singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,974
- 10,361
- Thread starter
- #3,941
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI: SINGANOJR
Vanity of vanities , all is vanity
SEHEMU YA 793.
“Zeus..!1”
Roma moyo ulimsinyaa , alijiuliza inamaana wimbi la sauti ambalo ni kama lilikuwa likitaka kuharibu anga lilitoka kwa Zeus?, ni palepale alipata kujua lazima sauti aliokuwa akiisikia kwenye akili yake ilipitia kwenye uungu wa Hades
Wakati huo mara baada ya kusikika kwa sauti, radi ya rangi ya dhahabu na bluu yenye urefu wa zaidi ya futi kumi ilipasua anga kama ilivyokokotwa kutoka kwenye kitu kisichoweza kuonekana na kwenda moja kwa moja kupasua radi na mawingu ambayo yalikuwa chini ya udhibiti wa Roma.
Mkono imara ulijitokea kutoka mawinguni na kunyakua shoti ya radi bila kujeruhi ule mkono kwa namna yoyote licha ya kwamba radi ile ilionekana kuushambulia ule mkono.
Ndani ya sekunde tu lile wingu lote lilitawanyika na hatimae mwili wa miraba minne ulionekana juu angani.
Alikuwa na ndevu ndefu nyeupe ambazo zilikuwa zikipeperushwa na upepo huku mashavu yake yakiwa na kingo kama za mawe pamoja na kona zake.
Macho yake yote mawili ni kama yametawaliwa na umeme na kufanya yatoe mng’ao wa ajabu ambao mweupe sio mweupe ni kama rangi ya majivu.
Mwili wake ulikuwa umesitiriwa na joho la rangi nyeupe lenye mikono mifupi ilioacha wazi mikono yake , huku misuli yake iliotuna ikionekana waziwazi na ilikuwa ni kama vile mwili wake wote umejaa kutu.
Roma aliishia kutoa macho yake tu asiweze kuamini , aliekuwa juu yake ni kama hakuwa amebadilika kabisa , kama alivyokuwa miaka elfu mbili iliopita.
Imewezekana vipi?
Miungu wote ambao walikuwa wamepoteza miili yao mara baada ya kuja duniani na kuvaa miiili ya binadamu, alishangaa mara baada ya kumuona Zeus akiwa na mwili wake wa awali.
Mara baada ya miungu kushuka hawakukaa hata siku moja wote waliamua kuivamia miili ya binadamu na kutelekeza ya kwao lakini kwa wale ambao walikuwa na uwezo wa juu ikiwemo miungu kumi na mbili waliweza kuishi nayo kwa muda mfupi kidogo kabla ya kuhamia katika miili ya binadamu.
Inasemekana Zeus ndio ambae alidumu katika mwili wake kwa muda mrefu na aliingia na mwili wake katika gereza la Roho.
Ndio maana muda huo Roma anashangaa ameweza vipi kutohamia katika mwili mwingine na kuishi na mwili wake licha ya kwamba katika mazingira ya dunia haiwezekani.
Alijiuliza je kulikuwa na sababu ya kipekee ndani ya gereza la Roho ambayo ilimfanya kuishi na mwili wake tofauti na mazingira ya dunia, maana kwa anavyoonekana ni kama haikuwa swali bali jibu.
“Kuwa na uungu wa Hades halafu kuwa adui wa miungu hustahili kabisa uungu wake na haustahili kabisa kuwa sehemu ya miungu , leo nitakuuwa na radi hii iliopo kwenye mikono yangu”Aliongea Zeus akimwangalia Roma kwa macho makali..
Na mara baada ya kauli hio aliinua mkono wake mkubwa juu na bila ya kuchezesha chezesha aliachia radi yote kutoka kwenye mikono yake kumshambulia Roma.
Mara baada ya miungu kuona tukio hilo wengine walikuwa katika hali ya heshima kwa Zeus na wengine walikuwa na furaha.
Ilionekana walikuwa wakijua fika kama Zeus ataamua kuingilia kati, Roma hana nafasi ya kushinda tena.
Roma spidi yake ilikuwa kubwa mno , hata kama ni radi ya Zeus haikuwa rahisi kutokuiona kwa macho yake na kabla radi ile haijamtoka Zeus alikuwa tayari ashajiandaa kukwepa.
Lakini sasa mara baada ya Roma kusogea upande mwingine kwenye hewa akijua kabisa amefanikiwa kukwepa shambulizi lile alipigwa na boriti tatu nyingine za radi na kusababisha mlipuko mkubwa wa shoti.
BOOM!
Roma alishindwa kuamini na hakujua ni nini kinaendelea , ilikuwa ni ile radi imetoka alipokuwa amesimama na kumfuata alipokuwa amehamia na kuvunja ukuta wake na kisha kumshambulia.
Ilikuwa ni kama vile radi ile ilikuwa na ufahamu kwamba atasogea hivyo ilibadilisha uelekeo bila ya taarifa.
Mwili wake wote ulionekana kuungua kwa kiwango cha juu cha joto, huku viungo vya ndani vikionyesha kuumia pia na kujinyonga nyonga, alishindwa kuzuia sauti zaidi ya kupiga yowe.
Maumivu hayo yalikuwa makubwa mno kuliko yale yaliosababishwa na siraha ya Athena wakati wa kumshambulia.
“Arghh..!!”
Roma macho yake ni kama yanapasuka na ni kama anajua sasa nama maumivu halisi ya radi yanavyokuwa
Mwili wake ni kama unaelekea kupalalaizi huku maumivu ni kama yameungana na mwili wake na kumfanya akitamani kifo kuliko kuendelea kuishi.
Uwezo wa Zeus ni sawa na kusema ulikuwa wajuu kiasi kuliko ule wa Athena , jambo ambalo lilimaanisha shoti ya radi yake ilikuwa na nguvu mara mbili na ya jini au mtu aliepitia mapigo elfu kumi ya radi.
Sasa Roma uwezo wake ulikuwa katika mapigo mengi ya radi na pengine ni sawa na kusema ni bahati kwake hajafa mara baada ya kupigwa na radi hio , ilimuwia vigumu kupona haraka kuliko mwanzo.
“Athena kwanini unasita sita, radi yangu itamfanya kuwa dhaifu , tumia mkuki wako kumchoma eneo la moyo na kisha tukiondoe kichwa chake”Aliongea Zeus.
Alikuwa akimwangalia Roma kwa madharau kutokana na kushindwa kwake kusogea huku akiongea na Athena.
“Huna haja ya kunifundisha cha kufanya”Aliongea Athena na palepale aliishikilia vyema siraha yake.
Roma alijikuta akipatwa na kiwewe mara baada ya kuona Zeus na Athena wanataka kumchangia kumshambulia .
“Sikutugemea kuishi lakini siwezi kufa bila ya kupambana”Aliwaza Roma.
“Ni mapema sasa kuniua”
Roma aliongea kwa nguvu akionyesha tabasam lake la ukichaa wakati akiwa anavumilia maumivu ya pigo la mwanzo.
Alikusanya mawingu kwa kasi ya ajabu ili kuanza kutengeneza radi na wakati huo huo alitoa Shoka lake na kumshambulia nalo Zeus.
Lakini sasa kumsogelea Zeus kwa ajili ya kumshambulia halikuwa swala jepesi hata kidogo kwani Athena ni kama alikuwa ashamtabiria ni njia gani Roma atapita na alitumia ngao yake ya Aegis kumzuia.
Bang!!!
Sauti kubwa ya kishindo ilisikika, radi pamoja na shoka lile viligongana na Ngao ya Aegis na ni ndani ya sekunde hio hio Athena alitoa ile ngao na kilichomkuta Roma ni pigo lingine la radi kutoka kwa Zeus.
BOOM!!
Shambulizi lingine la radi ya dhahabu lilimpata Roma na kufanya harufu ya kuungua kwa mwili kusambaa na Roma alijikuta akipiga yowe la maumivu huku akidondoka kutoka angani kama kimondo.
Radi ya Zeus kama ilivyosimuliwa na wagiriki inaweza kumshambulia adui na pasionekane mahali pa kujificha.
Radi hio ilikuwa na uwezo wa kumfuata adui eneo lolote hata kama ajaribu kukwepa vipi, hivyo ni sawa na kusema siku zote lazima ifikie shabaha, sasa ukijumlisha na uwezo wa Athena katika kutabili ilikuwa hatari kabisa kwa Roma.
Pengine dakika chache zilizopita alikuwa na uwezo wa kushambulia Mti Mama lakini muda huo ni kwamba hata uwezo wa kujilinda alikuwa hana na hata kama aamue kupokea mapigo ya Zeus kama alivyoamua kupokea ya Athena basi anaweza kuuliwa mara moja.
Haikushangaza kabisa kwani ki uwezo anaanza Zeus na kisha anaingia Athena lakini mara nyingi watu wanasema Zeus na Athena wapo levo sawa ila kinachomfanya Zeus kuwa juu zaidi ni kwamba Athena anao uwezo mkubwa wa kujilinda huku Zeus akiwa na uwezo mkubwa wa kufanya mashambulizi.
Kwa mfano kama ikatokea Zeus na Athena wakapambana inaweza asitokee mshindi kutokana na utofauti wao, Athena hatoweza kumshambbulia Zeus kutokana na kwamba hana mashambulizi imara na wakati huo huo Zeus kama atamshambulia Athena mashambulizi yake hayatopita kutokana na Athena kumiliki Aegis , ngao yenye uwezo mkubwa sana wa kukinga mashambulizi mengi.
Mpaka kufikia hatua hio ni kwmaba Roma hakuwa na uwezo wa kushambulia tena , kwani akishambulia Athena tayari ashatabilia mashambulizi yake na kuyakinga na ngao yake wakati huo huo Zeus radi yake ni kama ina ufahamu wakati wa kumshambuilia.
“Nadhani huu ni mwisho ambao hujautarajia?”Aliuliza Athena na sauti ya kikauzu huku akiwa na hali ya kihisia isiokuwa ikielezeka.
Roma ambae alikuwa akidondoka kutoka juu angani alijitahidi kutingisha kichwa chake kwa taabu.
Athena alikuwa na uwezo wa kumuongelesha Roma kutokana na kwamba alikuwa akishuka na Roma sambamba, tofauti ni kwamba Roma alishindwa kujizuia kudondoka wakati Athena ni kama anamfatilia Roma kwa karibu.
Sasa wakati alipomaliza kuuliza kwa kauli hio aliinua mkuki wake akinuia kumchoma nao Roma eneo la moyo.
“Sio kirahisi hivi , siwezi kufa kirahisi”Roma aliongea kwa sauti iliojaa maumivu.
“Kweli..?”
Muonekano wa Athena ulikuwa katika utulivu sana , yaani ni kama vile hana uadui na Roma lakini mikono yake ilikuwa tofauti.
“Pfff..!”
Mkuki wa Pallas uliokuwa ukitoa mng’ao wa rangi ya bluu ulikuwa tayari ushamchoma Roma eneo la kifuani kuingia kwenye moyo wake lakini hata hivyo haukuweza kupita kama ambavyo kila mmoja alitarajia .
Kabla Athena hajafanikiwa kumchoma kifuani , Roma alikuwa ashafanikiwa kuushikilia ule mkuki kwa nguvu usipite japo ya kwamba ulimchoma nchi kadhaa kuingia ndani lakini hakujali.
Damu ya moto ilimtoka Roma mkononi na kwenye kifua chake na kusambaa.
“Hatimae nimekukamata … Mkuki wako hatimae nimeushikilia na usione unaweza kuuchukua kutoka kwangu kirahisi”Aliongea Roma huku macho yake ni kama vile yanataka kumtoka pengine ni kutokana na maumivu.
“Kwel?”Athena aliuliza kana kwamba Roma alikuwa akiongea vitu visivyo na maana.
Sekunde iliofuata Athena alimbutua Roma na mguu wake kwa nguvu zote.
“Bang!!
Muda ambao Roma aliweza kusikia sauti ya kishindo alikuwa ni kama vile amegeuka kuwa satilaiti akiizunguka dunia huku yeye mwenyewe akijizungusha katika mhimili wake , kichwa chake kilipindishwa kwa angle mia na sitini na kwenda kuvaa mlima wa barafu.
Miungu wote waliweza kuona namna Roma alivyoenda kuvamia mlima wa barafu na kudidimia ndani asionekane kwa nje.
Athena alirudisha siraha yake iliokuwa imechafuliwa na damu na kuishia kuangalia sehemu ambayo Roma ametumbukia
“You… you can’t win against us”Athena alionekana kumung’unya maneno kwa lugha ya kingereza akimaanisha Roma hawezi kushinda zidi yao.
Zeus alieshikilia kitenesi cha shoti ya radi hatimae aliweza kufika juu ya barafu na alijikuta akikunja sura yake.
“Uungu wake unapotea kwa haraka sana!”Aliongea.
Miungu wengine na wao pia walifika kwenye barafu na waliweza kugundua pia uungu wa Hades unaisha kwa spidi kubwa mno
Ilikuwa ni kama kibatari ambacho kishaishiwa na mafuta na muda wowote kinakwenda kuzima na hio ndio namna uungu wa Hades ulivyokuwa ukipotea na palepale Christen machozi yalimjaa.
“Hades..!.ni kweli umeamua kumuua?”Aliongea Christen akimlaumu Athena akidhania amemuua Roma.
“Hapana, Aphrodite hebu tumia hisia zako kwa umakini, ijapokuwa uungu wake unapotea lakini mkandamizo wa nishati za mbingu na ardhi…”
“Uwezo wake unaongezeka … huyu mwanaharamu anatumia nafsi ya mnyama kuunyonya uungu wa Hades na kuubadilisha kuwa nishati za mbingu na ardhi”Aliongea Hera kwa kupaniki.
“Nini?!”Wengine wote sasa ni kama wanajua kinachotokea na kupiga kelele huku Zeus akiishia kumwangalia Athena.
“Hio ni mbinu yake nyingine?”Aliuliza Zeus lakini Athena hakukubali wala kukataa na wahenga wanasema kimya ni jibu hivyo moja kwa moja ilieleweka bila ya neno.
Dakika hio mlima wa barafu ambao ulikuwa katika hali ya utulivu ulianza kutingishika kwa nguvu kama vile unataka kuporomoka na ikafuatia wimbi ambalo lilikuwa likitoka chini yake.
Ni kitendo cha sekunde tu mlima wote wa barafu ulipasuka na kurusha mapande ya barafu juu angani kwa mita kadhaa na palepale Roma aliweza kuonekana tena ikiwa ni kama vile hakuwa ameumizwa eneo lolote.
Lakini muda huo miungu hao hawakuweza kabisa kumjua Roma kama mwenzao tena kwani uungu wa Hades ulikuwa ushamtoka kabisa.
Mtu ambae alikuwa mbele yao hakuwa tena Hades bali alikuwa ni binadamu mkamilifu mwenye mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba Roma sio Hades tena kwani jina hilo lilitokana na nusu ya uungu wa Hades, hivyo ni sawa na kusema Roma amerudi kuwa Denisi binadamu kamili aliezaliwa duniani.
Uungu ndio mzizi wa miungu au unaweza kusema ndio asili yao ambao hubeba uwezo wao wa hali ya juu sana na kuwafanya kuwa na nguvu kubwa ya kiroho mpaka kuwawezesha kuhama kutoka katika mwili mmoja kwenda katika mwili mwingine.
Chaos ni mnyama wa machafuko ambae anao uwezo wa kumeza kila kila kitu ndani ya ulimwengu, hivyo hata kwa uungu ni kitu ambacho kinaweza kumezwa na Chaos kutokana na kwamba uungu hubeba nguvu ya kiroho ambayo chanzo chake sio ardhi bali ni ulimwengu(Universe).
Roma aliamua kufikiria nje ya boksi na akaamua kuitumia nafsi ya Chaos kuumeza uungu wa Hades ambao alikuwa akimiliki kwa ajili ya kupandisha uwezo wake kwa levo ya juu zaidi ndani ya muda mfupi.
Mara baada ya kufufuka kwa moyo wa Gaia uungu wa Hades na wenyewe ni kama ulikuwa unapona na kufikia uwezo ambao ni sawa na mapigo elfu moja ya radi.
Yaani kwa lugha rahisi ni kwamba Roma alikuwa na uwezo wa kutumia kanuni za anga na kama utamfananisha na mtu anaevuna nnishati za mbingu na ardhi basi ni katika levo ya mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi uwezo ambao ni wajuu sana.
Sasa unapaswa kuelewa mara baada ya Chaos kumeza uungu wa Hades aliugeuza kuwa nishati ya mbingu na ardhi ambayo moja kwa moja ilienda kwa Roma.
Sasa katika mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi Roma alikuwa levo ya mapigo mengi ya radi huku upande wa kanuni za anga ni hivyo hivyo , kwa lugha nyepesi ni kama Roma ameunganisha uwezo wake wote kuwa kitu kimoja yaani alichanganya uungu wa Hades na nishati ya mbingu na ardhi.
Zamani ilimpasa Roma kutumia kanuni za anga peke yake na vilevile nishati za mbingu na ardhi peke yake , lakini muda huo vyote vilikuwa pamoja mara baada ya kufanikiwa kuubadilisha uungu kuwa nishati ya mbingu na ardhi.
Ukweli ni kwamba hio ndio mbingu ya kipekee ambayo Roma alifanya na miungu hawakutarajia kabisa.
Maana kitendo cha kufanya hivyo ni kama Roma kaamua kuachana na amswala ya kanuni za anga kwa ajili tu ya kuongeza uwezo wake.
Bila hata ya maelezo kutoka kwa Athena miungu hao walijua ni namna gani uwezo wa Roma umeongezeka na kuwa wa kutisha.
“Mkandamizo wa nguvu zake ni mkubwa mno , nashindwa hata kuangalia ni levo gani kafikia, ukijumlisha na uwezo wake wa mwanzo naogopa kusema kwasasa kafikia levo ya mapigo elfu kumi ya radi”Aliongea Hera akiwa na wasiwasi .
Roma sasa ni kama amekidhi vigezo vya kupambana na Zeus na Athena kikamilifu..
******
Sharif , Aoiline na wengine wote walikuwa wakiangalia kilichokuwa kikitokea katika ncha ya kaskazini kwa kutumia kioo cha maajabu.
Clark mwanzoni alijua Roma ameshindwa vita na kumfanya aanze kulia lakini mara baada ya kumuona mpenzi wake akisimama tena akiwa na uwezo uliongezeka haraka hakuweza kujizuia na kushangilia kwa furaha.
“Hehe .. huyu mtoto hatimae amegundua kwanini Hades alimwachia nusu ya uungu wake bila fahamu , alipaswa kujua siri hii mapema kama angeacha kujali sana maswala ya wanawake…”Aliongea Sharif.
Moja ya sababu kubwa ya Athena kumuomba Hades kutii takwa lake na kumwachia Roma uungu ni kwasababu tu alitaka kuweza kumtabiria kirahisi hata kama apande levo za juu sana , ilikuwa rahisi kumtabiria Roma kupitia uungu kuliko akiwa binadamu kamili.
Yaani kwa lugha nyepesi uungu wa Hades katika mwili wa Roma ilikuwa ni njia ya mawasiliano ya kinabii kati ya Roma na Athena.
Kulingana na maelezo ya Sharif kitendo cha Roma kufikia levo ya mapigo elfu moja ya radi ilimaanisha Athena hana uwezo tena wa kumtabiria lakini ajabu ni kwamba Athena bado alikuwa na uwezo wa kumtambiria Roma hio yote ni kutokana na uungu wa Hades ambayo ni njia ya mawasiliano.
Sababu ya pili Athena kutaka Roma aachiwe uungu ni kwa ajili ya kumfanya kuwa sehemu yao.
Ikumbukwe mara baada ya Athena kufika duniani aliweza kuangalia nini kitakuja kutokea mbeleni na kupitia unabii wake aliweza kugundua ni binadamu Roma Ramoni atakaeweza kuzuia mipango yake ya kufufua ndugu zake.
Sasa kwanzia miaka elfu ishirini iliopita Athena alikuwa akipambana na unabii kwa kubadilisha historia.
Kitendo cha kutaka Hades kumpatia Roma uungu ukiachana na dhamira ya kutaka kumtabiria kwa urahisi lakini vilevile alitaka kumfanya mmoja kati yao.
Lakini kitu ambacho Athena hakukifahamu ni kwamba Hades alikubaliana nae kirahisi akiwa na ajenda nyingine kabisa, kwa Athena Roma alipewa uungu kwa ajili ya kurahisisha mipango yake kwa Hades wa Zamani alimwachia Roma uungu wake kwa ajili ya kukwamisha mipango ya Athena.
Hivyo Roma kutumia uungu kupandisha uwezo wake ndio kete ya mwisho ambayo Hades wa Zamani alitarajia Roma kuicheza ili kuja kumshinda Athena na wenzake lakini hata hivyo hakumwambia Roma juu ya siri hio, ni kama alimpa mtihani wa kugundua yeye mwenyewe.
Hayo yote Sharif aliyajua tokea mwanzo wa mpango LADO unaanzishwa na yeye pia hakutaka kumpatia Roma siri hio kama anao uwezo wa kupandisha mara mbili uwezo wake kupitia uungu wa Hades.
Sasa Roma alishindwa kugundua siri hio mapema kutokana na Christen mpenzi wake Hades wa zamani kuwa rafiki yake, pengine kama asingekuwa na mfungamano wa kirahifi na Christen angeweza kugundua siri hio mapema sana.
Sasa Sharif alikuwa kwenye mshangao mara baada ya kuona Roma anazidi kushambuliwa na Athena na Zeus bila ya kutumia uwezo wake wote, yaani uungu wa Hades, alijiuliza au bado hajajua siri hio.
Sharif hakuwa mjinga kumtaka Roma apambane licha ya kwamba kimahesabu levo aliokuwa amefikia kulinganisha na wapinzani wake ni ndogo lakini ukweli ni kwamba hakuwa akibahatisha , alikuwa akijua tokea mwanzo njia pekee ya Roma kushinda ni kutumia Chungu chake kuubadilisha uungu kuwa nishati za mbingu na ardhi na kupandisha uwezo wake kwa haraka.
Aoiline macho yake yalicheza na haikujulikana anafikiria nini na aliishia kuangalia kioo bila ya kuongea neno.
Xumei na Mzee Yasu walikuwa na furaha , ijapokuwa walikuwa wakiyaheshimu maamuzi ya mwalimu wao kwa kuwapa binadamu na miungu nafasi sawa , wao walikuwa bado ni binadamu na walitamani kuona Roma anawaua miungu wote na dunia kubakia salama.
Sharif alikuwa ni kama Hades wa zamani tu wote walikuwa Neutral , Sharif hakutaka kuwazuia miungu kutokuitawala dunia kama uwezo huo wanao lakini pia hakutaka kujisumbua kama binadamuw atashindwa kulinda dunia yao.
Kama miungu wangeshinda na Mkuu wa Enzi kutokuingilia basi moja kwa moja Dunia ingekuwa chini ya miungu , kama binadamu wangeshinda kwa kuilinda sayari yao basi pengine ndio mapenzi ya Mkuu wa enzi, na moja kwa moja uangalizi angemkabidhi Roma
Hakukuwa na haja ya kati y a miungu kuwa na muangalizi kwani alijua fika wanao uwezo wa kuilinda sayari lakini kwa binadamu wote waliwakilishwa na Roma hivyo kama Roma angeshinda ilimaanisha ndio yeye kati ya binadamu wote mwenye uwezo wa kuilinda dunia.
*****
Muda huo namna ambavyo miungu walimwangalia Roma haikuwa ikielezeka kama walikuwa wakihisi kitu cha namna gani kwenye mioyo yao.
Mara baada ya kupoteza uungu, Roma alikuwa sasa amekuwa adui yao kikamilifu , hata kwa Apollo na Poseidon ambao walikuwa na urafiki na Roma hawakuwa na huruma nae tena.
Walikuwa wakimchukulia kama mwenzao kwasababu ya uungu wake na sio kwasababu alikuwa binadamu.
Lakini kubwa zaidi kwa wakati huo ni kwamba Roma alikuwa tishio kubwa kwa ajili ya ufufuo wao.
“Inavutia sana kwa ulichofanya , ni kheri kuua binadamu aliekamilika kuliko kumuua kaka yangu Hades”Aliongea Zeus huku akitoa kicheko kizito.
Upande wa Roma ni kama vile hakuwa akimsikia Zeus anachoongea na alikuwa amefumba macho yake huku akichanua mikono yake kama vile anaomba baraka kutoka juu mawinguni.
Ni dakika hio hio waliweza kuhisi kitu cha ajabu , kutoka kila pande nguvu kubwa ya kiroho ilikuwa ikijikusanya kumsogelea Roma.
Roma alikuwa ni kama sumaku na kuanza kuvuta kila aina ya nguvu ya kiroho iliokuwa karibu yake
Nguvu hio ya kiroho ilimwingia Roma na kubadilika kuwa nishati ya mbingu na ardhi na kuzidi kufanya sehemu ambayyo Roma amesimama kuwa na upepo mkali unaomzunguka kama kimbunga.
Kitendo cha upepo mkali kumzunguka Roma ilifanya kuwa ni kama Dhoruba ya kimbunga kikali na kufanya hewa kusukumwa kwenda juu angani kwa spidi kubwa , hatimae sehemu ambayo Roma alikuwa amesimama hakukuwa na hewa ya aina yoyote ni sawa na kusema Roma alikuwa ndani ya Ombwe(vacuum)
“Hii ni hatua ya mwisho ya mapigo ya radi , levo elfu tisa mia tisa tisini na tisa ya radi, levo ya mwisho wa Dhiki na mwanzo mwa ufunuo mkuu”Aliongea Hera ambae ni kama sauti imempotea.
Hakuwahi kushuhudia radi ya levo hio na inakwenda kuwa mara yake ya kwanza , ukweli ni kwamba ni majini wachache sana ambao wameshuhudia radi ya mapigo elfu kumi na wengi wao waliamini ni ngano tu katika vitabu.
“Ukali wa nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi kumzunguka ni kama chuma kigumu , hii ndio levo ya mwisho kabisa ya ufahamu wa mbingu..”Aliongea Hephaestus akiwa katika mshangao.
“Inaonekana hii levo ya dhiki ya mwisho haitokei kwa kukusanya mawingu , hicho kizingia cha nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi kinataka kufanya nini?”Aliuliza Apollo kwa mshangao.
“Mnashangaa nini sasa , tumieni nafasi hii kabla Dhiki haijaisha , muueni”Aliongea Hermes.
Zeus ni kama amekumbuka cha kufanya na palepale aliongezea nguvu ya radi iake na kuirusha katika eneo ambalo Roma amesimama.
“Chwiiiii….!!!”
Dakika ambayo radi ile inataka kumkaribia Roma ilizuiwa na kizuizi ambacho hakionekani na kusababisha msuguano kama vile ni wa breki a gari uliopelekea mlipuko.
“Ule ni ulinzi wa kiroho?!”Hera aliuliza akiwa katika hali ya mshangao mkubwa
“Hicho kizingia kimemzunguka tayari na inaonekana ni kama ulinzi”Aliendelea kuongea.
Miungu walikumbwa na mshangao mkubwa mara baada ya kuona radi ya mapigo elfu kumi ilikuwa na tabaka lake la kumlinda mpitia Dhiki.
Kizingia cha mkusanyiko mkubwa wa nguvu ya kiroho ilikuwa ni tabaka la ulinzi kwa mtu yoyote au jini anaepitia mapigo ya levo ya mwisho wa Dhiki ili asiwe na mawasiliano na ulimwengu wa nje na isitokee yoyote wa kufaidika.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba radi hio inampata yule tu ambae anapitia mapigo hayo na si vinginevyo na ombwe ambalo limetengezwa na kizingia hicho ni kama njia maalumu ambayo radi itapita.
Ukweli ni kwamba sio kama radi hio inataka kumlinda Roma au nini bali ili radi hio kuweza kutokea lazima kuwe na mkondo maalumu , ni kama mfereji au useme njia maalumu ya radi hio kupita.
Roma alikuwa amesimama kwenye ombwe hilo la kisingia akiwa ametulia kabisa huku macho yake akiwa ameyafumba , ni kama vile alikuwa amesahau kila kitu kinachoendelea ulimwengu wa nje.
“Uzio umeweza kuzuia radi kupita , inamaana huo ulinzi una nguvu kiasi hicho”Walishangaa.
Hata radi ya Zeus ambayo ilisifika kwa ukali haikuweza kupita au kusababisha mtingisho wa aina yoyote ile
Miungu hao hatimae washajua hawana uwezo wa kumshinda Roma akiwa ndani ya kizingia na waliishia kuangalia namna anavyopitia mapigo ya radi.
Zues uso wake ulikunjamana , macho yake yaliwaka mwanga na aliongea kwa sauti.
“Kwasababu mambo yamefikia hatua hii , basi na tuogeni utukufu wa Mama Gaia na turudi katika miili yetu ya Titani”Aliongea Zeus.
Miungu walimwangalia kwa mshangao mkubwa kutokana na maamuzi yake.
“Zeus ni lazima kufanya hivyo ..tutakula nguvu nyingi kutoka kwenye Mti Mama na uungu unaochipua utanyauka na kuzuia roho nyingine kuchelewa kufufuka”Aliongea Poseidon kwa uangalifu.
“Naunga mkono , hata kama atafanikiwa kupita levo ya mapigo elfu kui ya radi uwepo wako na Athena ukijumlisha na sisi haina haja ya kurudi katika miili yetu ya Titan”Aliongea Hera.
“Na tuanzeni , tunahitaji kurudi katika miili yetu ili kumaliza hii vita”Aliongea Athena ambae alikuwa kimya muda wote.
Miungu walijikuta wakishangaa na kwasababu alioengea ni Athena basi waliamini kuna sababu hivyo maamuzi ya Zeus kutokupingwa na wengine.
Ijapokuwa baadhi yao waliona haina haja ya kwenda mbali hivyo lakini kilichokuwa mbele yao ni vita ambayo hawapaswi kushindwa.
Mwishowe miungu wote walifanya maamuzi na kupaa mpaka kwenye kilele cha mti mama na kutengeneza duara.
Sekunde ileile miungu wote walianza kutoa miale ya mwanga na anga kuwazunguka lilianza kupinda pinda na kucheza huku eneo la katikati nguvu ya kiroho ikichemka kwa kasi kubwa.
Kadri walivyokuwa wakiendelea kiasi kingi cha nguvu ya kiroho kiliungana na Mti Mama na palepale mwanga wa dhahabu uliokuwa kama uji uliwafunika wote hata wasiweze kuonekana kwa nje.
Muda huo huo upande wa Roma ambaye alikuwa kwenye kisingia cha nguvu ya kiroho hakushituka hata kidogo licha ya kujua kila kitu kinachoendelea nje yake, alikuwa amezama kwenye utambuzi wa Adhabu ya mapigo ya radi.
Roma alikuwa akiitikia wito wa mapigo elfu kumi ya radi na kupanua ubongo wake kukwea katika mbingu za ufahamu , kujua asili ya vitu vyote na kutafuta uthibitisho.
Upande wa miungu walikuwa tayari washafanikuwa kuunganisha ufahamu wao na mti mama na miili yao ilizidi kufuka miale ya mwanga.
Katika anga hilo ndani ya ncha ya kaskazini hatimae sauti zilipaa angani na kugonga huku na huko mawinguni, zilikuwa ni sauti za wimbo ambazo lugha yake haikufahamika.
Hio ndio lugha ya miungu waliokuwa wakitumia.ilikuwa ni ushairi(Ode) ambao miungu pekee ndio wanaoweza kuelewa.
“Wakati wa kuyeyuka kwa barafu juu ya Olympos , ukuu wa mungu utatanda ulimwenguni kote, tutauvaa utukufu wa ardhi na kuzisikiliza sauti za ngurumo ya radi , mambo yote chini ya utawala wa kifalme wa miungu milele ivukayo kesho, Hiki ni kizazi cha Titani”
Waliimba kwa kurudia rudia maneno na kufanya dunia yote sauti zao kusambaa kwa kasi sana.
Na muda uleule mti ule ulianza kufuka mwanga wa rangi ya Dhahabu na kuvamia juu ya duara walilotengeneza miungu , huku mwanga ule ni kama vile unazama mwilini na kuungana.
Miili ya miungu ilikuwa ni mwanga kulingana na aina ya nishati na kufanya kila mtu kung’aa kwa namna ya kipekee , huku ming’ao yao ikiendelea kuongezeka na kupanuka na nguvu yao ya kiroho ilizidi kuongezeka maradufu na kufanya mkandamizo wa hewa kuwa mkubwa kuliko isivyokawaida.
Mwili wa rangi ya Dhahabu na bluu ulionekana kutoka kwa Zeus , mwili wa jitu kabila la Titani , Zeus ndio aliekuwa wa kwanza kubadilika na ndani ya sekunde tu alikuwa ni jitu likubwa mno.
Mara baada ya kunyanyua mguu wake na kukanyaga juu ya bahari barafu yote ilipasuka pasuka vipande vipande na wimbi alilosababisha lilitengeneza Tsunami.
SEHEMU YA 794.
Ili kurudiwa na uwezo wao asilimia mia ilikuwa ni lazima warudi katika miundo yao ya Kititani , ilikuwa ndio njia moja tu ya kujipandisha ki uwezo zaidi na zaidi.
Ndani ya dakika chache tu mti wote ulipoteza nishati ya kutosha kwa kuwavalisha miungu miili yao kupitia uungu.
Ijapokuwa walikuwa wamekosa damu ya Titani kama ilivyokuwa kwa miili yao ya awali Mti mama ulikuwa na uwezo wa kuwapatia nguvu ileile.
Kitendo hicho kingeweza kusababisha mti kuathirika na kusababisha uungu uliokuwa ukihipua kunyauka kwa kiasi kikubwa lakini hilo ni swala ambalo miungu hawakutaka kulifikiria kwa wakati huo.,
Walihitajji nguvu ya kutosha kwa ajili ya kumdhibiti Roma ambae anapitia levo ya mwisho ya mapigo ya radi.
Kilichokuwa kikiogofya ni kwamba ukijumlisha na mwili wa kititani wa Zeus , miungu wote wlaikuwa wamebadilika kutoka katika miili ya kibinadamu na kuwa katika maumbvo yenye nguvu kubwa.,
Kama ambavyo binanamu huitwa binadamu , jini kuitwa jini na malakka kuitwa malakika ndio ilivyokuwa kwa iungu hawakuwa binadamu tena walikuwa ni Watitani.
Walikuwa na maumbo marefu mno ni kama vile viuno vyao ndio vinatenganisha mbingu na ardhi
Kila dakika walivyopiga hatua walisababisha wimbi kubwa la upepo na kila dakika walivyochezesha mkono ilikuwa ni Dhoruba.
Mara baada ya miungu yote kuzunguka mti ,mti huo haukuwa mkubwa tena.
Kitu kingine cha ajabu zaidi ni kwamba Dhana zao walizokuwa wakimiliki na zenyewe zilikuwa zimeongezeka ukubwa , haikujalisha ni Athena ngao yake au upinde wa Apollo na Artemis kila kitu kiiongezeka ukubwa kulingana na miili yao.
Bila shaka kama hazikuongezeka basi zisingeweza kuitwa Dhana za kititani.
Kuwa katika miili ya kititani iliwapa uwezo wa juu sana wa kutengeneza mashambulizi , kitu kikubwa zaidi miungu hao walikuwa wakipata bado nishti kutoka kwenye mti mama.
Jua , bahari , madini na kila kitu kingine ni rasilimali za kulisha siraha zao na ngao zao pamoja na miili yao.
Miili yao ilikuwa ni nishati , haikuwa miili ya nyama kama ya kibinadamu , ilikuwa ni kama wamegeuka na kuwa mwanga lakini katika maumbo ya watu.
Lekcha na wao kulikuwa na tofauti kidogo tu , pengine Lekcha alikuwa na mwili wa nishati wa Ant matter lakini wao walikuwa na miili ya kinishati inayotokana na Mti mama , nishati ambayo ilionekana kabisa wanapaswa kuipata ili kuendelea kuishi.
Pengine siku mmoja nishati ya dunia itaisha lakini wasingejali , pengine wangeweza kutafuta sayari nyingine na kurudisha uhai wao kama waivyovamia dunia.
Sasa kitendo cha miungu hao kupata miili yao ya kinishati , miili ya Titani inawafanya kuwa katika muonekanno wao wa awali isipokuwa tu kwa Zeus ambae mwili wake alionekana kuudumisha hivyo kumfanya kuwa na mwili wa damu na sio wa nishati kama wenzake.
Hera alikuwa amevalia taji la shaba huku mwili wake wote ukitoa mwanga wa rangi ya Cyani, mkonno wake wa kulia mkubw aulikuwa umeshikilia Golden Apple huku vazi lake likifanana na mng’ao wa mwanga aliokuwa akitoa.
Viumbe hao kwa jinsi walivyokuwa wakitoa mwanga wa ajabu pengine unaweza kuwafananisha na malaika kwa jinsi walivyosimuliwa tofauti tu ni kwamba walikuwa na maumbo makubwa kuliko malaika lakini kwa jinsi wlaivyokuwa wakitoa mngao wa kuumiza macho inaweza kuwa moja ya sifa ya kufanana.
“Kwasababu aaendelea kupitia Dhiki , tutamshabulia kwa uwezo wetu wote na pengine tunaweza kuvunja kizuizi kinachomlinda”Aliongea Hera,
Mara baada ya kubadilika katika maumbo yao ya kititani sauti zao ni kama zinatoka juu angani na kufanya sauti kusambaa umbali mrefu sana kama sio dunia nzima.
“Hatuwezi kuvunja , ilishapangwa kufanikiwa kufikia katika levo hio ya mwisho wa dhiki ya radi”Sauti ya Athena iligonga ngoma zao a masikio
Athena yeye alikuwa akitoa mng’ao mtakatifu wa rangi ya fedha , nywele zake ndefu zilionekana kuwa laini kupita kiasi zilizojisokota kwa kutengeneza mawimbi , alidhihirisha ushujaa na kufanya sura yake isichoshe kuangalia.
Kama malaika alikuwa amevalia na yeye gauni la kitambaa cha hariri huku eneo la kifuani kukiwa na mchoro wa jani la mzeituni , alinyoosha mikono yake na kuinua ngao ya Aegis usawa wa kifua chake na Siraha ya Pallas upande wa kulia , chuma hicho kilitoa mngao na msisimko unaoendana na mwili wake.
“Unaweza kuona nani anakwenda kushinda ?”Aliuliza Poseidon ambae alikuwa ameshikilia Chusa kubwa ya meno matatu.,
Mfale huyo wa bahari alikuwa katika muonekano usiokuwa ukivutia m nywele zake zilikuwa zimetapakaa na alikuwa na mwili mkubwa unaotoa mng’ao wa rangi ya bluu , alikuwa na mgogo wenye ncha kali kama vile ni mnyama wa baharini , kuanzia kwenye kiwiliwili kwenda chini alikuwa na umbo kama la nyoka wa baharini.
“Mimi na Zeus katika miili yetu uwezo wetu ni sawa na kusema levo a mapigo elfu kumi ya radi , uwezo wa Roma mara baada ya kuipita Dhiki ni sawa na wa kwetu au uliongezeka kidogo , kwa adui wa uwezo huo pamoja na kutokuwa na uungu unabii wangu hauwezi kuwa sahihi”Aliongea Athena akimjibu Poseidon,
“Haiwezekani , haijalishi ni kwa spidi kiasi gani uwezo wake unaongezeka hawezi kufikia mwisho mwa levo mwa mapigo elfu kumi ya radi “Aliongea Hephaestus mungu wa moto.
Alikuwa na nywele ambazo ni kama vile zinawaka moto akiwa nusu mtupu na mwili wake wa rangi ya shaba , alikuwa na utimamu wa kutosha wa kimwili na misui yake imepinda pinda kama jiwe huku akiwa na makovu kama vile yamechongwa katika mwili wake makusudi , upande wa hini kabisa alikuwa amevalia suruali ambayo imeunganisha na vyuma kwa namna flani hivi kama magamba.
Ijapokuwa alikuwa jitu kubwa sana, muonekano wake ni kama ulikuwa ukiadilika badilika na kumfanya kuwa mwepesi kama mwewe.
“Wewe Hephaestus kwanini usijaribu na hilo nyundo lako kuvuruga Dhiki yake?”Aliongea Hermes huku akitoa kiheko.
Tofauti ya Hermes na wengine ni kwamba hakuwa na mwili mkiuubwa na alikuwa na muonekano kama wa binadamu lakini sura yake ikiwa imezidi uzuri kimuonekano , alikuwa na kiuno chembamba mno, alikuwa ni kama vile amevaa vazi la kutengenea ambalo limeunganishwa na mbawa.
Hakuwa mpana sana bali alikuwa mrefu kwenda juu na kumfanya kuonekana kuwa mwepesi zaidi.
“Unadhani nashindwa kufanya hivyo , kwanini uwezo wa sisi Titanni kuwa mdogo mbele ya binadamu?”Alliongea Hephaestus kwa jeuri na palepale aliinua lishoka lake juu ambalo liliweza kushika moto mara moja na kuanza kuyeyusha anga.,
Faida nyingine ya miili ya kititani ni kwamba miili yao imeunganishwa na namna kanuni za anga zinavyofanya kazi , mashambulizi yao hayakuhitaji kutumia kanuni za anga kwa nia maalumu bali anga lenyewe ndio huwapatia nguvu.
Ni kama Hephaestus alivyoinua tu nyondo yake palepale ilishika moto na kuana kuunguza anga,
“Nyundo ya moto mtakatifu”
Hephaestus aliruka huku akifyatua lile linyundo na kulifanya lionekane ni kama linadondoka mahali Roma alipo , nyundo hio ilienda moja kwa moja kuvamia kizingia kilichomfunika Roma.
BOOM!!!
Mshindo mkubwa wa sauati uliweza kusikika mara baada ya kizingia kutingishika , nguvu yake ilisambaa kila kona
Wimbi hilo lililoambatana na moto liliyeyusha barafu yote iliokuwa katika nha ya kaskazini na kuwa bahari kikamilifu,
Lakini bado tu licha ya kizingia hicho kupigwa na kanuni za anga kupitia nyundo hakikuharibika wala kusogea hata kidogo
Hephaestus aliishia kukunja sura na miungu wengine pia walikuwa katika hali ya mshangao.
“Ni tabia gani ya ki elementi imetumika kutengenezea nguvu ya kiroho mpaka kutfengeneza kizuizi chenye nguvu namna hio kiasi cha kutoarhirika na kanuni za anga?”Aliuliza Hera.
Upande wa Roma alikuwa akijua mabadiliko ambayo yametokea upande wa ncje na uwezo wa miungu ulikuwa umeongezeka katika levo nyingine kabisa na wanajarbu kuigilia Dhiki yake,
Lakini ujio wa radi ya mapigo elfu kumi ulimfanya kutojali sana kile kinachoendelea
Katika Ombwe la mfereji uliotengenezwa na nguvu za kiroho hali ya giza ilitanda huku msukumo wa mawimbi ya hewa yakiongezeka na msisimko wa nguvu ya ajabu ulivamia ndani yake.
Kadri msisimko wa nguvu ya kimaajabu kungezeka ndivyo namna uzio uivyoendelea kuimarika zaidi na zaidi , kisingia kilizidi kuzunguka kwa kasi kubwa mbo na kufanya mfereji wa ombwe kuzidi kwenda angani
Roma aliweza kuhisi mvutano wa hali ya juu mno wa nguvu ya ajabu na tabasamu la ahueni lilijjionyesha kwenye midomo yake
“Kwahio kumbe ipo hivi”Roma alijisemesha moyoni.
Dakika ileile ilikuwa ni kama vile nyoka mweusi anashuka kutoka juu angani kupitia lile ombwe la mfereji na kufanya iwe kitu cha ajabu mbo kwa miungu wote waliokuwa katika eneo hilo.
Ukiachana na Sharif na Aoiline wlaiokuwa katika ulimwengu unaojitegemea hakuna ambae alitarajia radi ya mapigo elfu kumi ni nyeusi.
Radi hio yenye rangi nyeusi ya kimaajabu ilionekana kama vile ni wino na urefu wake ulifanya kuwa kama kamba nyeusi ndefu inayoheza cheza kutoka juu mawinguni,
Kilichowashangaza zaidi ni kwamba , radi hio nyeusi ilishuka bila ya ngurumo , yaani hali ilikuwa tulivu mno na ilikuwa ni kama hakuna kilihokuwa kimetokea.
Mandhari yalikuwa ya kimaajabu kwa wote na walizidi kuona ni maajabu mara baada ya pigo la radi kumfikia Roma bila ya sauti kabisa.
Waliweza kumuona Roma ndani ya ombwe la mfereji akiwa amezingirwa na ile radi nyeusi.
Radi hio haikutoa mwanga kama radi nyingine , ki ufupi ni kwamba unaweza kusema sio radi ni kitu kingine kabisa
Ukichana na mfereji huo mazingira yanayozunguka eneo hilo yalikuwa hayajaaathirika hata kidogo hata bahari iliokuwa chini ya Roma ilionekana kuwa tulivu.
“Hii ndio radi ya mapigo elfu kumi kwanini ni nyeusi?”Aliuliza Hermes lakini ilikuwa wazi miungu wote waliokuwa ndani ya hilo eneo hawakuwa na majibu.
Roma ambae alikuwa amezingirwa na kiza cha radi nyeusi ni kama vile alikuwa kwenye ulimwengu mwigine kabisa.
Akiwa amefumba macho yake aliruhusu radi ile nyeusi kuungana na mwili wake kidogo kidogo.
Alizuia pumzi na kuindoa akili yake katika mazingira ya mbingu na ardhi , alikuwa pia amezuia nishati za mbingu na ardhi kutofanya kazi .
Katika macho yake alichoweza kuoa ni anga lisilokuwa na mwisho , Roma aliweza kugundua alikuwa katika kundi la nyota za galaksi ya Milk way.
Nyota alizokuwa akiona zilitoa mingao ya kucheza cheza kama vile ni madini ya thamani kubwa yaliokuwa gizani.
Ulimwengu ulikuwa katibu yake na kumpa hali flani ya ukawaida ambayo hakuwahi kuihisia hapo kabla , katika eneo ambalo akili yake ilikuwa mwili wake ni kama vile ulikuwa ukijongea bila shida yoyote na kumfanya kusafiri mamilioni ya maili ndani ya sekunde tu.
Alikuwa ni kama samaki anaeogelea katika maji mengi au ndege anaepaa angani , ulimwengu aliokuwa ulimshangaza sana.
Radi ile iliendelea kuwa endelevu ikimzunguka kana kwamba inamlaki Roma . haikumletea maumivu yoyote wala usumbufu.
Lakini sasa Roma kila alipojaribu kuishikilia na mkono wake alishindwa kabisa
“Nini nakosa , bado nashidwa kuidhibiti?”Roma alijiuliza.
Katika radi hio Roma alikuwa akiona kabisa nishati za aina tatu ambazo ni kama anazijua
Nishati ya moto wa Zambarau , moto wa rangi ya bluu na moto wa rangi ya samawati”
Ni radi au moto wa rangi tatu ambao umetokana na elementi za moto , maji na nishati ya hasi na chanya lakini ajabu ni kwamba nishaati zote tatu zilionekana kuungana pamoja na kutengeneza radi hio nyeusi.
Kuungana kwa moto wa zambarau na bluu kunatengeneza radi ya mapigo tisini na tisa , kuungana kwa moto wa bluu na samawati ilitengeneza radi ya mapigo elfu moja ya radi
Je kuna uwezekano wa radi ya mapigeo elfu kumi kutokea kwa kuunganishwa kwa elementi zote tatu za moto ? hapana…
Kwa akili zake za haraka aliwez akuhisi kuna kitu cha ziada kilihokuwa katika hio radi ya kimaajabu , ilikuwa na nguvu zaidi kuliko elementi zote tatu za rangi ya moto.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba kutokea kwa radi hio nyeusi ni unganiko la nguvu za aina nne na kufanya radi hio kuvuka vizuizi vya kanuni ya nafasi na muda na nguvu yake ni kama ufunguo wa kuvunja vizuizi vyote vya mbingu na ardhi na kumfanya kuingia katika ulimwengu wa anga.
Roma alikumbuka swali la Clark akimuuliza je anao uwezo wa kupaa kwenda anga za mbali bila shida yoyote na alimjibu kwamba hawezi kwasababu hana nishati ya kutosha kuishi katika anga za mbali
Sasa radi ilikuwa mbele yake ilikuwa ni kama ufunguo wa kumuwezesha kwenda anga za mbali
Bila kujielewa Roma alikuwa ameingia katika mbingu nyingine yenye ufumbuzi tofauti na muda ulikuwa umesimama na kanuni za anga ni kama hazifanyi kazi katika mbingu hio.
Alikuwa ni yeye na ulimwengu ulikuwa wake, ilikuwa ni kama amefanaishwa na ulimwengu wa anga za mbali.
Taratibu kila kitu katika ulimwengu wake wa kawaida kilipotea , miungu waliokuwa wakimshambulia , Mti mama , bahari , hewa , dunia , anga na kila kitu kilipotea.
Hata zile nyota ambazo zlikuwa akiangalia zilianza kupotea tena katika ufahamu wake na hakuona tena , lakini sasa hata kama kila kitu kilikuwa kikipotea katika ufahamu wake hata muda kusimama lakini kila kitu kilikuwepo licha ya kuonekana kutokuwa na athari zozote,
Hio ndio ilikuwa ni asili ya anga tokea mwanzo , hio ndio ilikuwa ni nishati ya awali kabisa iliokuwa imefunika kila kitu ikiwemo dunia na sayari nyingine.
Roma kwa haraka sana alihisi ni kama alikuwa na macho manne ambayo mawili yametokea ndani kabisa katika nafsi yake, yaani ilikuwa ni kama vile kuna mtu anaemfunilia kila kitu kilichokuwa mbele yake.
Kila kitu alichofahamu kuhusu ulimwengu kilibadilika kabisa kutoka katika ujazo mpaka kuwa mtupu na tena kutoka kuwa mtupu mpaka ujazo.
Radi ya mapigo mengi ilikuwa imebadilika mara moja kutoka kutokushikika mpaka kushikika.
Kwa kutingishika tu hatimae aliweza kurudi kutoka uliwengu wa ufahamu mpaka katika uhalisia na kilichofuatia ni tabasamu la kutoka katika ujinga lililopamba uso wake na alianza kucheka kwa furaha kubwa kiasi cha kumfanya atingishike mwili na taratibu akayafumbbua macho yake.
Katika ombwe la mfereji ile nguvu ya kimaajabu ni kama ilihisi kitu na kuanza kujikusanya kwa kujitosheleza.
Kizingia kilichokuwa kikimzunguka kilianza kupotea taratibu na hatimae kabisa na kufanya iwe ni kama hakuna kilichotokea na amani ikarudi duniani.
Jambo hilo liliwashangaza miungu kwa mara nyingine , radi ya mapigo elfu kumi haikuwa kama matarajio yao kwani ilipiga mara moja tu na kisha kupotea.
“Hapo tunaweza kusema kafanikiwa ?”Aphrodite aliuliza akiwa na muonekano usioelezeka.
Kama alivyopewa utu wa jina la mapenzi na urembo hakika alikuwa na muonekano wa kuvutia mno , alitoa mng’ao wa rangi ya dhahabu , mtu anaweza kumsifia kwa kumfanya kielelezo cha ustadi safi , gauni lake la hariri nyeupe lilipambwa na udarizi wa maua yaliochanua na ndege wa dhahabu anaeruka , kiunoni alikuwa amefunga mkanda wa dhahabu ambao ulikuwa na utajiri wa mchoro wa kuvutia mno, mkanda huo ndio ulipewa jina la Magical Girdle.
“Nashindwa kuhisi mkandamizo wowote kutoka kwenye nguvu ya nishati na mbingu , hivyo ninaamini atakuwa amefanikiwa kupita Dhiki kwa asilimia mia moja”Aliongea Zeus akimjibu Aphrodite.
“Vyovyote vile , hii ndio vita yetu ya mwisho”Aliongea Ares.
Ares alikuwa ni kama vile ni mwanavita wa zama zile za kale , ukiachana na mkuki wake mrefu wa chuma alikuwa amevalishwa mwili mzima na cchuma kizito na kumfanya aonekane pua tu.
“Wote kaeni pembeni katika hili na mlinde mti mama , mimi pekee na Zeus ndio tupo na uwezo wa kupambana nae , kama tukipoteza nyie msipoteze muda wa kupambana nae”Aliongea Athena akimwangalia Roma,
Watitani hao wote hususani Hera na Poseidon walionekana kukasirishwa na maneno ya Athena , ijapokuwa uwezo wao haukulingana na wa Zeus na Athena lakini pengine walilingana na jini wa levo ya mapigo elfu kumi ya radi mara baada ya kujibadilisha kuwa mwili wa nishati , kubwa zaidi Hera alikuwa na mti wa matunda ya shufaa na kila tunda moja linaweza kumsaidia kufukuza aina yote ya mashambulizi.
“Acha kujiona unaweza kila kitu , umeshakiri wewe mwenyewe huna uwezo wa kumtabiria , nini kinakufanya uamini una uwezo wakushindana nae ukijumlisha na alivyo na akili , ukweli wa kwamba amefanikiwa kuigia katika levo ya mapigo elfu kumi ya radi na akapita moja kwa oja anatakuwa katikati mwa levo ya mwisho wa Dhiki, hebu achaneni na huyo malaya anachoongea na tumuueni huyu mwanaharamu na kuiharibu kabisa nafsi yake ili ajue ni kosa gani amelifanya kuua uungu wa Hade”Aliongea Hera.
Mara baada ya kutaja kuua uungu wa Hades , viumbe hao wote wa kititani waliharuka kwa hasira na kutupia pembeni wasiwasi wao na kumnyooshea Roma siraha zao.
Apollo alikuwa amekwisha kurudi katika umbo linalofanana na mngao wa madini ya almasi na bahari kumzunguka iliana kugeuka mvuke kutokaa na mngao wake kuwa na joto kali.
Artemis na yeye alikuwa katiak umbo la kititani na alitoa mngao mweupe kama wa mwezi , katika kiichwa chake amejifunga kibanio cha rangi ya dhahabu huku nywele zake ni kama vile zina umeme kwa namna inavyocheza cheza. amevalia gauni refu kama vile ni la harusi huku akimshambulia Roma kupitia Selene, bahari chini yake ilikuwa imeganda kutokana na nishati ya ubaridi aiokuwa akitoa.
Poseidon , Ares , Hephaestus na Hermes wote waliinua siraha zao wakipgana kummaliza Roa na pigo moja.
Nishati ya anga ilijikusanya karibu yao na kutengeneza umbo la chusa linalotoa mngao wa rangi ya bluu iliokolea , upande wa mungu wa vita Ares alikuwa ni kama vile anadidimiza anga katika eneo alilosimama Roma huku Caduceus ikiana kumtengenezea Roma ndoto na kuingilia usikivu wake.
Ukimtoa Aphrodite pekee , miungu wote ni kama wamepamba kutumuia uwezo wao wote kushambulia , hata hivyo hakuna wa kumlaumu kwani siraha yake ya magical girdle haikuwa kama siraha zao ambazo zinafanya mashambilizi ya moja kwa moja , hivyo kumfanya kuwa mnyonge kati yao.
Ares ambae alichujuliw akama mdhaifu sasa alikuwa na uwezo sawa na mwishoni wa mapigo mengi ya radi na kwa kuagalia tu miungu wote walionekana uwezo wao wakutumia kanuni za anga umeimarika maradufu.
Zaidi sana ni kwamba miungu wote walijua mashambulizi ya rasha rasha hayana maana hivyo walihitaji mbinu yakinifu ambayo inaweza kumzimisha Roma na kumtengenezea majeraha makubwa.
Mara baada ya kuona hakuna wa kumsikiliza Athena hakutaka kuongea lolote na aliinua siraha yake a kisha wakapenda ishara na Zeus na ghafla tu alimsogelea Roma kwa spidi kwa ajili ya kumshambulia.
MTUNZI: SINGANOJR
Vanity of vanities , all is vanity
SEHEMU YA 793.
“Zeus..!1”
Roma moyo ulimsinyaa , alijiuliza inamaana wimbi la sauti ambalo ni kama lilikuwa likitaka kuharibu anga lilitoka kwa Zeus?, ni palepale alipata kujua lazima sauti aliokuwa akiisikia kwenye akili yake ilipitia kwenye uungu wa Hades
Wakati huo mara baada ya kusikika kwa sauti, radi ya rangi ya dhahabu na bluu yenye urefu wa zaidi ya futi kumi ilipasua anga kama ilivyokokotwa kutoka kwenye kitu kisichoweza kuonekana na kwenda moja kwa moja kupasua radi na mawingu ambayo yalikuwa chini ya udhibiti wa Roma.
Mkono imara ulijitokea kutoka mawinguni na kunyakua shoti ya radi bila kujeruhi ule mkono kwa namna yoyote licha ya kwamba radi ile ilionekana kuushambulia ule mkono.
Ndani ya sekunde tu lile wingu lote lilitawanyika na hatimae mwili wa miraba minne ulionekana juu angani.
Alikuwa na ndevu ndefu nyeupe ambazo zilikuwa zikipeperushwa na upepo huku mashavu yake yakiwa na kingo kama za mawe pamoja na kona zake.
Macho yake yote mawili ni kama yametawaliwa na umeme na kufanya yatoe mng’ao wa ajabu ambao mweupe sio mweupe ni kama rangi ya majivu.
Mwili wake ulikuwa umesitiriwa na joho la rangi nyeupe lenye mikono mifupi ilioacha wazi mikono yake , huku misuli yake iliotuna ikionekana waziwazi na ilikuwa ni kama vile mwili wake wote umejaa kutu.
Roma aliishia kutoa macho yake tu asiweze kuamini , aliekuwa juu yake ni kama hakuwa amebadilika kabisa , kama alivyokuwa miaka elfu mbili iliopita.
Imewezekana vipi?
Miungu wote ambao walikuwa wamepoteza miili yao mara baada ya kuja duniani na kuvaa miiili ya binadamu, alishangaa mara baada ya kumuona Zeus akiwa na mwili wake wa awali.
Mara baada ya miungu kushuka hawakukaa hata siku moja wote waliamua kuivamia miili ya binadamu na kutelekeza ya kwao lakini kwa wale ambao walikuwa na uwezo wa juu ikiwemo miungu kumi na mbili waliweza kuishi nayo kwa muda mfupi kidogo kabla ya kuhamia katika miili ya binadamu.
Inasemekana Zeus ndio ambae alidumu katika mwili wake kwa muda mrefu na aliingia na mwili wake katika gereza la Roho.
Ndio maana muda huo Roma anashangaa ameweza vipi kutohamia katika mwili mwingine na kuishi na mwili wake licha ya kwamba katika mazingira ya dunia haiwezekani.
Alijiuliza je kulikuwa na sababu ya kipekee ndani ya gereza la Roho ambayo ilimfanya kuishi na mwili wake tofauti na mazingira ya dunia, maana kwa anavyoonekana ni kama haikuwa swali bali jibu.
“Kuwa na uungu wa Hades halafu kuwa adui wa miungu hustahili kabisa uungu wake na haustahili kabisa kuwa sehemu ya miungu , leo nitakuuwa na radi hii iliopo kwenye mikono yangu”Aliongea Zeus akimwangalia Roma kwa macho makali..
Na mara baada ya kauli hio aliinua mkono wake mkubwa juu na bila ya kuchezesha chezesha aliachia radi yote kutoka kwenye mikono yake kumshambulia Roma.
Mara baada ya miungu kuona tukio hilo wengine walikuwa katika hali ya heshima kwa Zeus na wengine walikuwa na furaha.
Ilionekana walikuwa wakijua fika kama Zeus ataamua kuingilia kati, Roma hana nafasi ya kushinda tena.
Roma spidi yake ilikuwa kubwa mno , hata kama ni radi ya Zeus haikuwa rahisi kutokuiona kwa macho yake na kabla radi ile haijamtoka Zeus alikuwa tayari ashajiandaa kukwepa.
Lakini sasa mara baada ya Roma kusogea upande mwingine kwenye hewa akijua kabisa amefanikiwa kukwepa shambulizi lile alipigwa na boriti tatu nyingine za radi na kusababisha mlipuko mkubwa wa shoti.
BOOM!
Roma alishindwa kuamini na hakujua ni nini kinaendelea , ilikuwa ni ile radi imetoka alipokuwa amesimama na kumfuata alipokuwa amehamia na kuvunja ukuta wake na kisha kumshambulia.
Ilikuwa ni kama vile radi ile ilikuwa na ufahamu kwamba atasogea hivyo ilibadilisha uelekeo bila ya taarifa.
Mwili wake wote ulionekana kuungua kwa kiwango cha juu cha joto, huku viungo vya ndani vikionyesha kuumia pia na kujinyonga nyonga, alishindwa kuzuia sauti zaidi ya kupiga yowe.
Maumivu hayo yalikuwa makubwa mno kuliko yale yaliosababishwa na siraha ya Athena wakati wa kumshambulia.
“Arghh..!!”
Roma macho yake ni kama yanapasuka na ni kama anajua sasa nama maumivu halisi ya radi yanavyokuwa
Mwili wake ni kama unaelekea kupalalaizi huku maumivu ni kama yameungana na mwili wake na kumfanya akitamani kifo kuliko kuendelea kuishi.
Uwezo wa Zeus ni sawa na kusema ulikuwa wajuu kiasi kuliko ule wa Athena , jambo ambalo lilimaanisha shoti ya radi yake ilikuwa na nguvu mara mbili na ya jini au mtu aliepitia mapigo elfu kumi ya radi.
Sasa Roma uwezo wake ulikuwa katika mapigo mengi ya radi na pengine ni sawa na kusema ni bahati kwake hajafa mara baada ya kupigwa na radi hio , ilimuwia vigumu kupona haraka kuliko mwanzo.
“Athena kwanini unasita sita, radi yangu itamfanya kuwa dhaifu , tumia mkuki wako kumchoma eneo la moyo na kisha tukiondoe kichwa chake”Aliongea Zeus.
Alikuwa akimwangalia Roma kwa madharau kutokana na kushindwa kwake kusogea huku akiongea na Athena.
“Huna haja ya kunifundisha cha kufanya”Aliongea Athena na palepale aliishikilia vyema siraha yake.
Roma alijikuta akipatwa na kiwewe mara baada ya kuona Zeus na Athena wanataka kumchangia kumshambulia .
“Sikutugemea kuishi lakini siwezi kufa bila ya kupambana”Aliwaza Roma.
“Ni mapema sasa kuniua”
Roma aliongea kwa nguvu akionyesha tabasam lake la ukichaa wakati akiwa anavumilia maumivu ya pigo la mwanzo.
Alikusanya mawingu kwa kasi ya ajabu ili kuanza kutengeneza radi na wakati huo huo alitoa Shoka lake na kumshambulia nalo Zeus.
Lakini sasa kumsogelea Zeus kwa ajili ya kumshambulia halikuwa swala jepesi hata kidogo kwani Athena ni kama alikuwa ashamtabiria ni njia gani Roma atapita na alitumia ngao yake ya Aegis kumzuia.
Bang!!!
Sauti kubwa ya kishindo ilisikika, radi pamoja na shoka lile viligongana na Ngao ya Aegis na ni ndani ya sekunde hio hio Athena alitoa ile ngao na kilichomkuta Roma ni pigo lingine la radi kutoka kwa Zeus.
BOOM!!
Shambulizi lingine la radi ya dhahabu lilimpata Roma na kufanya harufu ya kuungua kwa mwili kusambaa na Roma alijikuta akipiga yowe la maumivu huku akidondoka kutoka angani kama kimondo.
Radi ya Zeus kama ilivyosimuliwa na wagiriki inaweza kumshambulia adui na pasionekane mahali pa kujificha.
Radi hio ilikuwa na uwezo wa kumfuata adui eneo lolote hata kama ajaribu kukwepa vipi, hivyo ni sawa na kusema siku zote lazima ifikie shabaha, sasa ukijumlisha na uwezo wa Athena katika kutabili ilikuwa hatari kabisa kwa Roma.
Pengine dakika chache zilizopita alikuwa na uwezo wa kushambulia Mti Mama lakini muda huo ni kwamba hata uwezo wa kujilinda alikuwa hana na hata kama aamue kupokea mapigo ya Zeus kama alivyoamua kupokea ya Athena basi anaweza kuuliwa mara moja.
Haikushangaza kabisa kwani ki uwezo anaanza Zeus na kisha anaingia Athena lakini mara nyingi watu wanasema Zeus na Athena wapo levo sawa ila kinachomfanya Zeus kuwa juu zaidi ni kwamba Athena anao uwezo mkubwa wa kujilinda huku Zeus akiwa na uwezo mkubwa wa kufanya mashambulizi.
Kwa mfano kama ikatokea Zeus na Athena wakapambana inaweza asitokee mshindi kutokana na utofauti wao, Athena hatoweza kumshambbulia Zeus kutokana na kwamba hana mashambulizi imara na wakati huo huo Zeus kama atamshambulia Athena mashambulizi yake hayatopita kutokana na Athena kumiliki Aegis , ngao yenye uwezo mkubwa sana wa kukinga mashambulizi mengi.
Mpaka kufikia hatua hio ni kwmaba Roma hakuwa na uwezo wa kushambulia tena , kwani akishambulia Athena tayari ashatabilia mashambulizi yake na kuyakinga na ngao yake wakati huo huo Zeus radi yake ni kama ina ufahamu wakati wa kumshambuilia.
“Nadhani huu ni mwisho ambao hujautarajia?”Aliuliza Athena na sauti ya kikauzu huku akiwa na hali ya kihisia isiokuwa ikielezeka.
Roma ambae alikuwa akidondoka kutoka juu angani alijitahidi kutingisha kichwa chake kwa taabu.
Athena alikuwa na uwezo wa kumuongelesha Roma kutokana na kwamba alikuwa akishuka na Roma sambamba, tofauti ni kwamba Roma alishindwa kujizuia kudondoka wakati Athena ni kama anamfatilia Roma kwa karibu.
Sasa wakati alipomaliza kuuliza kwa kauli hio aliinua mkuki wake akinuia kumchoma nao Roma eneo la moyo.
“Sio kirahisi hivi , siwezi kufa kirahisi”Roma aliongea kwa sauti iliojaa maumivu.
“Kweli..?”
Muonekano wa Athena ulikuwa katika utulivu sana , yaani ni kama vile hana uadui na Roma lakini mikono yake ilikuwa tofauti.
“Pfff..!”
Mkuki wa Pallas uliokuwa ukitoa mng’ao wa rangi ya bluu ulikuwa tayari ushamchoma Roma eneo la kifuani kuingia kwenye moyo wake lakini hata hivyo haukuweza kupita kama ambavyo kila mmoja alitarajia .
Kabla Athena hajafanikiwa kumchoma kifuani , Roma alikuwa ashafanikiwa kuushikilia ule mkuki kwa nguvu usipite japo ya kwamba ulimchoma nchi kadhaa kuingia ndani lakini hakujali.
Damu ya moto ilimtoka Roma mkononi na kwenye kifua chake na kusambaa.
“Hatimae nimekukamata … Mkuki wako hatimae nimeushikilia na usione unaweza kuuchukua kutoka kwangu kirahisi”Aliongea Roma huku macho yake ni kama vile yanataka kumtoka pengine ni kutokana na maumivu.
“Kwel?”Athena aliuliza kana kwamba Roma alikuwa akiongea vitu visivyo na maana.
Sekunde iliofuata Athena alimbutua Roma na mguu wake kwa nguvu zote.
“Bang!!
Muda ambao Roma aliweza kusikia sauti ya kishindo alikuwa ni kama vile amegeuka kuwa satilaiti akiizunguka dunia huku yeye mwenyewe akijizungusha katika mhimili wake , kichwa chake kilipindishwa kwa angle mia na sitini na kwenda kuvaa mlima wa barafu.
Miungu wote waliweza kuona namna Roma alivyoenda kuvamia mlima wa barafu na kudidimia ndani asionekane kwa nje.
Athena alirudisha siraha yake iliokuwa imechafuliwa na damu na kuishia kuangalia sehemu ambayo Roma ametumbukia
“You… you can’t win against us”Athena alionekana kumung’unya maneno kwa lugha ya kingereza akimaanisha Roma hawezi kushinda zidi yao.
Zeus alieshikilia kitenesi cha shoti ya radi hatimae aliweza kufika juu ya barafu na alijikuta akikunja sura yake.
“Uungu wake unapotea kwa haraka sana!”Aliongea.
Miungu wengine na wao pia walifika kwenye barafu na waliweza kugundua pia uungu wa Hades unaisha kwa spidi kubwa mno
Ilikuwa ni kama kibatari ambacho kishaishiwa na mafuta na muda wowote kinakwenda kuzima na hio ndio namna uungu wa Hades ulivyokuwa ukipotea na palepale Christen machozi yalimjaa.
“Hades..!.ni kweli umeamua kumuua?”Aliongea Christen akimlaumu Athena akidhania amemuua Roma.
“Hapana, Aphrodite hebu tumia hisia zako kwa umakini, ijapokuwa uungu wake unapotea lakini mkandamizo wa nishati za mbingu na ardhi…”
“Uwezo wake unaongezeka … huyu mwanaharamu anatumia nafsi ya mnyama kuunyonya uungu wa Hades na kuubadilisha kuwa nishati za mbingu na ardhi”Aliongea Hera kwa kupaniki.
“Nini?!”Wengine wote sasa ni kama wanajua kinachotokea na kupiga kelele huku Zeus akiishia kumwangalia Athena.
“Hio ni mbinu yake nyingine?”Aliuliza Zeus lakini Athena hakukubali wala kukataa na wahenga wanasema kimya ni jibu hivyo moja kwa moja ilieleweka bila ya neno.
Dakika hio mlima wa barafu ambao ulikuwa katika hali ya utulivu ulianza kutingishika kwa nguvu kama vile unataka kuporomoka na ikafuatia wimbi ambalo lilikuwa likitoka chini yake.
Ni kitendo cha sekunde tu mlima wote wa barafu ulipasuka na kurusha mapande ya barafu juu angani kwa mita kadhaa na palepale Roma aliweza kuonekana tena ikiwa ni kama vile hakuwa ameumizwa eneo lolote.
Lakini muda huo miungu hao hawakuweza kabisa kumjua Roma kama mwenzao tena kwani uungu wa Hades ulikuwa ushamtoka kabisa.
Mtu ambae alikuwa mbele yao hakuwa tena Hades bali alikuwa ni binadamu mkamilifu mwenye mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba Roma sio Hades tena kwani jina hilo lilitokana na nusu ya uungu wa Hades, hivyo ni sawa na kusema Roma amerudi kuwa Denisi binadamu kamili aliezaliwa duniani.
Uungu ndio mzizi wa miungu au unaweza kusema ndio asili yao ambao hubeba uwezo wao wa hali ya juu sana na kuwafanya kuwa na nguvu kubwa ya kiroho mpaka kuwawezesha kuhama kutoka katika mwili mmoja kwenda katika mwili mwingine.
Chaos ni mnyama wa machafuko ambae anao uwezo wa kumeza kila kila kitu ndani ya ulimwengu, hivyo hata kwa uungu ni kitu ambacho kinaweza kumezwa na Chaos kutokana na kwamba uungu hubeba nguvu ya kiroho ambayo chanzo chake sio ardhi bali ni ulimwengu(Universe).
Roma aliamua kufikiria nje ya boksi na akaamua kuitumia nafsi ya Chaos kuumeza uungu wa Hades ambao alikuwa akimiliki kwa ajili ya kupandisha uwezo wake kwa levo ya juu zaidi ndani ya muda mfupi.
Mara baada ya kufufuka kwa moyo wa Gaia uungu wa Hades na wenyewe ni kama ulikuwa unapona na kufikia uwezo ambao ni sawa na mapigo elfu moja ya radi.
Yaani kwa lugha rahisi ni kwamba Roma alikuwa na uwezo wa kutumia kanuni za anga na kama utamfananisha na mtu anaevuna nnishati za mbingu na ardhi basi ni katika levo ya mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi uwezo ambao ni wajuu sana.
Sasa unapaswa kuelewa mara baada ya Chaos kumeza uungu wa Hades aliugeuza kuwa nishati ya mbingu na ardhi ambayo moja kwa moja ilienda kwa Roma.
Sasa katika mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi Roma alikuwa levo ya mapigo mengi ya radi huku upande wa kanuni za anga ni hivyo hivyo , kwa lugha nyepesi ni kama Roma ameunganisha uwezo wake wote kuwa kitu kimoja yaani alichanganya uungu wa Hades na nishati ya mbingu na ardhi.
Zamani ilimpasa Roma kutumia kanuni za anga peke yake na vilevile nishati za mbingu na ardhi peke yake , lakini muda huo vyote vilikuwa pamoja mara baada ya kufanikiwa kuubadilisha uungu kuwa nishati ya mbingu na ardhi.
Ukweli ni kwamba hio ndio mbingu ya kipekee ambayo Roma alifanya na miungu hawakutarajia kabisa.
Maana kitendo cha kufanya hivyo ni kama Roma kaamua kuachana na amswala ya kanuni za anga kwa ajili tu ya kuongeza uwezo wake.
Bila hata ya maelezo kutoka kwa Athena miungu hao walijua ni namna gani uwezo wa Roma umeongezeka na kuwa wa kutisha.
“Mkandamizo wa nguvu zake ni mkubwa mno , nashindwa hata kuangalia ni levo gani kafikia, ukijumlisha na uwezo wake wa mwanzo naogopa kusema kwasasa kafikia levo ya mapigo elfu kumi ya radi”Aliongea Hera akiwa na wasiwasi .
Roma sasa ni kama amekidhi vigezo vya kupambana na Zeus na Athena kikamilifu..
******
Sharif , Aoiline na wengine wote walikuwa wakiangalia kilichokuwa kikitokea katika ncha ya kaskazini kwa kutumia kioo cha maajabu.
Clark mwanzoni alijua Roma ameshindwa vita na kumfanya aanze kulia lakini mara baada ya kumuona mpenzi wake akisimama tena akiwa na uwezo uliongezeka haraka hakuweza kujizuia na kushangilia kwa furaha.
“Hehe .. huyu mtoto hatimae amegundua kwanini Hades alimwachia nusu ya uungu wake bila fahamu , alipaswa kujua siri hii mapema kama angeacha kujali sana maswala ya wanawake…”Aliongea Sharif.
Moja ya sababu kubwa ya Athena kumuomba Hades kutii takwa lake na kumwachia Roma uungu ni kwasababu tu alitaka kuweza kumtabiria kirahisi hata kama apande levo za juu sana , ilikuwa rahisi kumtabiria Roma kupitia uungu kuliko akiwa binadamu kamili.
Yaani kwa lugha nyepesi uungu wa Hades katika mwili wa Roma ilikuwa ni njia ya mawasiliano ya kinabii kati ya Roma na Athena.
Kulingana na maelezo ya Sharif kitendo cha Roma kufikia levo ya mapigo elfu moja ya radi ilimaanisha Athena hana uwezo tena wa kumtabiria lakini ajabu ni kwamba Athena bado alikuwa na uwezo wa kumtambiria Roma hio yote ni kutokana na uungu wa Hades ambayo ni njia ya mawasiliano.
Sababu ya pili Athena kutaka Roma aachiwe uungu ni kwa ajili ya kumfanya kuwa sehemu yao.
Ikumbukwe mara baada ya Athena kufika duniani aliweza kuangalia nini kitakuja kutokea mbeleni na kupitia unabii wake aliweza kugundua ni binadamu Roma Ramoni atakaeweza kuzuia mipango yake ya kufufua ndugu zake.
Sasa kwanzia miaka elfu ishirini iliopita Athena alikuwa akipambana na unabii kwa kubadilisha historia.
Kitendo cha kutaka Hades kumpatia Roma uungu ukiachana na dhamira ya kutaka kumtabiria kwa urahisi lakini vilevile alitaka kumfanya mmoja kati yao.
Lakini kitu ambacho Athena hakukifahamu ni kwamba Hades alikubaliana nae kirahisi akiwa na ajenda nyingine kabisa, kwa Athena Roma alipewa uungu kwa ajili ya kurahisisha mipango yake kwa Hades wa Zamani alimwachia Roma uungu wake kwa ajili ya kukwamisha mipango ya Athena.
Hivyo Roma kutumia uungu kupandisha uwezo wake ndio kete ya mwisho ambayo Hades wa Zamani alitarajia Roma kuicheza ili kuja kumshinda Athena na wenzake lakini hata hivyo hakumwambia Roma juu ya siri hio, ni kama alimpa mtihani wa kugundua yeye mwenyewe.
Hayo yote Sharif aliyajua tokea mwanzo wa mpango LADO unaanzishwa na yeye pia hakutaka kumpatia Roma siri hio kama anao uwezo wa kupandisha mara mbili uwezo wake kupitia uungu wa Hades.
Sasa Roma alishindwa kugundua siri hio mapema kutokana na Christen mpenzi wake Hades wa zamani kuwa rafiki yake, pengine kama asingekuwa na mfungamano wa kirahifi na Christen angeweza kugundua siri hio mapema sana.
Sasa Sharif alikuwa kwenye mshangao mara baada ya kuona Roma anazidi kushambuliwa na Athena na Zeus bila ya kutumia uwezo wake wote, yaani uungu wa Hades, alijiuliza au bado hajajua siri hio.
Sharif hakuwa mjinga kumtaka Roma apambane licha ya kwamba kimahesabu levo aliokuwa amefikia kulinganisha na wapinzani wake ni ndogo lakini ukweli ni kwamba hakuwa akibahatisha , alikuwa akijua tokea mwanzo njia pekee ya Roma kushinda ni kutumia Chungu chake kuubadilisha uungu kuwa nishati za mbingu na ardhi na kupandisha uwezo wake kwa haraka.
Aoiline macho yake yalicheza na haikujulikana anafikiria nini na aliishia kuangalia kioo bila ya kuongea neno.
Xumei na Mzee Yasu walikuwa na furaha , ijapokuwa walikuwa wakiyaheshimu maamuzi ya mwalimu wao kwa kuwapa binadamu na miungu nafasi sawa , wao walikuwa bado ni binadamu na walitamani kuona Roma anawaua miungu wote na dunia kubakia salama.
Sharif alikuwa ni kama Hades wa zamani tu wote walikuwa Neutral , Sharif hakutaka kuwazuia miungu kutokuitawala dunia kama uwezo huo wanao lakini pia hakutaka kujisumbua kama binadamuw atashindwa kulinda dunia yao.
Kama miungu wangeshinda na Mkuu wa Enzi kutokuingilia basi moja kwa moja Dunia ingekuwa chini ya miungu , kama binadamu wangeshinda kwa kuilinda sayari yao basi pengine ndio mapenzi ya Mkuu wa enzi, na moja kwa moja uangalizi angemkabidhi Roma
Hakukuwa na haja ya kati y a miungu kuwa na muangalizi kwani alijua fika wanao uwezo wa kuilinda sayari lakini kwa binadamu wote waliwakilishwa na Roma hivyo kama Roma angeshinda ilimaanisha ndio yeye kati ya binadamu wote mwenye uwezo wa kuilinda dunia.
*****
Muda huo namna ambavyo miungu walimwangalia Roma haikuwa ikielezeka kama walikuwa wakihisi kitu cha namna gani kwenye mioyo yao.
Mara baada ya kupoteza uungu, Roma alikuwa sasa amekuwa adui yao kikamilifu , hata kwa Apollo na Poseidon ambao walikuwa na urafiki na Roma hawakuwa na huruma nae tena.
Walikuwa wakimchukulia kama mwenzao kwasababu ya uungu wake na sio kwasababu alikuwa binadamu.
Lakini kubwa zaidi kwa wakati huo ni kwamba Roma alikuwa tishio kubwa kwa ajili ya ufufuo wao.
“Inavutia sana kwa ulichofanya , ni kheri kuua binadamu aliekamilika kuliko kumuua kaka yangu Hades”Aliongea Zeus huku akitoa kicheko kizito.
Upande wa Roma ni kama vile hakuwa akimsikia Zeus anachoongea na alikuwa amefumba macho yake huku akichanua mikono yake kama vile anaomba baraka kutoka juu mawinguni.
Ni dakika hio hio waliweza kuhisi kitu cha ajabu , kutoka kila pande nguvu kubwa ya kiroho ilikuwa ikijikusanya kumsogelea Roma.
Roma alikuwa ni kama sumaku na kuanza kuvuta kila aina ya nguvu ya kiroho iliokuwa karibu yake
Nguvu hio ya kiroho ilimwingia Roma na kubadilika kuwa nishati ya mbingu na ardhi na kuzidi kufanya sehemu ambayyo Roma amesimama kuwa na upepo mkali unaomzunguka kama kimbunga.
Kitendo cha upepo mkali kumzunguka Roma ilifanya kuwa ni kama Dhoruba ya kimbunga kikali na kufanya hewa kusukumwa kwenda juu angani kwa spidi kubwa , hatimae sehemu ambayo Roma alikuwa amesimama hakukuwa na hewa ya aina yoyote ni sawa na kusema Roma alikuwa ndani ya Ombwe(vacuum)
“Hii ni hatua ya mwisho ya mapigo ya radi , levo elfu tisa mia tisa tisini na tisa ya radi, levo ya mwisho wa Dhiki na mwanzo mwa ufunuo mkuu”Aliongea Hera ambae ni kama sauti imempotea.
Hakuwahi kushuhudia radi ya levo hio na inakwenda kuwa mara yake ya kwanza , ukweli ni kwamba ni majini wachache sana ambao wameshuhudia radi ya mapigo elfu kumi na wengi wao waliamini ni ngano tu katika vitabu.
“Ukali wa nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi kumzunguka ni kama chuma kigumu , hii ndio levo ya mwisho kabisa ya ufahamu wa mbingu..”Aliongea Hephaestus akiwa katika mshangao.
“Inaonekana hii levo ya dhiki ya mwisho haitokei kwa kukusanya mawingu , hicho kizingia cha nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi kinataka kufanya nini?”Aliuliza Apollo kwa mshangao.
“Mnashangaa nini sasa , tumieni nafasi hii kabla Dhiki haijaisha , muueni”Aliongea Hermes.
Zeus ni kama amekumbuka cha kufanya na palepale aliongezea nguvu ya radi iake na kuirusha katika eneo ambalo Roma amesimama.
“Chwiiiii….!!!”
Dakika ambayo radi ile inataka kumkaribia Roma ilizuiwa na kizuizi ambacho hakionekani na kusababisha msuguano kama vile ni wa breki a gari uliopelekea mlipuko.
“Ule ni ulinzi wa kiroho?!”Hera aliuliza akiwa katika hali ya mshangao mkubwa
“Hicho kizingia kimemzunguka tayari na inaonekana ni kama ulinzi”Aliendelea kuongea.
Miungu walikumbwa na mshangao mkubwa mara baada ya kuona radi ya mapigo elfu kumi ilikuwa na tabaka lake la kumlinda mpitia Dhiki.
Kizingia cha mkusanyiko mkubwa wa nguvu ya kiroho ilikuwa ni tabaka la ulinzi kwa mtu yoyote au jini anaepitia mapigo ya levo ya mwisho wa Dhiki ili asiwe na mawasiliano na ulimwengu wa nje na isitokee yoyote wa kufaidika.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba radi hio inampata yule tu ambae anapitia mapigo hayo na si vinginevyo na ombwe ambalo limetengezwa na kizingia hicho ni kama njia maalumu ambayo radi itapita.
Ukweli ni kwamba sio kama radi hio inataka kumlinda Roma au nini bali ili radi hio kuweza kutokea lazima kuwe na mkondo maalumu , ni kama mfereji au useme njia maalumu ya radi hio kupita.
Roma alikuwa amesimama kwenye ombwe hilo la kisingia akiwa ametulia kabisa huku macho yake akiwa ameyafumba , ni kama vile alikuwa amesahau kila kitu kinachoendelea ulimwengu wa nje.
“Uzio umeweza kuzuia radi kupita , inamaana huo ulinzi una nguvu kiasi hicho”Walishangaa.
Hata radi ya Zeus ambayo ilisifika kwa ukali haikuweza kupita au kusababisha mtingisho wa aina yoyote ile
Miungu hao hatimae washajua hawana uwezo wa kumshinda Roma akiwa ndani ya kizingia na waliishia kuangalia namna anavyopitia mapigo ya radi.
Zues uso wake ulikunjamana , macho yake yaliwaka mwanga na aliongea kwa sauti.
“Kwasababu mambo yamefikia hatua hii , basi na tuogeni utukufu wa Mama Gaia na turudi katika miili yetu ya Titani”Aliongea Zeus.
Miungu walimwangalia kwa mshangao mkubwa kutokana na maamuzi yake.
“Zeus ni lazima kufanya hivyo ..tutakula nguvu nyingi kutoka kwenye Mti Mama na uungu unaochipua utanyauka na kuzuia roho nyingine kuchelewa kufufuka”Aliongea Poseidon kwa uangalifu.
“Naunga mkono , hata kama atafanikiwa kupita levo ya mapigo elfu kui ya radi uwepo wako na Athena ukijumlisha na sisi haina haja ya kurudi katika miili yetu ya Titan”Aliongea Hera.
“Na tuanzeni , tunahitaji kurudi katika miili yetu ili kumaliza hii vita”Aliongea Athena ambae alikuwa kimya muda wote.
Miungu walijikuta wakishangaa na kwasababu alioengea ni Athena basi waliamini kuna sababu hivyo maamuzi ya Zeus kutokupingwa na wengine.
Ijapokuwa baadhi yao waliona haina haja ya kwenda mbali hivyo lakini kilichokuwa mbele yao ni vita ambayo hawapaswi kushindwa.
Mwishowe miungu wote walifanya maamuzi na kupaa mpaka kwenye kilele cha mti mama na kutengeneza duara.
Sekunde ileile miungu wote walianza kutoa miale ya mwanga na anga kuwazunguka lilianza kupinda pinda na kucheza huku eneo la katikati nguvu ya kiroho ikichemka kwa kasi kubwa.
Kadri walivyokuwa wakiendelea kiasi kingi cha nguvu ya kiroho kiliungana na Mti Mama na palepale mwanga wa dhahabu uliokuwa kama uji uliwafunika wote hata wasiweze kuonekana kwa nje.
Muda huo huo upande wa Roma ambaye alikuwa kwenye kisingia cha nguvu ya kiroho hakushituka hata kidogo licha ya kujua kila kitu kinachoendelea nje yake, alikuwa amezama kwenye utambuzi wa Adhabu ya mapigo ya radi.
Roma alikuwa akiitikia wito wa mapigo elfu kumi ya radi na kupanua ubongo wake kukwea katika mbingu za ufahamu , kujua asili ya vitu vyote na kutafuta uthibitisho.
Upande wa miungu walikuwa tayari washafanikuwa kuunganisha ufahamu wao na mti mama na miili yao ilizidi kufuka miale ya mwanga.
Katika anga hilo ndani ya ncha ya kaskazini hatimae sauti zilipaa angani na kugonga huku na huko mawinguni, zilikuwa ni sauti za wimbo ambazo lugha yake haikufahamika.
Hio ndio lugha ya miungu waliokuwa wakitumia.ilikuwa ni ushairi(Ode) ambao miungu pekee ndio wanaoweza kuelewa.
“Wakati wa kuyeyuka kwa barafu juu ya Olympos , ukuu wa mungu utatanda ulimwenguni kote, tutauvaa utukufu wa ardhi na kuzisikiliza sauti za ngurumo ya radi , mambo yote chini ya utawala wa kifalme wa miungu milele ivukayo kesho, Hiki ni kizazi cha Titani”
Waliimba kwa kurudia rudia maneno na kufanya dunia yote sauti zao kusambaa kwa kasi sana.
Na muda uleule mti ule ulianza kufuka mwanga wa rangi ya Dhahabu na kuvamia juu ya duara walilotengeneza miungu , huku mwanga ule ni kama vile unazama mwilini na kuungana.
Miili ya miungu ilikuwa ni mwanga kulingana na aina ya nishati na kufanya kila mtu kung’aa kwa namna ya kipekee , huku ming’ao yao ikiendelea kuongezeka na kupanuka na nguvu yao ya kiroho ilizidi kuongezeka maradufu na kufanya mkandamizo wa hewa kuwa mkubwa kuliko isivyokawaida.
Mwili wa rangi ya Dhahabu na bluu ulionekana kutoka kwa Zeus , mwili wa jitu kabila la Titani , Zeus ndio aliekuwa wa kwanza kubadilika na ndani ya sekunde tu alikuwa ni jitu likubwa mno.
Mara baada ya kunyanyua mguu wake na kukanyaga juu ya bahari barafu yote ilipasuka pasuka vipande vipande na wimbi alilosababisha lilitengeneza Tsunami.
SEHEMU YA 794.
Ili kurudiwa na uwezo wao asilimia mia ilikuwa ni lazima warudi katika miundo yao ya Kititani , ilikuwa ndio njia moja tu ya kujipandisha ki uwezo zaidi na zaidi.
Ndani ya dakika chache tu mti wote ulipoteza nishati ya kutosha kwa kuwavalisha miungu miili yao kupitia uungu.
Ijapokuwa walikuwa wamekosa damu ya Titani kama ilivyokuwa kwa miili yao ya awali Mti mama ulikuwa na uwezo wa kuwapatia nguvu ileile.
Kitendo hicho kingeweza kusababisha mti kuathirika na kusababisha uungu uliokuwa ukihipua kunyauka kwa kiasi kikubwa lakini hilo ni swala ambalo miungu hawakutaka kulifikiria kwa wakati huo.,
Walihitajji nguvu ya kutosha kwa ajili ya kumdhibiti Roma ambae anapitia levo ya mwisho ya mapigo ya radi.
Kilichokuwa kikiogofya ni kwamba ukijumlisha na mwili wa kititani wa Zeus , miungu wote wlaikuwa wamebadilika kutoka katika miili ya kibinadamu na kuwa katika maumbvo yenye nguvu kubwa.,
Kama ambavyo binanamu huitwa binadamu , jini kuitwa jini na malakka kuitwa malakika ndio ilivyokuwa kwa iungu hawakuwa binadamu tena walikuwa ni Watitani.
Walikuwa na maumbo marefu mno ni kama vile viuno vyao ndio vinatenganisha mbingu na ardhi
Kila dakika walivyopiga hatua walisababisha wimbi kubwa la upepo na kila dakika walivyochezesha mkono ilikuwa ni Dhoruba.
Mara baada ya miungu yote kuzunguka mti ,mti huo haukuwa mkubwa tena.
Kitu kingine cha ajabu zaidi ni kwamba Dhana zao walizokuwa wakimiliki na zenyewe zilikuwa zimeongezeka ukubwa , haikujalisha ni Athena ngao yake au upinde wa Apollo na Artemis kila kitu kiiongezeka ukubwa kulingana na miili yao.
Bila shaka kama hazikuongezeka basi zisingeweza kuitwa Dhana za kititani.
Kuwa katika miili ya kititani iliwapa uwezo wa juu sana wa kutengeneza mashambulizi , kitu kikubwa zaidi miungu hao walikuwa wakipata bado nishti kutoka kwenye mti mama.
Jua , bahari , madini na kila kitu kingine ni rasilimali za kulisha siraha zao na ngao zao pamoja na miili yao.
Miili yao ilikuwa ni nishati , haikuwa miili ya nyama kama ya kibinadamu , ilikuwa ni kama wamegeuka na kuwa mwanga lakini katika maumbo ya watu.
Lekcha na wao kulikuwa na tofauti kidogo tu , pengine Lekcha alikuwa na mwili wa nishati wa Ant matter lakini wao walikuwa na miili ya kinishati inayotokana na Mti mama , nishati ambayo ilionekana kabisa wanapaswa kuipata ili kuendelea kuishi.
Pengine siku mmoja nishati ya dunia itaisha lakini wasingejali , pengine wangeweza kutafuta sayari nyingine na kurudisha uhai wao kama waivyovamia dunia.
Sasa kitendo cha miungu hao kupata miili yao ya kinishati , miili ya Titani inawafanya kuwa katika muonekanno wao wa awali isipokuwa tu kwa Zeus ambae mwili wake alionekana kuudumisha hivyo kumfanya kuwa na mwili wa damu na sio wa nishati kama wenzake.
Hera alikuwa amevalia taji la shaba huku mwili wake wote ukitoa mwanga wa rangi ya Cyani, mkonno wake wa kulia mkubw aulikuwa umeshikilia Golden Apple huku vazi lake likifanana na mng’ao wa mwanga aliokuwa akitoa.
Viumbe hao kwa jinsi walivyokuwa wakitoa mwanga wa ajabu pengine unaweza kuwafananisha na malaika kwa jinsi walivyosimuliwa tofauti tu ni kwamba walikuwa na maumbo makubwa kuliko malaika lakini kwa jinsi wlaivyokuwa wakitoa mngao wa kuumiza macho inaweza kuwa moja ya sifa ya kufanana.
“Kwasababu aaendelea kupitia Dhiki , tutamshabulia kwa uwezo wetu wote na pengine tunaweza kuvunja kizuizi kinachomlinda”Aliongea Hera,
Mara baada ya kubadilika katika maumbo yao ya kititani sauti zao ni kama zinatoka juu angani na kufanya sauti kusambaa umbali mrefu sana kama sio dunia nzima.
“Hatuwezi kuvunja , ilishapangwa kufanikiwa kufikia katika levo hio ya mwisho wa dhiki ya radi”Sauti ya Athena iligonga ngoma zao a masikio
Athena yeye alikuwa akitoa mng’ao mtakatifu wa rangi ya fedha , nywele zake ndefu zilionekana kuwa laini kupita kiasi zilizojisokota kwa kutengeneza mawimbi , alidhihirisha ushujaa na kufanya sura yake isichoshe kuangalia.
Kama malaika alikuwa amevalia na yeye gauni la kitambaa cha hariri huku eneo la kifuani kukiwa na mchoro wa jani la mzeituni , alinyoosha mikono yake na kuinua ngao ya Aegis usawa wa kifua chake na Siraha ya Pallas upande wa kulia , chuma hicho kilitoa mngao na msisimko unaoendana na mwili wake.
“Unaweza kuona nani anakwenda kushinda ?”Aliuliza Poseidon ambae alikuwa ameshikilia Chusa kubwa ya meno matatu.,
Mfale huyo wa bahari alikuwa katika muonekano usiokuwa ukivutia m nywele zake zilikuwa zimetapakaa na alikuwa na mwili mkubwa unaotoa mng’ao wa rangi ya bluu , alikuwa na mgogo wenye ncha kali kama vile ni mnyama wa baharini , kuanzia kwenye kiwiliwili kwenda chini alikuwa na umbo kama la nyoka wa baharini.
“Mimi na Zeus katika miili yetu uwezo wetu ni sawa na kusema levo a mapigo elfu kumi ya radi , uwezo wa Roma mara baada ya kuipita Dhiki ni sawa na wa kwetu au uliongezeka kidogo , kwa adui wa uwezo huo pamoja na kutokuwa na uungu unabii wangu hauwezi kuwa sahihi”Aliongea Athena akimjibu Poseidon,
“Haiwezekani , haijalishi ni kwa spidi kiasi gani uwezo wake unaongezeka hawezi kufikia mwisho mwa levo mwa mapigo elfu kumi ya radi “Aliongea Hephaestus mungu wa moto.
Alikuwa na nywele ambazo ni kama vile zinawaka moto akiwa nusu mtupu na mwili wake wa rangi ya shaba , alikuwa na utimamu wa kutosha wa kimwili na misui yake imepinda pinda kama jiwe huku akiwa na makovu kama vile yamechongwa katika mwili wake makusudi , upande wa hini kabisa alikuwa amevalia suruali ambayo imeunganisha na vyuma kwa namna flani hivi kama magamba.
Ijapokuwa alikuwa jitu kubwa sana, muonekano wake ni kama ulikuwa ukiadilika badilika na kumfanya kuwa mwepesi kama mwewe.
“Wewe Hephaestus kwanini usijaribu na hilo nyundo lako kuvuruga Dhiki yake?”Aliongea Hermes huku akitoa kiheko.
Tofauti ya Hermes na wengine ni kwamba hakuwa na mwili mkiuubwa na alikuwa na muonekano kama wa binadamu lakini sura yake ikiwa imezidi uzuri kimuonekano , alikuwa na kiuno chembamba mno, alikuwa ni kama vile amevaa vazi la kutengenea ambalo limeunganishwa na mbawa.
Hakuwa mpana sana bali alikuwa mrefu kwenda juu na kumfanya kuonekana kuwa mwepesi zaidi.
“Unadhani nashindwa kufanya hivyo , kwanini uwezo wa sisi Titanni kuwa mdogo mbele ya binadamu?”Alliongea Hephaestus kwa jeuri na palepale aliinua lishoka lake juu ambalo liliweza kushika moto mara moja na kuanza kuyeyusha anga.,
Faida nyingine ya miili ya kititani ni kwamba miili yao imeunganishwa na namna kanuni za anga zinavyofanya kazi , mashambulizi yao hayakuhitaji kutumia kanuni za anga kwa nia maalumu bali anga lenyewe ndio huwapatia nguvu.
Ni kama Hephaestus alivyoinua tu nyondo yake palepale ilishika moto na kuana kuunguza anga,
“Nyundo ya moto mtakatifu”
Hephaestus aliruka huku akifyatua lile linyundo na kulifanya lionekane ni kama linadondoka mahali Roma alipo , nyundo hio ilienda moja kwa moja kuvamia kizingia kilichomfunika Roma.
BOOM!!!
Mshindo mkubwa wa sauati uliweza kusikika mara baada ya kizingia kutingishika , nguvu yake ilisambaa kila kona
Wimbi hilo lililoambatana na moto liliyeyusha barafu yote iliokuwa katika nha ya kaskazini na kuwa bahari kikamilifu,
Lakini bado tu licha ya kizingia hicho kupigwa na kanuni za anga kupitia nyundo hakikuharibika wala kusogea hata kidogo
Hephaestus aliishia kukunja sura na miungu wengine pia walikuwa katika hali ya mshangao.
“Ni tabia gani ya ki elementi imetumika kutengenezea nguvu ya kiroho mpaka kutfengeneza kizuizi chenye nguvu namna hio kiasi cha kutoarhirika na kanuni za anga?”Aliuliza Hera.
Upande wa Roma alikuwa akijua mabadiliko ambayo yametokea upande wa ncje na uwezo wa miungu ulikuwa umeongezeka katika levo nyingine kabisa na wanajarbu kuigilia Dhiki yake,
Lakini ujio wa radi ya mapigo elfu kumi ulimfanya kutojali sana kile kinachoendelea
Katika Ombwe la mfereji uliotengenezwa na nguvu za kiroho hali ya giza ilitanda huku msukumo wa mawimbi ya hewa yakiongezeka na msisimko wa nguvu ya ajabu ulivamia ndani yake.
Kadri msisimko wa nguvu ya kimaajabu kungezeka ndivyo namna uzio uivyoendelea kuimarika zaidi na zaidi , kisingia kilizidi kuzunguka kwa kasi kubwa mbo na kufanya mfereji wa ombwe kuzidi kwenda angani
Roma aliweza kuhisi mvutano wa hali ya juu mno wa nguvu ya ajabu na tabasamu la ahueni lilijjionyesha kwenye midomo yake
“Kwahio kumbe ipo hivi”Roma alijisemesha moyoni.
Dakika ileile ilikuwa ni kama vile nyoka mweusi anashuka kutoka juu angani kupitia lile ombwe la mfereji na kufanya iwe kitu cha ajabu mbo kwa miungu wote waliokuwa katika eneo hilo.
Ukiachana na Sharif na Aoiline wlaiokuwa katika ulimwengu unaojitegemea hakuna ambae alitarajia radi ya mapigo elfu kumi ni nyeusi.
Radi hio yenye rangi nyeusi ya kimaajabu ilionekana kama vile ni wino na urefu wake ulifanya kuwa kama kamba nyeusi ndefu inayoheza cheza kutoka juu mawinguni,
Kilichowashangaza zaidi ni kwamba , radi hio nyeusi ilishuka bila ya ngurumo , yaani hali ilikuwa tulivu mno na ilikuwa ni kama hakuna kilihokuwa kimetokea.
Mandhari yalikuwa ya kimaajabu kwa wote na walizidi kuona ni maajabu mara baada ya pigo la radi kumfikia Roma bila ya sauti kabisa.
Waliweza kumuona Roma ndani ya ombwe la mfereji akiwa amezingirwa na ile radi nyeusi.
Radi hio haikutoa mwanga kama radi nyingine , ki ufupi ni kwamba unaweza kusema sio radi ni kitu kingine kabisa
Ukichana na mfereji huo mazingira yanayozunguka eneo hilo yalikuwa hayajaaathirika hata kidogo hata bahari iliokuwa chini ya Roma ilionekana kuwa tulivu.
“Hii ndio radi ya mapigo elfu kumi kwanini ni nyeusi?”Aliuliza Hermes lakini ilikuwa wazi miungu wote waliokuwa ndani ya hilo eneo hawakuwa na majibu.
Roma ambae alikuwa amezingirwa na kiza cha radi nyeusi ni kama vile alikuwa kwenye ulimwengu mwigine kabisa.
Akiwa amefumba macho yake aliruhusu radi ile nyeusi kuungana na mwili wake kidogo kidogo.
Alizuia pumzi na kuindoa akili yake katika mazingira ya mbingu na ardhi , alikuwa pia amezuia nishati za mbingu na ardhi kutofanya kazi .
Katika macho yake alichoweza kuoa ni anga lisilokuwa na mwisho , Roma aliweza kugundua alikuwa katika kundi la nyota za galaksi ya Milk way.
Nyota alizokuwa akiona zilitoa mingao ya kucheza cheza kama vile ni madini ya thamani kubwa yaliokuwa gizani.
Ulimwengu ulikuwa katibu yake na kumpa hali flani ya ukawaida ambayo hakuwahi kuihisia hapo kabla , katika eneo ambalo akili yake ilikuwa mwili wake ni kama vile ulikuwa ukijongea bila shida yoyote na kumfanya kusafiri mamilioni ya maili ndani ya sekunde tu.
Alikuwa ni kama samaki anaeogelea katika maji mengi au ndege anaepaa angani , ulimwengu aliokuwa ulimshangaza sana.
Radi ile iliendelea kuwa endelevu ikimzunguka kana kwamba inamlaki Roma . haikumletea maumivu yoyote wala usumbufu.
Lakini sasa Roma kila alipojaribu kuishikilia na mkono wake alishindwa kabisa
“Nini nakosa , bado nashidwa kuidhibiti?”Roma alijiuliza.
Katika radi hio Roma alikuwa akiona kabisa nishati za aina tatu ambazo ni kama anazijua
Nishati ya moto wa Zambarau , moto wa rangi ya bluu na moto wa rangi ya samawati”
Ni radi au moto wa rangi tatu ambao umetokana na elementi za moto , maji na nishati ya hasi na chanya lakini ajabu ni kwamba nishaati zote tatu zilionekana kuungana pamoja na kutengeneza radi hio nyeusi.
Kuungana kwa moto wa zambarau na bluu kunatengeneza radi ya mapigo tisini na tisa , kuungana kwa moto wa bluu na samawati ilitengeneza radi ya mapigo elfu moja ya radi
Je kuna uwezekano wa radi ya mapigeo elfu kumi kutokea kwa kuunganishwa kwa elementi zote tatu za moto ? hapana…
Kwa akili zake za haraka aliwez akuhisi kuna kitu cha ziada kilihokuwa katika hio radi ya kimaajabu , ilikuwa na nguvu zaidi kuliko elementi zote tatu za rangi ya moto.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba kutokea kwa radi hio nyeusi ni unganiko la nguvu za aina nne na kufanya radi hio kuvuka vizuizi vya kanuni ya nafasi na muda na nguvu yake ni kama ufunguo wa kuvunja vizuizi vyote vya mbingu na ardhi na kumfanya kuingia katika ulimwengu wa anga.
Roma alikumbuka swali la Clark akimuuliza je anao uwezo wa kupaa kwenda anga za mbali bila shida yoyote na alimjibu kwamba hawezi kwasababu hana nishati ya kutosha kuishi katika anga za mbali
Sasa radi ilikuwa mbele yake ilikuwa ni kama ufunguo wa kumuwezesha kwenda anga za mbali
Bila kujielewa Roma alikuwa ameingia katika mbingu nyingine yenye ufumbuzi tofauti na muda ulikuwa umesimama na kanuni za anga ni kama hazifanyi kazi katika mbingu hio.
Alikuwa ni yeye na ulimwengu ulikuwa wake, ilikuwa ni kama amefanaishwa na ulimwengu wa anga za mbali.
Taratibu kila kitu katika ulimwengu wake wa kawaida kilipotea , miungu waliokuwa wakimshambulia , Mti mama , bahari , hewa , dunia , anga na kila kitu kilipotea.
Hata zile nyota ambazo zlikuwa akiangalia zilianza kupotea tena katika ufahamu wake na hakuona tena , lakini sasa hata kama kila kitu kilikuwa kikipotea katika ufahamu wake hata muda kusimama lakini kila kitu kilikuwepo licha ya kuonekana kutokuwa na athari zozote,
Hio ndio ilikuwa ni asili ya anga tokea mwanzo , hio ndio ilikuwa ni nishati ya awali kabisa iliokuwa imefunika kila kitu ikiwemo dunia na sayari nyingine.
Roma kwa haraka sana alihisi ni kama alikuwa na macho manne ambayo mawili yametokea ndani kabisa katika nafsi yake, yaani ilikuwa ni kama vile kuna mtu anaemfunilia kila kitu kilichokuwa mbele yake.
Kila kitu alichofahamu kuhusu ulimwengu kilibadilika kabisa kutoka katika ujazo mpaka kuwa mtupu na tena kutoka kuwa mtupu mpaka ujazo.
Radi ya mapigo mengi ilikuwa imebadilika mara moja kutoka kutokushikika mpaka kushikika.
Kwa kutingishika tu hatimae aliweza kurudi kutoka uliwengu wa ufahamu mpaka katika uhalisia na kilichofuatia ni tabasamu la kutoka katika ujinga lililopamba uso wake na alianza kucheka kwa furaha kubwa kiasi cha kumfanya atingishike mwili na taratibu akayafumbbua macho yake.
Katika ombwe la mfereji ile nguvu ya kimaajabu ni kama ilihisi kitu na kuanza kujikusanya kwa kujitosheleza.
Kizingia kilichokuwa kikimzunguka kilianza kupotea taratibu na hatimae kabisa na kufanya iwe ni kama hakuna kilichotokea na amani ikarudi duniani.
Jambo hilo liliwashangaza miungu kwa mara nyingine , radi ya mapigo elfu kumi haikuwa kama matarajio yao kwani ilipiga mara moja tu na kisha kupotea.
“Hapo tunaweza kusema kafanikiwa ?”Aphrodite aliuliza akiwa na muonekano usioelezeka.
Kama alivyopewa utu wa jina la mapenzi na urembo hakika alikuwa na muonekano wa kuvutia mno , alitoa mng’ao wa rangi ya dhahabu , mtu anaweza kumsifia kwa kumfanya kielelezo cha ustadi safi , gauni lake la hariri nyeupe lilipambwa na udarizi wa maua yaliochanua na ndege wa dhahabu anaeruka , kiunoni alikuwa amefunga mkanda wa dhahabu ambao ulikuwa na utajiri wa mchoro wa kuvutia mno, mkanda huo ndio ulipewa jina la Magical Girdle.
“Nashindwa kuhisi mkandamizo wowote kutoka kwenye nguvu ya nishati na mbingu , hivyo ninaamini atakuwa amefanikiwa kupita Dhiki kwa asilimia mia moja”Aliongea Zeus akimjibu Aphrodite.
“Vyovyote vile , hii ndio vita yetu ya mwisho”Aliongea Ares.
Ares alikuwa ni kama vile ni mwanavita wa zama zile za kale , ukiachana na mkuki wake mrefu wa chuma alikuwa amevalishwa mwili mzima na cchuma kizito na kumfanya aonekane pua tu.
“Wote kaeni pembeni katika hili na mlinde mti mama , mimi pekee na Zeus ndio tupo na uwezo wa kupambana nae , kama tukipoteza nyie msipoteze muda wa kupambana nae”Aliongea Athena akimwangalia Roma,
Watitani hao wote hususani Hera na Poseidon walionekana kukasirishwa na maneno ya Athena , ijapokuwa uwezo wao haukulingana na wa Zeus na Athena lakini pengine walilingana na jini wa levo ya mapigo elfu kumi ya radi mara baada ya kujibadilisha kuwa mwili wa nishati , kubwa zaidi Hera alikuwa na mti wa matunda ya shufaa na kila tunda moja linaweza kumsaidia kufukuza aina yote ya mashambulizi.
“Acha kujiona unaweza kila kitu , umeshakiri wewe mwenyewe huna uwezo wa kumtabiria , nini kinakufanya uamini una uwezo wakushindana nae ukijumlisha na alivyo na akili , ukweli wa kwamba amefanikiwa kuigia katika levo ya mapigo elfu kumi ya radi na akapita moja kwa oja anatakuwa katikati mwa levo ya mwisho wa Dhiki, hebu achaneni na huyo malaya anachoongea na tumuueni huyu mwanaharamu na kuiharibu kabisa nafsi yake ili ajue ni kosa gani amelifanya kuua uungu wa Hade”Aliongea Hera.
Mara baada ya kutaja kuua uungu wa Hades , viumbe hao wote wa kititani waliharuka kwa hasira na kutupia pembeni wasiwasi wao na kumnyooshea Roma siraha zao.
Apollo alikuwa amekwisha kurudi katika umbo linalofanana na mngao wa madini ya almasi na bahari kumzunguka iliana kugeuka mvuke kutokaa na mngao wake kuwa na joto kali.
Artemis na yeye alikuwa katiak umbo la kititani na alitoa mngao mweupe kama wa mwezi , katika kiichwa chake amejifunga kibanio cha rangi ya dhahabu huku nywele zake ni kama vile zina umeme kwa namna inavyocheza cheza. amevalia gauni refu kama vile ni la harusi huku akimshambulia Roma kupitia Selene, bahari chini yake ilikuwa imeganda kutokana na nishati ya ubaridi aiokuwa akitoa.
Poseidon , Ares , Hephaestus na Hermes wote waliinua siraha zao wakipgana kummaliza Roa na pigo moja.
Nishati ya anga ilijikusanya karibu yao na kutengeneza umbo la chusa linalotoa mngao wa rangi ya bluu iliokolea , upande wa mungu wa vita Ares alikuwa ni kama vile anadidimiza anga katika eneo alilosimama Roma huku Caduceus ikiana kumtengenezea Roma ndoto na kuingilia usikivu wake.
Ukimtoa Aphrodite pekee , miungu wote ni kama wamepamba kutumuia uwezo wao wote kushambulia , hata hivyo hakuna wa kumlaumu kwani siraha yake ya magical girdle haikuwa kama siraha zao ambazo zinafanya mashambilizi ya moja kwa moja , hivyo kumfanya kuwa mnyonge kati yao.
Ares ambae alichujuliw akama mdhaifu sasa alikuwa na uwezo sawa na mwishoni wa mapigo mengi ya radi na kwa kuagalia tu miungu wote walionekana uwezo wao wakutumia kanuni za anga umeimarika maradufu.
Zaidi sana ni kwamba miungu wote walijua mashambulizi ya rasha rasha hayana maana hivyo walihitaji mbinu yakinifu ambayo inaweza kumzimisha Roma na kumtengenezea majeraha makubwa.
Mara baada ya kuona hakuna wa kumsikiliza Athena hakutaka kuongea lolote na aliinua siraha yake a kisha wakapenda ishara na Zeus na ghafla tu alimsogelea Roma kwa spidi kwa ajili ya kumshambulia.