Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

Simulizi ya kijasusi - Nilimdhania kahaba kumbe bikra

NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI: SINGANOJR

Mono no aware

SEHEMU YA 767.
Haikuwa na ubishi kabisa Roma aliweza kuona namna ambavyo Lekcha uwezo wake ulivyokuwa umeongezeka , kwa mahesabu ya haraka haraka ilikuwa tayari ni mwaka na Roma alishangazwa kwa namna ambavyo Lekcha ameimarika na ukweli ni kwamba hakuwa binadamu , alionekana kama kiumbe ambacho kipo katika umbo la nishati.
Aoiline upande wake alikuwa amechanguka na alionekana alikuwa akihangaika sana kujilinda na ngao ya kijini , yaani ilionekana uwezo wa kushambulia hakuwa nao zaidi ya kujilinda.
Nywele zake zilizokuwa za kirembo zilikuwa zimejikunja kunja kunja huku gauni lake likiwa limechanika chanika, mikia yake yote tisa ilikuwa ikionekana na kuwa kama kinga kwake.
Kama sio kwa uzuri wake wa uso ingekuwa ngumu kudhania mwanamke huyo alikuwa na hadhi kubwa kati ya majini wa jamii ya Mbweha.
Wawili hao pia walionekana kuhisia uwepo wa Roma na mara baada ya kumuona akishuka kutoka juu haikuwa kwa Aoiline tu lakini hata kwa Lekcha mwenyewe alikuwa katika hali ya mshangao.
“Ni wewe!, Wewe mjinga hukuweza kufanikiwa kutoka wakati ule?”Aliongea Aoiline akipandisha sauti na ni wakati uleule alifanya uchunguzi wa haraka haraka wa kumkagua Roma na uso wake ulikunja ndita.
“Embu subiri kwanza… naona uwezo wako umeimarika sana!?”Aliongea akiwa katika hali ya hamaki.
Roma nae alikuwa kwenye mshangao baada ya kugundua watu hao walikuwa katika floor hio kwa mwaka mzima wakiendelea kupigana.
“Hahaha…Hades wewe mpuuzi muoga muoga umekuja wakati muafaka, usije ukakimbia awamu hii wakati ukijiona unataka kufanya hivyo”
Lekcha alionekana kufurahi mno kama vile ameokota hela na ari yake ya kutaka kupigana ilipanda maradufu , nguvu ya Ant- matter ambayo ilikuwa ni kama mlima iliweza kuongezeka zaidi na zaidi.
Roma alijua wakati huo sio wa kujielezea na aliruka na kwenda kutua upande aliopo Aoiline huku akijilinda na Chaos Cauldron.
“Nitajielezea baadae , kwasasa rekebisha hali yako ya kimwili na niachie nidili na hili”Aliongea Roma.
Aoiline hakuwa msichana mdogo ambaye uwezo wake wa kufikiria ni mdogo , ijapokuwa uwezo wake ulikuwa ukizuiwa na kanuni za kifizikia za ulimwengu huo lakini uono wake haukuwa mdogo.
Hivyo alipanga kumpatia Roma nafasi kudili na maswala yao , isitoshe Lekcha alifika katika ulimwengu huo kwasababu ya ugomvi wake na Roma na yeye ni kama alinunua vita hio.
“Kijana, mimi Master wako nimeweza kushindana na huyu mshenzi kwa zaidi ya mwaka sasa hivyo usiniangushe”Aliongea.
Aoline alimwangalia Roma kwanzia chini na hali isiokuwa ikielezeka ilionekana katika uso wake na aliishia kutoa tabasamu hafifu sana na kisha alisogea pembeni kuangalia pambano.
“Sijawahi kuwaza juu ya uwezo wako lakini ushaanza kuniwazia vibaya , ngoja nikuonyeshe kwamba nilichokuwa nikifanya huko nje hakikuwa kitu cha kupuuzwa”Aliwaza Roma.
Kutoka kuwa chokoraa anaelala chini ya daraja mpaka kuwa mtu mwenye nguvu wa kuweza kushindana na Aoiline kwa zaidi ya mwaka mzima si jambo dogo na Roma alijikuta akimkubali Lekcha bila ya wasiwasi , maana uwezo wake sio wa kawaida.
Wakati Roma akiingia ulimwengu wa majini pepo na kukutana na Aoiline kwa mara ya kwanza alishindwa kabisa kushindana nae , lakini Lekcha aliishi katika ulimwengu huo kwa muda mfupi sana lakini alikuwa ameweza kupandisha uwezo wake kwa viwango vya juu hivyo kwake aliona kabisa hakuwa mtu wa kawaida lakini hata hivyo Roma wakati huo uwezo wake sio wa kawaida na alitaka kumuonyesha Lekcha maana ya nguvu halisi.
Unaweza kusema kwamba Lekcha alifika katika uwezo huo kwasababu ya Roma kumsukumia Kizwe kwake.
Yaani kama Roma asingempa adhabu Kizwe ya kubakwa na machokoraa basi ni hakika Lekcha asingeweza kukutana na Kizwe na hatimae kumuua Yan Buwen na kurithi uwezo wake.
Roma hakutarajia athari ya kile alichokifanya ingemfikisha katika hatua hio, wanasema kila unachokifanya leo kina athari mbeleni na ndio ambacho Roma aliweza kushuhudia na kwa namna yoyote ile kwasababu yalikuwa maamuzi yake wakati ule hakuwa na budi ya kuyakabili matokeo.
“Kwa vyovyote vile kwasababu Mungu amenileta na kukutana nae hapa ,, basi ni wakati wa kuhitimisha huu uhusiano mbaya kwa mikono yangu miwili”Aliwaza tena Roma.
“Inaonekana umekula vitu vingi ndani ya huu mnara”Aliongea Roma akiwa na tbaasamu.
“Kuna haja ya kuuliza , au ndio ushaanza kuniogopa , hivi unadhani mwaka wote niliokuwa ndani ya huu mnara nilikuwa napoteza muda , ijapokuwa nimeshindwa kumuua huyo mbweha lakini ilikuwa ni swala la muda tu .. majani ya kiroho na matunda yaliopo ndani ya huu mnara yamenifanya kuwa wa tofauti kabisa”Aliongea Lekcha akiwa katika hali ya kujiamini kabisa.
“Basi tuchukulie hii ni bahati maana hata mimi nimekuwa wa tofauti kuliko mwanzo , ngoja tuone nani alikuwa akipoteza muda”
Mara baada ya Roma kuongea tu mazingira yaliokuwa yakimzunguka ni kama vile yanaganda na kusababisha msuguano mkali wa elementi za hewa na kufumba na kufumbua radi ya Zambarau ilianza kujitengeneza kama vile ni transfoma la umeme linapiga shoti ambazo ziliruka kwa kunyongorota kama umbo la nyoka.
“Radi ya zambarau!!!”
Aoline ambaye alikuwa akiangalia kwa mbali alimaka huku akiingia katika tafakari nzito, ni kitu ambacho hakutegemea kukiona kwa Roma.
Roma licha ya kuonyesha karata yake hio kwa Lekcha hakubadilika hata kidogo na aliishia kutoa tabasamu la dharau katika uso wake na mkono wake ulibadilika na kuwa kama mkono wa chuma uliotengenezwa na nishati ya Ant- Matter, Shoti za nguvu ile zilikuwa zikitisha mno na ziiongezeka kila sekunde na kutaka kummeza Roma.
Ilikuwa ni sawa kusema mwili wa Lekcha kwa wakati huo ulikuwa ni nguvu ya Ant Matter na ilionekana ni kama vile alikuwa ashapata ufuno wa namna ya kuendeleza kuziongeza maradufu.
Kama sio kwa mnara huo kutokuwa wa kawaida , nguvu ambayo alikuwa akidhalisha Lekcha mnara huo ungekuwa umedondoka muda mrefu sana.
Roma ili kupambana na nguvu ile ya nishati isio maada palepale alibadilisha radi ile na kuwa kama mkuki na kisha alimrushia Lekcha ule mkuki kumchoma.
Nguvu ya radi haikuwa ya kawaida kabisa pia , ijapokuwa nishati ya Lekcha kila ilipokutana na radi ambayo huundwa na maada kulitokea ‘annihilation’ yenye nguvu kubwa kiasi kwamba uwiano ulikosekana.
BOOM, BOOM, BOOM!
Mlipuko mkubwa wa nishati zote mbili kukataana ulikuwa mkubwa mno na ulilipuka katika mfululizo na shambulizi la Lekcha likawa limesabaratishwa namna hio
Lekcha macho yake yalionyesha hali ya kukasirika , hakuamini shambulizi lake hilo ambalo alikuwa ameliongezea nguvu kwa muda mrefu lingeweza kusambaratishwa na nguvu ya radi.
Roma alikuwa mjanja mara baada ya kusambaratisha pigo la Lekcha alikuwa ameongezea nguvu kubwa mno shambulizi lake na mara baada ya mlipuko kutokea mshale mwingine uliweza kutoka na kumpata Lekcha katika kifua na kutengeneza shimo lakini hakukuwa na damu yoyote ilioweza kutokea zaidi ya nishati ambayo iliziba shimo lile haraka sana .
“Hey ..hahaha…Good .. what a powerfull move”Lekcha aliongea kwa kingereza huku akitingisha kichwa chake na kushika eneo la kifua chake ambacho kilitobolewa.
“Inasikisha kwamba huwezi kuniua kizembe namna hii na viradi vyako”
Roma aliishia kukunja sura , aliamini pengine shambulizi la radi lingeweza kumyeyusha lakini ilionekana nguvu ya Ant Matter ilikuwa kubwa mno na kufanya mwili wa Lekcha kuwa na kinga ilio imara.
Lekcha mara baada ya kupona palepale macho yake yalibadilika na aligeuka na kuwa kama lichuma lililotengenzwa kwa uji uji na ilikuwa ni kama mwili wake unaungua kwa shoti na kuzisambaza katika eneo lote.
Roma hakutaka nishati zile kumpata na alijikinga kwa kutumia Chaos Cauldron , chungu kile ni kama kilikuwa kikisubiria fursa hio kwani ile roho ya mnyama iliokuwa ndani yake iliweza kujitokeza kuonyesha ukali wake na kani kubwa ya mvutano ilidhalishwa na kutaka kummeza Lekcha.
“Aaah..ni yale yale , unadhani nitakuogopa kwa kutumia hilo lijichungu lako?”
Lekcha alitoa kicheko kama mwehu na bila ya kukwepa chungu kile alikisogelea na kukivaa na mara baada ya kufikiana na mwili wa Lekcha alilipuka kama bomu la nyuklia.
“Bang!!
“Hoooo…!!!
Ile nafsi ya Chaos ilinguruma kwa sauti kubwa mara baada ya kufunikwa na mlipuko wa nishati ile isiokuwa ya kawaida na kisha kiliachiwa na Lekcha alirudi katika umbo lake la kawaida.
Roma alijikuta akishangazwa na kitu kile , Dhana hio ya Cauldron ilikuwa imeunganishwa na nguvu zake na kama kikipigwa na kuathirika na yeye alikuwa akiumia.
Kilichomshangaa Roma ni mara baada ya roho ile ya mnyama kujificha mara baada ya kuachiliwa na nguvu ya nishati ya ant- matter na hii ilimaanisha kwamba Lekcha alikuwa na nguvu kubwa kiasi kwamba Dhana hio imekuwa sio tishio kwake tena.
“Unashangaa nini wewe ndio unaefuatia baada ya kuharibi chungu chako”Aliongea Lekcha.
Ilikuwa ni muda uleule Lekcha alitengeneza ngome ya nishati ya Ant- Matter na kuifanya iwe ni kama gunia na kutaka kumfunika nalo Roma.
Roma alishangazwa, nishati ile nyingi haikumtoka Lekcha bali ilikuwa ni kama vile ameitengeneza katika mazingira , yaani likuwa ni kama vile yeye alivyokuwa na uwezo wa kukusanya nishati za mbingu na ardhi ndio alichokifanya Lekcha.
“Nenda kuzimu mshenzi wewe”
Lekcha aliongea kwa sauti na palepale lile boma la nishati alilotengeza lilipuka na kuwa kama vile ni fataki na zile cheche zote kumvaa Roma huku zikiwa zimechanganyika na nguvu nyingine ambayo Roma hakuweza kuitambua lakini ambayo ni hatarishi.
Lekcha alikuwa akibweka kama vile alikuwa kwenye maumivu , chuki yake yote ya zaidi ya miaka aliokuwa nayo zidi ya Roma alionekana aliiwekeza katika ngurumo aliokuwa akitoa
Muonekano wake ulikuwa umebadilika kabisa na kuwa kama mtu mwingine na alionekana kabisa alikuwa akipambana kwa ajili ya kulipa kisasi.
Yaani ile hamasa aliokuwa nayo wakati akipambana na Aoiline ilikuwa ni tofauti wakati huo alivyokuwa akipambana na Roma.
Roma hakutaka kuwa mzembe , aliamua kukiongezea nguvu chungu chake na kisha akakipa kazi ya kunyonya nishati ile ya Ant Matter ili kuipunguza nguvu isimdhuru kwa kiasi kikubwa.
Lakini hata hivyo hakikuweza kuimeza yote na pale ilipomwangukia ilimfanya kujihisi ni kama vile anashambuliwa na nyuki.
Maumivu aliokuwa akihisi hapo yalikuwa ni mara mbili na yale ambayo aliyahisi wakati akiwa ndani ya kizimba cha Dhana ya mafuvu na misumari tisa ya Joka.
Katika hali hio ya kupambana na nguvu kubwa hata ule ugonjwa wake ni kama vile umeshituka kiasi cha kufanya macho yake kuanza kubadilika rangi na kuwa ya kijani..
“Arghh…!!”
Roma alitoa mguno mkubwa mno huku mishipa yake ya damu ni kaa vile inataka kumpasuka na mwili wake ulionyesha hali ya kutaka kupitia mabadiliko , ilionyesha ni dhahiri virusi ambavyo vilikuwa vimelala kwenye mwili wake viilitaka kuamka na kumfanya kuwa jitu.
Lakiini hata hivyo lilikuwa shambulizi dogo sana la kuweza kummaliza Roma kwani maumivu yale ni kama vile yalimfungua ubongo na kujikuta akiingiwa na utashi wa kutaka kufanya shambulizi kubwa zaidi.
“Radiii…!!
Roma alibweka na palepale kimbuka cha nishati ya nguvu ya mbingu na ardhi kilijikusanya juu na kugeuka kuwa moto wa zambarau na wa bluu na mara baada ya kuunganika tu radi ilimshukia Lekcha kutoka pande zote na kuanza kupambana na ile nishati ya Ant- Matter.
Roma nguo hakuwa nazo tena kwenye mwili wake na alikuwa yupo uchi kabisa na mwili wake ni kama vile unapigwa na shoti ya radi kwani ulikuwa ukitetema sio mchezo.
Wakati radi ikishambuliana na nishati ile ya nguvu isiokuwa maada Roma alishuka chini kama vile ni kimondo na mara baada ya kujipigiza chini aliweza kutengenza wimbi kubwa mno la nishati ya nguvu za kijini liloambanta na nguvu ya radi na kumshambulia Lekcha kwa chini.
Roma hakuishia palepale alifyatuka kama mshale huku akiwa amekunja ngumi na kumsogelea Lekcha kwa kasi na kumchapa ngumi ya kichwa iliokuwa na uzito wa tani nyingi mno.
“Pfff!!”
Lekcha alijikuta akipokea mashambulizi matatu kwa wakati mmoja na kufanya nguvu yake ya nishati ya anti-matter kusambaratika lakini wakati uleule ikiyeyushwa na shoti za radi.
Roma mpango wake ulikuwa mwepesi , alijua nishati ya Lekcha ilikuwa na kikomo na kwasababu dunia ki asili ni maada basi uwezo wa Lekcha kuidhibiti nguvu hio ilimhitaji uwezo mkubwa hivyo alimshambulia Lekcha kwa kasi kusambaratisha nguvu zake huku akitumia shoti za umeme wa radi kuziyeyusha ili zismrudie.
Mashambulizi yale ya haraka yalimfanya Aoiline aliekuwa akiangalia kwa mbali kuwa katika hali ya kutokuamini kile alichokuwa akiona.
Alikuwa ni jini wa uwezo wa juu sana ambaye alishawahi kuwepo na alikuwa ameona vitu vingi na mbinu nyingi ambazo majini wanazotumia lakini havikumshangaza , lakini upande wa Roma kila alichokuwa akifanya kilikuwa kipya kwake na kumfanya kushangaa.
Unachopaswa kuelewa hata ukiwa ndani ya mnara huo bado sheria za ulimwengu wa mapeppo zilikuwa zikitumika hapo hivyo kufanya uwezo wake kuwa wa chini , lakini sasa kama kwa nusu ya uwezo wake aliweza kupigana na Lekcha kwa mwaka mzima lakini hakufanya shambulizi kubwa kama ambalo Roma amefanya bali alimuona ameimarika nje ya matarajio yake.
Hivyo kimahesabu ni kwamba Roma na yeye alikuwa akitumia nusu ya uwezo wake na moja kwa moja aliona lazima Roma atakuwa amemuacha mbali sana hata kama akitoka katika ulimwengu wa kawaida na kurudiwa na uwezo wake wote.
Mbaya zaidi alichoona ni kwamba Roma anaonekana uwezo wake huongezeka kila ndani ya dakika.
“Huyu kijana ubora na utimamu wa kimwili unafaida kubwa kwake, kautoa wapi huo mwili?”Alijiwazia.
Aoiline aliamini mwili wa Roma ndio chanzo cha kuweza kufunikiwa kwa muda mfupi na alimfananisha na ukoo wa majini joka wa zama zile.
Kadri ambavyo Roma hakuwa akimpa nafasi Lekcha kujikusanya ndio ambavyo alikuwa akizidi kupoteza nishati yake ya Ant- Matter na ilichukua muda mfupi ilionekana Lekcha alibakiwa na nguvu kidogo sana.
Nishati ya Ant matter inaweza kuwa na nguvu lakini ni ghali sana , hii inamaanisha kwamba ni muda mwingi sana unahitajika kwa ajili ya kuikusanya tofauti na nishati ya mbingu na ardhi ambayo mara nyingi haina kikomo ili mradi tu ubongo wako unafanya kazi vizuri, hasara kubwa ya nishati hio ni kwamba asili yake sio ya kidunia hivyo huharibika kwa kasi.
Lakini sasa wakati Roma akiwa na mawazo kwamba amemzimisha Lekcha mpaka kuwa dhaifu Lekcha alirudi katika umbo la kawaida na kumfanya Roma amuone ni kama ndoto ambayo hawezi kuifuta.
Lekcha mara baada ya kurudi katika umbo la mfanano wa kibinadamu alianza kukunja shingo yake kama vile anaweka mwili sawa kana kwamba anamwambia Roma pigo zako ni za kitoto.
“Vipi tena bwana mdogo Roma Ramoni A.k. a Hades dhaifu, hicho ndio ambacho unaweza kujivunia , hii radi yako inaonekana kuwa na nguvu kweli lakini athari zake kwangu ni ndogo”Aliongea Lekcha huku akitoa tabasamu la uovu.
Roma moyo wake ulisinyaa , alidhania akitumia mahesabu ya kikanuni ya nishati ya nguvu hio anaweza kummaliza Lekcha kwa kumshambulia bila kukoma kwa kasi lakini ilionekana kuna kitu ambacho hakukitambua kutoka kwa Lekcha.
“Roma usichokijua na wasichokijua wanasayansi ni kwamba wakati wa nishati ya matter na anti matter zinapogongana hakutokei kitu kinachoitwa Annihilation kama wanavyoamini bali asilimia mia moja kunatokea nishati nyingine yenye tabia tofauti , nishati hii ndio ilionifanya uwezo wangu kuimarika maradufu kadri nilivyokuwa nikipambana na yule Mbweha , bomu la nyuklia ambalo hutengenezwa kwa kurutubisha viini vya atomu ni sawa na asilimia moja tu ya nishati inayotokea wakati wa kugongana kwa nishati hizi mbili , hivyo ninao uwezo wa kuharibu kisiwa kwa kukadiria tu uwezo nishati ninayotaka itokee , sasa hebu jiulize gunduzi yangu hii ndio nataka kuiajaribisha kwako”
Aliongea Lekcha na palepale alitengeneza kitenesi cha nguvu ya nishati ya Ant-Matter na kukirusha aliposimama Roma kwa kasi.
Roma alitaka kutumia Chaos Cauldron kuweza kukijikinga na shambulizi lile lakini Chaos alionyesha hali ya kunywea kutokana na ukubwa wa shambulizi lile.
Roma alijikuta akikosa chaguo lingine na kung’ata meno yake kwa hasira na kisha palepale kwa spidi ya haraka sana alichoropoa lile Shoka kutoka katika hifadhi yake ya pete.
Inasemekana katika ulimwengu wa majini kulikuwa na Dhana kumi na saba ambazo zilikuwa na nguvu sana enzi hizo na kati ya Dhana hizo ni Shoka hilo la Pangea ambalo halikueleweka namna linavyofanya kazi , kuna tetesi kwamba linaweza kuingia katika shimo jeusi la anga na kutoka.
Kitu kingine ni kwamba nguvu yake pia ni kama ilivyokuwa kwa Cauldron, shoka hilo linaonyesha uwezo wake kulingana na uwezo wa mtumiaji. Lakini kitu cha uhakika ni kwamba Shoka hilo lilikuwa na uwezo wa kuchana anga na kwenda kinyume na kanuni za anga.
Katika kanuni za kifizikia kutoka kwa mgunduzi Einstein anasema anga ni kama kitambaa, ijapokuwa hakumaanisha kitambaa kama kitambaa lakini ndio namna rahisi ya kuelewa kwamba anga linaweza kuharibika kikanuni.
Sasa Shoka hilo lilikuwa na uwezo wakuchana hiko kitambaa ambacho ni kama anga sasa kwa kukiuka sheria za anga.
Unaweza kushangaa hizi Dhana zinafanyake kazi lakini teknolojia ambayo ipo nyuma yake ni nje ya uelewa wa fahamu za kibinadamu na hata viumbe wenye akili sana kama majini na hata miungu hawakuwa wakijua siri iliopo nyuma ya uhunzi wa Dhana hizo..
Chukulia mfano safu ya ulinzi ya gereza la Roho katika miliki ya Hongmeng mpaka wakati huo sio Athena wala kiumbe chochote aliweza kujua teknojia ya safu hizo za ulinzi zinafanyaje kazi.
Hivyo hata kwa Roma mwenyewe hakuwa akijua namna Dhana hizo zilivyotengenezwa alichokuwa akijua ni namna ya kutumia tu.
Sasa Roma aliamini kwasababu kanuni za anga hazikufanya kazi vizuri katika ulimwengu huo kutumia Shoka hilo ambalo linaenda kinyume na kila sheria ya asili ndio tumaini pekee la kuhimili nguvu ya Ant- matter.
Kitendo cha Shoka lile kutua katika mkono wa Roma na kuliingizia nguvu za kijini lilibadilika palepale muonekano wake na zile herufi ambazo zilikuwa zimechorwa katika Shoka hilo ziling’aa.
Ijapokuwa lilionekana kama shoka la kawaida lakini uzito wake haukuwa wa kawaida na pengine hata Rose ambaye yupo mwishoni mwa levo ya Nafsi asingeweza kulishika mkononi.
Kwa namna ambavyo liliamshwa na nguvu za mbingu na ardhi za Roma ilikuwa ni kama vile shoka hilo lilikuwa likitawaliwa na nafsi lakini ukweli ni kwamba hakukuwa na nafsi yoyote , ilikuwa ni kama kifaa tu ambacho kimelala na muda huo kimepata nishati na kuingia katika matumizi.
Roma hata yeye ndio inakuwa mara yake ya kwanza kujaribisha shoka hilo na kitendo cha kuamka kwake ile sehemu aliosimama ni kama vile upepo unakimbia , msisimko ulioweza kutoka ilikuwa ni kama vile kiumbe mwenye nguvu sizizokuwa za kawaida anawavamia.
“Arghh…!!!”
Roma alipiga yowe na kwa kutumia nguvu zake zote za kijini aliinua lile shoka juu na kisha akalipigiza chini ndani ya sekunde.
BOOM
Wimbi la nguvu iliotokana na shoka hilo ilikuwa ni kama vile inakwenda kutenganisha mlima wa gereza la nafsi za giza na kuziachia.
Shambulizi lile la Lekcha mara baada ya kugongana na msisimko wa nguvu ya lile shoka mwanga wake ulibadilika katika rangi zisizokuwa zikihesabika na shambulizi lake nikama vile limetumbukia kwenye shimo.
Aoiline ambaye alikuwa mbali aliweza kuhisi msisimko usiokuwa kawaida kutoka kwa nguvu ya nishati ya Ant-matter iliotengenezwa na Lekcha , aliamini kama Lekcha angetumia shambulizi hilo kumshambulia basi angepatwa na majeraha makubwa mno, lakini sasa alishangaa pale Roma akitoa kitu kilichomwacha mdomo wazi.
Licha ya kwamba aliishi miaka mingi hakutegemea kuona Roma angeweza kumiliki kitu cha ajabu kama hicho , alikuwa akisikia kuhusu shoka hilo lakini hakuwahi kuona katika uhalisia.
Unajua bwana majini wengi wana historia kama ilivyokwa binadamu lakini utofauti wa majini na binadamu ni kwamba majini wa zamani walikuwa na akili nyingi sana na kufanya vitu vya ajabu kuliko hawa wa sasa lakini kwa sisi binadamu uwezo wetu wa akili unaongezeka kulingana na muda.
Yaani wakati binadamu akiendeea kutafuta siri za dunia kwa kupanua uwezo wa kufikiria upande wa majini wao wanataka kufikia levo za kufikiria za watangulizi wao.
Sasa katika vitabu vya kihistoria vya majini walikuwa wakisoma uwepo wa Dhana kumi na saba na kati ya Dhana hizo ni Chaos Cauldron , Shoka la kipangea , kioo cha nafsi, Fimbo ya muujiza na zinginezo lakini licha ya kuishi miaka mingi sana hakuwahi kushuhudia hizo Dhana.
Sasa alijjiuliza Roma amewezaje kumiliki Dhana mbili kati ya Dhana kumi na saba za kihistoria. Alijiambia huyu mtoto katoa wapi vitu hivyo.
Lakini licha ya kuwa kwenye mshangao hakuonyesha hali ya kufurahi mara baada ya kuona nguvu halisi ya shoka hilo , hakujali nguvu yake itauathiri vipi mnara lakini alitaka kuona matokeo tu.
Ile sehemu ambayo amesimama Roma kulionekana hali ambayo haikuwa ikielezeka ilikuwa ni kama vile kataratasi ya nailoni linaungua katikati na kutengeneza ufa katikati.
Roma mwenyewe alishangazwa na kitu kile na palepale wazo lilimwingia na kuhamaki na kujiambia kwahio kuchanika kwa anga ndio kupo hivi.
Roma alishangazwa na jambo hio radi yake ilikuwa ikileta machafuko lakini shoka hilo ilionekana ni kweli ilikuwa ikiharibu anga na kumfanya yeye kuwa kati , yaani ni kama lile shoka linaharibu anga na wakati huo huo kunatengenezeka anga lingine jipya ambalo ndio anaonekana yupo yeye sasa.
Roma alijua kabisa anga la ulimwengu huo sio ‘Parallel dimension’ kama ilivyokuwa kwa ulimwengu wa majini watu, bali ni tofauti kabisa ndio maana ukiwa katika huo ulimwengu huwezi kufanya mawasiliano kwa namna yoyote ile na ulimwengu wa kawaida, pili kanuni zake za anga hufanya kazi kitofauti.
Kama anga la uimwengu huo lilikuwa la kawaida basi majini hao wasingeweza kufungiwa kirahisi hivyo.
Moja kwa mmoja ilimaanisha kwamba Shoka hilo lilikuwa na sheria zake za ufanyaji kazi.
Kuna kitu kilikuwa kikimwambia kuna uwezekano wa Roma kubadilisha utendaji kazi wa ulimwengu huo kwa kutumia hilo shoka , ikimaanisha kwamba ameshikilia ufunguo ambao unaweza kuruhusu njia ya kutokea.
Yaani ni kama ilivyokuwa kwa mfalme Wuja mkuu wa majoka kutengeneza Dhana ambayo itakuwa na uwezo wa kutengeneza njia ya kutokea ulimwengu wa kawaida ndio ambavyo Roma alihisi uwezo wa shoka lake ulivyo.
Shambulizi ambalo Lekcha aliamini kwamba linaweza kuharibu kisiwa lilisambatatishwa na Sururu la Roma na moja kwa moja alijihisi kukasirika mno kwani hakutegemea hilo.
“Haiwezekani… Hadae nasema haiwezekani ukapangua shambulizi langu namna nyepesi hivyo”
Lekcha aling’aa meno yake kwa hasira, nguvu yake ya nishati ambayo ilikuwa kama dhoruba baharini ilijikusanya upya katika mkono wake na kwa mara nyingine alijaribu kumshambulia Roma.
Roma baada ya kuona utukufu wa shoka lake hali ya kujiamini iliongezeka na kujiambia yes ni muda wa majaribio na palepale alifyeka anga na shoka lake kutengenza wimbi lingine la mchaniko uelekeo wa shambulizi la Lekcha.
Shambulizi la Lekcha lilikuwa kubwa kweli lakini shoka lile liliteneneza hali ya kuyumba kwa anga hivyo kufanya shambulizi lake kusambaratika , kwa bahati nzuri ni kwamba anga lina nguvu ya kinishati kubwa sana hivyo hata kama shoka hilo lilikuwa na uwezo wa kubadilisha utedaji kazi wa kawaida wa anga ilikuwa ni eneo dogo tu hivyo athari zake zilikuwa katika mzingo mdogo na pia ile sehemu ambayo huonekana kuharibika inarudi upya kwa kasi.
Lekcha alikasirika mno mara baada ya kuona ana mashambulizi yenye nguvu lakini bado hakuweza kumfanya chochote Roma kutokana na shoka lake na aliamua kupotezea kila kitu na kuanza kukusanya kiwango kikubwa cha nishati ya ant matter.
Roma alijua Lekcha yupo katika hali ambayo ni ngumu kumuua , alikuwa ni kama nishati na ili kumaliza lazima kuyeyusha nishati yake hivyo alitumia Chungu , radi na shoka kushambulia kwa wakati mmoja.
Wakati huo ni kama Cauldron imeweza kutambua uwepo wa shoka na hali ya roho ile ya mnyama kujiamini ilirudi.
Wakati huo sasa katika floor hio ukiangalia kwa juu ni kama vile kuna nishati mbili ambazo zilikuwa zikivamiana huku watu waliokuwa wakidhalisha nishati hizo hawaonekani.
Aoiline aliekuwa akiangalia pambano hilo uwezo wake ulikuwa umerudi lakini hata hivyo hakutaka kuingilia.
Sio kwamba hakutaka lakini nguvu ya kimauaji iliokuwa ikimtoka Roma ilimfanya kuona kabisa hana haja ya kuingilia.
Lakini hata hivyo Roma asingependa maana katika maisha yake hakupenda kumtumia mwanamke kama chombo cha mafanikio yake ndio maana tokea amuache Aoiline ndani ya mnara huo roho iikuwa ikimsuta.
Kadri Roma alivyokuwa akishindana na nguvu ile ya Ant-Matter ni kama vile kichwa chake kinakuwa kizito mno kiasi kwamba ule ugonjwa uliokuwa umempotea ulianza kurudi kwa kasi na kufanya macho yake kuwaka taa nyekundu.
Ilikuwa ni kama vile ile nishati ya Ant- matter inashitua hali flani ya utendaji wa mwili wake.





SEHEMU YA 768.
Wakati huo huo vita hio ikiendela katika ngome ya makao makuu ya kambi ya kitafiti ya Zeros organisation alionekana Madam Dyana akiwa na tabasamu la aina yake usoni huku akiangaia kitu kwenye skrini , ilikuwa ni kama vile alitamani kuona kitu cha namna hio kwa muda mrefu.
Dyana ni mwanamama ambae ni Chief wa kitengo cha usimamizi wa maendeleo ya mpango LADO yaani idara ya PLMC.
Kitengo hicho kwa muda mrefu sana kilikuwa kimya sana na hakukuwa na dalili yoyote ya taarifa kutoka kwa ajent wao na hata wale wanasayansi ambao walikuwa wakihusika walikuwa wakilala tu muda mwingi lakini siku hio ilionekana kuwa tofauti katika miezi mingi.
Licha ya kwamba ulimwengu ulikuwa katika hali ya sinfofahamu lakini kazi zilikuwa zikiendelea kawaida ndani ya kambi hio na ukweli ni kwamba ubize ulikuwa umeongezeka kwa kiwango kikubwa sana.
Sasa ni miezi kadhaa tokea Dyana kupokea maagizo kutoka kwa mheshimiwa Barack Mabo.
Unajua katika jumuia yoyote ambayo inahusisha viumbe binadamu lazima kuna wale ambao wana mtazamo tofauti na hio ilionekana ndani ya umoja wa Zeros organisation.
Inaaminika kwamba Barack Mambo ndio moja ya wanachma wa vyeo vikubwa ndani ya jumuia hio ya siri tena akiwa mkuu chini ya The First Black lakini ndio mtu pekee ambaye alikuwa na mawazo tofauti na malengo ya Zeros.
Mpango LADO ni mpango ambao una sahihi yake na sio kwake tu karibia kwa maraisi wote waliopitia katika nyumba nyeupe mpango huo hujumuishwa katika viapo vyao ili kuulinda na kuudumisha.
Ki uhalisia haukuwa mpango mbaya kwani malengo yake yalikuwa wazi , malengo ya mpango LADO hayakuwa kwa ajili ya kumtengeneza ajent mwenye nguvu pekee lakini ukweli ni kwamba ni mpango ambao uliundwa kwa ajili ya kupata binadamu mwenye DNA tofauti, yaani kwa lugha nyepesi kilichokuwa kikilengwa ni kutengeneza kizazi kipya.
Illuminat ndio jamii ambayo ‘ideology’ yake imepewa kipaumbele katika zeros organisation kuliko jamii yoyote ile , waliamini ili dunia izidi kuwa salama kuelimika kwa binadamu lazima kuendane na kasi ya muda na ili hilo kufanikiwa lazima kuwepo binadamu wenye uwezo tofauti wa kufikiria na huo ndio utakuwa mwanzo wa gunduzi mpya tofauti na mwendelezo wa teknolojia zilizopo.
Upande wa Ant-Illuminat wao umoja wao ulianzishwa kupinga ‘ideology’ za Illuminat kwamba ii dunia iendelee kuwa salama maendeleo ya teknolojia yanatakiwa kuendelea katika spidi sawa na ukuaji wa kifikra wa kibinadamu , yaani kusiwe na ‘hacking’ ya aina yoyote ile ya kujaribu kuharakisha ukuaji wa kufikiria kwa binadamu.
Sasa Barack Mabo katika mawazo hayo mawili yeye ni vuguvugu, ikimaanisha kwamba nusu anakubali ajenda za illuminat na nusu anakubali ajenda za Ant-Illuminat na hili ndio ilimfanya kujikuta kuwa na mawazo tofauti.
Kati ya watu ambao anafanana nao kimawazo ni Dyana mwanamama ambaye ndio aliepewa jukumu la usimamizi wa maendeleo ya mpango LADO.
Sasa ni miezi kadhaa tokea yatokee mabadiliko ya hali ya hewa duniani , moja ya watu ambao hawakuwa na utulivu na kile kilichokuwa kikiendelea alikuwa ni yeye.
Na wasiwasi ulimfanya kufanya vikao vingi sana na wadau wengi kuzungumzia kile kinachoendelea na nia halisi ya viumbe hao kutoka sayari nyingne zidi ya binadamu.
Ijapokuwa ni kweli Athena aliwahakikishia kwamba ili kuibadilisha dunia kutoka katika hali ya sasa ya Dystopia na kwenda kuwa ulimwengu wa Utopia kuna kafara itahitajika lakini bado haikutosha kumuamini moja kwa moja na kutokufanya chochote au kutokuchukua tahadhari.
Ieleweke kwamba Athena licha ya kuanzisha umoja huo hakuwahi kujionyesha hadharani na hata pale alipokuwa akijionyesha ni katika hali ya kuogofya pengine hii iliwafanya watu kuwa na imani dhaifu juu ya mipango yake.
Ukweli ni kwamba hakuanzisha Zeros kwa njia ya moja kwa moja bali ni binadamu wenyewe ambao walitoa pendekezo na yeye akaingiza ushawishi wake na mwisho wa siku ikaonekana ni kama yeye alieanzisha.
Sasa Barack Mabo na wanachama wengine walikuwa katika vikao vya kila siku na ajenda kubwa iliokuwa ikizungumziwa katika vikao hivyo ni kufumbua fumbo gumu ambalo Athena amelitega.
Fumbo lenyewe ni kwamba kama Athena alikuwa na nguvu kubwa kwanini akataka mpango LADO kufanikiwa kwa silimia mia moja na kumfanya Roma kuendelea kuwa na nguvu kila uchao.
Yaani viongozi hao na wanasayansi hao waliona kabisa hakukuwa na uhusiano wowote uliopo kati ya mipango ya Athena na kupanda madaraja ya ki uwezo kwa ajent Thirteen.
Athena aliwaambia kufanikiwa kwa Roma ni kwa ajili ya kutengeneza uzao mpya , binadamu ambaye atakuwa na uwezo wa kufikiria tofauti lakini kwanini inaonekana ni kama vile Athena anataka kuua binadamu wote.
Yamkini ni kwamba binadamu hao ambao wanajiita ndio watu waliokuwa karibu na mwishoni mwa piramidi la uongozi wa dunia walikosa majibu , walikosa majibu kutokana na kwamba waliekuwa wakimuuliza maswali hakuwepo na hakujisumbua hata kujitokeza kwao.
Walijikuta kama vile ni viumbe ambavvyo vimetelekezwa kwani hali ya dunia ilizidi kuwa mbaya lakini hakukuwa na majibu kwamba hali hio ingedumu kwa muda gani na matokeo yake ni nini ,walijuliza je hali hio ndio dunia ambayo Athena anataka kutengeneza lakini kimahesabu wanaonna hakuna namna Athena akawa na nia nzuri kwa binadamu.
Mwisho wa maamuzi ya vikao ndio wengine wanashauri kujengwa kwa Safina kuokoa binadamu asipotee , huku kundi la watu wakipinga pendekezo hilo na kutaka kushindana na miungu.
Moja ya watu ambao waliona kujenga Safina sio suruhu ni mstaafu Barack Mabo na kutokana na kuwa na mawazo ya tofauti aliamini mtu mmoja pekee ambaye anaweza kutatua kitendawili kilichokuwa kikiwasumbua wengi ni Hades pekee kwani alikuwa ni nusu binadamu na nusu viumbe hao.
Sasa ule wakati ambao walikuwa wakitamani Roma aingilie kati ndio wakati ambao Roma ametoweka ghafla tu na asijiulikane alipo.
Ni muda wa mchana usiokuwa na jua nchini Marekani , licha ya kwamba dunia ilikuwa katika hali ya baridi kali lakini baadhi ya raia waliokuwa wakijiweza kiuchumi hawakuwa na hali mbaya.
“Dyana nipe ripoti , naamini simu hii sio ya bure kuna matokeo chanya?”Aliongea Raisi Barack Mabo akiwa nyumbani kwake na hio ni mara baada ya simu yake kuita na kupokea kwa haraka haraka.
“Ndio mheshimiwa tumeweza kupata dalili ya mabadiliko ya kimwili ya Ajent 13 na taarifa zimeingia katika mfumo wetu dakika chache zilizopita”
“Nini! Dyana unamaanisha mmepata Hades?”
“Mheshimiwa tokea tuanze kutafuta taarifa za Hades alikopotelea ni leo tu mifumo yetu imeonyesha uhai , vijana walikuwa macho kutokokosa hata viashiria kidogo ndani ya mfumo na juhudi zao za kuwa macho leo hii zimezaa matunda, inaonekana Hades yupo katika hali ya mapambano makali na signal za sayansi ya Devine light zimetuma taarifa hatujui kwa uhakika ni nini kinaendeea na katika lango lipi la anga lakini ni dalili nzuri”Aliongea Dyana na Mheshiimiwa Barack Mabo alionekana kuonyesha hali ya mabadiliko kidogo katika wasiwasi wake.
“Dyana nataka kujua kama Hades anaweza kurudi?”
“Mheshimiwa ili mradi yupo hai naamini atarudi , ndio tegemeo letu kwasasa kujibu maswali ya kinachoendelea, Barrack mpaka sasa umeshindwa kuwaamini watu wa Vatican?”
“Sio kama siwaamini lakini wamekuwa ni watu wa njama sana na mitego , wanasema kuna unabii unaopaswa kutimia ndio maana hawachukui hatua yoyote lakini mpaka leo hii hawatupi maelezo”Aliongea na kumfanya Dyana kutulia.
“China na Japani msimamo wao upoje , nasikia hawakushiriki katika vkao vyote vya kimataifa vya dharula lakini walikuhitaji kama mjumbe wao”Aliongea na kumfanya Barrack Mabo kukumbuka namna alivyofuatilia kikao cha viongozi wa China.
*****
Wiki kadhaa ndani ya Zhongnahai Beijing kulikuwa na kikao kizito ambacho kilihusisha viongozi wote wa juu wa taifa hilo na wale wastaafu waandamizi(Country senior’s).
Kiongozi mkuu namba moja mwandamizi ndio ambaye alikuwa akiongoza kikao hicho , pembeni yake kulikuwa na viongozi akiwemo Li Moshen waziri wa ulinzi , YangChen mkuu wa majeshi , Cai Yuncheng mkuu wa kikosi cha wachawi na Ning Guanyao ambaye ni waziri mkuu hao ni baadhi tu.
Katika watu waliokuwa na wasiwasi ndani ya kikao hicho ni Cain Yuncheng huyu ndie ambaye ni kama anahusika na utendaji wa Hongmeng katika ulimwengu wa kawaida na wasiwasi wake ni kwamba Hongmeng inaweza kukosa nguvu kutokana na kwamba Anjiu mkuu wa miliki ya Xia alikuwa akiwashambulia.
Ijapokuwa baridi ilikuwa kali sana ndani ya taifa hilo lakini China ni moja ya nchi ambazo zina hakiba kubwa ya chakula lakini pia limeeendelea katika urahisishaji wa social service delivery kwa raia wake.
Yaani haikuwa na haja kwa raia kutoka nje kwa ajili ya kwenda sokoni wala dukani bali teknolojia ilirahisisha kazi hio hivyo kufanya nchi hio yenye watu wengi zaidi duniani kwa mara ya kwanza kuonekana kama vile haina watu.
Bila shaka sio kwamba watu wote hawakutoka , kuna wafanyakazi walitoka lakini ilikuwa kwa tahadhari maalumu na hata wale wenye vipato kidogo walikuwa wakisaidiwa.
Baada ya kimya kirefu cha mkuu wa nchi hio hatimae alianza kuongea.
“Hatuwezi kuendelea kukalia mikono yetu zaidi , kwanzia sasa tutajitegemea sisi wenyewe na sio wengine”Aliongea lakini hakuna ambaye aliongea kwani wote walikuwa kimya wakimwangalia , licha ya kwamba dunia ilikuwa katika hali isiokuwa ya kawaida lakini tabasamu halikumtoka.
“Kutokana na janga hili linaloendelea nchi yetu yote na hata kwa binadamu tunapitia changamoto , kama unachochote cha kuongea waziri Ning tafadhari sema, kwanini upo kimya sana siku hizi?”
“Mheshimiwa ulimwengu wa majini sasa hivi upo kwenye machafuko kutokana na vita inayoendelea , miliki ya Xia kwa kutumia watu wao ambao wamefikia levo ya radi wanajaribu kuvamia miliki nyingine , ikumbukwe Xia ipo ndani ya bara la Asia na kwa muda mwingi wamekuwa na wivu na Hongmeng , je uhakika tunao kama wakiiteka Hongmeng hawatotaka kuchukua nafasi yao na kuingilia maswala yetu?”
“Usiwe na wasiwasi , hawawezi”Alijibu Raisi na kisha akaendelea.
“Ijapokuwa miliki ya Xia imepanda na kuwa na nguvu ndani ya ulimwengu wa majini kuliko miliki zote , kutumia nguvu zao kutaka kuingilia maswala ya ulimwengu wa kawaida hakutowasaidia chochote , zaidi ya kujiingiza hatarini kwa kuwachokoza wajumbe wa muungano wa ulinzi wa dunia na ulimwengu wao,sidhani wanaweza kuwa wajinga hivyo”
Mara baada ya kutajwa wajumbe wa ulinzi wa umoja kila mmoja alionyesha hali ya msisimko.
Haikuwa kwa majini tu ambao walikuwa wakijua uwepo wa umoja wa ulinzi wa dunia , ukweli ni kwamba historia hio haijawahi kufutika katika uso wa dunia tokea siku ambayo viumbe kutoka sayari nyingine kutua duniani.
Ni wajumbe hao hao wa umoja ndio waliohusika na ambao waliendelea kushikilia ulinzi wa usalama wa dunia.
Katika hali kama hio ya dunia kuwa hatarini na vilevile kupotea kwa Roma kitu pekee ambacho binadamu wenye kuelewa siri ya uwepo wa wajumbe hao waliomba waingilie kati.
Walinzi wa dunia au The Guardians jukumu lao kubwa ni kuhakikisha dunia inaendelea kuwa salama na wajumbe hao wa ki’umoja hawakujali maswala ya nchi na nchi , ukweli ni kwamba hawakujihangaisha na maswala ya kiserikali ya kibinadamu wala majini.
Hawajali Israeli kumvamia Mpalestina wala Mchina kumvatia Mtaiwani au Mrusi kumvamia Ukraine , ajenda yao kuu ni kulinda uwiano wa usalama wa kidunia hii ikimaanisha katika malango yote ya dunia , iwe ni ulimwengu wa kawaida ama ulimwengu wa ajini pepo au ulimwengu wa majini watu lakini vilevile kuzuia jamii moja ya viumbe kushambulia viumbe wengine.
Majini wa Panas , walitakiwa kubakia Panas na majini wa Xia walitakiwa kubakia Xia na kama wataamua kushambuliana wao kwa wao hakuna tatizo lakini kama watashambulia binadamu na kutaka kuteka nchi ndio tatizo hutokea ambalo lilipaswa wajumbe hao kuingilia.
Lakini kilichokuwa kikiwasumbua sio serikali ya China tu bali serikali zote ambazo ziikuwa zikijua historia ya uwepo wa watu hao ambao haikueleweka ni majini , binadamu au malaika ni kwamba hawajui walikuwa na ajenda gani na pili hawafahamika kwa sura ni wakina nani na wanatokea nchi gani au wanaishi nchi gani.
Inasemekana ni matiafa makubwa duniani tu ambao wameweza kukutana na mmoja ya wajumbe hao yaani Mkuu namba moja na mara nyingi alijitokeza kwao kwa ajili ya kutoa onyo tu na haikuwa vinginevyo.
Nchi pekee ambayo ni ndogo na mkuu namba moja alijitokeza kwa kiongozi wake ni Rwanda tu na hio yote ni kutokana na Jeremy kushikirikiana na miliki ya Panas kutaka kuingilia maswala ya kibinadamu,
Mtu binafsi tu ambaye aliweza kukutana na mkuu namba moja ambaye huunda baraza la usalama wa ulimwengu ni Roma pekee.
Ki ufupi ni kwamba Master Namba moja mwenyewe alikuwa na nguvu sana kiasi kwamba alikuwa na uwezo wa kukutana na raisi wa Urusi kwa kutumia sura ya Singanojr na vilevile akakutana na raisi wa Korea Kaskazini kwa sura ya mtu mwingine , ili mradi amefikisha ujumbe haikujalisha ni sura ya nani inatumika.
Sasa Raisi wa China na baadhi ya watu tofauti tofauti ndio walijua siri hio ya uwepo wa hivyo viumbe lakini hawakujua ni wakati gani watachukua hatua hivyo tofauti na kusubiri waendelee kuteseka ni bora kujitegemea wao kwa wao.
Wakati kikao hicho kikiendelea upande mwingine Raisi Barack Mabo alikuwa akifatilia kila kitu, ni kama alipewa ruhusa ya kuangalia namna kikao hicho kinavyoendelea.
Ukweli ni kwamba Raisi Barak Mabo alikuwa akiamini kwamba wajumbe hao wa ulinzi wa dunia walikuwa na mawasiiano na taifa la China na hio yote ni kutokana na uwepo wa Hongmeng lakini matokeo yake ni kwamba hata raisi mwenyewe wa China hakuwa na mawasiliano nao lakini licha ya hivyo Barack Mabo hakumuamini na ndio maana mheshimiwa alimpa nafasi ya kuangalia kikao chake na vongozi wake waandamizi ili aweze kuamini maneno yake.
“Mheshimiwa dunia nzima ipo katika hili janga la baridi na miungu wanaendelea kutukandamiza , Hongmeng ambao ni tegemeo letu wenyewe wapo na matatizo , je hakuna uwezekano wowote wa hawa walinzi kutusaidia ?”Aliuiza mkuu wa kikosi cha uchawi.
“Bado hamjanielewa tu nilichojaribu kuwaelezea..?”Aliongea na kisha akawaangalia mmoja mmoja na kisha alivuta pumzi na kuendelea.
“Sio mimi tu ambaye nimejaribu lakini wenzangu wengi wamejaribu lakini hakuna uwezekano wowote ambao nimeweza kuwasiliana nao”
“Kwaho hii inamaanisha hawana mpango wa kusaidia binadamu?”Aliuliza Ning.
“Hilo sijui lakini na wenyewe wana falsafa yao mpaka kuamua kuingilia maswala ya kibinadamu, pengine wanaona dunia haipo hatarini”
“Hawana lolote hao nina uhakika wanawaogopa miungu”Aliongea waziri mkuu Ning kwa hasira.
“Waziri chunga mdomo wako”Aliofokewa na mheshimiwa Raisi
“Kila kitu kinatokea kwasababu maalumu mheshimiwa waziri , mzunguko wa kimaisha unatafsiriwa kutoka kuzaliwa mpaka kufa , uwezekano wa hawa watu kuwepo ni kweli lakini haijalishi kama wapo au hawapo , hatua ambayo binadamu tumefikia haijatokana na wao , ni kwa maarifa yetu na upumbavu wetu wenyewe , dunia ilipofikia sio kwa msaada wa kiumbe chochote bali ni sisi binadamu wenyewe na ndio sisi ambao tunapaswa kuipambania kurudi katika hali yake ya kawaida”Aliongea mkuu wa majeshi.
“Mr Yang upo sahihi katika hali kama kila taifa linataka kujitegemea hatuna budi na sisi kujua namna ya kujilinda”
Kwa mheshimiwa Barack Mabo ilikuwa ni kama vile anaangalia filamu , alichokuwa akitarajia hakukipata ijapokuwa kwa namna flani alijua ni kweli kuna uwepo wa hao viumbe lakini bado hakuamini.
Na swali hata yeye kwake lilibakia je ni kweli kama inavyosadikika kwamba kuna viumbe wasiofahamika wanaojiita walinzi wa dunia kama wapo ni lini watajitokeza na ni viumbe wa namna gani.
Mpaka mwisho hakuwa na majibu na alijikuta akirudi nchini kwake akiwa mnyonge.












SEHEMU YA 768.
Ilikuwa ni vita ya wanaume wawili na ingekamilika vizuri kama mmoja kati wao angeshinda bila kuongezewa nguvu ndio maana Aoiline hakutaka kuingilia.
Vita hio ya Roma na Lekcha ilikuwa sio ya kawaida kabisa iliojaa mizungusho , kurushiana makombora ya nishati na kuoteana.
Radi ya zambarau na bluu ndani ya mnara huo ilikuwa ikipiga mara kwa mara lakini katika floor hio ya kwanza haikufika
Roma alizidi kuwa jasiri kila sekunde ilivyokuwa ikisonga na alijiua licha ya kwamba akili yake ni kama vile imetawaliwa na mdudu na kufanya macho yake kubadilika rangi mara kwa mara lakini uungu wake ulikuwa imara mno na haikuwa kama kipindi cha nyuma ambapo hakuweza kujitawala kiakili.
Roma aliweza kuhisi mwili wake ukipitia maumivu mara baada ya kupigwa na mlipuko wa nishati ya ant-matter na kuhisi kupoteza kiasi flani cha nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi lakini hata hivyo alijiponyesha kwa haraka sana.
Kwa jinsi mwili wake ulivyokuwa ukifanya kazi , illikuwa ni kama vile alikuwa na mawasiliano na kila kiungo cha mwili , hata pale seli ambazo zilikufa na kujitengeneza zingine ni kama vile alikuwa akijua kinachofanyika.
Hisia za namna hio katika wakati huo zilikuwa ni za kipekee sana na ilimfanya kuhisi ulimwengu uliokuwa mbele yake ulikuwa sio , ilikuwa ni kama vile yupo katika lango jipya la anga.
Kila kitu ambacho kilionekana kuwa halisi katika macho yake ni tofauti..
“Hahaha…”
Roma wakati akiwa anahangaika ni kama vile alipata utashi flani hivi uliomfanya kucheka na hakujua hata ni kwa namna gani alisogea na hakujali ni shambulizi gani ambalo Lekcha atampiga nalo.
Kwa wakati huo upande wa Roma vita hio haikuwa ya kifo na uhai bali furaha mpya ili ujaza moyo wake, ni kama vile alikuwa akifurahia kinachoendelea katika wakati huo.
“Mvulana mjinga huyu … anacheka nini sasa”
Hata kama uwezo wa kufikiria wa Aoiline ni mkubwa kuliko wa Roma lakini hakuweza kuelewa ni kitu cha namna gani Roma alikuwa akipitia , hakuelewa hisia zake zilikuwa zikimaanisha nini.
Baada ya muda mfupi Aoiline alikunja ndita na aliangalia juu katika sehemu walipokuwa wakipambana Lekcha na Roma.
Kipande cha anga katika eneo waliopo ni kilikuwa kikiharibika kwa kasi , kwa macho ya kawaida unaweza usione kinachoendelea lakini kwa macho ya kijini au ya kiuungu lazima uone kinachotokea na kufanya nishati ya Ant-Matter aliokuwa akizalisha Lekcha kuwa na mawasliano na ulimwengu wa nje ya mnara hhuo.
Ilikuwa ni mnara huo umetengeneza ufa ambao ulikuwa ukipitisha hewa kwa juu.
“Hii nii…”
Aoiline aliwaza lakini macho yake yalichanua kama vile alikuwa ametegemea kitu ambacho kinakwenda kutokea.
Roma ambaye alikuwa akipambana na Lekcha alikuwa akicheka kama vile ni kichaa na uso wake ulikuwa umejaa hali ya kujiamini, hali flani ya utambuzi na ukuu kama vile ni mtawala mbele ya watawaliwa.
Lekcha ambaye alikuwa akipambana na Roma alijikuta akikasirika sana mara baada ya kutumia njia zote kujaribu kumfikia Roma kimashambulizi na kushidwa , kilichompa kero zaidi moyoni ni namna ambavyo Roma hakumchukulia siriasi.
“Siwezi kushindwa , siwezi kushindwa nimetoka mbali kufika hapa siwezi kushindwa leo , lazima nikumalize leo Hades”
Lekcha alibwatuka kama vile ni kichaa lakini sauti yake ilimezwa na ngurumo ya radi kubwa sana ambayo ilisikika kutoka nje ya mnara.
BOOM!!
Ilikuwa ni sauti kubwa ya kuumiza masikio ambayo ni kama vile mnyama ananguruma katika lindi la ukiwa wa milele au kama vile ni Mungu anafungua makufuli ya mateso k wa viumbe wake binadamu.
Ilikuwa ni ngurumo ambayo haikuwa ya kawaida , ambayo kwa haraka haraka haikuwa na asili ya mnara huo na kufanya waliokuwa wamesikia ni kama vile masikio yao yanasikia Kengele ya tahadhari .
Na ile sehemu ambayo walikuwa wamesimama Roma na Lekcha palikuwa na tundu ambalo limejitokeza kwa juu kupitia kwenye ule ufa ambalo lilikuwa na mawasiliano na ulimwengu wa nje.
“Hio ngurumo ya Dhiki ya mapigo elfu moja ya radi!! , Aisee huyu mtoto hazuiliki , kijana umefanikiwa vipi kuelewa haraka hivi tamaduni zetu na kupanda levo kila unapokuwa kwenye changamoto?”
Ailione ambaye alikuwa tayari amekwisha kupitia adhabu ya mapigo mengi ya radi alikuwa akijua kani ya radi ya mapigo mengi , alikuwa amepitia adhabu ya mapigo zaidi ya elfu moja hivyo asingeweza kushindwa kujua kinachoendelea.
Lakini sasa umri wa Roma ni miaka ishirini kwenda therathini kitu ambacho sio cha kawaida kwa umri huo kuweza kusababisha radi ya mapigo mengi.
Alijiambia mtoto huyo ambaye alionekana kuwa na tamaa ya pesa na maisha ya anasa haijalishi nini amefanya au wapi ametokea uwezo wake wa kutambua siri za mbingu na ardhi ni mkubwa mno kiasi kwamba unamfanya yeye mwenyewe kuona wivu.
Lekcha alijikuta akihamaki kwani hakutgemea mabadiliko ya namna hio.
Alikuwa akielewa kuhusu radi na mateso yake tokea siku ambayo aliweza kuuvaa mwili wa mkuu wa majoka mfalme Wuja , ijapokuwa alikuwa akijiamini kutokana na nguvu yake ya nishati ya Ant -matter lakini hakuwa na uhakika kama anaweza kupona kama atapigwa na radi ya mapigo elfu moja.
“Muda wowote radi itafika ndani ya hili eneo , je bado unataka kuendelea kushindana na mimi?”Aliuliza Roma huku akiona ishara ya wasiwasi kutoka kwa Lekcha
Lekcha alijikuta akiona ni kama vile anadhalilishwa na aliishia kutoa tabasamu la kejeli akionekana hataki kushindwa.
“Inaonekana umekasirisha anga na muda wowote radi inakuja kukupa adhabu yako ,hivi wewe mwenyewe unao uwezo wa kupona kabla ya kuniuliza , nina ngungu ya ant-matter ambayo inawea kulinda mwili wangu , unadhani radi hio itaweza kunifanya nini?”Aliongea Lekcha kwa kujiamini.
Roma hakuwa akipanga kumkasirisha Lekcha ukweli ni kwamba alijua kumdhibiti Lekcha lilikuwa ni swali la muda tu.
Hata kama hatomuua Lekcha Roma bado alikuwa na uwezo wa kutumia shoka lake na kumfungia katika space crack au kumpoteza mazima katika malango ya anga.
Lakini kwasababu Lekcha alionekana kuwa na hamu ya kupitia uzoefu wa nguvu ya radi akiwa na yeye hakuona haja ya kumjali
Mara baada ya kusita kidogo palepale alikiita chungu chake cha maafa kwa mara nyingine lakini hakutumia kwa ajili ya kujikinga na radi ambayo inatarajia kushuka alisimama na kisha alikizibia na mwili wake
Yaani alichokifanya Roma ni tofauti kabisa na mwanzo , kwani ili kupita dhiki hio ya mapigo mengi alitakiwa kukiweka chungu hicho juu ake kama kinga lakini awamu hio ni kama anakilinda chungu hicho na radi.
Kitendo kile kilimfanya Aoiline kuwa katika hali ya mshangao na alitaka kumuuliza Roma anajitafutia kifo lakini mara baada ya kufikiri kwa haraka alioneakna kupata wazo ambalo Roma anajaribu kufanya na macho yake yalijaa mshituko na kuamua kukaa kimya akitarajia namna Roma anavyokwenda kupita dhiki hio.
Upande wa nje mnara wote ulifunikwa na dhoruba ya wingu zito mno kiasi kwamba ni hakika wale ambao wapo karibu na mnara huo wasingewea hata kuuona kwani ulifunikwa mpaka kwenye maji na ni cheche tu na ngurumo ambazo zilikuwa zikisikika.
Katika ile floor ambao walikuwepo Roma ile ufa ambao umejitengeneza ulionekana muda wowote unakwenda kuporomoka kutokana na presha ambayo inajiandaa kuingia ndani.
Hali ya giza ilizidi kuongezeka ndani ya mnara na hakukuwa na mwanga tena kama mwanzo.
Roma upande wake hakuwa na muda tena wa kumfirikia Lekcha , ukweli ni kwamba aliacha kabisa kupambana nae.
Kulikuwa na nafasi ndogo sana kwa Lekcha kuweza kukwepa radi ile kwani alikuwa amekaribiana sana na Roma.
Ilionekana ni dhahiri baada ya Dhiki hio ambaye atafanikiwa kutoka hapo wa kuipita hio dhiki basi moja wa moja anaweza kuwa mshindi.
Boom!!
Palepale mwanga ulionekana ndani ya eneo lile mara baada ya shoti ya radi iliokuwa katika mwanga wa rangi ya fedha(silver), yaani ni mwanga ambao haukuwa mweupe sana wala mweusi sana.
Shoti ile ilianza kidogo kidogo na kwa nje ilikuwa ni kama vile anga linashambulia ule mnara na radi na kutaka kuangusha kwani wingu lilikuwa likizunguka kwa kasi kubwa mno , ni kama vile kuna panya yupo shimoni na paka anatafuta namna ya kupita ndo ilivyokuwa kwa namna wingu hilo lilivyokuwa likizunguka kupata upenyo wa kumpa Roma anachostahili.
Kitendo kile kilifanya mnara wote kuwa na hali flani ya umeme ambao ulikuwa endelevu , yaani ni radi ambayo haikukoma ni kama vile umeme umewashwa kutoka mawinguni na kuingia ndani ya mnara huo.
Upande wa Roma na Lekcha walikuwa wamefunikwa na shoti za radi ambazo ni kama hazina mpango wa wa kuwaachia na kuwafanya hata miili yao isionekane.
Zile nguvu za nishati ya Ant-Matter ambazo zilikuwa zimesambaa zote ziliyeyushwa na shoti za radi na kupotea mara moja , ikionekana kabisa hakuna uwezekano wa kuhimili nguvu yake.
“Arghhhh…uwiii!!”
Lekcha alipiga yowe kubwa mno la kilio cha kusaga meno na hio yote ni kutokana na kuyeyuka kwa kasi kwa nishati yake ya Ant Matter na kugeuka mvuke ambao ulipotelea angani. Alikuwa akibabuka kama vile ni magamba ya mti.
Upande wa Roma hakuonyesha ishara yoyote kama alikuwa akipitia maumivu .
Ukweli ni kwamba ile radi ilikuwa imemfunika Roma sio kwamba ilikuwa ikimshambulia lakini ni kama vile ilikuwa ikimzingira na kushidwa kupita katika mwili wake hivyo kutokumsambabishia maumivu yoyote.
Ilikuwa ni kama vile inamuogopa Roma kumshambulia kabisa tofauti na ilivyo kwa Lekcha.
Katika mkono wa kulia wa Roma alikuwa akibadilisha kwa kiwango kikubwa nishati za mbingu na ardhi na kutengeneza moto wa rangi nyeusi huku mkono wa kulia alikuwa ametengeneza kiwango kikubwa cha moto wa rangi ya bluu.
Moto ule ulikuwa ukimzingira na kutengeneza kitu kama gamba la radi ya rangi ileile ambayo ilikuwa ikisukumana na ile ya radi ya Dhiki.
Yaani ilikuwa ni kama vile nguvu ambayo Roma anadhalisha ilikuwa ikikataana na dhiki ile ya radi ndio maana ilitengeneza ‘magnetic field’ ambayo ilifanya radi ile kumzunguka Roma na kutokumgusa.
Ushawahi kuona filamu ambayo binadamu yupo msituni na anakutana na Dubu na yupo katika hali ya kutoweza kukimbia na anafumba macho kusubiria kuraruliwa na lile Dubu lakini ajabu mnyama yule aina ya Dubu anapiga magoti na kukusujudia basi hali hio ilikuwa ni kama vile kwa radi ile ya mapigo mengi.
Kitendo cha Roma kudhalisha moto mweusi na bluu na kisha kuunganisha kulimfanya kuweza kutengeneza radi yenye tabia sawa na ile ya Dhiki na kumfanya isihindwe kumsogelea.
Kifizikia kilichokuwa kikitokea ni sheria ya Ki’Electrostatic , sheria ambayo inaelezea kwamba kunapotekea chaji mbili zinazofanana ziwe aidha ni chanya au hasi ili mradi ziwe zimefanana basi zitakataana na kama zikitofautiana zitavutana.
Kwa lugha nyepesi ni sawa na kusema hakuna mvutano wowote kati ya mwanaume na mwanaume bali kuna mvutano mkali ambao huleta madhara pale mwanamke na mwanaume wanapokutana sasa chukulia radi aliotengeneza Roma ni radi dume na iliotaka kumuadhibu ni radi dume pia hivyo ki asili zitakataana.
Sasa ni kwamba kabla ya radi hio kushuka Roma alishajua kwamba akiunganisha elementi za moto mweusi na moto wa bluu atatengeneza shoti ya radi ya rangi ya fedha ambayo ndio rangi hio hio ya Dhiki.
Unachopaswa kuelewa ni kwamba radi ya mapigo tisini na tisa ilikuwa na rangi yake na radi ya mapigo tisa ilikuwa na rangi yake vilevile na radi ya mapigo mia tisa tisini na tisa ilikuwa na rangi yake vilevile.
Utofauti huu wa rangi inamaanisha namna inavyotokea kuna utofauti mkubwa wa elementi za chaji.
Roma hakuhitaji chungu kujilinda na radi tena hio yote ni kwamba anao uwezo tayari wa kutengeneza radi ya rangi ya silver kwa kuunganisha moto wa rangi nyeusi na moto wa rangi ya bluu na matokeo yake ni kwamba akawa anafanana na radi ya mapigo mia tisa tisini na tisa na kama sheria kifizikia ya asili inavyosema radi ile ilimtambua Roma kama mwenzake kutokana na kudhalisha nguvu inayolingana na kwake na matokeo yake ilishindwa kumdhuru.
Upande wa Lekcha yeye ni kama vile alikuwa Chanya na radi ilikuwa hasi na sheria ya asili inaelezea kwamba ikitokea nguvu mbili hazifanani basi zitavutana na ikitokea hizo nguvu mbili moja ni dhaifu basi itamezwa na ile iliokuwa na nguvu.
Hivyo ant Matter ilikuwa ni dhiafu na radi ilikuwa na nguvu hivyo moja kwa moja nishati ile ilifunikwa.
Radi ile ilikuwa ni endelevu , pengine ni aina ya radi ambayo binadamu wa kawaida hajawahi kuishuhudia na kadri ilivyokua ikiendelea kushambulia upande wa Roma alikuwa akipitia steji mbili muhimu sana ambayo ya kwanza ni Soul Evolution(Kukua kwa nafsi) na pili ni Soul Cleansing(Usafi wa nafsi) ambazo steji hizi zote mbili ukiziunganisha majini wanaita Ubatizo wa moto wa mbingu(heavenly fire baptism) ama ubatizo wa radi katika lugha ya kibinadamu.
Ukumbuke majini hawaiti radi kama radi bali kwao radi ni sawa na moto wa mbingu au moto wa Mungu na wao wanaamini kwamba moto wa mbingu ndio huwatengeneza au ni kama chanzo cha kukua kwao.
Katika hatua za juu kabisa za uwezo wao au unaweza kusema levo ambazo majini wa viwango vya juu sana ambao walipitia ni katika hatua ya ubatizo wa moto wa mbingu.
Lakini sasa tokea enzi zile hakuna jini ambaye ashafanikisha kupitia hatua ya ubatizo wa moto.
Roma hakupata faida ya kusafishwa kwa nafsi au kukua kwa nafsi pekee bali pia alipata usafisho wa mwili , yaani ni kama vile mwili wake uliondolewa kitu ambacho kilikuwa kikimsumbua kwa muda mrefu na kumfanya kuzidi kuwa imara.
“Hatimae imetokea… huyu mtoto amekwisha kupata ufunuo wa radi ya mapigo mengi na namna unavyotokea , hii radi ya kimungu haina tena madhara kwake zaidi ya kuwa ndugu aisee sijatarajia baada ya maisha yangu marefu kushuhudia kitu cha namna hii”Aliongea Aoiline mwenyewe .
Huku hisia mbalimbali zikipita katika moyo wake , ilionekana kwamba ukiachana na Roma kuweza kujua siri ambayo ipo katika adhabu ya mapigo tisini na tisa ya radi lakini pia alikuwa amefahamu siri iliopo nyuma ya mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi.
Kwa mtu wa kawaida anaweza kusema kwanini majini waogope radi ilihali Roma anaweza kuwaambia siri ya radi hizo lakini ukweli ni kwamba ili waweze kufanikisha hilo lazima wakaanze moja katika hatua za uvunaji wa nishati za anga kwa kutumia mbinu ya andiko la urejehso.
Roma aliweza kudhibiti siri ya radi hizo kutokana na kwamba alikuwa amepitia njia ndefu ya mafunzo hayo ambayo ndio kama msingi na hii ilimpelekea kuwa na uwezo wa kutengeneza moto adimu sana ambayo una elementi zote za kutengeneza radi , mfano wa moto wa bluu , maji ya kiroho na moto mweupe.
Siraha za namna hio ni majini wachache sana ambao wanaweza kutengeneza au hakuna kabisa ndio maana tokea mwanzo miliki zote za majini watu zilikuwa zikimuwekea Roma njama ya kutaka kumpa siri hio.
Ikumbukwe kwamba katika hatua za andiko la urejesho mbinu ya hatari zaidi ni ile ya kufa na kufufufuka , yaani steji ya kifo na uhai.
Kwahio basi mpaka muda huo Roma aliweza kupitia hatua muhimu ambayo ya kwanza ni mapigo tisa ya radi ambayo steji hii alitumia uwezo wa mwii wake kujiponyesha kwa haraka na andiko la urejesho , hatua ya pili ya dhiki ni mapigo tisini na tisa ambayo aliyapata katika mnara huo wakati wa kutoka kwa msaada wa Cauldron na hatua ya tatu ni mara baada ya kumshuhudia Anjiu akipitia levo ya mapigo ya radi alikuja kufahamu siri ya kutengeneza radi ya zanbarau na hatua nyingine ni hio ya sasa ya kupitia mapigo mia tisa tisini na tisa lakini awamu hio hakuumia zaidi ya kwamba aliidhibiti ile radi kwa kujifananisha nayo ili sheria ya asili(law of nature) ifanye kazi.
Wakati Roma akifurahia namna ambavyo radi ya mapigo mengi ilivyokuwa ikimzunguka na kuendelea kunyonya nishati yake Lekcha yeye alikuwa katika kilio cha kusaga meno.
Ilikuwa ni ngumu sana kwake kujiokoa katika hali ambayo alikuwepo , iapokuwa radi ya Zambarau ilikuwa na uwezo wa kuharibu mwili wake lakini ukubwa wa nguvu ya ant matter iliuwa na uwezo wa kumrejesha lakini awamu hio radi ya rangi ya fedha haikuwa mchezo kabisa , sio tu kuharibu mwili lakini pia ilianza kuharibu na nafsi yake.
Haikujalisha nishati ya Ant Matter ilikuwa na nguvu namna gani lakini hakuweza kulinda kitu muhimu sana ambacho ni roho au nafsi , ilimaanisha kwamba Lekcha alianza kukosa ufahamu wa kujiendesha na kuwa kichaa na kadri sekunde zilivyokuwa zikisonga angepotea moja kwa moja.
Alijitahidi kukusanya kiwango kikubwa cha nishati kulinda roho yake lakini hakufua dafu kwani nishati yake ilikuwa na kikomo lakini kwa mapigo elfu moja ya radi hakukuwa na kikomo cha ukubwa wake.
Aliweza kuona kabisa nguvu ya radi hio ilikuwa ni kubwa sana kiasi kwamba hawezi kuvumilia tena na kifo kilikuwa kikimsogelea kwa kasi ya 5G.
BOOM
Awamu ya pili kubwa zaidi ya pigo la radi ilishuka , haikueleweka pigo moja lina uzito wa nguvu kiasi gani kukamilisha hesabu ya 999 lakini ni dhahiri mapigo yasingekuwa moja moja.
Roma alikuwa katika hali ya furaha ya ubatizo wa radi hio na mabadiliko ya kiakili aliokuwa akipitia ilimfanya kumpotezea kabisa Lekcha aliekuwa akilia kama mtoto.
Ajabu ni kwamba ni nje ya mahesabu ambayo Roma alitarajia kwani alipitia mapigo matatu tu ambapo kila pigo moja lilidumu kwa dakika kumi na tano.
Haikueleweka ni kwa namna gani majini waliweza kutoka na hesabu ya mapigo tisini na tisa katika awamu tatu lakini kutokana na ukubwa wa radi hio na nguvu yake Roma aliamini inawezekana awamu tatu kukamilisha mapigo yote mia tisa tisini na tisa.
Mara baada ya dakika kumi na tano kumalizika za pigo la mwisho hali ya hewa ilirudi katika hali yake ya kawaida kwa kasi sana.
Na hata ule mwanga wa rangi ya silver ambao ulidumu ndani ya mnara huo kwa dakika arobaini na tano ulirudi katika hali ya kawaida.
Hali ya hewa ndani ya mnara huo ilikuwa ni harufu flani hivi kama ya baruti iliochanganyika na kuungua kwa mimea na kuyeyuka kwa baadhi ya dhana zilizopo ndani humo.
Roma alivuta pumzi nzito na kisha alishuka taratibu na kukanyaga floor hio ambayo ilikuwa imepata moto , chungu cha machafuko kilimzhuguka Roma kwa namna flani hivi ya kumlaki kikimuelezea kwamba licha ya kumkinga na radi lakini pia kimefaidika .
Roma palepale aliamua kuficha Shoka lake la kimaajabu na chungu kile kwani hakuwa na uhitaji navyo kwa muda huo.
Mwili wake ulikuwa ukitoa harufu flani hivi isiokuwa ikielezeka lakini kwa mbali ni kama vile kuna cheche za shoti zilizokuwa zikionekana katika mwili wake uliokuwa umetuna kwa mazoezi.
Hakuwa na nguo hata moja wakati huo alikuwa uchi wa mnyama na kwanzia vidoleni mpaka chini alikuwa akitoa shoti za umeme na ilikuwa ni kama vile mwili wake unapo kwani shoti zile zilikuwa zikififia.
Roma alishangazwa na nguvu ya radi hio lakini alijua kabisa hapo sio mwisho , inasemekana majini wa enzi hizo walipitia mpaka hatua ya mwisho kabisa ya mapigo 9999 , sasa alijiuliza kama ni hivyo waliwezaje kupita hatua hio au na wao walikuwa kama yeye tu walijifananisha na radi hio na matokeo yake radi ilifuata kanuni ya asili.
Roma mara baada ya kuwaza kwa muda hatimae sasa akili yake iliwaza kuna Lekcha na aligeuka palepale na alipoangalia sehemu Lekcha alipo aliona vijicheche kwa mbali ambavyo vilikuwa vikipotelea.
Kama ilivyo kwa Roma mwili wake kupoa upande wa Lekcha alikuwa amerudi kawaida na mwili wake ulikuwa umepoa kabisa kwa kupoteza nishati yote ya Ant-Matter.
Ilionekana radi yote ilikuwa imekula nishati yake na kumbakisha mweupe na kuwa kama binadamu wa kawaida tu.
“Hukutakiwa kuwa na kiburi…. Vinginevyo ungeweza kupata nafasi ya pili , isitoshe mwili wako unaonekana kutokuwa wa kawaida”
Roma aliongea huku akitembea kumsogelea Lekcha aliekuwa akitetemeka kama vile mgonjwa wa Malaria kali.
Lekcha aliepiga goti alijikuta akivuta pumzi nyingi na kisha kwa unyonge aliinua kichwa chake , alikuwa amefubaa kama karatasi lakini hata hivyo hakupoteza ile hali ya ukejeli kwenye uso wake , ilikuwa ni kama vile hakujali tena kifo.
“Acha kunionyesha hio tabia yako ya kujiona unajua kila kitu , hivi unajua kinachonifanya kukuchikia zaidi ni nini , kinachonifanya ni kuchukie sana ni tabia yako ya majigambo”
“Inaonekana una chuki binafsi zidi yangu lakini niwe tu mkweli sijawahi kukuchukulia kama tishio kwangu lakini hata hivyo umenishangaza , sijui kuhusu mengine lakini kitu ninachojua ni kwamba sijali namna yoyote ile unavyonifikiria”
“Hahahaha… , kwaio ndio unajigamba , naona mwishoni nimekushindwa kama alivyoshindwa yule mjinga Yan Buwen na mjinga wake Denisi , mpaka mwishoni inaonekana hakuna ambaye anakuweza na yamkini hapo mwenyewe unajihisi sio wa kawaida lakini Roma ngoja nikuambie kitu , mimi Lekcha a.k.a Joseph Bikindi hujanishawishi juu ya uwezo wako wala siwezi kukubali, hata kama nikifa siwezi kukuruhusu ujione shujaa au kukufanya ufikirie umeniweza .. kitu pekee ambacho kimenifanya kuwa katika hali ya kushindwa ni bahati basi , najiuliza kwanini sikuwa na bahati ya kupata fursa ya kukutana na master ambaye ni mzuri kwangu , kwanini niligeuzwa na kuwa mtumwa , kwanini kuna watu nyuma yako ambao wapo tayari kukusaidia ,, Hades umefanikiwa hayo yote kwasababu bahati ilikuangukia na ukawa upande mzuri , tokea ulivyozaliwa Mungu alishakuandikia utafanikiwa kwa kutuchukulia sisi kama ngazi , lakini hebu jiangalie sasa hivi unavyojiona mwenyewe, sio juhudi zako pekee zilizokufikisha hapo mwanaharamu wewe”
Lekcha alitumia kadri ya uwezo wake wote kuongea kwa sauti lakini hata hivyo sauti yake ilionekana kunyongea sekunde hadi sekunde.
Roma aliishia kucheka kivivu kama vile ashajichokea hata kumgusa Lekcha lakini hata hivyo hali flani ilionekana katika macho yake mara moja.
“Huu ni muda wa wewe kuacha kuwa mpumbavu , najua haina maana kukuelewesha tena lakini nikuambie tu wewe ni moja kati ya maadui zangu ambae umechukua muda mrefu , ukweli sio kwamba nakuchukia kihiivyo , kabla roho yako haijauacha mwili wako nataka nikuambie kitu ,, pengine ulichosema ni kweli kwamba ni neema za Mugnu zilizonifikisha leo hii lakini unaweza kushangaa kwamba wakati wewe ukiwa mwanafunzi mzuri na kinara shuleni kwenu, unaependwa na walimu kwangu mimi sikuwa hata na uhuru wa kuitwa chokoraa .. hivi unadhani umeshindwa na mtu ambae alikuwa na kila kitu , ngoja nikuambie umeshindwa na mtu ambaye hakuwahi hata kujua alikuwa na familia wala ni wapi alizaliwa , mtu ambaye alitegemea nyama ya binadamu kuishi , mtu ambaye alikuwa ni sehemu ya majaribio ya kisayansi ambayo maumivu yake sio ya kawaida , kwasababu tu ya kupoteza ndugu na kuwa kilema ndio useme Mungu amenipendelea , ninachomshukuru Mungu leo hii kunipa nafasi ya kuendelea kuishi mpaka leo hii licha ya changaoto zote nilizopita na hii ndio tofauti yako na yangu , unaamini Mungu kanipendelea lakini mimi namshukuru kwa kunipa nafasi ya kuishi”
Machozi ndio dalili pekee ya uhai iliomtoka Lekcha na mara baada ya kuvuta pumzi ndefu palepale nywele zake zilianza kubadilika rangi na kuwa nyeupe na hatimae rangi ya kijivu na ngozi yake ikakauka na kujikunja na hatimae kukosa sifa ya ubinadamu na uhai wake ulionekana ndio unafikia mwisho taratibbu taratibu.
Katika uso wake huo ambao ulikuwa ni kama udongo hali ya furaha, huzuni na makasiriko iliweza kuonekana na alionekana kuwa wa tofauti sana kuliko mwanzo , hakuna neno ambalo liliweza kutoka katika kinywa chake kana kwamba alikuwa akisubiria wakati wake wa mwisho.
Roma aliendelea kumwangalia Lekcha jinsi alivyokuwa akibadilika rataribu kadri nishati ya ant-matter ilivyokuwa ikipotea hewani na palepale alivuta pakiti ya sigara kutoka katika hifadhi yake ya anga na kuchomoa moja.
“Vipi nikupatie moja?”Aliuliza Roma, ndio kitu pekee ambacho alikuwa na uwezo wa kumpatia Lekcha muda huo katika hatua zake za mwisho.
“Pengine hujawahi kuvuta sigara ghali kama hii maisha yako yote”Aliongea Roma na kisha alichuchumaa na kumshikisha Lekcha ile sigara na alisita kidogo na hatimae Lekcha alionekana kuishikilia japo kwa taabu na kisha akaitumbukiza katika mdomo wake, mara baada ya Roma kuiwasha Lekcha alivuta moshi kidogo tu na kushikwa na kikohozi kilichomfanya sifara kudondoka.
“Naona unanikejeli , nimepokea hii sigara kwasababu inaonekana ya thamani sana na ingesikitisha nikifa kabla ya kuonja moshi wake … usijione wewe ndio mtu pekee ambaye umepitia mengi na una uzoefu wa kuishi maisha ya kifahari”
Roma alivuta kwanza moshi na kuupuliza hewani na kisha alitoa tabasamu huku akiona kiwango cha mwisho mwisho cha nishati ya Ant-Matter kikipotea katika mwili wa Lekcha.
“Kama ningekuwa mtu mkarimu pengine ningekupatia bia ya ya thamani kubwa lakini nimekupa sigara kwani ndio kitu pekee cha thamani ndogo nilichokuwa nacho”Aliongea Roma na kumfanya Lekcha kutoa tabasamu la dhati lisilo na unafiki kwa mara ya kwanza mbele ya Roma.
Muda huo ndio aliweza kufika Aoiline kwani alijitenga mbali sana na eneo hilo na mara baada ya kutua alimwangalia Roma kwa namna ya kushangazwa nae.
Alimwangalia namna ambavyo Roma alikuwa akiwasha sigara moja baada ya nyingine huku akiangalia namna ambavyo Lekcha anavyochukuliwa na Israeli mtoa roho.
Roma baada ya kuona hakuna tumaini lolote kwa Lekcha alisimama na kisha alimsogelea Aoline na ni muda uleule aliruhusu radi kumpiga Lekcha na akageuka kuwa majivu na huo ndio ukawa mwisho wake.
“Inaonekana angalau mwishoni chuki yake zidi yako imempotea”Aliongea Aoiline.
“Labda , kumalizana nae ni kama kuagana na kipindi kingine cha maisha yangu , Ni nani ajuaye kinachonisubiri mbele”
Aliongea Roma huku akitoa tabasamu hafifu kana kwamba ashaona nini kinamngojea huko duniani.
ITAENDELEA.
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI: SINGANOJR

Mono no aware .

ILIPOISHIA
Alimwangalia namna ambavyo Roma alikuwa akiwasha sigara moja baada ya nyingine huku akiangalia namna ambavyo Lekcha anavyochukuliwa na Israeli mtoa roho.
Roma baada ya kuona hakuna tumaini lolote kwa Lekcha alisimama na kisha alimsogelea Aoline na ni muda uleule aliruhusu radi kumpiga Lekcha na akageuka kuwa majivu na huo ndio ukawa mwisho wake.
“Inaonekana angalau mwishoni chuki yake zidi yako imempotea”Aliongea Aoiline.
“Labda , kumalizana nae ni kama kuagana na kipindi kingine cha maisha yangu , Ni nani ajuaye kinachonisubiri mbele”
Aliongea Roma huku akitoa tabasamu hafifu kana kwamba ashaona nini kinamngojea huko duniani.

SEHEMU YA 770.
“Inaonekana upo kwenye matatizo makubwa yanayokusubiri”Aliongea Aoiline mara baada ya kuona mabadiliko ya Roma.
“Haijalishi ukubwa wa matatizo yangu lakini kwa mbweha kama wewe ulieishi miaka elfu hamsini itakuwa si kitu , ukweli ni kwmaba nimeshangazwa kupigana na Lekcha kwa mwaka mzima”Aliongea Roma.
“Kwetu sisi majini pepo kama sio kwa ulimwengu huu kuzuia uwezo wetu asingeweza hata kuhimili mapigo kumi kutoka kwangu , naona unanichukulia poa , wakati wa enzi zangu nilikuwa nikipambana na maadui wenye nguvu mara tatu ya uwezo wake”Aliongea huku akiweka vizuri gauni lake safi ambalo alikuwa amebadilisha.
“Nina amini maneno yako , maana sio jambo dogo mpaka vitukuu zako kukujengea sanamu kwa ajili ya kukuabudia, kama nisingeona mwenyewe kwa macho nisingeweza kuamini “Aliongea Roma ambae mara baada ya kukumbuka alichokiona kule ulimwengu wa jangwa tenganifu kilimfanya kuamini anachoongea..
Lakini sasa mara baada ya kutaja vitukuu na sanamu uso wa Aoiline ulibadilika palepale.
“Wewe..umekutana na wana ukoo wenzangu?”
“Yeah .. waliweza kuingia katika ulimwengu wa jangwa tenganifu miaka elfu hamsini iliopita mapema tu mara baada ya wewe kuingia huku”
“Wanaendeleaje , hawajaonewa kweli na hao majini watu wanaojiona wapenda haki?”
“Wapo vizuri sana , kwa mfano kiongozi wa ukoo wa Dhehebu la Mbweha afahamikae kwa jina la Latina kwa sasa ana mikia saba na ameishi zaidi ya miaka elfu nne , uwezo wake ni wa kutosha kabisa”Aliongea Roma na kumfanya Aoiline kutoa pumzi ya ahueni.
“Ninajionea aibu mwenyewe hata kwenda kukutana nao , nimewaangusha sana”
“Hapana , hivyo sio wanavyoamini , wewe ndio mtangulizi wao na shujaa wao , wameenda mbali kufanya ukaribu na mimi kwa ajili tu ya kukupitisha kwenye huu mnara”
“Unaweza ukawa sahihi lakni lazima watakuwa wananichukia kwa maamzi nilioyafanya wakati ule na kuishia katika ulimwengu wa majini pepo, pengine hali zao kwa sasa zingekuwa tofauti”Aliongea na kumfanya Roma kushindwa kujua aongee nini lakini muda uleule alikatishwa na Aoiline.
“Ukiachana na hayo , hujaniambia imekuwaje mpaka ukaingia kwenye huu mnara tena?”
Roma mara baada ya kuulizwa swali hilo alianza kuelezea kila kitu mpaka kumfanya kuja kutua katika huo mnara , yaani namna alivyovutwa katika ulimwengu wa jicho la anga na kuendelea , hakuacha kuelezea pia namna ambavyo alifanikiwa kupata Dhana yake ya Shoka la Pangea.
Aoiline wakati wa kusikiliza maelezo yake alijikuta akishangaa mno na kuonekana kama vile haamini.
“Acha kunidanganya , ijapokuwa umefanikiwa kupita levo ya mapigo mengi ya radi lakini haimaanishi unaweza kunidanganya”
“Nimekuonyesha na ushahidi kwanini nikudanganye , mimi mwenyewe inakuwa ngumu hata kuamini , kwanza hizo roho nilizokutana nazo si ndio waliokuwa ni viongozi wa koo zenu kabla ya kufa?”Roma aliuliza akimaanisha wale Roho kutoka ulimwengu wa jicho la Anga.
“Kama unaongea ukweli , basi nitakuwa nawajua kwa majina yao kabla hawajafariki , lakini unapaswa kujua kulikuwa na majini wenye nguvu kubwa zaidi kabla hata ya kuzaliwa kwangu , kwa mfano vita ya binadamu , majini watu na majini pepo ilidumu kwa muda wa miaka elfu moja , katika kipindi hicho pamoja na hali ya ulimwengu ilivyokuwa si ajabu kuwepo kwa majini waliotumia Dhana kama hio ya shoka , lakini nikuambie tu hio Dhana sio ya kawaida na hata wakati huo hakuna ambaye alikuwa akijua alieitengeneza ni nani zaidi ya ukweli wa kiimani tu , lakini jambo kubwa la uhakika hata wale majini ambao walikuwa juu ya levo za mapigo elfu tisa hawakuwahi kutumia uwezo wake wote, Katika Dhana zote za kijini ukiachana na Dhana ya Chaos Cauldron , Dhana ya kioo cha Nafsi ndio ambayo siri yake mpaka leo hii haijafahamika na namna ambavyo inafanya kazi, pengine huwezi jua unaweza ukaipata kwasababu tayari umepata hilo shoka”Aliongea Aoiline.
“Mimi sina mashaka , chochote kitakachonitokea najua ni swala la kihatua , kinachonipa shauku ya kujua ni nani ambaye aliweza kupata ufunguo wa muunganiko wa ulimwengu wa jicho la anga na ulimwengu wa majini pepo , labda awe alifika katika huu mnara na kisha akaondoka”Aliongea Roma na kumfanya Aoiline hali yake ya uso kubadilika lakini alipotezea maramoja.
“Naona kuna kitu unakijua?”Aliuliza Roma kwani ashajua Aoiline kuna kitu anajaribu kumficha.
“Kama jibu ni ‘ndio’ unatakaje , au unataka kunilaziisha nikuambie?”
Roma alishangazwa na kauli ile na kukosa neno kwa wakati mmoja , alijiambia mwanamke huyo alikuwa na tabia ya kubadilika badilika kama kinyonga bila sababu yoyote.
Lakini kabla hata hajajua aongee nini walishituliwa na sauti ambayo ilitokea katika floor ya chini kabisa yaani kwenye mlango wa kuingilia katika ulimwengu huo kupitia ulimwengu wa majini pepo.
“Imewezekanaje , kwanini mlango umefunguka ili hali ni mwaka mmoja tu tokea ufunguke?”Aliongea Aoiline kwa mshangao, aliweza kugundua mara moja sauti walioweza kusikia ni ya mlango wa mnara huo kufunguka, sasa alishangaa kwasabbau mara nyingi hufunguka kila baada ya miaka sitini.
“Una uhakika haijawahi kutokea ukafunguka mapema?”Aliuliza Roma.
“Duh! Nimeishi ndani ya huu ulimwengu kwa miaka mingi sana na huu mnara mlango wake hufunguka kila baada ya miaka sitini na haijawahi kutokea vinginevyo”
Mawazo mengi yalipita katika kichwa cha Roma na mara baada ya kuwaza kwa dakika hatmae aliinua kichwa chake na kumwangalia Aoiline.
“Nadhani kuja kwetu kwenye huu mnara kwa kutumia njia isiokawaida ndio imesababisha mlango kufunguka kabla ya wakati , tatizo lazima litakuwa mwishonni mwa mnara , tena kuna mtu ananisubiria huko hebu tuondoke kwanza”Aliongea Roma.
“Mwishoni mwa mnara , kwahio unaniambia twende pamoja?”Aliuliza Aoiline kwa mshangao.
“Sioni tatizo kama upo tayari kuondoka na mimi isitoshe unanidai fadhila”
“Kama nikitoka uwezo wangu utakuwa mkubwa sana na kuna uwezekano wa wengi kutokunifikia”Aliongea huku akitoa tabasamu la uchokozi.
“Kama kweli ulikuwa na nia mbaya na binadamu usingeweza kuja katika ulimwengu wa majini pepo miaka elfu hamsini iliopita , hii inanifanya niamini kwamba wewe sio hatari hata ukiwa katika ulimwengu wa kawaida , isitoshe nimeua watu wengi kuliko hata wewe”
“Hicho ndio ninachokupendea , una maamuzi”Aliongea Aoiline huku akicheka na palepale aliruka huku mkia wake mrefu ukimtangulia mbele.
“Unataka kufanya nini , unapanga kupita katika kizuizi cha hio radi , haina haja ya kujiingiza hatarini namna hio ninaweza kukuazima chungu changu” Aliongea Roma.
“Acha ujinga kijana , unadhani radi ya mapigo tisini na tisa inaweza kunizuia nisitoke kwenye huu mnara?”
“Nini!, si uliniambia hujiamini kupitia mapigo yote?”
“Na ukaniamini kabisa?”
“Kwahio unasema ulikuwa na uwezo wa kuondoka kwenye huu mnara muda mrefu tu?”
“Pengine sikuwa na uwezo huo miaka elfu hamsini iliopita lakini sikupoteza miaka yote hio kwa kutokufanya chochote , sikutaka uwe mzembe ndio maana nilikuficha kipindi kile , nilitaka kila mmoja aweze kufahamu utendaji wa huu mnara kwa uwezo wake binafsi na nilikuwa na uhakika ingekuwa rahisi kwako kwasababu ya Chaos Cauldron”
Walikuwa tayari washafika floor ya ishirini wakati wakiendelea kuongea , radi ilikuwa ikiwapiga kila walipokuwa wakipita katika kila floor lakini haikuwa na madhara kwao.
Wakati Roma alipokuwa akijifananisha na radi hio ili isimdhuru upande wa Aoiline kwa kutumia ile mikia yake tu aliweza kujikinga na radi.
“Kama ni hivyo kwanini usingemuacha Lekcha mwenyewe kwenye huu mnara na ukaondoka wewe?”Aliuliza Roma.
“Umekuwa kichaa , ilikuwa rahisi kumshinda akiwa hapa kuliko akienda huko nje na kujificha kwa kutumia sura ya mtu mwingine”
Roma alishangaa kumbe alikuwa na mawazo hayo , alijikuta akitoa tabasamu la wasiwasi.
“Kwahio ulikuwa ukitaka kuendelea kupigana nae milele kama nisingekuja?”
“Hapana , Ningemuacha kama nisingeweza kumzuia tena , isitoshe ingekuwa rahisi zaidi kumuua akiwa katika ulimwengu wa kawaida kuliko ndani ya mnara kwani uwezo wangu utakuwa umerudi wote , hofu yangu ni kwamba binadamu wa kawaida wangeathirika , ni jambo zuri umekuja mapema nadhani ilipangwa kuwa hivyo”
Muda huo huo waliweza kufika floor ya sabini mahali ambako radi ilikuwa kubwa na kali si mchezo.
Roma alikuwa na wasiwasi kuivamia moja kwa moja , ingawa Aoiline alionekana akilemewa lakini hakukuwa na mabaduliko yoyote ya nguvu zake za kijini.
“Kwasababu geti la mnara upande wa ulimwengu wa majini pepo limefunguka itakuwa rahisi kwako kumfuata Master Chi , una mpango wa kufanya hivyo ?”
“Nimefikiria hilo pia lakini huko duniani hakupo sawa kabisa hivyo sio muda muafaka isitoshe huu mnara wa anga hauna madhara kwangu , mambo yakikaa sawa nitarudi tu kumtembelea na kumuuliza kama anataka kuondoka”Aliongea Roma na Aoiline alitingisha kichwa.
Roma upande wake alikuwa na wazo kama kweli angemleta Tang Chi duniani na sio wale majini wengine wa koo ya mashetani atapata shida sana kudili na majini wa miliki ya Braki.
Kubwa zaidi Tang Chi mwenyewe alionyesha hana nia ya kutoka kuja ulimwengu wa kawaida pale Roma alipomuomba watoke pamoja , na zaidi ni kwamba anaweza kupatwa na shida kama atatoka kutokana na uwezo wake.
“Bwana , kwanini upo tayari kuondoka ulimwengu wa majini pepo kwa hiari au ndio umewamisi wana ukoo wenzako?”Aliuliza Roma.
“Usiniite Bwana, niite Dada Aoiline au Aoiline inatosha nikishatoka kwenye huu mnara sitokuwa tena malkia wa jumba la Jedi , nimekaa huku kwa miaka elfu hamsini ambayo inatosha kabisa , kuhusu kwanini nataka kuondoka ni kwasababu kuu mbili, mosi nataka kukutana na wana ukoo wangu , pili nataka kuona tukio linaloikumba dunia”Aliongea na Roma hakuweza kuamini namna ambavyo alikuwa moja kwa moja katika majibu yake, lakini Roma alijiambia hawezi kuita jini wa miaka elfu hamsini ‘dada’ hata iweje hivyo aliona amwite kwa jina lake tu.
“Aoiline unaweza kuniambia ni kitu gani ulitaka kuniambie kipindi kile kabla sijaingia kwenye manra?”Aliuliza Roma ambaye alikuwa akikumbuka kuna kipindi ambacho Aoiline alitaka kumwambia kitu kabla ya kuondoka na Sophia.
“Hivi kumbe kuna kitu nilitaka kukuambia, tutaongea kuhusu hilo siku nyingine , isitoshe utajua tu kama sio leo ni kesho”
Roma macho yake yalisinyaa lakini hakuwa na chakufanya , mwishowe hakutaka kuuliza zaidi .
Katika floor za mwisho mwisho ngurumo a radi zilikuwa kali mno na kumpelekea hata Aoiline kusimama kwa muda lakini hatimae aliweza kufanikiwa kupita.
Ilikuwa ni wakati ambao Roma aliweza kugundua msingi wa nguvu za Aoiline ni mkubwa mno kuliko wa kwake., hata kama hakutumia chungu chake kwa asilimia mia moja lakini bado ukweli ni kwamba alitumia hivyo sio kwamba alikuwa akipita radi yote bila msaada.
Sasa Aoiline hakutumia Dhana ya aina yoyote ile na alitegemea uwezo wake wa kijini tu pekee kupita mapigo ya radi ya zambarau.
Mara baada ya kufika katika kilele cha mnara huo Aoiline alianza kuangaza macho kulia na kushoto kabla ya kumwangalia Xiao kwa macho yaliojaa shauku.
Xiao ambaye alikuwa na wasiwasi alidhania Roma angechukua muda mrefu kukaa chini ya mnara huo lakini mara baada ya kuona amerdi mapema alijikuta akifurahi mno.
Lakini mara baada ya kuona sura ya mrembo Aoiline alijikuta akinywea huku akianza kujilinganisha nae na palepale hisia za ‘inferiority’ zilimvaa kwani Aoiline alikuwa mrembo mno kiasi cha kumfanya hata aogope kusalimiana nae licha ya kwamba wote ni wanawake na kitu pekee alichoweza kufanya ni kumfinya Roma huku akimuuliza kama alikuwa ni mpenzi wake.
Roma alikuwa ashamtajia jina lake kwake lakini kwa wakati huo hakuweza kuamini kama mwanamke aliekuwa akizungumziwa ndio huyo.
Roma palepale alikataa kwani hakuweza kumwangalia Aoiline machoni, isitoshe alijua akishatoka katika huo ulimwengu uwezo wa Aoiline pengine unaweza kuwa unalingana na wa Athena au zaidi.
Hivyo Roma hakutaka kumfanya Aoiline akasirike kwa namna yoyote ile kwani hakutaka kuwa na adui mwenye nguvu kama huyo , kitu kingine alikuwa akimjua Aoiline ni mwepesi sana kubadilika ndio maana alijihami.
“Wow! naona umeambatana na mrembo mwingine awamu hii , sio mbaya , huyu mtoto anaonekana kuwa na kipaji , kuna uwezekano atakuja kuwa kwenye levo ya juu sana kama ataongeza juhudi , kama utamuacha kwenye mikono yangu nitamfanya kuwa kifaa cha kupandishia uwezo wako”Aliongea Aoiline na maneno yake yalimuogopesha Xiao na kumfanya kukasirika palepale.
“Wewe ni nani , Roma ni mtu mzuri usimpotoshe”
“Usimjali na maneno yake , Aoiline acha kumuogopesha bwana , tunapaswa kutafuta namna ya kutoka kwanza”
“Nadhani utavutiwa na kitu tofauti kabla ya kutoka”Aliongea Aoiline huku akiwa ametabasamu kana kwamba kuna kitu amegundua katika mnara huo na alipaa palepale na kwenda kutua katika eneo la wazi la juu.
Roma alishangaa kidogo lakini na yeye pia alimchukua Xiao na kisha kupaa nae kumfuata Aoiline upande wa juu na hatimae aliweza kuona kitu amabcho Aioline amesogelea.
Kulikuwa na kitu kama Ngoma ya mduara iliokuwa katika rangi ya kahawia yenye ukubwa urefu wa nchi sita na nusu hivi na pana , upande wake wa juu namna ilivyotengenezwa ilikuwa ikishangaza mno na ilikuwa na pembe katika kona kali mno kama upanga ambapo jumla yake zilikuwa nane.
Malighafi iliotumika kutengenezea kifaa hicho hazikujulikana , lakini ngoma hio ilikuwa imezingirwa na radi nyingi mno kiasi kwamba haikuonekana vizuri.
Ilikuwa rahisi kuamini radi ambayo ilikuwa ikipiga katika huo mnara ilikuwa ikitoka katika hicho kifaa.
“Dogo sikia sasa kati ya Dhana za kimungu ambazo zinaaminika kuwa na nguvu moja wapo ni hii, jina lake hatujui lakini sisi majini pepo tunaita Ngoma ya Naoni, angalau unapata maarifa mapya”






SEHEMU YA 771.
Kwa maelezo ya Aoiline Naoni alikuwa ni mjumbe mwenye mguu mmoja ambaye kazi yake ilikuwa ni kupiga ngoma katika falme ya mkuu wa enzi , mara baada ya Naoni kuasi alifurumushwa na ngoma yake na kuja duniani.
Sasa licha ya uwepo wa hadithi hio haikuwahi kuthibitishwa kama ilikuwa ni ya kweli kama Naoni ndio aliekuwa mmiliki wa ngoma hio lakini tokea ionekane katika ulimwengu wa majini iliaminika ilitokana na jini huyo wa mguu mmoja aliefahamika kwa jina la Naoni ndio maana wakaipatia jina la Ngoma ya Naoni.
Moja ya maajabu makubwa ya ngoma hio ni kwamba ilikuwa na uwezo wa kudhibiti radi , ngozi ambayo imetumika kutengenezea ngoma hio inaaminika kwamba ni ya mnyama ambaye hakuwahi kuonekana katika uso wa dunia na majini wanaichukulia ngozi hio kama Dhana inayojitegemea.
“Umewezaje kuijua kwa kuangalia tu , ulishawahi kuiona hapo kabla?”Aliuliza Roma.
“Sijawahi lakini katika vitabu vya koo ya miliki yetu kuna maelezo yake na hata mchoro wake upo , leo ndio naiona kwa mara ya kwanza na inaonekana hakuna alieweza kuiona kutokana na kuwekwa kwenye huu mnara , haishangazi radi ya zambarau kuwa na nguvu namna hio kama inatokana na hii ngoma”Aliongea.
“Hebu angalia kuna radi nyingi ya zambarau imejikusanya lakini kadri tunavyopiga hatua ndio inavyoachia”Aliongea Xiao kwa hamaki na kumfanya Aoiline na Roma kuangalia kwa umakini na ilionkena ilikuwa sahihi kadri walivyokuwa wakiisogelea ile ngoma ndio radi ilikuwa ikiachia kana kwamba inawaruhusu wasogee karibu.
“Inaonekana hii Dhana haina mmiliki”
“Kwahio unamaanisha inasubiri mmiliki?”Aliuliza Roma.
“Ndio , ukisikia Dhana za kimungu ipo hivi kadri zinavyokuwa na nguvu ndio uwezekano mkubwa kuwa na ufahamu wao , hii ipo pia kwa hii ngoma ya naoni , nadhani lazima ina kiasi flani cha nafsi kama ilivyo kwa Chaos Cauldron , nadhani muda wote ilikuwa ikisubiria mtu ambaye ataitoa katika hili eneo ndio maana radi inajiondoa ili tuweze kuikaribia”Alielezea Aoiline.
Roma alijikuta akikunja ndita huku akikumbuka maneno ya wale majini kutoka Braki.
Walisema hazina yao ilikuwa na uwezo wa kufufua majini pepo jamii ya mashetani , sasa Roma alijiuliza je walichokuwa wakilenga ni hio ngoma.
“Acha kurahisisha vitu , hii ngoma inaweza kudhibiti mapigo ya radi namna yanavyopiga lakini ni tofauti kama itatumiwa kama Dhana kwani itakuwa na nguvu isiokuwa na kikomo , lakini hata hivyo haijalishi Dhana ina nguvu kiasi gani kama anaeitumia uwezo wake ni mdogo basi yenyewe haitoweza kuonyesha uwezo wake wote , hivyo ni kichekesho kama majini pepo jamii ya masherani kuweza kufufuliwa na kifaa cha namna hii”aliongea Aoiline kana kwamba alikuwa akijua kile Roma anachowaza.
“Nani anajali sasa , Roma ichukue tu hio ngoma , inaonekana imekaa kipweke pweke hapa sio vizuri kuiacha”Aliongea Xiao na kumfanya Roma kushangazwa na fikra za msichana huyo mdogo , ni kweli ilionekana kuwa na nguvu ijapokuwa alikuwa na Dhana zenye nguvu lakini kama angekuwa nazo nyingi ingeleta faida.
“Mimi situmii Dhana hivyo unaweza kuichukua tu lakini unpaswa kufikiria mara mbilimbili , ukishaiondoa hapo kuna uwezekano huu mara ukakosa tena radi ya zambarau kitu kinachomaanisha kwamba majini pepo wote wataweza kutoka”Aliongea Aoiline mara baada ya kuona Roma anamwangalia.
“Hata mimi naona , haishangazi wale majini pepo walisema Hazina yao ni njia ya kufufua watangulizi wao kumbe walikuwa wakimaanisha kuruhusu majini pepo waliofungiwa huku kurudi katika ulimwengu wa kawaida , nawaza kama kweli nitaiondoa hii Dhana na kuruhusu watoke si watakuja kuwafyeka binadamu”
“Kama ndio alivyosema basi upo sahihi , maana hii ngoma ndio kizuizi kikubwa cha majini pepo kutotoka katika huu mnara kutokana na radi yake”Aliongea Aoiline na kumfanya Roma sasa kuona ashafumbua kitendawili kilichokuwa kikimsumbua muda mrefu.
Wakati Roma akiendelea kufikiria kuhusu ngoma hio kuichukua au kuiacha hapo hapo upande wa Aoiline alionekana kuona kitu na alipaa mpaka juu kabisa ya ngoma hio na palepale waliweza kuona maandishi ya rangi ya Dhahabu ambayo yalikuwa yakin’gaa.
Ilionekana ni maandishi ambayo yalikuwa yameachwa hapo makusudi kabisa.
“Ni maandishi gani hayo?”Aliuliza Roma mara baada ya kumfikia Aoiline.
“Huu ni mfumo adimu wa ki uandishi wa enzi za kale , vitabu vyetu vyote ambavyo tunatumia sisi majini tunatumia maandishi ya namna hii , ni binadamu wachache sana wanaojua huu mfumo wa ki uandishi kutokana na ugumu wake na ilivyokuwa ngumu kuukariri lakini angalau bado naweza kusoma”
“Kama ni hivyo haya maneno maana yake ni nini?, au ni mbinu ya kuvuna nishati?”Aliuliza Xiao.
“Ni maandiko ambayo yanaelezea muunganiko kati ya ulimwengu wa majini pepo , mnara wa anga , ulimwengu wa jicho la anga na safu ya ulinzi wa Gereza la roho”Aliongea na kumfanya Roma kutaka kudondosha mate kutokana na mshangao mara baada ya kusikia gereza la roho limehusishwa.
Alikuwa akikumbuka kabisa gereza hilo lilikuwa katika miliki ya majini wa Hongmeng katika kisiwa cha anga inakuwaje kukawa na muunganiko na mnara huo pamoja na ulimwnegu wa majini pepo na ulimwengu wa jicho la Anga.
Aoiline hakujali mshangao wa Roma na alianza kutafsiri maneno mwanzo mwisho.
Kwa maelezo yake ilionekana kwamba ulimwengu wa jicho la anga , ulimwengu wa majini pepo , mnara na gereza la roho vyote vilitengenezwa na wajumbe wa Mkuu wa Enzi licha ya kwamba ilionekana hakuna uhusiano kati yao.
Miaka elfu arobaini iliopita , ili kuweza kufungia majini pepo na mashetani wa anga wengi , wajumbe wa mkuu wa enzi walitengeneza gereza la roho.
Lakini hata hivyo walikuja kugundua kwamba majini pepo na mashetani walikuwa wengi sana na walikuwa wakizidi kuleta ukinzani ndani ya gereza la roho kitu kilichopelekea kiwango kikubwa cha nguvu hasi kuongezeka na kama ingeendelea ilimaanisha safu ya ulinzi wa gereza ingedondoka.
Hivyo mara baada ya kutafuta suluhu walikuja kufanya maamuzi ya kutumia ulimwengu wa jicho la anga na ulimwengu wa millenia wa majini pepo.
Kutokana na tabia ya ulimwengu wa jicho la anga na ulimwengu wa majini pepo waliweza kuona ni mahali sahihi kwa ajili ya kufyonza nguvu nyingi hasi kutoka katika Gereza la Roho.
Hivyo hao wajumbe waliingia kazini na kuchokonoa safu ya ulinzi wa gereza la roho na kuruhusu kiwango kikubwa cha nguvu hasi yaani ile ya giza kuelekea katika ulimwengu wa jicho la anga na kwa kufanya hivyo waliweza kutatua tatizo ambalo lilikuwa likikumba gereza la roho.
Lakini hata hivyo ulimwengu wa jicho la anga kama ungeendelea kupokea kiwango kikubwa cha nguvu hasi ilimaanisha siku moja ungezidiwa na kungetokea matokeo hasi na ili kukinga tukio la namna hio walitengeneza mfereji wa anga ambao unaunganisha ulimwengu wa jicho la anga na ulimwengu wa majini pepo kupitia mnara.
Mfereji huo waliotengeneza ndio shimo sasa ambalo Roma na Xiao walipitia , kwa lugha nyepesi ni kwamba hao wajumbe wa anga ndio walitengeneza lile shimo na kazi yake ilikuwa ni kwa ajili ya kuzuia kujaa kwa nguvu hasi katika ulimwengu wa jicho la anga na kusababisha matatizo.
Hivyo kiasi kidogo cha nguvu za giza kilikuwa kikitoka katika ulimwengu wa jicho la anga na kisha kuingia katika ulimwengu wa majini pepo , na kiasi cha nguvu hizo ndio kilitumika kuwazuia majini pepo waliokuwa ndani ya ulimwengu huo kutoweza kutumia uwezo wao wote kutokana na kwamba hakukuwa na uwiano wa nishati zote mbili yaani ile hasi na chanya kama ilivyokuwa katika ulimwengu wa kawaida.
Lakini hata hivyo ilionekana haikuwa ikitosha kuwazuia majini hao ambao ni waharibifu , hivyo walitengeneza njia moja tu ya kutoka katika ulimwengu wa majini pepo ambapo ni mnara na ili kutowaruhusu majini hao kutotoka kirahisi walitumia Dhana ya ngoma ya Naoni kwa ajili ya kuachia mapigo ya radi kama kizuizi cha kutotoka.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba Dhana hio ya Ngoma kazi yake ilikuwa ni kubadilisha nishati yoyote ile aidha iwe ni chanya au hasi na kugeuka kuwa radi kila inapodunda.
Na kwa mantiki hio ilifanya ulimwengu wa jicho la anga , gereza la roho ambalo lipo Hongmeng na ulimwengu wa jicho la anga kuunganika pamoja.
Kazi kubwa ya mnara ilikuwa sio njia tu lakini pia ilikuwa ni kuzuia ile nguvu hasi kutoingia katika ulimwengu wa majin pepo moja kwa moja ili kuepusha kuharibu mazingira ndio maana ulimwengu wa jicho la anga ni tofauti na ulimwengu wa majini pepo kwani mnara ulikuwa ni kama chujio.
Roma sasa mara baada ya kusikiliza maelezo hayo akiwa na Xiao walijikuta wakishindwa hata kusogea inchi.
Kwahio lugha ambayo ilikuwa ipo katika Dhana ya Shoka na hapo kwenye mnara ni lugha ambayo ilitumiwa na hao wajumbe wa mkuu wa Enzi.
Roma mara baada ya kuisikia stori hio kutoka kwa Aoiline alijikuta ni kama vile haamini , haikuwa kwake tu hata kwa Xiao.
Ukweli kwa mfano Xiao alikuwa amesoma vitu vingi ambavyo vilikuwa vikihusiana na wajumbe wa mkuu wa enzi na kwao ilikuwa ni kama motisha kuweza kuwazidi hao wajumbe.
Roma haikuwa mara yake ya kwanza na ukweli ni kwamba kwa mara ya kwanza akili yake inafunguka juu ya kazi kubwa ambayo ilifanywa na Wajumbe wa mkuu wa Enzi kwa ajili ya kuifanya dunia sehemu salama kwa binadamu.
Ile raha yote ambayo alikuwa nayo kwa kuweza kupitia radi ya rangi ya fedha ilikuwa imepotezwa na mshangao wa tafsiri ya maandishi ya lugha ya wajumbe wa mkuu wa enzi.
“Kama ulichosema ni sahihi , hawa Wajumbe hawakuweza kuwa na wasiwasi juu ya watu kuiba hii ngoma na kisha kuwaruhusu majini pepo na mashetani , si mababu wa miliki ya Braki walikuja mpaka hapa na kisha wakaondoka na ufunguo ambao ni hazina?”Aliuliza Roma.
“Ndio nini sasa kama watafanya hivyo , hii ndio kazi ambayo waliona wanaweza kufanya katika wakati huo kwa ajili ya kulinda viumbe na dunia kwa ujumla , kuhusu kuibiwa nina uhaika lazima walifikiria kuhusu hilo , ninaweza kukuambia kitu , huyo unaemwita mtangulizi wa miliki ya Braki pengine alikuja kweli lakini alishindwa kuchukua hio ngoma na sababu ya kushindwa hata kama nikikuambia hutoelewa”Aliongea Aoiline.
“Nini tena , kwanini unatuacha hewani sisi sio watoto”Aliongea Xiao ambaye alikuwa akifuatisha maongezi kwa umakini mkubwa.
“Dogo nina umri wa miaka elfu hamsini , kwa umri wako hakika una ujasiri wa kuuliza maswali”
Aliongea Aoiline huku akimfinya Xiao shavu mara baada ya kuona anamletea u’cute.
Upande wa Roma aliona Aoiline alikuwa akimficha mambo mengi sana lakini aliamini ilikuwa haina maana hata kuuliza.
Kwa mfano alijua pemgine kuna maandiko mengi ambayo yameachwa na hao wajumbe wa mkuu wa enzi katika huo mnara lakini kwasababu asingeelewa lugha yao aliamua kumuamini tu.
Licha ya sababu zote Roma hakutaka kujali kwanini mnara huo wa anga umefungika .
Ukweli ni kwamba mnara huo ulitengenezwa ili muda wote kuwa wazi na kuvuta majini pepo wote ambao wapo katika ulimwengu wa kawaida , lakini kwasababbu ufunguo wake ulitolewa katika kile kisahani basi ulijifunga na hii yote ni kutokana na kukosa nishati hasi ya kutosha.
Kutokana na hilo mnara huo hukusanya nguvu kidogo kidogo katika muda wa miaka sitini na pale inapotosha sasa ndio hufunguka.
Sasa mara baada ya Roma kurudi na funguo yake ambayo ni ile hazina sasa inamaanisha kwamba mnara huo umefunguka upya kama ilivyokusudiwa.
“Hey , Dhana ya ngoma ipo mbele ya macho yako kama unaitaka kuichukua ichukue , maamuzi yapo juu yako”Aliongea Aoiline.
“Kwahio unaniambia nichague , wewe hutaki majini wenzio wakitoka katika huu ulimwengu?”
“Kwanini niwaruhusu watoke , mimi nimeondoka kutokana na uwezo wangu mwenyewe hivyo hawawezi kunilaumu”Aliongea na kumfanya Roma kufikiria kwa muda.
“Kama sitowaruhusu watoke itakuwa ngumu kujielezea mbele ya majini wa Braki , ila sijali , kama hata wewe mtangulizi wao hujali kwanini mimi binadamu nijali , hawawezi kunifanya chochote hivyo naiacha hapa hapa”Aliongea Roma akimaanisha haichukui hio ngoma.
“Kwanini? , unapaswa kujua ukishaichuku mamia ya majini pepo na majini shetani wa anga watakuwa na deni kubwa kwako na kama wakitoka katika ulimwengu wa kawaida watakuwa katike levo za mapigo ya radi ya Zambarau au hata Rangi fedha”Aliongea akimaanisha kwamba pengine wanaweza kumsaidia Roma katika vita yake.
“Itasaidia nini ili hali ulimwengu upo katika machafuko , kwasasa sitaki kuongezea matatizo ijapokuwa nimeua watu wengi lakini siwezi kuwafanya binadamu waaanze kuwaza tena kuhusu kuuliwa”
“Basi inasikitisha , nilijua utaichukua kutokana na matatizo yanayokuongojea”Aliongea Aoiline.
Mwishowe Roma aliacha ngoma kama ilivyo kwa ajili ya kuendelea kukusanya radi na kuwaadhibu majini pepo ili wasitoke.
Baada ya kuachana na maswala ya Ngoma wote kwa pamoja walianza kutafuta njia ya kutokea na walikuja kupata njia hio karibu na mfereji wa kuelekea katika ulimwengu wa jicho la Anga na bila kujiuliza mara mbili mbili kila mmoja aliingia na kupotea.
Macho yao yaliingiwa na ukungu kwa sekunde lakini uliisha na hatimae walianza kuona namna dunia ilivokuwa imebadilika , kila kitu kilionekana kufunikwa na theluji.
Walikuwa wametokea sehemu ileile , katika eneo la Dehebu la Shushani katika milima ya Emei na kwa wakati huo ndani ya eneo hilo hakukuwa hata na kuku anaetambaa, yaani ki ufupi eneo lote lilikuwa limetelekezwa na theluji ilikuwa imefunika matemple mpaka kufikia nusu.
Dakika hio Roma vinyweleo vyake vilisimama , huku moyo wake ukizama mara baada ya kugeka na kumwangalia Aoiline.
Ilikuwa ni kama vile ameshikiliwa hewani na anapitishwa katika anga karibu na vilele vya milima kwa kasi kubwa sana.
Mbweha wa mikia tisa hakuonekana tena yule mwanamke mrembo badala yake ni kama vile ameongezeka ukubwa katika viwango vya juu sana , ilikuwa ni kama vile ni mungu wa kike wa vita.
Kilichomuogofya Roma zaidi ni kwamba nguvu ambayo ilikuwa ikimvaa Aoiline ni kama vile haikuwa na Kikomo.
Upepo uliokuwa ukivuma haukuwa wa kawaida kabisa na ajabu ni kwamba mwanamke huyo hakuna alichokuwa akifanya , alikuwa amesimama tu na mabadiliko hayo ndio ambao yalikuwa yakitokea mwenyewe kama vile dunia inamlaki.
Ijapokuwa Roma alikuwa na uwezo wa kutumia andiko la urejesho lakini hawezi kusababisha kitu cha namna hio kwa kutokeza tu katika dunia.
Kama angeweza kuweka maelezo hayo katika maneno ni kama vile Aoiline alikuwa ni Zaidi ya nguvu za nishati za mbingu na ardhi.
Cha kushangaza ni kwamba mnara uliokuwa eneo hilo haukushituka kabisa kutokana na mabadiliko hayo.
Baada ya dakika kadhaa za nguvu zake kumrudia hatimae alitoa tabasamu ambalo licha ya kuwa zuri lakini linamfan ya yoyote anaemwangalia kumuogopa.
Roma wakati wa mabadiliko hayo alikuwa amemkinga Xiao na msuguano wa nguvu za Aoiline na kama asingefanya hivyo angedondoka kutoka hewani kwani nguvu aliokuwa akitoa Aoiline ni kama vile anga halikuwa likimtosha.
“Mniwie radhi , nishasahau nguvu zangu zitaongezeka mara baada tu ya kutoka”
Mara baada ya kuongea tu hatimae amani ilirudi kana kwamba hakuna kilichotokea na kumfanya Roma kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha.
“Wewe… inamaana ni robo tatu ya uwezo wako ulifungiwa katika ulimwengu wa majini pepo?”Roma aliuliza kwa mshangao kwani Aoiline uwezo wake uliongezeka kwa zaidi ya mara tatu zaidi nje ya mategemeo yake.
“Ukishafikia katika levo flani utakuja kuelewa nisingeweza kupigana na Lekcha kwa mwaka mzima kama ningekuwa dhaifu , mimi ndio niliharibu Dhana yake ya mfupa wa damu ya Dragoni , unapaswa kuelewa ulimwengu wa majini unatufungia nguvu zetu kwa namna tofauti tofauti ,hiyo nakubali kwamba mimi ndio uwezo wangu ulishikiliwa kwa kiwango kikubwa kuliko wengine wote, lakini usijali sina ugomvi na wewe wala binadamu…”Aliongea na kumfanya Roma kupagawa.
Kwa levo ambayo alifikia Aoiline Roma hakuwa akimfikia hata kidogo kama angeshambulia.
Ukweli ni kwamba aliamini kuna uwezekano hata Athena anaweza asimfikie Aoiline , lakini hayo yote ni makisio tu kwani upande mwingine Athena haikujulikana uwezo wake ni levo ipi.
Lakini alikuwa na uhakika Aoiline alikuwa ni juu ya levo ya mapigo elfu tisa mia tisa tisini na tisa na kwa Roma yote hayo yalikuwa makisio tu kwani hakuwa akijua levo ya mapigo elfu kumi kasoro moja yapoje.
“Kwanini kuna baridi sana?”Xiao ambaye alikuwa akiangalia mazingira yalivyoganda aliuliza kwa shauku kwani mara ya mwisho alivyoiona dunia ni tofauti na alivyokuwa akiona kwa wakati huo.
Kutokana na baridi iliokuwa ikiendelea katika maeneo ya mwambao wa Kaskazini hata kama ni kiumbe kutoka sayari nyingine akifika lazima utajua hilo baridi na barafu sio la kawaida.
Upande wa Roma aliweza kuhisi namna ambavyo uungu wake ulivyoimarika , yaani pengine kama atatumia kanuni za anga basi levo yake inaweza kufanana na jini aliepitia mapigo tisini na tisa ya radi.
“Moyo wa gaia unazidi kuleta usumbufu”Roma aliwaza.
“Inaonekana ni kweli kuna tatizo kubwa limejitokeza katika huu ulimwengu lakini haya hayanihusu , dogo nataka kuonana na wana ukoo wenzangu ongoza njia”Aliongea Aoiline.
“Nataka kumpeleka Xiao kwao kwanza na kumaliza kinyongo kati yangu na Anjiu , kiongozi wa ukoo wako watakuwa kwenye miliki yangu, kama vipi nifuate na baada ya hapo tutaelekea huko pamoja”Aliongea Roma.
“Hakuna shida , sijakuwepo kwenye huu ulimwengu kwa miaka elfu hamsini , sio mbaya kama utanipeleka kwenye baadhi ya maeneo ya kushangaza nifurahi”Aliongea akiwa na tabasamu na kwa wakait huo alirudi katika hali yake ya kawaida akipotezea ule ukuu wake.
“Roma nakukumbusha tu uliniahidi mwenyewe hutomuua baba yangu na utapatana nae”Aliongea Xiao .
“Lini nilikuahidi mimi”Roma aliwaza kwenye kichwa chake.
“Hio haipo juu yangu , kama baba yako atakubali kufunika Kombe mengine yatafuatia”Aliongea Roma.













SEHEMU YA 772.
Roma alikuwa ashapanga kumsamehe Anjjiu kutokana na kwamba alikuwa na mahusiano na Master yake Magdaena lakini ilitegemeana na Anjiu mwenyewe kama atakuwa tayari kujali maswala yake na aachane na yeye.
Roma hakuwa na mpango wa kuamini maneno ya Anjiu moja kwa moja na alitaka kutafuta namna ya kuhakikisha nia yake akishafka huko.
Ijapokuwa alikuwa ameikumbika familia yake sana , lakini aliona ngoja kwanza adili na hilo.
Wakati wakisafiri Roma aliweza kuona namna ambavyo Dhoruba ya Theluji ilivyokuwa tishio kwa dunia , kila kona katika maeneo ya miinuko kulikuwa na baridi kama vile ni bara la Antarctica.
Hali hio ilimfanya Roma kukunja sura huku upande wa Aoiline muonekano wake ulibadilika kidogo kama vile alikuwa akishangaa namna ambavyo dunia imebadilika nje ya mategemeo yake.
“Inaonekana ukubwa wa tatizo lako sio wa kupuuzwa”Aliongea Aoiline kwa kutania.
“Hili sio tatizo kwangu lakini ni tofauti sana kwa binadamu wa kawaida”Aliongea Roma.
Haikuwachukua muda mrefu kuingia katika ulimwengu wa majini watu na kuelekea moja kwa moja katika miliki ya Xia.
Kutokana na uwezo wa Roma pamoja na wa Aoiline ilikuwa ngumu kuingia katika ulimwengu huo bila kushitukiwa , kwani mmoja alikuwa katika levo ya mapigo mengi ya radi na mwingine pengne alikuwa ni zaidi ya mapigo mengi ya radi.
“Roma hivi unadhani baba yangu atakubali tuwe wapenzi , vipi kama atakataa tutafa…”Aliongea Xiao mara baada ya kuona wanakaribia na kwao lakini kabla hata hajamaliza kauli yake Roma alikuwa tayari ashamzimisha na kumfanya Aoiline kumwangalia na tabasamu la uchokozi.
“Wewe mtukutu , mpenzi wako mpya wa awau hii naona ni muwazi wa hisia zake sana , kwanini sasa umemzimisha huo ni ukatili jamani haha..”
“Yaani huwa nashindwa kuelewa uwezo wake wa kufikiria upoje. Sikumbuki kumuahidi chochote wala hakuna kilichotokea baina yetu lakini tayari ashafikiria kuwa na mimi kimapenzi , niliambatana nae kwasababu ya huruma zangu tu , vinginevyo ningeshawaua wote”
“Tsk .. tsk damu nyingi ipo mikononi mwako , hio haiendani na sheria za mbingu na ardhi ujue”
“Tofauti ipo wapi , unadhani sheria zitakuwa na maana kama nitakuwa na uwezo wa kutawala namna mbingu na ardhi inavyofanya kazi…”Aliongea lakini palepale rabasamu lake lilipotea mara baada ya kuhisi kitu
Alikuwa ni Aoline aliesababisha hewa kubadilika , kwani Roma mara baada ya kugeuka aliweza kumuona akichana nywele zake kama vile hakuna kilichotkea ila ukweli kuna kitu alimfanyia.
Unaweza kuona ni hali ya kawaida lakini kwa namna ambavyo Roma alikuwa akihisi haikuwa kawaida kabisa , ilikuwa ni nje ya ufahamu wake.
Roma aliishia kumeza mate mengi akijitahidi kujituliza kutokana na muonekano wa Aoiline.
Upande wa Aoiline alionekana kumwangalia Roma na palepale aliwaza na kujiambia huyu mtoto nafasi anayo.
Kufumba na kufumbua walikuwa washafika katika miliki ya Xia kwa juu na Roma alimuomba Aoiline kumshikilia Xiao kwanza kutokana na kwamba hakuna mtu yoyote atakaeweza kuwaona kutokana na uwezo wake.
Roma mara baada ya kumkabidhi Xiao kwa Aoiline yeye alichukua kile kidani na kisha kwa kutumia Dhana yake ya jani la upofu alirekebisha uwezo wake katika levo aliokuwa nayo kabla ya kwenda katika ulimwengu wa jicho la anga na kisha alishuka katika miliki ya majini hao.
Dakika tu mara baada ya mkandamizo wake kuweza kuhisiwa , kundi kubwa la majini walijitokeza kutoka pande zote na kati yao kati ya kumi na tano walikuwa katika levo ya maji ya upako.
Lakini hao wote hawakupewa kipaumbele kwani katika miliki hio kulikuwa na Anjiu na baba yake ambao wote walikuwa juu zaidi katika kuipita Dhiki ya radi.
Anjiu alimkagua Roma kwanzia chini mpaka juu na mara baada ya kuona hana majeraha yoyote wasiwasi ulimvaa
“Binti yangu yupo wapi?”
“Eeh .. nilidhani utaniuliza kwanza ni wapi nilienda na kwanini nipo hapa?”Aliongea Roma mara baada ya kuona Anjiu anachojali ni binti yake tu.
“Hayo ni maswala kati yangu na wewe .. nataka kujua yu wapi binti yangu?”Aliongea kwa mara nyingine huku sauti yake ikizidi kuwa nzito.
Roma akiwa katika hali ya huzuni alitoa kile kidani na kisha akamrushia Anjiu na mara baada ya kukipokea alikiangalia na kisha akasema;
“Hiki kidani nilimpatia XiaoXiao kwanini upo nacho wewe?”
“Bila kujua tulijikuta tukivutwa kwenda katika ulimwengu wa jicho la anga , unapaswa kuelekwa kwamba katika ulimwengu huo kuna kundi kubwa la roho za giza za kimashetani , ingawa hazina madhara kwangu lakini upande wa binti yako uwezo wake ulikuwa mdogo sana na wakati nilipokja kumpata alikuwa amepoteza kiasi kkuwa cha nguvu ya uhai wake na alikuwa akikaribia kufa..”
Roma mara baada ya kuongea hivyo Anjiu alifubaa palepale huku macho yae yakianza kubadilika , akiwa anaangalia kidani hicho alianza kutngisha kichwa chake kwa nguvu kana kwamba hakuwa akimwamini Roma.
“Unaongea upuuzi , kwa ukubwa wa nguvu zango za mbingu na ardhi umeshindwa vipi kumlinda binti yangu”
“Hakukuwa na kitu ambacho ningeweza kufanya kwa wakati huo , sikuwa na kidonge cha aina yoyote kwani sikuwa nikitembe navyo , nilichoweza kufanya ni kurefusha maisha yake kwa dakika kadhaa lakini kutokana na kupoteza damu nyingi ilishindikana kumuokoa”
“Kimya ! , Utakuwa umemuua binti yangu wewe , si ndio?”Anjiu alibweka huku macho yake yakianza kutoa machozi , hakuonekana tena kama mkuu wa mmiliki bali alionekana kama baba anaemlilia mtoto wake.
Upande mwingine pasipo ya kujua katika kizuizi chenye nguvu alichotengeneza Aoiline Xiao alikuwa ameamshwa na Aoiline
Hayakuwa maagizo ya Roma lakini alijiamulia yeye mwenyewe kumwamsha Xiao ili aone kile kinachoendelea.
Mwanzoni Xiao hakuelewa nia ambayo Roma alikuwa nayo lakini mara baada ya kuona namna baba yake alivyokuwa katika majonzi alishindwa kujizuia na kuanza kulia na yeye.
Alitamani kuruka na kwenda kutua chini na kumwambia baba yake alikuwa hai lakini alikuwa ameshikiliwa vizuri na Aoiline kiasi cha kushindwa hata kufurukuta.
Roma alikuwa vizuri sana katika maigizo kwa namna ambavyo alikuwa akionyesha uso uliojaa huzuni usingekataa kabisa maneno yake.
“Haijalishi tena kama unaniamini au lah lakini Xiao amenipatia hiki kidani kabla ya kupoteza maisha na aliniambia alikuwa na jina la utani la Leilei ikimaanisha ulikuwa ukimpenda sana kuliko hata kaka yake na wewe sio mtu mbaya , ameniusia kwamba unapaswa kuacha ugomvi wako na mimi kwasababu hataki kukuona ukipoteza maisha”
Kabla hata hajamaliza sentensi yake Anjiu alikuwa akitetemeka mno huku akishikilia kile kidani kwa nguvu , ilionekana ni kama vile anapatwa na ukichaa.
Alijitahidi kuzuia machozi yake kudondoka kutokana na kwamba kulikuwa na watu wengi waliomzunguka lakini hata hivyo muonekano wake ulifanya wengi wamuonee hurum na kumsikitikia.
“Unapaswa kujua mpaka sasa mimi siwaogopi kama mnataka kupigana na mimi , kama sio kwa Rufi na mimi kutokuwa na deni kwa Xiao nisingeyachukulia maneno yake siriasi lakini kwasasa nipo tayari kutimiza wosia wake ukizingatia kwamba wewe na wana ukoo wako wote hamna uwezo wowote wa kunishinda , mnapaswa muelewe sina matamanio ya kusumbuka kuja mara kwa mara kwenye huu ulimwengu wenu wala sina matamanio na maswala ya nani ana nguvu kuliko nani , watu wangu na mimi mwenyewe tuna maisha mazuri tu ya kutohitaji kitu kingine”
Roma mara baada ya kuongea maneno hayo majini walioweza kumsikia walikumbwa na hali ya furaha.
Hawakuwa majasiri kama ilivyo kwa Anjiu na walitamani kuishi muda mrefu , isitoshe haikuwa rahisi kufikisha nguvu zao katika levo hizo hivyo hawakutaka kushiriki katika vita ambayo matokeo yake yanajulikana.
Ndani ya dakika macho yote yalimwangukia Anjiu ili aweze kufanya maamuzi , hata baba yake Chaopi hakutaka kumuingilia mtoto wake lakini kwa muonekano wake ilionekana ni kama vile yupo tayati kutotaka ugomvi na Roma , lakini hata kama akiamua kwamba ni vita asingekuwa na jinsi kwani ndio mkuu wa miliki.
Baada ya dakika kadhaa za Anjiu kuwaza alijitahidi kujirudisha katika uwezo wake na kuachana na ubaba kwanza na kuwa mkuu wa miliki na alivuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha akamwangalia Roma kwa kumchunguza.
“Uwezo wako umeongezeka kwa kiasi kikubwa sana , kwanini bado unauficha wakati unao uwezo wa kuweka dunia yote chini yako?”
Roma hakuwa ndie alieshangaa tu kutokana na maneno ya Anjiu bali hata Chaopi mwenyewe alikuwa katika mshangao.
Roma akiwa amekunja sura alijikuta akijiuliza Anjiu amejuaje uwezo wake umeimarika zaidi na zaidi.
“Ulikuwa mshindani wangu mkubwa hivyo nakujua vizuri nje ndani , ijapokuwa inaonekna kama vile upo levo ileile lakini msisimko wako umebadilika mno tofauti na mwanzo na hali ya kujiamini katika macho yako imeongezeka pia , nina uhakika ni mimi pekee ambaye ninaweza kuona vitu vidogo kama hivyo”
“Umesema ulikuwa mshindani wangu , kwahio unamaanisha..”
“Ninakataaje wosia wa binti yangu , isitoshe sitaki kilichotokea Panas kijirudie hapa”Aliongea Anjiu
Ukweli ni kwamba alikuwa bize kuvamia miliki nyingine na kuziweka chini yake kwa msaada ya wanajeshi wake wa kitengo cha Taisha lakni kutokana na habari mbaya iliomfikia ni kama mafanikio yake ni nusu tu.
Alitaka mafanikio yake kuyasherehekea akiwa na binti yake lakini ndio hivyo hakuwa akipatikana popote na taarifa zinarudi akiwa amefariki.
Katika kipindi chote ambacho Xiao alikuwa amepotea alikuja kugundua kuna vitu vingine havikuwa na umuhimu sana kama ilivyo kwa binti yake na alitamani anga limshangaze kwa binti yake kurudi akiwa hai lakini hata hivyo alikuwa amekwisha kuchelewa.
Sasa Roma mara baada ya kujihakikisha hana ugomvi tena na Anjiu alishuha pumzi za ahueni na palepale aligeuza shingo yake juu.
“Nishamaliza , unaweza kumleta sasa”
Aliongea Roma na wakati wakiwa katika hali ya mshangao wa maneno yake , uono mbele ya macho yao ulijaa ukungu mara baada ya mwanamke ambaye alikuwa na uzuri usiokuwa wa kawaida kusimama katikati yao.
Aoiline alikuwa amemshikilia Xiao ambaye alikuwa akilia kwa kwikwi kutokana na kumuonea huruma baba yake.
Chaopi na Anjiu walikuwa katika hali ya mshangao mara baada ya kugundua wameshindwa kujua uwepo wa mtu mwingine ambaye alikuwa akiwaangalia kutoka juu tena zaidi akiwa na mtu mwingine , palepale mawazo yao yaliwaambia lazima mtu huyu atakuwa na uwezo wa juu sana wa nishati ya mbingu na ardhi.
“Dad!!”
Xiao mara baada ya kauchiwa alimrukia baba yake kwa furaha
“Xiao wewe mtoto si ume…”
Xiao alikuwa katika furaha ya juu hakujali mshangao wa watu waliokuwa wakimwangalia na aliishia kumchafua baba yake na mate kutokana na kumbusu wa pupa.
Mpaka wakati ambao Anjiu akili ilimrudia alikuja kugundua namna ambavyo binti yake alikuwa akimtia aibu mbele za watu.
“Unafanya nini , hebu acha kunibusu”Alibweka na kufanya waliokuwa wakimwangalia kuangua kicheko.
“Dogo umefanya kazi nzuri awamu hii , nilidhani unachojua ni kupigana tu”Aliongea Aoiline
“Una mengi ya kujifunza kutoka kwangu bibie.. tuondoke zetu sasa hili tushalimaliza”Aliongea Roma na palepale yeye na Aoiline walipotea.
Xiao mara baada ya kurudi katika akili yake alikuja kugundua Roma amemuacha tena na aliishia kung’ata meno yake kwa hasira huku akiliita jina lake kwa hasira.
“Roma wewe mshenzi umenitoroka tena , ila nitakutafuta tu na tutaendeleza tulipoishia”
Xiao aliambiwa aeleze kilichotokea na alielezea kwa namna ambayo ilikuwa ni kama vile anataka kumuaminisha baba yake kwamba Roma ni Husband Material na anafaa kuolewa nae maana sio kwa kuongeza chumvi.
*******
Roma mara baada ya kutoka ulimwengu wa kijini hakuelekea moja kwa moja visiwa vya wafu , kutokana na mambo mengi yaliotokea na alichoshuhudia katika ulimwengu wa majini watu alijikuta akimkumbuka mama yake sana hivyo safari yake ilikuwa ni kuelekea Tanzania kwanza.
Kutokana na kwamba alikuwa na mengi ya kumwambia Aoiline njiani walitembea mdogo mdogo.
Ukweli ni kwamba hali ya dunia ilikuwa ikisikitisha mno , kila Kona ilikuwa ni barafu tupu , sehemu pekee ambayo ilikuwa na unafuu ni ndani ya bara la Afrika katika baadhi ya maeneo tu.
Yaani kwa wakati huo ni kama vile maafa yanatokea upande wa kaskazini na kusini na yanaelekea katikati mwa dunia.
Katika hali kama hio ni raia wa vipato vya chini ndio waliokuwa wakiteseka mno kwani matajiri wengi walikuwa wamehamia katika maeneo ambayo yana joto mathalani katika bara la Afrika sehemu pekee yenye unafuu zaidi na baadhi ya nchi za kilatini.
Dakika chache tu waliweza kufika nchini Tanzania na ukweli ni kwamba Afrika mashariki yote na kati kwenda Ethiopita na Sudani huko hali ya hewa ilikuwa nzuri kabisa , ijapokuwa haikuwa ya joto sana lakini hakukuwa na mabadiliko makubwa.
Kitu pekee kilichobadilika ni wingi wa watu , ilikuwa ni kama vile dunia yote imekutana sehemu moja kwani kila rangi ilionekana , iwe ni wahindi , waarabu , wazungu , wachina , wakorea , wayahudi na makabila mengine yalionekana.
Miundo mbinu ilikuwa ikirekebishwa kwa kasi sana ndani ya miji na shughuli za kibinadamu zilikuwa ni za juu mno , ilikuwa ni kama vile binadamu wote washajua hapo ndio eneo ambalo litakuwa salama kwa wakati wote.
“Hii ndio sehemu pekee tu ina unafuu na mazingira yake yanavutia kweli”Aliongea Aoiline aliekuwa akishangazwa na mazingira.
Roma hakuwa na mudi hata ya kumsikiliza porojo zake kwani ni kama vile Aoiline hakuwa akijali kinachoendelea.
Wakati huo alikuwa tayari ashamtafuta mama yake katika anga la Dar es salaam na kilichomfurahisha aligundua mama yake yupo sehemu moja na babu yake Afande Kweka.
Roma alimpa ishara Aoiline ya kumfuata kukutana na ndugu zake na mrembo huyo hakuwa na hiyana.
Alikuwa amevaa gauni rangi nyeupe la kitambaa cha hariri , ijapokuwa lilionekana kama la kitamaduni lakini lilikuwa limejaa urembo wa thamni ya hali ya juu.
Kufumba na kufumbua Roma na Aoiline walitua katia bustani ndani ya jumba la Afande Kweka maeneo ya Mapinga Bagamoyo.
Ilionekana familia yote ilikuwa hapo na hata wale watu ambao Roma hakuonana nao kwa muda mrefu walikuwepo.
Ashley mdogo wake , Madam Damasi mke wa raisi Senga , Raisi Senga Mwenyewe na baadhi ya waandamizi wa nchi walikuwepo hapo ndani , ilionekana kama kulikuwa na kikao flani hivi ambacho kilikuwa kikitamatika.
“Roma…!!!”
Blandina ndie aliekuwa wa kwanza kumuona Roma na kumkimbilia , alikuwa ashasahau kila kitu na kumkumbatia mwanae.
“Mwanangu hatimae umerudi , ulienda wapi jamani wewe mtoto mbona hutulii , upo sawa , umenipa mawazo na kuniogopesha , kwanini ulikuwa hupatikani kwa muda mrefu hivyo?”
Blandina na usomi wake alikuwa mama tu , pengine alikuwa ameathiriwa na kumpoteza Roma mara ya kwanza ndio maana alijikuta akiangua kilio.
ITAENDELEA
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI :SINGANOJR

Mono no aware.

SEHEMU YA 773.
Afande Kweka na familia nzima kwa ujumla ilikuwa katika hali ya furaha , hata Raisi Senga ambaye alikuwa ametulia muda wote alijikuta akikunja viganja vya mikono kwa namna ya kufurahi.
Hakukuwa na shaka kwamba wote walikuwa na wasiwasi mara baada ya kupotea kwa Roma.
Ukweli ni kwamba kwa kipindi chote hicho raisi Senga na Afande Kweka walikuwa wakitembelewa na watu wengi sana na wengi wao walikuwa ni viongozi wa juu wa nchi zilizoendelea ikiwemo China , Japani , India , Ufaransa na Marekani na wote hao walikuwa wakiulizia habari za Roma.
Katika wakati wa hatari kama huo binadamu wote matumaini yao waliyaweka kwa Roma kama muokozi wao.
Hata familia hio kukusanyika ndani ya eneo hilo ilikuwa ni katika kufanya ibada maalumu ya kumuombea Roma.
Raisi Senga kipindi cha nyuma alikuwa mzito sana pale linapokuja swala la Roma lakini katika kipindi cha muda mfupi alikuwa ameamka sana.
Pengine ni kutokana na kukosa mtoto wa kiume kwani katika uzao wake mrithi wake ambaye alikuwa akimuona kwa wakati huo ni Roma pekee kwani mke wake Damasi alikuwa ashapita katika wakati wa kuzaa tena.
Ashley licha ya kwamba alikuwa na akili na ni tegemezi lakini bado alikuwa ni mwanamke ambaye leo au kesho atataka kuanzisha familia yake na ukoo mwingine.
Roma moyo wake ulijisikia joto mara baada ya kuona namna ambavyo mama yake alikuwa akimngojea kwa mapenzi makubwa.
“Usilie mama yangu , nitakuelezea kila kitu , nipo sawa”Aliongea Roma akiwa na tabasamu , ilimchukua juhudi kumtuliza Blandina.
Sasa wote macho yao yalikuwa kwa Roma na ni wakati ambao waliweza kugundua kulikuwa na mwanamke mrembo wa kutisha alieambatana nae.
Ijapokuwa Aoiline alijitahidi kuuficha uzuri wake kwa kutumia nguvu za kijini lakini hakuacha kutamanisha kwa macho , ilikuwa ni ngumu kwa binadamu wa kawaida kutoa macho kwake.
Kwa bahati nzuri ni kwamba watu wote waliokuwa ndani ya eneo hilo sio wale wa kawaida , walikuwa ni watu walioelimika hivyo hawakumkodolea macho sana, hata hivyo ilikuwa ni kama imezoeleka kwani Roma alikuwa na wanawake warembo sana.
“Huyu dada ni…”
Blandina alimchukulia Aoiline kwa matamanio na kutokumkubali kwa wakati mmoja , aliotea pengine kupotea kwa Roma ni kutokana na kula bata na huyo mrembo.
Tabasamu la uchungu lilimvaa Roma na kwa haraka sana kusafisha hewa alimtambulisha Aoiline na kutokana na hali ilivyo Roma hakuona haja ya kuficha kama Aoiline sio binadamu bali ni jini ambaye alimsaidia sana kipindi cha mwisho alichopotea.
Pengine kwa familia za kawaida kama ungemtambulisha mwanamke kama huyo ni jini wangetimua nduki lakini Afande Kweka aliishi na Zenzhei mwanamke jini kwa muda mrefu sana na ilikuwa ni kama washaanza kuchukulia viumbe hao ni wa kawaida.
Bila shaka haikuwa kwa familia nyingine , ilikuwa kwa familia ya Roma tu ambayo sio ya kawaida ndio walioona mambo ni ya kawaida.
Afande Kweka alishangazwa mno mara baada ya kusikia huyo mrembo ni jini jamii ya mbweha wa mikia tisa ambaye ameishi umri wa miaka elfu hamsini , kutokana na urembo wake ilikuwa ngumu kwake kuamini.
Blandina hatimae lilimshuka mara baada ya kugundua Aoiline sio mpenzi wa Roma , vinginevyo hakujua ni kwa namna gani angeongea na mke mwana yaani Edna.
Aoiline ni kama hakuwa na ‘interest’ na maongezi ya binadamu na alikuwa bize kushika kitabu hiki na kile pamoja na vifaa vya kieletroniki kwa namna ya kuvishangaa.
Mara baada ya Roma kuelezea kila kitu katika safari yake ya ajabu hatimae kila mmoja alivuta pumzi lakini mtu kama Ashley na Damasi walikuwa katika hali ya mshangao mkubwa , hakuna ambaye alikuwa akiamini kulikuwa na ulimwengu mwingine lakini kwa namna moja simulizi ya Roma ni kama ilikuwa ikiwaambia kwamba kulikuwa na mbinguni au Akhera sehemu ambayo Mungu huishi hivyo kiimani Damasi aliimarika zaidi.
Upande wa Ashley yeye alikuwa ni mwanasayansi ,ijapokuwa hakushangaa sana lakini ni moja ya binadamu ambao wamejazwa na shauku ya kuthibitisha vitu kisayansi.
“Roma je Edna na wengine washafahamu umerudi?”Aliuliza Blandina.
“Hapana , nimekuja nyumbani kwanza mara baada ya kutokea ulimwengu wa majini watu”
Jibu lake lilimfanya Blandina kuwa na furaha na ile hali ya huzuni ilikuwa ishampotea kabisa , kwa Blandina Roma alikuwa ni mtoto tu haikujalisha anapitia mapigo mangapi ya radi au ni majukumu ya namna gani alikuwa nayo.
“Nilijua tu mtoto wangu una akili , nani angejua ungeniwazia mimi wa kwanza na kuja kunitembelea”Aliongea Blandina na kumfanya Roma kuona aibu kidogo maana mama yake alikuwa akimchukulia kama Lanlan na kitendo kile kilimfanya Aoiiline kuishia kucheka
Baada ya maongezi kidogo ya kutaniana ya hapa na pale Afande Kweka alichukua nafasi yake kuongea.
“Roma unapaswa kuwaambia umerudi mapema , maana kuna kitu kimetokea huko kisiwani wakati ukiwa haupo”
“Mhmh , inawezekana vipi , niliacha majini watatu wenye utaaalamu wajuu kulinda , sidhani kuna binadamu ambaye ana uwezo wa kuwashinda”Aliongea Roma akiwa amekunja sura.
“Hakuna alieumia , Princess Clark alichukuliwa na jeshi la umoja wa Ulaya na Marekani …”Aliongea Blandina na kuanza kuelezea kile kilichotokea.
Roma muonekano wake ulibadilika palepale , hakuwa akijali chochote kuhusu maswala ya Safina lakini alikasirika mara baada ya kumchukua Clark kinguvu licha ya kwamba walikuwa wakijua alikuwa ni mwanamke wake.
“Ashley sidhani kwa akili zako umeachwa hivi hivi tu , una projekti gani kwa sasa?”Aliuliza Roma.
Ukweli ni kwamba ni kama vile ameshikwa na hatia kwani alikuwa ni mdogo wake lakini walikuwa wakikaa pamoja mara chache sana , lakini hakupaswa kulaumiwa kwani Ashley alikuwa ni mtu bize hususani tokea atoke kwenye mikono ya Profesa Clark na kujitegemea katika maswala ya utafiti.
“Ashley kwa sasa yupo chini ya ya serikali katika utafiti wa maswala ya tiba”Aliongea Damasi.
“Unaweza kuambatana na mimi kuelekea kisiwani , Mwalimu wako amefungua maabara kule inaweza kukusaidia zaidi kama mtakuwa karibu”Alipendekeza Roma.
“Asante Bro lakini kwasasa nimeamua kujitegemea , ndio namna pekee ya kuonekana kuliko kuendelea kuwa chini ya kivuli cha Profesa”
“Mjukuu wangu yupo sahihi ni wakati wake wa kuifikiria Tanzania kwanza”
“Mzee unavyoongea ni kama vile mimi siifikirii Tanzania , anyway naona huku mmebarikiwa joto wakati nchi nyingi zikitaabika”
“Ni kweli lakini haimaanishi kwamba hatupo kwenye hofu , tafiti zinaonyesha mpaka miezi saba kupita kuna uwezekano na Afrika kuanza kuganda , sisi ni tofauti na wazungu na watu wa Asia kama hili likitokea inamaanisha tutaathirika zaidi kwani miili yetu haiendani na baridi kali”Aliongea Raisi Senga kwa mara ya kwanza na Roma aliishia kutingisha kichwa.
Wazungu wao wanasifika katika kuhimili baridi na miili yao imeumbwa kwa staili hio lakini upande wa Afrika wenyewe uwezo wao ni kustahimili joto, ndio maana mazingira ya uzunguni sio ya baridi sana wala ya joto sana hii ilimaanisha joto hata likishuka katika nyuzi sifuri tu Waafrika wengi wangepoteza maisha.
Maongezi yaliendelea kwa muda mfupi sana kabla ya Roma kuaga, maana alikuwa na hamu ya kuona familia yake na mtoto wake.
Wakati akitaka kutoka Afande Kweka alimsimamisha na kisha akamshika beganin.
“Mtoto kinachoendelea sio swala la utaifa bali ni swala la maisha ya binadamu , kadri nguvu zako zinavyokuwa kubwa ndo wajibu wako unavyokuwa mkubwa na kwasababu ya hili hakuna ambaye atakulazimisha kubeba majukumu yote , kama utajikuta upo njia panda , usiathiriwe na maoni ya watu na wewe fuata moyo wako kufanya maamuzi, hakikisha tu hujutii kwa lolote lile”Aliongea Afande Kweka.
Roma alijikuta akikaa kimya kwa dakika kadhaa akifikiria maneno yake na mwishowe alitingisha kichwa chake akionyesha kukubali.
Blandina aliishia kumpungia mtoto wake wa pekee kana kwamba alishaelewa kinachoendelea katika majukumu anayoenda kukabiliana nayo na aliishia kuwaangalia mpaka walipopotelea katika upepo wa macho yake na kuishia kufuta machozi.
*****
Katika eneo la visiwa vya wafu joto lilikuwa ni nyuzi sifuri kwa visiwa vyote na barafu ilikuwa imeifunika bahari lakini upande wa visiwani theluji ilikuwa kidogo sana.
Lakini hata hivyo miti mingi na mimea ilikuwa imekwisha kukauka tayari na kufanya kisiwa hicho kuonekana kama ardhi isiokuwa na kitu.
Upande wa wana visiwa walikuwa ndani ya nyumba zao na uzuri ni kwamba nyumba zao zilikuwa zimejengwa kwa ajili ya kutunza joto kwa kuchoma kuni na kuwasha AC.
Na bahati nzuri ni kwamba chakula walikuwa nacho kingi kama cha akiba hivyo hawakuwa na wasiwasi na maswala ya chakula.
Bi Wema , Sui na Qiang Xi wote walikuwa wamehamia katika makazi ya Roma ya ngome kwasababu kulikuwa na jenereta kubwa ambalo lilitosha kuzalisha kiwango kukubwa cha joto lakini pia ukubwa wa ngome hio uliwafanya kuishi bila shida yoyote.
Ijapokuwa Tanzania kulikuwa na joto lakinni waliona ni kheri kuendelea kuishi ndani ya kisiwa hicho wakimsubiri Roma kwani waliona ndio namna pekee wanaweza kuwa salama zaidi.
Sasa wakati huo wanawake hao walikuwa wamekaa katika meza ya chakula ikiwa ni nyakati za usiku , ijapokuwa chakula kilichokuwa kimeandaliwa hakikuwa cha kifahari kama ilivyokuwa kawaida lakini bado kilikuwa cha kutamanisha lakini kwa bahati mbaya wote walionekana kukosa hamu ya kula hivyo kumpa uwanja Lanlan wa kushughulika na share zao.
Lanlan alikuwa amekaa katikati na pembeni yake alikuwepo Edna ambaye mara kwa mara alikuwa akimfuta midomo kwa kutumia kitambaa na kisha kumlisha mboga za majini licha ya kwamba alikuwa akikataa, uwepo wa mtoto ndani ya familia hio ilifanya hali iwe ni ya amani.
“Edna dunia ndio inafika mwisho na Hubby hajulikani alipo , kwanini huonyeshi wasiwasi wa aina yoyote ile , hata Da’Neema ameshindwa kuvumilia na kinachoendelea na kwenda kufanya tahajudi kwenye basement , lakini wewe upo na amani kabisa na unamlisha Lanlan”Aliongea Mage ambaye uvumilivu ulimshinda kwani ni Edna pekee ambaye ni kama vile inachoendelea huko Duniani hakikuwa kikimuhusu.
Edna alimwangalia Mage na kutoa tabasamu hafifu na kisha hakutoa jibu na kuendelea kumlisha Lanlan mboga za majini.
“Miss Edna anaweza kuonekana hana wasiwasi lakini yupo kama wengine tu ni kwamba tu haonyeshi waziwazi kile anachojisikia , ndivyo alivyo”Aliongea Bi Wema akijaribu kumtetea.
Maneno yake yalifanya wengine wote kucheka , kutokana na kukaa na Edna kwa kipindi kirefu ni kama walijua hakuwa hivyo kwa makusudi bali ndio tabia yake.
Walimheshimu kwani kwa kipindi chote ambacho Roma hakuwepo ni kama ndio aliekuwa kiongozi.
“Mommy Where is sister Lati?”Lanlan aliuliza akimaanisha yu wapi jini Latina , Lanlan hakuwa akiogopa kabisa majini hao , tokea siku wampeleke Uingereza kucheza na Ujerumani alikuwa akiwaita dada licha ya kwamba walikuwa na umri zaidi ya miaka elfu mbili.
“Atakuwa hapa kisiwani , kwanini unauliza?”Aliongea Edna.
“Da’Lati ameniahidi atanipeleka kwao nikacheze lakini ni siku nyingi tu hatimizi ahadi”Aliongea.
“Anatakiwa kuwepo hapa kisiwani kwa ajili ya kulinda kila mmoja , hawezi kuondoka kwenda nyumbani na wewe kwa ajili ya kucheza , unapaswa usubiri mpaka baba yako arudi sawa”Aliongea Edna huku akichezea kichwa chake.
“When is Daddy coming back then?”Aliuliza akimaanisha ni lini sasa baba anarudi.
“Baba yako….”Edna alionekana akifikiria lakini palepale macho yake yalichanua.
“Baba yako naona tayari amekwisha rudi”
Mara baada ya kauli hio watu wawili walitokeza nje ya Ngome hio na kuanza kutembea kuelekea upande wa mlango mkubwa
Wanawake ndani ya ngome hio waliweza kuhisi kitu na wote walilirupukwa na furaha.
Muda uleule wale majini pepo watatu waliweza kutokea katika upande mmoja , ilionekana hata wao waliweza kuhisi ujio wao.
Kutokea kwa Roma kulisababisha kila moja kupatwa na hali ya kihisia , mara baada ya kuushinda mshituko wao wa mwanzo wote walionekana kushangilia kwa furaha , warembo hao walishindwa kuzuia machozi yao na wasiwasi wao uliokuwa umewashika kwa wiki kadhaa zilizopita.
Roma mara baada ya kuona machozi yao na wasiwasi wao alijikuta akishikwa na hatia na alifosi tabasamu.
Licha ya kwamba alikuwa na uwezo wa juu sana wa nishati ya mbingu na ardhi lakini jasho liliweza kuonekana katika paji la uso wake.
“Nimerudi , naomba mnisamehe nilipatwa na ajali na kuwasababishia mawazo”Aliongea Roma akiwa katika hali ya utulivu na wote waliishia kutingisha vichwa.
Roma aliishia kutoa tabasamu huku akimkagua mmmoja baada ya mwingine , alishindwa kuzuia aibu yake kwani kutoweka kwake ni kama vile mwanaume aliekimbia majukumu.
Mara baada ya kukutanisha macho yake na Edna kwa dakika kadhaa aliweza kugundua ndio mwanamke pekee ndani ya makazi yake ambaye alikuwa katika hali ya utulivu , ilikuwa ni kama vile alijua Roma angerudi mapema tu.
Pengine alipaswa kufurahi kutokana na utulivu wa Edna lakini ajabu ni kwamba alijikuta yeye ndio anaona wasiwasi zaidi.
“Daddy where did you run off to play , did you bring a present for me?”Aliuliza Lanlan akimaanisha baba yake alikimbilia wapi kucheza na je amemletea zawadi.
Joto lilimshika Roma kwenye moyo wake na alijikuta akiinama na kumbeba juu juu na kumbusu binti yake shavuni.
Tokea siku aitwe baba fikra zake zilikuwa zimebadilika mno , wakati alipokuwa katika ulimwengu wa jicho la anga alimuwazia mno binti yake , uhusiano wa damu kati ya mtoto na baba alikuja kugundua sio wa kawaida kabisa.
“Kabla ya kuomba zawadi napaswa kumuuliza mama yako kama ulikuwa mtoto mtiifu”Aliongea Roma na kumfanya Lanlan kumwangalia Edna kwa macho ya kubembeleza asimseme vibaya mbele ya baba yake
Muonekano wake uliwafurahisha watu wazima waliokuwa wakimwangalia na hali ilionekana kubadilika kutokana na Lanlan.
Wote walijikuta wakijituliza na kumsogelea Roma na kumuuliza kile kilichokuwa kimetokea.
Bila shaka walikuwa wamekwisha kumuona Aoiline tokea muda mrefu , wakati macho yao yanatua kwa mrembo huyo ambaye amevalia mavazi ya kitamaduni ilikuwa nguvu kwao kujituliza , alikuwa mrembo kama Edna lakini aliekuwa akitamanisha zaidi.
Aoiline hakujali kabisa namna wanavyomwangalia na alikuwa bize kushangaa mapambo ndani ya ngome hio , macho yake yalionyesha furaha mara baada ya macho yake kukutanisha na runinga kubwa mbele yake pamoja na mfumo wa kisasa wa mziki.
Roma aliwaambia kila mmoja kutulia kwenye kiti chake ili aweze kuwaelezea.
Lakini kabla ya hayo upande wa Latina , Winu na Yunu walikuwa wamesimama nje ya ngome hio bila ya kuingia ndani , ilionekana ni kama vile walikuwa kwenye mshituko na mara baada ya kupungua ndio waliingia ndani kwa tahadhari mno.
Majini jamii ya Mbweha walikuwa na uwezo wa kipekee wa kuweza kutambuana wao kwa wao , kuweka katika lugha nyepesi ni kwamba wanao uwezo wa kunusa harufu kama mbwa.
Ijapokuwa hawajawahi kukutana na Aoiline lakini waliweza kumtambua kutokana na harufu yake na uwezo wake mkubwa wa nguvu za kijini.
Lakini sasa jambo hilo limetokea ghafla sana kwao mpaka wanashindwa kuamini.
Majini hao watatu waliishia kusimama kwenye Korido huku macho yao yakimwangalia Aoiline ambae alikuwa bize kuangalia mapambo ya nyumba kwa mbali , hawakuthubutu kupiga hatua na waliishia kushikilia magauni yao kwa nguvu huku wakitetemeka na macho yao yakianza kubadilika rangi .
Kutokana na muonekano wao Roma aliona aachane kwanza na maswala yake na aliamua kumgeukia Aoiline.
“Hey , Aoiline si umesema unataka kukutana na wana ukoo wenzako , hao hapo ndio wana ukoo wa mbweha kutoka Braki”
Mara baada ya Latina na Wenzake kumsikia Roma akitaja jina la Aoiline miguu yao ilikosa nguvu na wote walipiga magoti chini.
“Mhenga..!!!!”(Haha I mean Ancestor)
Mabadiliko ya hali yaliwafanya waliokuwa ndani ya eneo hilo kushangaa , hawakuaini mwanamke huyo mrembo hivyo ni mtangulizi wa majini jamii ya Mbweha.
Moja kwa moja walimwangalia Roma kwa macho ya shauku na ilimfanya Roma aelezee kile ilichotokea katika ulimwengu wa majini pepo
Muda huo ndio Aoiline alirudi katika hali ya kawaida na kuwageukia vitukuu wake.
“Mnaweza kusimama , nilikuwa nikishangaa vitu vya hapa ndani , vimekaa kimaajabu ajabu na kuishia kupotezea vitu vingine , mnaitwa nani?”Aliongea Aoiline.
Majiini hao watatu walisimama kwa umakini mkubwa na kisha wakajitambulisha.
Majini hao watatu kwa mara ya kwanza walionyesha hali ya kuogopa na kuwafanya binadamu waliokuwa wakiwaangalia kuona kama vile wamekutana na mtu wa heshima kubwa.
Muda uleule katika hali ya kutambuana Aoiline ndie aliekuwa wa kwanza kubadilisha macho yake na yakawa ya kijani na wale watatu wengine wote walibadilisha macho yao na yakawa ya kijani lakini mng’ao wa macho yao haukuwa mkali kama wa Aoiline ikionyesha damu yake ilikuwa safi zaidi yao.
“Nimewaangusha sana kama kiongozi wa ukoo kwa zaidi ya miaka elfu hamsini lakini nimefurahi kuona mmeweza kurithi damu yetu , nina shukuru kwa kuona kile nilichokuwa nikiwazia hakijatokea”Aliongea
“Hapana hapana , wewe ndio mtangulizi wetu na utukufu wetu , kukua na kuanguka kwa ukoo wetu hakutegemeani na wewe pekee , tumekuwa tukiamini upo hai na kuanzia sasa tunakuhitaji utuongoze katika levo za juu”Aliongea na kumfanya Aoiline kutabasam.
“Msiniite Mhenga , kwani naonekana mzee?”
“Ah .. haana , hatujamaanisha hivyo”Majini hao warembo waliogopa kumkasirisha Aoiline.
Aoiline alikaa katika Sofa na kisha akamgeukia Roma.
“Dogo sina haraka sana kuongea na wana ukoo wenzangu , si una maswala muhimu ya kuongea , endelea”
Muda huo huo Neema na Magdalena pamoja na wanawakewengine waliokuwa wakivuna nishati za mbingu walitokea na kusalimiana nae na kisha kuketi kusubiri simulizi ya Roma huko alikotoka.
Roma alielezea kila kitu huku akiruka matukio ya XiaoXiao kadri awezavyo pamoja na wale mapepo na roho za giza kutoka ulimwengu wa jicho la anga na alielezea kwanini amechelewa kurudi, mwishonni aliulizia kilichompata Clark.
Ukilinganisha kati ya Clark na kushuka kwa joto la Dunia Roma alikuwa na wasiwasi na mpenzi wake zaidi.
“Hubby wakati ambao hukuwepo tumeweza kufanya uchunguzi na tumeweza kugundua Marekani na Muungano wa Ulaya wamejenga kambi kubwa ya kijeshi katika nyanda za juu za milima ya Ethiopia , joto ndani ya nchi hio lipo juu tofauti na maeneo yote ya dunia na halina watu wengi , lakini pia usafirishaji kuingia nchini huko ni rahisi , wanapanga kujenga safina ndani ya nchi hio na kisha kuipeleka majini , tunaamini Clark atakuwa huko.. alienda kwasababu walimtishia kuua binadamu ndo maana , vinginevyo angekuwa amekwisha kurudi ukilinganisha na uwezo wake”
“Safina ya Nuhu ? huo ni uongo wa kujifariji tu , kwa teknolojia iliopo haina maana kama miungu wanapanga kuua binadamu wote , hata Clark hawezi kushindana na miungu kwa teknolojia”
Alikuwa na uwezo wa kuhisia namna uungu wa Hades ndani yake ulivyoimarika , kama angetumia kanuni za anga angekuwa na uwezo wa kumshina hata jini Anjiu bila ya kutumia uwezo wa kijini.
Roma aliona kama hali itaendelea hivyo basi uwezo wake unaweza kufikia juu zaidi , pengine angefikia katika levo inayolingana na uwezo wake wakati huo wa mapigo mengi ya radi.
Hivyo moja kwa moja Roma aliamini kuna uwezekano wa Poseidon uwezo wake wa kutumia kanuni za anga kufika sawa na mapigo elfu tisa tisini na tisa ya radi.
Sasa kutokana na hisia hizo bado hakuwa na ile hali ya kujiamini kushindana na miungu hio ana kwa ana hata kama alikuwa tayarii ashapitia mapigo mengi ya radi.
Roma aliamini pale miungu kusema walikuwa na asilimia ishirini mpaka theratini ya uwezo wao , kipindi ambacho viumbe hao wanatua hapa duniani nguvu zao zilizima kutokana na kwamba hawakuwa na miili yao kamili lakini pia moyo wa Gaia haukuwa hai.
Unapaswa kuelewa katika sayari yao Moyo wa Gaia uliendelea kuwa hai na ilikuwa ni kama chanzo cha wao kuishi , yaani kama ilivyo hapa duniani kutegemea oksijeni na jua kuishi basi kwao mti Mama ambao kiini chake ni moyo wa Gaia ndio ilikuwa sehemu ya uhai wao na utimamu wao.




SEHEMU YA 774,
Mara baada ya kumsikia Roma kukosa kujiamini kupambana ana kwa ana na miungu walijikuta nyuso zao zikisawijika , ingawa walijua kinachoendelea kitaishia katika vita kati ya binadamu na miungu lakini hawakutarajia kama Roma hatokuwa na ujasiri wa kupambana nao wakati huo.
“Kwahio tunafanya nini , je tutaendelea kuangalia joto likishuka zaidi na zaidi?”Aliuliza Nasra katika hali ya wasiwasi.
“Tuachane na hili kwanza , ninapaswa kumrudisha Clark kwanza na aachane kupoteza muda kujenga hio safina , ni muhimu zaidi kwake kuwa hapa kwani usalama wake utakuwa mkubwa”
Warembo hao hawakuwa na pingamizi , hawakuthubutu kufanya maamuzi wakati Roma hakuwepo lakini sasa alisharudi na wangefuata kila maamuzi atakayo fanya.
Upande wa Aoiline hakutaka kuendelea kupoteza muda mbele ya Roma na alichukuana na majini wenzake na kisha walipotea kuelekea ulimwengu wa jangwa tenganifu.
Roma hakuwa na wasiwasi nini kitatokea mara baada ya urudi kwake katika ukoo wake , haikujalisha majini pepo jamii ya mashetani watalichukulia vipi swala hilo kwa kutowasaidia kurudisha wakuu wao lakini wasingemfanya chochote isitoshe Aoiline alitoka katika ulimwengu wa majini pepo kwa nguvu zake.
Mara baada ya kutafuta uelekeo wa kambi ya jeshi kunakojengwa hio Safina aliamua kuelekea huko akiwa peke yake.
Maeneo mengi ndani ya Ethiopia yalikuwa yakipatikana katika nyanda za juu zaidi ya mita elfu nne kutoka usawa wa bahari , kulikuwa na vyanzo vinne vya mito ikiwemo mto Atbarah.
North Atlantic Organisation(NATO) na jeshi la Urusi walichagua eneo hilo kujenga kambi ya kijeshi kutokana na sababu kuu mbili , mosi ukiachana na vyanzo vikubwa vya maji walikuwa na uwezo wa kutengeneza njia kutoka juu milimani kwenda upande wa baharini hivyo isingekuwa ngumu kuihamisha safina kutoka eneo la matengenezo.
Roma mara baada ya kufika katika nyanda za juu na kuangalia upande wa baharinni aliweza kuona meli nyingi za kivita zilizokuwa zimeegeshwa zikiwa zimewekewa mifumo ya kivita ya Aegis.
Nchi zote duniani ukiachana na taifa la China walikuwa wamefanya muungano wa pamoja , hivyo wanajeshi waliokuwwepo walikuwa ni wengi mno , yaani kwa jicho moja tu aliweza kugundua walikuwa ni zaidi ya wanajeshi milioni moja ndani ya eneo moja.
Roma alichunguza mazingira ya kambi hio kabla ya kushuka chini.
Karibu na mlimani kulikkuwa kumezungushiwa ukuta mkubwa mno wa chuma kigumu ambao urefu wake ulikuwa ni kama mita mia moja , geti tu lilikuwa na upana wa mita mia tatu.
Roma mara baada ya kujitokeza na kukanyaga juu ya ndege iliokuwa ikiendeshwa na mfumo wa nyuklia palepale wanajeshi wengi waliweza kumuona.
“Simama hapo hapo , wewe ni nani?”
Mwanajeshi alieonekana kama na miaka hamsini hivi alievalia sare za jeshi la maji aliongea akiwatangulia wanajeshi kadhaa wa ngozi nyeusi.
Roma hata hakuwajali na hakujisumbua kuongeleshana nao , mara baada ya kutembea mpaka mbele ya geti aliruka mita kama kumi na mbili hivi kwenda juu na kisha alirusha ngumi katikati lile geti.
“Thudd !!!
Mshindo ulikuwa mkubwa mno kiasi cha kutetemesha mlima na mawe makubwa yalianza kuporomoka kwenda chini na kuwashitua wanajeshi waliokuwa upande wa chini.
Roma akiwa na uso wa kutisha aliweza kutengeneza tobo kubwa tu kwenye geti lile , shimo ambalo lilikuwa na upana wa mita kumi , iliwezekana kutokana na kwamba alitumia nguvu za kijini.
Mara baada ya kutengeneza shimo lile aliingia ndani na kuwaacha wale wanajeshi wakiwa wamebung’aa wasiamini wanachoona.
Eneo ambalo lilikuwa limechimbwa katika mlima huo lilikuwa kubwa mno kiasi cha kumshangaza Roma
Ilikuwa ni kama vile wametengeneza ulimwengu mwingine kabisa ghafla tu, juu kabisa walionekana kubadilisha uelekeo wa maji kwa kutengeneza bwawa kubwa ambalo lilionekana lilifungwa mitambo ya kuzalisha umeme.
Upande wa juu kabisa kulikuwa kumejengwa kitu meli sio meli wala ndege sio ndege kitu chenye ukubwa wa meli ya kivita ya Marekani
Ilikuwa ni kama vile Roma anaangalia filamu za kisayansi , kwani kila kitu kilionekana katika umbo la kushangaza na kubwa licha ya kwamba unaweza kujua moja kwa moja pengine ni Manowari.
Kila kitu kilichokuwa kimetengenezwa hapo ndani ilikuwa ni kwa ajili ya kutengeneza malighafi za ujezi wa Safina.
Kulikuwa na watu wengi mno ambao kila mmoja alikuwa bize , kulikuwa na watafiti , wafanyakazi na wasimamizi.
Roma alishangazwa kwani ilionyesha binadamu alikuwa na uwezo mkubwa wa kuchimba pamoja na kujenga , kwani usingeamini kama eneo hilo limechimbwa na kujengwa ndani ya siku chache tu , haikuwa projekti ndogo hata kidogo.kambi hio unaweza kuiita ya kimiujiza .
Kwasababu ya Roma kuingia kimabavu king’ola kilianza kupiga makelele katika eneo lote na taa mbalimbali za tahadhari kuwanza kuwaka.
“Tuu tuuuu… Attention !, Everyone! Attention! , Everyone An Intruder has breached the perimeter!!”
Wakati wafanyakazi wakishangaa upande wa wanajeshi na siraha zao walikimbia kutoka pande zote kumsogelea Roma.
Palepale aliweza kujua hali ilikuwa ngumu kuliko alivyokuwa ametarajia kwani sio binadamu pekee ambao walikuwa ndani ya hilo eneo.
Kundi kubwa la watu waliokuwa na ngozi kama ufinyanzi walisogea , walikuwa ni wanajeshi wa daraja la juu wa kabila la wanywa dam.
Nyuma yao kulikuwa na kundi lingine la watu ambao wote walikuwa na nguvu za ziada walikuwa ni Werewolves moja ya maadui wakubwa wa Vampire na walikuwa wamechomoza kucha zao zilizorefuka kwa ajili ya kumrarua Roma.
Kilichomshangaza zaidi hata wavatican na Wajihad walikuwepo hapo ndani na wanachama wa Bunge la Giza.
Tabasamu la kichekesho lilimvaa Roma mara baada ya kundi kubwa kumzunguka , ilikuwa ni hali iliompa ufahamu wa vitu vingi sana.
Binadamu waliweza kujenga na kuchimba eneo kubwa namna hio kutokana na msaada ya Werewolves , Blood race na watu wa nguvu za ziada.
Mfamo wachawi kutoka Uingereza chini ya Merlin Magic Association walikuwa na uwezo wa kutumia uchawi wao kupasua miamba hivyo kufanya zoezi la uchimbajij kuwa jepesi zaidi , upande wa Wolverines na Vampires walikuwa na uwezo wa kubeba vitu vizito ambavyo mashine na binadamu hawawezi kubeba.
Kati ya kundi lote wa kwanza kujitokeza mbele yake ni wanywa damu na mmoja kati yao aliweza kumtambua Roma.
Alikuwa ni mwanamke mrembo wa kuita aliefahamika kwa jina la Lilith ambaye Roma ashawahi kuonja mbususu yake.
“Everyone stop , it’s His Majesty Pluto”Aliongea Lilith kwa nguvu akimaanisha waache kwani ni Mfalme Pluto.
Lilith alikuwa katika hali ya mshangao mara baada ya kumuona Roma lakini akili ilimrudia na kutoa maagizo ya haraka
Muda huo huo ma’prince wa kundi la wanywa damu na wazee wa jamii ya Wolverines pamoja na majemadari wa jeshi walisogea
Kati yao Roma alikuwa akiwatambua kwani alikuwa ni Sargaras baba yake Lilith , Mkurugenzi wa FBI Baloteli na Fodesa Mkurugenzi wa DGSE na wote hao walimjua Roma.
Lakini walkuwa na wasiwasi mnno kwani hawakujua nia iliomleta Roma ndani ya hilo eneo.
Roma mara baada ya kuona wanajeshi hao ambao walikuwa katika madaraja tofauti tofauti alishindwa kujizuia kuwaza.
“Tch , nilikuwa nikidhania Jihad , Vatican na Bunge la Giza siku zote watakuwa maadui, kusingekuwa na wakati wa amani kati ya Wolverine na Vampires , lakini vile vile FBI wasingekubali kuonekana pamoja na KGB , inaonekana uhalisia umeniaminisha tofauti , haha..yaani wote nyie mnashirikiana?”Aliongea Roma huku akitabasamu kifedhuli.
Viongozi wa juu walikuwa washajua kuonekana kwa Roma ndani ya eneo hilo kwani wanamtambbua kama Hades sehemu ya miungu, sasa kutokana na ukinzani uliotokea kati ya miungu na binadamu walijikuta wakiwa na wasiwsi.
“Your Majesty Pluto it isn’t appropriate for you to show up here”Aliongea Sargaras akimaanisha sio vizuri kwa Roma kujitokeza hapo.
“Sargaras hivi jeraha lako ulilopata kipindi ile limekwisha kupona , lile jeraha sio rahisi kuponyeka kwa muda mfupi”Aliongea Roma.
“Bado sijapona kabisa lakini siwezi kuendelea kulala , kupotea kwa kizazi cha binadamu kunaweza kusababisha kupotea pia kwa wanywa damu”
“Mfalme Pluto ijapokuwa wewe ni sehemu ya miungu lakini bado ni binadamu , tafadhari usifanye mambo kuwa magumu kwetu , tunajua uwezo wako ni mkubwa lakini tutapambana kama ni swala la kutufanya tuishi..”Aliongea Lilith akiwa na hali ya huzuni kwenye macho yake lakini mikono yake haikulegea katika kushikilia siraha yake.
“Nyie watu mnafikiria mbali , sijaja hapa kupigana na nyie bali kumchukua mwanamke wangu na kumrudisha nyumbani , Niambieni Clark yupo wapi? Mbona sihisi uwepo wake?”
Ijapokuwa Roma alikuwa na hasira kwa nchi hizo kushirikiana na kumlazmisha Clark kufanya vitu asivyopenda lakini alikuwa ni mwelewa kwa binadamu kupigania uhai wao
Lakini kwasababu asharudi hakutaka kuangalia tu Clark akiteseka ndio maana alifika hapo kumchukua.
Lakinji katika wakati huo hali ya wasiwasi ilimvaa mara baada ya kushindwa kupata msisimko wa nishati za mbingu na ardhi kutoka kwa Clark.
Mara baada ya kusikia swali lake watu wale walionekana kuwa na hali ya wasiwasi katika macho yao.
“Kuna kilichompata Clark?”Aliuliza Roma mara baada ya kuona wanaangaliana tofauti na kujibu swali lake.
“Your Majesty we cant hide it from you , Princess Clark was Abducted”Aliongea Lilith akimaanisha kwamba hawawezi kumficha Roma kwani Clark alitekwa.
Muonekano wa Roma ulibadilika palepale na ukawa ni wa kugopesha , macho yake yalipita kwa kila mmoja aliekuwa ndani ya hilo eneo na kuwasabibishia jaso kuwatoka.
“Unamaanisha nini ?”
“Ilitokea wiki tatu zilizopita , adui alivunja katika kambi yetu na kumchukua Clark , tulishindwa kujua amewezaje kufanya hivyo lakini kulingana na alivyokuwa akisafiri na kutoa msisimko ni mtu mwenye mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi , kwani Clark alifurukuta kidogo tu na nguvu zake zote zilifungiwa”Aliongea Sargaras.
Roma wasiwasi ulimvaa palepale na alijiuliza au ni majini kutoka ulimwengu wa majini watu au ni majini pepo kutoka Braki?”
“Mfalme Pluto hatukuweza kutoa taarifa kuhusu hili mapema kwasababu hatukujua wapi ulipo , ujenzi wa Noah Ark unaendelea kuwa malengo yetu hata baada ya kupotea kwa Clark , hatutaki kuwa na kikwazo kwani tunakimbizana na muda “General aliekuwa kwenye mavazi ya kijseshi aliongea.
Roma aliona haitokuwa na maana kuwa na wasiwasi , ilionekana ni kweli kuna mtu amemteka Clark lakini nia zao hazikuwa zikifahamika lakini hata hivyo alijua atakuwa sawa kwani kama wangetaka kumuua wasingemteka hivyo ilimaanisha kuna kitu walitaka kutoka kwake
“Bado mnaweza kuendelea na ujenzi bila ya uwepo wake?”
“Princes Clark ashamaliza kutengeneza Blueprint za Noah Ark , ijapokuwa kuna taarifa ndogo ndogo zilizobakia zinazohitaji mahojiano tunajiamini katika kumaliza ujenzi ndani ya muda kutokana na nguvu ya watu kutoka pande zote za dunia”
Jibu hilo lilimshangaza Roma na kujiuliza inamaana Clark ameweza kusanifu ujenzi wa Meli hio kubwa ya kivita , au ni kwamba alishawaza kutengeneza kitu kama hicho hapo kabla.Roma alijiuliza nini kipo katika akili ya mwanamke huyo.
Licha ya wasiwasi wake Roma alijua hawakuwa kipaumbele kwake kwa wakati huo , alipaswa kutafuta njia ya kujua wapi alipo Clark , ili mradi yupo duniani alijua lazima atampata.
Kuhusu Moyo wa Gaia alijiambia lazima apate suluhisho pia ili kuokoa binadamu.
Roma kabla ya kutaka kuondoka sauti iliongea kutoka nyuma yake na kumfanya asimamae.
“Mfalme Pluto je utatusaidia?”Alikuwa ni Lilith alieuliza ni kama anataka kujua kama Roma atakuwa upande wa Binadamu.
Licha ya kwamba ujenzi ulikuwa ukiendelea vizuri lakini walijua fika tatizo sio tu kushuka kwa joto lakini vipi kama miungu hio ikaamua kuua binadamu wote.
Watu kama Sargaras walikuwa washaona uwezo wa Roma hivyo walihisi kufahamu matokeo ya mapigano na miungu mingine.
Kila mmoja alimwangalia Roma kwa kusubiria jibu lakini upande wa Roma alijikuta akipatwa na hisia ambazo hakuwahi kuzipata hapo kabla.
Zamani hakuona kuna utofauti wowote kwa kuwa sehemu ya miungu au kuwa sehemu ya binadamu , alikuwa ni Roma Ramoni binadamu lakini pia mwenye uungu unaomuweka katika sehemu ya miungu.
Ilikuwa ndio wakati sasa akili yake inamwambia kwamba miungu na binadamu ni viumbe viwili tofauti
Katika ulimwengu wa wanyama , viumbe viwili tofauti vinaweza kuishi pamoja kwa miaka muda flani lakni upo uwezekano wa moja kati ya viumbe hao kuwa na nguvu kubwa na kutaka kumla aliekuwa kiumbe dhaifu kutokana na njaa.
Sasa ilikuwa ni swala la muda hata kwa miungu hao , ilikuwa ni muda wao wa kuamsha uwezo wao na kutokana na kwamba washakuwa na nguvu ilikuwa ni swala la muda tu kutaka kuwala binadamu ambao ni wadhaifu na ni swala ambalo halihusiani kabisa na mambo ya maadili wala sentimentals(hisia).
Roma alitaka kuongea lakini neno halikumtoka na alichoweza kutoa ni pumzi iliojaa wasiwasi.
Hali ya masikitiko ilikuwa imemvaa mara baada ya kushindwa kutoa jibu ni upande gani alipo , lakini sio kosa lake kwani ni kama alikuwa akijua nini kitatokea kama atataka kupigana na kundi lote hilo la miungu ambao wana uwezo wao asilimia mia moja.
Roma hakutoa jibu wala hakugeuka nyuma na aliondoka katika eneo hilo kurejea visiwa vya wafu.
Wakati akiwa njiani alijitahidi kupunguza mwendo ili kurudisha mudi yake lakini sasa dakika ambayo anaingia katika anga la visiwa vyake aliweza kuhisi kuna kitu hakipo sawa na kumfanya apige hatua kubwa kuingia katika ngome.
Katika eneo la sebuleni ndani ya ngome hali ya hewa ilikuwa kinzani yenye kutisha , wanawake hao na ndugu walikuwa wamekaa wote wakimwangalia mwanaume wa ajabu aliekuwa mbele yao
Mwanaume huyo alikuwa amekaa kama bosi katika nafasi ambayo Roma hukaa siku zote kama kiongozi wa familia.
Mwanaume huyo alikuwa akishaganza mno kwani ukiachana na kuwa na uwezo mkubwa wa kijini usiotamithilika , kwanza alikuwa mzee hakuwa na nywele wala nyusi usoni , yaani alikuwa ni kama vile ni Skeleton lililopata mwili kwa bahati mbaya lakini hata hivyo alionekana kwa mbaali kuwa Handsome.
Roma mara baada ya kupiga jicho vizuri aliweza kuona mwanaume yule alikuwa ameshikilia ile bangiri ambayo Edna alipewa na Afande Kweka kama ishara ya kuwa mkwe wa familia.
ITAENDELEA.
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI: SINGANOJR

Mono no aware.

SEHEMU YA 774.
Roma aliishia kukunja sura mara baada ya kuona bangiri ya Edna ikiwa katika mikono ya yule mtu wa maajajbu, kwa jinsi mtu yule alivyokuwa ameishikilia ni kama vile ni kitu cha thamani kubwa sana kwake.
“Hubby umerdi .. huyu mzee alikuwa akikusubiria”Aliongea Edna mara baada ya kumsogelea Roma akiwa ameshikilia Lanlan.
Pengine ni Edna pekee ambaye alikuwa katika hali ya utulivu , ilikuwa ni kama vile hakujali sana kutembelewa na mtu ambaye hakuwa akimjua.
“Kwanini amechukua bangiri yako?”Aliuliza Roma.
“Ameichukua sekunde tu mara baada ya kufika, hatuna uwezo wa kudili nae”Aliongea Edna huku akionyesha tabasamu la uchungu
Roma alimchunguza Lanlan na kila mmoja na alipatwa na ahueni mara baada ya kuona hawana tatizo lolote.
“Wewe ni nani?”Aliuliza Roma na yule mtu wa kushangaza aliinua kichwa chake na kumwangalia na kisha akatoa cheko.
“Kijana hupaswi kuongea na mtu mzima kwa ukorofi namna hio”Aliongea yule mzee huku akigeuzia macho kwenye ile bangiri.
“Hio bangiri ni ya mke wangu naomba uirudishe”Aliongea Roma anbaye alionekana hayupo katika hali ya furaha lakini hakumpokonya kwa nguvu kutokanaa sababu maalumu.
“Kauli yako inashangaza hii bangiri pia ni ya mke wangu”Aliongea yule mzee na kufanya kila mmoja kushangaa akiwemo Roma mwenyewe.
“Ijapokuwa upo juu katika levo ya mapigo mengi ya radi , kuna uwezekano mkubwa usiniweze , hivyo nakusihi kistaarabu rudisha bangiri hio kwa mke wangu kabla hujanikasirisha”
Kauli ya Roma iliwashangaza kila mmoja aliekuwa humo ndani ukweli ni kwamba walijua huyo mzee alikuwa na uwezo wa kijini lakini hawakujua ni katika levo ipi.
Sasa muda mchache uliopita waliweza kusikia kutoka kwa Roma alikuwa amepanda levo mpaka mapigo mengi ya radi na waliamini hakuna binadamu ambaye anaweza kuwa na uwezo mkubwa kuliko yeye lakini ajabu ametokea mtu mwenye uwezo mkubwa.
“Naona upo katikati ya levo ya mapigo mengi ya radi lakini umeweza kutambua levo ya uwezo wangu , inaonekana haupo chini yangu sana likija sawala la ufahamu wa mbingu na ardhi”Aliongea yule mzee huku akimwangalia Roma kwa namna ya kuridhika.
Roma mara baada ya kupata maelezo machache kutoka kwa Aoiline na pamoja na uwezo wake mkubwa wa utambuzi aliweza kupata uwelewa wa haraka sana wa kutambua levo hata ya mtu ambaye yupo juu yake, ni hivyo tu ameshindwa kukusanya nishati ya kutosha kupanda levo mpaka mwishoni mwa mapigo mengi hivyo yupo katikati.
Ilimshangaza pia kuona mzee huyo alikuwa akimsifia kwa dhati kabisa , ilikuwa ni kama mwalimu anavyompongeza mwanafunzi.
“Wewe ni nani lakini , kwanini umekuja kunitafuta?”Roma aliendelea kuuliza huku akiwa amekunja ndita.
Yule mwanaume alisimama kutoka katika sofa na kisha alitembea kumsogelea Roma , hakujali kuwa mstaarabu katika kumwangalia Roma.
“Hakuna kubwa lililonileta nimekuja tupimane uwezo”Aliongea na ni muda ulule alikuwa ashafanya shambulizi kwa kumshika Roma kola ya shati.
Roma macho yake yalipanuka kwa mshangao mara baada ya kugundua ameshindwa kumkwepa.
Spidi ambayo mtu huyo alitumia inaweza kuonekana ya kawaida kwa mtu wa kawaida lakini kwake ilikuwa ya ajabu kwani haikumtoa katika eneo alilokuwa amesimama mpaka akafikiwa
Hata kwa wanawake wa Roma walishangaa kwani mwanaume huyo kwa macho alionekana alitumia spidi ndogo sana lakini kwa Roma bado alishindwa kumkwepa.
“Hii sio sehemu nzuri ya sisi kupigana , nitakupa lift”Aliongea yule mwanaume na palepale alimsukuma Roma kama mpira kumtoa nje ya ngome hio.
Roma alijikuta akisukumwa na nguvu isiokuwa ya kawaida kwenda kilomita kadhaa juu angani akiwa hana uwezo wa kujidhibiti.
Muda ambao aliweza kujiimarisha angani mwanaume yule alikuwa ashatoka kwenye ngome na kumfikia huku akimwangalia na tabasamu usoni .
Muda huo huo Roma aliweza kutambua mtu huyo hakuwa na uadui na yeye na ilionekana yupo hapo pekee kwa ajili ya kushindana nae na kama sio hivyo angeweza kumshambulia tokea mwanzo wakati alipokuwa amezubaa.
“Hili eneo lina uwazi wa kutosha na hatutoweza kuumiza watu wa visiwani kama tutakuwa makini”Aliongea yule mtu na palepale alikunjua mikono yake kwa kumpa ishara ya kuanza pambano , yaani alifanya kama vile wanamisumbwi wanavyopeana ishara ya kuanza kushambuliana.
Ijapokuwa Roma alikuwa tayari kupambana lakini bado alikuwa na wasiwasi na ufunuo wa kisiraha wa huyo mtu lakini hata hvyo hakuwa mwepesi kushindwa na alijiambia atampiga kwanza na baada ya hapo watakaa chini na kuongea.
Nguvu ya mbingu na ardhi karibu yao ilianza kuzunguka kwa kasi mno na kusababisha upepo mkali mno na dakika ileile vitu vyeusi vyeusi viliweza kujitengeneza katika anga kwenye umbo flani hivi kama la farasi.
Waliokuwa wakiangalia kwa chini walikuwa na uwezo wa kuona umbo hilo la rangi nyeusi la kushangaza na kuwafanya wanawake wa Roma kushikwa na mshituko
Ijapokuwa walijua uwezo wa Roma ni mkubwa kwa kuweza kufikia levo ya mapigo mengi ya radi lakini hawakutegemea mashambulizi ya mtu yule kuwa ya aina yake kwani hapo walipo ni kama wanahisi nguvu flani ambayo inataka kuharibbu dunia.
Roma na yeye hakuwa nyuma alikuwa tayari ashatengeneza mashambulizi ya uharibufu kwa ajili ya kumkabili mpinzani wake.
“Hivi unadhani unaweza kunitisha na aina hio ya mashambulizi?”Aliuliza yule mzee.
“Acha kujiamini kwa kupitiliza”
Aliongea Roma na muda uleule aliita radi ya rangi ya zambarau kutoka kwenye kiwingu kilichojitengeneza juu angani.
“Rumble….”
Radi zile zilikunjana kama vile ni vinyoka nyuka ikionekana inajikusanya nguvu na kutengenza mwanga mkali chini ya bahari wa rangi ya bluu na zambarau.
Radi ile mara baada ya kumshukia yule mtu alonekana kuipotezea kwani hakujali kabisa na aliacha impige.
Roma alishangazwa na jambo lile na alijiuliza au hana spidi ya kukwepa shambulizi lake.
“Haileti maana ninaweza bado kuhisi nguvu zake hazijadhoofika hata kidogo au inawezekana.. hapana
Roma moyo wake ulisinyaa , dakika ambayo aliingiwa na hsia zisizozakawaida alishapokea pigo kutoka nyuma.
Thud !!
Ukiachana na sauti kubwa ya kishindo , uzito uliompiga mgongoni ulikuwa ni wa tani nyingi sana kiasi cha kumpeleka chini kama furushi.
Alikuwa kama mshale namna ambavyo aliruka lakini Roma alijiimarisha kwa kukimbia umbali mrefu katika juu ya bahari.
Lilikuwa ni pigo kubwa sana kwake ambalo lilimfanya kujihisi ni kama vile viungo vyake vimepasuliwa pasuliwa na kidogo tu ateme damu.
Roma mwili wake kisayansi ulikuwa na uwezo wa kuhimili mapigo makubwa lakini teke ambalo alipokea kutoka kwa mtu huyo wa maajiabu lilikuwa limeambatana na nguvu ya nishati ya levo za mapigo mengi ya radi , bila kusahau mzee huyo alikuwa ameweka umakini wote katika miguu yake hivyo kusababisha nguvu kubwa sana kuzidi hata ya mapigo mengi ya radi.
Roma alijikuta akiona nyota nyota na nishati zake za mbingu na ardhi mara baada ya kusambaratishwa na kile kiwingu cha radi pia kilipotea.
Alijikuta akihema kama mbwa mara baada ya kurudi tena angani huku akiwa na hali kubwa ya makasiriko na ilidhihirika katika macho yake.
“Unakitafuta kifo”Roma alibweka.
“Hakuna namna , hata kama una ufunuo mkubwa wa mashambulizi huwezi kushindana na mimi kutokana na kwamba huna uzoefu wa kutosha… naona kukutafuta kwangu tupigane kushaanza kuniboa ..bado nakuona ni mdogo sana na inaonekana haikufai kubeba majukumu makubwa”Aliongea
“Acha kuongea upuuzi nenda moja kwa moja kwenye pointi yako wewe ni nani?”
Roma hakutaka kutumia uwezo wake wote kushindana na huyo mzee kwani aliogopa anaweza kumua lakini alijutia kuwa na huruma.
“Kwanini unajifanysiha kama mtoto ambaye hataki kukubali kushibdwa baada ya kushindwa , bado huelewi tu kwamba haijalishi kama ni radi ya Zambarau au ya rangi ya fedha au hata radi ya nyekundu huwezi kunishinda kwasababu huwezi kunifikia na mashambulizi yako , mtu yoyote akifikia katika levo flani za mbingu ukali wa kisu hauna maana tena zaidi ya mbinu, kisu chako kinaonekana kuwa na makali mara mia moja kuliko cha kwangu lakini ujuzi wako ni mdogo , radi yako inaweza kufanya kazi zidi ya wanaojiita watu wa ulimwengu wa majjini watu kwasababu uelewa wao ni mdogo kuliko wako .. lakini ukijilinganisha na mimi nimekuacha mbali kwa vitu vingi sana”
Roma alijikuta akifubaa mara baada ya kuona pengine huyo mtu ana pointi , hio ilikuwa ni kwasababu hata Aoiline kule ujinini alimfanyia kitu ambacho kilimfanya kujua mbinu zake ni ngumu sana kueleweka , kipindi cha nyuma hakuelewa kuhusu hilo na wala hakulipa kipaumbele mara baada ya kuamini kwasababu uwezo wa kushinda anao haina haja lakini sasa alikuja kugundua kwamba katika mapigano ya levo za juu anaweza asishinde kwani atakuwa amekosa mbinu licha ya uwezo alikuwa nao.
Kwa lugha nyepesi ni kwamba Roma siraha anazo lakini hana mbinu nzuri y a kutumia hizo siraha kumshambulia Adui ndio alichomaanisha huyo mzee , hivyo akijikuta katika mashambulizi ya levo ya juu siraha zake zinaweza zisilete madhara kwa adui kwani hana mbinu ya kuwashambulia nazo.
Ni sawa sawa una Kombora lako la nyuklia hapa Tanzania na unataka kushambulia Marekani lakini huna mbinu ya kulifikisha Marekani.
Lakini hata hivyo Roma hakutaka kushindwa kizembe namna hio , radi ya mapigo mengi ya rangi ya silver ilianza kumzunguka kwa kasi kubwa sana kama shoti za umeme na kutengeneza kitu kama ngao vile , ilikuwa ndio radi halisi ya mapigo mengi.
Kadri ilivyokuwa ikiongezeka palepale mnyororo wa radi wa urefu kama wa mita kumi uliweza kujitokeza mkononi mwake , ulikuwa ukinesa nesa kama nyoka.
“Oh! Naona wewe ni mtu ambaye hukubali kushindwa kirahisi nimependa lakini kwa bahati mbaya huwezi kushinda zidi yangu”Aliongea yule mtu huku macho yake yakisinyaa.
Roma hakutaka kutoa jibu na palepale alipiga hatua kwenda mbele na aligeuza ile radi na kuwa boriti akiwa na nia ya kumpiga nayo yule mtu na kumuua hapo hapo , hakuwa na haja tena ya kumjua ni nani.
Radi ile ya rangi ya silver ilikuwa ni kama vile ni mabawa ya samaki na ilifanya kila ilichokuwa ikielekezwa.
Radi hio iliokuwa ni kama mnyororo unaokwenda kumfunga jambazi ilichana anga kwa spidi kali mno , ijapokuwa radi za kutengeneza hazikuwa na nguvu kubwa kama zile zinazoshuka kutoka mawinguni kiasili lakini uwezo wake wa kuzikontrol na kuzichezesha atakavyo ulikuwa ni mkubwa.
Lakini sasa kwa namna zote alizojaribu kushambulia yule mtu alipotea ile sehemu aliolenga na kutokea sehemu nyingine
Yaani ni kama Roma alikuwa akitegwa arushe na bwana yule apotee na pigo lake kupita na hali hio ilimfanya kuzidi kuchanganyikiwa.
Ndani ya dakika kumi na tano Roma aliweza kutengeneza mashambulizi matano ambayo yote hayakuweza kumpata mshindani wake.
Hata warembo wake waliokuwa wakiangalia shindano hilo waliweza kuona radi tu lakini hawakuweza kuona mtu akidhulika nazo.
Kwa Roma ilikuwa ni kama vile amekutana na Master wake na anamwambia ajaribu kumshambulia lakini kila shambulizi Master ana kwepa na kumfanya kujikatia tamaa.
Yule mtu aliishia kutoa tabasamu la uchokozi huku akimwangalia Roma kama mtoto.
“Umeelewa sasa , kama nilitaka kukimbia ningekuwa nishafanya hivyo muda mrefu na hata usingejua , kama ningetaka kukushambulia wakati ulipokuwa ukizubaa ningekuwa nishafanya hivyo na usingeweza kukwepa shambulizi langu , kama mimi ni adui yao ninaweza nisikuue lakini nina uhakika kwamba usingeweza kunifanya chochote”
“Aina yako ya mshambulizi mbona kama yanafanya watu kuchanganyikiwa?”Aliuliza Roma na kumfanya yule mzee kushangaa kidogo.
“Inaonekana angalau umeweza kurudi ila kwa bahati mbaya umekosea , ufunuo wangu wa kimashambulizi ni kweli unafanana na ule wa kumfanya mtu kuchanganyikiwa lakini utakuwa ni mwepesi sana kama upo hivyo pekee”
Roma alishangaa kidogo na alionekana kukumbuka kitu dakika chache zilizopita.
“Ni Deviation? Kwasababu kila kitu kinabadilika na hata kwa kanuni za ulimwengu pia zinabadilika , ufunuo wako ni ushahidi wa dunia kubadilika hivyo kufanya wengine kuchanganyikiwa”Aliongea Roma.
“Deviation? Hehe hilo ni jina la kipekee lakini unapaswa kujua kwamba sio kwamba najaribu kukuficha ukweli ni kwamba tu ufunuo wa mtu wa nishati za mbingu na ardhi hauelezeki kwa maneno”Aliongea lakini Rima pia alikuwa akijua hilo.
Nishati za mbingu na ardhi mara nyingi ukishafikia katika mwanzo wa levo ya utambuzi ambayo ni levo ya nafsi unachopata ni kitu kama maono , sasa maono hayo yanakuwa kama hisia flani hivvi ambazo unashindwa kuziweka katika maneno.
Njia rahisi ya kuthibitisha hili ni kupitia wachungaji wanaotumia nishati za mbingu na ardhi kujaribu kuombea watu , ile hali inayompata yule anaeombewa mpaka kudondoka chini ndio ambacho kinatokea katika ufunuo wa nishati za mbingu na ardhi ni vitu ambavyo havielezeki yaani unajua tu ni kama vile unatunukiwa.
Lakini jambo moja la kufurahisha ni kwamba kadri unavyopanda viwango vya juu vya uelewa wa siri ya nishati za mbingu za ardhi unaweza kutatua fumbo la ufunuo wa aliechini yako.
Roma anashindwa kuelewa ufunuo wa mtu aliekuwa akipambana nae kwasababu alikuwa amemzidi kila kitu.
Sasa Roma alijua hakuna uwezekano ambao anaweza kumshinda mtu aliekuwa mbele yake na hata kama atumie Dhana asingeweza kufanikiwa kama nishati zake za mbingu na ardhi zimeshindwa .
“Basi acha kuzunguka zunguka na niambie wewe ni nani”Aliongea Roma mara baada ya kuzima radi yake na kurudi kawaida akionyesha hana mpango wa kushambulia.
“Acha kuwa na wasiwasi , ni muda wa kukaa wakati tukiongea”Aliongea yule mtu huku akiwa na tabasamu na kufumba na kufumbua wote waliweza kufika katika ngome kwa mara nyingine.
Roma aliishia kukunja ndita lakini aliamua kumkubalia tu na mara baada ya wote kukaa chini katika eneo la sebuleni ni kama sasa yule mtu aliweza kumuona Lanlan aliekuwa katika mikono ya Edna.
“Katoto jina lako si Lanlan , hebu njoo hapa kwanza nina zawadi yako”Aliongea yule mzee.
Kibonge huyo aliishia kupesha tu ijapokuwa hakuwa akimjua mtu huyo ni nani lakini alikuwa amejifunza kutoka kwa baba yake kutokukataa zawadi hivyo alitoka katika mikono ya Edna.
Edna hakumkatalia kana kwamba aliona hakuna tatizo ambalo litampata Lanlan.
“Mjomba ni zawadi gani hio ,je ni kitu cha kula?”Aliongea Lanlan mara baada ya kwenda kusimama mbele ya yule mwanaume.
Katika macho ya kila mmoja bwana yule alitoa bangiri kutoka katika hifadhi ya pete iliokuwa na vigoroli vya kung’aa sana ambavyo ni kama madinni ya rubi lakini sio rubi.
“Inavutia mno…”Sophia aliekuwa kimya muda wote aliongea
Wote waliangalia haraka haraka kuona kama ilikuwa ni Dhana lakini palepale waliweza kugundua madini yaliotumika ni yale yale yaliotumika kutengenezea ile bangiri , ijapokuwa ni kitu kama Dhana lakini ni ngumu kujua kiwango cha nguvu yake.
Hali ya kukata tamaa ilionekana katika macho ya Lanlan , alipenda vitu vizuri lakini bangiri haikuwa ikivutia zaidi kama kitu cha kula.
Mwanaume yule aliweza kuona mabadiliko ya LanLan na alishia kucheka na kumfinya Lanlan mashavu yake.
“Huna shukrani wewe kibonge”
Licha ya kuongea hivyo alikuwa akimvalisha Lanlan ile bangiri.
“Hii Bangiri inaitwa Hufe na ilitengeenzwa kuvutana na hii bangiri ya Fehu, haya majina aliyataja mke wangu wakati huo na ni lugha ambayo hamuwezi kuielewa lakini maana yake ni Hufe nakuombea maisha marefu kwa mwanaume na Hefu nakuombea maisha marefu kwa mwanamke”
“Hebu subiri sana umesema bangiri ilikuwa ya mke wako , huyo mke wako ni nani?”Aliuliza Roma.
“Kijana mjinga sana wewe , unafikiri ilitua kwenye mikono ya familia yenu bahati mbaya tu , mimi na mke wangu kwako wewe sisi ni mababu zako , jina langu naitwa Mzee Yasu kutoka miaka elfu nne iliopita”
“Hebu acha utani basi au ndio unapendwa kuitwa mababu tu kisa una nguvu za mbingu na ardhi”Aliongea Roma alikuwa hana mshangao kama ilivyo kwa wengine.
Lakini sasa yule mtu hakujali sana maneno ya Roma ya kutokumwamini na palepale sijui alifanya nini lakini ile bangiri iliokuwa kwenye mkono wake ilitoa rangi ya kijani na ile ya Lanlan ilitoa pia rangi ya kijani na zilipokutana hewani zilitengeneza picha kama ya binadamu aliekuwa kama ndege kutokana na mabawa na ilidumu kwa dakika chache tu na kupotea na hali ikawa kimya kama vile hakuna kilchotokea.
“Dhana ya kiuungu hio!!”
Roma alishangazwa na jambo hile , ilikuwa ndio ni Dhana ya kiuungu yaani hio ni Dhana tofauti na Dhana za majini ni Dhana ambayo ina roho ya kiuungu ndani yake unaweza kuitwa Dhana za kimalaika.
“Ni miaka elfu nne imepita hatimae gurudumu la upepo na moto vimekutana”
“Gudurudumu la moto na upepo!!”
Kila mmoja alishangazwa na maneno yake , vitu vingi vilikuwa vimetokea na kila aliemsikia hakuweza kuelewa mara moja.
“Unaamnisha gurudumu la upepo na moto ambalo alitumia jini Nezha katika kuwashambulia miungu?”Aliuliza Roma.
“Hehe eti kuwashambulia miungu , ulichosikia wewe ni hadithi tu za kufikirika lakini hii bangiri pamoja na mwenzake nguvu yake ni ya Gurudumu la upepo na moto, Dhana ya kiuungu ambayo Master wangu mimi ndio alinipatia na nikampatia mke wangu kama zawadi lakini kwa bahati mbaya alikuwa ni binadamu wa kawaida ambae uwezo wake ulikwa wa kawaida hivyo alifariki miaka elfu nne iliopita…Ukitaja neno Gurudumu la moto na upepo inaweza kuwa Dhana yenye nguvu lakini kwa mtu ambaye uwezo wake ni mdogo inakuwa ni bangiri ya ulinzi tu… hizi bangiri zikiungana na ndio inakamilika kutoka kuwa zana na kuitwa Dhana. wakati wa kutafuta familia yenu nilifuata tu msisimko wa hii bangiri ndio maana ilinifikisha hapa”
Kwa maelezo yake ni kama iliwafanya wamuamini na kumwangalia kwa heshima awamu hio.
“Ila inawezekanaje ukwa unaishi wakati wewe ni binadamu..inamaana umeishi kwa kuangalia wengine kufa kwa miaka yote hio?”Aliuliza Roma.
“Umekosea sijawahi kuishi katikati ya binadamu kwa wakati wote , kuhusu wapi nimetokea sitoweka wazi kwa faida yako , babu yako alipaswa kukuelezea kwanini DNA za mwilini mwako tokea unazaliwa ni tofauti na binadamu wa kawaida na sio kwako tu kwa familia nzima”
“Yule mzee anapenda kuongea ujinga kama wewe tu .. lakini kama kweli wewe ni sehemu ya mababau zetu kwanini umejitokeza sasa hivi au ndio upo hapa kwa ajili ya kunisaidia kutokana na matatizo yanayonikabili ..tena umesema unae Master , je huyo Master wako mpaka sasa bado anaishi na kama alikuwa na uwezo wa kukupatia hii Dhana ya kiuungu ya Gurudumu la upepo na moto unaonaje na mimi ukinipa hizo Dhana zenye nguvu pengine zinaweza kusaidia kupandisha joto la dunia .. unapaswa kujua sasa hivi binadamu wanakufa je hampo tayari kuokoa dunia, mimi nipo njia panda imekuwa ngumu kwangu kudili na binadamu na miungu kwa wakati mmoja , Athena ni mjanja sana na siwezi kushindana nae”Aliongea Roma na kwa jinsi alivyokuwa akiongea kwa kutia huruma iliwafanya warembo wake kuangua kicheko
Lakini licha ya hivyo mzee Yasu alionekana kutojali sana tabia ya Roma ya kubembeleza bembeleza.
“Nini napaswa kukuambia ? kidogo tu unichanganye”Aliongea na kisha alisimaa na akaendelea kuongea.
“Kinachoendelea ni janga la kinabii la hatima ya binadamu , wewe ndio utacheza katika nafasi ya kuamua kuishi kwao au kufa kwao , sijaja hapa kwa matakwa yangu mwenyewe na kabla ya kuja hapa niliomba ruhusa kwa wakubwa ili kupimana na wewe ki uwezo , itakuwa ni vizuri zaidi kama nitakuwezesha kuimarika lakini siwezi kukusaidia kupigana na maadui zako , sio kwasababu sipo tayari bali ni kitu ambacho kipo nje ya uwezo wangu?”
Tabasamu usoni mwa Roma lilipotea palepale mara baada ya kuona maelezo yote hayo hayaeleweki.
“Naona unanitania , sio kwamba wewe ni dhiafu kuliko mimi na kama hili likiendelea kila mtu juu ya uso wa dunia atakufa lakini bado tu wewe na huyo unaemwita sijui Master wako hampo tayari kusaidia , je mnataka kuniona nikifanya mazungumzo na miungu , mpenzi wangu ashapotea na napaswa kumtafuta sina muda wa kujali maswala ya binadamu mimi”Aliongea Roma kwa hasira.
Roma mwanzoni alifurahi mara baada ya kugundua kuna watu wenye nguvu kama yeye tu katika uso wa dunia kama Aoiline ataendelea na msimamo wake wa kutotaka kujali kinachoendelea na kukataa kusadia, Roma aliona kuna wengine wangekuwa tayari kutoa msaada lakini hao wanaojiita sijui walinzi wa dunia wanaonekana kutokujali kabisa.
Sasa alijiuliza wanafanya nini ili hali wanajua hana nguvu ya kutosha lakini wanamtaka yeye mwenyewe ndio akadili na miungu , kwa vigezo vipi? Roma aliionekana kukasirika sana.
Mara baada ya Edna na wengine kusikia mpenzi wake amepotea walishajua lazima atakuwa anamzungumzia Clark na kila mmoja aliingiwa na wasiwasi kwani ni kama hali inazidi kuwa mbaya zaidi na zaidi.
Licha ya Roma kuonyesha hasira zake waziwazi , upande wa yule Mzee Yasu alionekana katika utulivu , ilionekana ni kama alitegemea Roma kuwa katika hali hio.
“Kwanza kabisa mambo mengine sio marahisi kama unavyoyaona wewe , wakati tukiwa tunatokea katika mazingira yenye mitazamo tofauti ki asili lazima tutakuwa na maoni tofauti , pili punguza presha mwanamke wako atakuwa sawa lakini hatorudi kwako mpaka saa ya mwisho ya hili janga kuisha”
“Kwahio wewe ndio uliemteka Clark , unajaribbu kufanya nni?”
Roma alikuwa na hasira mmno na alitamani kumpiga mzee huyo palepale lakini ndio hivyo tu hakuwa na uwezo wa kushinda ndio maana aliishia kukasirika.
“Wakati sahihi ukiwadia utajua kila kitu , unachokabiliana nacho hakiepukiki mtoto , umechagua njia yako mwenyewe na utatakiwa kufanya maamuzi ya mwisho , unatakiwa kukumbuka kwamba maamuzi yako ndio yataamua hatima ya binadamu , najua uliweza kufanya maamuzi na kuwa na nguvu lakini kwasasa kila kitu kinategemeana na wewe unapenda au hupendi , hivyo acha kujisumbua kuniuliza neno ‘Kwanini’ wakati unajua jibu kwa maswali mengi”
Dakika ambayo alitamka maneno hayo uso wa Roma ulizidi kuwa mweusi na aliishia kukunja ngumi yake huku akishindwa kuongea neno.
Yasu mara baada ya kumwangalia Roma kwa muda kidogo alianza kukagua wanawake wake mmoja baada ya mwingine na macho yake yalikuja kukwama katika sura ya Rufi.
“Ninaweza nisikusaidie katika maswala mengine lakini huyu mwanamke wako mwili wake una kiwango kikubwa cha nishati ya Yin na inaonekana anakutegemea wewe ili uje kumponyesha sumu iliopo ndani ya mwili wake , ninaweza kukusaidia kumponyesha sasa hivi”
Mara baada ya sentensi yake hio mkononi ilionekana karatasi lililokunjwa kunjwa na ilionekana lilikuwa na maandishi ya mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi na alimrushia Rufi.
“Hio ni mbinu ya kubadilisha Yin na Yang unachotakiwa kufanya ni kutumia asili ya mwili wako kufumua meridiani za mwili wako na utafikia hatua ya kutengeneza uwiano, majini wengi hawajui kwamba mwili wako ni mzuri sana kwa kuweza kupanda daraja katika levo za juu , kama utafuata maelekezo yote katika hio karatasi nakutabiria mazuri”
Rufi aliangalia karatasi lile na alionekana kuwa na furaha kubwa mno kiasi cha kufanya macho yake kuwa mekundu , hakuamini kama ilikuwa ni kweli anakwenda kuvuna nishati za mbingu na ardhi kama wenzake.
Mzee Yasu hakuongea zaidi kwani mara baada ya kutoa ishara flani ya kuaga alimgeukia Lanlan na kisha akatoa tabasamu flani hivi la matumaini na kisha akaondoka.
Roma hakuweza kumzuia kuondoka hapo kwani hata hivyo asingeweza kumzuia kwa lolote.
Wakati huo wanawake wote walikuwa wakimwangalia , waliona Roma alikuwa katika hali ya hatari muda huo na walitaka kuonyesha namna walivyokuwa na wasiwasi juu yake.
“Hubby unapanga kufanya nini , je unataka kwenda kuwatafuta miungu katika Ncha ya Kaskazini?”Aliuliza Edna.











SEHEMU YA 775.
Roma alijikuta akimwangalia mke wake katika macho ambayo yalikuwa na hisia ambazo hazikuwa zikielezeka , ilikuwa ni kama vile kuna kitu anakitafuta lakini mwishowe aliishia kuonyesha hali ya majonzi na kukata tamaa hali iliomfanya kulazimisha tabasamu.
“Nataka kwanza kukaa chini na kufikiria ,,hebu kwanza niangalie hio mbinu ambayo Rufi anakwenda kuanza nayo katika kuvuna nishati za mbingu na ardhi, isije yule mzee akawa amedanganya”Aliongea Roma na palepale alimsogelea Rufi na kisha akachukua ile karatasi na kukariri maneno yote yaliokuwepo.
Dakika chache mbele Roma alionekana kukunja sura huku akitafakari na kisha alimwangalia Rufi kwa uso wa tumaini na kumtingishia kichwa cha kukubali.
“Inaonekana huyo mzee amefanya kitu , hii mbinu inashangaza mno na ya upekee , naona kipenzi chetu Rufi anaenda kuvuna nishati kama wengine..”Aliongea Roma huku akiwa na tabasamu.
Roma alijiambia kama Rufi ataweza kupanda levo kile kitu kilichokuwa kikimuumiza kichwa kwa muda mrefu hatimae kitakuwa kimeisha
Kwake ilikuwa ni kama kupatwa na hali ya joto katika baridi kali..
******
Ni kilomita kadhaa juu ya bahari ya Hindi Mzee Yasu alionekana akipita ndani ya eneo hilo bila ya kujulikana uelekeo wake ni kwenda wapi.
Lakini sasa muda ulele aliweza kuonyesha wasiwasi katika uso wake na kumfanya kuinua mkono na kujaribu kushika hewa iliokuwa mbele yake.
“Thud..!!!
Kilikuwa ni kishindo kikubwa kilichoweza kusikika katika hewa , , ilikuwa ni kama vile juu angani mbele yake kulikuwa na ukuta ambao ulimfanya kushindwa kuendelea kusonga mbele.
Ni kama ukuta huo ulikuwa hapo kwa muda mrefu na kama sio kujaribisha na mkono pengine angeweza kujigonga kwa nguvu na kurudishwa nyuma.
Lakini kwa bahati nzuri ni kwamba ukuta huo ulionekana kuwekwa na mtu ambaye alionyesha kutaka kumzuia ambaye hakuwa na uadui na yeye.
Sasa kutokana na uwezo wake kulikuwa na watu wachache sana ambao wanaweza kumtengenezea ukuta kama huo na kumzuia hivyo kwa haraka sana aliweza kujua aliemfanyia hivyo ni nani.
“Mkuu kwanini unataka kunisumbua , wewe ni mkuu mwenye karama kubwa kama ilivyo kwa kizazi cha Master wangu , si ni kujishushia hadhi kujaribu kumtega mtu mdhaifu kama mimi”Aliongea Yasu huku akionyesha hali flani ya kunyenyekea.
Ijapokuwa alishindwa kumjua aliemuwekewa mtego wa kumzuia ni nani lakini hakutaka kujifanya kijogoo.
Kufumba na kufumbua , mwanamke mrembo sana mwenye nywele zilizokuwa zikipeperushwa na upepo alijitokeza akiwa amezungukwa na mawingu , alikuwa mzuri kama malaika wa kike.
Mwanamke huyu hakuwa mwingine bali ni Aoiline jini jamii ya mapepo wa Mbweha wa mikia tisa.
Wakati huo hakuonekana yule mwanamke mchangamfu bali aliekuwa kauzu na siriasi.
“Dogo vipi , mkufunzi wako yupo wapi , nataka unipeleke kwake”Aliongea Aoiline akimwitwa Yasu Dogo
Upande wa Yasu alikuwa katika kiwewe mara baada ya kuhisi msisimko usiokuwa wa kawaida umemzunguka.
Master wake alikuwa sahihi , ukiachana na yeye mwenyewe kulikuwa na Mbweha wa mikia tisa ambaye alikuwa na uwezo wa juu sana , kwa jinsi alivyokuwa akijisikia ni kama vile yupo mbele ya Master wake, aliwaza hivyo Yasu.
Ilikuwa ni kama vile mtoto amesimama mbele ya jitu kubwa la miraba minne na angeuliwa pengine kwa teke moja tu.
Ukweli ni kwmaba Roma hajawahi kumuona Aoiline akitoa msisimko wa aina hio , ni kwamba Aoiline hajawahi kufanya hivyo mbele ya Roma.
“Madam , Mkufunzi wangu ametarajia hili na ameniambia nitakutana na wewe njiani na wakati huo nitapaswa kukupeleka kwake , hivyo huna haja ya kuomba ruhusa yangu”Aliongea Yasu.
Aoiline alikunja sura na aliondoa mkanamizo wa nguvu ake za kijini na kumwangalia Yasu kwa mshangao kidogo .
“Kwahio unasema master wako ameonyesha nia ya kutaka kukutana na mimi?”
“Ndio amesema ana shukrani kubwa kwako kwa kutoingilia hali ya dunia ilivvo kwa sasa , amesema pia wewe ndio mtu pekee unaemjua vizuri kwa miaka elfu hamsini na zaidi..”Aliongea Yasu na kwa mara ya kwanza Aoiline alionyesha hali flani ya aibu za kike lakini iliodumu kwa sekunde chache tu na kumpelekea hata Mzee Yasu mapigo yake ya moyo kusimama.
Yasu hakuamini angeweza kuona mwanamke mrembo wa namna hio , lakini hata hivyo kwa miaka yote elfu nne alioishi alikuwa na hamu mno ya kukutana na Aoiline kwani alishazisikia habari zake nyingi.
Alijiambia ni Master wake tu pekee ambaye ana uwezo wa kuvumilia kutokuonana na mrembo wa naman hio kwa miaka mingi namna hio.
“Kama ni hivyo ongoza njia , nataka kuona huyo mzee aliamua kujifichia wapi maana nimetafuta dunia nzima bila ya kumuona”Aliongea Aoiline
Yasu hakutaka kuthubutu kumchelewesha mrembo huyo hata kwa sekunde na palepale alimpa ishara kisha akageuza na kupaa kuelekea upande wa mashariki.
Walikuwa wakisafiri kwa spidi kali sana na ndani ya sekunde tu walikuwa washatokezea upande mwingine wa dunia katika ardhi ya kitropical ndani ya kisiwa cha Jamaica kwa Walatini huko.
Hiko kisiwa kilionyesha kutokuwa na maendeleo makubwa kulikuwa na makazi ya watu wachache sana yaliokuwa yakionekana na asilimia kubwa ya nyumba zilijengwa kwa nyasi na matope , karibia wakazi wote ni Wamerika wa kihindu.
Aoiline macho yake ya kijjini yalisafiri katika eneo lote hilo na alionyesha kushangaa kiasi.
“Mkufunzi wako ndio anaishi hapa?”Aliuliza
Sio kwamba Aoiline alikuwa akidharau hayo maeneo lakini hakuweza kuamini mtu ambaye ana chaguzi nyingi kuamua kuishi katika eneo kama hilo.
Kubwa zaidi ni kwamba kile ambacho kisiwa hicho ilikuwa ikijivunia nacho hakikuwepo tena kutokana na dunia kupoteza joto, misitu iliokuwa ikionekana ilikuwa ni swala la muda tu kupotea.
Jamaica ilikuwa na hali ya joto pia lakini ilikuwa ni swala la muda tu na sehemu hio kuganda kwa baridi
Yasu aliishia kutingisha kichwa kumwitikia Aoiline na kisha aliendelea kusonga mbele.
Katikati ya kisiwa hicho karibu na upande wa Kaskazini kulikuwa na mwinuko mkubwa kama bonde, mita mia tatu usawa wa bahari na juu yake kileleni kulikuwa na vijumba vidogo vya matope vilivyokuwa vikionekana.
Usipo angalia makini usingedhania kama eneo hilo kuna binadamu ambaye anaishi.
Dakika hio hio alionekana mwanamke ambaye amevaa nguo kwa kujifunga na matambara hivi kama wale watu wa zama za kale huku nywele zake ndefu akionekana kuzibana na kibanio cha mti.
Alionekana kuwa katika umri wa miaka therathini hivi au arobaini na alikuwa na umbo matata sana na muonekano , ni kwamba tu mavazi yake yalikuwa yameuficha ule uzuri na kumfanya kuonekana kama maskini.
Mara baada ya Yasu kutokeza akiwa na Aoiline yule mwanamke aliweka chini kikapu kilichotengenzwa kwa mianzi na alisugua mikono yake kwenye nguo zake kabla ya kugeuza uso wake na kumwangalia Aoiline.
Ijapokuwa hakutabasamu lakini aliinamisha kichwa chake kwa namna ya heshima kumsalimia Aoiline.
“Salamu kwako Madam”
Mara baada ya kusalimia aliendelea na shughuli yake , alionekana alikuwa bize kupangilia dawa aina ya mizizi ili ikauke lakini ukweli ni kama hajafurahishwa na ujio wa Aoiline.
Aoiline alimwangalia yule mwanamke hasa umbo lake kwa macho ya kidadisi na kumwangalia Yasu katika tabasamu.
“Huyu ni mwanafunzi mwandamizi mwenzako?”Aliuliza.
“Haha.. ndio jina lake anaitwa Li Xuemei ni binadamu mtangulizi wa ukoo wa Li kutoka China , ni mtu mkimya sana lakini anakuheshimu tafadhari usijali sana tabia yake”Aliongea Yasu.
“Hehe.. ananipotezea kama vile nimemuibia bwana , kama ningekuwa nimekasirika asingekuwa hai mpaka sekunde hii na hata Master yako hawezi kunizuia”
Licha ya muonekano wake wa uchangamfu na tabasamu lake kwenye uso lakini hakutoa macho kwenye mlango wa kutokea wa nyumba iliokuwa mbele ake.
Hali ya kihisia ilionekana katika macho yake kwa wingi mno.
Ni muda huo huo mwanaume alionekana akitoka nje ya kijumba hicho cha matope.
Alionekana kuwa wa kawaida sana kwa macho ya kibinadamu , akiwa na makadirio ya umri kama miaka hamsini hivi , alikuwa ni kama msomali au tuseme muarabu na nywele zake zilikuwa fupi na tabasamu hafifu sana lilionekana katika uso wake , ukimwangalia kwa ukaribu lazima ungejua ni Handsome ni hivyo tu alionekana kama vile amekosa matunzo.
Ukweli ni kwamba kwa muoneano wake hakuna mrembo yoyote ambaye angempenda hasa wale wanawake wanaoangalia maokoto zaidi kwani alikaa kama vile ni mkulima wa Tumbaku alieishi kijini ambaye anavuta tumbaku hio hio.
Miguuuni alikuwa amevalia viatu kama ndara rangi nyeusi pamoja na kanzu iliokuwa imefubaa sana ya rangi ya ugoro.
Wanasema umdhanie kumbe sie ndio kilichokuwa kikiendelea kwa wewe binadamu ungemuona ni binadamu ambae hatamanishi lakini wataalamu au watu wenye uwezo wa juu sana wa mafunzo ya kijini wangejua huyo mtu sio wa kawaida.
Wasifu wake halisi ulikuwa umezikwa chini kabisa ya bahari na ulikuwa ni wa kipekee sana.
Mwanaume huyo alionekana kama mpita njia ndani ya mtaa na mwanamke alikuwa ni kama malaika alieshushwa kutoka mbinguni.
“Za siku nyingi Aoiline!?”
Mwanaume ndio aliekuwa wa kwanza kuvunja ukimya mara baada ya kuangaliana na mrembo huyo kwa muda mrefu.
Sauti yake ilikuwa ya kizee tofauti kabisa na muonekano wake, ni salamu nyepesi lakini ilimfanya mrembo Aoiline macho yake kuwa mekundu kama vile anataka kulia.
Ghafla tu upepo ulianza kuvuma kwa kasi na nguvu za kijini zilianza kujikusanya katika eneo walilosimama, zilikuwa ni nguvu kutoka kwa Aoiline.
Na ilikuwa ni kama vile juu ya kilele hicho kumetegeshwa mabomu mia moja ya nyuklia ambayo yanakwenda kulipuka mara baada ya sekunde kumaliza kuhesabu , jambo ambalo lilimfanya Li Xuemei na Yasu kushangaa mno.
Uwezo wa jini Aoiline ulikuwa sio kitu ambacho wanaweza kuelewa kwa fahamu zao , wawili hao walikuwa wakipata shida kuvuta pumzi kutokana na mkandamizo unaotokea na walishindwa hata kusoge kwani ni kama wameshikwa na jinamizi.
Ulikuwa ni mkandamizo wa kisheria ambao upo nje ya fikra zao, kama sio Aoiline kujizuia pengine kisiwa hicho kingeporomoka.
Dakika hio hakueleweka kilichotokea lakini yule mwanaume alipotea alipokuwa amesimama na alipokuja kuibukia alikuwa mbele ya mwanamke mrembo Aoiline na kuweka mkono wake kwenye bega lake kwa namna ya kumtuliza na ndio wakati ambao ule mkandamizo uliokuwa ukitokea ni kama vile umeshikiliwa na mwanamume huyo.
“Ine kwanini unafanya hivi , kama unataka kuniona haina haja ya kuwa hivi”Aliongea akifupisha jina la Aoiline na kutaja ine.
“Kwanini nisiwe hivi Sharif , umenitelekeza kwa miaka elfu hamsini kisa tu ya majukumu kwangu ilikuwa sawa lakini kwannini ulinidanganya kuhusu jina lako na wasifu wako , kwanini nisiwe hivi au unataka kusema kila kitu ilikuwa ni mipango yako , au niliona vitu vile kwa bahati mbaya … kwanini hukuniambia wewe ni binadamu tena mtangulizi wa Koo ya Sharif , mshenzi weweulipaswa kufa muda mrefu sana”.
“Najua unachojisikia mara baada ya kupita kizingiti kwa mguu mmoja, nadhani umeona maandishi niliokuachia juu ya paa la mnara , lakini juu ya yote unapaswa kuelewa nia yangu haikuwa mbaya , je unataka yaliopita yakuendeshe?”Aliongea mwanaume aliefahamika kwa jina la Sharf.
“Upo sahihi nimepita mnara na mguu mmoja lakini usisahau ninao mguu mwingine”
“Nilidhani utakuwa umebadilika baada ya miaka yote hio lakini upo vilevile , kama sikosei ungeweza kupita kwenye mnara muda mrefu lakini ukaacha kufanya hivyo”
“Hata kama ningetaka kupita nisingechagua mbinu kama yako ..”Aliongea na kisha alijitahidi kujituliza kwa kuvuta pumzi nyingi.
“Sitaki kuendelea kuongea vitu vinavyonikasirisha haikidhi nguvu zangu kwa mzee kama wewe”
Alionekana ni kam ameyegemea kauli hio na aliinua kidole chake kumnyooshea Aoiline.
“Wewe..”
“Nini! , unadhani nashangaza , unataka kuniona nikiendelea kulia lia mbele yako na kushindana na wewe , sitaki kuua wanafunzi wako kwani najua kujifurahisha mwenyewe vinginevyo nisingeishi miaka yote katika ulimwengu wa majini pepo”Aliongea Aoiline na kumpa jicho la pembeni kwa kujiona hayumbishwi na hisia na kisha aliingia ndani ya kibanda cha mzee huyo.
Eneo lote lilikuwa likinuka madawa tu huku kuta za kijumba hicho zilionekana kujengwa lwa tamaduni za makabila ya eneo hilo.
Sharif aliingia ndani akiwaacha wanafunzi wake nje.
“Nilifika kisiwani hapa miaka ishirini iliopita , nilikuwa natembea tembea tu huko na huko na ndipo nilipo kuja kukutana na mtoto mdogo ambaye ameng’atwa na nyoka , kwa bahati nzuri mama yake alikuwa akiomba msaada na kwasababu nilikuwa mnyonge kipindi hicho niliona bora nijichangamshe kwa kumuokoa huyo mtoto , nilimsaidia kumponyesha kwa baadhi ya dawa za mitishamba na baadae wakazi wakaamua kunipatia chakula na eneo kama shukrani , hali ya hewa ya hii nchi ni nzuri na tulivu kiasi cha kunifanya kuamua kuweka makazi yangu hapa na kujikusanyia mimea misituni na kusaidia wanakijiji .. ni miaka mingi ijapokuwa kwa watu kama sisi inaweza kuwa siku chache lakini kwa binadamu ni muda mrefu”
“Ndio maana nilishindwa kukupata mara baada ya kukutafuta mara kibao , nadhani kwasababu ya uwezo wako kuwa mkubwa kiasi kuliko wa kwangu ndio maana nilishindwa kukupata lakini kulingana na uelewa wangu nilienda katika maeneo ambayo niliamini ungekuwepo lakini sikukuona , kwahio unataka kusema umebadilika ndio maana umeamua kuja kuwa dokta katika eneo kama hili”Aliongea Aoiline.
“Nilitaka kubadilisha mazingira na vitu ninavyofanya , unajua kutokana na uwezo wangu inaboa kukaa bila cha kufanya”
“Mh ndio ipo hivyo..”Aliongea Aoiline na ghafla tu alihama alipokuwa amesimama na kutokezea mbele ya Sharf na kumkodolea macho karibu zaidi na kufanya pumzi zao kugusana.
“Kwahio kujipa huu muonekano ndio kusema unainjoi maisha , huonekani mzee sana wala kijana lakini una sura mbaya , usiniambie sauti yako imezeeka mara baada ya miaka elfu hamsini”
“Nisingekumbuka kabisa kama usingeongea sasa hivi , nilijibadilisha katika huu muonekano na katika hii sauti mara baada ya kuanza projekti maalumu ya kufundisha binadamu namna ya kuvuna nishati ya mbingu na ardhi miaka elfu nne iliopita”
“Oh..! Unamaanisha hao watoto wawili hapo nje au kuna wengine?”Aliuliza Aoiline na Sharif alisogea mpaka kwenye kijikabati na kisha alimimina chai ambayo ni dawa ya kijani kwenye kikombe na kumpatia Aoiline.
“Ni stori ya kufurahisha sana , nitakuelezea siku nyingine ila ni maamuzi magumu nilioyafanya mara baada ya kutoka katika ulimwengu wa majini na kukutana na kiumbe ambae anabakia kutokuwa na jina mpaka leo hii ..nimefanikiwa kufundisha binadamu makabila yote , mzungu , Mchina , Mwafrika .Waraabu na kuendelea lakini kwa bahati mbaya walioweza kufanikiwa kunielewa ni watatu tu”
“Unamaanisha hao wawili hapo nje , kama ni hivyo wa tatu yupo wapi?”
“Ndio ni hao wawili hapo nje kuhusu mtu wa tatu ni Mwarabu na anapambana kuendesha jamii yake , ni swala la muda tu utaweza kukutana nae”Aliongea.
Ilionekana walikuwa na mambo mengi sana ya kuongea , kwani walitumia muda mrefu sana na Aoiline alionekana kufurahi baadhi ya stori alizokuwa akiongea.
Yasu na Li Xumei hawakuwaingilia , ukweli ni kwamba ni mara ya kwanza kwa Master wao kuongea kwa muda mrefu namna hio.
“Unaweza ukashangaa lakini wanafunzi wangu wote wamejipatia umaarufu mkubwa kipindi hicho na wameandikwa katika historia lakini mambo mengi yalivumishwa tofauti na kile walichofanya , kwa mfano Li Xumei alifahamika kama Nuba katika stori za kichina na Yasu alivuma kama Walumbe ndani ya Afrika , baada ya kuridhika nao niliwaachia kazi ya kuangalia Gereza la Roho na kulinda binadamu zidi ya majini watu wasivamie dunia… hawakufanya chochote kile kinachohusiaa na maswala ya siasa”
Waliongea kwanzia mchana mpaka siku iliofuata , walionekana kukummbusiana mambo mengi yaliopita.
Siku iliofuatia wakazi wa kisiwa hicho waliweza kufika na kumfanya Aoiline na Sharif kutoka.
Mzee Yasu aliweza kuona mwanaume mmoja wa kizungu ambae ngozi yake ilikuwa na vijidoti doti vyeusi , alikuwa ni mtoto wa mkuu wa ukoo afahamikae kwa jina la Chriss.
Watu wa visiwa hivyo walikuwa wakiwachukulia Sharf na wenzake kama ndugu , hawakujua kama walikuwa na uwezo wa kupaa au kufanya maajabu , yaani ki ufupi hawakuhisi chochote kutoka kwao.
“Chris kuna tatizo?”Aliuliza Yasu kwa lugha ya kingereza.
“Dokta Yasu kuna habari mbaya , haraka mnapaswa kuondoka kwa boti kuelekea bandari iliopo upande wa kusini Magharibi , jeshi la Ulaya limeingia kisiwani na wanapanga kugeuza hiki kisiwa kama kambi yao , baba na wazee wanajaribu kuwazuia kwa kuongea nao lakini nadhani ni swala la muda tu mazungumzo kuvunjika .. baba kaniambia niwajulishe muondoke kabla hamjachelewa , kama wataanza kuua watu na kuiba tutapigana nao mpaka kufa lakini nyie wengine hampaswi kufia hapa”Aliongea kwa haraka haraka.
Ilionekana ni kama vile dunia imerudi katika enzi ile za ukoloni kwani wazungu walikuwa wakilazimisha vitu lakini awamu hii haikuwa kwa ajili ya kuchukua mali bali kwa ajili ya kupata hifadhi.
Yasu na Li Xuemei waliishia kuangaliana kabla ya kuchuuguza kisiwa hicho kwa uwezo wa kitambuzi na kweli waliweza kuona meli za kivita upande wa Kaskazini.
Walikuwa hawana tabia ya kuangalia usalama hivyo walishindwa kuona meli hizo kabla.
Katika hali ya dunia inavyoenda ilikuwa ni sawa kwa wazungu kutaka kuvamia kisiwa hicho kwani kilikuwa ni moja ya maeneo yenye joto na kipo chini ya Serikali ya Jamaica nchi ambayo haina uwezo wa kujilinda na uvamizi.
Dunia ilikuwa kwenye machafuko na hakuna aliekuwa akijali ni nchi gani inavamia nchi ipi.
Lakini sasa hapo kisiwani watu wake walikuwa hawajaendelea kabisa na ilikuwa ni swala la muda kuuliwa wote kama watataka kuingai vitani kwani siraha zao zilikuwa za kawaida sana.
Yasu na mwenzake waliishia kukunja sura kwani Aoiline na Master hawakuwa wametoka bado nje lakini wakati wakijuliza cha kufanya ndio muda ambao waliweza kutoka.
Ilionekana ni kama vile Sharif alikuwa amemlegeza mrembo Aoiline kwani hakukuonekana dalili ya chuki , ki ufupi alionekana kuwa na furaha.
Yasu na Xumei walionekana kushangaa mara baada ya kuona Master wao alikuwa amebadilika muonekano na kuwa kijana kabisa , palepale waliamini lazima itakuwa ndio sura halisi ya Master wao.
Upande wa Chriss alionekana kuwa katika hali ya mshangao mara baada ya kuona watu wawili ambao hakuwa akiwajua wakitoka nje ya nyumba hio.
Yasu na Xumei waliishia kutoa heshima mbele yao na kabla hawajaeleea kinachoendelea Sharif alivunja ukimya.
“Tumewasikia”
“Je unataka tuchukue hatua , nina uhakika watu wa kisiwa hawatojua sisi ndio tunahusika”Aliongea Yasu tena kwa lugha ya kiswahili akionekana alikuwa na mpango wa kutaka kuvamia hizo meli za kijeshi.
“Haina haja , kwasababu Chriss ametuambia tuondoke , basi tunapaswa kuondoka”
“Aa..!”
Wanafunzi hao wawili wa Sharf walionekana kushangaa , ijapokuwa hawajali sana maisha ya watu wa visiwa hivo lakini walikuwa wamewafahamu na kuzoeana nao kwa miaka mingi
Lakini mara baada ya Sharf kuwaambia hivyo , ilikuwa ni kama agizo kwao na hakuna ambaye alikuwa na uwezo wa kukataa na kwa haraka waliishia kuwaaga wale binadamu wa kawaida na kisha walitokomea upande wa kusini magharibi.
Unadhani wana Ajenda gani hao na kinachoendelea
Inayokuja Anjjiu na Wenzake wanamuomba Roma hifadhi baada ya miliki zote kuvamiwa na kupigwa kama ngoma unadhani Roma atawakubalia.
ITAENDELEA
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI: SINGAJOJR

Mono no aware


SEHEMU YA 776.
ILIPOISHIA
Waliongea kwanzia mchana mpaka siku iliofuata , walionekana kukumbushiana mambo mengi yaliopita.
Siku iliofuatia wakazi wa kisiwa hicho waliweza kufika/
Mzee Yasu aliweza kuona mwanaume mmoja wa kizungu ambae ngozi yake ilikuwa na vijidoti doti vyeusi , alikuwa ni mtoto wa mkuu wa ukoo afahamikae kwa jina la Chriss.
Watu wa visiwa hivyo walikuwa wakiwachukulia Sharf na wenzake kama ndugu , hawakujua kama walikuwa na uwezo wa kupaa au kufanya maajabu , yaani ki ufupi hawakuhisi chochote kutoka kwao.
“Chriss kuna tatizo?”Aliuliza Yasu kwa lugha ya kingereza.
“Dokta Yasu kuna habari mbaya , haraka mnapaswa kuondoka kwa boti kuelekea bandari iliopo upande wa kusini Magharibi , jeshi la Ulaya limeingia kisiwani na wanapanga kugeuza hiki kisiwa kama kambi yao , baba na wazee wanajaribu kuwazuia kwa kuongea nao lakini nadhani ni swala la muda tu mazungumzo kuvunjika .. baba kaniambia niwajulishe muondoke kabla hamjachelewa , kama wataanza kuua watu na kuiba tutapigana nao mpaka kufa lakini nyie wengine hampaswi kufia hapa”Aliongea kwa haraka haraka.
Ilionekana ni kama vile dunia imerudi katika enzi ile za ukoloni kwani wazungu walikuwa wakilazimisha vitu lakini awamu hii haikuwa kwa ajili ya kuchukua mali bali kwa ajili ya kupata hifadhi.
Yasu na Li Xuemei waliishia kuangaliana kabla ya kuchuuguza kisiwa hicho kwa uwezo wa kitambuzi na kweli waliweza kuona meli za kivita upande wa Kaskazini.
Walikuwa hawana tabia ya kuangalia usalama hivyo walishindwa kuona meli hizo kabla.
Katika hali ya dunia inavyoenda ilikuwa ni sawa kwa wazungu kutaka kuvamia kisiwa hicho kwani kilikuwa ni moja ya maeneo yenye joto na kipo chini ya Serikali ya Jamaica nchi ambayo haina uwezo wa kujilinda na uvamizi.
Dunia ilikuwa kwenye machafuko na hakuna aliekuwa akijali ni nchi gani inavamia nchi ipi.
Lakini sasa hapo kisiwani watu wake walikuwa hawajaendelea kabisa na ilikuwa ni swala la muda kuuliwa wote kama watataka kuingia vitani kwani siraha zao zilikuwa za kawaida sana.
Yasu na mwenzake waliishia kukunja sura kwani Aoiline na Master hawakuwa wametoka bado nje lakini wakati wakijuliza cha kufanya ndio muda ambao waliweza kutoka.
Ilionekana ni kama vile Sharif alikuwa amemlegeza mrembo Aoiline kwani hakukuonekana dalili ya chuki , ki ufupi alionekana kuwa na furaha.
Yasu na Xumei walionekana kushangaa mara baada ya kuona Master wao alikuwa amebadilika muonekano na kuwa kijana kabisa , palepale waliamini lazima itakuwa ndio sura halisi ya Master wao.
Upande wa Chriss alionekana kuwa katika hali ya mshangao mara baada ya kuona watu wawili ambao hakuwa akiwajua wakitoka nje ya nyumba hio.
Yasu na Xumei waliishia kutoa heshima mbele yao na kabla hawajaeleea kinachoendelea Sharif alivunja ukimya.
“Tumewasikia”
“Je unataka tuchukue hatua , nina uhakika watu wa kisiwa hawatojua sisi ndio tunahusika”Aliongea Yasu tena kwa lugha ya kiswahili akionekana alikuwa na mpango wa kutaka kuvamia hizo meli za kijeshi.
“Haina haja , kwasababu Chriss ametuambia tuondoke , basi tunapaswa kuondoka”
“Aa..!”
Wanafunzi hao wawili wa Sharf walionekana kushangaa , ijapokuwa hawajali sana maisha ya watu wa visiwa hivo lakini walikuwa wamewafahamu na kuzoeana nao kwa miaka mingi
Lakini mara baada ya Sharf kuwaambia hivyo , ilikuwa ni kama agizo kwao na hakuna ambaye alikuwa na uwezo wa kukataa na kwa haraka waliishia kuwaaga wale binadamu wa kawaida na kisha walitokomea upande wa kusini magharibi.
Unadhani wana Ajenda gani hao na kinachoendelea

ENDELEA SASA :
Aoiline na yeye alikuwa amekwisha kuelewa kile kilichokuwa kikiendelea na mara baada ya kumuona Sharif anataka kuondoka bila ya kuchukua hatua aliishia kuguna.
“Aoiline huelewi tu kinachoendelea?’Aliuliza Sharf.
“Hawa watu hawana maana sana kwangu lakini kuna kitu kimoja nataka kuuliza , vinginevyo nitakuwa na mgogoro wa nafsi kupotezea kitu kama hiki”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Kwanini umeandaa mpango mrefuu halafu unasubiri Roma aufanyie kazi , kwanini usiachane na kila kitu na ukaondoka hapa duniani kuacha binadamu wafe”Aliuliza Aoiline katika sauti iliojaa maringo.
“Mara baada ya kufanikiwa kupita kwenye mnara miake elfu hamsini iliopita , mawazo yangu yote yalikuwa juu ya kile nilichoweza kugundua, sitakiwi kufungwa na sababu wala athari za mbingu na ardhi , siwezi kuelezea namna ya kudili na hili ninao uamuzi binafsi”Aliongea Sharif.
“Nimechoshwa na visingizo vvako mimi”Aliongea Aoiline huku uso wake ukionyesha dalili ya chuki.
“Kwanini unakasirika sasa , kama umeficha tafsiri ya maandishi nilioacha kwenye mnara mbele ya Roma inaonyesha unakubaliana na mimi kwa kila ninachokifanya , je kuna ulazima kwa mtu kama wewe na mimi kugombana kwa vitu visivyo na msingi kama hivi?”
“Umeotea nusu ya nia yangu ya kuuficha ukweli mbele ya Roma, nakubaliana na ulichofanya licha ya kwamba hakieleweki moja kwa moja lakini nadhani nayaona matarajio yako , ni hiari yangu kufanya hvi sio kwasababu nakuamini lakini kwasababu naamini katika maono yangu mwenyewe .. yule binadamu mjinga Roma Ramoni atakuja kukufanya ulichokuwa ukikifahamu katika miaka yote hio hakipo sahihi”
“Oh! , matarajio yangu kwa Roma ni makubwa kama hata wewe unaweza kuongea kauli hio kuhusu yeye”
Aoiline alizungusha kiini cha macho yake kama vile anamkagua na palepale kufumba na kufumbua alitoweka.
Kamanda Alex aliekuwa juu ya meli ya kivita alijihisi ni kama vile anaangalia malaika akishuka kutoka mbinguni na vigoti vake vya miguu vililainika akitaka kusujudu.
Lakini ilikuwa ni ndani ya dakika hio hio masikio ya kila mmoja yaliweza kukumbwa na milipuko.
Meli hizo za kivita zilikuwa zimejengwa kwa kuimarishwa na chuma kigumu sana lakini Aoiline aliweza kuzamisha meli zile kwa kutumia nguvu kidogo mno.
Aoiline mara baada ya kumaliza kuzamisha wanajeshi wa Ulaya na meli zao alirudi mlimani kumfuata Sharif na kumwangalia usoni.
“Kama ulitaka kuwatelekeza ni maamzi yako na hayakuwa yangu”Aliongea Aoiline.
Sharf hakujisumbua na matendo yake kwani alimwangalia kama vile ni msichana ambaye anajaribu kumkasirisha mpenzi wake makusudi.
“Siku zangu ndani ya hili eneo zimefikia mwisho , hivyo twende ninakoishi , kuna mgeni huko na hapaswi kuachwa mwenyewe kwa muda mrefu na kujisikia ametelekezwa”Aliongea Sharif.
Kauli hio ilimfanya Aoiline kushangaa lakini hakuuliza swali ni mgeni gani Sharif anazungumzia bali alifuata nyuma nyuma.
****
Ni katika ulimwengu mdogo uliokuwa kimya sana , ndege walikuwa wakiimba na kulikuwa na maua na vichaka kila mahali.
Hewa ilijaa harufu nzuri ya asili , joto lilikuwa la wastani na jua lilikuwa liking’aa.
Katikati ya kipande cha ardhi kulikuwa na majengo mazuri ya mbao ya vyumba juu na chini kama ghorofa yaliozungukwa na maua pembeni ya asili na mengie ambayo yalikuwa ni ya kigeni yalipandwa kwa ukubwa wa ekari moja.
Hasa ndani kabisa ya eneo hilo alionekana mwanamke mzungu alievalia gauni la rangi ya kahawia ya asali akiwa amekaa juu ya ukingo wa jukwaa la mawe nje ya jengo, mkononi alikuwa ameshikiria vitu kama vigongo vilivyokuwa vikiteleza katika usawa kamili vilivyofungwa kwa kamba. ukiangalia kwa mbali unaweza kusema ni vijiti vya mianzi lakini ukiangalia kwa ukaribu utagundua ni vijiti vya mawe ya madini ya jedi.
Safu hio ya mawe ya jedi ya rangi ya bluu bahari ni sehemu inayotumika kutekodi maandishi ambayo huwezi kuyasoma mpaka uweze kuingiza nguvu za kijini.
Yaani kwa lugha nyepesi ni kwamba kifaa hicho ni kama karatasi za kuandikia lakini sio katarasi kwani kifaa hicho chenyewe maandishi yake huwezi kuyaona mpaka uwezo na nguvu za mbingu na ardhi.
Mwanamke huyo mzungu alikuwa akiangalia kifaa hicho kwa furaha kubwa , juu ya jiwe pembeni yake kulikuwa na vifaa vingine kama alichoshikiria.
Muonekano uliokuwa ukionekana mbele ya kiambaza cha jengo hilo ulibadilika mara baada ya watu wa nne kujitokeza kama vile wametokea katika kioo kwa namna walivoibukia .
Alikuwa ni Sharif , Aoiline na wanafunzi wake wawili yaani Yasu na Xumei.
“Sharif naona una maisha mazuri sana , kitendo cha kufanikiwa kutoka ulimwengu wa majini pepo umeweza kujjitengenezea sehemu kama hii ndani ya dunia yenye mandhari mazuri hivi … natamani kuja kujaribisha kitu kama hichi pia”Aliongea Aoiline.
“Ungeweza kufanya hivi kama ungetaka , hebu acha kunidhihaki basi”Aliongea Sharif huku akitembea kumsogelea yule mwanamke wa kizungu.
/Wakati huo yule mwanamke wa kizungu ambaye alikuwa bize kusoma maandishi ya kile kifaa aliweza kugundua uwepo wa watu wengine wakimsogelea na mara baada ya kukunja sura aliweza chini alichokuwa ameshikiria na kumwangalia Sharif na muonekano usiokuwa ukielezeka.
“Senior”Aliongea yule mwanamke kwa kingereza.
“Clark , did you get anything from reading these Jade slips?”Aliongea Sharif kwa kingereza.
Mwanamke huyo mrembo mzungu alikuwa ni Clark ambaye aliletwa hapo na Master Yasu.
“Nilitegemea mtu kama wewe kufuata maswala ya mbingu na ardhi pekee na kutokuwa na ufahamu mbele ya maswala ya kisayansi…”aliongea Clark huku akiwa na tabasamu pana usoni.
“Hata hivyo huu utafiti uliopo katika haya maandhishi umeniacha mdomo wazi…”Aliendelea kuongea Clark.
Taarifa ambayo alikuwa akisoma Clark ilikuwa imechaguliwa na Sharif mwenyewe na alimruhusu asome , haikuwa rekodi ya maandishi ya namna ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi bali ni mawazo ya kitaalamu kabisa kutoka kwa Sharif aliokuwa nayo juu ya maswala sayansi, kwa lugha nyepesi gunduzi zilizokuwa ndani ya maandishi hayo ni vumbuzi ambazo pengine baso hazijagunduliwa katika wakati huu.
“Ni kawaida , kama utaweza kuishi kama mimi kwa maelefu ya miaka utajikuta tu unaanza kujifunza vitu vingi sana hata vile ambayo hujawahi kufikiria , uwelewa wako katika maswala ya kisayansi ni mkubwa sana kuliko wa kwangu , nilichokuzidi ni miaka tu na uwezo lakini likija swala la ubunifu umeniacha mbali”Aliongea Sharif.
“Senior unaenda mbali kunisifia”Aliongea Clark aliekuwa katika tabasamu.
“Kama usingekuwa vizuri kama nilivyosema nisingekusifia , pili wewe ni dhahabu iliojificha na kipimo cha matokeo yasiotarajiwa , kama sio hivyo nisingekuruhusu kuja kukaa na mimi muda wote huu”
Clark mara baada ya kusikia kauli hio na kugundua ni sifa anamwagiwa aliishia kutoa cheko kwa namna ya kivivu .
“Unaongea nini , kwanini unasema huyu mrembo ni kipimcho cha matokeo?”Aliuliza Aoiline.
“Aoiline huyu mtoto sio wa kawaida ,kama ilivyo uwezekano wa Roma kuwa sababu ya mabadiliko ya hili janga linaloendelea , huyu msichana pia ni mtu ambaye anaweza kuutegemea ubongo wake tu na kubadilisha matokeo , sikuwa na jinsi bali kumtenganisha na Roma vinginevyo kwa msaada wake ingemfanya Roma kutofikiria nje ya boksi na kufikia kiwango chake chote cha akili yake”Aliongea Sharif na kumfanya Aoiline asiamini kama Clark alikuwa na uwezo huo.
Clark pia alimwangalia Aoiline kwa shauku , kama isemekanavyo wazuri huangaliana pamoja kwa macho yasiokuwa ya kawaida .
“Unanitania sio , ijapokuwa huyu msichana ni mrembo lakini uwezo wake wa mafunzo ya mbingu na ardhi unakaribia Dhiki …mh uelewa wake na msingi wa mifupa yake ni mzuri lakini kuna gepu kubwa ukimfahanisha na Roma .. nadhani unapaswa kujua kama huyu mtoto atafanya kazi kwa juhudi basi si muda mrefu uwezo wake utaongezeka mara mbili lakini kwanini huyu awe ufunguo?”Aliuliza Aoiline.
“Nini , Senior unamjua Roma , amekwisha rudi , yuko wapi sasa hivi?”Clark aliuliza mara baada a kusikia jina la Roma linatajwa sana.
Aoiline alifikiria kwa muda na alikumbuka Roma alikuwa akimtafuta mwanamke kumbe alikuwa ni huyo mrembo.
“Kumbe ndio wewe ,, ndio mwanamke wake ambaye alichukuliw akw anguvu ,, hehe usiwe na wasiwasi yupo salama ni kwamba tu anaonekana kutokuwa na furaha kutokana na kukosekana kwako”Aliongea Aoiline na kumfanya Clark kushusha pumzi za ahueni.
“Usiwe na wasiwasi , Roma ashajua upo salama , kwasasa ana kazi muhimu sana anaapswa kufanya na anapaswa kufanya maamuzi mapema , kila kitu kikitulia nitakupeleka kwake”Aliongea sharif.
Clark alitingisha kichwa lakini wasiwasi wake ulikuwa haujamtoka , alikuwa na wasiwasi na hatima ya Roma kwani kinachoendeea ni kama vile hakitafsirini kimantiki.
Aoiline na yeye alionyesha hamu ya kutaka kujua kitakachotokea , hakupanga kutoka na angekaa ndani ya eneo hilo hilo ili kuona ni maamui gani Roma anaenda kuchukua.
“Vipi kuhusu Idriss ushamweleza nahitaji kuongea nae?”Aliulia Sharf.
“Ndio Master muda si mrefu ataji.., Naona ashafika Master”Aliongea palepale ni kama vile anga linapasuka kwani mtu mweupe mwarabu aliweza kujitokeza mbele yao.
Alikuwa ni Shekhe Idriss moja vya wanachama wa umoja wa Ant0 Illuminat , kwa namna ambavyo amejitokeza ilionyesha ni dhahiri alikuwa na nguvu za kijini.
“Huyu ndio mwanfunzi mwingine uliekuwa ukimzungumzia?”Aliuliza Aoiline huku akimwangalia Idriss kwa macho ya shauku.
“Salamau kwako Madam”Alisalimia Idriss.
******
Ni juu ya boti upande wa kusini mwa visiwa vya wafu, Ijapokuwa oto wakati wa mchana lilikuwa ni nyuzi tano mpaka sita za joto lakini upepo haukuacha kuwa wa baridi mno.
Ingawa jua halikuwa kali sana lakini Roma alikuwa amevalia miwani ya jua katika kiti cha kuegamia , alikuwa amevalia shati la mikono mifupi na bukta.
Mkononi alikuwa ameshikilia ndoano kwa mkono mmoja huku mkono mwingine alikuwa ameshikiria sigara na alikuwa akivuta moshi na kuupuliza hewni mara kwa mara.
Ukiachana na Roma kulikuwa na kiti kidogo sana maalumu cha watoto na kibonge nyanya Lanlan alikuwa amevaa nguo rangi kama ya baba yake na yeye pia alikuwa ameshikilia ndoano lakini muonekano wake ulikuwa himahima na alikuwa akilamba sana lipsi za midomo yake kama vile alikuwa na njaa.
Sababu ambayo ilimfanya Lanlan kutokuoenkana kuwa na furaha ni kwabsabu Roma alikuwa amekamata samaki wengi sana lakini yeye hakuwa amekamata hata mmoja hivyo ilimfanya kudhihirisha ni namna gani hajaridhika na matokeo.
Wengine wote waliokuwa juu ya boti hio walikuwa wamekamata samaki pia na walikuwa wamejaza katika vyombo vyao na walikuwa washaacha kuvua na kukaa nyuma ya Lanlan na Roma.
Nasra , Dorosi , Neema na wengine ambao walikuwa wajuzi katika mapigshi walikkuwa bize kuandaa Sashimi ,Sushi na Fish steak.
Kila mara harufu ya limao kutoka kwa samaki ilivyozifikia pua za Lanlan ile hali yake ya kutokuwa na furaha ilikuwa ikimpotea na alijikuta akigeuza kichwa chake akianwangalia Nasra anavyokaangiza na aliishia kulamba midomo.
Roma mara baada ya kuona Lanlan hayupo makini alimpiga na kipisi cha sigara kwenye mikono yake na kumfinya.,
“Unaangalia nini , weka umakini wako katika kuvua la sivyo hutoruhusiwa kula kama hutokamata samaki hata mmoj”Aliongea Roma akiwa na tabasamu la uchokozi.
Lanlan alitaka kulia kutokana na maneno ya kukatisha tamaa ya baba yake na kuiambia kwanini baba ni mkatili namna hio.
“Daddy unaonaje nikizama chini ya bahari na kukamata samaki na mkono , kuvua na ndoano hakunifurahishi”
“Uvumilivu wako ni mdogo sana na kila baada ya dakika tatu au tano u shatoa ndoano nje , ndio maana unashindwa kukamata samaki yoyote , kama unaona kuingia majini na kukamata samaki kwa mkono ni rahisi kwanini umepoteza muda mwingi kuvua na ndoano”
“Lanlan alidhania hao samaki ni wajinga lakini naona ni wajanja sana na hawataki kula chambo yangu”
“Acha visingizio , kaa chini kwa utiifu na endelea kuvua”
Roma alisisitiza na hakuwa tayari kukubali kirahisi , alijikuta kama baba mkali lakini ukweli ndani kwa ndani alikuwa na furaha , kuwa na mtoto mjinga ilimfanya kuwa na furaha.
Warembo waliokuwa nyuma yake walishindwa kuvumilia na kuishia kucheka kwa siri , walijua Roma alikuwa akimchokoza Lanlan makusudi
Nasra kama kawaida yake aliweka steki mbili za samaki kwenye sahanni na kisha akampelekea Lanlan.
“Usiwe na wasiwasi kuhusu baba yako anajaribu kukuogopesha tu , hebu kula kwanza”
Lanlan hayo ndio mambo ambayo alipenda na hakusubiri swala la uma wala kisu na alitumia mkono mmoja kushika kipande cha samaki na kungata.
Mara baada ya kuonja utamu wa samaki hakujali tena maswala ya kuvua kwa muda mrefu na alitimua nduki kumsogelea Neema ili kupewa Sushi.
Roma alitaka kumkamata lakini aliishia njiani mara baada ya kumuona Edna akitokea kwenye Cabin akiwa ameshikilia simu monnoni , na ilionekana alikuwa akiangalia kitu.
“Honey mama kanipigia simu , anasema Dar kumetokea vurugu na jeshi linajitahidi kutuliza watu, kutokana na usalama wanahamia mkoaniTanga”Aliongea Edna.
“Nilijua ni swala la muda tu ,kadri nchi inavyofurika wageni ndio nana abavyo wazawa watakosa amani”
“Hata mimi naona ipo hivi , inasemekana imeanzia Zanzibar wazawa hawawataki wageni kwani wanaamini wao ndio chanzo cha kinachotokea duniani , Mungu amekasirika kwa ajili ya madhambi yao’Aliongea Edna.
Ni kweli na haikuwa Tanzania tu nchi nyingi za Afrika fukuto lilikuwa likiendelea chini chini , wazawa wengi wanaamini yanayotokea duniani ni kutokana na Dhambi za wazugu hivyo wale watu wa imani wanaona kuwakaribisha hao wageni ni kujiingizia mkosi.
“Halafu kuna kitu kingine maa amesema nikuambie… Maraisi kumi kutoka mataifa yalioendelea ikiwemo China wanaomba kuonana na wewe kwa ajili ya kikao , wametuma maombi hayo kupitia kwa Raisi Senga”Aliongea Edna
“Hapana , sitaki kabisa kukutana nao najua ni kipi wanataka kuongea hata kabla sijaonana nao , wanachotaka ni mimi kulumbana na miungu na sio vinginevyo lakini mimi sio mjinga wala sio shujaa wa dunia , tkea mwanzo walikuwa wakijifanyisha wajanja sana na walienda mbali hata kumtumia mtu mwenyewe nguvu kuliko mimi kunitishia amani.. lakini sasa hivi tumaini hawana tena na wanataka kunituma kufa”AliongeaRoma akionyesha kukasirika.
“Hey , You are so petty ..”Aliongea Edna huku akimwangali Roma kwa tabasamu lakini hata hivyo alikubaliana na maneno yake , kwanza hakutaka Roma kujiingiza matatizoni kwa ajili ya kupambania binadamu.
Ilikuwa imepita takribani mwezi sasa tokea Roma akutane na Mzee Yasu na arudi duniani.
Upande wa dunia , vifo , njaa na joto la rundia lilizidi kuporomoka na kusababisha uhalifu kutokea kwa viwango vya juu sana kila mahali ndani ya dunia.
Haikuwa katika nchi tu ambazo hazijaendelea bali mpaka nchi ambazo zimeendelea hali haikuwa nzuti kabisa, tena ile sehemu ambazo kulikuwa na nafuu ya joto ndio hali ilikuwa mbaya zaidi kwani kila mtu anataka kuishi ndani ya maeneo hayo.
Binadamu walikuwa wakifa kila siku kwa idadi ya mamilioni na haikuwa hivyo tu ilionekana ndani ya muda mpupitu idadi itaongezeka kwa siku .
Nafasi ya binadamu kuishi ukichana na wale waliokuwa wajuu mfano wa matajiri na viongozi ilikuwa ni ndogo sana.
Sasa katika kipindi chote hicho Roma alikuwa kisiwani kwake tu akitumia muda wake kuwa pamoja na mke wake na mtoto wake licha ya kile kinachoendelea.
Pengine bora hata asingekutana na Yasu , lakini mara baada a kukutana nae palepale hali ilimwingia na kujiambia kwanini yeye ndio ahangaike na maswala ya binadamu ili hali kuna watu wenye nguvu zaidi yake ambao hawataki kusaidia.
Tena wakaenda mbali kabisa na kumteka mwanamke wake ili tu kumfanya akubali hatima yake lakini Roma alijiambihe wote waende kuzimu hatoi mguu wake nje ya kisiwa kwa namna yoyote ile , kama mbwai na iwe mbwai.
Roma hakujiona kama mtu mkubwa ambaye anatumikia raia hivyo aliaua kujificha.
Katika kipindi hicho Roma alikuwa amejua vitu vingi , alikwisha kujua mtu ambaye alikutana nae dodoma mara ya mwisho na kumuonyeshea uwezo mkubwa lazima atakuw ani Mzee Yasu au mtu mwingine mwenye uwezo mkubwa kama mzee huyo.
Kilichomfanya ajue hivo ni kutokana na kwamba walimtumia baba yake raisi Senga kukutana nae ndio maana hitimisho lake lilimwambia mtu yule ni Yasu lakini swali liliibuka je huyu Yasu ndio Master namba moja ambae alikuwa akizungumziwa au kuna binadamu wengine kam Yasu amao wana uwezo mkubwa kumzisi hata yeye.
Roma hakujua kama kulikuwa na binadamu zaidi ya watatu wambao walikuwa katika levo za juu kabisa, mmoja wapo akiw ani Yasu mwafrika , Idriss mwarabu na Xumei mchina.
Moja ya vitu vingine ambavyo Roma aliweza kujua taarifa zake ni kuhusu Zeros umoja unaoundwa na viongozi wa juu kutoka mataifa yalioendelea , wote hao walikuwa nyuma ya kufanikisha kufufuka kwa moo wa Gaia wakitumiwa na Athena lakini mara baada ya athari kutokea ni kama vile Athena amewatelekeza.
Hivyo binadamu hao ambao aliwaona ni kama wajinga waliojiingiza mtegoni wenyewe mwanzoni walikuwa wakiona dunia ipo kwenye mikono yao lakini katika wakati huo ile hali ya kujiamini hawakuwa nayo tena.
Kitu kingine ambacho Roma alijua ni kuhusu uwepo wa wanaojiita walinziwa dunia , tena alijua walikuwa na mawasiliano yakaribu na serikali ya China na hata kiongozi wao wa China alitegemeaa wangeweza kuingilia kile kinachoendelea ndio maana hawakutaka kujihusisha na ujenzi wa safina.
Kama ilivyokuwa kwa Yasu kujiweka karibu na mataifa ya Afrikailikuwa hivyo hivyo kwa Xumei kuiweka karibu na taifa la China , ilionekana raisi wa China alikuwa na ukaribu zaidi na Xumei na alikuwa akimpa kiburi lakini katika hatua ya machafuko kama hio ni kama alipoteza mawasiliano na Xumei kabisa.
Roma hakutafutwa na binadamu tu waliokuwa wakitaka msaada wake lakini hata majini pepo kutoka miliki ya Braki walikuja wakiongozwa na Zike mkuu wa Dhehebu la majini shetani na Latina.
Upande wa Latina alikuja kwa Roma kumuuliza Aoiline kaenda wapi maana inasemekana mara baada ya kufika katika ulimwengu wa jangwa tenganifu hakukaa muda mrefu na alitoweka bila ya kuaga na isijulikane alipo.
Sasa kupotea kwake pamoja na fukuto lililokuwa likiendelea kiasili Latina kama kiongozi alikuwa na wasiwasi.
Upande wa Zike yeye dehebu la majini watunza hazina walimtaka Roma kusaidai ndugu zao waliopo katika ulimwengu wa majinni pepo awatoe , lakini Roma aliibua visingizio vya hapa na pale tu ili mradi kumkatalia , Zike hakuridhishwa na jibu la Roma lakini kwasababu Roma uwezo wake ulikuwa wa juu sana hakutaka kulazimisha hivyo airudi nyumbani kishingo upande.
Lakini sasa kupotea kwa Aoiline kulimfanya Roma kuhisi kabisa ni swala linalohusiana na Mzee Yasu akini hata hivyo zilikuwa ni hisia tu maana hakuwa na uhakika.
Ukiachana na hayo kinachoendelea kati ya miungu na binadamu mwishowe aliona hakuna anaeweza kumlaumu kwnai anachokifanya ni kulinda familia yake
Aliona anapaswa kuishi maisha ya furaha na familia yake na kuhusu kuokoa binadamu aliona wenye nguvu zaidi yake watafanya kazi hio maana alijua si wapo kwanini ahangaike.
Mara baada ya kuongea kwa muda mfupi na Edna Roma na warembo wake walikaa mezani kwa ajili ya kula chakula cha baharini.
Rufi , Yezi na wengine waliongezeka , upande wa Rufi alikuwa ameshavunja kizuizi ambacho kilikuwa kikimfanya ashinwe kuvuna nishati za mbingu na ardhi na muda wowote angeweza kuingia katika levo ya nafsi.
Ukweli ni kwmaba kilammoja alionekana kuwa na furaha kwani wote wlaikuwa wakivuna nishati na kuishi maisha ya starehe , hawakuwa na shinda na hata kama dunia ingezidi kuwa na baridi miili yao ingeweza kustahimili kwa muda mrefu tu labda oksijeni isiwepo.
Roma pia hakuacha kumtafutia Lanlan eneo la peke yake kwaajili ya kuendelea kutambua siri ya andiko la urejesho , ukweli ni kwamba alikuwa amepiga hatua kubwa sana na alimfundisha mapigano ya kawaida na alionekana kubobea sana licha ya utoto wake.
Roma alikuwa na majuto wakati akiwa mdogo hakupta fursa kama aliokuwa nayo Lanlan hivyo hakutaka Lanlan kupitia aliopitia yeye ndio maana alitumia kila fursa kuhakikisha kile ambacho hakuweza kukifanya yeye akiwa utotoni Lanlan anakifanya.
Ikiwa ni muda mfupi baada ya chakula wakati Roma akijiandaa kuondoka katika boti hio aliweza kugundua kuna majini wengi wlaiokuwa wakisogea upande wao na wengi wao msisimko wao aikuwa akiujua.
Kufumba na kufumbbua kundi kubwa la majini watu kutoka miliki za majini walionekana mbele yake.
Kati yao kulikuwa na majini wa miliki ya Kekexil , Xia na Hongmeng na kiongozi wa kundi hilo alikuwa ni Jini Anjiu , Umini na Shombeli
Karibia wote waliokuwa hapo walikuwa katika elvo za maji ya upako lakini kulikuwa na baadhi ya majini ambao walikuwa katika levo za chini mpaka levo ya nafsi akiwemo Xiaoxiao , Zenzhei na wengine
Roma alishangazwa na ujio wao maana ulikuwa sio wa kutegemea kabisa , na haikuwa kwake tu hata kwa wengine wote walishangazwa.
Kwa haraka hraka namna walivyotokea ilikuwa hawajafika hapo kwa fujo bali nyuso zao zilikuwa zimejanzwa na hali ya simanzi.
Ukweli hata Roma mwenyewe alishajua hawapo hapo kwa ajili ya vurugu na hata kama wakitaka vurugu wasingemuweza maana alikuwa amewaacha mbali.
Kitu kingine ambacho Roma aligundua kutoka kwao ni kwamba walikuwa na alama za kutosha za huko walikotoka hakukuwa salama , wengi wao walikuwa na nguo ambazo zimeshachanika , ni kama vile ni wanajeshi waliokimbia vitani.
Kuna ambao walikuwa wametapakaa damu pia kwenye mashati yao ikionyesha walikumbana na mkandamizo mkubwa.
“Mna matatizo gani nyie?”Roma aliuliza mara baada ya kutua katika fukwe akiwa na moyo mzito mno na alionyesha hali ya kuwa siriasi mno kama vile walifoika hapo ni wageni ambao hakuwa akiwahitaji.
Anjiu macho yake yalikuwa mekundu na alikuwa akionyesha ishara za kukata tamaa na hata sauti yake ilikuwa imemkauka.
“Imekwisha ,,, imekwisha…”Aliongea kwa sauti ya kitetemeshi.
“Unamaanisha nini , hebu ongea ueleweke nini kimewapata?”Aliuliza Roma kwa mshangao maana ni kama vile wanataka kulia.
XiaoXiao alikosa uvumilivu tena na alijikuta akiangua kilio na kwenda kumvaa Roma na kuanza kulia.
“Roma.. hiihiii.. miungu wameteka miliki zetu zote na sasa zipo chini yao , babu yangu amefariki kwa kuuliw ana miungu ,.,. sasa hivi hatuna kitu , tumebakiwa watupu.. hii .. hiii”
Roma muoenakno wake ulibadilika alaepale na alishindwa kushituka mara moja mara baada ya kusikia miungu ikihusishwa.
Hakuamini mara baada ya kusikia miungu walikuwa wameiteka miliki za majini watu.
Roma alijua babu yake Xiao atauwa ni Chaopi, uwezo wake ulikuwa mkubwa kama wa Anjiu tu lakini ameuliwa.
Ilionekana miungu wamewapiga majini mpaka maji wakayaita mma , maana sio kwa kutia huruma huko.
Ilikuwa dhahiri kwake kwamba miungu uwezo wao hauvumiliki kabisa , pengine walitaka kuonyesha namna gani wamerudiw ana nguvu kwa kuwapiga majini.
Mshituko ulimfanya Roma kusahau alikuwa mbele ya wanawake wake maana Xiao alikuwa akionyesha mahaba ya waziwazi na alijiuliza huyu mwanamke katokea wapi ghafla tu na kumvaa?’
Roma mara baada ya mshituko kumtoka aliishia kumtoa Xiao katika mwili wake na hakuongea neno kwani aliona angezidi kumtia huzuni mwanamke huyo ambaye alionekana kupoteza kila kitu.
“Hebu nyamaza kwanza kwasasa”
Aliongea Roma na palepale alipiga hatua kumsogelea Zenzhei na ndugu zake akiwepo Nefi.
Lakini wakati huo majini hao kutoka Hongmeng wlaionekan katika hali ya majonzi hata Zenzhei ambaye Roma alimjua kama mtulivu alionekana kuwa hayupo kawaida.
“Mr Roma…”
“Bi Zenzhei nini kimetokea na ni miungu ipo iliowashambulia?”Aliuliza Roma akimaanisha ni yupo kati ya viumbe hao wamewashambulia.
Zenzhei aliinua mdomo wake kutaka kuongea kitu lakini alionekana kushindwa kwani ni kama amemeza kitu kizito shingoni na machozi mengi yalimtoka.
“Roma acha kumalizimisha Zenzhei kuongea , Mzee Wucheni amefariki wakati wa vita na ndugu hao wanapitia wakati mgumu wa kumuomboleza”Aliongea Shombeli.
Roma alishangaa mara baada ya kusikia Wucheni alikuwa amefariki , lakini hata hivyo aliona ni sawa kama Chaopi amekufa licha ya kuwa na uwezo wa juu.
Ndio maana Zenzhei na nduguze walionekana kuwa na huzuni mno , hata kama ilionekana kuna kizuizi kati yake na mjomba wake lakini kifo chake kilimtingisha.
“Ni Master Yanyu na Rozu dada wa tatu kutoka Panas na mwingine ambaye alionekana kama mzungu lazima atakuwa ni moja wapo ya miungu”Alijibu Anjiu.
Roma alishangaa alikuwa amemsikia Yanuni ni moja wapo ya majini wanaokamilisha ya wazee wanne kutokaHongmeng.
Kwa taarifa alizokuwa nazo ni kwamba Yanyu alikuwa aksihiriki mara chache katika matukio yaliojumuisha miliki hio na alikuwa ni moja wapo ya muumini mzuri tu wa dini ya Kibuddha.
Sasa alishangaa kama Hongmeng na Panas zote kulikuwa na miungu kati ao , ilishangaza kweli kweli
“Sikuwahi kuwaza kama Master Yanyu atakuwa sehemu ya miungu , kulingana na mbinu zake za kivita alikuwa akitengeneza moto wa ajabu , sio yeye tu ni ngumu pia kuamini hata kwa Rozu pia”Aliongea Umini.
Roma aliwaza palepale kwa kuunganisha matukio na mara baada ya kufika katika sura ya Hermes kuna kitu kilimjia, kwa maelezo ya Anjjiu moja ya watu waliowashambulia alionekana kuwa mzungu alievalia viatu vya mbawa ikimaanisha moja kwa moja ni Hermes na kama ndio hivyo basi Rozu atakuwa ni Hera maana Athena ni mwenye tabia ya kupenda kufana vitu peke yake.
Roma alijiuliza viumbe hao ni kipi wanachokiwaza maana tayari washawasukumia binadamu kwenye hatari na niswa na kusem wanaitawala dunia sasa kulikuwa na haja gani ya kuvamia na majini.
Lakini hata hivyo Roma hakuwa na mpango wa kuelezea kile ambacho anajisikia. Ukweli ni kwamba majini hao hawakuwa marafiki zake na angalau wanapaswa kushukuru alikuwa mkarimu na kutowaua.
“Nimeshasikia kilichowatokea lakini bado sijajua dhumuni lenu la kuja kisiwani kwangu?”Aliongea Roma.
Majini hao hawakuonekana vizuri sana , ilikuwa ni kama vile tumaini lao la mwisho limepotea na Roma aliweza kuona namna ambavyo walikosa hiari na hali ya kujishusha.
“Nakumbuka kuna watu hapa walitaka kutuua tena kwa namna ya kidhalimu , kilichopwata ni Karma ya asili ambayo mmejitegeshea wenyewe lakini hebu jiangalieni sasa hivi mmekuja kwa ajili ya kuomba hifadhi hamuoni kwamba mmekosa aibu?”Aliongea Mage katika sauti ya makasiriko.
Magdalena upande wake katika wakati huo aliona yaliopita wapotezee , isitoshe ni swala zito ambalo halikuwa likihusisha majini tu bali binadamu wote na alimvuta Mage mdogo wake ili asiendelea kuingilia maamuzi ya Roma lakini Mage aliojnekana kukataa.
“Sister kwanini unanivuta , nimekosea wapi , wanajifanyishya kama vile hakuna kilichotkea na kuja kutuomba hifadhi , najihisi kichefu chefu hata kuwaaangalia”
“Magee..!!”
Magdalena aiishia kuita jina la mdogo wake kwa sauti ya chini huku akiwaangalia watu hao kutoka ulimwengu wa majini watu
Magdalena aliona licha ya wamba majini hao walikuw ana chuki zidi ya roma lakini hakuwa na haki ya kuwahukumu kama walivyotaka kufanya.
Maini hao mara baada ya kusikia kauli ya Mage sura zao zilizidi kujikunja kwa huzuni huku wakishindwa kuongea neneo.
Walikuwa wakijiona ni wa juu sana kwa zaidi a miaka mia mbili na inaweza kuaminika kwamba walikuwa wakichukulia binadamu kama viumbe dhaifu.
Lakini wakati huo kuamka kwa miungu na binadamu majiniasi imewafikisha katika hatua ambayo makazi yao yamekuwa sio neema tena na wanapaswa kwenda kumuomba kijana wa miaka ishirini makazi.
Waliamini ni Roma anaeweza kuwassaidia kwani ndio mtu pekee anaewaelewa.
“Mr Roma Mage yupo sahihi , ijapokuwa baba yangu alishiriki peke yake lakini sisi ni familia moja , hakuna mwenye haki ya kukuomba msaada hapa”
Roma alichukia kuona kundi la majini vijana kutoka Xia lakini hakutaka kuwalenga kutokana na heshima yake kwa Zenzhei
“Bi Zenzhei huna haja ya kuwa mnyenyekevu hivyo , ninaweza kupotezea kila mmoja hapa lakni sio wewe , umenisaidai sana kunifikisha hapa nilipo leo , mimi bado ni muumini mzuri wa falsafa ya shukrani na kulipa fadhila , isitoshe wanufaika wangu ni wachache”
“Asante sana Mr Roma kwa kushukuru , kwa maneno yako hayo nimeridhika lakini hawa wakuba wote waliokuwa hapa wana umuhimu mkubwa kuliko wangu , ulimwengu wa majini umekwisha kusambaratika na kizazi pekee cha majini watu kilichobakia ni hawa , kama hawa watu watapotea wasiwasi wangu kizazi chote kitatoweka na dunia itakosa uwiano”

“Bi Zenzhei ijapokuwa nakuheshimu sana lakini kuna vitu siwezi kufanya kwani ni kwenda kinyume na sheria zangu , busara hulipwa kwa busara na kisasi kwa kisasi na sitokuja kuwa jinga kwa kumlipa mtu busara ili hali hastahili .. karibia ya kila mmoja aliefika hapa hahusiani kwa chochote na mimi na pia ni maadui zangu , sina mpango wa kuwaua mbele ya binti yangu na sitaki damu yao kuchafua nyuma yangu lakini siwakaribishi kukaaa hapa kisiwani pia , zaidi ya yote kama miungu watakuja na kuona nipo upande wao si itaniletea tu matatizo , ni kweli uwezo wangu ni wakushangaza lakini shidhani ninao uwezo wa kumshinda Athena ambaye uwezo wake wote umarudi , hivyo sitaki kufanya kitu ambacho kitaharatisha usalama wa familia yangu”
Zenzhei alitaka kuendelea kumbembeleza Roma lakini Nefi alimzuia kwa kupita mbele.
‘”Haina haja tena dada , huyu mtoto ashajipambanua wazi anaogopa na anataka kuficha kichwa chake kwenye hiki kisiwa kama kobe anavyojificha katika nyumba yake , haijalishi kwa namna gani utambembeleza atajifanyisha ni mwenye kuchanganyikiwa , isitoshe anaweza akawa anashirikiana na miugu , uwezo wetu unaweza usiwe mzuri kama wa wengine lakini angalau tunao ujasiri wa kufa tukipambana”
“Ndio Mzee Wucheni anapaswa kujivunia kwa kuwa na watoto wa namna hii , tupo hapa na ni kweli hatuna chochote tunachowez akufanya lakini sio kwamba tunatamaasana ya kuishi na kuogopa kifo , sasa kizazi chote cha majini watu kipo hatarini ni bora kwenda ncha ya kaskazini na kupambana hadi kifo na miungu , angalau tutakufa bila soni kwenye mioyo yetu”Aliongea Shombeli.
Baada ya kuamshwa munkari majini wote wlaiitikia kwa nguvu na hamu ya kiwnago cha juu ilikuwa ikionekana kwenye maco yao.
Lakini Anjiu na Umini ambao walionekana kuw awatulivu hawakuongea neneo , walijua kwa hakiak kwamba kwenda ncha ya kaskazini ni kujitafutia kifo na kutokana na hil haina maana.
Roma alipotezea hali yao ya msisimko na alichokuwa akijali hapo pengine ni maisha ya Xiao na Zenzhei pekee wengine alijiambia wanaweza kufa kama wanataka.
Muda huo huo juu ya bahari upande wa mashariki jini ambaye alionekana kushikilia mkuki wa mwanga alionekana akiwa ametangulizana na kundi la majini wengine.,
Alikuwa ni Master Shagoni ambaye alipotea kwenye ulimwengu wa majini mara baada ya wenzake kuja kupiganana na roma wakati ul.
Roma kwa kumwangalia mara moja tu Shafoni aliongekana tayari ashapitia mapigo tisini na tisa ya radi ya ambarau , ijapokuwa hakujua ni lini imetokea lakini ilionekana sio muda mrefu , hakika ilionekana bwana huyo alikuwa ni jiniasi na kwa levo hio alikuwa katika levo sawa na Anjiu.
“Shagoni ni wapi ulikuwepo , je unajua miliki yenu ipo hatarini ?”Aliuliza mzee mmoja kutoka Kekexil.
Shagoni alikuwa akigemewa sana ndani ya miliki ya Kekexil lakini pale atatizo yalipot0kea alikuwa haonekani hivyo kufanya wana miliki kutoridhishwa nae.
“Hata sijawaulia bado lakini mshaanza , nilijitafutia sehemu ya kujitenga na kupigia Dhiki yangu ya radi , imewezekana vipi zaidi ya majini mia moja kufariki baada ya kurudi?”
“Unaongea nini wewe , mbona ni kama unaona ni miliki yenu ilioathirika tu , unapaswa kuelewa ulimwengu wetu wote umeangushwa na miungu watatu na koo zote zimepata hasara kubwa, wewe ndio unajikuta kuumia tu na sisi wengine hatuumii”
“Upo sahih, hasara iliotokea ni nje ya mategemeo , nyie siku zote mlichojari ni uhai wenu tu na mkakimbia huku mkiacha majini kiao waliopo levo za chini wakiwa peke ao , kwa bahati nzuri nimewakuta na kuja nao hapa , kuna mtu ameniambia kuna uwezekano nikawakuta hapa”Baada ya kuongea hivyo aliwapoteea wale wazee wa kijini na kisha alimwangalia Roma.
“Wewe mwanaharamu yaani muda ambao najiona nipo katika levo ya kupambana na wewe ndio unapanda levo ambayo inaonekana kabisa sikuwezi tena”Aliongea mara baada ya kumchungua Roma.
Roma alikuwa akichafukw ana roho kutokana na tabia ya ukiburi ya Shagoni
“Kwahio na wewe pia umekuja kuomba hifadhi?”
“Sina kinyongo chochote na wewe na sio kwamba napenda sana kukaa hapa lakini ndio hivyo sina sehemu nyingine ya kukimbilia , kama hutaki niishi hapa nitaondoka”
Roma alionekana kufikiria kwa uda huku akijiuliza je awarhusu hao majini kuishindani ya kisiwa hico , isitoshe aliona kuna baadhi yao hakuwa na kinyongo nao lakini muda huo huo Muonekano wa Magdalena ulionekana kubadilika.
“Master umekuja pi?”
Binadamu mwanamke alievalia gauni la kupendea alionekana akifika ndani ya visiwa hivyo , alikuwa ni Master yake Magdalena anaefahaika kwa jina laa Tang Luyi kutokaDehebu la Tang .
Ni muda huo huo Roma aliweza kugundua Tang Luyi alikuwa mwishoni mwa levo ya nafsi , ilionekana aliingia ulimwengu wa majini na ndiopo alipoweza kukutana na Shagoni na kuafuara nyuma.
Upande wa Tang Luyi alionekana kutokumsikia Magdalena kwani macho yake yote yalikuwa kwa Anjiu , alionekana kama vile ameona kitu kilichomfanya kupaniki kiasi cha kumpelekea kutokushindwa kupumua vizuri.
Wkati huo huo \ Anjiu aliweza kugeuka na dakika ambayo aliwez akumuona Anjiu muonekano wake ulikuwa umejaa mshituko.
“Wang..Sheng ni wewe kweli?”Aliongea Tang Luyi huku akionyesha kutoa machozi.
Roma naMagdalena wote wlaionekana kushangaa , kwa Roma haikwua san akwnai tokea mwanzo alishaotea uhusiano ulipo kati ya Anjjiu na Tang Luyo na Xiao kuwa mtoto wa mwanamke huyo,
Anjiu aliishia kukunja ngumi yake kwa nguvu na Xiao aliishia kumwangalia baba yake na mwanamke asie mjua kwa macho ya kiulizo.
Hali ya hewa ilibadilika na ilikuwa ni kama sasa majini waliofika hapo wanajua kwamba Anjiu mkuu wao alishawahi kuwa na mahusiano na bindamu ambaye yupo katika levo ya nafsi.
“Sijakosea kabisa , ni wewe kweli , ijapokuwa umebadilika lakini siwezi kusahau macho yako , Wang Sheng hebu nijibu mara moja wewe mwanaume muogo sana , ongea”
Tang Luyi alionekana kubadilika ghafla tu na hasira zilianza kumpata na alimshika Anjiu kwa nguvu na kuana kumtingisha akimtaka kutoa majibu huku machozi yakimtoka.
Kila moja hapo alijua kinachoendelea , ilionekana Anjiu alimdanganya jina Tang Luyi , ukweli ni kwamba ilikuwa kamakwa Bi Wema tu alivyodanganywa na jini.
“Hey mwanamke ,kwanini unamfanyia hivyo baba yangu , huruhusiwi kumgusa baa yangu”Xiao alionekana kukosa uvumilivu na alitaka kumuondia Tang luyi mbali na baba yake.
Lakini mara baada ya Tang Luo kusikia msichana huyo anamwita Anjiu baba palepale alibadilika na kmshika mkono na kumnwagalia kwa fuarha kubwa.
“Wewe mtoto , umemuitaje hivi sasa huyu mwanaume , wewe ni binti yake , una miaka mingapi mwaka huu?”
Xiao aliona huyu mwanamke ni kama kichaa na aliishia kumwangalia baba yake kwa kuomba majinu lakini alikuja kugundua baba yake macho yake yalishabadilika na kuwa mekundu.
“Baba ni nini hiki..”
“Anjiu acha zako , ndio kwamba haupo tayari kumtambua , hata hivyo haijalishi kwani atabakia kuwa mama mzazi kwa binti yako”Aliongea Roma mara baada ya kuchoshwa na maigizo.
Lakini kauli nyake ilimfanya kila mmoja kumwangalia kwa mshangao mara baada ya kuona Roma alikuwa akijua kinachoendelea.
Roma mwenyewe hakuwa na uhakika sana , ukweli ni kwmaba aliona ni kheri kwa xiao kumjua mama yake maana mara ya kwanz akukutana nae alionekana kama vile alichagua nchi ya Tanzania kujakumtafuta mama yake baada ya kudaganywa na baba yake kama mama yake ni muafrika.
Nusu saa mbele hatimae Xiao aliweza kumtambua kwa mara ya kwanza mama yake mara baada ya kuthibirishiw a na baba yae , ilikuwa ni furaha kubwa kwake kujua mama yake alikuwa hai na alifurahi kuona pia mama yake alikuwa mrembo na kijana.
Kutokana na tukio hilo ambalo lilimgusa Roma pengine kutokana na maisha alioishi hata yeye ya kuroahamu wazazi wake ndio maana aliamua kuruhusu majini hao kuishi hapo kisiwani , hara hivyo aliona hakuna tatizo ili mradi hawana madhara na pili majini hawakuwa na haja ya kuepwa nyumba kwani hata nnje wanaishi.
Upande wa Shagoni na yeye hakuwa na jinsi zaidi ya kubaki hapo visiwa vya wafu licha ya kwamba alikuja kugundua dungu zakewengi hawakuwepo hapo na hata alipoenda kutafuka wengi wao walionekana kukimbia kusikojulikana.
Ndani ya muda mchache tu visiwa vya wafu vilikuwa ni kama miliki ya majini , kulikuwa na visiwa vingi ambavyo vingine havikuwa vikiishi watu hivyo walienda kujichimbia huko lakini pia wengi wao walionekana kama binadau wa kawaida , ukiachana na kamba wanapaa kwa binadamuw a kawaida wa visiwa hivyo wasingewaofgopa na isitoshe wangeonekana mara chache sana kwani wanafisiwa wengi wanaishi ndani tu kutokana na baridi kali.
Athena alionekana kuwa na intelijensia pana sana kwani kati ya majini wa Hongmeng mmoja wapo kuwa kiumbe kutoka sayari nyigine haikuwa bahari mbaya , ilionekana yote hayo yalifanyika ili kujua namna ya kumtuoa Zeus katika gereza la roho lakini pia kutoa taarifa juu ya uzaifu wa safu ya ki ulinzi wa kisiwa hicho cha anga.
Upande wa Hera ambaye ni Rozu ilionekana alikuwa na ajanda zake za siri kama ilivyoikuwa kwa Athena tu na aliamua kuuvaa mwili wa jini kwa kutimiza mipango yake.
Roma pia alikuja kuwaza maneno ya Aphrodite na Apollo , kwmaba licha ya Hephastus mungu wa moto kutokuwa na nguvu kubwa kama wengine lakini alikuwa ameejaaliwa uwezo wa kutengeneza Dhana.
Hata siraha yake ambayo ilifahamika kwa jina la Vulcan Hummer iliaminika sio tu kuweza kusababisha tetemeko ra ardhi na kulipuka kwa volkano lakini muhimu zaidi inaweza kuunganisha nguvu ya Dhana mbili pamoja.
Sasa Roma muda mrefu alikuwa akijiulia ule mshipi feki wa Aphrodite uliotookea nchini Tanzania umetokea wapi na wakati huo ni kama sasa ametegua kitendawili , ilikuwa ni kazi ya Hephaestus.
Kutokana na kukosa malighafi na teknolojia ilimfanya kushindwa kutengeneza siraha nyingi zaidi zenye nguvu.
Kwahio kitendo cha Rozu , Hephaestus na Hermes kwenda pamoja ujinini kushambulia ilimaanisha kwa muda mrefu sana walikuwa na ushirikiano mzuri.,
Kuhusu Rozu ambaye aliamini laima atakuwa Hera aliamini lazima atakuwa amefanya vitu vingi vya siri tena zidi ake lakini kwa muda huo hakuwa akijua kama anaweza kuchukua hatua kwa kila kitu.










SEHEMU YA 777.
Mpaka muda huo sasa Roma alikuwa ashaelewa baadhi ya vitu ambayyo Christen na wengine wlaikuwa wakijaribu kumficha.
Ilionekana kwasababu ya kutaka kufanikisha kufufuka kwa Moyo wa Gaia Christen alikuwa akijua kinachoendelea kwa ngudu zake wengine lakini aliamua pia kumficha.
Ingekuwa ni uongo kusema Roma hakujali isitoshe swala hilo haikuwa dogo hata kidogo na ingekuwa ngumu zaidi kwake kucheza kwenye nafasi ya nusu binadamu nusu miungu lakini hata kama wakati huo ashajua hila zao je atawazuia.
Kuja kwa kundi la maini na baadhi ya jumbe zinazomfikia kila siku ilimfanya Roma kuzidi kukosa maamuzi , ilionekana ni kama baadhi ya vitu vimechanganyika ana anashikwa kuchambua kipi ni kipi.
Siku nne zilipita na hatimae majini waliokuwa wameomba hifadhi ndani ya kisiwa hicho waliweza kupona na hata uwezo wao kuwarudia , watu hao hawakuwa masikini walikuwa wakitembea na vidonge vyo.
Roma hakuwajali sana kwani alijua sio binadamu na hawawei kufa njaa au kufa kwa baridi , hata kama angetaka kuwaweka ndani ilikuwa ni ngumu wote kutosha.
Lakini kutokana na kwamba alikuwa amewapa mahali pa kuishi Zenzhei na wengine basi aliona awapatie na wakuu wa miliki hizo sehemu za kuishi akiwemo Anjiju na Xiao..
Master Shagoni na Anjiu ndio majini pekee abao uwezo wao ulikuwa wa juu na baada ya siku nne kupita walijikusanya pamoja kwa ajili ya kikao na ajanda ilikuwa ni kurudi kwenye ulimwengu wao.
Roma hakuwa kama wao , yeye pengine alikuwa na uwezo wa kuwa na urafiki na miungu lakini wao haiwezekani , hivyo walikaa hapo kwenye miliki yake kwa ajili ya kurudisha nguvu.
Alijua miugu hawawezi kukaa ujinini kwa muda mrefu kwani kilichowapeleka ni kumtoa Zeus kwenye gereza la roho lakini hata hivyo jambo hilo liliwatia hofu zaidi na zaidi.
Majini walijua fika kama Zeus atafanikiwa kutoka , kwa uwezo mkubwa aliokuwa nao basi wao hawatakuwa na aani
Mwisho wa kikao walifanya maamuzi kwmaba Shagoni kwasababu ana spidi kubwa aende Hongmeng akaangalie kinachoendelea , kuna waliokuwa wakiamini safu ya ulinzi wa gereza la roho haivunjiki lakini kuna waliokuwa wakiamini kutokana na kwamba miungu walikuwa wamerudiwa na uwezo wake wote na pia uwepo wa Yanyu ndani ya Hongmeng kwa miaka mingi ni kama alikuwa akisoma udhaifu wa safu hizo.
Siku tatu baada ya kupitaShaogini alirudi akiwa na taarifa mpya juu ya miungu kufanikiwa kukiweka kisiwa cha Anga ndani ya Hongmeng chini yao na mfumo wa ki ulinzi wa kanuni za anga umewekwa.
Master Shagoni anasema hakuwa na ujasiri wa kusogea karibu sana lakini hata kwa mbali aliweza kguundua kwmaba safu ya ulinzi wa gerea la Roho inaonekana kukosa uhimili na muda wowote ingeporomoka .
Alichokuwa akimaanisha ni kama vile utando wa buibui utingishike hivyo eneo lote kutngishika.
Taarifa ya Shaogini iliwafanya kukaa kikao kingine na kufanya maamuzi na mwishowe wote walionekana kukubaliana.
Hawakutaka kuendelea kujifiacha bila ya kufanya kitu na walikubalina majini wote ambao wapo levo ya maji ya barafu kupanda kesho wanaelekea ulimwengu wao kwa ajili ya kupambana na miungu.
*****
Nyakati za usiku Roma alikuwa akuongea na wanawake wake mpaka pale Anjiu alipokuja kumtafura.
Anjjiu hakuingia katika ngome hio bali aliruma ishara za kumuita akiwa nje ya mlima akiangalia mwezi akimsubiria Roma kutoka.
Katika siku zilizopita wapenzi hao wa zamani walikuwa wamerudiana na kuishi pamoja na Roma hakujua hata wanaendeeaje lakini alijua na uwepo wa Xiao basi hali haitookuw ambaya zaidi.
Roma aliweza kutokeza katika kijimlima na kwenda kusimama pembeni ya jini Anjjiu , Anjiu suura yake ilionekana kujikunja ni kama ameeeka ndani ya siku mbili tu.
“Unaangalia nini?”Roma aliuliza mara aada ya kuona Anjiu alivyokuwa akishangaa mwezi , ukweli ni kwamba hakuwa na kinyongo kabisa na jini huyo .
Anjiu alisimama vilevile kwa muda mrefu na alionekana kuvuta pumzi na kisha akamgeukia Roma na kuinamisha kichwa chake kwa heshima.
Jambo lile lilimshngaza Roma na kujiuliza kwanini anamwinamia kwa heshima hivyo.
“Najua mimi Anjiu sina haki ya kusema lakini kitu pekee ninachoweza ni kukuomba kuniahidi kitu kimoja ..”Aliongea na kumfanya Roma kujua anachotaka kusema Anjiu.
“Unataka nikuahidi kupambana na miungu , nadhani nishaweka wazi kwamba si..”
“Hapana..”Aliongea Anjjiu na kisha alisimama.
“Sitarajii wewe kuja kupambana na adui mwenye nguvu na sisi ambao tulikuwa maadui zako , miungu sasa wapo katika levo ambao ni nje ya uwezo wetu”
“Kama ni hivyo nini unataka kutoka kwangu?”
“Luyi na Xiaoxiao ..”Anjiu uso wake ulikuwa ukicheza akionekana kujizuia kile alichokuwa akijisikia moyoni.
“Namaanisha kama kitu chochote kitanipata , tafadhari naomba uwe mwangalizi wao badae”
Roma alishangazwa na kauli ile na kujiuliza kwanini anachosikia ni kama vile wosia wa mtu anaeenda kufa , mwanaume ambaye alikuwa mbele yake alionekana sio yule mjanja mnjanja kutoka miliki ya Xia.
“Inaonekana tayari ushajindaa na huna mpango wa kruudi mara baada ya kwenda kupambana na miungu?”Aliulia Roma akiwa na tabasamu lililojaa uchungu.
“Wewe ndio ujuae vizuri , una uuungu ndani yako hivyo unajua kabisa ni kwa namna gani miungu wameimarika , tunaenda Hongeng kwa ajili ya kuwazuuia miungu wasimtoe Zeus katika gereza la roho .. lakini nikuambie tu ukweli tunaenda kupambana ili historia isije kutuandika vibaya ni sala la kikanuni tu , tunaenda kujitoa kafara”
“Kama ni hivyo kwanini bado mnaraka kwenda kujitafutia kifo , unaweza kujificha kwa muda mrefu , si ndio umeweza kuunganisha familia yako hivi juzi tu?”
“Hapana ni kweli Luyi ni mke wangu na sikuwahi kumsahau hata siku moja …”Alionekana kuwaza kwa muda na kwa jinsi Anjiu alivyokuwa akionekana usingedhania hata kidogo ni jini.
“Najua Xiao anahisia za kimapenzi kwako lakini wewe ni tofauti lakini bado naamini ana sehemu yake katika moyo wako mara baada ya kuweza kukaa nae nyakati zote ulizokuwepo katika ulimwengu wajicho langa .. sitaki binti yangu kuwa na mwanaume kama wewe mimi kama baba yake…siku nilipokuja kugundua mlikutana nilikuwa na wasiwasi atakupenda na mwishowe atafoma kurudi ujinini . ni mtoto anaetia huruma ambaye anastahili mwanaume ambaye atampenda kwa dhati … lakini sasa hivi sina jinsi zaidi ya kutaka kukuamini”
Mara baada ya Anjiu kuongea hivyo aliinamisha mgongo wake na kumwinamia Roma.
Roma alitaka kuongea kitu lakini maneno yalishindw akumtoka.
Kama mwanaume ambaye ana madeni mengi ya mapenzi anaweza kukataa lakini kama baba ilionekana ngumu kumkataliamwanaume mwenzake alietokea kumwamini.
Mara baada ya Roma kumuona Anjiu akitaka kuondoka alimsimamisha.
“Kwanini ?, kwanini unataka kumuacha mkeo na binti yako na kwenda kufa , unajua unaweza kuchagua njia nyingine kwa kutokwenda , hata kama miungu wanataka kuwaua majini wewe unao uwezo wa kukikwepa kifo , kwa niaba ya Master wa mpenzi wangu nakupatia hifadhi , unawez akuishi hapa”Aliongea Roma.
‘Kama nitasema ni kwasababu ya msemo wa kidunia unaosema ‘Kusimama na kuanguka kwa ulimwengu ni jukumu la mtu binafsi utaniamini?”
“Lakini wewe sio mtu ambaye unakumu hilo na sio wewe tu majini wote walipo ndani ya hiki kisiwa sio jukumu lao”
“Umekosea , kila kiumbe chenye utashi ndani ya huu ulimwengu tupo katika daraja moja, sisi wote ni watu wa dunia kabla ya jamii zetu , uwezo wetu na tamaduni zetu na hakuna kinachoweza kubadilisha huo msingi . pengine wewe bado ni kijana mdogo na umeishi maisha yako nje na nyumbani kwa muda mrefu , labda ni kwabsabu una uungu ndani yako na sio binadamu kamili , lakini unapaswa kujua kinachotokea kwa binadamu kina athari za moja kwa moja kwa sisi majini, adui wa majini ndio adui wa binadamu … tunaweza kupigana wenyewe kwa wenyewe lakini kuna mahali tutafikia katika maelewano na kuweka tofauti zetu mbali hii ni kwasababu sisi wote ni wa ulimwengu mmoja licha ya kutenganishwa na vizuizi , sisi wote ni wa hii dunia na huo ndio msingi .. kama viumbe kutoka sayari nyingine wanataka kuondoa mpaka mizizi yetu basi ni sawa kwetu kuinyweshea ardhi yetu na virutubisho vya damu yetu”
Anjiu hakuonekana na huzuni wala na furaha wakati wa kuongea bali alikuwa akiongea katika sauti ya ukweli lakini maneno yake yalimfanya moyo wa Roma kuungua.
Mwanaume aliekuwa mbele yake alionakan kupoteza hadhi yake na alikuwa akipotezea kila kitu , uwezo wake na madaraka yake
Katika wakati huo alijiona si kitu , si kiumbe mwenye nafasi kubwa kam wengine , hakujiona mkubwa kama binadamu bali alijona kwama mwanajeshi kati ya kundi la wanajeshi ambae anajianda akwenda vitani kwa ajini ya familia yake , mapenzi yake na uzalendo wake.
Sio kwmaba hakuwa akikiogopa kifo lakini hakuwa tayari kuigopa hatiima yake.
Pengine hilo ndio kusudi la mwanzo kabisa la Mungu juu ya viumbe wote katika uso wa dunia.. Roma hakuweza kujizuia ali kufikiria.
Mpaka Anjiu anaondoka Roma aliendele akubakia katika kijimlima akiwaza.
Roma aliinua uso wake na kuangalia nyota na mwezi huku baridi kali ikimpuliza na hakuna aliemsumbua..
Siku iliofuata asubuhi majini wote kuanzia levo ya kupita Dhik maji ya barafu waliondoka kwenda ujinini vitani , maagano na ndugu na wapendwa wao ilikuwa jambo lisiloepukika.,
Zenzhei na binamu yake waliweza kuagana na kaka yao Nefi kwa machozi wakati Tang Luyi na XiaoXiao wakiomboleza kuondoka kwa Anjiu.
Mwanzoni XiaoXiao alitaka kumlazimmisha Roma kuchukua hatua lakini Anjiu alimzimisha palepale kabla hata hajaongea neno.
Roma hakuongea neno na kimya kimya aliangalia namna mamia ya majini walivyokuwa wakipoptelea katika upeo wa macho yake.



SEHEMU YA 778.
Milikiya Roma ya visiwa vya wafu hatimae ni kama ilirudi katika hali ya amani na kulikuwa na kimya sio cha kawaida.
Mamia ya majini waliokuwa na uwezo wa chinin walikuwa wamejikusanya katika eneo moja katika kipande cha ardhi huku hali ya hewa ikiwa ni ile ya kimajonzi na kufanya eneo lote kufunikwa na kiwingu cheusi.
Roma aliesimama kandokado ya fukwe alikuwa ameinamisha kichwa chake chini , macho yake yalikuwa kama kioo kana kwmaba alikuwa akifikiria kitu kwa kujiangalia.
Baridi inayotoakana na uepo wa baharini ilikuwa imemloanisha nguo zake lakini hata hakutambua.
Bila ya kujua hatimae mwanadada Rose alimsogelea na kisha kushika mkono wake huku macho yake yakiwa na mahaba mazito.
“Unafikiria nini , unaonekana kuangalia eneo moja bila kutoa macho?”Aliuliza kwa sauti hafifu huku akiwa na tabasamu.
Roma taratibu alikiinua kichwa chake na kumwangalia mwanamke huyo.
“Darling hivi .. hivi unadhani nimefanya kitu sahihi?”
Rose alionekana kushangazwa na swali hilo pengine ni kutokana na kwama amemjua kwa muda mrefu sana kuliko wanawake wote na ilionekana wazi ni kitu gani alichokuwa akiulia , Rose mara baada ya kuwaza kwa muda alionekana kupata cha kuongea.
“Tokea uwe siriasi sana juu ya kufanya maamuzi kwanini hujawahi kutuomba maoni yetu , kwanini umeomba sasa hivi?”
“Unajua kuwaza namna hii sio staili yangu lakini maamuzi yangu yana athari kwa kila mtu na ndio maana nina mawazo”
“Kwanini usifanye hivi mpenzi , naomba uniruhusu nikuulize maswali?”
“Uliza”
“Je unawaogopa miungu , hasa hasa Athena?”
“Hapana , naomba tu niwe mkweli kwako , nisingeweza kuwa hai mpaka sasa kama ningekuwa naonyesha uwezo wangu wote , ijapokuwa ninaweza nisiwashinde wote lakini ni ngumu kwangu kushindwa”
“Je kama hutoenda , unajihisi utakuja kujutia baadae kwa maisha yako yote?”
“Kujutia … dah hapo sijui”
“Vipi kama utajutia , je upo tayari kukabiliana na majuto”
“Bila shaka sitaki kujutia lakini hakuna mtu anaeweza kuishi bila kujutia baadhi ya vitu kwenye maisha yake , ni afadhali ni waone wote mkiwa salama”
“Je unaamini utaendelea kwa nje ya hili kama hotujiunga katika mgogoro kati ya miungu na binadamu?”
“Unamaanisha nini?”
“Unaweza kutokujali maneno ya watu wengine na kupotezea chuki zao lakini kila mtu ni tofauti , ukiachana na wewe hapa kila mtu ni binadamu bila ya kumsahau Lanlan ambaye ni mtoto wako, awamu hii ni vita kati ya miungu na viumbe wa dunia na wewe ni kama mwakilishi wa binadamu ambaye utaamua hatima yao , haijalishi nani atashinda utachukiwa na pande zote kwa kutokuingilia ,miungu watakuchukia kama hutoungana nao na binadamu watakulaumu kama hutoungana nao , binadamu watakuona kama ndio chanzo kwasababu wataamini wewe ndio mtu pekee uliekuwa na uwezo wa kupindua meza lakini ukaamua kujificha na kuwaangalia wanakufa..;
Roma alijikuta akiinua mdomo wake kuongea neneo lakini alishindw akuongea , hakuwhai kufikiria katika uelewa huo.
Iikuwa ni kweli aingilie asiingilie ilimaanisha angechukiwa tu naupande wowote.
Ijapokuwa Rose alionekana hajamaliza kuongea kile alichokusidia lakini alijua ni wapi anaelekea
Kwasababu ya wasifu wake asingeweza kujiweka mbali na kinachoendelea kwa namna yoyote ile.
Hata kama asingejali miungu na binadamu na kuamua kutofanya chochote binadamu au miungu wangeinyooshe mikono familia yake.
Iwe ni kwa miungu au kwa binadamu kama wataamua kuonyesha chuki yake zidi yake kwa familia yake basi asingeweza kuwazuia wote.
“Usiwe na wasiwasi sana haijalishi ni maamuzi gani utachukua lakini hatutakuja kukulaumu wala kujali kama yalikuwa sio sawa au sawa , isitoshe wewe sio mwamuzi wa kinachokwenda kutokea”Aliongea Rose.
“Hapana..!!
“Rose umekosea awamu hii , sijawahi kutamani kuwa nje ya maamuzi ya kile kinachokwenda kutokea”
“Hubby unataka…’”
Rose alijisi kitu kikichafua nafsi ake na hakuweza kujizuia ilionekan kama kwamba ufahamu wa Roma umeamka.
“Siwezi kuvumilia hii hali ya kishenzi kuendelea hivi , haijalishi ni hatari kiasi gani ninapaswa kuzuia kama inaathiri watu wangu wa karibu , hakuna wa kunizuia kwa lolote juu ya hili”Aliongea Roma na palepale alimvuta Rose na kumkumbatia na kisha akambusu kwenye paji la uso.
“Thank you”
Mara baada ya kuongea kauli hio alikuwa tayaria shapotea na kuja kuibukia nje ya ngome yake.
Kwa bahati nzuri alimkuta Edna alikuwa akitaka kuingia ngomeni kutokea nje akiwa ameshikilia Lanlan mkono .
Yeye na wanawake wengine walionekana kuwa na wasiwasi mara baada ya kuja kusimama mbele yake.
Roma alivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kisha aliinama chini na kumkumbatia Lanlan na kumbusu shavuni na kisha akasimama na kumwnagalia Edna.
“Mpenzi ni….”
“Usije ukathubutu ”
Kabla hata hajamaliza sentensi Edna ashabwatuka na kumnyooshea Roma kidole huku akionyesha mabadiliko.
Uso wake ulikuwa siriasi mno na alionekana kuwa kauzu isivyokuwa kawaida , alikuwa ni barafu.
Mabadiliko yake na namna alivyofoka iliwaogopesha kila mtu ndani ya hilo eneo lakini palepale waliweza kuona kitu katika macho ya Roma.
Roma muonekano wake ulibadilika mno wakati akiwa anamwangalia mke wake , ilionyesha alikuwa na majonzi na hali ya kuomboleza kwa namna alivyokuwa akimwangalia Edna
“Lakini sijaongea chochote…”Roma alibwabwaja.
“Najua unachopanga kufanya hata usiponiambia , nakukataza kwenda vitani Roma”Aliongea tena na kutaja jina la Roma kwa mara ya kwanza kwa muda mrefu sana kuonyesha namna gani alikuwa akisisitiza , kwa jinsi alivyokuwa akiongea ni kama swala hilo halina mjadala.
Roma aliishia kukunja ndita , ijapokuwa siku zote alikuwa akiwasilikila wnawake wake lakini akuamua lake hakuna wa kumzuia.
“Edna I have made a decision , take care of Lanlan , I’ ll came back as soon as possible”Aliongea Roma akimaanisha Edna mwangalie Lanlan kwani nishafanya maamuzi na nitarudi mapema iwezekanavyo.
Edna alionekana kutetemeka na kauli hio na haikujulikana kutokana na woga wa Roma kuwa hatarini au hasira , ghalfa tu alisogea mbele na kumshika Roma mkono.
“Naomba tafadhari usiende , Please don’t go , kwa ajili yangu na mtoto naomba usiende”
Edna alibembeleza na alikuwa amebadilika akiwa ameinamisha kichwa chake chini na ilikuwa ni kama vile anaogopa kukutanisha macho na Roma.
Lanlan aliekuwa akiangalia alikuwa akingata lips zake kwa wasiwasi kwani aliona muda wowote mama yake na baba yake watagombana hivyo hakuweza kuongea chochote, upande wa Roma aliishia kutoa kicheko cha kivivu mno.
“Nilikuwa na chembe ya kusita dakika chache zilizopita lakini sasa nadhani napaswa kwenda , kuna vitu napaswa kukabiliana navyo mapema au baadae..”
Edna mkono wake ulitetemeka na kinyongea sana alimwachia Roma na kupiga hatua moja kurudi nyuma.
“Naomba umwangalie Lanlan , napaswa kwenda”Aliongea Roma na kisha alimshika Edna mkono kwa sekunde na kisha akauchia na akapotea.
Upande wa Edna alikuwa ni kama mwanamke ambaye haamini kilichokuwa mbele yake , aliishia kukosa nguvu na kidogo tu angekaa chini , ilikuwa ni kama vile kitendo cha kumwachia Roma mkono ni kama vile alikuwa yupo tayari kwenye maisha yake kuacha kila kitu lakini sio kumwachia Roma lakni mwisho wa sikualikuwa amemuacha.
Unadhani ni siri gani Edna anayo nawakumbusha hii simulizi inaitwa Niliemdhania ni kahaba kumbe bikra.
Maana yae ni kwamba mwanamke niliemdhania ni kahaba kumbe bikra kuna kingine….. ni kichwa endelevu hakikuishia mbagala tu pale bali ulikuwa ndio mwanzo.

ITAENDELEA
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI: SINGAJOJR

Mono no aware


SEHEMU YA 776.
ILIPOISHIA
Waliongea kwanzia mchana mpaka siku iliofuata , walionekana kukumbushiana mambo mengi yaliopita.
Siku iliofuatia wakazi wa kisiwa hicho waliweza kufika.
Mzee Yasu aliweza kuona mwanaume mmoja wa kizungu ambae ngozi yake ilikuwa na vijidoti doti vyeusi , alikuwa ni mtoto wa mkuu wa ukoo afahamikae kwa jina la Chriss.
Watu wa visiwa hivyo walikuwa wakiwachukulia Sharf na wenzake kama ndugu , hawakujua kama walikuwa na uwezo wa kupaa au kufanya maajabu , yaani ki ufupi hawakuhisi chochote kutoka kwao.
“Chriss kuna tatizo?”Aliuliza Yasu kwa lugha ya kingereza.
“Dokta Yasu kuna habari mbaya , haraka mnapaswa kuondoka kwa boti kuelekea bandari iliopo upande wa kusini Magharibi , jeshi la Ulaya limeingia kisiwani na wanapanga kugeuza hiki kisiwa kama kambi yao , baba na wazee wanajaribu kuwazuia kwa kuongea nao lakini nadhani ni swala la muda tu mazungumzo kuvunjika .. baba kaniambia niwajulishe muondoke kabla hamjachelewa , kama wataanza kuua watu na kuiba tutapigana nao mpaka kufa lakini nyie wengine hampaswi kufia hapa”Aliongea kwa haraka haraka.
Ilionekana ni kama vile dunia imerudi katika enzi ile za ukoloni kwani wazungu walikuwa wakilazimisha vitu lakini awamu hii haikuwa kwa ajili ya kuchukua mali bali kwa ajili ya kupata hifadhi.
Yasu na Li Xuemei waliishia kuangaliana kabla ya kuchuuguza kisiwa hicho kwa uwezo wa kitambuzi na kweli waliweza kuona meli za kivita upande wa Kaskazini.
Walikuwa hawana tabia ya kuangalia usalama hivyo walishindwa kuona meli hizo kabla.
Katika hali ya dunia inavyoenda ilikuwa ni sawa kwa wazungu kutaka kuvamia kisiwa hicho kwani kilikuwa ni moja ya maeneo yenye joto na kipo chini ya Serikali ya Jamaica nchi ambayo haina uwezo wa kujilinda na uvamizi.
Dunia ilikuwa kwenye machafuko na hakuna aliekuwa akijali ni nchi gani inavamia nchi ipi.
Lakini sasa hapo kisiwani watu wake walikuwa hawajaendelea kabisa na ilikuwa ni swala la muda kuuliwa wote kama watataka kuingia vitani kwani siraha zao zilikuwa za kawaida sana.
Yasu na mwenzake waliishia kukunja sura kwani Aoiline na Master hawakuwa wametoka bado nje lakini wakati wakijuliza cha kufanya ndio muda ambao waliweza kutoka.
Ilionekana ni kama vile Sharif alikuwa amemlegeza mrembo Aoiline kwani hakukuonekana dalili ya chuki , ki ufupi alionekana kuwa na furaha.
Yasu na Xumei walionekana kushangaa mara baada ya kuona Master wao alikuwa amebadilika muonekano na kuwa kijana kabisa , palepale waliamini lazima itakuwa ndio sura halisi ya Master wao.
Upande wa Chriss alionekana kuwa katika hali ya mshangao mara baada ya kuona watu wawili ambao hakuwa akiwajua wakitoka nje ya nyumba hio.
Yasu na Xumei waliishia kutoa heshima mbele yao na kabla hawajaeleea kinachoendelea Sharif alivunja ukimya.
“Tumewasikia”
“Je unataka tuchukue hatua , nina uhakika watu wa kisiwa hawatojua sisi ndio tunahusika”Aliongea Yasu tena kwa lugha ya kiswahili akionekana alikuwa na mpango wa kutaka kuvamia hizo meli za kijeshi.
“Haina haja , kwasababu Chriss ametuambia tuondoke , basi tunapaswa kuondoka”
“Aa..!”
Wanafunzi hao wawili wa Sharf walionekana kushangaa , ijapokuwa hawajali sana maisha ya watu wa visiwa hivo lakini walikuwa wamewafahamu na kuzoeana nao kwa miaka mingi
Lakini mara baada ya Sharf kuwaambia hivyo , ilikuwa ni kama agizo kwao na hakuna ambaye alikuwa na uwezo wa kukataa na kwa haraka waliishia kuwaaga wale binadamu wa kawaida na kisha walitokomea upande wa kusini magharibi.
Unadhani wana Ajenda gani hao na kinachoendelea

ENDELEA SASA :
Aoiline na yeye alikuwa amekwisha kuelewa kile kilichokuwa kikiendelea na mara baada ya kumuona Sharif anataka kuondoka bila ya kuchukua hatua aliishia kuguna.
“Aoiline huelewi tu kinachoendelea?’Aliuliza Sharf.
“Hawa watu hawana maana sana kwangu lakini kuna kitu kimoja nataka kuuliza , vinginevyo nitakuwa na mgogoro wa nafsi kupotezea kitu kama hiki”
“Kwanini unasema hivyo?”
“Kwanini umeandaa mpango mrefuu halafu unasubiri Roma aufanyie kazi , kwanini usiachane na kila kitu na ukaondoka hapa duniani kuacha binadamu wafe”Aliuliza Aoiline katika sauti iliojaa maringo.
“Mara baada ya kufanikiwa kupita kwenye mnara miaka elfu hamsini iliopita , mawazo yangu yote yalikuwa juu ya kile nilichoweza kugundua, sitakiwi kufungwa na sababu wala athari za mbingu na ardhi , siwezi kuelezea namna ya kudili na hili ninao uamuzi binafsi”Aliongea Sharif.
“Nimechoshwa na visingizo vvako mimi”Aliongea Aoiline huku uso wake ukionyesha dalili ya chuki.
“Kwanini unakasirika sasa , kama umeficha tafsiri ya maandishi nilioacha kwenye mnara mbele ya Roma inaonyesha unakubaliana na mimi kwa kila ninachokifanya , je kuna ulazima kwa mtu kama wewe na mimi kugombana kwa vitu visivyo na msingi kama hivi?”
“Umeotea nusu ya nia yangu ya kuuficha ukweli mbele ya Roma, nakubaliana na ulichofanya licha ya kwamba hakieleweki moja kwa moja lakini nadhani nayaona matarajio yako , ni hiari yangu kufanya hivi sio kwasababu nakuamini lakini kwasababu naamini katika maono yangu mwenyewe .. yule binadamu mjinga Roma Ramoni atakuja kukufanya ulichokuwa ukiamini katika miaka yote hio hakipo sahihi”
“Oh! , matarajio yangu kwa Roma ni makubwa kama hata wewe unaweza kuongea kauli hio kuhusu yeye”
Aoiline alizungusha kiini cha macho yake kama vile anamkagua na palepale kufumba na kufumbua alitoweka.
Kamanda Alex aliekuwa juu ya meli ya kivita alijihisi ni kama vile anaangalia malaika akishuka kutoka mbinguni na vigoti vake vya miguu vililainika akitaka kusujudu.
Lakini ilikuwa ni ndani ya dakika hio hio masikio ya kila mmoja yaliweza kukumbwa na milipuko.
Meli hizo za kivita zilikuwa zimejengwa kwa kuimarishwa na chuma kigumu sana lakini Aoiline aliweza kuzamisha meli zile kwa kutumia nguvu kidogo mno.
Aoiline mara baada ya kumaliza kuzamisha wanajeshi wa Ulaya na meli zao alirudi mlimani kumfuata Sharif na kumwangalia usoni.
“Kama ulitaka kuwatelekeza ni maamzi yako na hayakuwa yangu”Aliongea Aoiline.
Sharf hakujisumbua na matendo yake kwani alimwangalia kama vile ni msichana ambaye anajaribu kumkasirisha mpenzi wake makusudi.
“Siku zangu ndani ya hili eneo zimefikia mwisho , hivyo twende ninakoishi , kuna mgeni huko na hapaswi kuachwa mwenyewe kwa muda mrefu na kujisikia ametelekezwa”Aliongea Sharif.
Kauli hio ilimfanya Aoiline kushangaa lakini hakuuliza swali ni mgeni gani Sharif anazungumzia bali alifuata nyuma nyuma.
****
Ni katika ulimwengu mdogo uliokuwa kimya sana , ndege walikuwa wakiimba na kulikuwa na maua na vichaka kila mahali.
Hewa ilijaa harufu nzuri ya asili , joto lilikuwa la wastani na jua lilikuwa liking’aa.
Katikati ya kipande cha ardhi kulikuwa na majengo mazuri ya mbao ya vyumba juu na chini kama ghorofa yaliozungukwa na maua pembeni ya asili na mengine ambayo yalikuwa ni ya kigeni yalipandwa kwa ukubwa wa ekari moja.
Hasa ndani kabisa ya eneo hilo alionekana mwanamke mzungu alievalia gauni la rangi ya kahawia ya asali akiwa amekaa juu ya ukingo wa jukwaa la mawe nje ya jengo, mkononi alikuwa ameshikiria vitu kama vigongo vilivyokuwa vikiteleza katika usawa kamili vilivyofungwa kwa kamba. ukiangalia kwa mbali unaweza kusema ni vijiti vya mianzi lakini ukiangalia kwa ukaribu utagundua ni vijiti vya mawe ya madini ya jedi.
Safu hio ya mawe ya jedi ya rangi ya bluu bahari ni kifaa kinachotumika kurekodi maandishi ambayo huwezi kuyasoma mpaka uweze kuingiza nguvu za kijini.
Yaani kwa lugha nyepesi ni kwamba kifaa hicho ni kama karatasi za kuandikia lakini sio katarasi kwani kifaa hicho chenyewe maandishi yake huwezi kuyaona mpaka nishati ya mbingu na ardhi itumike.
Mwanamke huyo mzungu alikuwa akiangalia kifaa hicho kwa furaha kubwa , juu ya jiwe pembeni yake kulikuwa na vifaa vingine kama alichoshikiria.
Muonekano uliokuwa ukionekana mbele ya kiambaza cha jengo hilo ulibadilika mara baada ya watu wanne kujitokeza kama vile wametokea katika kioo kwa namna walivoibukia .
Alikuwa ni Sharif , Aoiline na wanafunzi wake wawili yaani Yasu na Xumei.
“Sharif naona una maisha mazuri sana , kitendo cha kufanikiwa kutoka ulimwengu wa majini pepo umeweza kujitengenezea sehemu kama hii ndani ya dunia yenye mandhari mazuri hivi … natamani kuja kujaribisha kitu kama hichi pia”Aliongea Aoiline.
“Ungeweza kufanya hivi kama ungetaka , hebu acha kunidhihaki basi”Aliongea Sharif huku akitembea kumsogelea yule mwanamke wa kizungu.
Wakati huo yule mwanamke wa kizungu ambaye alikuwa bize kusoma maandishi ya kile kifaa aliweza kugundua uwepo wa watu wengine wakimsogelea na mara baada ya kukunja sura aliweka chini alichokuwa ameshikiria na kumwangalia Sharif na muonekano usiokuwa ukielezeka.
“Senior”Aliongea yule mwanamke kwa kingereza.
“Clark , did you get anything from reading these Jade slips?”Aliongea Sharif kwa kingereza.
Mwanamke huyo mrembo mzungu alikuwa ni Clark ambaye aliletwa hapo na Master Yasu.
“Nilitegemea mtu kama wewe kujikita katika maswala ya mbingu na ardhi pekee na kutokuwa na ufahamu mbele ya maswala ya kisayansi…”aliongea Clark huku akiwa na tabasamu pana usoni.
“Hata hivyo huu utafiti uliopo katika haya maandishi umeniacha mdomo wazi…”Aliendelea kuongea Clark.
Taarifa ambayo alikuwa akisoma Clark ilikuwa imechaguliwa na Sharif mwenyewe na alimruhusu asome , haikuwa rekodi ya maandishi ya namna ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi bali ni mawazo ya kitaalamu kabisa kutoka kwa Sharif aliokuwa nayo juu ya maswala ya sayansi, kwa lugha nyepesi gunduzi zilizokuwa ndani ya maandishi hayo ni vumbuzi ambazo pengine bado hazijagunduliwa katika wakati huu.
“Ni kawaida , kama utaweza kuishi kama mimi kwa maelfu ya miaka utajikuta tu unaanza kujifunza vitu vingi sana hata vile ambayo hujawahi kufikiria , uwelewa wako katika maswala ya kisayansi ni mkubwa sana kuliko wa kwangu , nilichokuzidi ni miaka tu na uwezo lakini likija swala la ubunifu umeniacha mbali”Aliongea Sharif.
“Senior unaenda mbali sana kunisifia”Aliongea Clark aliekuwa katika tabasamu.
“Kama usingekuwa vizuri kama nilivyosema nisingekusifia , pili wewe ni dhahabu iliojificha na kipimo cha matokeo yasiotarajiwa , kama sio hivyo nisingekuruhusu kuja kukaa na mimi muda wote huu”
Clark mara baada ya kusikia kauli hio na kugundua ni sifa anamwagiwa aliishia kutoa cheko kwa namna ya kivivu .
“Unaongea nini , kwanini unasema huyu mrembo ni kipimo cha matokeo?”Aliuliza Aoiline.
“Aoiline huyu mtoto sio wa kawaida ,kama ilivyo uwezekano wa Roma kuwa sababu ya mabadiliko ya hili janga linaloendelea , huyu msichana pia ni mtu ambaye anaweza kuutegemea ubongo wake tu na kubadilisha matokeo , sikuwa na jinsi bali kumtenganisha na Roma vinginevyo kwa msaada wake ingemfanya Roma kutofikiria nje ya boksi na kufikia kiwango chake chote cha akili yake”Aliongea Sharif na kumfanya Aoiline asiamini kama Clark alikuwa na uwezo huo.
Clark pia alimwangalia Aoiline kwa shauku , kama isemekanavyo wazuri huangaliana pamoja kwa macho yasiokuwa ya kawaida .
“Unanitania sio , ijapokuwa huyu msichana ni mrembo lakini uwezo wake wa mafunzo ya mbingu na ardhi unakaribia Dhiki …mh uelewa wake na msingi wa mifupa yake ni mzuri lakini kuna gepu kubwa ukimfananisha na Roma .. nadhani unapaswa kujua kama huyu mtoto atafanya kazi kwa juhudi basi si muda mrefu uwezo wake utaongezeka mara mbili lakini kwanini huyu awe ufunguo?”Aliuliza Aoiline.
“Nini , Senior unamjua Roma , amekwisha rudi , yuko wapi sasa hivi?”Clark aliuliza mara baada ya kusikia jina la Roma linatajwa sana.
Aoiline alifikiria kwa muda na alikumbuka Roma alikuwa akimtafuta mwanamke kumbe alikuwa ni huyo mrembo.
“Kumbe ndio wewe ,, ndio mwanamke wake ambaye ulichukuliwa kwa nguvu ,, hehe usiwe na wasiwasi yupo salama ni kwamba tu anaonekana kutokuwa na furaha kutokana na kukosekana kwako”Aliongea Aoiline na kumfanya Clark kushusha pumzi za ahueni.
“Usiwe na wasiwasi , Roma ashajua upo salama , kwasasa ana kazi muhimu sana anapswa kufanya na kufanya maamuzi mapema , kila kitu kikitulia nitakupeleka kwake”Aliongea sharif.
Clark alitingisha kichwa lakini wasiwasi wake ulikuwa haujamtoka , alikuwa na wasiwasi juu ya hatima ya Roma kwani kinachoendeea ni kama vile hakitafsiriki kimantiki.
Aoiline na yeye alionyesha hamu ya kutaka kujua kitakachotokea , hakupanga kutoka na angekaa ndani ya eneo hilo hilo ili kuona ni maamuzi gani Roma anaenda kuchukua.
“Vipi kuhusu Idriss ushamweleza nahitaji kuongea nae?”Aliulia Sharf.
“Ndio Master muda si mrefu ataji.., Naona ashafika Master”Aliongea palepale ni kama vile anga linapasuka kwani mtu mweupe mwarabu aliweza kujitokeza mbele yao.
Alikuwa ni Shekhe Idriss moja vya wanachama wa umoja wa Ant-Illuminat , kwa namna ambavyo amejitokeza ilionyesha ni dhahiri alikuwa na nguvu za kijini.
“Huyu ndio mwanafunzi mwingine uliekuwa ukimzungumzia?”Aliuliza Aoiline huku akimwangalia Idriss kwa macho ya kidadisi.
“Salamau kwako Madam”Alisalimia Idriss.
******
Ni juu ya boti upande wa kusini mwa visiwa vya wafu, Ijapokuwa joto wakati wa mchana lilikuwa ni nyuzi tano mpaka sita za joto lakini upepo haukuacha kuwa wa baridi mno.
Ingawa jua halikuwa kali sana lakini Roma alikuwa amevalia miwani ya jua katika kiti cha kuegamia , alikuwa amevalia shati la mikono mifupi na bukta.
Mkononi alikuwa ameshikilia ndoano kwa mkono mmoja huku mkono mwingine alikuwa ameshikilia sigara na alikuwa akivuta moshi na kuupuliza hewani mara kwa mara.
Ukiachana na Roma kulikuwa na kiti kidogo sana maalumu cha watoto na kibonge nyanya Lanlan alikuwa amevaa nguo rangi kama za baba yake na yeye pia alikuwa ameshikilia ndoano lakini muonekano wake ulikuwa himahima na alikuwa akilamba sana lipsi za midomo yake kama vile alikuwa na njaa.
Sababu ambayo ilimfanya Lanlan kutokuonekana kuwa na furaha ni kwasababu Roma alikuwa amekamata samaki wengi sana lakini yeye hakuwa amekamata hata mmoja hivyo ilimfanya kudhihirisha ni namna gani hajaridhika na matokeo.
Wengine wote waliokuwa juu ya boti hio walikuwa wamekamata samaki pia na walikuwa wamejaza katika vyombo vyao na walikuwa washaacha kuvua na kukaa nyuma ya Lanlan na Roma.
Nasra , Dorisi , Neema na wengine ambao walikuwa wajuzi katika mapishi walikuwa bize kuandaa Sashimi ,Sushi na Fish steak.
Kila mara harufu ya limao kutoka kwa samaki ilivyozifikia pua za Lanlan ile hali yake ya kutokuwa na furaha ilikuwa ikimpotea na alijikuta akigeuza kichwa chake akimwangalia Nasra anavyokaangiza na aliishia kulamba midomo.
Roma mara baada ya kuona Lanlan hayupo makini alimpiga na kipisi cha sigara kwenye mikono yake na kumfinya.
“Unaangalia nini , weka umakini wako katika kuvua la sivyo hutoruhusiwa kula kama hutokamata samaki hata mmoja”Aliongea Roma akiwa na tabasamu la uchokozi.
Lanlan alitaka kulia kutokana na maneno ya kukatisha tamaa ya baba yake na kujiambia kwanini baba ni mkatili namna hio.
“Daddy unaonaje nikizama chini ya bahari na kukamata samaki na mkono , kuvua na ndoano hakunifurahishi”
“Uvumilivu wako ni mdogo sana na kila baada ya dakika tatu au tano ushatoa ndoano nje , ndio maana unashindwa kukamata samaki yoyote , kama unaona kuingia majini na kukamata samaki kwa mkono ni rahisi kwanini umepoteza muda mwingi kuvua na ndoano?”
“Lanlan alidhania hao samaki ni wajinga wajinga lakini naona ni wajanja sana na hawataki kula chambo yangu”
“Acha visingizio , kaa chini kwa utiifu na endelea kuvua”
Roma alisisitiza na hakuwa tayari kukubali kirahisi , alijikuta kama baba mkali lakini ukweli ndani kwa ndani alikuwa na furaha , kuwa na mtoto mjinga ilimfanya kuwa na furaha pia.
Warembo waliokuwa nyuma yake walishindwa kuvumilia na kuishia kucheka kwa siri , walijua Roma alikuwa akimchokoza Lanlan makusudi
Nasra kama kawaida yake aliweka steki mbili za samaki kwenye sahani na kisha akampelekea Lanlan.
“Usiwe na wasiwasi kuhusu baba yako anajaribu kukuogopesha tu , hebu kula kwanza mtoto mzuri”
Lanlan hayo ndio mambo ambayo alipenda na hakusubiri swala la uma wala kisu na alitumia mkono mmoja kushika kipande cha samaki na kung’ata.
Mara baada ya kuonja utamu wa samaki hakujali tena maswala ya kuvua kwa muda mrefu na alitimua nduki kumsogelea Neema ili kupewa Sushi.
Roma alitaka kumkamata lakini aliishia njiani mara baada ya kumuona Edna akitokea kwenye Cabin akiwa ameshikilia simu mkononi , na ilionekana alikuwa akiangalia kitu.
“Honey mama kanipigia simu , anasema Dar kumetokea vurugu na jeshi linajitahidi kutuliza watu, kutokana na usalama wanahamia mkoaniTanga”Aliongea Edna.
“Nilijua ni swala la muda tu ,kadri nchi inavyofurika wageni ndio namna ambavyo wazawa watakosa amani”
“Hata mimi naona ipo hivyo , inasemekana imeanzia Zanzibar wazawa hawawataki wageni kwani wanaamini wao ndio chanzo cha kinachotokea duniani , Mungu amekasirika kwa ajili ya madhambi yao”Aliongea Edna.
Ni kweli na haikuwa Tanzania tu nchi nyingi za Afrika fukuto lilikuwa likiendelea chini chini , wazawa wengi wanaamini yanayotokea duniani ni kutokana na Dhambi za wazungu hasa maswala ya uchoga nakadhalika hivyo wale watu wa imani wanaona kuwakaribisha hao wageni ni kujiingizia mkosi.
“Halafu kuna kitu kingine mama amesema nikuambie… Maraisi kumi kutoka mataifa yalioendelea ikiwemo China wanaomba kuonana na wewe kwa ajili ya kikao , wametuma maombi hayo kupitia kwa Raisi Senga”Aliongea Edna
“Hapana , sitaki kabisa kukutana nao najua ni kipi wanataka kuongea hata kabla sijaonana nao , wanachotaka ni mimi kulumbana na miungu na sio vinginevyo lakini mimi sio mjinga wala sio shujaa wa dunia , tokea mwanzo walikuwa wakijifanyisha wajanja sana na walienda mbali hata kumtumia mtu mwenyewe nguvu kuliko mimi kunitishia amani.. lakini sasa hivi tumaini hawana tena na wanataka kunituma kufa”AliongeaRoma akionyesha kukasirika.
“Hey! , You are so petty ..”Aliongea Edna huku akimwangali Roma kwa tabasamu lakini hata hivyo alikubaliana na maneno yake , kwanza hakutaka Roma kujiingiza matatizoni kwa ajili ya kupambania binadamu.
Ilikuwa imepita takribani mwezi sasa tokea Roma akutane na Mzee Yasu na arudi duniani.
Upande wa dunia , vifo , njaa na joto la dunia lilizidi kuporomoka na kusababisha uhalifu kutokea kwa viwango vya juu sana kila mahali ndani ya dunia.
Haikuwa katika nchi tu ambazo hazijaendelea bali mpaka nchi ambazo zimeendelea hali haikuwa nzuri kabisa, tena zile sehemu ambazo kulikuwa na nafuu ya joto ndio hali ilikuwa mbaya zaidi kwani kila mtu anataka kuishi ndani ya maeneo hayo.
Binadamu walikuwa wakifa kila siku kwa idadi ya mamilioni na haikuwa hivyo tu ilionekana ndani ya muda mfupi tu idadi itaongezeka.
Nafasi ya binadamu kuishi ukiachana na wale waliokuwa wajuu mfano wa matajiri na viongozi ilikuwa ni ndogo sana.
Sasa katika kipindi chote hicho Roma alikuwa kisiwani kwake tu akitumia muda wake kuwa pamoja na mke wake na mtoto wake licha ya kile kinachoendelea.
Pengine bora hata asingekutana na Yasu , lakini mara baada ya kukutana nae palepale hali ilimwingia na kujiambia kwanini yeye ndio ahangaike na maswala ya binadamu ili hali kuna watu wenye nguvu zaidi yake ambao hawataki kusaidia.
Tena wakaenda mbali kabisa na kumteka mwanamke wake ili tu kumfanya akubali hatima yake lakini Roma alilaani kwa kusema ‘wote waende kuzimu’ hatoi mguu wake nje ya kisiwa kwa namna yoyote ile , kama mbwai na iwe mbwai hawezi pigana ilihali wao wamekaa.
Roma hakujiona kama mtu mkubwa ambaye anatumikia raia hivyo aliamua kujificha.
Katika kipindi hicho Roma alikuwa amejua vitu vingi , alikwisha kujua mtu ambaye alikutana nae Dodoma mara ya mwisho na kumuonyeshea uwezo mkubwa lazima atakuwa ni Mzee Yasu au mtu mwingine mwenye uwezo mkubwa kama mzee huyo.
Kilichomfanya ajue hivyo ni kutokana na kwamba walimtumia baba yake raisi Senga kukutana nae ndio maana hitimisho lake lilimwambia mtu yule ni Yasu lakini swali liliibuka je huyu Yasu ndio Master namba moja ambae alikuwa akizungumziwa au kuna binadamu wengine kama Yasu ambao wana uwezo mkubwa kumzidi hata yeye.
Roma hakujua kama kulikuwa na binadamu zaidi ya watatu ambao walikuwa katika levo za juu kabisa, mmoja wapo akiwa ni Yasu mwafrika , Idriss mwarabu na Xumei mchina.
Moja ya vitu vingine ambavyo Roma aliweza kujua taarifa zake ni kuhusu Zeros umoja unaoundwa na viongozi wa juu kutoka mataifa yalioendelea , wote hao walikuwa nyuma ya kufanikisha kufufuka kwa moyo wa Gaia wakitumiwa na Athena bila kujielewa kwa ahadi feki ya kutengenezewa ulimwengu mkamilifu(utopia) lakini mara baada ya athari kutokea ni kama vile Athena amewatelekeza.
Hivyo binadamu hao ambao aliwaona ni kama wajinga waliojiingiza mtegoni wenyewe mwanzoni walikuwa wakiona dunia ipo kwenye mikono yao lakini katika wakati huo ile hali ya kujiamini hawakuwa nayo tena.
Kitu kingine ambacho Roma alijua ni kuhusu uwepo wa wanaojiita walinzi wa dunia , tena alijua walikuwa na mawasiliano ya karibu na serikali ya China na hata kiongozi wao wa China alitegemeaa wangeweza kuingilia kile kinachoendelea ndio maana hawakutaka kujihusisha na ujenzi wa safina.
Kama ilivyokuwa kwa Yasu kujiweka karibu na mataifa ya Afrika ilikuwa hivyo hivyo kwa Xumei kujiweka karibu na taifa la China , ilionekana raisi wa China alikuwa na ukaribu zaidi na Xumei na alikuwa akimpa kiburi lakini katika hatua ya machafuko kama hio ni kama alipoteza mawasiliano na Xumei kabisa na kujihisi kutelekezwa.
Roma hakutafutwa na binadamu tu waliokuwa wakitaka msaada wake lakini hata majini pepo kutoka miliki ya Braki walikuja wakiongozwa na Zike mkuu wa Dhehebu la majini shetani na Latina.
Upande wa Latina alikuja kwa Roma kumuuliza Aoiline kaenda wapi maana inasemekana mara baada ya kufika katika ulimwengu wa jangwa tenganifu hakukaa muda mrefu na alitoweka bila ya kuaga na isijulikane alipo.
Sasa kupotea kwake pamoja na fukuto lililokuwa likiendelea kiasili Latina kama kiongozi alikuwa na wasiwasi.
Upande wa Zike yeye dhehebu la majini watunza hazina walimtaka Roma kusaidia ndugu zao waliopo katika ulimwengu wa majinni pepo watoke , lakini Roma aliibua visingizio vya hapa na pale tu ili mradi kumkatalia , Zike hakuridhishwa na jibu la Roma lakini kwasababu Roma uwezo wake ulikuwa wa juu sana hakutaka kulazimisha hivyo alirudi nyumbani kishingo upande.
Lakini sasa kupotea kwa Aoiline kulimfanya Roma kuhisi kabisa ni swala linalohusiana na Mzee Yasu lakini hata hivyo zilikuwa ni hisia tu maana hakuwa na uhakika.
Ukiachana na hayo kinachoendelea kati ya miungu na binadamu mwishowe aliona hakuna anaeweza kumlaumu kwani anachokifanya ni kulinda familia yake.
Aliona anapaswa kuishi maisha ya furaha na familia yake na kuhusu kuokoa binadamu aliona wenye nguvu zaidi yake watafanya kazi hio maana alijua si wapo kwanini ahangaike.
Mara baada ya kuongea kwa muda mfupi na Edna Roma na warembo wake walikaa mezani kwa ajili ya kula chakula cha baharini.
Rufi , Yezi na wengine waliongezeka , upande wa Rufi alikuwa ameshavunja kizuizi ambacho kilikuwa kikimfanya ashindwe kuvuna nishati za mbingu na ardhi na muda wowote angeweza kuingia katika levo ya nafsi.
Ukweli ni kwamba kila mmoja alionekana kuwa na furaha kwani wote walikuwa wakivuna nishati na kuishi maisha ya starehe , hawakuwa na shida na hata kama dunia ingezidi kuwa na baridi miili yao ingeweza kustahimili kwa muda mrefu tu labda oksijeni isiwepo.
Roma pia hakuacha kumtafutia Lanlan eneo la peke yake kwa ajili ya kuendelea kutambua siri ya andiko la urejesho , ukweli ni kwamba alikuwa amepiga hatua kubwa sana na alimfundisha mapigano ya kawaida na alionekana kubobea sana licha ya utoto wake.
Roma alikuwa na majuto wakati akiwa mdogo hakupata fursa kama aliokuwa nayo Lanlan hivyo hakutaka Lanlan kupitia aliopitia yeye ndio maana alitumia kila fursa kuhakikisha kile ambacho hakuweza kukifanya yeye akiwa utotoni Lanlan anakifanya.
Ikiwa ni muda mfupi baada ya chakula wakati Roma akijiandaa kuondoka katika boti hio aliweza kugundua kuna majini wengi waliokuwa wakisogea upande wao na wengi wao msisimko wao alikuwa akiujua.
Kufumba na kufumbua kundi kubwa la majini watu kutoka miliki za majini walionekana mbele yake.
Kati yao kulikuwa na majini wa miliki ya Kekexil , Xia na Hongmeng na kiongozi wa kundi hilo alikuwa ni Jini Anjiu , Umini na Shombeli
Karibia wote waliokuwa hapo walikuwa katika levo za maji ya upako lakini kulikuwa na baadhi ya majini ambao walikuwa katika levo za chini mpaka levo ya nafsi akiwemo Xiaoxiao , Zenzhei na wengine
Roma alishangazwa na ujio wao maana ulikuwa sio wa kutegemea kabisa , na haikuwa kwake tu hata kwa wengine wote walishangazwa.
Kwa haraka haraka namna walivyotokea ilikuwa hawajafika hapo kwa fujo bali nyuso zao zilikuwa zimejazwa na hali ya simanzi.
Ukweli hata Roma mwenyewe alishajua hawapo hapo kwa ajili ya vurugu na hata kama wakitaka vurugu wasingemuweza maana alikuwa amewaacha mbali.
Kitu kingine ambacho Roma aligundua kutoka kwao ni kwamba walikuwa na alama za kutosha za huko walikotoka hakukuwa salama , wengi wao walikuwa na nguo ambazo zimeshachanika , ni kama vile ni wanajeshi waliokimbia vitani.
Kuna ambao walikuwa wametapakaa damu pia kwenye mashati yao ikionyesha walikumbana na mkandamizo mkubwa.
“Mna matatizo gani nyie?”Roma aliuliza mara baada ya kutua katika fukwe akiwa na moyo mzito mno na alionyesha hali ya kuwa siriasi mno kama vile waliofika hapo ni wageni ambao hakuwa akiwahitaji.
Anjiu macho yake yalikuwa mekundu na alikuwa akionyesha ishara za kukata tamaa na hata sauti yake ilikuwa imemkauka.
“Imekwisha ,,, imekwisha…”Aliongea kwa sauti ya kitetemeshi.
“Unamaanisha nini , hebu ongea ueleweke nini kimewapata?”Aliuliza Roma kwa mshangao maana ni kama vile wanataka kulia.
XiaoXiao alikosa uvumilivu tena na alijikuta akiangua kilio na kwenda kumvaa Roma na kuanza kulia kifuani.
“Roma.. hiihiii.. miungu wameteka miliki zetu zote na sasa zipo chini yao , babu yangu amefariki kwa kuuliwa na miungu ,.,. sasa hivi hatuna kitu , tumebakiwa watupu.. hii .. hiii, hatuna pakwenda sisi”
Roma muonekano wake ulibadilika palepale na alishindwa kushituka mara moja mara baada ya kusikia miungu ikihusishwa.
Hakuamini mara baada ya kusikia miungu walikuwa wameziteka miliki za majini watu.
Roma alijua babu yake Xiao atakuwa ni Chaopi, uwezo wake ulikuwa mkubwa kama wa Anjiu tu lakini ameuliwa.
Ilionekana miungu wamewapiga majini mpaka maji wakayaita mma , maana sio kwa kutia huruma huko.
Ilikuwa dhahiri kwake kwamba miungu uwezo wao hauvumiliki kabisa , pengine walitaka kuonyesha namna gani wamerudiwa na nguvu kwa kuwapiga majini.
Mshituko ulimfanya Roma kusahau alikuwa mbele ya wanawake wake maana Xiao alikuwa akionyesha mahaba ya waziwazi na alijiuliza huyu mwanamke katokea wapi ghafla tu na kumvaa?
Roma mara baada ya mshituko kumtoka aliishia kumtoa Xiao katika mwili wake na hakuongea neno kwani aliona angezidi kumtia huzuni mwanamke huyo ambaye alionekana kupoteza kila kitu.
“Hebu nyamaza kwanza kwasasa”
Aliongea Roma na palepale alipiga hatua kumsogelea Zenzhei na ndugu zake akiwepo Nefi.
Lakini wakati huo majini hao kutoka Hongmeng waliionekan katika hali ya majonzi hata Zenzhei ambaye Roma alimjua kama mtulivu alionekana kuwa hayupo kawaida.
“Mr Roma…”
“Bi Zenzhei nini kimetokea na ni miungu ipi iliowashambulia?”Aliuliza Roma akimaanisha ni yupi kati ya viumbe hao wamewashambulia.
Zenzhei aliinua mdomo wake kutaka kuongea kitu lakini alionekana kushindwa kwani ni kama amemeza kitu kizito shingoni na machozi mengi yalimtoka.
“Roma acha kumlazimisha Zenzhei kuongea , Mzee Wucheni amefariki wakati wa vita na ndugu hao wanapitia wakati mgumu wa kumuomboleza”Aliongea Shombeli.
Roma alishangaa mara baada ya kusikia Wucheni alikuwa amefariki , lakini hata hivyo aliona ni sawa kama Chaopi amekufa licha ya kuwa na uwezo wa juu.
Ndio maana Zenzhei na nduguze walionekana kuwa na huzuni mno , hata kama ilionekana kuna kizuizi kati yake na mjomba wake lakini kifo chake kilimtingisha.
“Ni Master Yanyu na Rozu dada wa tatu kutoka Panas na mwingine ambaye alionekana kama mzungu lazima atakuwa ni moja wapo ya miungu”Alijibu Anjiu.
Roma alishangaa alikuwa amemsikia Yanyu ni moja wapo ya majini wanaokamilisha idadi ya wazee wanne kutoka Hongmeng.
Kwa taarifa alizokuwa nazo ni kwamba Yanyu alikuwa aikshiriki mara chache katika matukio yaliojumuisha miliki hio na alikuwa ni moja wapo ya muumini mzuri tu wa dini ya Kibuddha.
Sasa alishangaa kama Hongmeng na Panas zote kulikuwa na miungu kati yao , ilishangaza kweli kweli.
“Sikuwahi kuwaza kama Master Yanyu atakuwa sehemu ya miungu , kulingana na mbinu zake za kivita alikuwa akitengeneza moto wa ajabu,sio yeye tu ni ngumu pia kuamini hata kwa Rozu pia”Aliongea Umini.
Roma aliwaza palepale kwa kuunganisha matukio na mara baada ya kufika katika sura ya Hermes kuna kitu kilimjia, kwa maelezo ya Anjjiu moja ya watu waliowashambulia alionekana kuwa mzungu alievalia viatu vya mbawa ikimaanisha moja kwa moja ni Hermes na kama ndio hivyo basi Rozu atakuwa ni Hera maana Athena ni mwenye tabia ya kupenda kufanya vitu peke yake.
Roma alijiuliza viumbe hao ni kipi wanachokiwaza maana tayari washawasukumia binadamu kwenye hatari na ni sawa na kusema wanaitawala dunia, sasa kulikuwa na haja gani ya kuvamia na majini.
Lakini hata hivyo Roma hakuwa na mpango wa kuelezea kile ambacho anajisikia. Ukweli ni kwamba majini hao hawakuwa marafiki zake na angalau wanapaswa kushukuru alikuwa mkarimu na kutowaua.
“Nimeshasikia kilichowatokea lakini bado sijajua dhumuni lenu la kuja kisiwani kwangu?”Aliongea Roma.
Majini hao hawakuonekana vizuri sana , ilikuwa ni kama vile tumaini lao la mwisho limepotea na Roma aliweza kuona namna ambavyo walikosa hiari na hali ya kujishusha.
“Nakumbuka kuna watu hapa walitaka kutuua tena kwa namna ya kidhalimu , kilichowapata ni Karma ya asili ambayo mmejitegeshea wenyewe lakini hebu jiangalieni sasa hivi mmekuja kwa ajili ya kuomba hifadhi hamuoni kwamba mmekosa aibu?”Aliongea Mage katika sauti ya makasiriko.
Magdalena upande wake katika wakati huo aliona yaliopita wapotezee , isitoshe ni swala zito ambalo halikuwa likihusisha majini tu bali binadamu wote na alimvuta Mage mdogo wake ili asiendelee kuingilia maamuzi ya Roma lakini Mage alionekana kukataa.
“Sister kwanini unanivuta , nimekosea wapi , wanajifanyishya kama vile hakuna kilichotkea na kuja kutuomba hifadhi , najihisi kichefu chefu hata kuwaaangalia”
“Magee..!!”
Magdalena aliishia kuita jina la mdogo wake kwa sauti ya chini huku akiwaangalia watu hao kutoka ulimwengu wa majini watu
Magdalena aliona licha ya kwamba majini hao walikuwa na chuki zidi ya Roma lakini hakuwa na haki ya kuwahukumu kama walivyotaka kufanya.
Majini hao mara baada ya kusikia kauli ya Mage sura zao zilizidi kujikunja kwa huzuni huku wakishindwa kuongea neno.
Walikuwa wakijiona ni wa juu sana kwa zaidi ya miaka mia mbili na inaweza kuaminika kwamba walikuwa wakichukulia binadamu kama viumbe dhaifu.
Lakini wakati huo kuamka kwa miungu na binadamu majiniasi imewafikisha katika hatua ambayo makazi yao yamekuwa sio neema tena na wanapaswa kwenda kumuomba kijana wa miaka ishirini makazi.
Waliamini ni Roma anaeweza kuwasaidia licha ya chuki baina yao kwani ndio mtu pekee anaewaelewa.
“Mr Roma, Mage yupo sahihi , ijapokuwa baba yangu alishiriki peke yake lakini sisi ni familia moja , hakuna mwenye haki ya kukuomba msaada hapa”
Roma alichukia kuona kundi la majini vijana kutoka Xia lakini hakutaka kuwalenga kutokana na heshima yake kwa Zenzhei
“Bi Zenzhei huna haja ya kuwa mnyenyekevu hivyo , ninaweza kupotezea kila mmoja hapa lakni sio wewe , umenisaidia sana kunifikisha hapa nilipo leo , mimi bado ni muumini mzuri wa falsafa ya shukrani na kulipa fadhila , isitoshe wanufaika wangu ni wachache”
“Asante sana Mr Roma kwa kushukuru , kwa maneno yako hayo nimeridhika lakini hawa wakubwa wote waliokuwa hapa wana umuhimu mkubwa kuliko wangu , ulimwengu wa majini umekwisha kusambaratika na kizazi pekee cha majini watu kilichobakia ni hawa , kama hawa watu watapotea wasiwasi wangu kizazi chote kitatoweka na dunia itakosa uwiano”
“Bi Zenzhei ijapokuwa nakuheshimu sana lakini kuna vitu siwezi kufanya kwani ni kwenda kinyume na sheria zangu , busara hulipwa kwa busara na kisasi kwa kisasi na sitokuja kuwa mjinga kwa kumlipa mtu busara ili hali hastahili .. karibia ya kila mmoja aliefika hapa hahusiani kwa chochote na mimi na pia ni maadui zangu , sina mpango wa kuwaua mbele ya binti yangu na sitaki damu yao kuchafua nyumba yangu lakini siwakaribishi kukaa hapa kisiwani pia , zaidi ya yote kama miungu watakuja na kuona nipo upande wao si itaniletea tu matatizo , ni kweli uwezo wangu ni wakushangaza lakini sidhani ninao uwezo wa kumshinda Athena ambaye uwezo wake wote umerudi , hivyo sitaki kufanya kitu ambacho kitahatarisha usalama wa familia yangu”
Zenzhei alitaka kuendelea kumbembeleza Roma lakini Nefi alimzuia kwa kupita mbele.
‘”Haina haja tena dada , huyu mtoto ashajipambanua wazi anaogopa na anataka kuficha kichwa chake kwenye hiki kisiwa kama kobe anavyojificha katika nyumba yake , haijalishi kwa namna gani utambembeleza atajifanyisha ni mwenye kuchanganyikiwa , isitoshe anaweza akawa anashirikiana na miungu , uwezo wetu unaweza usiwe mzuri kama wa wengine lakini angalau tunao ujasiri wa kufa tukipambana”
“Ndio Mzee Wucheni anapaswa kujivunia kwa kuwa na watoto wa namna hii , tupo hapa na ni kweli hatuna chochote tunachoweza kufanya lakini sio kwamba tunatamaa sana ya kuishi na kuogopa kifo , kizazi chote cha majini watu na binadamu kipo hatarini ni bora kwenda ncha ya kaskazini na kupambana hadi kifo na miungu , angalau tutakufa bila soni kwenye mioyo yetu”Aliongea Shombeli.
Baada ya kuamshwa munkari majini wote waliitikia kwa nguvu na mchecheto wa hali ya juu ulikuwa ukionekana kwenye macho yao.
Lakini Anjiu na Umini ambao walionekana kuwa watulivu hawakuongea neno , walijua kwa hakika kwamba kwenda ncha ya kaskazini ni kujitafutia kifo na kutokana na hilo haina maana.
Roma alipotezea hali yao ya msisimko na alichokuwa akijali hapo pengine ni maisha ya Xiao na Zenzhei pekee wengine alijiambia wanaweza kufa kama wanataka.
Muda huo huo juu ya bahari upande wa mashariki jini ambaye alionekana kushikilia mkuki wa mwanga alionekana akiwa ametangulizana na kundi la majini wengine kusogelea visiwa vya wafu.
Alikuwa ni Master Shagoni ambaye alipotea kwenye ulimwengu wa majini mara baada ya wenzake kuja kupigana na Roma wakati ule.
Roma kwa kumwangalia mara moja tu Shagoni alionekana tayari ashapitia mapigo tisini na tisa ya radi ya zambarau , ijapokuwa hakujua ni lini imetokea lakini ilionekana sio muda mrefu , hakika ilionekana bwana huyo alikuwa ni jiniasi na kwa levo hio alikuwa katika levo sawa na Anjiu.
“Shagoni ni wapi ulikuwepo , je unajua miliki yenu ipo hatarini ?”Aliuliza mzee mmoja kutoka Kekexil.
Shagoni alikuwa akitegemewa sana ndani ya miliki ya Kekexil lakini pale matatizo yalipotokea alikuwa haonekani hivyo kufanya wana miliki kutoridhishwa nae.
“Hata sijawauliza bado lakini mshaanza , nilijitafutia sehemu ya kujitenga na kupitia Dhiki yangu ya radi , imewezekana vipi zaidi ya majini mia moja kufariki baada ya kurudi?”
“Unaongea nini wewe , mbona ni kama unaona ni miliki yenu ilioathirika tu , unapaswa kuelewa ulimwengu wetu wote umeangushwa na miungu watatu na koo zote zimepata hasara kubwa, wewe ndio unajikuta kuumia tu na sisi wengine hatuumii”
“Upo sahihi, hasara iliotokea ni nje ya mategemeo , nyie siku zote mlichojali ni uhai wenu tu na mkakimbia huku mkiacha majini kibao waliopo levo za chini wakiwa peke yao , kwa bahati nzuri nimewakuta na kuja nao hapa , kuna mtu ameniambia kuna uwezekano nikawakuta hapa”Baada ya kuongea hivyo aliwapotezea wale wazee wa kijini na kisha alimwangalia Roma.
“Wewe mwanaharamu yaani muda ambao najiona nipo katika levo ya kupambana na wewe ndio unapanda levo ambayo inaonekana kabisa sikuwezi tena”Aliongea mara baada ya kumchunguza Roma.
Roma alikuwa akichafukwa na roho kutokana na tabia ya ukiburi ya Shagoni
“Kwahio na wewe pia umekuja kuomba hifadhi?”
“Sina kinyongo chochote na wewe na sio kwamba napenda sana kukaa hapa lakini ndio hivyo sina sehemu nyingine ya kukimbilia , kama hutaki niishi hapa nitaondoka”
Roma alionekana kufikiria kwa muda huku akijiuliza je awaruhusu hao majini kuishi ndani ya kisiwa hicho , isitoshe aliona kuna baadhi yao hakuwa na kinyongo nao lakini muda huo huo Muonekano wa Magdalena ulionekana kubadilika.
“Master umekuja pia?”
Binadamu mwanamke alievalia gauni la kupendea alionekana akifika ndani ya visiwa hivyo , alikuwa ni Master yake Magdalena anaefahaika kwa jina laa Tang Luyi kutokaDehebu la Tang na ilionekana ameambatana na Shagoni.
Ni muda huo huo Roma aliweza kugundua Tang Luyi alikuwa mwishoni mwa levo ya nafsi , ilionekana aliingia ulimwengu wa majini na ndipo alipoweza kukutana na Shagoni na kuafuata nyuma.
Upande wa Tang Luyi alionekana kutokumsikia Magdalena kwani macho yake yote yalikuwa kwa Anjiu , alionekana kama vile ameona kitu kilichomfanya kupaniki kiasi cha kumpelekea kutokushindwa kupumua vizuri.
Wakati huo huo Anjiu aliweza kugeuka na dakika ambayo aliweza kumuona Tang Lui muonekano wake ulikuwa umejaa mshituko.
“Wang..Sheng ni wewe kweli?”Aliongea Tang Luyi huku akionyesha kutoa machozi.
Roma naMagdalena wote walionekana kushangaa , kwa Roma haikwua sana kwani tokea mwanzo alishaotea uhusiano ulipo kati ya Anjjiu na Tang Luyi na Xiao kuwa mtoto wa mwanamke huyo.
Anjiu aliishia kukunja ngumi yake kwa nguvu na Xiao aliishia kumwangalia baba yake na mwanamke asie mjua kwa macho ya kiulizo.
Hali ya hewa ilibadilika na ilikuwa ni kama sasa majini waliofika hapo wanajua kwamba Anjiu mkuu wao alishawahi kuwa na mahusiano na bindamu ambaye yupo katika levo ya nafsi.
“Sijakosea kabisa , ni wewe kweli , ijapokuwa umebadilika lakini siwezi kusahau macho yako , Wang Sheng hebu nijibu mara moja wewe mwanaume muongo sana , ongea”
Tang Luyi alionekana kubadilika ghafla tu na hasira zilianza kumpata na alimshika Anjiu kwa nguvu na kuanza kumtingisha akimtaka kutoa majibu huku machozi yakimtoka.
Kila moja hapo alijua kinachoendelea , ilionekana Anjiu alimdanganya jina Tang Luyi , ukweli ni kwamba ilikuwa kama kwa Bi Wema tu alivyodanganywa na jini.
“Hey mwanamke ,kwanini unamfanyia hivyo baba yangu , huruhusiwi kumgusa baba yangu”Xiao alionekana kukosa uvumilivu na alitaka kumuondia Tang Luyi mbali na baba yake.
Lakini mara baada ya Tang Luyi kusikia msichana huyo anamwita Anjiu baba palepale alibadilika na kumshika mkono na kumnwagalia kwa furaha kubwa.
“Wewe mtoto , umemuitaje hivi sasa huyu mwanaume , wewe ni binti yake , una miaka mingapi mwaka huu?”
Xiao aliona huyu mwanamke ni kama kichaa na aliishia kumwangalia baba yake kwa kuomba majibu lakini alikuja kugundua baba yake macho yake yalishabadilika na kuwa mekundu.
“Baba ni nini hiki..”
“Anjiu acha zako , ndio kwamba haupo tayari kumtambua , hata hivyo haijalishi kwani atabakia kuwa mama mzazi kwa binti yako”Aliongea Roma mara baada ya kuchoshwa na maigizo.
Lakini kauli yake ilimfanya kila mmoja kumwangalia kwa mshangao mara baada ya kuona Roma alikuwa akijua kinachoendelea.
Roma mwenyewe hakuwa na uhakika sana , ukweli ni kwamba aliona ni kheri kwa xiao kumjua mama yake maana mara ya kwanza kukutana nae alionekana kama vile alichagua nchi ya Tanzania kuja kumtafuta mama yake baada ya kudaganywa na baba yake kama mama yake ni muafrika.
Nusu saa mbele hatimae Xiao aliweza kumtambua kwa mara ya kwanza mama yake mara baada ya kuthibirishiwa na baba yake , ilikuwa ni furaha kubwa kwake kujua mama yake alikuwa hai na alifurahi kuona pia mama yake alikuwa mrembo na kijana.
Kutokana na tukio hilo ambalo lilimgusa Roma pengine kutokana na maisha alioishi hata yeye ya kutofahamu wazazi wake ndio maana aliamua kuruhusu majini hao kuishi hapo kisiwani kwa muda , hata hivyo aliona hakuna tatizo ili mradi hawana madhara na pili majini hawakuwa na haja ya kupewa nyumba kwani hata nje wanaishi.
Upande wa Shagoni na yeye hakuwa na jinsi zaidi ya kubaki hapo visiwa vya wafu licha ya kwamba alikuja kugundua ndungu zake wengi hawakuwepo hapo na hata alipoenda kutafuta wengi wao walionekana kukimbia kusikojulikana.
Ndani ya muda mchache tu visiwa vya wafu vilikuwa ni kama miliki ya majini , kulikuwa na visiwa vingi ambavyo vingine havikuwa vikiishi watu hivyo walienda kujichimbia huko lakini pia wengi wao walionekana kama binadamu wa kawaida , ukiachana na kwamba wanapaa kwa binadamu wa kawaida wa visiwa hivyo wasingewaogopa na isitoshe wangeonekana mara chache sana kwani wanavisiwa wengi wanaishi ndani tu kutokana na baridi kali.
Hera alionekana kuwa na intelijensia pana sana kwani kati ya majini wa Hongmeng mmoja wapo kuna kiumbe kutoka sayari nyigine haikuwa bahari mbaya , ilionekana yote hayo yalifanyika ili kujua namna ya kumtoa Zeus katika gereza la roho lakini pia kutoa taarifa juu ya uzaifu wa safu ya ki ulinzi wa kisiwa hicho cha anga.
Upande wa Hera ambaye ni Rozu ilionekana alikuwa na ajenda zake za siri kama ilivyokuwa kwa Athena tu na aliamua kuuvaa mwili wa jini kwa kutimiza mipango yake.
Roma pia alikuja kuwaza maneno ya Aphrodite na Apollo , kwmaba licha ya Hephaestus mungu wa moto kutokuwa na nguvu kubwa kama wengine lakini alikuwa amejaaliwa uwezo wa kutengeneza Dhana.
Hata siraha yake ambayo ilifahamika kwa jina la Vulcan Hummer iliaminika sio tu kuweza kusababisha tetemeko la ardhi na kulipuka kwa volkano tu lakini muhimu zaidi inaweza kuunganisha nguvu ya Dhana mbili pamoja.
Sasa Roma muda mrefu alikuwa akijiuliza ule mshipi feki wa Aphrodite uliotokea nchini Tanzania umetokea wapi na wakati huo ni kama sasa ametegua kitendawili , ilikuwa ni kazi ya Hephaestus.
Kutokana na kukosa malighafi na teknolojia ilimfanya kushindwa kutengeneza siraha nyingi zaidi zenye nguvu.
Kwahio kitendo cha Rozu , Hephaestus na Hermes kwenda pamoja ujinini kushambulia ilimaanisha kwa muda mrefu sana walikuwa na ushirikiano mzuri.
Kuhusu Rozu ambaye aliamini lazima atakuwa Hera aliamini lazima atakuwa amefanya vitu vingi vya siri tena zidi yake lakini kwa muda huo hakuwa akijua kama anaweza kuchukua hatua kwa kila kitu.















SEHEMU YA 778.
Mpaka muda huo sasa Roma alikuwa ashaelewa baadhi ya vitu ambayyo Christen na wengine walikuwa wakijaribu kumficha.
Ilionekana kwasababu ya kutaka kufanikisha kufufuka kwa Moyo wa Gaia Christen alikuwa akijua kinachoendelea kwa ndugu zake wengine lakini aliamua pia kumficha.
Ingekuwa ni uongo kusema Roma hakujali , isitoshe swala hilo halikuwa dogo hata kidogo na ingekuwa ngumu zaidi kwake kucheza kwenye nafasi ya nusu binadamu nusu miungu lakini hata kama wakati huo ashajua hila zao je atawazuia?.
Kuja kwa kundi la majini na baadhi ya jumbe zinazomfikia kila siku ilimfanya Roma kuzidi kukosa maamuzi , ilionekana ni kama baadhi ya vitu vimechanganyikaana anashindwa kuchambua kipi ni kipi.
Siku nne zilipita na hatimae majini waliokuwa wameomba hifadhi ndani ya kisiwa hicho waliweza kupona na hata uwezo wao kuwarudia , majini watu hao hawakuwa masikini walikuwa wakitembea na vidonge vyao.
Roma hakuwajali sana kwani alijua sio binadamu na hawawezi kufa njaa au kufa kwa baridi , hata kama angetaka kuwaweka ndani ilikuwa ni ngumu wote kutosha.
Lakini kutokana na kwamba alikuwa amewapa mahali pa kuishi Zenzhei na wengine basi aliona awapatie na wakuu wa miliki hizo sehemu za kuishi akiwemo Anjiju na Xiao..
Master Shagoni na Anjiu ndio majini pekee ambao uwezo wao ulikuwa wa juu na baada ya siku nne kupita walijikusanya pamoja kwa ajili ya kikao na ajenda ilikuwa ni kurudi kwenye ulimwengu wao kuangalia kinachoendelea.
Roma hakuwa kama wao , yeye pengine alikuwa na uwezo wa kuwa na urafiki na miungu lakini wao haiwezekani , hivyo walikaa hapo kwenye miliki yake kwa ajili ya kurudisha nguvu.
Alijua miugu hawawezi kukaa ujinini kwa muda mrefu kwani kilichowapeleka ni kumtoa Zeus kwenye gereza la roho lakini hata hivyo jambo hilo liliwatia hofu zaidi na zaidi.
Majini walijua fika kama Zeus atafanikiwa kutoka , kwa uwezo mkubwa aliokuwa nao basi wao hawatakuwa na nafasi tena , jini huyo lazima angelipa kisasi.
Mwisho wa kikao walifanya maamuzi kwamba Shagoni kwasababu ana spidi kubwa aende Hongmeng akaangalie kinachoendelea , kuna waliokuwa wakiamini safu ya ulinzi wa gereza la roho haivunjiki lakini kuna waliokuwa wakiamini kutokana na kwamba miungu walikuwa wamerudiwa na uwezo wao wote na pia uwepo wa Yanyu ndani ya Hongmeng kwa miaka mingi ni kama alikuwa akisoma udhaifu wa safu hizo.
Siku tatu baada ya kupita Shagoni alirudi akiwa na taarifa mpya juu ya miungu kufanikiwa kukiweka kisiwa cha Anga ndani ya Hongmeng chini yao na mfumo wa ki ulinzi wa kanuni za anga umewekwa.
Master Shagoni anasema hakuwa na ujasiri wa kusogea karibu sana lakini hata kwa mbali aliweza kgundua kwamba safu ya ulinzi wa gerea la Roho inaonekana kukosa uhimili na muda wowote ingeporomoka .
Alichokuwa akimaanisha ni kama vile utando wa buibui utingishike hivyo eneo lote kutngishika.
Taarifa ya Shagoni iliwafanya kukaa kikao kingine na kufanya maamuzi na mwishowe wote walionekana kukubaliana.
Hawakutaka kuendelea kujifiacha bila ya kufanya kitu na walikubalina majini wote ambao wapo levo ya maji ya barafu kuendelea kesho wanaelekea ulimwengu wao kwa ajili ya kupambana na miungu ili kuzuia Zeus asitoke.
*****
Nyakati za usiku Roma alikuwa akiongea na wanawake wake mpaka pale Anjiu alipokuja kumtafura.
Anjjiu hakuingia katika ngome hio bali alituma ishara za kumuita akiwa nje ya mlima akiangalia mwezi akimsubiria Roma kutoka.
Katika siku zilizopita wapenzi hao wa zamani walikuwa wamerudiana na kuishi pamoja na Roma hakujua hata wanaendeeaje lakini alijua na uwepo wa Xiao basi hali haitookuwa mbaya zaidi.
Roma aliweza kutokeza katika kijimlima na kwenda kusimama pembeni ya jini Anjjiu , Anjiu sura yake ilionekana kujikunja ni kama amezeeka ndani ya siku mbili tu.
“Unaangalia nini?”Roma aliuliza mara baada ya kuona Anjiu alivyokuwa akishangaa mwezi , ukweli ni kwamba hakuwa na kinyongo kabisa na jini huyo .
Anjiu alisimama vilevile kwa muda mrefu na alionekana kuvuta pumzi na kisha akamgeukia Roma na kuinamisha kichwa chake kwa heshima.
Jambo lile lilimshangaza Roma na kujiuliza kwanini anamwinamia kwa heshima hivyo.
“Najua mimi Anjiu sina haki ya kusema hili lakini kitu pekee ninachoweza ni kukuomba kuniahidi kitu kimoja ..”Aliongea na kumfanya Roma kujua anachotaka kusema Anjiu.
“Unataka nikuahidi kupambana na miungu , nadhani nishaweka wazi kwamba si..”
“Hapana..”Aliongea Anjjiu na kisha alisimama.
“Sitarajii wewe kuja kupambana na adui mwenye nguvu na sisi ambao tulikuwa maadui zako , miungu sasa wapo katika levo ambao ni nje ya uwezo wetu”
“Kama ni hivyo nini unataka kutoka kwangu?”
“Luyi na Xiaoxiao ..”Anjiu uso wake ulikuwa ukicheza akionekana kujizuia kile alichokuwa akijisikia moyoni.
“Namaanisha kama kitu chochote kitanipata , tafadhari naomba uwe mwangalizi wao badae”
Roma alishangazwa na kauli ile na kujiuliza kwanini anachosikia ni kama vile wosia wa mtu anaeenda kufa , mwanaume ambaye alikuwa mbele yake alionekana sio yule mjanja mjanja kutoka miliki ya Xia.
“Inaonekana tayari ushajindaa na huna mpango wa kruudi mara baada ya kwenda kupambana na miungu?”Aliuliza Roma akiwa na tabasamu lililojaa uchungu.
“Wewe ndio ujuae vizuri , una uuungu ndani yako hivyo unajua kabisa ni kwa namna gani miungu wameimarika , tunaenda Hongmeng kwa ajili ya kuwazuuia miungu wasimtoe Zeus katika gereza la roho .. lakini nikuambie tu ukweli tunaenda kupambana ili historia isije kutuandika vibaya m ni swala la kikanuni tu , tunaenda kujitoa kafara”
“Kama ni hivyo kwanini bado mnataka kwenda kujitafutia kifo , unaweza kujificha kwa muda mrefu , si ndio umeweza kuunganisha familia yako hivi juzi tu?”
“Hapana ni kweli Luyi ni mke wangu na sikuwahi kumsahau hata siku moja …”Alionekana kuwaza kwa muda na kwa jinsi Anjiu alivyokuwa akionekana usingedhania hata kidogo ni jini.
“Najua Xiao anahisia za kimapenzi kwako lila wewe huna lakini bado naamini ana sehemu yake katika moyo wako mara baada ya kuweza kukaa nae nyakati zote ulizokuwepo katika ulimwengu wa jicho la langa .. sitaki binti yangu kuwa na mwanaume kama wewe mimi kama baba yake…siku nilipokuja kugundua mlikutana nilikuwa na wasiwasi atakupenda na mwishowe atagoma kurudi ujinini . ni mtoto anaetia huruma ambaye anastahili mwanaume ambaye atampenda kwa dhati kwa madhaifu yake yote … lakini sasa hivi sina jinsi zaidi ya kutaka kukuamini”
Mara baada ya Anjiu kuongea hivyo aliinamisha mgongo wake na kumwinamia Roma.
Roma alitaka kuongea kitu lakini maneno yalishindwa kumtoka.
Kama mwanaume ambaye ana madeni mengi ya mapenzi anaweza kukataa lakini kama baba ilionekana ngumu kumkatalia mwanaume mwenzake alietokea kumwamini.
Mara baada ya Roma kumuona Anjiu akitaka kuondoka alimsimamisha.
“Kwanini ?, kwanini unataka kumuacha mkeo na binti yako na kwenda kufa , unajua unaweza kuchagua njia nyingine kwa kutokwenda , hata kama miungu wanataka kuwaua majini wewe unao uwezo wa kukikwepa kifo , kwa niaba ya Master wa mpenzi wangu nakupatia hifadhi , unaweza kuishi hapa”Aliongea Roma.
“Kama nitasema ni kwasababu ya msemo wa kidunia unaosema ‘Kusimama na kuanguka kwa ulimwengu ni jukumu la mtu binafsi utaniamini?”
“Lakini wewe sio mtu ambaye unajukumu hilo na sio wewe tu majini wote waliopo ndani ya hiki kisiwa sio jukumu lao”
“Umekosea , kila kiumbe chenye utashi ndani ya huu ulimwengu tupo katika daraja moja, sisi wote ni watu wa dunia kabla ya jamii zetu , uwezo wetu na tamaduni zetu na hakuna kinachoweza kubadilisha huo msingi . pengine wewe bado ni kijana mdogo na umeishi maisha yako nje na nyumbani kwa muda mrefu , labda ni kwabsabu una uungu ndani yako na sio binadamu kamili , lakini unapaswa kujua kinachotokea kwa binadamu kina athari za moja kwa moja kwa sisi majini, adui wa majini ndio adui wa binadamu … tunaweza kupigana wenyewe kwa wenyewe lakini kuna mahali tutafikia katika maelewano na kuweka tofauti zetu mbali hii ni kwasababu sisi wote ni wa ulimwengu mmoja licha ya kutenganishwa na vizuizi , sisi wote ni wa hii dunia na huo ndio msingi .. kama viumbe kutoka sayari nyingine wanataka kuondoa mpaka mizizi yetu basi ni sawa kwetu kuinyweshea ardhi yetu na virutubisho vya damu yetu”
Anjiu hakuonekana na huzuni wala na furaha wakati wa kuongea bali alikuwa akiongea katika sauti ya ukweli lakini maneno yake yalimfanya moyo wa Roma kuungua.
Mwanaume aliekuwa mbele yake alionekana kupoteza hadhi yake na alikuwa akipotezea kila kitu , uwezo wake na madaraka yake
Katika wakati huo alijiona si kitu , si kiumbe mwenye nafasi kubwa kam wengine , hakujiona mkubwa kama binadamu bali alijona kama mwanajeshi kati ya kundi la wanajeshi ambae anajiandaa kwenda vitani kwa ajili ya familia yake , mapenzi yake na uzalendo wake.
Sio kwamba hakuwa akikiogopa kifo lakini hakuwa tayari kuigopa kuikabili hatiima ya maisha yake.
Pengine hilo ndio kusudi la mwanzo kabisa la Mungu juu ya viumbe wote katika uso wa dunia.. Roma hakuweza kujizuia bali kufikiria hivyo.
Mpaka Anjiu anaondoka Roma aliendelea kubakia katika kijimlima akiwaza.
Roma aliinua uso wake na kuangalia nyota na mwezi huku baridi kali ikimpuliza na hakuna aliemsumbua..
Siku iliofuata asubuhi majini wote kuanzia levo ya kupita Dhiki maji ya barafu waliondoka kwenda ujinini vitani , maagano na ndugu na wapendwa wao ilikuwa jambo lisiloepukika.,
Zenzhei na binamu yake waliweza kuagana na kaka yao Nefi kwa machozi wakati Tang Luyi na XiaoXiao wakiomboleza kuondoka kwa Anjiu.
Mwanzoni XiaoXiao alitaka kumlazimisha Roma kuchukua hatua lakini Anjiu alimzimisha palepale kabla hata hajaongea neno.
Roma hakuongea neno na kimya kimya aliangalia namna mamia ya majini walivyokuwa wakipotelea katika upeo wa macho yake.


















SEHEMU YA 778.
Miliki ya Roma ya visiwa vya wafu hatimae ni kama ilirudi katika hali ya amani na kulikuwa na kimya sio cha kawaida.
Mamia ya majini waliokuwa na uwezo wa chini walikuwa wamejikusanya katika eneo moja katika kipande cha ardhi huku hali ya hewa ikiwa ni ile ya kimajonzi na kufanya eneo lote kufunikwa na kiwingu cheusi.
Roma aliesimama kandokado ya fukwe alikuwa ameinamisha kichwa chake chini , macho yake yalikuwa kama kioo kana kwamba alikuwa akifikiria kitu kwa kujiangalia.
Baridi inayotokana na upepo wa baharini ilikuwa imemloanisha nguo zake lakini hata hakutambua.
Bila ya kujua hatimae mwanadada Rose alimsogelea na kisha kushika mkono wake huku macho yake yakiwa na mahaba mazito.
“Unafikiria nini , unaonekana kuangalia eneo moja bila kutoa macho?”Aliuliza kwa sauti hafifu huku akiwa na tabasamu.
Roma taratibu alikiinua kichwa chake na kumwangalia mwanamke huyo.
“Darling hivi .. hivi unadhani nimefanya kitu sahihi?”
Rose alionekana kushangazwa na swali hilo pengine ni kutokana na kwamba amemjua kwa muda mrefu sana kuliko wanawake wote na ilionekana wazi ni kitu gani alichokuwa akiuliza , Rose mara baada ya kuwaza kwa muda alionekana kupata cha kuongea.
“Tokea uwe siriasi sana juu ya kufanya maamuzi kwanini hujawahi kutuomba maoni yetu , kwanini umeomba sasa hivi?”
“Unajua kuwaza namna hii sio staili yangu lakini maamuzi yangu yana athari kwa kila mtu na ndio maana nina mawazo”
“Kwanini usifanye hivi mpenzi , naomba uniruhusu nikuulize maswali?”
“Uliza”
“Je unawaogopa miungu , hasa hasa Athena?”
“Hapana , naomba tu niwe mkweli kwako , nisingeweza kuwa hai mpaka sasa kama ningekuwa naonyesha uwezo wangu wote , ijapokuwa ninaweza nisiwashinde wote lakini ni ngumu kwangu kushindwa”
“Je kama hutoenda , unajihisi utakuja kujutia baadae kwa maisha yako yote?”
“Kujutia … dah hapo sijui”
“Vipi kama utajutia , je upo tayari kukabiliana na majuto?”
“Bila shaka sitaki kujutia lakini hakuna mtu anaeweza kuishi bila kujutia baadhi ya vitu kwenye maisha yake , ni afadhali ni waone wote mkiwa salama”
“Je unaamini utaendelea kuwa nje ya hili kama hutojiunga katika mgogoro kati ya miungu na binadamu?”
“Unamaanisha nini?”
“Unaweza kutokujali maneno ya watu wengine na kupotezea chuki zao lakini kila mtu ni tofauti , ukiachana na wewe hapa kila mtu ni binadamu bila ya kumsahau Lanlan ambaye ni mtoto wako, awamu hii ni vita kati ya miungu na viumbe wa dunia na wewe ni kama mwakilishi wa binadamu ambaye utaamua hatima yao , haijalishi nani atashinda utachukiwa na pande zote kwa kutokuingilia ,miungu watakuchukia kama hutoungana nao na binadamu watakulaumu kama hutoungana nao , binadamu watakuona kama ndio chanzo kwasababu wataamini wewe ndio mtu pekee uliekuwa na uwezo wa kupindua meza lakini ukaamua kujificha na kuwaangalia wanakufa..
Roma alijikuta akiinua mdomo wake kuongea neno lakini alishindwa kuongea , hakuwahi kufikiria katika upeo huo.
Iikuwa ni kweli aingilie asiingilie ilimaanisha angechukiwa tu na upande wowote.
Ijapokuwa Rose alionekana hajamaliza kuongea kile alichokusidia lakini alijua ni wapi anaelekea
Kwasababu ya wasifu wake asingeweza kujiweka mbali na kinachoendelea kwa namna yoyote ile.
Hata kama asingejali miungu na binadamu na kuamua kutofanya chochote binadamu au miungu wangeinyooshea mikono familia yake.
Iwe ni kwa miungu au kwa binadamu kama wataamua kuonyesha chuki zao kwa familia yake basi asingeweza kuwazuia wote.
“Usiwe na wasiwasi sana haijalishi ni maamuzi gani utachukua lakini hatutakuja kukulaumu wala kujali kama yalikuwa sio sawa au sawa , isitoshe wewe sio mwamuzi wa kinachokwenda kutokea”Aliongea Rose.
“Hapana..!!, Rose umekosea awamu hii , sijawahi kutamani kuwa nje ya maamuzi ya kile kinachokwenda kutokea”
“Hubby unataka…’”
Rose alijihisi kitu kikikoroga nafsi yake na hakuweza kujizuia ilionekan kama kwamba ufahamu wa Roma umeamka.
“Siwezi kuvumilia hii hali ya kishenzi kuendelea hivi , haijalishi ni hatari kiasi gani ninapaswa kuzuia kama inaathiri watu wangu wa karibu , hakuna wa kunizuia kwa lolote juu ya hili”Aliongea Roma na palepale alimvuta Rose na kumkumbatia na kisha akambusu kwenye paji la uso.
“Thank you”
Mara baada ya kuongea kauli hio alikuwa tayari ashapotea na kuja kuibukia nje ya ngome yake.
Kwa bahati nzuri alimkuta Edna aliekuwa akitaka kuingia ngomeni kutokea nje akiwa amemshikilia Lanlan mkono .
Yeye na wanawake wengine walionekana kuwa na wasiwasi mara baada ya kuja kusimama mbele yake.
Roma alivuta pumzi nyingi na kuzishusha na kisha aliinama chini na kumkumbatia Lanlan na kumbusu shavuni na kisha akasimama na kumwnagalia Edna.
“Mpenzi ni….”
“Usije ukathubutu ”
Kabla hata hajamaliza sentensi Edna ashabwatuka na kumnyooshea Roma kidole huku akionyesha mabadiliko.
Uso wake ulikuwa siriasi mno na alionekana kuwa kauzu isivyokuwa kawaida , alikuwa ni barafu.
Mabadiliko yake na namna alivyofoka iliwaogopesha kila mtu ndani ya hilo eneo lakini palepale waliweza kuona kitu katika macho ya Roma.
Roma muonekano wake ulibadilika mno wakati akiwa anamwangalia mke wake , ilionyesha alikuwa na majonzi na hali ya kuomboleza kwa namna alivyokuwa akimwangalia Edna.
Ni sawa na pale unapomwangalia mpendwa wako akiwa hospitalini huku ukijua hana muda mrefu wa kuishi ndio namna Roma alivyokuwa lakini haikueleweka muonekano wake unahisia za namna gani.
“Lakini sijaongea chochote mke wangu…”Roma aliongea kwa kusita.
“Najua unachopanga kufanya hata usiponiambia , nakukataza kwenda kupigana na miungu Roma”Aliongea tena na kutaja jina la Roma kwa mara ya kwanza kwa muda mrefu sana kuonyesha namna gani alikuwa akisisitiza , kwa jinsi alivyokuwa akiongea ni kama swala hilo halina mjadala.
Roma aliishia kukunja ndita , ijapokuwa siku zote alikuwa akiwasikiliza wnawake wake lakini akiamua lake hakuna wa kumzuia.
“Edna I have made a decision , take care of Lanlan , I’ ll came back as soon as possible”Aliongea Roma akimaanisha Edna mwangalie Lanlan kwani ashafanya maamuzi na atarudi mapema iwezekanavyo.
Edna alionekana kutetemeka na kauli hio na haikujulikana kutokana na woga wa Roma kuwa hatarini au hasira , ghalfa tu alisogea mbele na kumshika Roma mkono.
“Roma mume wangu naomba tafadhari usiende , Please don’t go , kwa ajili yangu na mtoto naomba usiende”
Edna alibembeleza na alikuwa amebadilika akiwa ameinamisha kichwa chake chini na ilikuwa ni kama vile anaogopa kukutanisha macho na Roma.
Lanlan aliekuwa akiangalia alikuwa aking’ata lips zake kwa wasiwasi kwani aliona muda wowote mama yake na baba yake watagombana hivyo hakuweza kuongea chochote, upande wa Roma aliishia kutoa kicheko cha kivivu mno.
“Nilikuwa na chembe ya kusita dakika chache zilizopita lakini sasa nadhani napaswa kwenda , kuna vitu napaswa kukabiliana navyo mapema au baadae..”
Edna mkono wake ulitetemeka na kinyonge sana alimwachia Roma na kupiga hatua moja kurudi nyuma.
“Naomba umwangalie Lanlan , napaswa kwenda Edna”Aliongea Roma na kisha alimshika Edna mkono kwa sekunde na kisha akauchia na akapotea palepale.
Upande wa Edna alikuwa ni kama mwanamke ambaye haamini kilichokuwa mbele yake , aliishia kukosa nguvu na kidogo tu angekaa chini , ilikuwa ni kama vile kitendo cha kumwachia Roma mkono ni kama vile alikuwa yupo tayari kwenye maisha yake kuacha kila kitu lakini sio kumwachia Roma lakni mwisho wa siku alikuwa amemuacha.
Wakati warembo wengine wakiwa na wasiwasi juu ya usalama wa Roma Edna yeye alionyesha hali ya huzuni kama vile hatomuona tena.
Unadhani ni siri gani Edna anayo? , nawakumbusha hii simulizi inaitwa Niliemdhania ni kahaba kumbe bikra.
Maana yake ni kwamba mwanamke niliemdhania ni kahaba kumbe bikra kuna kingine kuhusu yeye ….. ni kichwa endelevu hakikuishia Mbagala tu bali ulikuwa ndio mwanzo wa unabii.
Unadhani nani ataibuka kidedea katika hio vita
Usiache kunipa motsha kwa namna yoyote ile…
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 780.
Ni katika ulimwengu wa majini watu ndania ya miliki ya Hongmeng , hali iliokuwa ikiendelea katoka miliki hio ilikuwa ni ya kutisha
Yale.majengo mazuri na makubwa ambayo yakikuwa fahari ya miliki hio yalikuwa yamebakia vifusi.
Eneo lote.lilikuwa ni vumbi na michanga iliochanganyika damu na viungo vya miili , kilichokuwa kikionekana ilikuwa ni maana halisi ya eneo la.vita.
Licha ya hali hio ya kusikitisha katikati ya eneo hilo upande wa amgami kulikuwa na jengo ambalo limezungukwa na mwanga ambao mwezoi sio mwezi ni kama mwanga wa platinum ule ambao haujakolea .
Naam eneo hilo mdio linapatikana Gereza la Roho na majini pepo, ndio.sehemu pekee ambayo miungu wameshindwa kuiangushha kutokana na uimara wake.
Sasa katika safu hio ya ki ulinzi ya mwanga wa dhahabu wanaonekana watu wa tatu wakiwa wamesimama , ilikuwa ni kama vile wamefanya kazi kubwa sana na ishara flani za kukata tamaa zilikuwa zimegubika nyuso zao .
“Hepheastus una uhakika hii mbinu itafanya kazi??”Mwanamke mrembo Rozu kwa jina la kijini na Hera kwa jina la.viumbe kutoka dayari nyingine aligeuka na kumwangalia Monk aliekuwa pembeni yake na kumuuliza.swahi hilo.
Mwanaume ambaye alikuwa na kioara alievalia Kissaya mavazi maalumu ya kimonk alikuwa ndio Master Yanyu ambae.mwili wake inaishi nafsi ya Hephaestus nafsi ya kiumbe kutoka sayari nyinhine ambae wasifu wake ni mungu wa moto.
Kwenye mikono yake alikuwa ameshikilia gurudumu ya kuwaka waka ambayo ilionekana ni Dhana yenye maandishi ya herufi ambazo hazikutafsirika.
Lakini kama Sharif na Aoiline wangeona herufi hizo wangezitambua mara moja ni lugha ya wajumbe wa Mkuu wa Enzi, lugha ambayo ilitumika.miaka.minhi iliopit wakti.wa wajumbe hao kufika duniani kwa misheni maalumu.
“Numekuwa katika hiki kisiwa kwa muda wa miaka mia tatu na niliishi kwa kufanya utafiti wa namna ya kuvunja hili gereza kila siku, Busara na hekima iliotumika kujenga sio ya kawaida na ni ngumu mno na hatuwezi kutumia nguvu kulivunja, hata kama tukiweza mutengeneza shimo msukumo wa presha ndani yake utalifunga ndania ya sekunde tu, ukweli ni kwamba tukifanya hivyo kutatokea misukosuko ambayo itafanya ulinzi wake kuimarika zaidi, lakinj nilikuja kugundua njia pekee ya kufanikisha hili ni wakati wa presha ya safu yenyewe kuwa juu na hii ni kwasababu ni kama herufi zilizowekwa ndani yake ni kama program maalumu.Kwahio nilitumia miaka yangu mingi kukusanya vitabu vya kale ambavyo vina tafsiri mbalimbali ya maandishi hayo na nilipo fanikiwa ndio nikatumia miaka mia moja mingineyo kutengeneza hii Dhana nilioioa jina la Reverse Dhamachakra, Hii Dhana haiwezi kufungua hii safu ya ulinzi mara moja lakini ino uwezo wa kupunguza kasi ya ufanyaji kazi mpaka kwenye hatua hatarishi na hapo ndipo presha ya nishati iliopo ndani ya gereza igapungua na kumfanya Zeus kutoka”
“Hehe..mbona ni maajabu hivyo Hephaestus, kama umefanikiwa kwanini unaendelea kusimama? “
“Hatuwezi kuharakisha, nishaona hili muda muda muhimu wa kugeuka ni mchana na safu hii inakuwa haipo imara wakati huo kutokana na kujaa kwa wingi wa nishati chanya, itakuwa ni salama zaidi nikiingiza mfumo wangu wa Reverse Dhamachakra kwanj tutakuwa salama muda huo”
“I don’t care about anything that you said as long as Zeus can come out soon. Humph. I don’t want that b*tch to be so arrogant”Aliongea Hera akisema hajali chochote ambacho amesema ilimradi zeus aweze kutoka mapema... Anasema hataki yule malaya kuwa na kiburi.
“Muone unavyoongea Hera, hata kama Zeus moenzi wako wa zama akitoka hawezi kukufanya wa kwanza kabla ya Athena, siku zote nguvu inatawala, haina maana kuendelea kumuonea wivu, kila. Kila kitu kipo usawa wa kiganja chake, ashakushinda muda mrefu tu”Aliongea Hermes na kumfanya Hera kumwangalia kwa ukauzu na wakati anataka kusema jambo mara alikunja sura baada y kuhisi kitu.
TUTAMALIZIA WIKIEND
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.


MTUNZI: SINGANOJR.


Mono no aware

SEHEMU YA 728.
Tabasamu la uovu ambalo alikuwa akionyesha ‘Roma’ liliwafanya wale majini kujihisi ubaridi usiokuwa wa kawaida.
“Uwezo wake sio wa kawaida”Aliongea Jini Anjiu kwa hamaki mara baada ya kuona Roma amebadilika.
Senjii na Sena wote walionyesha nyuso za wasiwasi na kweli waliweza kuona uwezo wa Roma ulikuwa umeongezeka kwa kiasi kikubwa tofauti na dakika kadhaa zilizopita.
Ijapokuwa hawakuweza kukadiria uwezo wake ulikuwa mkubwa kiasi gani lakini mkandamizo wa nguvu za kijini aliokuwa akitoa ulikuwa ni wa levo nyingine kabisa kuliko mwanzo.
Chaos hakutaka kujisumbua kabisa na namna majini hao walivuokuwa wakimwangalia badala yake alionyesha furaha kwa namna ya kupumua kwa nguvu.
“Tamuuu…. Pumzi yenu inatamanisha sana”Chaos aliekuwa katika sura ya Roma aliongea na kumfanya Senji kuzidi kuwa na wasiwasi.
“Anajaribu kututania huyu… msiwe na wasiwasi , lazima atakuwa ametumia mbinu ya hadaa kujaribu kutuaminisha uwezo wake umeongezeka , hakuna jini au binadamu mwenye uwezo wa kupandisha uwezo wake ndani ya dakika kadhaa tu”
“Upo sahihi hakuna kumuachia aondoke hapa”Aliunga mkono Senji na palepale alitoa Dhana yake ya alama ya kiganja cha mkono na kurushia hewani na palepale maandishi ya njano yaliweza kuonekana.
“Mkondo nyota , kupasuka kwa anga!!”.
Ndani sekunde tu kulikuwa na wingu kubwa la nguvu za mbingu na ardhi ambazo zilikuwa zimejikusanya juu ya Chaos na ziliongezeka na kutengeneza nguzo kubwa ya kinishati ni shambulizi ambalo lilitolewa na Senji.
“Boom!!!”
Nguzo ile kubwa ya kinishati ilidondoka kutoka juu kwenda chini na kusambaza mionzi ambayo ilisambaa karibia eneo lote la chini yake , ilikuwa ni kama vile anga linaharibika.
Lakini hata hivyo Chaos hakuonyesha kujali kabisa na shambulizi hilo na aliruhusu kushambuliwa na palepale aligeuza nguvu zote hizo na kuzisharabu kwa kuzigeuza nishati za mbingu na ardhi.
Katika spidi ya kupepesa macho mashambulizi hayo yalionekana kuwa ya kawaida mbele ya Chaos.
Takribaki miaka elfu nne iliopita majini wa enzi hizo waliweza kumiliki nguvu ya Radi , ni sanaa ambayo waliweza kuistadi kwa kuweza kuvuna nishati za mbingu na ardhi lakini licha ya hivyo iliwachukua miaka kumi katika kumfungia Chaos katika gereza la Cauldron.
Kitendo cha Chaos kuweza kumiliki mwili wa Roma alihamisha nguvu zote ambazo zilikuwa kwenye Cauldron na kuziingiza katika mwili wa Roma ndio maana alionekana kuwa na uwezo wa juu sana tofauti na mwanzo.

Kwasababu Chaos alikuwa tayari ashamiliki mwili huo hakutaka kuficha uhusika wake kamili na iliamua kufanya mashambulizi kwa kasi kubwa.
Siku zote Chaos alitaka kupata mwili wenye nguvu ambao utamuwezesha kurudisha utukufu wake kuliko kuendelea kukaa katika gereza la chungu.
Yaani njia pekee ya Chaos kuweza kutoka katika gereza ni kuweza kuvamia mwili wa Roma
“Hayo ndio mashambulizi yenu , nyie majini hamna kitu kizuri zaidi cha kunipiga nacho tofauti na hii mitekenyo yenu?”Chaos alitoa tabasamu la kejeli na baada ya kauli yake hio ilimrushia Rufi ndani ya kile chungu ili kuendelea kumpatia ulinzi.
Rufi alishajua mtu ambaye yupo mbele yake sio Roma bali ni Chaos na Roho ya Roma ilikuwa imefungiwa , alikuwa kwenye hali ya wasiwasi lakini alishindwa kutoa hata sauti kutokana na hali ya woga aliokuwa nao.
Anjiu alionekana kufikria jambo na kugundua kitu na palepale akapaza sauti kubwa.
“Wewe sio Roma Ramoni , wewe ni mnyama wa kishetani wa machafuko , The Chaos!”
“Nini?”Kauli ya Anjiu ilishitua wale wengine lakini Chaos alitoa cheko kubwa la kishetani.
“Haijalishi mimi ni nani , muhimu ni kwamba nyie wote mnakwenda kuwa chakula changu”
“Unajiona ni nani wakati ndio mwisho wako leo ,Ewe Joka sanaa ya wino tokaa… Hasira ya Joka kuu!!”Aliongea Sena kwa nguvu na hakuonyesha kuogopa kabisa.
Dakika ileile wino ulifyatuka kutoka kwenye mwili wake na kutengeneza kizingia ambacho ndani ya dakika tu kilibadilika na kuwa Joka kubwa mno ambalo lina meno marefu na kuanza kushambuliana na Chaos.
Chaos hakuweza kukwepa shambulizi lake na alikutana nalo ana kwa ana lakini kabla hajaguswa palepale ule wino uliyeyuka na kugeuzwa nishati ya mbingu na ardhi na ukamezwa palepale , shambulizi hilo linaweza kuonekana la kimaajabu lakini mbele ya Chaos lilikuwa ni la kitoto sana.
“Bi Sena kuwa makini”Anjiu aliongea kwa nguvu lakini alionekana kuchelewa kumtahadharisha.
Chaos tayari alikuwa akimsogelea Bi Sena kwa spidi na Sena alionekana hakutegemea Chaos angeweza kumsogelea kwa kasi na muda huo kitu pekee alichokumbuka kutoa kama siraha yake ni Dhana ya Kilio cha pepo.
“Cling , Clng , Cling!!!”
Dhana ya kawaida kama hio mbele ya macho ya Chaos ilikuwa ni kama kijiti na ilivunjwa vunjwa palepale.
“Arghhhh…!!!”
Sena aliishia kutoa kilio kikali mno ambacho kilisambaa na kutengeneza mwangwi mara baada ya kukamatwa na Chaos na kupigwa kibao cha kichwani.
Kichwa cha Bi Sena kilipasuliwa palepale kama vile ni tikiti lililopigwa na nyundo na damu zilifyatuka kama vile ni Fountain.
Tabasamu la Chaos lilikuwa la ukichaa kabisa mara baada ya shambulizi hilo lakini kwa majini wengine walaikuwa katika hali ya mshituko kwa kile ambacho kimetokea.
Roma ambaye sasa ndio Chaos mwenyewe mara baada ya kumpasua Sena kichwa chake ilichomoa mishipa mikubwa ya damu iliokuwa shingoni na kuanza kuinyonya damu yake kwa starehe zote kama vile alikuwa na kiu ya damu ya muda mrefu sana.
Baada ya damu kukauka ilirarua mwili wake palepale na kisha kuanza kutafuna nyama yake , ijapokuwa kwa nje alikuwa akionekana kama Roma lakini matendo aliokuwa akiyafanya ni ya kimnyama kabisa hasa wakati alivyokuwa akitafuna nyama ya jini Sena.
“Arghhhh…!!!”
Rufi alishindwa kuvumilia na kuishia kutoa kilio mara baada ya kuona mpenzi wake akitafuna nyama mbichi , ijapokuwa alikuwa akijua anaemwangalia sio Roma ni Chaos lakini bado hakuamini macho yake.
Majini wengine wa miliki hio ambao walikuwa kwa mbali waliishia kushikwa na bumbuazi huku miguu yao ikilainika na nyuso zao kupauka, hawakuelewa ni kwa namna gani meza imegeuzwa.
Jini ambaye alikuwa amefikia mwishoni mwa levo ya maji ya kiroho alikuwa ameuliwa kwa kuraruliwa namna hio na mtu kama mnyama ambaye yupo katika sura ya Roma.
Machafuko aliangalia juu mara baada ya kumaliza kutafuna na sura yake yote ilikuwa imefunikwa na damu na vipande pande vya nyama , ilikuwa ni kama vile imeibukia kutoka kwenye dimbwi la damu , ijapokuwa alikuwa amefunikwa na damu mwili mzima lakini alikuwa akitoa tabasamu kama vile alikuwa akiufurahia muonekano wake.
“Utamu ambao nilikuwa nikiuota mara kwa mara hatamae nimeweza kuuonja katika uhalisia .. Daah …!!”Aliongea huku akilamba midomo.
Kama kuna yoyote ambaye angeweza kusikia kauli yake , na kuona tukio hilo na pia kama usingeweza kuamini maneno ya Anjiu alioongea basi hakika mtu huyo angesema Roma ni kichaa tena zaidi ya neno lenyewe la ukichaa.
Machafuko au Maafa ndio jina lake halisi , alikuwa ni mnyama aliepewa jina hilo kutokana na matendo yake, alikuwa ni mnyama wa Ghasia, mnyama wa kigaidi ambaye wakati huo alikuwa akimiliki mwili wa Roma na kuonyesha uhalisia wake.
Dakika chache zilizopita walikuwa wana uhakika wa kumshinda Roma lakini sasa hivi mashambulizi yao yalikuwa ni kama vile wanarusha mayai kwenye jiwe na hatimae wanakuja kuelewa sababu ni nini.
“Kimbieni , Kimbieini wote katika uelekeo tofauti tofauti!!”
Anjiu mara baada ya kuona hali sio hali palepale aliona sulushisho ni kukimbia kwa majini hao katika kila pande , maana aliona hakuna namna wanaweza kushinda pambano hilo mbele ya Machafuko kwa tukio lile la kuweza kumuua Sena kwa shambulizi moja tu.
Anjiu hata yeye hakutaka kubakia tena katika eno hilo na alitimua nduki kuelekea upande wa kusini magharibi, wakati huo akipaza sauti kuwaamrisha majini wengine kukimbia bila kufuatana.
Uelekeo ambao alichukua nni kuelekea upande wa miliki ya Panas , Anjiu alijiua kama Chaos ataamua kumfukuzia basi ni vizuri kuelekea upande ambao kuna wajuzi wa mbinu za kijini za juu ili kuweza kusaidiana katika kumdhibiti.
Lakini sasa wakati Anjiu yeye akifanikiwa kushituka kwa dakika na kuanza kutimua jini ambaye alifika hapo pamoja na Senji yeye alichelewa kidogo licha ya kwamba alijua kabisa hana uwezo wa kushinda na alipaswa kukimbia hata kabla ya kauli ya Anjiu.
Kitendo cha Anjiu kutoa agizo la majini kukimbia, Machafuko alionekana kukasirika sana na kujiambia hawa kunguni wanathubutu vipi kukimbia , haileti tofauti yoyote kwani tayari yupo katika mwili wa Roma hivyo ingekuwa ni swala la muda tu kuwararua wote na kuwatafuna.
Lakini sasa kitendo cha majini hao kukimbia katika uelekeo tofauti ilimuia vigumu kuwakamata wote kwa wakati mmoja na alibakiwa na chaguo moja tu la kuchagua upande wa kufukuzia na hapo ndio iliona jini mzee ambaye yupo katikati mwa levo ya maji ya kiroho ambaye alizubaa.
“Arghh…!!!, tafadhari usinitafunee”
Jini yule mzee mara baada ya kuona Machafuko amemuungia spidi alipiga makelele huku akiwa na wasiwasi namna ambavyo anakwenda kuraruriwa , hakuamini miaka yake mia moja aliotumia kuvuna nishati za mbingu na ardhi itaishia katika mdomo wa Chaos.
Licha ya kujitahidi kukimbia huku akipiga yowe Chaos alikuwa na spidi kuliko yeye na ndani ya dakika tu alishikiliwa mkono na kuvutwa kwa nguvu na kukamatwa shingo ambayo ilivunjwa palepale na kuanza kunyonya damu na nishari yake yote ya mbingu na ardhi na kisha kugeuzwa majivu.
Majini wote wa miliki ya Xia walikuwa wametoweka katika makao hayo kwa kukimbia pande tofauti tofauti na Chaos hakutaka kujisumbua kuwafukuzia.
Chaos aliona hana haja ya kujisumbua ili hali ana uelewa juu ya Roma alichoona mara baada ya kufika katika miliki ya Kekexil , kama ni kutaka kwenda kuendelea kujipatia vitoweo basi tofauti na kufukuzia majini waliosambaa itakuwa vizuri kuelekea Kekexil kula nyama ya majini na baada ya hapo angeenda na Hongmeng na kisha Panas kumalizia na hatimae utukufu wake ungeonekana.
Kutokana na Chaos kuwa mnyama ambaye hana mwisho , mnyama ambaye hafi na wa kishetani uwezo wake wa kiakili ulikuwa mkubwa mno lakini licha ya hivyo kitu kimoja ambacho hakuwa na uwezo wa kujizuia ni tamaa ya kunyonya kila aina ya nguvu ambayo ipo katika ulimwengu huo na kisha kuhamia katika ulimwengu wa kawaida na kula kila kiumbe kinachovuta pumzi.
Ilikuwa ni kwasababu hio hio ya tamaa ya mnyama huyo ndio maana aliishia kwenye mtego wa chungu na kufungiwa kwani kama sio hivyo angeweza kufuta jamii ya kibinadamu na majini mara moja.
Hayakuwa maamuzi ya mnyama huyo bali ilikuwa ni hatima yake , ni swala ambalo ili kuendelea kuishi asingeweza kuepuka kufanya hivyo.
“Mh wapo vizuri kwenye mikimbio…”Aliongea huku akimalizia utamu wa mwisho mwisho wa nyama mbichi na mara baada ya kukamilisha iligeuza macho yake kwa Rufi ambaye alikuwa amemhifadhi kwenye chungu.
Rufi mara baada ya kukutanisha macho na Chaos alihisi kutetemeka kusikokuwa kwa kawaida.
“Umemfanyia nini mume wangu?”Aliongea Rufi kwa kujikaza.
“Bado tu unapata ujasiri wa kuniongelesha wewe msichana… mwanaume wako tayari hayupo hapa na kuanzia leo na kuendelea huu mwili ni mali yangu na si vinginevyo”
“Wewe ni muongo , mpenzi wangu hawezi kukupatia mwili wake kirahisi hivyo”Aliongea Rufi huku machozi mengi yakimtoka akiwa na tumaini hafifu kwenye moyo wake na kujiambia Roma ataweza kuishinda nafsi hio.
“Hahahaha…. Hahahaha.. sina muda wa kupoteza na binadamu usie na thamani kama wewe.. Roma alileta ujuaji na kuniambia oh eti nilindie mpenzi wangu mpuuzi yule , nilimkubalia ndio lakini haikuwa nia yangu ya dhati kukulinda, nilitaka akubaliane na matakwa yangu tu, ili kurudisha uwezo wangu katika viwango ninatakiwa kuendelea kunywa damu ya
majini na sina muda wa kujibishana na binadamu mimi”
Chaos muda huo alikuwa akiendeshwa na roho ya kisasi kwa kile majini walichomfanyia mpaka kumfukia katika chungu na alitaka kulipa kisasi kwa kuwatafuna.
“Roma anadharau sana ameshiindwaje kuniheshimu wakati nilipokuwa dhaifu na kunifanya mbwa wake, sasa ili kulipiza machungu ya kunidharau nitaanza na wewe mwanamke wake na baada ya hapo nikimalizana na kunywa damu ya majini nitaenda kisiwani kwake na kula wengine ili kutuliza chuki yangu, lakini kwasasa ninachotamani ni kuona wewe mrembo ukiomba huruma yangu hahahaha… nitakusamehe kama utanifurahisha pengine unaweza kuwa mpenzi wangu”
“Wewe ni mnyama tu unaesikitisha na kutia huruma na utabakia kuwa hivyo , niue kama unataka unafikiri nitaomba uniache hai , mwanamke dhaifu kama mimi bado tu pia ninao uwezo wa kukudharau”Aliongea Rufi kwa hasira na kumfanya
Chaos kutoa tabasamu la kifedhuli na hasira kuongezeka maradufu huku macho yake yakizidi kuwaka taa nyekundu.
“Kwasababu unaleta ujeuri mbele yangu nitararua mwili wako vipande vipande na kukutafuna , sipati picha Roma atakavyojiskia mara baada ya kujua amemtafuna mpenzi wake”
Baada ya kumaliza kauli hio Chaos alimsogelea Rufi kwa spidi kwa kulenga kifua chake akidhamiria kunyofoa moyo wake nje.
Lakini kadri alivyokuwa akijitahidi kunyoosha mkono wake kumfikia Rufi alishindwa kabisa kumfikia na aliishia kufurukuta na kutetemeka kaa vile anaishiwa na nguvu.
“Nini… imewezakenaje… pumbavu.. noo!!”
Chaos alijikuta akizidi kupagawa huku mwili wake ukitetemeka , kiini cha macho yake ambacho kilikuwa ni cha rangi nyekundu kilianza kufifia na nguvu yake ya giza ilianza kupungua pia.
Rufi ambaye alikuwa amefumba macho yake na
masikio yake akiwa tayari kufa ghafla tu alihisi jambo ambalo halikuwa la kawaida na kujikuta akiingiwa na tumaini na wasiwasi kwa wakati mmoja.
Wakati huo kulikuwa na vita kali vya kifahamu kati ya Chaos na Roma, ufahamu wa Roma ulikuwa ni kama unaibukia ulikolala na kumfaya Chaos kuzidi kupambana lakini alionekana kushindwa vita.
“Wewe mwanaharamu nilijua tu huwezi kutii ahadi yako ulidanganya kwa kuniahidi kulinda wanawake wangu , lakini je unaona mimi ni mtoto mdogo mpaka kukuamini sio?”
Fahamu mbili zilikuwa zikishindana Roma alikuwa akiongea akionekana alikuwa na ngauvu zaidi ya fahamu ya Chaos.
“Huu uwezo wako umetokana na kuimarika kwa uungu wako!!?”Chaos hatimae alielewa nini kinacheondela , alichokuwa akipambana nacho sio
Roma bali ni uungu wa Hades ambao Roma aliurithi.
Lakini sasa kwa namna isioelezeka uungu huo ulionekana kuimarika sana kuliko ilivyokuwa mwanzo na hakutarajia hilo wala kugundua.
Roma alitoa tabasamu huku macho yake yakionyesha hali ya msisimko kuendelza vita hivyo ya kifahamu.
“Unaonaje, nadhani hukutegemea nilikuwa na mpango wangu kichwani , ijapokuwa umeweza kurejesha sehemu ya uwezo wako lakini Caulrdon imefungia kiini cha nafsi yako ndio maana unao uwezo wa kutumia mwili wangu lakini Roho yako halisi ya ndani kama sikosei haina nguvu ya kutosha kumeza nafsi yangu vinginevyo ungekuwa ushannimeza muda mrefu na usingeanza kunibembeleza bembeleza kukuruhusu kutumia mwili wangu”
Kauli hio ilifanya nafsi ya Roho ya Chaos kuchanganyikiwa na kuwa na hasira kwa wakati mmoja , ilikuwa ni kweli roho yake ilikuwa imefungiwa katika Cauldron na hakuna njia rahisi ya kutoka huko kutokana na vizuizi.
Kutokana na athari ya Chungu ilikuwa pia ni ngumu kupata uwezo wake wote na kukimbia au kujitoa na kitu pekee kupata nguvu zake ni kujiambatanisha katika nafsi ya Roma.
Kama nafsi yake halisi ilikuwa na nguvu zake za kutosha roho hio ingekuwa ishammeza Roma muda tu tena bila hata ya kumbembeleza mbeleza.
Sasa muda huo mara baada ya kuona Roma yupo kwenye majanga iliona hio ndio nafasi adhimu ya kumfanya Roma kumwachia mwili wake kihalali na kujikusanyia nguvu kwa haraka na kuizima Roho ya Roma moja kwa moja kumbe alikuwa akitegwa.
Nafsi hio iliamini haijalishi uwezo wa Roma upoje ili mradi Roma atatoa mwili wake kwa hiari yake hatokuwa na uwezo wa kulera ukinzani katika kurudisha nafsi yake , sasa yote hayo yalikuwa ni makisio tu na ilionekana mpango wake haukwenda kama alivyokuwa amepanga kutokana na kutokutegemea uwezo wa akili wa Roma ugekuwa na nguvu kubwa namna hio.
“Imekuwaje , imekuwaje utimamu wako wa akili ukaongezeka kiasi hicho?”Roho Chaos aliongea.
“Kitu pekee ambacho unaweza kuona katika akili yangu ni tabia yangu lakini huwezi kujua mawazo yangu ya ndani , siku chache zilizopita tokea kuanza kwa kufufuka kwa moyo wa Gaia uwezo wangu wa kiuungu wa akili umeongezeka kwa kiasi kikubwa mno , haikuwa kwangu tu hata kwa miungu uwezo wao wa akili pia ulikuwa ukiimarika , usingeweza kujua hili kwasababu mimi situmii kanuni za anga mara kwa mara hivyo ulishindwa kujua kama uwezo wangu wa akili umeongezeka au lah , kitendo cha kuanza kufufuliwa kwa moyo wa Gaia nafsi yangu iliimarika licha ya kwamba uwezo wangu wa
nishati za mbingu na ardhi ulibakia vilevile , hivi unadhani utimamu wangu wa akili unaweza kulingana na huo wa kwako dhaifu , ki ufupi ni kwamba nishakupita muda mrefu na hakuna namna unaweza kunifikia na ukatawala akili yangu labda nikuruhusu”
Maneno ya Roma yalishusha hali ya majigambo ya roho ya Chaos , haijalishi roho hio ilijitahidi vipi lakini haikuweza kufanikiwa hata kutingisha ufahamu wa Roma.
Ki ufupi ni kwamba Chaos aliingia kwenye mtego wa Roma kwa kuamini Roma wa kule Korea aliemeza moyo wa Kibudha ni huyo huyo mara baada ya moyo wa Gaia kuanza kufufuka.
“Hapana , siwezi kupoteza kwako kizembe hivi , hii sio sawa,, arghhh..”
Chaos alijikuta akipambana lakini ilikuwa haina maana tena kwasababu ufufuo wa Moyo wa Gaia ulikuwa ukiimarisha nafsi za miungu hii ni kwasabau nafsi zao zimeungana na Gaia.
Mpango wa Athena ulikuwa ni kufufua ndugu zake ambao nafsi zao zilimezwa na binadamu hivyo njia pekee ya kufanikisha hilo ni kufanya moyo wa Gaia kuwa na nguvu zaidi ambayo itawezesha zile Roho ambazo zilimezwa kuamka, sasa kwasababu na Roma alikuwa na uungu ndani yake moja kwa moja ni kwamba anakuwa na Koneksheni na moyo wa Gaia hivyo kadri moyo huo unavyofufuka ndio ambavyo uwezo wake wa akili pia huimarika.
“Nilishakuambia kwangu wewe huna tofauti na mbwa tu , unatoa wapi ujasiri wa kutaka kummiliki anaekufuga , nina madaraka kamili zidi yako na kitendo chako cha kuonyesha uwezo ambao ulikuwa umeficha muda si mrefu nitaweza kutawala Radi kama siraha , kama unataka kuendelea kula keki yangu basi hakikisha unaendelea kuwa mbwa mtiifu” “Binadamu fisadi sana wewe… hapana.. kafiri wewe”
Nguvu ya Chaos katika fahamu za Roma iliendelea kufifia na mwishowe ikapotea kabisa katika ufahamu wake na kurudi katika Cauldron.









SEHEMU YA 729.
Sasa mara baada ya Roma kuweza kumiliki mwili wake kikamilifu kwa kumfukuza Chaos katika ufahamu wake na kwenda kwenye Chungu macho yake yalirudi katika muonekano wa kawaida , ukiachana na damu ambazo zilikuwa zimemchafua lakini kila kitu kilikuwa sawa.
Kitendo cha Chaos kutumia mwili wa Roma ilimfanya kutoa uwezo wake wa kijini ambao alikuwa ameficha na hilo lilikuwa kosa kwake kwani Roma aliweza kumiliki uwezo huo , ukijumlisha na mapigo matatu ya awamu za radi alijihisi kujiamini maradufu zaidi na kuamini anao uwezo wa kuwashinda Anjiu na wengine.
Baada ya kumtoa Rufi kwenye Chungu na kumkumbaita palepale Roma alikificha, ki ufupi ni kwamba Roho ya mnyama huyo milele itakuwa chini ya Roma na kuwa kama mbwa tu wa kumsaidia kushambulia maadui.
Roma mara sasa baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha hatimae aligeuza macho yake na kumwangalia Rufi na kutoa tabasamu.
“Rufi wewe kilaza unalia nini sasa hebu kaone ? Si nipo sawa?”Aliongea Roma mara baada ya Rufi kuanza kulia kilio cha Kwikwi kama kafiwa vile.
“Hubby…nili ,,,nilijua umesha..”Mwili ulimsisimka kila akikumbuka tukio ambalo limetokea dakika kadha zilizopita.
“Nilikuambia pale kwamba ninabetia uwezo wa Cauldron na sio kwamba nilisema ninakipa mwili wangu , inamaana hukuniamini na ulijua nitamezwa?”
“Mimi ningejua vipi unachomaanisha … hukuniambia nikaelewa”
“Kaone sasa kalivyo kajinga … kama ningekuambia kila ninachowaza Chaos angenishtukia na mpango ungefeli”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kutoa kicheko kilichoambatana na aibu.
“Roho ya Chaos imeingia cha kike , Babe wewe ni mjanja sana unajua”
“Hehe sikuwa na jinsi muda ule , hawa majini walikuwa wamenipania si mchezo na kabla ya kuanza pambano nilijua ninaweza kuingia katika hatari hivyo niliiandaa ‘ escape plan’ mapema … nimefaidika sana hata hivyo kwasasa uwezo wangu umeongezeka maradufu na ninaweza kuwaua muda wowote nitakaotaka”Aliongea Roma huku akikumbuka Lahani na baba yake walivyotoroka lakini hata hivyo alikuwa ashaua majini zaidi ya wa nne wa levo za maji ya kiroho katika miliki hio.
Kama utafananisha na hasara waliopata kati ya Kekexil na Xia basi miliki ya Xia imepoteza zaidi majini wenye nguvu kuliko ilivyokuwa kwa Kekexil ambao walipoteza kwa kiasi kikubwa madawa hivyo hasara ni ya kawadai kwani ni rahisi kutafuta madawa na vidonge kuliko kupandisha uwezo wa kijini.
Rufi sasa alipatwa na msisimko na furaha mara baada ya kutoka katika hali ya hatari.
“Hubby kwahio muda si mrefu utakuwa na uwezo wa kudhibiti Radi , nadhani kwa msaada wa Cauldron haitokuwa ngumu kupita dhiki ya radi ya mapigo mengi , ukijumlisha na utimamu wako wa mwili kila kitu kinafaida kwako”
“Upo sahihi kwasasa nguvu zangu ni za kutosha na busara pia zimeimarika lakini bado nitahitajika kuwa na muda sahihi kabla ya kupita , nataka kupata fursa ya kuelewa kanuni za mbingu zinavyofanya kazi , ni kama Anjiu tu ambaye alisubiri muda mrefu ili kuja kuelewa fumbo la kaunni za mbingu
zilivyo”Aliongea Roma na Rufi alitingisha kichwa na furaha ilikuwa imemtawala na alishindwa kuyazuia mahaba yake na kumkumbaita Roma na kumbusu shavuni licha ya kwamba alikuwa amechafuka na damu.
“Hey embu acha kunibusu huoni namna ambavyo Chaos amechafua mwili wangu , Babe Rufi ninafuraha hatujapata majeraha na pia tumeweza kupata faida kubwa , nitakupeleka sasa visiwani , nikishakamilisha maswala yangu huko duniani nitarudi tena na kuwaua wote”
Rufi alitingisha kichwa kwa mchecheto huku akiwa na hamu kubwa ya kukutana na mlezi wake Sui.
Roma bila ya kuchelewa alimshikilia vizuri na kumuwekewa kinga ili aweze kupumua na kisha alianza safari ya kuelekea kusini magharibi, ilikuwa ndio ulelekeo ambao Anjiu alikimbilia lakini Roma hakuwa na mpango wa kumfukuzia tena, mpango wake ilikuwa ni kurudi Visiwa vya wafu mapema kadri iwezekanavyo kwani misheni ya kumuokoa Rufi ilikuwa imekamilika.
Wakiwa njiani Roma alimuuliza Rufi namna ambavyo alilelewa kwani aliletwa katika ulimwengu huo akiwa mdogo sana na ilionekana Rufi aliweza kuwa mkubwa kutokana na kunyonyshwa maziwa ya kopo ambayo yalitokea katika ulimwengu wa kawaida.
Ukweli ni kwmaba majini kwao hawakuwa wakipika chakula kama binadamu kwao wale wasile haina madhara kwao vyakula vyao vimekaa kama madawa madawa , wanatafuna mizizi na majani si mchezo.
Hatimae bila ya kukutana na jini mwingine njiani waliweza kufanikiwa na kutokea katika ulimwengu wa kawaida kupitia baharini.
Baada ya safari ndefu ya nusu dunia hatimae waliweza kufika Mediterranian muda wa jioni kabla ya machweo na kukaribishwa na upepo wa bahari.
Uwezo wa utambuzi wa Roma ulikuwa mkubwa mno hivyo aliweza kuchunguza eneo ambalo Sui alipo na ndani ya muda tu aliweza kugundua Sui yupo na Bi Wema na wengine wamekaa nje ya kijumba kilchotengenezwa kwa miti pembezoni mwa fukwe mita kadhaa kutoka ngome ilip.
Roma kabla ya kufika katika visiwa hivyo alikuwa ashabadili mavazi na kujisafisha kabisa ili asije kutisha watu hivyo moja kwa moja alienda mpaka walipo.
Ilikuwa ni nyumba ya miti ambayo ilikuwa ikitumiwa na Ron kwa mapumziko na ndani yake alikuwa sio Bi Wema tu walikuwepo Neema Luwazo , Nasra na Doris.
Wakati huo huo Edna na Lanlan walikuwa wakicheza kwenye bembea katika bustani ambayo imezungukwa na maua ya kuvutia katika eneo hilohilo.
Ijapokuwa Lanlan alikuwa na uwezo wakuharibbu bembea hio ya chuma kwa uwezo wake lakini alijitahidi kujifanyisha mtoto wa kawaida.
Mara baada ya Roma kutua kutoka angani akiwa na Rufi kila mmoja aligeuza shingo yake na kuwaangalia kwa mshituko na furaha pamoja na shukrani ya kuona wote walikuwa wazima wa afya.
“Hubby !, Rufiii..!!!””Nasra ndio aliekuwa wa kwanza kutoka kwenye mshituko na kupiga kelele za shangwe.
“Omg,,, naona mnatufanyia surprise si mtoe hata taarifa jamani kabla ya kuja”Aliongea Neema kwa utani.
Lanlan ambaye hakuwa mbali na eneo hilo alitoka kwenye bembea na kutimua mbio kwenda kumlaki baba yake, huku Edna ambaye bado alikuwa amekalia bembea aliishia kutoa tabasamu hafifu huku akitingisha kichwa chake kwa namna ya kusikitika kutokana na spidi ya Lanlan.
Bi Wema upande wake palepale aliangua kilio mara baada ya kuwaona na mara baada ya kujihakikisha hakuwa akiota alikimbia na kwenda kumkumbatia Rufi.
“Mwanangnu …. jamani binti yangu mimi…. umejua kunitia wasiwasi”Rufi alianza kuchunguzwa kwanzia nywele mpaka vidole ili kuona kama kuna sehemu iliokuwa na jeraha.
Laiti angemuona Rufi na yale makovu pengine angepoteza fahamu hapo hapo na ilikuwa afahdali Roma alikuwa amechukua hatua ya kumponyesha kabla ya kumrudisha.
Rufi aliishia kumkumbatia mama yake huku machozi yakimtoka na aliishia kuangaliana na Sui na wote kwa pamoja waliishia kutokwa na machozi na aliishia kuita jina la mlezi wake’ nanny’ ijapokuwa alitaja kwa sauti ya chini lakini Sui alisihindwa kujizuia na yeye kwenda kuungana nao katika kukumbatiana.
Onesho la wanawake watatu wakiwa wamekumbatiana huku wakilia ilimfanya Roma kuguswa , ilikua hivyo lakini kwa namna moja alihisi kutojisikia vizuri na aliishia kukumbaitia na Lanlan na kisha alimwangalia Edna wa kwanza na kumpa tabasamu la ushindi na kisha akageuza macho yake kwa wengine na kuwapa ishara zinazofanana.
“Hehe… mnaonaje ushujaa wa mume wenu katika misheni za ki uokozi”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu la kihuni huku akiangaliwa na warembo wake.
Hakuna ambaye alikwepesha macho na wote walikuwa na sura za kutaka kujua kile kilichojiri katika ulimwengu huo wa majini.
“Punguzeni munkari …. nitawaambia stori yote baadae, ukiachana na hivyo huyu mzee Ron yuko wapi?”Aliongea Roma na dakika ileile aliweza kuhisi uwepo wa Ron kwenye msitu uliokuwa nyuma ya kibanda hicho.
“Wewe Ron hebu leta uzee wako hapa”
Kiongozi wa kundi la kimafia Ron alikuwa bize kupunua bustani yake ya miti na mua kwenye msitu huo na mara baada ya kusikia sauti ya Roma aliacha kila alichokuwa akifanya na kukimbia.
“You have returned , your Majesty Pluto”Aliongea Ron huku akitoa tabasamu la kiaina hivi , alikuwa amevalia mavazi ya kishamba na kofia aina ya hat huku akiwa ameshikilia koleo.
“Una maagizo yoyote mfalme?”
“Mzee hayo mavazi naona yamekupendeza sana… ninataka kusherehekea kuungana kwa Rufi , Bi Wema na Sui , nataka uandae mvinyo mzuri kutoka kwenye Cellar”
“Does the 1982 Margarita sound good, Your majesty Pluto?”Aliuliza Ron.
“Ndio itafaa , kwanza sijui ni mvinyo upi umebakia kule chini lakini nikipata chupa kadhaa za aina hio itakuwa bomba”Aliongea Roma na Ron alitingisha kichwa lakini Edna alimkodolea macho Roma .
“Ron ni mbunifu wa kimataifa lakini pia mzee wa kuheshimika kwanini unamfanya kama vile ni kijakazi wako , huo ni ukorofi huoni Lanlan anakuangalia?”
“Ohoo.. Wife hapo sasa ndio unakosea , kama nitakuwa mpole mbele ya hawa watu wataona labda napanga kuwaua lakini nikiwa mkorofi mbele yao kwao ndio wananiona mkarimu”Aliongea Roma huku akicheka na kumfinya Lanlan shavu lake , alijisikia amani sana mara baada ya kurudi nyumbani.
Bi Wema, Rufi na Sui hatimae walipoa na kisha kurudi na kukaa kwenye banda hilo la mapumziko
Sui na Bi Wema walitaka hata kumpigia Roma magoti kuonyesha shukrani zao lakini Roma aliwazuia na palepale alimshusha Lanlan chini.
“Kwanini ndio nyie tu , Yezi , Rose na wengine wapo wapi?”
“Hao wadada wameenda mbali kule kisiwani kwa ajili ya kuendelea kujifunza kwani hawakutaka kusumbua watu wakati wakipambana wao kwa wao”Alijibu Dorisi.
“Mage na Yezi pia wameenda? , unamaanisha washaingia..”
“Ndio wamefanikiwa .. Mage aliingia levo ya nafsi masaa kadhaa baada ya wewe kuondoka , sijajua nini lilikuwa tatizo lake lakini kitendo cha Amina kufanikiwa ilimfanya kuwa na wasiwasi lakini wasiwasi huo ndiio uliomsaidia kuingia levo ya nasi , kwa Yezi inaonekana ana kipaji na alifuatia mara baada ya Mage na sasa wanalingana”Aliongea Neema.
Roma alishangaa na hakutegemea kama Yezi ambaye alianza kwa kuchelewa kuweza kufikia levo ya nafsi ndani ya muda mfupi hivyo.
Ijapokuwa walikuwa wakitumia vidonge lakini kupata uelewa na ufumbuzi ilikuwa ni kitu kingine kabisa.
Inaonekana maisha ambayo Yezi amekulia ndio ambayo yamempa uzoefu ambao umemsaidia kupata ufunuo kwa haraka..
Ni Edna , Dorisi , Neema , Nasra na Najma ndio ambao hawakuwa wamefikia levo ya nafsi ,Rufi yeye hakuwa akihesabika kwani hakuwa na uwezo wa kujifunza.
“Wenzenu wamefanikiwa kupita nyie hamna wasiwasi?”
“Ndio tulichokuwa tukijadiliana hapa , na kujiuliza au ni kwasababu ya umri , wenye umri mdogo wanaonekana kupanda levo kwa haraka kuliko sisi ambao umri umeenda kidogo”Aliongea Dorisi na kumfanya Roma kutoa tabasamu na kumwagalia Edna.
“Honey , huoni kuna kitu hakipo sawa katika maneno ya Dorisi , ninachojua unalingana na Mage na Magdalena au nimekosea?”
Upande mwingine Edna hakuonyesha wasiwasi na alikuwa na muonekano wa maringo na alichukua juisi yake ya matunda nakunywa kidogo na kisha akamwnagalia Roma.
“Sina haraka”
Jibu hilo la kawaida lilimfanya Roma kukosa usemi lakini hata hivyo aliishia kutoa tabsamu bila ya kuongea chochote.
“Ukiachana na hayo , Hubby, Mage akirudi hebu angalia ufunuo ambao amepata ni wa ajabu mno”
“Kwanini ni wa ajabu?”
Muda huo wakati wakiongea ndio Ron aliweza kufika akiwa na chupa za mvinyo mwekundu wa Margarita , mvinyo huo gharama yake haina kiwango maalumu sokoni , Margarita ya kawaida ambayo haijazeeshwa kwa muda mrefu inagharimu zaidi ya dola elfu moja sasa hizo ambazo zina umri mkubwa thamani yake ilikuwa ngumu kueleweka.
Lakini Roma kutokana na kuwa na koneksheni dunia nzima marafiki zake walimletea kama zawadi na aliishia kuzihifadhi katika chumba cha ardhi katika Cellar.
Roma mara baada ya kufungua chupa baadhi alimwambia Ron kubakia hapo na kuungana nao kwani alikuwa na maswali anataka kumuuliza lakini pia ilikuwa siku nzuri kwa Roma.
Roma alikuwa na hamu kubwa ya kuwasubiria Rose kurudi pia.
Harufu nzuri ya mvinyo huo iligusa pua za warembo huo na Edna ndio aliekuwa wa kwanza kuomba na yeye apatiwe lakini sasa mara baada ya kuonja aliitema chini akisema mvinyo huo mwekundu ulikuwa hata ukizidiwa utamu na maziwa na juisi ya matnda.
Muda huo huo Roma pia alianza kuelezea kile ambacho kilitokea katika ulimwengu wa majini watu na namna ambavyo Rufi alitoa ushirikiano kwa kutokuwa na hofu kubwa katika kupitia hali hio ya kuogofya.
Mara baada ya kuona Roma alikuwa amepanda zaidi kilevo walishangaa na kuwa na furaha kwa ajili yake.
Kwa upande wa Roma alijua kabisa bado hakuwa juu zaidi ya sehemu ambayo anataka , bado hakuwa na uwezo wa kupambana na jini yule ambaye alikutana nae Dodoma yaani Master namba moja.
Ron hakuelewa chocho te ambacho walikuwa wakiongea kwani kiswahili ndio kilichokuwa kikitumika zaidi na kingereza mara chache.
“Mfalme Pluto , kwasababu ndio umerudi nina taarifa ya kukupatia”Aliongea Ron mara baada ya maongezi kukauka.
“Oh , ni taarifa gani hio?”
“Ni kuhusu Princess Clark , amepanga kugeuza makazi yake hapa kisiwani kuwa maabara , tayari ashasafirisha vifaa vya kimaabara kuja na baadhi ya nyaraka na malighafi kutoka London, muda ambao vitu hivyo vinakaridiwa kufika ni usiku na atafika wakati huo”
“Yale ni makazi yake hivyo muache afanye anachotaka , pia inamuokolea muda kwenda na kurudi kwa ajili ya majaribio ana ukichaa na maswala ya kitafiti ni kama vile hawezi ishi bila ya kuwa na maabara”Aliongea Roma akiwa hana mshangao.
Tokea siku ambayo Roma aliweza kupatiwa hatimiliki ya visiwa hivyo Catherine na Clark walikuwa wakipenda sana kuja kutembelea na walikuwa na ardhi yao kabisa na ilikuwa kubwa mno saizi ya kisiwa na walijenga majengo kama hoteli kwa ajili ya mapumziko.
Zamani Clark alikuwa akija kisiwani hapo mara chache sana lakini furaha ya kuja kisiwani hapo kuungana na wavuna nishati wenzake ilikuwa kubwa ndio maana alitaka kufanya makazi yake kuwa katika eneo hilo ili kuwa rahisi kuendeleza kazi yake na kupata uzoefu katika mafunzo kwa kupambana na wenzake.
Lisaa limoja mbele hatimae wanawake waliokuwa na muonekano wa kimaringo waliweza kufika kutokea kusini , alikuwa ni Rose na wengine na mara baada ya kumuona Roma na Rufi iliwafanya kuwa na furaha isiokuwa na kifani , awamu nyingine ya vicheko na maelezo ilihitajika.
Roma kwa kuwachunguza Rose , Magdalena na Amina walikuwa washaanza kuingia katika mwisho mwa levo ya nafsi , uwezo wa Amina ulikuwa umeongezeka kwa spidi kubwa nje ya matarajio na kuwakaribia Rose na Magdalena na kitu kingine kilichomfanya Roma kushangazwa na Amina kiini cha macho yake ni kama kimebalika na kuwa na ukijani ndani yake na alikuwa akikumbuka aina ya macho hayo kuna mahali aliyaona ila hakuwa akikumbuka vizuri.
Upande wa Yezi na Magdalena walikuwa wamepiga hatua na Roma alijua kutokana na uwepo wa vidonge basi muda si mrefu watafikia mwishoni mwa levo hio.
“Babe otea nilichoweza kufanikisha?”Mage hakutaka hata kuulizwa na alikuwa na hamu ya kumuonyesha Roma.
“Nitajuaje sasa wakati kila mmoja anasema ni kitu cha kushangaza?”


















SEHEMU YA 730.
Mage alikuwa na hamu ya kumuonyesha Roma ufunuo ambao amepata kwa kugeuza nguvu za mbingu na ardhi na kuwa siraha na ndani ya sekunde tu aliweza kubadilisha nguvu zile na kutengeneza moto mweupe kama wingu kwenye mkono wake.
Roma alishangazwa na kitu kile na hakujua moto ule ni wa aina gani kwani hakuwahi kuuona.
“Huo utakuwa ni moto wa maajabu!!”Aliongea Roma aliekuwa katika hali ya mshangao.
“Hubby kumbe unaujua ?, Aunt Sui amesema inawezekana ikawa ni Heart flame sehemu ya moto wa kimaajabu”
“Heart flame!!!?”
Roma alishangazwa na kauli ile na kugeuza macho yake kwa Sui na palepale alielezea.
Heart flame maana yake moto wa moyo , ilikuwa ni kweli ni sehemu ya moto wa kimaajabu , ambao mara nyingi huweza kutengenezwa kwa kugeuza nguvu za mbingu na ardhi na majini ambao wana hasira za haraka, sasa kutokana na tabia zao zilivyo majini wa namna hio hawanaga muda wa kukaa chini na kuvuna nishati hivyo moto wa namna hio kuona unatumika kama siraha ni mara chache sana.
Isitoshe hata hivyo kuwa na hasira za haraka haitoshi kugeuza nishati za mbingu na ardhi kwenda kuwa moto huo bali lazima kwanza mtu kuwa na moyo wa barafu ikimaanisha kwamba tofauti na kuwa na hasira za haraka lazima uwe na kiasi walau kidogo katika kutuliza hasria zako.
Sasa Afande Mage tabia yake ilikuwa ikijulikana kabisa , alikuwa ni mwanamke ambaye ana hasira za karibu na ni hasira hizo hizo ambazo zilimkutanisha na Roma. Hivyo kutokana na tabia yake hio alijikuta akibatatika kupata moto wa namna hio.
Roma alimwambia Mage kujaribu kumshambulia na huo moto na alikuja kugundua sio moto ambao ulikuwa ukiunguza bali ni moto ambao ulikuwa ukifanya akili yako kupatwa na ukichaa ni kama vile shambulizi la kichawi hivi.
Ilikuwa ni kwasababu uwezo wa Roma ulikuwa juu sana ndio maana athari zake zilikuwa kidogo lakini kama Mage atakutana na mshindani ambaye ni wa levo yake akigusana na huo moto kuna uwezekano wa kumfanya kuwa kichaa.
Upande wa yezi licha ya kuingai levo ya nafsi lakini bado ufunuo wa kisiraha hajapata bado, lakini hata hivyo haikuwa na maana kwamba kila ukiingia katika levo ya nafsi ndio moja kwa moja unapata ufunuo wa kisiraha.
“Hii ni kwa ajili yako , upanga wa daraja la kati huu,
ninaona unakufaa sana hivyo usiwe na huzuni”aliongea Roma akimkabidhi Yezi upanga kwasababu bado hakuwa na uwezo wa kisiraha.
Wote walijikuta wakishangazwa na uzuri wa upanga huo ambao katikati ulikuwa umeandikwa jina la Manjushage.
“Manjushage? Hii ni Dhana ya daraja la kati ambayo ni maarufu ndani ya ulimwengu wa kijini , hubby umeipata mara baada ya kuua jini wa miliki ya Xia?”Aliuliza Rufi.
“Ndio nimeaua majini wengi na kuangalia siraha zao lakini ni huu upanga tu ambao mashambulizi yake yamenifurahisha na nimeona unafaa kabisa kutumiwa na Yezi , kwanini unasema ni maarufu sana?”
“Hii ni Dhana ambayo ni mbili kwa moja kadri uwezo wako unavyoongezeka neno manjushage linagawanyika mara mbili na kuwa Manju na Shage, ukishajigawanya mmoja unaweza kutumia kama siraha ya mashambulizi na nyingine unaweza kutumia kama kinga, faida nyingine ni kwamba ukitumia unakuongezea spidi wenywe katika mshambulizi , kama una msingi mzuri wa mashambulizi ya upanga basi inageuka kuwa Dhana ya hatari sana ambayo inaweza kuua hata jini wa nafasi ya maji ya barafu, lakini kama uwezo wako ni wa chini basi inaweza kutokuwa na maana kubwa na inaweza kuwa hatari kwani wenyewe unanyonya nguvu za kijin”
Licha ya Yezi kutokuwa na msingi mzuri wa kutumia panga lakini hakutaka kupokonywa na alificha upanga wake..
“Haijalishi ili mradi nimepewa basi ni zawadi yangu , nitajifunza namna ya kutumia na naahidi kutoitumia kabla sijaelewa namna ya kuitumia”
Uzuri wa upanga huo wa kioo ulimfanya Amina kuwa na wivu na kumwangalia Roma kwa macho ya kurembua na kutia huruma.
“Hubby kwanini unakuwa na upendeleo kwa kumpa
Yezi zawadi peke yake?”
“Sister Amina aisee huna aibu na umri wako huo bado tu unafanya hivyo?”Aliongea Yezi na kumfanya Amina kuona aibu na kujiweka sawa
Roma mara baada ya kuona kila mmoja alitegemea zawadi aliamua kutoa kila Dhana aliopata , Magdalena alipatiwa ule mkanda wa ngurumo radi , upande wa Rose alipewa siraha ya Sanyua na Mage akapewa kisu cha mfupa wa Dragon.
Kila mmoja alipata Dhana kasoro Edna tu ambaye yeye alikuwa na bangiri kwenye mkono wake.
Ukweli ni kwamba licha ya Roma kuwa na uwezo mkubwa sana wa nguvu za kijini lakini mpaka wakati huo alishindwa kujua nguvu halisi ya bangiri hio ambayo amevaa Edna ikoje.
Kwa namna moja ama nyingine ni kama bangiri hio ilikuwa na muunganiko wa moja kwa moja na mvaaji.
Roma hakumsahau kipenzi chake Lanlan pia kwani na yeye alimpa siuraha za daraja la chini kwa ajili ya kuchezea.
Ikiwa giza limeingia kabisa hatimae Roma alihisi ongezeko la mtu mwenye uwezo wa nafsi na alipotumia uwezo wake wa utambuzi alikuja kugundua ni Clark
Kwasababu hawakuwa na chakufanya Roma na warembo wake walianza kutemba kandokando ya fukwe hio na ndio wakati ambao waliweza kuona meli kubwa ya mizigo ya Uingereza iliokuwa na chata la ‘British Royal Cargo’ ikielea taratibu kuelekea kwenye gati.
Ilikuwa na bendera ya jumba la kifalme la Wales kama utambulisho ambayo ilikuwa ikipeperushwa na upepo.
Ni kama nusu saa mbele wanajeshi wa jeshi la majini wa Uingereza ambao wamevalia kombati za kijeshi walionekana kuwa bize kushusha maboksi kadhaa na baadae makontena na kupandishwa kwenye gari na kunza kusafirisha kuelekea makazi ya Clark , sehemu ambayo ndio anapanga kufungua rasmi maabara ya ki utafiti.
Dakika chache mbele helicopter ilionekana kushuka tataribu upande wa mbali kidogo na kushusha baadhi ya watu.
Alionekana mwanamke alievalia shati la kola lenye vifungo kutoka chini mpaka juu ambalo limemkaa vizuri rangi nyeupe , huku akiwa na suruali yenye michirizi miwili ya rangi nyeupe pande zote , nywele zake za kahawia ziliuwa zimechanguka kutokana na upepo uliokuwa ukizipeprusha, ni umaridadi na hadhi ya utukufu ndio vilionekana kutoka kwake..
Clark alitembea kwa kuwasogelea Roma akiwa na tabasamu huku nyuma yake akifatiwa na wanawake wawili wote wakiwa ni wazungu , mmoja alikuwa na muonekano wa kitajiri na mwingine alikuwa ni mwenye wasiwasi na kutokuwa na hali ya kujiamini kidogo.
Mwanamke mrembo mwenye muonekano wa ki utu uzima alikuwa akifanana na Clark kwa vitu vingi , alikuwa ni Catherine mama yake , alikuwa ni ‘hot’ na ‘sexy’ hususani na mavazi yake aliokuwa amevalia.
“Oh my , Clark walk slower , wait fo mama..”
Catherine alikuwa akimpigia makelele Clark akimwambia atembee taratibu lakini Clark ni kama vile hajamsikia na alitembea kuelekea kwenye kundi la watu waliokuwa mbele yake.
Edna na Roma pamoja na wengine wote walisalimiana na Clark huku Roma akimkumbatia kawaida.
“Mama yako anafanya nini hapa?”Aliuliza Roma huku akiwa na wasiwasi kidogo na muonekano wa Catherine.
“Alikuwa akijua mara baada ya kuanza harakati za kuhamisha vitu vyangu na alilazimisha kuja na mimi huku kwa kuogopa namkimbia na kumuacha mwenyewe”
Roma aliishia kutingisha kichwa kwa maneno hayo, yalienda sawa na haiba ya Catherine.
Muda huo huo mara baada ya Catherine kumfikia Roma alishindwa kuzuia furaha yake na kumsogelea akiwa amchanua mikono yake na kumkumbatia.
“Oh my Dear Roma Ramoni , it has been a while don’t you mis me? Mwaaaahh.”
Catherine alimpiga busu shavuni kiasi cha kuacha alama na muda huo Roma alijihisi ubaridi mgongoni na kuishia kugeuka na kuangalia warembo wake ambao walikuwa wakimwangalia kwa macho ya kutisha.
Roma alijihisi kuogopa ,ijapokuwa mabusu hayo kwa wazungu ni kitu cha kawaida na yeye na Catherine ni marafiki lakini ukweli ni kwamba urafiki wao ni wa faida kwani walikuwa wakinyanduana.
Isitoshe kwa wakati huo Clark alikuwa tayari ni mpenzi wake hivyo ni kama Roma anakula kuku na mayai yake.
“Hello , your majesty Pluto”
Sauti ya wasiwasi ilitoka kwa mwanadada ambaye alikuwa ameongozana nao.
Roma alikuwa bize wakati huo na hakuwa amesalimiana nae na palepale alimkumbuka na kutoa tabasamu.
“You must be Grace , the student Clark
Accepted?”Aliuliza Roma akimaanisha kwamba huyo atakuwa ni Grace mwanafunzi ambaye alikubaliwa na Clark.
“Ndio Mfalme Pluto bado unanikumbuka?”
“Bila shaka , ndio ulieokoa maisha ya Rufi lazima nikukumbuke”Aliongea Roma na kisha alisalimiana nae kwa kumpatia mkono,
“Ni Profesa ndio ambaye alimponya Rufi mimi nilifanya wajibu wangu tu”
Wanawake hao hawakuelewa kwanini maongezi yako hivyo lakini Clark aliwaelezea kile kilichomkuta Rufi kule kwenye msitu wa Australia mpaka kumpeleka hospitali ya London kwa ajili ya matibabu na Grace akaonyesha ujasiri wa kutaka kumsaidia Rufi licha ya kuwa nesi asiwe na cheo chochote.
“Kwanini umekuja nae?”Aliuliza Roma mara baada ya kuona Grace alikuwa akijua jina kamili la Roma.
“Ni mwepesi kujifunza na ana kipaji , na zaidi ya yote ana mtazamo chanya na mkarimu , nadhani kipaji chake kilikuwa kimejificha tu kutokana na mazingira pamoja na kutopata elimu sahihi , nipo katika hatua za kumfunza ili kuwa msaidizi wangu namba moja ili baadae aje kutidhi tafiti zangu , hivyo nimekuja nae kwa ajili ya kuona mahali ambapo masomo yake yataanzia”
Grace aliishia kuona aibu huku akifurahia kwa wakati mmoja namna bosi wake anavyomsifia.
Roma aliishia kumchokoza Clark kwa kumgonga kwenye paji la uso, ilikuwa ni Roma na Catherine tu ambao walikuwa wakiruhusiwa kumfanyia hivyo Clark kutokana na cheo chake cha uprincess.
“Hivi tayari ndio ushazeeka mpaka kutaka mrithi , jifanyishe mbele ya wanafunzi wengine lakini sio mble yangu ,… haya waachieni wanajeshi hio mizigo na tutarudi ngomeni kwa ajili ya chakula cha usiku .. oh ?yeah Grace na wewe ungana na sisi”Aliongea Roma akiona amkaribishe na Clark aliishia kutabasamu akimwangalia namna Grace ambavyo alikuwa na wasiwasi.
Kwa kutembea wote walirudi ngomeni huku stori zikiendelea kimakundi makundi na ziliendelea hata wakati wa chakula cha usiku na ilikuwa ni lugha ya kisawahi na kingereza ndio iliokuwa ikisikika hapo ndani ,
Roma alimuuliza Clark kama alikuwa na uhitaji wa Dhana lakini alikataa na sababu ni kwamba Dhana hizo aliona ni dhaifu sana.
Upande wa Catherine alitaka na yeye vidonge vya kuendeleza urembo wake na Roma alimpatia mpaka mbinu za kufanya ili kuendelea kudumisha ujana wake asizeeke haraka na kuhusu kufanikiwa Roma hakutaka kujisumbua sana.
Ki ufupi kila mmoja alionekana kuwa na furaha ndani ya eneo hilo , upande wa Lanlan Roma Ramoni alikuwa amekaa kwenye kiti chake maalumu cha kitoto akiendelea kufurahia nyama yake.
“Hubby unapanga kukaa hapa kwa muda gani , nimesikia kutoka kwa Rufi unapanga kurudi kwenda kuua wanafamilia wa miliki ya Xia?”Aliuliza Afande Mage huku akioneysha hali ya msisimko sana na kumfanya Roma atabasamu kwani ni kama vile anajua anachofikiria.
“Mage najua unachofikiria lakini lazima nikuambie ijapokuwa unamiliki moto huo wa kimaajabu lakini uwezo wako upo chini , Anjiu yule mshenzi anao uwezo wakuua watu wa levo yako elfu moja kwa shambulizi moja tu la moto wake wa ndege wa Dhahabu, hivyo usifikirie kabisa mimi kukupeleka”
“Acha hizo basi , wewe si utakuwepo na utatulinda ?”Mage alibembeleza , kwa haiba ya Mage kwake ilikuwa ni mateso kuvuna nishati bila ya kupambana katika mapigao ya uhalisia , alikuwa ni polisi
mpenda haki na alikuwa na hamu ya kuua jini hata moja ambaye amemsababishia Rufi mateso.
“Mage inatosha bwana ukienda nae utamuongezea tu mzigo , atakuwa mwepesi akiwa peke yake lakini na sisi itakuwa ni udhaifu kwake”Aliongea Magdalena.
“Dada unaongea kama vile hutaki kwenda , mimi shauku yangu ni kuona ulimwengu wa majini ulivyo tu”
“Hakuna kikubwa cha kushangaza , ulimwengu wa majini ni ardhi ya kimisitu na barafu tu kama Antarctica pamoja na nyumba za kimaajabu ajabu”Aliongea Roma huku akicheka.
“Kwahio ukirudi huko kumuua baba na mtoto si itakuwa kazi rahisi?”Aliuliza Rose,
“Nataka kwanza kuacha kufikiria kuhusu hili na kufanya mazingatio mengi lakini kwasababu nina uhakika ninao uwezo wa kuwaua sina haraka , ninachotaka ni kupata uwezo wa juu zaidi kupitia uzoefu wa kule hasa katika kudhibiti radi , pia natamani wao ndio waje huku niwapigie huku huku na kujaribisha na kanuni za anga lakini sidhani kama watakuja kutokana na hofu ya kukutana na miungu , ila kwa siku hizi chache kwanza nataka kukaa na nyie huku nikiangalia ukuaji wa Lanlan, sio kwamba napenda sana kuua majini ila nafanya yote kwa ajili ya maisha yetu kuwa salama yasiokuwa na misuko suko”
Kila mmoja alikuwa kimya wakati Roma akiongea na walimwangalia Roma kwa macho ya shukrani.
“Kama sio wewe vile wa kuongea maneno ya namna hio ukiwa na muonekano wa usiriasi hivyo?”
Edna ambaye alikuwa pembeni ya Roma aliongea huku akimwangalia Roma kwa macho ya kuibia ibia.
“Haha … mwanaume ambaye amekwisha oa mara nyingi hupevuka haraka , tumeona kwa miaka inaenda mitatu sasa na yote hayo ni kutokana na juhudi zako boss wangu”
“Acha kuwa chawa basi”Aliongea huku akimzodoa kichwa chake kwenda pembeni na kumfanya Roma kucheka.
“Nataka kusubiri subiri pia kwani Kule Bagamoyo nimemuacha Tannya ambaye anejifanyisha kuwa Maimuna , nataka nipate taarifa ya nguvu ambayo ipo nyuma ya familia ya Sharif kuchukua hatua, hilo ni jambo ambalo napaswa kushughulika nalo pia , ukiachana na hayo nasubiria uwezo wenu kuwa mkubwa ili niwe na amani hata kama hao washenzi wakitoka huko na kuvamia muweze kudili nao”
“Unaongea kama vile upo vizuri sanaa na hatuwezi kupambana pia lakini jua kama kitu kibaya kitakupata na sisi tutapotea hivyo uelewe kwamba katika hili haupo peke yako”Aliongea Nasra.
Maneno yake yalipeleka wimbi la usiriasi katia sura za wanawake hao na kuanzia muda huo walijua wanapaswa kujiandaa kwa lolote lile baya ambalo linaweza kutokea.
Malkia Catherine kutokana na usriasi wa maongezi hayo alishindwa kuvumilia na akaweza uma na vijiko vyake chini.
“I say since Roma has returned and everyone is here , staying on the island may be too monotonous ,what about going to London to see a football game? Its all on me”
(“Nasema kwasababu Roma amesharudi na kila mmoja yupo hapa , kuendelea kubakia hapa kisiwani kunakuwa kunachosha sana vipi kama tukienda London kuangalia mechi ya mpira miguu , gharama zitakuwa juu yangu”
Alishauri Catherine na mtu wa kwanza kukunja sura alikuwa Clark kama vile hajaridhika na pendekezo hilo.
“Mama kwanini mpira ghafla hivyo na tangu lini tukapenda maswala ya mipira sisi?”
“Hicho sio nilichomaanisha , Clark unachojua ni utafiti tu na hujali nini kinatokea katika mazingira ya kukuzunguka tarehe nane ya mwezi ujao fainali ya UEFA Champion leagued inaenda kuchezwa katika uwanja wa Wembley”.
“Kama ni UEFA inahusiana nini na sisi?”
“Bila shaka lina wahusu , nadhani hamjapata taarifa Sophia msanii kutoka Tanzania amealikwa kutumbuiza, hivi unajua ni wasanii wangapi wameweza kupata nafasi ya kutumbuiza laivu katika mashindano makubwa kama hayo , hii ni mara ya kwanza kwa msani chipukizi kupewa nafasi hio “Kila mmoja alishangazwa na habari hizo kwani hakuna aliekuwa akijua.
“Pumbavu kabisa yaani Sophia ameshindwa kuniambia kuhusu hili , ni hatua kubwa mno amepiga halafu kutoka hapa kwenda Uingereza sio mbali”
“Wewe kama mwenyekiti wa Multinational Campany
unafikiri unao muda wa kujisumbua na kinachoendelea ndani ya kijikampuni kidogo cha habari na utamaduni? Nina uhakika Sophia yupo bize kujiandaa na kakosa muda wa kukupa taarifa”Aliongea Roma kwa kutania.
Kutokana na ukaribu uliopo kati ya hapo na Uingereza kila mmoja aliona hakuna haja ya kukataa kutokwenda kuona mechi hio isitoshe hata kama hawapendi mpira wachukulie kama kitendo cha kumsapoti Sophia.
Kutokana na kurudi kwa Roma hawakuona haja ya kuwa na wasiwasi na waliona kwasababu pesa wanayo sio mbaya kama watembelee taifa hilo kwenda kujifanyia manunuzi na kushangaa shangaa staarabu zingine.
*****
Upande mwingine katika ulimwengu wa majini katika miliki ya Panas kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea , Gefu hakuonyesha kuwa katika hali nzuri katika kusikia ripoti iliowafikia kutoka kwa shushu ambaye yupo ndani ya miliki ya Xia,
“Okey inatosha”Aliongea kwa kuonyesha ishara ya mkono na yule shushu alitoka katika chumba hicho cha mikutano.
Baada ya kutoka Gefu aligeuza macho yake na kuangalia ndugu zake na wazee wa ukoo huku akiweka tabasamu la uchungu usoni mwake.
“Huyu Roma Ramoni hakika ni binadamu mwenye bahati sana , ameweza kupona”
“Cha kuogopesha ni kwamba kama alichosema
Shushu ni sahihi basi hata Anjiu na Senji pamoja na wazee wengine waliopo levo ya maji ya kiroho ni kwamba wamemshindwa na kusambaratika kwa kukimbia , hili linamaanisha vitu viwili mosi Roma anaweza akawa tayari ashapitia mapigo zaidi ya mia moja…..”Aliongea Gefu.
“God damn it… huyu nwanaharamu imewezekanaje akawa na uwezo mkubwa hivi kuliko hata sisi majini wenyewe hakuwa ni wa kutsha sana mara ya mwisho nilivyomuona… uwezo huo ni wa majini wa karne zilizopita ambao ni wachache sana na ni levo ambayo ni ngumu kufikiwa katika kipindi hichi”Master namba nne aliongea.
“Kuweza kumiliki Dhana ya kihistoria kama Chaos Cauldron inamaanisha kwamba Roma sio binadamu wa kawaida , Mkuu hata kama miliki yetu haina uhusiano wa karibu na Roma hatupaswi kuwa na uadui nae vinginevyo hata kama wazee wetu wa miliki kuja kupambana bado tunaweza kumshindwa”Mwanaume mweupe ambaye alikuwa amevalia nguo za rangi ya majivu aliongea.
“Namba nne nadhani uende ulimwengu wa kawaida na kumpatia taarifa Jeremy kuwasiliana na binti yake , kupitia yeye nina imani Roma atakubali kukutana na sisi kwa siri”
“Nini , Kaka mkubwa ,,, hio ni hatari sana , huyu binadamu ni muuaji”Maneno yalimtoka Master namba nne akiwa na wasiwasi.
“Bila hatari bila faida”Aliongea




















SEHEMU YA 731.
Siku mbili mbele wanajeshi wa majini wa Uingereza waliondoka kisiwani mara baada ya kukamilisha utengenezaji wa maabara katika ukamilifu uliohitajika.
Roma alikuwa akiinjoi maisha bila mawazo kabisa katika siku mbili zote usiku na mchana , alikuwa akicheza na warembo wake kila wakati aliojisikia.
Hakujali mazingira ni kwenye mchanga wa fukwe au kwenye meli au chumbani kwao yeye aliendeleza kazi.
Viashiria vya kufanya mapenzi na wanawake hao viikuwa vikonekana kila mahali , Stamina yake isiokuwa kawaida ilidhihirika kwa mara nyingine.
Hajawahi kuwa mtakatufu hata hivyo hivyo hakuweza kuona aibu kuzungukwa na wanawake wengi namna hio , zaidi sana ni kwamba kila mwanamke wake alitaka kupata mimba yake hivyo hakuna ambaye alikataa kutoa utamu kwa Roma labda pale ambapo wanajishi kuwa wachomvu sana.
Roma hata pale anapofumwa na mwanamke mwingine asingeona aibu na kumwambia na yeye na ajiunge , ki fupi alijihisi ni kama yupo mbingu ya saba , maisha kwake yalikuwa ya burudani kiasi kwamba hakujua hata muda unavyoenda.
Upande mwingine wanawake ambao hakuwa nao karibu zaidi ni Clark na Yezi , sio kwamba hakuwahitaji lakini ni kama hakujisikia huru mbele ya Yezi na kuhusu Clark ni kwamba muda wote yupo bize na maswala yake ya kisayansi , alikuwa akifanya kazi bila ya kupumzika na msaidizi wake Grace.
Roma alilewa na marafiki zake wanajeshi ambao walifika kisiwani hapo kwa ajili ya kumtembelea , siku ya tatu wakati akirudi ngomeni moja kwa moja alienda hadi chumba cha Master ambacho analala Edna na alimkuta Edna akiwa bize kusoma nyaraka ambazo zimetumwa na Recho.
Alikuwa amevalia Lace blouse kama gauni hivi fupi la kulalia , na alikuwa ameupa mlango mgongo.
Roma aliekuwa amesismama nyuma yake aliweza kumwangalia mrembo huyo kuanzia chini mpaka juu na namna ambavo shepu ilivyojiachia kwenye kiti.
Roma aliishia kumeza mate mengi huku akimsogelea na kisha akamkumbatia kwa nyuma huku mkono wake ukitambaa kwenye mlima wa manyonyo yake.
Edna aliishia kutoa nywele zake ndefu ambazo zimemfunika uso na kumwangalia usoni.
“Nenda kalale kwenye chumba kingine , Lanlan anataka kulala na mimi”
“Aa.. Honey acha hizo basi , Lanlan anaweza kuja muda wowote tu kwani sio kwamba kuna utundu nitakufanyia , si itakuwa vizuri kama sisi wote watatu tukilala kitanda kimoja”Aliongea Roma huku akiminya minya na kufurahia manukato ya mke wake.
Edna alionekana kushindana na msisimko aliokuwa akisikia na aliishia kufumba macho na kulamba lipsi na hatimae alijitahidi na kuondoa mkono wa Roma kwenye nyonyo lake.
“Inatosha bwana , nina jambo muhimu nataka kuongea na wewe”
Roma alishangaa kidogo na aliishia kuweka tabasamu la kihuni kwenye uso wake.
“Jambo gani la usiriasi , ni kweli Mama alikupigia simu tena ? ,kuna kitu ameongea ambacho hakijakufurahisha , usiwe na wasiwasi siku zote lazima kuwe na migogoro na mama mkwe na mke ,
nadhani ni sahihi kwake kuwa na wasiwasi kwasababu tumeamua kukaa nje ya nchi , kesho nitaenda kumtembelea na Lanlan”
“Sio kuhusu mama …”Aliongea huku akionyesha ishara ya wasiwasi kwenye macho yake na aliishia kung’ata lipsi zake huku akionekana kama mwanamke ambaye anatafuta ujasiri.
“Ni kuhusu mheshimiwa Jeremy?”
Roma mara baada ya kusikia kauli hio tabasamu na hali ya utani ilimpotea palepale.
“Nini kuhusu Jeremy amekuambia nini awamu hii?”
Edna mara baada ya kuona muonekano wa Roma alijua kabisa hakuwa katika hali ya matani tena.
“Alitaka nikuambie kwamba mkuu wa miliki ya
Panas… anataka mkutane kwa siri . sasa nawaza kama unaweza kufanya hivyo kwa ajili yangu , wewe mwenyewe ndio utachagua mahali na muda”
Roma alishangazwa na jambo hilo mkuu wa miliki ya Panas anataka kukutana na yeye , ilikuwa sio kawaida kwa wakuu wa majini kutaka kuonana nae katika ulimwengu wa kawaida.
“Edna umesema nifanye hivyo kwa ajili yako , hilo limekuja katika moyo wako mwenyewe au amekulazimisha uongee hivyo mbele yangu?”
“Kauli yangu italeta utofauti wowote hata nikibaadilisha?”
“Ndio , kama wewe ndio umeamua hivyo kwa utashi wako nitaenda kukutana nae kwasababu siwezi kukataa ombi la mke wangu lakini kama ni Jeremy ambaye anajaribu kuchukulia kwa faida uhusiano wetu ili nikutane na nao sitoenda sitaki kuonana na mtu ambaye hawezi kuwa rafiki yangu , ni aidha nisiwe kabisa na uhusiano nae au nimuue kabisa , maana majini sio wa kuaminika kabisa siku zote wana ajenda zao za siri”
Edna aliishia kumwangalia mwanaume wake huku akiwa amezuia pumzi , sekunde kadhaa mbele alitoa tabasamu kana kwamba kuna mzigo ametua.
“Kama ni hivyo basi usiende , nitampatia jibu ake na usisumbuke kwa ajili yangu”
“Kwani kuna haja ya kuendelea kuwasiliana nae .. kwanini usiache kabisa kudili nae tena?”
“Kwasasa naona ni sawa tu .. siwezi fanya kitu cha kijinga ninao uwezo wa kufanya maamuzi”
“Yule mwanaume Jeremy sio mtu wa kuaminika kabisa , ni mtu ambaye haoni tatizo kuitelekeza damu yake… wasiwasi wangu ni baadae kukuumiza”Aliongea Roma hakuacha kufikiria namna mwisho wa Kizwe na Desmond ulivyowafika.
Edna aliishia kuinamisha kichwa chini bila ya kuongea chochote na Roma kwa wakati huo alijua hata kumshauri hakuna maana na ambacho anapaswa kufanya ni kumlinda pekee.
Kwasababu ya jambo hilo Roma alikosa mudi kabisa na baada ya Lanlan kufika na nguo zake za vidoti doti kwa ajili ya kulala alimlaza kitandani na kisha aliondoka.
Roma mara baada ya kutoka nje alienda kusimama juu kabisa ya ngome hio akiangalia mwezi angani , alikuwa na wasiwasi pengine kuna mtego Jeremy na familia yake ya majini wana kitu wanamwandalia.
Wakati akiangalia mandhari ya kisiwa hicho macho yake yalitua upande wa kilomita moja kutoka alipo na kuona mwanga na kumfanya kutoa tabasamu , ilikuwa ni maabara ya Clark ilioanzisha hapo rasmi ilikuwa ikitoa mwanga ikionyesha Clark hakuwa amelala bado.
Palepale alikumbuka alikuwa na maswali kwa Jiniasi huyo hivyo alielekea moja kwa moja upande huo , mara baada ya kuona hakuna mtu nje ya jengo hilo anaeangalia palepale alikwenda kutua katika floor ya kwanza na kuanza kutembea kupandisha juu
Jengo hilo lilikuwa ni la Ghorofa saba kwenda juu na mbili kwenda chini ya ardhi na ni floor moja tu ambao ndio hutumika kama makazi na floor zote ni maabara na maktaba.
Yaani kila floor ilikuwa ikihusiannisha tafiti zake , kulikuwa na vifaa vingi vya ajabu ndani ya eneo hilo ambavyo Roma aliamini hata wanasayansi wanaweza wasijue namna ya kuviendesha kutokana na ukisasa wake.
Hio ilikuwa ni Hazina ya Clark , wasichana wa umri wake wanapenda kuwa na mapochi ya brand kubwa au kumiliki vito lakini mapenzi ya princess huyo ni tofauti kabisa.
Kwa namna ambavyo jengo hilo lilivyo ilionyesha Clark alikuwa na mpango wa muda mrefu wa kuhamishia maabara hapo lilikuwa ni jengo ambalo hata madirisha yake hayakuw aya kawaida na ambayo yamefunwa kwa nje lilionekana kama boksi la kioo.
“Teacher the accelerator has reached the critical point of the force field..”
“What is the conversion efficency?”
“99.99% and above “
“Cordinates checked , start the countdown ..”
“Yes 5,4,3,1!”
Roma ambaye alikuwa ndio anafika floor ya juu kabisa ya jengo hilo ndio maneno ambayo alikuwa akisikia na alijiuliza ni nini hicho wanafanya au wanataka kurusha roketi kwenda angani.
Kidogo tu adondoke mara baada ya kuona hicho ambacho walikuwa wakifanya .
Katikati ya maabara hio kulikuwa na Silinda ya rangi
nyeupe kama darubini kubwa hivi ambayo inaangaliana na anga.
Boriti ya mwanga hafifu kama wa Laser ulitoka katika silinda ile na kuelekea angani.
Roma alishangazwa na jambo lile ijapokuwa hakujua ni nini lakini uwezo wake ulihisi mwanga huo haukuwa wa kawaida kabisa kutokana na nguvu yake ya kutisha.
Baada ya mwanga ule kufifia maabara hio ulirudi katika mwanga wake wa kawaida na ndio sasa Roma aliweza kumuona Clark na Grace wote wakiwa wamevalia mamiwani makubwa ya kujikinga na mwanga.
“Mwalimu kulingana na taarifa , ni kiasi cha 0.1 Attometer nje ya Accuracy ya tageti ,tumefikia malengo”Aliongea Grace huku akionyesha furaha.
Clark ambaye alikuwa upande mwingine kwenye mavazi ya kimaabara alivua miwani yake ile kubwa na kionyesha tabasamu usoni na ndio muda ambao aligeuzia macho yake na kumwangalia Roma.
“Grace umefanya kazi nzuri leo , unaweza kwenda kupumzika sasa nitamalizia palipobakia”
Grace pia alikuwa ashamuona Roma na kwa hali ya aibu kidogo alipita na kuanza kushuka kuelekea chini mara baada ya kuwatakia usiku mwema.
“Inaonyesha ulichagua mwanafunzi sahihi , anaonyesha kuridhika kabisa na utafiti mnaofanya”Aliongea Roma sasa akitembea kuelekea katikati ya maabara hio.
“Grace alikuwa akipenda maswala ya kitabibu mwanzoni lakini nilikuja kugundua ana kipaji cha kuwa mtafiti ..”Aliongea huku akivua gloves na kuzitupia kwenye dustbin na kisha akamsogelea Roma.
“Honey kujitokeza kwako usiku usiku kwenye muda kama huu sio kama wewe vile”
“Hebu tusiende huko kwanza , niambie kwanza mlichokua mkifanya hapa ni nini , mbona
inaonekana kama siraha yenye nguvu hivi?”Aliongea
Roma na Clark alianza kushika ile silinda kana kwamba anaparaza kwa kuoneysha ni kitu cha thamani.
“Huu ni utafiti ambao nilikuwa nikifanya kwa nusu mwaka mpaka sasa ni teknolojia ambayo nimeipatia jina la Cumberbatch Particle lightbeam Cannon’ unaiuonaje si inapendeza kwa kuangalia tu”
“Kupendeza tena?”
Mara baada ya kuelewa anachotaka kuongea Roma aliishia kutingisha kichwa huku akitabasamu.
“Inaonekana kupendeza sana”
Mara baada ya kupewa sifa na Roma macho yake yalionyesha furaha na kuanza kumuelezea Roma kuanzia Wazo la kimuundo , fizikia , mekanikia na nadharia za kimahesabu.
Roma alishangazwa na maneno ya Clark na mara baada ya kuona Clark anaenda mbele katika kuelezea vitu ambavyo vinamuumiza kichwa alimzuia asiendelee.
“Clark kuhusu hiki kifaa…. Kwanini usiende moja kwa moja na kuniambia inahusiana na nini na kazi yake ni nini au ni siraha ya kuua watu?”
“Kuu watu tena?”
“Unaweza kuwa sahihi kwani inaweza kuua lakini nimeitengeneza kwa ajili ya kuzuia vimondo na
Magimba kwa ajili ya spaceships hapo baadae”.
“Hebu rudia”
Roma alikuwa katika mshangao na kujiuliza kwanini maswala ya Spaceship tena.
“Alichosema Hawking ni sahihi , kuna mamilioni ya sayari angani , katika mtazamo wa kitakwimu uwepo wa viumbe tofauti na sisi binadamu ambavyo vipo vinaishi katika Cosmos havihesabiki bila hata ya kwamba hakuna viumbe kutoka sayari nyingine ambao wamegundulika mpaka sasa ukiachana na the gods , hiyo kama Alien wakitupata sisi kabla ya sisi kuwapata inamaanisha sisi bindamu ambao hatuna hata uwezo wa kupeleka kiumbe kwenye sayari ya Mars tutakuwa hatarini , kama mwanasayansi mchango mkubwa ambao anaweza kutoa ni kuwezesha binadamu kutoka duniani na kwenda kuishi katika sayari nyingine ili kulinda jamii yetu , imethibitishwa kwamba binadamu atafikia katika nyakati za Galactic kipindi ambacho tutakuwa na uwezo wa kusafiri kutoka sayari moja kwenda nyingine kwa urahisi tofaut na kusafiri bara moja kwenda bara lingine, sasa kama ni hivyo tunaweza kukutana na vitu kama Magimba , vimondo na mambo mengi hatarishi , sasa ndio wakati ambao kifaa hichi kitaingia katika matumizi , pili binadamu hawezi kusafiri kwenda sayari nyingine akiwa na mizigo mingi , hivyo niliona itakuwa sawa kama nitetengeneza siraha ambayo msingi wake ni
particle light beams, ni sawa na siraha ambazo
unaona kwenye muvi za sayansi fikirishi. Ofcoz hapa nimefanya mjaribio tu haimaanishi kwamba nimeshakamilisha , kama tutataka kutumia katika spaceship tutahitajika kujenga particle accelarotor kubwaa na ongezeko la sayansi itakayofiti muda huo , kukuelezea kwa kifupi ni kwamba sio ngumu kutengeneza siraha kwa kutumia hii Prototype, ninachojaribu kugundua ni kwamba ni namna ipi naweza kupata nishati yenye usanifu wa hali ya ambayo itatumika katika anga za mbali , lakini hilo sio tatizo kwasasa kwani naamini nikiendeleza juhudi nitapata majibu hata miaka mitatu ijayo?”
Roma mara baada ya kusikia maelezo hayo macho yake yalionyesha kutokuamini na kujiuliza hiko kitu kina uwezo wa kuharibu kimondo au magimba , kwahio inamaana kama nguvu yake itaongezeka ni kwamba risasi yake moja itaweza kusabaratisha mji,
“Bora tu mimi ndio mwanaume wako vinginevyo dunia itakuwa katika hatari kama dunia itakuibia tafiti zako hizi za hatari”
“Usiwe na wasiwasi mpenzi , najua mwisho wangu, katika kila vifaa hatarishi nilivyotengeneza nimeweka itifaki za ki usalama ngumu sana kuzijua , ukilazmisha tu inamaanisha unaharbu kabis kifaa hicho , hivyo hata kama mtu akiiba tafiti zangu itakuwa ni bure kabisa , hakuna mtu ambaye anaweza kuiba tafiti yangu na ikawa na maana kwake au kudukua mifumo yangu , ukweli ni kwamba hajawahi kutokea mtu wa aina hio ambaye anaweza kushindana na mimi ni Profesa Shelukindo na Yan Buwen pekee ndio waliokuwa wakinifikia, nimemkumbuka Yan Buwen sana alikuwa ni mwanasansi mwenye akili sana kuwahi kuwepo” “Sitaki hata ujaribu kumkumbuka , mwanaume pekee ambaye anatakiwa kutokea katika mawazo yako ni mimi tu”
Aliongea Roma huku akikaa katika kiti kilichokuwa wazi na kisha akamruhusu Clark kumkalia kwenye mapaja.
“Clark nina kitu ambacho siku zote nilitaka kukuuliza”Aliongea kwa namna ya kumnong’oneza sikioni na msisimko alioupata Clark ulimfanya kujihisi aibu na kuwa mwekundu kama yai.
“Niulize”
“Miezi kadhaa iliopita nilipokuwa Korea mara baada ya kukutana na Athena alisema sielewi msingi halisi wa nadharia ya kanuni za anga ni nini ,na pia alisema katika Anga hakuna ‘force’ kauli yake hii imenifanya kutokumuelewa kabisa , sasa kwasababu wewe ni mtaalamu wa maswala ya fizikia na unajimu kwanini usinielezee ni nini amemanisha kusema Angani hakuna ‘force’”
Aiseeeeeeeee
 
Elimu niliyopata katika hii Hadithi yako, hakika mitazamo yangu mingi imebadilika!! Mi binafsi najua ugumu wakuandika tamthilia Kama hii!! Wew nikati ya binadamu ambao ni extra ordinary! Uzi wako umejibu maswali meengi sana katika ubongo wangu hakika umejua kutuheshimisha great thinker! Maneno ni mengi sana lakn itoshe tu kusema wewe ni extraordinary
 
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA

MTUNZI: DR SINGANO JR

Mono no aware

SEHEMU YA 732.
Macho ya bluu ya Clark yalichanua baada ya Roma kuuliza swali lake , yalikuwa yakivutia kama vile ni madini na kutamani kuyaangalia muda wote.
“Vizuri , ukweli ni kwamba ni rahisi kuelewa ni kwamba tu wewe mwenyewe hukujaribu kuelewa..”
Akiwa ameng’ata lips zake alitoa tabasamu na kisha palepale akashika mkono wa Roma na kuuweka katika nyonyo lake.
Roma alikuwa akihisi kabisa mlima huo wenye ardhi tifutifu , licha ya kwamba bado alikuwa bikra lakini kifua chake kilikuwa kimetuna mno.
“Nisaidie kufungua basi”Aliongeea kwa sauti ya chini na Roma alimeza mate mengi bila kuelewa anachotaka kufanya mwanamke huyo lakini aliishia katika kumfungua na kufanya maembe dodo kuchomoka kutoka katika kizuizi chake na kuanza kupata hewa safi .
Clark alikuwa mtundu na hakuwa na aibu na aliishia kufurahi kwa namna ambavyo Roma alikuwa akimwangalia kwa uchu.
“Honey , basi chukulia haya manyonyo yangu kama ndio Anga na hii chuchu kama sayari , wewe chukulia ni sayari yoyote iwe dunia au jua , halafu tuseme labda uzito wa sayari umeongezeka..”
Wakati akiendelea kuongea Clark kwa utaratibu sana alimfanya Roma kushika ile chuchu na kuiminya na kufanya nyoyo kutuna upande wa chini .
“Sasa uzito wa sayari ukiongezeka anga linabadilika umbo na kuwa kama hivi na kila maada inakuwa katika udhibiti … labda tu iwepo sayari nyingine ambayo ina uzito mkubwa zaidi na kutengeneza huu mbonyeo na kuzifanya sayari nyingine kuwa katika duara kwa kusukumwa mbali..”
Roma alikuwa makini katika kusikiliza mlelezo hayo na alikuwa amependa namna ambavyo Clark alikuwa akimwelezea kwa njia ya ki ubunifu zaidi , hakuwahi kujua kumbe sayansi ilikuwa tamu namna hio.
Muda huo Clark alikuwa akihisi mkuki wa mwanaume wake ukinyooka kuelekea mbele kama vile unataka kumtoboa suruali yake na pumzi yake ilizidi kuongezeka.
“In Other word … in space , there is exists no force because the presence of mass will alter the shape of the space which eventually produces the ‘force’ we are talking about , but ofcourse this is just the most surfaced knowledge I shares ….”
Ghafla tu Roma alishika kiuno cha Clark na kukivutia kwake na kuanza kumbusu kwenye lips zake.
Busu hilo la papatupapatu lilimpelekea Clark kulala kwenye meza huku Roma akiendelea kubonyeza sayari na anga kwa spidi kubwa.
“Inatosha… nishakuelewa sasa kama nitaendelea kukusikiliza ninaweza kupatwa na ukichaa kwa kuvumilia muda mrefu”
Roma na tamaa zake alimbusu mrembo huyo kwenye shingo na kushuka kuelekea chini , alikuwa akifurahia kila eneo katika mwili wa Clark huku akifurahia manukato mazuri yaliochanganyika na harufu ya mwili wa kizungu pamoja na sanitaiza.
Ijapokuwa harufu hio ilikuwa na maajabu yake lakini bado Roma alionekakan kufurahi.
Ilikuwa hivyo hivyo kwa Clark , alionekana kutoa ushirikiano wa kutosha na kufurahia kile ambacho anafanyiwa na alitaka kuvua koti lake la kimaabara na kulitupia kule lakini Roma alimzuia.
“Usilivue hilo koti unaweza kuvua vya ndani vyote lakini sio hilo koti … ninapenda unavyoonekana ukiwa umevaa hio sare”Aliongea Roma akiwa na tabasamu la kifedhuli kama kawaida yake.
Clark alikuwa kwenye mshangao wa sekunde lakini aligeuza macho yake pembeni lakini kwa wakati mmoja alitii maagizo.
Dakika chache mbele alikuwa uchi kasoro koti tu ambalo lipo mwilini mwake na kuegamizwa kwenye meza na kufanya shepu yake yote kumwagika , alimwangalia Roma na macho yake kama vile ni ya paka na kufanya moyo wa Roma kumiminika.
Kilichofuatia hakikuwa tegemeo lake , utimamu wa mwili wa Clark ulikuwa haumpi nafasi ya kuhisi maumivu kabisa kwani alishitukia tu kifimbo cheza kikimwingia na alichoweza kuhisi ni hamu ya kutaka kuongezewa ujazo.
Roma aliishia kuinama mara baada ya kuhisi mkuki wake kubanwa kila kona na aliishia kutoa tabasamu huku akimwangalia mrembo wake usonni na tabasamu.
“Vipi hupati maumivu?”Aliuliza na kumfanya Clark kuona aibu.
“Honey , jana mama aliniambia kitu yako ni kubwa mnoo na unapenda kumgeuza , nimeamini sasa lakini usinifanyie hivyo maana vitauma”
Kutajwa kwa jina la Catherine katika wakati muhimu kama huo ilimfanya Roma kushangaa na kidogo tu shetani lake kulegea lakini Roma kwa bahati nzuri aliweza kuzizuia hsia zake na kumbusu mdomoni Clark ili asiendelea kuongea.
“Wewe mtoto unafikiri nitaacha ninachokifanya kwa kutaja jina la mama yako , kadri unavyozidi kuleta ukinzani ndio tamaa zinavyozidi kunivaa”
Clark aliishia kucheka bila ya kuongea chochote huku akijisikia vizuri kwa wakati mmoja namna ambavyo Roma anampa vitisho vya uongo.
Bila ya kuonyesha udhaifu wowote kama mwanamke ambaye ni bikra Roma alianza kazi ya kupeleka moto ndani ya maabara hio .
Uwazi wa maabara huo uliojaa baridi ulifunikwa na sauti ya vilio vya kimahaba ambavyo vilidumu mpaka saa saba za usiku.
Baada ya kumaliza Roma alimbeba na kwenda kutua nae katika floor ya juu kabisa ya jengo hilo na kuanza kupulizwa na upepo wa baharini huku wakiangalia nyota.
“Babe kwa uwezo wako huo si utaweza kusafiri kwenda anga za mbali?”
“Siwezi , ijapokuwa naweza kuingia katika anga za juu lakini kadri ninavyozidi kwenda anga za mbali nitakosa mawasiliano ya mbingu na ardhi na nishati itapungua sana ,, itafikia sehemu hakutakuwa na nishati ya mbingu na ardhi kabisa , kingine pia angani hakuna oxygen bila ya uwepo wa elementi hizo muhimu siwezi kumudu hata kwa sekunde na mionzi intaniua”
“Kama nilivyotarajia hakuna nishati ya kutosha , ni kama ‘spaceship’ tu, tatizo hapa ni namna ya kupata rasilimali kutoka huko”
“Babe usiniambie unawaza mambo ya majaribio hata muda kama huu?”
“Oops , I’ m not on purpose it’s just an occupational hazard..”
“Ni sawa tu hata kama umefanya makusudi bado napenda”
“Ndio maneno yenu hayo ya uongo ya kutulegeza sisi wanawake”
“Hapana , naongea kutoka katika uvungu wa moyo wangu”
“Hahaha..najua”
******
Nii katika ulimwengu wa majini katika miliki ya Xia , viashiria vya pambano lililotokea hapo siku kadhaa vilikuwa vikionekana wazi , jengo kubwa la Jade ambalo lilikuwa limesimama siku kadhaa nyuma lilikuwa limeharibika na kutokuwa katika ufahari wake.
Lakini haikuwa imekwisha kwani majini karibia wote bado walikuwa hai.
Katika nyumba ya makazi ya mkuu wa miliki kulikuwa na kikao kilichokuwa kikiendelea na Anjiu kama mkuu wa miliki ndie ambaye alikuwa akiongoza kikao hicho.
Chini yake kulikuwa na majini watu waliosimama katika mistari mwili na kila mmoja alikuwa aidha na cheo cha kifamilia au alikuwa na kazi ndani ya makao makuu hayo katika nafasi ya juu ya kumuwezesha kuhudhuria kikao.
Kwa namna ambavyo walisimama ni kama vile bado wanaishi katika enzi zile za kale.
Kila mmoja alikuwa amekakamaa mwili huku vichwa vyao walikuwa wameviinamisha chini wakisubiria Anjiu kuongea.
Wakati Jinii Anjiu akiwa katika levo ya maji ya kiroho majini hao walikuwa wakimuogopa mno na hakuna ambaye ashawahi kukataa maagizo yake lakini muda huo alikuwa ni jini ambaye amevuka steji ya radi , hofu yao zidi ya Anjiu ilikuwa kubwa mno.
“Kama nilivyokwisha kusema Roma ni Mhalifu muovu , ameshirikiana na yule msichana mwenye mwili wa Yin nyingi ili kuingia katika miliki yetu na kumuua Laofi , Mtumishi Lao na wazee wetu wawili kwa msaada wa roho ya mnyama inayoishi kwenye Cauldron… hii dharau haikubaliki hivyo nimewaita nyie wote hapa kwa ajili ya kufanya kazi pamoja na kuhakikisha Roma analipia mara mia kwa kile alichofanya”
Sauti ya Anjiu iligonga ngoma za masikio ya kila mhudhuriaji na kufanya kila kiongozi kuonyesha wasiwasi wake na hofu.
“Mkuu , kwasababu Roma ana nguvu nyingi je tutaweza vipi kujilinda kama atakuja kwenye miliki yetu kwa mara nyingine?”Aliuliza mzee mmoja aliekuwa mbele kabisa.
“Kiongozi Ngapu haina haja ya kuwa na wasiwasi ili kuweza kushindana na Roma babu yangu Senji amekuja na wazee wengine wa levo ya maji ya kiroho , pia baba yangu Chaopi amerudi na wazee ambao walikuwa wakilinda miliki , kwasababu nishapita levo ya Radi ninalingana ki uwezo na Roma na nitaendelea kuongeza uwezo wangu kadri siku zinavyosogea kama Roma akija tena ninatumaini tutafanya kazi pamoja na kumuonyesha uhalisia wa nguvu zetu, tuna mamia ya majini ndani ya makao makuu yetu hakuna haja ya sisi kumuogopa binadamu mmoja ambaye amejifunza tamaduni zetu” “Oh kumbe mkuu aliepita amerudi?”
Majini hao walionyesha kufurahia mara baada ya kusikia Chaopi mkuu wa miliki aliepita amekwisha kurudi , ijapokuwa babu yake Anjiu bwana Senji alikuwa na nguvu, jini ambaye aliweza kuiba kiti cha umiliki kwa kutumia uwezo wake tu wa kimapigano alikuwa ni jini Chaopi.
Baada ya Chaopi kuachia ngazi alipotea katika ulimwengu huo wa kijini na alikuwa akifahamika kwa uwezo wake wa kutumia siraha , Master Shagoni anaweza kuwa na uwezo lakini alikuwa cha mtoto sana mbele ya Chaopi.
Sasa jiniasi kama huyo akiamua kurudi kama Anjiu mtoto wake ameivuka radi basi pengine na Chaopi pia alikuwa juu zaidi.
Lakini Anjiu kwa wakati huo hakuongea chochote kuhusu levo ambayo baba yake amefikia katika kuvuna nishati za mbingu na Arrdhi.
Maili kadhaa kutoka makao makuu hayo kulikuwa na ardhi ambayo ilikuwa tambararae ambayo imejazwa na mimea ya aina yake ambayo ilikuwa ikitoa harufu mchanganyiko.
Katikati ya eneo hilo ambalo ni kama bustani kulikuwa na nyumba ndogo tatu au nne hivi ambazo ziliendana na eneo hilo , ilikuwa ni kama Utopia mbali na madhira ya dunia.
Katika wakati huo katika meza ya jiwe la mzunguko Senji alionyesha kucheza mchezo ambao haukufahamika na mzee mwingine ambaye alikuwa na ndevu.
Mara baada ya Anjiu kutua ndani ya eneo hilo kwa nje alisogelea eneo ambalo wazee wake walipo na kuangalia mchezo ambao walikuwa wakicheza lakini kwa namna gemu hilo linavyochezwa ilionyesha mwanaume ambaye hakuwa mzee sana ndio anaelekea kushinda lakini hakutaka kuongea neno lolote.
“Salamu kwenu babu na baba”
Haijalishi alikuwa akiogopesha vipi ndani ya ulimwengu huo wa majini watu lakini bado alikuwa akionyesha heshima mbele ya babu yake na baba yake, hao majini wawili ambao walikuwa mbele yake ndio ambao walikuwa na nguvu kubwa ambao wanastahili heshima yake.
“Vipi wakuu wa familia na koo washaondoka na kurudi makwao?”Aliuliza Senji ambaye alikuwa ameshikilia kete yake ya jiwe kwa namna ya kusita sita kuicheza.
“Ndio na nimeshawapaitia herufi za mawasiliano , kama Roma ataamua kurudi na kuua mmoja wapo
taarifa zitatufikia mara moja ., nishawapatia taarifa pia kurudi kwako baba”Alitingisha kichwa.
“Vipi huyo Binadmau Roma Ramoni bado hajachukua hatua yoyote?”
“Mashushu wetu ambao wameenda ulimwengu wa kawaida wamerudi na taarifa na kusema Roma alirejewa na ufahamu wake kwani aliwasiliana na familia yake , sina uelewa ni kwa namna gani ameweza kruudi katika hali yake ya kawaida lakini inasemekeana yupo nchi ya mbali na mashushu wetu bado wanatafuta kujua nchi hio , pengine pia anapanga kupumzika nadhani na hii inatupatia muda wa sisi kujijega upya”
“Inawezekana pia anataka kuingia katika levo zingine kabla ya kurudi huku , pengine anataka kujua mbinu ya kukitawala chungu vizuri au kuelewa matumizi ya radi ili kuja kutuzima kwa shambulizi moja tu”Aliongea Senji huku akikunja sura kwani mtoto wake alionekana kucheza vizuri.
“Lakini mimi naona tunawaza mbali , kudhibiti radi ya mapigo mengii sio jambo ambalo linawezekana kirahisi , ile siku alikuwa na bahati sana yule mnyama amemsadia , baba na mimi wote tushaipita radi na ni sawa na kusema analingana nae ki uwezo , kama Roma atarudi sidhani kama Chungu chake kitaweza kumsaidia tena”
“Nadhani pia nilishakuambia usijifikitie wa juu sana ki uwezo , adui ambaye ameweza kumuua Bi Sena na Tigola sio wa kawaida , kuingia tu katika levo ya kuipita Radi unajikuta kujiamini hivyo inaweza kukukost.”Aliongea Chaopi na kumfanya Anjiu kunywea.
“Ndio baba nimetambua makosa yangu”
“Wakati ambao unachukua nafasi kama mkuu wa miliki nilikuambia wewe na mimi tageti yetu ni nini , yule mtu hawezi hata kutuangalia kwa nafasi tuliopo na kuhusu kilichotokea juu ya Roma Ramoni ni swala dogo isitoshe hajakuua wakati nikiwa sipo , lakini kwasasa nimerudi na hakuna kingine ambacho naweza kufanya achana na huo mtazamo wako finyu na usijiweke katika kundi la majini wa kawaida ndani ya ulimwengu huu vinginevyo utakuwa mwenyewe siku zote”
“Nitakumbuka maneno yako baba”
“Vizuri , Chaopi inatosha sasa, Anjiu amekuwa akifanya kazi nzuri kuliko hata wewe wakati alipochukua nafasi yako , hakuna kosa katika kupanua miliki yetu isitoshe katika umri wake huo hamkua kwenye levo sawa hivyo ni kama amekuzidi”
“Najua unapaswa kudili na Zianji na wengineo hivyo sitaki kuongea sana , yeye pia ni mtoto wangu na ni mdogo wako maamuzi yapo juu yako , wewe ndio mkuu nina uhakika utakuwa na busara katika kudili na hilo swala”
Anjiu alikaa kimya kwa muda na kisha aliinamisha kichwa chake kama ishara ya heshima na kisha akaaga na kuondoka.
“Mtoto wangu na mjukuu wangu naona mshanizidi sasa”
“Wakati nikiwa mdogo ulikuwa ukiniambia kama mtoto akiwa dhaifu kuliko baba yake basi hapaswi kuzaliwa kabisa”Aliongea Chaopi.
Upande mwingine katika ngome ya makao makuu ya miliki, Anjiu alikuwa amesharudi na kumuiata mdogo wake Zianji na mke wake Leiana.
Zianji mtazamo wake mbele ya kaka yake ulikuwa umebadilika , ile hali ya maringo aliokuwa nayo ilikuwa imepotea na sasa alionekana kukata tamaa kutokana na nafasi ambayo kaka yake yupo.
Dakika ambayo aliingia katika chumba aliishia kuinamisha kichwa chake chini akiogopa hata kumwangalia Anjiu usonni.
Upande wa Leaiana yeye muda wote alikuwa amepamba uso wake kwa tabasamu kama vile hakuna kilichotokea.
Licha ya kwamba Anjiu ndio aliewaita lakini hakuongea neno na alikuwa amekaa tu kwenye kiti chake cha ukuu bila ya kuongea akiwa anawaangalia.
Baada ya kimya cha muda mfupi , Leiana alivunja ukimya.
“Anjiu umetuitia nini?”Aliuliza na kumfanya Anjiu kumwangalia.
“Lahani amejificha nyumbani kwako si ndio?”
“Ndio , amesema atakaa nyumbani kwangu kwa muda , nadhani anamuogopa yule mwizi”
“Haha,,, muoga kama nini , sidhani kama atakuja kufanikisha jambo lolote”Kwa mtazamo wake alijua Lahani alikuwa amejificha kwasababu anaogopa kukosolewa.
Wakati akipambana na Roma alishaona ni mtoto gani ambaye anapaswa kumuandaa kutokana na namna walivyochukulia tatizo lile,.
Ijapokuwa alimwambia Lahani kukimbia lakini mtoto wake wa kike ambaye ni Dhaifu hakukimbia na sio tu kuangalia lakini alijaribu kumuokoa baba yake , kupitia jambo hilo alijua ujasiri ambao upo ndani yake upo kwa uchache katika majini wengi wa kiume.
“Ukiwa na uwezo huwezi kukimbia matatizo”Ndio ambacho aliwaza Anjiu na kuamini.
Baada ya kusimama taratibu kwenye kiti chake ghafla tu Anjiu palepale aligeuza nguvu zake za kijini na kutengeneza kitenesi cha moto kama cha umeme vile katika kiganja chake ambacho kilikuwa kikitoa msisimko wa nguvu za giza.
Ni siraha ambayo ilikuwa imejazwa na nguvu ya kali mno na kubwa ambayo iliwafanya Zianji na Leaiana kurudi nyuma.
“Vipi mnahisi nguvu yake?”
“Taowu!!?”Aliongea Zianji kwa kumaka.
“Ndio , shukrani sikuendee wewe , Laofi na Mohi nimeweza kujipatia nguvu ya ajabu kutoka katika nafsi ya mnyama Taowu , inaweza kuonekana nguvu ya giza lakini imeweza kunipaisha ki uwezo sana na kufanya mbinu yangu ya kimashambulizi ya mshale wa radi uvukao anga kuwa mkubwa sana”
Kauli yake iliwaondolea hali ya tabasamu kabisa katika nyuso za Leaiana na Zianji na kukumbwa na huzuni.
“Kaka inamaana ulijua kila kitu kilichokuwa kikiendelea??”
“Nilijua wewe na Laofi mlikuwa na mahusiano na huyu mwanamke na kisha mkamuingiza na Lao mtumishi , hivi mnadhani lile banda lenu kule bwawani ni sehemu ambayo sifiki … lakini hata hivyo sikuwahi kuwaza mnaweza kupata damu ya mnyama Taowu na kuitumia kwangu , nilionekana mahesabu yangu hayakukaa sawa lakini hata hivyo haijalishi mlikuwa makini vipi mpango wenu umefeli , ninapaswa kuwashukuru kwa kutumia damu hio katika mwili wangu kwani imesaidia sana kupandisha uwezo wangu”
“Kaka .. kaka tafadhari yarehemu maisha yangu”Aliongea Zianji huku akipiga magoti na kutetemeka.
“Relax … sina mpango wa kukufanyia chochote bado una thamani kwa miliki kutokana na uwezo wako isitoshe umelala tu na huyo mwanamke na kufeli kuniwekewa sumu , baba ameniachia haya maamuzi na nimeamua kukuacha hai , lakini utambue hii ni nafasi yako ya mwisho”
“Baba .. amerudi kama ni hivyo kwanini haja…?”
“Kwanini hajakutana na wewe ,kwanini afanye hivyo?”
Maneno yake hayo yalimfanya Zianji kurudi nyuma nyuma kwa kujikongoja.
Ilikuwa ni kweli kutokana na uwezo wake mdogo baba yake hakuwa na haja hata ya kuonana nae kwani hakuwa kitu.
“Asante sana kaka ,,”Aliongea Zianji kwa kujikaza na kisha alisimama na kuondoka kwenye chumba hicho na kumuacha Leiana mke wa Anjiu.
“Kwanini ?... kama ulijua nilikuwa na mahusiano nao kwanini ukaamua kujizuia?”
“Haha.. kujizuia!?.Leiana usifikirie sana , kwanini nifanye hivyo , uhusiano wako na wanaume wengine haunihhusu”
“Mimi sio mkeo ,? Mimi ni mama mtoto wako kumbuka”
“Haha.. kwahio ndio nini sasa , wewe ni mke wangu tu kijina na mtoto wa mtoto wangu bado tu huelewi , nilichotaka kutoka kwako ni kuwa mwanamke wa nyumba yangu lakini haina maana unapaswa kulinda uanamke wako kwa ajili yangu , isitoshe umekuwa ukifanya mahusiano yako ni siri, si ndio?”
Maneno yale yalimuuma sana Leiana , ni zaidi ya Adhabu ambayo angepatiwa kwa usaliti na aliishia kutingisha kichwa akiwa kama haamini.
“Unanidanganya ,, kwanini unanifanyia hivi?”
“Leiana nimekuita hapa ili kukuonya uache mara moja kufanya hila zako zidi yangu , hakuna haja ya miliki yetu kuwa na mke wa mkuu au kuendelea kuwa mama kwa Lahani , isitoshe huna faida yoyote kwangu”
“Haha.. kwahio unasema kwamba unachojali ni madaraka yako na uwezo wako na vitu vingine havina maana kwako?”Anjiu alibakia kimya akionekana kukubaliana na kauli yake.
“Anjiu wewe hakika ni muoga kama Kunguru , hivi unajua ni kwanini nilitaka kukusaliti , kwasababu hujawahi kunijali tokea nilipo kuzalia mtoto , tokea nikiwa mtoto familia yangu iliniambia jina langu litabadilika kwasababu ninakwenda kuolewa na mtu mwenenguvu na kwa moyo mkunjufu nikakubali na
nikajitahidi kwa uwezo wangu kuwa mke mwema lakini nini ulikuwa ukinifanyia , ulijifanyisha tu unanipenda na kunipotezea , hukujaribu hata kuniangalia usoni, wewe ni mwanaume muoga ambaye uliogopa kukataa hisia zangu waziwazi na kuendelea kuwa mnafiki”Aliongea na kumfanya Anjiu kumwangalia kwa macho makali.
“Umemaliza? , kama umemaliza ondoka mbele yangu”
“Sijamaliza , niue hicho ndio ninachojali , tokea siku ambayo nilianza kushirikiana na Laofi na wengine sijawahi kuwaza kuishi , Anjiu mimi nakujua kuliko unavyojijua wewe wenyewe , wewe ni mwanaume ambaye unatia huruma na ambaye hujui ni kipi unapenda na kipi hupendi , ijapokuwa unapambana katika mafunzo ya nishati lakini umeshindwa kupotezea yaliokutokea ulimwengu wa kawaida , tokea siku ambayo umemleta Xiao katika huu ulimwengu nilishajua tayari ulikuwa na mtu umempenda , huyo mwanamke kutoka ulimwengu wa kawaida umempenda na umeshindwa kumpotezea , kwa ninavyokujua usingeruhusu akuzalie mtoto”
“Lakini hebu jiangalie unajitahidi kupotezea hizo hisia ili kuendelea kuwa na nguvu na kujifanyisha hujali lakini ukweli ni kwamba unashindwa kujizuia kumlinda , umemfanya Xiao uwezo wake kuwa wa chini ili asionekane kuwa tishio , hivi huchoki tu , mimi hata kwa kukuangalia hivi ninajichokea , huongei chochote na siku zote ni mtu wa kujifanyisha tu lakini nilishakuona tokea muda mrefu hujali uwepo wangu , Anjiu nakudharau, nakudharu sio kwasababau hunipendi au kuwa bize na kuvuna nishati lakini ni kwasababu upo tayari kupenda binadamu dhaifu kuliko mimi mwanamke ambaye nipo pembeni yako siku zote”
“Kimyaa..!!!”
Anjiu alipandisha hasira na nguvu nyingi za kijini huku akiwa amemkaba Leiana koo na kumfanya asipate hewa na kuishia kukohoa kwa kutema damu.
Mara baada ya kuona huo sio muda wake wa kufariki , aliamua kumauchia na kumsuumia mbali.
“Ondoka , usinifanye nipoteze uvumilivu wangu kwako”
Leaina alijikongoja na kusimama huku akishika shingo yake na kuonyesha tabasamu lililojaa kejeli.
“Naona una hasira , vizuri sana hatimae umeonyesha hisia zako”Aliongea na kumwangalia Anjiu kwa sekunde kadhaa na kisha akageuza na kuondoka lakini kabla hajatoka kabisa aligeuka.
“Hata kama hujawahi kunipenda lakini huwezi kukataa mimi ndio nakujua vizuri , kwasababu dakika ambayo unamfikiria huyo malaya wako mimi nipo nakuangalia usoni”Aliongea na kisha akaondoka na kufanya ukimya kutanda.
Anjiu aliishia kupumua kwa nguvu na dakika ileile alitoa pete ya madini ya Jade kutoka kwenye hifadhi yake na kuanza kuisugua sugua kama vile ina uchafu.









SEHEMU YA 733.
Ilikuwa tayari ni siku kadhaa kufikia siku ya fainali ya mashindano ya UEFA champion League , watu wengi wenye ushawishi na matajiri kutoka pande za dunia walikuwa wakielekea London na wengi ya matajiri waliamua kuegesha boti zao za kifahari ndani ya eneo la Canary Wharf.
Kwasababu ilikuwa ni eneo maarufu ndani ya jiji hilo la London kwa kuwa na biashara nyingi pamoja na mall za kufanyia Shopping wiki hio Mooring fees ilikuwa juu mno na iligharimu zaidi ya paundi elfu kumi kwa kuegesha boti kwa masaa ishirini na nne tu.
Lakini licha ya gharama hio kuwa kubwa haikuwa kikwazo kwa matajiri kwani kwao pesa waliichukulia kama namba tu, ukweli ni kwamba hata kam walikuwa na pesa nyingi eneo hilo halikuwa likitosha.
Mooring fees ni ada ambayo hulipwa kwa kuegesha chombo mfano wa boti katika eneo maalumu ambalo limetengwa karibu na biashara.
Sasa kuweza kuegesha boti yako katika eneo la Canary Wharf ni ishara ya kamili ya utajiri na hadhi.
Dakika hio hio boti moja kuubwa ya kifahari ambayo ilizidi kimo cha boti zote zilizokuwepo mahali hapo ilijongea taratibu na kwenda kusimama eneo la katikati ya Canary Wharf , wanaita sehemu ya Dhahabu ambayo inakupa nafasi ya kupata chochote.
Kitu cha kushangaza zaidi katika mbavu za boti hio kulikuwa kumeegeshwa makombora makubwa ambayo yalikuwa yakiwaka waka kutokana na kupigwa jua.
Kilichowauzi mabilionea wengi ni kwamba mtu huyo mmiliki wa hio boti alikuwa amenunua nafasi mbili zaidi za wazi kana kwamba hataki usimbufu wa kusogelewa na viboti vyao jambo ambalo walichukulia ni kama dharau.
Boti hio kubwa ya kifahari kuliko zote ndani ya eneo hilo ilikuwa ni Erebos , boti ambayo inamilikiwa na mfalme Pluto.
Baada ya kukubali mualiko wa Malkia Catherine
Roma alichukua wanawake wake wote na binti yake Lanlan na kuwapelekea London kwa ajili ya kuangalia onyesho la utumbuizaji wa Sophia kabla ya kuanza kwa fainali , ilikuwa hivyo kwasababu Roma alitumia muda huo kama likizo ya muda mfupi kutokana na kuvuna nishati kwa muda mrefu.
Kama vile iliikuwa ni trip ya kifamilia Roma hakusahau kusafiri na Bi Wema , Sui , Mlezi wa Lanlan Qiang , mama yake na ndugu zake na wengine wengi ambao aliwatumia mualiko na kukubali.
Mama yake Magdalena na Mage, Mama T alikuwa amefika pia , Mama yake Nasra kutoka kijijini Mponde aliweza kufika pia kwa mara ya kwanza katika jiji la raha , Shangazi yake Dorisi na mjomba wake pia walifika , bila kumsahau mke wa Juma pamoja na shangazi yake wote waliweza kusafiri.
Shangazi yake Dorisi na Mama T walikasirika mara baada ya kuona kundi hilo la wanawake wa Roma bila ya kufahamishwa lakini kwasababu watoto hao walikuwa washawaelezea kuwa Roma hakuwa wa kawaida basi hakuna ambaye alimkasirikia na kuishia kumuona sio mtu wa kawaida, hata mara baada ya kusikia kwamba wanao uwezo wa kuishi muda mrefu bila ya kuzeeka walifurahi.
Na Roma ili kuwapamba pamba aliwaahidi kuwapatia vidonge vya kuendelea kuwa vizuri kiafya na kuongeza umri wao wa kuishi.
Hata kama wewe ndio mzazi na watoto wako wote wanampenda mwanaume mmoja na huyo mwanaume mmoja anakuambia anao uwezo wa kukupatia kidonge cha kukuongezea miaka angalau hata kumi
ya kuendelea kuishi unadhani ungekataa , ki ufupi unaweza kwenda mbali na kumwambia’ Mkwe nitazaa mwingine nikupatie’ kwasababu hakuna biandamu ambaye anapenda kufa mapema licha ya kwamba kuna siku ya kifo.
Haikuwa hivyo tu Roma alikuwa tajiri wa kutisha , boti hio ya kifahari ilikuwa ni sababu tosha ya kukufunga mdomo na Roma hakuishia hapo tu hata huko Tanzania kwenyewe walifuatwa na ndege binafsi na kuwasomba wote kuja Uingereza na kuingia katika boti ya kifahari na baada ya hapo kila mmoja akapatiwa kijakazi wa kumsaidia shida zake zote.
Ki ufupi ni kwamba maisha yao ndani ya jiji hilo la London ni kama vile wapo ndotoni katika miliki ya Mfalme Pluto.
Mama T licha ya kuwa na pesa na kumiliki biashara kubwa ndani ya jiji la Dar es salaam hajawahi kuonja ufahari wa namna hio , waliopagawa zaidi ni mama yake Nasra na ndugu wa Najma yaani wifi yake na Shangazi yake..
Hakuna ambaye alikuwa jinga , walijua kwa uwezo wa Roma wa nguvu za kimaajabu wao ni kama sisimizi tu hivyo walijikuta automatiki wakiwa na adabu.
Ndani ya muda mchache tu boti hio ya Erebos ilijaa neema ya watu wengi.
Ijapokuwa London haikuwa na maeneo maarufu ya kufanyia Shopping kama Ginza, Avenue des champes elysee na Fifth Avenue lakini
Knightsbridge and Harrods ilikuwa ni sehemu nzuri kwao kufanya kufuru ya manunuzi.
Hata kwa mwanamke mpole kama Edna , Magdalena na Neema hawawezi kujizuia kuingia katika maduka makubwa ya kifahari ya eneo hilo.
Kuhusu Yezi na Rufi ambao hawakuwa na uelewa mkubwa kuhusu brand maarufu walikuwa na shauku ya kutaka kujua vitu vingi kwa kuuliza maswali.
Wazazi wao walikuwa ni umri tofauti tofuati lakini mwishowe walizoeana kupitia kufanya vitu pamoja.
Mwanzoni Roma alitaka kuwasindikiza kwenda kufanya shopping lakini haraka sana aligundua hawezi kuingilia hivyo aliacha wafanye wenyewe na yeye alikaa eneo la Lounge kusubiria akiwa na Lanlan.
Kwasababu Lanlan alikuwa bado mdogo hakuwa na haja ya kufanya shopping na alichokuwa akipenda sana ni midoli , kuhusu mavazi mashangazi zake na mama yake wangemnunulia tu.
Baba yake pia sio mtu wa mambo mengi isitoshe Roma alikuwa na furaha kuwa na Lanlan pembeni yake ambaye alikuwa mtiifu kuliko hata ya Edna mke wake.
Wanawake uwezo wao wa kununua mavazi na vitu vingine ulikuwa mkubwa mno na siku ya tatu kila mtu alikuwa amejaza hifadhi yake ya pete na wale wasiokuwa na pete walikuwa wamejeza kwenye vyumba vyao.
Siku ya nne kila mmoja hakuwa na hamu ya kununua kitu kingine tena hivyo walihamia kwenye kula vyakula vitamu juu ya boti hio ya kifahari.
Meza zilikuwa zimepangiliwa juu hapo na vijakazi ili kufanya eneo liwe la kutosha kwa kila mmoja.
Sasa jambo la ajabu ni kwamba licha ya kwamba ni mchana tena wa jua kali lakini wazee wote ambao hawakuwa na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi kila mmoja alikuwa amevalia majaketi mazito mno na haikuwa kwao tu hata kwa raia wengi wa jiji la Uingereza.
Roma kwa kuona jambo hilo kuna kitu aliona kabisa hakipo sawa na aligeuza uso wake na kumuangalia Clark.
“Clark hali ya hewa ya kipindi hichi si inakuwaga ni ya kati kwanini inaonekana kama ni kipindi cha baridi hapa Uingereza?”
Kwasababu Clark alikulia London basi alikuwa akijua majira ya nchi hio kwa mwaka mzima.
“Ndio umegundua sasa hivi , joto limeshuka sana dunia nzima katika miezi hii , kawaida joto la London katika mwezi huu linapaswa kuwa kati ya nyuzi kumi na nane mpaka kumi na tisa lakini leo ni kumi na inaonekana linaendelea kushuka”Alijibu.
“Inaonekana hamuangalii taarifa ya habari , tokea wiki iliopita taarifa zinasema kwamba joto la dunia limeporomoka kwa kiwango kikubwa mno kama vile hakuna kabisa’ Global warming’ , hata katika ncha ya Kusini na Kaskazini inaripotiwa ukubwa barafu umeongezeka , wanasayansi duniani wapo katika utafiti ili kujua sababu ni nini”Aliongea Mjomba wake Dorisi ambaye alikuwa akikata kipande cha nyama , alionekana kuwa msomi na tajiri hivyo licha ya Roma na Clark kuongea kingereza alisikia.
Lakini pale pale ndio alipokuja kujua alikuwa akielewa kuongea kingereza na kirusi kwani elimu yake amepatia nchini Urusi na Marekani.
“Kama hata wanasyansi wameshindwa kujua nini tatizo kwanini wewe Clark hufanyii kazi swala hili?”Aliuliza Roma.
“Nishajua kuhusu tukio hili la ajabu hivyo nilishampa kazi Grace kukusanya taarifa kutoka pande zote za dunia , naamini nitaanza utafiti wiki inayokuja”
“Sister Clark you are amaizing , its like you excel in every field”Aliongea Yezi huku akimtolea Clark ulimi kumkejeli lakini kwa wakati mmoja akiwa na hali ya kumkubali.
“Every group has someone who is the best and one who is mediocre , I’m just luck to have a great mind”Aliongea Clark.
Wakati wakiwa wanaongea palepale simu ya Roma ilianza kuita na mara baada ya kuitoa mfukoni aligundua ni namba ngeni kutoka nje ya nchi yaani Tanzania kutokana na mwanzo wa code zake
Roma alikuwa akiijua hio namba na aliishia kumwangalia Mage na Magdalena na mama yao na aliona hawakuwa na uelewa kama ni Afande Tobwe ambaye alikuwa akipiga simu.







SEHEMU YA 734.
Roma alipokea simu na kuweka tabasamu usoni na kisha akaongea kwa sauti bila ya kujiuma uma.
“Hello , nnikusaidie tafadhari”Roma alienda moja kwa moja kama vile hamjui mzee huyo.
“Roma Balozi wa Hongmeng anataka kuonana na wewe”Aliongea Afande Tobwe kijeshi.
“Balozi wa Hongmeng? Nani huyo?”
“Amejitambuliza kwa jina la Xuan Jizi , amesema ni mjumbe wa majini wa Hongmeng katika upande wa dunia”
“Xuan Jizi?”Aliuliza Roma huku akijiambia pengine ni yule ambaye alimhonga vidonge au mwinginekwani hakujua jina lake halisi.
“Amesema sababu ya kutaka kukutana na mimi ni ipi?”
“Hajaongea chochote , hivyo nataka jibu kutoka kwako kama upo tayari kuonana nae au lah”
“Kama ni hivyo mwambie nipo vacation na siwezi kuongea nae chochote na kama anashida sana na mimi mwambie aje London atanikuta lakini sina uhakika kama anaweza kurudi hai maana hili ni eneo ambalo lipo chini ya Apollo na Artemis”
“Nilijua tu utajibu hivyo lakini usijali sana, kwasasa umekuwa na nguvu kubwa mno na unatisha hivyo siwezi kukushauri chochote , nitakupigia kama kuna tatizo”
“Asante sana baba mkwe”Aliongea Roma mara baada ya kucheka kidogo na kisha akakata simu.
“Hubby huyo ni baba yangu uliekuwa ukiongea nae? , kuna tatizo nyumbani au kuna mtu anataka ugomvi na wewe?”
“Ameniuliza ni lini atapata mjukuu ,, mzee ana tabu huyu”Aliongea Roma akiwa siriasi.
“Wewe…!”Mage aliishia kuangalia pembeni baada ya kupewa jibu hilo , tokea aanze kuwa mpnezi wa Roma ule ujeuri wake wote ulikuwa umeisha.
Mama T aliishia kushika nywele za Mage na kutabasamu bila ya kuongea chochote , ukwei ni kwamba licha ya kwamba ameridhia kishingo upande watoto wake wote kujihusisha kimapnzi na mwanaume mmoja lakini bado hakujisikia vizuri na alikuwa mkimya mno.
“Sir nnimesikia hilo jina , ni binadamu ambaye ana mafunzo ya kijini ambaye alijipatia umaarufu kwa miaka kadhaa kutoka Hongmeng , kama ndio ameagizwa kuja kama balozi basi naamini swala hilo sio jepesi”Aliongea Sui.
“Ngoja wafanye wanachotaka , haijalishi ni nini wanataka , kwasasa jambo hilo ni kiporo mpaka Sophia atakapo maliza show yake”
“Halitokuwa tatizo? , kumbuka babu na ndugu zeu wengine bado wapo Tanzania”Aliongea Edna.
“Ndio Roma usivuke mpaka wewe kwasasa ni mtanzania si ajabu wamemtumia Afande Tobwe kuwasiliana na wewe”Aliongea Blandina mama yake.
“Haina haja ya kuwa na wasiwasi kwasababu amekuja kama balozi hawezi kufanya kitu chochote kwani maamuzi hayo hana , wametumia serikali kutaka kuwasiliana na mimi ili waonekane ni kama wazito na muhimu lakini siwezi kuwapa nafasi hio , wakiona siwachukulii siriasi watagundua nguvu yao ni ndogo zidi yangu na hawawezi kuniamrisha amrisha , kama watagusa mtu yoyote ndani ya Tanzania itakuwa ni kukiuka sheria na isitoshe wao ndio wamepewa jukumu la kusimamia sheria hizo”
Wote walikubaliana nae na ukweli waliamini labda Hongmeng wamesikia kile ambacho Roma amekifanya katika ulimwengu huo wa majini maana miliki ya Xia ipo karibu sana na Hongmeng.
Baada ya chakula cha mchana kila mmoja alitawanyika wengine walienda kupumzika wengine walienda kuendelea na mafunzo na wengine kujaribisha kile walichonunua , Mage na Lanlan wao walichukuana na kwenda kuendesha speedboat.
Upande wa Roma alienda kuzamia katika chumba cha Neema Luwazo ambako alikaa muda mfupi sana na kisha akarudi juu kabisa na alimkuta Edna peke yake akiwa ameshikilia kikombe cha chai .
Edna ni kama vile alimtarajia na mara baada ya kumfikia aligeuka na kumwangalia.
“?Hebu kaa kwanza, vipi Neema yupo sawa naona amekuwa mnyonge?”Aliuliza Edna na kumfanya Roma kushangaa kidogo.
“Kwanini ghafla tu ukaanza kumjali Neema wewe ninachokumbuka ni kwamba humpendi”
“Hicho ndio unachowaza , mimi kama mwanamke namuona Neema ni mtu mzuri”Aliongea Edna na kisha akageuzia macho yake na kuangalia jiji, sauti yake ilikuwa nyororo na ya chini kana kwamba alikuwa akijiongelesha yeye mwenyewe.
“Edna umebadilika sana hivi karibuni na nashindwa kukuzoea unajua?”
“Unamaanisha nini?”
“Sijawahi kuwaza utakuja kupatana nao vizuri , ijapokuwa nilitamani ije kutokea lakini mabadiliko yako yamekuwa ya haraka sana na nashindwa kujizuia na kuona kuna kitu ambacho hakipo sawa ,unaweza kuniona labda ni mtu mgumu kufurahisha lakini hisia zangu zinaniambia kivingine kabisa”
“Unaogopa?”Aliuliza Edna akiwa na nusu tabasamu kwenye uso wake na swali lile lilimshangaza sana Roma lakini kwa namna moja swali hilo ni kama amejua kile ambacho Roma anajisikia.
“Unaona mambo kwa upeo wa tofauti nje ya matarajio yako na wasiwasi wako ni kesho yetu ambayo haijulikani , unajifanyisha kutokunielewa lakini ninachoona mimi hapa ni wewe ambae hutaki mimi nikuone kama unanishuku na mabadiliko yangu ndio maana unaniongelesha kwa namna hio”Aliongea na kumfanya Roma kulazimisha tabasamu kwani ni kama amekamatika.
“Ukiachana na hayo nadhani ni jambo zuri , kwangu ni sawa tu hata usiniambie sababu ya mabadiliko yako , nilikuwa na wasiwasi kwamba huwezi kuishi nao lakini sasa hivi naona kabisa upo hiari kufanya nao shopping na kucheka wanapokutannia na kula nao , kwangu nashukuru sana kwa hili”Aliongea Roma na kumfanya Edna kumwangalia kwa muda.
“Ukweli ni kwamba sijui siku nzuri kama hizi zitadumu kwa muda gani na ninachotaka ni kuwa na maisha ya utulivu na yasiokuwa na mawazo , vipi kama kila kitu kikibadilika siku moja , si itakuwa ni zaidi ya huzuni kwa kuwa na kumbukumbu pekee za sisi kugombana muda wote?”
“Kwanini unaongea hivyo ghafla tu?”Aliuliza Roma kwa kufosi tabasamu huku kope za macho yake zikitetema lakini Edna hakutoa jibu na aliweka kikombe chini na kusimama.
“Naenda kukaa na mama kwanza , kama utakuwa free nenda kamwangalie Lanlan na Mage , sitaki wasababishe matatizo kama jana baada ya kuvamia boti ya mtu mwingine na wenyewe kuwaona kama wezi”
“Sawa nimekuelewa nitaenda mpenzi”Aliongea Roma mara baada ya kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha huku akijitahidi kujituliza na kujiambia Edna yupo sawa na hakuna anamchomficha.
Unafikiri nini kinafanya joto la dunia
kushuka??Roma atarudi ujinini je akirudi atafanikiwa Aluta Continuara.
Tukutane jumanne kwa wale ambao siwadai.

Hatimae siku ya kesho yake iliwadia, siku ambayo ndio maalumu kwa fainali ya UEFA na Roma aliweza kuichukua familia yake katika eneo la watu mashuhuri(VIP) ndani ya uwanja wa Wembley.
Ijapokuwa walkuwa hapo kumwangalia Sophia atakavyo perfom tofauti na mecho lakini mazingira hayo ya shamra shamra yalikuwa mazuri kwao pia.
Malkia Catherine ambaye alikuwa mwenyeji wao aliwakariibisha , ilikuwa mara yake ya kwanza kukutana na Blandina mama yake Roma na walianza kuongea kwa pamoja kama vile wlaikuwa wakilingana umri.
Blandina na yeye alichukua fursa hio kumwelezea
Catheirne kile anachokifanya na ilimfurahisha
Catherine na kumwambia aatoa mchango wake katika taasisi yake ya vituo jumuishi vya kuelela Yatim.
Kitendo cha kukutana na mtu mzito kama huyo ilimfanya kujisikiavizuri kwa kuwa na mtoto kama Roma.
Kabla ya mecho kuanza Show ya Sophia na wasanii wengine ilipaswa kuanza na Sophia alikuwa ni msanii wa pili kutumbuiza na aliweza kuonekana akiwa amevalia viatu vya kimichezo.
Kutokana na muonekano wake wa umaridadi na urembo ilimfanya kuonekana vizuri mno katika runinga.
Sophia hakuwa tena yule msichana wa kawaida, wakati huo alikuwa ni Superstar ambaye ameshafanya kolabo na msanii mkubwa duniani kama Christen na wengine wengi na kazi zake zikafanya vizuri kimataifa.
Aliimba wimbo ambao ulikuwa na mchanganyiko wa lugha mbili kati ya kiswahili na kingereza na kutokana na kuwa na Vocal nzuri sauti yake iliteka hisia za watu wengi,
Baada ya Sophia kuondoka aliingia msannii mwingine mkubwa tu kutoka Marekani na alitumbuiza na kisha akaondoka na baada ya taratibu zingine kuisha hatimae mpira ulianza.
Baada ya kumaliza Show yake Sophia alikimbilia kwenda chumba cha VIP kwa ajili ya kukutana na ndugu zake , hata mama yake mzazi pia alikuwepo.
“Superstar wetu anazidi kuwa maarufu kadri siku zinavyosonga , naamini atakuwa ana mwingizia mapesa ya kutosha bosi wake Edna ?”Aliongea Mage kwa kutania.
“Ninachoingiza kwenye kampuni yake ni kidogo kulinganisha na anachokipata kwenye biashara zake zingine”Aliongea Sophia.
“Impressive perfomance “Aliongea Edna akimsifia na Sophia alijisikia vizuri kwa kauli hio , alijua kutokana na kilichotokea kati yake na Edna basi asingeongea nae hata kidogo lakini alifurahi kwamba hana kinyongo.
Baada ya kila mtu kuketi hatimae kila mtu alikaa kimya na kuendelea kuangalia mechi,
Mechi ilikuwa ni timu moja maarufu kutoka Hispania na ilikuwa ikishindana na timu kutoka moja Ufaransa hivyo shangwe ziliuwa juu sana kwa upande wa timu zote mbili.
Asilimi ya wote walikuwa hawana timu na hawakuwa bize sana na mpira kasoro ya Lanlan ambaye alikuwa amekodoa macho.
“Kwanini hawashindi ,mbona ni dhaifu vile na mpira
hauendi mbal, Mommy kwanini wanakimbia taratibu taratibu vile?”
Lanlan alikuwa kaiuliza maswali kama mashine huku Edna akijitahidi kujibu yote , ilionekana hakuelewa sheria za mpira zilivyo.
Baada ya kipindi cha kwanza kuisha wote wakiwa katika eneo la VIP kundi la watu ambao wamevalia mavazi ya suti walifika katika eneo hilo huku wengi wakiwa nnii weusi.
Walinzi waliofoka hapo hawakuoneysha kuzuia mwanaume mmoja ambaye ni mzungu alieongozana na wanaume wawili ambao wote walikuwa weusi.
Mshangao uliwashika warembo hao mara baada ya kugundua mtu ambae amefika katika eneo hilo , alikuwa ni Raisi Jeremy.
Edna alimwangalia Roma akimpa ishara kwamba hajui kama mtu huyo atafika Uingereza.
“Callum Boris I’ m sure you could have gotten a private room of your own to watch the match”Aliongea Catherine
“My apologies your Majesty”Aliongea m mwanaume huyo ambaye alikuwa ametanguliwa alikuwa ni waziri mkuu waUingereza afahamike kwa jina la Boris.
“Ni kwasababu rafiki yetu kutoka Rwanda mheshimiwa Jeremy amefika hapa akiwa na nia ya kuonana na kila moja lakini mathalani zaidi anataka kuonana na Mr Roma Ramoni”Aliongea , alikuwa akijua ubini halisi wa upluto wa Roma.
ITAENDELEA.
WATSAPP ONLY 0687151346
Sawaaa
 
Elimu niliyopata katika hii Hadithi yako, hakika mitazamo yangu mingi imebadilika!! Mi binafsi najua ugumu wakuandika tamthilia Kama hii!! Wew nikati ya binadamu ambao ni extra ordinary! Uzi wako umejibu maswali meengi sana katika ubongo wangu hakika umejua kutuheshimisha great thinker! Maneno ni mengi sana lakn itoshe tu kusema wewe ni extraordinary
Asante mkuu kwa positive feedback
 
Natamani ungegusia na Imani ya wale wanaoamini Dunia tambarare!! Ukatutoa dukuduku letu
 
Natamani ungegusia na Imani ya wale wanaoamini Dunia tambarare!! Ukatutoa dukuduku letu
Achana na hizo porojo, eti dunia tambarare. Sasa singanoJr anao uwezo gani wa kuthibitisha hilo zaidi ya astronomical evidence zilizopo?
 
Kwa huu mzigo nimeridhika kwa Kweli, hamu ya kuzid kusonga mbele inanizidi, inaonekana Shariff ndiye mwenye mchoro mzima wa namna Hedes wa zaman alivyouchora mpango wa anti-illuminant
 
Elimu niliyopata katika hii Hadithi yako, hakika mitazamo yangu mingi imebadilika!! Mi binafsi najua ugumu wakuandika tamthilia Kama hii!! Wew nikati ya binadamu ambao ni extra ordinary! Uzi wako umejibu maswali meengi sana katika ubongo wangu hakika umejua kutuheshimisha great thinker! Maneno ni mengi sana lakn itoshe tu kusema wewe ni extraordinary
Pendelea kusoma vitabu na hadithi mbalimbali za kale. Teknolojia imekuwa sasa, Yale masimulizi yaliyo kwenye vitabu vya kale sasa wanayaweka kwenye mfumo wa movies/series. Utang'amua kitu kikubwa zaidi
 
Kwa huu mzigo nimeridhika kwa Kweli, hamu ya kuzid kusonga mbele inanizidi, inaonekana Shariff ndiye mwenye mchoro mzima wa namna Hedes wa zaman alivyouchora mpango wa anti-illuminant
Ila Roma muda mwengine liko kama zezeta zezeta fulani hivi, yaani Rose ndio anamfunua akili na kuchukua maamuzi baada ya binadamu wengi kuanza kufa. Ndiomana sharif anamwita Roma binadamu mjinga, ameweka sana mapenzi mbele🤣🤣
 
Elimu niliyopata katika hii Hadithi yako, hakika mitazamo yangu mingi imebadilika!! Mi binafsi najua ugumu wakuandika tamthilia Kama hii!! Wew nikati ya binadamu ambao ni extra ordinary! Uzi wako umejibu maswali meengi sana katika ubongo wangu hakika umejua kutuheshimisha great thinker! Maneno ni mengi sana lakn itoshe tu kusema wewe ni extraordinary
Unaweza kusema hii ni story tu lakini ina asilimia kubwa za uhalisia wa Maisha ya binadam na Viumbe wengine (Creatures of universe).

Kwa asilimia kubwa matukio yanayotokea kwenye simulizi hii yanatokea pia kwenye dunia yetu hii ya Leo. Hapa unasikia habari za kupanda Level kwa Majini, hii Scenarial ina apply pia kwa binadama kwa asilimia nyingi. Mwili wa binadamu ukiwa msafi kimwili na kiroho huwa kuna ufunuo unakujia wa uelewa na uwezo fulani wa kufanya mambo katika Maisha.

Mfano:
1) Mtoto mdogo anapo balehe huwa anapata ufunuo(anapanda level) wa kujitambua (Biologicaly) na napata uwezo mkubwa wa kiakili.

2) Kijana aliyebalehe akitoa bikra(kufanya tendo kwa Mara ya kwanza) huwa anapata ufunuo(Anapandanda Level)

3) Kijana huyo akifikia umri fulani anapata ufunuo mwingine (Anapanda levo) na kupata uwezo wa kubeba majukumu fulani na hata kuanzisha familia.

4) Pia unapofikia hatua ya mtu mzima/ mzee huwa napata ufunuo (kupanda level ) unajawa na busara na Maono.

Sasa kinachotokea ni kwamba tuna vitu vingi mno vinatutoa kwenye reli (Distractions) na kushindwa kupata ufunuo mkubwa zaidi na kuwa na uwezo wa kufanya mambo makubwa hapa duniani Mfano: Ngono zembe(Uchafu wa kiroho) ,Pombe, Vyakula vibovu, matumizi yaliyopitiliza ya Teknologia, kukosa Mwongozo wa Misingi ya Maisha ya Mwanadamu na Mengine Mengi.

Binadamu Tuna uwezo wa kimaajabu ila wajanja wanaojua hizi siri wamezificha na wanatuwekea vizuizi tusijitambue kwa Wingi.

"The greatest Potential, Strength and Powers of Human being are hiden within us, Within our Mind"
 
Back
Top Bottom