Sharif aliona hata wao wana haki ya uhai ndani ya mhimili wa sayari ya dunia na hakutaka kutofautisha viumbe kwa kuwaita Alliens.
Kipindi hicho ndio ambapo Sharif wazo lilimwingia na kuona kama dunia itatawaliwa na miungu basi moja kwa moja misheni yake inaweza kufikia mwisho.
Aliona kabisa miungu walikuwa na uwezo wa kulinda dunia na isipotee kwa kugongana na magimba au vimondo na wakati huo huo ustaarabu wao ulikuwa umekuwa sana kuliko hata ilivyokuwa binadamu.
Ukumbuke kipindi hichi miungu wakati wanashuka binadamu hawakuwa hata wakijua gari ni nini na walitegemea miguu yao kusafiri.
Sharif katika misheni yake ilikuwa ni kulinda viumbe wa dunia wasipatwe na majanga ya nje ya dunia lakini sio kuwafanya binadamu kuwa juu ya viumbe wegine au kuwa chini ya viumbe wengine , alijua kama miungu watakuwa ndio viumbe wenye nguvu zaidi ya binadamu kutokana na maendeleo yao basi wasingepoteza rasilimali za dunia katika kupambana wao kwa wao bali wangefikiria namna ya kuendeleza dunia jambo ambalo si baya.
Wajumbe wa mkuu wa enzi walikuwa tayari wamekisha andaa kila kitu , kulikuwa na safu ya ulinzi wa gereza la roho kwa ajili ya mashetani , mapepo na mazimwi kutokana na kwamba hawakutaka kuwaua wote na kutokana na hilo Sharif aliona hata kabila la waliostaarabika la miungu Mkiuu wa enzi na wajumbe wake wataweza kuwavumilia , isitoshe ndio walikuwa wakitafuta mahali pa kuishi.,
Ukweli ni kwamba Sharifi wakati huo alikuwa katika kujiluliza kwingi kama angeweza kufanya maamuzi hayo angeenda kinyume na mipango ya mkuu wa enzi lakini kwasababu hayakuwa maamuzi rahisi basi aliamua kuangalia kwanza kitakahotokea.
Katika miaka iliofuata ya miungu kufanikiwa kutawala baadhi ya miili ya kibinadamu , Sharif aliweza kugundua ni miungu wamepoteza miili yao na hawawezi kuendeleza kizazi chao.
Kitendo cha miungu kutelekeza miili yao ilimfanya Sharif kuingia katika uchunguzi na alichokuja kugudua kilimshangaza sana , ilionekana miungu hawakutegemea jua moja kwa moja kwa ajili ya kuishi na miili yao kusapoti maisha bali walitegemea jua kwa njia isiokuwa ya moja kwa moja.
Sharif alifungua miungu waliishi chini ya mti na huo mti kazi yake ilikuwa ni kubadilisha nishati ya jua kuwa nishati tofauti ambayo husapoti miili yao na kuwapelekea kuzaliana na mti kuwatunuku uungu.
Mara baada ya sayari yao kukubwa na janga lililowafanywa wakimbie Astreus moja ya viumbe hao aliamua kuficha moyo wa Gaia katika teknolojia ya kipekee na kuja nayo duniani , moyo wa Gaia ilikuwa ni kama mbegu ya mti huo.
Sasa Sharif mara baada ya kufanya utafiti wake wa chini chini alikuja kugundua mengi , alishangaa mara baada ya kugundua ni kweli mti maa ndio ulikuwa chanzo cha nguvu za miungu lakini nguvu zao walizipata kwa gharama ya nishati ya sayari yao kiasi cha kuipelekea kupoteza sifa ya uhai kwa spidi kubwa sana.
Ufumbbuzi wa jambo hilo ulimfanya kusita na mpango wake wa kuwafanya miungu kuwa juu ya binadamu
Alijua kama miungu wangepatia dunia kuitawala ni swwala la muda tu kuupata moyo wa Gaia na kisha kuufufua na kupanda Mti Mama tena ili kuarudisha uzao wao.
Misheni yake ilikuwa ni kulinda dunia na kama jambo hilo angeruhusu ilikuw ani kama anaangalia dunia ikiangamia.
Sharif ambae alikuwa na cheo cha uangalizi kutoka kwa Mkuu wa Enzi alijikuta akishindwa kufanya maamuzi ya moja kwa moja aidha kuwapa ukuu miungu kuitawala dunia au kuendelea kulinda ustaarabu uliopo wa kiumbe binadamu.
Wakati huo huo aliikuwa akiataka kuungana na wajumbe kwa Mkuu wa enzi haraka iwezekanavyo lakini hakuwa na uwezo wa kuondoka duniani kabla misheni yake haijaisha baada ya kupata mrithi.
Hivyo ilimpelekea Sharif kuchukua hatua kama Mwangalizi na kisha kuwaza maswala mengine baadae.
Alijifanyisha ni jini mtu kutokea Hongmneng kwa kubadili muonekano wake pamoja na uwezo wake kuushusha kidogo na hivyo kumfanya awe moja ya kiumbe jini mtu mwenye nguvu kubwa.
Baada ya kujifanyisha anapigana na Zeus alimtega na kumwingiza katika ulimwengu wa majini watu na kisha akamfungia katika gereza la roho huku Athena akimwahia huru makusudi.
Kufungiwa kwa Zeus ilimaanisha miungu kukosa nguvu ya kivita kwa asilimia hamsini na kushindwa kutamba mbele ya majini watu hivyo wakaona waache vita na hapo ndipo ulipotokea mkataba wa The Gods Treaty .
Maongezi hayo kati ya Roma na Master namba moja yalidumu kwa muda mrefu sana tokea mhana mpaka usiku.
Roma kadri alivyokuwa akimsikiliza Sharif akielezea historia hio ya miaka mingi alijikuta akkishindwa kujizuia na kutoa tabasamu hafifu.
“Dogo hivi unadhani kwa yote ambayo nimefikiria na kufanya ilikuwa ni kupoteza muda?”
“Sidhani kama ilikuwa ni kupoteza muda , kwako wewe haikujalisha ni binadamu , majini au miungu walikuwa ni kama kunguni tu ambao hupambana wao kwa wao na wewe ulikuwa ukiifurahia vita yao , haikujalisha maamuzi yako yalikuwaje lakini mwisho wa siku kila kitu ni juu yako”Aliongea Roma na kumfanya Sharif kuoekana ni kama vile ametegemea jibu la aina hio.
“Kama kweli hicho ndio unachofikiria , kwanini ukamuacha Athena ili hali ulikuwa na uwezo wa kufanya hivyo , kama hutaki kumua unafanya nini hapa peke yako?, unazo nguvu za kufanya maamuzi yoyote yale lakini bado upo hapa kujisahaulisha , vitu nilivyofanya vinaweza kuwa nikupoteza juhudi zangu lakini ni angalau kuliko chaguzi uliofanya
Mara baada ya neno Athena kutamkwa macho ya Roma yalicheza huku akikunja ngumi yake na kihisia alikosa mhimili lakini mara baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzitoa alionekana kutulia , kwani bado alikuwa katika bumbuwazi juu ya maneno ya Sharif.
Roma alijiuliza hata kama ni kweli anao uwezo wa kufanya maamuzi yoyote je ni maamuzi ambayo anaweza kufanya kirahisi.
“Muunganiko wangu na hii sayari pamoja na viumbe vyote hai ni kama muunganiko wako na Athena , ijapokuwa ni toafuti lakini kuna uhusiano , umeshindwa kufanya maamuzi kwa sababu ya mwanamke mmoja , je unadhanni ilikuwa rahisi kwangu kufanya maamuzi kwa niaba ya viumbe wote?”
Awamu hio Roma hakuonyesha kumcheka ni kama kwa namna flani alikuwa akizielewa hisia zake , lakini kwa wakati mmoja alikuwa amekasirika kwasababu alijua nia yake kwake.
“Umefanya mambo mengi na bado ukasubiri kwa miaka elfu ishirini je ni kwasababu ulishindwa kufanya maamuzi wewe mwenyewe , ndio maana unataka mimi ndio niamue ni nani anapaswa kuitawala dunia?”Aliuliza Roma na Sharif aliishia kutingisha kichwa asikatae.
“Ndio , unaweza chukulia hivyo , lakini haya sio maamuzi yangu ni hatima yako kama unabii ulivyotabiriwa , wewe ndio mtu pekee ambae utaathiri matokeo”Aliongea Sharif.
“Nini kilichopo nyuma ya huu unabii ambao Athena ameshikilia , je atakuwa alikujua tokea mwanzo na uwezo wako na misheni yako, lazima utakuwa unajua kila kitu kuhusu Athena alichokifanya lakini ukamuacha tu makusudi , je ni kweli?”Aliuliza Roma huku akisaga meno yake.
“Dogo haina haja ya kuwa na hasira ,najua kila kitu unachotaka kufahamu na nisikilize nitakuambia taratibu , nimekuja kwako kuondoa hali ya kuchangayikiwa kwenye moyo wako …”Alionekana kuvuta pumzi na akaendelea.
“Kinachosemekana kama unabii pengine mtu ambae anaweza kukielewa ni Athena mwenyewe, lakini ninaweza kufanya makisio kwa kuangalia tu uungu wake , inasemekana karama ya unabii ndio upekee wa uungu wake , kwa kutegemea tu kanuni za anga anao uwezo wa kujua nini kitatokea baadae , inaweza kuwa ni sekunde ijayo ,dakika , siku , miaka na hata zaidi ya milenia ya wakati ujao …”
Njia pekee ambayo humfanya hupta huo unabii ni kitu ambacho anakifahamu yeye mwenyewe na hakuna mtu anaeweza kuelewa , ni kama sisi tu tunavyopata ufunuo , hata hivyo ukubwa wa athari za mtu , eneo au elementi nyingine za unabii wake katika anga ndio nguvu yake ya kiroho inavyotumika sana , isitoshe mbinu hio ya unabii mkubwa unatokana na kanuni za anga”
Kwa maneno mengine kama Athena atataka kutabiri kesho ya mtu wa kawaida basi ni sawa na kutumia chembe ya nguvu yake ya kiroho lakini kama atata kutabiri kesho yangu haiwezekani.. hii ni kwasababu nimepanda na kuwa juu ya kanuni za anga ambazo anazifahamu , sipo kwenye dimension sawa na yeye
Hatas kama atataka kukutabiria wewe Roma Ramoni itakuwa ngumu mno kwake , hio ni kwasababu wewe Roma wa sasa umebadilika sana tofauti na zamani , unabii wake ulikuwa sahihi tu kabla ya wewe kuingia levo ya mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi , unabii wake ni kama unafamna kujua unafikiria nini na unataka kufanya nini katika sekunde inayofuata hivyo kama utapigana nae atashindwa kuyatabiria mashambulizi yako hivyo hatojisumbua kutumia uwezo wake wa kutabiri na atashindana na wewe bila ya hira yoyote”
Kwa lugha nyepesi ni kwamba Athena anaonekana kuwa na nguvu kutokana na kwamba anao uwezo mkubwa wa kutabiri tukio litakalotokea ndani ya sekunde moja kuendelea na hii inamfanya kuweza kukudhibiti kabla hata hujafanya shambulizi lakini kama mtu ana uwezo wa juu na yupo juu ya kanuni zake za anga basi moja kwa moja unabii wake unakuwa sio sahihi, alikuwa akimuweza Roma kutokana na kwamba alikuwa na uwezo wa kumtabiria na kujua kila kitu atakachofanya lakini hio yote ilikuwa ni kipindi kabla hajapitia mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi.
“Kwahio Athena hajui kabisa wewe ni nani?”Aliuliza Roma.
“Hapana , ijapokuwa hawezi kutumia unabii wake kukadiria uwezo wangu pamoja na wasifu wangu lazima atakuwa anajua uwezo wangu kupitia njia zingine , ukweli ni kwamba ashajua muda mrefu nitakubali kila kitu anachofanya hivyo hakuwa na haja ya kunitaja kwa yoyote , ni kama tu alivyoweza kuupata moyo wa Gaia , ijapokuwa alishindwa kutabiri eneo husika utakapotokea lakini alikuwa na uelewa ulikuwa ndani ya Taifa la Korea na wewe ndio utakuwa kama ramani kwake”
“Kama mimi wa sasa nitajiweka katika levo ambayo atakuwa na uwezo wa kufanya unabii sahihi , je atakuwa anajua kama unabii huo ni sahihi?”Aliuuliza Roma na kumfanya Sharif kuangau kicheko.
“Ukweli ni kwamba mbingu yake ya utabiri mkuu ishathibitishwa muda mrefu sio sahihi”
“Unamaanisha nini kusema hivyo?”Aliuliza Roma akiwa katika mshangao.
“Umenisikia vizuri , unabii wake mkuu wa Athena sio sahihi kwa asilimia mia moja , kuna mbinu za moja kwa moja za kuharibu utabiri wake kuliko kwenda mbali kwa kujiweka katika levo anayoweza kutabiri”Aliongea na kumfanya Roma kuonekana kuchanganyikiw .
“Ili kufanikisha hilo ni kumhusisha yeye mwenyewe kama kipengele cha unabii”Aliongea Sharif na kumfanya Roma kuwa na ufahamu unaokuja kwa mbaali.
“Athena ndio wa kwanza , mtu anawez akusema ni yeye pekee anaejua kila kitu anachotabiri kwa ukamilifu , hii inamaanisha kwamba ikiwa anataka kuathiri mustakabali wa jambo , anachohitajika kufanya ni kurekebisa tu baadhi ya hatua alizokuwa amepanga kuchukua na historia itabadilika yenyewe na mustakabali utafuatia”
“Kama ni hivyo , uliposema unabii wake haupo sahihi miaka kadhaa iliopita , je ni kwasababu alifanya kitu ambaho hakupwaswa kufanya?”Aliuliza Roma.
“Upo sahihi , ni kipindi kilichopita ambacho kinakuhusisha wewe zaidi, Athena hakutarajia atakuzalia mtoto na kumfanya ahame mwili mapema”Aliongea Sharif na ilikuwa ni kama ameshusha bomu.
“Unasema nini!!”Roma alijikuta akishindwa kuedelea kukaa na kujikuta akisimama huku macho yake yakimtoka wakati akuongea.
“Lanlan ?! , unamaanisha Seventeen alikuwa…”Aliuliza Roma kwa kuchanganyikiwa lakini Sharif alikunja nne kwa pozi murua.
“Hivi bado hujawahi kuwaza , hakukuwa na hali isiokuwa kawaida wakati ulipokuwa nae ?,Seventeen ni mwanamke ambae Athena alitawala mwili wake wakati akiwa hatua za mwisho za uhai wake , yote haya alikuwa ni sehemu ya unabii wake wa mwanzo”
Roma alijikuta akipata picha ya Lanlan kulazimisha Edna kuwa mama yake mzazi kila muda na Roma kukumbuka wakati ambao Edna alikuwa akitamka maneno ya Seventeen aliowahi kuongea.
Roma alikuwa na hisia za namna hio lakini mara baada ya kuthibitisha kwa masikio yake ilifmanya ajione ni kama amepigwa na radi.
“Sina uhakika unabii wa Athena wa mwanzo ulikuwaje lakini nilikuwa nikimwangalia hatua kwa hatua , ni wazi kabisa mara baada ya kuhamia katika mwili wa Seventeen hakutaka kabisa kuwa karibu na wewe lakini alishindwa kutabiri wakati atakapoamka katika mwili wa Seventeen tayari ana hisia za kimapenzi kwako na kubeba mimba yako”
“Unapaswa kuelewa kanuni za anga hazina athari yoyote mbele ya mapenzi ya kibinadamu ambayo huvuka nafasi na muda , upendo ni hisia nyeti ambazi hata miungu na akili zao zote wameshindwa kuelewa , ndio nguvu ya ajabu ambayo binadamu anayo ambayo haipo chini sana na uungu wa miungu”
Athena anaweza kutabiria kila kitu isipokuwa tu upendo anaokaribia kukutana nao , kwani mapenzi ya kibinadamu kadri yanavyosababisha hisia kali ndivyo unavyokosa maana na mantiki , Wakati Athena nafsi yake inaamka katika mwili wa Seventeen tayari alikuwa ni mjamzito na mtoto wako na ni wakati alipokuwa amezama baharini , labda unaweza kujiuliza kwanini aliamua kujificha kwa kutumia helmeti , kuzaa mtoto na kisha kumkabidhi kwa Tang Chi , lakini hayo yote yalibadilisha historia nzima , mapenzi ya kweli na mtoto ambae hakupaswa kuwepo kwenye maisha yake ilimfanya kufanya chaguzi nyingine ili kurekebisha makosa ya unabii wake wa mwanzo”
“Hembu subiri”
Roma alionekana kuingialia maneno ya Sharif huku akiwa na muonekano ambao una wasiwasi.
“Kama uyasemayo ni kweli , si inamaanisha Edna tokea mwanzo hakuwa ni Athena na hata Seventeen hakuwa Athena wakati tulipoanza kupendana pia?”Roma aliuliza na kumfanya Sharif kutingisha kichwa kukubaliana nae na palepale kumfanya Roma kupambwa na tabasamu la ahueni.
“Asante kwa kuniambia haya .. tafadhari endelea ..nataka kujua kila kitu”
Muda huo alonekana kuwa na furaha kana kwamba amezaliwa upa , miale ya mwanga ilipiga katika maisha yae na kufukuza kiza chote.
Iwe ni kwa Edna na pacha wake Seventeen hao wanawake wote wlaikuwa ni halisi , hawakuwa udanganyifu uliotengenezwa na Athena.
Ukweli ni kwamba hakuwa na chuki na Athena kwasababu yalikuwa ni maamuzi yake ammbayo yaliwezesha Lanlan kuzaliwa.
Kwa sababu zozote zile Roma hakutaka kuvuta taswira ni kwa namna gani Seventeen angejisikia kama angepoteza uhai akiwa na mtoto tumboni kama Athena asingeamua kumzaa.
Kwa ufupi ni kwamba Athena ili kuhakikisha anachotaka kitokee ni sahihi atafanya vitu ambavyo vinachangia mustakabali wa tukio husika , udhaifu mkubwa wa unabii wake ni pale tu anaposhindwa kujitabiria yeye mwenyewe , kitendo cha kushindwa kujitabiria mwenyewe ilimtokea kufanya kitu ambacho hakupaswa kufanya ambacho ni kumzaa Lanlan ambae ni mtoto wa Roma.
Yaani Athena alipanga kuutawala mwili wa Seventeen kwa kuhamisha nafsi yake na uungu wake lakini ikumbukwe kuhamisha nafsi kutoka kwenye mwili mmoja kwenda kwa mwingine sio kitu kinachotokea mara moja , nafsi inapohama hulala kwa kipindi cha muda flani na kisha ndipo huamka , kuwahi au kuchelewa inategemeana sana na uwezo wa uungu wao.
Sasa Athena mara baada ya kuhamisha nafsi yake kwenda kwa Seventeen kutokana na kushindwa kujitabiria wakati anaamka katika mwili wa Seventeen tayari alikuwa mjamzito wa Roma na ndio kipindi ambacho Seventeen anakaribia kupoteza uhai mara baada ya kuzama baharini wakati wa kulipuliwa na bomu na kundi laTakamagahara
Hivyo ni kama Athena alivaa mwili ambao ulikuwa ni mjamzito tayari a tofauti na kuua kiumbe kilichokuwa tumboni aliaamua kulea ujauzito kwa siku kadhaa na kisha akajifungua na baada ya hapo ndipo alipoenda kumkabidhi Lanlan kwa Tang Chi ili kumpelekea Roma , hivyo ni sawa kusema Seventeen na Athena walishikiana kumzaa Lanlan , Seventeen kama Seventeen alimpenda Roma na kubeba ujauzito wake , huku Athena yeye akarithi ujauzito wa Seventeen na kumzaa Lanlan.
Sasa ili kurekebisha unabii ambao Athena alitaka utokee alifanya maamuzi mengine na pengine ndio maamuzi yalioacha akaamua kuuvaa mwili wa Edna pacha wake Seventeen, Roma anafurahi kwa kuona kwamba tokea mwanzo Edna na Seventeen walikuwa halisi na kama walimpenda walimpenda kweli kabla ya kupoteza nafsi zao kwa Athena.
“Nadhani sasa unaweza kudhania ni kipi Athena alifanya ili tu kusahihisha makosa ili apate matokeo ya unabii wa mwanzo kuliko mustakabali ambao huamuiwa na hatima , ingawa kuhamisha nafsi inahitaji nguvu nyingi mno za kiroho lakini mwili wa Seventeen ulikuwa ukipoteza uhai taratibu na hata kama angekurudia ingekuwa tayari amekwisha chelewa kubadilidha unabii na katika maamuzi ya mwisho nipo Athena alipojikuta hana jinsi na kumtumia mtu ambae anaweza kuirudisha hitimisho la unabii wake wa mwanzo na mtu huyo ni Edna na alihama punde tu mara baada ya kuuachia mwili wa Seventeen , aliona kwasababu Edna na Seventeen ni mapacha wa kufanana basi anakuwa mtu sahihi kabisa wa kutengeneza mustakabali wa kesho ambao utakuwa sawa na unabii wake , hivyo maamuzi hayo alifanya mara baada ya kosa la mwanzo
Unapaswa kuelewa ugumu uliopo kuhamisha nafsi kwenda kwa mtoto ni tofauti na kwenda kwa mtot , bila kusahau anahamisha nafsi yake akiwa na asilimia ishirini tu ya nguvu zake zote
Ijapokuwa alikuwa na helmet la kumfanya asionekane na kuhama kimya kimya lakini ilikuwa haiwezekani kuamka mara moja na kwa kukamilika hivyo alichoweza kufanya ni kuufufua uungu wake tu katika mwili wa Edna huku akiitumia nafsi yake kumdhibiti Edna kila muda akihitaji
Wakati Edna anakuja katika hii hoteli sio yeye bali alikuwa ni Athena ambae alicheza na akili ya Edna , alitaka kuwakutanisha na kusababisha kilichotokea baadae , lakini hata hivyo kila kilichowatokea ilikuwa ni wewe na Edna katika uhalisia na sio Athena”
“Athena hakutaka kuhatarisha mpango wake kwa kumgundua mapema ndio maana hakutaka kuupandisha uungu wake wote katika mwili wa Edna ili kumtawala kikamilifu kwa muda mrefu , hivyo kuna muda aliuteka ufahamu wa Edna na mwili wake na kukutana na washirika wake akiwemo Yan Buwen , Athena hakumtawala sana Edna na mara zote aliibadilisha sura yake na kuonekana kama Mzungu mwanadada maarufu ambae ana historia nae nadhani unamjua”Aliongea.
“Clelia Allisanto”Aliongea Roma na hapo sasa ni kama akili yake inakaa sawa vizuri lakini kidogo akionekana kuchanganyikiwa Dorisi alisema alikutana na mwanamke alieitwa Clelia Allisanto wakati huo huo Edna alikutaa na mwanamke alieitwa Clelia Allisanto wakati Athena alikuwa akiishi ndani ya mwili wa Edna wakati huo
“Bila shaka kila kitu kilihotokea kati yako na Eda kilikuwa katika mipango ya Athena kutimiza unabii wake na ndio hizo hatua mlizokuwa mkipiga pamoja ndio zilizomuwezesha kufanikisha kurudisha hitimisho la unabii wake , lakini awamu hii hakutaka kuzembea kama alivyozembea kwa Seventeen baada ya kuchelewa kuamsha ufahamu wake bali aliamua kuwa macho wakati akiwa amejificha ili asifanye kosa tena , lakini hata hivyo kwasababu ya haraka kipindi cha muda wa kujihamisha ulikuwa mfupi sana na kwasababu hakutaka kulala tena kufuta kumbukumbu za Seventeen ndio maana ni kama Edna amekuwa na kumbukumbu zake ndio maana ilitosha kwa binti yako kuamini Edna ni mama yake mzazi , kwa maana hio nafsi ya Edna ina sehemu ya nafsi ya Seventeen ambayo imetokana na haraka za Athena”
Maneno yake yalimfanya Roma mapigo yake kwenda mbio mno kwasabu alikuwa amejua kitu amabcho hakutaka kukifikiria mwanzo.
“Kwahio unamaanisha Athena wa sasa .. ah namaanisha Edna licha ya nafsi yake kutawaliwa na Athena yeye pamoja na Seventeen hawajapotea , si ndio unachomaanisha?”Aliuliza Roma.
“Sahihi , ukweli ni kwamba kipindi ambacho Edna ameweza kutawala nafsi yake lazima kuna wakati alijihisi ana tatizo la akili lakini hakuweza kuongea chochote kutokana na nafsi ya Athena kumzuia , licha ya kwamba alikuwa akijua nafsi yake ilikuwa imetekwa ni kama kuna mtu mwingine katika akili yake lakini asingeweza kuongea chochote kwani Athena anamlinda, lakini sasa hivi ni tofauti kutokana na kufufuka kwa Moyo wa Gaia basi nguvu zake zote zitamrudia na atakuwa na uwezo wa kuzizima nafsi zote mbili za mapacha hao na kumiliki mwili wake kikamilifu na kwa kile ninachojua , miungu wote wakuu kumi na mbili hawawezi kupoteza kumbukummbu kila wanapohamisha nafsi zao lakini wanapoteza kwanza nafsi ya mwili uliopita kabla ya kuamka ambayo ni ya mmiliki wa mwili na ndio maana huchelewa kuamka hata kwa zaidi ya miaka ishirini kulingana na nguvu ya nafsi husika , lakini kwasbabau Athena alikuwa na haraka aliamua kulazimisha kuamsha nafsi yake kwa haraka katika mwili wa Edna na hakuwa na muda tena wa kufuta nafsi ya Seventeen , ndio maana utaona kuna muda mkeo ni kama anaropoka kitu alichofanya Seventeen lakini ni mara moja moja kutokana na kwamba ufahamu wake umekwisha kupotea hivyo nafsi yake inakuwa kama mtu ambae yupo ndotoni , haijalishi atakuwa makini namna gani lakini kuna muda atakuwa anatamka maneno kama vile anaota “
Roma sasa alielewa na ndio maana Edna kuna muda alikuwa kama Seventeen mtupu , iijapokuwa walikuwa mapacha lakini haikumaanisha walikuwa wakifanana , lakini hata hivyo Roma ni kama tumaini lilimwingia.
“Kwa maneno mengine kama nitaweza kufuta nafsi ya Athena nitaweza kufufua nafsi za wote wawili Edna na Seventeen”
“Haha.. aisee wewe ni mjinga”Sharif alijikuta akicheka huku akiatgisha kihwa chake , ni kama alikuwa akijua Roma anawaza nini.
“Unafikiri itakuwa rahisi , Athena ashatarajia utafikiria hivyo , alifanya makusudi kutozima nafsi zote mbili ili kuungana nazo , sasa hivi ni mtu katika nafsi tatu ndani yake, kwa maneno mengine labda tu Athena yeye mwenyewe aisalimishe nafsi yake na kufa , lakini chochote ambacho unapanga kuifanyia nafsi yake basi hivyo hivyo utaimiza nafsi ya Edna na Seventeen , Athena kafanya yote haya makusudi kabisa ili tu usije ukamgusa mpaka mipango yake itimie”
Maelezo hayo yalikuwa ni kama boriti ya radi ya bluu kwa kumfanya Roma matumaini yake yote kupot3ea.
Nini kitafuta usikose
ITAENDELEA.