Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Na tatizo lako ambalo hujalijua bado ni kuhisi ww ni mwandishi mzuri wakati ni mwandishi mbovu[emoji3][emoji3]unajaza visa visivyo na umuhimuTatizo lako wewe ni old school na tabia yenu kubwa ni kukariri , unadhani simulizi ndefu haziwezi kuhaririwa , hebu tumia hio simu yako kuingia hata Amazon kindle kuna simulizi zina episode 5000 ujifunze funze acha kuishia kuangalia makalio ya malaya ununue kama ulivyojinadi.
Kwa taarifa yako hii simulizi ipo kwa mhariri tayari na ina ISBN number.
Sema wazee wengine bwana mnajifanya wajuaji ila Exposure ndogo mno[emoji706][emoji706]
Na sipo hapa kwa ajili ya kuungwa mkono ndugu mwandishiHapa hutopata watakao kuunga mkono , ni kwa watu wenye akili kubwa tu
Nchi siku hizi imekuwa ya kupenda kuona pongezi kila kona,,hamtaki kukosolewa popoteKuna mmoja kashindwa kuuelewa uzi kaishia kulalamika ni mrefu sana kumbe kazoea simulizi za kimalaya malaya.
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Mkubwa, hukukosoa bali ulitoa kejeri sio kwa mwandishi tu bali hadi kwa wasomaji.Nchi siku hizi imekuwa ya kupenda kuona pongezi kila kona,,hamtaki kukosolewa popote
Hii ni hatari kwa Taifa
Siwezi kupokea ushauri kwa mtu ambae hajamaliza simulizi yangu yote Ila Shukrani kwa kutoa ya moyoni, kama unamkubali George kamsome , mimi nisomaji mzuri pia kuna waandishi sipendi kazi zao lakini kwangu haimaanishi sio wazuri ni radha tu inatofautianaNa sipo hapa kwa ajili ya kuungwa mkono ndugu mwandishi
Ukitaka kuwa bora pokea yote na sio kila makofi ni ya pongezi...usitegemee kusifiwa na kila mtu lazima wengine wakukosoe ndo utakuwa bora....
Na umemaliza yote kuisoma mkuu yaani wewe ni mpenzi wa simulizi za Singano ila unashupaza shingo tu. Ungekuwa haikubali angeacha muda mrefu wala usingekuwa unaonekana kwenye huu uzi unalalama. Karibu tuendelee kule kwa HamzaNa tatizo lako ambalo hujalijua bado ni kuhisi ww ni mwandishi mzuri wakati ni mwandishi mbovu[emoji3][emoji3]unajaza visa visivyo na umuhimu
Kwahiyo umetuletea kabla haijamaliza kumehaririwa??
Jitahidi kusoma waandishi wa umri wako nilishakupa mmoja Iron mosenya tafuta kazi zake,kuna mwingine nae muhusuka mkuu huwa ni Martin Nguzu pitia pia uone namna riwaya za ujasusi zinakuwa
Riwaya ya ujasusi unajaza mavisa ya kufikirika mara Majini,mara mashtani[emoji3]
Simulizi yako mimi sikuisoma hapa Jf niliinunua kwa 10k nikasoma mwezi mzima haiishi na nikajikuta badala ya kupata burudani inachosha yani inanipa uchovu [emoji848]ikabidi niende Kipande cha mwisho kuona Roma na Edna wataishia wapi na ndo nikajilaumu kupoteza mwezi mzima kusoma Simulizi mbovu ya kiwango chako....Siwezi kupokea ushauri kwa mtu ambae hajamaliza simulizi yangu yote Ila Shukrani kwa kutoa ya moyoni, kama unamkubali George kamsome , mimi nisomaji mzuri pia kuna waandishi sipendi kazi zao lakini kwangu haimaanishi sio wazuri ni radha tu inatofautiana
Ushauri wako sio lazima ni uchukue so tuishie hapa .
Hii simulizi nimesoma vipande kadhaa nikaishia ROMA anaanda tamasha kwenye kampuni ya Media nikaona inachosha tu mwiliNa umemaliza yote kuisoma mkuu yaani wewe ni mpenzi wa simulizi za Singano ila unashupaza shingo tu. Ungekuwa haikubali angeacha muda mrefu wala usingekuwa unaonekana kwenye huu uzi unalalama. Karibu tuendelee kule kwa Hamza
Hongera mkuu kwa kumuunga mkono mwandishi, hakika wewe ni muungwanaMnachopaswa kuelewa sikusubiria kuisoma bure hapa niliamua kuunga juhudi za Mwandishi kwa kuinunua
Nyie mlopewa Bure sifieniView attachment 2975206
Hamza mzee😂😂😂Na umemaliza yote kuisoma mkuu yaani wewe ni mpenzi wa simulizi za Singano ila unashupaza shingo tu. Ungekuwa haikubali angeacha muda mrefu wala usingekuwa unaonekana kwenye huu uzi unalalama. Karibu tuendelee kule kwa Hamza
Oooooky nduguNILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI: DR SINGANO JR
Mono no aware
SEHEMU YA 732.
Macho ya bluu ya Clark yalichanua baada ya Roma kuuliza swali lake , yalikuwa yakivutia kama vile ni madini na kutamani kuyaangalia muda wote.
“Vizuri , ukweli ni kwamba ni rahisi kuelewa ni kwamba tu wewe mwenyewe hukujaribu kuelewa..”
Akiwa ameng’ata lips zake alitoa tabasamu na kisha palepale akashika mkono wa Roma na kuuweka katika nyonyo lake.
Roma alikuwa akihisi kabisa mlima huo wenye ardhi tifutifu , licha ya kwamba bado alikuwa bikra lakini kifua chake kilikuwa kimetuna mno.
“Nisaidie kufungua basi”Aliongeea kwa sauti ya chini na Roma alimeza mate mengi bila kuelewa anachotaka kufanya mwanamke huyo lakini aliishia katika kumfungua na kufanya maembe dodo kuchomoka kutoka katika kizuizi chake na kuanza kupata hewa safi .
Clark alikuwa mtundu na hakuwa na aibu na aliishia kufurahi kwa namna ambavyo Roma alikuwa akimwangalia kwa uchu.
“Honey , basi chukulia haya manyonyo yangu kama ndio Anga na hii chuchu kama sayari , wewe chukulia ni sayari yoyote iwe dunia au jua , halafu tuseme labda uzito wa sayari umeongezeka..”
Wakati akiendelea kuongea Clark kwa utaratibu sana alimfanya Roma kushika ile chuchu na kuiminya na kufanya nyoyo kutuna upande wa chini .
“Sasa uzito wa sayari ukiongezeka anga linabadilika umbo na kuwa kama hivi na kila maada inakuwa katika udhibiti … labda tu iwepo sayari nyingine ambayo ina uzito mkubwa zaidi na kutengeneza huu mbonyeo na kuzifanya sayari nyingine kuwa katika duara kwa kusukumwa mbali..”
Roma alikuwa makini katika kusikiliza mlelezo hayo na alikuwa amependa namna ambavyo Clark alikuwa akimwelezea kwa njia ya ki ubunifu zaidi , hakuwahi kujua kumbe sayansi ilikuwa tamu namna hio.
Muda huo Clark alikuwa akihisi mkuki wa mwanaume wake ukinyooka kuelekea mbele kama vile unataka kumtoboa suruali yake na pumzi yake ilizidi kuongezeka.
“In Other word … in space , there is exists no force because the presence of mass will alter the shape of the space which eventually produces the ‘force’ we are talking about , but ofcourse this is just the most surfaced knowledge I shares ….”
Ghafla tu Roma alishika kiuno cha Clark na kukivutia kwake na kuanza kumbusu kwenye lips zake.
Busu hilo la papatupapatu lilimpelekea Clark kulala kwenye meza huku Roma akiendelea kubonyeza sayari na anga kwa spidi kubwa.
“Inatosha… nishakuelewa sasa kama nitaendelea kukusikiliza ninaweza kupatwa na ukichaa kwa kuvumilia muda mrefu”
Roma na tamaa zake alimbusu mrembo huyo kwenye shingo na kushuka kuelekea chini , alikuwa akifurahia kila eneo katika mwili wa Clark huku akifurahia manukato mazuri yaliochanganyika na harufu ya mwili wa kizungu pamoja na sanitaiza.
Ijapokuwa harufu hio ilikuwa na maajabu yake lakini bado Roma alionekakan kufurahi.
Ilikuwa hivyo hivyo kwa Clark , alionekana kutoa ushirikiano wa kutosha na kufurahia kile ambacho anafanyiwa na alitaka kuvua koti lake la kimaabara na kulitupia kule lakini Roma alimzuia.
“Usilivue hilo koti unaweza kuvua vya ndani vyote lakini sio hilo koti … ninapenda unavyoonekana ukiwa umevaa hio sare”Aliongea Roma akiwa na tabasamu la kifedhuli kama kawaida yake.
Clark alikuwa kwenye mshangao wa sekunde lakini aligeuza macho yake pembeni lakini kwa wakati mmoja alitii maagizo.
Dakika chache mbele alikuwa uchi kasoro koti tu ambalo lipo mwilini mwake na kuegamizwa kwenye meza na kufanya shepu yake yote kumwagika , alimwangalia Roma na macho yake kama vile ni ya paka na kufanya moyo wa Roma kumiminika.
Kilichofuatia hakikuwa tegemeo lake , utimamu wa mwili wa Clark ulikuwa haumpi nafasi ya kuhisi maumivu kabisa kwani alishitukia tu kifimbo cheza kikimwingia na alichoweza kuhisi ni hamu ya kutaka kuongezewa ujazo.
Roma aliishia kuinama mara baada ya kuhisi mkuki wake kubanwa kila kona na aliishia kutoa tabasamu huku akimwangalia mrembo wake usonni na tabasamu.
“Vipi hupati maumivu?”Aliuliza na kumfanya Clark kuona aibu.
“Honey , jana mama aliniambia kitu yako ni kubwa mnoo na unapenda kumgeuza , nimeamini sasa lakini usinifanyie hivyo maana vitauma”
Kutajwa kwa jina la Catherine katika wakati muhimu kama huo ilimfanya Roma kushangaa na kidogo tu shetani lake kulegea lakini Roma kwa bahati nzuri aliweza kuzizuia hsia zake na kumbusu mdomoni Clark ili asiendelea kuongea.
“Wewe mtoto unafikiri nitaacha ninachokifanya kwa kutaja jina la mama yako , kadri unavyozidi kuleta ukinzani ndio tamaa zinavyozidi kunivaa”
Clark aliishia kucheka bila ya kuongea chochote huku akijisikia vizuri kwa wakati mmoja namna ambavyo Roma anampa vitisho vya uongo.
Bila ya kuonyesha udhaifu wowote kama mwanamke ambaye ni bikra Roma alianza kazi ya kupeleka moto ndani ya maabara hio .
Uwazi wa maabara huo uliojaa baridi ulifunikwa na sauti ya vilio vya kimahaba ambavyo vilidumu mpaka saa saba za usiku.
Baada ya kumaliza Roma alimbeba na kwenda kutua nae katika floor ya juu kabisa ya jengo hilo na kuanza kupulizwa na upepo wa baharini huku wakiangalia nyota.
“Babe kwa uwezo wako huo si utaweza kusafiri kwenda anga za mbali?”
“Siwezi , ijapokuwa naweza kuingia katika anga za juu lakini kadri ninavyozidi kwenda anga za mbali nitakosa mawasiliano ya mbingu na ardhi na nishati itapungua sana ,, itafikia sehemu hakutakuwa na nishati ya mbingu na ardhi kabisa , kingine pia angani hakuna oxygen bila ya uwepo wa elementi hizo muhimu siwezi kumudu hata kwa sekunde na mionzi intaniua”
“Kama nilivyotarajia hakuna nishati ya kutosha , ni kama ‘spaceship’ tu, tatizo hapa ni namna ya kupata rasilimali kutoka huko”
“Babe usiniambie unawaza mambo ya majaribio hata muda kama huu?”
“Oops , I’ m not on purpose it’s just an occupational hazard..”
“Ni sawa tu hata kama umefanya makusudi bado napenda”
“Ndio maneno yenu hayo ya uongo ya kutulegeza sisi wanawake”
“Hapana , naongea kutoka katika uvungu wa moyo wangu”
“Hahaha..najua”
******
Nii katika ulimwengu wa majini katika miliki ya Xia , viashiria vya pambano lililotokea hapo siku kadhaa vilikuwa vikionekana wazi , jengo kubwa la Jade ambalo lilikuwa limesimama siku kadhaa nyuma lilikuwa limeharibika na kutokuwa katika ufahari wake.
Lakini haikuwa imekwisha kwani majini karibia wote bado walikuwa hai.
Katika nyumba ya makazi ya mkuu wa miliki kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea na Anjiu kama mkuu wa miliki ndie ambaye alikuwa akiongoza kikao hicho.
Chini yake kulikuwa na majini watu waliosimama katika mistari mwili na kila mmoja alikuwa aidha na cheo cha kifamilia au alikuwa na kazi ndani ya makao makuu hayo katika nafasi ya juu ya kumuwezesha kuhudhuria kikao.
Kwa namna ambavyo walisimama ni kama vile bado wanaishi katika enzi zile za kale.
Kila mmoja alikuwa amekakamaa mwili huku vichwa vyao walikuwa wameviinamisha chini wakisubiria Anjiu kuongea.
Wakati Jinii Anjiu akiwa katika levo ya maji ya kiroho majini hao walikuwa wakimuogopa mno na hakuna ambaye ashawahi kukataa maagizo yake lakini muda huo alikuwa ni jini ambaye amevuka steji ya radi , hofu yao zidi ya Anjiu ilikuwa kubwa mno.
“Kama nilivyokwisha kusema Roma ni Mhalifu muovu , ameshirikiana na yule msichana mwenye mwili wa Yin nyingi ili kuingia katika miliki yetu na kumuua Laofi , Mtumishi Lao na wazee wetu wawili kwa msaada wa roho ya mnyama inayoishi kwenye Cauldron… hii dharau haikubaliki hivyo nimewaita nyie wote hapa kwa ajili ya kufanya kazi pamoja na kuhakikisha Roma analipia mara mia kwa kile alichofanya”
Sauti ya Anjiu iligonga ngoma za masikio ya kila mhudhuriaji na kufanya kila kiongozi kuonyesha wasiwasi wake na hofu.
“Mkuu , kwasababu Roma ana nguvu nyingi je tutaweza vipi kujilinda kama atakuja kwenye miliki yetu kwa mara nyingine?”Aliuliza mzee mmoja aliekuwa mbele kabisa.
“Kiongozi Ngapu haina haja ya kuwa na wasiwasi ili kuweza kushindana na Roma babu yangu Senji amekuja na wazee wengine wa levo ya maji ya kiroho , pia baba yangu Chaopi amerudi na wazee ambao walikuwa wakilinda miliki , kwasababu nishapita levo ya Radi ninalingana ki uwezo na Roma na nitaendelea kuongeza uwezo wangu kadri siku zinavyosogea kama Roma akija tena ninatumaini tutafanya kazi pamoja na kumuonyesha uhalisia wa nguvu zetu, tuna mamia ya majini ndani ya makao makuu yetu hakuna haja ya sisi kumuogopa binadamu mmoja ambaye amejifunza tamaduni zetu” “Oh kumbe mkuu aliepita amerudi?”
Majini hao walionyesha kufurahia mara baada ya kusikia Chaopi mkuu wa miliki aliepita amekwisha kurudi , ijapokuwa babu yake Anjiu bwana Senji alikuwa na nguvu, jini ambaye aliweza kuiba kiti cha umiliki kwa kutumia uwezo wake tu wa kimapigano alikuwa ni jini Chaopi.
Baada ya Chaopi kuachia ngazi alipotea katika ulimwengu huo wa kijini na alikuwa akifahamika kwa uwezo wake wa kutumia siraha , Master Shagoni anaweza kuwa na uwezo lakini alikuwa cha mtoto sana mbele ya Chaopi.
Sasa jiniasi kama huyo akiamua kurudi kama Anjiu mtoto wake ameivuka radi basi pengine na Chaopi pia alikuwa juu zaidi.
Lakini Anjiu kwa wakati huo hakuongea chochote kuhusu levo ambayo baba yake amefikia katika kuvuna nishati za mbingu na Arrdhi.
Maili kadhaa kutoka makao makuu hayo kulikuwa na ardhi ambayo ilikuwa tambararae ambayo imejazwa na mimea ya aina yake ambayo ilikuwa ikitoa harufu mchanganyiko.
Katikati ya eneo hilo ambalo ni kama bustani kulikuwa na nyumba ndogo tatu au nne hivi ambazo ziliendana na eneo hilo , ilikuwa ni kama Utopia mbali na madhira ya dunia.
Katika wakati huo katika meza ya jiwe la mzunguko Senji alionyesha kucheza mchezo ambao haukufahamika na mzee mwingine ambaye alikuwa na ndevu.
Mara baada ya Anjiu kutua ndani ya eneo hilo kwa nje alisogelea eneo ambalo wazee wake walipo na kuangalia mchezo ambao walikuwa wakicheza lakini kwa namna gemu hilo linavyochezwa ilionyesha mwanaume ambaye hakuwa mzee sana ndio anaelekea kushinda lakini hakutaka kuongea neno lolote.
“Salamu kwenu babu na baba”
Haijalishi alikuwa akiogopesha vipi ndani ya ulimwengu huo wa majini watu lakini bado alikuwa akionyesha heshima mbele ya babu yake na baba yake, hao majini wawili ambao walikuwa mbele yake ndio ambao walikuwa na nguvu kubwa ambao wanastahili heshima yake.
“Vipi wakuu wa familia na koo washaondoka na kurudi makwao?”Aliuliza Senji ambaye alikuwa ameshikilia kete yake ya jiwe kwa namna ya kusita sita kuicheza.
“Ndio na nimeshawapaitia herufi za mawasiliano , kama Roma ataamua kurudi na kuua mmoja wapo
taarifa zitatufikia mara moja ., nishawapatia taarifa pia kurudi kwako baba”Alitingisha kichwa.
“Vipi huyo Binadmau Roma Ramoni bado hajachukua hatua yoyote?”
“Mashushu wetu ambao wameenda ulimwengu wa kawaida wamerudi na taarifa na kusema Roma alirejewa na ufahamu wake kwani aliwasiliana na familia yake , sina uelewa ni kwa namna gani ameweza kruudi katika hali yake ya kawaida lakini inasemekeana yupo nchi ya mbali na mashushu wetu bado wanatafuta kujua nchi hio , pengine pia anapanga kupumzika nadhani na hii inatupatia muda wa sisi kujijega upya”
“Inawezekana pia anataka kuingia katika levo zingine kabla ya kurudi huku , pengine anataka kujua mbinu ya kukitawala chungu vizuri au kuelewa matumizi ya radi ili kuja kutuzima kwa shambulizi moja tu”Aliongea Senji huku akikunja sura kwani mtoto wake alionekana kucheza vizuri.
“Lakini mimi naona tunawaza mbali , kudhibiti radi ya mapigo mengii sio jambo ambalo linawezekana kirahisi , ile siku alikuwa na bahati sana yule mnyama amemsadia , baba na mimi wote tushaipita radi na ni sawa na kusema analingana nae ki uwezo , kama Roma atarudi sidhani kama Chungu chake kitaweza kumsaidia tena”
“Nadhani pia nilishakuambia usijifikitie wa juu sana ki uwezo , adui ambaye ameweza kumuua Bi Sena na Tigola sio wa kawaida , kuingia tu katika levo ya kuipita Radi unajikuta kujiamini hivyo inaweza kukukost.”Aliongea Chaopi na kumfanya Anjiu kunywea.
“Ndio baba nimetambua makosa yangu”
“Wakati ambao unachukua nafasi kama mkuu wa miliki nilikuambia wewe na mimi tageti yetu ni nini , yule mtu hawezi hata kutuangalia kwa nafasi tuliopo na kuhusu kilichotokea juu ya Roma Ramoni ni swala dogo isitoshe hajakuua wakati nikiwa sipo , lakini kwasasa nimerudi na hakuna kingine ambacho naweza kufanya achana na huo mtazamo wako finyu na usijiweke katika kundi la majini wa kawaida ndani ya ulimwengu huu vinginevyo utakuwa mwenyewe siku zote”
“Nitakumbuka maneno yako baba”
“Vizuri , Chaopi inatosha sasa, Anjiu amekuwa akifanya kazi nzuri kuliko hata wewe wakati alipochukua nafasi yako , hakuna kosa katika kupanua miliki yetu isitoshe katika umri wake huo hamkua kwenye levo sawa hivyo ni kama amekuzidi”
“Najua unapaswa kudili na Zianji na wengineo hivyo sitaki kuongea sana , yeye pia ni mtoto wangu na ni mdogo wako maamuzi yapo juu yako , wewe ndio mkuu nina uhakika utakuwa na busara katika kudili na hilo swala”
Anjiu alikaa kimya kwa muda na kisha aliinamisha kichwa chake kama ishara ya heshima na kisha akaaga na kuondoka.
“Mtoto wangu na mjukuu wangu naona mshanizidi sasa”
“Wakati nikiwa mdogo ulikuwa ukiniambia kama mtoto akiwa dhaifu kuliko baba yake basi hapaswi kuzaliwa kabisa”Aliongea Chaopi.
Upande mwingine katika ngome ya makao makuu ya miliki, Anjiu alikuwa amesharudi na kumuiata mdogo wake Zianji na mke wake Leiana.
Zianji mtazamo wake mbele ya kaka yake ulikuwa umebadilika , ile hali ya maringo aliokuwa nayo ilikuwa imepotea na sasa alionekana kukata tamaa kutokana na nafasi ambayo kaka yake yupo.
Dakika ambayo aliingia katika chumba aliishia kuinamisha kichwa chake chini akiogopa hata kumwangalia Anjiu usonni.
Upande wa Leaiana yeye muda wote alikuwa amepamba uso wake kwa tabasamu kama vile hakuna kilichotokea.
Licha ya kwamba Anjiu ndio aliewaita lakini hakuongea neno na alikuwa amekaa tu kwenye kiti chake cha ukuu bila ya kuongea akiwa anawaangalia.
Baada ya kimya cha muda mfupi , Leiana alivunja ukimya.
“Anjiu umetuitia nini?”Aliuliza na kumfanya Anjiu kumwangalia.
“Lahani amejificha nyumbani kwako si ndio?”
“Ndio , amesema atakaa nyumbani kwangu kwa muda , nadhani anamuogopa yule mwizi”
“Haha,,, muoga kama nini , sidhani kama atakuja kufanikisha jambo lolote”Kwa mtazamo wake alijua Lahani alikuwa amejificha kwasababu anaogopa kukosolewa.
Wakati akipambana na Roma alishaona ni mtoto gani ambaye anapaswa kumuandaa kutokana na namna walivyochukulia tatizo lile,.
Ijapokuwa alimwambia Lahani kukimbia lakini mtoto wake wa kike ambaye ni Dhaifu hakukimbia na sio tu kuangalia lakini alijaribu kumuokoa baba yake , kupitia jambo hilo alijua ujasiri ambao upo ndani yake upo kwa uchache katika majini wengi wa kiume.
“Ukiwa na uwezo huwezi kukimbia matatizo”Ndio ambacho aliwaza Anjiu na kuamini.
Baada ya kusimama taratibu kwenye kiti chake ghafla tu Anjiu palepale aligeuza nguvu zake za kijini na kutengeneza kitenesi cha moto kama cha umeme vile katika kiganja chake ambacho kilikuwa kikitoa msisimko wa nguvu za giza.
Ni siraha ambayo ilikuwa imejazwa na nguvu ya kali mno na kubwa ambayo iliwafanya Zianji na Leaiana kurudi nyuma.
“Vipi mnahisi nguvu yake?”
“Taowu!!?”Aliongea Zianji kwa kumaka.
“Ndio , shukrani sikuendee wewe , Laofi na Mohi nimeweza kujipatia nguvu ya ajabu kutoka katika nafsi ya mnyama Taowu , inaweza kuonekana nguvu ya giza lakini imeweza kunipaisha ki uwezo sana na kufanya mbinu yangu ya kimashambulizi ya mshale wa radi uvukao anga kuwa mkubwa sana”
Kauli yake iliwaondolea hali ya tabasamu kabisa katika nyuso za Leaiana na Zianji na kukumbwa na huzuni.
“Kaka inamaana ulijua kila kitu kilichokuwa kikiendelea??”
“Nilijua wewe na Laofi mlikuwa na mahusiano na huyu mwanamke na kisha mkamuingiza na Lao mtumishi , hivi mnadhani lile banda lenu kule bwawani ni sehemu ambayo sifiki … lakini hata hivyo sikuwahi kuwaza mnaweza kupata damu ya mnyama Taowu na kuitumia kwangu , nilionekana mahesabu yangu hayakukaa sawa lakini hata hivyo haijalishi mlikuwa makini vipi mpango wenu umefeli , ninapaswa kuwashukuru kwa kutumia damu hio katika mwili wangu kwani imesaidia sana kupandisha uwezo wangu”
“Kaka .. kaka tafadhari yarehemu maisha yangu”Aliongea Zianji huku akipiga magoti na kutetemeka.
“Relax … sina mpango wa kukufanyia chochote bado una thamani kwa miliki kutokana na uwezo wako isitoshe umelala tu na huyo mwanamke na kufeli kuniwekewa sumu , baba ameniachia haya maamuzi na nimeamua kukuacha hai , lakini utambue hii ni nafasi yako ya mwisho”
“Baba .. amerudi kama ni hivyo kwanini haja…?”
“Kwanini hajakutana na wewe ,kwanini afanye hivyo?”
Maneno yake hayo yalimfanya Zianji kurudi nyuma nyuma kwa kujikongoja.
Ilikuwa ni kweli kutokana na uwezo wake mdogo baba yake hakuwa na haja hata ya kuonana nae kwani hakuwa kitu.
“Asante sana kaka ,,”Aliongea Zianji kwa kujikaza na kisha alisimama na kuondoka kwenye chumba hicho na kumuacha Leiana mke wa Anjiu.
“Kwanini ?... kama ulijua nilikuwa na mahusiano nao kwanini ukaamua kujizuia?”
“Haha.. kujizuia!?.Leiana usifikirie sana , kwanini nifanye hivyo , uhusiano wako na wanaume wengine haunihhusu”
“Mimi sio mkeo ,? Mimi ni mama mtoto wako kumbuka”
“Haha.. kwahio ndio nini sasa , wewe ni mke wangu tu kijina na mtoto wa mtoto wangu bado tu huelewi , nilichotaka kutoka kwako ni kuwa mwanamke wa nyumba yangu lakini haina maana unapaswa kulinda uanamke wako kwa ajili yangu , isitoshe umekuwa ukifanya mahusiano yako ni siri, si ndio?”
Maneno yale yalimuuma sana Leiana , ni zaidi ya Adhabu ambayo angepatiwa kwa usaliti na aliishia kutingisha kichwa akiwa kama haamini.
“Unanidanganya ,, kwanini unanifanyia hivi?”
“Leiana nimekuita hapa ili kukuonya uache mara moja kufanya hila zako zidi yangu , hakuna haja ya miliki yetu kuwa na mke wa mkuu au kuendelea kuwa mama kwa Lahani , isitoshe huna faida yoyote kwangu”
“Haha.. kwahio unasema kwamba unachojali ni madaraka yako na uwezo wako na vitu vingine havina maana kwako?”Anjiu alibakia kimya akionekana kukubaliana na kauli yake.
“Anjiu wewe hakika ni muoga kama Kunguru , hivi unajua ni kwanini nilitaka kukusaliti , kwasababu hujawahi kunijali tokea nilipo kuzalia mtoto , tokea nikiwa mtoto familia yangu iliniambia jina langu litabadilika kwasababu ninakwenda kuolewa na mtu mwenenguvu na kwa moyo mkunjufu nikakubali na
nikajitahidi kwa uwezo wangu kuwa mke mwema lakini nini ulikuwa ukinifanyia , ulijifanyisha tu unanipenda na kunipotezea , hukujaribu hata kuniangalia usoni, wewe ni mwanaume muoga ambaye uliogopa kukataa hisia zangu waziwazi na kuendelea kuwa mnafiki”Aliongea na kumfanya Anjiu kumwangalia kwa macho makali.
“Umemaliza? , kama umemaliza ondoka mbele yangu”
“Sijamaliza , niue hicho ndio ninachojali , tokea siku ambayo nilianza kushirikiana na Laofi na wengine sijawahi kuwaza kuishi , Anjiu mimi nakujua kuliko unavyojijua wewe wenyewe , wewe ni mwanaume ambaye unatia huruma na ambaye hujui ni kipi unapenda na kipi hupendi , ijapokuwa unapambana katika mafunzo ya nishati lakini umeshindwa kupotezea yaliokutokea ulimwengu wa kawaida , tokea siku ambayo umemleta Xiao katika huu ulimwengu nilishajua tayari ulikuwa na mtu umempenda , huyo mwanamke kutoka ulimwengu wa kawaida umempenda na umeshindwa kumpotezea , kwa ninavyokujua usingeruhusu akuzalie mtoto”
“Lakini hebu jiangalie unajitahidi kupotezea hizo hisia ili kuendelea kuwa na nguvu na kujifanyisha hujali lakini ukweli ni kwamba unashindwa kujizuia kumlinda , umemfanya Xiao uwezo wake kuwa wa chini ili asionekane kuwa tishio , hivi huchoki tu , mimi hata kwa kukuangalia hivi ninajichokea , huongei chochote na siku zote ni mtu wa kujifanyisha tu lakini nilishakuona tokea muda mrefu hujali uwepo wangu , Anjiu nakudharau, nakudharu sio kwasababau hunipendi au kuwa bize na kuvuna nishati lakini ni kwasababu upo tayari kupenda binadamu dhaifu kuliko mimi mwanamke ambaye nipo pembeni yako siku zote”
“Kimyaa..!!!”
Anjiu alipandisha hasira na nguvu nyingi za kijini huku akiwa amemkaba Leiana koo na kumfanya asipate hewa na kuishia kukohoa kwa kutema damu.
Mara baada ya kuona huo sio muda wake wa kufariki , aliamua kumauchia na kumsuumia mbali.
“Ondoka , usinifanye nipoteze uvumilivu wangu kwako”
Leaina alijikongoja na kusimama huku akishika shingo yake na kuonyesha tabasamu lililojaa kejeli.
“Naona una hasira , vizuri sana hatimae umeonyesha hisia zako”Aliongea na kumwangalia Anjiu kwa sekunde kadhaa na kisha akageuza na kuondoka lakini kabla hajatoka kabisa aligeuka.
“Hata kama hujawahi kunipenda lakini huwezi kukataa mimi ndio nakujua vizuri , kwasababu dakika ambayo unamfikiria huyo malaya wako mimi nipo nakuangalia usoni”Aliongea na kisha akaondoka na kufanya ukimya kutanda.
Anjiu aliishia kupumua kwa nguvu na dakika ileile alitoa pete ya madini ya Jade kutoka kwenye hifadhi yake na kuanza kuisugua sugua kama vile ina uchafu.
SEHEMU YA 733.
Ilikuwa tayari ni siku kadhaa kufikia siku ya fainali ya mashindano ya UEFA champion League , watu wengi wenye ushawishi na matajiri kutoka pande za dunia walikuwa wakielekea London na wengi ya matajiri waliamua kuegesha boti zao za kifahari ndani ya eneo la Canary Wharf.
Kwasababu ilikuwa ni eneo maarufu ndani ya jiji hilo la London kwa kuwa na biashara nyingi pamoja na mall za kufanyia Shopping wiki hio Mooring fees ilikuwa juu mno na iligharimu zaidi ya paundi elfu kumi kwa kuegesha boti kwa masaa ishirini na nne tu.
Lakini licha ya gharama hio kuwa kubwa haikuwa kikwazo kwa matajiri kwani kwao pesa waliichukulia kama namba tu, ukweli ni kwamba hata kam walikuwa na pesa nyingi eneo hilo halikuwa likitosha.
Mooring fees ni ada ambayo hulipwa kwa kuegesha chombo mfano wa boti katika eneo maalumu ambalo limetengwa karibu na biashara.
Sasa kuweza kuegesha boti yako katika eneo la Canary Wharf ni ishara ya kamili ya utajiri na hadhi.
Dakika hio hio boti moja kuubwa ya kifahari ambayo ilizidi kimo cha boti zote zilizokuwepo mahali hapo ilijongea taratibu na kwenda kusimama eneo la katikati ya Canary Wharf , wanaita sehemu ya Dhahabu ambayo inakupa nafasi ya kupata chochote.
Kitu cha kushangaza zaidi katika mbavu za boti hio kulikuwa kumeegeshwa makombora makubwa ambayo yalikuwa yakiwaka waka kutokana na kupigwa jua.
Kilichowauzi mabilionea wengi ni kwamba mtu huyo mmiliki wa hio boti alikuwa amenunua nafasi mbili zaidi za wazi kana kwamba hataki usimbufu wa kusogelewa na viboti vyao jambo ambalo walichukulia ni kama dharau.
Boti hio kubwa ya kifahari kuliko zote ndani ya eneo hilo ilikuwa ni Erebos , boti ambayo inamilikiwa na mfalme Pluto.
Baada ya kukubali mualiko wa Malkia Catherine
Roma alichukua wanawake wake wote na binti yake Lanlan na kuwapelekea London kwa ajili ya kuangalia onyesho la utumbuizaji wa Sophia kabla ya kuanza kwa fainali , ilikuwa hivyo kwasababu Roma alitumia muda huo kama likizo ya muda mfupi kutokana na kuvuna nishati kwa muda mrefu.
Kama vile iliikuwa ni trip ya kifamilia Roma hakusahau kusafiri na Bi Wema , Sui , Mlezi wa Lanlan Qiang , mama yake na ndugu zake na wengine wengi ambao aliwatumia mualiko na kukubali.
Mama yake Magdalena na Mage, Mama T alikuwa amefika pia , Mama yake Nasra kutoka kijijini Mponde aliweza kufika pia kwa mara ya kwanza katika jiji la raha , Shangazi yake Dorisi na mjomba wake pia walifika , bila kumsahau mke wa Juma pamoja na shangazi yake wote waliweza kusafiri.
Shangazi yake Dorisi na Mama T walikasirika mara baada ya kuona kundi hilo la wanawake wa Roma bila ya kufahamishwa lakini kwasababu watoto hao walikuwa washawaelezea kuwa Roma hakuwa wa kawaida basi hakuna ambaye alimkasirikia na kuishia kumuona sio mtu wa kawaida, hata mara baada ya kusikia kwamba wanao uwezo wa kuishi muda mrefu bila ya kuzeeka walifurahi.
Na Roma ili kuwapamba pamba aliwaahidi kuwapatia vidonge vya kuendelea kuwa vizuri kiafya na kuongeza umri wao wa kuishi.
Hata kama wewe ndio mzazi na watoto wako wote wanampenda mwanaume mmoja na huyo mwanaume mmoja anakuambia anao uwezo wa kukupatia kidonge cha kukuongezea miaka angalau hata kumi
ya kuendelea kuishi unadhani ungekataa , ki ufupi unaweza kwenda mbali na kumwambia’ Mkwe nitazaa mwingine nikupatie’ kwasababu hakuna biandamu ambaye anapenda kufa mapema licha ya kwamba kuna siku ya kifo.
Haikuwa hivyo tu Roma alikuwa tajiri wa kutisha , boti hio ya kifahari ilikuwa ni sababu tosha ya kukufunga mdomo na Roma hakuishia hapo tu hata huko Tanzania kwenyewe walifuatwa na ndege binafsi na kuwasomba wote kuja Uingereza na kuingia katika boti ya kifahari na baada ya hapo kila mmoja akapatiwa kijakazi wa kumsaidia shida zake zote.
Ki ufupi ni kwamba maisha yao ndani ya jiji hilo la London ni kama vile wapo ndotoni katika miliki ya Mfalme Pluto.
Mama T licha ya kuwa na pesa na kumiliki biashara kubwa ndani ya jiji la Dar es salaam hajawahi kuonja ufahari wa namna hio , waliopagawa zaidi ni mama yake Nasra na ndugu wa Najma yaani wifi yake na Shangazi yake..
Hakuna ambaye alikuwa jinga , walijua kwa uwezo wa Roma wa nguvu za kimaajabu wao ni kama sisimizi tu hivyo walijikuta automatiki wakiwa na adabu.
Ndani ya muda mchache tu boti hio ya Erebos ilijaa neema ya watu wengi.
Ijapokuwa London haikuwa na maeneo maarufu ya kufanyia Shopping kama Ginza, Avenue des champes elysee na Fifth Avenue lakini
Knightsbridge and Harrods ilikuwa ni sehemu nzuri kwao kufanya kufuru ya manunuzi.
Hata kwa mwanamke mpole kama Edna , Magdalena na Neema hawawezi kujizuia kuingia katika maduka makubwa ya kifahari ya eneo hilo.
Kuhusu Yezi na Rufi ambao hawakuwa na uelewa mkubwa kuhusu brand maarufu walikuwa na shauku ya kutaka kujua vitu vingi kwa kuuliza maswali.
Wazazi wao walikuwa ni umri tofauti tofuati lakini mwishowe walizoeana kupitia kufanya vitu pamoja.
Mwanzoni Roma alitaka kuwasindikiza kwenda kufanya shopping lakini haraka sana aligundua hawezi kuingilia hivyo aliacha wafanye wenyewe na yeye alikaa eneo la Lounge kusubiria akiwa na Lanlan.
Kwasababu Lanlan alikuwa bado mdogo hakuwa na haja ya kufanya shopping na alichokuwa akipenda sana ni midoli , kuhusu mavazi mashangazi zake na mama yake wangemnunulia tu.
Baba yake pia sio mtu wa mambo mengi isitoshe Roma alikuwa na furaha kuwa na Lanlan pembeni yake ambaye alikuwa mtiifu kuliko hata ya Edna mke wake.
Wanawake uwezo wao wa kununua mavazi na vitu vingine ulikuwa mkubwa mno na siku ya tatu kila mtu alikuwa amejaza hifadhi yake ya pete na wale wasiokuwa na pete walikuwa wamejeza kwenye vyumba vyao.
Siku ya nne kila mmoja hakuwa na hamu ya kununua kitu kingine tena hivyo walihamia kwenye kula vyakula vitamu juu ya boti hio ya kifahari.
Meza zilikuwa zimepangiliwa juu hapo na vijakazi ili kufanya eneo liwe la kutosha kwa kila mmoja.
Sasa jambo la ajabu ni kwamba licha ya kwamba ni mchana tena wa jua kali lakini wazee wote ambao hawakuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi kila mmoja alikuwa amevalia majaketi mazito mno na haikuwa kwao tu hata kwa raia wengi wa jiji la Uingereza.
Roma kwa kuona jambo hilo kuna kitu aliona kabisa hakipo sawa na aligeuza uso wake na kumuangalia Clark.
“Clark hali ya hewa ya kipindi hichi si inakuwaga ni ya kati kwanini inaonekana kama ni kipindi cha baridi hapa Uingereza?”
Kwasababu Clark alikulia London basi alikuwa akijua majira ya nchi hio kwa mwaka mzima.
“Ndio umegundua sasa hivi , joto limeshuka sana dunia nzima katika miezi hii , kawaida joto la London katika mwezi huu linapaswa kuwa kati ya nyuzi kumi na nane mpaka kumi na tisa lakini leo ni kumi na inaonekana linaendelea kushuka”Alijibu.
“Inaonekana hamuangalii taarifa ya habari , tokea wiki iliopita taarifa zinasema kwamba joto la dunia limeporomoka kwa kiwango kikubwa mno kama vile hakuna kabisa’ Global warming’ , hata katika ncha ya Kusini na Kaskazini inaripotiwa ukubwa barafu umeongezeka , wanasayansi duniani wapo katika utafiti ili kujua sababu ni nini”Aliongea Mjomba wake Dorisi ambaye alikuwa akikata kipande cha nyama , alionekana kuwa msomi na tajiri hivyo licha ya Roma na Clark kuongea kingereza alisikia.
Lakini pale pale ndio alipokuja kujua alikuwa akielewa kuongea kingereza na kirusi kwani elimu yake amepatia nchini Urusi na Marekani.
“Kama hata wanasyansi wameshindwa kujua nini tatizo kwanini wewe Clark hufanyii kazi swala hili?”Aliuliza Roma.
“Nishajua kuhusu tukio hili la ajabu hivyo nilishampa kazi Grace kukusanya taarifa kutoka pande zote za dunia , naamini nitaanza utafiti wiki inayokuja”
“Sister Clark you are amaizing , its like you excel in every field”Aliongea Yezi huku akimtolea Clark ulimi kumkejeli lakini kwa wakati mmoja akiwa na hali ya kumkubali.
“Every group has someone who is the best and one who is mediocre , I’m just luck to have a great mind”Aliongea Clark.
Wakati wakiwa wanaongea palepale simu ya Roma ilianza kuita na mara baada ya kuitoa mfukoni aligundua ni namba ngeni kutoka nje ya nchi yaani Tanzania kutokana na mwanzo wa code zake
Roma alikuwa akiijua hio namba na aliishia kumwangalia Mage na Magdalena na mama yao na aliona hawakuwa na uelewa kama ni Afande Tobwe ambaye alikuwa akipiga simu.
SEHEMU YA 734.
Roma alipokea simu na kuweka tabasamu usoni na kisha akaongea kwa sauti bila ya kujiuma uma.
“Hello , nnikusaidie tafadhari”Roma alienda moja kwa moja kama vile hamjui mzee huyo.
“Roma Balozi wa Hongmeng anataka kuonana na wewe”Aliongea Afande Tobwe kijeshi.
“Balozi wa Hongmeng? Nani huyo?”
“Amejitambuliza kwa jina la Xuan Jizi , amesema ni mjumbe wa majini wa Hongmeng katika upande wa dunia”
“Xuan Jizi?”Aliuliza Roma huku akijiambia pengine ni yule ambaye alimhonga vidonge au mwinginekwani hakujua jina lake halisi.
“Amesema sababu ya kutaka kukutana na mimi ni ipi?”
“Hajaongea chochote , hivyo nataka jibu kutoka kwako kama upo tayari kuonana nae au lah”
“Kama ni hivyo mwambie nipo vacation na siwezi kuongea nae chochote na kama anashida sana na mimi mwambie aje London atanikuta lakini sina uhakika kama anaweza kurudi hai maana hili ni eneo ambalo lipo chini ya Apollo na Artemis”
“Nilijua tu utajibu hivyo lakini usijali sana, kwasasa umekuwa na nguvu kubwa mno na unatisha hivyo siwezi kukushauri chochote , nitakupigia kama kuna tatizo”
“Asante sana baba mkwe”Aliongea Roma mara baada ya kucheka kidogo na kisha akakata simu.
“Hubby huyo ni baba yangu uliekuwa ukiongea nae? , kuna tatizo nyumbani au kuna mtu anataka ugomvi na wewe?”
“Ameniuliza ni lini atapata mjukuu ,, mzee ana tabu huyu”Aliongea Roma akiwa siriasi.
“Wewe…!”Mage aliishia kuangalia pembeni baada ya kupewa jibu hilo , tokea aanze kuwa mpnezi wa Roma ule ujeuri wake wote ulikuwa umeisha.
Mama T aliishia kushika nywele za Mage na kutabasamu bila ya kuongea chochote , ukwei ni kwamba licha ya kwamba ameridhia kishingo upande watoto wake wote kujihusisha kimapnzi na mwanaume mmoja lakini bado hakujisikia vizuri na alikuwa mkimya mno.
“Sir nnimesikia hilo jina , ni binadamu ambaye ana mafunzo ya kijini ambaye alijipatia umaarufu kwa miaka kadhaa kutoka Hongmeng , kama ndio ameagizwa kuja kama balozi basi naamini swala hilo sio jepesi”Aliongea Sui.
“Ngoja wafanye wanachotaka , haijalishi ni nini wanataka , kwasasa jambo hilo ni kiporo mpaka Sophia atakapo maliza show yake”
“Halitokuwa tatizo? , kumbuka babu na ndugu zeu wengine bado wapo Tanzania”Aliongea Edna.
“Ndio Roma usivuke mpaka wewe kwasasa ni mtanzania si ajabu wamemtumia Afande Tobwe kuwasiliana na wewe”Aliongea Blandina mama yake.
“Haina haja ya kuwa na wasiwasi kwasababu amekuja kama balozi hawezi kufanya kitu chochote kwani maamuzi hayo hana , wametumia serikali kutaka kuwasiliana na mimi ili waonekane ni kama wazito na muhimu lakini siwezi kuwapa nafasi hio , wakiona siwachukulii siriasi watagundua nguvu yao ni ndogo zidi yangu na hawawezi kuniamrisha amrisha , kama watagusa mtu yoyote ndani ya Tanzania itakuwa ni kukiuka sheria na isitoshe wao ndio wamepewa jukumu la kusimamia sheria hizo”
Wote walikubaliana nae na ukweli waliamini labda Hongmeng wamesikia kile ambacho Roma amekifanya katika ulimwengu huo wa majini maana miliki ya Xia ipo karibu sana na Hongmeng.
Baada ya chakula cha mchana kila mmoja alitawanyika wengine walienda kupumzika wengine walienda kuendelea na mafunzo na wengine kujaribisha kile walichonunua , Mage na Lanlan wao walichukuana na kwenda kuendesha speedboat.
Upande wa Roma alienda kuzamia katika chumba cha Neema Luwazo ambako alikaa muda mfupi sana na kisha akarudi juu kabisa na alimkuta Edna peke yake akiwa ameshikilia kikombe cha chai .
Edna ni kama vile alimtarajia na mara baada ya kumfikia aligeuka na kumwangalia.
“?Hebu kaa kwanza, vipi Neema yupo sawa naona amekuwa mnyonge?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushangaa kidogo.
“Kwanini ghafla tu ukaanza kumjali Neema wewe ninachokumbuka ni kwamba humpendi”
“Hicho ndio unachowaza , mimi kama mwanamke namuona Neema ni mtu mzuri”Aliongea Edna na kisha akageuzia macho yake na kuangalia jiji, sauti yake ilikuwa nyororo na ya chini kana kwamba alikuwa akijiongelesha yeye mwenyewe.
“Edna umebadilika sana hivi karibuni na nashindwa kukuzoea unajua?”
“Unamaanisha nini?”
“Sijawahi kuwaza utakuja kupatana nao vizuri , ijapokuwa nilitamani ije kutokea lakini mabadiliko yako yamekuwa ya haraka sana na nashindwa kujizuia na kuona kuna kitu ambacho hakipo sawa ,unaweza kuniona labda ni mtu mgumu kufurahisha lakini hisia zangu zinaniambia kivingine kabisa”
“Unaogopa?”Aliuliza Edna akiwa na nusu tabasamu kwenye uso wake na swali lile lilimshangaza sana Roma lakini kwa namna moja swali hilo ni kama amejua kile ambacho Roma anajisikia.
“Unaona mambo kwa upeo wa tofauti nje ya matarajio yako na wasiwasi wako ni kesho yetu ambayo haijulikani , unajifanyisha kutokunielewa lakini ninachoona mimi hapa ni wewe ambae hutaki mimi nikuone kama unanishuku na mabadiliko yangu ndio maana unaniongelesha kwa namna hio”Aliongea na kumfanya Roma kulazimisha tabasamu kwani ni kama amekamatika.
“Ukiachana na hayo nadhani ni jambo zuri , kwangu ni sawa tu hata usiniambie sababu ya mabadiliko yako , nilikuwa na wasiwasi kwamba huwezi kuishi nao lakini sasa hivi naona kabisa upo hiari kufanya nao shopping na kucheka wanapokutannia na kula nao , kwangu nashukuru sana kwa hili”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia kwa muda.
“Ukweli ni kwamba sijui siku nzuri kama hizi zitadumu kwa muda gani na ninachotaka ni kuwa na maisha ya utulivu na yasiokuwa na mawazo , vipi kama kila kitu kikibadilika siku moja , si itakuwa ni zaidi ya huzuni kwa kuwa na kumbukumbu pekee za sisi kugombana muda wote?”
“Kwanini unaongea hivyo ghafla tu?”Aliuliza Roma kwa kufosi tabasamu huku kope za macho yake zikitetema lakini Edna hakutoa jibu na aliweka kikombe chini na kusimama.
“Naenda kukaa na mama kwanza , kama utakuwa free nenda kamwangalie Lanlan na Mage , sitaki wasababishe matatizo kama jana baada ya kuvamia boti ya mtu mwingine na wenyewe kuwaona kama wezi”
“Sawa nimekuelewa nitaenda mpenzi”Aliongea Roma mara baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha huku akijitahidi kujituliza na kujiambia Edna yupo sawa na hakuna anamchomficha.
Unafikiri nini kinafanya joto la dunia
kushuka??Roma atarudi ujinini je akirudi atafanikiwa Aluta Continuara.
Tukutane jumanne kwa wale ambao siwadai.
Hatimae siku ya kesho yake iliwadia, siku ambayo ndio maalumu kwa fainali ya UEFA na Roma aliweza kuichukua familia yake katika eneo la watu mashuhuri(VIP) ndani ya uwanja wa Wembley.
Ijapokuwa walkuwa hapo kumwangalia Sophia atakavyo perfom tofauti na mecho lakini mazingira hayo ya shamra shamra yalikuwa mazuri kwao pia.
Malkia Catherine ambaye alikuwa mwenyeji wao aliwakariibisha , ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na Blandina mama yake Roma na walianza kuongea kwa pamoja kama vile wlaikuwa wakilingana umri.
Blandina na yeye alichukua fursa hio kumwelezea
Catheirne kile anachokifanya na ilimfurahisha
Catherine na kumwambia aatoa mchango wake katika taasisi yake ya vituo jumuishi vya kuelela Yatim.
Kitendo cha kukutana na mtu mzito kama huyo ilimfanya kujisikiavizuri kwa kuwa na mtoto kama Roma.
Kabla ya mecho kuanza Show ya Sophia na wasanii wengine ilipaswa kuanza na Sophia alikuwa ni msanii wa pili kutumbuiza na aliweza kuonekana akiwa amevalia viatu vya kimichezo.
Kutokana na muonekano wake wa umaridadi na urembo ilimfanya kuonekana vizuri mno katika runinga.
Sophia hakuwa tena yule msichana wa kawaida, wakati huo alikuwa ni Superstar ambaye ameshafanya kolabo na msanii mkubwa duniani kama Christen na wengine wengi na kazi zake zikafanya vizuri kimataifa.
Aliimba wimbo ambao ulikuwa na mchanganyiko wa lugha mbili kati ya kiswahili na kingereza na kutokana na kuwa na Vocal nzuri sauti yake iliteka hisia za watu wengi,
Baada ya Sophia kuondoka aliingia msannii mwingine mkubwa tu kutoka Marekani na alitumbuiza na kisha akaondoka na baada ya taratibu zingine kuisha hatimae mpira ulianza.
Baada ya kumaliza Show yake Sophia alikimbilia kwenda chumba cha VIP kwa ajili ya kukutana na ndugu zake , hata mama yake mzazi pia alikuwepo.
“Superstar wetu anazidi kuwa maarufu kadri siku zinavyosonga , naamini atakuwa ana mwingizia mapesa ya kutosha bosi wake Edna ?”Aliongea Mage kwa kutania.
“Ninachoingiza kwenye kampuni yake ni kidogo kulinganisha na anachokipata kwenye biashara zake zingine”Aliongea Sophia.
“Impressive perfomance “Aliongea Edna akimsifia na Sophia alijisikia vizuri kwa kauli hio , alijua kutokana na kilichotokea kati yake na Edna basi asingeongea nae hata kidogo lakini alifurahi kwamba hana kinyongo.
Baada ya kila mtu kuketi hatimae kila mtu alikaa kimya na kuendelea kuangalia mechi,
Mechi ilikuwa ni timu moja maarufu kutoka Hispania na ilikuwa ikishindana na timu kutoka moja Ufaransa hivyo shangwe ziliuwa juu sana kwa upande wa timu zote mbili.
Asilimi ya wote walikuwa hawana timu na hawakuwa bize sana na mpira kasoro ya Lanlan ambaye alikuwa amekodoa macho.
“Kwanini hawashindi ,mbona ni dhaifu vile na mpira
hauendi mbal, Mommy kwanini wanakimbia taratibu taratibu vile?”
Lanlan alikuwa kaiuliza maswali kama mashine huku Edna akijitahidi kujibu yote , ilionekana hakuelewa sheria za mpira zilivyo.
Baada ya kipindi cha kwanza kuisha wote wakiwa katika eneo la VIP kundi la watu ambao wamevalia mavazi ya suti walifika katika eneo hilo huku wengi wakiwa nnii weusi.
Walinzi waliofoka hapo hawakuoneysha kuzuia mwanaume mmoja ambaye ni mzungu alieongozana na wanaume wawili ambao wote walikuwa weusi.
Mshangao uliwashika warembo hao mara baada ya kugundua mtu ambae amefika katika eneo hilo , alikuwa ni Raisi Jeremy.
Edna alimwangalia Roma akimpa ishara kwamba hajui kama mtu huyo atafika Uingereza.
“Callum Boris I’ m sure you could have gotten a private room of your own to watch the match”Aliongea Catherine
“My apologies your Majesty”Aliongea m mwanaume huyo ambaye alikuwa ametanguliwa alikuwa ni waziri mkuu waUingereza afahamike kwa jina la Boris.
“Ni kwasababu rafiki yetu kutoka Rwanda mheshimiwa Jeremy amefika hapa akiwa na nia ya kuonana na kila moja lakini mathalani zaidi anataka kuonana na Mr Roma Ramoni”Aliongea , alikuwa akijua ubini halisi wa upluto wa Roma.
ITAENDELEA.
WATSAPP ONLY 0687151346
Pomoja sana mkuu it was nice to have you here tuhamie Kwa.Hamza sasaMkuu singanojr hakika kazi yako ni njema sana. Nimeburudika na nimejifunza vitu vingi sana ila nilipatwa na huzuni sana na nilikuwa naogopa kuendelea kusoma baada ya Roma kuanza kufa sikutaka kabisa afe mwamba!
Thank you very much and wishing you all the best.
Naona kama imeisha mapema hadi nawiwa kurudiaa aiseePomoja sana mkuu it was nice to have you here tuhamie Kwa.Hamza sasa
Naam tuko pamoja sisi wengine niwadau wako hata simulizi imalize miaka 3 tumoPomoja sana mkuu it was nice to have you here tuhamie Kwa.Hamza sasa
Hili hata mimi nililiona,Riwaya ya ujasusi unajaza mavisa ya kufikirika mara Majini,mara mashtani[emoji3]
Hii ni contemporary fantansy novel ambapo ndani yake kuna Subgenre za espionage , labda nielekeze tu ujasusi sio lazima uhusishe mambo ya kisiasa hapo sasa kwenye Majini na miungu weka Fantansy maana sio proven facts.Hili hata mimi nililiona,
Hii riwaya haikupaswa kabisa kuitwa ya Ujasusi hata kidogo. Yaani sio riwaya mbaya ila haina ujasusi wowote ule.
Ingeitwa SIMULIZI YA KIJINI, NIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA