NILIEMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
CREATOR: SINGANOJR
SEHEMU YA 790.
“Yaliokuwako ndio yatakayokuwako ,yaliotendeka ndio yatakayotendeka, wala jambo jipya hakuna chini ya jua .Je! kuna jambo lolote ambalo watu husema juu yake , Tazama , ni jambo jipya?,Hilo limekwisha kuwako , tangu zamani za kale zilizokuwa kabla yetu sisi(Mhubiri 1:9-10)”
Mara baada ya kusikia habari za kurudi kwa Roma , wanawake wote pande zote za dunia wakipambana na mapepo , mizimu na maskeleton walirudi mara moja Visiwa vya wafu.
Blandina alilia sana kwa furaha akiishikilia mikono ya mwanae huku akimsihi asifanye jambo lolote la kijinga na kuuona ukweli waziwazi na kutoendelea kufanywa kipofu na Athena.
Roma aliishia kutingisha kichwa kukubaliana nae na mwishowe kumfanya Blandina mama yake ambae hakupata usingizi kwa muda mrefu kwenda kulala sasa kwa amani kufidia siku zote alizokuwa macho.
Upendo wa familia na wapenzi wake ulimfanya Roma kuhisi hali isioelezeka , kulinganisha na siku ziliozopita katika hali hio upendo huo ulikuwa na nguvu kuliko kitu chochote.
Hakuna aliemuuliza Roma alikuwa wapi , wala anachopanga kufanya ni nini na hata kama Roma hakupanga kumtaja Edna hakuna ambae angethubutu kutaja jina lake.
Roma upande wake alimfariji Bi Wema na kumwambia kwamba Edna hajafa ni kwamba tu hawezi kuamka kwa muda.
Bi Wema alielewa alichokuwa akimaanisha Roma na alijisikia vizuri japo kidogo tu , isistoshe alikuwa akiogopa nafsi ya Edna imeuliwa na Athena , alihisi maumivu makali kwa kipindi chote kwa kudhania ameshindwa kumlinda Edna kama alivyopewa jukumu na wazazi wake na ndio imekuwa kwaheri.
Ron , Sauron , Makedon na viongozi wa juu wa jeshi la The Eagles waliokuwa karibu na Roma walifika haraka wakiwa na wasiwasi na Roma alikutana nao na kufanya kikao cha muda mfupi huku akiwapa maelekezo ya siri ambayo hakuna mwanafamilia alieweza kuyajua.
Lakini kwa kuangalia nyuso za wazungu hao wakati wakitoka nje ya ukumbi wa kikao haikuwa ngumu kuelewa jambo ambalo Roma alikuwa akiongea nao lilikuwa siriasi mno.
Wakati wa usiku Roma aliamua kujituliza na kukaa katika ukumbi wa chakula na familia yake yote na kupata chakula cha usiku.
Lanlan alikaa karibu na baba yake na aliuliza ni wapi mama yake alipo mara kwa mara lakini Roma alichoweza kusema ni kwamba mama yake atarudi muda wowote , Kibonge huyo alikuwa na uelewa mkubwa mno wa akili na nikama kuna tatizo kwa mama yake lakini angalu kwa muda huo hamu yake ya kula imerudi.
Roma akiwa ndio anamalizia kula alionekana kukumbuka kitu na palepale aliweza kutoa siraha za kimaajabu kutoka katika hifadhi yake ya pete ambazo zlitoka nazo ulimwengu wa jicho la Anga.
Dhana na siraha hizo ziliwafanya wanawake wote kubung’aa kwa mshangao mkubwa.
Roma alisema akiwa na tabasamu kwamba anaomba msahama kwa kuwafana kuwa na wasiwasi kwa siku kadhaa na hakurudi nyumbani mapema hivyo amewalerea zawadi kufidia.
Kitendo cha Sui kuona Roma anawapatia wasichana hao Dhana za kale kama vile anagawa chakula , alijikuta akielewa uzito wa hali na kidogo tu apaliwe,
Alijua Roma alikuwa akihangaika huko na huko kutafuta hazina kama hizo lakini hakuja kuwazia Roma atakuwa tajiri namna hio.
Kwa Sui ambae ni jini pesa majengo na mambo yaayoonekana hayakuwa utajiri kwake , majini utajiri wao haukupigwa kwa kiasi gani cha pesa wanachomiliki bali kwa Dhana , ziwe Dhana zilizotumiw ana watangulizi wao au Dhana zilizotumiwa na wajumbe wa mkuu wa enzi.
Kwa wingi wa Dhana ambazo Roma anamiliki ni sawa na kusema ni utajiri wote waliokuwa nao miliki zote za majini katika ulimwengu usioonekana.
Ijapokuwa Dhana hizo zina thamani kubwa lakini kitendo cha Roma kuwapatia siraha hizo iliwafanya wapatwe na wasiwasi , ni kama washajua ni nini Roma anapanga lakini waliishia kutoa tabasamu na kupokea.
Baada ya chakula Roma alienda vyumba vya ardhini na kisha alitumia Chaos Cauldron na kuanza kutengeneza vidonge vya daraja la juu sana kwa kutumia malighafi zote alizokuwa nazo na kisha alivigawa vidonge hivyo katika makundi kulingana na idadi ya wanawake wake.
Mara baada ya kumaliza swala hilo Roma alirudi juu na akaingia katika humba cha Lanlan na kumwangalia binti yake ambae amelala baada ya kushiba , alimkodolea maho kwa muda mrefu na kisha alishikwa nywele zake na kumbusu kwenye paji la uso na kisha akaondoka.
Roma alivuta pumzi nyingi na kufanya unyevunyevu uliokuwa katika macho yake kupotea , haraka sana Roma alionyesha tabasamu la kifedhuli na kisha alisogelea chumba cha Rose na kuingia ndani.
Pengine huo unaweza kuwa usiku wa ajabu kwa Roma maisha yake yote.
Wanawake wote ndani ya ngome hio walikuwa na wofa kufa kutokana na ukichaa wa Roma.
Rose , Nasra , Amina , Neema , Dorisi , Magdalena , Mage , Najma na Yezi wote baada ya kuwa na Roma kitandani walitolewa katika vyumba vyao na kwenda kutupiwa kwenye kitanda kikubwa katika chumba cha Master.
Mwishonni hata kwa Yezi na Sophia ambao bado hawakuwa wameonja tunda lililokatazwa walikamatwa na Roma na bila aibu wakatupiwa juu ya kitanda.
Wanawake hao walishajua ni nini Roma anachotaka kufanya lakini ilikuwa ngumu kwao kukabiriana na uhalisia kirahisi.
Kati yao kulikuwa na wale ambao washashughulikiwa kwa wakati mmoja lakini awamu hio wanawake kumi na moja pamoja wamekusanywa sehemu moja walikuwa wakielekea kupatwa na ukichaa.
Wengine walikuwa wamevalia vyupi tu wengine magauni ya kulalia , wangine walivurugiwa muda wao wa kuvuna nishati , kila kitu kilikuwa tafrani.
Waliishia kuangaliana wakiwa na aibu mno na hawakujua nini chakufanya , aidha wakasirike au wacheke , waliona maji yamezidi unga.
Upande wa Roma makusudi alitengeneza ngao katika chumba hicho ili isionekane hata mmoja ambae atakimbia , hakuna ambae alikuwa na uwezo wa kuvunja ngao yake kwa namna yoyote ile.
Mara baada ya wote kukusanywa kitanda kilionekana hakitoshi na Roma alikuwa na uso uliojaa tabasamu la kifedhuli na alijirusha katikati ya fusi hilo la wanawake na kusababisha vilio.
Roma aliishia kusugua ngozi laini za wanawake hao kama vile anaogelea , haikuwa na haja ya kuangalia kwani wote walikuwa ni wake na alikuwa akimbusu huyu na kisha kuhabia kwa huyu na hakujali ni nani.
Ndani ya masaa mnne mbele wanawake wote aibu zilishawatoka tena na akili zishawacharuka , hata Yezi na Sophia ambao ndio mara yao ya kwanza walijikuta wakinogewa.
Roma alikuwa ni kama ameamua kufanya komesha maana ilikuwa ni vita, ilikuwa ni kama vile yupo miaka ile ambayo binadamu hakuwa amestaarabika.
******
Asubuhi hatimae kijua hafifu kiliweza kuingia ndani ya humba hicho kukubwa.
Roma alikaa kitandani kutoka katikati na mara baada ya kuona wanawake wengi namna hio aliishia kutingisha kichwa kwa kujisitikia na kujicheka mwenyewe.
Aliona kabisa kucheza rafu na wanawake hao kwa zaidi ya kumi alikuwa amezidisha.
Chumba kilijaa harufu nzito mno na ukweli ni kwamba hakuna ambae alikuwa amelela , wote walikuwa wakijifanyisha wapo usingizini lakini Roma mwenyewe alilijua hilo na palepale alionekana kutoa kijichupa kwenye hifadhi yake ya pete kilichokuw ana unga unga wa rangi ya kijani na kwa kutumia nishati ya mbingu na ardhi alisambaza poda ile hewani na wote walijikuta wakipoteza fahamu kwa kulala usingizi mzito.
Baada ya hapo Roma alisimama akaingia bafuni na kuoga na kisha akabadili mavazi mengine na kisha aligeuka na kuwaangalia.
“I am sorry babies .. no matter whether I Live or die , I cant escape this is my destiny”
Mara baada ya kuali hio hakuangalia nyuma tena na alipotea palepale akionyesha kabisa amekwisha kufanya maamuzi.
*****
NORTH POLE
Kadri macho yalivyozidi kuona , mti Mama kivuli chake kilikuwa kimetanda na kufanya iwe ni kama bahari ya njano , ilikuwa ni kama vile matawi yake hayakuwa na mwisho.
Juu kabisa ya mti huo Roma aliweza kuonekana akitokea kwa spidi kubwa.
Na ikiwa ni kama vile wamefahamu ujio wake Athena na miungu wengie ni kama vile wanatapikwa na anga na kutokea mbele kwa umbali flani.
Ilikuwa ni wazi kwa Athena unabii wake mkuu ulimtabiria Roma atarudi hivyo kufanya miungu hao kutokuwa na mshangao.
Kulikuwa na hisia zisiosomeka katika nyuso zao pekee , haikuwa kwa Venus au Artemis , au kwa Poseidon na Ares kila mmoja alikuwa katiika muoekano ambao haukuwa ukisomeka anawaza nini.
Ni kama wanatoa taarifa ya kwamba kubadilika kwa dunina ni swala ambalo halizuiliki.
Athena uso wake ulionekana kuwa katika hali ya utulivu kabisa , Edna na Seventeen licha ya kwamba nafsi zao zilikuwa hai lakini zilikuwa chini ya utawala wa Athena.
Ukiburi wake haukutaka kuyumbishwa na jambo ambalo limepangwa kutokea.
Upande wa Roma na yeye alionekana kuwa katika hali ya utulivu kabisa , tokea afikirie safari ya kufika hapo tayari alikuwa ameshajituliza.
Akiwa na tabasamu hafifu aliwaangalia marafiki zake wa kitambo ambao wakati huo walikuwa ni kama watu wageni machoni pake.
Mwishoni kabisa maho yake yalisimama kwa mmoja ambae alimsaidia kumpatia utulivu wa akili , sura ya kirembo ambayo si rahisi kusahaulika , mwanamke ambae alimpata kwa kumdhania ni kahaba.
“Bado tu umekuja?”Aliongea Athena kwa sauti ya chini.
“Nadhani unabii wako umetabiri ujio wangu hapa , je umetabiri nini kitatokea leo hii?”Aliuliza Roma akiwa na tabasamu hafifu.
“Ningekuwa na uwezo huo..nisingetumia nguvu nyingi kuandaa kila kitu , nimefanya kila kitu ndani ya uwezo wangu”Aliongea Athena na kumfanya Roma macho yake kuangaza ndani ya eneo hilo.
“Mtu muhimu naona haonekani hapa , Zeus bado tu hajatoka?”Aliuliza Roma.
“Mh , kwa uwezo wetu tuliokuwa nao haina hata ya Zeus kutoka , huna uwezo wa kushinda hata kidogo”Aliongea Hera kwa dharau.
Roma macho yake yalisinyaa na kwa umakini kabisa aliangalia mazingira kupitia uwezo wake nusu wa uungu na alijikuta akishangaa
“Zeus yupo ndani ya huo Mti?”Roma aliongea kwa mshangao mkubwa.
Roma alishangaa mara baada ya kugundua mtu ambae ana nguvu kubwa mno na asiemfahamu alikuwa amejikusanya juu ya tawi la Mti mama, mtu huyo nguvu zake hazikuwa kidogo kuliko za Athena.
Ilionekana kupitia Zeus na lile tunda ambalo lilichipuka katika mti huo ni kama kifaa ha kukusanya nishati za dunia na kuzibadilisha kisha kunyonywa na mti huo kkwa spidi kubwa kuliko mwanzo.
Ni sawa na kusema uwezo wa Zeus ulikuwa ukirahisisha ufiifuo wa nguvu za mti huo kwa spidi kubwa.
“Naona umeweza kuona?, Uungu wa Zeus ndio ulikuwa wa kwanza kuzaliwa kutoka mtini , ana muunganiko wa kipekee na mti mama , Zeus anasaidia mti huu kupona kwa haraka na ndani ya siku chache zijazo roho zote zilizopotea zitajikusanya juu ya mti na kuzaliwa upya katika miili ya miungu”Aliongea Hera.
“Kwahio tunapaswa kupambana haraka haraka ili huu mti usiendelee kukua kwa muda mrefu?”Aliuliza Roma akishika paji la uso wake kwa mawazo.
“Hades!”
Aphrodite alipiga hatua mbele , macho yake yalikuwa kama ya mwanamke aliepandwa na hasira a ilionekana alikuwa akishindana na wasiwasi wake.
“Ni kweli unataka tufikie huku , hatutakuwa familia sekunde ambayo utashambulia”Aliongea.
“Nilijaribu kuepuka kufanya chaguzi lakini nimegundua siwezi kukaa nje ya hili , samahani sana Christen , ilikuwa furaha sana kuwa na rafiki kama wewe ..lakini kuanzia leo hii mimi naitwa Roma Ramoni Kweka binadamu niliezaliwa na kukua katika dunia , wewe ni Aphrodite kiumbe kutoka sayari ya Mars hivyo usiwe na huruma tena”
“Umeongea vizuri sana , staili yako nimeipenda na kama unataka kupigana basi pigana acha kuzunguka zunguka , sogea sasa”Aliongea Ares huku akitoa cheko kubwa na palepale uungu wake ni kama ulibadilika na kuwa nguvu ya kiroho na anga lilianza kucheza kama bendera inapeperushwa na upepo na ghafla tu mkuki wa mungu huyo wa vita ulionekana.
Hata kama Ares alikuwa wa mwisho likija swala la nguvu lakini alikuwa na uwezo unaolingana na nguvu ya mapigo elfu moja ya radi kutokana na kufufuka kwa mti.
“Kwasababu umeamua haina haja ya kujizuia tena”Aliongea Apollo akijiangaa kushambulia pamoja na wenzake.
Apollo , Artemis na Hephaestus ambao walikuwa na uwezo wa juu kuliko Ares kwa haraka sana walionyesha uwezo wao mkubwa kupita levo ya mapigo mengi ya radi.
Ukiachana na Hera na Poseidon ambao uwezo wao ni kupita wa Apollo na wenzake Zeus na Athena walikuwa tayari washaonyesha uwezo wao wote ambao ukifananisha na mbinu za ardhi na mbingu ni mwanzoni mwa mapigo elfu kumi ya radi.
Nguvu hio kubwa ya kanuni za anga na usaidizi wa Mti Mama ilimzunguka Roma kama wimbi kubwa la bahari.
Siraha mbalimbali zilikuwa mikononi wa miungu , iwe ni Hellius , Selene , Nyundo , Mjeledi na nyoka wa vichwa viwili zote zilikuwa tayari kushambulia.
Kitendo cha Athena kuita siraha zake ikiwemo ngao ya Aeigis na mkuki Pallas anga lote la Ncha ya kaskazini ni kama linataka kudondoka.
Achana na Hera na Poseidon , ilikuwa ni msuguano wa hali ya juu mno wa anga , kwa mtazamo wa Roma mtu au jini aliefikia katika levo ya mapigo elfu kumi ya radi ndio anaweza kupambana nao.
Roma uwezo wake ulikuwa ukiiongezeka kwa kasi lakini bado alikuwa katikati mwa levo ya mapigo elfu moja ya radi , kwa wakati huo miugu ambao walikuwa na uwezo wa chini ni kama alilingana nao ki uwezo kinadharia.
Lakini uso wa Roma haukuonyesha hofu , ukiahana na kuwa na utulivu hakuyumba hata kidogo.
“Njooni wote kwa pamoja , hamniwezi mkiwa mmoja mmoja”
Mara baada ya Roma kuongea mawingu yaliosababisha ngurumo yalijikusanya kutoka pande zote , radi ya rangi ya silver ilianza kucheza cheza bila kutulia kuzunguka mwili wake.
Maneno ya Roma yaliwafanya miungu waone ni kama kichekesho ,ingawa hawakuamini Roma kuwa mdhaifu lakini hawakutarajia anataka kuwashambulia na radi ya mbingu.
Unachopaswa kuelewa licha ya kwamba Athena ndio pekee anaeweza kushindana na radi lakini haikumaanisha miungu wengie watakufa baada ya kushambuliwa nayo , kingine Roma anaweza ashindwe kuwashambulia.
“Hahahaha.. naona ukiburi hakuishia , adhani ukishapigwa kidogo ndio adabu itakushika , huwezi kukubali hitimisho lililotimia juu ya kufeli kwa binadamu”
Ares aliongoza na mkuki wake wa mungu wa vita ulionekana ghafla tu ukirushwa na kusimamisha anga kuzunguka eneo Roma aliposimama , alikuwa amesimaamisha muda ili kumfanya Roma asisogee huku mkuki ule ukifanya kazi na kumsogelea Roma kwa kasi kulenga kifua.
Katika mapigano ya namna hio , mbinu za kujionyesha onyesha hazikufanya kazi na nguvu halisi ndio kila kitu , kadri wepesi wako ulivyo ndio ufanisi wako.
Roma hakukwepa wala kupangua , alifungua kiganya chake na kubadilisha nguvu za mbingu na ardhi na kuwa radi na kisha alipasua anga ambalo lilikuwa limeshikilia na akaishikilia ile siraha moja kwa moja.
Miungu wote walishangaa , hata kama Ares uwezo wake ulilingana na wa Roma ilikuwa ni ngumu mno kuelewa siri ya mbinu ya nishati za mbingu na ardhi ambayo ina uwezo wa kusambaratisha anga lililosimama kutoka katika siraha ya Ares kirahisi namna hio.
Roma mara baada ya kuishikilia ule mkuki wa Ares aliuurusha kumrudishia akiwa ameunganisha na radi juu yake , Ares hakuthubutu kuidaka siraha yake na alikwepa ikapita kwenda angani.
Katika sekunde iliofuata miungu hawakuona haja ya kuangalia , walijua fika Roma hakuwa akiongea tu , iliaminika kwamba kama hawatopambana kwa kushirikiana basi hawatoweza kumzuia Roma kutokuharibu mti wao.
Hawakutaka kuona mti wao unaharbiwa wakati umefikia hatua hio.
Ghafla tu mshale wa jua , mshale wa nguvu ya kupatwa kwa mwezi , ndoto danganyifu na moto vilidondoka kwa pamoja kumshambulia Roma.
Roma uwezo wake wa kupambana ulitokana na majaribio mengi ya kifo na uhai , ijapokuwa amefikia katika levo inayomuhitaji maamuzi ya haraka lakini alikuwa na uwezo wa juu wa kuendana na mashambulizi.
Mwili wake wote ulikuwa umezingirwa na radi iliokuwa ikimzunguka kama kimbunga na kuendelea kuvunja kila mtego wa anga aliowekewa.
Roma aliita hungu cha maafa na kumpa amri nafsi ya mnyama kumeza kila mashambulizi yanayomsogelea kutoka pande zote na kuyageuza kuwa nishati ambayo inamfaa Roma.
Ingawa ilionekana Hera na Poseidon kuwa na uwezo mkubwa kuliko Roma kinadharia lakini kwasababu ya radi ya nguvu mara elfu moja ilikuwa sumu kwao walirudi nyuma.
Athena alieshikilia ngao ya Aegis alikuwa akizuia kila mashambulizi ambayo yalisogelea mti mama mara kwa mara na hakuonekana kushiriki katika vita hio kwa kukurupuka.
Vita ilikuwa ni kubwa mno , Roma alikuwa akikabiliana na mashambulizi yasiokuwa ya kawaida na mbingu mbalimbali lakini licha ya hivyo hakuonekana kuwa dhaifu
Dakika chache walikuja kujua Roma alikuwa akitegemea mashambulizi yao makubwa ili kukilisha chungu chake na kupandisha uwezo wake.
SEHEMU YA 791.
Waliona kama itaendelea hivyo muda mfupi tu Roma atafikia mwishonni mwa levo ya radi ya mapigo mengi.
Iisitoshe elementi za anga ambazo zilikuwa zikigeuzwa na miungu kupitia kanuni zao za anga zilikuwa kubwa mno kulinganisha na uchawi wa majini.
Kama ni chakula basi ni sawa na kusema mashambulizi yao ni chakula cha daraja la juu chenye kila aina ya virutubisho mbele ya Cauldron.
Poseiodon mara baada ya kuona hali hio ilikuwa ngumu kwake kumdhibiti Roma na aliita chusa(Trident), ilikuw ani kama vile kivuli cha rangi ya bluu kinadondoka kutoka juu angani kama kimondo na kudondoke bahari ya barafu na kuipasua vipande vipande na hatimae ile chusa ilionekana kutoboa.
“Boma la kiposeidon!!!!”
Aliongea kwa nguvu na palepale barafu zote zilizokuwa zimefunikwa maji zilitawanyika na maji ya baridi kali yalionekana hini yake.
Mlipuko huo haukuwa na athari zozote kwa Mti mama , mizizi yake haikuwa imeshikiliwa na bahari bali ilikuwa imeenda sana chini kupita miamba.
Punde tu nyoka wa baharini walijitengeneza kutoka katia maji hayo na kufnyatuka kuelekea angani huku wakiachama kumlenga Roma na kileChungu.
Kila pale chungu kilipotaka kumeza nyoka hao wa kibaharini walionekana kukwepa kana kwamba walikuwa hai na kusababisha roho ya uovu ya chaos kugeuka geuka bila mafanikio.
Roma palepale alipata ufahamu , ingawa nyoka hao walikuwa wameitwa kupitia kanuni za anga na vilevile wametokana na elementi za dunia kama atatumia radi kushambulia basi zitamiliki radi yake na kuwa na nguvu zaidi.
Kwa msaada wa majoka hayo ya baharini ilimfanya Roma kuhama hama na kumtenganisha na nafsi ya Machafuko na ghafla tu ni kama uwezo wa miungu umepanda mara mbili.
Kila mara Poseidon alipopunga hewani chusa yake kulitokea wimbi kubwa la sauti , sauti hizo ni kama vile simulizi juu ya mnyama mkubwa wa baharini ambae alishwahi kuwepo na kumfanya Roma kuhisi ukichaa.
Roma hakujisaidia na aliishia kukunja sura kwani hisia zake ni kama zinacheza cheza na alishidwa kuepuka mashambulizi kadhaa.
Miungu hawakujjizuia tena kushambulia kwa kumheshimu mshindani wao pamoja na kutotaka tatizo katika ufufuo wa ndugu zao walimshambulia kisawa sawa.
Mishale ya moto wa jua , mishale ya mwanga mweupe kama mwezi na Nyundo ya moto vyote vilimpiga Roma na kumwachia makovu.
Kwa bahati nzuri Roma aliweza kupona kwa haraka kupitia Andiko la urejesho wa azimio na hakupatwa na majeraha lakini aliona kama hali ikiendelea hivyo nni swala la muda tu atafikia hatua hawezi kupona.
Hera aliunganisha kanuni zake za anga na nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi huku akiwa ameshikilia upinde wa machweo na kuendelea kumshambulia roma na mishale kwa nguvu kubwa mno.
Hio mishale sio tu kuwa na nguvu ya ajabu ya kanuni a anga lakini pia ilibeba athari za nishati ya mbingu na ardhi na kuwa na nguvu ya mishale miwili kwa wakat mmoja na hilo lilimfanya Roma kuwaza.
Katika eneo ambalo Roma alikuwa amesimama anga lake lilikuwa likilipuka huku miale ya mwanga ikitokea.
Ijapokuwa Roma alikuwa na namna ya kulinda mwili wake lakini nguvu ya miungu haikuwa ya kudharauliwa kabisa na alikuwa ametumia nguvu nyingi katika kujilinda na kukwepa mashambulizi , hakukuwa na amna ya yeye kushambulia.
“Duuh , huyu jamaa ni mgumu mno , inakuwaje bado yupo hai tu?”Mkonno wa Hera ulishaachia mishale mfufulizo kama dhoruba lakini bado anaona Roma hakuwa amedhulika kabisa na hakujizuia kukasirika.
Usiwe na wasiwasi , kadri tukavyoendelea hivi ni swala la muda tu atashindwa kujilinda , kwa uwepo wa huu mti nguvu zetu hazina kikomo”Aliongea Hephaestus akiwa ameshikilia nyundo yake ambayo ilikuwa imepata moto na kuwa nyekundu.
Lakini unadhani Roma alikuwa na mpango wa kuwaacha wafikirie upuuzi wa namna hio , mwanzoni alikuwa akiwaza kumaliza vita hivo kupitia radi lakini aliona hawezi hivo hakutaka kujisumbua kuficha vitu tena.
Palepale Roma aliamua kuchoropoa shoka lake la rangi ya shaba ambalo lilikuwa na upanda wa futi kumi kutoka katika hifadhi ya pete.
Ilikuwwa ni Dhana ya Wajumbe wa mkuu wa Enzi iliofahamika kwa jina la Pangea lakini baadae ikaja kutumiwa na jini pepo mmoja aliefahamika kwa jina la Pangu , jini huyo mara baada ya kupata Shoka hilo alijigamba kwamba yeye ndio alitenganisha mbingu na ardhi kupitia shoka hilo.
Roma alifoka na kwa nguvu ya sauti yake alipigisha hewani lile shoka pande zote.
Yale majoka ya bahari ambayo yalitaka kumshambulia Roma yalisambatasiwa mara moja na hayakurudi upya kama mwanzo na kugeuka maji ambayo yalidondoka baharini.
“Nini!!!... inaawezekana vipi , ukuta wangu haufanyi kazi”Poseidon alimaka.
Hephaestus na Hera ambao walikuwa wamesoma elimu ya majini na hadithi zao walijikuja nyuso zao zikisawijika , walibung’aa wasiamini kama ni kweli wanashuhudia shoka hilo.
“Inawezekanaje , lile nni shoka la Pangea , si ilisemekana lilipotea na Pangu, kwanini lipo katika mikono ya huyu mtoto?”Hera alipiga kele
Miungu wengine pia walionyesha hali za kushangaa , licha ya kwamba hawakuwahi kusikia uwepo wa hilo shoka lakini walijua siraha ya Roma ilikuwa ikitisha mno.
Wote walijikuta wakimwangalia Athena na ilionekana ni kama alikuwa ametarajia swala hilo kutokana na utulivu wake na alionekana kabisa alifahamu hawezi kumdhibiti Roma kwa muda ndio maana alisubiri akiwa pembeni.
“Bitch , kwanini hujaongea chochote kama ulijua fika ana hii Dhana?”Aliongea Hera kwa hasira
“Ungefanya nini hata kama ningekuambia?”Aliulia Edna kikauzu na kumfanya Hera kuishiwa na pumzi kwa kukosa neno.
Upande mwingine Roma alikuwa tayari katika matumizi ya Shoka na alilazimisha miungu kurudi nyuma kwa kulifyatua mara chache tu.
Haikujalisha ni aina gani ya sheria za anga zinatumika , ili mraadi tu iwe ni sheria za anga basi Shoka hilo lingefanya kazi yake.
Miungu walijua mbele ya shoka hilo kubwa katika mikono a Roma mashambulizi yao hayana nguvu yoyote kama vile wanatupa mayai kwenye jiwe.
“Pumbavu bora hata ingekuwa Dhana nyigine kwanini kati ya Dhana zote liwe hili Shoka lenye kuweza kupangua kanuni za anga ?”Hera alijikuta akisugua meno na alionekana kukosa jinsi zaidi ya kupunguza mashambulizi yake.
Mbinu zao zote za mashambulizi lazima zitokee kwenye neno sheria ya nafasi katika anga lakini kwa bahati mbaya shoka hilo lilitengenezwa na Wajumbe wa mkuu wa enzi kwa ajili ya kuharibu sheria hizo.
Kwa maneno mengine ni kama miungu wanatumia nafasi ya anga kama matofali na kujenga ukuta ambapo bumu liwe kama shoka la kubomoa ukuta wao ndio kilichokuwa kikitokea.
Haijalishi utajenga ukutwa wako kwa uimara wa naa gani lakini ukikutana na bomu lazima uporomoke.
Viumbe hao hatimae walijua kwanini Athena alimuona Roma kama mshindani wake licha ya kwamba alionekana kuwa na uwezo wa hini kidogo kuliko yeye.
Kwa matumizi ya shoka hilo kwenye mikoo ya Roma hila zote za Athena zinaweza sizifanye kazi pia.
“Hamuwezi kushindana na Shoka hilo la kipangea , lindeni Mti Mama mimi nitapigana nae”Aliongea Athena.
“Acha majigambo , hivi unadhani kupambana mwenyewe ndio utakuwa na uwezo tofauti na jumla yetu?”Aliongea Hera kwa hasira
Athena hakuongea neno na palepale alirusha ngao ya Aegis iliokuwa kwenye mikono yake.
“Bang
Ilitokea sauti kali ya kuumiza kama mshindo baada ya Shoka kugongana na ngao ya Athena kiasi cha kuifanya itoa mlio wa kulalamika.
Ambae amelidwa kutoka kwenye shambulizi hio alikuwa ni Hera ambae alikuwa bize kujibizana na Athena
Hera alifubaa mara baada ya kujua kama sio Athena kumuokoa angekuwa vipande vya nyama kwa kushambuliwa na hilo shoka , alijikuta akikosa jinsi na kutuliza hasira zake.
Mara baada ya miungu hao kuona tukio hilo walijua ni Athena pekee ambae anaweza kuhimili mapigo ya Shoka na Roma ambae yupo levo ya mapigo mengi ya Radi.
Kundi hilo kwa haraka sana walirudi nyuma na kumuachia Athena nafasi ya kupambana na Roma.
Roma alikuwa ashajua lazima kutakuwa na hio mechi na hakuonyesha utofauti wowote.
Mara baada ya kuona Roma anamsogelea kwa kasi na ngao yake pamoja na mkuki kwa kutokuwa na furaha kabisa usoni alifyatua shoka lake hewani
Lakini kabla hata shambulizi lile halijamfikia Athena alionekana kuhama kimaajabu tena kabla hata Roma hajafanikiwa kumalizia kufyatua shoka
Uwezo wake wa kitabiri hatimae ulionyesha faida zake muda huo , hata kama Aqthena hakuwa na uwezo wa kuona kila kitu kitkaacho tokea haikumwaannisha kwamba hawezi kutabiri nia ya mashambulizi ya Roma.
Mkuki wa pallas uliokuwa kwenye mikono yake uling’aa na mwanga wa ajabu wa bluu ulionekana na ulikwepa wimbi na shambulizi la shoka na kama shoti ulimsogelea Roma kwa kasi
Athena alihofanya ni kuunganisha maelfu ya matabaka ya anga kutoka kwenye parallel space na kisha akaunganisha na nguvu ya Pallas a kutengeneza nguvu kama vile ni Tsunami na kumgonga Roma kwa nguvu.
BOOM!!
Roma alipigwa na nguvu kubwa ya wimbi mgongoni lenye uzito wa tani zaidi ya laki moja na kufyatuuliwa kama vile ni mpira na ilikuwa ni rasha rasha ya mtu kutema damu angani ilioweza kuonekana.
Hata miungu hawakuamini , Roma pia alijikuta akishikwa na mshituko kwani ilikuwa ni raundi moja tu na ameshambuliwa nama hio.
Ukweli ni kwamba kama isingekuwa kwa mwili wa Roma ulivyo kwa mtu mwingine angekuwa amebakia vipande vipande kama sio uji uji
Roma alifurumushwa kilomita kadhaa huku akijjitahidi kujituliza na kuanza kuhema kw anguvu kama mbwa , aliishia kufuta damu zilizokuwa zikimtoka mdomoni na kuishia kutoa tabasamu la ukauzu akimwangalia Athena.
“Inaonekana umedhamiria kabisa kuniua”Aliongea Roma akimwangalia Athena ambae yupo katika sura ya kirembo ya mke wake.
Tabasamu ambalo Roma alikuwa nalo ni chungu huku uso wake ni kama ule wa mtu anaonyesha malalamishi.
Upande wa Athena alikuwa katika utulivu , gauni lake jeusi lilikuwa likipeperushwa na upepo na nywele zake ndefu zilifika mpaka kwenye mashavu yake.
“Na wewe si unataka kuniua ..nilidhani kwa ajili ya Edna na Seventeen hautoniua lakini sijategemea utakuwa mkatili hivi”
Roma majeraha yake yaliweza kupona kwa haraka na sasa aliweza kunyoosha mwili wake.
“Ukweli ni kwamba sina haja ya kukuua , angalau mashambulizi yako yananifanya none nafasi ninayo”
Athena aliishia kukunja ndita kiasi kama vile alikuwa akijaribu kuelewa Roma anamaaisha nini lakini haraka sana alishatarajia Roma anachotaka kwenda kufanya.
“Wewe mwanaume kichaa..”:
Athena muonekano wake ulibadilika palepale na alionekana kuonea kitu ambacho kiliwafanya miungu wengine kutokuelewa.
Ndani ya dakika hio hio Roma alionekana kucheka kama kichaa na kumuacha Athena peke yake.
Alichukua shoka lake la kipangea na kukimbia moja kwa moja mpaka katikati ya mti , Roma aliamua kupotezea swala la kujilinda mara baada ya kugundua mashambulizi ya Athena hayawezi kumuua na badala yake aliona aanze kucharanga mti na shoka lake ili kuudondosha.
Shoka lile lilikuwa na uwezo wa kuzivunja kanuni za anga ikiaanisha kwamba ingekuwa ngumu sana kwa miungu kulinda Mti Mama kudondoshwa na yeye.
Lakini katika mchakato huo Roma mwenyewe angeshambuliwa na miungu , alipanga kuvumilia hata kama maumivu na majeraha yatakuwa siriasi namna gani , ili mradi hawezi kufa na mpango wake kufanikiwa basi hakuna tatizo.
Mi9ungu kwa haraka sana waliamua kutumia kaununi za anga na kutengenza matabaka zaidi ya elfu moja kuwa ngao za anga wakijaribu kuzuia shoka kugusana na mti.
Lakini shoka lile lilikuwa ni kama kisu cha moto kinachokata plastiki wakati wa kudili na kanuni a anga.
Ngao hio ya anga hakuweza kuzuia shoka kupita kwani ilipasuliwa mara moja.
“Unadhani nitakuacha ufanikiwe?”
Athena alikuwa katika kiwango cha juu ha hasira , huku sauti yake ikiwa ya kikauzu kama vile ni barafu ya kuumiza mifupa na kufumba na kufumbua alikuwa tayari ashafika mbele ya Roma huku ngao yake ya Aegis ikimtoka mikononi mwake na dude kubwa rangi ya silver lilianza kuonekana mbele ya ngao ile.
Fuvu la Medusa , mwanamke aliesimuliwa kuwa na vichwa vya nyoka alionekana katikati ya ngao ile kana kwamba amerudi uhai , wale nyoka kichwani walionekana kuheza cheza huku ikiwa ni kama wanangea.
Inasemekana Medusa macho yake meusi yalikuwa yakitoa mng’ao wa rangi ya damu ya mzee huku yakiwa kama mashimo yaliojaa damu.
Roma alihisi kutetemeka kusiko kwa kawaida huku akiwaza tabia ya nguvu ya uchawi wa Medusa kugeuza mtu kuwa jiwe , alikuwa akielewa kwmaba hapaswi kuangalia macho yale ya damu hivyo kwa haraka aligeuza kichwa chake mbali.
Medusa alifahamika kama jitu la kutisha ambalo lilikuwa na nguvu huko katika sayari ya Mars , halikuwa kama ambavyo alivumishwa kwenye hadithi za wagiriki lakini ilikuwa ni kweli kwaba macho yake yalikuwa na uwezo wa kimaajabu wa kumgeuza mtu jiwe.
Medusa alikuja kuuliwa na shujaa wa sayari ya mars afahamikae kwa jina la Perseus na baada ya hapo akakata kichwa chake na kwenda kumtunuku Athena kwa ajili ya kuweka kwenye ngao ake.
Kitendo cha kuufanya uchaawi wa Medusa kuwa hai ilimpatia Athena nafasi ya kufanya shambulizi.
Athena alionekana kama vile ni kivuli cheusi huku akirusha ile siraha ake ya Pallas na kutengeneza mwanga wa bluu wa kimaajabu na kuufyatua kuelekea upande wa Roma.
Kitendo cha Roma kugeuza kichwa chake alihisi chembechembe za anga zisizokuwa zikihesabika zikimzunguka kuanzia kwenye mikono ake kama vile ameutumbukiza kwenye majij ya bahari.
“Arghhh..”
Roma alipigwa na wimbi la uhakika kwa mara nyingine na kufyatuliwa na kutokana na maumivu makali alijikuta akitoa kilio , ilikuwa ni kama vile mkono wake wa kulia umepondwa na aliishia kubiringita huku vipande vya nyama vilivyomtoka vikigeuka uji.
Athena alitabiria namna ambavyo Roma angekwepa shambulizi lake na katika eneo lilelile ambalo akili yake ingemwambia angesimama alirusha pigo na alimpiga kwa nguvu zake zote .
Roma alikuwa kwenye maumivu makali lakini hakuwa na nia ya kuacha , haraka sana aliponyesha mwili wake na kuushambulia mti mama bila ya kupumzika.
Chaos pia alijaribu kumpunguza kasi Athena na miungu lakini licha ya miungu kuwa rahisi kuzuiwa lakini kwa Athena ilikuwa tofauti .
Haikujalisha ni radi au Shoka Athena alikuwa akitabiri mashambulizi hayo na kukwepa na muda huo huo kurudisha shambulizi.
Mapigano hayo makali yalidumu kwa dakika chache tu huku wakipigana kwa raundi zaidi ya mia moja lakini mwishoni Roma ndie aliojnekana kuumia zaidi.
Pengine kama sio uwezo wa Roma kupona kwa haraka nafsi yake ingekuwa ishaharibiwa muda mrefu.
Lakini hata kama Roma alikuwa na uwezo wa kutumia nishati ya mmbingu na ardhi bila kikomo kulikuwa na mwisho wa uvumilivu, alikuwa akipata majeraha kila sekunde na kutopona kwa haraka na damu ilikuwa ikimtoka sana.
Roma alijua kabisa hana uwezo wa kuvunja kizuizi cha miungu kwa spidi hio na angeshindwa mapema tu kabla ya kutimiza lengo , hivyo aliona atumie mbinu nyingine.
Roma alipata wazo palepale na alibadilisha uelekeo akikimbia kuelekea upande wa bahari ya Arctic chini
Barafu ambayo ilisambaratishwa na Poseidon muda huo ilikuwa imejikusanya na kutengeneza mlima.
Roma alitumbukia katika kina cha maji kwa mamia ya mita na akapotea kabisa.
“Anafanya nini?”Hermes alijikuta akikunja sura kwa muda.
Uso wa Athena ulikuwa mkavu na alitumia uwezo wake wa kanuni za anga kutengeneza shimo katika maji hayo ili kuona hini yake sehemu ambayo Roma alitumbukia.
Roma ni kama amekitoa kafara chungu cha maafa kwani kilitoa sauti kama tanuru la moto kikijaribu kushambulia mti mama lakini ilikuwa ngumu kwa Chaos kufanikiwa.
Mbinu ya Roma ilikuwa nyepesi sana , kwasababu hakuwa na uwezo wa kukata mti basi aliona akachimbe na kuharibu mizizi yake na kama mizizi ikifa utanyauka wenyewe bila hata ya kushambuliwa.
Faida kubwa ya kushambulia mizizi katika kina kirefu cha maji ni kwamba kama miungu watataka kumzuia Roma basi wataishia kumshammbuulia kwa kutuma mashambulizi na ndio hayo hayo mashambulizi ambayo yyangeharibu mizizi.
“Kwa msaada wa nafsi ya mnyama wa mahafuko Cauldron njoo na uozeshe mizizi ya mti”
Athena ni kama alishajua nini Roma anataka kufanya lakini hakuona njia bado ya kudili na hali hio kwa muda.
Hio ndio moja ya udhaifu wa unabii wake , hata kama utaweza kumwambia nini kitatokea mbeleni lakini anaweza asibadili kitu.
Alichoonyshwa kinatokea sio kitu ha baadae ambacho angepata muda wa kupanga namna ya kutatua tatizo lakini alipatiwa sekunde tu na unabii wake
Mara baada ya kujua hawezi kuchelewa hata sekunde , Athena alichoweza kufanya ni kukiuka sheria na kutengeneza shimo la anga kutoka juu kwenda chini na kisha kupasua mfumo wa miamba ili kumfukuza Chaos.
Roma alikuwa ashatarajia hilo litatokea na alitumia shoka kuharibu mzito wa kanuni za anga wa Athena wakati huo juu angani radi zilianz akupoiga kwa kasi mno.
Boom , Boom
Juu ya bahari ngurumo zilizoambatana na radi zilipiga mfululizo na matokeo yake ni kama maji yameshika umeme na nguvu ya nishati za mbingu na ardhi.
Kitendo hicho kiliwafanay miungu kutogusa maji ya bahari kutokana na kukosa ngao kama Aegis hivyo wataathirika.
Lilikuwa tukio la kutisha kwelikweli namna wingu lilivyofunika bahari na kushambulia maji ya bahari kama vile Mungu ameunganisha umeme kati ya mbingu na ardhi.
Athena alitengenza nafasi na kwenda nusu kina ambacho amefikia Roma na kugundua alikuwa tayari ashaharibu mzingo wake wa kanuni za anga na maji yaliokuwa katika eneo hilo yamejaa umeme wa radi. Na hatiimae ndio alipata kujua kila kitu.
Roma kutumia Cauldron kuozesha mizizi ilikuwa hatua ya kwanza na ya pili ni kuyageuza maji ya bahari kuwa radi ambayo itashambulia mti.
Ijapokuwa Athena hilo ni jambo ambalo aliona linakwenda kutokea ndani ya dakika chache kulingana na unabii wake lakini alikosa namna ya kukabiliana nalo kwani hakuwa na uwezo wa kumuua Roma mara mmoja.
Uso wa Athena ulizidi kuwa mbaya lakini hakuwa na nguvu tena , ki ufupi kazidiwa ujanja na Roma , mara baada ya kuita ngao yake ya Aegis ili kujilinda aliishia kurudi juu ya bahari akiepuka kuyeyushwa na radi iliosambaa katika maji.
“Khaa… mti unaathirika na radi ?”Poseidon alipiga makelele
Athena mara baada ya kugeuza macho yake aliweza kuona moja ya matawi yalikuwa yameshambuliwa na radi lakini hata hivyo sehemu ndogo ya matawi haina athari sana kwa ukubwa wa mti huo.
Lakini Roma alikuwa akiendelelea kuunganisha mti huo na radi kutokea chini , yaani alikuwa akizalisha radi chini ya maji na kuziingiza katika mti na kusafiri kwenda juu na kusababisha mti ulioshikilia matawi kuanza kuharibika na ile ishati iliokuwa katika mngao wa dhahabu kupungua.
“Ni ngumu kuzuia hili , anao uwezo wa kutawala radi na mawingu anavyotaka na ikamtii , hivyo hii radi haiwezi kuzuilika kabisa”Aliongea Hephaestus akiwa na huzuni.
“Damn ….tatizo ni kwamba huyu mtoto ni ngumu sana kumuua lakini tunaweza kuelekeza uwezo wotu wote kujilinda”Aliongea Hera huku akisaga meno.
“Nilijua haitokuwa rahisi kudili nae , haijaisha bado , msiwe na wasiwasi sana”Aliongea Athena ambae alikuwa na maho kama nyota.
Miungu walishangaa kwanza kabla ya kushangaa zaidi.
Dakika hio hio mwili wa mti huo ghafla tu ulianza kutoa nishati kubwa mno na kutengeneza mzunguko kama wa kimbunga wa rangi ya Dhahabu kuanzia katikati ya mti.
Ilikuwa ni kama vile kiwanda cha kutengenezea mabomu ya nyuklia kinalipuka na mabomu yake katika eneo moja tu na wimbi la msukumo lilianza kusukuma maji yote mbali kwenda chini.
Kama utaangalia kwa juu ungeweza kuona maji yote ambayo yalikuwa yamezzingira mti huo yamepotea ndani ya sekunde kwa maili kadhaa.
Walioweza kusukumbwa na kimbunga hizo cha msukumo ni Roma na chungu chake
Ilikuwa ni kama vile bahari imegeuka lijimkono likuubwa na kumtupia Roma mbali na hakuweza hata kujizuia kwani nguvu hio haikuwa ya kawaida hata kidogo.
Roma akiwa angani akipeperushwa na kimbunga alijikuta ni kama kuna sauti imeingia katika akili akili yake na kusikia sauti nzito ikiongea na fahamu zake kwa lugha ya kimaajabu na pengine ameweza kutafirisi kupitia uungu wa Hades.
“Those who disobey the oracle , be punished”